Category Archive Maana ya maneno

Nini maana ya Selahamalekothi?

Ilikuwa ni desturi ya wayahudi kuyapa majina, maeneo yote ambayo walikutana na Mungu kipekee.

Kwamfano Yakobo alipokutana na Mungu mahali fulani palipoitwa Luzu, kwa kuona maono yale ya ngazi kushuka kutoka mbinguni, na malaika wanashuka na kukwea, hakuondoka hivi hivi bali alipaita mahali pale Betheli yaani ‘ nyumba ya Mungu’ (Mwanzo 28:10-22).

Sehemu nyingine Mungu alipowasaidia Israeli kuwapiga wafilisti kwa kishindo kikubwa, Samweli alilisimamisha jiwe na kuliita Eneb-ezeri akimaanisha ‘hata sasa Bwana ametusaidia’ na 1Samweli 7:12.

Hivyo pia tukisoma kisa cha Mfalme Sauli na Daudi, tunaona mara nyingi Daudi alipowindwa ili auawe alifanikiwa kumtoroka Sauli, lakini upo wakati ambao alihusuriwa pande zote, Daudi akawa hana namna isipokuwa kungojea tu kuuliwa palepale pangoni, sasa wakati ambapo Sauli amemkaribia sana Daudi. Taarifa za ghafla zilimfikia na kuambiwa kwamba wafilisti wamevamia Israeli, hivyo ikambidi aache kumfuatilia Daudi arudi Israeli kupambana na adui zake.

Sasa tendo hilo la wokovu halikumwacha Daudi awe vilevile kinyume chake, alipaita mahali pale Selahamalekothi

1 Samweli 23:26-28

[26]Sauli akaenda upande huu wa mlima, na Daudi na watu wake wakaenda upande huu wa mlima; naye Daudi akafanya haraka sana kwenda zake kwa hofu ya Sauli; kwa sababu Sauli na watu wake wakamzunguka Daudi na watu wake ili kuwakamata.

[27]Lakini akaja mjumbe kwa Sauli, kusema, Njoo upesi, kwa kuwa Wafilisti wameishambulia nchi.

[28]Basi Sauli akarudi kutoka kumwinda Daudi, akaenda kinyume cha Wafilisti; kwa hiyo wakapaita mahali pale, Selahamalekothi.

Selahamalekothi ni neno la kiebrania lenye maana ya MWAMBA WA KUTOROKEA.

Daudi na watu wake walipaita mahali pale hivyo kufuatana ba jinsi Mungu alivyowaepusha na mkono wa Sauli, kwa njia isiyodhaniwa/ kutegemewa hata kidogo.

Ni kwanini wayaite majina maeneo hayo?

Ni Ili kuendelea kukumbuka matendo makuu Mungu aliyowatendea wasizisahau wafidhili zake kabisa.

Je na sisi ni alama gani tunaacha mahali ambapo tunamwona Mungu ametutendea makuu. PENDA kuandika shuhuda zako, ili wakati ujao zikusaidie kukumbuka fadhili za Mungu umshukuru.

Kikawaida Mungu huwa anatufanyia maajabu mengi Sana kila siku, lakini tunakuwa wepesi kuyasahu, ni vema tujifunze kwa namna yoyote kutunza kumbukumbu, hata kama si kwa kuandika lakini kwa njia zozote zile, mfano wa mababa zetu hawa.

Mungu akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Pango la Makpela ni lipi, je lina umuhimu wowote kwetu?

HII NDIO TABIA YA WATU WA KEILA, USIIGE

SIKU YA HOFU YANGU NITAKUTUMAINI WEWE.

Print this post

Theofania ni nini?

Theofania ni neno la kiyunani lenye muunganiko wa maneno ya mawili “theos (Mungu)” na “faino (kuonekana)”. Hivyo ukiunganisha linazalika neno “kuonekana kwa Mungu”

Theofania sio kuonekana kwa Mungu katika ule utimilifu wake wote, hapana, kwasababu maandiko yanasema hakuna mtu awezayo kumwona Mungu akaishi (Kutoka 33:20). Hivyo Theofania ni njia mbadala (isiyo ya moja kwa moja) ambayo Mungu  aliitumia kujitokeza na kuongea na watu, kuthibitisha agano lake, au kuwapa maagizo.

Mfano wa njia hizo,

> Ni kijiti cha moto, alichotumia kuzungumza na Musa kule jangwani. (Kutoka 3)

> Mtu Yule aliyeshindana na Yakobo mweleka (Mwanzo 32:24-30)

> Melkizedeki (Mwanzo 14: 18-20)

> Yule mtu wanne aliyewatokea Shedraka, Meshaki na Abednego ndani ya moto (Danieli 3)

> Nguzo ya moto na wingu jangwani (Kutoka 13:21-22)

> Mungu kumtokea Samweli  (1Samweli 3:10)

> Maono ya Ezekieli (Ezekieli 1)

Je! theofania ipo hadi sasa?

Yesu Kristo alipozaliwa katika mwili, sio tena theofania, Bali ni utimilifu wote wa Mungu katika mwili.

Wakolosai 2:9 Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili.

Hapo mwanzo watu hawakumwona Mungu katika utimilifu huo, kwasababu kama wangemwona Mungu wangekufa kwasababu ya dhambi. Lakini Kristo alipokuja kuondoa dhambi kwa damu yake, wanadamu wote tunamwona Mungu katika utilimilifu wote, kwa Roho Mtakatifu aliyemweka ndani yetu.

Tunakikaribia kiti cha rehema, na neema kwa ujasiri bila kufa kama kule mwanzo, kwasababu damu ya Yesu inanguvu ya kuzificha dhambi zetu zote. Ukimwona Kristo(moyoni) umemwona Mungu (Yohana 14:6-11)

Ndio maana ni kwanini leo hii mtu huwezi kumfikia Mungu bila Yesu Kristo.

Okoka leo upokee neema hii, ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya toba. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Theolojia ni nini?. Na je ni sahihi kuisoma?

Mwanazuoni ni mtu gani kibiblia?

NINI TUNAJIFUNZA KWA THEOFILO MTUKUFU?

Print this post

Wanethini ni watu gani kwenye biblia?

Wanethini ni kundi la watu ambao walitumika katika hekalu, ambao sio asili ya wayahudi. Wanatajwa sana kwenye kitabu cha Nehemia na Ezra. Maana ya neno ‘Nethini’  kwa kiyahudi linamaanisha “waliotolewa”. Wakimaanisha watu waliotelewa kuwasaidia walawi katika shughuli za hekaluni.

Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyowataja;

Ezra 8:20 na katika Wanethini, ambao Daudi, na wakuu, walikuwa wamewaweka kwa ajili ya utumishi wa Walawi, Wanethini mia mbili na ishirini; wote wametajwa kwa majina yao.

Nehemia 7:73 Hivyo makuhani, na Walawi, na mabawabu, na waimbaji, na baadhi ya watu, na Wanethini, na Israeli wote, wakakaa mijini mwao. Hata ulipowadia mwezi wa saba, wana wa Israeli walikuwa wakikaa katika miji yao.

Soma pia, (Ezra  2:43, 2:58, 7:24)

Asili yao:

Biblia haituonyeshi moja kwa moja asili yao ni wapi, lakini wanazuoni wengi huamini walitokea katika chimbuko la wale wagibeoni waliowadanganya Israeli wakati ule mpaka wakafanya nao maagano, Ambao Yoshua aliwapa kazi ya kupasua kuni, na kuteka maji.

Yoshua 9:27 Siku iyo hiyo Yoshua akawafanya kuwa ni wenye kupasua kuni, na wenye kuteka maji, kwa ajili ya mkutano, na kwa ajili ya madhabahu ya Bwana, hata siku hii ya leo, katika mahali hapo atakapopachagua

Mbali na hawa wagibeoni wengine wanaweza wakawa ni wageni au mateka., ambao baadaye wakaja kuwekwa kwenye utumishi wa hekaluni.

Kazi yao:

Wanethini hawakufanya kazi zozote za kikuhani, ikumbukwe kuwa ilikuwa ni kosa, mtu ambaye sio myahudi tena wa kabila la Lawi kufanya shughuli zozote za kihekalu, Hawa walikuwa wanafanya kazi za usaidizi ule wa nje, kama vile kutweka maji, kukusanya kuni, usafi, na kazi nyingine zilizohitaji msaada wa pembeni.,Ili kuwaruhusu walawi wasilemewe  wajikite zaidi katika kazi za hekaluni.

Maandiko yanaonyesha walikuwa na makao yao maalumu palipoitwa Ofeli kule Yerusalemu karibu na hekalu (Nehemia 3:26)

Hata Baadaya ya uhamisho wa Babeli, tunaona mabaki yaliyorudi Israeli kufanya shughuli za kihekalu, hawa wanethini pia walirejea

Kwa ufupi wanethini walikuwa ni la watu (wasio-wayahudi) waliowekwa kwa ajili ya kusaidia shughuli za hekaluni.

Kwanini Bwana aruhusu jambo hili?

Licha ya kwamba Mungu ameliita kanisa lake na amelitenga, limtumikie lenyewe katika shughuli zote za kimadhabahu. Lakini Bado Bwana anaweza kunyanyua watu wengine nje ya kanisa, kusaidia kanisa kusonga mbele. Mfano wa hawa ni Yule akida wa kirumi ambaye alilipenda taifa la Israeli na  kulijengea sinagogi (Luka 7:1-5). Hakuwa myahudi lakini aliwasaidia wayahudi.

Hata sasa wanethini wapo wengi, hawapaswi kuzuiliwa, endapo wanasaidia kanisa au kazi ya Mungu, kwasababu ni Bwana ndiye aliyewavuta.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Nini maana ya neno kumwamba (Zaburi 78:19)

Zaburi 78:18-19

[18]Wakamjaribu Mungu mioyoni mwao Kwa kutaka chakula kwa tamaa zao. [19]Naam, walimwamba Mungu, wakasema, Je! Mungu aweza kuandika meza jangwani? 

Kumwamba kama ilivyotumika hapo ni “kuzungumza kinyume”

Hivyo hapo anaposema 

“Naam, walimwamba Mungu, wakasema, Je! Mungu aweza kuandika meza jangwani?”

Ni sawa na kusema..

Naam, walizungumza kinyume na Mungu, wakisema Je! Mungu aweza kuandika meza jangwani?

Wana wa Israeli kule jangwani, vinywa vyao havikuwa vya shukrani au vya kuomba, bali vivywa vya kumjaribu Mungu na manung’uniko, ijapokuwa walijua uweza wake wote, lakini walijifanya kama Mungu wao hawezi kuwaokoa, wakawa wanauliza maswali yaliyoonekana magumu, kumbe nafsini mwao wanajua yote yanawezekana, wanafanya tu makusudi ili waone Yehova atafanya nini. Na ndio sababu iliyomfanya Mungu asipendezwe nao.

Na sisi pia tusiwe watu wa kumwamba Mungu, kwa kusema maneno ya kutoamini.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

Kama Musa aliandika vitabu vya torati, Je! kifo chake alikiandikaje mule?

BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.

Biblia inamaana gani kusema “vipo sita, naam saba”?

Rudi Nyumbani

Print this post

msalaba ni nini.

Msalaba ni kipande cha mti, kilichochongwa kwa kupishanishwa na kingine kwa juu. chenye lengo la kumuulia mwanadamu kwa kifo cha mateso.

Tofauti na sasa, ambapo adhabu nyingi za kifo kwa mataifa mbalimbali huwa ni kunyongwa, au kupigwa risasi, au kuwekwa kwenye kiti cha umeme, n.k.. Lakini katika falme za zamani watu waovu kupita kiasi, kwamfano wauaji, au wenye makosa ya uhaini, adhabu yao, ilikuwa ni kutundikwa au kugongelewa pale msalabani mpaka ufe. Ni mateso ambayo utataabika hapo kwa saa nyingi sana kabla ya kufa, hata siku mbili.

Hivyo kwa lugha rahisi tunaweza kusema msalaba ni chombo cha kuulia mtu.

Kwetu sisi tuliomwamini Kristo. Msalaba ni ishara kuu ya ukombozi tulioupata kwa kifo cha mwokozi wetu. Kufahamu kwa undani ni kwanini fungua link hizi; usome..

AMELAANIWA AANGIKWAYE MSALABANI.

Nini maana ya sulubu/ sulubisha?

nini maana ya kujikana nafsi na kujitwika msalaba?

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> 

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.


Mafundisho mengine:

Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?

Je! msalaba kaburini una umuhimu wowote?

Print this post

Simo ni mtu gani? (Ayubu 17:6).

Swali: Simo ni nini, au ni nani kama tunavyosoma katika Ayubu 17:6.

Jibu: Tusome mistari hiyo mpaka ule wa saba (7).

Ayubu 17:6 “Amenifanya niwe simo kwa watu; Nimekuwa mwenye kuchukiwa kwa wazi. 

7 Jicho langu nalo limekuwa giza kwa sababu ya majonzi, Na via vyangu vyote vimekuwa kama kivuli”

Neno hili “Simo” linasomeka tena katika Ayubu 30:9.

Ayubu 30:9 “Na sasa mimi nimekuwa wimbo wao, Naam, nimekuwa simo kwao

10 Wao hunichukia, na kujitenga nami, Hawaachi kunitemea mate usoni”.

Na maana ya neno hilo (simo) ni “MTU ANAYEDHARAULIKA”

Wakati Ayubu mtumishi wa MUNGU anapitia yale majaribu ya kufiwa na wanawe na kupoteza mali zake zote, na zaidi ya yote kupitia matatizo ya kiafya, ile fahari yake yote iliisha na kusababisha watu wengi kumdharau ikiwemo mke wake, mpaka hatimaye naye kuliona hilo na kusema hayo maneno.

Lakini pamoja na kuwa SIMO mbele ya watu, kwa MUNGU alikuwa LULU kubwa sana, kwani majaribu yale hayakuwa kwasababu ya yeye kumwacha MUNGU bali ni kwasababu ya yeye kumkaribia Mungu zaidi, na wakati ulipofika alipata mara mbili, ya alivyovipoteza na miaka mingi zaidi ya kuishi (Ayubu 42:12-16).

Na sisi tunajifunza mambo hayo hayo, kuwa tujaribiwapo kwaajili ya haki tuna heri…

Lakini tupitiapo majaribu mfano wa yale ya Ayubu tukiwa katika dhambi, tunapaswa tujifikiri mara mbili, kwani huenda ni mapigo na laana kutoka kwa Mungu ili tutubu na si kwa lengo la kuzijaribu imani zetu kama Ayubu.

Ndivyo Neno linavyoma katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati 28.

Kumbukumbu la Torati 28:15-16,37-39 “Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya BWANA, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata. 

16 Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani. 

37 Nawe utakuwa ushangao, na mithali, na dharau, kati ya mataifa yote huko atakakokuongoza BWANA. 

38 Mbegu nyingi utazichukua nje shambani, lakini utavuna haba, kwa kuwa nzige watazila. 

39 Utapanda mizabibu na kuitengeza, wala hutakunywa katika divai yake, wala kuichuma kwani italiwa na mabuu”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI KWA NAMNA GANI TUTASHINDA MAJARIBU?

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

Kwanini Mungu alimkataa Sauli? (1Samweli 15:23)

MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO

Rudi Nyumbani

Print this post

Neno Siuze linamaanisha nini kwenye biblia?

Siuze ni ‘Sembuse’, kwa uandishi mwingine.

Kwamfano mtu anaposema kauli hii

 “Kama Bwana Yesu alikuwa mwombaji siuze mimi, kuzidi hapo?


.Ni sawa tu  na kusema “Kama Bwana Yesu alikuwa mwombaji sembuse mimi, kuzidi hapo?

Maana ya Neno hilo ni. “Si zaidi

‘Kama Bwana alikuwa mwombaji si zaidi mimi kuzidi hapo’.

Vifuatavyo ni baadhi ya vifungu ambavyo utalisoma neno hili kwenye biblia;

 

2 Mambo ya Nyakati 6:18

[18]Lakini Mungu je! Yamkini atakaa na watu duniani? Tazama, mbingu na mbingu za mbingu za mbingu hazikutoshi; siuze nyumba hii niliyoijenga! 

 

2 Wakorintho 3:9

[9]Kwa maana ikiwa huduma ya adhabu ina utukufu, siuze huduma ya haki ina utukufu unaozidi. 

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Neno vuruvuru linamaanisha nini katika biblia?

Nini maana ya mbingu na nchi zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe? (Mathayo 24:35).

Kuna Mbingu ngapi?

Rudi Nyumbani

Print this post

Ukaufu ni nini? (Kumbukumbu 28:22).

Swali: Ukaufu ni nini na Koga ni nini kama tunavyosoma katika Kumbukumbu 28:22?


Jibu: Turejee.

Kumbukumbu 28:22 “Bwana atakupiga kwa kifua kikuu, na kwa homa, na kwa kuwashwa, na kwa hari ya moto, na kwa upanga, na kwa UKAUFU, na kwa KOGA; navyo vitakufukuza hata uangamie”

“Ukaufu” ni ugonjwa wa mazao unaotokana na utandu (fangasi), tazama picha juu. Ugonjwa huu unaposhambulia zao la nafaka basi linapata mabaka mabaka na kisha kunyauka na mwishowe kutozalisha chochote.

Sasa hapo Bwana alikuwa anasema na watu wake  Israeli (ambao ni sisi pia) kwamba tutakapomwacha Bwana na kufuata miungu mingine na kuiabudu basi tutakuwa tumefungua milango ya laana juu ya maisha yetu,  kwani tutapigwa kwa magonjwa ya mwilini lakini pia mazao ya mashamba yetu yatapiwa kwa magonjwa.. na pia tutapigwa kwa misiba na majanga ya nchi.

Mfano wa magonjwa ya mwilini ni hayo yaliyotajwa hapo (Kifua kikuu, homa na kuwashwa).. na mfano wa magonjwa yatakayoshambulia mimea yetu hata tusipate chakula ni hayo yaliyotajwa hapo (Koga na UKAUFU),

Koga ni utandu mweupe unaoshambulia mimea ambao nao pia ukikamata zao la chakula, basi zao lile linadhoofika na hatimaye kufa. (Tazama picha chini).

koga ni nini

Lakini pia mfano wa majanga nchi yatakayotupata ikiwa tutamwacha Bwana ni hayo yaliyotajwa hapo juu (hari ya moto na upanga)..Hari ya moto inayozungumziwa hapo ni vipindi vya ukame na jua kali na upanga unaozungumziwa hapo ni vita (au umwagaji damu).

Na sio kwa mambo hayo tu, bali pia kwa mambo mengine mengi yaliyotajwa hapo katika Kumbukumbu 28 na yasiyotajwa… yote yatatupata ikiwa tutamwacha BWANA MUNGU WETU, na kujitumainisha katika mambo mabaya…

Kumbukumbu 28:58 “Kama hutaki kutunza kufanya maneno yote ya torati hii yaliyoandikwa katika kitabu hiki, upate kulicha jina hili la fahari na utisho, Bwana, MUNGU WAKO;

59 ndipo atakapofanya Bwana mapigo yako yawe ya ajabu, na mapigo ya uzao wako, mapigo makubwa kwa kweli, ya kudumu sana, na magonjwa mazito ya kudumu sana.

60 Naye atakurejezea maradhi yote ya Misri juu yako uliyokuwa ukiyaogopa, nayo yataambatana nawe.

61 Tena kila ugonjwa, na kila pigo yasiyoandikwa katika kitabu cha torati hii, atakutia nayo Bwana juu yako, hata utakapokwisha kuangamizwa”.

Lakini kinyume chake, ikiwa tutamtii Bwana MUNGU WETU, na kwenda katika njia zake, basi tutafanikiwa sana kufungua milango ya Baraka nyingi, wala hatutapatwa na hayo yote (Saswasawa na Kumbukumbu 28:1-14)

Bwana atusaidie na kutuneemesha.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAGONJWA YAKUPATAYO MARA KWA MARA.

Kwanini kuwe na kitabu Cha kumbukumbu la Torati na kwanini kiitwe vile?

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

ATAANGAMIZWA NA KUTENGWA NA WATU WAKE.

Ukoma wa nyumba ulifunua nini zamani?

Rudi Nyumbani

Print this post

Hadhari ni nini kibiblia? (Mithali 1:4)

Hadhari ni nomino ya kitenzi tahadhari. Neno Lenye maana ya “uangalifu”.

>Kwamfano mwalimu anayesahisha mitihani ya wanafunzi tunasema huwa na hadhari kubwa katika usahishaji.

  • Kula bila hadhari ya usafi huweza sababisha magonjwa.

Katika biblia neno hili utalisoma kwenye vifungu hivi;

Danieli  2:13 Basi ile amri ikatangazwa, na hao wenye hekima walikuwa karibu na kuuawa; watu wakamtafuta Danielii na wenzake ili wauawe.  14 Ndipo Danieli kwa busara na HADHARI akamjibu Arioko, akida wa walinzi wa mfalme, aliyekuwa ametoka ili kuwaua wenye hekima wa Babeli;  15 alijibu, akamwambia Arioko, akida wa walinzi wa mfalme, Mbona amri hii ya mfalme ina ukali namna hii? Ndipo Arioko akamwarifu Danielii habari ile

Mithali 1: 1 Mithali za Sulemani, mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli.  2 Kujua hekima na adabu; kutambua maneno ya ufahamu;  3 kufundishwa matendo ya busara, katika haki na hukumu na adili.  4 Kuwapa wajinga werevu, na kijana maarifa na HADHARI;

Yoshua 22:24 au kama sisi tumefanya jambo hili kwa HADHARI sana, tena makusudi, huku tukisema, Katika siku zijazo wana wenu yamkini wakanena na wana wetu, na kusema, Ninyi mna nini na Bwana, yeye Mungu wa Israeli?

Sisi pia kama watakatifu, tuwe na hadhari, katika maisha ya ulimwenguni. Tunaishi ulimwenguni lakini hatupaswi kufungwa nira na huo kwa jinsi isivyo sawasawa. Kwasababu watu wanaokosa jambo hili husongwa na anasa, udanganyifu wa mali na shughuli za ulimwengu huu, na tamaa ya mambo mengine hatimaye hawazalishi kitu.

Shalom.

Je! Umeokoka? Unatamani leo kupokea msamaha wa dhambi? Ikiwa jibu ni ndio basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya kumkaribisha Yesu moyoni mwako.>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Akida ni nani kibiblia, na kazi yake ni ipi? (Mathayo 8:5)

NGUVU YA HEKIMA NA AKILI

AGANO LA MOYO LENYE NGUVU

JE! WEWE NI MWANA WA IBRAHIMU?

Rudi Nyumbani

Print this post

Heshima ni nini kibiblia?

Heshima ni kitendo cha kumpa mtu hadhi yake, au uthamani wake anaostahili. Kwa kawaida kila mwanadamu anastahili heshima. Na hivyo kama mwamini huna budi kujua jinsi ya kuigawanya heshima kulingana na mtu husika. Kwasababu ukosefu wa heshimu, kwanza ni zao la kiburi (Mithali 15:33), lakini pia hukuondolea Baraka na kibali  popote pale uendapo. Lakini pia ukitoa heshima isiyompa mtu ni kosa pia.

Warumi 13:7  Wapeni wote haki zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahiliye hofu, hofu; astahiliye heshima, heshima

Heshima kwa Mungu ipo wapi?

  1. Ipo katika kuliamini na kuliishi Neno lake: Si katika kulipamba jina lake, na huku hufanyi anayokuambia. Alisema. Luka 6:46  Na kwa nini mnaniita, Bwana, Bwana, walakini hamyatendi nisemayo? 47  Kila mtu ajaye kwangu, na kuyasikia maneno yangu na kuyatenda, nitawaonyesha mfano wake.
  2. Ipo katika uaminifu katika  utoaji: Mithali 3:9 Mheshimu Bwana kwa mali yako, Na kwa malimbuko ya mazao yako yote
  3. Ipo katika ibada :  Anayestahili kuabudiwa, kusujudiwa, kupigiwa magoti, kuhimidiwa ni Mungu tu peke yake, na wala si mwanadamu au kiumbe kingine pamoja naye, heshima hii inamuhusu yeye peke yake. Ufunuo 4:11 “ Umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo vikaumbwa”

Heshima kwa Wazazi ipo wapi?

  1. Kuwasaidia. Biblia inasema kuwaheshimu wazazi ni pamoja na kuwasaidia kimahitaji (Mathayo 15:1-7)
  2. Kuwasikiliza na kushika maagizo yao: Mithali 1: 8 Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,

Heshima kwa Viongozi wako wa kiroho ipo wapi?

Kutii maelekezo yao.

Waebrania 13:17  Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.

Heshima kwa watoto ipo wapi?.

Kutowakwaza,

Waefeso 6:4  Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana.

Heshima kwa Viongozi wa nchi.

Kutenda agizo lao.

Warumi 13:1  Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu. 2  Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu

Heshima kwa Mabwana ipo wapi?

Kuwatumikia kwa uaminifu na adabu. (Waefeso 6:5-8)

Hivyo kwa hitimisho, ni kwamba kila mwanadamu anastahili heshima, haijalishi, tajiri, au maskini, mrefu au mfupi, mgonjwa au mzima, mwenye elimu au asiye na elimu, bwana au mtumwa, ameokoka au hajaokoka. Wote ni agizo tuheshimiane.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?

CHUJIO HILI NI LA AJABU SANA!

JIWE LILILO HAI.

Rudi Nyumbani

Print this post