(Masomo maalumu kwa wanawake).
Kama wewe ni mwanamke na unatamani kupata kibali cha ndoa, au kupata mtu sahihi wa atakayekupenda, basi kuwa kama Esta, ambaye alikuwa na tabia ya kutokupenda-penda vitu!… Wengi wanadhani ubikira ndicho kigezo cha juu ya kupata kibali… Nataka nikuambie sivyo!.. walijitokeza mabikra wengi mbele ya Mfalme Ahasuero, lakini ni mmoja tu aliyechaguliwa..
Sasa ni kigezo gani cha juu kilichompa Esta umalkia??….Turejee maandiko tutapata majibu..
Esta 2:15 “Hata ilipowadia zamu yake Esta, binti Abihaili, mjomba wake Mordekai, ambaye alimtwaa kuwa binti yake, ili aingie kwa mfalme, YEYE HAKUTAKA KITU, ila vile vilivyoagizwa na Hegai, msimamizi wake mfalme, mwenye kuwalinda wanawake. Naye huyu Esta alikuwa amepata kibali machoni pa wote waliomwona.
16 Basi Esta alipelekwa kwa mfalme Ahasuero, katika nyumba ya kifalme, mwezi wa kumi, ndio mwezi wa Tebethi, mwaka wa saba wa kumiliki kwake.
17 MFALME AKAMPENDA ESTA KULIKO WANAWAKE WOTE, NAYE AKAPATA NEEMA NA KIBALI MACHONI PAKE KULIKO MABIKIRA WOTE; BASI AKAMTIA TAJI YA KIFALME KICHWANI PAKE, AKAMFANYA AWE MALKIA BADALA YA VASHTI”.
Esta hakuwa na tabia ya kupenda-penda vitu (kwa ufupi hakuwa na tamaa) na wala hakuwa na mambo mengi!!.. aliingia kwa mfalme yeye kama yeye, katika uhalisia wake!.. wakati wengine walitaka waingie kwa mfalme na marashi yao, na mitindo yao, na wapambe wao, ili wakubalike, Esta yeye hakutaka hayo yote, aliona ni ulimbukeni, aliingia yeye kama yeye, isipokuwa vitu vichache ambaye yule msimamizi aliyeitwa Hegai alimshauri.
Hata leo ni hivyo hivyo, Biblia bado ni Neno la Mungu lililo hai, kupitia hilo tunajifunza kanuni nyingi.. kama wewe ni binti!, au mwanamke!.. ukitaka kibali na Neema.. basi KUWA WEWE!!!... Usianze kujibadili maungo yako, au sauti, au chochote kile katika mwili wako ambacho umeumbwa katika ualisi wake, vile vile usiwe mtu wa tamaa ya vitu (kila unachokiona unakitamani)..
Ukiwa mtu wa namna hiyo ni rahisi sana kupata kibali.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mistari ya biblia kuhusu kibali.
Ulawiti na Ufiraji vina tofauti gani, kulingana na 1Wakorintho 6:9?
Jibu: Turejee…
1Wakorintho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, WALA WAFIRAJI, wala WALAWITI”
“Ulawiti” ni kitendo cha mwanaume kumwingilia mwanaume mwingine kinyume na maumbile… Na “Ufiraji” ni kitendo cha Mwanaume kumwingilia mwanamke kinyume na maumbile.
Mambo haya yote mawili ni machukizo makuu mbele za Mungu, na “wafiraji na walawiti” hawataurithi uzima wa milele sawasawa na maandiko hayo.
Kama wewe ni mwanaume na una mke jiepushe na Ufiraji!.. na kama wewe ni mwanamke na una mume kataa ufiraji, kama mwenzako anataka kukuacha kwasababu hiyo ya wewe kuukataa ufiraji, hapo yupo huru kuondoka!.. na wewe upo huru kuoa au kuolewa na mwingine mwenye kufanana na wewe, (asiyefanya mambo hayo na aliyeokoka)!
1Wakorintho 7:15 “Lakini yule asiyeamini akiondoka, na aondoke. Hapo huyo ndugu mume au ndugu mke hafungiki. Lakini Mungu ametuita katika Amani”.
Neno “Ulawiti” limeonekana mara moja tu katika biblia na ni tendo baya kuliko ufiraji (Maana humu ndio wamo mashoga, jamii za wale watu wa Sodoma na Gomora).. Kwa ujumla Mkristo hapaswi kulawiti/kulawitiwa… kufira/kufirwa. Wote wafanyayo hayo, wana roho nyingine ndani yao, na sehemu yao itakuwa katika lile ziwa la moto.
Maran atha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mshahara wa Mbwa ni upi? Kama tunavyousoma katika Kumbukumbu 23:18
Hapo ndipo, atakapompa Mungu Baba ufalme wake.
Fahamu maana 1Wakorintho 14:20 “Ndugu zangu msiwe watoto katika akili zenu;
Swali: Kwanini biblia ikataze kujiongezea hekima, kwani kuna ubaya gani katika kuongeza hekima?
Jibu: Turejee..
Mhubiri 7:16 “Usiwe na haki kupita kiasi; Wala usijiongezee hekima mno; Kwani kujiangamiza mwenyewe?”.
Hekima inayozungumziwa hapo si hekima ya KiMungu, ambayo hiyo tumeagizwa tuitafute sana..
Yakobo 1:5 “Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa”.
Tena maandiko yanasema mtu aonaye hekima (hiyo ya kiMungu), biashara yake ni Zaidi ya fedha..
Mithali 3:13 “Heri mtu yule aonaye hekima, Na mtu yule apataye ufahamu.
14 Maana biashara yake ni bora kuliko biashara ya fedha, Na faida yake ni nyingi kuliko dhahabu safi.
15 Yeye ana thamani kuliko marijani, Wala vyote uvitamanivyo havilingani naye”.
Kwahiyo hekima iliyozungumziwa hapo katika Mhubiri 7:16b ambayo mtu akiwa nayo nyingi inamharibu si hekima ya kiMungu, bali ni HEKIMA YA KIDUNIA.. Ambayo hiyo kwa Mungu ni upuuzi sawasawa na 1Wakorintho 3:18
1Wakorintho 3:18 “Mtu asijidanganye mwenyewe; kama mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu, ili apate kuwa mwenye hekima.
19 Maana HEKIMA YA DUNIA HII NI UPUZI MBELE ZA MUNGU. Kwa maana imeandikwa, Yeye ndiye awanasaye wenye hekima katika hila yao.”
Umeona?.. kumbe hekima ya dunia ni upuuzi mbele za Mungu na hiyo mtu akijiongezea sana itamwangamiza!!!.
Sasa mfano wa hekima ya kidunia ni ile inayosema “mwanadamu asili yake ni nyani”.. sasa hii ni elimu/hekima ya kidunia..ambayo imetukuka miongoni mwa wasomi wengi wakubwa, kiasi kwamba mtu aliyezama sana katika hiyo hekima, anajiangamiza mwenyewe, kwani atafikia hatua ya kusema hakuna MUNGU.
Ndio maana hapo biblia inasema “usijiongezee mno”… Maana yake usizame sana katika kuzitafuta, kwani zimejaa upotofu mwingi na ukweli kidogo…
Bwana atusaidie.
Kwa maarifa Zaidi kwanini biblia iseme “usiwe na haki kupita kiasi” fungua hapa >>>>>USIWE NA HAKI KUPITA KIASI.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini Mungu alimkataa Sauli? (1Samweli 15:23)
NINI MAANA YA KUISHI KWA KUUKOMBOA WAKATI?.
Mithali 24:17 inamaana gani kusema Tengeneza kazi yako huko nje?
Wengi, tumeshasikia kuwa Yesu atarudi, lakini mpaka mtu anasema atarudi, maana yake ni kuwa alishawahi kuja hapo nyuma. Na kama tunavyojua Bwana wetu Yesu Kristo alikuja mara moja tu, miaka karibu elfu mbili iliyopita, akaishi, akafa,akazikwa, akafufuka, akapaa mbinguni. Lakini wakati wote alipokuwa hapa duniani aliwaahidi wanafunzi wake kuwa atarudi tena.
Hivyo somo hili, ni muhimu kufahamu, namna ambazo Yesu alisema atarudi, ili usikose maarifa, kwasababu wengi hapa wanakosa shabaha katika kutambua kauli za Yesu. Naomba Soma kwa utulivu somo hili mpaka mwisho.
Sasa kuhusu kurudi kwake duniani, alizungumza katika nyakati tofuati tofauti kurudi kwa namna mbili.
Tuangalie kwa undani, namna hizi mbili. Husasani tutailenga hiyo ya pili.
Je! ni kwa namna gani, alirudi kama Roho,Aliwaambia hivi mitume wake;
Yohana 14:18 “Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu. 19 Bado kitambo kidogo na ulimwengu haunioni tena; bali ninyi mnaniona. Na kwa sababu mimi ni hai, ninyi nanyi mtakuwa hai.
20 Siku ile ninyi mtatambua ya kuwa mimi ni ndani ya Baba yangu, nanyi ndani yangu, nami ndani yenu”.
Soma pia, katika Yohana 16:16, amerudia maneno hayo hayo,
Unaona? Mitume walidhani hawatamwona tena, lakini siku ile aliyopaa mbinguni,siku kumi baadaye, biblia inasema walikuwa wamekusanyika wote mahali pamoja, akawajilia Roho Mtakatifu akawakalia wote, wakajazwa Roho Mtakatifu. Na kama tunavyojua tangu huo wakati na kuendelea, kila mmoja alijua anaye Yesu moyoni mwake, hakuna mtu aliyeuliza Yesu yupo wapi.
Uyatima uliondoka kabisa, kabisa, ndipo wakatambua maana ya yale maneno. Hivyo tumeshaona kurudi kwake kwa kwanza duniani, kulikuja kwa namna hiyo ya Roho Mtakatifu, na mpaka sasa Kristo yupo ndani ya mioyo ya waliomwamini, na kupokea Roho Mtakatifu.
Lakini pia katika maneno yake mengine, alisema atarudi kama mwizi.
Soma,
Mathayo 24:43 Lakini fahamuni neno hili; kama mwenye nyumba angaliijua ile zamu mwivi atakayokuja, angalikesha, wala asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.
44 Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja.
Unaona tena?, Hajasema, atarudi kama askari, au mfanya biashara, bali kama mwizi. Sasa ni vema tujue sifa za mwizi, ni zipi kibiblia, ndipo tuelewe jinsi kurudi kwake kwa namna hiyo kutakavyokuwa.
Ukisoma Yohana 10:10 Yesu anasema hivi; “Mwivi haji ila AIBE na KUCHINJA na KUHARIBU; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele”.
Kumbe mwizi hasaa, anayezungumziwa ni mfano wa jambazi, na sio wale wadokozi, ni wale wanaobeba silaha, ili kuharibu na kuua wanaowaona, wachukue mali yao waondoke.
Na Yesu ndivyo atakavyokuja katika siku za mwisho hizi, atatimiza sifa hizo zote tatu.
1.) Jambo la kwanza Atakuja saa tusiyodhani, Kisha ATAIBA kitu chake cha thamani duniani. Ni hicho si kingine zaidi ya watakatifu wake. Hapo ndio suala la unyakuo linapoibukia.
Mathayo 24:40 Wakati ule watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa; 41 wanawake wawili watakuwa wakisaga; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa.
2) Lakini pamoja na hilo, kuja kwake kutaambatana na KUCHINJA.
Maana yake ni kwamba, kama unyakuo utakupita, dunia itakuwa inajiandaa kuingia katika siku ile ya mapigo ya ghadhabu ya Mungu, ambayo mwisho wake utaishia na Kristo kuonekana katika umbile la kibinadamu kabisa, kuwaua mataifa yote ambayo yatakusanyika kupigana naye katika ile vita kuu ya Harmagedoni.
Ufunuo 19:11 Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.
12 Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.
13 Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.
14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.
15 NA UPANGA MKALI hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.
16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANAWA MABWANA.
Huu ni wakati ambao Yesu, atauangamiza ulimwengu, mfano wa mwizi, asiyekuwa na huruma. Usitamani uwepo wakati huo ndugu, ni majuto vilio na kusaga meno.
3) Lakini mwisho kabisa, ATAHARIBU.
Tunafahamu kuwa mwizi, huvunja, mahali ili aingie, huvuruga kila kitu anachokiona, vivyo hivyo na hii dunia itafumuliwa yote, mifumo yote itaangushwa, itafinyangwa upya, yote hayo yatatokea katika siku hiyo hiyo ya Bwana, ambayo itaharibu kila kitu.
2Petro 3:10 Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea. 11 Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa, 12 mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka?
Soma pia,(Ufunuo 16:17-21), kuongeza maarifa..
Hivyo ndugu, wakati huu wa Yesu kurudi kama mwizi umekaribia sana, ambao utaanza Kwanza kwa tukio la unyakuo. Bwana anatutaka sisi tukeshe(rohoni), asitukute tumelala. Ili Siku hiyo isitujilie ghafla, tukabaki hapa duniani.
1Wathesalonike 5:1 Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.
2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.
3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.
4 Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi.
5 Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza.
6 Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.
7 Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku. 8 Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu.
Bwana atupe macho ya kuona haya.
Je! Umempokea Yesu maishani mwako, Je! Ameziondoa dhambi zako? Kama jibu ni la, unasubiri nini? Hujui kesho kama utakuwepo, hujui kama leo atarudi. Hivyo tubu sasa, mwamini Yeye upate ondoleo la dhambi zako, kisha utapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. Ikiwa utapenda kupokea wokovu basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii bure. Bwana akubariki.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
USILALE USINGIZI WAKATI WA KUMNGOJEA BWANA.
SWALI: Naomba kuelewa tafsiri ya mithali 30:32-33, isemayo;
Mithali 30:32 Ikiwa umefanya kipumbavu kwa kujikuza; Au ikiwa umewaza mabaya; Basi weka mkono wako juu ya kinywa chako.
33 Kwa maana kupiga maziwa huleta siagi; Na kupiga pua hutokeza damu; kadhalika kuchochea hasira hutokeza ugomvi.
JIBU: Hekima inatueleza matokeo ya kila tendo linapofanyiwa kazi liwe ni zuri au baya litaleta majibu fulani tu. Hapa anatumia mfano wa siagi ambayo inatolewa katika maziwa. Kwa kawaida siagi huwa imejificha ndani ya maziwa, hivyo ili kuipata tu ile siagi, ni kitendo cha kuipiga basi hutokea kwa juu yote,
Sasa kupiga hapo sio kuyachapa maziwa hapana, bali kuyakoroga, ndani chombo Fulani maalumu kwa muda mrefu, baadaye maziwa na siagi hujitenga vyenyewe.
Halikadhalika, pia damu huwa ipo ndani ya pua, lakini haiwezi kutoka yenyewe tu bila kuisumbua pua kwa kuipiga. Kwamfano mtu akikupiga ngumi ya pua ni wazi kuwa damu itatoka tu.
Ndivyo anavyofananisha na ugomvi, kwamba ni jambo ambalo lipo tu, wakati wowote katikati yetu. Mfano tu wa siagi ndani ya maziwa na damu ndani ya pua. Lakini mpaka ugomvi huo ujitokeze, unahitaji kuchochewa, kukorogwa, korogwa, kupigwa pigwa.
Anasema hasira inapoanza, aidha kwa kuzungumza maneno mabaya, mwenzako akakereka, haraka sana, weka mkono wako kinywani, usiendelee kuzungumza, kwasababu kitakachofuata ukiendelea sana ni ugomvi, yaani mapigano, na kudhuriana.
Mauaji, visasi, chuki, asilimia kubwa vimetokana na hasira zilizochochewa.
Lakini, uwezo huu wa kujizuia, una nguvu endapo mtu yupo ndani ya Kristo. Je! Umemwamini? Kama bado na upo tayari kumpokea leo, basi wasiliana nasi kwa namba zetu chini.
Bwana akubariki
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini iwe ni nchi ibubujikayo maziwa na asali?
Maziwa yasiyoghoshiwa ni nini? Kwanini biblia inatumia mfano huo?
Waamuzi 16:28 “Samsoni akamwita Bwana, akasema, Ee Bwana MUNGU, unikumbuke, nakuomba, ukanitie nguvu, nakuomba, mara hii tu, Ee Mungu, ili nipate kujilipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili”.
Samsoni haombi kujilipiza kisasi kwaajili ya Nywele zake zilizokatwa, bali kwajili ya “MACHO YAKE MAWILI”.. Maana yake macho yake yalikuwa ni bora kuliko nguvu zake… Laiti angeambiwa achague nguvu ziondolewe na macho yabaki, ni Dhahiri kuwa angechagua macho yabaki.. Na huo ungeweza kuwa uchaguzi wa kila mtu.
Macho ni Zaidi ya mikono, ni Zaidi ya miguu, ni Zaidi ya nguvu za mwili.. Na ndicho shetani alikitafuta kwa SAMSONI.. Macho yake!!!!… lakini ni jinsi gani angeyatoa?? Inahitajika kuziondoa kwanza nguvu zake za mwili.. Shetani alikuwa haziogopi nguvu za Samsoni, alichokuwa anakiogopa ni macho yake…
Kwani baada ya kumtoa macho alizitumia nguvu zake kusaga ngano za wafilisti…
Na leo hii adui anatafuta macho ya watu kama shabaha yake ya kwanza.. na macho anayoyatafuta si ya kimwili, bali yale ya kiroho..na anaanza kwanza kwa kudhoofisha nguvu za kiroho za mtu na kisha anamaliza kwa kumpofusha Macho ya kiroho … (hapo anakuwa amemaliza kazi!).. na hapo anaanza kumtumikisha kama alivyomtumikisha Samsoni.
2Wakorintho 4:4 “ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu”.
Lakini habari njema ni kwamba ipo NEEMA kuu juu yetu Zaidi ya ile iliyokuwa juu ya Samsoni. Kwani Samsoni alipomwomba Mungu amrejezee Nguvu zake alirejeshewa kweli na kuwaaharibu maadui zake lakini bado aliendelea kuwa kipofu..
Lakini katika wakati huu wa agano jipya tunaponyenyekea kwa Baba na kuomba msaada, kwa kumaanisha kabisa mbele zake, basi zile nguvu zetu adui alizoziteka zinarejea tena upya na pia macho yetu yanatiwa nuru.. Hiyo ndio faida ya kuwa ndani ya KRISTO.
Je nguvu zako za Kuomba zimeisha???, nguvu zako za kufunga zimeisha??..Nguvu za kumtumikia Mungu zimeisha??…. Kama ndio jua hiyo pia ni dalili ya kupofushwa macho na Ibilisi… Hivyo huwezi kuona mbele wala kutafakari yaliyopita… unahitaji msaada wa Mungu, kwa nguvu zako huwezi!!!
Huu ni wakati wa wewe kunyenyekea kwa Mungu kama Samsoni ili Bwana azirejeshe nguvu zako upya na macho yako yatiwe nuru.
Waamuzi 16:28 “Samsoni akamwita Bwana, akasema, Ee Bwana MUNGU, unikumbuke, nakuomba, ukanitie nguvu, nakuomba, mara hii tu, Ee Mungu, ili nipate kujilipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili”.
Omba kwa kumaanisha, na ikiwezekana funga! Ili Toba yako iwe na nguvu.. Na matokeo utayaona!
Waefeso 1:18 “macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo”
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
JE! NYWELE ZAKO ZINAOTA AU ZIMESIMAMA?
Nini maana ya kumpenda Bwana kwa moyo,roho, akili na nguvu zetu zote?
Kiburi ni hali ya moyo wa mtu kuinuka kutokana na kitu fulani alichonacho, au alichokipata au atakachokipata ambacho kinamtofautisha au kitamtofautisha yeye na mwingine.
Hali hii inamfanya mtu anakuwa na majivuno, dharau na jeuri na asiyetii na hata kukosa staha.
Mtu huyu anakuwa ni mgumu kushaurika, na wakati wote yeye ndio anajiona yupo sahihi na wengine wote wana kasoro.
Vifuatavyo ni vitu vichache ambavyo vinatengeneza kiburi ndani ya mtu.
1.MALI
Hiki ni kitu cha kwanza ambacho kinatengeneza kiburi ndani ya mtu, na kiburi chenyewe ni “kiburi cha uzima” tunachokisoma katika 1Yohana 2:16.
Hapa mtu anakuwa anaamini anao uzima au maisha kupitia vile alivyonavyo.. Hivyo hahitaji kuambiwa kingine chochote ambacho kitampa yeye uzima, tayari yeye anakuwa anaamini mali alizonazo ndizo jawabu la mambo yote..hivyo hata ukimpelekea Neno la Mungu ambalo ndilo uzima hawezi kukusikiliza…
Na kiburi hiki pia kwa sehemu kipo kwa watu wasio na mali, wanaozisaka wakiamini kuwa watakapozipata zintawapa majibu yote…na hawa ndio wale ukiwapelekea Neno la Mungu wanadharau na kukejeli na kuulizia pesa.
Lakini Bwana YESU alisema kuwa uzima wa mtu haupo katika wingi wa vitu mtu alivyonavyo..(Luka 12:15).
2. ELIMU
Maarifa hususani ya kidunia ni mlango wa pili wa kuzalisha kiburi ndani ya mtu.
Hapa ni pale mtu kapata elimu ambayo ni ya juu kuliko wengi..moyo wake unanyanyuka na kuona wengine wote hawawezi kumzidi akili au uwezo wa kutafakari..
Hivyo anapoletewa Neno la Mungu basi anaanza kumpima yule aliyemletea na anapogundua kuwa ana elimu ndogo ya kidunia kuliko yake, basi hamsikilizi akiamini kuwa atakuwa na upambanuzi hafifu…pasipo kujua kuwa elimu ya mbinguni haipatikani katika shule za wanadamu..kwani hata Mitume wa Bwana Yesu hawakusoma isipokuwa Mathayo tu..lakini leo mafunuo yao tunayasoma na kutusaidia.
3. KIPAWA/KARAMA
Kipawa/kipaji/Karama mtu alichonacho ni mlango wa tatu wa kuzalisha kiburi ndani ya mtu.
Hapa ni pale mtu anapotambua kuwa anao uwezo pengine wa kuimba kuliko wengine, anauwezo wa kufundisha kuliko wengine, ana uwezo wa kutenda jambo fulani kuliko wengine, na badala atumie uwezo huo kujaza pale palipopunguka, kinyume chake anautumia uwezo huo kujisifia au kujionyesha yeye ni bora na hivyo hata kusikiliza wengine au kushawishwa na wengine inakuwa ni ngumu.
4. CHEO/NAFASI.
Cheo au nafasi ni mlango wa nne wa kiburi kuzalika ndani ya mtu..
Hapa ni pale mtu anapopata nafasi fulani katika kanisa, au jamii au kazi…na kuona wote walio chini yake hawawezi kumwongezea chochote.
5. MWONEKANO
Huu ni mlango wa tano ambao unatengeneza kiburi ndani ya mtu..
Hapa ni pale mtu inatokea kujiona anavutia kimwonekano kuliko wengine, na kuamini kuwa yeye ni mzuri/mrembo zaidi ya wote na hakuna wa kumzidi..
Na kiburi hiki kinazalika pale anapopokea maoni ya kusifiwa na mtu mmoja au wawili.. Mtu kama huyu anapotokea mtu mwingine na kutaka kuzungumza naye inakuwa ni ngumu kumsikiliza kwasababu alijiona kama atachafuliwa mwonekano wake.
Sasa yafuatayo ni madhara ya kiburi juu ya mtu kibiblia.
1.Kiburi kinaondoa Neema ya Mungu.
Petro 5:5 “Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema”.
Neema ya Mungu inapokuwa juu ya mtu inamwongezea kibali kwake Mungu na kwa wanadamu…
Mtu mwenye neema ya Mungu tele juu yake, inakuwa ni vyepesi kwake kushinda dhambi tofauti na yule ambaye amepungukiwa neema, vike vile inakuwa vyepesi kwake kufanya jambo likafanikiwa.
2. Kiburi kinamletea mtu Aibu.
Mithali 11:2 “Kijapo kiburi ndipo ijapo aibu…”
Watu wengi wenye kiburi wanaishia kuabika, kutokana na majivuno yao na dharau zao hivyo mwisho wake huwa hawapati vile wanavyovitafuta na hivyo wanakuja kuaibika baadaye.
3. Kiburi kinaharibu Nyumba
Mzazi mmoja au wote wanapokuwa na kiburi wanaiharibu familia yao wenyewe…
Mithali 15:25 “BWANA ataing’oa nyumba ya mwenye kiburi..”
4. Kiburi kinamshusha mtu chini (kimaisha).
Wote wenye kiburi Mungu anawashusha chini..
Mithali 29:23 “Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa”.
5. Kiburi kitamshusha mtu kuzimu.
Wote wenye kiburi hawataurithi uzima wa milele.
Isaya 2:12 “Kwa maana kutakuwa siku ya BWANA wa majeshi juu ya watu wote wenye kiburi na majivuno, na juu ya yote yaliyoinuka; nayo yatashushwa chini……..
17 Na majivuno ya mwanadamu yatainamishwa, na kiburi cha watu kitashushwa; naye BWANA, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo”
Tabia nyingine ya mtu wenye kiburi pia ni mashindano na ubishi
Mithali 21:24 “Mwenye kiburi na kutakabari, jina lake ni mbishi; Hutenda mambo majivuno ya kiburi chake”.
Mithali 13:10 “Kiburi huleta mashindano tu…”
Jihadhari na kiburi..Na tunajihadhari nacho kwanza kwa kuokoka kisha kujazwa Roho Mtakatifu katika maisha yetu na kujitahidi kwa bidii kukaa mbali na mazingira yote yanayochochea kiburi.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo, Karibu tujifunze maneno ya uzima.
Katika agano la kale ilikuwa ni sheria, ili sadaka ya upatanisho, au ya dhambi ambayo ilihusisha kafara za wanyama, kuwa kamili, ni lazima uhusishwe na sehemu kuu mbili, ya kwanza ni ndani ya kambi, na ya pili ni nje ya kambi.
Ndani ya kambi au ndani ya lango, ndio ilichukuliwa damu ya mnyama huyo na kuingizwa kwa ajili ya upatanisho kwa kunyunyizwa. Lakini ilikuwa ni sharti pia viungo, ngozi na vinyesi, vya mnyama huyo vikateketezwe mbali nje ya kambi. Na kama jambo hilo lisipofanyika, haijalishi damu ya kunyunyiza ya mnyama huyo itakuwa ni njema kiasi gani, utapatanisho hauwezi kutokea.
Ndani ya kambi ni mahali patakatifu, lakini je! Ya kambi ni mahali pa uovu.
Sasa tukirudi kwenye agano jipya, tunaona mwokozi wetu Yesu Kristo, anafananisha na mnyawa huyo wa upatanisho, Hivyo ilimbidi, ahusishwe pia na sehemu zote mbili, yaani ndani ya kambi na nje ya kambi.
Alimwaga damu yake, ambayo kwa kupitia hiyo, ameingia nayo patakatifu pa patakatifu kule mbinguni, kutuombea sisi, Lakini hilo lisingewezekana, kama asingeteketezwa nje ya kambi.
Ndio Hapo tunaona Bwana wetu, ilimpasa, aache enzi na mamlaka mbinguni, (Atoke nje ya kambi), akutane na waovu huku duniani, ateketezwe kabisa mahali pa aibu pa waovu pale Golgota, ili sasa damu yake ipatikane kufanya upatanisho wetu kule mbinguni, kwa Baba ambapo ndio ndani ya kambi.
Na matokeo yake ndio haya tunayoyaona sasa hivi, sote kupata neema na ondoleo la dhambi zetu.
Lakini sasa maandiko yanasema..
Waebrania 13:11 Maana wanyama wale ambao damu yao huletwa ndani ya patakatifu na kuhani mkuu kwa ajili ya dhambi, viwiliwili vyao huteketezwa nje ya kambi.
12 KWA AJILI HII YESU NAYE, ILI AWATAKASE WATU KWA DAMU YAKE MWENYEWE, ALITESWA NJE YA LANGO.
13 BASI NA TUTOKE TUMWENDEE NJE YA KAMBI, TUKICHUKUA SHUTUMU LAKE.
14 Maana hapa hatuna mji udumuo, bali twautafuta ule ujao.
Umeona hapo? Kumbe na sisi, hatuna budi kumfuata Yesu nyayo zake, kwasababu alisema mimi nilipo na mtumishi wangu atakuwepo. Sasa hapo anasema, na sisi tutoke nje ya kambi, tuchukue shutumu lake. Akiwa na maana, tukubali kujitoa sadaka na sisi, nje ya lango, waovu walipo ili tuwavute wengine kwa mwokozi.
Kama mashahidi wa kweli wa Kristo, ni lazima tuwe tayari kuhatarisha maisha yetu, kwa ajili ya wengine. Tusiwe tu ndani ya lango, walipo watakatifu, ni kweli ni vizuri kufanya semina za ndani makanisani zina nafasi yake, ni vizuri kuhubiri mikutano ya ndani. Lakini je! Tunaweza tukawa tayari pia kwenda katikati ya watu wa dini nyingine kuwahubiria Kristo, tukawa tayari kwenda mahali pa jamii zenye vita na kuzitangaza habari za Yesu. Kanisa la Kwanza la mitume lilikuwa tayari kutoka nje ya kambi, kukutana na ukinzani wa wayahudi, kuburutwa, kupigwa mawe hata kuawa, walikuwa tayari kuwaendea wapagani sugu, na jamii za wachawi kuwatangazia Kristo. Vivyo hivyo na sisi hatuna budi kutoka nje ya kambi, kuliendea na kundi lingine ambalo halijamjua Kristo.
Hatuna budi kuwa tayari hata kuhatarisha afya zetu, fedha zetu, kazi zetu, vyeo vyetu, elimu zetu inapobidi ili wengine waokoke, wamjue Kristo. Huko ndiko kutoka nje ya kambi. Bwana Yesu ilimpasa aache enzi na mamlaka juu mbinguni, awaendee makahaba na watoza ushuru, awaendee waliosumbuliwa na ibilisi na mapepo, na sio kwa makuhani na waandishi, ijapokuwa na hao pia alikuja kuwafia, lakini nguvu zake nyingi zilikuwa kwa wenye dhambi.
Bwana atupe neema hiyo.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
(Masomo maalumu kwa watumishi wa Mungu).
Katika agano la Kale, Mungu aliwafundisha Haruni (aliyekuwa kuhani mkuu) pamoja na wanawe wote, jinsi ya kuwabarikia wana wa Israeli, na kupitia sala hiyo, au matamko hayo wana wa Israeli walibarikiwa kweli kweli.
Sala hiyo pia inaweza kutumika na watumishi wa Mungu leo, kulibarikia kundi la MUNGU, kwani nao pia ni makuhani kwa Mungu sawasawa na Ufunuo 1:6
Sala hiyo tunaisoma katika Hesabu 6:22-27.
Hesabu 6:22 “Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
23 Nena na Haruni na wanawe, uwaambie, HIVI NDIVYO MTAKAVYOWABARIKIA WANA WA ISRAELI; MTAWAAMBIA
24 Bwana akubarikie, na kukulinda;
25 Bwana akuangazie nuru za uso wake, na kukufadhili;
26 Bwana akuinulie uso wake, na kukupa Amani
27 Ndivyo watakavyoweka jina langu juu ya wana wa Israeli; nami nitawabarikia”
Na baraka hizo ni lazima zitamkwe baada ya watu kufundishwa kanuni za kubarikiwa, na kupokea Amani ya kiMungu na ulinzi.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)
Kutoka 14:13 “Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa Bwana atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele.
14 BWANA ATAWAPIGANIA NINYI, NANYI MTANYAMAZA KIMYA”.
Matokeo ya kupiganiwa na Bwana ni “Mwisho wa Manung’uniko, malalamiko, masononeko, huzuni na maumivu”.
Ndicho kilichowatokea wana wa Israeli pale walipoliona jeshi la Farao likija nyuma yao, na mbele yao kuna kizuizi cha bahari, (nyuma mauti inakuja, mbele mauti inawangojea).. wakaogopa mno na kupaniki na kuanza kumlaumu Musa, wakasahau mambo makuu waliyotendewa na Mungu masaa kadhaa na siku kadhaa nyuma, jinsi alivyompiga Farao kwa mapigo makuu.
Sasa ni rahisi sana kuwalaumu wana wa Israeli kuwa ni wajinga na wasiokumbuka!.. Lakini majaribu kama hayo hayo yanatukuta wengi leo na tunakuwa tunasahau fadhili za Mungu alizotutendea siku kadhaa au miaka kadhaa nyuma.
Hivyo unapotazama na kuona mauti mbele yako na nyuma yako unaona Giza, kiasi kwamba unajikuta unakosa utulivu na hata wakati mwingine kujiona upo katika hatari ya kutoa maneno mabaya kutoka katika kinywa chako… unapofikia hiyo hatua, basi huo si wakati wa kunung’unika, wala kulalamika, ni wakati wa wewe kumwomba MUNGU AKUPE UTULIVU.
Na unamwomba UTULIVU kwa wewe kumsihi asimame AKUPIGANIE VITA VILIVYOPO MBELE YAKO, Na ikiwa moyo wako umenyooka mbele zake basi utaona mkono wake akikupigania kama alivyowapigania waIsraeli NAWE UTAKAA KIMYA, ile huzuni itayeyuka, ile aibu itapotea, ile kiu ya kusema maneno mabaya na ya makufuru itayeyuka, nawe utajaa nyimbo za shangwe na sifa na shukrani kama wana wa Israeli walizoziimba baada ya bahari kupasuka na kuwameza maadui zao.
Kutoka 15:1 “Ndipo Musa na wana wa Israeli wakamwimbia Bwana wimbo huu wakanena, na kusema, Nitamwimbia Bwana, kwa maana ametukuka sana; Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini.
2 Bwana ni nguvu zangu, na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu. Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu; Ni Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza.
3 Bwana ni mtu wa vita, Bwana ndilo jina lake.
4 Magari ya Farao na jeshi lake amewatupa baharini, Maakida yake wateule wamezama katika bahari ya Shamu.
5 Vilindi vimewafunikiza, Walizama vilindini kama jiwe.
6 Bwana, mkono wako wa kuume umepata fahari ya uwezo, Bwana, mkono wako wa kuume wawasetaseta adui.
7 Kwa wingi wa ukuu wako wawaangusha chini wanaokuondokea, Wapeleka hasira yako, nayo huwateketeza kama mabua makavu.
8 Kwa upepo wa mianzi ya pua yako maji yalipandishwa, Mawimbi yakasimama juu wima mfano wa chungu, Vilindi vikagandamana ndani ya moyo wa bahari.
9 Adui akasema, Nitafuatia, nitapata, nitagawanya nyara, Nafsi yangu itashibishwa na wao; Nitaufuta upanga wangu, mkono wangu utawaangamiza.
10 Ulivuma kwa upepo wako, bahari ikawafunikiza; Wakazama kama risasi ndani ya maji makuu”.
Maran atha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je Farao alikufa kwenye maji pamoja na jeshi lake au alipona?