Amri ya kwanza tuliyopewa na Bwana, ni kumpenda yeye kwa mioyo yetu yote, kwa nguvu zetu zote na kwa akili zetu zote, na nyingine inayofanana na hiyo ni kupendana sisi kwa sisi. Kila mmoja kumchukulia mwenzake bora kama nafsi yake mwenyewe. Lakini mtu mmoja alimuuliza Bwana, jirani yangu ni nani…akiwa na maana kuwa nini maana ya ujirani?.
Ndipo Bwana akatoa mfano ambao tunausoma katika Luka 10.
Luka 10:25 “Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?
26 Akamwambia, Imeandikwa nini katika torati? Wasomaje?
27 Akajibu akasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako.
28 Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi.
29 Naye akitaka kujidai haki, alimwuliza Yesu, NA JIRANI YANGU NI NANI?
30 Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa.
31 Kwa nasibu KUHANI mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando.
32 Na MLAWI vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando.
33 Lakini, MSAMARIA mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia,
34 akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza.
35 Hata siku ya pili akatoa dinari mbili, akampa mwenye nyumba ya wageni, akisema, Mtunze huyu, na cho chote utakachogharimiwa zaidi, mimi nitakaporudi nitakulipa.
36 Waonaje wewe, katika hao watatu, ni yupi aliyekuwa jirani yake yule aliyeangukia kati ya wanyang’anyi?
37 Akasema, Ni huyo aliyemwonea huruma. Yesu akamwambia, Enenda zako, nawe ukafanye vivyo hivyo”.
Katika mfano huu tunajifunza, makundi matatu ya watu, wa kwanza ni KUHANI, wa pili MLAWI, na watatu ni MSAMARIA.
Kama tunavyofahamu kuhani ni mtu aliyekuwa ametiwa mafuta na Mungu kuhudumu katika nyumba ya Mungu, ni mtu aliyemkaribia Mungu sikuzote, kwa kazi ya kufukiza uvumba na kufanya upatanisho kwa makosa ya watu wa Mungu, katika patakatifu. Ni mtu mwenye bidii ya kumtumikia Mungu usiku na mchana, kiufupi ni mtu aliyeheshimika mbele za Mungu na mbele za wanadamu. Lakini ilipokuja katika jambo dogo kama hili, aliikosa shabaha, pengine alijua kumtumikia Mungu ni hekaluni tu na kwenye masinagogi! mahali penye mikusanyiko mikubwa ya watu wengi. Hakufanya vibaya, ni kwasababu hakupata ufunuo wa neno “JIRANI HASA NI NINI?”. Yeye alidhani kuwa kule aendako ndipo majirani zake walipo.
Kadhalika na yule Mlawi nae, kumbuka mlawi naye anafanya kazi zinazofanana na za kikuhani katika nyumba ya Mungu, isipokuwa yeye haingii katika patakatifu pa Mungu, tofauti ya Mlawi na Kuhani ni kwamba Kuhani yeye ni Mlawi aliyeteuliwa kutenda kazi katika patakatifu pa Mungu, hivyo kwa cheo huwa anaanza Mlawi, kisha kuhani, na mwisho kabisa ni Kuhani Mkuu. Sasa huyu naye alipomuona yule mtu mwenye majeraha, pengine huruma ilimjia kidogo, lakini alipogundua kuwa hizo sio kazi za Walawi, akaamua naye kupita kando. Naye pia hakufanya kosa, ni kwasababu tu hakupata ufunuo wa “JIRANI HASA NI NANI?”.
Lakini tunamsoma mwingine wa mwisho ambaye ni MSAMARIA. Kumbuka katika Israeli kulikuwa na Eneo linaloitwa Samaria na watu waliokuwa wanaishi kule walikuwa ni watu ambao sio wayahudi kamili, ni kama mchanganyiko wa watu wa mataifa na wayahudi, hivyo walikuwa nao wanaishika torati ya Musa japo wayahudi walikuwa hawawaatambui wala kuchangamana nao. Ni watu ambao hawakuruhusiwa kuingia au kuhudumu katika nyumba ya Mungu kwa namna yoyote ile, ni kama watu-baki au najisi mbele za wayahudi lakini walikuwa wanamjua Mungu na baadhi yao wanamcha.
Hivyo huyu Msamaria naye alipokatiza katika njia ile. alimuona yule mtu mwenye majeraha na “KUMUHURUMIA”, na pasipo kujali yule mtu ni wa namna gani, au ni kwasababu gani kapata hayo matatizo, yule msamaria akaghairi yote, pengine shughuli zake za kumwingizia kipato, ili tu aokoe maisha ya yule mtu kwa ule wakati. Hivyo kama tunavyosoma akayafunga majeraha yake, na kuyatia MAFUTA NA DIVAI. Kisha akaona hiyo tu haitoshi akampeleka hospitali, kwa gharama zake mwenyewe akamuuguza mpaka alipopona.
Na ndipo baada ya mfano huo Bwana Yesu akamuuliza yule mwanasheria ni yupi aliye JIRANI YAKE?. Naye akajibu; NI yule aliye MUHURUMIA(Msamaria).
Na sisi tunajifunza nini hapo?.
Katika hali tulizopo ni rahisi kudhani kuwa kuhudumu katikati ya umati mkubwa ndio chachu ya kudhani Mungu anakuona una upendo kwa jirani zako! lakini nini maana hasa ya kuwa JIRANI kwa mwenzako?.. Tukijifunza katika hiyo mifano hapo tunaona ni yule aliyekaribu sana na wewe, na unaona anahitaji msaada wa haraka sana kutoka kwako huyo ndiye jirani yako. Yule Kuhani na yule Mlawi walidhani umati mkubwa wa watu wanaowatumikia kule kila siku ndio wanaweza wakawa majirani zao. Lakini mtu alipotokea mbele yao ghafla mwenye uhitaji mkubwa na wa haraka kuliko wale, wakapita kando. Na mtu asiyemjua Mungu sana ndiye akaja kumsaidia.
Vivyo hivyo na sisi hatuhitaji tuwe wahubiri wakubwa, tunahubiria mamilioni ya watu ndipo tuonekana tuna upendo mkubwa kwa ndugu zetu mbele za Mungu.. Hauhitaji kwenda masafa ya mbali kuhubiri ukidhani kuwa hichi ni kipimo cha kuonyesha kuwa una upendo mkubwa kwa ndugu zako wakati jirani yako hapo karibu nawe yupo katika hali ya dhambi, na hamjui huyo Mungu unayekwenda kumuhubiri ulaya.
Unao rafiki zako ni makahaba, au walevi au waabudu sanamu. unawaacha waangamie unasema mimi nataka nikahubiri makanisani na kwenye makongamano tu…unachofanya sio dhambi lakini bado hujaonyesha ule upendo kwa jirani yako kama Mungu anavyotaka.
Lakini yule msamaria alimpaka mafuta na divai na kufunga majeraha yake, na baadaye akampeleka kwa matabibu wamtunze. Kadhalika na sisi tunapaswa tuwatazame ndugu zetu wote waliokaribu na sisi sana ambao wapo katika dhambi wamepigwa na kutiwa majeraha na shetani, tunapaswa kuwatia mafuta na divai, kwa kuwahubiria habari njema ili wapokee Roho Mtakatifu kisha wakishapokea Roho ndipo tuwapeleke kwa viongozi wa kiroho wawakuze. Na kwa kufanya hivyo Tutakuwa tumekidhi vigezo vya kuwapenda jirani zetu kama nafsi zetu. Japo mbele za wanadamu unaweza ukaonekana hujafanya kitu lakini mbele za Mungu, ni mtu mwenye maana sana.
Mungu akubariki.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
MPENDE JIRANI YAKO KAMA NAFSI YAKO.
NITAONGEZAJE NGUVU ZANGU ZA ROHONI?
JE! BIKIRA MARIA NI MALKIA WA MBINGUNI?
Ili kuelewa uzito wa Neno hili “KUZALIWA MARA YA PILI”, Ni vizuri tukarejea katika maisha ya kawaida kujifunza vitu gani vinaambatana na kuzaliwa kwa mtu. Mtu kabla hajazaliwa sehemu kubwa ya maisha yake yanakuwa yameshaandaliwa na vizazi vilivyomtangulia ni machache sana ambayo atakuja kuyaongeza yeye mwenyewe atakapozidi kukua, lakini asilimia kubwa mambo yake yanakuwa yameshakamilika.Na ndio maana inakuwa rahisi kumtabiri mtu atakuja kuwa wa namna gani kabla hata hajazaliwa.
Kwamfano wewe kabla hujazaliwa ndugu zako walishajua kabisa utakuja kuwa mwafrika mwenye rangi nyeusi, na nywele za katani, na sio mchina au mzungu! na ndivyo ilivyokuja kuwa baada ya kuzaliwa kwako, hivyo hawakushangaa kukuona wewe uko jinsi ulivyo leo. Lakini Kwanini hawakustaajabia kukuona hivyo, ni kwasababu mababa zako na wenyewe wako hivyo hivyo kama wewe,
Kadhalika kama jamii yenu ni watu warefu au wafupi, ni rahisi watu kutabiri kimo chako kabla hata hujazaliwa. Pia Kama familia yenu ni ya kifalme, ni rahisi watu kutabiri kuwa utakuwa mfalme kabla hata hujazaliwa..na siku utakapokuwa mtu mzima na kuwa mfalme hawatastaajabia kukuona wewe hivyo.
Ni kwasababu gani?. Jibu ni kwamba wameweza kusoma ukoo wako, na kuangalia tabia za mababa zako na mwenendo wao, na vyeo vyao wakaweza kuhitimisha maisha yako yatakavyo kuja kuwa. kadhalika na vitu kama majina,mtu kabla hajazaliwa watu wataishiakumuita majina ya ukoo kama Massawe, Wambura, Lema, Laiza, n.k. ni kwasababu gani?. Jibu ni kwasababu ni lazima aje kuyarithi kutoka kwa mababa zake, Vivyo hivyo kama mababa wana magonjwa fulani ya kurithi, au tabia au laana fulani ni rahisi kutabiri hali ya mtoto atakayezaliwa itakuwaje mbeleni.
Tukirudi katika mambo ya rohoni kuna kuzaliwa pia mara ya pili. Na ukishazaliwa mara ya pili moja kwa moja unaingizwa katika ukoo husika ambao utakufanya urithi kila kitu kinachohusiana na ukoo huo. Kuanzia jina, tabia, cheo, mwenendo n.k.
Ukiamua leo hii kwa moyo wako wote kujiunga na Dini ya UBUDHA, kwa kufata taratibu zao walizokuwekea moja kwa moja utakuwa umezaliwa na kujiingiza katika Ukoo wa Budha, hivyo mambo yote yamuhusuyo Bhuda utabeba na ndio maana huwezi kushangaa kwanini wale mabudha wote wanafanana,. kimavazi, kimienendo na kitabia ni kwasababu wamezaliwa humo katika roho..Kadhalika na dini nyingine zote na vikundi vyote viwe vya kishirikina n.k..
Lakini pia kuna kuzaliwa mara ya pili katika ukoo unaoitwa UKOO wa YESU KRISTO. Huu ni ukoo ulio juu sana kuliko koo zote, ni uzao mteule, wa kifalme wa Mungu mwenyewe, Huku nako watu wanazaliwa. Lakini kabla mtu hajaamua kuzaliwa katika huu ufalme ni lazima ajue ni nani anayemzaa, pili jina la ukoo wake ni lipi, tatu tabia za huo ukoo ni zipi, nne, je! ataweza kuendana nazo?. Kumbuka jina la ukoo huo Ni YESU KRISTO huo ndio msingi kukutambulisha kwamba wewe ni unamilikiwa na mwenye huo ukoo. kwasababu biblia inasema.
Matendo 4: 12 “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo. “
Hivyo hatua ya kwanza ya kuzaliwa kama tunavyojua wakati wa utungu kwa mwanamke huwa yanaanza kutoka kwanza maji, kisha damu baadaye kiumbe, kadhalika katika roho mtu anapodhamiria kuzaliwa mara ya pili kwa KUTUBU kabisa kwa kumaanisha kuziacha dhambi, anapaswa akabatizwe kwanza katika ubatizo sahihi wa MAJI MENGI.. Na ni lazima abatizwe kwa JINA LA YESU KRISTO..Zingatia hilo JINA YESU huo ndio msingi wa kukutambulisha wewe kuwa umezaliwa katika ukoo wa Yesu. Kumbuka wengi wanabatizwa kwa jina la Baba, mwana na Roho Mtakatifu kimakosa. Mitume hawakufanya hivyo soma
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja KWA JINA LAKE YESU KRISTO, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.
Soma pia (Matendo 8:16, 10:48, na 19:5) utathibitisha jambo hilo. Hivyo unapobatizwa kifasaha baada ya kutubu dhambi zako, zinakuwa zinaondolewa na unakuwa umeingizwa katika Ukoo wa kifalme, Sasa hatua ya mwisho ni kupokea Roho Mtakatifu mpaka hapo utakuwa una uhakika kuwa wewe ni mwana wa YESU KRISTO.
Kuanzia hapo unakuwa umepanda daraja una haki zote za kukanyaga nguvu zote za yule adui, kwa Jina la YESU na hakuna lolote litakalokusumbua kwasababu umepewa mamlaka yote ya kifalme. Lakini haishii hapo, baada ya kuzaliwa unaanza kurithi zile tabia za ukoo huo uliouingia. Mfano BABA yako YESU KRISTO alipenda kuishi maisha matakatifu, wewe nawe utaanza kujiona mwenyewe unachukia maisha ya uovu, utaanza kuona hamu ya pombe, sigara, uasherati, rushwa, wizi, utukanaji, tamaa vinaanza kuisha, ndani yako pasipo hata kujilazimisha au kutumia nguvu,..
Ni kwasababu gani? jibu ni kwamba zile tabia za Baba yako YESU zinaanza kujidhihirisha ndani yako pasipo hata wewe mwenyewe kuamua hivyo. Huu ndio uwezo wa kufanyika mwana unaotoka kwa Mungu aliouzungumzia katika
Yohana 1: 12 ” Bali wote waliompokea ALIWAPA UWEZO wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;
13 waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu”.
Kadhalika kama Baba yako(YESU), na mababa (mitume na manabii) walikuwa wanatabia za unyenyekevu, tabia za kusali, kufunga, kuwapelekea wengine habari njema, n.k. vivyo hivyo na mtoto naye atarithi tabia hizo, na zitatoka zenyewe ndani pasipo kulazimishwa kwasababu hizi unazaliwa nazo, haujifunzi..na ndio maana ya Neno hatuishi chini ya sheria, kwasababu sheria ya Mungu imefungwa ndani ya mioyo yetu haitutawali inatoka yenyewe.
Kadhalika pia kama baba yetu YESU alichukiwa na ulimwengu, vivyo hivyo na watoto pia watarithi na hayo..kwasababu yeye mwenyewe alitangulia kuwaonya akisema “mtakuwa watu wa kuchukiwa na mataifa yote kwa ajili ya jina langu”..
Lakini huu UWEZO hauji hivi hivi na ndio maana tunasema kuna watu WALIOJIUNGA na watu WALIOZALIWA. Wengi wanasema wamezaliwa mara ya pili, lakini hawajazingatia hatua za kuzaliwa mara ya pili, ikiwa na maana kuwa hawajatubu dhambi zao kwa kumaanisha kuziacha, na hawajabatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa, na kwa jina la YESU KRISTO.
Hivyo zile tabia za kurithi maisha ya YESU KRISTO haziwezi kuonekana ndani yao, hawa ndio waliojiunga badala ya kuzaliwa. Watajilazimisha kuwa kama wakristo, watajilazimisha waache uasherati watashindwa, watajilazimsha waache sigara, pombe, watashindwa kwasababu wao wamejiunga na sio kuzaliwa.
Biblia inasema
1Yohana 3:9 “Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, KWA SABABU UZAO WAKE WAKAA NDANI YAKE; wala hawezi kutenda dhambi KWA SABABU AMEZALIWA KUTOKANA NA MUNGU ”.
Unaona hapo? Ule UZAO WA MUNGU unakaa ndani yako. Lakini kama haupo ndani yako kamwe hutakaa uweze kuishinda dhambi au kumshinda shetani.
Hivyo ndugu, kumbuka dunia nzima na vizazi vyote vinajua, kuwa hakuna UFALME mwingine zaidi ya Ufalme wa YESU KRISTO. Huo ndio unaomiliki sasa dunia, na ndio utakaokuja kumiliki baadaye. Ndugu BWANA YESU sio mtu wa kawaida kabisa, sasahivi tunavyoongea anamiliki Mbingu zote, malaika wote, na sayari zote, na dunia yote, na kuzimu yote, na tunavyovijua na tusivyovijua,.amekaa katika mbingu za mbingu asikoweza kufika mtu yeyote huko sio malaika yoyote au mwanadamu. Na atakuja tena kuwachukua walio wake ikiwa na maana ule UZAO WAKE. kwenda kumiliki vyote naye, watu wa milki yake milele na milele..
Kwanini ukose baraka zote hizo, kwa mambo yasiyokuwa na maana ya kitambo tu?. Siku ile wenzako wanaenda kung’aa kama Jua kama yeye alivyo wewe utakuwa wapi ndugu?. Bwana Yesu alisema dhahiri kabisa, katika..
Yohana 3: 5 ” Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.
6 Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.
7 Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili”.
Hivyo ndugu fanya juu chini uzaliwe mara ya pili kabla mlango wa neema haujafungwa.
Ubarikiwe.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?
JE! MKRISTO ANARUHUSIWA KULA NGURUWE, NA KUVUTA SIGARA NA KUNYWA POMBE?
Utaketi pamoja na Ibrahimu katika ufalme wa Mungu katika siku ile?. Ni vigezo gani vitakufanya ukidhi viwango vya kufanana na Ibrahimu. Jibu lipo dhahiri ni IMANI. Unapaswa uwe na imani kama ya Ibrahimu, Ikiwa na maana kuwa uyachunguze maisha yake, Jinsi alivyoenenda mbele za Mungu kwa IMANI na uyaige. Sio kuiga alichokifanya, bali ni kuiga mwenendo wake.
Ibrahimu alimchukulia Mungu, au ALIMUHESABIA Mungu kuwa anauwezo wa kufanya mambo yote. Aliweza kuamini vitu visivyowezekanika, na ndio maana aliweza kutembea na Mungu kwa muda wote ule pasipo kujikwa kwaa, aliamini Mungu angeweza kumpa mtoto hata kama akiwa na miaka 100 au 1000, kwasababu aliufahamu ukuu wake, hivyo hakudhubutu kumwekea Mungu mipaka, kwamba hapa anaweza, na hapa hawezi. Na alipopewa mtoto Bwana akamuhitaji kwa ajili ya dhabihu,.Lakini Ibrahimu hakusua sua kuuliza mara mbili, kwasababu alijua Mungu anaweza hata kumfufua tena mtoto wake na kumrudisha kutoka katika wafu.
Waebrania 11: 17 ” Kwa imani Ibrahimu alipojaribiwa, akamtoa Isaka awe dhabihu; na yeye aliyezipokea hizo ahadi alikuwa akimtoa mwanawe, mzaliwa pekee;
18 naam, yeye aliyeambiwa, Katika Isaka uzao wako utaitwa,
19 AKIHESABU YA KUWA MUNGU AWEZA KUMFUFUA HATA KUTOKA KUZIMU; akampata tena toka huko kwa mfano. “
Ibrahimu alizingatia vitu kama hivyo AKIMUHESABIA Mungu anaweza mambo yote, na ndio maana hadi leo hii anaitwa Baba wa Imani. Na wote wenye Imani zinazofanana na hiyo yake wataitwa WANA WA IBRAHIMU, na watarithi ahadi zile zile Ibrahimu alizoahidiwa na Mungu.
Hivyo Mungu anapendezwa na watu wenye kumwamini kwa asilimia zote, Kuna mahali Bwana Yesu alipokuwa anafuatwa na makutano makubwa ya watu, alikutana na akida mmoja, aliyemshangaza sana..tusome.
Mathayo 8:5-13
“5 Hata alipoingia Kapernaumu, akida mmoja alimjia,
6 akamsihi, akisema, Bwana, mtumishi wangu amelala nyumbani, mgonjwa wa kupooza, anaumwa sana.
7 Yesu akamwambia, Nitakuja, nimponye.
8 Yule akida akamjibu, akasema, Bwana, mimi sistahili wewe uingie chini ya dari yangu; LAKINI SEMA NENO TU!, na mtumishi wangu atapona.
9 Kwa maana mimi nami ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, mwenye askari chini yangu; nikimwambia huyu, Nenda, huenda; na huyu, Njoo, huja; na mtumwa wangu, Fanya hivi, hufanya.
10 Yesu aliposikia hayo, alistaajabu, akawaambia wale waliomfuata, Amin, nawaambieni, SIJAONA IMANI KUBWA NAMNA HII, KWA YE YOTE KATIKA ISREALI.
11 Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao WATAKETI PAMOJA NA IBRAHIMU, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni;
12 bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
13 Naye Yesu akamwambia yule akida, Nenda zako; na iwe kwako kama ulivyoamini. Mtumishi wake akapona saa ile ile”.
Kumbuka akida huyu hakuwa myahudi (mwisraeli), au mtu aliyeijua torati ya Musa, hapana bali alikuwa ni mtu wa mataifa, tena Mrumi, jamii ya watu wa Pontio Pilato isipokuwa yeye alikuwa na hofu ya Mungu tofauti na wale wengine. Wakati huo aliposikia kidogo tu ya Kwamba Bwana YESU anaponya wagonjwa na kufufua wafu na kutenda miujiza… moja kwa moja akafahamu ule ni uweza mkubwa wa Mungu. Hivyo akamwamini kwa KUMUHESABIA, kuwa ataweza kufanya pia na mambo ambayo yanaonekana hayawezekani machoni pa watu.
Tofauti na desturi za watu wengine, ambao walitaka mpaka waende kuwekewa mikono na Bwana Yesu, ndio waamini kwamba wataponywa, wengine mpaka watembelewe manyumbani kwao ndipo waamini, wengine mpaka waone kwanza ishara ndipo waamini.
Lakini huyu moja kwa moja alisema “sema Neno tu na mtumishi wangu atapona”..Na jibu la Bwana lilikuwa ni ” Sijaona imani kubwa namna hii, kwa ye yote katika Israeli. “…Imani hii iliwavuka wayahudi wote wa Israeli, iliwapita makuhani wote ambao kwa wakati huo walikuwa wanavukiza uvumba katika nyumba ya Mungu..Imani kama ya Ibrahimu Iliwapita mitume wa Yesu ambao kila siku walikuwa wanatembea naye..Iliwapita mafarisayo na waandishi na wazee wote wa Israeli wenye hekima na ujuzi wa torati, iliwapita hata yale makutano makubwa yaliyokuwa yanamfuata Yesu pale.
Na haikuishia hapo tu, Bwana alisema pia.
” 11 Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni;
12 bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno “
Umeona hapo, watatoka wengine wengi kutoka pembe 4 za dunia, ikiwa na maana kuwa watatoka watu sehemu zisizojulikana zilizodharauliwa, sehemu ya watu wasiokuwa na maana, pengine wasiojulikana na kanisa, watu wasio na umaarufu n.k. hao wote watakuja kuketi na Ibrahimu yaani watashiriki pamoja baraka Mungu alizomuahidia Ibrahimu. kwasababu wameonekana kuwa na Imani kama ya Ibrahimu mfano wa yule akida.
Ukichunguza kwa karibu utaona kuwa Bwana alikuwa katika utaratibu wa kuwaponya watu wote waliokuwa wanamfuata lakini hakuwa anazungumza chochote baada ya kuwaponya, kwasababu hakuona kitu kingine cha ziada ndani yao. Lakini kwa akida aliona kitu cha ziada, vivyo hivyo na kwa yule mwanamke aliyekuwa anatokwa na damu kwa muda wa miaka 12 (Luka 8:43), aliona makutano wote wanataka njia zile zile za kuponywa tu, kuwekewa mikono, kutembelewa nyumbani, kuombewa, wengine walishatuma maombi ya kumwona Bwana pengine mwezi mmoja kabla, wengine walikuwa wameshamaliza ngazi za chini, wameshatoka kuwaona mitume, sasa wanakaribia ngazi ya juu ya kumfikia YESU, n.k.
Lakini yeye alisema kwanini nipitie shida zote hizo,pengine angetaka kusubiria mpaka zamu yake ifike ingemchukua mwaka mzima, isitoshe kulikuwa na watu wenye matatizo makubwa hata kuliko yeye, lakini yeye alisema “nikishika pindo la vazi lake tu nitapona saa hiyo hiyo”, ALIMUHESABIA kuwa kama mikono yake inaponya kwanini na vazi lake lisiponye pia?. Kadhalika na yule mwanamke wa Tiro (Mathayo 15:21), Kadhalika na Zakayo naye. n.k.
Lakini leo hii wengi, tunataka tumfikie BWANA kwa njia zile zile za makutano, kumbuka hata leo jambo lile lile linajirudia Bwana Yesu kazungukwa na makutano mengi,(Mabilioni ya watu duniani) kila mtu anataka kumwona Bwana, kila mtu anataka kuponywa, kila mtu anataka kupewa hitaji la moyo wake. n.k. Fahamu tu, mpo wengi wenye shida za kukutana na BWANA. Na wote amewaahidia kuwaponya kwa majira yake, lakini je! ni wangapi kati ya hao wanaugusa moyo wa BWANA, kwa mfano wa yule AKIDA, au yule mwanamke aliyekuwa anatokwa damu? Kiasi cha kufikia kuahidiwa kuketi pamoja na Ibrahimu katika ufalme wa mbinguni?.
Unapopata shida, au unapokuwa na mahitaji fulani kwanini jambo la kwanza unakimbilia kwa watumishi au wachungaji wakuombee?, Wewe kwani Mungu wako hayupo?, kwanini unakimbilia mataifa mengine au Israeli kutafuta suluhisho la matatizo yako, angali Bwana wako yupo karibu na wewe hapo ulipo? Fanya tu kitu cha ziada ndugu, MUHESABIE BWANA, kama anauwezo wa kumtumia mtumishi fulani kuniponya, vivyo hivyo anaweza akanitumia mimi mwenyewe kwa kinywa changu kunitimizia mahitaji yangu. Mungu hana ngazi, kwamba ukitaka umfikie yeye sharti uanze kwanza kwa shemasi kisha mchungaji halafu Mungu. hapana. Akitoka Mungu ni wewe. Sio Padri, wala kasisi wala Nabii anapaswa kuwa kiunganishi chako wewe na Mungu. Yesu pekee ndiye anayesimama hapo katikati.
Pengine watu walimdhihaki yule akida, anachezea nafasi ya kipekee ya kutembelewa na Bwana nyumbani kwake, lakini badala yake Mungu ndiye aliyependezwa na yeye kuliko watu wote. Vivyo hivyo wengine wanatamani mpaka watokewe na YESU au Malaika,au watembelewe na mchungaji ndipo waamini, na kuanza kumtumikia Mungu, wakidhani kuwa hayo ndio mapenzi ya Mungu. Lakini wapo ambao hawatayaona hayo wala hawatayahitaji hayo yote, na watakumpendeza Bwana na kuketi pamoja na Ibrahimu siku ile. Na wana wa Ufalme (ambao wangepaswa wenyewe ndio wawe vielelezo) watatupwa nje.
Hivyo ndugu yangu, tujitahidi sote, tupige mbio tufikie vile viwango vya IMANI kama ya ibrahimu ya kumpendeza Mungu kwa kufanya kitu cha ziada kwake, njia ambazo hazijazoeleka na wengi na hii haiji isipokuwa kwa KUMUHESABIA Mungu kuwa anaweza yote, anaweza kufanya mambo yasiyowezekanika.
Mungu akubariki.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali share kwa wengine ujumbe huu na Mungu wetu atakubariki.
Mada Nyinginezo:
NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?
JE! INAKUBALIKA KUMTOLEA MTU MWENGINE DAMU?(BLOOD TRANSFUSION).
Habari za Elifazi, Sofari, na Bildadi tunazipata katika kitabu cha Ayubu, kama wewe ni msomaji wa biblia utakumbuka kuwa walikuwa ni marafiki wa Ayubu wa karibu sana waliokuja kumlilia pale alipopatwa na yale matatizo ambayo tunayoyasoma kwenye biblia. Lakini kabla ya hao kuja tunasoma pia Ayubu alikuwa ni MWELEKEVU sana aliyemcha Mungu na kuepukana na uovu wa kila namna, na baada ya shetani kuona wivu juu yake,ndipo akaamua kwenda kumshitaki kwa Mungu, ajaribiwe ili aiache Imani yake. Kama tunavyofahamu, baadaye Mungu alimruhusu shetani amjaribu Ayubu. Na ndipo shetani akaenda kuzimu kuandaa MAJARIBU yake mazito MATATU(3), ambayo katika hayo alipata uhakika kabisa kwamba Ayubu hawezi kunusurika ni lazima amkane Mungu na kuachana na uelekevu wake. Embu tuyapitie kwa ufupi.
Jaribu la kwanza lilikuwa ni la nje ya mwili wake na nafsi yake:
Hili lilihusisha vitu vyote vilivyomzunguka Ayubu, vitu kama mali zake, wanyama wake, biashara zake pamoja na watumwa wake, n.k. Hawa wote shetani aliwapiga kama tunavyosoma habari katika Ayubu sura ya 1, lakini hakuishia hapo alizidi kupiga kufikia hatua kuwaua mpaka na watoto wake, na kumfanya Ayubu abaki peke yake, Lakini shetani alipoona hayo majaribu bado hayamtikisi Ayubu kwa namna yoyote zaidi ya yote aliishia kulibariki jina la BWANA. ibilishi akakusudia kubadilisha kinyago na kuamia kwenye ngazi ya juu iliyo nzito zaidi. (lile Neno linatimia mtu hujaribiwa kulingana na Imani yake.)
Jaribu la Pili lilikuwa ni katika mwili wake:
Tunasoma shetani alianza kumpiga Ayubu kwa magonjwa ya ajabu, majipu yaliyozuka mwili mzima yalimfanya Ayubu kufikia hatua ya kukonda sana na kukaa kwenye majivu muda wote akijikunia vigae. Kumbuka hili ni jaribu baya zaidi kuliko lile la kwanza kwasababu hili lilimuhusu yeye moja kwa moja. Afya yake ilidorora ghafla hivyo aliona kama mlango wa mauti unamwita muda wowote. Lakini pamoja na hayo Ayubu aliushikilia uelekevu wake, hatua hii ndiyo iliyomfanya hata mke wake Ayubu amkufuru Mungu, kwa kuona kuwa huyo Mungu waliyekuwa wanamtumainia kwa hatua hiyo waliofikia sasa hana msaada wowote kwao, kwa mume wake na kwa familia yake, Hivyo hakuna sababu ya kumtumikia tena. Lakini alizidi kuvumilia kwa muda mrefu na shetani alipoona ameshindwa, akaamia kwenye hatua nyingine ya juu zaidi ambayo ndiyo ngumu na ya hatari kuliko zote kiasi kwamba ingekuwa ni rahisi Ayubu kuchukuliwa na shetani kama asingesimama kikamilifu na Mungu wake. Hii ndio silaha ya mwisho shetani anayoitumia kuwamaliza watu wa Mungu. Na hakuna nyingine iliyojuu ya hiyo.
Jaribu la Tatu lilikuwa la rohoni:
Kule Ayubu alipokuwa anapashikilia ndipo, hapo hapo shetani alipopajia. Kumbuka kitabu cha Ayubu sehemu kubwa kinaeleza juu ya hili jaribu la tatu, ambalo ndio msingi na kila mtu anapaswa afahamu kwasababu hapo ndipo siri hii ilipokaa, (hivyo unaposoma biblia soma kwa kujifunza vinginevyo masomo makuu na ya msingi yaliyo ndani yake yatakupita kama utakuwa unasoma tu kama gazeti). Sasa hapa tunaona ni mapambano ya moja kwa moja kati ya Shetani na Ayubu. Sasa kama tunavyosoma mara baada ya Ayubu kuzidi kushikilia msimamo wake na Mungu wake licha ya kwamba ana magonjwa na kufiwa na watoto wake, lakini bado yupo na Mungu wake. Shetani ndipo sasa akaingia kazini kwa kawatia mafuta watumishi wake wa uongo, ili waende kumgeuza moyo Ayubu kwa mafundisho ya udanganyifu. Na hawa si wengine zaidi ya ELIFAZI, SOFARI, NA BILDADI.
Hawa walikuwa ni marafiki zake na Ayubu wa Karibu, ni watu pia waliomcha Mungu lakini sio kwa kiwango cha Ayubu. walikuwa ni Wazee wenzake, washauri wenzake, ambao pengine kwa wakati wakiwa pamoja waliweza kuwafundisha hata watu wengine njia za haki, na ukamilifu. Walipata sifa nzuri kwa Ayubu na ndio maana Ayubu aliweza kuwachagua wao tu! kuwa kama marafiki zake na washauri wake wa karibu. Lakini katika hatua kama hii walionekana kama wapo kinyume na Ayubu. Hii inadhihirisha kuwa mtazamo wao juu ya UKAMILIFU ulikuwa ni tofauti na wa AYUBU. Sasa kama tukichunguza habari zao kwa karibu tunaona moja kwa moja kwa kumtazama Ayubu katika hali aliyokuwa nayo wakaanza kumuhukumu kuwa, hakika kuna mahali amemkosea Mungu. Lakini sababu zao walizozitoa za Ayubu kumkosea Mungu hazikuwa za “rohoni” bali za nje tu, lakini wenyewe waliangalia vya “mwilini” wakilinganisha na vya rohoni (kwamba ndio kigezo cha kukubaliwa na Mungu). Na hii ndio sababu kubwa iliyowafanya wapishane na Ayubu.
Sasa ukitazama moyo wa Ayubu utaona yeye alijua kuwa ushahidi mkubwa wa kukubaliwa na Mungu upo katika moyo wake(uhusiano binafsi alionao na Mungu wake, na si vinginevyo.) pasipo kujali anapitia hali ya namna gani ya nje! iwe ni umaskini, shinda, njaa, uchi, magonjwa n.k. na ndio maana vilipotokea aliweza kustahimili kwasababu alijua ndani ya moyo wake hakijaharibika kitu, hajaona kama amefanya jambo la kumkosea Mungu. Uwepo wa Mungu ndani yake ulikuwa upo pale pale. Lakini wale marafiki zake watatu ambao wao walitumiwa na shetani kutenda kazi ile, walitazama kwa jicho lingine lisilo la ki-Mungu, na kuhitimisha kwamba kigezo pekee cha Mtu kukubaliwa na Mungu, ni kufanikiwa katika mambo yote, afya, familia, mali,mifugo umri, n.k.basiii!!! sasa ukiona umepungukiwa na hayo yote basi ni dhahiri kuwa Mungu amekukataa na hayupo na wewe hivyo unapaswa UTUBU. ndio yalikuwa mahubiri yao kwa Ayubu kuanzia mwanzo mpaka mwisho (Pata muda taratibu mwenyewe upitie kitabu cha Ayubu chote), na kibaya zaidi waliyathibitisha hayo waliyokuwa wanayasema kwa kutumia maandiko matakatifu, na mengine kufunuliwa kupitia maono usiku. Kiasi kwamba unaweza ukadhani ni Mungu kweli anazungumza na wewe kupitia watumishi wake. Embu Tusome baadhi ya maneno yao waliokuwa wanamuhubiria Ayubu..
Elifazi alianza kwa kumwambia Ayubu tukisoma Ayubu 4:6-9..
“6 Je! Dini yako siyo mataraja yako, Na matumaini yako si huo uelekevu wa njia zako?
7 Kumbuka, tafadhali, NI NANI ALIYEANGAMIA AKIWA HANA HATIA? Au hao waelekevu, walikatiliwa mbali wapi?
8 Kama mimi nilivyoona, hao walimao maovu, Na kupanda madhara, huvuna yayo hayo.9 Kwa pumzi za Mungu huangamia. Na kwa kuvuma kwa hasira zake humalizika. “
Akiwa na maana kuwa kwamba Ayubu angekuwa ni mwelekevu kweli asingepatikana na shida zote hizo kwasababu walijua maandiko kwamba mwenye haki hawezi kukatiliwa mbali,(Na ni kweli ndivyo yanavyosema lakini yalitumika mahali pasipoyapasa)na pia waliongezea “watu wapandao madhara huvuna hayo hayo” hivyo Ayubu kuwa vile ni kwasababu huko nyuma alikuwa ni mkaidi, hivyo kavuna alichokipanda.
Bildadi rafiki yake wa pili naye akaongezea na kumwambia Ayubu:
Mlango 8
“1 Ndipo Bildadi huyo Mshuhi akajibu, na kusema,
2 Wewe utanena maneno haya hata lini? Maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo mkuu hata lini?
3 Je! Mungu hupotosha hukumu? Au, huyo Mwenyezi hupotosha yaliyo ya haki?
4 KWAMBA WATOTO WAKO WAMEMFANYIA DHAMBI, NAYE AMEWATIA MKONONI MWA KOSA LAO;
5 Wewe ukimtafuta Mungu kwa bidii, Na kumsihi huyo Mwenyezi;
6 UKIWA WEWE U SAFI NA MWELEKEVU; HAKIKA YEYE SASA ANGEAMKA KWA AJILI YAKO, NA KUYAFANYA MAKAZI YA HAKI YAKO KUFANIKIWA.
7 Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, Lakini mwisho wako ungeongezeka sana.
8 Basi, uwaulize, tafadhali, vizazi vya zamani, Ujitie kuyaangalia yale baba zao waliyoyatafuta;
9 (Kwani sisi tu wa jana tu, wala hatujui neno, Kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli tu;)
10 Je! Hawatakufunza wao, na kukueleza, Na kutamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
11 Je! Hayo mafunjo yamea pasipo matope Na makangaga kumea pasipo maji?
12 Yakiwa yakali mabichi bado, wala hayakukatwa, Hunyauka mbele ya majani mengine.
13 Ndivyo ulivyo mwisho wa hao wamsahauo Mungu; Na matumaini yake huyo mbaya huangamia;
14 Uthabiti wake utavunjika, Na matumaini yake huwa ni nyuzi za buibui.
15 Ataitegemea nyumba yake, isisimame; Atashikamana nayo, isidumu.
16 Yeye huwa mti mbichi mbele ya jua, Nayo machipukizi yake huenea katika bustani yake.
17 Mizizi yake huzonga-zonga chuguu, Huangalia mahali penye mawe.
18 Lakini, aking’olewa mahali pake, Ndipo patamkana, na kusema, Mimi sikukuona.
19 Tazama, furaha ya njia yake ni hii, Na wengine watachipuka kutoka katika nchi.
20 Tazama, Mungu hatamtupa mtu mkamilifu, Wala hatawathibitisha watendao uovu.
21 Bado atakijaza kinywa chako kicheko, Na midomo yako ataijaza shangwe.
22 Hao wakuchukiao watavikwa aibu; Nayo hema yake mwovu haitakuwako tena”.
Unaona hapo tunaona Bildadi anamwambia Ayubu sababu pekee ya watoto wake kuangamizwa ni kwasababu watoto wake walikuwa ni waovu. Lakini tunasoma Ayubu alikuwa kila siku anaamka alfajiri kuwaombea watoto wake rehema na dua kwa Mungu. Yaani kwa ufupi Bildadi alimaanisha kuwa kifo, misiba, wakati wote ni matokeo ya kutokuwa mwelekevu mbele za Mungu. Bildadi aliendelea kumlaumu Ayubu kwamba kama kweli angekuwa ni mkamilifu mbele za Mungu, basi Mungu mwenyewe angenyanyuka amtete, lakini sasa mbona bado anaonekana hali yake iko vile vile tena ndio ikizidi kuwa mbaya zaidi. Kwahiyo matatizo yale ni ushahidi tosha kwamba maisha yake hayapendezi hata kidogo mbele za Mungu.
Na rafiki yake wa mwisho Sofari aliendelea kumvunja moyo Ayubu na kusema..
Mlango 20
“1 Ndipo Sofari, Mnaamathi, akajibu, na kusema,
2 Kwa hiyo mawazo yangu hunipa jawabu, Kwa ajili ya haraka niliyo nayo ndani yangu.
3 Nimesikia maonyo yanayonitahayarisha, Nayo roho ya ufahamu wangu hunijibu.
4 Je! Hujui neno hili tangu zamani za kale, Tangu wanadamu kuwekwa juu ya nchi,
5 YA KUWA SHANGWE YA WAOVU NI KWA MUDA KIDOGO, NA FURAHA YA WAPOTOVU NI YA DAKIKA MOJA TU?.
6 Ujapopanda ukuu wake mpaka mbinguni, Na kichwa chake kufikilia mawinguni;
7 HATA HIVYO ATAANGAMIA MILELE KAMA MAVI YAKE MWENYEWE; HAO WALIOMWONA WATASEMA, YUKO WAPI?
8 Ataruka mfano wa ndoto, asionekane; Naam, atafukuzwa kama maono ya usiku,
9 Jicho lililomwona halitamwona tena; Wala mahali pake hapatamtazama tena.
10 Watoto wake watataka fadhili kwa maskini, Na mikono yake itarudisha mali yake.
11 Mifupa yake imejaa ujana wake, Lakini utalala nchi naye mavumbini.
12 Ingawa uovu una tamu kinywani mwake, Ingawa auficha chini ya ulimi wake;
13 Ingawa auhurumia, asikubali kuuacha uende zake. Lakini akaushika vivyo kinywani mwake;
14 Hata hivyo chakula chake matumboni mwake kinabadilika, Kimekuwa ni nyongo za majoka ndani yake.
15 Amemeza mali, naye atayatapika tena; Mungu atayatoa tumboni mwake.
16 Ataamwa sumu ya majoka; Na ulimi wa fira utamwua.
17 Hataiangalia hiyo mito ya maji, Vile vijito vilivyojaa asali na siagi.
18 Aliyoyataabikia kazi atayarudisha, asiyameze; Kwa mali aliyoyapata, hatafurahi.
19 Kwa maana amewaonea na kuwaacha maskini; Amenyang’anya nyumba kwa jeuri, wala hataijenga.
20 Kwa sababu hakujua utulivu ndani yake, Hataponya cho chote katika hicho alichokifurahia.
21 Hakikusalia kitu asichokula; Kwa hiyo kufanikiwa kwake hakutadumu.
22 Katika kujaa kwa wingi wake atakuwa katika dhiki; Mkono wa kila anayesumbuliwa utamjia.
23 Hapo atakapo kulijaza tumbo lake, Mungu atamtupia ukali wa ghadhabu zake, Na kuunyesha juu yake akiwa anakula.
24 Ataikimbia silaha ya chuma, Na uta wa shaba utamchoma kwa pili.
25 Yeye autoa, nao watoka mwilini mwake; Naam, ncha ing’aayo yatoka katika nyongo yake; Vitisho viko juu yake.
26 Giza lote linawekwa kwa ajili ya hazina zake; Moto ambao haukuvuviwa na mtu utamla; Utayateketeza yaliyosalia hemani mwake.
27 Mbingu zitafunua wazi uovu wake, Nayo nchi itainuka kinyume chake.
28 Maongeo ya nyumba yake yataondoka, Yatamwagika mbali katika siku ya ghadhabu zake.
29 Hii ndiyo sehemu ya mtu mwovu itokayo kwa Mungu, Na urithi aliowekewa na Mungu”.
Kama tunavyosoma hapo, Sofari naye hakuona haya kumwambia Ayubu kwamba yeye alikuwa katika “shangwe za watu waovu ambazo hazidumu ni za muda tu”. Akiwa na maana kuwa Mali Ayubu alizokuwa nazo kwanza zilikuwa ni za muda tu! kwasababu hazikuwa ni za haki, akimaanisha kuwa uthibitisho pekee wa Mungu kuwa na Ayubu ni mali zidumuzo na kama hazidumu basi hizo ni shangwe za waovu. Hivyo hatuwezi kueleza habari zao zote lakini ukiwa na muda pitia kitabu cha Ayubu chote utaona Injili ya hawa watu ilivyokuwa kwa Ayubu na jinsi walivyoweza kutumia maandiko na maono kuthibitisha uongo wao ili tu wamfanye Ayubu auache uelekevu wake mbele za Mungu. Hawa ndio walimfadhaisha Ayubu mara mia elfu zaidi hata ya kupotelewa na watoto na mali zake, kwasababu walikuwa wanataka kumfanya Ayubu atilie shaka uelekevu wake mbele za Mungu. walifanyika kama vyombo vya shetani kumjaribu Ayubu.
Mambo hayo yameandikwa ili kutuonya sisi watu wa zamani hizi, Shetani anapomaliza kumjaribu mkristo kwa magonjwa, kwa dhiki, kwa misiba, kwa udhaifu, kwa kupungukiwa na mali, kwa vifungo, kwa mateso, kwa shida, kwa njaa, n.k na kuona kuwa mtu huyo bado kasimama katika imani yake na uelekevu wake kama Ayubu basi huwa anabadilisha mfumo wake wa majaribu, na kuleta majaribu magumu zaidi, na ya hatari zaidi, anakuletea watu aliowatia yeye mafuta, mfano wa akina ELIFAZI,SOFARI, NA BILDADI ambao watatumia maandiko kukushawishi na kukuhakikishia kwamba njia unayoiendea sio sahihi, na kama hauna Roho wa Mungu ni rahisi sana kuchukuliwa na uongo wa watu hao, watakwambia KIGEZO PEKEE cha Mungu kukukubali ni wewe kuwa na MALI, kigezo pekee cha kuwa Mungu hajakutupa ni kutokupitia shida kabisa, watakwambia ukipitia misiba basi kuna tatizo kwenye imani yako, watakwambia ukipitia magonjwa basi kuna mahali umemuudhi Mungu, ukiwa na ulemavu fulani basi kuna laana fulani inakufuata kwasababu wenye haki lazima wawe na afya, watakuhakikishia kwa maandiko kabisa “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo. “
watu kama hawa hata siku moja hawataangalia AFYA YA ROHO YAKO, kwamba je! unaishi maisha matakatifu?, au unayo imani? au una upendo? au je! unamzalia Mungu matunda ya haki?? au unamfanyia Mungu ibada ya kweli? wao wataangalia AFYA YA MWILI wako tu! na siku ikitetereka kidogo tu, basi umekwisha chukuliwa nao utaishia kuudharau ukristo na kusema ni ulokole tu,
Ndugu jiepushe nao, wanaipotosha kweli ya Mungu, ni shetani kawainua kuwajaribu watu wa Mungu, na kuwavunja moyo na kuwakatisha tamaa ili waiache imani, kwasababu laana kubwa mbele za Mungu sio kupungukiwa mali, au kukosa afya,au kupitia misiba au dhiki, hapana bali laana kubwa mbele za Mungu ni kutomwamini yeye aliyetumwa na yeye (yaani Yesu Kristo),na kukosa uhusiano binafsi na Mungu kwasababu biblia inasema..
Warumi 8: 35 “Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?
36 Kama ilivyoandikwa, ya kwamba, Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa, Tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa kuchinjwa.
37 Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.
38 Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo,
39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu”.
Hivyo ndugu yatangeneze maisha yako kwa kumpenda Bwana Mungu wako pasipo kupelekwa na upepo huku na huku au kundi hili la waalimu na manabii wa uongo,(Hao ndio manabii wa uongo wa siku za mwisho) Biblia inasema kila jambo na majira yake wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna, wakati wa kulia na wakati wa kucheka, wakati wa kujenga na wakati wa kubomoa, mkumbuke Ayubu baada ya yale majaribu Bwana alimrudishia mara mbili ya vile alivyovipoteza, lakini kama angewasikiliza wale rafiki zake leo hii angekuwa wapi?. Si angeishia kumwangalia Mungu katika kioo cha mafanikio tu??. lakini hakuruhusu imani yake ipotee na zile mali za kwanza alizokuwa nazo, alitunza uhusiano wake binafsi na Mungu katika hali yoyote aliyopo, nasisi vivyo hivyo tuwe matajiri, au maskini, tuwe na vitu au tusiwe na vitu, tuwe wazima au tuwe wagonjwa, uhusiano wetu na Mungu unapaswa uwe pale pale kama Ayubu, usiyumbishwe na mazingira ambayo shetani anayaleta kupitia watumishi wake wa uongo ambao ndio sasahivi wamezagaa kila mahali kuwarubuni watu na mafundisho yao ya kujigamba.
Bwana akubariki sana.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
AYUBU 28 : HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?
‘’MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI’’..NA NDIVYO ILIVYO KWA UASHERATI
AYUBU ALIJARIBIWA KWA MUDA GANI?.
KITABU CHA YASHARI KINACHOZUNGUMZIWA KATIKA 2SAMWELI 1:17-18, NI KITABU GANI?
KWANINI SAMWELI ALIRUHUSIWA KUHUDUMU HEKALUNI KAMA VILE WALAWI WAKATI YEYE NI MU-EFRAIMU?
Licha ya kuwa na INJILI YA MSALABA,ambayo ndio kiini cha kila mwanadamu ipo injili nyingine pia ijulikanayo kama INJILI YA MILELE, hii ni tofauti na injili ya msalaba. Injili ya msalaba yenyewe inatangaza wokovu kwa mwanadamu tu, kwa kupitia mmoja naye ni YESU KRISTO BWANA wetu. Kwahiyo injili nyingine yeyote inayodai kumkomboa mwanadamu na haimweki Bwana Yesu kama kiini cha injili yenyewe, basi injili hiyo ni batili, kwasababu yeye pekee ndiye Njia, kweli na uzima, hakuna mtu yeyote atakayemwona Mungu, pasipo kupitia kwake yeye biblia inasema hivyo(Yohana 14:6).. Kwahiyo zipo injili nyingi zinazodai zinaweza kumkomboa mwanadamu lakini kati ya hizo ni moja tu itakayoweza kumkomboa mwananadamu! Nayo ni Kwa kupitia Yesu Kristo, na ndio maana Mtume Paulo alisema|:
2Wakoritho 11: 4 “Maana yeye ajaye akihubiri Yesu mwingine ambaye sisi hatukumhubiri, au mkipokea roho nyingine msiyoipokea, au INJILI NYINGINE msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye!”
Unaona hapo? Biblia inasema kuna Yesu mwingine, roho mwingine na injili nyingine tofauti na ile iliyohubiriwa na mitume. Kwahiyo injili yoyote inayohusishwa na ukombozi wa mwanadamu inapaswa imlenge YESU KRISTO ALIYESULIBIWA,akafa na kufufuka kama kiini cha Ukombozi wenyewe, kwa asilimia mia yeye peke yake na sio pamoja mtu mwingine.
Lakini leo kwa ufupi tutaitazama INJILI YA MILELE ambayo ipo na imezungumziwa katika biblia..kama tunavyosoma katika;
Ufunuo 14: 6 “Kisha nikaona malaika mwingine, akiruka katikati ya mbingu, mwenye INJILI YA MILELE, awahubiri hao wakaao juu ya nchi, na kila taifa na kabila na lugha na jamaa,
7 akasema kwa sauti kuu, Mcheni Mungu, na kumtukuza, kwa maana saa ya hukumu yake imekuja. Msujudieni yeye aliyezifanya mbingu na nchi na bahari na chemchemi za maji”.
Sasa hii injili ya milele ni ipi?
Kama jina lake lilivyo “Milele” inamaana kuwa ni injili ambayo Ipo milele yote, ilikuwepo kabla ya mwanadamu kuumbwa, ipo sasa, na itaendelea kuwepo milele na milele, Kumbuka INJILI YA MSALABA ilikuwa na mwanzo, na itakuwa na mwisho, mwanzo wake ilikuwa ni Kalvari, na mwisho wake itakuwa katika Unyakuo. Baada ya hapo hakutakuwa na nafasi tena ya ukombozi, kwasababu mlango wa neema utakuwa umefungwa. Kitakachokuwa kimebaki ni ile ile injili ambayo ilikuwepo milele na milele.
Na ndio maana ukisoma mstari huo hapo juu utaona kuwa yule malaika(mjumbe) anapita kuitangaza hiyo injili ambapo kwa wakati huo unyakuo wa kanisa utakuwa umeshapita na mlango wa neema ya kuokolewa utakuwa umefungwa kwa watu wa mataifa.
Kwahiyo injili hii ni tofauti na ya msalaba tuliyonayo sasa, hii ya msalaba tunaifahamu kwa “kuhubiriwa”. Hatuwezi kuifahamu pasipo kuhubiriwa ndio maana biblia inasema katika;
Warumi 10: 13 “kwa kuwa, Kila atakayeliitia Jina la Bwana{YESU KRISTO} ataokoka.
14 Basi wamwiteje yeye wasiyemwamini? Tena wamwaminije yeye wasiyemsikia? TENA WAMSIKIEJE PASIPO MHUBIRI?
15 Tena wahubirije, wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, Ni mizuri kama nini miguu yao wahubirio habari ya mema!{INJILI YA MSALABA}”
Kwahiyo unaona hapo, ni lazima awepo mtu wa kuihubiri ndipo watu waokolewe.
Tofauti na ilivyo INJILI YA MILELE. Injili hii haisambazwi kwa kuhubiriwa na mtu yeyote, Ni Mungu mwenyewe anaiweka ndani ya mtu, katika eneo maalumu la moyo wa mwanadamu linaloitwa “DHAMIRA”..ambayo kila mtu anazaliwa nayo. Na inafanya kazi ya kuhukumu njia zote mbaya zinazokwenda kinyume na mapenzi ya Mungu ndani ya mtu..Na Injili hii haipo tu kwa wanadamu, ilikuwepo hata kwa malaika, kwasababu ni ya milele, ilikuwepo huko enzi na enzi, ipo na itakuwepo.
Kwahiyo sasa kitendo tu cha mtu kuwa mwanadamu, tayari moja kwa moja kuna kitu ndani yake kitakuwa kinamshuhudia mambo yanayofaa na yasiyofaa, bila hata kuhubiriwa na mtu yeyote, au kukumbushwa na mtu yeyote, kwamfano, kila mtu anafahamu kuwa uuaji sio sawa, iwe anayo hofu ya Mungu au hana hofu ya Mungu, kila mtu anafahamu kuwa dhuluma ni mbaya, hata kama sheria isingesema hivyo, ndani ya moyo wake dhamira inamuhubiria kuwa kitendo hicho ni kibaya, Kadhalika haihitaji kuifahamu biblia kujua kuwa uonevu ni makosa, wizi ni makosa, utukanaji, ubakaji, rushwa ni makosa hayo yote hata kama mtu hajawahi kumsikia Mungu, au chochote kinachoitwa Mungu anajua kabisa hayo mambo hayafai kufanya, pia haihitaji kwenda katika vyuo vya biblia kutambua kuwa kulala na ndugu yako wa damu ni makosa, kadhalika na ushoga au usagaji ni makosa, utajikuta tu wewe mwenyewe unachukia kufanya hivyo au unalipinga hilo wazo ndani yako pale linapokuja kwasababu unajua kabisa kuwa hayo ni makosa.
Sasa hiyo ndio inayoitwa INJILI YA MILELE, Mungu anayoihubiri ndani ya moyo wa mtu. Na ndiyo hiyo siku za mwisho itakuja kukumbushwa kwa watu, wamche Mungu.wakati huo unyakuo utakuwa umeshapita.
Kwahiyo usidhani kuwa wale watu ambao hawajasikia habari za YESU(Injili ya msalaba) mahali popote, hawatahukumiwa. Hapana Watahukumiwa tu kama wale wengine kwa injili hiyo. Watu wa kipindi cha Nuhu hawakuwa na sheria waliyopewa na Mungu kama watu wa Musa na kuendelea,Na ndio maana Mtume Paulo alieleza habari za watu hawa kama tunavyosoma katika…
Warumi 1: 17 Kwa maana haki ya Mungu inadhihirishwa ndani yake, toka imani hata imani; kama ilivyoandikwa, Mwenye haki ataishi kwa imani.
18 Kwa maana GADHABU YA MUNGU imedhihirishwa kutoka mbinguni juu ya uasi wote na uovu wa wanadamu waipingao kweli kwa uovu.
19 Kwa kuwa MAMBO YA MUNGU YANAYOJULIKANA YAMEKUWA DHAHIRI NDANI YAO, KWA MAANA MUNGU.
20 Kwa sababu mambo yake yasiyoonekana tangu kuumbwa ulimwengu yanaonekana, na kufahamika kwa kazi zake; YAANI, UWEZA WAKE WA MILELE NA UUNGU WAKE; hata wasiwe na UDHURU;
21 kwa sababu, walipomjua Mungu hawakumtukuza kama ndiye Mungu wala kumshukuru; bali walipotea katika uzushi wao, na mioyo yao yenye ujinga ikatiwa giza.
22 Wakijinena kuwa wenye hekima walipumbazika;
23 wakaubadili utukufu wa Mungu asiye na uharibifu kwa mfano wa sura ya binadamu aliye na uharibifu, na ya ndege, na ya wanyama, na ya vitambaavyo.
24 Kwa ajili ya hayo Mungu aliwaacha katika tamaa za mioyo yao, waufuate uchafu, hata wakavunjiana heshima miili yao.
25 Kwa maana waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakakisujudia kiumbe na kukiabudu badala ya Muumba anayehimidiwa milele. Amina.
26 Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili;
27 wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.
28 Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.
29 Wamejawa na UDHALIMU, UOVU na TAMAA na UBAYA; wamejawa na HUSUDA, na UUAJI, na FITINA, na HADAA; watu wa NIA MBAYA, wenye KUSENGENYA,
30 wenye KUSINGIZIA, wenye KUMCHUKIA MUNGU, wenye JEURI, wenye KUTAKABARI, wenye MAJIVUNO, wenye KUTUNGA MABAYA, WASIOTII WAZAZI WAO,
31 wasio na UFAHAMU, wenye KUVUNJA MAAGANO, WASIOPENDA JAMAA ZAO, WASIO NA REHEMA;
32 ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.
Umeona hapo ndugu, biblia inasema wakijua kabisa watendao mambo kama hayo wamestahili mauti lakini bado wanayatenda. Dhamira zao zikiwashuhudia ndani kuwa wanayoyafanya sio sahihi lakini wanaendelea kuyafanya, Na wewe je! Ambaye upo kwenye dhambi utahitaji mhubiri siku moja aje kukuthibitishia kwenye biblia kwamba, uvutaji sigara ni dhambi, au uasherati ni dhambi?? Angali ndani ya moyo wako dhamira inakushuhudia kabisa unachofanya ni makosa?..hakika unaweza usilione lakini fahamu kuwa hukumu inakungojea.!
Wewe unayevaa vimini, na kutembea nusu uchi barabarani unasema Mungu haangalii mavazi lakini moyo wako unakuambia kabisa hayo ni makosa unayoyafanya na bado unaweka moyo mgumu, wewe unayevaa suruali,unayepaka wanja, na kupaka lipstick, na kuvaa wig na hereni, Hukumu ipo mbeleni dada!, wewe unayesengenya, wewe ambaye ni shoga, wewe unayejisaga, wewe unayetoa mimba, wewe uliye mwasherati, wewe uliye mlevi, wewe unayetazama pornography, wewe unayefanya masturbation, wewe unayeabudu sanamu za watakatifu waliokufa zamani angalia biblia inavyokuambia hapo juu < wakaubadili utukufu wa Mungu asiye na uharibifu kwa mfano wa sura ya binadamu aliye na uharibifu(sanamu), na ya ndege, na ya wanyama, na ya vitambaavyo >..Unaona unajua kabisa Mungu hawezi kufananishwa na mfano wowote wa kinyago cha kuchonga lakini wewe bado unakwenda kuvipiga magoti na kuviabudu..
2Wakorintho 6: 16 inasema “Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu?”..
Lakini biblia inaendelea kusema kwa jinsi utakavyozidi kuweka moyo wako mgumu, kuna kipindi kitafika Mungu anakuacha uendelee hivyo hivyo kwasababu umekataa kuitii hiyo sauti inayosema ndani yako, mpaka ile siku ya hukumu ije na utaingia kuzimu!! Alisema “”28 Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa”.
Kwahiyo dada/kaka hukumu ya Mungu haikwepeki hata uwe nje ya kanisa, njia pekee ni kujisalimisha maisha yako kwa BWANA YESU ambaye yeye ndiye aliyetoa uhai wake ili akuokoe, Tubu geuka, ukapewe uwezo wa kushinda dhambi. Muda umekwenda kuliko unavyodhani, na Injili ya msalaba sio ya milele utafika wakati utatamani uingie utakosa, muda ndio huu, mpe Bwana maisha yako tangu sasa.
Ubarikiwe.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali “Share” kwa wengine na Mungu atakubariki.
Mada Nyinginezo:
MLINZI, NI HABARI GANI ZA USIKU?
Yapo maswali kadha wa kadha umekuwa ukijiuliza kama mkristo (tukisema mkristo tunamaanisha mtu aliyegeuka na kudhamiria kwa gharama zake zote kubeba msalaba wake na kumfuata Kristo). Wakati mwingine unajikuta aidha ndani ya moyo wako au nje na maswali unayokosea majibu!!.
Kwamfano pengine unasema tangu nilipompa Bwana maisha yangu ni kweli ndani ya moyo wangu nilipata amani kubwa ya ki-Mungu lakini nje! Naona mambo mengi hayapo sawa, nilipojaribu kuishi maisha matakatifu marafiki na ndugu wakanitenga , nilipojaribu kuacha usengenyaji ndipo nilipoanza kuonekana mbele ya marafiki zangu ninajidai,
Nilipoacha rusha ndipo visa vikainuka kazini na kupelekea kuongeza idadi ya watu wanichukiao, niliposaidia watu badala ya kupokea shukrani ndio napokea lawama, nilipoanza kufunga na kuomba badala ya matatizo kupungua ndio yaliendelea kuwa vile vile, nilipoanza kufanya kazi ya Mungu ndipo matatizo ya kiuchumi yakanyanyuka zaidi,
Mpaka unafikia hatua ya kusema mbona huku kuishi maisha ya kujinyima na mambo ya dunia hakuna faida yoyote ninayoipata, zaidi ya kuwa vile vile tu siku zote!, mbona wale wasiomcha Mungu wana raha siku zote, ni matajiri pamoja na kwamba wanamkana Mungu, wanazidi kufanikiwa katika mambo yao,mbona wazinzi ndio wanao afya nzuri?.
Mimi pamoja na utakatifu wangu wote na wema wangu wote, Mungu kama hanioni na kunipa raha kama hao wengine, japo ninafanya mema kushinda wao?, kwani ni laana gani ninayo hadi yanipate hayo yote, au wao wana kitu gani cha ziada cha kushinda mimi mpaka wao wayapate hayo yote?,..Kumbuka Hayo ni mawazo yaliyopo ndani ya watakatifu wengi wa Mungu, Hata Daudi naye pia alizungumza maneno kama hayo tusome katika:
Zaburi 69: 7 “Maana kwa ajili yako nimestahimili laumu, Fedheha imenifunika uso wangu.
8 Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, Na msikwao kwa wana wa mama yangu.
9 Maana wivu wa nyumba yako umenila, Na laumu zao wanaokulaumu zimenipata.
10 Nilipolia na kuiadhibu roho yangu kwa kufunga, Ikawa laumu juu yangu.
11 Nilipofanya gunia kuwa nguo zangu, Nikawa mithali kwao.
12 Waketio langoni hunisema, Na nyimbo za walevi hunidhihaki”.
Zaburi 73:1 “Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, Kwa hao walio safi mioyo yao.
2 Nami miguu yangu ilikuwa karibu na kupotoka, Hatua zangu zilikuwa karibu na kuteleza.
3 MAANA NALIWAONEA WIVU WENYE KUJIVUNA, NILIPOIONA HALI YA AMANI YA WASIO.
4 Maana hawana maumivu katika kufa kwao, Na mwili wao una nguvu.
5 Katika TAABU YA WATU HAWAMO, Wala hawapati mapigo pamoja na wanadamu.
6 Hivyo kiburi kimekuwa mkufu shingoni mwao, Jeuri huwavika kama nguo.
7 Macho yao hutokeza kwa kunenepa, Wameipita kadiri ya mawazo ya mioyo yao.
8 Hudhihaki, husimulia mabaya, Husimulia udhalimu kana kwamba wako juu.
9 Wameweka kinywa chao mbinguni, Na ulimi wao hutanga-tanga duniani.
10 Kwa hiyo watu wake hugeuka huko, Na maji yaliyojaa humezwa nao.
11 Nao husema, Mungu ajuaje? Yako maarifa kwake aliye juu?
12 Fahamu, ndivyo walivyo wasio haki, Na kwa kustarehe sikuzote wamepata mali nyingi”.
Zaburi 42: 3 “Machozi yangu yamekuwa chakula changu mchana na usiku, Pindi wanaponiambia mchana kutwa, Yuko wapi Mungu wako”.
Kama tunavyosoma Daudi pamoja na wema wake wote wa kuwaombea watu wengine fadhili mbele za Mungu kwa kufunga na wakati mwingine kwa machozi lakini bado alionekana kuwa kama ni kituko na mgeni mbele zao. Mpaka kufikia hatua ya kuwaonea wivu watu waovu.
Kadhalika na mambo haya haya yanawazwa na watakatifu walioko leo duniani , Wanasema aidha kwa midomo yao au kwa mioyo yao: Mungu wetu yuko wapi? Mbona hatuoni faida yoyote ya kumtumikia, mbona hatuoni faida yoyote ya kuacha kuvaa vimini, hereni, suruali, kuacha kupaka lipstick na wigi, wale wanaoendelea kufanya hivyo hao ndio wanaolewa kwa harusi nzuri, wana watoto wazuri lakini mimi bado nipo vile vile tu!.
Utasema mbona sioni faida yoyote ya kuacha pombe na sigara, mbona sioni faida yoyote ya kuacha uasherati, disco, anasa,na kucheza kamari na ku-bet, wenzangu wanafanikiwa kirahisi mimi nipo vile vile tu, Mbona sioni faida yoyote ya kuacha kula rushwa, zile pesa nilizokuwa ninapata mwanzoni sizioni tena nikizipata sasahivi, wale wenzangu tuliokuwa tunakula nao rushwa zamani wanazidi kunawiri na kusomesha watoto wao na kujenga majumba makubwa na mimi nimebaki katika hali ile ya kawaida tu!.n.k.
Haya yote yamekuwa ni maswali ya WATAKATIFU tangu zamani, Lakini Bwana naye aliyasikia na kuyatolea majibu yake: Kama tunavyosoma katika Malaki 3 Bwana anasema.
Malaki 3:13 “Maneno yenu yamekuwa magumu juu yangu, asema Bwana. Lakini ninyi mwasema, Tumesema maneno juu yako kwa namna gani?
14 MMESEMA, KUMTUMIKIA MUNGU HAKUNA FAIDA; na, TUMEPATA FAIDA GANI KWA KUYASHIKA MAAGIZO YAKE, NA KWENDA KWA HUZUNI MBELE ZA BWANA WA MAJESHI?
15 Na sasa twasema ya kwamba wenye kiburi ndio walio heri; naam, watendao uovu ndio wajengwao; naam, wamjaribuo Mungu ndio waponywao.
16 Ndipo wale waliomcha Bwana waliposemezana wao kwa wao. NAYE BWANA AKASIKILIZA, AKASIKIA; na KITABU CHA UKUMBUSHO KIKAANDIKWA MBELE ZAKE KWA AJILI YA HAO WAMCHAO BWANA, NA KULITAFAKARI JINA LAKE.
17 Nao watakuwa wangu, asema Bwana wa majeshi, katika siku ile niifanyayo; naam, watakuwa hazina yangu hasa; nami nitawaachilia, kama vile mtu amwachiliavyo mwanawe mwenyewe amtumikiaye.
18 Ndipo mtakaporudi, nanyi mtapambanua kati ya wenye haki na waovu, na kati ya yeye amtumikiaye Mungu na yeye asiyemtumikia”.
Unaweza ukaona hapo?. Hakuna wema wowote wa mtakatifu atakaoufanya ukapita bure bure tu! , mbinguni kuna KITABU CHA KUMBUKUMBU kimewekwa kwa watu maalumu, kinarekodi mambo yote mema watakatifu wanayoyafanya kila siku huku duniani.
Na kama ni kitabu basi inaamanisha ili kiwe kitabu kamili ni lazima kiwe na kurasa nyingi na sio chache, na kitabu hichi cha watakatifu, ni matendo mema tu ndio yanayoandikwa huko, na sio kingine. Kwahiyo wingi wako wa kumcha Mungu na matendo yako mema mbele za Mungu kila siku yanarekodiwa katika kitabu kile na ndio yatakayoelezea wingi wa thawabu utakazopewa mbinguni katika siku ile ya mwanakondoo.
Hivyo ndugu/dada ukiwa ni mkristo kweli kweli uliyedhamiria kusimama katika Imani huu sio wakati wa kudhani kumtumikia hakuna faida yoyote,Faida zipo nyingi sana utazijua kwa marefu na mapana utakapofika katika urithi uliowekewa na Mungu wako.
Mambo ya ulimwengu huu sio urithi wetu, wewe upate usipate, uwe tajiri uwe maskini, uwe una afya usiwe na afya, vyovyote wewe endelea kumcha Mungu bila kujali lolote lile ukijua siku ile ni Mungu wako aonaye taabu yako ndiye atakayekulipa, maadamu unajiona upo sawa na Mungu wako usikwamishwe na kitu kingine chochote,songa mbele! endelea kuliweka Kumbukumbu lako sawa mbinguni, usidanganyike na mafundisho ya watumishi bandia kwamba kuwafanikiwa au kutokufanikiwa kifedha ndio uthibitisho kwamba Mungu yupo na wewe au Mungu amekuacha, hapana uthibitisho pekee ni maisha unayoishi ya kumpendeza Mungu wako sikuzote, kwasababu kitabu cha kumbukumbu kipo mbinguni.
Ongeza bidii, ikiwa umekataa rushwa endelea kuipinga, ukiwa umekataa uasherati endelea kufanya hivyo kwa bidii zaidi, ikiwa umekataa kuenenda kama mfano wa watu wa ulimwengu huu kuvaa vimini, suruali endelea hivyo hivyo kumbukumbuku lako kila siku linawekwa na thawabu yako ya siku haitapita bure..Bwana aliyeumba macho anaona yote!.
Lakini ukisema nitafanya hivyo nikifika umri fulani au wakati fulani, hujui kesho yako itakuwaje, na utakosa kumbukumbuku bora siku ile wakati wenzako wanafarijiwa kwa mambo mazuri yasiyoelezeka ya umilele na wewe haupo.Usiwaige watu waovu katika njia zao?
Na ni kwasababu gani Mungu anaruhusu waovu wafanikiwe sasa? .
Ni kwasababu urithi wao upo katika dunia ya sasa iliyoharibika na hawana sehemu yoyote katika urithi katika ulimwengu unaokuja. Hivyo faraja yao ipo katika mambo ya ulimwengu wa sasa kule hawana sehemu ndio sababu Bwana karuhusu wapate faraja yao hapa.
Bwana alimwambia Daudi.
Zaburi 92:7 “WASIO HAKI WAKICHUPUKA KAMA MAJANI NA WOTE WATENDAO MAOVU WAKISTAWI. NI KWA KUSUDI WAANGAMIZWE MILELE”
Kwahiyo sababu pekee ya waovu kufanikiwa sio kwasababu wanampendeza Mungu, ni ili waangamizwe milele, je! Na wewe unapenda kuwa miongoni mwao?, unafanikiwa katika rushwa yako ili uje uangamizwe milele?, unafanikiwa katika uasherati wako,na ulevi wako, na biashara yako haramu ili uje uwe miongoni mwa hao watakaoangamizwa milele?
Unafanikiwa katika utapeli wako na kamari yako na betting yako, ili uje uangamie milele?? Biblia inasema ITAKUFAIDIA NINI UPATE ULIMWENGU MZIMA, NA KUPATA HASARA YA NAFSI YAKO?, itakufaidia nini uonekane ni wakisasa kuliko watu wote duniani, kwa kujichora, kwa kuvaa vimini, na suruali na mawigi na kisha upate hasara ya nafsi yako? Ndugu KUMBUKUMBU LA WENYE HAKI LINAANDIKWA MBINGUNI kamwe usitamani mambo yao wala njia zao, kama hujampa Kristo maisha yako ni vema ukafanya hivyo sasa angali wakati upo, kabla mlango wa Neema haujafungwa.
Mungu akubariki.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali “share” kwa wengine ujumbe huu, na Mungu atakubariki.
Kwa msaada wa maombi/Ushauri/ubatizo/mafundisho/Whatsapp: Namba zetu ni hizi: +255693036618/ +255789001312
Mada Nyinginezo:
SIKU YA BWANA INAYOTISHA YAJA!
JE! NI SAHIHI MTU KUBATIZWA KWENYE MAJI YA KISIMANI?
Mara nyingi sana Mungu huwa anazungumza na sisi kupitia maisha yetu ya kawaida tunayoishi kila siku, tunapokosa shabaha ni pale tunapotarajia Mungu aseme nasi kwa njia zile tunazozifahamu, kwamfano, kuona maono au ndoto, unabii au kutokewa na malaika, mambo ambayo sio muda wote Mungu anayatumia kuzungumza na watu wake.
Sehemu kubwa Mungu anayotumia kuzungumza na watu wake ni kupitia maisha, na ndio maana inatugharimu kuyasoma maisha ya BWANA wetu Yesu Kristo na maisha ya watakatifu waliotangulia nyuma ili kuichuja na kuitambua sauti ya Mungu nyuma ya maisha yao.Kwamfano tunasoma tunaposoma kitabu cha mwanzo, au wafalme au Esta au Ruthu, au Nehemia au Ezra au hata safari ya wana wa Israeli hivyo ni vitabu vinavyoelezea maisha ya watu, na huko huko tunajua kusudi la Mungu kwetu sisi ni lipi.
Siku zote Mungu anajifunua katika mambo madogo, ambayo inahitaji utulivu vinginevyo tutaishia kusema Mungu hajawahi kuzungumza na sisi kabisa kama watu wengine wanavyosema..na kumbe alishazungumza na sisi mara nyingi, lakini hutukutia mioyo yetu ufahamu na kuelewa.
Kuna wakati Fulani mahali tulipokuwa tumepanga tulipata nafasi ya kuwa pamoja na wachezaji wawili wanaochezea timu moja maarufu hapa Tanzania, kwetu sisi hatukuona ni kitu cha ajabu sana kukutana nao kwa mwanzoni (kwasababu sisi sio washabiki wa michezo,hata hivyo ni kinyume kwa mkristo kuwa mshabiki wa mambo kama hayo) lakini maisha yao kwa jinsi tulivyoendelea kukaa nao yalitustaajabisha kidogo, kwa jinsi yalivyokuwa ya kipekee sana. Kwasababu kama wachezaji wa kidunia tulitazamia watakuwa ni watu wasiokuwa na nidhamu katika jamii (yaani kuishi maisha kama tu ya wasanii wengine wa kidunia), lakini kwa hawa tuliona utofauti wa mbali wa ya tulivyodhania.
Ratiba yao ilikuwa ni hii ; Kila siku wanaamka asubuhi sana saa 12 kamili, na kwenda uwanjani kufanya mazoezi mpaka saa 3, wakisharudi kutoka huko wana pumzika kidogo mpaka saa 7 mchana wakati wa jua kali, wanarudi tena uwanjani (saa 7 na saa 8) peke yao kufanya mazoezi ya nguvu kuliko waliyoyafanya asubuhi kwenye jua kali, kisha wanarudi kupumzika tena mpaka saa 11 jioni ndio warudi tena uwanjani kujumuika na wengine katika mazoezi ya kawaida, na hayo ndiyo yalikuwa maisha yao asubuhi, jioni, kila siku.
Lakini hicho nacho hakikutushangaza sana, kilichotushawishi zaidi mpaka kufikia hatua ya kutaka kuwauliza ni baada ya kuwatazama kwa muda mrefu, na kuwaona wakijiweka mbali na wanawake,na ulevi, uzururaji, na kuwa na idadi ndogo ya marafiki wanaokuwa nao..wao kazi yao ilikuwa ni mazoezi tu na kupumzika basi!!..hawakuwa wanafanya kitu kingine cha ziada.
Na ndio Siku hiyo moja tukawauliza ni kwanini nyie mnaishi maisha kama hayo tofauti na wengine, wakatujibu; Mambo yanayowakosesha wengi katika michezo na kuwafanya washuke viwango vyao kwa haraka, ni kuchanganya mambo mawili kwa wakati mmoja,wakasema; unapokuwa mchezaji na unataka kiwango chako kisishuke ni lazima uzingatie mambo yafuatayo;
1) Kukaa mbali na uasherati.
2) kukaa mbali na pombe na sigara
3) kukaa mbali na uzuraraji (ANASA).
4) Na kuzingatia mazoezi kwa bidii hususani katika wakati mgumu..hivyo mtu akizingatia yeyote akizingatia mambo hayo michezo haitakuwa na ugumu wowot kwake .
Sasa baada ya watu hao wa kidunia(ambao sio wakristo) kutuambia maneno kama hayo, tulifahamu hiyo ni sauti ya Mungu inayosema na sisi moja kwa moja, na andiko la kwanza lililotujia kichwani ni hili..;
1Wakorintho 9: 24 “Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate.
25 NA KILA ASHINDANAYE KATIKA MICHEZO HUJIZUIA KATIKA YOTE; BASI HAO HUFANYA HIVYO KUSUDI WAPOKEE TAJI IHARIBIKAYO; bali sisi tupokee TAJI isiyoharibika .26 Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa;
27 bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa”.
Ikiwa hao hawajapewa neema ya kuishinda dhambi kama tuliopewa sisi katika Bwana wetu Yesu Kristo pale tunapomwamini lakini wanao uwezo wa kuyakataa mambo ya kidunia ili tu wasipoteze mataji yao, Inatupasaje sisi tunaojiita wakristo?. Wao wanajua kabisa huko wanapokwenda watakutana na watu wenye ujuzi mkubwa kama wa kwao, hivyo wanagharimika sasa hivi kujitaabisha katika mazingira yote magumu ili watakapoenda kule kushindana na wale wengine iwe ni rahisi kwao kushinda na kupokea tuzo iliyobora ambayo inagombaniwa na wengi
Mtume Paulo aliandika ..
2Timotheo 2: 4 “Hakuna apigaye vita ajitiaye katika shughuli za dunia, ili ampendeze yeye aliyemwandika awe askari.
5 HATA MTU AKISHINDANA KATIKA MACHEZO HAPEWI TAJI, ASIPOSHINDANA KWA HALALI”.
Katika Maneno hayo tunaona Mungu anatufundisha Neno lake katika maisha yanayotuzunguka, kumbuka ukiwa mkristo, haimaanishi kuwa ndio umefika, hivyo kuanzia huo wakati ustarehe tu hapana! ni lazima ujue kuwa huko unapokwenda pia kuna TUZO zimeandaliwa, tena tuzo zenyewe ni tuzo zisizoharibika..na ni watakatifu wengi wanaozigombania, na yeye aliyestahili ndiye atayeipokea Tuzo ya juu zaidi kuliko wengine.. Bwana Yesu alisema “12 Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo”. (Ufunuo 22:12)
Lakini Tuzo hiyo hatuipati kama hatutaziingia gharama kama Paulo alizozisema ..”Ninautesa mwili wangu na kuutumikisha”… Ikiwa wachezaji wa ulimwengu huu wanaitesa miili yao na kuitaabisha (sio kana kwamba wenyewe wana madhaifu hapana! Bali Wanafahamu wanachokitafuta,) watawashinda wakristo kwa kujizuia na mambo mengi ili tu kupokea taji ambayo kesho inakwisha thamani yake..Unadhani inatupasa tuingie gharama kubwa kiasi gani sisi tunaojiita wakristo ili kupokea ile TUZO isiyoharibika (yaani inayodumu milele?)…Bila shaka ni kubwa zaidi ya wale, ni kujizuia zaidi ya wale, ni kujinga na mizigo ya dhambi mara nyingi zaidi ya wale.
Biblia inasema lipo WINGU kubwa la MASHAHIDI linalotuzunguka katika mashindano yaliyopo mbele yetu ukipata nafasi lisome hili wingu lote katika Waebrania sura ya 11, utaona ni jinsi gani walishinda mbio kwa saburi, na kama sisi tusipokuwa na juhudi katika mashindano yaliyowekwa mbele yetu, basi zile tuzo nono kule zitachukuliwa na wengine waliostahili, ukisoma biblia inatuambia watu wale(wingu kubwa la mashahidi) ulimwengu haukustahili kuwa nao,
Walikuwa ni wasafiri duniani, watu ambao mawazo yao waliyaelekeza katika ulimwengu ujao mpaka kuhesabu maisha ya hapa duniani kuwa si kitu (mfano Ibrahimu), mpaka kufikia hatua Mungu mwenyewe anajivunia kuitwa Mungu wao kwa vile walivyoyaelekeza mawazo yao mbinguni, walikatwa na misumeno, walipigwa, walisulibiwa lakini hawakuikana imani yao,na sisi je! Tutapate kuwa kama hao kama tusipojikana na tusipojitesa na kuitumikisha miili yetu sasa hivi?..(soma waebrani 11 yote utaona jambo hilo)
Ukizidi kuisoma habari ya hilo Wingu la Mashahidi mpaka kufikia sura ya 12, ndio mtume Paulo anahitimisha kwa kusema…
Waebrania 12: 1 “Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, NA TUWEKE KANDO KILA MZIGO MZITO, NA DHAMBI ILE ITUZINGAYO KWA UPESI; NA TUPIGE MBIO KWA SABURI KATIKA YALE “MASHINDANO” YALIYOWEKWA MBELE YETU,
2 tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.
3 Maana mtafakarini sana yeye ALIYESTAHIMILI MAPINGAMIZI MAKUU NAMNA HII ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu”.
Dada/Kaka nawe pia hawa wanamichezo wanaokuzunguka wanakufundisha nini? siku ile utajisikiaje kuona waliokuwa warembo kuliko wewe, ambao wangeweza kuutumainia uzuri wao kupata kila kitu katika dunia hii lakini walijizuia na tamaa za kitambo na zaidi ya yote unawafahamu, utajisikiaje kuwaona siku ile wanang’aa kama nyota na wewe unakuwa sio kitu mbele yao milele?, siku ile wanapewa tuzo wewe utakua uko wapi?
Utajisikiaje kuona yupo ndugu unayemfahamu mwenye uwezo kuliko wewe ambaye angeweza kuutumainia uwezo wake kupata kila kitu katika hii dunia lakini alijizuia kwa ajili ya Kristo na kuhesabu dunia ya miaka 70 sio kitu kulinganisha na umilele unaokuja huko mbeleni na siku ile anakuwa mfalme na wewe si kitu..utajisikiaje? ??
Ndugu ufalme wa mbinguni unapatikana kwa nguvu na wenye nguvu ndio wanaouteka biblia inasema hivyo, Weka mbali mambo ya ulimwengu huu, kajiwekee hazina sasa mbinguni, Kama hujamkabidhi Bwana maisha yako huu ndio wakati, fanya hivyo sasa ili uanze kuiunda tuzo iliyo bora tutakapofika kule siku ile….
Swali ni lile lile ninakuuliza tena hawa wanamichezo wanaokuzunguka wanakufundisha nini katika mashindano ya aina yako ya kikristo?.
Mungu akubariki.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali share ujumbe huu kwa wengine na Bwana atakubariki.
Kwa msaada wa maombi/Ushauri/ubatizo/mafundisho/Whatsapp: Namba zetu ni hizi:
+255693036618/ +255789001312
Mada Nyinginezo:
TUKAZE MWENDO KWA TULIYOANDALIWA.
NAOMBA KUJUA UTOFAUTI KATI YA DHAMBI, UOVU NA KOSA KIBIBLIA.
Jina la mwokozi wetu YESU KRISTO lihimidiwe milele na milele.
Huu ni mwendelezo wa kitabu cha Danieli leo tukiwa katika ile sura ya mwisho ya maono Danieli aliyoonyeshwa yahusuyo siku za mwisho. Katika sura hii tunaona Gabrieli akiendelea kumfunulia Danieli mfululizo wa mambo yaliyoanzia sura ile ya 10 na 11 ambapo tuliona jinsi Danieli akiambiwa kwa undani mambo yaliyojiri katika utawala wa Uajemi na Uyunani ambao uliishia na mtawala mkatili wa kiyunani aliyeitwa Antiokia IV Epifane aliyewatesa wayahudi. Lakini tukitazama katika sura hii ya mwisho ya 12 tunaona Danieli akionyeshwa picha (japo kwa sehemu) ya matukio yatakayokuja kutokea katika utawala wa mwisho (yaani RUMI).
Tukisoma ule mstari wa kwanza,..unasema
“Danieli 12:1 Wakati huo Mikaeli atasimama, jemadari mkuu, asimamaye upande wa wana wa watu wako; na kutakuwa na wakati wa taabu, mfano wake haukuwapo tangu lilipoanza kuwapo taifa hata wakati uo huo; na wakati huo watu wako wataokolewa; kila mmoja atakayeonekana ameandikwa katika kitabu kile.”
Kumbuka Mikaeli ni malaika anayesimama kwa ajili ya kulipigania taifa la Israeli (Ni malaika wa vita), hata ukitazama katika sura ya 10, utaona Mikaeli alikuja kumsaidia Gabrieli katika vile vita ili kuufikisha ujumbe wa Mungu, Na amekuwa akiwapigania Israeli dhidi ya wale wakuu (au mapepo) ya Falme zile zote zilizotangulia kuwapo. Hivyo ili Mikaeli na jeshi lake waipiganie Israeli vizuri na kushinda inategemea kiwango cha kumcha Mungu cha wayahudi, kikiwa chini inamaana wale wakuu wa giza wanapata wigo mkubwa zaidi ya kuwatesa watu wa Mungu(Wayahudi), vivyo hivyo kiwango cha kumcha Mungu kikiwa juu, ndivyo Mikaeli na jeshi lake linavyoweza kupata nguvu ya kuipigania Israeli na kushinda dhidi ya wale wafalme wa giza. Kwahiyo vita vya malaika vinatemea hali za kiroho za watu wa Mungu.
Na ndio maana utaona wakati wowote waisraeli wakimuacha Mungu maadui zao wanakuja kuwashambulia, lakini wanapomrudia Mungu na kuzishika sheria zake, Mungu anawaokoa na maadui zao kwa kuwapigania. Na ndivyo ilivyo hata kwa wakristo, Kuna malaika amesimama kwa ajili yetu, hakuna malango yoyote ya kuzimu yatakayosimama mbele ya kanisa la Kristo kama likienda katika hali ya utakatifu.
Tukiendelea katika mstari huu tunaona biblia inasema Mikaeli atasimama, na kutakuwa na wakati wa taabu ambayo haijawahi kutokea tangu Israeli iwe taifa, hii inafunua kuwa mambo hayo yatatokea katika siku za mwisho kwenye ule utawala wa RUMI, wakati wa dhiki kuu pale mpinga-kristo atakaponyanyuka na kuwaua wayahudi wengi, biblia imekiita hicho kipindi kama “wakati wa taabu ya Yakobo (Yeremia 30:7)”
Na ndio kipindi alichotabiri Bwana Yesu katika Mathayo 24: 21 “Kwa kuwa wakati huo kutakuwapo dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe.”.
Na pia pale anasema.”wakati huo watu wako wataokolewa”. hii ikiwa na maana kuwa wayahudi wengi watapewa neema ya kumwamini Yesu Kristo kama ndiye Masihi wao aliyetabiriwa kumbuka kwasasa wayahudi wamefumbwa macho hawamwamini Yesu Kristo lakini watakuja kupewa neema hiyo baadaye.
(Ukisoma Warumi 11: 25 inasema..“Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu UGUMU umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.
26 Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake.
27 Na hili ndilo agano langu nao, Nitakapowaondolea dhambi zao.).
Jambo hili litatimia pale juma la 70 la Danieli litakapoanza ambapo wale wayahudi 144000 watatiwa muhuri kama tunavyosoma katika ufunuo 7.
Tukiendelea mistari inayofuata…
“Danieli 12:2 Tena, wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi wataamka, wengine wapate uzima wa milele, wengine aibu na kudharauliwa milele.
3 Na walio na hekima watang’aa kama mwangaza wa anga; na hao waongozao wengi kutenda haki watang’aa kama nyota milele na milele.”
Hapa tunaweza kuona Danieli akifunuliwa siri zihusuzo ufufuo wa wafu, kwamba wakati utakuja ambapo wafu wote watafufuliwa. jambo ambalo Bwana Yesu alishalizungumzia katika Yohana 5:25”
28 Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake.
29 Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu.”
Kadhalika alionyeshwa pia wenye hekima watang’aa kama mwangaza wa jua, pamoja na hao waongozao wengine kutenda haki. Kila mtu anayawafundisha watu katika njia za haki na utakatifu na kuwafanya watazame mambo ya mbinguni, biblia inasema siku ile atang’aa kama nyota za mbinguni.
Mstari wa 4 unasema..
“4 Lakini wewe, Ee Danielii, yafunge maneno haya, ukakitie muhuri kitabu, hata wakati wa mwisho; wengi wataenda mbio huko na huko, na maarifa yataongezeka.”
Danieli anaambiwa aufunge unabii huo mpaka wakati wa mwisho ulioamriwa ikiwa ikiashiria kuwa wakati wa mwisho(ambao ndio tuliopo sisi) mambo hayo yatafunuliwa, na watu wataelewa yaliyoandikwa humo ndani, na ndio maana ukienda mbele kidogo anasema MAARIFA yataongezeka.
(Maarifa yataongezeka):Kumbuka maarifa haya, ni maarifa ya kumjua Mungu, siku hizi za mwisho maarifa yameongezeka juu ya masuala ya kimungu, japo sio kwa watu wote bali kwa watu wachache wenye hekima, ilikuwa ni ngumu kwa wakati ule wa Danieli, kumuelewa mpinga-kristo atakuja kwa namna gani, au shetani anafanyaje kazi, lakini kwa wakati wetu kwa kupitia Bwana YESU, mambo hayo yapo wazi, na historia ikithibitisha hayo yote kuwa mpinga-kristo atatokea si pengine zaidi ya kanisa Katoliki la RUMI,.
Vivyo hivyo maarifa juu ya utawala wa amani wa YESU KRISTO wa miaka 1000 hayakujulikana kwa wakati ule, lakini sasahivi tunafahamu, n.k.; Na maarifa haya yanaendelea kuongezeka siku baada ya siku kwa msaada wa Roho wa Mungu mpaka tutakapofikia kilele cha utimilifu.
Kadhalika na maarifa katika mambo ya ulimwengu, yameongezeka, kama tunavyoona Jinsi Teknolojia inavyozidi kuongezeka, usafiri umekuwa wa haraka sana, watu wanaenda huku na huko dunia imekuwa kama kijiji. Na maarifa yataongezeka katika kila eneo.
Tukiendelea…
“Danieli 12:5 Ndipo mimi, Danielii, nikatazama, na kumbe, wamesimama wengine wawili, mmoja ukingoni mwa mto upande huu, na mmoja ukingoni mwa mto upande wa pili.
6 Na mmoja akamwuliza yule mtu aliyevikwa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, Je! Itakuwa muda wa miaka mingapi hata mwisho wa mambo haya ya ajabu?
7 Nami nikamsikia yule mtu aliyevikwa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, hapo alipoinua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni; akaapa kwa yeye aliye hai milele na milele, ya kwamba itakuwa wakati, na nyakati mbili, na nusu wakati; tena watakapokuwa wamekwisha kuvunja nguvu za hao watu watakatifu, ndipo mambo hayo yote yatakapotimizwa”.
Tunaona baada ya Danieli kuelezwa juu ya dhiki kubwa itakayokuja huko mbeleni, Hapa tunaona malaika mmoja akimuuliza yule mtu aliyekuwa juu ya mto, kwamba hayo mambo yatadumu kwa miaka mingapi hadi yaishe, ndipo yule mtu akawaambia itakuwa ni kwa wakati na nyakati mbili na nusu wakati (ikiwa na maana ni MIAKA MITATU NA NUSU). Hii inaonyesha kuwa kipindi cha dhiki kuu kitadumu kwa muda wa miaka mitatu na nusu.
Danieli 12:8 Nami nikasikia, lakini sikuelewa; ndipo nikasema, Ee Bwana wangu, mwisho wa mambo haya utakuwaje?
9 Akasema, Enenda zako, Danieli; maana maneno haya yamefungwa, na kutiwa muhuri, hata wakati wa mwisho.”
Tunaona tena hapa Danieli kwa jinsi alivyokuwa “mtafutaji na mchunguzaji” alitaka kujua kwa undani tena juu ya matukio yatakayotokea katika utawala wa mwisho wa Rumi, kama alivyoelezewa na Gabrieli juu ya utawala wa Uajemi na Uyunani katika sura ya 11. Lakini aliambiwa Enenda zako Danieli, maana maneno haya yamefungwa, na kutiwa muhuri mpaka wakati wa mwisho ikiwa na maana kuwa asitafute kujua zaidi ya hapo, kwani yaliyosalia yamewekwa kwa ajili ya watu wa siku za mwisho yaani mimi na wewe.
Swali ni je! Na sisi tunatafuta kufahamu mambo hayo kama Danieli alivyotafuta kujua ya kwake?.
Danieli anaendelewa kuambiwa..
“Danieli 12:10 Wengi watajitakasa, na kujifanya weupe, na kusafika; bali wabaya watatenda mabaya; wala hataelewa mtu mbaya awaye yote; bali wao walio na hekima ndio watakaoelewa.”
Umeona hapo wakati wa mwisho dunia ikiwa katika kilele cha maovu, watu wamemsahau Mungu kwa mambo maovu kama anasa, ulevi, uasherati, matendo ya kikatili, fashion, udanganyifu wa mali n.k. wapo ambao watajitakasa na kujifanya kuwa watakatifu zaidi. Mfano dhahiri tunauona kwa Nabii Eliya wakati Israeli yote imegeukia kuabudu mabaali, na maovu yamezidi kila mahali, na pale Eliya alipojaribu kuwashitaki Israeli wote mbele za Mungu akidhani ya kuwa amebakia peke yake anayemcha Mungu. Lakini Mungu alimwambia kuwa amejisazia watu ELFU SABA wasiopigia goti baali.
Na vivyo hivyo kwa kizazi hichi kilichopotoka pale unapodhani hakuna tena watu wanaompendeza Mungu, hakuna tena wanawake wanaovaa vizuri, hakuna watu wanaomwabudu Mungu katika Roho na kweli , hakuna watakatifu n.k. fahamu kuwa Mungu amejisazia watu wake wachache kila mahali wanaoupendeza moyo wake na hao ndio watakaokuwa na hekima na kuzidi kujisafisha na kuelewa mambo hayo. Lakini kwa wale waovu biblia inasema wataendelea kuwa wabaya na hawatajua chochote na siku ile itawajilia kama mwivi, hivyo jiangalie na wewe upo kundi gani?. Usidanganyike na upepo wa huu ulimwengu kwamba wengi wanafanya hivi na mimi ngoja nifanye..Utaangamia.
Mwisho kabisa Danieli anaambiwa..
“Danieli 12:11 Na tangu wakati ule ambapo sadaka ya kuteketezwa ya daima itaondolewa, na hilo chukizo la uharibifu litakaposimamishwa, itapata siku elfu na mia mbili na tisini.
12 Heri angojaye, na kuzifikilia siku hizo elfu na mia tatu na thelathini na tano.
13 Lakini enenda zako hata utakapokuwa mwisho ule; maana wewe utastarehe, nawe utasimama katika kura yako mwisho wa siku hizo.”
Kuanzia kipindi kile mpinga-kristo atakapoingia katika HEKALU na kuwazuia wayahudi wasiendelee kutoa sadaka ya daima katika nyumba ya Mungu, ambayo itakuja kutengenezwa tena huko Yerusalemu (kumbuka maandalizi yote ya kujengwa sasa hivi yapo tayari), kwahiyo kuanzia hicho kipindi mpaka mwisho wa dhiki kutakuwa na siku 1290.
Sasa kumbuka biblia inasema kipindi cha dhiki kuu kitadumu kwa siku 1260 Yaani miaka mitatu na nusu ambapo mpinga-kristo atakuwa anafanya mauaji duniani kote, lakini hapa utaona zimeongezeka siku nyingine 30 za ziada yaani (1290-1260=30). Hizi siku 30 zilizoongezeka, ni kipindi kinachojulikana kama SIKU YA KUOGOFYA YA BWANA kwa kuajili ya kujilipizia kisasi kwa waovu wote wakaao juu ya nchi. Ni kipindi kitakachodumu katika hizi siku 30 ambacho kitahusisha mapigo ya vile vitasa saba vya ghadhabu ya Mungu. (Ufunuo 16).
Ukiendelea mstari wa 13…utaona kuna siku nyingine tena 45 zimeongezea juu ya zile 1290 na kuwa siku 1335. Hichi kitakuwa ni kipindi cha matengenezo pamoja na hukumu ya mataifa,ambapo Bwana atakuja na mawingu na wafu watafufuliwa wahukumiwe (Ufunuo 20:14).
Hivyo kulingana na ukali wa hiyo dhiki yaani (dhiki ya mpinga-kristo pamoja na mateso ya SIKU YA BWANA) ni watu wachache sana watakaopona (wateule-wayahudi), Biblia inasema katika siku hiyo watu wataadimika kuliko DHAHABU (soma Isaya 13:9-13)
Na kama Bwana Yesu alivyosema katika Mathayo24:
22 “…..kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo.”..Na ndio maana utaona ni siku 1335 ambazo ni chache sana ukilinganisha na kama ingekuwa ni miaka 10 hakika asingepona mtu yeyote.
Mwisho wa yote Danieli anaambiwa “12 HERI ANGOJAYE, na kuzifikilia siku hizo elfu na mia tatu na thelathini na tano.”
Kumbuka ni wayahudi ndio wanaoambiwa HERI wakizifikia hizo siku, hivyo ni uvumilivu na kujificha, na saburi nyingi zinahitajika kwao, pamoja na hekima ya kuzihesabu hizo siku mpaka huo wakati utakapotimia wa Mungu kulipiza kisasi kwa mataifa yote yaliyoshirikiana na yule mnyama ambapo wakati huo Bwana atakapokuja hatarudi peke yake bali atarudi na Bibi-arusi wake(Kanisa) waliokwisha kunyakuliwa kabla ya dhiki kuanza..
Ndipo baada ya hayo utawala wa miaka 1000 utaanza ambapo BWANA atatawala kama MFALME WA WAFALME na BWANA WA MABWANA, na watakatifu wake watakuwa makuhani na wafalme milele na milele. Haleluya.
Je! Ndugu utakuwepo kwenye huo utawala? Je! umeokolewa?, angalia hatari iliyopo mbeleni, shetani anataka ubaki katika hali hiyo hiyo ili siku ile uijutee milele, anataka uzidi kupuuzia ivyo hivyo kila siku, usione kuwa Bwana anakaribia kuja, usipotaka kuacha ulevi,ushirikina, usengenyaji, uzinzi, vimini, suruali, fashion,pornography, kilichosalia mbele yako ni Hukumu tu.
Kumbuka Mungu hapendezwi na kufa kwake mwenye dhambi ..na ndio maana alisema.
Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.”
Mpe Bwana maisha yako leo upate uzima wa milele…usiidharau damu ya thamani iliyomwagika kwa ajili yako pale Kalvari.
Na yeye alisema pale msalabani kwa wale waliompokea.. “IMEKWISHA!!”
Bwana akubariki.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara, kwa njia ya whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255789001312. Na kama utapenda kwa njia ya E-mail basi tuandikie email yako katika boksi la maoni chini.
Mada Nyinginezo:
SEHEMU YA MAANDIKO ILIYOFICHWA.
AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA.
Mungu wetu MKUU YESU KRISTO, asifiwe.
Karibu katika mwendelezo wa kitabu cha Danieli, kama tulivyoona katika mlango uliopita, Danieli akionyeshwa maono yale na Gabrieli, akiwa kando ya ule mto Hidekeli jambo hili tunalisoma katika ile sura ya 10, Lakini kwenye hii sura ya 11 na 12 tunaona ni mwendelezo ule ule wa mazungumzo kati ya Gabrieli na Danieli, Kumbuka baada ya Danieli kujinyenyekeza mbele za Mungu kwa kufunga na kuomba alionyeshwa mambo yatakayokuja kutokea katika kipindi chake na katika nyakati za mwisho, kwa undani zaidi.
Tukisoma…
Mlango 11:1 Tena mimi, katika mwaka wa kwanza wa Dario, Mmedi, mimi nalisimama nimthibitishe na kumtia nguvu.2 Nami sasa nitakuonyesha yaliyo kweli. Tazama, watasimama wafalme watatu katika Uajemi; naye mfalme wa nne atakuwa tajiri kuliko hao wote; naye atakapopata nguvu kwa utajiri wake, atawachochea wote juu ya ufalme wa Uyunani.
Kumbuka sasa hapa ni Gabrieli anazungumza mazungumzo yaliyoanzia tokea sura ya 10, anamwambia Danieli, watasimama wafalme watatu katika ufalme wa Uajemi ambao aliyeko yeye, na watakapoondoka hao atakuja mfalme wa nne, ambaye atakuwa na nguvu kuliko hao wa kwanza. Historia inaonyesha walipita wafalme wanne katika utawala wa Uajemi baada ya Mfalme Koreshi, na inaonyesha huyo mfalme wa nne, alikuwa ni AHASUERO, yule wa malkia Esta, ambaye alikuwa na utajiri mwingi, ndio maana ukisoma kitabu cha Esta utaona aliweza kutawala kutoka bara Hindi mpaka Kushi majimbo 127, hivyo alikuwa ni mtawala mkuu sana, lakini mwisho wa utawala wake, alikuja kushindana na wafalme wa uyunani, lakini hakufanikiwa bali aliangamizwa na ufalme wake ukaanguka katika mikono ya wayunani.
Tukiendelea mstari wa 3-4..
“3 Na mfalme hodari atasimama, atakayetawala kwa mamlaka kubwa, na kutenda apendavyo.
4 Naye atakaposimama, ufalme wake utavunjika, na kugawanyika katika pepo nne za mbinguni; lakini hautakuwa wa uzao wake, wala hautakuwa kama mamlaka yake ambayo alitawala kwayo; kwa maana ufalme wake utang’olewa, hata kwa ajili ya wengine zaidi ya hao. “
Huyu Mfalme Hodari ni “Alexanda mkuu” ndiye aliyesimama na kuiangusha Uajemi, Na historia inaonyesha alikuwa na nguvu nyingi kila mahali alipokwenda kupigana alifanikiwa,hii ndio ile pembe moja mashuhuri ya yule beberu kama tulivyoiona katika ile sura ya 8, lakini kama hapo inavyosema ufalme wake utavunjika, ni kweli maana alikufa katika umri mdogo miaka 32, na uzao wake haukusimama na kuurithi ufalme wake, kinyume chake ufalme wake uligawanyika katika pande nne, zilizomilikiwa na majenerali waliokuwa chini yake ndio zile pepo nne za mbinguni.
Mstari wa 5.
” Na mfalme wa kusini atakuwa hodari; na mmoja wa wakuu wake atakuwa hodari kuliko yeye, naye atakuwa na mamlaka; mamlaka yake itakuwa mamlaka kubwa. “
Historia pia inaeleza baada ya huu Ufalme kugawanyika katika pande nne; kaskazini ilikuwa chini ya Lisimakusi, magharibi chini ya Kasanda, Mashariki chini ya Selekusi na kusini chini ya Ptolemi. Hivyo mmoja kati ya hawa majemedari wake (Alexanda) atakuwa hodari kuliko Ptolemi mfalme wa kusini na huyo sio mwingine zaidi ya SELEKUSI aliyekuwa mfalme wa Mashariki, ambaye historia inasema alifanikiwa kuwaangusha wafalme wale wawili yaani wa kaskazini na wa Magharibi na kumiliki mbili ya tatu ya ufalme wa Alexanda yaani mashariki, magharibi na Kaskazini, wakati Ptolemi alibakiwa na kusini tu.. Hivyo ufalme ukabakia katika pande mbili tu, kaskazini na Kusini.
Tukiendelea mstari wa 6.
“Na baada ya miaka kadha wa kadha watashirikiana; kwa kuwa binti wa mfalme wa kusini atakuja kwa mfalme wa kaskazini, ili kufanya mapatano naye; lakini hatakuwa na nguvu za mkono wake sikuzote; wala mfalme yule hatasimama, wala mkono wake; lakini yule binti atatolewa, na hao waliomleta, na yeye aliyemzaa, na yeye aliyemtia nguvu, zamani zile. “
Baada ya kipindi fulani kupita historia inarekodi Mfalme wa Pili wa Kaskazini (Antiokia Theo) na Mfalme wa tatu wa kusini (Ptolemi Filadelfia) walikuja kufanya mapatano, Mfalme wa kusini alimtoa Binti yake anayeitwa Berenisi, aolewe na mfalme wa kaskazini kwa mapatano kuwa mtoto atakayezaliwa amiliki falme zote mbili yaani ufalme wa Kaskazini na Ufalme wa kusini, Hivyo mfalme wa Kaskazini alimwacha mke wake wa kwanza(aitwaye Laodika) na kumuoa Berenisi na kuzaa naye mtoto.
Lakini biblia inasema hayo hayatawezekana, kwasababu baada ya baba yake Berenisi kufa, Mfalme wa kaskazini alimtalakia Berenisi na kurudiana na mke wake wa zamani Laodika, aliyeachiwa watoto wawili, Hivyo Laodika alipoona amerudishwa katika nafasi yake ya umalkia alimfanyia hila mfalme na kumpa sumu, Hivyo akafungua wigo wa watoto wake kuurithi ufalme, zaidi ya yote alikuja kumuua Berenisi pamoja na mtoto wake ili asipatikane wa kuchukua nafasi ya watoto wake, Hivyo mtoto wa Laodika aliyeitwa SELEKUSI KALINIKUSI akatangazwa kuwa mfalme mahali pa baba yake, ili kutimiza maono Danieli alioonyeshwa kwamba mfalme, wala yule binti wala mkono wake wala aliyemzaa hawatasimama.
Tukiendelea…
“7 Lakini katika chipukizi la mizizi yake atasimama mmoja mahali pake atakayeliendesha jeshi la askari, naye ataingia katika ngome ya mfalme wa kaskazini, na kuwatenda mambo, na kuwashinda;
8 na miungu yao, pamoja na sanamu zao, na vyombo vyao vizuri vya fedha na dhahabu atavichukua mpaka Misri; kisha atajizuia miaka kadha wa kadha asimwendee mfalme wa kaskazini. “
Hili chipukizi la mizizi yake (yaani Berenisi) ambaye atasimama mahali pake, alikuwa ni Kaka yake Berenisi aliyeitwa PTOLEMI UGRETESI aliyerithi ufalme wa kusini baada ya Baba yake na dada yake kufa. Hivyo kwa hasira na ghadhabu ya kuuliwa kwa dada yake alipanga jeshi kubwa na kwenda kupambana na mfalme wa kaskazini, alifanikiwa kuingia kwenye ngome ya kaskazini akisaidiwa na mataifa ya kando kando yaliyokuwa yanamchukia mfalme wa kaskazini, hivyo aliweza kuteka nyara nyingi na kurudi nazo Misri, aliweza pia kuteka majimbo baadhi ya Asia ndogo na Siria yaliyokuwa yanamilikiwa na mfalme wa kaskazini na kuyafanya kuwa yake.
Mstari wa tisa unasema..
“9 Naye huyo ataingia katika ufalme wa mfalme wa kusini, lakini atarudi mpaka nchi yake mwenyewe.
10 Na wanawe watafanya vita, na kukusanya mkutano wa majeshi makuu; watakaokuja na kufurika na kupita katikati; nao watarudi na kufanya vita mpaka penye ngome yake.”
Mistari hii inaonyesha jinsi mfalme wa Kaskazini atakavyokwenda katika ufalme wa Kusini lakini alikuja kurudi katika nchi yake, lakini watoto wake wawili ambaye mmoja wao alikuja kufa baadaye walipanga majeshi kwenda kupigana na mfalme wa kusini ili kulipiza kisasi na kufanikiwa kurudisha majimbo yaliyochukuliwa na mfalme wa Kusini (Ptolemi ugretesi), Hivyo mmoja wa wale watoto aliyeitwa “ANTIOKIA MAGNUSI” alimpiga Ptolemi ugretesi na kufanikiwa kurejesha baadhi ya majimbo yaliyochukuliwa nayo ni Siria na Seleukia.
Tukiendelea..
“11 Na mfalme wa kusini ataingiliwa na ghadhabu, naye atatoka na kupigana naye, yaani, na mfalme wa kaskazini; naye atapanga jeshi kubwa; na jeshi hilo litawekwa mikononi mwake. “
Baada ya Ptolemi ugretesi kufa, “PTOLEMI FILOPATA” akamiliki badala yake, huyu ndiye aliyeingiliwa na ghadhabu kubwa kuona kwamba mfalme wa Kaskazini anamjia na jeshi kubwa, lakini kama biblia inavyotabiri jeshi hilo litawekwa mikononi mwake na ndivyo ilivyokuwa, Mfalme wa Kaskazini alikuja kupigwa na Mfalme wa Kusini katika vita vya Rafia pembezoni mwa Gaza mwaka 217 KK.
Tukiendelea..
“12 Atakapokwisha kuchukua lile jeshi, moyo wake utatukuzwa; naye atawaangusha makumi elfu; lakini hataongezewa nguvu. “
Baada ya kushinda vita dhidi ya ufalme wa Kaskazini moyo wake ulijitukuza..
Tukiendelea..
“13 Kwa maana mfalme wa kaskazini atarudi, naye atapanga jeshi kubwa kuliko lile la kwanza; naye hakika atakuja mwisho wa zamani zile, yaani, baada ya miaka kadha wa kadha, pamoja na jeshi kubwa na mali nyingi.
14 Na zamani zile watu wengi watasimama ili kumpinga mfalme wa kusini; pia, wenye jeuri miongoni mwa watu wako watajiinua ili kuyathibitisha maono; lakini wataanguka.
15 Basi mfalme wa kaskazini atakuja, na kufanya kilima, na kuupiga mji wenye maboma; na silaha za kusini hazitaweza kumpinga, wala watu wake wateule, wala hapatakuwa na nguvu za kumpinga.
16 Maana ajaye kupigana naye atatenda kadiri apendavyo, wala hapana mtu atakayesimama mbele yake; naye atasimama katika nchi ya uzuri, na uharibifu utakuwa mkononi mwake. “
Hili lilikuja kutimia pale Mfalme wa Kaskazini (Antiokia III Magnus) alipopanga majeshi makubwa, na kwenda kupambana na mfalme wa Kusini, na kumshinda, na baadhi ya wayahudi wenye kiburi walimuunga mkono Antiokia kumpinga mfalme wa Kusini,ili kuyathibitisha maono, hivyo ilimsaidia Antiokia kupata nguvu, lakini hawakujua kama hayo yatawageukia kuwa mwiba kwao, kwasababu baada ya huyo atanyanyuka mfalme atakayewatesa na kuwaua. Hivyo aliposhinda akawa na nguvu juu ya NCHI YA UZURI (yaani Israeli) na hakuna taifa lililoweza kusimama dhidi yake.
“17 Naye atakaza uso wake ili aje pamoja na nguvu zote za ufalme wake, naye atafanya mapatano naye; naye atatenda kadiri apendavyo; naye atampa binti wa watu ili amharibu; lakini hilo halitasimama wala kumfaa. “
Zaidi ya yote Antiokia III, alitaka kumiliki mpaka ufalme wa kusini yaani Misri, hivyo alitumia hila kwa kumpa Binti yake (aitwaye Kleopatra) mfalme wa Kusini (Ptolemi) ili kwamba amsaliti na kisha baadaye auchukue ufalme wote lakini hilo halikufanikiwa kwasababu Kleopatra badala ya kumsaliti Ptolemi moyo wake uliambatana naye.
“18 Baada ya hayo atauelekeza uso wake kwenye visiwa, naye atavipiga visiwa vingi; lakini mkuu mmoja ataikomesha aibu iliyoletwa na yeye; naam, aibu yake hiyo atamrudishia mwenyewe.
19 Ndipo atauelekeza uso wake kwenye ngome za nchi yake mwenyewe; lakini atajikwaa na kuanguka, wala hataonekana tena”.
Historia inaonyesha baada ya Antiokia III, kuona amelaghahiwa na binti yake, alimua kuhamishia jitihada zake katika nchi za visiwa vya mbali ambavyo ni Asia ndogo na Ugiriki ili kutanua milki yake, lakini Jenerali mmoja wa Kirumi aliyeitwa “LUKAS KORNELIO SKOPIO” alimpiga na kumshinda kabisa na kumnyang’anya alivyokuwa navyo alipojaribu kuivamia Ugiriki, Hivyo aibu yake ikamrudia mwenyewe kama biblia ilivyosema badala ya kushinda, alishindwa.
Na hata aliporudi kwake hakuwa salama baada ya muda mfupi aliuawa.
Tukiendelea..
“20 Ndipo badala yake atasimama mmoja, atakayepitisha mwenye kutoza ushuru kati ya utukufu wa ufalme wake; lakini katika muda wa siku chache ataangamizwa, si kwa hasira, wala si katika vita. “
Baada ya Antiokia III mfalme wa kaskazini kufa mtoto wake aliyeitwa SELEUKIA FILOPATAalitawala mahali pake, huyu alikuja na sera ya kuongeza kodi katika ufalme wake ili kuzidisha mapato. Alijaribu kufanya hivyo hata katika Israeli na kufikia hatua ya kutaka kujaribu kuteka Hekalu la Mungu lililopo Yerusalemu kwa nguvu lakini hilo halikuwezekana, alikuja kufa baada ya muda mfupi hakufanikiwa kutawala kwa muda mrefu kama Baba zake. Kama ilivyotabiriwa.
“21 Kisha badala yake atasimama mmoja, mtu astahiliye kudharauliwa, ambaye hawakumpa heshima ya ufalme; naye atakuja wakati wa amani, naye ataupata ufalme kwa kujipendekeza. “
Huyu alikuwa ni “ANTIOKIA IV EPIFANE”, ndugu yake Seleukia, alinyanyuka japo alishutumiwa kwa kumuua kaka yake hakupata ufalme kwa njia ya halali, bali alitumia njia za kujipendekeza za kutoa ahadi za kulaghai,kujinyanyua, na rushwa, ili kupata ufalme na jambo hilo lilifanikiwa mikononi mwake. Mfano dhahiri wa mpinga-kristo atakayekuja atatafuta ufalme kwa kujipendekeza.
Mstari wa..
“22 Na wale wenye silaha mfano wa gharika watagharikishwa mbele yake, na kuvunjika, naam, mkuu wa maagano pia.
23 Na baada ya maagano atatenda kwa hila; maana atapanda, naye atakuwa hodari pamoja na watu wadogo.
24 Wakati wa amani atapaingia mahali palipofanikiwa sana pa wilaya hiyo; naye atatenda mambo ambayo baba zake hawakuyatenda, wala babu zake; atatawanya kati yao mawindo, na mateka, na mali; naam, atatunga hila zake juu ya ngome, hata wakati ulioamriwa.
25 Naye atachochea nguvu zake na ushujaa wake juu ya huyo mfalme wa kusini kwa jeshi kubwa; na mfalme wa kusini atafanya vita kwa jeshi kubwa mno lenye nguvu nyingi; lakini hatasimama; maana watatunga hila juu yake.
26 Naam, walao sehemu ya chakula chake watamwangamiza, na jeshi lake litagharikishwa; na wengi wataanguka wameuawa. “
Tunasoma katika historia, Antiokia IV Epifane alishuka kupigana na Misri lakini hakushinda kwasababu Misri ilisaidiwa na Rumi, na zaidi ya yote washauri wake walimfanyia hila hivyo akapigwa katika vita.
“27 Na katika habari za wafalme hao wawili, mioyo yao watanuia kutenda madhara, nao watasema uongo walipo pamoja mezani; lakini hilo halitafanikiwa; maana mwisho utatokea wakati ulioamriwa.
28 Ndipo atakaporudi mpaka nchi yake mwenye utajiri mwingi; na moyo wake utakuwa kinyume cha hilo agano takatifu; naye atafanya kama apendavyo, na kurudi mpaka nchi yake. “
Antiokia alipotoka Misri kwa hasira ya kushindwa vita, alifika Yerusalemu na kuwakasirikia wayahudi pamoja na Hekalu la Mungu, ndipo dhiki ya wayahudi ilipoanzia.
Mstari wa..
“29 Kwa wakati ulioamriwa atarudi, na kuingia upande wa kusini; lakini wakati wa mwisho mambo hayatakuwa kama yalivyokuwa wakati wa kwanza.
30 Maana merikebu za Kitimu zitakuja kupigana naye; basi atavunjika moyo, naye atarudi na kulighadhibikia hilo agano takatifu; na kutenda kadiri apendavyo; naam, atarudi, na kuwasikiliza walioacha hilo agano takatifu.”
Merikebu za Kitimu ni Warumi waliowasaidia wamisri kupigana naye..lakini aligeuza moyo wake ni kurudi Yerusalemu kupambana na hao walioonekana kwenda kinyume na yeye (wayahudi).
“31 Na wenye silaha watasimama upande wake, nao watapatia unajisi mahali patakatifu, ndiyo ngome, nao wataondoa sadaka ya kuteketezwa ya kila siku, nao watalisimamisha chukizo la uharibifu. “
Historia inasema Antiokia IV, aliingia kwenye hekalu la Mungu huko Yerusalemu na kuweka sanamu ya Mungu wake ZEU, na kuwazuia wayahudi wasitoe sadaka za kuteketezwa za daima katika hekalu la Mungu.
Tukiendelea..
“32 Na wao wafanyao maovu juu ya hilo agano atawapotosha kwa maneno ya kujipendekeza; lakini watu wamjuao Mungu wao watakuwa hodari, na kutenda mambo makuu.
33 Na hao walio wenye hekima katika watu watafundisha wengi; hata hivyo wataanguka kwa upanga, na kwa moto, na kwa kufungwa, na kwa kutekwa nyara, siku nyingi.
34 Basi watakapoanguka, watasaidiwa kwa msaada kidogo; lakini wengi wataambatana nao kwa maneno ya kujipendekeza.
35 Na baadhi yao wenye hekima wataanguka, ili kuwatakasa, na kuwasafisha, na kuwafanya weupe, hata wakati wa mwisho; kwa maana ni kwa wakati ulioamriwa, ambao haujaja.
36 Naye mfalme atafanya kama apendavyo; naye atajitukuza na kujiadhimisha juu ya kila mungu, naye atanena maneno ya ajabu juu ya Mungu wa miungu, naye atafanikiwa mpaka ghadhabu itakapotimia; maana yaliyokusudiwa yatafanyika.”
Antiokia ni mfano dhahiri wa mpinga-kristo atakayekuja, kama tunavyosoma kwenye 2Wathesalonike 2:3-4, inasema…3 Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu; yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu.
Hivyo unaona hapo Antiokia ni kivuli halisi cha mpinga-kristo (PAPA) atakayekuja.
“37 Wala hataijali miungu ya baba zake; wala yeye aliyetamaniwa na wanawake; wala hatamjali mungu awaye yote; maana atajitukuza mwenyewe juu ya wote.
38 Lakini katika mahali pake atamheshimu mungu wa ngome; na mungu ambaye baba zake hawakumjua atamheshimu, kwa dhahabu, na fedha, na vito vya thamani, na vitu vipendezavyo.
39 Naye ataziteka nyara ngome zenye nguvu kwa msaada wa mungu mgeni; na yeye atakayemkubali atamwongeza kwa utukufu; naye atawapa kumiliki wengi; naye ataigawa nchi kwa rushwa,
40 na wakati wa mwisho mfalme wa kusini atashindana naye; na mfalme wa kaskazini atamshambulia kama upepo wa kisulisuli, pamoja na magari ya vita, na wapanda farasi, na merikebu nyingi; naye ataingia katika nchi hizo, na kufurika na kupita katikati.
41 Tena ataingia katika hiyo nchi ya uzuri, na nchi nyingi zitapinduliwa; lakini nchi hizi zitaokolewa na mkono wake, Edomu, na Moabu, na wakuu wa watu wa Amoni.”
Hizi nchi za Edomu, na Moabu pamoja na Edomu hakuzigusa kwasababu zilimsaidia kwenda kinyume na Israeli (Nchi ya Uzuri).
“42 Naye ataunyosha mkono wake juu ya nchi hizo, hata na nchi ya Misri haitaokoka.
43 Lakini atakauwa na nguvu juu ya hazina za dhahabu na fedha, na juu ya vitu vyote vya Misri vyenye thamani; na Walibia na Wakushi watafuata nyayo zake.
Historia inaonyesha alifanikiwa kuwa na hazina nyingi za fedha na dhahabu mfano dhahiri wa mpinga-Kristo atakayekuja..(PAPA), Ukitazama utaona hazina kubwa ya dunia sasa ipo Roma.
Mstari wa 44..
“44 Lakini habari zitokazo mashariki na kaskazini zitamfadhaisha; naye atatoka kwa ghadhabu nyingi, ili kuharibu, na kuwaondolea mbali watu wengi.
45 Naye ataweka hema zake za kifalme kati ya bahari na mlima mtakatifu wa uzuri; lakini ataifikilia ajali yake, wala hakuna atakayemsaidia. “
Antiokia IV Epifane alikuja kufa, Kifo chake kilikuja ghafla na hakuna aliyemsaidia pamoja na kujiiunua kwake kama mungu na kujitukuza vile alianguka ghafla,. Kuonyesha kuwa hakuna tumaini lolote kwa mpinga-kristo atakayekuja na kwa watu wake, Biblia inasema.Ufunuo 18:8″ Kwa sababu hiyo mapigo yake yatakuja katika SIKU MOJA, mauti, na huzuni, na njaa, naye atateketezwa kabisa kwa moto. Kwa maana Bwana Mungu aliyemhukumu ni mwenye nguvu. “
Kumbuka Dhumuni kubwa la Gabrieli kumuonyesha Danieli mambo haya yote moja baada ya lingine yatakayotokea katika utawala aliokuwa anaishi na kwa sehemu utawala utakaokuja, ni kumfanya Danieli aelewe mpango wa Mungu kwa kina. Kama tunavyosoma katika sura zilizopita Danieli hakuonyeshwa mambo haya kwa undani juu ya hizi falme kama alivyoonyeshwa katika Sura hii..
Vivyo hivyo na kipindi tunachoishi sasa, Bwana anayo AGENDA, kwa Kanisa lake, lilipotoka,lililopo na linapokwenda! swali ni je! Unafahamu AGENDA ya Mungu kwa wakati unaoishi??..je unajua kuwa kanisa unaloishi ni la mwisho kati ya yale saba ambayo Kristo aliyataja katika Ufunuo 2 na 3,
Je! Unafahamu kuwa mihuri saba ilishafunuliwa?, Je unafahamu kuwa ile chapa ya mnyama imeshaanza kutenda kazi,? tena kibaya zaidi inatenda kazi ndani ya makanisa?..Kama huyafahamu hayo, ni vizuri ukatenga muda umuombe Mungu akufunulie kama Danieli alivyoomba ili siku ile isije ikakujia kama mwivi kwa kukosa kuwa na maarifa..Kumbuka tunaishi katika kizazi ambacho kitaweza kushuhudia kuja kwa pili kwa Kristo, je! umeokolewa?
Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo UTAKATIFU, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao; “
Mungu akubariki.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Katika sura ya 12 tutaona jinsi yule malaika(Gabrieli) akimfunulia Danieli mambo ambayo yatakuja kutokea katika ule ufalme wa mwisho wa RUMI.
Kwa mwendelezo >>> Mlango wa 12
Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara, kwa njia ya whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255789001312. Na kama utapenda kwa njia ya E-mail basi tuandikie email yako katika boksi la maoni chini.
Mada Nyinginezo:
MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA.
JE! MBINGUNI KUTAKUWA NA KULA NA KUNYWA?
Jina la Bwana wetu YESU KRISTO libarikiwe.
Karibu katika mwendelezo wa kitabu cha Danieli, leo tukitazama ile sura ya 10, Kama tukiangalia kwa undani kitabu hichi tutaona kuwa sehemu kubwa ya Unabii Danieli aliopewa ulikuwa unahusu zile FALME 4 zitakazotawala mpaka mwisho wa dunia, ambazo ni 1) BABELI 2) UMEDI na UAJEMI 3) UYUNANI na 4) RUMI.
Lakini kama ukichunguza ile sura ya pili, utaona Danieli alifunuliwa kwa juu juu picha inayohusu falme hizo, kwa kupitia ndoto ya mfalme Nebukadneza aliyoiota juu ya ile sanamu, tunaona pale hakupewa maelezo yoyote marefu kuhusu hizo falme, alionyeshwa tu utaanza ufalme wa kwanza ambao ni wa dhahabu, kisha fedha, halafu shaba na mwisho chuma, hakupewa hata majina ya falme hizo zitakazokuja kutawala baadaye isipokuwa Babeli tu.
Lakini pamoja na hayo Danieli hakuridhika aliendelea kumsihi Mungu amfunulie undani wa mambo hayo na ndio maana tunaweza kuona katika sura ya 7, akionyeshwa maono yanayohusu jambo lilelile isipokuwa hapa yameingia kwa undani zaidi tofauti na alivyoonyeshwa kule kwanza.
Tunasoma aliona wanyama 4 wakitoka baharini ambao ndio zile zile falme 4 zenyewe. Mnyama wa kwanza ndio yule kama simba(Babeli), wa pili alikuwa kama dubu na mifupa mitatu ya mbavu mdomoni mwake ambayo tulishaona tafsiri yake ni nini, wa nne alikuwa mfano wa chui mwenye vichwa vinne, na tunaona Danieli alipewa tafsiri juu ya vichwa vile akaelezwa kuwa watakuwa ni wafalme 4 watakaonyanyuka katika huo utawala wa tatu ambao ni wa uyunani, pia akaonyeshwa mnyama mwingine wa mwisho wa 4 ambaye alikuwa mbali sana na wale wengine kimaumbile.
Pamoja na hayo Danieli katika maono haya alitajiwa na majina ya falme hizi 2 zitakazofuata, tofauti na maono yale ya kwanza hapa alifunuliwa kuwa ufalme wa pili utakuwa ni UMEDI NA UAJEMI, na watatu utakuwa ni ufalme wa UYUNANI. Kwa undani wa maelezo haya unaweza ukasoma mlango wa 7 tuliokwisha kuupitia.
Lakini bado tunaona Danieli baada ya kuona hayo picha bado haikuwa dhahiri kwake hivyo alikuwa na shauku ya kuzidi kufahamu juu ya mambo hayo yataishiaje, na ndio tunaona katika ile sura ya 8 Mungu aliendelea kumfunulia juu matukio yatakayokuwa yanatendeka ndani ya hizo falme, hapa tunaona akionyeshwa yule kondoo mwenye pembe mbili na Beberu, ambapo yule Beberu alikuja kumshambulia yule kondoo na kumuua kwa ile pembe moja aliyokuwa nayo, ambayo baadaye ilikuja ikavunjika na kuzuka pembe nyingine nne.
Sasa Danieli alizidi kuonyeshwa kwa ufafanuzi zaidi mambo yatakayokuja kutokea katikati ya hizi falme, kwamba yule kondoo mwenye pembe mbili ni ufalme wa Umedi na Uajemi, na yule beberu ni ufalme wa uyunani, na ile pembe moja ni mfalme wa kwanza wa uyunani ambaye atanyanyuka na kuuvunja ufalme wa Uajemi, kumbuka mambo hayo yote Danieli hakuonyeshwa katika maono mengine yaliyotangulia, hivyo unaweza ukaona ni mambo yale yale isipokuwa Danieli anafunuliwa kwa undani zaidi, ukiendelea kusoma utaona alionyeshwa pia kutakuwa na pembe nyingine ndogo itakayozuka katikati ya zile pembe 4, itakayojitukuza mbele za Mungu na huyu si mwingine zaidi ya ANTIOKIA EPIFANE 1V. wa uyunani kama historia inavyoonyesha.
Kumbuka Danieli wakati anaonyeshwa juu ya Falme hizi ukisoma katika ile sura ya 7 aliona pembe ndogo(mpinga-kristo) ikizuka katika ufalme wa mwisho wa 4 ambao tunafahamu ni Rumi, lakini hakuonyeshwa pembe nyingine ndogo itakayozuka katika Ufalme wa 3 wa uyunani, lakini hapa tunaona ameonyeshwa pembe hii katika sura hii ya 8. Hivyo tunaona ni mwendelezo wa maono yale yale isipokuwa kwa undani zaidi.
Vivyo hivyo ukiendelea sura ya 10, 11 na ya 12, utaona jinsi Danieli akifunuliwa maono yale yale kwa uchambuzi zaidi, tukio baada ya tukio, mpaka maono yale yakawa dhahiri kwake.
Kwenye Sura hii ya 10 tunaona Danieli akijisogeza mbele za Mungu kwa unyenyekevu akimsihi Mungu ampe ufahamu zaidi juu maono hayo aliyokuwa anafunuliwa na ndio maana utaona baada ya kufunuliwa biblia inasema “alifahamu na kuelewa maono yale”, ikiwa na maana hapo mwanzo mambo yale hayakuelewa vizuri kwake.
Tukisoma..
Mlango 10:1-21”
1 Katika mwaka wa tatu wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, Danieli, ambaye jina lake aliitwa Belteshaza, alifunuliwa neno; na neno lile lilikuwa kweli; maana ni VITA VIKUBWA; naye akalifahamu neno lile, akaelewa na maono hayo.
2 Katika siku zile mimi, Danieli, nalikuwa nikiomboleza muda wa majuma matatu kamili.
3 Sikula chakula kitamu, wala nyama wala divai haikuingia kinywani mwangu, wala sikujipaka mafuta kabisa, hata majuma matatu kamili yalipotimia.
4 Na siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kwanza, nilipokuwa kando ya ule mto mkubwa, Hidekeli;
5 naliinua macho yangu, nikatazama, na kumbe, mtu aliyevikwa nguo za kitani, viuno vyake vimefungwa dhahabu safi ya Ufazi;
6 mwili wake pia ulikuwa kama zabarajadi safi, na uso wake mfano wa umeme, na macho yake kama taa za moto, na mikono yake na miguu yake rangi yake kama shaba iliyosuguliwa sana, na sauti ya maneno yake kama sauti ya umati wa watu.
7 Nami, Danielii, nikaona maono haya peke yangu; maana wale watu waliokuwa pamoja nami hawakuyaona maono haya; lakini tetemeko kuu liliwashika, hata wakakimbia ili kujificha.
8 Basi nikaachwa peke yangu, nikaona maono haya makubwa, wala hazikubaki nguvu ndani yangu; maana uzuri wangu uligeuzwa ndani yangu kuwa uharibifu, wala sikusaziwa nguvu.
9 Walakini naliisikia sauti ya maneno yake; nami niliposikia sauti ya maneno yake, ndipo nikashikwa na usingizi mzito, na uso wangu umeielekea nchi.
10 Na tazama, mkono ukanigusa, ukaniweka juu ya magoti yangu, na vitanga vya mikono yangu.
11 Akaniambia, Ee Danieli, mtu upendwaye sana, yafahamu maneno nikuambiayo, ukasimame kiwima-wima; maana kwako nimetumwa sasa. Na aliponiambia neno hili, nalisimama nikitetemeka.
12 Ndipo akaniambia, Usiogope, Danieli; kwa maana tangu siku ile ya kwanza ulipotia moyo wako ufahamu, na kujinyenyekeza mbele za Mungu wako, maneno yako yalisikiwa; nami nimekuja kwa ajili ya maneno yako.
13 Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga siku ishirini na moja; bali, tazama, huyo Mikaeli, mmoja wa hao wakuu wa mbele, akaja kunisaidia; nami nikamwacha huko pamoja na wafalme wa Uajemi.
14 Sasa nimekuja kukufahamisha mambo yatakayowapata watu wako katika siku za mwisho; maana maono hayo ni ya siku nyingi bado.umed
15 Na alipokwisha kusema nami maneno hayo, nikauelekeza uso wangu chini, nikawa bubu.
16 Na kumbe, mmoja mfano wa wanadamu akanigusa midomo yangu; ndipo nikafumbua kinywa changu, nikanena, nikamwambia yeye aliyesimama karibu nami, Ee Bwana wangu, kwa sababu ya maono haya huzuni zangu zimenipata tena; hata asikusaziwa nguvu.
17 Maana, mtumishi wa Bwana wangu huyu atawezaje kusema na Bwana wangu huyu? Kwa maana kwangu mimi, mara hazikusalia nguvu ndani yangu, wala pumzi haikusalia ndani yangu.
18 Kisha mmoja mfano wa mwanadamu akanigusa tena, akanitia nguvu.
19 Akasema, Ee mtu upendwaye sana, usiogope; amani na iwe kwako, uwe na nguvu, naam, uwe na nguvu. Aliposema nami nikapata nguvu, nikasema, Ee Bwana wangu, na aseme Bwana wangu; kwa maana umenitia nguvu.
20 Ndipo akasema, Je! Unajua sababu hata nikakujia? Na sasa nitarudi ili nipigane na mkuu wa Uajemi; nami nitakapotoka huku, tazama, mkuu wa Uyunani atakuja.
21 Lakini nitakuambia yaliyoandikwa katika maandiko ya kweli; wala hapana anisaidiaye juu ya hao ila huyo Mikaeli, mkuu wenu.
Kumbuka sura hii inaeleza jinsi Gabrieli alivyomtembelea Danieli, akimweleza sababu ya kukawia kwake, kwamaana hata baada ya Danieli kumaliza kufunga na kuomboleza majibu yalikuwa hayajafika bado, Lakini ujumbe kamili Gabrieli aliomletea ulikuwa unahusu maelezo ya ndani kabisa yahusuyo zile falme na sio kitu kingine, ambayo tutakuja kuona katika sura ya 11 na 12.
Lakini katika sura hii tutaona SIRI zilizopelekea Danieli kupokea mafunuo makubwa kama yale, Awali ya yote Danieli alisema NI VITA VIKUBWA, ikiwa na maana kuwa kuna upinzani mkubwa katika kuyapata mambo hayo, Tunaweza kusoma pale Gabrieli alimwambia “Tangu siku ile ya kwanza alipoutia moyo wake ufahamu maombi yake yalisikiwa Lakini mkuu wa ufalme wa uajemi alimpinga siku 21…”
Tunajifunza nini hapo? Mungu huwa hamjibu mtu maombi yake baada ya kufunga na kuomba, hapana bali huwa anamjibu mtu maombi yake pale tu anapotia moyo wake ufahamu, na ndipo maagizo yanatolewa papo hapo na ndio maana Bwana Yesu alisema (Mathayo 6:8) “Baba yetu anajua tunachohitaji kabla hata hatujamwomba” unaona?.. Lakini sasa adui yupo huyo ndiye anayehakikisha majibu hayafiki kwa muhusika, hivyo inahitaji kupigana vita kumshinda.
VITA KATIKA ANGA.
Kama ukisoma hapo juu utaona kuwa mkuu wa ufalme wa uajemi alimpinga Gabrieli, pia ukiendelea kusoma utaona alisema “atakapotoka huko kupigana na mkuu wa uajemi, mkuu mwingine w a Uyunani atakuja”. Sasa kumbuka hawa wakuu wa uajemi na uyunani sio wafalme wa dunia, bali ni roho za mashetani zilizokuwa zinaendesha hizo falme 4 za dunia, kumbuka wakati Danieli anafunuliwa maono haya alikuwa katika Ufalme wa Uajemi, Babeli ilikuwa imeshaanguka, Hivyo mkuu wa ufalme wa Babeli (PEPO) alikuwa ameshaondoka, lililopo hapo ni la uajemi, kisha litakuja PEPO la Uyunani na mwisho litakuja la RUMI, ambalo ndio lipo sasahivi likitenda kazi.
Lakini kumbuka kama biblia inavyosema Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya FALME na mamlaka, juu ya WAKUU WA GIZA HILI, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. “
Neno hilo likiwa na maana kuwa hatutumia njia za kibinadamu kushinda na hizi FALME za giza, Kushindana kwetu sio kusema ninatuma kombora, au moto, kuzimu, au maombi ya kuteketeza anga na wakuu wa anga, hapana Danieli hakufanya hivyo, njia hiyo ni kwa namna ya damu na nyama na haiwezi kumshinda shetani hata kidogo, bali biblia inaendelea kusema..
Waefeso 6: 13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.
14 Basi simameni, hali mmejifunga KWELI viunoni, na kuvaa dirii ya HAKI kifuani,
15 na kufungiwa miguu UTAYARI tupatao kwa Injili ya amani;
16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya IMANI, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.
17 Tena ipokeeni chapeo ya WOKOVU, na upanga wa ROHO ambao ni NENO LA MUNGU;
Hivyo malaika kabla ya kuwasilisha maombi ya mtu kwanza huwa anakutana na MSHITAKI HAPO JUU (mkuu wa giza na mapepo yake), ambaye anatushitaki sisi mbele za Mungu (Ufunuo 12:10)kwa kuonyesha kwamba hatustahili kukipokea kitu tunachokiomba, na hoja yake ikiwa na nguvu, majibu hayatufikii anayazuia kwa kuwa ana hati miliki yako, (kwamfano, mtu anaomba jambo fulani kwa Mungu halafu bado anamashaka mashaka kama kweli atajibiwa maombi yake au la!. biblia inasema lolote muombalo aminini ya kwamba mmepokea nalo litakuwa lenu. Sasa mwovu, akikuangalia na kuona kuwa hauna Imani ya kupokea jambo hilo mitikisiko fulani inakutokea unakataa tamaa, yeye anatumia hiyo nafasi kukushitaki mbele za Mungu kuwa huyu mtu hana uhakika na anayemwomba hivyo hastahili kupokea hicho kitu, hapo shetani anakuwa ameshinda vita, hivi ndio vita vinavyopiganwa. Na ndio maana biblia inasema Imani ni ngao itakayoweza kuzima mishale yote ya moto ya yule mwovu.
Yakobo 1:5-8″ Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.
6 Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku.
7 Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana.
8 Mtu wa nia mbili husita-sita katika njia zake zote. “
Mfano mwingine mtu anaomba Neno fulani kwa Mungu, halafu hajakoloewa, tatizo sio kwamba maombi yake hayajasikiwa, hapana bali MKUU WA GIZA yupo hapo juu akipeleka hoja juu ya maisha yako mbele za Mungu, kwamba Neno linasema ” Mtu yeyote asiye na Roho wa Kristo huyo sio wake (Warumi 8:9)” Hivyo yule malaika aliyetumwa kukuletea majibu akikutana na hoja zenye nguvu kama hizo atakwama, maana yule mshitaki atamwambia, Mtu huyu ni mali yangu kwasababu hana Roho wa Mungu, hivyo haya majibu hayamuhusu. Sasa mtu wa namna hii kakosa CHEPEO YA WOKOVU na UPANGA WA ROHO. hivyo lazima vita hivi vimshinde tu na akose anachokitafuta.
Mfano mwingine mtu anayeabudu sanamu (sanamu za bikira Maria, na watakatifu, pamoja na kusali rozari), halafu bado unakwenda kumwomba Mungu, mkuu wa giza atapeleka hoja, za kimaandiko “Kutoka 20:4 inasema Mungu atawapatiliza maovu yao hao wote wanaoabudu sanamu kwa wivu wake”, Hivyo badala ya kupokea baraka, yanageuka kuwa laana kwa mtu huyo.
Neno la Bwana linasema..
Ezekieli 14: 3, & 7-8 “Mwanadamu, watu hawa wametwaa VINYAGO vyao na kuvitia mioyoni mwao, nao wameweka kwazo la uovu wao mbele ya nyuso zao. Je! Ni laiki yangu NIULIZWE na wao katika neno lo lote?
…….7 Kwa maana kila mtu wa nyumba ya Israeli, au wa wageni wakaao katika Israeli, ajitengaye nami, na kuvitwaa vinyago vyake na kuvitia moyoni mwake, na KULIWEKA KWAZO LA UOVU MBELE YA USO WAKE, kisha kumwendea nabii, na kuniuliza neno kwa ajili ya nafsi yake; mimi, Bwana, nitamjibu, mimi mwenyewe;
8 nami nitaukaza uso wangu juu ya mtu yule, na kumfanya kuwa ajabu, awe ishara na mithali, nami nitamkatilia mbali, asiwe kati ya watu wangu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana. “
Kwahiyo kwa Danieli mpaka majibu kama hayo kumfikia, aliweza kumshinda (mkuu wa uajemi) katika nyanja zote katika ulimwengu wa roho, hivyo shetani alishindwa kwasababu hakuwa na hoja yoyote ya kumshitaki mbele za Mungu yamfanye asipokee majibu yake.
Na faida aliyoipata Danieli baada ya kushinda tunaweza kuiona katika sura zinazofuata, Mungu aliweza kumfunulia agenda na mpango mzima wa mambo yanayokuja mbeleni juu ya ufalme aliokuwepo na unaokuja wa Uyunani pamoja na ule wa mwisho. hatua kwa hatua tofauti na maono aliyokuwa anayaona mwanzo, mambo hayo utayaona katika sura ya 11 na 12.
Kwahiyo kwa ujumla tunaweza kujifunza katika sura hii Danieli ni mtu aliyekuwa anahama kutoka utukutu hata utuktufu, ono moja halikumfanya aridhike na hali aliyopo aliendelea kutafuta kwa kusoma vitabu na kuomba mpaka mambo yote ya mbeleni yakawa wazi kwake, na sisi vivyo hivyo tunahitaji kusoma sana maandiko na kuomba, mpaka mambo yatakayotukabili huko mbeleni yawe wazi kwetu, hatupaswi kuridhika tu katika hali tulizopo angali tukijua hatufahamu yanayokuja mbeleni.
Biblia inasema Bwana Yesu alikuwa akiongezeka KIMO na HEKIMA, kumbuka sio KIMO cha urefu bali Kimo cha kumjua Mungu, na aliongezeka hekima pia ya kuyajua mapenzi ya Mungu, ikiwa na maana kuwa alipozaliwa sio kwamba alikuwa anajua kila kitu kama ndio hivyo alipokuwa na miaka 12 asingekuwa anawasikiliza na kuwauliza maswali marabi, Hii inaonyesha kuwa alikuwa anakua kwa hekima. Sasa kama yeye ambaye ni Bwana wetu alifanya hivyo inatupasaje sisi?. Tunapaswa tukue tufikie cheo cha kimo cha utimilifu wake (Waefeso 4:13).
Kumbuka pia mkuu wa giza tulilopo sio tena wa uyunani au uajemi bali ni RUMI, na ni roho inayowapofusha watu wasione mbele, wala wasitake kufahamu mambo ya mbele kama wale wengine walivyomzuia Danieli asione mambo ya mbeleni, kwahiyo fahamu kuwa vita vilivyopo sasahivi ni vikubwa kuliko vile vya Danieli. Si ajabu watu wamepoteza hamu ya kufahamu mambo ya mbeleni na mbinguni, injili wanazopenda kuzisikia ni za mafanikio tu, na mambo ya ulimwengu huu yanayopita, ni dhahiri kabisa mkuu wa giza hili amewapofusha macho.
Hivyo ndugu kama unaabudu sanamu, kama hujaokolewa, kama unaishi katika dhambi, kama Huliamini Neno la Mungu, una mashaka upo vuguvugu, fahamu upo chini ya mamlaka ya mkuu wa anga hili, na yeye ndiye mshitaki wako mbele za Mungu usiku na mchana ili usione mambo ya mbeleni au usipokee baraka za Mungu na mwisho kabisa usiione mbingu.
Bwana akubariki.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Kwa mwendelezo >>> Mlango wa 11
Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara, kwa njia ya whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255789001312. Na kama utapenda kwa njia ya E-mail basi tuandikie email yako katika boksi la maoni chini.
Mada Nyinginezo:
VITA VYA KIFIKRA BAADA YA KUZALIWA MARA YA PILI.
NIFANYE NINI ILI NIIKWEPE HUKUMU.