Category Archive maswali na majibu

Hii ni maana ya Mathayo 6:29 hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo

SWALI: Naomba kufahamu nini maana ya vifungu hivi; 

Mathayo 6:29

[29]nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo.


JIBU: Katika habari hiyo Mungu anaeleza jinsi anavyoweza kutujali na kututunza sisi kipekee kwa uweza wake wa ki-Mungu, akifananisha na jinsi anavyoyatunza maua yake ya kondeni ambayo leo yapo kesho yananyauka na kutupa tanuruni.

ndio hapo anasema tusiwe na shaka ya leo tuvae nini,  kama Mungu anayavika vizuri maua hayo ambayo ni kwa muda mfupi tu huchanua baadaye hunyauka, si zaidi sisi tulio na thamani nyingi zaidi ya hivyo vyote?

Tena anasisitizia hata Sulemani katika fahari yake yote, hakuvikwa vizuri kama mojawapo ya maua hayo.

Kumbuka Sulemani alikuwa ni mtu tajiri sana, mavazi yake yalikuwa ni ya thamani sana, lakini yalitegemea kuchovywa na kurembwa kwa rangi mbalimbali, ambazo hizo baada ya kipindi fulani hupauka au kuchuja.

Lakini maua hayapakwi rangi bali uzuri ule ni rangi yao kwa asili itokayo ndani. hayafifi rangi. Sulemani hakuwahi kuwa na vazi la namna hiyo.

Isitoshe maua nayo licha ya kuwa na mwonekano mzuri lakini pia hutoa harufu yao nzuri ya asili, kitu ambacho hawezi kukiona kwenye vazi la aina yoyote zuri duniani kutoa harufu yake yenyewe, yanategemea kupuliziwa marashi.

Hivyo hiyo ni kutufundisha kuwa Mungu anaweza kutunawirisha na kutupendezesha zaidi ya matarajio yetu, lakini hiyo hutimia kwanza pale tunapojishughulisha  na mambo ya ufalme wake, ndio hayo mengine sasa ya chakula na mavazi atuzidishie.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ONA FAHARI JUU YA BWANA.

Nyinyoro ni nini?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Rudi Nyumbani

Print this post

Biblia inasema nini kuhusu mtu ‘Mwenye kujipendekeza (Mithali 29:5)

SWALI: Naomba kufahamu ujumbe ulio katika Mithali 29:5

‘Mwenye kujipendekeza kwa jirani yake, Hutandika wavu ili kuitega miguu yake’.

JIBU: Mithali hii inazungumzia madhara yanayoibuka katika tabia ya kujipendekeza.

Kujipendekeza ni kitendo cha mtu kumthaminisha mtu, hata kama alikuwa hastahili sifa hizo, ili tu upate kitu Fulani kutoka kwake. Kumthaminisha kunaweza kuwa kumsifia, au kumpongeza, au kumzungumzia mema yake kupita kiasi, au kueleza mabaya ya wengine kwa huyo mtu, n.k.

 Na yote hayo hayawi kwa lengo la kuuthamini kweli uzuri wa Yule mtu, hapana bali  ni aidha upate kupendwa wewe zaidi ya wengine, au usaidiwe, au upewe cheo,  au kipaumbele Fulani. Hata kama utaona mabaya yake huwezi kumwambia kwasababu, huna lengo la kusaidia bali upate matakwa yako tu.

Sasa  hilo ni kosa, matokeo ya hilo biblia inatuambia “unamtandikia wavu ili kuitega miguu yake”. Yaana unampeleka kwenye mtego au aungamivu wake kabisa.  Hii ni kweli, tunaona hata viongozi wengi wa nchi wameponzwa na wasaidizi wao wa karibu,na matokeo yake wakaiharibu  nchi, kwasababu tu ya kupokea sifa za uongo kutoka kwao, kwamba wanafanya vema, wanawajibiki vizuri n.k..  Kama ilivyokuwa kipindi kile cha Mfalme Sedekia na wale manabii wa uongo wajipendekezao, walimtabiria uongo, lakini Yeremia alimweleza mfalme ukweli  hawakutaka kumsikiliza. Matokeo yake Mfalme Sedekia akaingia katika matatizo makubwa ya kutobolewa macho na kupelekwa utumwani, hiyo yote ni kwasababu alikaa na manabii wajipendekezao (Yeremia 34-41), kama tu ilivyokuwa Kwa Mfalme Ahabu naye na manabii wake mia nne wa uongo.

Hii ni kutufundisha nini?

Hasaa biblia hailengi, tuwe makini na watu wajipendekezao. Hapana, kwasababu wakati mwingine si rahisi kuwatambua, inahitaji neema ya Mungu. Lakini inalenga hasaa katika upande wetu , kwamba sisi tujiepushe na ‘tabia ya kujipendekeza”. Kwasababu tunaweza kudhani tunatafuta faidi yetu tu wenyewe, lakini kumbe tunamsababishia madhara Yule mtu ambaye tunajipendekeza kwake. Tunategea wavu mbaya sana, aanguke na kupotea kabisa, na huo si upendo.

Itakusaidia nini akutendee mema, halafu yeye aangamie?

Hivyo, pastahilipo kweli kusifia tusifie, lakini si kwa lengo la kujipendekeza, kwasababu tukienda huko, tunatenda dhambi kubwa zaidi. Hiyo ndio maana ya hivyo vifungu, tufikiriapo kujipendekeza, tuone kwamba ni watu wasio na hatia tunawategea wavu waangamie.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TUZIJARIBU HIZI ROHO.

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

USIJISIFIE KARAMA KWA UONGO.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kama ni Mungu ndiye kaumba zao la Bangi kwanini tena iwe dhambi kuitumia??

Swali: Biblia inasema tumepewa mboga za majani kuwa chakula chetu, na Bangi pia ipo miongoni mwa zao la mboga za majani…sasa kwanini iwe dhambi kulitumia kama mboga au kiburudisho cha kusisimua (kuvuta) na ilihali ni Mungu mwenyewe ndio kaumba?


Jibu: Turejee..

Mwanzo 9:3 “Kila kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula chenu, kama nilivyowapa MBOGA ZA MAJANI, kadhalika nawapeni hivi vyote”.

Ni kweli maandiko hayo yanathibitisha ulaji wa mboga, lakini si mboga zote!.. Tukisema kila mboga iliyopo kondeni tumepewa tule, tutakuwa hatujayaelewa vizuri maandiko kwasababu  kuna mboga nyingi sana ambazo sumu!, ambazo zinamwonekano mzuri lakini hazifai kwa chakula… na Mungu hawezi kumpa ruhusa Mtu wake aliyemuumba, ale SUMU!..

Zipo mboga kwaajili ya chakula cha wanadamu, nyingine kwaajili ya wanyama na hazifai kwa wanadamu… vile vile zipo mboga zisizofaa kwa chakula cha wanadamu na wanyama… Mboga hizo zinabaki tu kwa utukufu wa Mungu, au kwaajili ya urembo, mfano wa mboga hizo ni MAUA.

Kuna Maua ambayo yana mwonekano mzuri sana lakini ni SUMU kali sana, mfano wa hayo ni kama haya yanavyoonekana hapa chini.

maua sumu

Hayo ni mfano wa Mboga, lakini si kwaajili ya kula bali kwaajili ya urembo tu.. yameumbwa na Mungu kwa lengo hilo, hivyo mtu akila hayo anaweza kupata madhara makubwa ya kiafya au hata kifo.

Vile vile na Bangi, inaweza kuwepo katika kundi hilo la MAUA, kama itatumika kwa urembo si vibaya, lakini kwa matumizi mengine ya ndani ya mwili wa binadamu ni hatari.

Kwahiyo si kila kilicho halalishwa basi kinafaa kwa matumizi yote.. hapana!.. Mboga zimehalalishwa lakini si kwa matumizi ya chakula tu, ndivyo maandiko yanavyotufundisha..

1Wakorintho 10:23  “Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo”.

Kwahiyo ulaji, au uvutaji wa Bangi ni dhambi kibiblia, vile vile matumizi ya tumbaku kula au kuvuta ni dhambi, kwani miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, na tena maandiko yanasema mtu akiliharibu hekalu hilo Mungu naye atamharibu mtu huyo (Soma 1Wakoritho 3:16-17 na 1Wakorintho 6:19).

Na Bangi inaharibu ufahamu wa mtu, ambao ndani yake kunazalika hasira, kutokujali, vurugu, matukano, mauaji, uasherati na mambo yote mabaya..

Hivyo Bangi ni haramu, vile vile tumbaku na mazao mengine yaletayo matokeo kama hayo.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nyungu ni nini kibiblia?(Ayubu 41:20,31, Waamuzi 6:19)

MTINI, WENYE MAJANI.

JE UNAZAA MATUNDA NA KUWAPONYA MATAIFA?

WENGINE WANAKESHA KWAAJILI YAKO.

Nini maana ya mmoja alikufa kwaajili ya wote hivyo walikufa wote? (2Wakorintho 5:14)?

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini Bwana MUNGU aliwazuia Adamu na Hawa wasile matunda ya Mti wa uzima waishi milele?

Swali: Kulikuwa na ubaya gani wa Adamu na Hawa kula matunda ya mti wa Uzima, ili wapate tena uzima wa milele baada ya kuupoteza? (Mwanzo 3:22-24).


Jibu: Turejee mistari hiyo..

Mwanzo 3:22 “Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, AKALA, AKAISHI MILELE;

23 kwa hiyo Bwana Mungu akamtoa katika bustani ya Edeni, ailime ardhi ambayo katika hiyo alitwaliwa”.

Sababu pekee ya Bwana MUNGU kuwazuia wazazi wetu wa kwanza (Adamu na Hawa) kula yale matunda ya Mti wa Uzima, si kwamba Mungu alikuwa hataki waishi milele!. La!.. kinyume chake ni mpango wake mkamilifu wa Mungu kwamba mwadamu aishi milele.

Tito 1:2 “katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu asiyeweza kusema uongo aliuahidi tangu milele”

Soma pia 1Yohana 2:25 utaona jambo hilo hilo…

Lakini kwasababu tayari mwanadamu alikuwa ameshaiingiza dhambi ndani yake na katika kizazi chake, hivyo asingeweza kuishi milele katika dhambi, hivyo ni lazima dhambi iondoke kwanza ndani yake ndipo aishi milele, kwasababu kama akiishi milele na dhambi imetawala maisha yao, ni uharibifu mkubwa utaendelea na maisha yatakuwa nje na mpango wa Mungu, kwasababu yeye Mungu ni mkamilifu, hivyo kanuni ya maisha ya milele, ni sharti yasiwe na dhambi.

Kwahiyo BWANA MUNGU akaweka mpango kwanza wa kuiondoa dhambi ndani ya mtu, na mzizi wake, kisha yule mtu apate tena uzima wa milele.

Na mpango wa Mungu wa kuondoa dhambi ndani ya Mtu na kumrejeshea Uzima wa milele, ameushona ndani ya Mwanae YESU KRISTO, kwamba kwa kupitia njia ya kumwamini yeye, na kutubu basi tunaoshwa dhambi zetu na kupata uzima wa milele.

Warumi 5:21 “ili kwamba, kama vile dhambi ilivyotawala katika mauti, vivyo hivyo kwa njia ya haki neema itawale hata uzima wa milele kwa Yesu Kristo Bwana wetu”.

17  Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye”.

Hivyo kamwe hatuwezi kupata uzima wa milele, tukiwa katika dhambi..ni lazima kutubu kwanza na kumwamini Bwana YESU ndipo tupate uzima wa milele.

Na hiyo ndio sababu ya Bwana MUNGU kuifunga ile njia ya MTI WA UZIMA pale Edeni, ilikuwa ni sharti kwanza ADAMU na HAWA watakaswe ndambi zao kwa damu ya Mwanakondoo… Na majira yalipofika Mungu alimtuma mwanae ili afe kwaajili ya wote walio hai, na waliokwisha kutangulia, waliokufa katika haki, ili kwamba wote tutakaswe na kupata uzima wa milele.

Na hili ni la kujua siku zote, kwamba hakuna uzima wa milele kwa mwingine yeyote Zaidi ya YESU KRISTO.

Yohana 3:35 “Baba ampenda Mwana, naye amempa vyote mkononi mwake.

36  Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele; asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia”.

Mistari ifuatayo inazungumzia uzima wa milele ndani ya YESU KRISTO (1Yohana 5:11-13, Yohana 3:16, Yohana 5:24,  Yohana 6:54,  Yohana 12:50, Yohana 17:2, na Warumi 6:23)  .

Je umempokea BWANA YESU?… kama bado unangoja nini?..Fahamu kuwa hizi ni siku za mwisho, majira yameenda sana na ule mwisho umekaribia.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

INJILI YA MILELE NI IPI KATIKA BIBLIA?

MJUE SANA YESU KRISTO.

NGUVU YA UPENDO WA KRISTO.

Rudi Nyumbani

Print this post

Wote wampendao Bwana wetu Yesu Kristo katika hali ya kutokuharibika. 

SWALI: Nini maana ya Waefeso 6:24, pale inaposema “katika hali ya kutoharibika”?

[24]Neema na iwe pamoja na wote wampendao Bwana wetu Yesu Kristo katika hali ya kutokuharibika.


JIBU: Mtume Paulo alipokuwa anahitimisha ujumbe wa waraka wake kwa waefeso, alimalizia kwa kuwatamkia neno la heri watu watu wale akiwaambia ‘NEEMA  ikae pamoja nao.

Lakini tunaona hapo hakukusudia tamko hilo kwa watu wote,  bali anasema ikae kwa wale wampendao Bwana, lakini bado sio tu kwa  wampendao Bwana.. Bali wampendao katika “hali ya kutokuharibika”.

Yaani kwa ufupi upendo usio poa.. Ndio upendo usio haribika.

Ndio ule unaozungumziwa kwenye 1Wakoritho 13. Kwamba hustahimili yote, huvumilia yote, huamini yote, haupungui Neno wakati wowote.

Ni kuonyesha kuwa Bwana wetu Yesu Kristo anastahili kupendwa daima, zaidi ya vitu vyote, kwasababu ya upendo wake mkuu aliotuonyesha sisi wa kuacha vyote mbinguni kwa ajili yetu, ili tukombolewe. Na kwa rehema zake akatupa na vipawa kabisa, na uwezo wa kuitwa wana wa Mungu, kwa nguvu za Roho wake Mtakatifu aliyetupa . Hakika anastahili kupendwa  sana bila ukomo.

Zingatia: Waraka huu sio wa waefeso tu, bali ni wetu pia sote tumeandikiwa. Hivyo tutaongezewa neema ikiwa tutampenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa upendo usio haribika. Sio njaa itufanye tumwache, au ufukara, au mke, au kazi, au uzuri, au ubaya, au ndugu, au mali, au afya, au ugonjwa.. au kitu chochote, Bali kila wakati sisi shauku yetu kwa Kristo iwe ni ile ile. Kuomba ni kule-kule, kumtafuta Mungu ni kule-kule. Amen

Neema ya Bwana iwe nasi.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE! SISI KAMA WAKRISTO NI DHAMBI KUSHEHEREKEA KRISMASI?.

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

Lalama kwa uhai wa watoto wako wachanga wazimiao kwa njaa(Maombolezo 2:19)

Rudi Nyumbani

Print this post

NIONYESHE MARAFIKI ZAKO, NIKUAMBIE TABIA ZAKO.

Mithali 13:20 Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.

Tulipokuwa watoto wazazi wetu walitufundisha kubagua baadhi ya marafiki tuliokuwa nao, na cha ajabu vigezo walivyotumia  havikuwa hata rangi zao, au kimo chao, au afya zao, bali tabia zao na akili zao. Wale watoto waliokuwa na nidhani, na akili shuleni wazazi wetu walitushurutisha sana kukaa nao karibu, kwasababu waligundua kuwa na sisi tutaambukizwa tabia zao, lakini wale waliokuwa watukutu, hata tulipokutwa tunacheza nao tu, tuliadhibiwa, sisi tuliona kama ni uonevu usio kuwa na tija, lakini baadaye tulipokuwa watu wazima, na kuona hatma ya wale watoto, ndio tulijua ni nini wazazi wetu walikuwa wanakiona.

Vivyo hivyo katika maisha ya rohoni, tunaambiwa.

Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.

Mbele za Mungu wenye hekima ni watu gani?

Ni watu waliookoka, wenye hofu ya Mungu ndani yao.

Mtu yeyote aliyemwamini Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yake, huku akiendelea katika kumcha Mungu kwelikweli, huyo ni wa kukaa karibu naye sana. Kwasababu na wewe utajifunza njia za wokovu, utaambukizwa kuomba, utaambukizwa mifungo, utaambukizwa upendo wa ki-Mungu, lakini pia na maarifa ya Neno la Mungu, pamoja na uinjilisti.

Watu hawafahamu kuwa hata hekima ya mwokozi wetu Yesu haikuja tu kwa kutegemea hekima kutoka juu kwa baba yake, hapana, ilichangiwa pia  na watu aliowachagua kukaa nao karibu, tangu alipokuwa mdogo, tunalithibitisha hilo pindi alipokuwa amekwenda Yerusalemu na wazazi wake kwa ajili ya kuila sikukuu, kama kijana angeweza kukaa na wenzake, kujifunza uchezaji wa kamari, au kutembea mitaani kutafuta wasichana, au kwenda kwenye dansi na sinema, na kujiunga na makundi ya wavuta bangi. Lakini, haikuwa hivyo kwake, yeye alichagua watu ambao wangekuwa ni wa muhimu kwake, ndio wale viongozi wa imani na waalimu waliotwa marabi, akawa akiwasikiliza hao na kuwauliza maswali, na ghafla akaambukizwa tabia zao, mpaka akawa yeye ndio RABI wao mkuu.

Luka 2:40  Yule mtoto akakua, akaongezeka nguvu, amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake. 41  Basi, wazee wake huenda Yerusalemu kila mwaka, wakati wa sikukuu ya Pasaka.

42  Na alipopata umri wake miaka kumi na miwili, walipanda kama ilivyokuwa desturi ya sikukuu;

43  na walipokwisha kuzitimiza siku, wakati wa kurudi kwao, yule mtoto Yesu alibaki nyuma huko Yerusalemu, na wazee wake walikuwa hawana habari.

44  Nao wakadhani ya kuwa yumo katika msafara; wakaenenda mwendo wa kutwa, wakawa wakimtafuta katika jamaa zao na wenzao;

45  na walipomkosa, wakarejea Yerusalemu, huku wakimtafuta. 46  Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, AMEKETI KATIKATI YA WAALIMU, AKIWASIKILIZA NA KUWAULIZA MASWALI.

47  Nao wote waliomsikia walistaajabia fahamu zake na majibu yake. 48  Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni.

49  Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu? 50  Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia

Mambo mengine hutaweza kuyaacha, au tabia nyingine hutaweza kuziondoa ndani yako. Kama hutaweka machaguzi ya watu sahihi wa kuongozana nao. Utakuta ni mkristo analalamika ni mzito wa kuomba, au kushuhudia, au kufunga. Ukiangalia kampani ya watu wake muda wote, ni wafanyakazi wenzake wa ofisini, ni marafiki zake wa chuo, ni majirani zake hapo mtaani. Lakini wapendwa, au watumishi wa Mungu waaminifu, ni jumapili tu kukutana nao kanisani, hata anapotafutwa, kukumbushwa wajibu wake kiroho, anawakwepa. Na wakati huo huo anatumainia awe moto kiroho. Hapo ni kujidanganya.

Tunahitaji  kupashana moto, kamwe huwezi simama kipeke yako, haijalishi wewe ni nani, au unamjua Mungu kwa ukubwa kiasi gani. Tembea na waombaji  ili  uwe mwombaji, tembea na washuhudiaji ili uweze  kushuhudia, kaa na waalimu ili uwe mwalimu. Nje ya hapo utageuzwa na ulimwengu,.

 Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Usimwache rafiki yako mwenyewe, wala rafiki ya baba yako.

NGUVU YA HEKIMA NA AKILI

IVUMBUE INJILI YA KRISTO KUTOKA KATIKA KILA JAMBO.

Rudi Nyumbani

Print this post

JINSI YA KUSHINDA VISULISULI(Mithali 10:25)

SWALI: Nini maana ya hii Mithali 10:25

Kisulisuli kikiisha pita asiye haki hayuko tena; Bali mwenye haki ni msingi wa milele.


JIBU: Mstari huo unajifafanua vizuri kwenye ule mfano Bwana Yesu aliutoa kuhusiana na watu wanaoyasikia maneno yake, halafu hawayatendi. Tusome.

Mathayo 7:24  Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;

25  mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba.

26  Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;

27  mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.

Hivyo tukirejea katika vifungu vile vya kwenye mithali. Unaweza kuelewa mtu asiye haki hasaa ni nani?

Ni Yule ambaye anaisikia injili, halafu hatii.  Mtu Yule anayesema ameokoka, lakini zao la wokovu halionekana ndani yake. Rohoni anaonekana hana tofauti na yule ambaye hajamjua Mungu kabisa. Wote hao huitwa wasio haki. Bado wapo dhambini, hawajakombolewa na damu ya Yesu Kristo.

Hawa wataonekana kwa nje kama vile ni watakatifu. Lakini kinapokuja tu kisulisuli  aidha  cha majaribu, shida, dhiki, udhia,au mapigo kwa ajili ya Kristo, mara ghafla wanarudi nyuma, wanakuwa kama watu ambao hawajawahi kumjua Mungu kabisa, kwasababu hakujikita katika mwamba. Wengine sio majaribu ya shida, bali yale ya mafanikio makubwa, ndio hapo anasa zinawazidi wanamsahau Mungu, wanaiaga imani, kwani walimfuata Yesu kwasababu ya shida tu. Wengine ndoa, elimu, vyeo wakishavipata, huwaoni tena kwa Yesu.

Lakini mtu anayeyasikia maneno ya Kristo na kuyatii, ni kinyume chake, huitwa msingi wa milele. Huyo hatikiswi na wimbi, kisulisuli au dhoruba yoyote. Kwasababu yupo juu ya mwamba.

Okoka, upokee msamaha wa dhambi, kisha ishi kufuata na toba yako, ili uhakika wa kusimama uwe nao wakati wote.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MWAMBA WETU.

Mtu asiye na akili ni nani kibiblia?

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

Rudi Nyumbani

Print this post

Maelezo ya Mithali 28:28 Wasio haki wainukapo, wanadamu hujificha; Bali waangamiapo, wenye haki huongezeka.

SWALI: Nini maana ya  Mithali 28:28 Wasio haki wainukapo, wanadamu hujificha; Bali waangamiapo, wenye haki huongezeka.


JIBU: Mithali hii hulenga hasaa watawala, iwe ni serikalini, kwenye mataasisi, makanisa n.k. endapo waongozao ni waovu, basi hufanya hata watu (hususani wale wema) kujificha, Au kutoonekana kabisa.

Ndio kama ilivyokuwa katika kipindi cha mfalme Ahabu, alipoiharibu nchi yote ya Israeli kwa kuweka miungu migeni, akichochewa na mkewe Yezebeli. Wakati huo Manabii wengi wa Mungu waliuliwa, na wale waliosalia walijificha wasionekane kabisa, wakabakia tu makuhani wa baali na wenye dhambi. Kiasi kwamba Eliya akadhani ni yeye tu peke yake nabii aliyebakia Israeli. Kuonyesha ni jinsi gani wenye haki, walivyokuwa adimu wakati huo. Lakini Mungu alimwambia Eliya, nimejisazia watu elfu saba wasiopigia goti baali.

Warumi 11:3  Bwana, wamewaua manabii wako, wamezibomoa madhabahu zako, nami nimesalia peke yangu, nao wananitafuta roho yangu.

4  Lakini ile jawabu ya Mungu yamwambiaje? Nimejisazia watu elfu saba wasiopiga goti mbele ya Baali.

5  Basi ni vivi hivi wakati huu wa sasa, yako mabaki waliochaguliwa kwa neema.

Ni kama leo tu ulimwenguni, tunavyoona kiwango cha watenda maasi na  maasi kinavyozidi kuongezeka, ndivyo inavyokuwa ngumu kukutana na watakatifu halisi, na hiyo inaweza pelekea pengine ukajidhani mpo wachache, au hakuna kabisa kama wewe.

Ukiwa katika mazingira kama haya usipumbazike, ukafanana na ulimwengu. Bali fahamu kuwa wapo, isipokuwa Mungu amewaficha tu. Siku watakapoondolewa waovu duniani ndipo utajua kuwa Mungu anao watakatifu wake, wengi.

Ndio maana ya hilo neno Bali “waangamiapo wasio haki, wenye haki huongezeka”.

Binti ambaye unatembea kwa kujisitiri barabarani, na huwenda huoni aliye kama wewe mtaa mzima, usife moyo, ni kwasababu wasio haki ni wengi. Kijana uliyeamua kuishi maisha ya mbali na uzinzi na anasa usijidhani upo peke yako, songa mbele tambua, ni  Mungu amewaficha tu watu wake. 

Kwasababu ni Neno la kweli kabisa wasio haki wastawipo, wenye haki hujificha, (sio kwamba wamekufa, bali wapo). Wakati utafika waovu wataondolewa, na sisi tutamiliki na kuangaza. Usiwe mfauta wimbi, nyakati hizi ni za hatari. Ni sawa na kichuguu tu, waweza kudhani hakina kumbikumbi ndani, kina huoni chochote kinachotoka humo,  lakini wakati wa mvua, unastaajabia wingi wao umetoka wapi. Vivyo hivyo na wewe endelea kutembea kwa ujasiri katika wokovu wako. Unyakuo umekaribia. Tambua Bwana analo jeshi lake.

Mithali 28:28 Wasio haki wainukapo, wanadamu hujificha; Bali waangamiapo, wenye haki huongezeka.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Miungu wasio na kikao pamoja na wenye mwili.

Nawiwa na Wayunani na wasio Wayunani.

Semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; (Luka 17:10) 

Rudi Nyumbani

Print this post

Tafsiri ya Mithali 27:15 Kutona-tona daima siku ya mvua nyingi, Na mwanamke mgomvi ni sawasawa;

SWALI: Nini maana ya Mithali 27:15 Kutona-tona daima siku ya mvua nyingi, Na mwanamke mgomvi ni sawasawa;


JIBU: Neno Kutona-tona kama lilivyotumika hapo, ni “maji yanayovuja darini”.

Hivyo anaposema Kutona-tona daima siku ya mvua nyingi. Anamaanisha kitendo cha kuvuja sana kwa dari siku ya mvua nyingi, na kitendo cha kukaa na mwanamke mgomvi ndani ni sawasawa.

Kwa namna gani?

Tunajua ukikaa kwenye nyumba ambayo dari lake halikujengwa vizuri, mvua kubwa inaponyesha maji mengi huchuruzika na kuingia ndani. Wakati umelala utashangaa maji yanakudondekea kitandani mwako, yanachuruzikia kwenye makochi, yanakwenda mpaka kwenye makapeti, jambo ambalo litakufanya usitulie hata kidogo humo ndani utakuwa tu bize, kusogoza vitu ovyo ovyo visilowe, na mbaya ni pale mvua inapokuwa kubwa, na maji kuongezeka ndani, mwisho huwa ni kutoka kabisa nje na kuiacha nyumba.

Ikiwa umeshawahi kupitia changamoto kama hiyo ya kuvujiwa nyumba, unaelewa ni kero kiasi gani.

Ndivyo anavyofananisha kutendo hicho na kuishi na mwanamke mgomvi. Ikilenga hasaa wanandoa. Kumbuka aliyeandika mithali hizi ni Sulemani, alikuwa anatambua anachokisema, kwasababu aliishi na wanawake elfu moja(1000) kama wake zake, na alijua masumbufu yao. Alikutana na changamoto za baadhi yao.

Mwanamke mgomvi, kibiblia ni Yule asimheshimu mumewe, ni Yule anayemwendesha mumewe, anayemkaripia, asiyekuwa msikivu, kila jambo analolifanya mumewe ni kulikosoa tu, mwenye kiburi na mwenye maneno mengi, asiye na staha.

Wanawake wa namna hii, huwataabisha waume zao sana, na hatimaye wengine huwafanya wahame kabisa nyumba, kukaa mbali na familia zao. Ni dari linalovuja utawezaje kukaa kwenye nyumba hiyo?

Andiko hilo limerudiwa pia katika;

Mithali 19:13 Mwana mpumbavu ni msiba kwa babaye; Na ugomvi wa mke kama kutona-tona daima.

Uonapo familia zenye migogoro ya namna hii ni kuziombea sana Bwana aziponye.

Maandiko hayo yamewekwa sio kuonyesha mabaya kwa jinsia ya kike, hapana, bali imetoa tahadhari ili yasitokee kwa wanawake wa kikristo.

Biblia imetoa mwenendo wa mwanamke halisi wa kikristo, inasema  awe ni wa kumtii mume wake. Awe ni mwenye kiasi, na MPOLE, na adabu. Akifanya hivyo atasimama vema kwenye nyumba yake, badala ya kuiharibu kinyume chake ataijenga.

1Timotheo 2:9  Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;

10  bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.

11  Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna.

Soma pia.

1Petro 3:1  Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;

2  wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu. 3  Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

4  bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, ROHO YA UPOLE NA UTULIVU, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.

5  Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.

6  Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote.

Hivyo wewe kama mwanamke ukitembea katika hayo, utakuwa katika upande salama wa Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Wokovu wa milele/ Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?

HUIJUI KAZI YA MUNGU, AFANYAYE MAMBO YOTE.

ALIJARIBIWA SAWASAWA NA SISI KATIKA MAMBO YOTE.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je kazi ya udalali ni dhambi?

Swali: Je kazi ya udalali ni dhambi, na Mkristo anaruhusiwa kuifanya?


Jibu: Dalali ni yule mtu anayeuza kitu kwa niaba ya mwingine na kisha kuchukia asilimia fulani ya faida ya kile kilichouzwa.

Au pia dalali anaweza kuwa mtu mwenye kutafuta soko la bidhaa ya mtu mwingine na kisha kuchukua asilimia ya faida inayopatikana.

Kama hiyo ndio maana au tafsiri ya udalali, basi mtu akiifanya “SI DHAMBI”, Kwani hata ununuaji wa bidhaa kiwandani na uuzaji masokoni kwa namna moja au nyingine ni “Udalali”, kwani utanunua kwa gharama ndogo na kuuza kwa gharama kubwa na kisha kuichukua ile faida….Hapo tayari umeshakuwa dalali wa wenye kuitengeneza ile bidhaa..

Kwahiyo udalali si dhambi ikiwa tu haujahusisha mambo yafuatayo.

   1. UONGO.

Labda umepewa kazi ya kutafuta mteja wa bidhaa husika, halafu ukampata na kumwekea kiwango cha juu sana nje na mapatano na yule aliyekupa bidhaa (lengo la kufanya hivyo ni ili wewe upate faida kubwa na ya haraka)…

Au mteja amehitaji bidhaa au nyumba na wewe ukamlaghai kwa uongo na kumpa kitu ambacho kiko chini ya viwango na huku ukijua kabisa kuwa kitu hiko hakistahili hiyo gharama, Huo wote ni Uongo na udalali huo ni haramu.

   2.Dhuluma.(Utapeli).

Unapomdhulumu mtu fedha au bidhaa yake, aidha kwa kumlipa kisasi au kwasababu nyigine yoyote udalali huo ni haramu.

3. Haifanyiki ndani ya nyumba ya Mungu..

Udalali unaofanyika ndani ya Nyumba ya MUNGU ni haramu..

Utaona Bwana YESU aliwafukuza wale madalali wote waliokuwa wanabadili fedha ndani ya nyumba ya MUNGU.

Yohana 2:15 “Akafanya kikoto cha kambaa, akawatoa wote katika hekalu, na kondoo na ng’ombe; akamwaga fedha za wenye kuvunja fedha, akazipindua meza zao;”

Vivyo hivyo kanisani si sehemu ya minada, na udalali, ni sehemu ya Ibada takatifu ya roho na kweli.

Swali lingine je?…Fedha ya udalali inaweza kutolewa sadaka ikiwemo Zaka?.

Jibu ni Ndio!.. kama  udalali huo haujahusisha mambo hayo hapo juu, basi inaweza kutolewa sadaka ikiwemo Zaka(yaani fungu la Kumi), na ikakubalika mbele za Mungu.

Na je mkristo anaweza kufanya kazi ya udalali??..

Jibu ni Ndio! Anaweza kufanya, ikiwa hatatumia Uongo, au dhuluma, au rushwa, au kufanya ndani ya kanisa la Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KAMA MHUBIRI USIWE MFANO WA DIOTREFE.

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

TUZIJARIBU HIZI ROHO.

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

WALA HAKUSIMAMA MTU PAMOJA NAYE, YUSUFU ALIPOJITAMBULISHA KWA NDUGUZE

Rudi Nyumbani

Print this post