Category Archive maswali na majibu

Falaki ni elimu gani? (Isaya 47:13).

Falaki ni nini katika biblia?

Jibu: Turejee,

Isaya 47:12 “Simama sasa na uganga wako, na wingi wa uchawi wako, uliojitaabisha nao tangu ujana wako; labda utaweza kupata faida, labda utaweza kushinda. 

13 Umechoka kwa wingi wa mashauri yako; basi, na WASIMAME HAO WAJUAO FALAKI, wazitazamao nyota, watabirio kila mwezi mambo ya mwezi huo, wakakuokoe na mambo yatakayokupata”.

“Falaki” ni “elimu ya nyota na sayari na jua”.

Wanaofanya Falaki, wanaamini kuwa  “mpangilio wa nyota, mwezi na jua na sayari angani, unaathiri tabia ya nchi na tabia ya mtu/watu”. Jambo ambalo kwa sehemu moja ni kweli na sehemu nyingine uongo!.

Ni kweli Mpangilio wa Jua na mwezi, unaweza kuathiri tabia ya nchi, kama  vile vipindi vya mvua, kiangazi, au kipupwe….ipo miezi ambayo mvua inanyesha, na miezi ambayo mvua hainyeshi, ipo miezi ya kiangazi na miezi ya kipupwe…Majira ya mwezi wa 6 na 7 ni Kipindi ambacho jua linakuwa mbali na dunia na kweli nchi inaathirika na baridi kali, katika ukanda wa kusini wa dunia.

Vile vile tabia za mimea zinaathiriwa na majira na nyakati, yanayotokana na mpangilio wa mwezi na jua angani, mfano tabia za miembe kuzaa maembe zinaathiriwa na mwezi wa 12, kwamba yanapofika majira ya mwezi huo wa 12 mpaka wa 1 basi miti yote ya miembe inazaa sana, tofauti na kipindi kingine chote (kwahiyo kwa sehemu ni kweli).

Sasa kwa mantiki hiyo wana-falaki wanaamini kuwa kama mpangilio wa jua, mwezi na nyota angani unaweza kuathiri mazingira na hali ya hewa, basi vile vile mpangilio huo huo unaweza kuathiri tabia za watu, na hisia zao, na maamuzi yao na hata hatima yao!.

Kwamba kila tarehe na mwezi unabeba matukio yake kulingana na mtu na mtu, na pia kulingana na tarehe aliyozaliwa, vile vile mpangilio wa nyota na mwezi unaweza kuelezea ni kitu gani mtu atafanya, au atakitenda, au kitampata, vile vile ni bahati gani ipo mbele yake au hatari gani inamkabili.

Kwahiyo wote waliohitaji kujua mambo yatakayowapata mbeleni waliwatafuta hawa wana-Falaki, au kwa lugha nyingine wanajimu kujua hatima zao.

Lakini swali ni je! Elimu hii ina ukweli wowote na je wakristo ni sahihi kuitafuta, ili kujua hatima zetu kupitia falaki?

Jibu ni LA! Elimu hii haina ukweli wowote, mpangilio wa sayari na nyota, na mwezi hauwezi kuelezea tabia, hisia, maamuzi au hatima ya Mwanadamu!…mpangilio huo unaweza kufaa katika utabiri wa hali ya hewa na misimu ya kupanda na kuvuna (tena kwa sehemu ndogo) lakini hauwezi kutabiri maisha ya mtu.

Maisha ya mtu hayatabiriwi wala kusomwa kwa kutazama jua, au mwezi au nyota au sayari, kama ndivyo kulikuwa hakuna haja ya Kristo kuja, au hata kama angekuja basi angetuhubiria sana hiyo elimu, bali maisha ya mtu yanatabiriwa kwa KULITAZAMA NENO LA MUNGU peke yake!.

Ukitaka kujua kesho yako itakuwaje, isome biblia, itakuambia sio tu kesho utakuwa wapi, bali MILELE UTAKUWA WAPI!!!.

Utauliza vipi wale Mamajusi, mbona walioiona nyota ya Bwana YESU kutoka mashariki?.

Mungu alipenda kutumia ishara ya nyota kuelekeza utukufu wa mwanae alipozaliwa, lakini hakuwa anahubiri elimu ya nyota pale!, ni sawa na alivyotumia ishara ya Nguzo ya wingu au nguzo ya moto juu ya wana wa Israeli walipokuwa jangwani,.. ilikuwa ni kwa lengo la kuelekeza utukufu wa wana wake mahali walipo, lakini hakuwa anahubiri elimu za mawingu na moto, kwamba zikasomwe kwa bidii ili kuelezea utukufu juu ya mtu/watu.

Vile vile leo hii shetani anapenyeza elimu hii ya Nyota(Falaki) ndani ya kanisa kwa kasi sana!. Elimu hii inatoka kwa waganga na inahamia kanisani kwa kasi sana..Watu hawasomi tena biblia wanatafuta kusomewa nyota zao! Hawaombi tena kulingana na Neno wanaombea nyota kwa kurejea elimu ya falaki.

Ndugu usidanganyike!..Elimu ya nyota (Falaki) ni elimu ya shetani asilimia mia.

Kama unataka kusafisha hatima yako itii biblia, wala usitafute maombi ya kutakasiwa nyota!, hiyo ni elimu nyingine!… Vile vile ukitaka kujua kesho yako itakuwaje kasome biblia, usitafute utabiri wa kusomewa nyota kutoka kwa yoyote yule iwe mganga au anayejiita mtumishi wa Mungu.. Biblia pekee ndiyo itakayokuonyesha tabia yako na kukupa utabiri sahihi wa maisha yako ya kesho na ya milele.

Je umemwamini Yesu?, je umebatizwa ubatizo sahihi? Je umepokea Roho Mtakatifu?.

Bwana Yesu anarudi.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MSHIKE SANA ELIMU.

NYOTA ZIPOTEAZO.

Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?

Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.

MIEZI 13 YA KIYAHUDI.

Rudi nyumbani

Print this post

Haki ni Nini katika biblia. Haki ya Mungu ni ipi?

Haki maana yake ni kitu ambacho mtu anastahili kukipata. Kwamfano kuishi ni haki ya Kila mwanadamu, Hakuna mtu anayepaswa kumzuia mwingine kuishi, kisa ni mwanamke au ni mfupi, au ni kichaa, au mlemavu. Maadamu tu amekuwa mwanadamu tayari anayo haki ya kuishi.

Mfano mwingine wa haki, ni mtu aliyesoma  ukahitimu katika shahada Fulani labda tuseme ya utatibu, mtu kama huyo tunasema ana haki ya kuitwa daktari kwasababu amesomea jambo Hilo.

Vivyo hivyo katika Roho. Mungu naye anayo haki yake, katika kutoa vitu vyake.

Mwanzoni ilikuwa Ili kumkaribia Mungu na kupata kibali kwake na mema yote na baraka zote ilikupasa kwanza uishike Sheria yake yote. Hivyo yoyote aliyeweza kufanya hivyo alipatiwa haki hiyo. Soma Kumbukumbu 28

Lakini Kwa bahati mbaya hakukuwa na mtu aliyestahili kumkaribia Mungu kwasababu Hakuna mwanadamu aliyekwenda katika maagizo yote ya Mungu Kwa ukamilifu wote, bila kosa. Kwahiyo tangu zamani hakukuwa na mwanadamu hata mmoja aliyefanikiwa kumkaribia Mungu. Wote walitenda dhambi (Zaburi 14:3)

Hivyo Mungu akabuni mpango mwingine wa kumwokoa mwanadamu ili awe amestahili kupokea mambo yote ya rohoni ya Mungu, ikiwemo uzima wa milele na kumkaribia yeye.

Ndipo akamleta Yesu duniani, Ili Kila amwaminiye asipotee Bali apokee kuhesabiwa haki bure, bila kutegemea Tena matendo ya Sheria. Kwasababu Kwa matendo ya Sheria hakukuonekana aliyestahili.

Hivyo Mimi na wewe tunapomwamini Kristo kama ndiye Bwana na mwokozi pekee wa maisha yetu na kuukubali msamaha wake wa dhambi, basi tunahesabiwa tumestahili kuitwa watakatifu, na hivyo tunamkaribia Mungu katika ukamilifu wote, kumwomba yeye na kupokea vyote kutoka kwake bila sharti. Haleluya!

Warumi 3:21-24

[21]Lakini sasa, haki ya Mungu imedhihirika pasipo sheria; inashuhudiwa na torati na manabii; 

[22]ni haki ya Mungu iliyo kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote waaminio. Maana hakuna tofauti; 

[23]kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; 

[24]wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu; 

Hivyo ikiwa umekombolewa na Yesu Kristo, basi unapaswa uwe na ujasiri wote kumkaribia Mungu, bila kutegemea ukamilifu wako,Bali Kristo tu, na hivyo utapokea mema, yote kutoka Kwa Mungu.

Waebrania 4:16

[16]Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji. 

Hiyo Ndio inaitwa “HAKI itokayo Kwa Mungu” ambayo tunaipata kwa kupitia Yesu Kristo tu peke yake.

Kwa Yesu tunapokea uzima wa milele bure. Kwa Yesu Tunapokea majibu ya mahitaji yetu yote bure. Kwa Yesu tunaitwa watakatifu.

Lakini Swali ni je! Umemwamini Kristo? Kumbuka kamwe huwezi kumpendeza Mungu Kwa matendo yako pekee, Kila mwanadamu chini ya jua anamuhitaji Kristo.

Ikiwa Bado hajaokoka basi mlango upo wazi Leo. Tubu mgeukie Bwana akuponye. Ikiwa upo tayari kupokea msamaha wa dhambi Leo, na kufanywa kiumbe kipya, basi fungua hapa Kwa Mwongozo huo. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

SI KWA MATENDO BALI NEEMA.

NJONI, NUNUENI MLE NA MNYWE.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mithali 16:30 Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka; 

SWALI: Nini maana ya Mithali 16:30

Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka;  Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya. 

JIBU: Mstari huo haumaanishi mtu anayefumba macho yake, Huwa anaishia kuwaza mawazo mabaya, hapana kama ni hivyo basi,  tungekuwa tunafanya makosa kufumba macho tunapoomba.

Zaidi sana mtu mwenye hekima huwa anapoona jambo la kutisha ovu, au lenye aibu Ndio anayekuwa wa kwanza kufumba macho yake asiruhusu kuona kinachoendelea.. kama vile walivyofanya watoto wa Nuhu.(Mwanzo 9:23)

Hali kadhalika anaposema mtu aikazaye (aifumbaye), midomo yake. Haimaanishi mtu asiyezungumza-zungumza, Huwa anaishia kuyazungumza maneno yasiyofaa. Kama ni hivyo biblia isingesema;

Mithali 21:23

[23]Mtu azuiaye kinywa chake na ulimi wake, Atajilinda nafsi yake na taabu. 

Lakini je? Vifungu hivyo vilimaanisha Nini?

Hapo anaposema afumbaye macho yake ni kuwaza yaliyopotoka,..alimaanisha afumbaye macho asitazame kweli (ambayo ni Neno la Mungu), linapomfundisha au kumwonya. Mtu huyo lengo lake ni kuendelea katika mawazo yake mabaya ya dhambi. Mfano aambiwapo kuishi na mke ambaye si wako ni uzinzi, na wazinzi sehemu Yao ni Katika ziwa la moto, lakini hataki kuliona au kulisikia Hilo andiko, jibu lake ni kuwa anataka kuendelea katika matendo yake ya giza.

Ndicho kilichokuwa Kwa waliompinga Yesu., Ndio maana akasema  maneno haya; 

Mathayo 13:15 Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema, 

Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya. 

Vilevile anaposema “Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya”

Anamaanisha, aizuiaye midomo yake kusema maneno ya uzima, ya staha, ya kujenga, ya adabu, ya maarifa, ya busara n.k.. Mwisho wake utakuwa ni kunena maneno mabaya tu.

Bwana alisema..

Luka 6:45

[45]Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake. 

Vivyo na hivyo na sisi, hatuna budi tujipime na kujichunguza…macho yetu hutazama Nini, vinywa vyetu vimejawa na maneno gani.? Lakini fahamu kuwa huwezi kushinda jicho lako, au ulimi wako ikiwa Kristo hajaumbika ndani yako.

Je! Unataka msaada Kwa Yesu Kristo? Kama jibu ni Ndio, basi unachopaswa kufanya cha kwanza ni kuyaachilia maisha yako kwake. Ili akusamehe dhambi zako. Ndipo akupe nguvu ya kushinda dhambi.

Hivyo bofya hapa Kwa ajili ya Mwongozo wa Sala ya Toba.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

NI WAKATI UPI UTAUONA USO WA KRISTO?

MWANANGU, NIPE MOYO WAKO;

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya mbingu na nchi zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe? (Mathayo 24:35).

Jibu: Turejee,

Mathayo 24:35  “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe”

Ili tuelewe vizuri, tutafakari kwanza mstari ufuatao…

Waebrania 13:8 “Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele”.

Mpaka maandiko yaseme kuwa “Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele”… Maana yake kuna watu, au vitu ambavyo haviwezi kuwa vile vile jana, leo na hata milele.

Kwa mfano mtu hawezi kuwa na tabia ile ile, au msimamo ule ule jana na leo na hata milele,..ni lazima tu utafika wakati tabia yake itabadilika, mtazamo wake utabadilika, utendaji wake utabadilika au hata msimamo wake!…. lakini KRISTO YESU yeye ni yule yule, kitabia, na kiutendaji, hajawahi kusema jambo halafu akajikosoa.. ni yeye yule na ataendelea kuwa vile vile Milele.

Hali kadhalika, vitu tunavyoviona katika mbingu kama jua, mwezi  na nyota, ijapokuwa tunaona vimedumu kuwa vilevile kwa maelfu ya miaka, lakini biblia inatabiri kuwa siku moja vitatoweshwa vyote…

Ufunuo 6:12 “Nami nikaona, alipoifungua muhuri ya sita, palikuwa na tetemeko kuu la nchi; jua likawa jeusi kama gunia la singa, mwezi wote ukawa kama damu,

13  na NYOTA ZIKAANGUKA juu ya nchi kama vile mtini upukutishavyo mapooza yake, utikiswapo na upepo mwingi.

14  MBINGU ZIKAONDOLEWA KAMA UKURASA ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake”.

Vile vile vitu tunavyoviona katika “NCHI” kama vile milima, na habari ambavyo tunaviona kama zimedumu kwa maelfu ya miaka, lakini bado biblia inatabiri kuwa siku moja vitafutika..

Ufunuo 16:20  “Kila kisiwa kikakimbia, wala milima haikuonekana tena”

Soma pia Ufunuo 21:1..

Lakini wakati ambapo vitu vyote hivi vinaondolewa (maana yake VINAPITA) Bado Kristo atabaki kuwa yeye yule, na maneno yake yatabaki kuwa yale yale, na yana nguvu ile ile katika umilele wote.

Kwamfano maneno ya Yesu anayosema yeye ni ALFA na OMEGA, yaani Mwanzo na Mwisho (katika Ufunuo 21:6 na Ufunuo 22:13) yataendelea kuwa hivyo hivyo Milele, hakuna wakati utafika Kristo ataacha kuwa Alfa na Omega…jua na mwezi na nyota na wanadamu watapita, lakini maneno hayo yataeendelea kuwa halisi hivyo hivyo milele na milele.

>Vile vile maneno yake aliyosema kuwa “Yeye ndio Njia, Kweli na Uzima (Yohana 14:6)” yataendelea kuwa hivyo milele na milele, hakuna wakati utafika ambao Kristo ataacha kuwa Njia, au ataacha kuwa  Kweli au ataacha kuwa Uzima..Kristo YESU sasa ni Uzima, na ataendelea kuwa UZIMA hivyo hivyo milele na milele.

>Vile vile aliposema kuwa yeye ni “Nuru ya Ulimwengu (Yohana 8:12)”…Maneno hayo hautafika wakati ambao yata-expire… Jua na mwezi kuna wakati vitaisha muda wake wa matumizi, jua litaondolewa halitamulika tena, na mwezi utaondolewa hautaangaza tena.. lakini Kristo ataendelea kuwa NURU hata kipindi ambacho jua na mwezi havipo..

Ufunuo 21:23  “Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, KWA MAANA UTUKUFU WA MUNGU HUUTIA NURU, NA TAA YAKE NI MWANA-KONDOO”.

> Vile vile maneno yake mengine yanamtaja yeye kama “Mwaminifu na wa Kweli (katika Ufunuo 3:14, na Ufunuo 19:11)”. Yeye atabaki kuwa hivyo Milele na milele, hakuna wakati ambao atabadilika na kukosa uaminifu!… Sisi wanadamu tunaoishi chini ya jua na juu ya nchi, tutakuwa waaminifu tu kwa kitambo Fulani lakini si milele. Lakini yeye ataendelea kuwa mwaminifu milele na milele hata wakati ambao mbingu zitafutwa, na kuletwa mbingu mpya na nchi mpya, bado ataendelea kuwa mwaminifu.

> Pia alisema wote wamwaminio yeye watakuwa na uzima wa milele, hakuna wakati hilo Neno litabadilika, kwamba awanyime uzima wa milele wale wote waliomwamini na kuishi kwa kuzifuata amri zake.. Majira yatabadilika, vipindi vitabadilika lakini milele na milele hawezi kujisahihisha maneno yake hayo. AKIAHIDI AMEAHIDI!!.. Na milele habadiliki.

Na maneno mengine yote yaliyosalia aliyoyasema BWANA YESU hakuna hata moja litapita!!! , yote yatabaki kuwa vile vile

Je umemwamini huyu Mkuu wa UZIMA asiyeweza KUBADILIKA?, Au Unawatumainia wanadamu ambao leo wapo na kesho hawapo, leo wanaahidi na kesho wamebadilika, leo wanakupenda kesho wanakuchukia.. Ni heri ukaanza kumtumainia yeye asiyeweza kubadilika, YESU KRISTO, MFALME WA WAFALME, na BWANA WA MABWANA.

Mungu akubariki.

Mafundisho Mengine

Mbinguni ni sehemu gani?

Kuna Mbingu ngapi?

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

INJILI YA MILELE NI IPI KATIKA BIBLIA?

Je! Sulemani alienda mbinguni?

Rudi Nyumbani:

 

 

Print this post

Gudulia ni nini? (1Samweli 26:11).

Jibu: Tusome,

1Samweli 26:11 “Hasha! Nisiunyoshe mkono wangu juu ya masihi

12 Basi Daudi akalitwaa lile fumo, na lile GUDULIA LA MAJI, kichwani pa Sauli; nao wakaenda zao, wala hapana mtu aliyeliona jambo hili wala kulijua, wala kuamka; maana wote walikuwa wamelala; kwa kuwa usingizi mzito kutoka kwa Bwana umewaangukia”.

Gudulia ni chombo maalumu kilivyotengenezwa kwa lengo la kuhifadhia maji ya kunywa ya watu wachache, kwa lugha ya sasa hivi tunayaita “majagi”

Magudulia/majagi ya zamani yalitengenezwa kwa malighafi tofauti na ya zama hizi. Zamani majagi/magudulia waliyatengeneza kwa kutumia udongo wa (mfinyanzi tazama picha juu), lakini sasa yanayotumika mengi yao yametengenezwa kwa glasi au plastiki.(tazama picha chini).

Gudulia ni nini?

Mistari mingine inayotaja chombo hiki (gudulia) ni pamoja na 1Wafalme 19:6, Yeremia 19:1 na Yeremia 19:10.

Je umemwamini Bwana Yesu?, je unajua kuwa tunaishi katika majira ya kurudi kwa YESU mara ya pili, na wakati wowote unyakuo wa kanisa utatokea?.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Shilo ni wapi?

TWEKA MPAKA VILINDINI.

WALA HAKUACHA MTU ACHUKUE CHOMBO KATI YA HEKALU.

Ni nani aliyemshawishi Daudi akawahesabu Israeli? Ni Mungu au shetani?

JINSI YA KUISHINDA HALI YA MSONGO WA MAWAZO.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “SAA INAKUJA” na “SASA IPO” (Yohana 4:23).

Jibu: Turejee,

Yohana 4:19  “Yule mwanamke akamwambia, Bwana, naona ya kuwa u nabii!

20  Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia.

21  Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.

22  Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.

23  Lakini SAA INAKUJA, NAYO SASA IPO, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba KATIKA ROHO NA KWELI. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu”.

Maana ya kumwabudu Baba katika roho na kweli, ni KUMFANYIA MUNGU IBADA, KATIKA ROHO MTAKATIFU NA KATIKA KWELI YA NENO LAKE.

Yohana 16:13 “Lakini yeye atakapokuja, huyo ROHO WA KWELI, ATAWAONGOZA AWATIE KWENYE KWELI YOTE…”

Sasa BWANA YESU aliposema kuwa “SAA INAKUJA”, alimaanisha kuwa kuna kipindi kinakuja  mbeleni, ambacho waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli, na wakati huo si mwingine Zaidi ya ule wa Pentekoste. Kipindi ambacho Roho Mtakatifu atamwagwa juu ya kanisa kwa mara ya kwanza, baada ya BWANA YESU kuondoka!.

Huo ndio uliokuwa mwanzo wa watu kumwabudu Baba katika roho na kweli. (Matendo 2:1-15)

Lakini pia aliposema kuwa..“NA SASA IPO”…. maana yake hata huo wakati tayari Baba ameshaanza kuabudiwa katika roho na kweli. Na aliyekuwa anamwabudu baba katika ROHO NA KWELI ni yeye mwenyewe BWANA YESU KRISTO. Kwasababu tayari alikuwa na Roho Mtakatifu ndani yake, ambaye alipoondoka ndipo akammwaga juu ya kanisa.

Yohana 16:7 “Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu”.

Na hata sasa tupo kipindi ambacho Neema ya Roho Mtakatifu bado ipo duniani kwa kila anayemwitaji sawasawa na Matendo 2:38, Na kumbuka Roho Mtakatifu pekee ndiye funguo za mtu kumwabudu Mungu katika roho na kweli, na pasipo yeye haiwezekani kumwabudu Mungu katika roho.

Kwa somo refu lihusuyo jinsi ya kumwabudu Mungu katika roho na kweli fungua hapa >>Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “Saa yangu haijawadia?”

Ni muda gani Bwana Yesu alisulibiwa. Je! Ni saa 3 au saa 6?

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

UWEZO WA KIPEKEE.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya  Mithali 21:1 Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana;

SWALI: Nini maana ya  Mithali 21:1

“Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana; Kama mifereji ya maji huugeuza po pote apendapo”.


JIBU: Kuna mithali inayosema “maji hufuata mkondo”. Ikiwa na maana, palipo na mfereji kule kule unapoelekea ndipo maji nayo huelekea. Mfano ukielekeza mrefeji shambani mwako, basi maji yale yataelekea huko si kwingineko, ukielekezea mfereji nyumbani mwako, basi maji yatakuja ndani mwako. Kamwe maji  hayajiamulii  pa kuririkia.

Vivyo hivyo na Mungu, ndivyo anavyofananisha mamlaka yake juu ya wafalme na wakuu wa dunia hii. Kwamba mashauri yao, hawajiamulii tu peke yao kwa kujitakia. Kwamfano utakumbuka kuna wakati  Mungu alimnyanyua Moyo Koreshi mtawala wa Uajemi ili awape ruhusu wayahudi warudi katika nchi yao wakamjengee nyumba.

Ezra 1:1 Ikawa katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, ili kwamba neno la Bwana alilolisema kwa kinywa cha Yeremia lipate kutimizwa, Bwana akamwamsha roho yake Koreshi, mfalme wa Uajemi, hata akapiga mbiu katika ufalme wake wote, akaiandika pia, akisema,  2 Koreshi, mfalme wa Uajemi asema hivi;  3 Basi kila mtu katika ninyi nyote mlio watu wake, Bwana, Mungu wake, na awe pamoja naye, na akwee mpaka Yerusalemu, ulioko Yuda, akaijenge nyumba ya Bwana, Mungu wa Israeli, (yeye ndiye Mungu), iliyoko Yerusalemu.  4 Na mtu awaye yote aliyesalia mahali po pote akaapo hali ya ugeni, na asaidiwe na watu wa mahali pake, kwa fedha, na dhahabu, na mali, na wanyama, zaidi ya vitu vitolewavyo kwa hiari ya mtu, kwa ajili ya nyumba ya Mungu, iliyoko Yerusalemu

Mungu huyo  huyo ndiye aliyemfanya mfalme Nebukadreza kuwa na moyo mkatili ili awachukue watu wake utumwani kwasababu ya makosa yao.(Yeremia 27:6, 43:10)

Mungu anaweza kuwatumia watawala kuadhibu taifa, au kuwabariki watu wake. Hii ni kuonyesha kuwa hakuna tawala yoyote katika hii dunia inamilikiwa na fikra za mwanadamu asilimia 100, bali mengi ya mashauri ya wakuu hutoka juu mbinguni, au yameruhusiwa na Mungu. Wao ni kama maji tu yanayofuata mkondo wa kusudi la Mungu.

Ndio jambo ambalo Mungu alimwambia Mfalme Nebukadreza kwamba “aliye juu ndiye anayetawala”(Danieli 5:21) lakini yeye alidhani ni uongo, mpaka siku alipoondolewa kwenye ufalme wake kwa miaka 7, na kurudishwa baadaye.

Hivyo, jambo hili, sio tu la viongozi wa kidunia, lakini pia hata wa kanisani. Ikiwa kanisa ulilopo linasimamia kweli na utakatifu na Kristo Yesu ndio kiini cha fundisho lao, basi waheshimu sana viongozi wako, kwasababu si kila shauri linalotoka kwenye vinywa vyao, ni wao wamefikiria. Wao ni kama maji tu yaliyomwagwa kwenye mfereji, ili kukuongoza wewe. ukishandana nao, au ukipuuzia kuongozwa nao, wakati mwingine unapingana na maamuzi ya Mungu wako bila kujijua.

Waheshimu viongozi wako wanaokulea kiroho, kama vile unavyowaheshimu watawala ya kidunia.

Bwana akubariki.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Fahamu maana ya Mithali 29:4 “Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.

Ni kwa namna gani Kristo analitakasa kanisa kwa Maji katika Neno? (Waefeso 5:26)

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

ITAMBUE KARAMA YA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Mabibi wastahiki walikuwa ni watu gani? (Esta 1:18).

(Mada maalumu kwa wanawake)

Jibu: Mabibi Wastahiki ni “wanawake wa heshima”.. kundi hili la wanawake lilihusisha wake za Wafalme, Maliwali au Maakida au Majumbe..

Wakati mfalme Ahasuero alipowafanyia maakida wake na maliwali wake karamu, biblia inatuambia kuwa Malkia Vashti (mke wa mfalme), yeye naye aliwafanyia wanawake (ambao ni wake wa hao maakida na maliwali) karamu.

Esta 1:2 “siku zile mfalme Ahasuero alipoketi katika kiti cha enzi cha ufalme wake, huko Shushani ngomeni;

3 mwaka wa tatu wa kumiliki kwake, ikawa aliwafanyia karamu maakida wake wote na majumbe wake; wakuu wa Uajemi na Umedi, watu wenye cheo na maakida wa majimbo, wakihudhuria mbele zake. 

4 Akawaonyesha utajiri wa ufalme wake mtukufu, na heshima ya enzi yake bora siku nyingi, maana siku mia na themanini……………………..

9 Tena Vashti, malkia, naye akawafanyia karamu WANAWAKE NDANI YA NYUMBA YA KIFALME YA MFALME Ahasuero”.

Sasa hao wanawake waliokuwa wake za “maliwali na maakida” ndio waliojulikana kama “mabibi wastahiki”.. wakiongozwa na Malkia Vashti.

Lakini tunachoweza kujifunza ni kuwa ile karamu ya hawa wanawake haikuwa na utukufu wowote, kwani iliishia kuleta aibu kubwa katika ufalme wote wa Uajemi. Kwani Malkia Vashti alikosa utii kwa Mfalme alipoitwa, na Zaidi sana alionyesha dharau hizo mbele ya Mfalme na waliwali wake wote.

Na huenda pia kiburi hicho kilichochewa na jopo la wale wanawake wengine wastahiki waliohudhuria karamu hiyo ya Malkia Vashti. Hiyo ikifunua kuwa hakuna cha maana walichokuwa wanakizungumza au kukipanga katika hiyo karamu Vashti aliyowaandalia, huenda yaliyokuwa yanazungumziwa kule ni UMBEA TU na kusema mapungufu ya waume zao!

Hiyo ikamfanya Vashti apoteze umalkia wake, na hata hao wanawake wengine ambao wastahiki kuzidi kutawaliwa na waume zao.

Esta 1:16 “Basi Memukani akajibu mbele ya mfalme na maakida, Huyu Vashti, malkia, hakumkosa mfalme tu peke yake, ila na maakida wote, na watu wote pia walioko katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero. 

17 Kwa maana tendo hilo la malkia litajulikana na wanawake wote, hata waume zao watadharauliwa machoni pao, itakaponenwa ya kuwa mfalme Ahasuero aliamuru Vashti, malkia, aletwe mbele yake, bali hakuja. 

18 Hata na leo hivi mabibi wastahiki wa Uajemi na Umedi waliokwisha kuzisikia habari za tendo lake malkia watawaambia vivi hivi maakida wote wa mfalme. Hivyo kutatokea dharau nyingi na ghadhabu tele.

 19 Basi mfalme akiona vema, na itoke kwake amri ya kifalme, nayo iandikwe katika sheria za Waajemi na Wamedi isitanguke, ya kwamba Vashti asifike tena mbele ya mfalme Ahasuero; na umalkia wake mfalme ampe mwingine aliye mwema kuliko yeye.

 20 Basi mbiu ya mfalme atakayoipiga itakapotangazwa katika ufalme wake wote, nao ni mkubwa, wake wote watawaheshimu waume zao, wakubwa kwa wadogo.

 21 Basi neno hili likawapendeza mfalme na maakida; naye mfalme akafanya sawasawa na neno lake Memukani.

 22 Kwa maana alipeleka nyaraka katika majimbo yote ya mfalme, kila jimbo kwa mwandiko wake, na kila taifa kwa lugha yake, ya kwamba kila mwanamume atawale nyumbani mwake, na kuitangaza habari hii kwa lugha ya watu wake”.

Tabia kama hii inaendelea mpaka leo kwa baadhi ya wanawake walioolewa!, ambao baada ya kuolewa wanawaona waume zao kama si kitu tena, na hata kupoteza UTII kwao!. Pasipo kujua kuwa kwa kufanya hivyo wanazidi kujipotezea nafasi zao ndani ya familia zao, kwani badala ya kuwa kichwa Mungu anawaweka kuwa wa mwisho.

Neno la Mungu linasema wanawake na wawatii waume zao.

1Petro 3:1 “Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;

2  wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu.

3  Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

4  bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.

5  Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, NA KUWATII WAUME ZAO”

Soma tena Waefeso 5:24 na Tito 2:5 utaona jambo hilo hilo, sasa mwana-mama unatolea wapi kiburi!!!. Badilika, na anza kuwa mtii, ikiwa haupo ndani yako, na hiyo ni kwa faida yako na familia yako. Kitabu cha Esta, huenda kingepaswa kiitwe kitabu cha Vashti, lakini kwa kiburi chake, umalkia wake akapewa Esta.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

ESTA: Mlango wa 5, 6 & 7

LITANIA YA BIKIRA MARIA JE! NI SALA YA KIMAANDIKO?

YESU ANAKWENDA KUIBADILISHA OFISI YAKE.

NI KIJIJI CHA AINA GANI UPO?

MAJESHI YA PEPO WABAYA.

Rudi nyumbani

Print this post

Kipuli ni nini, na kimebeba ujumbe gani?.(Mithali 25:12).

Jibu: Turejee,

Mithali 25:12 “KIPULI CHA DHAHABU, na pambo la dhahabu safi; Ndivyo alivyo mwonyaji mwenye hekima kwa sikio lisikialo”

“Kipuli” ni jina lingine la “hereni za masikioni”.

Neno hili limeonekana mara moja tu katika biblia, katika kitabu cha Mithali 25:12.

Na mwandishi wa Mithali (Sulemani) kwa hekima ya roho alipata kuelewa vipuli (hereni) sahihi wanazopaswa wavae watu, tofauti na hizi tuzijuazo.

Anasema… “KIPULI CHA DHAHABU, na pambo la dhahabu safi; Ndivyo alivyo MWONYAJI MWENYE HEKIMA KWA SIKIO LISIKIALO”.

Maana yake ni kuwa sikio linalosikia hekima kutoka kwa wenye hekima, linafananishwa na sikio lililovishwa hereni ya dhahabu au pambo la dhahabu.

Kwa lugha nyingine ni kwamba, kama tukitaka kupamba masikio yetu kwa vitu vya thamani, basi tuwe wasikilizaji wa maneno ya hekima. (Kwani maneno hayo yataonekana kama mapambo ya thamani katika masikio yetu).

Na maneno ya hekima hatuyapati pengine isipokuwa katika biblia takatifu (Humo ndimo tutakapopata lulu na mapamba ya thamani ya masikio yetu)..

Mithali 2:1 “Mwanangu, kama ukiyakubali maneno yangu, Na kuyaweka akiba maagizo yangu;

2 HATA UKATEGA SIKIO LAKO KUSIKIA HEKIMA, UKAUELEKEZA MOYO WAKO UPATE KUFAHAMU;

3 Naam, ukiita busara, Na kupaza sauti yako upate ufahamu;

4 Ukiutafuta kama fedha, Na kuutafutia kama hazina iliyositirika;

5 Ndipo utakapofahamu kumcha Bwana, Na kupata kumjua Mungu”

Soma tena  Mithali 4:20, Mithali 5:1, na  Mithali 22:17 utaona maneno yanayopatana na hayo..

Mithali hizi zinalingana kabisa na ujumbe wa Roho Mtakatifu tunaousoma katika kitabu cha 1Petro 3:3. Na 1 Timotheo 2:9.

1 Petro 3:3 “Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

4 BALI KUWE UTU WA MOYONI USIOONEKANA, KATIKA MAPAMBO YASIYOHARIBIKA; YAANI, ROHO YA UPOLE NA UTULIVU, ILIYO YA THAMANI KUU MBELE ZA MUNGU.

5 Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.

6 Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote”.

Mstari wa 4 unasema… “ BALI KUWE UTU WA MOYONI USIOONEKANA, KATIKA MAPAMBO YASIYOHARIBIKA; YAANI, ROHO YA UPOLE NA UTULIVU, ILIYO YA THAMANI KUU MBELE ZA MUNGU”.

Je ni vipuli gani vipo masikioni mwako?…vya chuma au vya maneno ya hekima?.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Rudi nyumbani

Print this post

Mashonde ni nini? (Ezekieli 4:15).

Swali: Mashonde ni kitu gani kama tunavyosoma katika Ezekieli 4:15, na yamebeba ufunuo gani?

Jibu: Turejee..

Ezekieli 4:12“Nawe utakila kama mkate wa shayiri, nawe utakioka mbele ya macho yao juu ya MASHONDE YATOKAYO KATIKA MWANADAMU”.

“Mashonde” ni jina lingine la “kinyesi kikavu” aidha cha mwadamu au mnyama.

Zamani na hata sasa katika maeneno baadhi, kinyesi kikavu kimetumika kama chanzo cha nishati, kwasababu kinawaka kwa haraka zaidi hata ya kuni, Hivyo kinaweza kutumika kama mbadala ya wa kuni kama kikiwa kwa wingi.

Katika maeneo ya mashariki ya kati, vinyesi vikavu vya ngamia na ng’ombe vilitumika kwa sana kama chanzo cha nishati, na nyakati chache chache sana (hususani vipindi vya ukame na dhiki), na vilitumika hata vya wanadamu lakini vyote vilikuwa ni vikavu….lakini sasa vinatumika hata vibichi kutokana na kukuwa kwa teknolojia.

Sasa tukirejea katika biblia, tunasoma Nabii Ezekieli akipewa maagizo na Mungu kuwa aoke mkate aina ya shayiri juu ya Mashonde (yaani kinyesi) cha mwanadamu, maana yake atumie kinyesi cha mwanadamu kama chanzo cha nishati, badala ya cha Wanyama. Sasa changamoto ya kutumia vinyesi, aidha vya mwanadamu au mnyama kama nishati ni “harufu”.

Maana yake kile kitakachopikwa juu ya mashonde(kinyesi) fulani kitabeba harufu ya kile kinyesi husika, kwahiyo kama mkate utaokwa juu ya kinyesi cha ngamia, basi ule mkate kwa sehemu utatoa harufu ya kinyesi cha ngamia, vile vile kama umeokwa juu ya kinyesi cha mwanadamu basi utatoa harufu ya kinyesi cha mwanadamu.

Hivyo Mungu alimwambia Ezekieli atumie kinyesi cha Mtu, kutengeneza huo mkate na kisha aule!.. Lengo la kumwambia vile si kumwadhibu Ezekieli, la! Kwani Ezekieli alikuwa ni nabii wa Mungu mwaminifu sana, hivyo aliambiwa afanye vile ili awe ishara kwa Taifa la Israeli kama Hosea alivyokuwa ishara kwa Taifa la Israeli alipoambia akaoe mwanamke wa uzinzi.

Maana yake kwa Ezekieli kula mkate uliookwa juu ya kinyesi cha mtu, ni ujumbe kwa wana wa Israeli kuwa na wao watakwenda utumwami mahali pa dhiki nyingi, na watapitia shida na njaa kali hata kufikia hatua ya kukosa chanzo bora cha nishati na hivyo kuona hata kinyesi chao wenyewe chaweza kufaa kwa nishati ya kuokea mikate ili tu waweze kuzishibisha nafsi zao wasife kwa njaa.

Hivyo Bwana Mungu alimchagulia Ezekieli hiyo ishara, lakini tunasoma Ezekieli alimsihi Bwana ambadilishie hiyo ishara kwani hakuwahi kula kitu najisi tangu amezaliwa, (kwasababu kulingana na desturi za kiyahudi kitu chochote kilichookwa juu ya kinyesi ni najisi), Hivyo akamsikia kwa ombi hilo, na Bwana Mungu akambadilishia, badala ya kutumia kinyesi cha mtu, basi atumie cha Ng’ombe, na ndivyo Ezekieli alivyofanya kama tunavyosoma…

Ezekieli 4:13 “Bwana akasema, Hivyo ndivyo wana wa Israeli watakavyokula chakula chao, hali kimetiwa unajisi, kati ya mataifa nitakakowafukuza

14 Ndipo nikasema, Ee Bwana MUNGU, tazama, roho yangu haikutiwa unajisi; maana tangu ujana wangu hata sasa sijala nyamafu, wala iliyoraruliwa na hayawani; wala nyama ichukizayo haikuingia kinywani mwangu.

15 Ndipo akaniambia, Tazama, NIMEKUPA MASHONDE YA NG’OMBE badala ya mashonde ya mwanadamu, nawe utakipika chakula chako juu ya hayo.

16 Tena akaniambia, Mwanadamu, tazama, nitalivunja tegemeo la chakula katika Yerusalemu; nao watakula mkate kwa kuupima, na kwa kuutunza sana; nao watakunywa maji kwa kuyapima, na kwa kushangaa;

17 wapate kupungukiwa na mkate na maji, na kustaajabiana, na kukonda kwa sababu ya uovu wao”.

Ni nini tunajifunza katika Habari hiyo?

Kikubwa tunachoweza kujifunza ni kuwa “tunapomwacha Mungu na kufuata mambo yote, tunajiweka katika hatari ya kuharibu Maisha yetu kuanzia ya rohoni mpaka ya mwilini”.  Wana wa Israeli hapa walimwacha Mungu na matokeo yake Maisha yao yaliharibika kwa njaa na umasikini na utumwa mpaka kufikia hatua ya kula mikate iliyookwa juu ya vinyesi vyao wenyewe, na ni hivyo hivyo hata leo, (kwasababu Mungu ni yule yule hajabadilika)… kama tukigeuka na kufuata mambo yetu, basi Maisha yetu yataharibika hata zaidi ya hayo ya wana wa Israeli nyakati hizo.

Je umempokea YESU KRISTO, kama Bwana na Mwokozi wa Maisha yako?

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

EZEKIELI, ITABIRIE MIFUPA MIKAVU.

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

Roho Mtakatifu ni nani?.

Kuna tofauti gani kati ya  “Edeni” na “Adeni”?

Bawa la mbuni hufurahi; Lakini mabawa yake na manyoya yake, je! Yana huruma? 

Rudi nyumbani

Print this post