Swali: Je ni kweli biblia ni Neno la Mungu?
Kabla ya kujibu kwanini biblia ni Neno la Mungu, na si kitabu kingine chochote?… hebu tujiulize kwanza na tujadili kwanini
Biblia ni Neno la Mungu kwasababu lina maneno yaliyo hai..
Vivyo hivyo biblia ni kitabu cha Mungu, kwasababu kimebeba taarifa sahihi kumhusu Mungu.. Na taarifa KUU ndani ya kitabu hiko kitukufu, ni taarifa ya mwanadamu kuondolewa dhambi kupitia YESU KRISTO (Hiyo ndiyo taarifa kuu) ambayo inaleta “UZIMA WA MILELE KWA MTU”..Na ndio karama kuu ya MUNGU kwetu.
Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.
Vitabu vingine vyote vilivyosalia havijabeba suluhisho lolote la ondoleo la dhambi za Mtu, badala yake zimebeba tu taarifa za maadili, au staha, mambo ambayo yanapatikana hata katika vitabu vya sheria za nchi.
Lakini taarifa na njia ya ondoleo la dhambi zipo katika BIBLIA TU PEKE YAKE!!!..
Kwasababu “dhambi” ndio sumu pekee ya mwanadamu, na hiyo ndio kizuizi kikubwa cha mtu kumkaribia Mungu, hivyo mtu akiondolewa hiyo anakuwa ameokoka! Hata kama maisha yake hapa duniani bado yanaendelea.
Na ni kwa njia gani mtu anaondolewa dhambi zake moja kwa moja??
Matendo 2:36 “ Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo.
37 Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
38 Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, NANYI MTAPOKEA KIPAWA CHA ROHO MTAKATIFU”.
Kanuni ya kuondolewa dhambi, ni kutubu na kubatizwa (Marko 16:16). Na toba halisi ni ile inayotoka moyoni yenye madhamirio ya kugeuza mwelekeo moja kwa moja. Na ubatizo sahihi ni ule wa maji mengi (Yohana 3:23) na kwa jina la BWANA YESU (Matendo 8:16, na Matendo 19:5).
BWANA YESU AKUBARIKI.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
JIPE NAFASI KATI YA TAARIFA UNAYOIPOKEA NA MAAMUZI UNAYOYATOA.
UNYAKUO WA KANISA UMEPITA LEO!!
Jibu: Turejee…
Waamuzi 1:16 “Hao wana wa Mkeni, HUYO SHEMEJI YAKE MUSA, wakakwea juu kutoka katika huo mji wa mitende, pamoja na wana wa Yuda, na kuingia hiyo nyika ya Yuda, iliyo upande wa kusini wa Aradi; nao wakaenda na kukaa pamoja na watu hao”.
Wakeni walikuwa ni jamii ya watu waliokuwa wanaishi katika nchi ya “Midiani” (karibu na jangwa la Sinai).. Kwa urefu kuhusiana na waMidiani fungua hapa >>Midiani ni nchi gani kwasasa?.
Miongoni mwa hawa waMidiani ndiko alikotokea Babamkwe wake Musa aliyeitwa Yethro au jina lingine Rueli.. Huyu Yethro/Reueli ndiye aliyemzaa Sipora aliyekuwa mkewe Musa.
Na huyu Yethro alikuwa na watoto wengine wa kiume mbali na wale mabinti wake saba tunaowasoma katika Kutoka 2:16, na mmoja wa mtoto wake wa kiume aliitwa “Hobabu” ambaye sasa “ndiye shemeji yake Musa (maana yake kaka yake Sipora, mke wa Musa)”.
Huyu Hobabu shemeji yake Musa alikataa kusafiri na wana wa Israeli, kwani wana wa Israeli walimtumaini yeye awatangulie njia kwani aliifahamu Zaidi, lakini alikataa kama maandiko yanavyosema..
Lakini maandiko mbeleni yanaonyesha alikubali, kwani uzao wake ulionekana ndani ya nchi ya Ahadi
Hesabu 10: 28 “Ndivyo zilivyokuwa safari zao wana wa Israeli kwa majeshi: yao; nao wakasafiri kwenda mbele.
29 Kisha Musa akamwambia Hobabu, mwana wa Reueli Mmidiani, mkwewe Musa, Sisi twasafiri kwenenda mahali ambapo Bwana amenena habari zake hivi, Nitawapa ninyi mahali hapo; uje pamoja nasi, nasi tutakufanyia mema; kwa kuwa Bwana ametamka mema juu ya Israeli.
30 Naye akamwambia, Siendi mimi; ila nitairudia nchi yangu mwenyewe, na kwa jamaa zangu mwenyewe.
31 Naye akamwambia, Usituache, tafadhali; kwa kuwa wewe wajua jinsi tutakavyopanga nyikani, nawe utakuwa kwetu badala ya macho.
32 Itakuwa, ukienda pamoja nasi, naam, itakuwa mema yo yote Bwana atakayotutendea sisi, tutakutendea wewe vivyo
34 Na wingu la Bwana lilikuwa juu yao mchana hapo waliposafiri kwenda mbele kutoka kambini.
35 Ilikuwa, hapo sanduku liliposafiri kwenda mbele, ndipo Musa akasema, Inuka, Ee Bwana, adui zako na watawanyike; na wakimbie mbele zako hao wakuchukiao”.
Kwa funzo refu kuhusiana na habari hii ya Hobabu na Musa fungua hapa >>>>Kwanini Musa amtake Hobabu na tayari kulikuwa na Wingu linalowaongoza?
Kwahiyo huyu Hobabu ndiye aliyekuwa shemeji yake Musa na wanawe (yaani watoto wake) ndio hao wanaotajwa hapo katika Waamuzi 1:6 na Waamuzi 4:11 na pia wanatajwa katika sehemu mbali mbali za biblia.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kuiaua Nchi ni kufanya nini? (Waamuzi 18:2).
BWANA NITIE NGUVU TENA. (Waamuzi 16:28)
MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)
Swali: Kwanini Nabii Musa amtake Hobabu (shemeji yake) kama dira yake ya kuelekea Kaanani na tayari Mungu alishawafunulia juu yao nguzo ya wingu wakati wa mchana na Nguzo ya moto wakati wa usiku kama dira yao na kama kitu cha kuwaongozea?
Jibu: Lipo jambo kubwa sana hapa la kujifunza..
Awali ya yote kama bado hujamfahamu Hobabu ni nani na inakuwaje awe shemeji yake Musa fungua hapa >>>Huyu Mkeni shemeji yake Musa alikuwa ni mtu wa namna gani? (Waamuzi 1:16)
Sasa kwa muhtasari ni kwamba kipindi wana wana wa Israeli wanatoka Misri kuelekea Kaanani, ni kweli Bwana aliwapa wingu na nguzo ya moto iwaongoze mchana na usiku.
Lakini Zaidi ya hayo Musa alitafuta tena mtu ambaye atamwongoza njia yao kuelekea nchi ya ahadi.. sasa swali ni alifanya makosa?… na tena akataka kumfanya kama “Macho” katika safari hiyo..
Waamuzi 10:28 “Ndivyo zilivyokuwa safari zao wana wa Israeli kwa majeshi: yao; nao wakasafiri kwenda mbele.
29 Kisha Musa akamwambia Hobabu, mwana wa Reueli Mmidiani, mkwewe Musa, Sisi twasafiri kwenenda mahali ambapo Bwana amenena habari zake hivi, Nitawapa ninyi mahali hapo; uje pamoja nasi, nasi tutakufanyia mema; kwa kuwa Bwana ametamka mema juu ya Israeli.
30 Naye akamwambia, Siendi mimi; ila nitairudia nchi yangu mwenyewe, na kwa jamaa zangu mwenyewe.
31 NAYE AKAMWAMBIA, USITUACHE, TAFADHALI; KWA KUWA WEWE WAJUA JINSI TUTAKAVYOPANGA NYIKANI, NAWE UTAKUWA KWETU BADALA YA MACHO.
32 Itakuwa, ukienda pamoja nasi, naam, itakuwa mema yo yote Bwana atakayotutendea sisi, tutakutendea wewe vivyo
34 NA WINGU LA BWANA LILIKUWA JUU YAO MCHANA HAPO WALIPOSAFIRI KWENDA MBELE KUTOKA KAMBINI.
35 Ilikuwa, hapo sanduku liliposafiri kwenda mbele, ndipo Musa akasema, Inuka, Ee Bwana, adui zako na watawanyike; na wakimbie mbele zako hao wakuchukiao”.
Jibu ni La!.. Musa hakuwa Mjinga, wala hakuwa mtu wa kumtegemea Mwanadamu.. Daima alijua Mungu ndiye Ngao yake na watu wake, na wala hakuna mtu yeyote awezaye kumsaidia kazi. Lakini Nabii Musa alifikiri Zaidi, Alijua watu aliona ni watu wenye mioyo migumu, na shingo ngumu.
Alijua Imani yao kwa Mungu ilikuwa ni ndogo, na wengi wao ni watu wa mwilini, na alijua wasipopata mtu wa kuwapanga vyema kule nyikani, aliyemzoefu wa jangwa na njia, zitanyanyuka shida nyingi na hatimaye watamkufuru Mungu na kuadhibiwa wote.
Hivyo kwa faida ya watu wasiangamia aliwatafutia mwalimu wa mwilini ili awaongoze, na kuwafundisha jinsi ya kukaa jangwani, na hiyo ikawa dawa kwa sehemu kubwa sana.
Na utaona hii familia ya Yethro (babamkwe wake Musa na mashemeji zake), ilikuwa msaada mkubwa sana kiushauri katika safari ya wana wa Israeli jangwani na kwa Musa kwa ujumla. Kwani kipindi ambacho Musa alikuwa anawaamua watu wote peke yake kuanzia asubuhi mpaka jioni, alipokuja huyu babamkwe wake alimpa ushauri bora sana wa kuweka wakuu wa maelfu, wakuu wa mahamsini na wakuu wa mamia na wakuu wa makumi (Soma Kutoka 18:12-27).
NINI TUNAJIFUNZA KWA MUSA:
Musa alikuwa na “Macho juu” ambaye ni Roho Mtakatifu juu (kama wingu likimwongoza na watu wake) lakini pia alikuwa na “macho chini” (Hobabu, shemeji yake) kwaajili ya watu wake. Mambo haya yanaenda pamoja..
Wewe kwama Mzazi, unaye Roho Mtakatifu anayekuongoza wewe na familia yako kama Macho ya Juu, lakini hayo hayatoshi pekee, ni lazima watoto wako uwapatie waalimu watakaowafundisha njia za Roho Mtakatifu katika mashule yao waliopo, katika makanisa yao, katika shughuli zao n.k
Ukisema utawaacha na kuongozwa na Roho Mtakatifu kama wewe uongozwavyo, utawapoteza…wawekee waalimu.
Vilevile Mtumishi wa Mungu weka waalimu kwa watoto wako wa kiroho, weka wachungaji watakaowaangalia, itakuwa afya na heri kwao.
Bwana atusaidie
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
KAZI ZA ROHO MTAKATIFU
Je Musa kumwoa Sipora, Mkushi alifanya dhambi?
Katika biblia zipo aina mbalimbali za kumsifu Bwana, lakini kuna kuu saba ambazo zilitambuliwa na wayahudi kwa wakati wote. Hivyo ni vema kuzifahamu ili wigo wako uwe mpana zaidi katika eneo hili la sifa. Kwasababu ndio huduma kuu tuliyonayo duniani kwa Mungu wetu. Kumbuka chakula chetu ni Neno, lakini chakula cha Mungu wetu ni Sifa zetu. Hivyo ni lazima tujue tunamsifuje yeye kiufasaha kwa jinsi apendavyo.
Hizi ni aina saba za sifa.
Hii ni aina ya kumsifu Mungu ambayo, mwimbaji hujidai, hujigamba mbele za Mungu wake kwa kuuhusisha mwili wake, yaweza kuwa kuruka kuruka, au kucheza.
Agizo hilo lipo katika Zaburi 149:3 Na walisifu jina lake kwa kucheza, Kwa matari na kinubi wamwimbie.
Ndio lile Daudi na Israeli wote walilolifanya walipokuwa wanalileta sanduku la Bwana Yerusalemu,
2Samweli 6:14 Daudi akacheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote; na Daudi alikuwa amevaa naivera ya kitani.
15 Basi Daudi na nyumba yote ya Israeli wakalileta sanduku la Bwana kwa shangwe, na kwa sauti ya tarumbeta.
16 Ikawa, sanduku la Bwana lilipoingia mji wa Daudi Mikali, binti Sauli, akachungulia dirishani, akamwona mfalme Daudi akiruka-ruka na kucheza mbele za Bwana; akamdharau moyoni mwake.
Hivyo na wewe kama mtu uliyeokolewa na Kristo, kujidai kwa ujasiri wote mbele ya Mungu wako usijizuie, angalizo tu ni kwamba usifanye kidunia, kana kwamba unacheza dansi, huku moyoni mwako hakuna ibada. Hiyo sio sawa, lakini kumwimbia Mungu kwa kucheza hakuna kosa lolote ikiwa ni jambo la kububujika moja kwa moja kutoka moyoni mwako.
Hii ni aina ya kumsifu Mungu kwa kuinua mikono juu, Kama ishara ya kutambua tegemeo lako kwake, kama mtoto mdogo kwa mzazi wako anapomlilia. Na kuonyesha upendo wako wa dhati kwa Mungu wako.
Zaburi 63: 3 Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai; Midomo yangu itakusifu. 4 Ndivyo nitakavyokubariki maadamu ni hai; Kwa jina lako nitaiinua mikono yangu.
Kama mtakatifu jizoeze mara nyingi, kunyanyua mikono yako juu wakati unamwabudu Mungu, au wakati mwingine unapoomba. Binafsi, nimeona tofauti kubwa sana, niinuapo mikono yangu, pindi niombapo au nisifupo, najikuta nazama rohoni kwa haraka sana, zaidi ya napoweka mikono yangu chini. Kumbuka ile habari ya Musa, alipoinua mikono juu, Israeli ilishinda, lakini alipoweka mikono chini, Waamaleki walishinda. (Kutoka 17:11) Hivyo jifunze sana, kuiinua mikono yako juu, katika ibada zako.
Hii ni aina ya kumsifu Mungu kwa kumbariki Mungu, lakini kwa kuonyesha heshima kubwa kama mfalme, kujishusha chini, kusujudu au kupiga magoti, kuonyesha yeye ni mkuu sana wa kuogofya zaidi ya wafalme wote na wakuu wote ulimwenguni.
Zaburi 5:7 Bali mimi, kwa wingi wa fadhili zako, Nitaingia nyumbani mwako; Na kusujudu kwa kicho, Nikilielekea hekalu lako takatifu.
Kama mwamini, sifa zako zisiwe za mdomo tu wakati wote, jifunze kupiga magoti, au kusujudu ni ishara ya unyenyekevu wa hali ya juu. Fanya hivyo nyakati za sifa, nyakati za maombi.
Aina ya kusifu moyoni mwako, kwa namna isiyo na maandalizi Fulani maalumu, mfano wa kwaya, ni nyimbo ambazo zitainuka katikati ya mapito yako fulani, wakati mwingine unapopitia kutendewa mema mengi na Mungu, na hapo ghafla tu moyoni mwako unasikia kumsifu Mungu, kumpa utukufu.
Kwamfano Daudi alipokuwa anapitia magumu,au anashindaniwa na Mungu, akimtafakari Mungu, mara anaachilia kinywa chake, Mungu anaanza kububujisha nyimbo mpya ulimini mwake.
Mfano mwingine wa sifa kama hizi, ni pale Mungu alipowavusha wana wa Israeli, bahari ya Shamu, na kuona maadui zao wamefunikwa na habari, ndipo Israeli wote, pamoja na Miriamu na wanawake wakasimama kumwimbia Mungu nyimbo za Furaha (Kutoka 15).
Mfano mwingine ni pale Mariamu alipomtembelea Elizabeti, na kutolewa unabii kuwa atamzaa Masihi, alishangalia na ghafla akafungua kinywa chake kwa wimbo, kumsifu Mungu kwa namna hii, (Luka 1:46-56)
Hivyo kila mkristo, katika majira yote, vipindi vyote, viwe vyepesi, viwe vingine, hana budi kutafakari na kufungua kinywa chake kumsifu Mungu kwa aina hii ya sifa ya Tehillah. Ni muhimu sana, na inampendeza, Mungu, hii haina maandalizi, haina mpangilio maalumu, hutoka moyoni mwako, kwasababu Fulani Mungu alizokuonekania.
Mungu aliwaagiza pia watu wake, wamwimbie si kwa vinywa vyao tu na makofi, lakini pia pamoja na kuchanganya zana mbalimbali za muziki.
Zaburi 150:3 Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi;
4 Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi; 5 Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.
6 Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana. Haleluya.
Ni wazi kuwa kuchanganya ala mbalimbali,kama vile gitaa, vinanda, filipi, tarumbeta, ngoma, zeze, marumba, n.k. Katika kumwimbia Mungu, huongeza ladha na hisia njema katika kumsifu, na hivyo hupendeza sana machoni pake. Wapo watu hawaamini katika matumizi ya vyombo. Lakini maandiko yanatuagiza tumsifu Mungu kwa hivyo.
Aina hii ya sifa, ni kwa kupaza sauti yako juu sana kwa Mungu. Hii Huonyesha ujasiri wa Mungu unayemwabudu, na kuutangazia umati na ulimwengu kuwa yupo Mungu mahali hapo anayeabudiwa.
Zaburi 47:1 Enyi watu wote, pigeni makofi, Mpigieni Mungu kelele kwa Sauti ya shangwe.
Sifa hizi zina nguvu sana, ndio zile ambazo ziliangusha kuta za Yeriko. Wana wa Israeli walipoambiwa wapaze sauti zao kwa Mungu. Zile sauti hayakuwa makelele tu, bali zilikuwa ni sauti za kumtukuza Mungu.(Yoshua 6:20).
Tumwimbiapo Mungu, hatupaswi tuwe kama mabubu, au tuimbe kinyonge, au kwa kutegea-tegea. Mungu anajivunia sana watu wale wanaomwabudu kwa ujasiri, kwa kufumbua vinywa vyao na kupaza sauti zao kwa nguvu kumwadhimisha yeye.
Ni aina ya sifa inayofanana na ile ‘Yadah’,ya kumwinulia Mungu mikono kumwimbia. Isipokuwa hii, ni kumwadhimisha Mungu, kwa matendo ambayo bado hujayaona kwa macho. Kutambua uweza wa Mungu, hata kama huoni matokeo yoyote, na kumshukuru katika hayo. Hata pale ambapo hujisikii. .
Mfano ya sifa hizi, ni labda wewe ni mgonjwa, daktari amekuambia una siku chache za kuishi, ukiangalia umeombewa mara nyingi hakuna matokeo yoyote, lakini unakumbuka Neno la Bwana linalosema ‘kwa kupigwa kwake sisi tumepona’. Unaanza kufurahi, ukimwinulia mikono Mungu na kumshukuru ukisema asante, Bwana kwa kuniponya, huku ukimsifu katika hali yako hiyo hiyo ya udhaifu.
Sifa hizo ni muhimu sana kwetu, na zinaugusa moyo wa Mungu kwa namna ya kipekee, Kwasababu kamwe haziwezi kuwa na unafiki ndani yake.
Hizi zinapaswa ziwepo ndani yetu wakati wote. Unakumbuka ahadi za Mungu ambazo bado huoni zimetimia, unamsifu Mungu sana kwa furaha kana kwamba umekwisha vipata vyote sasa, umetafuta kazi umekosa, unamsifu Mungu kana kwamba umepokea ripoti ya kuajiriwa.
Hizi ndio aina saba za sifa, ambazo ukiziachilia katika maeneo yako yote ya kiibada. Utampendeza Mungu sana. Lakini pia zinapaswa ziwe katika Roho na Kweli, tafsiri yake, ni sharti mtu umsifuye Mungu uwe umeokoka, umeshatambua kazi ya Kristo ya ukombozi kwenye maisha yako ipoje. Tayari wewe ni mfuasi wa Kristo. Ndipo sifa hizo zitakubalika. Vinginevyo haziwezi kumpendeza Mungu hata kama utazifanya zote kwa ufasaha.
Ikiwa bado hujaokoka, na upo tayari kufanya hivyo leo. Basi kwa msaada unaweza fungua hapa kwa msaada wa mwongozo huo wa kumkaribisha Yesu maishani mwako.>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Shalom.
Usiishie kutafuta tu utakaso wa roho, bali tafuta pia UTAKASO WA MWILI, kwamaana vitu hivi viwili vinaenda sambamba, kwasababu vitu hivi vikichafuka vinaiharibu pia nafsi ya mtu.
2Wakorintho 7:1“Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na UCHAFU WOTE WA MWILI NA ROHO, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”.
Upo usemi kuwa Mungu wetu hatazami sana Mwili, lakini anatazama Zaidi Roho ya Mtu. (Hatuna budi kuwa makini na kauli hii!!)
Kutokana na kwamba asilimia kubwa ya maombi yetu yanalenga MAHITAJI YA MWILINI, basi ni wazi kuwa Mungu anaitazama pia miili yetu. Kwasababu kama mtu atamwomba Mungu Baba ampe fedha, au chakula, au makazi hayo yote si kwasababu ya “roho” kwasababu roho haili chakula, wala haivai nguo, wala haiishi kwa fedha.. bali mwili ndio unaohitaji hayo yote.
Sasa kama tutamlazimisha Mungu Baba aangalie miili yetu kwa mahitaji yetu, halafu wakati huo huo tunasema Mungu haangalii mwili, tutakuwa WANAFIKI!!.
Sasa ikiwa asilimia Zaidi ya asilimia 90 ya mahitaji yetu, yanalenga MIILI YETU, Basi ni wazi kuwa Mungu anaangalia Miili yetu na anajishughulisha nayo sana….
Ni lazima kulijua hili ili tusipotee na elimu ya uongo ya shetani,.. Ni lazima pia tujishughulishe kutafakari namna ya kuyafanya mapenzi ya Mungu katika miili yetu kama tu vile tunavyojishughulisha katika kumwomba mahitaji ya mwili..
1Wathesalonike 5:23 “Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; NANYI NAFSI ZENU NA ROHO ZENU NA MIILI YENU mhifadhiwe MWE KAMILI, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo”.
Katika mstari huo biblia imetaja mambo yote matatu; Nafsi, mwili na roho. (yanapaswa yawe makamilifu, bila lawama mpaka wakati wa kuja kwake Bwana YESU).
Hivyo zingatia yafuatayo:
1. NI NINI UNAFANYA KUPITIA MWILI WAKO.
Jipime ni nini unakifanya katika mwili,.. je shughuli au matendo unayoyafanya kupitia mwili wako ni kulingana na mapenzi ya Mungu??.. Kama unafanya kazi haramu (mfano ukahaba, au kazi ya kuuza vitu haramu kama pombe, sigara, na mengineyo), basi kazi hiyo unaifanya kupitia mwili wako hivyo ibadili ili isikupeleke jehanamu ya moto.
Kama matendo unayoyafanya katika mwili ni haramu mfano uzinzi (1Wakorintho 6:18), wizi, au mauaji n.k geuka leo yasije yakawa sababu ya kukupeleka hukumuni.
2. NINI UNAKIAMBATANISHA NA MWILI WAKO
Angalia ni nini unakiambatanisha/unakishikamanisha na mwili wako.. Hapa nazungumzia aina ya mavazi na urembo na michoro (tattoo). Je mavazi uvaayo ni sawasawa na Neno la Mungu?.. Je yanaipasa jinsia yako sawasawa na Kumbukumbu 22:5.
Je mavazi unayovaa ni ya kujisitiri?, kuzuia tamaa kwa upande mwingine na kutunza heshima yako? (1Timotheo 2:9 na Mathayo 5:28)
Je michoro uichorayo na rangi yako ya asili uiondoayo ni mapenzi ya Mungu? (Walawi 19:28)
Angalia ni nini kinanin’ginia mwilini mwako.. Je hizo cheni, hereni, mikufu, bangili, vikuku n.k ni mapenzi ya Mungu?? Je si ishara ya utumwa?? (hebu soma Kutoka 21:5-6 na Kumbukumbu 15:16-17).
3. NI NINI KINAINGIA MWILINI MWAKO.
Angalia ni kitu gani unakiingiza mwilini mwako.. Je Mungu amekusudia moshi uingia katika mapafu yako ambayo yanapaswa yavute hewa safi ili kutimiza miaka uliyopewa yakuishi duniani?..
Je Mungu amekusudia uingize vilevi na madawa ya kulevya ndani ya mwili wako na kukutoa ufahamu wako kwa muda?.. Jiulize kama si ruhusu kuendesha chombo chochote cha moto ukiwa umelewa/umekunywa pombe.. vipi kuuendesha huo mwili ukiwa umelewa??.. Huoni kama huo ni uvunjaji wa sheria kubwa Zaidi, kwasababu mwili ni bora kuliko gari au chombo kingine chochote cha usafiri.
2Wakorintho 7:1 “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
UTAKASO NI SEHEMU YA MAISHA YA MKRISTO YA KILA SIKU.
Vazi/Nguo kiroho linawakilisha “matendo ya mtu”, maana yake kiroho mtu mwenye mavazi masafi, maana yake matendo yake ni masafi, na kinyume chake mwenye mavazi machafu maana yake matendo yake si safi (Ufunuo 19:18).
Sasa Matendo yanatunzwa, lakini pia yanafuliwa (safishwa).. kama vile nguo inavyoweza kutunzwa lakini pia kufuliwa.
1. TUNZA MAVAZI YAKO.
Maana ya kutunza mavazi ni kuhakikisha hayaharibiki wala kuwa na kasoro yawapo mwilini. Vazi lililotoboka au kuchanika maana yake limekosa matunzo mwisho wa siku yule mtu atabaki Tupu.
Vivyo hivyo ni wajibu wetu kuyatunza Matendo yetu mema, yasiharibike.. Kwa kujiangalia mazingira tuliyopo na mambo tuyafanyayo…
Ufunuo 16:15” (Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, NA KUYATUNZA MAVAZI YAKE, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake)”.
Vitu vinavyoharibu matendo yetu mazuri/tabia nzuri ni pamoja kampani tulizonazo na mazungumzo tuzungumzayo..
1Wakorintho 15:33 “Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema”.
Chunguza makundi uliyonayo na aina ya mazungumzo unayozungumza.
2. FUA NGUO ZAKO.
Nguo isiyofuliwa inapoteza umaridadi na unadhifu kwa mtu, hata kama haijaharibika au kuchanika. Vile vile Matendo yasiyofuliwa yanapoteza unadhifu wa mtu kiroho.
Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.
13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.
14 HERI WAZIFUAO NGUO ZAO, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake”.
Sasa mtu anafuaje Matendo yake?… Si kwa njia nyingine Zaidi ya kuomba na kusoma Neno.
Na Utajuaje matendo yako yameanza kuingia dosari?.. si kwa kusubiri uambiwe na mtu au watu, bali kwa kusoma Neno (biblia). Unaposoma Neno ndipo utakapojijua kama una kasoro au la!, kwasababu Neno la Mungu ni kioo.. Ili ujijue kama una uchafu mwilini, si kusubiri uambiwe, kwasababu si wote wenye ujasiri wa kukwambia kasoro zako.
Kitu pekee kitakachoweza kuutambulisha uchafu usoni mwako ni KIOO
na ni lazima usomaji wa Neno uambatane na maombi.
Hivyo Maombi ni “Maji” na Neno la Mungu ni “sabuni” kwa mambo hayo, matendo yetu yatakuwa safi daima.
Bwana atuongezee Neema yake.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea.
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Nini maana ya kumpenda Bwana kwa moyo,roho, akili na nguvu zetu zote?
2Timotheo 4:21 “Jitahidi kuja kabla ya wakati wa baridi. Eubulo akusalimu, na Pude, na Lino, na Klaudia, na ndugu wote pia”
Mtume Paulo ni mtu aliyetambua kuwa kustawi kwa huduma yake kunategemea sana sapoti ya watendazi wenzake wengine wenye ni moja na yeye. Hivyo tunasoma wakati akiwa Rumi kama mfungwa, alimwandikia waraka mwanawe Timotheo, aiharakishe huduma yake, ili amfuate kule Rumi wasaidiane katika huduma kabla ya wakati wa bariki kuanza.
“Jitahidi kuja kabla ya wakati wa baridi”.
Paulo alijua mazingira yanaweza kukawiisha kusudi la Mungu. Hivyo alitambua kuwa mtu akiongeza jitihada anaweza kukamilisha mambo yake mapema kabla mazingira Fulani hayajamuathiri kutenda kusudi lingine la Mungu.
Kwa ukanda waliokuwa, ilikuwa ni ngumu sana, meli kusafiri nyakati za baridi kwasababu ya barafu baharini, hivyo safari zote za majini zilisitishwa kwa miezi kadhaa mpaka baridi itakapoisha ndipo safari zianze tena, Paulo aliliona hilo akatambua ni jambo la asili haliwezi kuepukika kwa kufunga na kuomba, isipokuwa kwa kupangilia tu ratiba vizuri.
Hii ni kutufundisha sisi, tufahamu kuwa mazingira Fulani, au nyakati Fulani zisizo rafiki sana huwa zinapita, au zitakuja mbele yetu ambazo zinaweza zikawa ni kikwazo cha utumishi kwa sehemu Fulani.
Kwamfano wakati wa baridi kwako, unaweza kuwa ni wakati wa ndoa. Kama wewe ni kijana hujaoa/ hujaolewa, unanafasi sasa ya kumtumikia Mungu kwa uhuru wote. Titahidi sana kufanya hivyo sasa, kwasababu nafasi hiyo inaweza ikapungua kwa sehemu uingiapo katika majukumu ya kindoa. Usipojitahidi sasa kujiwekea msingi mzuri kwa Mungu wako, utataabika sana kuujenga huo uwapo kwenye ndoa.
Wakati wa baridi unaweza ukawa ni kipindi cha kazini au masomoni. Ikiwa bado hujapata kazi, au upo likizo kazini au shuleni, embu tumia vema wakati wako, kuongeza kitu kikubwa katika ufalme wa Mungu, kwasababu shughuli zitakapokulemea, kuujenga tena huo msingi itakuwia ngumu sana, na kama ikiwezekana yaweza kukuchukua wakati mrefu. Uwapo ‘free’ usilale, bali tumia sasa kuongeza mikesha, maombi ya masafa marefu, kusoma biblia yote.
Wakati wa baridi waweza kuwa uzee. Kwa jinsi umri unavyokwenda ndivyo uwezo wa mwili wako unavyopungua, Hivyo utengenezapo mambo yako mapema na Bwana, basi wakati huo ukikukuta hautakuathiri sana, kwasababu tayari yale ya msingi uliyopaswa uyafanye umeshayafanya mapema, uzeeni ni kumalizia tu.
Zipo nyakati nyingi za baridi. Chunguza tu maisha yako ujue wakati wako wa baridi unafika lini na ni upi, kisha jitahidi sana, kuwekeza kwa Mungu sasa, kimaombi, kiusomaji Neno, na kiuinjilisti.
Bwana akubariki
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MCHE MWORORO.(Opens in a new browser tab)
Nini maana ya kikombe cha maji ya baridi(Mathayo 10:42)?
Je ni wakina nani ambao hawataonja mauti mpaka siku ya kuja Bwana?
(Opens in a new browser tab)Fahamu maana ya Mithali 25:13 Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno;(Opens in a new browser tab)
SWALI: Nini maana ya hivi vifungu?
Zekaria 13:7-9
[7]Amka, Ee upanga, juu ya mchungaji wangu, na juu ya mtu aliye mwenzangu, asema BWANA wa majeshi; mpige mchungaji, nao kondoo watatawanyika; nami nitaugeuza mkono wangu juu ya wadogo.
[8]Hata itakuwa, ya kwamba katika nchi yote mafungu mawili yatakatiliwa mbali, nao watakufa, asema BWANA; lakini fungu la tatu litabaki humo.
[9]Nami nitalileta fungu lile la tatu na kulipitisha kati ya moto, nami nitawasafisha kama fedha isafishwavyo, nami nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo; wataliitia jina langu, nami nitawasikia; mimi nitasema, Watu hawa ndio wangu; nao watasema, BWANA ndiye Mungu wangu.
JIBU: Unabii huu ulimtabiri Yesu, wakati wa kukamatwa kwake na wayahudi ili auawe, ukisoma Mathayo 26:31 utaona Bwana alinukuu yeye mwenyewe maneno hayo kwa kusema..
“Ndipo Yesu akawaambia, Ninyi nyote mtachukizwa kwa ajili yangu usiku huu kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika”.
Na kweli tunaona baada ya Yesu kukamatwa mwanafunzi wake wote wakamkimbia.
Kama mstari wa nane unavyosema mafungu mawili yatakatiliwa mbali, nao watakufa, lakini fungu la tatu litabaki humo.
Ni kuonyesha kwa lugha ya mifano kuwa ni idadi ndogo tu ya wanafunzi ambao hawakumuacha kabisa kabisa, mfano wa “theluthi moja”, lakini theluthi mbili zote zilirejea nyuma moja kwa moja. Na ndio maana utaona siku ile ya pentekoste ni watu 120 tu waliokuwepo pale kuingojea ahadi ya roho. Lakini yale maelfu ya makutano yaliyokuwa yakimfuata yalitawanyika.
Lakini katika mstari wa 9, anasema;
“Nami nitalileta fungu lile la tatu na kulipitisha kati ya moto, nami nitawasafisha kama fedha isafishwavyo, nami nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo; wataliitia jina langu, nami nitawasikia; mimi nitasema, Watu hawa ndio wangu; nao watasema, BWANA ndiye Mungu wangu.”
na hao ndio waliopitishwa katika moto, wakabatizwa na Roho, wakawa vyombo vikamilifu vimfaavyo Mungu kwa kazi ya uvuvi.
Lakini adui hakujua ulikuwa ni mpango wa Mungu iwe vile kwamba mchungaji afe, ili wokovu mkuu zaidi ya ule wa kwanza uje kwa kupitia kifo chake.Angelijua hilo hata asingedhubutu kumgusa.
Ndio hapo shetani hakuamini alipoona wale wachache waliojazwa Roho, wakivuta maelfu kwa mamilioni ya watu kwa kipindi kifupi mpaka dunia nzima ikawa imepinduliwa. Shetani hakujua misheni ya mchungaji ilikuwa ni kuingia ndani ya kondoo, sio kuwachunga tena kwa nje, kama hapo mwanzo.
Je! Wewe ni kundi lipi? Lile la tatu, au yale mawili ya kwanza. Ambayo yanapoona mtikisiko kidogo tu wa kimaisha hurudi nyuma, yanapoona kuyumba kidogo tu kwa kanisa hutoroka, yanapoona kutetereka kidogo kwa kiongozi wao yanarudi Misri? Kumbuka ni kusudi la Kristo wote tupitishwe katika moto, ili tuimarishwe tufae kwa ajili ya kazi njema ya utumishi wake.
Aliwapitisha wana wa Israeli jangwani, ili kuwaimarisha kabla ya kwenda kuwaangusha maadui zao kule Kaanani. Aliwapitishwa mitume wako, kwanini na wewe usipitishwe?
Vivyo hivyo ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, ambaye utapenda Bwana akutumie, basi liweke kichwani kwamba kuna mahali fulani utapitishwa ili kuimarishwa, huo ndio ubatizo wa Moto ulio wa Roho Mtakatifu. Wakati huo usimwache Bwana, kuwa fungu la tatu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Tofauti kati ya zaka na sadaka ni ipi?
(Opens in a new browser tab)MWANAMKE ULIYEKOMAA KI-UMRI, ITAMBUE HUDUMA YAKO.(Opens in a new browser tab)
Je unaielewa vyema hii sentensi? “..Naye Neno alifanyika Mwili”.
Yohana 1:14 “Naye NENO alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli”.
Je ulishawahi kuzungumza na mtu kwa simu?.. Je anapozungumza na wewe huwa unamwona?? Au unayasikia MANENO YAKE TU?.. Ni wazi kuwa humwoni ila unasikia MANENO YAKE.
Lakini atakapokujia na kusema nawe ana kwa ana..hapo utakuwa UNAMWONA na pia UNAYASIKIA MANENO YAKE YANAYOTOKA KATIKA KINYWA CHAKE.
Hivyo tunaweza kusema kuwa wakati anaongea nawe kwenye simu yalikuwa ni Maneno tu (Pasipo yeye kumwona), lakini alipokujia na kusema nawe ana kwa ana yalikuwa ni Maneno yale yale isipokuwa yanatoka ndani ya mwili unaoonekana..KWA LUGHA NYINGINE TUNAWEZA KUSEMA NI MANENO YALIYOUVAA MWILI.
Na siri ya UUNGU wa YESU, inaanzia hivyo hivyo… Kwamba hapo Mwanzo Mungu alisema nasi kwa NENO LAKE pasipo yeye kuonekana… Lakini baadaye yeye mwenyewe akaja katika mwili na kuonekana na kusema MANENO YALE YALE kupitia mwili unaoonekana…
Mtume Paulo kaielezea vizuri hiyo siri katika 1Timotheo 3:16
1Timotheo 3:16 “Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. MUNGU ALIDHIHIRISHWA KATIKA MWILI, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu”.
Lakini sio tu Mtume Paulo aliyefunuliwa hiyo siri, bali pia Mtume Yohana, aliyekuwa mwanafunzi wa BWANA YESU, alifunuliwa hiyo siri ya MUNGU kudhihirika katika mwili..
Yohana 1:1 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
2 Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.
3 Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika…………
14 NAYE NENO ALIFANYIKA MWILI, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.”
Na huyu Neno aliyevaa mwili alikuwa si mwingine Zaidi ya BWANA YESU KRISTO, MKUU WA UZIMA!!!.
Tena Mtume huyu huyu Yohana kazidi kuliweka hili wazi katika nyaraka yake nyingine aliyoiandika kwa watu wote.. na kusema kuwa lile NENO lililokuwa linasikiwa zamani, limefanyika mwili, na wakaushika ule mwili na kuupapasapasa (yaani mwili wa BWANA YESU).
1Yohana 1:1 “Lile lililokuwako tangu mwanzo, tulilolisikia, tuliloliona kwa macho yetu, tulilolitazama, na mikono yetu ikalipapasa, kwa habari ya Neno la uzima”
Kumbe hili Neno lilianza kwa kusikiwa, baadaye likaonekana (maana yake lilivaa mwili)..na Mitume wakalipapasa (maana yake waliushika mwili wa BWANA YESU) kabla na baada ya kufufuka.
Kwahiyo KRISTO ni Neno la MUNGU na ni MUNGU pia aliyeuvaa mwili, ni Mungu pamoja nasi (Imanueli) ndio maana katukuka kuliko vitu vyote na viumbe vyote.
Je umemwamini na kumpokea maishani mwako?..kama bado fahamu kuwa hakuna njia nyingine yoyote ya kufika mbinguni isipokuwa kwa njia ya yeye. Na pia hakuna mtu wala malaika, wala kiumbe kingine chochote kitakachoweza kukupenda wewe au mimi katika viwango atupendavyo BWANA YESU.
Sasa ni heri umtumainie huyu YESU ambaye si mnafiki katika upendo, mwanadamu anaweza kukunafikia, mchungaji anaweza kukunafikia, lakini YESU, ni wa UPENDO USIO NA UNAFIKI NDANI YAKE. Yasikilize maneno yake, yakubali na yapokee.
BWANA AKUBARIKI.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?
“WOKOVU WETU U KARIBU NASI KULIKO TULIPOANZA KUAMINI”
Nakusalimu katika jina kuu la mwokozi wetu Yesu Kristo, karibu katika kujifunza Neno la Mungu. Leo tutaona mambo Makuu sita (6), ambayo Mungu anatumia kuondoa uovu ndani ya mtu, na kumfanya awe mtakatifu kabisa kama yeye alivyo. Ikiwa wewe umemfuata Kristo basi tarajia mambo haya matano atayatumia katika maisha yako, kukukamilisha.
Tukianza na
Kumbuka sisi sote tulizaliwa na deni la dhambi. Hivyo tulistahili hukumu ya mauti, (Warumi 6:23), Lakini deni hilo lilikuja kulipwa na Bwana wetu Yesu kwa kifo chake pale msalabani (Warumi 5:8). Kumwagika kwa damu yake, sote tumepokea “msamaha wa dhambi” bure kwa neema. Hakuna mwanadamu yoyote anayeweza kukubaliwa na Mungu, kwa uweza wake mwenyewe. Kwahiyo damu ya Yesu imekuwa hatua ya kwanza ya sisi kukubaliwa na Mungu.
Sasa tunaweza kupokea msamaha kweli, tukasemehewa, lakini dhambi bado ikawepo ndani yetu. Na hilo sio kusudu la Mungu atusemehe tu, halafu atuache tuendelee kuwa watumwa wa dhambi ndani kwa ndani. Si lengo la Mungu, hata mtu mwenye upendo wa dhati wa Yule aliyekosewa naye, anapoona amemsamehe, huwa hamwachi tena kesho arudie kosa lile lile ili, amsamehe, hapana, bali humwonyesha njia ya kuepuka makosa ili yeye mwenyewe aweze kusimama kwa ujasiri mbele zake. Na ndivyo ilivyo kwa Mungu mara baada ya kupokea msamaha wa dhambi, huyo mtu anaanza hatua ya utakaso wa Mungu ambao sasa hufanywa na Roho Mtakatifu aliyeingia ndani yake, Ndio hapo inakuja hatua ya pili,
Biblia inasema Neno ni kama maji, ambayo yanasafisha.
Waefeso 5:26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno; 27 apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa.
Umeona, Kristo hulisafisha kanisa lake, kwa Neno, ndio maana wewe kama mtu uliyempokea Yesu, Ni lazima uwe na juhudu nyingi sana za kusoma Neno la Mungu kila siku, usikie maonyo, fundisho, agizo, njia, (2Timotheo 3:16), Na kwa jinsi unavyojifunza sana, ndivyo unavyosafishwa moyo wako na roho yako, hatimaye unaanza kujiona mtu ambaye huna hatia ndani yako. Na hapo ndipo unapojikuta unaacha baadhi ya mambo uliyokuwa unafanya huko nyuma. Kumbuka biblia uliyonayo sio kitambulisho cha mkristo au pambo la mkoba, bali ni maji hayo ya kukusafisha, hivyo oga kila siku, uwe msafi. Kwasababu usipofanya hivyo utakuwa mchafu tu sikuzote.
Kwa kawaida sio kila uchafu hutoka kwa maji, mwingine huitaji moto ili kuundoa. Kwamfano ukiupata mwamba wenye dhahabu ndani yake ukipitisha maji huwezi toa uchafu uliogandamana nao,hivyo wale wafuaji, wanaupitisha kwenye moto, kisha unayeyuka na baada ya hapo uchafu na dhahabu hujitenga kisha wanaikusanya dhahabu. Ndivyo ilivyo na Mungu kwa watoto wake. Upo moto ambao wewe kama mwana wa Mungu ni lazima tu utapitishwa hata iweje, kuondoa mambo sugu yaliyogandamana na wewe yasiyoweza kutoka kwa Neno tu bali kwa hatua ya kimaisha, ndio huo unaoitwa “ubatizo wa moto”. Mfano wa huu ndio ule uliompata mfalme Nebukadreza (Danieli 4), kukaa miaka saba maporini kula majani ili tu aondolewe kiburi ndani yake. Ni aina Fulani ya maisha ambayo kwako yatakuwa kama moto, lakini mwisho wake hukuletea faida ya roho yako.
1Petro 1:6 Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali;7 ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo.
Zipo tabia nyingine ambazo Mungu anaona mwanawe anakuwa nazo kwa ujinga tu, hivyo, ili kuundoa ujinga huo, haihitaji maji wala moto, bali kiboko. Anapoona unafanya jambo Fulani kwa makusudi na alishakukataza hapo awali fahamu pia kiboko kitapita juu yako.
Waebrania 12:6 Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, Naye humpiga kila mwana amkubaliye.
7 Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye?
8 Basi kama mkiwa hamna kurudiwa, ambako ni fungu la wote, ndipo mmekuwa wana wa haramu ninyi, wala si wana wa halali. 9 Na pamoja na hayo tulikuwa na baba zetu wa mwili walioturudi, nasi tukawastahi; basi si afadhali sana kujitia chini ya Baba wa roho zetu na kuishi?
10 Maana ni hakika, hao kwa siku chache waliturudi kama walivyoona vema wenyewe; bali yeye kwa faida yetu, ili tuushiriki utakatifu wake.
Biblia inasema pia..
Mithali 22:15 Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali.
Yohana mbatizaji kwa uvuvio wa Roho aliandika maneno haya kuhusu Bwana Yesu..
Mathayo 3:11 Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
12 Ambaye pepeto lake li mkononi mwake, naye atausafisha sana uwanda wake; na kuikusanya ngano yake ghalani, bali makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.
Yesu akija kwako, fahamu kuwa mkononi ameshika pepeto pia, na wewe utawekwa juu yake, Anajua kabisa ulipo wewe makapi pia yapo, uliyotoka nayo huko shambani (ulimwenguni), hivyo ili kukutenga nayo, ataanza kukupepeta, kama vile ngano, utarushwa juu, utashushwa chini, utarushwa juu utashushwa chini, huwezi kuachwa utulie, lengo ni kuhakikisha makapi yote yanapeperushwa na upepo, iwe ni watu, vitu, utaona tu unapelekwa mbele, unarudishwa nyuma..baadaye akishaona ni ngano tu imebakia chini, hapo ndipo anapokuacha, unaanza kuona ushwari. Hii ilimkuta Ibrahimu, Bwana anamtoa Uru, anampeleka kaanani, mara anakimbilia Misri, mara anarudisha, lakini baadaye Mungu alimpa pumziko, baada ya kuona wote waliokuwa wameshikamana naye hawapo naye.
Usishangae kutokuwa na utulivu katika nyakati fulani za maisha yako wokovu, wakati Fulani unafanikiwa, halafu unarudi chini, wakati Fulani unapata amani kotekote, gafla inaondoka, unapata, ghafla tena unapoteza, tulia tu, kuwa na amani ndani ya Kristo, utakuwa tu, imara, wala hiyo misukosuko haitakuwepo tena, ni kwanini iwe hivyo? Ni kwasababu makapi yanapeperushwa na upepo.
Kaa ukifahamu Yesu anajulikana pia kama tabibu,(Marko 2:17) na anajua maovu mengine unayoyafanya yanatokana na magonjwa na majeraha ya rohoni, anajua hali yako ilivyo hivyo anachokifanya ni kukutibu yeye mwenyewe, ndio hapo unashangaa tu mwingine anatokwa na mapepo yaliyokuwa yanamsumbua na kumpelekea kutenda dhambi mwingine anapona udhaifu fulani, uliokuwa unamfanya amkosee Mungu, mwingine anapokea faraja, amani, utulivu usio wa kawaida, anashangaa kuona tofauti kubwa ya sasa na hapo kabla. Hili nalo mtu aliyempokea Kristo ataliona kwenye maisha yake. Na atimaye anakuwa mwema yeye tu mwenyewe, asukumwi tena na presha ya dhambi fulani. Kwasababu tabibu mkuu ameshamponya, ambaye akikuweka huru, unakuwa huru kwelikweli.
Ufunuo 3:18
Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na DAWA ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.
Hivyo, wewe kama mwana wa Mungu, tambua yote hayo yatapita katika sehemu Fulani ya maisha yako. Usidhani kusafishwa tu na damu ya Yesu ndio basi, utatakaswa na hiyo ni katika maisha yako yote. Haiwezekani mtu aliyeokoka ambaye amepokea Roho maisha yake yote awe Yule Yule wa zamani, hizo sio kanuni za wokovu, wala sio kusudi la Mungu. Ukubali utakaso, au usiwe mkristo kabisa. Kwasababu hivi viwili huenda sambamba wala haviwezi kutenganishwa. Huo ndio upendo wa Mungu.
Utukufu na heshima ni vyake milele na milele.
Bwana akubariki.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> hhttps://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.
(Opens in a new browser tab)UTAKASO NI SEHEMU YA MAISHA YA MKRISTO YA KILA SIKU.