Category Archive Home

Yesu alikuwa na maana gani aliposema ‘tena siku ile hamtaniuliza neno lolote (Yohana 16:23)

SWALI: Yesu alikuwa na maana gani aliposema ‘tena siku ile hamtaniuliza neno lolote ’

Kwanini ajiangue kwa namna hiyo angali yeye ndiye mwokozi wa kutegemewa kila kitu?

Yohana 16:23

[23]Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu.

JIBU:

Kama tunavyojua hakukuwahi kutokea kiongozi aliyekuwa na matokeo makubwa duniani kama Yesu Kristo.

Namna ya uongozi wake, Kwa jinsi ulivyokuwa thabiti na bora Matokeo yake ndio tunayoana mpaka sasa duniani kwenye imani.

Hivyo maisha yake na huduma yake sio tu vinatufundisha njia ya wokovu lakini pia vinatufundisha namna kiongozi bora anavyopaswa Awe.

Matokeo Ya mitume wake kuwa nguzo kwa makanisa ya vizazi vyote ni matokeo ya namna ambavyo alivyowakuza anawakuza.

Bwana Yesu hakutengeneza Wafuasi, bali alitengeneza watu kama Yeye…Na hivyo katika kuwafundisha wanafunzi wake aliwakuza Ki vitendo zaidi kuliko maneno ya vitabu vingi vya kidini na mapokeo.

Kwamfano utaona kuna mahali anawatuma wawili waenda kuhubiri injili mahali ambapo angepaswa kwenda yeye mwenyewe, lakini aliwaacha waende.

Luka 10:1

Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.

Mahali pengine aliwaacha watoe pepo na waliposhindwa hakusema ‘wanangu nyie ni wachanga, basi nitakuwa nawasaidia tu’…hapana Kinyume chake aliwakemea Kwa upungufu wa imani zao.

Vivyo hivyo katika tukio hili, wanafunzi wake walitarajia kila siku watakaa naye wamuulize maswali yeye, kisha awajibie kutoka kwa Baba.. Ni sawa na mtoto mchanga ambaye kila siku anasubiria atafuniwe tu chakula apewe…unadhani hilo litaendelea sana?

Vivyo hivyo hilo halikuwa lengo la Bwana Yesu, bali alitaka kuwafundisha kanuni za wao wenyewe kumuuliza Mungu na kujibiwa moja kwa moja kama yeye alivyokuwa anajibiwa…

Na njia moja wapo ilikuwa ni yeye kuondoka, kisha kwa kile kitendo cha wao kumkosa Bwana wa kumuuliza, wajifunze kuomba kisha Roho ajae ndani yao, ndipo waanze sasa kupokea mafunuo ya kweli na ujasiri kutoka kwa Mungu..

Lakini pia waombe jambo lolote kwa jina la Yesu, wapokee mahitaji yao. Na Kweli mambo hayo yalianza Kutokea baadaya ya Pentekoste.. wote walikuwa ni kama ‘Yesu-dunia’ hakuna hata mmoja alifikiri au kuwaza kwamba kuna umuhimu tena wa Yesu kutembea nao, kimwili bali waliweza kuyafanya yote.

Hiyo ni tabia ya kiongozi bora…huwafanya wanafunzi wake kuwa kama yeye, na wakati mwingine kutenda hata zaidi ya yeye…Yesu aliwainua zaidi kwa kusema.

Yohana 14:12

[12]Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba.

Hiyo ndio sababu kwanini aliwaambia hayo maneno.

Yohana 16:23-24

[23]Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu.

Hata sasa Bwana anataka kuona ukomavu kama huu ndani ya maisha ya wakristo wengi.. Ikiwa kila siku utakuwa unategemea Mchungaji wako akuombee, ni lini utaweza wewe mwenyewe kuomba na kuwaombea wengine? Sababu ya watu wengi kutojibiwa maombi yao na Mungu ni hiyo.. Ameshakomaa kiroho, Mungu anaona anaouwezo wa kupambana na tatizo yeye mwenyewe, atataka kiongozi wake amsaidie..

Hicho kitendo kinapunguza utendaji Kazi wa nguvu za Mungu, kwasababu yeye hataki tumgeuze mwanadamu Mungu..Ukiokoka, fahamu kuwa Roho Mtakatifu yupo ndani yako, na kuanzia huo wakati na kuendelea unawajibu wa kuufanyia mazoezi wokovu wako, jifunze kuomba mwenyewe, jifunze kuombea watu, soma biblia mwenyewe Mungu akufundishe..

Hizo ndio hatua bora za ukuaji kiroho.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUNA WAKATI YESU ATAPITA NA WATU HAWATAJUA.

TOFAUTISHA KATI YA MAFUNDISHO YA YESU, NA YA WAANDISHI.

ALITOKA HUKO, AKAENDA MAHALI KARIBU NA JANGWA.

Print this post

FAIDA NYINGINE YA MAOMBI YA KUSHUKURU.

Jambo jingine Kuu la kujifunza kama mkristo ni Kumshukuru Mungu kila wakati na kwa kila jambo, kwamaana maandiko ndivyo yanavyotufundisha..

1Wathesalonike 5:18 “shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu”.

Kuna mambo yanafunguka tu yenyewe baada ya kumshukuru Mungu!..haihitaji nguvu nyingi.. Maombi ya shukrani ni maombi yanayougusa moyo wa Mungu zaidi hata ya kupeleka mahitaji!, kwani ni yanauelezea uthamani wa Mungu katika maisha ya mtu, ni maombi ya kushuka sana na ya kuithaminisha kazi ya Mungu katika maisha yako au ya wengine, na hivyo ni maombi yenye nguvu sana na kuugusa moyo wa Mungu kuliko tunavyofikiri.

Na kiuhalisia maombi ya kushukuru ndiyo yanayopaswa kuwa maombi ya kwanza kabisa kabla haya yale ya toba na mahitaji..kwasababu, uzima tu ulionao ni sababu ya kwanza kumshukuru Mungu, kwasababu usingekuwa nao huo hata maombi mengine usingeweza kuomba..

Leo tuangalie faida moja ya kumshukuru Mungu, kwa kujifunza kupitia Bwana wetu YESU KRISTO.

Kama wewe ni msomaji wa Biblia utagundua kuwa kila wakati ambapo Bwana YESU alitaka kufanya MUUJIZA usio wa kawaida, alianza kwanza kwa kushukuru..

Kwamfano kipindi anaigawa ile mikate kwa watu elfu nne alianza kwanza kwa kushukuru..

Mathayo 15:33 “Wanafunzi wake wakamwambia, Tupate wapi mikate mingi hapa nyikani, hata kushibisha mkutano mkuu namna hii?

34 Yesu akawaambia, Mnayo mikate mingapi? Wakasema, Saba, na visamaki vichache.

35 Akawaagiza mkutano waketi chini;

36 akaitwaa ile mikate saba na vile visamaki, AKASHUKURU AKAVIMEGA, akawapa wanafunzi wake, nao wanafunzi wakawapa makutano.

37 Wakala wote wakashiba; wakayaokota masazo ya vipande vya mikate makanda saba, yamejaa”.

Pengine unaweza usione uzito wa shukrani katika huo muujiza wa mikate… hebu tusome mahali pengine palipoonesha kuwa ni SHUKRANI ya Bwana ndio iliyovuta ule muujiza mkuu wa mikate.

Yohana 6:23 “(Walakini zikaja mashua nyingine kutoka Tiberia mpaka karibu na mahali pale walipokula mikate, WAKATI BWANA ALIPOSHUKURU)”..

Hapo anasema.. “wakati Bwana aliposhukuru”… Kumbe! Ile shukrani ilikuwa na maana kwa  sana kwa muujiza ule kutendeka.. Na wala pale hapaonyeshi kwamba Bwana YESU alimwomba Baba augawe ule mkate!.. la! Bali alishukuru tu kisha akaumega!, muujiza ukatendeka.

Kuna mambo mengine unahitaji kushukuru tu na kuendelea mbele!, na mambo yatajiweka sawa yenyewe, kuna nyakati hutahitaji kuomba sana.. bali kushukuru tu, na kumwachia Bwana..na maajabu yatatendeka..

Pia utaona kipindi kile kabla ya Bwana kumfufua Lazaro alianza kwanza kwa KUMSHUKURU MUNGU..

Yohana 11:39 “Yesu akasema, Liondoeni jiwe. Martha, dada yake yule aliyefariki, akamwambia, Bwana, ananuka sasa; maana amekuwa maiti siku nne.

40 Yesu akamwambia, Mimi sikukuambia ya kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu?

41 Basi wakaliondoa lile jiwe. Yesu akainua macho yake juu, akasema, BABA, NAKUSHUKURU KWA KUWA UMENISIKIA.

42 Nami nalijua ya kuwa wewe wanisikia sikuzote; lakini kwa ajili ya mkutano huu wanaohudhuria nalisema haya, ili wapate kusadiki kwamba ndiwe uliyenituma.

43 Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje.

44 Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake amefungwa leso. Naye Yesu akawaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake”.

Umeona? Ni shukrani tu, ndio iliyomtoa Lazaro kaburini..

Je na wewe unayo desturi ya kumshukuru Mungu?..  Maombi ya shukrani yanapaswa yale maombi marefu sana,  kwani tunazo sababu nyingi sana za kumshukuru Mungu, kama umeokoka, huo wokovu ulio nao ni sababu ya kumshukuru Mungu hata masaa sita mfululizo, kwasababu kama ungekufa kabla ya kuokoka leo ungekuwa wapi?.

Kama unapumua hiyo ni sababu ya kumshukuru Mungu, kwasababu wapo walioondoka na wengine ni wema kuliko hata mimi na wewe.

Na zaidi ya yote si tu kushukuru kwa mambo mema au mazuri Mungu anayokutendea, bali hata kwa yale ambayo yameenda kinyume na matarajio yako, ni lazima kushukuru, kwasababu hujui kwanini hiyo jambo limekuja kwa wakati huo, endapo Ayubu asingemshukuru Mungu kwa majaribu aliyokuwa anayapita zile Baraka zake mwishoni asingeziona.

Ni hivo hivyo mimi na wewe, hatuna budi kumshukuru Mungu kwa vyote, viwe vizuri au vibaya.. kwasababu tunajua mwisho wake utakuwa mzuri.

Yeremia 29:11 “Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UNAZO KILA SABABU ZA KUMSHUKURU MUNGU

Kwanini BWANA awaagize wakoma wakajionyeshe kwa Makuhani?(Luka 17:14

KWA KUWA FURAHA YA BWANA NI NGUVU ZENU. 

Maombi kama sehemu ya maisha ya mwamini mpya.

Nini maana ya Selahamalekothi?

Print this post

Je mapepo yanakufa? Na kama hayafi, tunashindanaje vita vya kiroho?

SWALI: Je mapepo yanakufa? Na kama hayafi, ni vita ya namna gani tunashindana nayo katika ulimwengu wa Roho?


JIBU: Katika biblia tunaposoma Neno “pepo”, ni vema tufahamu ufunuo wake upo katika namna mbili;

  1. Pepo: Kama malaika muasi
  2. Pepo: Kama pando la malaika muasi

Yote mawili unapaswa kufahamu, Ili ujue ni nani unashughulika naye katika vita hivyo vya kiroho.

Kwamfano, ukisoma ile waefeso 6:12 inayosema kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama, bali juu ya falme na mamlaka na wakuu wa giza hili pamoja na majeshi ya mapepo wabaya.. Sasa hao wanaotajwa hasaa ni malaika waasi.

Lakini hawa malaika waasi, huwa na mapando yao, ambayo huyapanda ndani ya watu, mfano wa hayo ni magonjwa, ukichaa, ububu, udhaifu (Marko 9:25)uuaji, uchungu, majivuno, kiburi, masengenyo n.k.. na haya mapando wakati mwingine huitwa mapepo, kwasababu asili yao ni kutoka kwa hao malaika waasi.

Luka 13:11 Na tazama, palikuwa na mwanamke aliyekuwa na pepo wa udhaifu muda wa miaka kumi na minane, naye amepindana, hawezi kujinyosha kabisa.

Pepo linalozungumziwa hapo, hasaa sio yale mashetani, bali ni pando la udhaifu waliloliweka ndani ya huo mwanamke.

Hizi zote ni kazi za shetani na malaika zake duniani. Sasa mapando haya ndio tunaweza kuyaua (kwa kuyang’oa), lakini sio wale malaika waasi. Ndio maana Bwana Yesu alisema..

Mathayo 15:13 Akajibu, akasema, Kila pando asilolipanda Baba yangu wa mbinguni litang’olewa

Wale malaika waasi (yaani wakuu wa giza, wafalme, majeshi ya mapepo yote)hatuwezi kuwaua, kwa maombi au kwa namna yoyote, isipokuwa tayari wameshawekewa hukumu yao, siku ile ya mwisho ambapo watatupwa wote kwenye lile ziwa la moto.

Na mapando haya, Bwana Yesu alitoa maelezo yake vema, wakati ambapo adui hupandwa ndani ya mtu..

alisema.

Mathayo 13:24 Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;
25 lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
26 Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.
27 Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu?
28 Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye?
29 Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo.
30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu.

Kumbe wakati ambapo watu wamelala, ndipo hupanda mbegu zake. Yaani wakati ambapo watu wamekuwa walegevu kiroho ndipo shetani hupata nguvu ya kuja kupachika, mbegu zake za uharibifu, zitakazokuja kusumbua baadaye. Ndio maana ni lazima ujue kanuni mbalimbali za kumpinga shetani.

Na haya mapando, yanaweza kuwekwa kwa mtu yeyote, hata mtu aliyeokoka, anaweza kuwa nayo. Ndio maana utaona wapo watu wengine wameokoka, lakini wanasumbuliwa na mapepo, kiuhalisia, hawana malaika wale waasi ndani yao, wanayo mapando yao.

Ni sawa, na mtu ambaye anamilika chombo kama komputa, akiwa anaitumia kwa matumizi yake tu ya sikuzote, tu ambayo ni lazima, si rahisi computa hiyo kuvamiwa na virusi, lakini akianza kutembea mitandaoni, kisha kubofya, au kupakua kila kitu anachokiona ni wazi kuwa chombo hicho kipo hatarini kuvamiwa na virusi, na matokeo yake ni kuwa mfumo wote wa kumpyuta unaliwa, au kuharibifu chombo kabisa, ndio maana wanaweka ulinzi (anti-virus) sikuzote,

Vivyo hivyo na maisha ya mwanadamu yakiwa ovyo ovyo, hawezi kukwepa mapando ya mashetani ambayo yamezaa kila mahali. Mtu yeyote ambaye hajaokoka tayari kuna pepo fulani ndani yake.

Kwamfano, mwingine, labda mkristo  ameokoka, halafu akiwa kanisani, anaanza kuruhusu masengenyo kinyume na mchungaji wake, au mama-mchungaji, sasa mtu kama huyo akiwa anaendelea na tabia hiyo..matokeo yake ni kwamba pepo la uchungu litamvaa, ataanza kuwachukia viongozi wake hata bila sababu, na kuzusha vita, na uharibifu hata  wengine. Yeye atadhani ni tabia yake kumbe sio, bali pepo limeshamvaa la uchungu.

Nikupe huu ushuhuda, Kulikuwa na mama mmoja kanisa, kipindi chote ulikuwa ukikutana naye, anamzungumzia vibaya mama mchungaji wa kanisa alilokuwa mwanzo, hapo mwanzo alikuwa vizuri tu kiroho, lakini kwa jinsi siku zilivyozidi kwenda, akiendeleza chuki zake, , hali yake ilikuja kubadilika ghafla, akaomba tumwombee, tulipomwombea alilipuka mapepo, lile pepo likawa linasema “mama mchungaji” yaani asili yangu ni chuki kwa mama mchungaji, tulipolikemea likamwacha akarudia hali yake ya kawaida, akawa mtu mzuri tu.

Samsoni, alipokwenda kuwashindana na wafilisti, hakushughulika  kwanza na wafilisti, bali mashamba yao ya ngano. (mapando yao). Kwa kuyachoma moto. Vivyo hivyo na sisi ili tuyamalize nguvu haya mashetani, tuangushe ngome zao. Ni lazima fikra zetu hasaa zielekee mapando yao.

NAMNA YA KUSHINDANA VITA VYA KIROHO:

Injili:

Kwamfano kuwaangusha wakuu wa giza sio kuwatumia makombora ya moto hapo angani. Hapana, bali ni kwenda kuhubiri injili ili watu wamsikie Kristo waokoke,

Ndio maana Yesu alipowatuma wanafunzi wake wawili wawili kuhubiri waliporudi Yesu aliwaambia ‘nalimwona shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme’.

Kumbe anguko lake lilikuwa katika kuhubiri na si kumtumia makombora.

Maombi:

Hii ni silaha kubwa, ya kumpinga shetani. Maombi huruhusu, utendaji kazi wa Mungu ndani ya maisha ya mwamini, usipokuwa mwombaji tarajia shetani kuyapangalia maisha yao. Yesu alituagiza tukeshe kuomba tusije ingia majaribuni.

Upendo:

Upendo hupinga, wivu, chuki, uchungu, mashindano, uzinzi, n.k. ambayo haya yote huzaliwa mahali ambapo hapana upendo. Ni lazima kila siku wewe kama mwamini kila siku ujifunze kutendea kazi upendo….ili uondoe mazingira ya mashetani kuangua mayao yao hapo.

Neno:

Ukiwa na Neno la Mungu la kutosha ndani yako, adui hawezi kukushinda. Utakumbuka kule jangwani, shetani alipojaribu kumpandia Kristo maneno ya uongo kwa kupitia biblia, yeye mwenyewe alilitumia Neno la Kweli, kumpinga. Watu wengi wanavamiwa na maroho ya upotevu, kwasababu hawana Neno la Mungu mioyoni mwao. Jifunze kusoma biblia. Ni silaha inayoitwa Upanga.

Imani:

Imani huzaa ujasiri, na ujasiri hutoa mamlaka ndani yako. Biblia huiita imani “Ngao” Shetani anapenda kutumia silaha ya woga, ili kuzimisha utendaji kazi wa Mungu mioyoni mwetu. Hatuna budi kusimama kwa utimilifu wa imani kumtumikia Mungu.

Kukemea:

Fahamu adui ni mpingamizi sikuzote, hapembelezwi, bali analazimishwa kutoka, Yesu alimkemea shetani alipotaka kumjaribu kwa kinywa cha Petro, aliyakemewa mapepo yote sugu, yaliyokuwa ndani ya watu yawatoke. Hivyo na wewe pia ukutanapo na kazi hizi za mwovu, jifunze kutumia kinywa chako, kwa mamlaka uliyopewa na Kristo kukemea haraka sana, kila pepo, au kimelea chochote cha uovu kinachozaliwa na adui.

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa, mashetani hawafi, lakini kazi zao zinakufa.. Hatuwaui hao, bali tunaziua kazi zao. Usipoteze muda mwingi kumrushia shetani mabovu hawezi kufa, bali tuma nguvu zako nyingi kurushia mabovu mapanda yake, kwa kanuni hizo tulizojifunza. Utawashinda kabisa kabisa.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?

MWANAMKE, USIFUNGUE MLANGO WA MAPEPO KUKUINGIA!.

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?

Print this post

LINDA CHEMCHEMI YA MOYO WAKO.

Mithali 4:23 “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako CHEMCHEMI ZA UZIMA”.

Chemchemi kazi yake ni kutoa “maji ya kunywa” lakini pia ya maji ya “kustawisha mimea”.

Kama chemchemi ikitoa maji ya chumvi au ya magadi, ni wazi kuwa maji yake hayatafaa kwa matumizi yoyote yale, hivyo mahali hapo hapana uhai, watu hawawezi kuishi wala wanyama wala mimea..

Lakini kama chemchemi ikitoa maji safi yasiyo na magadi wala chumvi, na tena masafi, basi mahali pale kila kitu kitasitawi ikiwemo watu, wanyama na mimea, na hata shughuli zote nyingine za kiuchumi.

Mfano wa maji machungu na yasiyofaa ni yale wana wa Israeli waliyokutana nayo kule ‘Mara’

Kutoka 15:22 “Musa akawaongoza Israeli waende mbele kutoka Bahari ya Shamu, nao wakatokea kwa jangwa la Shuri; wakaenda safari ya siku tatu jangwani wasione maji.

23 Walipofika mahali palipoitwa Mara hawakupata kuyanywa yale maji ya Mara, kwa kuwa yalikuwa machungu; kwa ajili ya hayo jina lake likaitwa Mara.

24 Ndipo watu wakamnung’unikia Musa, wakisema, Tunywe nini?

25 Naye akamlilia Bwana; Bwana akamwonyesha mti, naye akautia katika hayo maji, maji yakawa matamu. Basi akawawekea amri na hukumu huko, akawaonja huko”.

Sasa Biblia inafananisha “Mioyo yetu na chemchemi zinazotoa maji”… Maana yake yanayotoka mioyoni mwetu yanaweza kukuza, kustawisha au kudhoofisha afya zetu, wanyama wetu, mimea yetu…kwaufupi kila kitu kinachotuzunguka ikiwemo kazi zetu, elimu zetu, nafasi zetu, kibali chetu na mambo mengine yote yanategemea sana yanayotoka mioyoni mwetu.

Sasa najua utauliza haya maji machungu au matamu ni nini?.. Turejee maneno ya Bwana Yesu.

Mathayo 12:34 “Enyi wazao wa nyoka, mwawezaje kunena mema, mkiwa wabaya? Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake.

35 Mtu mwema katika akiba njema hutoa mema; na mtu mbaya katika akiba mbaya hutoa mabaya”.

Tusome tena Mathayo 15:18-20…

Mathayo 15:18 “Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi.

19 kwa maana MOYONI hutoka MAWAZO MABAYA, UUAJI, UZINZI, UASHERATI; WIVI, USHUHUDA WA UONGO, NA MATUKANO

20 hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi…….”.

Umeona hapo?.. kumbe moyoni ndiko kunakotoka matukano, uzinzi, wizi, uongo n.k mambo ambayo ndiyo yanayomtia mtu unajisi, na bila shaka hayo ndiyo Maji machungu yatokayo moyoni kupita kinywani, ambayo hayafai kwa kustawisha chochote…

Wengi wamepoteza na kuharibu maisha yao kwasababu ya uzinzi, na wengine kwasababu ya wizi, na wengine kwasababu ya mauaji, wapo waliopoteza kibali kwa Mungu na kwa watu kwasababu ya wizi, au uzinzi, au mauaji..wapo walipoteza kazi zao za mikono na huduma zao zilizokuwa zenye utukufu kwasababu ya uzinzi, au wizi au matukano..

Wapo walioharibu ndoa zao zilizokuwa za heshima na mfano kwasababu ya uzinzi, uongo, na mauaji (utoaji mimba) Kwanini?.. kwasababu chemchemi zao zinatoa maji machungu yanayoua ndoa, kazi, huduma, kibali, heshima na nguvu.

Yakobo 3:8 “Bali ulimi hakuna awezaye kuufuga; ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti.

9 Kwa huo twamhimidi Mungu Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa Mungu.

10 Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo.

11 Je! Chemchemi katika jicho moja hutoa maji matamu na maji machungu?

12 Ndugu zangu, Je! Mtini waweza kuzaa zeituni, au mzabibu kuzaa tini? Kadhalika chemchemi haiwezi kutoa maji ya chumvi na maji matamu”.

Lakini kama moyoni kukutoka mambo masafi, ambayo ni upendo, ukweli, utu wema, uvumilivu (kwa ujumla utakatifu)… hakika hiyo ni chemchemi bora inayostawisha kila kitu, maji yake yatastawisha wokovu, kazi ya Mungu, kazi ya mikono, elimu, heshima, ndoa, nafasi na mambo mengine yote mazuri.

Je wewe chemchemi ya moyo wako inatoa maji ya aina gani?.. machungu au matamu?.. Kama inatoa machungu ipo dawa leo?.. dawa hiyo ni Roho Mtakatifu… Mwamini YESU leo kisha ukabatizwe na Roho Mtakatifu ataingia ndani yako na kukutakasa moyo wako Bureeeee kabisa!

Baada ya hapo ndoa  yako iliyokufa itafufua upya, huduma yako, kazi yako, elimu yako au kitu kingine cha thamani ulichopewa na Bwana, kitafufuka kwani tayari maji yatokayo ndani yako ni masafi..

Lakini labda tayari chemchemi yako ni safi, nayo inatoa maji masafi.. bado kuna jambo lingine la ziada la kufanya nalo ni KUILINDA chemchemi yako..

Mithali 4:23 “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako CHEMCHEMI ZA UZIMA”.

Utaulinda moyo wako kwa MAOMBI, kusoma NENO, kujihadhari na ulimwengu na kushiriki ibada pamoja na watu wenye imani moja na wewe kila mara.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu?

Fahamu Maana ya Mithali 15:24 Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu;

MOYO ULIOELEKEA KWA MUNGU.

JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.

JIHADHARI NA MANENO YASIYO NA  MAANA 

Print this post

kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi

SWALI: Nini maana ya Yeremia 31:30 “Bali kila mtu atakufa kwa sababu ya uovu wake mwenyewe; kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi”.


JIBU: Zamani za agano la kale katika taifa la Israeli, kulikuwa na usemi maarufu, unaosema “Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi”.

Kikawaida zabibu au matunda mengine yenye asidi nyingi mtu alapo , huwa meno yanatia  ganzi, lakini kamwe haiwezekani mtu mwingine akatiwa ganzi kwa ulaji wa mwingine.

Hapa Waisraeli wakiwa wanamaanisha kuwa adhabu za Mungu huwa zinatembea hata kwa kizazi cha watu,  Lakini Mungu kwa kinywa cha Yeremia anawasahihisha kuwa hilo si jambo lake..Anawaambia kila mtu ataadhibiwa sawasawa na uovu wake, wala watoto hawatauchukua uovu wa wazazi wao..Jambo ambalo alilirudia pia kwa kinywa cha Nabii Ezekieli (Ezekieli 18:20).

Lakini pia ukisoma muktadha wa vifungu hivyo, utaona anatoa unabii wa agano jipya ambalo atalifanya na watu wake kupitia Yesu Kristo, akimaanisha kuwa wokovu wake pia , utakuwa ni wa mtu binafsi, mmoja mmoja. Tusome habari yote tokea juu.

Yeremia 31: 27 Tazama, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapoipanda nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda, mbegu ya mwanadamu na mbegu ya mnyama.
28 Tena itakuwa, kwa kadiri nilivyowaangalia, ili kung’oa, na kubomoa, na kuangusha, na kuangamiza, na kutesa; kwa kadiri iyo hiyo nitawaangalia, ili kujenga, na kupanda, asema Bwana.
29 Siku zile, hawatasema tena, Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi.
30 Bali kila mtu atakufa kwa sababu ya uovu wake mwenyewe; kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi.
31 Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda.
32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana.
33 Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.

Hivyo vifungu hivi, vinatupa kutambua kuwa wajibu wa kulitunza  agano la Mungu ni la mtu binafsi, sawasawa na alivyokuja kulifunua katika agano jipya kupitia Yesu Kristo, kwamba ijapokuwa wokovu umeachiliwa kwa wote, lakini haupokelewi kijumuiya, kifamilia, au kikabila, bali kibinafsi.

Kila mtu atalibeba furushi lake mwenyewe. (Wagalatia 6:5)

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Tafsiri ya Yeremia 29:12 Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.

Yeremia alikuwa na umri gani alipoitwa?

Mti wa MLOZI alioonyeshwa nabii Yeremia 1:12 tafsiri yake ni nini?

 

 

 

Print this post

Je! Ni sahihi kwa mkristo kufundishwa na AI mfano wa Chatgpt, deepseek n.k.

SWALI: Je! Ni sahihi kwa mkristo kujifunza, au kufundishwa na AI (Artificial Inteligence), mfano wa Chatgpt, deepseek n.k.


JIBU: Ili kujibu swali hili ni vema, kutambua mashine hizi za akili bandia (AI), zinafanya kazi gani.

Kwa ufupi ni kuwa AI, inafanya kazi ya kuchakata taarifa nyingi, kutoka katika vyanzo vingi vilivyopo mitandaoni, mfano vitabu, makala, sauti, machapisho n.k, na hivyo inazichanganya taarifa hizo zote kwa kuangalia muktadha unaofanana na kuzifupisha, na kukujibu.

Hivyo kimsingi, ni chombo ambacho kinatoa msaada mkubwa katika ulimwengu wa sasa, na ndio ukweli usiopingika..Kwasababu kinarahisisha utafutaji wa taarifa. Lakini pamoja na hayo haimaanishi kuwa kinatoa kwa ufasaha wote.

Sasa tukija kwenye eneo la kiroho. Je ni vema mkristo kwenda kuuliza AI, au kuandaa maombi au masomo kupitia hiyo, n.k.

Ukweli ni kwamba Imani, sio taarifa, ni zaidi ya taarifa.. Hizi AI, zinatoa tu taarifa lakini hazitoi mafunuo. Hazina pumzi ya Roho Mtakatifu ndani yake.

Ikiwa unataka kuongeza maarifa kwa sehemu fulani zinaweza kukusaidia, lakini sio kukujenga nafsi, kwani inahitaji pumzi ya Mungu na miongozo ya Mungu wewe kujengwa nafsi, na sio taarifa.

Kwamfano ikiwa wewe ni mchungaji halafu, kila inapokaribia jumapili unachowaza ni kwenda chatgpt, kuiambia ikuandalie somo la kufundisha jumapili,  ndugu hapo hesabu kuwa umepotea kama sio kukengeuka… Tumia hiyo kwenye biashara zako, masomo yako,  projekti zao lakini sio kwenye mambo ya kiroho. Hilo liepuke kabisa.

Kufundisha Neno inahitaji ‘Neno’ mwenyewe (Yesu) akae ndani yako, kwasababu ni UHAI sio taarifa (Waebrania 4:12) ndio hapo itakupasa kupiga magoti kwanza uombe, kwa muda mrefu, utafakari moyoni mwako, ukae kwenye utulivu wa kutosha, ndipo Mungu alipande somo lake moyoni mwako. Ambalo yeye mwenyewe anajua litakuwenda kuwagusa vipi watu wake, wenye changamoto mbalimbali, kwamfano, pengine mtu mmoja alikuwa anakaribia kwenda kujinyonga kwasababu ya ugumu wa maisha na mateso fulani, na Mungu kamwona anataka amsaidie, kwa kuliweka somo linalohusiana na mapito ya Ayubu ili ainuliwe imani. Kinyume chake kwasababu ya uvivu wako wewe unakwenda kuiambia chatgpt (akili bandia), ikuandalie somo. Halafu jumapili utakwenda na taarifa zao sio mafunuo. Badala uokoe roho inayokwenda kujinyonga, unaiambia, “leo tunajifunza kanuni kumi za kudumisha ndoa na mahusiano kibiblia”. Hapo unafanya nini sasa?

Au Neno fulani Bwana anataka kukupa la wakati wako, sasa ikiwa unakimbilia AI ikusaidie, hutaki kuchukua muda wako binafsi kutafakari na kuomba ‘jiandae kukutana na ukame wa kiroho.

Visaidizi hivi, hatupaswi kuvifanya ndio sehemu ya imani yetu, kwamba kila kitu tutegemee kule, hivi ni tone dogo sana kati ya bahari kubwa. Roho Mtakatifu alishatuandalia njia zake, kuu za kujengwa na yeye.

Wekeza zaidi, kuomba msaada kwa wakufunzi wako, viongozi wako, ndugu zako katika Kristo, wekeza katika maombi, mifungo, tafakari, na kujisomea mwenyewe Neno.  kwa njia hizi hakika Bwana atasema nawe na kujengwa zaidi kuliko visaidizi. Lakini pia ikiwa pana umuhimu wa kujiongezea taarifa kwa vile unavyovijua, visaidizi hivi vitakufaa (Katika uangalizi maalumu), vinginevyo utajidumaza kiroho.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>  https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Karismatiki ni nini?

Uinjilisti kama agizo kuu la Bwana.

Vita vya kiroho, na mwamini Mpya.

Print this post

JIHADHARI NA MANENO YASIYO NA  MAANA

Mathayo 12:36 “Basi, nawaambia, KILA NENO LISILO MAANA, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu.

37 Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa”.

Mfano wa maneno yasiyo na maana ni maneno yote ya kukufuru, kulaani, kutukana, mizaha, mashindano, mazungumzo machafu, nyimbo za kidunia na mengine yanayofanana na hayo.

    1.  Mizaha

Unapotumia baadhi ya mistari ya kwenye Biblia au matukio kwaajili ya kufanya utani, au mzaha au vichekesho…maneno hayo utayatolea hesabu siku ile. Biblia sio kitabu cha comedy.

Zaburi 1:1 “Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha”.

    2.  Dhihaka.

Unapotoa dhihaka juu ya Neno la Mungu, au Watumishi wa Mungu ambao unajua kabisa ni wa kweli, siku ya mwisho utatoa hesabu..

    3. Mabishano na Mashindano.

Unapobishana na ukweli, kwasababu tu unataka uonekane unajua au unatafuta ushindi wa maneno.. basi fahamu kuwa siku ya mwisho utatoa hesabu ya maneno yako yote… Biblia inasema mashindano ya dini yote ni maneno yasiyo na maana..

1Timotheo 6:20 “Ee Timotheo, ilinde hiyo amana; ujiepushe na maneno yasiyo ya dini, yasiyo na maana, na mashindano ya elimu iitwayo elimu kwa uongo”

     4. Kufuru

Unapotoa kufuru na kashfa juu ya kazi ya Mungu, na moyoni unajua kabisa ni kazi kamili ya Mungu,  mbeleni kuna kutoa hesabu ya maneno yaliyotoka kinywani.

Mafarisayo walinena maneno ya kumkufuru Roho Mtakatifu katika kitabu hiko cha Mathayo 12, na ndio sababu ya Bwana YESU kusema maneno hayo kuwa “kila neno lisilo maana watu watatoa hesabu yake siku ya mwisho”.

     5. Nyimbo za kidunia.

Maneno yaliyopo kwenye nyimbo za kidunia hayana maana na yanamtukuza shetani, na hivyo hata maneno ya nyimbo hizo yatatolewa hesabu.

Amosi 6:5 “ninyi mnaoimba nyimbo za upuzi pamoja na sauti ya vinanda, na kujifanyizia vinanda vya namna nyingi, kama vile Daudi”.

      6. Mazungumzo machafu.

Mazungumzo machafu ni yale yote ya kijiweni au ya mtu na mtu, ambayo ni mazungumzo ya uasherati, ushabiki, uhuni, na mipango mibaya, matusi na mambo mengine yote mabaya.. yote hayo mtu atayatolea hesabu siku ya mwisho.

Sasa nini maana ya kutoa hesabu?

Kutoa hesabu maana yake ni kutoa “maana au tafsiri ya kina ya kile kilichotoka kinywani”.  Kwamfano kama mtu umemtukana mtu na kumwita yeye ni Mbwa, basi siku ile utaeleza sababu za kumwita vile, na kama kweli yeye ni mbwa kama ulivyosema… kwaufupi maneno ambayo sisi tuliyatamka kwa utani tu na ufupi, kule yatarefushwa na kuwa mada ndefu mno.

Hivyo hatuna budi kuwa makini na yanayotoka kinywani mwetu.. kwamaana yanarekodiwa yote, na pia ni vizuri kama tumekosea kwa vinywa vyetu kuwahi kurudi kutubu kwa tuliyemtolea maneno mabaya, au tuwahi kurudi kwa Mungu kutubu ili tusiangukie hukumu.

Hukumu inakuja, hukumu inakuja, tumwamini YESU na kutubu na tuyashike sana maungamo yetu.

Ubarikiwe.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KILA MTU ATATOA HABARI ZAKE MWENYEWE.

Je mtu anayeua anabeba dhambi zote za yule aliyemuua?

UTASIMAMA PEKE YAKO SIKU ILE.

USIGEUZE JIWE KUWA MKATE.

USI..USI..USI.

Print this post

Majini wanaotajwa kwenye Walawi 17:7 ni viumbe gani?

Jibu: Turejee kuanzia mstari wa 6..

Walawi 17:6 “Naye kuhani atainyunyiza damu yake juu ya madhabahu ya Bwana, mlangoni pa hema ya kukutania, na kuyateketeza mafuta yake, yawe harufu njema mbele za Bwana.

7 WALA HAWATATOA TENA SADAKA ZAO KWA WALE MAJINI, ambao huwafuata ili wafanye uasherati nao. Sheria hii itakuwa sheria ya milele kwao, kizazi baada ya kizazi”.

“Majini” wanaotajwa hapo ni “mashetani”..

Katika agano la kale sadaka yoyote iliyotolewa nje ya hema  ya Mungu (maana yake katika madhabahu nyingine), sadaka hiyo ilihesabika kuwa imetolewa kwa majini/mashetani, na yeyote aliyetoa sadaka yake huko, akabainika sheria ilikuwa ni kutengwa na watu wake.

Walawi 17:8 “Nawe utawaambia, Mtu awaye yote katika nyumba ya Israeli, au miongoni mwa wageni, wanaokaa nao, atoaye sadaka ya kuteketezwa au dhabihu,

9 wala haileti mlangoni pa hema ya kukutania, ili aisongeze kwa Bwana BASI MTU HUYO ATATENGWA NA WATU WAKE”.

Mahali pekee Bwana Mungu alipopachagua pa kutolea sadaka ni katika “HEMA YA MUNGU”, katika kipindi cha Waamuzi na katika “NYUMBA YA MUNGU” aliyoitengeneza Sulemani katika kipindi cha Wafalme na kuendelea.

Kwahiyo sadaka yoyote inayopelekwa mahali panapoabudiwa ibilisi, basi sadaka hiyo ni imetolewa kwa majini/mashetani..na sadaka inayotolewa kwa mashetani basi mtu huyo au watu hao wanakuwa na ushirika na mashetani, ndivyo Neno la Mungu linavyosema..

1Wakorintho 10:20 “Sivyo, LAKINI VITU VILE WAVITOAVYO SADAKA WAVITOA KWA MASHETANI, wala si kwa Mungu; nami sipendi ninyi KUSHIRIKIANA NA MASHETANI. Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana na kikombe cha mashetani”.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba “majini” wanaotajwa katika Walawi 17:7 ni mashetani/mapepo ambao pia wanatajwa katika Isaya 13:21 na 2Nyakati 11:15 wakati wa mfalme Yeroboamu.

2Nyakati 11:15 “naye akajiwekea makuhani wa mahali pa juu, na wa WALE MAJINI, na wa zile ndama alizozifanya.”

Na pia zipo sadaka zitolewazo kwa Mungu na pia zitolewazo kwa mashetani, Mtu anayeenda kwa waganga wa kienyeji sadaka yake anaitoa kwa mashetani, na kafara yoyote iwe ya mnyama au kiumbe chochote inayofanyika katika agano jipya ni sadaka kwa mashetani na si kwa Mungu, kwani hatuna tena kafara za wanyama katika agano jipya, wala hakuna kafara za watu kwa Mungu na hazijawahi kuwepo huko kabla, kafara zote za namna hiyo ni za mashetani.

Zaburi 106:37 “Naam, walitoa wana wao na binti zao Kuwa dhabihu kwa mashetani.

38 Wakamwaga damu isiyo na hatia, Damu ya wana wao na binti zao, Waliowatoa dhabihu kwa sanamu”

Je umempokea YESU?.. fahamu kuwa hakuna wokovu kwa mwingine yoyote isipokuwa kwake!, na tunaishi majira ya kurudi kwa YESU, huu si wakati wa kucheza na dunia, bali kujitoa kwa MUNGU.

1Petro 4:2 “Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika MAPENZI YA MUNGU, WAKATI WENU ULIOBAKI WA KUKAA HAPA DUNIANI.

3 Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

MAJINI WAZURI WAPO?

Tunathibitisha vipi kuwa Yule Malaika wa (Yohana 5:4) ni wa MUNGU?

AINA ZA MAJINI, MAJINA YAO, KAZI ZAO, NA TIBA ZAKE.

Ipi tofauti kati ya Uhai na Uzima kibiblia?

Print this post

Uinjilisti kama agizo kuu la Bwana.

Kila mwamini ameitwa kuieneza injili ya Yesu Kristo. Ambayo huitwa habari njema.

Mathayo 28:19-20

[19]Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;

[20]na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.

Habari njema ni nini? Ni habari za wokovu kwa mwanadamu, ulioletwa na  kupitia mtu mmoja Yesu Kristo kwa tendo la kufa na kufufuka kwake kaburini.

Kwanini tunapaswa tuwashuhudie wengine habari njema?

1) Ni agizo la Bwana (Mathayo 28:19)

Kama tulivyotangulia kuona hapo juu, kuwa siku Yesu alipoondoka hakutuacha bila wajibu, bali kila mmoja wetu alipewa sehemu ya huduma katika shamba lake. Ya kuenenda ulimwenguni kote kuwafanya watu kuwa wanafunzi wake.

Kazi hii sehemu nyingine anaifananisha na talanta, ambayo amempa kila mwamini na anataka kila mmoja aizalishe (Mathayo 25:14-30), sehemu nyingine anaifananisha na matunda, anasema sisi ni matawi na yeye ni mzabibu  kwamba tumzalie matunda, (Yohana 15:1-7),sehemu nyingine nyingine anaiita posho, huku yeye  akijiita bwana, na sisi mawakili wake, akitutaka tutoe posho kwa wakati kwa watu wake, (Luka 12:42-48)

Sasa ukiangalia utaona sehemu zote hizo tunazofananishwa nazo, kama mtu hajafanya chochote au hajazalisha chochote, haachwi hivi hivi, bali kuna aidha kuondolewa sehemu ya thawabu yake, au kukataliwa kabisa.

Ndio maana ni lazima tujue mwamini yoyote yule, ni lazima aishi maisha ya kuwashuhudia wengine injili.

2) Watu wanapotea bila Kristo.

Warumi 10:14 Basi wamwiteje yeye wasiyemwamini? Tena wamwaminije yeye wasiyemsikia? Tena wamsikieje pasipo mhubiri?

Ni lazima ujue kuwa hukumu ipo na kuzimu pia ipo, na inawameza wengi, Na watu hawawezi kuokoka tu wenyewe hivi hivi bila kusikia injili kama wewe ulivyosikia.  Tengeneza picha unamwona baba yako, au mama yako kwenye ziwa la moto, halafu anakuambia laiti ningelijua ukweli nisingekuwa huku, utajisikiaje? Ukilijua hili basi huruma ya ki-Mungu itakujaa tu ndani yako, na utasukumwa kujitoa kuwaendea wenye dhambi, kama Kristo alivyotujia sisi, kutoka mbinguni, na kama mitume walivyowaendea watu, ili kuhakikisha wanaokoka.

3) Mbingu zinafurahi.

Luka 15:7 Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu

Mungu hufurahi malaika pia hufurahi, wanapoona roho za watu zinaokoka,duniani, Hivyo sisi kama wana wa Mungu ni wajibu wetu kuyatenda yale tu ambayo yanamfanya Baba yetu afurahi, na hilo si lingine zaidi ya kutoka na kwenda kuwashuhudia watu injili.Hapo tunaufanya moyo wa Mungu hufurahi sana.

4) Ushuhuda wa maisha yetu.

Ni ukweli usiopingika kuwa kila mmoja wetu kuna mahali Mungu amemtoa mpaka hapo alipomfikisha, anayo mengi ya kushuhudia kuhusu uzuri wa Kristo.

Wazia yule kichaa ambaye alikuwa katika hali mbaya kule makaburini, uchi, usiku na mchana, ameshindikana kwa vifungo vyote. Lakini Yesu alipokutana naye saa ile ile alipona, akataka kuambatana na Yesu, lakini Yesu akamwambia nenda nyumbani kwa watu wako uwasimulie matendo makuu ambayo Mungu amekutendea, Na tunaona alikwenda kusimulia yote mji ule, na watu wengi wakamwamini Kristo, kwa ushuhuda wake tu.

Marko 5:20 Akaenda zake, akaanza kuhubiri katika Dekapoli, ni mambo gani makuu Yesu aliyomtendea; watu wote wakastaajabu

Hata wewe, wazia uzuri ulioupata pindi ulipompokea Kristo, utamani pia mwingine aupate, na huo ndio upendo, umeonja uzuri wa Kristo unakwenda kuwaambia na wengine mfano tu wa yule mwanamke pale kisimani.

NI Njia zipi za kuhubiri?

i) Kwa kusimulia ushuhuda wa maisha yako, jinsi Yesu alivyokuokoa.

Sawasawa na agizo ambalo Yesu alimwagiza yule mtu ambaye aliteswa Na mapepo akamfungua. (Marko 5:19-20)

ii) Kwa kumkaribisha Kanisani.

Hii ni njia bora, ambayo utapata nguvu ya kikanisa, kwasababu mule akutanapo na vipawa mbalimbali vya Mungu, hurahisisha zaidi moyo wake, kuamini ujumbe uliompelekea.

iii) Kwa Mwenendo mwema wa  rohoni.

Ishi maisha yanayomuhakisi Kristo. Kwasababu matendo yako ni injili kuwa wengine kumgeukia Kristo. (1Petro 3: 1-2)

iv) Kwa kutumia Visaidizi

Hivi Ni kama vitabu, kanda, luninga, na kwa dunia ya sasa, Vitu kama whatsapp, websites,  panaweza pakawa mahali Ambapo injili yetu kupaa sana na kuwavuta wengi ndani ya ufalme. Ulimwengu wa sasa, upo mtandaoni, hivyo tumia fursa hiyo, kushea mafundisho, mahubiri sahihi ya Neno la Mungu kwa marafiki zako, familia, ndugu, majirani, huko huko Mungu ataanza kazi ya wokovu ndani yao.

Namna ya kushinda hofu.

Haya ni mambo ya kukumbuka kila uendapo kushuhudia, ili usishindwe na hofu.

1) Kile uendapo kushuhudia ukumbuke kuwa Roho Mtakatifu ndiye anayetupa nguvu na si kwa uweza wetu tu wenyewe. (Matendo 1:8)

2) Omba kabla ya kwenda kuwashuhudia watu.

3) Anza katika udogo, shuhudia mtu mmoja mmoja, kabla ya kufikia umati wa watu wengi.

4) Pia ukumbuke  jambo la kushawishi ni la Roho Mtakatifu, sisi ni kushuhudia.

Usiwe na hofu ikiwa huoni mwitikio wowote, kwa yule unayemweleza habari ya wokovu, fahamu kuwa ipo mbegu imemwingia ambaye itakuja kumea tu kwa wakati wake.

5)Ongozana na mtendakazi wenzako, au kiongozi wako. 

Uinjilisti wa wawili huwa mrahisi zaidi ya ule wa mmoja (isipokuwa unao uzoefu). Yesu aliwatuma wanafunzi wake wawili wawili, alijua ujasiri utaongezeka lakini wangeweza kufanya zaidi, pale mmoja anapochoka anamtia nguvu mwenzake. Vivyo hivyo na wewe katika hatua za awali ongozana na kiongozi wako, au mshirika mwenza katika kazi ya injili.

Vifungu vya kukariri, ambavyo unapaswa uwe navyo kichwani, katika hatua za kuwashuhudia watu.

Yohana 3:16

Warumi 3:23

Warumi 6:23

Warumi 10:9–10

2 Wakorintho 5:17

Kwa mwongozo wa namna ya kutembea katika baadhi ya vifungu hivyo, pitia hili fundisho >>> NJIA/BARABARA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.

Mafundisho ya ziada

KWANINI TUNAPASWA KWENDA KUIHUBIRI INJILI KWA UJASIRI WOTE?

IHUBIRI INJILI, KILA MAHALI KWASABABU AKUZAYE NI MUNGU.

HEKIMA NANE(8) ZA KIUINJILISTI, KATIKA KUWAVUA WATU KWA KRISTO.

JE UDHAIFU WANGU UNAWEZA KUZUIA INJILI?

KUTOKUIHUBIRI INJILI,KUNA MADHARA GANI?

KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Akaabudu akiegemea kichwa cha fimbo yake

Akaabudu akiegemea kichwa cha fimbo yake.

Waebrania 11:21

[21]Kwa imani Yakobo, alipokuwa katika kufa, akambariki kila mmoja wa wana wa Yusufu, akaabudu akiegemea kichwa cha fimbo yake.

Ulishawahi kujiuliza ni kitu gani Yakobo alikuwa anawaonyesha wana wake siku ile alipokuwa anakaribia kufa.. kitendo cha yeye kusujudu kwa kuegemea kichwa cha fimbo?

Kwanini biblia iseme akaegemea fimbo na sio ukuta, au kitanda au au kiti au isikae tu kimya, bila kueleza chochote?

Yakobo alikuwa na maana kubwa kufanya vile, kwasababu hata alipokuwa akiwabariki watoto wa Yusufu (Efraimu na Manase) alipishanisha mikono..wakidhani kuwa amekosea, akawaambia sijakosea naelewa ninachokifanya, leo ndio tunajua kumbe alikuwa anaunda msalaba, ambao kwa kupitia huo neema inawafikia mataifa kwanza.

Vivyo hivyo na alipokuwa anakufa alisujudu kwa kuegemea kichwa cha fimbo, na huwenda watoto wake walistaajabishwa na kusujudu kule, pengine walijaribu kumwondoa pale ili asujudu vema, lakini akawaambia niacheni naelewa…

Fimbo kibiblia inafunua mamlaka ya mfalme, mchungaji na safari.

Yakobo hakuishi bila tegemeo la mchungaji…udhihirisho Ulikuwa ndio ile fimbo..kwasababu sikuzote alijiona kama kondoo wa Mungu, hakutaka kuiacha fimbo ya mchungaji wake, popote alipokuwepo kwasababu ndio faraja yake.

Daudi alisema…Bwana ndiye mchungaji wangu…gongo lake, na fimbo yake vyanifariji..

Zaburi 23:1-4

[1]BWANA ndiye mchungaji wangu,  Sitapungukiwa na kitu.

[2]Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,  Kando ya maji ya utulivu huniongoza.

[3]Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza  Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

[4]Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya;  Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. 

Kwa ufupi ni kuwa palipo na fimbo ya mchungaji hapo hapo utaona Na kondoo wamejilaza. Yakobo alitembea na Kristo, Mpaka dakika ya mwisho wa maisha yake.

Lakini pia Fimbo inamfunua msafiri…zamani wasafiri walikuwa wanasafiri na fimbo kuwasaidia kutembea..

Wana wa Israeli walipokuwa wanajiandaa na safari ya kutoka Misri, utakumbuka usiku ule walipewa maagizo kila mmoja kushika fimbo yake.

Kutoka 12:11

[11]Tena mtamla hivi; mtakuwa mmefungwa viuno vyenu, mmevaa viatu vyenu miguuni, na fimbo zenu mikononi mwenu; nanyi mtamla kwa haraka; ni pasaka ya BWANA.

Kristo pia alipokuwa anawatuma wanafunzi wake katika ziara za injili aliwaagiza Kubeba fimbo zao..

Marko 6:8

[8]akawakataza wasichukue kitu cha njiani isipokuwa fimbo tu; wala mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni;

Hii ni kutufunulia kuwa Yakobo alikataa kuishi kama mwenyeji duniani.. bali msafiri..

Hivyo alitamani urithi wake ujue jumla ya mwenendo wa maisha yake hapa duniani ulikuwaje..

Hiyo ndio sababu kwanini historia za maisha ya watu kama hawa Mungu kazihifadhi tuzisome hadi leo.

Hata sasa, ujiulize je na Mimi je! fimbo ya mchungaji wangu(YESU KRISTO), ipo pamoja nami? ujiulize je mimi ni msafiri hapa duniani?

Fahamu tu Wazao wote wa Mungu huwakosi na fimbo ya Mungu, hiyo ndio alama yetu.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Yakobo alimaanisha nini kusema ‘ndipo BWANA atakuwa Mungu wangu’ Mwanzo 28:21

Kwanini Yakobo alimshinda Mungu, Je! Mungu huwa anashindwa na wanadamu?

Ni kwanini mifugo ya Yakobo iliongezeka kwa wingi kiasi kile?

Print this post