SWALI: Nini maana ya;
Mithali 10:5 Akusanyaye wakati wa hari ni mwana mwenye hekima; Bali asinziaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
JIBU: Kwa kawaida kipindi cha hari ( kiangazi), huwa ndio kipindi cha mavuno mengi. kwasababu mavuno yanakuwa yameshakomaa na kukauka.
Hivyo wakulima wengi kwa nyakati hizo wanakuwa mashambani kuvuna, kama vile tu walivyokuwa wakati wa masika walipokuwa wanapanda..
Na ni kipindi ambacho mkulima hufurahi pia kwasababu anakwenda kuona matunda ya kazi yake wakati si mwingi.
Lakini ni ajabu kuona, mtu ambaye hajasumbukia kupanda, halafu anaambiwa tu yeye akavune, tena kwa faida yake mwenyewe akauze, anaona uvivu kwenda kuvuna, hataki kabisa kwenda kujishughulisha na kazi hiyo, mpaka msimu mwingine unakuja, mazao yanaharibikia yote shambani. Mtu kama huyo utamchukuliaje? Ni sawa tu akiitwa “mwana mwenye kuaibisha”, Kwasasababu ni uvivu wa makusudi.
Sasa jambo kama hili kwasasa lipo pia rohoni.
Na lipo kwa namna mbili.
Bwana Yesu alisema..
Yohana 4:35-38
[35]Hamsemi ninyi, Bado miezi minne, ndipo yaja mavuno? Tazama, mimi nawaambieni, Inueni macho yenu myatazame mashamba, ya kuwa yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno.
[36]Naye avunaye hupokea mshahara, na kukusanya matunda kwa uzima wa milele, ili yeye apandaye na yeye avunaye wapate kufurahi pamoja.
[37]Kwa maana hapo neno hilo huwa kweli, Mmoja hupanda akavuna mwingine.
[38]Mimi naliwatuma myavune yale msiyoyataabikia; wengine walitaabika, nanyi mmeingia katika taabu yao.
Umeona? Kufuatana na vifungu hivyo Bwana anatuonyesha kuwa tupo wakati wa mavuno sasa, wakati wa hari, wa kiangazi, mashamba yamekwisha kuwa meupe, Hivyo sote kwa pamoja kwa moyo mmoja yatupasa tutoke tuanze kuifanya kazi ya Mungu bila ulegevu kwasababu Yesu alishatupa agizo kuu kuwa tutoke tuenende ulimwenguni kote kuwafanya mataifa kuwa wanafunzi.
Lakini ukilala na kusema huu si wakati, ndugu ni sawasawa na hilo neno unakuwa mwana mwenye kuaibisha. Kila mmoja wetu ameitwa kuwahubiria wengine habari njema za wokovu wa Yesu Kristo, haijalishi upo ofisini, shuleni, ugenini, jeshini, una wajibu wa kuvuna. Shika mundu yako washuhudie wengine habari njema, kwasababu huu ni wakati sahihi, na hautadumu milele.Hivyo tumia muda vizuri.
Neno la Mungu linasema..
Mhubiri 12:1
[1]Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo.
na pia linasema..
1 Yohana 2:14
[14]Nimewaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.
Katika umri wako wa ujana ambao una nguvu ndio wakati wa kwenda shambani kumtumikia Bwana wako. ndio wakati wako wa hari, lakini unapokuwa mlegevu, hujishughulishi na Mungu wako, unachowaza ni anasa, starehe, mihangaiko, unasema nitamtumikia Mungu uzeeni, fahamu kuwa wewe ni sawa na mwana mwenye kuaibisha, kwasababu wakati huo utakuwa umeshapita.
Komboa wakati wako, thamini majira uliyopo, etende kazi ya Bwana.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?
Maana ya Mithali 25:25 Kama vile maji ya baridi kwa mtu mwenye kiu
Nini maana ya Mithali 16:30 Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka;
Jibu: “Wahivi” walikuwa ni moja ya mataifa saba (7) yaliyoondolewa na Israeli katika ile nchi ya ahadi.
Mataifa mengine sita (6) yalikuwa ni Wakanaani, Wahiti, Wayebusi, Waamori, Waperizi na Wagirgashi (soma Yoshua 3:10).
“Wahivi” walionekana kuishi sehemu za vilima vya Lebanoni (kaskazini mwa Israeli mpakani).
Waamuzi 3:3 “aliwaacha wakuu watano wa Wafilisti, na Wakanaani wote, na Wasidoni, na WAHIVI WALIOKAA KATIKA KILIMA CHA LEBANONI, TOKA MLIMA WA BAAL-HERMONI MPAKA KUINGIA HAMATHI”
Na sehemu nyingine Wahivi waliyoonekana ni katika nchi ya Mispa karibu na Gibeoni
Yoshua 11:3 “na kwa Mkanaani upande wa mashariki, na upande wa magharibi, na kwa Mwamori, na Mhiti, na Mperizi na Myebusi katika nchi ya vilima, na kwa MHIVI PALE CHINI YA HERMONI KATIKA NCHI YA MISPA”.
Hivyo waliishi sehemu zaidi ya moja katika ile nchi, na ndio wale na ndio wale waliowalaghai wana wa Israeli na kuingia nao agano la kutowaua..kwasababu waliwaambiwa wana wa Israeli kuwa wenyewe ni wenyeji wa mbali kumbe pia walikuwa wanaishi karibu..(Soma Yoshua 9:1-27).
Sababu kuu ya Bwana MUNGU kiyatoa mataifa yale saba (7) kutoka katika nchi ya ahadi ni maovu waliyokuwa wanayatenda..
Walikuwa wanafanya uchawi, mauaji, uasherati, maonezi, dhuluma na mambo mengine mabaya bila hofu yoyote…hiyo ikawa sababu ya kwanza kuwaondoa katika ile nchi…na sababu ya pili ni ahadi Mungu aliyompa Ibrahimu.
Kumbukumbu 9:4” Usiseme moyoni mwako, BWANA, Mungu wako, atakapokwisha kuwasukumia nje mbele yako, ukasema, Ni kwa haki yangu alivyonitia BWANA niimiliki nchi hii; kwani ni kwa ajili ya uovu wa mataifa haya BWANA awafukuza nje mbele yako.
5 SI KWA HAKI YAKO, WALA KWA UNYOFU WA MOYO WAKO, HIVI UINGIAVYO KUIMILIKI NCHI YAO; LAKINI NI KWA UOVU WA MATAIFA HAYA BWANA, MUNGU WAKO, AWAFUKUZA NJE MBELE YAKO; tena apate kuliweka imara hilo neno BWANA alilowaapia baba zako Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo.
6 BASI JUA YA KUWA BWANA, MUNGU WAKO, HAKUPI NCHI HII NZURI UIMILIKI KWA AJILI YA HAKI YAKO, KWA MAANA U TAIFA LENYE SHINGO NGUMU”.
Na sababu hizo hizo pia ndizo zilizowatoa Israeli kutoka hiyo nchi ya ahadi na kupelekwa Ashuru na Babeli utumwani.
2 Nyakati 36:14 “Na zaidi ya hayo wakuu wote wa makuhani, na watu, wakakosa mno sawasawa na machukizo yote ya mataifa; wakainajisi nyumba ya BWANA aliyoitakasa katika Yerusalemu.
15 Naye BWANA, Mungu wa baba zao, akatuma kwao kwa mikono ya wajumbe wake, akiondoka mapema, na kutuma; kwa sababu aliwahurumia watu wake, na makao yake;
16 lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, hata ilipozidi ghadhabu ya BWANA juu ya watu wake, hata kusiwe na kuponya.
17 KWA HIYO AKALETA JUU YAO MFALME WA WAKALDAYO, ALIYEWAUA VIJANA WAO KWA UPANGA NYUMBANI MWA PATAKATIFU PAO, ASIWAHURUMIE KIJANA WALA MWANAMWALI, MZEE WALA MKONGWE; AKAWATIA WOTE MKONONI MWAKE”
Na sababu hizo hizo ndizo zinazotutoa wengi leo kutoka katika ahadi na baraka Mungu alizotuahidia na kujikuta tupo katika laana.
Kumbuka siku zote...SUMU ya kwanza wa Mtu ni DHAMBI na wala si shetani…kilichomwondoa mwanadamu wa kwanza katika nchinya ahadi pale Edeni ni DHAMBI!..
Kilichoshusha maisha ya mwanadamu kutoka umilele mpaka mpaka miaka 120 ni dhambi…hivyo cha kuogopa cha kwanza ni dhambi sio shetani…kwasababu shetani anatumia dhambi kumwaribu mwanadamu.
Hivyo mtu akiweza kuishinda dhambi kwa kudumu katika neno la Mungu, shetani anabaki kuwa kama karatasi tu…hana nguvu yoyote..ni sawa na askari aliyepokonywa silaha.
Kanuni ya kuishinda dhambi ipo kwa Bwana YESU tu na inaanza na TOBA kisha UBATIZO SAHIHI na mwisho UJAZO WA ROHO MTAKATIFU. (Matendo 2:38)
Mtu akiweza kukamilisha hatua hizo tatu kwa kumaanisha kabisa dhambi haiwezi kumshinda na atadumu daima katika ahadi na baraka za Mungu, bila kutumia mafuta,au chumvi au udongo ujulikanao kama wa upako.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Wayebusi walikuwa ni watu gani?
Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?
Swali: Huyu Kuhani wa Oni ambaye binti yake aliolewa na Yusufu, tunayemsoma katika Mwanzo 41:45 je alikuwa ni kuhani wa Mungu au wa kuhani wa miungu ya kiMisri?
Jibu: Terejee mistari hiyo…
Mwanzo 41:45 “Farao akamwita Yusufu, Safenath-panea; akamwoza Asenathi, binti POTIFERA, KUHANI WA ONI, kuwa mkewe Yusufu akaenda huko na huko katika nchi yote ya Misri”.
“Oni” lilikuwa ni eneo katika nchi ya Misri, kama vile ilivyo Mwanza, au Lindi nchini Tanzania au Nakuru Kenya.
Mji huu (wa Oni) Ulikuwa ni mji wa miungu ya kiMisri, na nchi ya Misri yote ilikuwa ni nchi inayoabudu miungu mingi, ikiwemo Bethshemeshi (soma Yeremia 43:13), sanamu za ng’ombe (1Wafalme 12:28) na mingine mingi (soma Yoshua 24:14).
Hivyo huyu kuhani “Potifera” hakuwa kuhani wa Mungu wa mbingu nan chi (YEHOVA), bali alikuwa ni kuhani wa miungu ya kimisri iliyokuwepo hapo “Oni”, na Yusufu alipofika kule alipewa binti yake awe mkewe.
Na Kwanini ulikuwa hivyo?(yaani kwanini Farao amchagulie mke na si Yusufu ajitafutie mwenyewe?)..
Jibu ni kwamba Farao aliona njia pekee ya kumheshimisha Yusufu na kumfanya apate kibali katikati ya waMisri ni kumuunganisha yeye na familia za watu wa kubwa na wenye hadhi wa nchi ya Misri.(wenye hadhi za kiimani), kwasababu naye Yusufu alikuwa mtu wa kiimani.
Hivyo na mtu wa kiimani na kidini aliyekuwa mkubwa huko ni huyo kuhani wa Oni, ndipo akapewa binti yake aliyeitwa Asenathi. Lakini hata baada ya Yusufu kupewa mwanamke huyo bado hakufuata miungu hiyo ya kiMisri, na Farao alilijua hilo, na wala hakumpatia huyo binti kwa lengo la kugeuza Imani ya Yusufu, bali kumheshimisha.
Lakini kwasababu pia ilikuwa ni mpango wa Mungu iwe hivyo (Yusufu aoe mwanamke wa kimataifa) basi hata mke aliyempata alikuwa ni sahihi kwake na wala hakumsumbua Yusufu baada ya hapo (huwenda hata alimtumikia Mungu wa Israeli baada ya hapo), na Zaidi sana tendo la Yusufu kumwoa Asenathi (binti wa kimataifa) limebeba ufunuo mkubwa juu ya Bwana YESU KRISTO na BIBI-HARUSI WAKE (yaani kanisa).
Kwa urefu marefu juu ya ufunuo wa maisha ya Yusufu fungua hapa >>>Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Musa aliua lakini bado Mungu alimchangua kuwaongoza wana wa Israeli, je! Mungu anaruhusu mauaji?
ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.
Ni kosa gani lililowafanya wana wa israeli wawe watumwa miaka 400 Misri?.
Ni lini na wapi Ibrahimu aliiona siku ya Bwana akashangilia?.
Jina la Bwana na Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe daima. Karibu katika mafundisho ya biblia, Neno la Mungu wetu lililo Taa na Mwanga wa Njia zetu (Zab.119:105).
Zipo njia Mbili tu zilizowekwa mbele ya kila mwanadamu, Nazo ni njia ya UZIMA, na njia ya MAUTI.
Yeremia 21:8 “Nawe waambie watu hawa, Bwana asema hivi, Tazama naweka mbele yenu NJIA YA UZIMA, na NJIA YA MAUTI”.
Njia ya Uzima, inamwongoza mtu “Uzimani”..na Njia ya Mauti inamwongoza mtu “Mautini (ziwa la moto)”.
Njia ya Uzima imenyooka haina migawanyiko mingi (sawasawa na Yohana 14:6), ambapo Bwana YESU alisema yeye ndio hiyo “Njia”, na mtu hafiki kwa Baba isipokuwa kwa njia yake yeye.
Yohana 14:6 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi”
(Maana yake hakuna njia mkato wala njia mbadala ya kumfikia Baba)…Ni moja tu! Tena iliyonyooka, nayo ni YESU KRISTO, na si kupitia mtu mwingine yoyote mashuhuri, au mtakatifu mwingine yoyote aliye hai au aliyekufa au nabii yoyote katika biblia.
Lakini ile ya Mauti inamigawanyiko mingi, inaanza kama njia moja lakini mwisho wake inamigawanyiko,
Mithali 14:12 “IKO NJIA ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni NJIA ZA MAUTI”
Hapo anamaliza na kusema mwisho wake ni “NJIA ZA MAUTI” na si “NJIA YA MAUTI” kana kwamba ni moja, bali nyingi. Na njia ya Mauti si mwingine Zaidi ya “shetani”…Kama jinsi njia ya UZIMA ilivyo Bwana YESU kadhalika njia ya Mauti ni “shetani”.
Na shetani anaabudiwa kupitia vitu vingi, anaweza kuabudiwa kupitia miti, mawe, udongo, au kupitia vitu vitu vingine kama fedha, watu, dini n.k..ndio maana hapo biblia inasema hiyo Njia (shetani) mwisho wake ni “Njia za Mauti” (maana yake zipo nyingi).
Na hiyo ndio sababu pia kwanini biblia inataja uwepo wa milango mingi ya kuzimu (Soma Mathayo 16:18). Milango ya kuzimu ndio hizo njia zote zinazoweza kumpeleka mtu kuzimu.
Nabii Isaya amezidi kuziweza vizuri njia hizi kwa ufunuo wa Roho… Amezitofautisha kama “NJIA” pamoja na “NJIA KUU”..
Isaya 35:8 “Na hapo patakuwa na NJIA KUU, na NJIA….”
“Njia Kuu” ni “Njia ya Uzima”…. Na “Njia” pekee yake “Ni njia ya Mauti”..
Lakini anaendelea kusema… hiyo “Njia kuu” itaitwa Njia ya utakatifu, na ya watu wasafirio..
Isaya 35:8 “Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, Njia ya utakatifu; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; wasafirio….”
Maana yake wote wanaiendea hiyo njia ya Uzima (YESU) Ni lazima “utakatifu” uwe muhuri wao sawasawa na kitabu kile cha Waebrani 12:14.
Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”.
Vile vile ni lazima wawe “wasafiri”.. Tabia ya msafiri huwa anadumu katika chombo cha usafiri awapo safarini, na hawezi kujishikisha na mambo akutanayo njiani au barabarani…. na chombo chetu cha usafiri ni NEEMA YA MUNGU. Tuwapo katika safari hii ya kwenda mbinguni kupitia njia ya Bwana YESU, mambo ya ulimwengu hayapaswi yashikamane na sisi.
1Petro 2:11 “Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho”.
Na mwisho anasema.. “wajapokuwa wajinga hawatapotea katika njia hiyo”
Isaya 35:8 “Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, Njia ya utakatifu; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; wasafirio, WAJAPOKUWA WAJINGA, HAWATAPOTEA KATIKA NJIA HIYO”.
Ikiwa utaonekana mjinga kwa kuwa umeamua kuifuata NJIA KUU ya UTAKATIFU na umeamua kuishi kama MSAFIRI duniani, basi biblia inasema “hautapotea/hatutapotea” katika njia hiyo..
Haijalishi dunia nzima itakuona kama umepotea, umerukwa na akili, umechanganyikiwa…Mungu yeye anakuona upo katika njia sahihi na una hekima nyingi.. kwasababu mwisho wa njia hiyo ni UZIMA WA MILELE, Na Utakutana na Bwana naye atakufuta machozi.
Ufunuo 7:15 “Kwa hiyo wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu, nao wanamtumikia mchana na usiku katika hekalu lake, na yeye aketiye katika kiti cha enzi atatanda hema yake juu yao
16 Hawataona njaa tena, wala hawataona kiu tena, wala jua halitawapiga, wala hari iliyo yote.
17 Kwa maana huyo Mwana-Kondoo, aliye katikati ya kiti cha enzi, atawachunga, naye atawaongoza kwenye chemchemi za maji yenye uhai, na Mungu atayafuta machozi yote katika macho yao.”
Je wewe leo umechagua njia ipi??… Njia kuu ya Uzima? Au Njia ya Mauti..
Kumbukumbu 30:14 “Lakini neno li karibu nawe sana, li katika kinywa chako na moyo wako, upate kulifanya.
15 ANGALIA, NIMEKUWEKEA LEO MBELE YAKO UZIMA NA MEMA, NA MAUTI NA MABAYA”.
CHAGUA NJIA YA UZIMA, na TEMBEA KATIKA NJIA KUU YA UTAKATIFU.
BWANA AKUBARIKI.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.
TABIA ZA NJIA YA MUNGU KWA MKRISTO
HATARI YA KUTOKUITAFAKARI BIBLIA VIZURI?
KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI
Hadhari ni nomino ya kitenzi tahadhari. Neno Lenye maana ya “uangalifu”.
>Kwamfano mwalimu anayesahisha mitihani ya wanafunzi tunasema huwa na hadhari kubwa katika usahishaji.
Katika biblia neno hili utalisoma kwenye vifungu hivi;
Danieli 2:13 Basi ile amri ikatangazwa, na hao wenye hekima walikuwa karibu na kuuawa; watu wakamtafuta Danielii na wenzake ili wauawe. 14 Ndipo Danieli kwa busara na HADHARI akamjibu Arioko, akida wa walinzi wa mfalme, aliyekuwa ametoka ili kuwaua wenye hekima wa Babeli; 15 alijibu, akamwambia Arioko, akida wa walinzi wa mfalme, Mbona amri hii ya mfalme ina ukali namna hii? Ndipo Arioko akamwarifu Danielii habari ile
Mithali 1: 1 Mithali za Sulemani, mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli. 2 Kujua hekima na adabu; kutambua maneno ya ufahamu; 3 kufundishwa matendo ya busara, katika haki na hukumu na adili. 4 Kuwapa wajinga werevu, na kijana maarifa na HADHARI;
Yoshua 22:24 au kama sisi tumefanya jambo hili kwa HADHARI sana, tena makusudi, huku tukisema, Katika siku zijazo wana wenu yamkini wakanena na wana wetu, na kusema, Ninyi mna nini na Bwana, yeye Mungu wa Israeli?
Sisi pia kama watakatifu, tuwe na hadhari, katika maisha ya ulimwenguni. Tunaishi ulimwenguni lakini hatupaswi kufungwa nira na huo kwa jinsi isivyo sawasawa. Kwasababu watu wanaokosa jambo hili husongwa na anasa, udanganyifu wa mali na shughuli za ulimwengu huu, na tamaa ya mambo mengine hatimaye hawazalishi kitu.
Shalom.
Je! Umeokoka? Unatamani leo kupokea msamaha wa dhambi? Ikiwa jibu ni ndio basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya kumkaribisha Yesu moyoni mwako.>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Akida ni nani kibiblia, na kazi yake ni ipi? (Mathayo 8:5)
Swali: Biblia inataja siri za Mungu katika 1Wakorintho 4:1, je hizi siri ni zipi na zipo ngapi?
Jibu: Turejee,
1Wakorintho 4:1 “Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu”
Awali ya yote tujue maana ya uwakili unaozungumziwa hapo?…. Uwakili unaozungumziwa hapo sio mfano wa ule wa “mahakamani” La! bali unamaanisha “Usimamizi”… Kibiblia mtu aliyepewa usimamizi wa nyumba au kazi Fulani, aliitwa “Wakili”..soma Luka 12:43-48 na Luka 16:1-13…
Hivyo hapo Mtume Paulo, aliposema “.. sisi ni mawakili wa siri za Mungu” maana yake “wameweka kuisimamia nyumba ya Mungu kwa kuzifundisha siri za Mungu”….Kwa urefu Zaidi kuhusu Uwakili katika biblia fungua hapa >>> Wakili ni nani kibiblia? Uwakili ni nini?
Sasa tukirudi katika swali letu, SIRI ZA MUNGU NI ZIPI na ZIPO NGAPI?
Jibu ni kwamba “SIRI ZA MUNGU” zimetajwa MBILI TU (2), katika biblia. Ambazo ni 1)YESU NI MUNGU. 2) MATAIFA NI WARITHI WA AHADI ZA MUNGU… Tutazame moja baada ya nyingine.
1.YESU NI MUNGU.
Wakolosai 2:2 “ili wafarijiwe mioyo yao, wakiunganishwa katika upendo, wakapate utajiri wote wa kufahamu kwa hakika, WAPATE KUJUA KABISA SIRI YA MUNGU, YAANI, KRISTO;
3 ambaye ndani yake yeye HAZINA ZOTE ZA HEKIMA NA MAARIFA ZIMESITIRIKA”.
Kwanini au kivipi “KRISTO” ni “SIRI YA MUNGU”?.. Kwasababu ndani yake hazina zote na hekima na maarifa zimesitirika..maana yake yeye ndio kila kitu, NDIYE MUNGU MWENYEWE katika mwili wa kibinadamu!!!!..Kiasi kwamba laiti Pilato angelijua hilo, asingeruhusu hukumu ipite juu yake, laiti wale makuhani na maaskari wangelijua hilo wasingepitisha misubari katika mikono yake na miguu yake, lakini walifumbwa macho ili tupate wokovu.
1Wakorintho 2:7 “bali twanena hekima ya Mungu KATIKA SIRI, ile hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu;
8 AMBAYO WENYE KUITAWALA DUNIA HII HAWAIJUI HATA MMOJA; MAANA KAMA WANGALIIJUA, WASINGALIMSULIBISHA BWANA WA UTUKUFU”.
Siri hii ya kwamba KRISTO NI MUNGU, inaanzia katika Isaya 9:6, na kisha Yohana 1:1, Yohana 14:9, Yohana 20:28, Tito 2:13, 1Timotheo 3:16 na Ufunuo 22:13-13.
Siri ya Bwana YESU Kuwa MUNGU, inajulikana pia kama “Siri ya Utauwa/Uungu” ambayo Mtume Paulo aliitaja katika 1Timotheo 3:16..
1Timotheo 3:16 “Na bila shaka SIRI YA UTAUWA NI KUU. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu”.
Kwahiyo BWANA YESU KRISTO ni MUNGU ALIYEDHIHIRISHWA KATIKA MWILI, na wote tunaomwamini tunapaswa tuwe mawakili wa SIRI HIYO, Maana yake “KUIAMINI na KUIHUBIRI KWA WENGINE, wasiofahamu” .
2. MATAIFA NI WARITHI WA AHADI ZA MUNGU.
Hii ni Siri ya pili (2) ambayo ilifichwa kwa vizazi vingi, lakini ikaja kufunuliwa baada ya KRISTO kupaa juu mbinguni.. Tangu wakati wa Musa mpaka wakati wa Yohana, manabii wote na wayahudi wote walikuwa wanajua na kuamini kuwa “hakuna namna yoyote, wala njia yoyote” itakayofanyika kwa watu wa mataifa wakubaliwe na MUNGU.
Wote walijua Taifa Teule la Mungu ni ISRAELI peke yake, na mataifa mengine yote ni watu najisi, lakini baada ya Bwana YESU kuondoka alianza kumfunulia Petro siri hiyo kuwa hata mataifa ni warithi sawa tu na wayahudi, kupitia msalaba wake (Bwana YESU).. Na alimfunulia siri hiyo wakati ule alipokwenda nyumbani kwa Kornelio aliyekuwa mtu wa mataifa (Matendo 10)..
Na baadaye Bwana YESU akaja kumfunulia Mtume Paulo siri hiyohiyo kuwa Mataifa nao ni warithi, tena wa ahadi moja na wayahudi, hivyo wanastahili injili, na kuhubiriwa habari njema..
Waefeso 3:5 “Siri hiyo hawakujulishwa wanadamu katika vizazi vingine; kama walivyofunuliwa mitume wake watakatifu na manabii zamani hizi katika Roho;
6 YA KWAMBA MATAIFA NI WARITHI PAMOJA NASI WA URITHI MMOJA, NA WA MWILI MMOJA, NA WASHIRIKI PAMOJA NASI WA AHADI YAKE ILIYO KATIKA KRISTO YESU KWA NJIA YA INJILI;
7 Injili hiyo ambayo nalifanywa mhudumu wake, kwa kadiri ya kipawa cha neema ya Mungu niliyopewa kwa kadiri ya utendaji wa uweza wake”.
Na sisi lazima tuwe wahudumu (Mawakili) wa siri hii kwamba “Wokovu ni haki ya watu wote” na Mungu anawapokea watu wote, ikiwa tu watakubali kutii na kunyenyekea mbele zake.
Kwahiyo kwa hitimisho, ni kwamba “Siri za Mungu” Si zile siri za kanisa, au zile za watumishi, au wapendwa kanisani…La! Bali ni hizo zilizotajwa hapo katika maandiko…Na kumbuka, shetani naye ana siri yake ijulikanayo kama “Siri ya Kuasi” iliyotajwa katika biblia ambayo inafanya kazi kwa kasi sana nyakati hizi…
Je umempokea YESU?..Kumbuka kipindi tulichopo ni cha Neema, lakini hii neema haitadumu milele, itafika wakati itaisha.. baada ya unyakuo hakuna neema tena, vile vile baada ya kifo hakuna Neema tena. Ni heri ukayasalimisha maisha yako kwa Bwana YESU maadamu unaishi, baada ya kifo hakuna nafasi ya pili.
Warumi 10:8 “Lakini yanenaje? Lile neno li karibu nawe, katika kinywa chako, na katika moyo wako; yaani, ni lile neno la imani tulihubirilo.
9 Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.
10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.
11 Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye hatatahayarika
12 Kwa maana hakuna tofauti ya Myahudi na Myunani; maana yeye yule ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao;
13 KWA KUWA, KILA ATAKAYELIITIA JINA LA BWANA ATAOKOKA”
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.
Hazina za gizani ni zipi? (Isaya 45:3).
SIRI YA KUASI KATIKA KANISA LA MUNGU.
Adabu, ni kitendo cha kuonyesha staha, kufuata miiko, kuonyeshaAdabu ni nini biblia? ustaarabu mzuri kwa wengine.
Adabu huonyeshwa kwa Mungu, lakini pia kwa wanadamu.
> Ni pamoja na mwonekano wako uwapo ibadani.
Yesu alipomwona Petro akiwa uchi alijivika vazi lake kwasababu alitambua anahitaji kuonyesha adabu kwa Mungu wake. (Yohana 21:7).
>Ni pamoja na kuwa mtulivu: Uwapo ibadani, mazungumzo ya ovyo, yasiyo ya kiibada yaepuke, minong’ono madhabahuni kwa Mungu acha, kuchati, mizunguko zunguko, kutafuna tafutana.havihitajiki,
>Ni pamoja na Kuwasalimia wengine. Yesu alisema.
Mathayo 5:47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo? 48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.
>Vilevile ni pamoja na kuwasikiliza wengine, kuzuia kinywa chako kunena zaidi ya wastani (Kiasi), kuonyesha upole, kuonyesha kujali, kuonyesha maadili, na kutojishughulisha na mambo ya wengine.
Maandiko yanatufundisha tunda mojawapo la upendo ni adabu.
1Wakorintho 13:4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; 5 HAUKOSI KUWA NA ADABU; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya.
>Vilevile Imetoa agizo kwa wanawake wacha Mungu,kwamba pambo lao mojawapo liwe ni adabu nzuri (1Timotheo 2:9). Ambapo huusisha pia Uvaaji wako kilemba uwapo ibadani ni adabu kwa Mungu wako kwasababu maandiko yameagiza hivyo. (1Wakorintho 11:5). Kujisitiri kwako ni adabu pia.
Lakini zaidi sana imetoa agizo kwa watawakatifu wote, tuenende kwa adabu kwa wale walio nje (1Wathesalonike 4:12).
Hivyo, sote kwa pamoja tuipe adabu nafasi maishani mwetu,ili tujengwe.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima; (Mithali 11:16)
Heshima ni kitendo cha kumpa mtu hadhi yake, au uthamani wake anaostahili. Kwa kawaida kila mwanadamu anastahili heshima. Na hivyo kama mwamini huna budi kujua jinsi ya kuigawanya heshima kulingana na mtu husika. Kwasababu ukosefu wa heshimu, kwanza ni zao la kiburi (Mithali 15:33), lakini pia hukuondolea Baraka na kibali popote pale uendapo. Lakini pia ukitoa heshima isiyompa mtu ni kosa pia.
Warumi 13:7 Wapeni wote haki zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahiliye hofu, hofu; astahiliye heshima, heshima
Kutii maelekezo yao.
Waebrania 13:17 Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.
Kutowakwaza,
Waefeso 6:4 Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana.
Kutenda agizo lao.
Warumi 13:1 Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu. 2 Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu
Kuwatumikia kwa uaminifu na adabu. (Waefeso 6:5-8)
Hivyo kwa hitimisho, ni kwamba kila mwanadamu anastahili heshima, haijalishi, tajiri, au maskini, mrefu au mfupi, mgonjwa au mzima, mwenye elimu au asiye na elimu, bwana au mtumwa, ameokoka au hajaokoka. Wote ni agizo tuheshimiane.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
(Masomo maalumu kwa wazazi/walezi).
Ni nini unafanya kama mzazi uwapo nyumbani?.. Je maisha yako ndani ya kanisa ni sawa na yale nje ya kanisa?..Je kile unachokifanya kanisani ndicho unachokifanya nyumbani?…je nyumbani kwako ni sehemu ya kuishi tu au ni sehemu pia ya ibada?.
Kama wewe ni mwalimu kanisani, ni lazima pia uwe mwalimu nyumbani kwako…kama wewe ni kiongozi katika nyumba ya Mungu ni lazima pia uwe kiongozi katika nyumba yako, kama wewe ni mchungaji katika nyumba ya Mungu ni lazima pia uwe mchungaji katika nyumba yako mwenyewe…Ndivyo biblia inavyotufundisha.
Mitume wa Bwana YESU ni kielelezo kwetu, wao walikuwa wakihubiri Neno HEKALUNI NA NYUMBANI, kama maandiko yanavyosema, hivyo kama na sisi tumejengwa juu ya msingi wao ni lazima tufanye kama wao walivyofanya..
Matendo 5:42 “Na kila siku, NDANI YA HEKALU na NYUMBANI MWAO, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema za Yesu kwamba ni Kristo”.
Umeona?.. Si hekaluni tu!, bali hata nyumbani…. Uharibifu mkubwa shetani anauanzia nyumbani… Hivyo ni lazima uwe na AMRI, katika nyumba yako mwenyewe… Ni lazima pafanyike ibada nyumbani kila siku, ni lazima pafanyike maombi, ni lazima watoto na wengine wanaoishi katika nyumba yako wajue kuomba na kuombea wengine.
Ni lazima watoto wajifunze biblia na kufundisha biblia tangu wakiwa wadogo, ni lazima pia wajifunze kutoa.. ni lazima wote wawe wa kiroho, ni lazima uwafundishe wawe vipaumbele katika Imani wawapo shuleni, maana yake wakiwa shuleni wawe vipaumbele katika kuongoza maombi kwa wanafunzi wenzao, na kuomba vile vile kufunga… Na si kuwaacha jumapili kwa jumapili tu wafundishwe kanisani hayo mambo..
Jenga tabia ya kuwafuatilia mienendo yao ya kiimani wakiwa mashuleni, fuatilia sifa zao za kiimani wawapo mashuleni, (na si tu taaluma yao)..wapo watoto taaluma zao zinaonekana nzuri lakini shetani kashawaharibu kitabia muda mrefu (matokeo yake yatakuja kuonekana baadaye).
Hivyo kama mzazi au mlezi, simama katika hiyo nafasi… kiasi kwamba NENO LA MUNGU nyumbani kwako ni AMRI sio OMBI!. Kama Nabii Yoshua alivyoazimia zamani zile..
Yoshua 24:15 “Nanyi kama mkiona ni vibaya kumtumikia Bwana, chagueni hivi leo mtakayemtumikia; kwamba ni miungu ile ambayo baba zenu waliitumikia ng’ambo ya Mto, au kwamba ni miungu ya wale Waamori ambao mnakaa katika nchi yao; LAKINI MIMI NA NYUMBA YANGU TUTAMTUMIKIA BWANA.
16 Hao watu wakajibu wakasema, Hasha! Tusimwache Bwana, ili kuitumikia miungu mingine”.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?
YESU HAYUPO KATIKA MAZINGIRA YALEYALE TU SIKUZOTE, USIJISAHAU.
Mafundisho maalumu kwa watumishi wa Mungu na Watenda kazi wote katika shamba la Bwana.
Maombolezo 2:19
[19]Inuka, ulalamike usiku, Mwanzo wa makesha yake; Mimina moyo wako kama maji usoni pa Bwana; Umwinulie mikono yako; KWA UHAI WA WATOTO WAKO WACHANGA WAZIMIAO KWA NJAA, Mwanzo wa kila njia kuu.
Ikiwa wewe ni mzazi au mlezi unaelewa ni uchungu mwingi kiasi gani unakupata pale unapoona mtoto wako anaangamia kwa kukosa mahitaji yake muhimu, mfano wa chakula. Ndicho kilichotokea kwa mama Hajiri siku alipofukuzwa kwa Ibrahimu, akiwa kule jangwani amepotea hali ilikuwa mbaya sana, kwani chakula na maji viliwaishia kabisa, huwenda zilipita siku kadhaa hawakuona dalili yoyote ya kupata msaada. Hivyo alichokifanya Hajiri, ni kwenda mbali kidogo na kumlilia sana Mungu wake, na Mungu akasikia, akaonyeshwa palipo na maji, akaenda kumpa mwanae, kuonyesha ni jinsi gani alivyouthamini uhai wa Ishmaeli.
Mwanzo 21:14 Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji, akampa Hajiri akimtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka, akapotea katika jangwa la Beer-sheba.
15 Yale maji yakaisha katika kiriba, akamlaza kijana chini ya kijiti kimoja.
16 Akaenda akakaa akimkabili, mbali naye kadiri ya mtupo wa mshale; maana alisema, Nisimwone kijana akifa; naye akakaa akimkabili, AKAPAZA SAUTI YAKE, AKALIA.
17 Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, Una nini, Hajiri? Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko.
18 Ondoka, ukamwinue kijana, ukamshike mkononi mwako, kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa.
19 Mungu akamfumbua macho, naye akaona kisima cha maji; akaenda akakijaza kiriba maji, akamnywesha kijana.
Umeona kama Hajiri asingemtafuta Mungu katika hali ile, ni wazi kuwa Yule kijana ambaye alikuwa amekusudiwa awe taifa kubwa angefia jangwani na yale maono yasingetokea.
Ndicho tunachojifunza katika vifungu hivyo, kwenye kitabu cha Maombolezo, anasema kesha, ulie, kwa ajili ya watoto wako wachanga wazimiao kwa njaa. Leo hii tuna watu wengi ambao wameokoka kwa kuisikia injili yetu. Lakini je, watu hao wanasimama au wanakufa?, Unapomhubiria mtu, hatutakiwi kusema yaliyobaki namwachia Mungu, bali ni kuhakikisha hafi kiroho kwa kukosa chakula cha uzima. Na hiyo inakuja kwa kuendelea kumfuatilia kumfundisha, Lakini zaidi sana KUMWOMBEA kwa Mungu usiku na mchana akue kiroho.
Tukiiga mfano wa Epafra jinsi alivyokuwa akiwaombea sana watu wa kolosai walioamini kwa injili yao.
Wakolosai 4:12 Epafra, aliye mtu wa kwenu, mtumwa wa Yesu Kristo, awasalimu, akifanya bidii siku zote kwa ajili yenu katika maombi yake, ili kwamba msimame wakamilifu na kuthibitika sana katika mapenzi yote ya Mungu.
Umeona? Ukomavu wa watu walio wachanga wa kiroho hutegemea sana maombi ya kina kwa waliowazaa. Hivyo wewe kama mtenda kazi hakikisha unakuwa na maombi mengi kwa ajili ya wale uliowahubiria injili wakaokoka vinginevyo watakufa kiroho, katika ulimwengu huu wa njaa na kiu ya Neno la Mungu, tenga masaa kuwaombea. Na maombi hayo yawe ya rohoni kabisa, sio ya juu juu, bali ya kuzama, ili Mungu awakuze, na matokeo ya kazi yako utayaona tu baada ya kipindi fulani, jinsi watakavyozidi kubadilika na kukomaa kidogo kidogo, hatimaye kuwa watumishi imara katika shamba la Mungu.
Bwana akubariki.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.