Title September 2022

SHAMBA HUWA HALIMTAMBUI WALA KUMSUBIRIA MKULIMA.

Karibu tujifunze hekima, zilizo katika Neno la Mungu, Tukisoma Mithali 4:30-34 inasema..

30 “Nalipita karibu na shamba la mvivu, Na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili.

31 KUMBE! LOTE PIA LIMEMEA MIIBA; Uso wake ulifunikwa kwa viwawi; Na ukuta wake wa mawe umebomoka.

32 Ndipo nilipoangalia na kufikiri sana; Naliona, nikapata mafundisho.

33 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, Bado kukunja mikono upate usingizi!

34 Hivyo, umaskini wako huja kama mnyang’anyi, Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha”.

Sulemani anaeleza, tukio alilokutana nalo katika shamba la huyu mtu ambaye alimtambua kama mvivu, Na tukio lenyewe lilimtafakarisha sana.. Yeye alidhani, kwa kulala kwake, na  kuchelewa kwake kulilima shamba lake, basi ndio litabakia vilevile, bila chochote kuwepo juu yake. Lakini kilichomstaajabisha ni kuona mazao mengi sana, tena makubwa yaliyostawi, lakini hayakuwa yale aliyoyapanda bali ni miiba.

Kuonyesha kuwa shamba halimsubirii wala halimtabui mkulima, kazi yake ni kuchepusha chochote kile kinachokuja kupandwa juu yake.. Kama ni mchicha, kama ni gugu, kama ni mwiba, kama ni mbigili, kama ni bangi, kama ni tumbaku, haijali kipandacho, hiyo ndio tabia ya shamba lolote Maandiko yanasema hivyo katika (Marko 4:26-29)

Hivyo mtu asipowajibika mwenyewe, kusafisha shamba lake, na kuhakikisha, anayatoa yale yasiyostahili, au analipalilia mara kwa mara, ajue kuwa ataangukia hasara, na mwisho wa siku kazi yake inakuwa bure. Sikuzote kazi nzito ya ukulima ipo katika kupalilia na kulitunza shamba, dhiki ya wavamizi, na magugu, na sio katika kupanda. Kwasababu kupanda kunaweza kuchukua siku moja au mbili basi. Lakini kulitunza shamba ni jambo lingine, linalomgharimu mkulima, kila siku awe anaamka asubuhi na mapema, na mara kwa mara kulitembelea shamba lake, kulitazama na kulipalilia.

Hii ikifunua nini?

Mioyo yetu ni mashamba..Chochote kinachopandwa iwe na Mungu, au ibilisi, au mwanadamu, ni lazima kimee tu, tupende  tusipende.. Hapo ndipo umakini unapohitajika sana, Hii ndio sababu kwanini maandiko yanasema, tuilinde mioyo yetu kuliko yote tuyalindayo (Mithali 4:23). Kwasababu chochote kile kinamea.

Hivyo, ikiwa huna tabia ya kuutazama tazama moyo wako, basi rohoni unatafsirika  kama mvivu wa hali ya juu, unalala,  pale unaposema, aaa, kesho nitasoma Neno, wiki ijayo, nitakwenda Ibadani, hujui kuwa shamba lako (moyo wako), unamea miiba  usiyoijua wewe na viwavi kila siku…

Ndugu kusema nimeokoka tu, hakutoshi, ni lazima kila siku uhakikishe umeongeza jambo jipya katika maisha yako ya kiroho, jiulize, je! Lile Neno ulilohubiriwa au ulilolisoma, umeliishi vipi katika siku yako, au wiki yako yote. Ni lazima ufanye hivyo kila siku.  Usijisahau, ukawa unaikumbuka roho yako, jumapili kwa jumapili, hiyo ni hatari kubwa sana,..Hata hiyo ibada haiwezi kukusaidia chochote, kwasababu magugu ni mengi kuliko ngano, hivyo utalemewa tu, ukristo wako utakuwa ni mzito sana..

Kama hujui kila inapoitwa leo shetani anaturushia mbegu zake mioyoni mwetu, unapopita barabarani na kusikia miziki ya kidunia, unapokuwa ofisini na kusikia lugha za mizaha kwa wafanyakazi wenzako, hizo ni mbegu, unapokuwa shuleni na kusikia matusi kwa wenzako, unapofungua tv, internet, whatsapp, youtube, na kuona mambo yasiyokuwa na maadili, zote hizo ni mbegu, ambazo kama usipozushughulikia mapema ndani ya siku, zitamea tu, haijalishi wewe ni nani…

Hivyo tunazishughulikia , kwa kusali kila siku, kutafakari maneno ya uzima, kujitenga na uovu, kukaa katika utulivu, kuomba rehema, na kujizuia sana. Tukizingatia haya kila siku. Basi mbegu halisi za Mungu tu, ndio zitakazokuwa zinamea mioyoni mwetu. Na matokeo yake tutakuja kula matunda yake baadaye.

Hivyo tusiwe watu, wa kukumbushwa kumbushwa habari za maisha yetu ya kiroho, tuamke usingizini, tuondoe uvivu, tukayatazame mashamba yetu kila siku. Anza sasa kuwajibika kwa kila kitu kinachoukaribia moyo wako, ikiwa hakimpendezi Mungu, hakikisha unashughulika nacho, hadi kiondoke.

Waefeso 5:14 “Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza.

15 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;

16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.

17 Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana”.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NI NANI ATAKAYEUCHUKUA MSALABA WA YESU?

MWENGE WAKO WA UHURU UPO WAPI?

AINA TATU ZA WAKRISTO.

Kwanini Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasichukue chochote isipokuwa fimbo tu?

UTENDAJI KAZI MWINGINE WA ROHO MTAKATIFU USIOUFAHAMU.

Wakati wakina Shadraka wanatupwa katika tanuru la moto, Danieli alikuwa wapi?

Rudi nyumbani

Print this post

MAZUNGUMZO MABAYA HUHARIBU TABIA NJEMA.

Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu..

Je umewahi kujua  kuwa mazungumzo mabaya, yanaharibu tabia njema?..

Biblia inasema katika.

1Wakorintho 15:33 “Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema”.

Hapo haisemi, “mazungumzo mabaya yanachochea tabia mbaya”.. La!, bali anasema “yanaharibu tabia njema”. Maana yake mtu mwenye tabia njema, na nzuri na inayovutia, anapoketi kuzungumza, au kusikiliza mazungumzo mabaya, kidogo kidogo anaanza kuiharibu ile tabia yake njema. Haijalishi, hatashiriki hayo mazungumzo, lakini hata kile kitendo cha kusikiliza tu!, tayari tabia yake itaanza kuathiriki.

Ndio maana biblia inatuonya hapo tukae mbali na mazungumzo yote mabaya!..

Na mazungumzo mabaya ni yapi?, ni mazungumzo yote yenye maudhui ya kizinzi, au usengenyaji, umbea, au wizi, au anasa na starehe za kidunia n.k,  na mazungumzo haya mabaya yanapatikana katika sehemu zifuatazo.

1.Kwenye Vijiwe.

Vijiwe ni sehemu yoyote watu wanapokutana kujifurahisha kwa maneno, au michezo.. kwamfano vijiwe vya watu wanaocheza michezo ya draft, au bao, wanaobashiri, au mipira n.k..

2. Kwenye mitandao

Unapotumia muda mwingi kukaa kwenye mitandao kama facebook, au whatsapp na unapojiunga kwenye makundi yasiyo ya neno la Mungu, au yasiyo ya na maana, hata kama huchangii chochote katika mijadala inayozungumziwa kule, wewe ni msomaji tu!, fahamu kuwa unaiharibu tabia yako njema.

3. Televisheni.

Unapotazama tamthilia za kidunia, pamoja na vipindi vingine vya kidunia na mijadala na midahalo mbali mbali katika luninga, ambayo maudhui yake ni ya kidunia, fahamu kuwa unaiharibu tabia yako njema, hata kama wewe huchangii chochote, ni mtazamaji tu!.. bado tabia yako inaharibika.

4. Vitabu vya simulizi.

Unapoketi na kusoma vitabu vya simulizi za kidunia, ambazo ni tungo za watu..ambazo nyingi maudhui zake ni kuchochea anasa, uasherati, na wakati mwingine kuamini uchawi.. Vitabu hivyo vinaharibu tabia njema uliyokuwa nayo, vinaharibu tabia nzuri, ambayo pengine Roho Mtakatifu alikuwa ameshaanza kuiimba ndani yako.

Hivyo ukitaka tabia yako isiharibike jihadhari na mambo hayo.. Kama ni mwanaume kaa mbali na kampani mbaya, nenda katika vijiwe kuhubiri injili, lakini si kusikiliza mambo yanayoendelea pale,  au kushiriki mijadala yao…kama ni mwanamke au binti, nenda vijiweni kuhubiri lakini si kwenye kusikiliza wala kushiriki mazungumzo yao.

Hebu tujifunze mfano mmoja kwenye biblia ya Binti mmoja aliyekuwa na tabia nzuri, kuliko wenzake wote katika familia yake, lakini siku alipotoka na kwenda kukutana na mabinti wengine wa kidunia, akajikuta kabadilika tabia na kuwa mwingine.

Na msichana huyo si mwingine zaidi ya Yule binti wa Yakobo, aliyeitwa Dina, Hebu tusome habari yake kidogo.

Mwanzo 34:1 “Basi Dina, binti Lea, ambaye Lea alimzalia Yakobo, AKATOKA KUWAONA BINTI ZA NCHI.

  2 Shekemu, mwana wa Hamori, Mhivi, mkuu wa nchi, AKAMWONA AKAMTWAA, AKALALA NAYE, AKAMBIKIRI. ”

Umeona chanzo cha Dina kuharibika tabia??.. Si nyingine zaidi ya kutoka na “kwenda kukutana na mabinti wa kidunia”, ambao stori zao ni huenda ni kuzungumzia wanaume tu, na hadhi zao, na Dina akiwa katika kusikiliza akajikuta kashawishika na kujikuta anazini na binti wa mfalme wa nchi, ambaye alikuwa ni mpagani!…Jambo ambalo ni baya sana, mbele za Mungu na mbele ya baba yake Yakobo!

Sasa kujua Dina alikuwa ni binti wa tabia gani hapo kwanza.. hebu tusome tena mstari ufuatao..

Mwanzo 34:19 “Na yule kijana hakukawia kulifanya neno lile, maana amependezewa na binti Yakobo, naye alikuwa MWENYE HESHIMA KULIKO WOTE NYUMBANI MWA BABAYE”.

Umeona?, Dina alikuwa ni mwenye heshima kuliko wote.. lakini ndiye aliye haribika kuliko wote..jambo linalohuzunisha sana!.. Sasa kama mwana wa Yakobo, mrithi wa ahadi za Mungu kaharibiwa.. wewe ni nani usiharibike??..

Kamwe usijivunie tabia yako, na kusema hakuna mtu anayeweza kukubadilisha wala hakuna chochote kitakachoweza kukubadilisha (na huku ni mtu wa kuzunguka katika vijiwe na mitandao).. fahamu kuwa Neno la Mungu ni thabiti.. limesema “tukae mbali na mazungumzo mabaya ili tusiharibu tabia zetu”... wewe na mimi hatuwezi kulisahihisha na kusema “si mazungumzo yanayoweza kumbadilisha mtu, bali ni mtu mwenyewe ndio anayeweza kujibadilisha”.

Watu wengi wanaorudi nyuma katika siku hizi za mwisho ni kwasababu hiyo.. wanazama katika kusikiliza na kushiriki mazungumzo mabaya na hatimaye wanajikuta tayari wameshapoa na kuikana imani kabisa.

Ndugu Kaa mbali na mazungumzo yote mabaya, na kinyume chake, tafuta mazungumzo mazuri ili ujenge tabia yako, na mazungumzo mazuri, utayapata kanisani, na kwenye biblia, na kwenye vipindi au makala za Neno la Mungu.

Bwana Yesu akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JIHUDHURISHE, ILI AANZISHE MAZUNGUMZO NA WEWE

KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

VITA VYA KIFIKRA BAADA YA KUZALIWA MARA YA PILI

YONA: Mlango wa 4

Rudi nyumbani

Print this post

WENYE KUHADAA ROHO ZISIZO IMARA.

SWALI: Naomba kufahamu biblia inaposema wenye kuhadaa roho zisizo imara ina maana gani? (2Petro 14)

JIBU: Tusome;

2Petro 2:14 “wenye macho yajaayo uzinzi, watu wasiokoma kutenda dhambi, WENYE KUHADAA ROHO ZISIZO IMARA, wenye mioyo iliyozoezwa kutamani, wana wa laana;

15 wakiiacha njia iliyonyoka, wakapotea, wakiifuata njia ya Balaamu, mwana wa Beori, aliyependa ujira wa udhalimu;

16 lakini alikaripiwa kwa uhalifu wake mwenyewe; punda, asiyeweza kusema, akinena kwa sauti ya kibinadamu, aliuzuia wazimu wa nabii yule.

17 Hawa ni visima visivyo na maji, na mawingu yachukuliwayo na tufani, ambao weusi wa giza ni akiba waliyowekewa”.

Katika siku za mwisho biblia inatabiri kuwa litatokea kundi Fulani la watu mahususi, lenye kazi ya “kuhadaa roho za watu watu”.

Kuhadaa ni kudanganya, Lakini biblia bado haisemi kundi hili litahadaa kila mtu tu, hapana bali inasema, litahadaa watu “wenye roho zisizo imara”.

Hivyo lazima ujiulize roho zisizo imara ni zipi?

Kwa kawaida kitu kisicho imara ni kitu kisichoweza kudumu kwa muda mrefu, kisichoweza kustahimili mazingira ya mtikisiko, au mazingira magumu kwa muda mrefu kwasababu kimeundwa chini ya ubora. Kwamfano, ukinunua kiatu cha ngozi, na mwingine akanunua kile cha plastiki, mkavitembelea wote kwa pamoja, utaona baada ya muda mfupi kile cha plastiki, kinachakaa na kuisha kabisa, lakini kile cha ngozi kinaendelea kudumu, Kwasababu gani? Ni kwasababu kiatu kile cha plastiki sio imara.

Vivyo hivyo katika roho siku hizi za mwisho, Kuna wakristo walio imara, na wengine ambao sio imara, kuna wenye nguvu ya kudumu katika wokovu haijalishi ni mitikisiko mingapi inawakumba kwasababu hapo mwanzo walimaanisha kweli kweli kumfuata Kristo.. Hawa wana heri sana, ibilisi hawezi kuwahadaa.

Lakini kundi lililo hatarini ni hili  ambalo leo linaokoka kwa Bwana, kesho linarudi nyuma, leo ni moto kesho ni vuguvugu, leo linahudhuria mikesha, kesho linasahau, leo linaeleweka, kesho halieleweki, leo lipo ibadani wiki ijayo halifiki kabisa, likiwa na wapendwa linazungumza habari za Mungu, lakini likikaa na watu wa kidunia, linabadilika rangi, linafanana na wao. Lipo hapo katikati, Kudondoka kiwepesi katika dhambi ni jambo la kawaida kwao, ukiliuliza mbona umefanya hivi litakuambia nimepitiwa tu na shetani.

Sasa watu kama hawa ni lazima shetani atawahadaa tu,kwa hila zake, Na watakapodanganywa hawawezi kufahamu kwasababu wao ni roho zisizo imara. Kama Balaamu alipowahadaa wana wa Israeli, kwa kuwashawishi wazini, na mwisho wa siku Mungu akawapiga kule jangwani,  Pale Edeni Hawa alipodanganywa na nyoka hakujua  chochote, kwasababu moyo wake haukuwa imara kwa Mungu.

Ndugu kama na wewe ni mmojawapo tubu dhambi mgeukie Bwana, kisha maanisha kabisa kumfuata Yesu kwa gharama zozote, Kumbuka hizi ni nyakati za mwisho. Watu waliovuguvugu Bwana ameahidi kuwatapika, na wewe angalia usitapikwe. Au kudanganywa na ibilisi. Simama imara kwa Bwana. Kataa ukristo feki, au wa juu juu usioingia gharama.

1Wakorintho 16:13 “Kesheni, simameni imara katika Imani, fanyeni kiume, mkawe hodari”.

1Wathesalonike 3:12 “Bwana na awaongeze na kuwazidisha katika upendo, ninyi kwa ninyi, na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tulivyo kwenu;

13 apate kuifanya imara mioyo yenu iwe bila lawama katika utakatifu mbele za Mungu, Baba yetu, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu pamoja na watakatifu wake wote”.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?

kwanini yule kijana aliitupa ile nguo ya kitani chini na kukimbia uchi?

Ni mlima gani Yule Mwanamke Msamaria aliokuwa anaumaanisha? (Yohana 4:19)

Ni wayahudi wa aina gani wanaotajwa kuwa sinagogi la shetani? (Ufunuo 2:9, Ufunuo 3:9)

Nini maana ya siku moja kwa Bwana ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja? (2Petro 3:8)

Rudi nyumbani

Print this post

Yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.

SWALI: Nini maana ya huu mstari? Hapo anaposema yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.

Mhubiri 10:8

[8]Mwenye kuchimba shimo atatumbukia ndani yake;  Na yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.


JIBU: Mistari hiyo inawazumgumzia watu ambao wanasababisha matatizo kwa wenzao. Au watu wanaowakosesha wengine waliokuwa tayari katika njia sahihi.

Na ndio maana hapo anaanza kwa kusema mwenye kuchimba shimo atatumbukia ndani yake..Akiwa na maana kuwa dhara lile unalolipanga kwa mwingine limpate ndilo hilo hilo litakupata wewe.

Mfano wa watu kama hawa katika biblia ni Hamani, ambaye alikua adui wa Mordekai na wayahudi wote, mpaka akafikia hatua ya kumtengenezea msalaba Mordekai, lakini kinyume chake msalaba ule ndio ukamtundika yeye mwenyewe.

Lakini kwenye hicho kipengele cha pili anasema Na yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.. Maana yake ni kuwa maboma sikuzote hujengwa kwa lengo la kudhibiti maadui, tukiachilia mbali wanadamu, lakini pia wanyama wakali kama fisi, mbweha na nyoka wasivamie mifugo.

Hivyo anaposema abomoaye boma..anamaanisha aondoaye ulinzi wa mwenzake ili maadui kama nyoka wapite, wawadhuru, kinyume chake atadhurika yeye.

Hii ikifunua nini? 

Wapo watu leo hii, wanaoondoa maboma ya watu wengine kwa hila zao. Na maboma yanayomaanishwa hapo si mengine zaidi ya YESU KRISTO. Yeye ndio boma letu, Biblia inasema hivyo..

Zaburi 18:2

[2]BWANA ni jabali langu, na boma langu, na mwokozi wangu,  Mungu wangu, mwamba wangu ninayemkimbilia,  Ngao yangu, na pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu.

Hivyo watu watu wanawakosesha kwa kuwalaghai ili ibilisi awameze, wanawazuia wasimwabudu Mungu sawasawa na mapenzi yake, wanawazuia wasimwombe Mungu wao, ili wapoe..lakini kinyume chake wao ndio watamezwa. Na Bwana atawaponya watu wake.

Mfano wa watu kama hawa,ni  wale maliwali wa Umedi waliompangia visa Danieli, ili asimwombe Mungu wake, kutwa mara tatu. Wakidhani kuwa ndio atapotelea mbali kwenye tundu la simba. Lakini kinyume chake wao ndio walimezwa na ibilisi.

Hivyo kamwe usijaribu kumkosesha mtu wa Mungu, wala usijaribu kumwondolea boma lake (Yesu Kristo), ukadhani ndio tayari atarudi nyuma. Wewe ndio utarudishwa nyuma na shetani.

Tusiwe watu wa kusababisha mabaya/madhara kwa wengine. Ndio kiini cha mistari hiyo.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UBATILI.

Wale Nyoka wa Moto jangwani, walikuwa ni wa namna gani?

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

Mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi nyumbani

Print this post

Kuota unasubiriwa mahali fulani uhutubie, halafu unachelewa.

SWALI: Kuota nasubiriwa mahali Fulani, nihutubie halafu mimi nachelewa, au natingwa na mambo mengine ina maana gani?


JIBU: Ndoto ya namna hii, mara nyingi huwa inaotwa na makundi ya watu ambao wanawajibika katika kuwahudumia wengine, aidha ni viongozi, au wahubiri.

Na huwa zinakuja katika sura tofauti tofauti, wengine wanaota wanasubiriwa kwenye mikutano wahutubie, lakini wanajikuta, wakicheleweshwa na mambo madogo madogo, pengine foleni, au watu, au vishughuli visivyokuwa na msingi. Wengine wanaota wanapaswa wapande madhabahuni wawahubirie wengine, lakini mara wanajiona wapo uchi, wanatafuta suti zao wavae, hawazioni, muda unazidi kwenda, mpaka mwishoni watu wanaondoka, wote na yeye bado hajatokea madhabahuni. N.k.

Hivyo ukiota ndoto ya namna hii tafsiri yake ni kuwa, wewe kama kiongozi kiwango chako cha utayari katika  nafasi hiyo Mungu aliyokuweka bado kipo chini. Na ndio maana unashindwa kufika pale, yapo mambo ambayo yanatia vikwazo kwako. Bwana anasema..

2Timotheo 4:2  “lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho”

Hivyo unachopaswa kufanya ni kuondoa visababu, au hivyo vizuizi vidogo vidogo, mbele yako, ambavyo pengine vinakusababishia uone huo sio wakati ufaao, kwa kumtumikia Mungu, kisha kuwa tayari, kusimama na Bwana kwa ukamilifu wote, kama askari ambaye amevitwa utayari miguuni kwa ajili ya  vita.

Waefeso 6:13  “Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.

14  Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

15  na kufungiwa miguu UTAYARI tupatao kwa Injili ya amani”

Kwa kuzingatia hayo, utakuwa umelitatua hilo tatizo, katika wito wako.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kuota unapigana na mtu.

KUOTA UPO KANISANI.

KUOTA UNALIA/UKIOTA UNALIA KWA UCHUNGU.

KUOTA UMECHOMWA KISU/KUOTA UMEPIGWA RISASI.

MTAWATUPIA MBWA NYAMA HIYO.

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

Kama Malkia Esta alijipamba je! Kuna ubaya gani wanawake wa wakikristo wa leo kujipamba?.

Rudi nyumbani

Print this post

TAFUTA KWA BIDII KUWA MTAKATIFU.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu.

Neno la Mungu linasema…

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”

Andiko hilo ni muunganiko wa maneno mawili, Neno la kwanza ni “TUTAFUTE KWA BIDII KUWA NA AMANI NA WATU WOTE”, na neno la pili, ni “TUTAFUTE KWA BIDII KUWA WATAKATIFU”.

Ni sawa na mtu aseme “katafute shati na kiatu chumbani”…tukiichambua sentensi hiyo tunapata maneno mawili, 1) Tukatafute shati na pia 2) Tukatafute kiatu.

Vivyo hivyo hapo biblia iliposema “Tutafute kwa bidii kuwa na amani na watu wote” na “huo utakatifu”..imemaanisha “tutafute amani” na pia “tuutafute kwa bidii utakatifu”.

Ikimaanisha kuwa utakatifu, ni wa kutafutwa, Tena kwa bidii sanaa!!..

Na ni kwanini tumeambiwa tuutafute kwa bidii???…Ni kwasababu hapana mtu atakayemwona Mungu asipokuwa nao.

Unaweza usiwe na Imani kama ile ya Eliya lakini bado ukamwona Mungu, unaweza usiwe mhubiri wa madhabahu  lakini bado ukamwona Mungu.(Kwa kumtumikia Mungu kwa njia nyingine).

Lakini ukikosekana utakatifu, kumwona Mungu haiwezekani.

Na utakatifu maana yake ni kukaa mbali na kila aina ya dhambi.

Mtume Paulo kwa ufunuo wa Roho alizidi kilisisitiza hilo katika kitabu cha Wagalatia 5:19-20.

Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,

20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, KATIKA HAYO NAWAAMBIA MAPEMA, KAMA NILIVYOKWISHA KUWAAMBIA, YA KWAMBA WATU WATENDAO MAMBO YA JINSI HIYO HAWATAURITHI UFALME WA MUNGU”.

Hapa mwisho anamalizia kwa kusema “watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”. Hii inaogopesha sana..

Sasa Utakatifu, tunautafutaje?..

  1. KWA KUZISHINDA TAMAA ZETU.

Dhambi yoyote kabla haijaleta madhara huwa inaanza kama mbegu ndogo..biblia inasema chanzo cha dhambi ni tamaa.

Yakobo 1:14 “Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.

15 Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti”.

Unapokuwa na uwezo wa kuzitawala tamaa zako, basi dhambi kwako itakuwa mbali, na hivyo siku zote utajiweka katika hali ya utakatifu..lakini kila kitu kinachokuja mbele yako wewe unakitamani, kila mtindo wa uvaaji, ulaji au mtindo wa kimaisha unaokuja mbele zako unautamani, basi fahamu kuwa upo hatarini kuupoteza ukamilifu wako.

2. KWA KUKAA MBALI NA VICHOCHEO VYOTE VYA DHAMBI.

Dhambi inayo vichocheo, kama vile hasira ilivyo na vichocheo, kwa mfano vichocheo vya dhambi ya uasherati ni utazamaji wa pornography, mazungumzo mabaya na ya mizaha, makundi mabaya ya watu, uvaaji mbaya, filamu za kidunia ambazo asilimia kubwa maudhui zake ni kuchochea tamaa ya zinaa, vile vile magroup na kurasa mbalimbali katika mitandao ya kijamii kama vile facebook, whatsapp, instagram na mengineyo.

Mtu anayekesha muda wote kwenye facebook au kwenye mitandao mingine ya kijamii, mtu huyo kamwe asitegemee atakuwa salama..

Biblia inasema “Tutafute kwa bidii!!”…Sio kwa ulegevu..Maana yake “ukamilifu” hatuwezi kuupata tukiwa walegevu.

3. KWA KUOMBA NA KUJIFUNZA NENO.

Tunapokuwa waombaji, katika ulimwengu wa roho shetani na mapepo yake yananakaa mbali nasi..Hivyo na viwango vyetu vya utakatifu vinapanda..Vile vile tunapokuwa watu wa kujifunza Neno la Mungu, tunakuwa tunatakasika kwasababu Neno la Mungu lina maonyo ndani yake, na linatufunza na kutukumbusha kudumu katika Imani na utakatifu. Dalili ya kwanza ya mtu anayerudi nyuma kiimani, ni kupungukiwa na nguvu ya kujifunza Neno. Hivyo ili na sisi viwango vyetu vya utakatifu vipande hatuna budi tuwe wasomaji wa Neno la Mungu (yaani biblia) .

Bwana atusaidie, tuupate utakatifu!

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TAFUTA MSAMAHA HALISI, NA SI MSAMAHA TU!

UTAKASO NI SEHEMU YA MAISHA YA MKRISTO YA KILA SIKU.

MAPENZI YA MUNGU NI YAPI?

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Kwanini Eliya alijulikana kama “Eliya Mtishbi”?

Rudi nyumbani

Print this post

KUMJUA YESU SI KUPATA UZIMA WA MILELE.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana libarikiwe… Karibu tuyatafakari maandiko pamoja.

Katika dunia hii ya siku za mwisho, ni watu wengi sana wanaomjua Yesu, na maisha yake yote, jinsi alivyokuwa kwamba alizaliwa wapi, mama yake katika mwili alikuwa ni nani, baba yake alikuwa ni nani, wanafunzi wake walikuwa ni wangapi, na sasahivi yupo wapi, na kwamba atarudi tena.. n.k N.k. Ni watu wengi sana wanamjua Bwana Yesu wanaamini kuwa katoka kwa Mungu. Ndio maana leo hii ukimwuliza mtu kama anamjua Bwana Yesu, atakuambia Ndio, ukizidi kumwuliza kama anamwamini Bwana Yesu atakuambia tena Ndio!. Ni wachache sana wanaosema kuwa hawamjua kabisa wala hawamwamini. Hiyo ndio hali ya siku hizi za mwisho.

Lakini leo napenda nikuambie au nikukumbushe kuwa “kumjua tu Yesu  peke yake, hakukufanyi wewe kuupata uzima wa milele”. Tusome maandiko yafuatayo..

Yohana 3:2 “Huyo alimjia usiku, akamwambia, Rabi, twajua ya kuwa u mwalimu, umetoka kwa Mungu; kwa maana hakuna mtu awezaye kuzifanya ishara hizi uzifanyazo wewe, isipokuwa Mungu yu pamoja naye.

3 Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu”.

Umeona?..Nikodemo pamoja na wenzake walimjua Yesu, na waliamini kuwa katoka kwa Mungu.. na hata wanakwenda mbele zake kumwambia Imani yao hiyo kwake. Lakini tunaona jibu la Bwana Yesu lilikuwa ni tofauti..

Kikawaida nilitegemea kuwa Bwana Yesu angemsifia Nikodemo na kumwambia “heri wewe Nikodemo kwa kuyajua hayo”.. lakini kinyume chake Bwana anamjibu Nikodemu na kumwambia…”Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu”.

Akiwa na maana kuwa haijalishi mtu amfahamu kiasi gani, au amwamini kiasi gani, kama mtu huyo hatazaliwa mara ya pili, imani yake hiyo ni bure..

Haijalishi Nikodemo na wenzake wanamjua Yesu kwa viwango gani, au wanamwamini kwa viwango gani, kama hawatakubali kuzaliwa mara ya pili, hawataurithi uzima wa milele.

Sasa swali linakuja katika vichwa vyetu, Nini maana ya kuzaliwa mara ya pili?

Swali hili hata Nikodeo alimwuliza Bwana, na Bwana Yesu alitoa maana yake, katika mistari inayofuata…

Yohana 3:4 “Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?

5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, MTU ASIPOZALIWA KWA MAJI NA KWA ROHO, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu”.

Umeona hapo?.. Kumbe tafsiri ya kuzaliwa mara ya pili, ni KUZALIWA KWA MAJI na KWA ROHO.

Sasa swali lingine, tunazaliwaje kwa Maji, na kwa Roho.

Tunazaliwa kwa Maji kwa njia ya Ubatizo, pale tunapobatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa Jina la Yesu Kristo, sawasawa na Matendo 2:38, hapo ndipo tunapozaliwa kwa Maji.  Watu wengi sana wanaupuuzia Ubatizo, na kusema si wa lazima!.. na kusema ukishaamini inatosha, si lazima ubatizwe.. Kumbuka hapo!, hata Nikodemo alimwamini Bwana Yesu, na alijua ndio kashakamilika, lakini Bwana Yesu anamwambia..Usipozaliwa kwa Maji, huna uzima.. Vivyo hivyo, na mtu yeyote ambaye hatabatizwa katika ubatizo sahihi, baada ya kuujua ukweli hana Uzima wa milele, hiyo ni kulingana na mananeo ya Bwana YESU.

Na tunazaliwaje pia kwa Roho?.

Tunazaliwa kwa Roho, kwa njia ya Ubatizo wa Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu ndio muhuri wa Mungu katika maisha yetu..

Waefeso 4:30 “Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye  MLITIWA MUHURI HATA SIKU YA UKOMBOZI”.

Kwahiyo mtu yeyote atakayemkataa Roho Mtakatifu, baada ya kuamini, huyo sio wa Mungu, haijalishi anamjua Bwana Yesu kwa kiwango gani!.

Warumi 8:9 “..Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake”.

Hivyo mtu anapobatizwa sahihi na kupokea Roho Mtakatifu wa kweli, hapo anakuwa kazaliwa mara ya pili, anakuwa ni kiumbe kipya, lakini si kilichokomaa bali ni kichanga, kilichozaliwa katika dunia mpya kisichojua chochote!.

Kwahiyo baada ya kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu, sio mwisho wa safari, bali ndio mwanzo wa safari, kama vile mtoto aliyezaliwa anavyopitia hatua za kukua mpaka kufikia utu uzima na kukomaa, vivyo hivyo na mtu aliyezaliwa mara ya pili, ni lazima apitia hatua za kukaa chini, kuukulia wokovu, kwa bidii zote, ili awe imara.. Lakini akiacha kuukulia wokovu, basi mtu huyo atakufa kiroho, na kazi yake itakuwa ni bure.Lakini zipo faida nyingi sana za kuzaliwa mara ya pili..Ni nyingi sana, hata katika maisha ya hapa hapa duniani, lakini faida iliyo kubwa kuliko zote ni hiyo Bwana Yesu aliyoitaja kwamba UTAUINGIA UFALME WA MUNGU.

Je umezaliwa mara ya pili?

Kama bado unangoja nini baada ya kuyajua haya yote?.. Tafuta ubatizo sahihi…wa maji mengi na kwa Jina la Bwana Yesu, na Ujazo wa Roho Mtakatifu.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

NUNUA MAJI YA UZIMA.

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

ILI TUONEKANE SAFI MBELE ZA MUNGU TUFANYE NINI?

Rudi nyumbani

Print this post