Title September 2022

Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?

Wajibu wa wanandoa ni upi?

Mume: Kumpenda mke wake Kama mwili wake mwenyewe, ( Waefeso 5:25):  Ikiwemo kumuhudumia kiafya, kimavazi, kimalazi, na kiroho.

Mke: Kumtii Mume wake: Kumsikiliza, kumuheshimu, kukubali kuongozwa. (Waefeso 5:22).

Wote: Haki ya ndoa. (1Wakorintho 7:5)

Lakini ikitokea mmoja, ameshindwa kusimama katika nafasi yake, labda tuseme, mume hamjali mkewe, anampiga, anatoka nje ya ndoa, anamtukana, hamtimizii majukumu yake ya kimwili na watoto wake. Afanyaje?

Au mke hamweshimu mume wake, anamdharau, anafanya ukahaba, anamzungumzia vibaya kwa watu wa nje, anajiamulia mambo yake mwenyewe pasipo kumshirikisha mumewe..afanyaje?

Je! na yeye aache kutimiza wajibu wake?

Jibu ni hapana:  Embu wazia hili jambo; Ulishawahi kuishi katika nyumba ya kupanga, ambapo mnajikuta wapangaji mpo 10 mnashea umeme au maji, na kila mwisho wa mwezi bili inakuja, na mnapaswa muigawanye sawa sawa kwa kila mmoja wenu.  Kwa kawaida hapo panakuwa na ukinzani mkubwa, kwasababu wapo wengine watasema, mimi sina matumizi mengi kama ya Yule.. Na hiyo inapelekea mwingine kujiongezea  matumizi yake kwa makusudi ilimradi tu afanane na wale wengine, labda atufungulia bomba la maji ili yamwagike, ili mwisho wa mwezi utakapofika alipe sawasawa na matumizi ya wale wengine.

Lakini hajui kuwa anajiumiza yeye mwenyewe na wale wenzake, kwasababu anapoongeza matumizi ndipo gharama inapokuja juu zaidi, atalipa zaidi ya mwanzo. Ni heri angebakia vilevile akubali kuumia yeye, ili wote wapone.

Ndivyo ilivyo katika ndoa ikiwa mmoja hatimizi wajibu wake wa kindoa, suluhisho sio mwingine kujibu mapigo, bali ni kuendelea hivyo hivyo katika nafasi yake.  Ili kuinusuru ndoa. Kama mwanaume hakupendi, wewe mtii, mweshimu, msikilize, kama mwanamke hakutii, wewe mpende, mpe haki yake, ..

Na faida yake ni ipi?

  1. 1) Utamgeuza mwenzako:

Biblia inasema; .. 1Petro 3:1 “Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno; 2 wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu”.

Inaendelea kusema;

1Wakorintho 7:16 “Kwa maana wajuaje, wewe mwanamke, kama utamwokoa mumeo? Au wajuaje, wewe mwanamume, kama utamwokoa mkeo?

 Haijalishi itachukua miaka mingapi. Kuwa mvumilivu, timizia wajibu kwao. Hayo mengine mwachie Mungu.

  • ) Utampalia makaa ya moto kichwani:

Mithali 25:21 “Adui yako akiwa ana njaa, mpe chakula; Tena akiwa ana kiu, mpe maji ya kunywa; 22 Maana utatia makaa ya moto kichwani pake; Na Bwana atakupa thawabu.

Hili andiko linaingia pia kwa wanandoa. Wakati unaona kama wewe unaonewa, hujui kuwa Yule mwingine anateswa rohoni  anapoona hurudishi mapigo, hilo jambo linakuwa ni moto mkubwa ndani yake, na sikumoja tu, atakuja kwa machozi, na kutubu mbele zako. Ni kitendo cha muda.

  • 3) Utampa Mungu nafasi ya kulipiza kisasi yeye mwenyewe:

Unapoumizwa, usidhani kuwa Mungu haoni, lakini unapomwachia Mungu yote, basi yeye peke yake ndiye atakayeshughulika kutafuta njia ya kutatua hilo tatizo. Kiboko cha Mungu kitapita, kitamnyoosha. Hivyo unapaswa uwe mtulivu, simama katika nafasi yako. Bwana atamtengeneza yeye mweyewe.. au atatengeneza njia kwa namna nyingine. Hivyo dumu katika utakatifu.

Warumi 12:17 “Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote.

18 Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.

19 Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana”.

Zingatia hayo, usirejeshe ubaya kwa mwanandoa mwanzako.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI, AU KUTOA TALAKA?

MJUE SANA YESU KRISTO.

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

NDOA NA HARUSI TAKATIFU.

VIJANA NA MAHUSIANO.

Kwanini Bwana Yesu alie machozi, na ilihali yeye ni Mungu?

Rudi nyumbani

Print this post

FAMILIA TAKATIFU: Marimu na Yusufu.

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WANA-NDOA; FAMILIA TAKATIFU: Marimu na Yusufu.


Karibu katika mwendelezo ya  Masomo ya wanandoa . Ikiwa wewe ni mwanandoa au unajiandaa kuingia katika ndoa, basi masomo haya ni muhimu sana kwako kuyajua.

Tulishatazama, huko nyuma jinsi ndoa ya kwanza ya wazazi wetu Adamu na Hawa ilivyokuwa, na changamoto walizokutana nazo, na jinsi walivyoweza kukabiliana nazo. Ikiwa hukupata masomo hayo, basi utatumia ujumbe inbox tukutumie.

Leo tutatazama familia nyingine takatifu. Ambayo ni ya Yusufu na Mariamu. Yapo mambo mengi sana ya kujifunza, juu ya wanandoa hawa, Na ndio maana kwanini Mungu alikusudia  mwokozi wa ulimwengu aje kwa kupitia watu hawa,  Ni Kwasababu kuna  mengi ya kujifunza kwao.  Tutaona pia utaratibu Mungu aliowawekea katika kutimiza kusudi lake hapa duniani.

1) Tukianzana na Yusufu.

Alikuwa ni mtu aliyeepuka madhara kwa wengine:  Yusufu hakuwa kama Samsoni, ambaye alipoona mwanamke aliyemchumbia amepewa rafiki yake, akakasirika, na kwenda kuchukua mbweha mia tatu, na kuwapeleka kwenye shamba la ngano la wafilisti, kuyateketeza ili ajilipizie kisasi (Waamuzi 15:1-20).

Lakini Yusufu hakuwa hivyo, yeye alipoona binti aliyemchumbua ana mimba, alitafuta njia ya kuepusha madhara kwa dada huyo, hivyo akakusudia ‘’kutomuabisha’’. Akapanga mipango yake ya kumuacha kwa siri,..huenda alipoulizwa vipi mbona humwoi msichana huyu, akawa anasema bado sijafikia muafaka, nitawapa majibu.

Mathayo 1:18 “Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi. Mariamu mama yake alipokuwa ameposwa na Yusufu, kabla hawajakaribiana, alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

19 Naye Yusufu, mumewe, kwa vile alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri”.

Sasa Ikiwa alikuwa na hofu ya kumwaibisha asipigwe mawe, unatazamia vipi mtu kama huyu, angeweza kumpiga mke wake hata baada ya ndoa , au awe anatoa siri za madhaifu ya mke wake kwa watu wa nje?

Mwanamke anapoteleza, sio lazima wakati wote upeleke taarifa kwa jamii, aaibike au umpige, au umfukuze, bali ni kumvumilia, kwasababu mengine yanatokea kwa sababu ambazo utakuja kuzijua mbeleni. Tabia hii alikuwa nayo Baba-wa-Yesu (kimwili)

2) Mariamu:

Alikuwa ni bikira:  Ni binti ambaye alijitunza tangu anazaliwa mpaka anakuwa mwanamke, Na hiyo ikapelekea kupata neema ya kuchumbiwa na mzao wa Daudi (Yusufu). Kumbuka ahadi ya kuzaliwa Kristo haikuwa kwa Mariamu, bali ilikuwa kwa uzao wa Daudi. Hivyo Mungu alipomuona Mariamu, na ukamilifu wake katika mwili ndipo akasema huyu anafaa kupata neema ya kukutana na Yusufu atimize kusudi la Mungu.

Maana yake ni nini, upo umuhimu sana, wa msichana kujitunza sana mwili wake, kwani hiyo itakupelekea kupata mwanaume bora, na uzao bora. Ni kweli si wote wataingia katika ndoa wakiwa bikira, lakini ikiwa umetambua sasa, wajibu wako, na umeokoka, huna budi kujitunza sana, na hata baada ya ndoa, ili hicho kitakachotoka tumboni mwako kiwe kitakatifu.

SASA BAADA YA KUONA SIFA HIZI KUU (2), WALIZOKUWA NAZO HAWA WANANDOA, TUONE UTARATIBU WA KIMAJUKUMU JINSI MUNGU ALIVYOUGAWANYA KWAO.

Malaika Gabrieli alitumwa kwa Mariamu, ili kumpa taarifa ya kupata mimba kwa uweza wa Roho na kwamba mtoto huyo ataitwa Yesu.

Lakini baada ya hapo, Mungu hakuendelea tena kusema na Mariamu moja kwa moja. Bali alimgeukia mumewe Yusufu, na kumwagiza kuwa atakapozaliwa amwite  jina lake YESU.

Mathayo 1:20 “Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

21 Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao”.

Na utaona baada hapo, wakiwa kule Bethelehemu, bado Malaika anamtokea Yusufu tu, na kumwambia, mchukue mtoto na mama yake, wapeleke Misri, kwasababu Herode anataka kumuua mtoto.(Mathayo 2:13-14)

Tengeneza picha Mariamu angekuwa ni mwanamke kiburi, angesema, mbona Mungu hajasema na mimi kuhusiana na hilo?, Kwanza si wewe uliyembeba masihi, mateso huyajui, huko Misri ni nani unayemjua, nangojea Mungu anithibitishie kwanza mimi..lakini hakuwa hivyo alikubali kutii, bila kujadili jadili.

Bado utaona, akiwa kule Misri, malaika anamtokea tena Yusufu peke yake na kumwambia, mchukue mke na mtoto urudi nao Israeli kwasababu Herode amekufa. Safari tena ya mihangaiko ikaanza, huku Mariamu akisikiliza maagizo ya mumewe na kutii (Mathayo 2:19-20).. Lakini wakiwa pale Bethelehemu,  wametulia ili sasa waanze maisha, saa hiyo hiyo, Yusufu anamwambia mke wake, tuondoke hapa tuende tena Nazareti, Mungu ameniagiza hivyo (Mathayo 2:22-23).

Mariamu hakuwa na kigugumizi kumsikiliza mume wake, hakuwa na kazi nyingine yoyote zaidi  ya kupokea maagizo ya uongozi kuhusu familia au mtoto kutoka kwa mumewe.

Hii ni kufundisha nini?

Kwa mwanamke: Tambua kuwa mume ndio kichwa cha familia, Mungu atamtumia yeye, kuyalinda na kuyatamia maono yako, huwezi kufanikiwa bila yeye. Haijalishi Mungu kakuonyesha mambo makubwa kiasi gani hapo mwanzoni. Ikiwa humtii mume wako, ujue kuwa unajiharibia wewe mwenyewe. Utiifu ni muhimu sana, hata wakati ambapo unaona sehemu unapopelekwa sio pa kuvutia.

Ndio maana unawajibu sana wa kumwombea mume wako, ikiwa ni mwenye dhambi, Mungu ambadilishe. Kwasababu yeye ndio usalama wa maono yako.

Kwa mwanaume: Umewekwa kama kichwa, ni lazima utambue kulinda maono mema ya mkeo, Si kila taarifa nzuri itakufikia wewe wa kwanza, Wakati mwingine inaanzia kwa mwanamke, kama ilivyokuwa kwa Mariamu, kisha wewe baadaye, hivyo uonapo hivyo, usipige vita, bali, sikiliza, tafakari, pia tendea kazi, Hapo ndipo Mungu atakapokutumia, kuijenga familia bora. Wewe kama mlinzi huna budi, kutimiza wajibu wako,wa kumtunza mkeo na kumpenda kama maandiko yanavyosema. Jambo lolote linaloihatarisha familia yako, shughulika nalo kwelikweli usimwachie mwanamke alitende.

Hivyo kwa kuzingatia mambo hayo,  Ndoa zetu zitakuwa bora, mfano wa ile ya Yusufu na Marimu. Na Bwana atatupa zawadi ya kuzaa vitakatifu kama Ilivyokuwa kwa Yesu na wadogo zake wote. Tambua wajibu wako, simama katika nafasi yako.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

WANA-NDOA: Baba Mkwe, Na mama Mkwe.

ONDOA TAKATAKA KATIKA FEDHA, NA CHOMBO KITATOKEA KWA MTAKASAJI.

KUWA RAFIKI WA DUNIA NI KUWA ADUI WA MUNGU.

VIJANA NA MAHUSIANO.

USIOGOPE KUMWADHIBU MWANAO.

Rudi nyumbani

Print this post

Wahuni ni watu gani katika biblia?

Jibu: Kibiblia “Mhuni” ni mtu anayefanya mambo yaliyo kinyume na maadili. Kwamfano mtu anayetanga kuzaa nje na ndoa, huyo kibiblia ni mhuni.

Katika biblia neno Mhuni/wahuni limeonekana mara moja tu! Katika kitabu cha Ayubu 30:8.

Ayubu 30:8 “Wao ni wana wa wapumbavu, naam, WATOTO WA WAHUNI; Walifukuzwa kwa mijeledi watoke katika nchi”

Na mambo mengine yote ambayo mtu anaweza kuyafanya kinyume na maadili, mfano uvaaji mbaya, uongeaji mbaya, utafutaji mbaya n.k mambo hayo ni mambo ya  kihuni, na hivyo anayeyafanya ni mhuni.

Na Wahuni wote hawatairithi Nchi, watafukuzwa watoke katika nchi..kulingana na hilo andiko.

Mathayo 5:5 “Heri wenye upole; Maana hao watairithi nchi”.

Jihadhari na uhuni, kama wewe ni binti uvaaji wa nguo fupi ni uhuni!, uvaaji wa vimini ni uhuni,  uvaaji wa suruali ni uhuni (biblia inasema mwanamke asivae mavazi yampasayo mwanaume na mwanaume asivae mavazi yampasayo mwanamke), kuvaa nguo unayoonyesha mapaja, au mgongo ni uhuni, kunyoa kijogoo kwa mwanaume ni uhuni, kuvaa nguo za mlegezo ni uhuni, kuvaa nguo za kubana ni uhuni n.k

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mshahara wa Mbwa ni upi? Kama tunavyousoma katika Kumbukumbu 23:18

Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.

MUNGU ATAKUUA UKIWA MBAYA MACHONI PAKE.

Nini maana ya “wanawake saba watamshika mtu mume mmoja”

MAPENZI YA MUNGU NI YAPI?

Rudi nyumbani

Print this post

HAMA KUTOKA GIZANI

Je unajua ni kwanini watu watahukumiwa?

Hebu tusome maandiko yafuatayo..

Yohana 3:19 “Na hii ndiyo hukumu; ya kuwa NURU IMEKUJA ULIMWENGUNI, NA WATU WAKAPENDA GIZA KULIKO NURU; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu”.

Umeona sababu ya hukumu ya Mungu juu ya watu siku ile?.. Ni kwasababu watu walipenda GIZA kuliko NURU.

Nataka tulitafakari hilo neno “wakapenda” na hilo neno “kuliko”. Unajua mtu akikipenda kitu kuliko kingine, maana yake amekichunguza, akakitafakari na mwisho akachukua uamuzi wa kukichagua hiko kitu.

Na ndivyo Neno la Mungu linavyosema, kuwa hukumu yake itakuja juu ya watu, kwasababu “WATU WALIPENDA GIZA KULIKO NURU”. Ni heri kama Nuru isingekuwepo, halafu watu walipende giza!… lakini hapa inamaanisha Nuru ilikuwepo halafu watu wakalipenda giza kuliko Nuru… hilo ni jambo baya sana..

Hebu tafakari mpo ndani ya chumba chenye giza, halafu taa inawashwa na kumulika nyumba nzima, halafu ghafla unaanza kuona watu wanatoka kwenye hicho chumba chenye nuru, wanaelekea gizani, na zaidi ya yote hawataki kuja kwenye nuru!.. bila shaka utashangaa sana…

Ndicho Bwana Yesu alichomaanisha hapa kuwa watu kwa mapenzi yao wenyewe, wamechagua giza kuliko Nuru, ijapokuwa Nuru wameiona!..

Watu walipenda anasa kuliko kumcha Mungu, watu walipenda uchafu kuliko usafi, ijapokuwa tayari Nuru ilikuwepo (Roho Mtakatifu wa kuwatakasa alikuwepo, lakini hawakumtaka)…Watu walipenda ulevi, uzinzi, uuaji, ulafi, ufiraji, utukanaji, tamaa mbaya kuliko UTAKATIFU. Kwasababu hiyo basi hawatakuwa na udhuru siku ile (kulingana na Neno hilo).

Na ni kwasababu gani watu wanalipenda giza kuliko Nuru?, ni kwasababu matendo ya giza siku zote ni ya aibu, na yasiyokubalika na huwa hayapatani na mwanga.. Wezi wanaiba usiku, wachawi wanafanya shughuli zao usiku, walevi wanalewa usiku, hali kadhalika wazinzi, na makahaba wanafanya kazi zao katika giza…

Ayubu 24:15 “Tena jicho lake mzinifu hungojea WAKATI WA GIZA-GIZA, Akisema, Hapana jicho litakaloniona; Naye huuficha uso wake.

16 Wao hutoboa nyumba gizani; Hujifungia ndani wakati wa mchana; Hawaujui mwanga”.

Umeona tabia za wazinifu na watu wafanyao mabaya?..huwa zinasubiria kagiza kaingie!!..hawawezi kufanya shughuli zao mbele za watu!.

Yohana 3:20 “Maana kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru, wala haji kwenye nuru, matendo yake yasije yakakemewa.

21 Bali yeye aitendaye kweli huja kwenye nuru, ili matendo yake yaonekane wazi ya kuwa yametendwa katika Mungu.”

Je! Na wewe umependa nini?,, umechagua nini?, NURU AU GIZA!, kwa matendo yako utatambulika umechagua nini, kamwe usimsingizie shetani!, kwasababu hapo Bwana hajasema “shetani akawachagulia kupenda giza” bali anasema “watu wakachagua wenyewe kupenda giza kuliko Nuru”. Kwahiyo ni watu wenyewe ndio wamechagua matendo ya giza, baada ya kukubali mapendekezo ya shetani.

Je! Na wewe umechagua nini leo?..kumbuka kama unafanya matendo ya giza, na huku unamjua Yesu…fahamu kuwa upo gizani, na umechagua giza kwa hiari yako mwenyewe, na upo hatarini kuangukia katika hukumu ya Mungu siku ile,.. Kwasababu Nuru ipo ulimwenguni na hujataka kuifuata, na Nuru hiyo si nyingine zaidi ya Yesu Kristo.

Yohana 9:5 “Muda nilipo ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu”.

Amua leo kutoka katika hilo giza la ulimwengu, na kuja Nuruni.. na Unaingia Nuruni kwa kumwamini Bwana Yesu, na kupokea Roho Mtakatifu ambaye atakutakasa na matendo yote ya giza, na kwa kufanya hivyo utakuwa umetoka gizani na kuingia uzimani, na hivyo utakuwa ni mwana wa Nuru.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Hazina za gizani ni zipi? (Isaya 45:3).

MKUU WA ANGA.

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

Je ni kweli imani ya mtu ndiyo itakayomuokoa, na si kitu kingine?

Nuru yetu inapaswa iangaze au isiangaze kulingana na Mathayo 5:16 na Mathayo 6:1?

Rudi nyumbani

Print this post

Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake

SWALI: Biblia inaposema “Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake”, ina maana gani?

Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.


JIBU: Ili kuelewa neno hilo, wazia mfano huu; Mtu mmoja ameshitakiwa na mahakama kwa kosa la uchafuzi wa mazingira, hivyo, akapewa adhabu ya kulipa faini ya sh. Milioni 5 ndani ya wiki 3, au jela miaka 3. Sasa ikatokea mtu huyu akawa hana cha kulipa,.. Unadhani atakuwa katika hali gani? Ni wazi kuwa atapoteza amani yote, hawezi kuwa katika furaha, hawezi kuwa katika raha wakati wote huo kwasababu anajua hukumu ya kifungo ipo mbele.. Ili amani yake irudi, hana budi apate kiwango hicho alipe. Lakini akatokea mtu, akasema mimi nitakuchukua adhabu hiyo nitamlipia deni lake. Bila shaka furaha na amani ya yule mdaiwa itarejea tena.

Hivyo tunaweza kusema, ili kuirejesha ile amani yake ya mwanzo, alikuwa hana budi kutumikia adhabu kwanza..

Sasa tukirudi katika huo mstari ..biblia inaposema;

Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.

Huyo ni Bwana Yesu anayezungumziwa hapo, sasa anaposema, Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”. Ni kwamba ili sisi kuipokea Amani yetu, tuliyoipoteza tangu kule edeni, ilitupasa kwanza tutumikie adhabu ya makosa.. Lakini ashukuruwe Kristo kwasababu alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, akapigwa na kuteswa ili sisi tupone. Adhabu ya amani yetu aliichukua yeye.

Na ndio maana Warumi 8:1 inasema; “Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu”.

Ukiwa ndani yake, amani yako inarejeshwa bila kulipa gharama yoyote. Lakini inastaajabisha kuona bado wapo watu hawataki kulipiwa deni zao. Wakidhani kuwa wataweza kustahimili hukumu ya Mungu siku ile. Ndugu ikiwa upo nje ya Kristo huna tumaini lolote. Ukifa ni moja kwa moja jehanamu kwenye ziwa la moto. Adhabu yako ni Mauti katika lile ziwa la moto milele.

Hiyo ndio sababu kwanini unamuhitaji Yesu Kristo leo, kwasababu ukishakufa leo hakuna tumaini, wala huna matendo yoyote ya kumshawishi Mungu, afute dhambi zako. Wasubiri nini, usimgeukie Bwana Yesu akusafishe Maisha yako angali ukiwa hai? Tubu sasa mpokee yeye. Muda ni mchache.

Maran Atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KAMA SI YESU, HABARI YETU INGEKUWA IMEISHA ZAMANI SANA.

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

Je Mungu ana njia ngapi za kuzungumza?

Sadaka ya Amani ilikuwaje?

Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?

Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote.

Rudi nyumbani

Print this post

Nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.

SWALI: Naomba kufahamu maudhui ya mstari huu,

1Timotheo 1:20 “Katika hao wamo Himenayo na Iskanda, ambao nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu”.


JIBU: Awali ya yote, kabla ya kufahamu ni kwanini Mtume Paulo anatoa hukumu kali kama hiyo tuangalie mistari ya juu yake ambayo inaeleza sifa, za hao watu.

Ukisoma mstari wa 19, Paulo anamuasa Timotheo, awe ni mtu mwenye Imani, lakini sio Imani tu, bali pia “dhamiri njema”.. Ni vitu vinavyokwenda sambamba.

1Timotheo 1:19 “uwe mwenye imani na dhamiri njema, ambayo wengine wameisukumia mbali, wakaangamia kwa habari ya Imani.

20 Katika hao wamo Himenayo na Iskanda, ambao nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.”

Dhamiri ni kile kitu cha ndani kinachomshuhudia mtu kwamba anachokifanya ni sahihi au sio sahihi. Hivyo pale mtu anapokuwa na dhamiri njema, maana yake ni kuwa, anaitii nafsi yake, inapofanya kosa, pale inaposuta, anakuwa tayari kugeuka. Hivyo mtu kama huyu huwa anaishi kwa kujichunga, na kuwahurumia na kwa kuogopa hukumu pale anapojaribu kuwapotosha watu.. Kwasababu dhamiri yake njema inamshitaki.

Lakini mtu ambaye hana dhamiri njema, ni kwamba, hata anapoona jambo Fulani alifanyalo ni baya, anastahili hukumu, yeye hajali, bali anafanya atakalo, kwa maslahi yake. Atakuwa tayari kuwafundisha watu mafundisho potofu kwa makusudi kabisa akijua kabisa alifanyalo ni upotevu, lakini yeye ataendelea kufanya, kwa furaha kabisa..

Sasa ndio hapo mtume Paulo, anawatolea mfano watu hao, waliokosa dhamiri njema. Ambao ni Himenayo, na Iskanda. Watu hawa walikuwa ni wabaya, kwasababu walikuwa wanapindua Imani za watu kwa makusudi, wala sio kwa bahati mbaya wakiwafundisha kinyume na mafundisho ya mitume,.

Kwamfano huyu Himenayo, tunasoma tena, Paulo akieleza mafundisho yake potofu, ya kuwaambia watu Ufufuo wa wafu tayari umeshatokea.. Hivyo watu wengi wakaiacha Imani na kumgeukia yeye.

2Timotheo 2:16 “Jiepushe na maneno yasiyo na maana, ambayo si ya dini; kwa kuwa wataendelea zaidi katika maovu,

17 na neno lao litaenea kama donda-ndugu. Miongoni mwa hao wamo Himenayo na Fileto,

18 walioikosa ile kweli, wakisema ya kwamba kiyama imekwisha kuwapo, hata kuipindua imani ya watu kadha wa kadha”.

Na mwezake Iskanda, ambaye wengi wanaamini ndio huyu aliyezungumziwa katika vifungu hivi; Ambaye alimpinga sana Paulo katika kazi zake za kihuduma.

2Timotheo 4:14 “Iskanda, mfua shaba, alionyesha ubaya mwingi kwangu; Bwana atamlipa sawasawa na matendo yake.

15 Nawe ujihadhari na huyo, kwa sababu aliyapinga sana maneno yetu”.

Hivyo, makundi haya, Mtume Paulo hakushughulika nayo kabisa, bali kwa mamlaka aliyopewa, aliwaacha mikoni mwa shetani, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.  Maana yake ni kuwa, ulinzi wa Mungu uliondolewa juu yao, ili shetani apate nafasi ya kuwashughulikia, ili yamkini watubu.

Aidha walikumbwa na magonjwa, au mapigo, au hata vifo hatujui.. Lakini kuwekwa mikoni mwa shetani, adhabu kali kama hizo utakumbana nazo.(Tunaona kwa ayubu pale  alivyoondolewa wigo wa ulinzi na Mungu, jinsi majangwa makali yalivyompata)..Ndivyo ilivyokuwa kwa hawa wakina Himenayo na mwenzake.

Hii ni kutufundisha  nini?

Yapo mamlaka ambayo Watakatifu wamepewa, kwa watu ambao wanauchezea ukristo, Ikiwa unafanya dhambi kwa makusudi, angali unaujua ukweli, na upo ndani ya mwili wa Kristo, kuwa makini sana, kwasababu hukumu yoyote itakayotolewa juu yako na wao lazima ikupate.. Na kama utakuwa unafanya kwa siri, kanisa halitajua, lakini Mungu atajua.. Na yeye mwenyewe atakuweka mikononi mwa ibilisi, upigwe. Ukishafikia hatua hii, waweza hata poteza Maisha yako.

Soma;

1Wakorintho 5:1 “Yakini habari imeenea ya kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika Mataifa, kwamba mtu awe na mke wa babaye.

2 Nanyi mwajivuna, wala hamkusikitika, ili kwamba aondolewe miongoni mwenu huyo aliyetenda jambo hilo.

3 Kwa maana kweli, nisipokuwapo kwa mwili, lakini nikiwapo kwa roho, mimi mwenyewe nimekwisha kumhukumu yeye aliyetenda jambo hilo, kana kwamba nikiwapo.

4 Katika jina la Bwana wetu Yesu, ninyi mkiwa mmekusanyika pamoja na roho yangu, pamoja na uweza wa Bwana wetu Yesu;

5 kumtolea Shetani mtu huyo, ili mwili uadhibiwe, ili na roho iokolewe katika siku ya Bwana Yesu”.

Bwana atupe Imani ya kweli na dhamiri safi.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

DHAMBI YA MAUTI

Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni ipi?

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

MAZUNGUMZO MABAYA HUHARIBU TABIA NJEMA.

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.

Gumegume ni nini? (Isaya 50:7)

Rudi nyumbani

Print this post

TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU

Jina la Bwana na Mwokozi Yesu libarikiwe. Karibu tujifunze biblia.

Je kuna utofauti wowote ya Ubatizo wa Yohana na ule wa Bwana Yesu?,

Jibu ni kwamba hakuna utofauti wowote, ubatizo ni ule ule mmoja  wa toba, lakini kinachoutofautisha ule wa Yohana na ule wa Bwana Yesu ni “jina” Lakini ubatizo ni ule ule.

Kumbuka kabla ya Bwana Yesu kuja watu walikuwa wanasali, walikuwa wanafanya maombezi, na vitu vingine lakini walikuwa hawalitumii jina lolote, kwasababu hawakupewa maagizo hayo na Mungu. Hali kadhalika na Yohana alipokuja na ufunuo mpya wa ubatizo, alibatiza pasipo kuhusisha jina lolote. Maana yake baada ya watu kutubu kwa kumaanisha kuziacha dhambi zao, ishara ya mwisho ya wao kutakasika ilikuwa ni “kuzamishwa katika maji, na kuibuka juu” pasipo kutaja jina lolote.

Lakini Bwana Yesu alipokuja, mambo yalibadilika.. Kila kitu cha KIMungu ni lazima kifanyike kwa jina lake yeye..

Wakolosai 3:17 “Na kila mfanyalo, KWA NENO AU KWA TENDO, FANYENI YOTE KATIKA JINA LA BWANA YESU, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”.

Kutokana na maagizo hayo, Mitume na wanafunzi wengine wa Bwana Yesu, walianza kulitumia jina la Yesu katika mambo yote yote ya kiMungu watakayoyafanya kwa NENO na kwa MATENDO.

Mfano wa MANENO ambayo walianza kutamka kwa jina la Yesu ni SALA zote NA MAOMBI  NA MAHUBIRI …ndio maana utaona walipokwenda kutoa pepo, na kuombea watu wenye magonjwa na madhaifu mbali mbali walitumia jina la Yesu,..

Luka 16:17 “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; KWA JINA LANGU watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya”.

Vile vile utaona walipoenda kuhubiri na kufundisha, walifundisha kwa jina la Yesu..

Luka 24:46 “Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu;

47 na kwamba mataifa yote watahubiriwa KWA JINA LAKE habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu”.

Soma pia Matendo 4:18

Mfano wa matendo hayo yalikuwa ni ubatizo!..

Hayo yalikuwa ni Maneno, sasa utauliza vipi kuhusu Matendo..je! kuna matendo yoyote ambayo yalikuwa yanafanywa kwa jina la Yesu?.. Jibu ni ndio!

Kumbuka ubatizo si yohana peke yake aliyekuwa anafanya, bali na wanafunzi wake pia walikuwa wanawabatiza watu..kwasababu Yohana aliwafundisha hivyo, na zaidi sana utaona pia Adrea kabla ya kuwa Mwanafunzi wa Bwana Yesu alikuwa ni mwanafunzi wa Yohana. Hivyo alikuwa anaujua ubatizo vizuri na alikuwa akibatiza, kabla hata ya Bwana Yesu.

Lakini baada ya Bwana YESU kuja, na kufahamu kuwa mambo yote, ni lazima yafanyike kwa jina la Bwana Yesu, ikiwemo ubatizo pia, ndipo wote wakaacha kubatiza kama Yohana, kwa kuzamisha bila kutaja jina lolote, na wakaanza kubatiza kwa jina la Yesu.

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.

Umeona?.. kumbe hata ubatizo, ni lazima uwe kwa jina la Bwana Yesu ili ulete matokeo.. Ndio maana Mtume Paulo, alipokutana na wale watu kipindi wapo Efeso, aliwaambia wakabatizwe upya kwa jina la Yesu, ijapokuwa tayari walikuwa wameshabatizwa kwa ubatizo wa Yohana.

Matendo 19:1 “Ikawa, Apolo alipokuwa Korintho, Paulo, akiisha kupita kati ya nchi za juu, akafika Efeso; akakutana na wanafunzi kadha wa kadha huko;

2 akawauliza, Je! Mlipokea Roho Mtakatifu mlipoamini? Wakamjibu, La, hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatukusikia.

3 AKAWAULIZA, BASI MLIBATIZWA KWA UBATIZO GANI? Wakasema, Kwa ubatizo wa Yohana.

4 Paulo akasema, Yohana alibatiza kwa ubatizo wa toba, akiwaambia watu wamwamini yeye atakayekuja nyuma yake, yaani, Yesu

5 WALIPOSIKIA HAYA WAKABATIZWA KWA JINA LA BWANA YESU.

6 Na Paulo, alipokwisha kuweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akaja juu yao; wakaanza kunena kwa lugha, na kutabiri.”

Ndugu unayesoma ujumbe huu, fahamu kuwa kama hutabatizwa katika ubatizo sahihi, baada ya kuujua ukweli, utakuwa umemkataa Mungu moja kwa moja!!!.. na kuna madhara makubwa sana ya kutokubatizwa kwa jina la Bwana Yesu, (siku zote usilisahau hilo kichwani mwako).

Ikiwa bado hujampokea Yesu, kumbuka hizi ni siku za Mwisho, Kristo anarudi hivyo ni vizuri ukayatengeneza maisha yako kabla nyakati za hatari hazijafika.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

UMUHIMU WA KUBATIZWA.

Je ni viatu gani Musa aliambiwa avivue?  Vya mwilini au vya rohoni? (Kutoka 3:5).

HAKUNA MTU ANIONDOLEAYE, BALI MIMI NAUTOA MWENYEWE

Rudi nyumbani

Print this post

Azidishaye mali yake kwa riba, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.

SWALI: Nini maana ya huu mstari; 

Mithali 28:8 “Yeye azidishaye mali yake kwa riba na faida, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.


JIBU: Huyo anayezungumziwa azidishiye mali zake kwa riba na faida ni mtu ajipatiaye mali kwa njia zisizo za haki, kuwadhulumu wanyonge.

Kwamfano katika biblia Mungu aliwaangiza wana wa Israeli, wasiwatoze riba maskini, pindi wawakopeshapo, na pia wasichukue faida kutoka kwa ndugu zao, isipokuwa kwa wageni tu.

Kutoka 22:25

“Ukimkopesha mtu aliye maskini, katika watu wangu walio pamoja nawe; usiwe kwake mfano wa mwenye kumdai; wala hutamwandikia faida”.

Soma pia, Walawi 25: 35-37, kumb 23

Hivyo kulikuwa na kundi kubwa la matajiri walioihasi hii sheria ya Mungu, wakawa wanawatoza riba na kujipatia faida isivyo haki, Matokeo yake Wakafanikiwa kujikusanyia mali nyingi kama mavumbi ya ardhini.

(Ayubu 27: 13-16 ) 

Lakini bado maandiko, yanatoa matokeo au hatma ya watu kama hawa. Mwisho wa siku Mungu anawapokonya na kuligawia kundi lingine la watu lenye kuwahurumia maskini.

Utajiuliza inawezekanikaje..biblia inasema mali ina mbawa, inaweza kupaa ghafla, au ikatumiwa kwa matumizi yasiyo ya muhimu ikapukutika yote, au wewe ukafa ukamwachia mwingine. Lakini kule inapoelekea, sio popote tu ilimradi, hapana,  bali ni kwa mtu yule ambaye anawahurumia maskini.

Ndio Mungu anaweza kufanya hivyo..usipoitumia talanta yako vema. Anasema mnyanganyeni yule mwenye moja mkampe yule mwenye 10 (Mathayo 25:28),.Bwana anaweza kukunyang’anya ulichonacho. 

Hii inatufunza nini? 

Tukiwa watu wa kutenda haki na kuwahurumia maskini, kwa kuwapa vitu, basi tujue kuwa tayari kuna watu wameshaandaliwa kwa ajili ya kutuletea  hazina hizo, na watu wenyewe ndio hao waovu, wanaojilimbikizia mabilioni ya pesa katika akaunti zao za benki kwa dhuluma, na hila, na biashara haramu, na sio kwa njia halali.

Hii ni kuonyesha kuwa watu wanaopenda kuwapa wengine vitu, wanayo hazina kubwa sana hapa dunia.

Bwana atusaidie kuzifahamu hekima hizi tupende kuwasaidia watu wanyonge.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

Kiburi cha Uzima ni nini? (1Yohana 2:16)

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

UBATILI.

Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?

SHINA LA UCHUNGU, LISICHIPUKE NDANI YETU.

DORKASI AITWAYE PAA.

Rudi nyumbani

Print this post

Utawanyiko wa Wayunani ulikuwaje?

Utawanyiko wa Wayunani unaozungumziwa katika Yohana 7:35 ulikuwaje?

Jibu: Tuanzie kusoma mstari wa 31, ili tupate maana kamili..

Yohana 7:31 “Na watu wengi katika mkutano wakamwamini; wakasema, Atakapokuja Kristo, je! Atafanya ishara nyingi zaidi kuliko hizi alizozifanya huyu?

32  Mafarisayo wakawasikia mkutano wakinung’unika hivi juu yake; basi wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakatuma watumishi ili wamkamate.

33  Basi Yesu akasema, Bado kitambo kidogo nipo pamoja nanyi; kisha naenda zangu kwake yeye aliyenipeleka.

34  Mtanitafuta wala hamtaniona; nami nilipo ninyi hamwezi kuja.

35  Basi Wayahudi wakasemezana, Huyu atakwenda wapi hata sisi tusimwone? ATI! ATAKWENDA KWA UTAWANYIKO WA WAYUNANI, NA KUWAFUNDISHA WAYUNANI?

36  Ni neno gani hilo alilolisema, Mtanitafuta wala hamtaniona; nami nilipo ninyi hamwezi kuja?”

Kabla ya kujua Utawanyko wa Wayunani ni kitu gani, ni vizuri kwanza kujua Wayunani walikuwa ni watu gani?.. Kujua Wayunani walikuwa ni watu gani unaweza kusoma hapa >>>>Nawiwa na Wayunani na wasio Wayunani.

Sasa tukirudi kwenye swali; “Utawanyiko wa Wayunani ulikuwaje”?.

Jibu ni kwamba, Utawanyiko wa Wayunani halikuwa tukio Fulani lililowatawanya Wayunani, Bali ni lugha iliyotumika kuwatambulisha Wayahudi waliotawanyika na kuishi katika nchi ya Wayunani, iliyokuwa nchi ya watu wa Mataifa.

Kumbuka si Wayahudi wote walikuwa wanaishi katika nchi ya Israeli, walikuwepo wengi waliokuwa wanaishi nchi nyingine za mbali, kama Rumi, Galatia, Misri, Babeli na ikiwemo hii ya Uyunani. Mfano wa hao utaona ni Mtume Paulo, yeye alikuwa ni Muisraeli kwa asili lakini hakuzaliwa Israeli bali katika mji wa Tarso, ambao ulikuwa upo mbali kabisa na nchi ya Israeli.

Na wengine ni wale waliomfuata Filipo na kumwomba awaonyeshe Bwana Yesu..

Yohana 12:20 “ Palikuwa na Wayunani kadha wa kadha miongoni mwa watu waliokwea kwenda kuabudu kwenye sikukuu.

21  Basi hao walimwendea Filipo, mtu wa Bethsaida ya Galilaya, wakamwomba, wakisema, Bwana, sisi tunataka kumwona Yesu”.

Na wakiwa katika hayo mataifa ya ugenini, wengi wao walikuwa bado wanashika dini yao ya kiyahudi, na hata huko walipokuwepo walijenga masinagogi yao ya ibada. (Matendo 13:43). Ni sawasawa na watu wa asili ya India, wanaoishi Tanzania leo, wakiwa huku bado wanajenga mahekalu yao na kuendeleza dini zao, na wayahudi walikuwa hivyo hivyo, walipokuwa huko katika nchi za ugenini. Walijenga mahekalu na kuendeleza desturi zao, kana kwamba wapo Israeli. Ndio maana utaona Petro anaandika waraka mmoja na kuwapelekea Wayahudi hao waliopo sehemu mbali mbali walizotawanyikia..

1Petro 1: 1 “Petro, mtume wa Yesu Kristo, kwa wateule wa Utawanyiko, wakaao hali ya ugeni katika Ponto, na Galatia, na Kapadokia, na Asia, na Bithinia”

Na zipo sababu kuu mbili zilizowafanya Wayahudi baadhi wawepo katika hizo nchi za mataifa.

1.Kuchukuliwa utumwani.

Utumwa wa Babeli, na Ashuru ndio ulikuwa sababu ya kwanza kuwafanya Israeli wabakie katika hizo nchi.. Kwani mbiu ilipotolewa ya Wayahudi warudi nchini kwao, si wote walirejea nyumbani, wengi walisalia katika nchi walizochukuliwa mateka.. na huko wakaendelea na maisha yao kama kawaida.

2. Biashara

Baadhi ya Wayahudi walikuwa wanasafiri kwenda kufanya biashara katika nchi za mbali, hivyo wengi wao walikuwa wanaanza maisha katika hiyo miji waliokuwa wanaiendea.

Kwahiyo sasa, Utawanyiko wa Wayunani  tafsiri yake ni “utawanyiko wa Wayahudi waliopo katika nchi ya Uyunani”

Kwahiyo Bwana Yesu alipowaambia Mafarisayo “kwamba mtanitafuta wala hamtaniona”….wenyewe walidhani Bwana ataenda Uyunani kuwahubiria na Wayunani, kwasababu wao wamekataa kumsikiliza.

Lakini Bwana hakumaanisha hivyo, bali alimaanisha kuwa “atakwenda zake kwa Baba (yaani mbinguni)” na “watamtafuta lakini hawatamwona”, na zaidi ya yote wao hawawezi kwenda kule aliko, kwasababu wamemkataa yeye.

Hiyo ikitufundisha kuwa na sisi tukimkataa sasa Bwana Yesu, utafika wakati “tutamtafuta lakini hatutamwona” na kule aliko “sisi hatutaweza kufika”.

Yohana 7:33 “Basi Yesu akasema, Bado kitambo kidogo nipo pamoja nanyi; kisha naenda zangu kwake yeye aliyenipeleka.

34  Mtanitafuta wala hamtaniona; nami nilipo ninyi hamwezi kuja”

Kaka/Dada ambaye bado hujaokoka, ambaye bado unaipuuzia injili kama hawa Mafarisayo, Bwana Yesu anakuambia leo “bado kitambo kidogo nipo na wewe”…. bado anakuvumilia sasa, lakini bado kitambo kidogo atakuacha… za baada ya kukuacha anasema “kule aliko wewe hutaweza kwenda”.

Ni jambo baya sana kuachwa na Mungu!..

Na mtu anaachwaje na Mungu?.. Ni pale anapoisikia injili kwa muda mrefu bila kubadilika!!.. Kikawaida Mungu ni Mungu wa uhuru, huwa hatulazimishi kufanya jambo, anachokifanya yeye kwa ule moyo mgumu, usio na toba, ni kuuacha tu!..  Utauliza hilo tunalisoma wapi katika biblia??.

Warumi 1:28  “Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, MUNGU ALIWAACHA WAFUATE AKILI ZAO ZISIZOFAA, WAYAFANYE YASIYOWAPASA.

29  Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya,

30  wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao,

31  wasio na ufahamu, wenye kuvunja maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema;

32  ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao”.

Tubu dhambi leo kwa kumaanisha kuziacha..na tafuta ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu, kukamilisha wokovu wako na Roho Mtakatifu atakuongoza kule anakotaka yeye uende.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Ni wayahudi wa aina gani wanaotajwa kuwa sinagogi la shetani? (Ufunuo 2:9, Ufunuo 3:9)

Je! wayahudi wote wataokolewa kulingana na Warumi 11:26?

YUKO WAPI MFALME WA WAYAHUDI?

Nini maana ya wokovu watoka kwa Wayahudi? (Yohana 4:22)

Je! Mtume Paulo alikuwa ni Mrumi, Myahudi au raia wa Tarso?

Rudi nyumbani

Print this post

YESU HAYUPO KATIKA MAZINGIRA YALEYALE TU SIKUZOTE, USIJISAHAU.

Bwana Yesu asifiwe, karibu tena tujifunze maneno ya uzima. Leo nataka tuone jambo ambalo, wengi wetu tuliookoka hatulifahamu kuhusiana na tabia ya Bwana wetu Yesu Kristo.

Ili tuelewe vema kiini cha somo, naomba tusome hivi vifungu vitatu, kwa umakini sana;

Mathayo 9:7 “Akaondoka, akaenda zake nyumbani kwake”.

Mathayo 13:1 “Siku ile Yesu akatoka nyumbani, akaketi kando ya bahari.

2 Wakamkusanyikia makutano mengi, hata akapanda chomboni, akaketi; na ule mkutano wote wakasimama pwani”.

Mathayo 14:13 “Naye Yesu aliposikia; hayo, aliondoka huko katika chombo, akaenda mahali pasipo watu, faraghani. Na makutano waliposikia, walimfuata kwa miguu kutoka mijini mwao.

14 Yesu akatoka, akaona mkutano mkuu, akawahurumia, akawaponya wagonjwa wao”.

Kama tunavyosoma hapo, kuna wakati Bwana Yesu alikaa nyumbani kwake, mahali ambapo panajulikana, kwamfano kama mtu angemuulizia angeambiwa anakaa pale kwenye kaya ile namba Fulani..Utamkuta ameketi  kwenye kochi lake, sebuleni kwake, au yupo jikoni kwake anajipikia chai, atakukaribisha na mtazungumza mengi tu.

Soma,

Yohan1:37 “Wale wanafunzi wawili wakamsikia akinena, wakamfuata Yesu.

38 Yesu aligeuka, akawaona wakimfuata, akawaambia, Mnatafuta nini? Wakamwambia, Rabi, (maana yake, Mwalimu), unakaa wapi?

39 Akawaambia, Njoni, nanyi mtaona. Wakaenda, wakaona akaapo, wakakaa kwake siku ile. Nayo ilikuwa yapata saa kumi”.

Lakini upo wakati aliondoka hapo, akaenda katika mazingira ambayo yana watu, lakini hayana nyumba ndio hapo unamwona anatoka nyumbani kwake anakwenda kuketi kando ya bahari.. Sasa kumpata hapa, si kurahisi kama ilivyokuwa nyumbani, Leo hii ni rahisi mtu kukwambia tuonane hoteli Fulani, au nyumba Fulani, kuliko kukwambia tuonane fukweni, wavuvi walipo. Ni ngumu kwasababu hakuna ofisi au makazi pale.

Lakini kama hiyo haitoshi, aliondoka tena huko fukweni ambapo alikuwa anakwenda mara kwa mara kuwafundisha watu, akakaa sehemu isiyokuwa na watu kabisa, maana yake nyikani/ jangwani. Huku ndiko kubaya kabisa, kwasababu hakuna upatikanaji wa mahitaji yoyote ya kijamii. Hakuna maji wala chakula, wala kivuli, ni jua tu, na vumbi..

Lakini katika sehemu zote hizi, watu waliokuwa na shida kwelikweli walimfuata, isipokuwa ni kwa ugumu sana, kwasababu iliwabidi watembee kwa miguu umbali mrefu, kama tunavyosoma hapo juu, waende mahali ambapo hawajui kama watarudi salama, au mizoga.

Na ndio maana kule nyikani, ilifikia hatua wanawafunzi wake wakamwambia Bwana awaage makutano, waende kujitafutia chakula kwasababu wamekaa naye siku tatu, usiku na mchana, bila chochote, watazimia,…Lakini Yesu alijua ni nini anakitengeneza ndani yao.

Mathayo 14:15 “Hata kulipokuwa jioni, wanafunzi wake walimwendea, wakasema, Mahali hapa ni nyika tupu, na saa imekwisha pita; uwaage makutano, waende zao vijijini, wakajinunulie vyakula”.

Ndugu yangu, pindi unapookoka, ni sawa na ile hatua ya kwanza ya Yesu kukaa nyumbani kwake. Wakati huu Kristo anakuwa karibu sana na wewe, mda wowote utampata, itakuwa ni rahisi yeye kuchukuliana na wewe kwa hali zako zote.. Lakini jambo hilo halitaendelea sana..

Ataondoka nyumbani kwake na kwenda ufukweni.. Hapo ndipo itabidi umfuate. Ukikaa katika mazingira yale yale, miezi inaenda miezi inarudi, huonyeshi bidii yoyote kwa Kristo, wewe mwenyewe utashuhudia tu ukame utakaouna moyoni mwako. Utadhani kwamba Kristo amekuacha, kwasababu ile raha uliyokuwa mwanzo, au vile vitu alivyokuwa anakuonyesha mwanzo vimekata. Ukishaona hivyo, hapo ndipo unapaswa ujiongeze, zidisha bidii yako, kufanya ibada, kuomba, kusoma Neno na kujitenga na uovu. Ukizingatia hayo, utaanza kumwona tena akikufundisha..

Lakini hapo napo hatadumu kwa muda mrefu sana kama unavyodhani.. Atapiga hatua nyingine na kwenda nyikani, pasipokuwa na kitu/watu. Na huko nako huna budi kumfuata.. Hapo ndipo inapokugharimu, kuuaga ulimwengu, inapokugharimu, kupoteza nafsi yako kwa ajili yake,. Unamfuata Yesu hujui kesho yako utakula nini, hujui hatma ya maisha yako itakuwaje, unakubali kupukutika naye pale nyikani, huku ukimsikiliza tu,

Wakati huu usijijali sana, ikiwa unahaja kweli na Yesu.. Kwasababu hatua hii ya kujikana nafsi, inafikiwa na wachache, lakini huku ndipo Kristo anajifunua kwa mtu kwa viwango vingine kabisa. Utaona wale makutano walioweza kustahimili naye, siku tatu kule nyikani, bila kitu chochote, walipata faida mbili, ya kwanza ni kupokea uzima wa milele, na ya pili, ni kugawanyiwa mikate, ambayo waliila na kusaza. Sasa mikate pale inafunua, [rizki zao], maana yake ni kuwa Kristo aliwabariki, rizki zao, kule waliporudi, walipata vingi, kupita kiasi mpaka wakasaza, Kama kulikuwa na muuza genge alipata wateja mara mbili zaidi n.k..yaani kwa ufupi uchumi wao ulirekebishwa na Bwana.(Mathayo 14:19-21)

Lakini hiyo yote ilitokana na nini?

Ni kuwa radhi, kujitwika msalaba wako na kumfata Yesu. Hili haliepukiki kwa mtu yeyote anayemaanisha kumfuata Bwana Yesu. Ikiwa hauwi tayari binti kutupa vimini na suruali, na maurembo ya kidunia, kuukana ulimwengu kweli kweli, huwezi kumwona Bwana katika viwango vingine, ikiwa kijana, upo nusu nusu, vuguvugu, mizaha, na matusi, miziki ya kidunia, kubeti, mipira, punyeto, pamoja na udunia vimekutawala, hapo usiseme nimemwona Bwana.

Marko 8:34 “Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate.

35 Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha.

36 Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake?

37 Ama mtu atoe nini badala ya nafsi yake?”

Tukizijua tabia hizi za Bwana Yesu, basi tutajifunza kuwa watu wa kupiga hatua kila siku, kumfikia yeye. Kwasababu Bwana hayupo sehemu moja. Tukatae ukristo mgando.

 Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KUNA WAKATI YESU ATAPITA NA WATU HAWATAJUA.

RABI, UNAKAA WAPI?

JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.

LEO WOKOVU UMEFIKA NYUMBANI HUMU

NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

Je! ni sahihi kuning’iniza picha nyumbani mwako kama ya Yesu?

“Bonde la vilio” ni nini katika biblia?(Zaburi 84:6)

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Rudi nyumbani

Print this post