Category Archive Home

ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.

Wengi tunafahamu habari za Yusufu, tunajua alikuwa ni mmoja wa watoto wa Yakobo aliyependwa sana na baba yake, Lakini baada ya kuota zile ndoto tu, ndugu zake walianza kumwonea wivu, na mwisho wa siku wakaamua kumuuza kama mtumwa kwa watu wa mataifa (Wamisri).

Na kama tunavyoisoma habari alipokuwa kule Misri Mungu alikuwa pamoja naye akamfanikisha katika mambo yote, akawa wa pili baada ya Farao mfalme wa Misri, kiasi cha kwamba hakuna mtu yoyote aliyeweza kufika kwa Farao bila kupitia kwanza kwake, Mali na vitu vyote vya Misri Farao alivikabidhisha kwa Yusufu,[Kumbuka Misri ndiyo iliyokuwa ngome yenye nguvu kuliko zote duniani kwa wakati ule], tunaweza kusema mfano leo hii taifa la Marekani lilivyo.

Lakini habari hii ya maisha ya Yusufu na yote aliyoyapitia imebeba siri na ujumbe mzito katika roho kwa kanisa,. Yusufu anafananishwa na Bwana wetu Yesu Kristo, na Farao anafananishwa na Baba yetu wa mbinguni. Wale wana 11 wa Yakobo wanafananishwa na wayahudi [yaani waisraeli], na Taifa la Misri Yusufu alipokimbilia linafananishwa na Kanisa la mataifa [wakristo], na Yule mke wa Yusufu (Asenathi) ambaye alimpata katikati ya wa-Misri kutoka katika jumba la kifalme la Farao, anafananishwa na BIBI-ARUSI safi wa Kristo.

Kama vile Yusufu alivyoonewa wivu na ndugu zake na kukataliwa, kisha kwenda kuuzwa utumwani, vivyo hivyo Bwana Yesu alipokuja duniani kwa ndugu zake wayahudi kama masihi wao waliyekuwa wanamtazamia kwa siku nyingi, walimwonea wivu, alipojishuhudia kuwa yeye ndiye mwana wa Mungu, wakamdharau hivyo wakamfanyia hila, wakamkataa kabisa na kumtia mikononi mwa warumi na kumuua [Huko ndiko kumuuza kwa watu wa Mataifa].

Na ndio maana ukisoma biblia utaona mtume Paulo anawaambia hivi wayahudi;

Matendo 13:46 “ Paulo na Barnaba wakanena kwa ushujaa wakasema, Ilikuwa lazima neno la Mungu linenwe kwenu kwanza [wayahudi]; lakini kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona nafsi zenu kuwa hamkustahili uzima wa milele, angalieni, twawageukia Mataifa.

47 Kwa sababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana, Nimekuweka uwe nuru ya Mataifa, Upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.

48 Mataifa waliposikia hayo wakafurahi, wakalitukuza neno la Bwana, nao waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini.

49 Neno la Bwana likaenea katika nchi ile yote”.

Unaona hapo walimkataa Kristo, ambaye alikuja kwa ajili yao..Bwana hakuwahi kujidhihirisha kwa mataifa hapo kabla, ile neema ilikuwa ni kwa wayahudi tu ndugu zake waliokuwa wakimtazamia kwa muda mrefu, Na ndio maana alisema katika Mathayo 15:24 “…. Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.” lakini kwa kuwa wao walimwonea wivu kama vile wale watoto wengine wa Yakobo walivyomwonea wivu ndugu yao Yusufu, basi ile neema ikaondoka kwao na kuja kwetu sisi watu wa mataifa [ambao katika habari hii tunaweza kusema wamisri],

Lakini jambo lingine pia la kuliangalia ambalo limejificha katika maisha ya Yusufu alipokuwa Misri, ni kwamba utaona watu wengi wa Misri hawakuwa na imani sana na Yusufu, kama alivyokuwa nayo Farao kwa Yusufu. Na ndio maana utaona, wakati wa kile kipindi cha miaka 7 ya neema, ni Yusufu peke yake aliyekuwa akifanya bidii kutimiza yale maono aliyoyaona juu ya njaa itakayokuja kuikumba karibia dunia nzima.

Kama wale watu wa Misri wangekwenda sambamba na Yusufu baadaye utaona baada ya njaa kuanza kuipiga dunia wasingekuwa nao pia wanatangatanga kwenda kuomba na kununua chakula kwa Yusufu, kwa kuwa ni raia wa nchi yao, Yusufu asingewauzia chakula, wala kubadilishana nao chakula kwa mali na mashamba yao..angewapa bure, au kuwauzia kwa gharama ambayo isingelazimu mpaka kutoa mali zao na vitu vyao.

Inaonyesha wazi kabisa wale watu, hawakuyasadiki maono ya Yusufu kwa kiwango kikubwa pindi alipowaambia wakusanye hazina kwa wakati wa ukame unaokuja huko mbeleni. Ni mfano dhahiri wa wingi wa wakristo waliopo leo ambao ni kweli walimpokea Masihi (yaani Kristo) kama Mwokozi wao, lakini wameyapuuzia yale aliyowaambia yatakayokuja kuipata dunia huko mbeleni pindi itakapopitia miaka ya njaa na ukame wa rohoni na wa mwilini ( yaani wakati wa ile dhiki kuu).

Mtu pekee ambaye hakuathirika na ile dhiki ya njaa ilipokuja duniani kote ni MKE WA YUSUFU tu peke yake kwasababu yeye alikuwa katika JUMBA LA KIFALME..Akizipeleleza zile siri za ndani kabisa zilizokuwa katika moyo wa Yusufu..na kama ukichunguza vizuri utaona yule mke Yusufu hakumtwaa ovyo ovyo tu mahali popote hapana, bali alipewa na Farao mwenyewe.. Ni mfano halisi wa BIBI-ARUSI wa KRISTO, wateule wa Mungu, ambao ni Mungu pekee yake ndio anayempa KRISTO.

Kumbuka ndugu, katikati ya wanaojiita wakristo yapo makundi mawili, yupo BIBI-ARUSI wa Kristo yaani MKE wa Bwana Yesu, na wapo Masuria, hawa wanafananishwa na wanawali werevu na wanawali wapumbavu.(Mathayo 25). Katika siku za mwisho makundi yote mawili yatakuwepo, na litakalokwenda kwenye unyakuo ni lile tu la wanawali werevu yaani BIBI-ARUSI wa Kristo.

Sasa kama vile Yusufu alivyokuwa ni mkuu wa Wamisri wote (yaani watu wa mataifa), waliomwendea na kumwomba chakula wakati wa dhiki, ambapo kwa wakati huo mke wa Yusufu alikuwa anakula raha katika jumba la kifalme.

kadhalika na katika siku za taabu za ile dhiki kuu ya mwisho, wapo wakristo vuguvugu ambao wao wasingepaswa kupitia dhiki, lakini wataipitia kwa upumbavu wao, wakati wenzao (wale BIBI-ARUSI wa Kristo) wapo mbinguni kwa Baba kwenye enzi ya kifalme katika karamu ya mwana-kondoo.

Na kama vile dalili ya kipindi cha dhiki kuanza ni kuona ndugu zake Yusufu wanaanza kwenda kutafuta chakula Misri pamoja na wamisri wenyewe kuanza kutangatanga huku na kule kutafuta chakula, Vivyo hivyo Na katika kipindi hichi tunachoishi sasa, Njaa ya kulisikia Neno la kweli inaongezeka.

Wayahudi kwa miaka mingi wamekuwa wakimtazamia masihi wao aje kuwakomboa, lakini hawaoni chochote kwa kipindi chote hicho, lakini nyakati hizi kidogo kidogo, tunaona wanaanza kujua makosa yao, kwamba hakuna Masia mwingine atakayekuja, wanaanza kutambua kuwa kuna chakula Misri yaani kwa Wakristo, wanaanza kuona mbona Yule waliyemkataa ndiye amekuwa TEGEMEO LA DUNIA NZIMA?.

Ndugu yangu siku ile watakapotubu tu!, basi ujue kile kipindi cha DHIKI KUU kimeshaanza, na neema haitakuwepo tena kwa watu wa mataifa, kama ndugu zake Yusufu walivyomlilia ndivyo itakavyokuwa kwa wayahudi kwa wakati huo, waisraeli watafumbuliwa macho kikabisa kabisa na kumtambua Yesu Kristo, biblia inasema watamwombolezea yeye waliyemchoma…

Zekaria 12: 10 “Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao WATAMTAZAMA YEYE AMBAYE WALIMCHOMA; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza.

11 Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika bonde la Megido”

Sasa baada ya hapo itakuwa imebaki miaka michache tu mpaka ile miaka 7 ya mwisho iishe, na baada ya hiyo dunia itakuwa imeisha, wakati huo duniani kutakuwa na dhiki isiyokuwa ya kawaida, huo ndio wakati watu wote watakapojua kuwa YESU KRISTO NDIYE JIWE KUU LA PEMBENI LILE LILILOKATALIWA NA WAASHI, Watu wa ulimwengu wote watajua kuwa ufalme na mamlaka yote ya mbinguni na duniani amekabidhiwa YESU KRISTO, na Hakuna WOKOVU NA UZIMA nje ya yeye. Kama vile watu wa kipindi cha Yusufu walivyofahamu kuwa malmlaka yote na ufalme amekabidhiwa Yusufu.

Unaweza ukaona ni wakati gani tunaishi, Taifa la Israeli linazidi kunyanyuka, hivi karibuni waisraeli watafumbuliwa macho yao na kumtambua Yesu Kristo, je! Wewe ni miongoni mwa Bibi-arusi atakayeenda kwenye unyakuo siku ile kabla ya DHIKI KUU KUANZA? Unamchukulia Bwana Yesu Kristo kwako kama nani?, je! Unamchukulia kama ni mtu wa kawaida tu, au mfalme?, kumbuka Yusufu alivyokuwa gerezani sio sawa na alivyofanywa mfalme, na vivyo hivyo Bwana Yesu Kristo, alivyokuwa pale msalabani kalvari sio sawa na alivyo sasa, Biblia inasema ameketi katika NURU ISIYOWEZA KUKARIBIWA, na maneno yake ni kweli na uzima..

Hivyo kama hujaingizwa katika ile familia ya kifalme, hautaweza kuikwepa dhiki, kama hujazaliwa mara ya pili kwa maji na kwa Roho, hautaweza kuuingia katika karamu ya mwana kondoo kule mbinguni, kwanini ukose hayo yote?? Jitahidi kufanya hivyo sasa kabla mlango haujafungwa. Tubu leo mgeukie Bwana azioshe dhambi zako, naye atakupa neema ya kuwa miongoni mwa Bibi-arusi wake. UNYAKUO NI SIKU YOYOTE.

Ubarikiwe!

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine.


Print this post

JE! NYWELE ZAKO ZINAOTA AU ZIMESIMAMA?

Mambo yote yaliyoandikwa katika agano la kale ni kivuli cha mambo yanayoendelea katika roho katika agano jipya tulilopo sasa. Kwamfano kama vile tunavyoweza kusoma Mungu alivyowaita wana wa Israeli kutoka Misri, kuelekea Kaanani kupitia jangwani, ndio hivyo hivyo Mungu anavyowaita watoto wake leo kutoka katika utumwa wa dhambi [Misri], kisha anawavusha katika bahari ya shamu [ambao ndio ubatizo 1Wakorintho 10], na baada ya hapo safari ya jangwani inaanza ambayo hiyo ni lazima kila mkristo aipitie, mahali ambapo atafundishwa kumcha Mungu, na kumtegemea yeye kwa kila kitu, mahali ambapo Mungu ataruhusu ajaribiwe kwa kila kitu lakini hataachwa. Na hatua ya mwisho ni Kuingia Kaanani, Ambayo nayo inaanzia hapa hapa duniani kisha kumalizikia kwenye nchi mpya na mbingu mpya..

Kadhalika tunajifunza pia jambo lingine katika habari ya Samsoni, ambayo nayo ni kivuli cha mambo yanayoendelea sasa hivi katika roho. Tunasoma Samsoni Mungu alimtia mafuta tangu alipokuwa tumboni mwa mama yake, akifananishwa na kanisa la Kristo jinsi lilivyoanza pale Pentekoste lilikuwa takatifu na safi lisilokuwa na waa lolote, Tunasoma pia Samsoni aliamuriwa na Mungu asikate nywele zake bali azifunge katika vishungi saba, Picha halisi ya kanisa la Kristo ambalo tunaona katika kitabu cha Ufunuo sura ya 2 &3 Bwana Yesu akitoa ujumbe kwa yale makanisa 7, Kumbuka kanisa la Kristo limekuwa likipita katika vipindi 7 tofauti tofauti vinavyojulikana kama NYAKATI 7 ZA KANISA kwa muda wa miaka 2000 sasa, na katika majira tunayoishi ni majira ya kanisa la mwisho la 7 linaloitwa LAODIKIA.

Kama vile Samsoni nguvu zake zilivyokuwa katika zile nywele, hivyo kanisa nalo katika nyakati zote saba limekuwa likitegemea nguvu zake katika NENO LA MUNGU ili likae. Lakini kwa habari mbaya tunasoma Samsoni alionyesha tabia za uasherati za kwenda kuzini na wanawake makahaba na wanawake wasio wa uzao wa Ibrahimu, na ndio hao baadaye waliokuja kujua siri ya nguvu zake, biblia inasema katika Mithali 31: 3 “Usiwape wanawake nguvu zako;”

Lakini Samsoni yeye hakufanya hivyo, badala yake alikubali kulaghaiwa na wale wanawake wasiomjua hata Mungu wa Israeli, wanawake wa kidunia, matokeo yake akaangukia katika mikono ya maadui zake wafilisti kwa muda mrefu, tunasoma;

Waamuzi 16: 15 “Mwanamke akamwambia, Wawezaje kusema, Nakupenda; na moyo wako haupo pamoja nami? Umenidhihaki mara hizi tatu, wala hukuniambia asili ya nguvu zako nyingi.

16 Ikawa, kwa vile alivyomsumbua kwa maneno yake kila siku, na kumwudhi, roho yake ikadhikika hata kufa.

17 Ndipo alipomwambia yote yaliyokuwa moyoni mwake, akamwambia, Wembe haukupita juu ya kichwa changu kamwe; maana mimi nimekuwa Mnadhiri wa Mungu, tangu tumboni mwa mama yangu; nikinyolewa, ndipo nguvu zangu zitanitoka, nami nitakuwa dhaifu, nitakuwa kama wanadamu wenzangu.

18 Delila alipoona ya kuwa amemwambia yote yaliyokuwa moyoni mwake, akatuma mtu akawaita wakuu wa Wafilisti, akisema, Njoni huku mara hii tu, maana ameniambia yote aliyo nayo moyoni mwake. Ndipo wakuu wa Wafilisti wakamwendea wakachukua ile fedha mikononi mwao.

19 Naye akamlaza usingizi magotini pake. Kisha akamwita mtu akavinyoa vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake; akaanza kumsumbua, nguvu zake zikamtoka.

20 Kisha akasema, Samsoni, Wafilisti wanakujia. Akaamka katika usingizi wake, akasema, Nitakwenda nje kama siku nyingine, na kujinyosha. Lakini hakujua ya kuwa Bwana amemwacha.

21 Wafilisti wakamkamata, wakamng’oa macho; wakatelemka naye mpaka Gaza, wakamfunga kwa vifungo vya shaba; naye alikuwa akisaga ngano katika gereza.

Unaona hapo?. Ndio jambo hilo hilo lililikuta kanisa la Kristo mara baada ya mitume kuondoka, Paulo aliandika hivi…

Matendo 20: 29 “Najua mimi ya kuwa baada ya kuondoka kwangu mbwa-mwitu wakali wataingia kwenu, wasilihurumie kundi;

30 tena katika ninyi wenyewe watainuka watu wakisema mapotovu, wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao.”

Hivyo katika agano jipya Delila anafananishwa na kanisa kahaba na hili kanisa si lingine zaidi ya kanisa Katoliki, ambalo lilianza kwa kuanza kupenyesha mafundisho potofu ya uongo ndani ya kanisa la Mungu, na hatimaye kufanikiwa kutengeneza dini kabisa, mnamo mwaka 325 WK katika Baraza la Nikea, lilifanikiwa kuyachanganya mafundisho ya kikristo na ibada za kipagani za kirumi, huko ndiko kulikozuka ibada za miungu mingi, ibada za sanamu, kusali rozari, kuomba kwa watakatifu waliokufa kale, mafundisho ya kwenda toharani, kanisa kuongozwa na vyeo vya kibinadamu badala ya karama za Mungu, mambo ambayo hayapo katika maandiko wala hayakuonekana katika kanisa la kwanza.

Na kanisa hili lilipozidi kupata nguvu kwa kuwashawishi watu na kuwadanganya kidogo kidogo nguvu za Roho Mtakatifu zikaanza kupungua katika Kanisa, na hatimaye kupoa kabisa isipokuwa kwa kikundi kidogo sana cha wateule, na kupelekea kanisa kupitia katika kipindi kirefu cha giza kwa zaidi ya miaka 1000, ni kipindi kinachojulikana katika historia kama KIPINDI CHA GIZA.

Katika siku ile kwenye hilo baraza la Nikea ndio siku hiyo huyu mwanamke kahaba [Kanisa Katoliki] anayefananishwa na Delila alifanikiwa kuzinyoa nywele za kanisa la Mungu kabisa, hivyo nguvu za kanisa zilipoa kwa muda mrefu sana, kukawa hakuna tena karama za rohoni, biblia ikazuiliwa kusomwa kwa washirika, zile nguvu za watu kumwamini Kristo zilizoanza pale Pentekoste zikafa, watu waliojaribu kushikilia mafundisho ya mitume waliuliwa, mafundisho ya watu kuhesabiwa haki kwa Imani katika Yesu Kristo yakafa badala yake watu wakawa wanafundishwa kuhesabiwa haki kwa kuwa mshirika wa kanisa Katoliki, utozwaji wa pesa wa vitu vinavyoitwa vya ki-Mungu ukaanza, kwamfano mtu akitaka kuombewa ni lazima atoe kiwango Fulani cha fedha kwa kasisi ili ahudumiwe, mtu akitaka kuwekewa wakfu mtoto wake au mali zake mbele za Mungu, sharti kwanza atoe kitu Fulani, na asipofanya hivyo basi hatapata huduma yoyote, mambo ambayo hayakuwepo katika kanisa la kwanza..n.k.

Lakini kama tunavyosoma baada ya Samsoni kutumika muda mrefu kusaga ngano katika magereza ya Wafilisti tunaona nywele zake zilianza kuota tena pasipo wao kujua. Na zilipomalizika kuota, madhara aliyoyaleta mwisho yalikuwa ni makubwa kuliko yale aliyoyafanya kule mwanzoni kama tunavyosoma..

Waamuzi 16: 22 “Lakini zile nywele za kichwa chake zikaanza kukua tena baada ya kunyolewa kwake.

23 Kisha wakuu wa Wafilisti wakakusanyika ili kumtolea sadaka Dagoni mungu wao, na kufurahi; maana walisema, Mungu wetu amemtia Samsoni adui wetu mikononi mwetu.

24 Na hao watu walipomwona wakamhimidi mungu wao, maana walisema, Mungu wetu amemtia mikononi mwetu huyu adui wetu, aliyeiharibu nchi yetu na kuwaua watu wengi miongoni mwetu.

25 Ikawa mioyo yao iliposhangilia, wakasema, Mwiteni Samsoni, ili atufanyie michezo. Basi wakamwita Samsoni atoke gerezani, akacheze mbele yao wakamweka katikati ya nguzo mbili.

26 Samsoni akamwambia yule kijana aliyemshika mkono, Niache nizipapase nguzo ambazo nyumba hii inazikalia, nipate kuzitegemea.

27 Basi nyumba ile ilikuwa imejaa watu waume kwa wake; na wakuu wote wa Wafilisti walikuwamo humo, na juu ya dari palikuwa na watu elfu tatu waume kwa wake waliokuwa wakitazama, wakati Samsoni alipocheza.

28 Samsoni akamwita Bwana, akasema, Ee Bwana MUNGU, unikumbuke, nakuomba, ukanitie nguvu, nakuomba, mara hii tu, Ee Mungu, ili nipate kujilipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili.

29 Kisha Samsoni akazishika nguzo mbili za katikati ambazo nyumba ile ilikaa juu yake, akazitegemea, moja kwa mkono wake wa kuume na moja kwa mkono wake wa kushoto.

30 Samsoni akasema; Na nife pamoja na hawa Wafilisti. Akainama kwa nguvu zake zote; ile nyumba ikawaangukia hao wakuu, na watu wote waliokuwa ndani yake. BASI WALE WATU ALIOWAUA WAKATI WA KUFA KWAKE WALIKUWA WENGI KULIKO WALE ALIOWAUA WAKATI WA UHAI WAKE”.

Kadhalika na katika kanisa jambo ni lile lile ulipofika wakati nywele za Kanisa kuanza kuota tena, [na kuota kwenyewe ni kurudi kwenye NENO kwenye mafundisho ya mitume]..Ndipo hapo Bwana akaanza kuwanyanyua watu wa kulitengeneza kanisa akawanyanyua wakina Martin Luther, mjumbe wa kanisa la tano, katika karne ya 16 akifundisha mafundisho ya kuhesabiwa haki kwa Imani katika Kristo Yesu, na sio katika dini ya kikatoliki, Bwana akawanyanyua wakina John Wesley na wenzake, katika karne ya 18 wakifundisha utakaso wa damu ya Yesu, kwamba Kristo amekuja ili umfanye mtu kuwa mtakatifu kwamba pasipo huo hakuna mtu atakayemwona Mungu, (Waebrania 12:14) na sio kwamba pasipo ushirika wa kanisa watu hawatamwona Mungu…

Vile vile katika kipindi cha kanisa la mwisho la Laodikia ambalo lilianza mwanzoni mwa karne ya 20 mpaka sasa, Bwana aliwanyanyua wakina William Seymor na wengine katika uamsho wa mtaa wa Azusa kule Marekani , na mafundisho ya Ubatizo wa Roho Mtakatifu, ya kwamba Roho Mtakatifu ndio MUHURI WA MUNGU (Waefeso 4:30). Na wote wasiokuwa na Roho wa Mungu hao sio wake (Warumi 8:9), Na ndio maana inajulikana kuwa tunaishi katika nyakati ya KI-Pentekoste kama ilivyokuwa kule mwanzo, na ndio maana katika nyakati hii zile karama zilizokuwa zimeuliwa na Kanisa Katoliki Bwana alianza kuzirejesha tena kuanzia mwanzoni mwa karne ya 20..(Yaani kuanzia mwaka 1900 na kuendelea)

Lakini haya yote ni kwa ajili ya kumwandaa BIBI-ARUSI wa kweli wa KRISTO kwa ajili ya unyakuo uliokuwa karibu kutokea. Zile nywele zimeshafikia ukomo, ni jambo moja tu linasubiriwa, Uamsho wa mwisho wa BIBI-ARUSI kupitia ufunuo wa zile ngurumo 7 kama tunavyosoma katika ufunuo 10:14, Ambazo hizo zitampa Bibi-arusi imani timilifu (Luka 18:8) ya kwenda katika unyakuo, ni uamsho wa kipekee, nao utakuwa ni wa muda mfupi sana utakaokuwa wa nguvu na wa ajabu kuliko hata ule uamsho wa kwanza uliotokea kule Pentekoste kama vile Samsoni baada ya nywele zake kukua tena, maangamizi aliyoyaletea mwishoni yalikuwa ni makubwa kuliko hata yale ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa Bibi-arusi wa Kristo katika hichi kipindi cha kukaribia na unyakuo.

Na wewe je! Ni miongoni mwa watu ambao nywele zao zimekuwa?? Au bado tu unatumikia katika dini na madhehebu? Kumbuka kuota nywele maana yake ni kurudi katika Neno, nguvu za mkristo yoyote Yule hazipo nje ya Neno la Mungu..Biblia inasema usiabudu sanamu, wala usijifanyie sanamu ya kuchonga, lakini kanisa lako linasema ni sawa kufanya hivyo..hapo unapaswa ufuate kile Neno linasema na uweke chini kile kanisa linasema.

Biblia inasema aaminiye na kubatizwa ataokoka, [na maana ya kubatizwa ni kuzamishwa kwenye maji mengi], lakini kanisa linasema haijalishi, linasema ubatizo wa kunyunyiziwa ni sawa..Hapo unapaswa uweke chini mapokeo ya kanisa na kuchukue kile mitume walichokifanya kwenye biblia…

Matendo 2: 37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.”

Hivyo ndugu hizi ni siku za mwisho, huu ni wakati wa kuhakikisha nywele zako zinakuwa, tafuta uhusiano wako binafsi na Mungu, Rudi kwenye Neno la Mungu, dini na madhehebu hayatakufikisha popote, kumbuka watakaokwenda kwenye unyakuo ni wachache biblia inasema hivyo..Je! umezaliwa mara ya pili? Kwa kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu.?Mungu akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali “share” kwa wengine ujumbe huu.


Mada Nyinginezo:

UTENDAJI KAZI WA MPINGA-KRISTO.

SIKU YA HASIRA YA BWANA.

SIRI YA MUNGU.

MKUU WA GIZA

NI HALALI KUBATIZA WATOTO WADOGO?

KUNA HUKUMU ZA AINA NGAPI?


Rudi Nyumbani

Print this post

UNAFANYA NINI HAPO?

1Wafalme 19: 9 Akafika kunako pango, akalala ndani yake. Na tazama Neno la BWANA likamjia, naye akamwambia, UNAFANYA NINI HAPA ELIYA?.

10 Akasema nimeona wivu mwingi kwa ajili ya BWANA Mungu wa majeshi ; Kwa kuwa wana wa Israeli wameyaacha maagano yako, na kuzivunja madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga; nami nimesalia mimi peke yangu; nao wanitafuta roho yangu, waiondoe.

11 Akasema, toka, usimame mlimani mbele za BWANA. Na tazama BWANA akapita; upepo mwingi wa nguvu ukaipasua milima, ukaivunjavunja miamba mbele za BWANA; Lakini BWANA hakuwamo katika upepo ule; Na baada ya upepo tetemeko la nchi; lakini BWANA hakuwamo katika lile tetemeko la nchi;

12 Na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto; Lakini BWANA hakuwamo katika moto ule; Na baada ya moto sauti ndogo ya utulivu.

13 Ikawa Eliya alipoisikia, alijifunika uso wake katika mavazi yake, akatoka, akasimama mlangoni mwa pango. Na tazama sauti ikamjia, Kusema, UNAFANYA NINI HAPA, ELIYA ?.

Tukirudi nyuma kidogo katika habari hii, tunasoma kabla ya Eliya kukimbilia mlima Horebu alienda kuwaua wale manabii wa Baali , baada ya kuona Israeli yote imekengeuka kwa kuigeukia miungu migeni, lakini pamoja na kuwaua hao, akapata taarifa nyingine kuwa malkia, [mke wa mfalme Ahabu aliyeitwa Yezebeli] anataka kumwangamiza yeye naye kama alivyowaua manabii wa baali, Kumbuka Yezebeli alikuwa ni mkatili sana alifanikiwa kuwaangamiza manabii wengi wa Mungu waliokuwa Israeli kwa wakati ule, na baadhi yao waliosalia walikuwa wanaishi kwa kujifichaficha mapangoni siku zote za maisha yao.

Hivyo njia pekee Eliya aliyoiona ya kupata suluhisho la mambo yote ni kukimbilia katika mlima wa Mungu uliokuwa mbali sana na Israeli, [Ni ule ule mlima ambao Mungu alisema na wana wa Israeli hapo kwanza] akae huko ajitete mbele za Mungu. Na ndio ule ule Mlima Mungu aliomwitia Nabii Musa ampe yale maagizo na sheria kwa wana wa Israeli kwamba wayashike siku zote za maisha yao, Sasa mlima huo ulikuwa ukijulikana kama mlima mtakatifu wa Mungu kwa wakati ule, ndio unaoitwa mlima Sinai au mlima Horebu.

Hivyo Eliya kwa kufikiria kwake aliona ni vema amwendee Mungu, kama Musa alivyomwendea, kwa kufuata kanuni zile zile,..Na ndio maana tunaona Eliya alifunga siku 40 usiku na mchana bila kula wala kunywa chochote, jambo ambalo Musa alilifanya. Akijua kuwa kule Mungu atazungumza naye kama alivyozungumza na Musa, pengine ataitikisa dunia tena na kuikomboa Israeli kwa Ishara na mapigo makubwa kutoka kwa ile miungu ya kipagani [ma-baali] aliyoacha Israeli kama kipindi kile Bwana alivyofanya kule Misri..Alifika mpaka kilele cha mlima Sinai na kukaa kule, katika pango mojawapo, akingoja Bwana azungumze naye. Na ni kweli tunasoma Bwana alishuka na kuzungumza naye kama alivyozungumza na Musa.

Ndipo sauti ya Mungu isiyoambatana na chochote ikasema naye na kumuuliza, ELIYA UNAFANYA NINI HAPA?. Lakini Eliya hakuielewa kwasababu matarajio yake hayakuwa hayo!!, yeye alitazamia Mungu atazungumza naye kwa moto, na tufani na upepo wa kisulisuli kama alivyofanya kwa Musa mtumishi wake na kwa wana wa Israeli zamani zile kwenye mlima huo huo.. Lakini baada ya kitambo kidogo Bwana akamwambia Eliya toka usimame nje! Utazame uone,…

Ndipo Mungu akapita kwa UPEPO mwingi sana uliopasua miamba, na MATETEMEKO, na MOTO kama Eliya alivyotazamia, kwa mfano ule ule aliojidhihirisha kwa wana wa Israeli na kwa Musa..Lakini pamoja na ishara zote hizo na maajabu yote yale Eliya alipata ufahamu na kugundua kuwa kuna kitu hakipo sawa kwenye hizo ishara zote kadhalika na kwenye ule mlima …

Na ndipo Mungu akazungumza naye tena kwa mara ya pili kwa sauti ya utulivu na kumuuliza.. ELIYA UNAFANYA NINI HAPA?, Hapo ndipo alipogundua ile ilikuwa ni sauti ya Mungu inayosema naye, hivyo kwa aibu na kwa hofu akijifunika uso wake jambo ambalo hapo mwanzo hakufanya iliposema naye kwa maneno hayo hayo!!.. Alipogundua kuwa Mungu hayupo katika mlima Sinai uwakao moto, Mungu hayupo katika matetemeko, Mungu hayupo katika upepo wa kisulisuli na tufani, Mungu hayupo katika nguzo ya moto, Mungu hayupo katika Wingu, Mungu hayupo katikati ya kijiti kinachowaka moto, Mungu hayupo katika mvua ya mawe..Alitambua kuwa Mungu yupo katika SAUTI NDOGO YA UTULIVU, Kwamba hata ishara zile wana wa Israeli Mungu alizokuwa anawaonyesha kule jangwani hazikuwa uthibitisho wa kuwa Mungu alikuwa katikati yao, Mungu alizutumia zile kama ishara tu, ili wamwamini atakapotaka kuzungumza nao wamsikie.. Eliya aliligundua hilo. Zile SHERIA Mungu alizompa Musa ndio iliyokuwa SAUTI NDOGO YA UTULIVU iliyokuwa inasema mioyoni mwao, > usiabudu miungu mingine, waheshimu baba yako na mama yako, usiue, usiibe, n.k..

Hivyo mtu yeyote ambaye angezitii zile sheria hata asingeona ishara yoyote ile, Mungu angekuwa katikati yake, angekuwa ameisikia sauti ndogo ya Mungu ya utulivu..Lakini wengi wao waliona upepo, na matetemeko, na moto, na bahari kugawanyika, na miamba kutoa maji, lakini hawakuitambua sauti ya Mungu iliyokuwa inazungumza nao katikati yao, walidhani kuwa ile zile ishara ndio utimilifu wa wote wa Mungu, mwisho wa siku wengi wakaangamia jangwani.

Kadhalika na katika wakati wetu huu wa agano jipya Kanisa lilipoanza tunasoma katika ile siku ya Pentekoste [Ambao ndio mlima Sinai wetu], Mungu alishusha vipawa na ishara nyingi katikati ya wateule wake, Bwana alishuka na UPEPO wa KISULISULI kama ulivyowashukia wana wa Israeli kule jangwani na Eliya, Soma;

Matendo 2: 1 Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja.

2 Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa UPEPO wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi.

3 Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama NDIMI ZA MOTO uliowakalia kila mmoja wao.

4 Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.

Unaona hapo? siku ile ya Pentekoste, Moto ulishuka kama ndimi za moto ukakaa juu ya watu, karama tofauti tofauti zikaanza kujionyesha katikati ya watu, wakaanza kunena kwa Lugha mpya, watu wakaanza kutabiri, miujiza na ishara zisizokuwa za kawaida zikafanyika katikati ya watakatifu, nchi ikatikiswa kwa matetemeko ya nguvu za Roho wa Mungu (Soma Matendo 4:23-31)…Lakini Mungu hakuwepo katikati ya hivyo vitu vyote, Mungu aliviruhusu viwepo kama ishara tu ya watu kuwa tayari kumsikia ni kati gani anataka kusema katikati yao. 

Hivyo lile kundi dogo lililokuwa limekusudiwa kumwona Mungu baada ya zile ishara, na maajabu liliisikia ile sauti ndogo ya utulivu na ndio maana tunaona katika ile siku tu ya kwanza ya Pentekoste watu walipokuwa wanazistaajabia zile ishara kuona watu wanashukiwa na ndimi za moto, na kuzungumza katika lugha nyingine mbali mbali ndipo wale watu wakamwambia Petro na mitume wengine, sasa tutendeje ndugu zetu?…Ndipo Petro akawajibu,

Matendo 2: 37 Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia TUBUNI, MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, NANYI MTAPOKEA KIPAWA CHA ROHO MTAKATIFU.

Unaona hapo, wale watu hawakumwambia Petro moto huu ni wa ajabu, upepo huu ni wa kipekee,Hakika Mungu kaonekana, Mungu kajifunua, Mungu ni mwema, leo katutembelea haleluya hapana.! Bali wao moja kwa moja walimuuliza Petro na mitume wenzake, TUTENDEJE NDUGU ZETU?.. Na ndipo ile sauti ndogo ya Mungu ya utulivu ikawaambia “TUBUNI” maana yake ni Geukeni mwache njia zenu mbaya .. Kama tu vile ile sauti ndogo ya utulivu ilivyomwambia Eliya kule mlima, UNAFANYA NINI HAPA ELIYA? “RUDI” KATIKA NJIA YA JANGWA, [maana ya kurudi ni kugeuka urudi ulikotoka].

Lakini katika hichi kipindi cha siku za mwisho, kile ambacho Bwana Yesu alisema katika

Mathayo 7:22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?.

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.” …Kimeshindwa kuisikia sauti ya Mungu inayonena katika utulivu badala yake kimeng’ang’ana na yale madhihirisho ya Roho kwamba ndio uthibitisho kuwa Mungu yupo katikati yao.

Ndugu yangu, ikiwa leo hii utadhani Mungu yupo katika karama yoyote uliyonayo, ukidhani kuwa kunena kwa lugha ndio uthibitisho kwamba umepokea kweli ubatizo wa Roho Mtakatifu, au kufanya miujiza, au kutoa pepo, ndio uthibitisho kwamba Mungu yupo na wewe, huku umeiweka kando ile sauti ya Mungu inayozungumza na wewe kwa utulivu na upole inayokuambia UACHE DHAMBI, NA UTUBU, UKABATIZWE KATIKA UBATIZO SAHIHI, wa jina la YESU KRISTO, Hutaki kuisikia, basi fahamu kuwa utakuwa umepotea bila hata wewe mwenyewe kujijua. 

Kama Leo hii hutaka kusikia Neno la Mungu, habari za TOBA na UTAKATIFU kwako hazina maana sana, wewe unachokifuata kanisani ni Upepo wa kisulisuli, na matetemeko na hisia za kiroho pamoja na moto wa Roho Mtakatifu na miujiza na uponyaji, ni kweli hivyo vinapaswa viwepo kanisani, na ni lazima kanisa liambatane navyo, lakini ile sauti ya Mungu iliyosema na Eliya hapo mwanzo bado itaendelea kusema na wewe ndani yako siku zote, UNAFANYA NINI HAPA? UNAFANYA NINI KATIKA DHAMBI??

Ni kitu gani unachokwenda kukitafuta katika nyumba ya Mungu, ni miujiza tu,? ni ishara? Ni uponyaji? Ni kufunguliwa biashara yako?, ni kuombewa upate mtoto?, ni Kufunguliwa upate mume/mke?, ni kuombewa tu ufaulu shuleni?.

Ndugu kama ni mojawapo ya hayo ndio yanayokupeleka huko ukidhani kuwa Mungu kukufanikisha katika hivyo ndio uthibitisho kwamba yupo na wewe, basi hujaisikia bado sauti ya Mungu, yeye alisema wazi kabisa,“mtu asipozaliwa mara ya pili hawezi kuuona ufalme wa mbinguni Yohana 3:3” na kuzaliwa mara ya pili ni KUTUBU (KUGEUKA) kwa kumaanisha kuacha maisha uliyokuwa unaishi ya kale, ya ulevi, uasherati, usengenyaji, ushirikina, kutokusamehe, ya chuki, ya wivu, ya ugomvi, ya utukanaji,maisha ya anasa, maisha ya uvaaji vimini, na suruali, maisha ya upakaji wanja na lipstiki na uvaaji mawigi na hereni, maisha ya ibada za sanamu na uvuguvugu.

Na baada ya kugeuka, hatua inayofuata ni kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa Jina la Yesu Kristo, ili hatia ya dhambi zako iondolewe mbele za Mungu na kisha Bwana mwenyewe atakupa uwezo wa kushinda dhambi kwa kupitia Roho wake Mtakatifu katika wakati uliobakia wa maisha yako.

Ndugu sauti ndogo leo ya utulivu inazungumza nawe kupitia maandiko kwamba hakuna mtu atakayemwona Mungu asipokuwa na huo UTAKATIFU, (waebrania 12:14.). Isikie sauti ya Mungu sasa inayosema katika kanisa lake na sio ishara, miujiza, maono, ndoto, uponyaji, n.k…Ukivifuata hivyo kanisani, bado ile sauti itakuuliza FULANI UNAFANYA NINI HAPA?..mimi sipo huko, nipo katika sauti ndogo ya utulivu..

Na kama ni ya utulivu basi ni rahisi kuidharau. Ni maombi yangu ndugu yangu sisi sote tusiiache itupite, Bwana atupe masikio ya kuisikia inaposema nasi katika Neno lake na sio katika miujiza. Hizi ni siku za mwisho tuwe macho.

Mungu akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali “share” kwa wengine ujumbe huu.


Print this post

UMETEKWA NA UPENDO WA KRISTO?

Ni rahisi kudhania kuwa mtu akizaliwa mara ya pili, basi anakuwa anampenda sana Mungu kiasi kwamba kukitokea kitu mfano shida, au tabu,au magonjwa, au dhiki na kadhalika anakuwa yupo tayari kupambana nacho ili asimwache Mungu wake au asimkane Kristo,..yaani kwa jinsi anavyompenda Bwana hataweza kuruhusu tabu zimtenge na yeye kama tunavyosoma ilivyoandikwa katika maandiko haya;

Warumi 8: 31 “Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu?

32 Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye?

33 Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki.

34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea.

35 NI NANI ATAKAYETUTENGA NA UPENDO WA KRISTO? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?

36 Kama ilivyoandikwa, ya kwamba, Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa, Tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa kuchinjwa.

37 Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.

38 Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo,

39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote HAKITAWEZA KUTUTENGA NA UPENDO WA MUNGU ULIO KATIKA KRISTO YESU BWANA WETU.”

Je! Ni kweli hiyo ndiyo maana halisi ya hiyo mistari hapo juu kwamba sisi tunao uwezo wa kupambana na dhiki, tabu, na mateso kwasababu ya upendo wetu mwingi kwa Kristo?. Jibu ni hapana, hakuna mwanadamu yeyote mwenye upendo wa kiwango hicho, ni muhimu kufahamu maana ya huo mstari hapo juu, Biblia inasema JE! NI NANI ATAKAYETUTENGA NA UPENDO WA KRISTO?..Unaona hapo, inasema ni UPENDO WA KRISTO na sio UPENDO WETU SISI KWA KRISTO.

Kuna tofuati kati ya upendo wetu sisi kwa Kristo, na upendo wa Kristo kwetu sisi.

Mtu anapozaliwa mara ya pili kweli kweli [Tutakuja kuona huko mbeleni mtu anazaliwaje mara ya pili], Kuanzia huo wakati na kuendelea ule Upendo wa Kristo unaingia ndani yake, huo sio upendo wake[huyo mtu] kwa Kristo, hapana! bali Upendo wa Kristo kwake. Hivyo Bwana Yesu ndiye anayekuwa anachukua jukumu lote la kuhakikisha ule upendo wake kwako unadumu milele haupotei kwa namna yoyote ile.

Hivyo kuanzia huo wakati linapotokea jambo lolote juu yako mfano iwe ni dhiki, shida, njaa, hatari, adha, upanga n.k. Ni Yesu Kristo ndiye anayehakikisha wewe haujitengi na yeye, na sio wewe utakayehakikisha kwamba hujitengi na yeye. Watu wanaojaribu kufanya hivyo, kwa kujizuia kwa akili zao kutokujitenga na Kristo hawafiki mbali, wanajikuta wanaanguka na watu wa namna hiyo huwa bado hajazaliwa mara ya pili.

Mtume Paulo anasema, …

“38 Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo,

39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote HAKITAWEZA KUTUTENGA NA UPENDO WA MUNGU ULIO KATIKA KRISTO YESU BWANA WETU.”

Hii ni faida kubwa sana kwa mtu aliyezaliwa kweli kweli mara ya pili, Unakuwa UMETEKWA na UPENDO WA YESU KRISTO mwenyewe, ndio hapo unakuta dhiki inapomjia mtu wa namna hiyo kwamfano, shetani anapomjaribu kwa misiba, badala ya yeye kufarijiwa yeye ndio anawafariji wengine, anapokuwa katika magonjwa ya kufisha, badala amkufuru Mungu yeye ndiye anaonekana mwenye tumaini kushinda hata mtu aliye na mzima, kama vile Ayubu, utashangaa mtu wa namna hiyo anapita katika hali ya kupungukiwa kupita kiasi na njaa lakini bado anafuraha na kumshukuru Mungu, mpaka watu wa nje wanamshangaa ni mtu wa namna gani, yupo katika hali kama hizi lakini bado anashikamana na Mungu wake,

Kadhalika utakuta mtu mwingine [tunawazungumzia waliozaliwa kweli kweli mara ya pili] ni tajiri, lakini hauangalii na kuutumainia utajiri wake kama ni kitu cha thamani sana katika maisha yake, mpaka watu wengine wa nje wanamshangaa wanasema tungekuwa na mali kama za kwako dunia nzima ingetujua, tungetembelea magari ya thamani, tungetia heshima, lakini mtu kama Ayubu pamoja na utajiri wake alisema maneno haya,

Ayubu 31: 25 “Kama nilifurahi kwa kuwa mali yangu yalikuwa mengi, Na kwa sababu mkono wangu umepata vitu vingi; ….

28 Hilo nalo lingekuwa uovu wa kuadhibiwa na waamuzi; Kwani ningemwambia uongo Mungu aliye juu. “

Unaona sasa uwezo wa namna hiyo, wa kuweza kuendana nayo na kushinda mambo yote hayo pasipo kumwacha Mungu, sio kwa jitihada za mtu binafsi kupambana na hizo hali, hilo haliwezekani kwa mtu yeyote Yule, hiyo ni YESU KRISTO mwenyewe ndio anafanya ndani ya mtu ili kuhakikisha kwamba hakupotezi wewe kipenzi chake, haungamii, hivyo tatizo linapokuja, kabla ya kukufikia wewe, linawasili kwanza kwake, kisha analipatia utatuzi, ndipo litakaposhuka kwako, na litakaposhuka linakuja na dawa madhubuti ya kulishinda, Uwezo wa kipekee unatoka kwa Mungu, na nguvu ya kushinda majaribu na mitikisiko yote..

Ndio hapo watu wa nje watakushangaa unawezaje kushinda hayo yote?, unawezaje kukaa katikati ya jamii ya wazinzi na wewe sio mmojawao?, unawezaje kuwa katika hali ya kutokuwa na pesa lakini bado unamtumikia Mungu, na unayo amani?, Unawezaje kuwa mgonjwa lakini unawaombea wengine, na hauna hofu ya kufa? Unawezaje kuwa na mali na usitamani anasa za ulimwengu huu, wala kiburi, unawezaje kuwa mzuri na bado huvai mavazi yasiyo na heshima n.k…Hawajui kwamba hayo yote hayatokani na upendo wako wewe kwa Mungu..hapana bali yanatokana na UPENDO wa KRISTO kwako .. Yeye ndiye anayefanya juu chini, wewe usipotee katika hizo njia mbovu na majaribu..kama biblia inavyosema:

Zaburi 125: 1 “Wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, wakaa milele.

2 Kama milima inavyouzunguka Yerusalemu, NDIVYO BWANA ANAVYOWAZUNGUKA WATU WAKE , TANGU SASA NA HATA MILELE. “

Sasa karama hii ya UPENDO WA MUNGU KWA MTU, haiji kwa watu wote wa ulimwenguni hapana! Bali inakujua kwa wale tu waliomtumainia yeye {yaani wale tu WALIOZALIWA MARA YA PILI}, wengine ambao hawajazaliwa mara ya pili hawataweza kushinda majaribu na misukosuko, yatakapotokea mawimbi wataanguka tu, zitakapotokea dhiki watakufuru, ikitokea misiba watalaani, hawana raha usiku na mchana, watajitahidi kwa nguvu zao kushinda dhambi na ulimwengu lakini hawataweza, hata wakipata utajiri utawaangamiza, hata wakiwa wagonjwa na maskini watataka kujaribu kuishikilia imani lakini watamkana Kristo, kwasababu hawajazaliwa mara ya pili.

Sasa Kuzaliwa mara ya pili kunakuja kwanza baada ya mtu kutubu dhambi zake, [kumbuka maana ya kutubu ni KUGEUKA], sio kuongozwa sala ya toba, unageuka kwa kudhamiria na kumaanisha kabisa kuacha dhambi zako, kuyaacha ya kale na kuanza maisha mapya kwa Kristo, na baada ya kutubu, bila kukawia hatua inayofuata ni kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji tele, na kwa JINA LA YESU KRISTO, (kulingana na Matendo 2:38), upate ondoleo la dhambi zako, na hatua ya tatu na ya mwisho ni Roho wa Kristo kuingia ndani yako, sasa hapo ndio lile PENDO LA KRISTO linamiminwa ndani yako. Mtu yeyote akiruka hatua yoyote kati ya hizo, bado hajazaliwa mara ya pili..Kumbuka ndugu hii sio dini wala dhehebu ni maagizo ya Bwana Yesu mwenyewe ambayo yapo kwenye biblia.

Biblia inasema wazi kabisa, katika Yohana 3: 5 “Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.”

Sasa kumbuka kuzaliwa kwa maji kunakozungumziwa hapo ndio UBATIZO WA MAJI, na kuzaliwa kwa Roho ndio UBATIZO WA ROHO MTAKATIFU. Hapo ndipo unakuwa umeshazaliwa mara ya pili. Lakini Wapo wengine wanataka kubatizwa lakini hawajadhamiria kuacha maisha yao ya kale ya dhambi, hao hata wakienda kubatizwa wanafanya kazi bure, hakuna chochote kitakachotokea katika maisha yao.. Kadhalika wapo wengine, wametubu lakini hawataki kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wanasema ubatizo wa maji hauna maana sana hawa nao pia hawataona mabadiliko yoyote katika maisha yao.. Maagizo yote aliyoyatoa Bwana Yesu hakuna hata moja lisilokuwa na maana, alisema aaminiye na kubatizwa atakoka, na sio aaminiye tu peke yake. Hapana bali vyote viwili vinakwenda pamoja.

Hivyo mtu akizingatia hizo hatua zote za yeye kuzaliwa mara ya pili utapokea UWEZO, wa kutokutenganishwa na chochote kile, iwe shida, dhiki, uzima, mauti, raha, malaika, mamlaka, utajiri, kupungukiwa, upanga, misiba, n.k. kwasababu lile PENDO LA YESU KRISTO tayari litakuwa limeshamiminwa ndani yake. Hivyo ANASHINDA siku zote na ZAIDI YA KUSHINDA.

Ubarikiwe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine na Mungu atakubariki.


Print this post

WAKATI WA JIONI KUTAKUWAKO NA NURU.

Zekaria 14: 6 “Tena itakuwa siku hiyo, ya kwamba nuru yake haitakuwa na mwangaza na kiwi;

7 lakini itakuwa siku moja, iliyojulikana na Bwana; si mchana, wala si usiku; lakini itakuwa, ya kwamba wakati wa jioni kutakuwako nuru”.

Jaribu kutengeneza picha mfano Inatokea siku moja, wakati wa jioni labda tuseme saa moja hivi muda ambao umezoea kila siku kuona jua likizama ghafla unashangaa kuona mwanga ni ule ule haufifii, tena inafikia saa mbili jioni jambo ni lile lile, kunamulika mwangaza kama wa saa 11 jioni hivi, ni wazi kuwa kwa namna ya kawaida utashangaa sana hiyo siku kimetokea nini?, mbona giza haliingii maana muda wa usiku umeshaanza na sasa ni saa 2 usiku lakini kunaonekana kama saa 11, kwa namna ya kawaida mtu yeyote atakayeliona jambo hilo atashtuka sana.

Kadhalika na katika roho pia Bwana alitabiri itakuja siku moja inayofanana na hiyo, kwamba wakati wa jioni kutakuwa na NURU. Lakini kwa hekima hatuna budi tufahamu huo wakati ni wakati gani, je! Umeshatimia au bado?. Hivyo ili kufahamu ni lazima pia tujue Nuru ni nini na giza ni nini? Na huo wakati wa jioni ni upi?.

Kama tunavyojua nuru ya dunia inaletwa na jua, na hili jua huwa linaangaza katika majira matatu yaani asubuhi, mchana na jioni,..Kadhalika na katika roho Bwana Yesu alisema:

Yohana 8: 12 “…, MIMI NDIMI NURU YA ULIMWENGU, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima”.

Unaona hapo yeye katika roho ndio jua letu lililoanza kuangaza asubuhi, na likaja kuangaza mchana, kadhalika na litaangaza jioni. Kazi yake ni kutia nuru ulimwengu, alianza kutia nuru asubuhi (yaani kanisa la kwanza lilioanza na mitume), akaendelea kutia nuru mchana(yaani katika wakati way ale makanisa 5 yaliyofuata), na akamaliza kuangaza Nuru yake wakati wa jioni (katika kanisa lile mwisho la 7 linaloitwa Laodikia ambalo ndilo hili tunaloishi sasa ). Ufunuo 2 & 3

Na kanisa hili la Laodikia ni wazi kabisa na inajulikana na watu wote kwamba lilianza katika karne ya ishirini, yaani kuanzia mwaka 1906 na kuendelea.. Hivyo sisi wote tuliopo leo tunaishi katika ile NURU ya BWANA ya jioni, kumbuka hakutakuwa na kanisa lingine zaidi ya hili, ni kanisa ambalo litashuhudia kuja kwa pili kwa Kristo. Ilijulikana Katikati ya wakristo wote kuanzia huo wakati wa mwanzoni mwa karne ya karne ya 20 kwamba wao ni WANA WA JIONI, kwasababu walikuwa wanafahamu kabisa ni kweli wanaishi wakati wa jioni kabisa wa nuru ya Kristo kumalizikia.

Sasa katikati mwa karne ya ishirini yaani kipindi cha miaka ya 1940-1980, wakristo wote kutokana na matukio yaliyokuwa yanayaona yakitokea duniani, wakilinganisha na unabii wa kibiblia, walifahamu kuwa karne ile haitaisha bila Kristo kurudi mara ya pili, na ni kweli walikuwa sahihi, ukizingatia kwamba asilimia kubwa wa yale Bwana Yesu aliyoyazungumza katika Mathayo 24 yalitimia katika huo wakati, kwamfano, Bwana alisema.

Kutakuwa na matetemeko ya nchi mahali na mahali, kwa wakati ule yalikuwa ni mengi mno duniani, alisema pia kutakuwa na vita na matetesi ya vita, taifa litaondoka kwenda kupigana na taifa lingine…Jambo ambalo lilionekana wazi katikati ya ile karne ya 20, vita viwili vikubwa vya dunia vilitokea kwa mpigo, jambo ambalo halikuwahi kuonekana hapo kabla katika historia ya dunia, mamilioni ya watu kufa, magonjwa ya ajabu ndio yalianzia kuzuka katika hicho kipindi, kansa, ukimwi, kisukari, Malaria n.k. mambo ambayo Bwana aliyatabiri yatatokea katika siku za mwisho, na kikubwa zaidi kilichowafanya watakatifu wa karne ya ishirini kunyanyua vichwa vyao juu, kama Bwana alivyowaambia katika

Luka 21:28 “Basi mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia”

Ni kutokea kwa kitendo cha kihistoria katika nchi takatifu Israeli, pale waliposhuhudia taifa la Israeli likichipuka tena baada ya ma-karne ya miaka kupita bila kuwa taifa huru, walishuhudia kuona Israeli kupata uhuru wao tena mwaka 1948 na kuwaona wayahudi wakitoka katikati ya mataifa yote ulimwenguni na kurudi katika nchi yao tena.

Ezekieli 36: 24 “Maana nitawatwaa kati ya mataifa, nami nitawakusanya na kuwatoa katika nchi zote, na kuwarudisha katika nchi yenu wenyewe. “

Huko ndiko kuchipuka kwa mtini Bwana Yesu alikokuzungumzia,Maana Taifa la Israeli linafananishwa na MTINI kadhalika pia watakatifu walipokuwa wanaona na miti mingine ikichipuka (yaani mataifa mengine tofauti na Israeli kupata uhuru wao yaani mataifa ya Afrika, Asia na Marekani ya kusini),ambayo hayo yote yalianza kupata uhuru wao mara baada tu ya Israeli kutangazwa kuwa taifa huru, wakilinganisha na maandiko Bwana Yesu aliyoyasema katika..

Luka 21:29 “Akawaambia mfano; Utazameni MTINI na MITI MINGINE YOTE.

30 Wakati iishapo kuchipuka, mwaona na kutambua wenyewe ya kwamba majira ya mavuno yamekwisha kuwa karibu.

31 Nanyi kadhalika, mwonapo mambo hayo yanaanza kutokea, tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu u karibu.

32 Amin, nawaambieni, Kizazi hiki hakitapita hata hayo yote yatimie. ”

Hivyo walivyokuwa wanayaona hayo yote yanatimia, walitambua kabisa kwamba karne ya 21 haitafika (yaani miaka ya 2000 haitakuwepo), na walikuwa wapo sahihi kabisa, Sasa kilichotokea na cha kustaajabisha, ni kuona mpaka karne ya 21 inaanza na mwisho bado haujafika…

Na ndio hapo tunarudi kwenye lile andiko letu la msingi..

Zekaria 14: 6 “Tena itakuwa siku hiyo, ya kwamba nuru yake haitakuwa na mwangaza na kiwi;

7 LAKINI ITAKUWA SIKU MOJA, ILIYOJULIKANA NA BWANA; si mchana, wala si usiku; lakini itakuwa, YA KWAMBA WAKATI WA JIONI KUTAKUWA NURU”.

Huo wakati ambao Bwana alisema JIONI KUTAKUWA NA NURU, ndio huu tunaoishi sasa (wakati huu wa karne ya 21), Mambo yote yalipaswa yaishe tokea karne ya 20, lakini kwa jinsi Mungu alivyokuwa wa rehema na neema, hataki mtu yeyote apotee bali wote waifikilie toba, akalazimika kuisimamisha NURU ya ulimwengu isizame ( yaani Neema ya Yesu Kristo isiishe) katika hichi kipindi cha wakati wa jioni wa kumalizia..

Ndugu yangu mwisho ungepaswa uwe umeshafika siku nyingi, moja ya hizi siku mambo yote yatabadilika ghafla, kama vile jua linavyokaribia kuzama kidogo kidogo giza linaingia..ndivyo walivyoweza kutambua watu wa karne ya 20, lakini sisi tunaoishi katika Hii NURU ya nyiongeza (watu wa karne ya 21), tupo katika hatari kubwa sana kwasababu Nuru hii haitadumu kwa kipindi kirefu, kadhalika na haitabiriki, siku ya kuondoka kwake haitakuwa taratibu taratibu tena kama mwanzo, hapana, bali itaondoka kwa ghafla, na saa hiyo hiyo giza nene sana litaikumbuka dunia (huo ndio uharibifu wake)…

Ndio lile neno litatimia

1Wathesalonike 5: 1 “Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.

2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.

3 WAKATI WASEMAPO, KUNA AMANI, NA SALAMA, NDIPO UHARIBIFU UWAJIAPO KWA GHAFULA, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa. “

Watu wengi wametokea badala ya kumkaribia Mungu awape neema ndio kwanza wanaanza kudhihaki, wakisema hakuna kitu kama hicho kurudi kwa Yesu, Yesu harudi leo wala kesho, miaka na miaka mambo yapo vilevile hawajui kwamba wanaishi katika muda wa nyiongeza wa ILE NURU YA JIONI.. ili watubu..

1Petro 3: 1 “Wapenzi, waraka huu ndio wa pili niwaandikiao ninyi; katika zote mbili naziamsha nia zenu safi kwa kuwakumbusha,

2 mpate kuyakumbuka yale maneno yaliyonenwa zamani na manabii watakatifu, na ile amri ya Bwana na Mwokozi iliyoletwa na mitume wenu.

3 Mkijua kwanza neno hili ya kwamba KATIKA SIKU ZA MWISHO WATAKUJA NA DHIHAKA ZAO WATU WENYE KUDHIHAKI, WAFUATAO TAMAA ZAO WENYEWE,

4 na kusema, IKO WAPI AHADI ILE YA KUJA KWAKE? Kwa maana, tangu hapo babu zetu walipolala, vitu vyote vinakaa hali iyo hiyo, tangu mwanzo wa kuumbwa.

5 Maana hufumba macho yao wasione neno hili ya kuwa zilikuwako mbingu tangu zamani, na nchi pia, imefanyizwa kutoka katika maji, na ndani ya maji, kwa neno la Mungu;

6 kwa hayo dunia ile ya wakati ule iligharikishwa na maji, ikaangamia.

7 Lakini mbingu za sasa na nchi zimewekwa akiba kwa moto, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu.

8 Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja.

9 BWANA HAKAWII KUITIMIZA AHADI YAKE, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, MAANA HAPENDI MTU YE YOTE APOTEE, BALI WOTE WAFIKILIE TOBA.

10 Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.

11 Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,

12 mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka? “

Unaona ndugu,..tunaishi wakati wa muda wa nyongeza muda wa ile siku iliyojulikana na Bwana, wakati wa jioni, wakati wa NURU YA NEEMA. Je! Bado unaishi katika dhambi? Bado hujazaliwa mara ya pili? Utajitetea vipi siku ile pamoja na huu muda wa nyongeza uliopewa katika hili giza lililopo duniani, utatoa udhuru gani mbele ya hukumu. Kumbuka baada ya hii nuru kuondoka, (ambayo itaisha na UNYAKUO), kutakuwa kumebakia miaka saba tu mpaka dunia kuisha, huko ndiko ile dhiki kuu ya mpinga-kristo pamoja yale mapigo yote yaliyoandikwa katika kitabu cha ufunuo 8 & 16 yatatimia, kisha baada ya hapo itakuja hukumu na kisha ziwa la moto.

Kama hujatubu kwa kumaanisha kuziacha dhambi zako, fanya hivyo leo, ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji tele na kwa jina la YESU KRISTO upate ondoleo la dhambi zako (kulingana na Matendo 2:38), na Bwana atakupa kipawa cha Roho Mtakatifu..

Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.

JE! NYWELE ZAKO ZINAOTA AU ZIMESIMAMA?

UNAFANYA NINI HAPO?

UMETEKWA NA UPENDO WA KRISTO?

KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE? NA TENA WANA WA ISRAEL WALIMFUKIZIA UVUMBA MALKIA WA MBINGUNI, NDIO YUPI HUYO?


Rudi Nyumbani

Print this post

TUZO UTAPEWA KULINGANA NA NAFASI YAKO.

Mambo ya asili yanafunua mambo ya rohoni, Bwana Yesu alituambia “wana wa ulimwengu huu katika kizazi chao wenyewe huwa na busara kuliko wana wa nuru. (Luka 16:8)”..Neno hili linatuhusu sisi tulio wakristo, Embu tujifunze mojawapo ya busara walionayo wana wa ulimwengu huu, Mtume Paulo alisema katika

“1Wakorintho 9: 24 Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate…”

Kama tunavyosoma katika andiko hilo tunaona jinsi Mtume Paulo alivyoweza kuwatazama wakimbiaji wa kidunia akapata hekima, kadhalika na sisi tujifunze ili tupate hekima mbele za Mungu wetu aliye mbinguni. Kama ulishawatazama wakimbiaji wanaoshiriki katika michezo ya mbio ndefu au fupi, utafahamu kuwa wao huwa hawashiriki tu watu wote ovyo ovyo, yaani tukiwa na maana kuwachanganya watoto, na wazee pamoja na wanawake na wanaume humo humo katika riadha moja, hapana, waligundua wakifanya hivyo basi kutakuwa hakuna usawa wowote na mwisho wa siku katika ugawaji wa tuzo, litapatikana kundi moja la kipekee litakalokomba tuzo hizo zote,(hivyo michezo haitakuwa na maana yoyote) Lakini ili kuweka mambo yote sawa, walifanikiwa kutenganisha mbio hizo kulingana na uwezo wa watu, umri wa watu, pamoja na jinsia za watu.

Kwamfano kama ukitazama wanaoshiriki katika mbio zile fupi tuseme labda zile za mita 100, utakuta zimetengwa mbio za wanaume kivyao na wanaweka kivyao, hawachanganywi kwasababu uwezo unatofautiana kulingana na jinsia, kwamfano kama wanawake watakaoshiriki wapo 10, na wanaume 10, tuseme wakimbie pamoja basi utakuta nafasi zote 10 za kwanza zitachukuliwa na wanaume wote, na kuanzia nafasi ya 11 ndipo mwanamke wa kwanza ataanza kutokea..Hivyo mwisho wa siku inatokea kuwa hatapatikana mwanamke atakaye pokea tuzo yoyote pamoja na taabu zake zote..

Sasa kwa kwa kulitatua hilo, wakatofautisha makundi mawili, wanaume kwa wanaume, na wanawake kwa wanawake,.. Mwanaume atakayemaliza wa mwisho, kwa sekunde tuseme 11, na mwanamke aliyeingia wa kwanza kwa sekunde 12..Yule mwanamke wa kwanza aliyeshinda katikati ya wanawake wenzake, unakuta anapokea tuzo sawa na yule mwanaume aliyeingia wa kwanza kule akiwa na sekunde 8 katika mashindano ya wanaume wenzake. Wote watapokea medali moja (labda tuseme ya dhahabu), kadhalika na wa pili na wa tatu hivyo hivyo kwa pande zote medali zao zitafanana..Ingawa kiuhalisia inaweza kuonekana kuwa wale wanaume wengine waliokosa medali wangestahili kupewa zile tuzo za wale wanawake , kwasababu wao walikimbia ndani ya muda mchache kuliko wao, lakini haiko hivyo katika utoaji wa medali (tuzo). Utoaji unategemea na kundi unaloshiriki. Kadhalika mbio za walemavu, na watoto haziwezi zikawa sana na mbio za watu wazima, lakini medali ya atakayeshinda katikati ya walemavu itakuwa na thamani sawa na medali za wale wazima.

Kadhalika na katika mbio za kikristo, wote tunashiriki mchezo mmoja, wote tunashindana katika mbio, lakini Mungu aliziweka hizo mbio katika makundi tofauti tofauti. Watoto kivyao, wanaume kivyao pamoja na wanawake kivyao. Lakini kwa kila kundi thamani ya tuzo kwa watakaoshinda hazitofautiani.. Lakini Bwana alisema kwetu sisi wana wa Nuru hatuna hekima katika mashindano yetu haya duniani..Wote tunataka tujichanganye tukimbie katika kundi moja wote, wanaume hukohuko, wanawake huko huko, watoto huko huko n.k. Ndugu kwa Mungu hakupo hivyo, Mungu alitoa majukumu katika kanisa, Majukumu ya wanaume na majukumu ya wanawake, na majukumu yanayopaswa yafanywe na wote.

Biblia inaposema katika 1Timotheo 2: 8 “Basi, nataka WANAUME WASALISHE KILA MAHALI, huku wakiinua mikono iliyotakata pasipo hasira wala majadiliano”, Haikukosea, Kama inavyotupa mwongozo, mahali popote panapohusiana na kuongoza ibada ikiwemo uongozaji wa maombi, kusalisha, kuelekeza, vyote hivyo vinapaswa katika kanisa vifanywe na wanaume tu. Kwasababu jukumu hili limewekwa katika upande wa mbio za wanaume.

Kadhalika biblia ilisema pia..1Timotheo 2: 11 “MWANAMKE NA AJIFUNZE KATIKA UTULIVU, , akitii kwa kila namna.

12 SIMPI MWANAMKE RUHUSA YA KUFUNDISHA, WALA KUMTAWALA MWANAMUME, bali awe katika utulivu.

13 Kwa maana Adamu ndiye aliyeumbwa kwanza, na Hawa baadaye”.

Unaona? Hili ni agizo la pili la Bwana kwa kanisa, kwamba kazi ya kufundisha, mfano uchungaji, ualimu, uaskofu na ushemasi, haupaswi ufanywe na mwanamke. Na Mungu alishatoa sababu ya kufanya hivyo hapo juu, Hivyo ikiwa mwanamke ataona kama hapewi haki yake na kutaka kwenda kuwa mchungaji au mwalimu ni sawasawa na ameingia katika mbio ambazo sio za jinsia yake, Hivyo matokeo yake mtu kama huyo, ataonyesha kweli nguvu nyingi na jitihada nyingi, lakini hatapokea tuzo yoyote katika siku ile,..Siku ile atasema Bwana mimi nilikuwa mchungaji wa kimataifa kanisani, nilifanya hivi nilifanya vile, lakini Bwana siku ile atamwambia hukupiga mbio mahali panapokupasa. Unaona hapo angepaswa akawe mchungaji, au mwalimu kwa wanawake wenzake, akawe muhubiri kwa wanawake wenzake, lakini sio kanisani penye mchanganyiko wa wanaume na wanawake.

1Wakoritho 14: 34 “Wanawake na wanyamaze katika kanisa, maana hawana ruhusa kunena bali watii, kama vile inenavyo torati nayo.

35 Nao wakitaka kujifunza neno lo lote, na wawaulize waume zao wenyewe nyumbani mwao; maana ni aibu wanawake kunena katika kanisa.

36 Au je! Neno la Mungu lilitoka kwenu? Au kuwafikia ninyi peke yenu?

37 Mtu akijiona kuwa ni nabii au mtu wa rohoni, na ayatambue hayo ninayowaandikia, ya kwamba ni maagizo ya Bwana.

38 Lakini mtu akiwa mjinga, na awe mjinga”.

LAKINI MBIO ZA WANAWAKE NI ZIPI?

Biblia ilisema tena pale pale kwenye..

 1Timotheo 2: 9; “Vivyo hivyo wanawake na WAJIPAMBE KWA MAVAZI YA KUJISITIRI, PAMOJA na ADABU NZURI, na MOYO WA KIASI; SI KWA KUSUKA NYWELE, wala KWA DHAHABU na LULU, wala KWA NGUO ZA THAMANI;

10 bali kwa MATENDO MEMA , kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.

11 Mwanamke na AJIFUNZE KATIKA UTULIVU, akitii kwa kila namna.”

Mwanamke akidumu katika hali ya utulivu, pamoja na adabu, pamoja na kiasi,(Ikiwa na maana awe mwenye nidhamu pia hasengenyi watu,) pamoja na kujisitiri mwili wake kwa kutokuvaa mavazi yanayoonyesha maungo yake, kwa kutokuvaa suruali kama wanaume, kutokuvaa vimini, haweki wigi, wala lipstick midomoni mwake, wala hereni, anadumu katika utakatifu wote, basi Huyo atakuwa katika mashindano miongoni mwa wanawake wenzake (akina Sara, Rebeka, Hana, n.k.) , na siku ile atapokea tuzo yenye thamani kubwa kuliko hata mwanaume ambaye ni mchungaji au muhubiri au mwalimu ambaye hajatumika katika uaminifu wote katika nafasi yake..Atakwenda kuketi pamoja na Kristo katika kiti chake cha Enzi katika siku ile.

Kuna muhubiri mmoja maarufu wa kimarekani anaitwa Rick Jonyer, anaeleza: siku moja alichukuliwa katika maono na Bwana Yesu juu mbinguni katika ulimwengu wa Roho, alipofika kule alianza kutembezwa katikati ya viti vya enzi, na alipokuwa anapita katikati ya baadhi ya hivyo viti vya enzi aligundua kitu, kwamba mbona viti vingi vinakaliwa na wanawake pamoja na watoto? Ndipo akamwambia Bwana inaelekea huku wanawake na watoto ndio wamechukua nafasi kubwa..Anasema alishangazwa sana kuona wale aliokuwa anadhani wangekuwa wana nafasi kubwa kule, kuona ni wadogo sana.

Unaona hapo Dada katika Kristo?, unaweza ukadhani ukidumu katika nafasi yako kama mwanamke hautapata chochote, hapana! Kinyume chake utapata vyote, Thawabu za Bwana zinapimwa kulingana na umri, jinsia na maumbile…talanta uliyopewa kulingana na jinsia yako itumie hiyo vizuri bila kuingilia mbio za jinsia nyingine, tumia talanta ulizopewa katika uaminifu wote ni mfano tu wa mwalimu aliyetoa jaribio kwa wanafunzi wake wawili, mmoja akampa mtihani wa maswali 10 marefu, mwingine akampa mtihani wa maswali 100 mafupi, Yule aliyepewa maswali kumi akapata 9 kati ya yale kumi na kukosa moja, hivyo akahesabiwa kuwa kapata asilimia 90 kati ya mia (yaani 90%). Lakini Yule aliyepewa maswali mia mafupi akapata hapo maswali 50 na maswali mengine 50 yaliyosalia akakosa hivyo akahesabika kapata asilimia 50 kati ya mia (yaani 50% ).

Hivyo mwalimu wakati wa kugawa tuzo akampa tuzo(zawadi) kubwa Yule wa kwanza aliyefanya maswali kumi na kupata hapo tisa,(asilimia 90% ) kuliko Yule pili aliyefanya maswali 100 mengi na kupata hapo asilimia 50% tu. Na ndivyo Baba wa mbinguni atakavyotoa Tuzo siku ile. Mwanamke Yule ambaye atajitunza katika utulivu wote, na kiasi na kujisitiri, na upole na uvumilivu, na utakatifu, na adabu atafananishwa na Yule mwanafunzi aliyepewa maswali 10 nakupata hapo 9, kuliko mwanaume aliyepewa maswali mia na kupata hapo 50.

Dada kabla ya kujifunza kwa Musa, hebu jifunze kwanza kwa Miriamu dada yake Musa alivyokuwa, kabla hujajifunza kwa Eliya nenda kwanza kajifunze kwa Yezebeli Yule mwanamke aliyempinga Eliya, kabla hujajifunza kwa Petro hebu kajifunze kwanza kwa Miriamu na Martha na Mariam Magdalena, na Susana (luka 8:1-3), wanawake walioshuhudiwa kumuhudimia Kristo kwa kila hali, kabla ya kujifunza kwa Paulo hebu kajifunze kwanza kwa Tabitha na mwanamke Lidia aliyewakaribisha wakina Paulo walipokosa mahali pa kukaa (Matendo 16:13-15).

Hivyo nakupa moyo dada, ambaye umeanza safari yako hii ya kumtii Kristo, na kubaki katika nafasi yako Mungu aliyokuweka, zidi kuwa mtakatifu na kujisitiri na kuwa kielelezo kwa wanawake wengine kwasababu kiti cha enzi mbinguni kinakuongojea.

Hivyo yapo pia majukumu tulikabidhiwa wote, nayo ni kuwa “mashahidi wa Kristo”. Kila mmoja wetu [awe mwanamke au mwanaume] anapaswa popote pale alipo awe kielelezo cha kuwavuta watu wengine katika ufalme wa mbinguni (kwa mienendo na matendo)..Biblia inasema katika

1Petro 3: 15 Mwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu.

16 Nanyi mwe na dhamiri njema,…

Ubarikiwe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali “share” kwa wengine ujumbe huu.


Print this post

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

Isaya 35: 8 “Na hapo patakuwa na NJIA KUU, na njia, NAYO ITAITWA, NJIA YA UTAKATIFU; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; WASAFIRIO, WAJAPOKUWA WAJINGA, HAWATAPOTEA KATIKA NJIA HIYO”.

Mtu yeyote anayejiita ni mkristo ni wazi kuwa yupo safarini, Na kama yupo safarini ni lazima afahamu malengo yake ni nini, kwamba anatoka wapi, na anakwenda wapi? Na Sababu ya yeye kumfanya utoke pale alipo aende huko anendako ni ipi?, Kadhalika ni lazima ajue ni njia gani atakayoipita, na chombo kipi atakachokitumia kusafiria pamoja na gharama zake..! Lakini ukiwa ni msafiri halafu hujui hayo yote, ni dhahiri kuwa utaitwa MTORO, kama vile Kaini alivyoambiwa na Bwana Mungu kwamba atakuwa“mtoro na mtu asiye na kikao duniani (Mwanzo 4:12)”. Na huo uzao wa Kaini unatenda kazi miongoni mwa kundi kubwa linalojiita la wakristo, hawana vikao, hawajulikana ni watu wa ulimwengu huu, au ni wasafiri wa kwenda mbinguni, Kumbuka Kaini na Habili wote walikuwa ni ndugu, isipokuwa mmoja hakuonekana kuwa mkamilifu mbele za Mungu.

Mtu aliye makini katika safari yake, siku zote anaona mwisho wa safari yake utakuwa ni upi hata kabla hajaianza hiyo safari, na atatambua ya kuwa wakati akiwa njiani atakutana na mambo mengi tofuati tofauti, na majira mengi tofauti tofauti, hivyo atakuwa makini akijua kuwa yupo safarini kwahiyo hatayatilia maanani mambo yanayopita ya njiani, hata akifika kituoni labda kwa muda mchache tu atashuka kuchuka chakula na kurudi kwenye chombo chake cha usafiri na kuendelea na safari yake, hatashikamana au kuambatana na shughuli zinazoendelea katika hicho kituo alichofika kwa muda tu, huwezi kuona anakwenda kuzunguka tena mijini, labda kwenye viwanja vya michezo, na majukwaa ya sinema, na kutangatanga huku na huko ni kwasababu gani? Kwasababu anajua akifanya hivyo muda wake hautamtosha hivyo ataachwa na kile chombo alichokuwa anasafiria, na hapo pia si sehemu yake aliyotarajia kufika, Kwahiyo yeye mahali popote anapopita atatafahamu ni mpitaji tu, 

kadhalika na katika ukristo wa kweli sisi ni wasifiriji tu, ulimwenguni sio kwetu,..Mkristo ni lazima afahamu yeye anatoka wapi, na anakwenda wapi, na kitu gani kinachompeleka huko aendako,,.Safari yetu sisi ni kutoka katika ulimwengu mmoja na kwenda katika ulimwengu mwingine, tunatoka katika ulimwengu huu uliopo sasa unaoharibika na kwenda katika ulimwengu mpya wa milele usioharibika, na ili kuufikia huo ulimwengu mpya ipo njia ya kuipitia, ndio hii Bwana anayoiita, “NJIA KUU”..Hii imeitwa Njia kuu kwasababu wanaopita juu yake ni wachache, na ni WATAKATIFU tu WALIOSAFARINI ndio watakaopita juu yake, Hakuna mtu mwingine yeyote atakayeweza kupita katika hiyo njia isipokuwa amekidhi hivyo vigezo.

Kumbuka katika huo ulimwengu ujao kutakuwa na MALANGO MAKUBWA ya kuuingilia, Na njia pekee itakayokuongoza kuuingia ni hiyo NJIA KUU inayojulikana kama Njia ya Utakatifu. Huko ndiko Yerusalemu mpya mji wa Mungu ulipo, (yaani bibi-arusi wa Kristo). Na ndio maana Bwana Yesu alisema,

Ufunuo 22: 14 “Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, NA KUINGIA MJINI KWA MILANGO YAKE.

15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya”.

Ndugu yangu, maneno ya Yesu Kristo ni kweli na uzima, hiyo njia ni NJIA KUU ni NJIA YA UTAKATIFU, haijasema ni njia ya dini, au ya dhehebu, au ya upako, au ya miujiza, au ya utajiri, au ya umaskini, hapana inasema ni NJIA YA UTAKATIFU, ikiwa na maana kuwa wale wasafiri ambao ni watakatifu ndio wanaoipita hiyo,na si mwingine yeyote unaweza ukadhani upo katika njia hiyo kwasababu tu wewe unayo dini, lakini ndugu kama huna UTAKATIFU haupo katika hiyo njia, hata kama utatoa zaka kiasi gani, kama wewe haujajiweka kama mtu anayesafiri, basi jua haupo katika njia hiyo. Biblia ipo wazi kabisa inasema.

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”;

Unaona hapo?, wewe unayesema ni mkristo na unasema upo safarini, umefika katikati ya safari yako umekutana na anasa na burudani za ulimwengu huu, unasahau kuwa wewe ni mkristo unayesafiri unaanza na wewe kushikamana na hivyo vitu vya ulimwengu huu vinavyopita, unaanza na wewe kuhudhuria karama za ulafi, unaanza kujishughulisha na rushwa, unaanza kujichanganya na watu waovu wa ulimwengu huu, ulikuwa ni mwombaji mzuri hapo mwanzo lakini sasa biashara na udanganyifu wa mali vinakusonga, wewe kila wakati ni mali tu, unasahau maisha yako ya rohoni, hujui kuwa muda unazidi kwenda na kile chombo ulichokuwa unasafiria (Neema) hakiwezi kikakusubiria muda wote huo,

Ulikuwa unavaa vizuri na kujisitiri hapo mwanzo, lakini ukafika kituo ukakutana na fashion za ulimwengu huu, ukasahau kuwa upo safarini ukauacha utakatifu uliokuwa nao hapo mwanzo na wewe ukaanza kuvaa suruali na kaptura, ukaanza kuvaa nguo fupi, ukaanza kuvaa nguo zinazochora maumbile yako, ukaanza kupaka ma-lipstick, na wanja, na hereni na ma-wigi kama wanawake wa ulimwengu huu, hujui kuwa muda unazidi kwenda na kile chombo ulichokuwa unasafiria kimeshaanza kukuacha.

Mwanzoni mwa safari yako mawazo yako yalikuwa yameelekea mbinguni tu, ulikuwa unatamani ufikie kilele cha safari yako mapema, ulikuwa unafikiria kila siku habari za mbingu mpya na nchi mpya lakini umefika mahali umegota safarini, umeiacha NJIA KUU YA UTAKATIFU, umeanza kutazama pornography, umeanza kusengenya, umeanza kutukana, umeacha upole wako na ukarimu wako, ndugu ukiendelea hivyo hivyo hautauingia ule mji Yerusalemu ya Bwana, usijidanganye na Dini yako ukadhani inatosha kukufikisha mbinguni, kwasababu biblia ilishasema..”

Mithali 14: 12 Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti”..Kumbuka kama ilivyosema..Pasipo huo utakatifu hakuna mtu atakayemwona Mungu…

Isaya 35: 8 “Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, NJIA YA UTAKATIFU; WASIO SAFI HAWATAPITA JUU YAKE; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; WASAFIRIO, WAJAPOKUWA WAJINGA, HAWATAPOTEA KATIKA NJIA HIYO.

9 Hapo hapatakuwa na simba, wala mnyama mkali hatapanda juu yake; hawataonekana hapo; bali waliokombolewa watakwenda katika njia hiyo.

10 Na hao waliokombolewa na Bwana watarudi, watafika Sayuni wakiimba; na furaha ya milele itakuwa juu ya vichwa vyao; nao watapata kicheko na furaha, huzuni na kuugua zitakimbia”.

Umeona biblia inasema watakaopita katika njia hiyo, ulimwengu utawaona ni wajinga, wataonekana kama watu wasiostahili kuwa katikati yao, wanawake waliokataa mitindo ya ulimwengu huu wataonekana washamba na wajinga, wanaume wasiokuwa walevi, wala waasherati, watu wanaoishi maisha matakatifu watadharauliwa, lakini hao ndio Mungu aliowachagua wapite katika njia ile KUU, Biblia inasema wajapokuwa ni wajinga machoni pa ulimwengu lakini hawatapotea katika njia hiyo.

Kumbuka ndugu, biblia imetuonya tufanane na wasafiri wenzetu wa Imani waliotutangulia, ambao walijikana kweli kweli, watu ambao mawazo yao yote yalikuwa ni mbinguni tu, kama tunavyowasoma katika

Waebrania 11: 36 “wengine walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa mafungo, na kwa kutiwa gerezani;

37 walipigwa kwa mawe, walikatwa kwa misumeno, walijaribiwa, waliuawa kwa upanga; walizunguka-zunguka wakivaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi; walikuwa wahitaji, wakiteswa, wakitendwa mabaya;

38 (WATU AMBAO ULIMWENGU HAUKUSTAHILI KUWA NAO), walikuwa wakizunguka-zunguka katika nyika na katika milima na katika mapango na katika mashimo ya nchi.

39 Na watu hao wote wakiisha kushuhudiwa kwa sababu ya imani yao, hawakuipokea ahadi;

40 kwa kuwa Mungu alikuwa ametangulia kutuwekea sisi kitu kilicho bora, ili wao wasikamilishwe pasipo sisi…”

Waebrania 11: 13 Hawa wote wakafa katika imani, wasijazipokea zile ahadi, bali wakaziona tokea mbali na kuzishangilia, NA KUKIRI KWAMBA WALIKUWA WAGENI, NA WASAFIRI JUU YA NCHI.14 MAANA HAO WASEMAO MANENO KAMA HAYO WAONYESHA WAZI KWAMBA WANATAFUTA NCHI YAO WENYEWE.

15 Na kama wangaliikumbuka nchi ile waliyotoka, wangalipata nafasi ya kurejea.

16 Lakini sasa waitamani nchi iliyo bora, yaani, ya mbinguni. Kwa hiyo Mungu haoni haya kuitwa Mungu wao; maana amewatengenezea mji”.

Ndugu hawa watu walijikana nafsi zao kwasababu waliuona uzuri uliopo mbele yao, waliona furaha isiyokuwa na kifani kuingia katika ule mji, waliona ni heri maisha yao ya miaka 80 yasiwe ni kitu kulinganisha na miaka ya umilele inayokuja huko mbeleni. Ndugu kosa kila kitu lakini usikose mbingu, Biblia inasema wenye haki watang’aa kama jua, Mambo ambayo Mungu amewaandalia wampendao ni mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia, hakutakuwa na uchungu tena, wala kudharauliwa, watapewa miili ya utukufu wa ajabu, watatawala na Kristo Yesu kama wafalme na makuhani, milele na milele, tujitahidi tusikose huko.

Utajisikiaje unyakuo umepita na wewe umeachwa? Wenzako wamekwenda katika karamu ya mwanakondoo mbinguni na wewe umebaki?hapa duniani ukisubiria ziwa la moto? 

Utajisikiaje??..Ifuate hiyo NJIA KUU LEO, kwa kumpa Yesu Kristo maisha yako kama hujafanya hivyo angali muda upo, ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa kwenye maji tele na kwa Jina la YESU KRISTO, upate ondoleo la dhambi zako (Matendo 2:38) na kisha utapokea kipawa cha Roho Mtakatifu kitakachokuwezesha kuwa mtakatifu ili uweze kuiendea hiyo NJIA KUU YA UTAKATIFU ili siku ile Uingie katika ile Yerusalemu mpya ya Bwana aliyowaandalia watakatifu wake

Ufunuo 21: 1 “Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.

2 Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe.

3 Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.

4 Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.

5 Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli.

6 Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure.

7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.

8 Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili..”

Ubarikiwe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Print this post

ILI TUONEKANE WAKAMILIFU MBELE ZA MUNGU.

Kama unamchukulia mtu ni adui yako kwasababu amekusengenya, au amekudharau, au amekutukana, au amekuibia, au amekurusha, au amekuaibisha, au amekata mazungumzo na wewe ghafla, au amejisifia mbele zako na kukuona kama wewe si kitu kwasababu yeye pengine anaye mtoto na wewe huna. Hivyo umekuwa ukitamani Mungu amlipize kisasi, aanguke, au ashushwe au ikiwezekana afe kabisa, basi ni dhahiri kabisa dua hizo unazomtakia huyo adui yako kwa namna moja au nyingine zitakurudia wewe mwenyewe..

Kwasababu, kwa mambo kama hayo hayo yanakufanya na wewe kuwa adui kwa mtu mwingine(usiyemtarajia), inawezekana ulishawahi kumkwaza mtu pasipo wewe kujua, au kumuumiza hisia zake pasipo kukusudia kwa maneno yaliyowahi kutoka kinywani mwako, au uliacha kuzungumza naye pengine kwasababu za msingi kabisa pengine huna simu, hivyo yeye akalichukulia jambo lile kwa namna nyingine tofauti, pengine ulijifisia mtoto wako mbele zake kwa nia ya kutokujiinua, na yeye akaona kama vile umewadharau wa kwake, n.k..

Yeye pia atakuona wewe kama adui yake, na pengine yeye naye anaomba mbele za Mungu kama wewe ulivyokuwa unaomba, asambaratishwe, anamwomba Mungu amwinue ili uone mafanikio yake, anamwomba Mungu vikwazo vikukute, upate hasara, au udhaifu pengine hata ufe, anakutaja kila siku kwenye dua zake mbele za Mungu ushushwe chini..Lakini je! ni kweli wewe unastahili kufanyiwa hivyo vitu??. Na kama sio kwanini wewe unamfanyia mwingine? Biblia inasema “Msilaumu, msije mkalaumiwa,” Kwasababu kipimo tutakachopima ndicho hicho hicho tutakachopimiwa.(Luka 6:37)

Cha kuhuzunisha haya ndiyo yamekuwa maombi ya wakristo wengi katika siku hizi za mwisho. Kupelekea maombi mbele za Mungu, ..“Mungu mpige Adui yangu”…Kadhalika na mwenzako anakuombea na wewe upigwe!! Vile vile , hivyo yanakuwa ni maombi ya siri kila mmoja kwa mwenzake. Maombi ya namna hiyo mbele za Mungu huwa hayana matunda yoyote kinyume chake ni kumuhuzunisha Mungu.

Jambo mojawapo ambalo lilimfanya Ayubu aonekane ni MKAMILIFU na MWELEKEVU mbele za Mungu, ni kutokufurahia pale adui zake walipoanguka. Tukisoma katika Ayubu 31,

Ayubu 31: 29 “KAMA NILIFURAHI KWA KUANGAMIA KWAKE HUYO ALIYENICHUKIA, AU KUJIKUZA ALIPOPATIKANA NA MAOVU;

30 (NAAM, SIKUKIACHA KINYWA CHANGU KUFANYA DHAMBI KWA KUUTAKA UHAI WAKE KWA KUAPIZA);”

Unaona hapo?. Ayubu aliogopa hata kumwapiza adui yake mbele za Mungu, kwamba Mungu autoe uhai wake.Walikuwepo watu waliomdharau sana na kumchukia, waliomnenea vibaya, waliokuwa wanamtukana pengine kwa ajili ya haki yake, wapo waliokuwa wanamwonea wivu kwa kufanikiwa kwake, lakini hao hao Ayubu alipoona wameanguka, au wamepatikana na shida, au wamepata madhara au misiba. Ayubu hakusema sasa huu ni wakati wa kusheherekea, kwasababu Bwana amewalipiza kisasi wale waliokuwa wananichukia, maadui zangu wote,.kinyume chake yeye aliwahurumia, na kuwaombea, na kuwatakia heri siku zote, na ndio sababu iliyomfanya Ayubu alionekana kuwa mtu wa kipekee sana mbele za Mungu..mpaka Bwana akamwambia shetani “Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, MTU MKAMILIFU na MWELEKEVU, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu. (Ayubu 1:8)”.

Kadhalika pia tukimwangalia Bwana wetu YESU, hakuna mtu yoyote duniani aliyekuwa na maadui wengi kama yeye, Wewe unasema unao maadui, lakini hao maadui zako hawana hata mpango wowote wa kutoa maisha yako kwa gharama zozote, lakini Bwana wetu Yesu alikuwa na maadui ambao baadaye walifanikiwa kuja kumshika na kumtukana,kumdhihaki, kumtemea mate,kumvua nguo, kumpiga, kumwaibisha hadharani na hatimaye kumuuwa,,Lakini je! Aliwatakia laana mbele za Mungu?. Jibu ni Hapana kinyume chake tunaona aliwaombea, na kusema..”Ee Baba uwasamehe, kwa kuwa hawajui walitendalo”.Aliwaombea rehema badala ya Laana..Aliwaombea amani badala ya misiba.

Mahali pengine alifika maadui zake wakamkataa, na wanafunzi wake walipomshauri ashushe moto awaangamize kama Nabii Eliya alivyofanya lakini yeye aliwaambia,

Luka 9: 54 “Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, walisema, Bwana, wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize; [kama Eliya naye alivyofanya]?

55 Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.]

56 Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine”.

Unaona hapo?. Swali ni lile lile na wewe leo ni roho gani ipo ndani yako?. Kuangamiza au kuokoa,? Biblia inatumbia “Upendo huvumilia yote”, Upendo HAUHESABU MABAYA,(1Wakorintho 13) , Unachopaswa kufanya ni kumwomba Mungu amwokoe na sio kumwangimiza kwa dua zako, Tunachopaswa kuomba, ni Mungu atuepushe na madhara yao, na sio Mungu awaangamize, na ndio maana Bwana Yesu alisema ili sisi tuwe WAKAMILIFU kama Ayubu, ili sisi tuwe WAKAMILIFU kama BABA yetu wa mbinguni tunapaswa tulizingatie Neno hilo…Alisema:

Mathayo 5: 43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;

44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,

45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.

46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?

47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?

48 Basi ninyi mtakuwa WAKAMILIFU, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo MKAMILIFU”.

Hivyo ndugu Mungu hapendezwi kila siku tunapompelekea mashtaka mabaya dhidi ya maadui zetu, hiyo inatufanya tunaonekana kuwa hatujakamilika mbele zake, sio kila mara tuzunguke huku na huku, tukisema ..Adui yangu apigwe!..Adui yangu afe!! Adui yangu ashushwe!!…Kwanini tusiseme Adui yangu Bwana ambadilishe!!..Kwanini tusiseme ..Mungu mpe rizki Adui yangu”…kwanini tusiseme Mungu mrehemu adui yangu, hajui alitendalo??… Badilika sasa, Acha kumgeuza mtu kuwa adui yako pale anapokusengenya, pale anapokutukana, pale anapokudharau, au anapojitukuza juu yako.. Kumbuka maisha yako ndiyo yatakayougeuza moyo wa huyo ndugu yako, Fuata ule ushauri wa Bwana, mwombee. Na ndivyo tutakavyoonekana kuwa WAKAMILIFU mbele za Mungu.

Ubarikiwe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine.


Mada Nyinginezo:

MADARAKA YA WAKATI MKAMILIFU.

LULU YA THAMANI.

NINI MAANA YA ELOHIMU?


Rudi Nyumbani

Print this post

TWEKA MPAKA VILINDINI.

NoLuka 5: 1 “Ikawa makutano WALIPOMSONGA wakilisikiliza neno la Mungu, yeye alikuwa amesimama kando ya ziwa la Genesareti,

2 akaona vyombo viwili vimekaa kando ya ziwa, lakini wavuvi wametoka, wanaosha nyavu zao.

3 Akaingia katika chombo kimoja, ndicho chake Simoni, akamtaka akipeleke mbali kidogo na pwani. Akaketi, akawafundisha makutano ali chomboni.

4 Hata alipokwisha kunena, alimwambia Simoni, Tweka mpaka kilindini, mkashushe nyavu zenu mvue samaki.

5 Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu; lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu.

6 Basi, walipofanya hivyo walipata samaki wengi mno, nyavu zao zikaanza kukatika;

7 wakawapungia mikono washirika wao waliokuwa katika chombo cha pili, waje kuwasaidia; wakaja, wakavijaza vyombo vyote viwili, hata vikataka kuzama”.

Tukio hilo lililowapata wakina Petro linaweza likaonekana ni dogo lakini linabeba siri kubwa sana ya mafanikio hususani kwa wale watu ambao shughuli zao za kujipatia kipato haziendi sawa. Hivyo kama wewe ni mmoja wapo somo hili litakufaa sana. Soma hadi mwisho, lakini kama mambo yako yanaenda vizuri basi halitakuhusu sana., Zidi tu kuendelea kujifunza masomo mengine yahusuyo utakatifu na ufalme wa mbinguni.

Ukitafakari hiyo habari utaona Bwana Yesu, alikuwa akihangaika sana katika kuwafundisha makutano, yale mazingira yalikuwa ni magumu sana kutokana na kwamba watu wengi walimsonga na yeye alitaka kuwafundisha zaidi katika utulivu, hivyo hakuona kama akiendelea katika hali ile ile atatimiza kusudi lake, ndipo akaamua atafute madhabahu ya kuwakutanisha wale watu pamoja, mahali atakapotulia ili awafundishe wale watu katika ustaarabu na utaratibu ambao Mungu ameukusudia..

Na alipogeuka akaona vyombo viwili vimeegeshwa pwani na wenye navyo wametoka, ndipo akikichagua cha mmojawapo na kukigeuza kuwa madhabahu yake ya muda.

Sasa Chombo kinawakilisha nini katika mazingira tuliyopo leo?. Chombo kinawakilisha kitu chochote cha kujipatia kipato, kumbuka chombo hicho Bwana alichokitumia kilikuwa ni cha akina Petro cha kuvulia samaki, kwasasa hivi chombo kinaweza kikawa, elimu ya mtu, ujuzi wa mtu, biashara ya mtu, fremu ya mtu, shamba la mtu, kiwanja cha mtu,n.k.

Lakini tunasoma katika habari hiyo, tunaona Bwana alipotazama hakuchagua vyombo vilivyokuwa kando kando vyenye wavuvi au samaki, kumbuka vilikuwepo tu vingi vizuri zaidi ya hivyo vilivyokuwa vinazungukazunguka maeneo yale, lakini yeye hakuchagua chochote kati ya hivyo bali alivichagua vile visivyokuwa na kitu ndani yake…(Na ndio maana somo hili linawahusu sana wale ambao shughuli zao haziendi sawa),

Sasa kilichotokea ni kwamba wakina Petro walifanya kazi ya kuchosha usiku kucha wakihangaika kutafuta samaki ukanda mzima wa ziwa la Genesareti kwa shida, na kujitoa kweli kweli lakini wasipate kitu, mpaka kulipokucha wakakata tamaa ya kuendelea kuvua tena, wakaona kilichobakia tu ni kukipumzisha chombo na kuzitengeneza nyavu zao tena, kisha kuzihifadhi mpaka wakati mwingine,

Lakini baadaye kidogo ndio tunamwona Bwana Yesu akisumbuka na wale makutano, ndipo wao wakamruhusu Bwana kutumia vile vyombo ili kutimiza kusudi lake la kuhubiri,. Na baada ya Bwana kumaliza kuhubiri, sasa wakati makutano yote wameshaondoka ndipo akawageukia wale wamiliki wa vile vyombo, na kuwaambia NENDENI VILINDINI MKASHUSHE NYAVU ZENU, MVUE SAMAKI.

Lakini wao walimwambia, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha pasipo mafanikio, na walipokubali tu kwenda kuvua walipata matokeo makubwa ya kushangaza, mpaka nyavu zao kuanza kukatika, mpaka kufikia hatua ya kuomba msaada kwa wingi wa Baraka hizo, maana rizki imekuwa nyingi na kuwalemea mpaka hawawezi tena kuimaliza wao wenyewe ikawabidi wawaite na marafiki zao na maadui zao waokote na wao pia wapate kidogo..

Bwana Yesu hajabadilika, ni yeye Yule jana, na leo na hata milele, njia aliyotumia kumbarikia Petro ndiyo hiyo hiyo atakayoitumia sasahivi kukubariki na wewe uliyefanya kazi ya kuchosha miaka na miaka bila mafanikio yoyote. Umejaribu kufanya kwa bidii kazi lakini unachokipata hakijitoshelezi…

Leo hii hicho chombo chako kigeuze kuwa MADHABAHU YA KRISTO kwasababu anakitafuta hicho ili ilifanye kusudi lake, kumbuka pale Bwana hakutafuta sinagogi la kuwakusanya wale makutano waliokuwa wanamsonga, hakutafuta hekalu, wala hakutafuta mahali patakatifu bali alitafuta MAHALI PA KUJIPATIA KIPATO KWA MTU, mahali ambapo mtu anapopategemea kujipatia mkate wake wa kila siku, na pia fahamu tu, siku zote Bwana anapaangalia mahali ambapo palipo patupu kama kwako wewe, Mahali ambapo pamefanyika kazi ya kuchosha miaka mingi, miezi mingi pasipo mafanikio yoyote, hapo ndipo anapopataka kwa ajili ya kazi yake, na akishamalizana napo hapo, ndipo atakwambia nenda katupe nyavu zako kilindini uvue samaki, kwa wingi wa atakachokupa Bwana utaita mpaka na marafiki na zako na maadui zako waje nao kushiriki Baraka zako Mungu alizokuandalia.

Leo Kazi yako wewe ni ya ufundi, una ujuzi wa kutosha kuhusu masuala ya ujenzi, na unaona mahali unapokusanyikia pengine ni kanisani kuna kasoro Fulani ya ujenzi, na shughuli zako za kijenzi haziendi sawa, umekuwa ukipata mapato kidogo kupitia hiyo,wakati mwingine unakosa kabisa kazi, huo ndio wakati wa kwenda kumruhusu Bwana atumie hicho chombo chako (ujuzi),

nenda mahali unapokusanyika (kanisa), kazi ya Mungu inapofanywa, angalia kasoro zinazohusiana na taaluma yako, na utumie ujuzi wako kurekebisha tatizo hilo bila kutazamia malipo yoyote, pengine umeona ukuta wa kanisa umebomoka au una ufa, uzibe, umeona mfumo wa maji haujakaa sawa na una ujuzi wa kufanya hivyo, urekebishe hata kama hauna chochote, umeona kanisa halina choo kinachostahili, na wewe una ujuzi wa namna ya kutengeneza vizuri, nenda kafanye hivyo, kajenge kwa ustadi wote, na maarifa yako yote, umeona kuna kasoro ya umeme na mfumo wa nyaya, na una ujuzi huo nenda karekebishe usisubiri hata mtu akamwambie, mruhusu Bwana atumie hicho chombo, na mwisho wa siku utaona tofauti yako na mtu asiyefanya hivyo wakati Fulani ukifika.

Au wewe ni polisi au mlinzi, anza kutoa mchango katika sekta hiyo ndani ya kazi ya Mungu..Usiseme Mungu kweli ataweza kutumia taaluma hii/ujuzi huu kwenye kazi yake??..kumbuka Bwana Yesu alitumia mtumbwi wa wavuvi kuwapelekea maelfu ya watu katika ufalme wa mbinguni…Na wewe vivyo hivyo mpe Bwana chombo chako.

Au wewe unafanya kazi ya upishi, na unaona kazi zako haziendi sawa, faida ndogo, na unaona kuna uhitaji mkubwa wa wapishi ndani ya nyumba ya Mungu, labda kwa ajili ya wazee wasiojiweza (wakristo), au wageni, au wenye mahitaji na mayatima (walio wakristo), ndani ya kanisa n.k usingoje uambiwe au uwe na kitu kwanza ndio ufanye, wewe mwenyewe anza kuchukua hatua ya kujitolea kwenda kuifanya, tena pasipo hata kuombwa.

Wewe ni mtengeneza bustani, na ndiyo kazi yako umekuwa ukifanya kwa ajili ya kujipatia kipato..Lakini mazingira ya kanisani ni machafu au hayavutii, panaonekana ni mahali pasipo tofauti na sehemu nyingine yoyote, Tumia chombo chako (ujuzi) kurekebisha mazingira ya Mungu, pakavutia kama vile unavyopendezesha bustani za watu wengine,..unaweza ukaona ni jambo dogo lakini linamaana kubwa na Bwana akisharidhika atakuambia shuka vilindini..utaona milango Mungu anayokufungulia katika hiyo hiyo kazi yako ilivyo ya ajabu.

Wewe ambaye ulikuwa unatafuta kazi,na bado hujapata, angali unao ujuzi Fulani, usiuache ulale utumie huo ujuzi katika kazi ya ufalme wa mbinguni, kwamfano labda wewe ni “ IT ” (mjuzi wa katika teknolijia ya Kompyuta), unaweza uka unda wavuti na tovuti kwaajili ya kutangaza ufalme wa mbinguni, unaweza ukabuni programu za kutangaza kazi ya Mungu kirahisi katika mitandao fanya kiuaminifu kabisa..Na Bwana akishamaliza kutenda kazi kwa kutumia chombo chako, atakuambia shuka vilindini…Utaona nafasi ambayo ulikuwa unaitafuta kwa kuhangaika kwa muda mrefu pasipo mafanikio kama wakina Petro walivyokuwa..unaipata ndani ya kipindi kifupi tena chenye faida mara 100 zaidi ya kile cha mwanzo ulichokuwa unakihangaikia..

Lakini hizo zote zinakuja kwanza kwa kumtolea Bwana chombo chako akitumie, kwa ajili ya kazi yake, lakini kuna wengine hawapendi kumpa Bwana nafasi lakini wanataka Baraka za Bwana, utakuta mtu analo eneo kubwa limekaa pasipo matumizi yoyote, hataki hata kukaribisha watu wafanyie kazi za mikutano ya injili hapo, na bado anataka Mungu ambariki, ndipo hapo zile roho za udanganyifu zilizoachiliwa katika siku za mwisho zinaanza kumdanganya na kumshawishi, akanunue mafuta ya upako, anunue chumvi na maji ya Baraka akanyunyuzie kwenye kiwanja chake na kwenye biashara yake, aanze kukemea roho za laana katika kiwanja chake, au biashara zake, ili mambo yake yaanze kwenda vizuri.

Utamkuta mwingine anazo fremu za vyumba na zimekosa mpangaji wa kufanyia biashara au tution,..na wakati huo huo kuna wakristo wenzake wamekuja kumwomba awape angalau fremu moja wawe wanafanyia bible study au maombi wakati wa jioni kwa muda huku wanatafuta eneo lingine..lakini kwasababu hajui uweza wa Mungu, anawazuilia na kuona bora tu ziendelee kuwa zimefungwa.na wakati huo huo anazunguka kutafuta kuombewa na kununua maji na mafuta ya upako huku na kule hata wakati mwingine nchi na nchi..Mtu wa namna hii hawezi kutazamia miujiza kama waliofanyiwa wakina Petro.

Bwana anasema nikaribieni, nami nitawakaribia… Wakati mwingine hilo pigo unalolipata la kuvuna haba, ni kwasababu kazi ya Mungu inakaa katika hali ya kusongwa songwa na wewe hutaki kulitazama hilo kwa kumzuilia Bwana chombo chako..(Soma Hagai 1:1-12). Anza leo kufanya kama akina Petro walivyofanya na Mungu atakubariki. Mtaijua kweli nayo kweli itawaweka huru.

Ubarikiwe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali “share” kwa wengine ujumbe huu.

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

Print this post

NINI MAANA YA KUTOKA KATIKA MADHEHEBU?

Kwanza jambo la kufahamu ni kwamba kila mkristo anapaswa awe na Roho Mtakatifu, ambaye kwa huyo biblia inasema ATATUONGOZA NA KUTUTIA KATIKA KWELI YOTE.

Yohana 16: 13 “Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake”.

Hivyo mtu yeyote asiyekuwa na Roho wa Mungu biblia inasema huyo si wake (Warumi 8:9), Haiwezekani   kumjua Mungu kwa namna yoyote ile,.  Sasa tatizo linatokea ni pale unakuta watu wengi walipokea kweli Roho Mtakatifu mwanzoni walipoamini, lakini ilifikia wakati Fulani wakamzimisha pasipo hata wao kujijua, Uthibitisho ni kwamba utasikia mtu anakwambia mwanzoni nilipompa Bwana maisha yangu nilikuwa ni moto sana, lakini siku hizi nimepoa, ile nguvu ya mwanzo sina..sasa hiyo ni dalili ya awali kabisa ya mtu aliyemzimisha Roho ndani yake,  biblia inasema, katika (1Wathesalonike 5: 19 MSIMZIMISHE ROHO; )

Unaweza ukaona hapo, Roho wa Mungu anaweza kuzimishwa, na anazimishwa kwenye nini?, ,Jibu ni kwamba anazimishwa katika eneo la kuendelea kukuongoza katika kweli yote.. Na madhara ya kutofikia kile kiwango kinachohitajika na Mungu ni kukaa katika hali hiyo hiyo ya kutokuwa na ufahamu wa kutosha kumuhusu Mungu,hivyo ni rahisi kudanganywa na kuchukuliwa na mafundisho mengi ya uongo, unakuwa ni kama unyasi unaotikiswa na upepo.

Sasa njia pekee inayowasababisha wengi wamzimishe Roho ni UDINI na UDHEHEBU, Kwa mfano wakati Bwana Yesu alipokuwa duniani, aliwakuta watu wakiwa katika dini zao na madhehebu yao, nao si wengine zaidi ya mafarisayo na masadukayo, Hawa watu sio kwamba walikuwa ni wabaya sana, hapana, kwanza vitu vingi walivyokuwa wanashika yalikuwa ni maagizo ya Mungu, na walikuwa wanafanya bidii kweli katika kuvishika na kuvisimamia, lakini torati waliyokuwa wanaishika haikuwa imekamilika, na alipokuja Bwana kuwaeletea habari ya kuitimiliza torati, walimpinga na kumkataa, lakini ni kwasababu gani?, sababu ilikuwa si nyingine zaidi ya kujikinai katika Dini zao na udhehebu wao. Na kukataa kumruhusu Roho Mtakatifu awafundishe zaidi na kuwatia katika kweli yote…

Sasa matokeo yake wakaukosa uzima waliokuwa wanautazamia na kupelekea kugeuka kuwa wapinga-Kristo badala yake. Kwasababu walihama kabisa katika kuongozwa na Roho wakaenda katika kuongozwa na dini, na taratibu za madhehebu yao..Pengine walianza kusema dhehebu letu ndio la zamani na la kipekee, lina watu wengi, tuna masinagogi mengi duniani kote,..Tunaheshimika na mataifa yote, tuna wasomi wengi, tunafadhili miradi mingi ya kijamii, tunaongoza katika kusaidia maskini na yatima,..Sasa huyu mtu anayejiita YESU, na Yohana Mbatizaji wanatuletea habari za ubatizo wa maji, wanazitolea wapi? Mambo hayo hayapo kwenye torati, kwanza ni watu wa kawaida, wanatafuta wafuasi,..Lakini Bwana Yesu aliwaambia kwa ufunuo wa Roho Mtakatifu, Yohana 3:5 ”….Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.”

Sasa wao walibakia tu katika sheria za dini na madhehebu, kwamba usipotahiriwa huwezi kumwona Mungu,

Kadhalika na katika wakati huu wa sasa, hakuna mahali popote Mungu alianzisha dhehebu, sisi wote kwa pamoja ni wakristo, na mikusanyiko yote yanapaswa yawe na imani moja, ubatizo mmoja na Roho mmoja, Bwana mmoja, Mungu mmoja, (Waefeso 4:4-5), lakini hiyo imekuwa ni tofauti katika kanisa la leo, imani ni nyingi tofauti tofauti, batizo ni nyingi tofuati tofuati, na kibaya zaidi ni kwamba kila mmoja anaamini cha kwake ndio sahihi,..wengine wanasema sisi ni wa Luther, wengine wanasema sisi ni wa Branham, wengine wanasema sisi ni wa Hellen White, wengine wanasema sisi ni wa John Wesley, n.k… Lakini Mtume Paulo baada ya kuliona jambo kama hilo la kanisa kugawanyika vipande vipande katika madhehebu alisema hivi…

1Wakorintho 1: 12 Basi, maana yangu ni hii, ya kwamba kila mtu wa kwenu kusema, Mimi ni wa Paulo, na, Mimi ni wa Apolo, na, Mimi ni wa Kefa, na, Mimi ni wa Kristo.

13 Je! Kristo amegawanyika? Je! Paulo alisulibiwa kwa ajili yenu? Au je! Mlibatizwa kwa jina la Paulo?

Unaona hapo? Kanisa la Kristo haligawanyiki kwasababu Kristo hajagawanyika, tungepaswa wote tunapokusanyika wote tunakuwa ni ndugu katika Imani moja. Sasa inapotokea Roho wa Mungu anapotaka kumwongoza mtu katika kuijua kweli zaidi, labda tuseme anamfundisha juu ya ubatizo sahihi ya kwamba anapaswa akazamishwe kwenye maji mengi, na kwa jina la YESU KRISTO,. Lakini mtu Yule mtu badala ya kuchunguza maandiko na kumwomba Roho Mtakatifu amsaidie, moja kwa moja atakwenda katika dhehebu lake, je! Wanaamini hivyo?, akikuta dhehebu lake hawaamini hivyo, basi na yeye analitupilia mbali. Hajui kwamba ameshamzimisha Roho pasipo hata yeye kujijua, na watu wa namna hiyo ukitazama maisha yao ya kiroho yanakuwa ni chini siku zote, na mwisho wa siku wanageuka kuwa wapinga-kristo kama walivyokuwa mafarisayo na masadukayo, kwa jambo dogo tu la udhehebu na udini. Wanaanza kuwapinga vikali wale wote wanaofundisha kinyume na mapokea yao.

Tukiyajua hayo sasa, biblia inaposema “TOKENI KWAKE ENYI WATU WANGU” (Ufunuo 18:4), haimaanishi kutoka kwa miguu, bali ni katika roho, na ufahamu, ni kutoka katika kamba za dini na madhehebu, kutoka katika makosa yaliyofanywa, kutokufungwa na mifumo ya dini na madhehebu inatakayokufanya usipige hatua moja ya kiroho (huko ndiko kumzimisha Roho).. Unapoona kweli sehemu Fulani inafundishwa, usikimbilie kulinganisha na dhehebu lako au dini yako inasemaje juu ya hilo..moja kwa moja kimbilia kulilinganisha na Neno la Mungu, hapo ndipo Roho Mtakatifu anaanza kupata nafasi ya kukufundisha na kukuongoza katika kweli yote…

Kwa mfano umesikia mahali unafundishwa ibada za sanamu ni machukizo mbele za Mungu, lakini katika dhehebu lako ni jambo ambalo mmekuwa mkilifanya siku zote. Sanamu imekuwa ni sehemu ya ibada zenu, sasa ili usimzimishe Roho, usikimbilie kwenda kuangalia dhehebu lako linasemaje, wewe kimbilia kuangalia Neno la Mungu linasemaje juu ya hilo, ndio Roho Mtakatifu unakuta anakuongoza katika huu mstari..

2Wakoritho 6: 15 “Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini?

16 Tena pana mapatano gani kati ya HEKALU LA MUNGU, na SANAMU? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.

17 KWA HIYO, TOKENI KATI YAO, MKATENGWE NAO, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.

18 Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike,”

Sasa ukishalifahamu hilo kwa usalama wa Roho yako, unapaswa uondoke hapo, utafute sehemu nyingine ambayo sanamu haichanganywi na ibada tukufu ya Mungu…kadhalika na mambo mengine kama hayo, kwa jinsi utakavyompa Roho Mtakatifu nafasi atakuwa anakuongoza katika kweli yote mpaka unafikia kimo cha mtu mkamilifu mbele za Mungu.

Kwahiyo unapokaa katika mkusanyiko wowote unaojiita ni wa Kikristo, chunguza ni vipi vinavyoendana na Neno la Mungu, ndivyo ushirikiane navyo, na vile visivyotokana na Neno, jitenge navyo tena mbali sana. Uongozo wako uwe ni BIBLIA na hapo ndipo Roho Mtakatifu atakapotumia kukuongozea.

Pia ni muhimu kukumbuka madhehebu ndiyo yatakayokuja kuunda ile chapa ya mnyama huko mbeleni..kwahiyo ni kuwa makini sana. Kadhalika katika siku za mwisho Bwana Yesu alisema kutakuwa na makundi mawili ya wakristo,. Kundi la kwanza linajulikana kama wanawali wapumbavu na la pili kama wanawali werevu (Mathayo 25). Ukisoma pale utaona Wale werevu walibeba Taa pamoja na mafuta yao ya ziada wakati wa kwenda kumlaki Bwana wao, lakini wale wapumbavu hawakubeba mafuta ya ziada, na wakati Bwana wao alipokaribia kuja taa zao zikaanza kuzima, kwasababu hawakuwa na mafuta ya ziada, hivyo hawakufanikiwa kuingia katika karamu ya Bwana wao japo nao walikuwa wanamngojea Bwana wao..

Lakini wale wanawali werevu wanawawakilisha wakristo waliopokea Roho Mtakatifu na kwasababu ni werevu hawakuridhika na mafuta waliyonayo machache, walitembea na mafuta mengine ya ziada ambayo yanawakilisha ufunuo na mafundisho ya Roho Mtakatifu hivyo mpaka Bwana alipokuja wakakutwa taa zao bado zinawaka, na ndipo wakaenda naye karamuni (huko ndiko kutokumzimisha Roho). Lakini wale wapumbavu ni wakristo ambao baada ya kumpa Bwana maisha yao, wakaridhika tu katika mapokeo ya dini zao na madhehebu yao, na siku Bwana atakapokuja atawakuta katika hali hiyo ya uvuguvugu, kuzimika kwa taa zao (kwasababu walishamzimisha Roho Mtakatifu zamani)..Hivyo watatupwa katika lile giza la nje, ambalo hilo linawakilisha dhiki kuu na ziwa la moto.

Hivyo ndugu unaona madhara ya kutotembea na Roho Mtakatifu katika safari yako ya ukristo? anza sasa kumruhusu Roho atende kazi ndani yako, toka katika kamba za dini na madhehebu, dumu katika Neno ili Mungu akufikishe mahali alipokusudia ufike.

Ubarikiwe sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MUUNGANO WA DINI NA MADHEHEBU YOTE, UMEKARIBIA.

UKIAMINI NA UKIMKIRI YESU KWA KINYWA CHAKO, UTAOKOKA

HATUA ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUTUONGOZA

JE! INAWEZEKANA MTU AKAWA ANAFANYA MIUJIZA NA BADO ASINYAKULIWE?


Rudi Nyumbani

Print this post