Jibu: Tusome,
Waamuzi 1:19 “Bwana alikuwa pamoja na Yuda; naye akawafukuza watu waliokaa katika nchi ya milimani; ASIWEZE KUWAFUKUZA HAO WALIOKAA KATIKA HILO BONDE, kwa kuwa wao walikuwa na magari ya chuma”.
Ni kweli Bwana hakuweza kuwafukuza hao watu waliokaa mabondeni… Lakini si kwamba alikuwa hana uwezo wa kuwafukuza, bali kulikuwa na kusudi kwanini hakuweza kuwafukuza..
Ili tuelewe vizuri tuanzie kuisoma habari hiyo kuanzia mstari wa 17..(zingatia maneno yaliyoanishwa kwa herufu kubwa).
Waamuzi 1:17 “Kisha Yuda akaenda pamoja na nduguye Simeoni, na WAKAWAPIGA WAKANAANI waliokaa katika Sefathi, na kuuharibu mji kabisa. Na jina la mji huo ulikuwa ukiitwa Horma.
18 Pamoja na haya Yuda aliutwaa Gaza pamoja na mipaka yake, na Ashkeloni na mipaka yake, na Ekroni na mipaka yake.
19 BWANA ALIKUWA PAMOJA NA YUDA; naye akawafukuza watu waliokaa katika nchi ya milimani; asiweze kuwafukuza hao waliokaa katika hilo bonde, kwa kuwa wao walikuwa na magari ya chuma”.
Mstari wa 19, unaanza kwa kusema “Bwana alikuwa pamoja na Yuda” maana yake ni kwamba, katika vita Yuda alivyokwenda kupigana, Bwana alikuwa pamoja naye..(kumbuka Yuda anayezungumziwa hapa sio Yule mwana wa Yakobo, wala sio Yule Yuda aliyemsaliti Bwana Yesu), bali ni kabila la Yuda kwa ujumla, ambalo wakati wa kuingia katika nchi ya Ahadi lilipaswa liupiganie urithi wake kwa kuwatoa wenyeji wa Kanaani ili kusudi wapate ardhi ya kukaa wao, kama urithi wa kabila zima.
Hivyo katika harakati za kupambania urithi wao huo walikutana na makabila mengi mbalimbali, ambayo mengine yalikuwa na nguvu sana na mengine manyonge, yale yaliyokuwa manyonge Yuda walikwenda kwa ujasiri na kuyapiga na kuyapokonya ardhi, kwasababu hayakuwa na silaha zenye nguvu za kuwazidi,
Lakini yale yaliyokuwa na Nguvu nyingi za kivita, Yuda waliyaogopa, hivyo hawakudhubutu kwenda kupigana nayo, na kwasababu hiyo Mungu asingeweza kuyaondoa kwasababu Mungu kamwe hatembei na watu wasio na Imani, hivyo akawaacha,
Lakini kama wangechukua hatua ya kwenda kupambana na hao maadui zao, pasipo kutazama ni silaha za aina gani wanazomiliki, ni wazi kuwa Mungu angewasaidia katika vita hiyo, na hatimaye wangewaondoa hao watu na kuutwaa urithi wao.
Sasa baadhi ya makabila ambayo Yuda waliyaogopa ndio hao waliokuwa wanakaa mabondeni, na sababu ya kuyaogopa biblia imeitaja pale kuwa “makabila hayo yalikuwa na magari ya chuma kwaajili ya vita”..Yuda wakaogopa wasiende kupigana nayo, jambo ambalo Yoshua mtumishi wa Mungu alishawaonya kuwa wasiyaogope makabila hayo..
Yoshua 17:17 “Kisha Yoshua alinena na nyumba ya Yusufu, maana, ni Efraimu na Manase, akawaambia, Wewe u taifa kubwa la watu, nawe una uwezo mwingi; hutapata kura moja tu;
18 lakini hiyo nchi ya vilima itakuwa ni yako; maana, ijapokuwa ni mwitu, wewe utaukata, na matokeo yake yatakuwa ni yako; kwa kuwa wewe utawafukuza hao Wakanaani, WAJAPOKUWA WANA MAGARI YA CHUMA, WAJAPOKUWA NI WENYE UWEZO”
Utaona pia hiyo sio mara ya kwanza wana wa Israeli kuyaogopa mataifa yenye nguvu kupita wao, soma pia Hesabu 13:33 na Waamuzi 4:3
Hiyo inatufundisha nini?
Tunachojifunza ni kuwa “Mungu hawezi kufanya jambo lolote kwetu pale tunapomkosea Imani” Hilo ndilo jambo ambalo Mungu hawezi kufanya!!! Na lingine ambalo hawezi kufanya ni DHAMBI!
Yakobo 1:6 “Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku.
7 Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana.
8 Mtu wa nia mbili husita-sita katika njia zake zote”.
Ukiamini kuwa Mungu hawezi kukuponya, basi fahamu kuwa KWELI HATAWEZA KUKUPONYA!, Ukiamini kuwa Mungu hawezi kukutendea jambo Fulani au kukupigania, basi fahamu kuwa ni KWELI MUNGU HATAWEZA KUKUTENDEA HILO JAMBO, wala KUKUPIGANIA katika hiyo vita iliyo mbele zako.
Siku zote fahamu kuwa PASIPO IMANI HAIWEZEKANI KUMPENDEZA MUNGU (Waebrania 11:6).
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Mtu akija kwangu naye HAMCHUKII baba yake hawezi kuwa mwanafunzi wangu?
Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia neno la Mungu wetu lililo taa ya miguu yetu na mwanga wa njia yetu (Zab.119:105).
Neno la Mungu linasema..
Warumi 5:1 “Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na mwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo”.
Je! ni haki gani hiyo tunayohesabiwa, ambayo tukiisha ipata basi tutapata amani?
Jibu ni kwamba si haki moja!, bali ni haki ZOTE Njema!… Mfano wa hizo ni kama zifuatazo…
1.HAKI YA KUISHI MILELE.
Tunapomwamini Bwana Yesu tunapata haki ya kupata UZIMA WA MILELE.. ambayo tuliupoteza pale Wazazi wetu wa kwanza walipoasi.
Yohana 11:25 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi;
26 naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo?”
Pia Yohana 3:36, Bwana Yesu anasema maneno kama hayo hayo…
2. HAKI YA KUWA NA UZIMA, NA AFYA.
Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”
Hivyo magonjwa hayatatutawala, bali uzima na afya, kama tukiwa ndani ya Yesu, maana yake AFYA ni haki yetu!.. tunapopitia maradhi ya muda mrefu maana yake hapo ni shetani katudhulumu haki yetu, hivyo hatuna budi kuishindania haki yetu mpaka tuipate katika mahakama ya kimbinguni, huku tukitumia katiba yetu biblia. Na tunapong’ang’ania kwa bidii bila kuchoka, wala kukata tamaa basi tunaipata haki yetu ya kuwa wazima siku zote.
3. HAKI YA KUMWONA MUNGU.
Unapomwamini Yesu ni haki yako kumwona Mungu katika maisha haya na katika yale yajayo.. Kumwona Mungu si lazima tumwone kwa macho, bali utamwona katika maisha.. Maana yake utapitia vipindi vingi vya maisha ambavyo vitakujulisha kuwa Mungu yupo nawe, pia utaona miujiza mingi ya kiMungu ambayo itakujulisha kuwa Mungu yupo nawe, na zaidi sana kila utakapomwita Mungu utamwona..
Mathayo 28:20 “……….na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari”.
4. HAKI YA KUPOKEA ROHO MTAKATIFU.
Zamani Roho Mtakatifu alikuwa anashuka juu ya baadhi ya watu tu (ambao ni manabii) tena kwa kitambo kidogo, lengo ni kuwapa ujumbe kutoka kwa Mungu, na baada ya hapo anaondoka.. Kwasababu ROHO TAKATIFU ya Mungu haiwezi kukaa ndani ya Mwanadamu aliye mchafu.
Lakini baada ya Bwana YESU kuja, kaja kutuletea Haki ya sisi kuwa na Roho Mtakatifu ndani yetu, jambo ambalo si la kawaida..
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”
Hivyo yale matunda ya Roho tunayoyasoma katika Wagalatia 5:22, ambayo ni upendo, amani, furaha n.k Hayo yote ni haki yetu sisi kuyapata.. Kuwa amani ni haki yako wewe uliye ndani ya Kristo, kuwa na furaha ni haki yako.
5. HAKI YA KUFANIKIWA KIMWILI NA KIROHO.
Tunapomwamini Bwana Yesu na kukaa ndani yake, hatupati tu haki ya vitu vya kiroho, bali pia tunapata haki ya vitu vingine vya kimwili ikiwemo mafanikio.
3 Yohana 1:2 “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo”
Pia Neno la Mungu linasema..
2Wakorintho 8:9 “Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake”.
Na haki nyingine zote zilizosalia, ni Ahadi yetu. Ndio maana kuna umuhimu mkubwa sana kuingia ndani ya Kristo.. Ukiwa nje ya Kristo, shetani atakudhulumu haki zako zote hizo na hakuna popote utakapokwenda kushitaki.
Bwana akubariki.
Maran atha.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?
Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?
JIBU: Wapo wanaofikiri kwamba shetani amefungwa, atakuja kufunguliwa kipindi Fulani huko mbele, lakini pia wapo wanaodhani, shetani anaishi mahali Fulani kuzimu( aidha chini ya bahari, au kwenye sayari fulani), ambapo huko kuna amesimika utawala wake unaofanana na huu wa duniani.
Lakini ukweli ni kwamba shetani hajafungwa, wala hayupo katika eneo Fulani rasmi la mwilini, ambalo unaweza kwenda ukakutana naye.
Ikumbukwe kuwa ibilisi anafanya kazi katika ulimwengu wa roho, alipoasi mbinguni, alitupwa chini duniani, akaanza kazi yake ya kuudanganya ulimwengu mpaka akafanikiwa kuuteka ukawa chini ya milki yake, Tunalithibitisha hilo katika maneno aliyomwambia Bwana Yesu.
Luka 4:5 Akampandisha juu, akamwonyesha milki zote za ulimwengu kwa dakika moja.
6 Ibilisi akamwambia, Nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi mwangu, nami humpa ye yote kama nipendavyo.
7 Basi, wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako. 8 Yesu akajibu akamwambia, Imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke
Hivyo shetani yupo anazunguka zunguka duniani hana makao rasmi, Alimwambia hivyo Mungu.
Ayubu 1:6 “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao. 7 Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo”.
Atakuja kufungwa kipindi ambacho utawala wa miaka 1000 wa amani wa Yesu Kristo kuanza, na baadaye atafunguliwa kidogo, lakini kwasasa hajafungwa yupo duniani ndio chanzo cha maovu yote, wala hana eneo Fulani rasmi kwamba amejijengea anaishi huko na mapepo yake, hapana bali wanafanya kazi katika ulimwengu wa roho, wakijigawanya tu katika vitengo mbalimbali, wengine katika anga, wengine, katika mataifa, wengine katika familia moja moja, na wengine katika kila huduma/au kanisa la Kristo lilipo, wengine katika uchawi n.k.
Hivyo, sisi tutamshinda na kumpinga tu kwa kulishika Neno la Mungu, na kudumu katika maombi daima.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
ZIFAHAMU HUDUMA KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.
ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.
Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia, Neno La Mungu wetu.
Mwanzo 8:6 “Ikawa baada ya siku arobaini, Nuhu akalifungua dirisha la safina, alilolifanya;
7 akatoa kunguru, naye akatoka akaenda huko na huko, hata maji yakakauka juu ya nchi.
8 Kisha akatoa njiwa, aone kwamba maji yamepunguka usoni pa nchi;
9 bali YULE NJIWA HAKUONA MAHALI PA KUTUA KWA WAYO WA MGUU WAKE, akamrudia Nuhu safinani, maana maji yalikuwa juu ya uso wa nchi yote; naye akanyosha mkono, akamtwaa, akamwingiza mle safinani”
Tunaona wakati wa Nuhu kutoka safinani… Aliwaachia ndege wawili ili kupima hali ya mazingira ya nje. Na ndege wa kwanza ambaye ni “KUNGURU” aliondoka lakini hakumrudia Nuhu.. lakini ndege wa pili ambaye ni “NJIWA” Alipoondoka na kukuta nje maji yamejaa kila mahali, alirudi safinani..
Sasa ni kwanini Njiwa arudi na kunguru asirudi?.
Siri ipo katika ile sura ya Saba, kuhusiana na wanyama Najisi na wasio Najisi.
Mwanzo 7:1 “Bwana akamwambia Nuhu, Ingia wewe na jamaa yako yote katika safina; kwa maana nimekuona wewe u mwenye haki mbele zangu katika kizazi hiki.
2 Katika wanyama wote walio safi ujitwalie saba saba, mume na mke; na katika wanyama wasio safi wawili wawili, mume na mke.
3 Tena katika ndege wa angani saba saba, mume na mke; ili kuhifadhi hai mbegu juu ya uso wa nchi yote”
Sasa Kunguru yupo katika kundi la Ndege Najisi,
Walawi 11:13 “Kisha katika ndege hawa watakuwa ni machukizo kwenu; hawataliwa, ndio machukizo; tai, na furukombe, na kipungu;
14 na mwewe, na kozi kwa aina zake,
15 na kila kunguru kwa aina zake”
Na njiwa yupo katika kundi la ndege Safi (yaani wasio najisi) ndio maana alikuwa anatumika katika matoleo.
Sasa tabia ya ndege/wanyama najisi ni za tofauti na zile za wasio najisi. Wanyama najisi wanakula chochote na wanaweza kuishi popote.. lakini Wanyama/ndege wasio najisi wanachagua vitu vya kula, vile vile wanachagua mazingira ya kuishi, si kila mahali wanaweza kuishi.
Ndio maana tunaona huyu kunguru alipoachiwa, alienda kuzunguka zunguka huko nje, lakini njiwa aliona mazingira ya nje si salama, bado wakati wake, na hatimaye akarudi safinani.
Sasa wanyama najisi kiroho wanafananishwa na watu wa ulimwengu huu, walio mbali na MUNGU, na wanyama Safi (yaani wasio najisi) wanafananishwa na watu wa Mungu, waliookolewa kwa damu ya thamani ya YESU KRISTO, ambao hawajitii unajisi na mambo ya dunia.
Kama vile njiwa alivyozunguka huko na huko na kuona safinani ni mahali salama katika dunia iliyoharibika.. vile vile watu wa Mungu, kamwe hawawezi kuona hii dunia ipo salama, au ni mahali pa kustarehe kuliko safinani. Na safina ni BWANA YESU!.
Ukiona unaifurahia dunia iliyochafuka, dunia iliyojaa anasa, dunia iliyojaa mabaya basi katika roho wewe ni najisi.. Ukiona unaufurahia uasherati, ulevi, wizi unaoendelea duniani, na hata wewe mwenyewe kuwa mshirika wa hayo, basi fahamu kuwa unafanana na Yule kunguru! Na hivyo ni najisi mbele za Mungu kulingana na biblia.
Mathayo 15:18 “….vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi.
19 Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano;
20 hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi…”
Je! wewe ni miongoni mwa walio najisi au safi? Kama bado dhambi inatawala maisha yako basi upo hatarini hivyo suluhisho ni kumgeukia Yesu kwa kutubu na kumaanisha kuacha dhambi, na Yesu atakupokea na kukupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu, ambaye kupitia huyo atakutakasa kwa kukupa uwezo wa kufanya yale mema ambayo ulikuwa unashindwa kuyafanya kwa nguvu zako.
Kataa ukunguru!
Bwana akubariki
maran atha!
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Kwanini Mungu aliwaita Adamu na Hawa jina moja?
JIHADHARI NA ROHO ZIDANGANYAZO.
Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?
Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?
Maandiko yanasema kuwa Bwana Yesu hakuwahi kumbatiza mtu yeyote kwa maji katika huduma yake yote…
Yohana 4:1 “Kwa hiyo Bwana, alipofahamu ya kuwa Mafarisayo wamesikia ya kwamba, Yesu anafanya wanafunzi wengi kuliko Yohana, na kuwabatiza,
2 (lakini Yesu mwenyewe hakubatiza, bali wanafunzi wake)”
Umeona?.. kila mahali Bwana Yesu alipofika aliwaachia wanafunzi wake wabatize!.. lakini yeye mwenyewe hakubatiza mtu yeyote kwa maji. Sasa hiyo haimaanishi kuwa ubatizo wa maji hauna maana!. (mbele kidogo tutaelewa zaidi umuhimu wake).
Sasa kufuatia mwenendo huo wa Bwana Yesu kutombatiza mtu yeyote, ni kuonyesha kuwa anao ubatizo mwingine ambao atawabatiza nao watu, ambao hakuna mwanadamu yeyote anayeweza kuufanya!… Ubatizo wa maji mwanadamu anaweza kuufanya kwa mwanadamu mwenzake, Lakini ubatizo huo ambao Bwana Yesu atakwenda kuwabatiza nao watu hakuna anayeweza kuufanya zaidi yake yeye mwenyewe.. Na ubatizo huo si mwingine zaidi ya ule wa Roho Mtakatifu.
Tunapobatizwa kwa Maji, miili yetu inazama kwenye maji mengi na kuibuka juu, kama ishara ya kufa na kufufuka na Kristo.. Lakini tunapobatizwa kwa Roho Mtakatifu ni kitendo cha Bwana Yesu kuzichukua roho zetu na kuzizamisha katika Roho Mtakatifu, Ni tendo kuu sana ambalo hakuna mwanadamu yeyote wala malaika yeyote anayeweza kulifanya.. kama maandiko yanavyosema katika Yohana 3:16.
Luka 3:16 “Yohana alijibu akawaambia wote, Kweli mimi nawabatiza kwa maji; lakini yuaja mtu mwenye nguvu kuliko mimi, ambaye mimi sistahili kuilegeza gidamu ya viatu vyake; YEYE ATAWABATIZA KWA ROHO MTAKATIFU NA KWA MOTO”
Hiyo ikimaanisha kuwa kama vile ubatizo wa maji ulivyo wa muhimu vile vile na ubatizo wa Roho Mtakatifu ni wa muhimu sana..Ni lazima tubatizwe na watu katika Maji na vile vile tubatizwe na Bwana Yesu katika Roho Mtakatifu.
Wapo watu wanaosema kuwa ubatizo wa Roho Mtakatifu sio wa muhimu, bali ule wa maji tu unatosha, na wapo wanaosema ubatizo wa Roho Mtakatifu ndio wa muhimu, hivyo mtu akishaupata ubatizo wa Roho Mtakatifu hakuna haja tena ya ubatizo wa maji. Nataka nikuambie kuwa hiyo imani ni imani potofu ambayo imetengenezwa na ufalme wa giza kuwaua watu kiroho, maandiko yanasema “…Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu (Yohana 3:5) ”
Kuzaliwa kwa maji ni ubatizo wa Maji, na kuzaliwa kwa Roho ni ubatizo wa Roho Mtakatifu (Haihitaji elimu kubwa kuelewa hili, ni tafakari nyepesi kabisa).
Na zaidi ya yote tunazidi kuthibitisha kuwa ubatizo wa maji ni wa muhimu hata baada ya kuupokea ule wa Roho Mtakatifu, wakati ule Petro alipofika nyumbani kwa Kornelio, maandiko yanasema baada ya wale watu wa nyumbani kwa Kornelio kushukiwa na Roho Mtakatifu, bado Mtume Petro aliwaagiza wakabatizwe katika maji na kwa jina la Yesu Kristo.
Matendo 10:44 “Petro alipokuwa akisema maneno hayo Roho Mtakatifu akawashukia wote waliolisikia lile neno.
45 Na wale waliotahiriwa, walioamini, wakashangaa, watu wote waliokuja pamoja na Petro, kwa sababu Mataifa nao wamemwagiwa kipawa cha Roho Mtakatifu.
46 Kwa maana waliwasikia wakisema kwa lugha, na kumwadhimisha Mungu. Ndipo Petro akajibu,
47 Ni nani awezaye kuzuia maji, hawa wasibatizwe, watu waliopokea Roho Mtakatifu vile vile kama sisi?
48 Akaamuru wabatizwe kwa Jina lake Yesu Kristo. Ndipo wakamsihi azidi kukaa siku kadha wa kadha”
Umeona?, hao watu walitangulia kubatizwa na Bwana Yesu mwenyewe kwa ubatizo wa Roho mtakatifu, lakini bado walikwenda kubatizwa tena na akina Petro kwa ubatizo wa Maji. Kwasababu Petro alijua kuwa hawa wasipozaliwa kwa Maji na kuwaacha tu wawe wamepokea ubatizo wa Roho hawataweza kuuona ufalme wa Mungu, sawasawa na maneno ya Bwana.
Je! na wewe umebatizwa kwa Maji?.. Kama bado na umeshasikia ukweli namna hii, upo hatarini sana…Na kumbuka kama ulibatizwa uchangani, basi huna budi kubatizwa upya kwa sababu hukuwa umejitambua wakati huo, zaidi sana kama pia ulibatizwa kwa maji machache, ni lazima ubatizwe upya kwa maji mengi (Yohana 3:23)
Na je! umeshabatizwa pia kwa Roho Mtakatifu?.. kama Bado msihi Bwana naye ni mwaminifu atakupa Roho wake mtakatifu, kwasababu yeye anatamani uwe naye kuliko wewe unavyotamani.. lakini ni sharti kwanza utubu kwa kumaanisha kuacha dhambi zako zote na kubatizwa kwa maji kama tayari umeshausikia ukweli, kwa kukamilisha mambo hayo, maandiko yanasema Yule Roho ni kwaajili yetu, na kwa vizazi vyetu, Bwana Yesu anatubatiza kwa huyo bureeeeeeeeee..
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU
JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?
MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.
Tunajua kuwa vya Kaisari tunavyopaswa tumpe ni “kodi” lakini je! Na Vya Mungu ambavyo tunapaswa tumpe ni vipi kulingana na Luka 20:25?
Tuanze kusoma mstari wa 21 ili tuelewe vizuri zaidi..
Luka 20:21 “Wakamwuliza, wakisema, Mwalimu, twajua ya kwamba wasema na kufundisha yaliyo ya haki, wala hujali cheo cha mtu, bali unafundisha njia ya Mungu kwa kweli
22 Je! Ni halali tumpe Kaisari kodi, au sivyo?
23 Lakini yeye alitambua hila yao, akawaambia,
24 Nionyesheni dinari. INA SURA NA ANWANI YA NANI? Wakamjibu, Ya Kaisari.
25 Akawaambia, Basi, vya Kaisari mpeni Kaisari, NA VYA MUNGU MPENI MUNGU.
26 Wala hawakuweza kumshitaki kwa maneno yake mbele ya watu; wakastaajabia majibu yake, wakanyamaa”.
Nataka tujifunze ni vigezo gani Bwana Yesu alitumia hapo kuhalalisha kuwa Kodi ni haki ya Kaisari, hiyo itatusaidia na sisi kujua vilivyo vya Mungu ni vipi?.. Na tunaona hakutumia kitu kingine chochote isipokuwa ile “Sura” inayoonekana kwenye ile sarafu pamoja na ‘Anwani” inayosomeka pale. Kwani Dinari ile ilikuwa na sura ya Kaisari na Anwani ya Kaisari, hivyo ni haki kuwa mali ya Kaisari.
Sasa kama vya Kaisari vilitambulika kwa sura iliyokuwa inaonekana juu ya Sarafu, ni wazi kuwa na vya Mungu vitatambulika kwa njia hiyo hiyo, Maana yake chochote chenye Sura ya Mungu hicho ni cha Mungu, na anapaswa apewe.. Sasa hebu tusome maandiko yafuatayo..
Mwanzo 1:27 “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba”.
Umeona?..Kumbe! sisi tumeumbwa kwa Mfano wa Mungu, Nyuso zetu ni nyuso za Mungu, na kama tumeumbwa kwa mfano na Sura ya Mungu basi ni wazi kuwa sisi (yaani miili yetu na roho zetu) ni mali ya Mungu na si yetu! na hivyo ni LAZIMA TUMPE MUNGU VILIVYO VYAKE…Biblia inasema hivyo kuwa sisi si mali yetu wenyewe..
1Wakorintho 6:19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? WALA NINYI SI MALI YENU WENYEWE”
Na tena inasema Miili yetu ni MALI INAPASWA ITOLEWE KWA BWANA..
1Wakorintho 6:13 “Vyakula ni kwa tumbo, na tumbo ni kwa vyakula; lakini Mungu atavitowesha vyote viwili, tumbo na vyakula. LAKINI MWILI SI KWA ZINAA, BALI NI KWA BWANA, naye Bwana ni kwa mwili”
Hiyo ikiwa na maana kuwa ni lazima tuitoe miili yetu kwa Bwana, ni lazima tumpe MUNGU vilivyo vyake, Tusipofanya hivyo tutakuwa tunafanya makosa makubwa sana..
Sasa tunampaje Mungu vilivyo vyake?
1.KWA KUOKOKA!
Kuokoka maana yake ni kumkabidhi Bwana roho zetu, kwa kutubu dhambi na kubatizwa kwa maji na kwa Roho.(Marko 16:16). Unapomwamini Bwana Yesu na kumkabidhi maisha yako, hapo umempa Mungu vilivyo vyake, na hivyo utakuwa umeyafanya mapenzi ya Mungu.. kwasababu Utu wako wa ndani umeumbwa kwa mfano wake.
2. KWA KUJITENGA NA DHAMBI.
1Wakorintho 6:13 “…LAKINI MWILI SI KWA ZINAA, BALI NI KWA BWANA, naye Bwana ni kwa mwili” Hapa maandiko yanaonesha dhahiri kuwa “mwili si kwa zinaa bali kwa Bwana ” maana yake mtu anayefanya zinaa inaiharibu mali ya Mungu, ambayo ni mwili wake.. Kwasababu mwili wake umeumbwa kwa mfano wa MUNGU, una anwani ya Mungu!!..
Hivyo si ruhusa kuuharibu kwa zinaa, au kwa pombe, au kwa sigara, au kwa kuuandika tattoo au kwa kuuvisha jinsi mtu atakavyo (nguo za kubana au zisizo za maadili) au kwa mambo mengine yote yanayofanana na hayo..
Hivyo kwa hitimisho ni kwamba.. Vya Mungu anavyopaswa apewe ni ROHO ZETU, na MIILI YETU. Kwasababu vitu hivyo vina sura na anwani ya Mungu mwenyewe, kama vile dinari iliyokuwa na sura na anwani ya Kaisari.
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Nini maana ya tumeumbwa kwa mfano na sura ya Mungu?
Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?
Naomba kufahamu maana ya “sura ya kijiti” katika Marko 12:26.
Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?
Nuru yetu inapaswa iangaze au isiangaze kulingana na Mathayo 5:16 na Mathayo 6:1?
Je unajua kwamba kuikaribia dhambi ni “DHAMBI”, Hata tu kabla ya kuifanya?.
Mungu hakumpa tu Adamu maagizo ya kutokula yale matunda ya mti wa katikati…bali pia alimwambia “Asiyaguse yale matunda”..asije akafa. Wengi wetu tunaona tu habari ya “kula” kama kosa, lakini hatujui kuwa Mungu aliwaagiza kwamba hata kuyagusa wasiyaguse, (maana yake wakae mbali nayo).
Mwanzo 3:2 “Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula;
3 lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala MSIYAGUSE, msije mkafa”.
Kumbe hata wangeyagusa tu yale matunda bila hata ya kuyala, bado Wangekufa!!.
Hii ni hatari sana..na inatupa fundisho kubwa sana..
Kwanini Mungu akataze wasiyaguse?..Je kuna ubaya wowote katika kuyagusa???… Jibu ni ndio!… kwasababu chanzo cha dhambi ya kula tunda ni kulishika lile tunda kwanza, (Hawa asingeweza kulipeleka mdomoni kabla ya kulishika) kabla ya kulichunguza chunguza kwanza, kabla ya kulidadisi dadisi, ndipo akaangukia katika ushawishi wa kulila.
Hivyo Mungu aliona chanzo cha dhambi kuwa ni “kushika” ndipo akatoa maagizo kwamba WASIYAGUSE!! Wasije wakafa… lakini wenyewe (Waligusa, na tena wakala) Hivyo ikawa ni makosa mawili yaliyozaa Mauti kamilifu.
Na hata leo Bwana anatuonya tukae mbali na dhambi, tusiikaribie kabisa dhambi, tusiiguse dhambi licha ya kuitenda!!..
Tukae mbali na Wizi kama ya wizi wenyewe kutendeka,…tukae mbali na Ulevi kabla ya ulevi wenyewe kutendeka… tukae mbali na Utukanaji, Uadui, Kiburi, Uasherati, kabla ya kufanya mambo hayo (Wagalatia 5:19-20)… Tusizikaribie kabisa hizi dhambi!!.. tukae nazo mbali maili nyingi sana, kwasababu kitendo cha kuzikaribia tu tayari ni kosa..
leo hii utaona mtu anasema hazini, wala hafanyi uasherati lakini katika simu yake kumejaa picha zinazochochea mambo hayo, kumejaa miziki inayochochoea mambo hayo, kumejaa filamu zi kidunia zenye maudhui hayo ya kiasherati, simu yake imejaa magroup ya mizaha, na uhuni, unaochochea mambo hayo…pasipo kujua kuwa anafanya makosa makubwa kuisogelea dhambi kwa namna hiyo..
Neno la Mungu linasema kwamba tuikimbie zinaa, sio tuishi nayo, au tuikemee!..bali tuikimbie (Soma 1Wakorintho 6:18 )...kama vile Yusufu alivyoikimbia mbele ya mke wa Potifa, na sisi tunapaswa tuikimbia hivyo hivyo Yusufu hata hakukubali kuzungumza na Yule mwanamke..
Lakini ni kinyume chake katika siku hizi za mwisho, utaona binti anayekiri kumpokea Yesu anapiga maneno na mwanaume anayemtaka, kijana anayekiri kumpokea Yesu anapiga maneno ya kidunia na binti anayemtamani, na hata kufanya naye mizaha..Hii ni hatari kubwa!, kumbuka ushawishi wa Hawa kula tunda haukuanzia mdomoni bali mkononi!..baada ya kulishika ndipo ushawishi ukamwingia..
Na sisi tukijishikamanisha na dhambi, basi ni lazima tutazitenda tu!, haijalishi itachukua muda gani ni lazima tutazitenda tu!…Hauwezi kusema umeacha utukanaji, lakini kila kukicha kampani zako ni za watu wanaotukana…ni lazima tu na wewe utatukana, haijalishi itakuchukua muda gani kudumu bila kutukana lakini mwisho wa siku utaishia kurudia matukano tu.
Hauwezi kukaa unasikiliza usengenyaji na wewe usiwe msengenyaji..ni suala la muda tu!, utajikuta na wewe upo kama wao.. Kumbuka Adamu na Hawa waliambiwa “wasiukaribie kabisa ule mti, na hata kuugusa”.. Vile vile na sisi leo hii tunapaswa tusiikaribie miti ya dhambi…wala tusiguse mashina yake wala matawi yake.. maana kugusa ndio chanzo cha kula..
Bwana atusaidie na kutuwezesha katika yote.
Maran atha!
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
MUME / MKE BORA KUTOKA KWA BWANA UTAMWONA UKIWA KATIKA MAZINGIRA GANI?
HUJAPEWA MBAWA ZA KUKIMBIA MATATIZO
FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.
Tofauti na Kalenda ya Kirumi ambayo ndiyo tunayoitumia sasa yenye miezi 12, Kalenda ya kiyahudi yenyewe inakuwa na miezi 13 kwa mara saba kila baada ya miaka 19. (Yaani katika kipindi cha miaka 19, miaka 7 inakuwa na miezi 13, na miaka 12 iliyosalia inakuwa na miezi 12 kama kawaida), Na miaka yenye miezi 13 ni inakuwa ni mwaka wa 3, 6,8,11,14, 17 na 19 na mzunguko wa miaka 19, unapoisha na unapoanza mzunguko mwingine, basi mgawanyo wa miezi unakuwa ni huo huo, wa baadhi ya miaka kuwa na miezi 13 na mingine 12.
Sasa mwezi wa 13, unaoongezeka juu ya miezi 12 ya kiyahudi ni mwezi ujulikanao kama Adari II, Sasa kabla ya kwenda kuutazama huu mwezi wa 13 wa Adari, hebu tuitazame miezi 12, na rejea zao katika biblia.
Mwezi wa 1: Abibu au Nisani.
Mwezi wa Abibu au Nisani ni mwezi wa kwanza katika kalenda ya kiyahudi, mwezi huu unaanza katika mwezi Machi katikati na kuisha mwezi Aprili katikati katika kalenda yetu ya kirumi tunayoitumia..
Mwezi wa Abibu ndio mwezi ambao wana wa Israeli walitoka Misri..
kutoka 13:3 Musa akawaambia hao watu, Kumbukeni siku hii, mliyotoka nchi ya Misri, kutoka nyumba ya utumwa; kwa kuwa Bwana aliwatoa mahali hapa kwa nguvu za mkono wake; na usiliwe mkate uliochachwa.
4 Ninyi mwatoka leo katika MWEZI WA ABIBU.
Na wakati ambapo Hamani ananyanyuka kutaka kuwaangamiza Israeli yote katika ufalme wote wa Ahasuero, tunasoma wazo hili lilimjia katika Mwezi wa Nisani/ Abibu..
Esta 3:7 “Basi mwezi wa kwanza, ndio MWEZI WA NISANI, mwaka wa kumi na mbili wa mfalme Ahasuero, wakapiga Puri, yaani kura, mbele yake Hamani; siku kwa siku, na mwezi kwa mwezi, hata mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari”.
Na pia tunausoma huu mwezi ukitajwa wakati Nehemia alipoingiwa na wazo la kwenda kuujenga Yerusalemu..
Nehemia 2:1 “Ikawa katika MWEZI WA NISANI, mwaka wa ishirini wa mfalme Artashasta, na divai imewekwa mbele yake, nikaishika ile divai, nikampa mfalme. Nami mpaka sasa sikuwa na huzuni mbele ya mfalme wakati wo wote.”.
Mwezi wa 2: Zivu au Ayari
Mwezi huu unaangukia kati ya mwezi Aprili na mwezi May kwa kalenda yetu tunayoitumia, na ni mwezi wa pili katika kalenda ya kiyahudi.
Mwezi huu ndio mwezi ambao Mfalme Sulemani alianza kulijenga Hekalu la Mungu katika Yerusalemu..
1Wafalme 6:1 “Ikawa katika mwaka wa mia nne na themanini baada ya kutoka wana wa Israeli katika nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa kutawala kwake Sulemani juu ya Israeli, katika MWEZI WA ZIVU, ndio mwezi wa pili, akaanza kuijenga nyumba ya Bwana.
2 Nayo nyumba hiyo mfalme Sulemani aliyomjengea Bwana, urefu wake ulikuwa mikono sitini, na upana wake ishirini, na kwenda juu kwake mikono thelathini”.
Mwezi wa 3: Siwani
Huu ni mwezi wa tatu kwa kalenda ya kiyahudi, lakini kwa kalenda yetu ni mwezi unaoangukia kati ya mwezi Mei na mwezi Juni.
Katika mwezi huu ndio mwezi ambao Mfalme Ahasuero, enzi za malkia Esta alitoa ruksa kwa wayahudi kujilipizia kisasi juu ya adui zao.
Esta 8:9 “Basi, waandishi wa mfalme wakaitwa pale pale, siku ya ishirini na tatu ya mwezi wa tatu, ndio MWEZI WA SIWANI; na kama vile Mordekai alivyoamuru, Wayahudi wakaandikiwa, pamoja na maakida na maliwali, na wakuu wa majimbo toka Bara Hindi mpaka Kushi, majimbo mia na ishirini na saba, kila jimbo kwa mwandiko wake, na kila taifa kwa lugha yake; na Wayahudi kwa mwandiko wao na kwa lugha yao”.
Mwezi wa 4: Tamuzi
Huu ni mwezi wa Nne katika kalenda ya kiyahudi, lakini kwetu sisi unaanguka katika ya mwezi Juni na mwezi Juni na mwezi Julai.
Mwezi huu katika bibli unaonekana kutajwa mara moja tu katika kitabu cha Ezekieli.
Ezekieli 8:14 “Ndipo akanileta mpaka mlango wa kuingilia katika nyumba ya Bwana, ulioelekea upande wa kaskazini, na tazama, wanawake wameketi wakimlilia TAMUZI”.
Mwezi huu wa nne umetajwa sehemu nyingine kama kwa namba na si kwa jina (Soma Yeremia 39:1-2, na Yeremia 52:6-7).
Mwezi wa 5: Avu
Huu ni mwezi wa tano kwa wayahudi na kwetu sisi unaangukia kati ya mwezi wa Julai na Mwezi Agosti.. Mwezi huu katika biblia haijatajwa kwa jina bali kwa namba..
Kwamfano tunasoma Ezra aliwasili Yerusalemu katika mwezi wa 5
Ezra 7:8 “Naye Ezra akafika Yerusalemu mwezi wa tano katika mwaka wa saba wa huyo mfalme”
Na pia katika (2 Wafalme 25:8-10, Yeremia 1:3 na Yeremia 52:12-30)
Mwezi wa 6: Eluli
Huu ni mwezi wa 6 kwa kalenda ya kiyahudi na unaangukia kati ya mwezi wa Agosti na Septemba katika kalenda yetu.
Katika biblia mwezi huu ndio mwezi ambao Nehemia alimaliza kati ya kuukarabati ukuta Yerusalemu..
Nehemia 6:15 “Basi huo ukuta ukamalizika siku ya ishirini na tano ya mwezi wa ELULI, katika muda wa siku hamsini na mbili”
Mwezi huu pia umetajwa kwa namba katika kitabu cha Hegai 1:14-15.
Mwezi wa 7: Ethanimu
Huu ni mwezi wa 7 kwa kalenda ya kiyahudi na kwa kalenda yetu unaangukia katika ya mwezi wa Septemba na Oktoba.
Hekalu la Sulemani liliwekwa wakfu katika mwezi huu wa Ethanimu
1Wafalme 8:1 “Ndipo Sulemani alipowakusanya wazee wa Israeli, na wakuu wote wa kabila, wakuu wa mbari za mababa wa wana wa Israeli, wamwendee mfalme Sulemani huko Yerusalemu, ili walipandishe sanduku la agano la Bwana kutoka mji wa Daudi, yaani, Sayuni.
2 Wakakutana mbele ya mfalme Sulemani watu wote wa Israeli wakati wa sikukuu, katika MWEZI WA ETHANIMU, ndio mwezi wa saba. 3 Wazee wote wa Israeli wakaja, nao makuhani wakajitwika sanduku”
Unaweza kuusoma pia mwezi huu katika..(1Wafalme 8:2, Walawi 23:24, Nehemia 8:13-15).
Mwezi wa 8: Buli.
Mwezi huu ni mwezi wa 8 kwa kalenda ya kiyahudi na unaangukia kati ya mwezi Octoba na mwezi mwezi Novemba katika kalenda yetu ya kirumi.
Katika mwezi huu ndio mwezi ambao Sulemani alimaliza kuijenga nyumba ya Mungu (Hekalu).
1Wafalme 6:38 “Hata katika mwaka wa kumi na mmoja, katika MWEZI WA BULI, ndio mwezi wa nane, nyumba ikaisha, mambo yake yote, na sharti zake zote. Basi muda wa miaka saba alikuwa katika kuijenga.
Unaweza kusoma pia habari za mwezi huu katika (1Wafalme 12:32-33, 1Nyakati 27:11).
Mwezi wa 9: Kisleu
Huu ni mwezi wa 9 kwa kalenda ya kiyahudi na unaangukia kati ya mwezi wa Novemba na Disemba katika kalenda yetu ya sasa ya kirumi.
Katika mwezi huu Nabii Zekaria alioneshwa maono juu ya Yuda na Israeli.
Zekaria 7:1 “Ikawa katika mwaka wa nne wa mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia Zekaria, siku ya nne ya mwezi wa kenda, yaani, KISLEU”
Mwezi wa 10: Tebethi
Huu ni mwezi wa 10 kwa Wayahudi na kwa kalenda ya kirumi unaangukia kati ya mwezi Disemba na January.
Katika biblia mwezi huu ndio mwezi ambao Esta aliingizwa katika nyumba ya kifalme..
Esta 2:16 “Basi Esta alipelekwa kwa mfalme Ahasuero, katika nyumba ya kifalme, mwezi wa kumi, ndio mwezi wa Tebethi, mwaka wa saba wa kumiliki kwake.
17 Mfalme akampenda Esta kuliko wanawake wote, naye akapata neema na kibali machoni pake kuliko mabikira wote; basi akamtia taji ya kifalme kichwani pake, akamfanya awe malkia badala ya Vashti”.
Na ndio mwezi ambao Nebukadreza aliuhusuru Yerusalemu (2Wafalme 25:1, Yeremia 52:4).
Mwezi wa 11: Shebati
Mwezi huu unaangukia kati ya mwezi Januari na mwezi Februari kwa kalenda ya kirumi na katika kalenda ya kiyahudi ni mwezi wa 11.
Katika mwezi huu ndio mwezi ambao Zekaria aliona maono tena juu ya Yerusalemu..
Zekaria 1:7 “Siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani, mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa Dario, neno la Bwana lilimjia Zekaria, mwana wa Berekia, mwana wa Ido, nabii, kusema,
8 Naliona wakati wa usiku, na tazama, mtu amepanda farasi mwekundu, akasimama kati ya mihadasi iliyokuwa mahali penye uvuli; na nyuma yake walikuwapo farasi wengine wekundu, na wa rangi ya kijivujivu, na weupe”.
Mwezi wa 12: Adari I.
Huu ni mwezi wa 12 na wa mwisho kwa kalenda za kiyahudi, ambapo kwa kalenda ya kirumi unaangukia kati ya Mwezi Februari na mwezi Machi.
Esta 3:7 “Basi mwezi wa kwanza, ndio mwezi wa Nisani, mwaka wa kumi na mbili wa mfalme Ahasuero, wakapiga Puri, yaani kura, mbele yake Hamani; siku kwa siku, na mwezi kwa mwezi, hata mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari”.
Kutokana na kuwepo na miaka mirefu na mifupi, Marabi wa kiyahudi katika karne ya 4, wakiongozwa na Rabbi Hillel II, waliongeza mwezi mmoja wa 13, katika kalenda ya kiyahudi ambao waliuita mwezi ADARI II (Adari wa pili).
Lengo la kuongeza mwezi huu ni ili kuziweka sikukuu za kiyahudi katika majira halisia, vinginevyo sikukuu za kiyahudi zingeangukia misimu ambayo sio, kwamfano sikukuu ya pasaka ambayo kwa wayahudi inaseherekewa katika mwezi wa March au April kwa kalenda yetu, kama kusingekuwepo huu mwezi wa 13, basi huenda miaka mingine sikukuu hii ingeangukia mwezi wa 8 kwa kalenda yetu, jambo ambalo lingekuwa halina uhalisia hata kidogo.
Lakini swali ni je!, sisi wakristo tunapaswa kuifuata kalenda ipi?, ya kiyahudi au hii inayotumika sasa ya kirumi?
Jibu ni kuwa Kalenda hazitusogezi karibu na Mungu wala hazipeleki mbali na Mungu, tukitumia kalenda ya kiyahudi, au ya kirumi au ya kichina au hata ya kichaga haituongezei chochote, kilicho cha muhimu ni kuishi kwa kuukomboa wakati kama biblia inavyosema katika..
Waefeso 5:15 “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;
16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu”
Na tunaukomboa wakati kwa kufanya yale yanayotupasa kufanya, ikiwemo Kujitakasa, kufanya ibada, kuomba, kusoma Neno, kuifanya kazi ya Mungu kupitia karama iliyo ndani yako kabla ya ule mwisho kufika na mambo mengine yote yanayohusiana na hayo.
Bwana akubariki.
Maran atha.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Mwandamo wa mwezi/Mwezi mpya Ni nini kibiblia?
UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?
Je! kuna sikukuu za pasaka mbili? (Hesabu 9:11)
Je! ni sahihi kwa Mkristo kusherekea siku yake ya kuzaliwa.[Birth day]?
2Timotheo 1:6 “Kwa sababu hiyo nakukumbusha, uichochee karama ya Mungu, iliyo ndani yako kwa kuwekewa mikono yangu”.
Nakusalimu katika jina la Yesu Kristo.
Neno la Mungu linatufundisha kuzichochea KARAMA tulizopewa,.. Ikiwa na maana kuwa “Kuwa na karamaa pekee haitoshi kuifanya kazi ya Mungu vizuri”..bali inahitajika Karama iliyochochewa. Na anayeichochoea si Mungu, bali ni sisi ndio tunaoichochea.
Mtu anapomgeukia Kristo na kuokoka, tayari Mungu anakuwa ameiweka karama ndani yake, kama mbegu ndogo sana.. Lakini karama ile isipochochewa inaweza kufa ndani ya mtu, na hatimaye mtu yule akabaki kama mtu asiye na karama kabisa.
Hata wanaoshiriki michezo ya kidunia, ijapokuwa wanavyo vipaji vya michezo hiyo, lakini wasipovifanya mazoezi ya kutosha, haijalishi wana vipaji vikubwa kiasi gani, bado vipaji vyao hivyo vitakuwa si kitu. Na vipaji vina muda wake, mwanamichezo akifikia umri Fulani kama hajakitumia vizuri kipaji chake, basi kinapungua nguvu chenyewe, kwasababu tayari umri umeshaenda!.
Na karama za rohoni au vipaji vya rohoni ni ivyo hivyo.. visipochochewa vinakufa na visipotumika katika muda fulani, vinaisha thamani nguvu ndani yake..Ndio maana maandiko yanasema..
Mhubiri 12:1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo.
2 Kabla jua, na nuru, na mwezi, Na nyota, havijatiwa giza; Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua”
Na pia inasema..
1Yohana 2:14 “…..Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu”
Sasa maandiko yanasema Bwana alitoa wengine kuwa mitume, wengine manabii, wachungaji, waalimu, wainjilisti, karama za kuponya, matendo ya miujiza, karama za lugha, karama za masaidiano, imani, hekima, maarifa n.k (kasome Waefeso 4:11-12, 1Wakorintho 12). Lakini wengi hawajijui kama wanazo hizo karama.. kwasababu wanadhani zinaanza katika ukubwa wanaotugemea wao.
Wengi sana leo hii ni wainjilisti tangu siku ile wanapookoka, lakini kwasababu hawajijui kama wao ni wainjlisti, pale wanapojiona kuwa hawafanani na mwinjilisti mmoja maarufu, basi moto unazima ndani yao, pasipo kujua kama wanamzimisha roho, wengi ni waalimu tangu siku ile wanapookoka, lakini kwasababu hawajui namna ya kuzitumia karama zao na wanapoona wao si kama waalimu Fulani maarufu wanaowajua basi moto unazima ndani yao, wanabaki kusubiria muujiza siku moja wajikute wamekuwa wahubiri wenye uwezo wa kuhubiri kama watu Fulani maarufu.
Wengi wamepewa karama za kumwimbia Mungu, tangu siku walipookoka lakini kwasababu wanajiona kama sauti zao bado zinakwaruza, kwa kujilinganisha na wengine ambao tayari wanamwimbia Mungu kwa muda mrefu, basi wanatulia huku wakisubiri muujiza mwingine uwashukie utakaowafanya wawe kama hao wengine.
Kungoja huko ndiko kunakuua karama za watu wengi ndani yao.
Leo tutatazama njia 3, za namna ya kuzichochea karama zetu ili zifanye kazi katika viwango ambavyo Mungu amevikusudia.
1.KUJIFUNZA NENO.
Msingi wa karama zote ni Neno la Mungu, mtu aliyepungukiwa Neno la Mungu ndani yake, tayari karama yake inazima yenyewe tu ndani yake.. Kwanini Neno la Mungu??… kwasababu Neno la Mungu linatia hamasa, linatia moyo, linatupa sababu ya kuzitumia karama zetu, linafundisha jinsi ya kuzitumia kupitia mifano mbali mbali ya watumishi wa Mungu ndani ya biblia, na pia linatuonya madhara ya kutozitumia karama zetu. Hivyo Mtu mwenye Neno la Mungu la kutosha ni lazima tu karama yake itanyanyuka.
2. MAOMBI.
Hii ni njia ya pili ya kuchochoe karama zetu, Maandiko yanasesema tuombe bila kukoma (1Wathesalonike 5:17), Na kuomba kunajumuisha pia na kufunga, vitu hivi viwili vinaenda pamoja..tunapoomba Bwana anatuongezea uwezo na upako katika karama zetu.
Mathayo 17:21 “Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.”
3. MAZOEZI.
Hii ni njia ya tatu na ya muhimu sana, chochote kisichofanyiwa mazoezi hakiwezi kuwa bora.. hata karama isipofanyiwa mazoezi haiwezi kuwa bora, maana yake ni kwamba kama wewe una karama ya kuimba, kamwe usitegemee utakuwa bora, bila kuifanyia mazoezi karama hiyo, ni lazima uwe na vipindi vya kuinoa sauti yako, kutafuta na kujifunza jinsi ya kuzipangilia sauti kupitia waliokutangulia au waalimu, huku wewe mwenyewe ukifanya mazoezi ya kurudia rudia mara kadhaa… hivyo ndivyo karama yako itakavyoongezeka nguvu, lakini ukiiacha tu na kujiona tayari unajua kila kitu, basi hutaweza kupiga hatua..
Vile vile kama umepewa karama ya kiualimu, au kiinjiilisti..kama utaketi tu kusubiri kufundishwa, basi kamwe hutaweza kufundisha wengine..unapaswa utenge muda wa wewe kwenda kufundisha wengine, hata kama bado hujui vitu vingi,.. wewe kafundishe hivyo hivyo, Bwana atakufundisha huko mbele ya safari, makosa utakayoyafanya ndiyo yatakuwa darasa lako la kufanya vizuri katika matukio ya mbele..hivyo usiogope, nenda kahubiri..
Vile vile kama umepewa karama ya matendo ya imani, au karama za kuponya, usingoje ngoje.. nenda mahospitalini, nenda sehemu mbali mbali kafanye maombezi huku ukiwahubiria habari za njema za wokovu, usiogope wala kuvunjika moyo, unapoona umeombea watu 10, na hakuna aliyepona hata mmoja.. wewe endelea mbele, hizo ni hatua za awali, katika matukio yanayokuja Bwana atakutumia kwa maajabu mengi.
Na karama nyingine zote ni hivyo hivyo, ni lazima UZICHOCHEE!!..kama vile moto unavyochochewa.
Na ulingo mzuri wa kuiona karama yako ikifanya kazi ni ndani ya KANISA, yaani unapokuwa katika kusanyiko la Kristo ni kipindi kizuri cha kuiona karama yako kuliko unapokuwa nje ya kusanyiko, kwasababu Biblia inasema karama hizi lengo lake la kwanza ni kuujenga mwili wa Kristo, maana yake kulijenga kanisa (Waefeso 4:11).
Ichochee karama yako!
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Nini tofauti kati ya Kipawa na Karama?
Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?
Kiburi ni nini?
Kulingana na biblia kiburi “ni hali ya mtu kujiinua kifikra, na kuamini kuwa hahitaji msaada wowote kutoka kwingine”. Hali hii inaambatana na kudhihirisha tabia nyingine ndogo ndogo kama majivuno, matukano, au kuwadharau wengine, au kuwa na ujasiri kupitiliza na hata kukufuru.
Viburi vimegawanyika katika sehemu mbili (2);KIBURI BINAFSI, na KIBURI CHA UZIMA.
KIBURI BINAFSI:
Kiburi binafsi ni kile kinachomfanya mtu aamini kuwa Mawazo yake, au maamuzi yake, au msimamo wake ni thabiti na hauwezi kubadilishwa na yeyote. Mtu mwenye kiburi binafsi hata aambiwe ukweli kiasi gani, au athibitishiwe jambo kiasi gani bado huwa habadiliki. Tayari anachokiamini, au alichokiamua amekiamua!. Mtu mwenye aina hii ya kiburi anakuwa pia ni mbishi na mtu wa mashindano, na anakuwa anajiona yeye ni bora kuliko wengine wote..
Mithali 13:10 “Kiburi huleta mashindano tu; Bali hekima hukaa nao wanaoshauriana”.
Kiburi binafsi kipo kwa Wakristo na kwa wasio waKristo..
Kwa wakristo ni pale ambapo mtu hataki kuambiwa jambo wala kuelekezwa ndani ya kanisa…yeye mawazo yake ndio bora siku zote, au njia zake ndio bora, na zaidi ya yote anakuwa anapenda kuwa juu ya wote, na anawadharau wengine wote…
WaKristo wenye kiburi cha namna hii Bwana amesema anapingana nao…
1Petro 5: 5 “..ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa SABABU MUNGU HUWAPINGA WENYE KIBURI, lakini huwapa wanyenyekevu neema”.
Mithali 29:23 “Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa”.
Kwa wasio wakristo ni pale ambapo mtu hashauriwi na yeyote, juu ya jambo lolote, hata aambiwe vipi anakuwa yupo vile vile, yeye ni wa kuelekeza tu na sio wa kuelekezwa.
KIBURI CHA UZIMA:
Kiburi cha uzima ni kile kinachozungumziwa katika.. 1 Yohana 2:16
“Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na KIBURI CHA UZIMA, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.”
Kiburi cha Uzima ni kiburi kinachompata mtu kutokana na Vitu alivyonavyo, au anavyotegemea kuwa navyo..
Watu wengi wenye mali wanakuwa na hiki kiburi(japokuwa si wote, bali asilimia kubwa).. Wanaona mtu asiyekuwa na mali kama wao hawezi kuwaambia chochote,..kiburi hiki cha mali kinamfanya mtu aone hata Mungu hana maana, Neno la Mungu kwake ni kama habari zilizopitwa na wakati.
Kulifanyia mizaha Neno la Mungu, ni habari ya kawaida kwao…hata wasikie maonyo ya Mungu kiasi gani, kwao ni habari tu upuuzi.. Mioyo yao imeinuka kutokana na Mali au vitu walivyonavyo, wanaona wanaweza kula hata pasipo kumwomba Mungu, wanaweza kuendeleza maisha yao hata pasipo kupiga magoti.. hivyo hawamhitaji Mungu tena..
Kiburi hiki ndio kibaya kuliko vyote, na ndicho kilichozungumziwa sehemu nyingi katika biblia.. naa watu wote wenye hiki kiburi, biblia imeandika hatima yao..
Isaya 2:12 “Kwa maana kutakuwa siku ya Bwana wa majeshi juu ya watu wote WENYE KIBURI NA MAJIVUNO, na juu ya yote yaliyoinuka; nayo yatashushwa chini.”
Mithali 16:5 “Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa Bwana; Hakika, hatakosa adhabu”.
Mithali 8:13 “Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; Kiburi na majivuno, na njia mbovu, Na kinywa cha ukaidi pia nakichukia.”’
Ayubu 40:12 “Mtazame kila mtu mwenye kiburi ukamshushe, Ukawakanyage waovu hapo wasimamapo”.
Zaburi 119:21 “Umewakemea wenye kiburi, Wamelaaniwa waendao mbali na maagizo yako”.
Soma pia Mithali 21:4, Mithali 16:18, Zaburi 31:18, Zaburi 119:51, Mithali 11:2, na Malaki 4:1 biblia imeelezea zaidi juu ya kiburi na madhara yake..
Tujiepushe na kiburi, tunyenyekee chini ya mkono wa Mungu ulio hodari
Bwana akubariki.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.