Category Archive Mafundisho

Maelezo ya Mithali 28:28 Wasio haki wainukapo, wanadamu hujificha; Bali waangamiapo, wenye haki huongezeka.

SWALI: Nini maana ya  Mithali 28:28 Wasio haki wainukapo, wanadamu hujificha; Bali waangamiapo, wenye haki huongezeka.


JIBU: Mithali hii hulenga hasaa watawala, iwe ni serikalini, kwenye mataasisi, makanisa n.k. endapo waongozao ni waovu, basi hufanya hata watu (hususani wale wema) kujificha, Au kutoonekana kabisa.

Ndio kama ilivyokuwa katika kipindi cha mfalme Ahabu, alipoiharibu nchi yote ya Israeli kwa kuweka miungu migeni, akichochewa na mkewe Yezebeli. Wakati huo Manabii wengi wa Mungu waliuliwa, na wale waliosalia walijificha wasionekane kabisa, wakabakia tu makuhani wa baali na wenye dhambi. Kiasi kwamba Eliya akadhani ni yeye tu peke yake nabii aliyebakia Israeli. Kuonyesha ni jinsi gani wenye haki, walivyokuwa adimu wakati huo. Lakini Mungu alimwambia Eliya, nimejisazia watu elfu saba wasiopigia goti baali.

Warumi 11:3  Bwana, wamewaua manabii wako, wamezibomoa madhabahu zako, nami nimesalia peke yangu, nao wananitafuta roho yangu.

4  Lakini ile jawabu ya Mungu yamwambiaje? Nimejisazia watu elfu saba wasiopiga goti mbele ya Baali.

5  Basi ni vivi hivi wakati huu wa sasa, yako mabaki waliochaguliwa kwa neema.

Ni kama leo tu ulimwenguni, tunavyoona kiwango cha watenda maasi na  maasi kinavyozidi kuongezeka, ndivyo inavyokuwa ngumu kukutana na watakatifu halisi, na hiyo inaweza pelekea pengine ukajidhani mpo wachache, au hakuna kabisa kama wewe.

Ukiwa katika mazingira kama haya usipumbazike, ukafanana na ulimwengu. Bali fahamu kuwa wapo, isipokuwa Mungu amewaficha tu. Siku watakapoondolewa waovu duniani ndipo utajua kuwa Mungu anao watakatifu wake, wengi.

Ndio maana ya hilo neno Bali “waangamiapo wasio haki, wenye haki huongezeka”.

Binti ambaye unatembea kwa kujisitiri barabarani, na huwenda huoni aliye kama wewe mtaa mzima, usife moyo, ni kwasababu wasio haki ni wengi. Kijana uliyeamua kuishi maisha ya mbali na uzinzi na anasa usijidhani upo peke yako, songa mbele tambua, ni  Mungu amewaficha tu watu wake. 

Kwasababu ni Neno la kweli kabisa wasio haki wastawipo, wenye haki hujificha, (sio kwamba wamekufa, bali wapo). Wakati utafika waovu wataondolewa, na sisi tutamiliki na kuangaza. Usiwe mfauta wimbi, nyakati hizi ni za hatari. Ni sawa na kichuguu tu, waweza kudhani hakina kumbikumbi ndani, kina huoni chochote kinachotoka humo,  lakini wakati wa mvua, unastaajabia wingi wao umetoka wapi. Vivyo hivyo na wewe endelea kutembea kwa ujasiri katika wokovu wako. Unyakuo umekaribia. Tambua Bwana analo jeshi lake.

Mithali 28:28 Wasio haki wainukapo, wanadamu hujificha; Bali waangamiapo, wenye haki huongezeka.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Miungu wasio na kikao pamoja na wenye mwili.

Nawiwa na Wayunani na wasio Wayunani.

Semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; (Luka 17:10) 

Rudi Nyumbani

Print this post

Tafsiri ya Mithali 27:15 Kutona-tona daima siku ya mvua nyingi, Na mwanamke mgomvi ni sawasawa;

SWALI: Nini maana ya Mithali 27:15 Kutona-tona daima siku ya mvua nyingi, Na mwanamke mgomvi ni sawasawa;


JIBU: Neno Kutona-tona kama lilivyotumika hapo, ni “maji yanayovuja darini”.

Hivyo anaposema Kutona-tona daima siku ya mvua nyingi. Anamaanisha kitendo cha kuvuja sana kwa dari siku ya mvua nyingi, na kitendo cha kukaa na mwanamke mgomvi ndani ni sawasawa.

Kwa namna gani?

Tunajua ukikaa kwenye nyumba ambayo dari lake halikujengwa vizuri, mvua kubwa inaponyesha maji mengi huchuruzika na kuingia ndani. Wakati umelala utashangaa maji yanakudondekea kitandani mwako, yanachuruzikia kwenye makochi, yanakwenda mpaka kwenye makapeti, jambo ambalo litakufanya usitulie hata kidogo humo ndani utakuwa tu bize, kusogoza vitu ovyo ovyo visilowe, na mbaya ni pale mvua inapokuwa kubwa, na maji kuongezeka ndani, mwisho huwa ni kutoka kabisa nje na kuiacha nyumba.

Ikiwa umeshawahi kupitia changamoto kama hiyo ya kuvujiwa nyumba, unaelewa ni kero kiasi gani.

Ndivyo anavyofananisha kutendo hicho na kuishi na mwanamke mgomvi. Ikilenga hasaa wanandoa. Kumbuka aliyeandika mithali hizi ni Sulemani, alikuwa anatambua anachokisema, kwasababu aliishi na wanawake elfu moja(1000) kama wake zake, na alijua masumbufu yao. Alikutana na changamoto za baadhi yao.

Mwanamke mgomvi, kibiblia ni Yule asimheshimu mumewe, ni Yule anayemwendesha mumewe, anayemkaripia, asiyekuwa msikivu, kila jambo analolifanya mumewe ni kulikosoa tu, mwenye kiburi na mwenye maneno mengi, asiye na staha.

Wanawake wa namna hii, huwataabisha waume zao sana, na hatimaye wengine huwafanya wahame kabisa nyumba, kukaa mbali na familia zao. Ni dari linalovuja utawezaje kukaa kwenye nyumba hiyo?

Andiko hilo limerudiwa pia katika;

Mithali 19:13 Mwana mpumbavu ni msiba kwa babaye; Na ugomvi wa mke kama kutona-tona daima.

Uonapo familia zenye migogoro ya namna hii ni kuziombea sana Bwana aziponye.

Maandiko hayo yamewekwa sio kuonyesha mabaya kwa jinsia ya kike, hapana, bali imetoa tahadhari ili yasitokee kwa wanawake wa kikristo.

Biblia imetoa mwenendo wa mwanamke halisi wa kikristo, inasema  awe ni wa kumtii mume wake. Awe ni mwenye kiasi, na MPOLE, na adabu. Akifanya hivyo atasimama vema kwenye nyumba yake, badala ya kuiharibu kinyume chake ataijenga.

1Timotheo 2:9  Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;

10  bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.

11  Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna.

Soma pia.

1Petro 3:1  Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;

2  wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu. 3  Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

4  bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, ROHO YA UPOLE NA UTULIVU, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.

5  Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.

6  Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote.

Hivyo wewe kama mwanamke ukitembea katika hayo, utakuwa katika upande salama wa Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Wokovu wa milele/ Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?

HUIJUI KAZI YA MUNGU, AFANYAYE MAMBO YOTE.

ALIJARIBIWA SAWASAWA NA SISI KATIKA MAMBO YOTE.

Rudi Nyumbani

Print this post

JE UNAZAA MATUNDA NA KUWAPONYA MATAIFA?

Sisi tuliookolewa pamoja na Bwana wetu Yesu Kristo, tunafananishwa na mti mmoja alioupanda Mungu mwenyewe ulimwengu. Na wote tunayo sehemu katika mti huo, na tumewekewa wajibu wa kufanya.

Bwana wetu Yesu Kristo anafananishwa na shina la mti, halafu sisi tunafananishwa na matawi.

Shina ni kuanzia kwenye mizizi, hadi mahali matawi yanapotokea. Hivyo Bwana wetu Yesu, ndiye anayechukua uhai wetu moja kwa kutoka kwa Mungu na kutuletea sisi. Lakini sisi ni kuanzia kwenye matawi mpaka kwenye matunda.

Yohana 15:1-2,5

[1]Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima. 

[2]Kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa; na kila tawi lizaalo hulisafisha, ili lizidi kuzaa….

[5]Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote. 

Sasa wengi wetu tunachoona katika mashina ni matunda tu peke yake. lakini leo ni vema tuone jambo hili kwa ndani. Kwa kawaida tawi huundwa na vitu viwili, cha kwanza ni majani, na cha pili ni matunda.

na vyote viwili vinapaswa vionekane katika shina. 

Hivyo mimi na wewe kama watakatifu, ni lazima tujiulize je majani yapo? na je matunda  yake pia yapo? 

Matunda ni nini?

Tafsiri ya awali ya matunda kama ilivyozungumziwa kwenye mfano ya mti, sio kuwavua watu kwa Kristo, kama inavyodhaniwa, hapana bali ni Kutoa tunda la wokovu wako. Yaani tunda la toba.

Yohana mbatizaji kwa uvuvio wa Roho alilifafanua vema..Tusome.

Mathayo 3:7-10

[7]Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja? 

[8]Basi zaeni matunda yapasayo toba; 

[9]wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto. 

[10]Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni. 

Aliwaona mafarisayo ambao walikiri kwa ujasiri wao ni wajumbe wa Yehova, uzao wa Ibrahimu, lakini mioyoni mwao, maovu na machafu ya kila namna yamewajaa. Hivyo wakaonekana ni miti isiyo na matunda.

Matunda ndio yale yanayojulikana kama tunda la Roho, ambayo kila mwamini anapaswa afanye bidii kuyatoa moyoni mwake katika maisha yake yote ya wokovu, awapo hapa duniani. Ambayo ni; 

Wagalatia 5:22

[22]Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu

[23]upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria. 

Mtu yeyote anayefanya bidii kuonyesha wokovu wake kimatendo, mtu huyo humzalia Mungu matunda, ambayo ndio chakula cha Roho wa Mungu. Na hivyo hufurahishwa sana na sisi..

Majani ni nini?

Lakini kama tulivyosema shina huundwa na majani pamoja na matunda. Sasa majani, ni utumishi ambao kila mmoja wetu amepewa wa kuwavuta wengine kwa Kristo, kwa karama aliyopewa ndani yake. 

Tuliagizwa na Bwana tuenende ulimwenguni kote, tukahubiri injili na kuwafanya mataifa kuwa wanafunzi wake (Mathayo 28:19),

Unapowashuhudia wengine, ni kwamba majani yako yanawaponya mataifa, na hivyo unawaokoa. Kumbuka majani kimsingi hayana ladha, mara nyingi hutumika kama tiba. Ndicho Bwana anachokifanya kwa wenye dhambi kupitia sisi, tunapowashuhudia.

Ufunuo wa Yohana 22:1-2

[1]Kisha akanionyesha mto wa maji ya uzima, wenye kung’aa kama bilauri, ukitoka katika kiti cha enzi cha Mungu, na cha Mwana-Kondoo, 

[2]katikati ya njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo mti wa uzima, uzaao matunda, aina kumi na mbili, wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na MAJANI YA MTI HUO NI YA KUWAPONYA MATAIFA. 

Umeona? Kumbe majani yake, ni lengo la kuwaponya mataifa, watu wasiomjua Mungu. Tujiulize je na sisi tunayaponya mataifa kwa kuhubiri injili?

Wewe kama mkristo uliyemshirika wa mti wa uzima huna budi kuwa mhubiri wa injili usikae tu, hivi hivi ukasema tayari nimeokolewa inatosha, fanya jambo kwa Bwana. Waeleze wengine habari za Yesu, waponywe. Usijidharau ukasema siwezi, kumbuka aitendaye kazi hiyo ni Kristo ndani yako, wewe ni tawi tu. washuhudie wengine.

Lakini si kuhubiri tu, halafu maisha yako yapo kinyume na Kristo, hapana hilo nalo ni hatari, ukiwa na majani tu, halafu huna matunda ya wokovu moyoni mwako..Utalaaniwa.

Marko 11:13

[13]Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda ili labda aone kitu juu yake; na alipoufikilia hakuona kitu ila majani; maana si wakati wa tini.

[14]Akajibu, akauambia, Tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia. 

Umeona hawa ni watu, wanaodhani kumtumikia Mungu tu yatosha hakuna haja ya kuishi maisha matakatifu. wanakutwa na majani tu peke yake.

Tuhakikishe tuna majani, lakini vilevile tuna matunda kwasababu sisi ni shina, ndani ya mti wa uzima. Na neema ya Mungu itatusaidia.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Tafsiri ya Mithali 27:18 Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake;

KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?

UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?

Rudi Nyumbani


 

Print this post

JE UMEJIFUNZA ULE WIMBO MPYA?

Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo, Tukijua kuwa ule mwisho unakaribia, hatuna budi siku baada ya siku tujichunguze je! Tumekamilika vema? ili siku ile tusionekane na mawaa mbele zake. Tulipokee taji timilifu tuliloandaliwa mbinguni na mwokozi wetu Yesu Kristo kwa neema zake.

Leo, napenda tufahamu juu ya wimbo mpya. Kama wewe ni msomaji mzuri wa kitabu cha Ufunuo. Utagundua zimetajwa nyimbo kuu tatu.

  1. Wimbo wa Musa
  2. Wimbo wa Mwanakondoo
  3. Wimbo mpya

Swali ni je! Hizi nyimbo ni zipi na zinatimiaje?

Wimbo wa Musa na wa mwanakondoo tunazisoma, katika Ufunuo 15:2-3

Ufunuo 15:2  Tena nikaona kitu kama mfano wa bahari ya kioo iliyochangamana na moto, na wale wenye kushinda, watokao kwa yule mnyama, na sanamu yake, na kwa hesabu ya jina lake, walikuwa wamesimama kando-kando ya hiyo bahari ya kioo, wenye vinubi vya Mungu.

3  Nao WAUIMBA WIMBO WA MUSA, MTUMWA WA MUNGU, NA WIMBO WA MWANA-KONDOO, wakisema, Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa

Wimbo wa Musa, ni injili ya Musa, ambayo iliwafanya watu wa kale, kutembea katika hiyo ili wamkaribie Mungu, ndiyo ile torati, ambayo wale waliokuwa katika agano la Ibrahimu kwa uzao, walirithi neema hiyo. Hivyo wana wa Israeli wote walikuwa wanauimba wimbo wa Musa. Yoyote ambaye hakuwa hana wimbo huo, basi wokovu au kumkaribia Mungu hakukuwezekana kwake.

Lakini wimbo wa Musa haukuwa na ukamilifu wote kwasababu ulikuwa ni wa mwilini, na wa kutarajia ahadi ya mwokozi mbeleni. Hivyo Mungu akaleta wimbo mwingine mpya kwa wanadamu wote. Ndio huo wimbo wa mwana-kondoo.

Ambayo ni injili ya neema iliyoletwa na Bwana wetu Yesu Kristo na kuhubiriwa na mitume wake. Kwa ufupi sisi wote tuliomwamini Yesu Kristo katika agano hili jipya, kwa pamoja tunauimba wimbo wa mwana-kondoo. Ndio maana kiini cha imani, na wokovu wetu ni Yesu Kristo. Mtu yeyote ambaye hajaoshwa dhambi zake kwa damu ya Yesu, hawezi kumwona Mungu, wala kamwe hataweza kumwelewa, haijalishi ataonyesha bidii zake nyingi kiasi gani. Kwasababu ndio utimilifu wote.

Lakini upo wimbo mwingine wa Tatu ndio huo wimbo mpya.

Wimbo huu, si wote watakaoweza kuuimba, lakini watakaoweza kuuimba watakuwa karibu sana na mwana-kondoo (Yesu Kristo), baada ya maisha haya. Ndio wale washindao, Ndio wale Yesu aliosema atawakiri mbele ya Baba na malaika zake, ndio wale watakaoketi pamoja naye katika viti vya enzi, ndio wale watakaotoka mashariki, magharibi, kaskazini na kusini, kula mkate naye mezani pake. Na vigezo amevianisha pale. Anasema..

Ufunuo 14:1  Kisha nikaona, na tazama, huyo Mwana-Kondoo amesimama juu ya mlima Sayuni, na watu mia na arobaini na nne elfu pamoja naye, wenye jina lake na jina la Baba yake limeandikwa katika vipaji vya nyuso zao.

2  Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni, kama sauti ya maji mengi, na kama sauti ya radi kuu. Na hiyo sauti niliyoisikia ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi, wakivipiga vinubi vyao;

3  na KUIMBA WIMBO MPYA mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele ya wale wenye uhai wanne, na wale wazee; WALA HAPANA MTU ALIYEWEZA KUJIFUNZA WIMBO ULE, ila wale mia na arobaini na nne elfu, WALIONUNULIWA KATIKA NCHI.

4  HAWA NDIO WASIOTIWA UNAJISI PAMOJA NA WANAWAKE, KWA MAANA NI BIKIRA. Hawa ndio wamfuatao Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamenunuliwa katika wanadamu, malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.

5  NA KATIKA VINYWA VYAO HAUKUONEKANA UONGO. MAANA HAWANA MAWAA

Kama tunavyoweza kuona hapo tabia za wale walioweza kuuimba wimbo huo ni mbili;

  1. Hawakutiwa unajisi na wanawake.

Hapo hamaanishi kuwa hawakuwa wazinzi, hapana, (ni kweli uzinzi sio jambo lao) bali anamaanisha hasaa uzinzi wa rohoni, yaani Kumwabudu Mungu pamoja na sanamu. Na sanamu kwa wakati wetu si tu vile vinyago vya kuchonga tu, bali pia ni kitu chochote kinachochukua nafasi ya Mungu wako moyoni. Wengine mali, wengine tv,  wengine mipira, wengine elimu, wengine ma-magemu, wengine ushirikina, wengine udhehebu. Hizo ni sanamu, unapozidhibiti wewe kama mkristo hiyo ni hatua mojawapo ya kuweza kuuimba wimbo huo mpya.

Lakini anasema..

  1. Katika vinywa vyao haukuonekana uongo, maana hawana mawaa.

Ni watu walionena kweli yote ya  Mungu (injili ya Kristo), wala hawakuibatilisha kwa ajili ya fedha, au maslahi, au cheo, au unafki au wafuasi. Bali waliitetea kweli yote ya Mungu na kuiishi pia, . Maana yake mimi na wewe tukiinena kweli ya Kristo na kuiishi, basi vinywani mwetu tunakuwa hatuna uongo.

Na matokeo ya mtu wa jinsi hii, ni kwamba anakuwa nafasi maalumu sana mbinguni(Ufunuo 5:8-9), Ni sawa na leo unajisikiaje unapoitwa uishi ikulu na raisi wako? Unajisikiaje kila mahali aendapo na msafara wake wewe upo pamoja naye. Anapopokea heshimu, na wewe unapokea naye.

Hivyo bidii ina malipo. Nyakati tulizonazo sio kusema nimeokoka hiyo inatosha!.. Ni nyakati za kujifunza wimbo huu mpya kwa bidii. Kutijahidi kumpendeza Bwana. Na yeye mwenyewe ameahidi neema yake itatusaidia.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KARAMU YA MWANA-KONDOO.

JE! NI DHAMBI KUIMBA WIMBO WA TAIFA?

Nanyi mtamweka hata siku ya kumi na nne ya mwezi ule ule(Kutoka 12:4)

Rudi Nyumbani

Print this post

Machela ni nini (Wimbo ulio bora 3:7)

Jibu: Turejee…

Wimbo 3:7 “Tazama, ni MACHELA yake Sulemani; Mashujaa sitini waizunguka, Wa mashujaa wa Israeli”

“Machela” yanayozungumziwa hapo si vile vitanda vinavyotumika zama hizi kwaajili ya kubebea wagonjwa walio mahutihuti!..Bali vilikuwa ni vitanda maalumu vilivyotumika kubebea Wafalme na Mamalkia enzi za zamani, walipotembea kutoka sehemu moja kwenda nyingine (umbali mfupi).

Kutokana na zama kubadilika, matumizi ya Machela kubebea wakuu wa nchi hayapo tena, bali sasa yanatumika magari ya kimakenika, na Machela yamebaki kuwa na matumizi ya kubebea wagonjwa wa dharura walio katika hali ya umahutihuti,..na zaidi sana Machela za zama hizi yana magurudumu na hayabebwi tena kwa mikono kama yale ya zamani.

Kasoro moja ya Machela ya zama za zamani ambayo yaliwabeba wafalme ni kwamba hayakuwa na uimara wa kutosha, kiasi kwamba ikitokea ajali kwa waliombeba bali yule aliyebebwa anaweza kuanguka, na pia kwasababu mwendo wa wanadamu unatofuatiana, hivyo basi hata aliyebebwa wakati wa safari atahisi hali ya kupanda na kushuka, au kurushwa rushwa, na kupepesuka na hivyo yupo hatarini saa yoyote kuanguka..

Na vivyo hivyo, dunia imefananishwa na mfalme aliyebebwa kwenye machela, anawaya-waya, anapepesuka wakati wowote yupo hatarini kuanguka (yupo katika wasiwasi).

Isaya  24:19 “Dunia kuvunjika, inavunjika sana; dunia kupasuka, imepasuka sana; dunia kutikisika, imetikisika sana.

20 Dunia inalewa-lewa kama mlevi, NAYO INAWAYA-WAYA KAMA MACHELA; na mzigo wa dhambi zake utailemea; nayo itaanguka, wala haitainuka tena.

21 Tena itakuwa katika siku hiyo, Bwana ataliadhibu jeshi la mahali palipo juu katika mahali palipo juu, na wafalme wa dunia katika dunia”

Kama dunia inawaya-waya, ya nini kuitumainia??.. Na kwanini inawaya-waya?..ni kwasababu imekaribia mwisho wake, wakati wowote inaisha…na kinachoifanya iwayewaye si kingine Zaidi ya Dhambi, iliyojaa ndani yake.

Kwa urefu zaidi kuhusu kuwaya-waya kwa dunia fungua hapa >>> Dunia inalewa-lewa kama mlevi, nayo inawaya-waya kama machela.

Je umempokea YESU maishani mwako?..au na wewe unawaya-waya na dunia?…anasa zimekutawala, udunia umekushika..ni wakati sasa wa kuikimbia dunia na mambo yake na kumfanya BWANA YESU kuwa msingi wa maisha yako.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TOA HUDUMA ILIYO BORA.

Podo ni nini na umuhimu wake ni upi rohoni?

KWA KUWA ROHO BORA ILIKUWA NDANI YAKE.

Kimiami ni nini? (Wimbo ulio bora 2:9).

INGIENI KWA KUPITIA MLANGO ULIO MWEMBAMBA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kusanyiko la makini/ mkutano wa makini ni upi?

Katika agano la kale, Israeli walikuwa na makusanyiko mengi, ambapo walikutanika kumfanyia Mungu ibada, na kuzishika sikukuu. Lakini pia yalichaguliwa makusanyiko mengine yaliyoitwa mikutano/makusanyiko ya makini. Makusanyiko haya yalifanyika  katika siku ya saba ya sikukuu ya Pasaka, na siku ya nane, baada ya sikukuu ya vibanda. Katika siku hiyo hawakuruhusiwa kufanya kazi yoyote. Bali ilitengwa kwa ajili ya kujitakasa, au kujisogeza karibu na Mungu,

Hivi ni vifungu baadhi vinavyoielezea siku hiyo;

Hesabu 29:35 Tena siku ya nane mtakuwa na kusanyiko la makini sana; hamtafanya kazi yo yote ya utumishi;

36 lakini mtasongeza sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya kusongezwa kwa moto, harufu ya kupendeza kwa Bwana; ng’ombe mume mmoja, na kondoo mume mmoja, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza wakamilifu saba.

Walawi 23:34 Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Siku ya kumi na tano ya mwezi huo wa saba ni sikukuu ya vibanda muda wa siku saba kwa Bwana.

35 Siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko takatifu; msifanye kazi yo yote ya utumishi.

36 Mtamsongezea Bwana sadaka kwa moto siku saba; siku ya nane kutakuwa na kusanyiko takatifu kwenu; nanyi mtamsongezea Bwana sadaka kwa moto; ni mkutano wa makini huu; msifanye kazi yo yote ya utumishi

Kumbukumbu 16:8 Siku sita utakula mikate isiyotiwa chachu; na siku ya saba na uwe mkutano mtukufu kwa Bwana, Mungu wako, usifanye kazi yo yote.

Huo mkutano mtukufu ndio kusanyiko la makini.

Hekalu la kwanza pia lilipomalizika liliwekwa wakfu katika siku hii ya kusanyiko la makini

2Nyakati 7:9 Hata siku ya nane wakaita kusanyiko la makini; kwa maana walishika kuitakasa madhabahu siku saba, na sikukuu siku saba.

Sehemu  nyingine mikusanyiko hii iliitishwa rasmi, kwa lengo la kujimimina kwa Mungu kuomba, kwa ajili ya maovu na majanga ambayo yanaipata nchi. (Yoeli 1:14 – 2:15). Kusanyiko hili liliitwa pia kama kusanyiko  kuu.

Je! Ufunuo wake ni upi leo?

Kama vile tulivyo na mikusanyiko ya aina mbalimbali leo, mfano  ya shule ya jumapili, ya semina, ya injili n.k. Vivyo hivyo hatuna budi kuwa na makusanyiko ya makini. Ambayo ni mikusanyiko ya mifungo na maombi. Ambapo tunapata muda wa kujimimina kwa undani kabisa uweponi mwa Mungu, kumtaka aingilie kati mambo yetu.

Je! unaithamini? Mungu aliyesema tusiache kukusanyika pamoja (Waebrania 10:25). Hakumaanisha tu mikusanyiko ya jumapili, lakini pia ya mifungo na maombi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

NYOSHA MKONO WAKO, UUGUSE MFUPA WAKE NA NYAMA YAKE.

Shetani huwa ana kauli zake, za uongo ambazo hupenda kuwaaminisha watu, kuwa kuna mambo mwanadamu hawezi kuyafanya akiwa hapa duniani hata iweje.

Tukisoma habari ya Ayubu wakati ule shetani alipokwenda kumshitaka kwa Mungu.

Mungu alipomuuliza kuhusu mwenendo wake, majibu ya shetani yalikuwa ni kwamba Mungu amemzungushia wigo, kutunza alivyonavyo, Na kama atapotezewa alivyonavyo, basi atamkufuru Mungu waziwazi. Hivyo Mungu akaruhusu shetani amjaribu Ayubu, amchukulie alivyo navyo vyote, lakini uongo wa kwanza, ukashindwa, alipoona Ayubu anamtukuza Bwana katika misiba yake. Hiyo ni kuonyesha kuwa mwanadamu yoyote anaweza  kuishi bila msukumo wa mali,wala mtu wala kitu chochote katika hii dunia.

Lakini baadaye tena, akaendelea mbele kuzungumza uongo mwingine, alipoona Ayubu bado yupo na Mungu, akamwambia Mungu, yote yanawezekana kwa mwanadamu kuvumilia, lakini hili la kuugusa mfupa wake,kumtesa, kamwe hawezi kuvumilia atakukufuru tu. Mimi ninawajua wanadamu uwezo huo hawana, nilishawafundisha pia huko duniani.

Ayubu 2:4 Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Ngozi kwa ngozi, naam, yote aliyo nayo mtu atayatoa kwa ajili ya uhai wake.

5 Lakini sasa nyosha mkono wako, uuguse mfupa wake na nyama yake, naye atakukufuru mbele za uso wako.

6 Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yeye yumo mkononi mwako; lakini tunza tu uhai wake.  7 Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana, akampiga Ayubu na majipu mabaya tangu wayo wa mguu hata utosi wa kichwa.

8 Naye akashika kigae cha kujikunia; akaketi majivuni.  9 Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washikamana na utimilifu wako? Umkufuru Mungu, ukafe.

10 Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake.

Hilo nalo likashindikana. Kumbe mtu, hata kuupoteza uhai wake kwa ajili ya Kristo, linawezekana.

Ni nini Bwana anatufundisha kwa mawazo ya adui kwetu sisi ?

Leo hii ni rahisi sana kusikia, kauli kama, hakuna mtakatifu duniani! Ni rahisi kuona mtu anaanguka ovyo katika dhambi, na kutumia kisingizio kuwa yeye sio malaika. Utasikia kauli kama haiwezekani mtu kuacha vyote alivyonacho kwa ajili ya Kristo. Ndugu tambua kuwa hizo ni kauli za ibilisi ndani ya moyo wako. Adui anapenda kumshusha thamani mtu, kumweka kama kiumbe ambaye hawezi kujisimamia, hafundishiki, haaminiki.

Ni kweli mwanadamu kuwa na ukamilifu wa Mungu haiwezekani (Ndio sababu Yesu akaja kutukomboa), lakini kuna viwango Fulani Mungu anajua tunaweza kuvifikia, akalithibitisha hilo kwa Ayubu. Kama Ayubu ameweza kwanini wewe ushindwe, usijishushe thamani.

Neema haijaja kutuambia kuwa sisi hatuwezi, bali  imekuja kutuwezesha zaidi kuwa wakamilifu mbele za Mungu, yaani pale Ayubu aliposhindwa sisi tunasaidiwa kwa hiyo, na kutufanya tupokelewe kikamilifu mbele za Mungu, hiyo ndio kazi ya Neema (Soma Tito 2:11-12).

Kamwe usiruhusu hayo maneno ya kushushwa thamani na ibilisi, kwamba wewe huwezi mpendeza Mungu, huwezi kuacha vyote kwa ajili yake. Yesu  alisema tutakuwa wakamilifu kama Baba yetu alivyomkamilifu. Tunachopaswa kufanya ni kuamini kuwa hilo linawezekana na kuonyesha bidii katika hilo kumpendeza yeye. Na neema ya Mungu itatusaidia kufikia kilele Hicho cha juu kabisa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

ILI TUONEKANE WAKAMILIFU MBELE ZA MUNGU.

Kwanini Labani aseme Yakobo ni Mfupa wake na nyama yake?(Mwanzo 29:14)

Rudi Nyumbani

Print this post

IFAHAMU KANUNI YA KUTAKA NA KUPATA.

Warumi 7:18  “Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema; kwa kuwa KUTAKA NATAKA, bali KUTENDA LILILO JEMA SIPATI.

19  Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo”.

Je na wewe ni miongoni mwa watu wanaosumbuliwa na utumwa wa namna hiyo?.. UNATAKA na kutamani lakini unajikuta HUPATI au HUWEZI au HUFANYI au HUPOKEI?.

> Unataka kumtumikia Mungu lakini unajikuta huwezi..

> Unataka kuwa msomaji wa Neno lakini unajikuta hufanikiwi.

> Unataka na kutamani kufanya mema na mazuri kwaajili ya Mungu wako lakini hufanikiwi n.k

Kama UMETAKA mambo mengi na huoni uelekeo wa kulipata, basi huwenda NJIA unayoitumia kutaka na kutafuta hayo mambo ina kasoro..

Hebu jaribu njia hii, ya kutaka mambo halafu uone kama hutapata uyatakayo,

Na njia hii si nyingine Zaidi ya ile aliyoitumia Danieli.

Danieli 9:3 “Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ILI KUTAKA kwa MAOMBI, NA DUA, PAMOJA NA KUFUNGA, NA KUVAA NGUO ZA MAGUNIA NA MAJIVU. 

4 Nikamwomba Bwana, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake”

Umeona kanuni Danieli aliyoitumia??… HAKUTAKA mambo kwa kupiga ramli, au kwenda kwa waganga wa kienyeji, wala kwa kwenda Kuwadhulumu watu au kukorofishana na watu au kula rushwa, au kujipendekeza kwa watu bali KWA MAOMBI, NA DUA NA KUFUNGA NA KUVAA NGUO ZA MAGUNIA NA MAJIVU, na matokeo yake alipata alichokuwa anakitafuta..

Na sisi tunajifunza mambo hayo hayo…

> Tukitaka Amani nyumbani.. kanuni ni hiyo > Kufunga na Kuomba.

> Tukitaka Amani katika ndoa.. Kanuni ni hiyo > Kufunga na Kuomba.

> Tukitaka Amani kazini.. Kanuni ni hiyo > Kufunga na Kuomba.

> Tukitaka Akili darasani.. Kanuni ni hiyo > Kufunga na Kuomba.

> Tukitaka Ulinzi na afya.. Kanuni ni hiyo > Kufunga na Kuomba.

> Tukitaka Ujazo wa Roho Mtakatifu.. Kanuni ni hiyo > Kufunga na Kuomba.

Luka 11:13 “Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?”

Kama Bwana YESU alivyosema kuwa “kuna mambo hayawezekaniki, isipokuwa kwa kufunga na kuomba”

Wafilipi 2:13 “Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, KUTAKA KWENU na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.

14  Yatendeni mambo yote pasipo manung’uniko wala mashindano”

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KANUNI JUU YA KANUNI.

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.

Nini maana ya “Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi”?

HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.

Rudi Nyumbani

Print this post

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA MFUNGO.

Yafuatayo ni mambo saba (7) ya kuzingatia wakati wa Mfungo.

1.MAOMBI

Mfungo wowote ili uwe ni mfungo ni lazima uambatane na Maombi.. Mfungo usiokuwa na maombi ni sawasawa na bunduki isiyo na risasi.

Marko 9:28 “Hata alipoingia nyumbani, wanafunzi wake wakamwuliza kwa faragha, Mbona sisi hatukuweza kumtoa?

29  Akawaambia, Namna hii haiwezi kutoka kwa neno lo lote, isipokuwa kwa kuomba”.

Mathayo 17:21  [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]

Kila siku utakayofunga hakikisha unaomba, (tena maombi ya masafa marefu, tofauti na siku nyingine).

 2. KUWA MTULIVU.

Unapofunga usiwe mtu wa kuhangaika na kuzurura huku na kule, bali kuwa mtu wa faragha muda mwingi, wakati wa mfungo si wakati wa kuzurura kwenye makao ya watu, au vijiwe..kuwa mtulivu, tafuta maeno tulivu na omba.

3. ZUIA KINYWA.

Mfungo sio tu kujizuia kula na kunywa, bali pia kujizuia kuzungumza kupita kiasi…. Unapofunga si wakati wa kusema na kila mtu, si wakati wa kujiachia (hususani kwa watu wasio wa kiroho) bali ni wakati wa faragha wewe na Mungu wako (kwa kutafuta sauti ya Mungu kupitia maneno yake)

4. EPUKA MATENDO YA MWILI.

Kama ni mwanandoa jizuie kwa kiwango kikubwa au chote kukutana kimwili na mwenzi wako..Vile vile Kama unafanya shughuli fulani inayohusisha mwili wako, ipunguze kwa kiwango kikubwa..

5. PUNGUZA KIWANGO CHA KULA.

Mfungo sio kuhamisha mlo wa asubuhi na mchana na kuupeleka jioni..La! bali ni  kuunyima mwili ili roho yako ije juu (inufaike).. Maana yake wakati wa kufungua (kufuturu) usile kiwango kikubwa cha chakula, kwa kufidia mlo wa asubuhi na mchana.. Ukifanya hivyo utakuwa hutendi dhambi, lakini mfungo wako unaweza usiwe na matokeo makubwa kama wa yule ajizuiaye kweli kweli.

6.USILE VYAKULA VITAMU-TAMU.

Wakati wa kufungua epuka kula vyakula vitamu tamu, hususani vile unavyovipenda sana, ambavyo vinakuburudisha sana.. “Kumbuka tena mfungo ni kuunyima mwili na si kuupendeza mwili”… Sasa unapoupa vile vitu ambavyo unavipenda sana, hapo bado kuna kaukasoro katika mfungo wako..

Danieli alikuwa ni mtu aliyejinyima vitu vitamu wakati wa mfungo… na hatimaye mfungo wake ukawa na matokeo makubwa.

Danieli 10:2 “Katika siku zile mimi, Danielii, nalikuwa nikiomboleza muda wa majuma matatu kamili.

3 Sikula chakula kitamu, wala nyama wala divai haikuingia kinywani mwangu, wala sikujipaka mafuta kabisa, hata majuma matatu kamili yalipotimia”.

7. USIWE MTU WA KUJITANGAZA.

Mathayo 6:16 “Tena mfungapo, msiwe kama wanafiki wenye uso wa kukunjamana; maana hujiumbua nyuso zao, ili waonekane na watu kuwa wanafunga. Amin, nawaambia, wamekwisha kupata thawabu yao.

17  Bali wewe ufungapo, jipake mafuta kichwani, unawe uso;

18  ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila na Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.

Mfungo unapaswa uwe siri hususani kwa watu walio wa nje (yaani wasiohusiana na wewe).. Kwa ndugu yako wa karibu sana, au mke au mume au watoto, mfungo wako ni ngumu kuwa siri kwao, kwasababu unaishi nao katika maisha ya kila siku (hata usipowaambia watafahamu tu)..Hivyo unaweza kuwashirikisha ikiwa lengo lako si upokee utukufu kutoka kwao.

Vile vile kiongozi wako wa kiroho, au mpendwa mwenzako (wa Imani moja na wewe) unaweza kumshirikisha mfungo wako (ikiwa lengo lako si kupata utukufu kutoka kwake) bali kupokea hamasa au kumhamasisha (Hilo ni jambo jema).

Lakini kama lengo lako ni wewe uonekane kwao ili utukuzwe, basi mfungo huo unaweza usizae matunda yale mtu anayoyategemea..

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?

Kwanini tunafunga na kuomba?

KWARESMA IPO KIMAANDIKO?

JUMATANO YA MAJIVU NI TENDO LA KIMAANDIKO?

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

Rudi Nyumbani

Print this post

TUNAPASWA TUWEJE WAKATI WA KUJA KWAKE  BWANA YESU?.

Ipo hali ambayo tunapaswa tukutwe nayo wakati wa kuja kwake Bwana YESU…na endapo akitukuta tupo nje na hiyo hali basi hatutaenda naye, badala yake tutabaki na kukumbana na hukumu ya MUNGU.

Sasa “hali” hiyo ni ipi?..

Hebu tusome maandiko yafuatayo.

1 Wathesalonike 5:23 “Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, WAKATI WA KUJA KWAKE BWANA WETU YESU KRISTO”.

Kumbe Bwana YESU atarudi tena!!!!….. na wakati atakaporudi anatazamia  tuwe tumetakasika katika maeneo hayo matatu 1) NAFSI 2) ROHO na 3)MWILI.

Vinginevyo mambo hayo matatu yasipokuwa masafi wakati wa kuja kwake Bwana YESU basi kuna hatari kubwa sana.

1.NAFSI.

Ndani ya nafsi kuna maamuzi, hisia na mawazo.. Hivi vinapaswa viwe visafi daima.

Na vinakuwaje visafi?… Kwa kumpokea YESU, kusoma Neno na kuomba.

Usipokuwa mwombaji nafsi yako haiwezi kuwa safi utakuwa mtu wa hasira tu, mtu wa uchungu tu..usipokuwa msomaji wa Neno la Mungu kamwe nafsi yako haiwezi kustahimili majaribu na pia utakuwa mtu usiye na mwongozo n.k.

2.ROHO.

Ndani ya roho ya mtu kuna uzima, na ndio chumba pekee cha ibada ambacho kinaongozwa na Imani. 

Roho ya mtu isipokuwa safi, mtu huyo hawezi kwenda na Bwana siku ya unyakuo…na hata maisha yake ya duniani hawezi kumwona Mungu.

3. MWILI.

Mwili ni vazi la roho ya mtu, na ndilo limejumuisha viungo vyote vya ndani na nje.

Na mwili unapaswa uwe safi (usafi wa kimatendo)..Mwili mchafu kibiblia sio ule wenye jasho au vumbi…mwili mchafu ni ule unaofanya uasherati na zinaa, ni ule unaojichua, ni ule unaotembezwa uchi barabarani, ni ule unaoshika fedha za wizi na utapeli.

Huo ndio mwili mchafu, ambao kama hautatakaswa wakati wa kuja kwake Bwana utampoteza mtu huyo.

Na mtu hautakasi mwili wake kwa kuoga na maji moto, au kwa kumeza vidonge vya matibabu au mitishamba…bali kwa kuacha matendo yote ya mwili yanayotajwa katika Wagalatia 5:19-20.

Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, 

20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, 

21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.

Kwa hitimisho ni kwamba kila mtu lazima ajitakase na kuhifadhi utakaso wake ambao ndio tiketi ya kumwona Bwana siku atakaporudi.

1 Wathesalonike 5:23 “Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, WAKATI WA KUJA KWAKE BWANA WETU YESU KRISTO”.

Je umempokea Bwana YESU?…Kama bado unasubiri nini??… Na kama tayari umeshampokea je! umetakaswa nafso yako, roho yako na mwili wako?..

Kwa mwongozo wa maombi ya kujijenga kiroho juu ya mambo hayo matatu (nafsi, mwili na roho) basi wasiliana nasi inbox.

Maran atha!.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MCHE MWORORO.

KWANINI TUNAPASWA KWENDA KUIHUBIRI INJILI KWA UJASIRI WOTE?

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

JITAHIDI KUJA KABLA YA WAKATI WA BARIDI.

Biblia inamaanisha nini kusema Yeye aliye na sikio, na asikie?

Rudi Nyumbani

Print this post