Category Archive maswali na majibu

Nini maana ya mbingu na nchi zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe? (Mathayo 24:35).

Jibu: Turejee,

Mathayo 24:35  “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe”

Ili tuelewe vizuri, tutafakari kwanza mstari ufuatao…

Waebrania 13:8 “Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele”.

Mpaka maandiko yaseme kuwa “Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele”… Maana yake kuna watu, au vitu ambavyo haviwezi kuwa vile vile jana, leo na hata milele.

Kwa mfano mtu hawezi kuwa na tabia ile ile, au msimamo ule ule jana na leo na hata milele,..ni lazima tu utafika wakati tabia yake itabadilika, mtazamo wake utabadilika, utendaji wake utabadilika au hata msimamo wake!…. lakini KRISTO YESU yeye ni yule yule, kitabia, na kiutendaji, hajawahi kusema jambo halafu akajikosoa.. ni yeye yule na ataendelea kuwa vile vile Milele.

Hali kadhalika, vitu tunavyoviona katika mbingu kama jua, mwezi  na nyota, ijapokuwa tunaona vimedumu kuwa vilevile kwa maelfu ya miaka, lakini biblia inatabiri kuwa siku moja vitatoweshwa vyote…

Ufunuo 6:12 “Nami nikaona, alipoifungua muhuri ya sita, palikuwa na tetemeko kuu la nchi; jua likawa jeusi kama gunia la singa, mwezi wote ukawa kama damu,

13  na NYOTA ZIKAANGUKA juu ya nchi kama vile mtini upukutishavyo mapooza yake, utikiswapo na upepo mwingi.

14  MBINGU ZIKAONDOLEWA KAMA UKURASA ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake”.

Vile vile vitu tunavyoviona katika “NCHI” kama vile milima, na habari ambavyo tunaviona kama zimedumu kwa maelfu ya miaka, lakini bado biblia inatabiri kuwa siku moja vitafutika..

Ufunuo 16:20  “Kila kisiwa kikakimbia, wala milima haikuonekana tena”

Soma pia Ufunuo 21:1..

Lakini wakati ambapo vitu vyote hivi vinaondolewa (maana yake VINAPITA) Bado Kristo atabaki kuwa yeye yule, na maneno yake yatabaki kuwa yale yale, na yana nguvu ile ile katika umilele wote.

Kwamfano maneno ya Yesu anayosema yeye ni ALFA na OMEGA, yaani Mwanzo na Mwisho (katika Ufunuo 21:6 na Ufunuo 22:13) yataendelea kuwa hivyo hivyo Milele, hakuna wakati utafika Kristo ataacha kuwa Alfa na Omega…jua na mwezi na nyota na wanadamu watapita, lakini maneno hayo yataeendelea kuwa halisi hivyo hivyo milele na milele.

>Vile vile maneno yake aliyosema kuwa “Yeye ndio Njia, Kweli na Uzima (Yohana 14:6)” yataendelea kuwa hivyo milele na milele, hakuna wakati utafika ambao Kristo ataacha kuwa Njia, au ataacha kuwa  Kweli au ataacha kuwa Uzima..Kristo YESU sasa ni Uzima, na ataendelea kuwa UZIMA hivyo hivyo milele na milele.

>Vile vile aliposema kuwa yeye ni “Nuru ya Ulimwengu (Yohana 8:12)”…Maneno hayo hautafika wakati ambao yata-expire… Jua na mwezi kuna wakati vitaisha muda wake wa matumizi, jua litaondolewa halitamulika tena, na mwezi utaondolewa hautaangaza tena.. lakini Kristo ataendelea kuwa NURU hata kipindi ambacho jua na mwezi havipo..

Ufunuo 21:23  “Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, KWA MAANA UTUKUFU WA MUNGU HUUTIA NURU, NA TAA YAKE NI MWANA-KONDOO”.

> Vile vile maneno yake mengine yanamtaja yeye kama “Mwaminifu na wa Kweli (katika Ufunuo 3:14, na Ufunuo 19:11)”. Yeye atabaki kuwa hivyo Milele na milele, hakuna wakati ambao atabadilika na kukosa uaminifu!… Sisi wanadamu tunaoishi chini ya jua na juu ya nchi, tutakuwa waaminifu tu kwa kitambo Fulani lakini si milele. Lakini yeye ataendelea kuwa mwaminifu milele na milele hata wakati ambao mbingu zitafutwa, na kuletwa mbingu mpya na nchi mpya, bado ataendelea kuwa mwaminifu.

> Pia alisema wote wamwaminio yeye watakuwa na uzima wa milele, hakuna wakati hilo Neno litabadilika, kwamba awanyime uzima wa milele wale wote waliomwamini na kuishi kwa kuzifuata amri zake.. Majira yatabadilika, vipindi vitabadilika lakini milele na milele hawezi kujisahihisha maneno yake hayo. AKIAHIDI AMEAHIDI!!.. Na milele habadiliki.

Na maneno mengine yote yaliyosalia aliyoyasema BWANA YESU hakuna hata moja litapita!!! , yote yatabaki kuwa vile vile

Je umemwamini huyu Mkuu wa UZIMA asiyeweza KUBADILIKA?, Au Unawatumainia wanadamu ambao leo wapo na kesho hawapo, leo wanaahidi na kesho wamebadilika, leo wanakupenda kesho wanakuchukia.. Ni heri ukaanza kumtumainia yeye asiyeweza kubadilika, YESU KRISTO, MFALME WA WAFALME, na BWANA WA MABWANA.

Mungu akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Mafundisho Mengine

Mbinguni ni sehemu gani?

Kuna Mbingu ngapi?

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

INJILI YA MILELE NI IPI KATIKA BIBLIA?

Je! Sulemani alienda mbinguni?

Rudi Nyumbani:

 

 

Print this post

Gudulia ni nini? (1Samweli 26:11).

Jibu: Tusome,

1Samweli 26:11 “Hasha! Nisiunyoshe mkono wangu juu ya masihi

12 Basi Daudi akalitwaa lile fumo, na lile GUDULIA LA MAJI, kichwani pa Sauli; nao wakaenda zao, wala hapana mtu aliyeliona jambo hili wala kulijua, wala kuamka; maana wote walikuwa wamelala; kwa kuwa usingizi mzito kutoka kwa Bwana umewaangukia”.

Gudulia ni chombo maalumu kilivyotengenezwa kwa lengo la kuhifadhia maji ya kunywa ya watu wachache, kwa lugha ya sasa hivi tunayaita “majagi”

Magudulia/majagi ya zamani yalitengenezwa kwa malighafi tofauti na ya zama hizi. Zamani majagi/magudulia waliyatengeneza kwa kutumia udongo wa (mfinyanzi tazama picha juu), lakini sasa yanayotumika mengi yao yametengenezwa kwa glasi au plastiki.(tazama picha chini).

Gudulia ni nini?

Mistari mingine inayotaja chombo hiki (gudulia) ni pamoja na 1Wafalme 19:6, Yeremia 19:1 na Yeremia 19:10.

Je umemwamini Bwana Yesu?, je unajua kuwa tunaishi katika majira ya kurudi kwa YESU mara ya pili, na wakati wowote unyakuo wa kanisa utatokea?.

Bwana atusaidie.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Shilo ni wapi?

TWEKA MPAKA VILINDINI.

WALA HAKUACHA MTU ACHUKUE CHOMBO KATI YA HEKALU.

Ni nani aliyemshawishi Daudi akawahesabu Israeli? Ni Mungu au shetani?

JINSI YA KUISHINDA HALI YA MSONGO WA MAWAZO.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “SAA INAKUJA” na “SASA IPO” (Yohana 4:23).

Jibu: Turejee,

Yohana 4:19  “Yule mwanamke akamwambia, Bwana, naona ya kuwa u nabii!

20  Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia.

21  Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.

22  Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.

23  Lakini SAA INAKUJA, NAYO SASA IPO, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba KATIKA ROHO NA KWELI. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu”.

Maana ya kumwabudu Baba katika roho na kweli, ni KUMFANYIA MUNGU IBADA, KATIKA ROHO MTAKATIFU NA KATIKA KWELI YA NENO LAKE.

Yohana 16:13 “Lakini yeye atakapokuja, huyo ROHO WA KWELI, ATAWAONGOZA AWATIE KWENYE KWELI YOTE…”

Sasa BWANA YESU aliposema kuwa “SAA INAKUJA”, alimaanisha kuwa kuna kipindi kinakuja  mbeleni, ambacho waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli, na wakati huo si mwingine Zaidi ya ule wa Pentekoste. Kipindi ambacho Roho Mtakatifu atamwagwa juu ya kanisa kwa mara ya kwanza, baada ya BWANA YESU kuondoka!.

Huo ndio uliokuwa mwanzo wa watu kumwabudu Baba katika roho na kweli. (Matendo 2:1-15)

Lakini pia aliposema kuwa..“NA SASA IPO”…. maana yake hata huo wakati tayari Baba ameshaanza kuabudiwa katika roho na kweli. Na aliyekuwa anamwabudu baba katika ROHO NA KWELI ni yeye mwenyewe BWANA YESU KRISTO. Kwasababu tayari alikuwa na Roho Mtakatifu ndani yake, ambaye alipoondoka ndipo akammwaga juu ya kanisa.

Yohana 16:7 “Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu”.

Na hata sasa tupo kipindi ambacho Neema ya Roho Mtakatifu bado ipo duniani kwa kila anayemwitaji sawasawa na Matendo 2:38, Na kumbuka Roho Mtakatifu pekee ndiye funguo za mtu kumwabudu Mungu katika roho na kweli, na pasipo yeye haiwezekani kumwabudu Mungu katika roho.

Kwa somo refu lihusuyo jinsi ya kumwabudu Mungu katika roho na kweli fungua hapa >>Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “Saa yangu haijawadia?”

Ni muda gani Bwana Yesu alisulibiwa. Je! Ni saa 3 au saa 6?

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

UWEZO WA KIPEKEE.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya  Mithali 21:1 Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana;

SWALI: Nini maana ya  Mithali 21:1

“Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana; Kama mifereji ya maji huugeuza po pote apendapo”.


JIBU: Kuna mithali inayosema “maji hufuata mkondo”. Ikiwa na maana, palipo na mfereji kule kule unapoelekea ndipo maji nayo huelekea. Mfano ukielekeza mrefeji shambani mwako, basi maji yale yataelekea huko si kwingineko, ukielekezea mfereji nyumbani mwako, basi maji yatakuja ndani mwako. Kamwe maji  hayajiamulii  pa kuririkia.

Vivyo hivyo na Mungu, ndivyo anavyofananisha mamlaka yake juu ya wafalme na wakuu wa dunia hii. Kwamba mashauri yao, hawajiamulii tu peke yao kwa kujitakia. Kwamfano utakumbuka kuna wakati  Mungu alimnyanyua Moyo Koreshi mtawala wa Uajemi ili awape ruhusu wayahudi warudi katika nchi yao wakamjengee nyumba.

Ezra 1:1 Ikawa katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, ili kwamba neno la Bwana alilolisema kwa kinywa cha Yeremia lipate kutimizwa, Bwana akamwamsha roho yake Koreshi, mfalme wa Uajemi, hata akapiga mbiu katika ufalme wake wote, akaiandika pia, akisema,  2 Koreshi, mfalme wa Uajemi asema hivi;  3 Basi kila mtu katika ninyi nyote mlio watu wake, Bwana, Mungu wake, na awe pamoja naye, na akwee mpaka Yerusalemu, ulioko Yuda, akaijenge nyumba ya Bwana, Mungu wa Israeli, (yeye ndiye Mungu), iliyoko Yerusalemu.  4 Na mtu awaye yote aliyesalia mahali po pote akaapo hali ya ugeni, na asaidiwe na watu wa mahali pake, kwa fedha, na dhahabu, na mali, na wanyama, zaidi ya vitu vitolewavyo kwa hiari ya mtu, kwa ajili ya nyumba ya Mungu, iliyoko Yerusalemu

Mungu huyo  huyo ndiye aliyemfanya mfalme Nebukadreza kuwa na moyo mkatili ili awachukue watu wake utumwani kwasababu ya makosa yao.(Yeremia 27:6, 43:10)

Mungu anaweza kuwatumia watawala kuadhibu taifa, au kuwabariki watu wake. Hii ni kuonyesha kuwa hakuna tawala yoyote katika hii dunia inamilikiwa na fikra za mwanadamu asilimia 100, bali mengi ya mashauri ya wakuu hutoka juu mbinguni, au yameruhusiwa na Mungu. Wao ni kama maji tu yanayofuata mkondo wa kusudi la Mungu.

Ndio jambo ambalo Mungu alimwambia Mfalme Nebukadreza kwamba “aliye juu ndiye anayetawala”(Danieli 5:21) lakini yeye alidhani ni uongo, mpaka siku alipoondolewa kwenye ufalme wake kwa miaka 7, na kurudishwa baadaye.

Hivyo, jambo hili, sio tu la viongozi wa kidunia, lakini pia hata wa kanisani. Ikiwa kanisa ulilopo linasimamia kweli na utakatifu na Kristo Yesu ndio kiini cha fundisho lao, basi waheshimu sana viongozi wako, kwasababu si kila shauri linalotoka kwenye vinywa vyao, ni wao wamefikiria. Wao ni kama maji tu yaliyomwagwa kwenye mfereji, ili kukuongoza wewe. ukishandana nao, au ukipuuzia kuongozwa nao, wakati mwingine unapingana na maamuzi ya Mungu wako bila kujijua.

Waheshimu viongozi wako wanaokulea kiroho, kama vile unavyowaheshimu watawala ya kidunia.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Fahamu maana ya Mithali 29:4 “Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.

Ni kwa namna gani Kristo analitakasa kanisa kwa Maji katika Neno? (Waefeso 5:26)

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

ITAMBUE KARAMA YA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Mabibi wastahiki walikuwa ni watu gani? (Esta 1:18).

(Mada maalumu kwa wanawake)

Jibu: Mabibi Wastahiki ni “wanawake wa heshima”.. kundi hili la wanawake lilihusisha wake za Wafalme, Maliwali au Maakida au Majumbe..

Wakati mfalme Ahasuero alipowafanyia maakida wake na maliwali wake karamu, biblia inatuambia kuwa Malkia Vashti (mke wa mfalme), yeye naye aliwafanyia wanawake (ambao ni wake wa hao maakida na maliwali) karamu.

Esta 1:2 “siku zile mfalme Ahasuero alipoketi katika kiti cha enzi cha ufalme wake, huko Shushani ngomeni;

3 mwaka wa tatu wa kumiliki kwake, ikawa aliwafanyia karamu maakida wake wote na majumbe wake; wakuu wa Uajemi na Umedi, watu wenye cheo na maakida wa majimbo, wakihudhuria mbele zake. 

4 Akawaonyesha utajiri wa ufalme wake mtukufu, na heshima ya enzi yake bora siku nyingi, maana siku mia na themanini……………………..

9 Tena Vashti, malkia, naye akawafanyia karamu WANAWAKE NDANI YA NYUMBA YA KIFALME YA MFALME Ahasuero”.

Sasa hao wanawake waliokuwa wake za “maliwali na maakida” ndio waliojulikana kama “mabibi wastahiki”.. wakiongozwa na Malkia Vashti.

Lakini tunachoweza kujifunza ni kuwa ile karamu ya hawa wanawake haikuwa na utukufu wowote, kwani iliishia kuleta aibu kubwa katika ufalme wote wa Uajemi. Kwani Malkia Vashti alikosa utii kwa Mfalme alipoitwa, na zaidi sana alionyesha dharau hizo mbele ya Mfalme na maliwali wake wote.

Na huenda pia kiburi hicho kilichochewa na jopo la wale wanawake wengine wastahiki waliohudhuria karamu hiyo ya Malkia Vashti. Hiyo ikifunua kuwa hakuna cha maana walichokuwa wanakizungumza au kukipanga katika hiyo karamu Vashti aliyowaandalia, huenda yaliyokuwa yanazungumziwa kule ni UMBEA TU na kusema mapungufu ya waume zao!

Hiyo ikamfanya Vashti apoteze umalkia wake, na hata hao wanawake wengine ambao wastahiki kuzidi kutawaliwa na waume zao.

Esta 1:16 “Basi Memukani akajibu mbele ya mfalme na maakida, Huyu Vashti, malkia, hakumkosa mfalme tu peke yake, ila na maakida wote, na watu wote pia walioko katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero. 

17 Kwa maana tendo hilo la malkia litajulikana na wanawake wote, hata waume zao watadharauliwa machoni pao, itakaponenwa ya kuwa mfalme Ahasuero aliamuru Vashti, malkia, aletwe mbele yake, bali hakuja. 

18 Hata na leo hivi mabibi wastahiki wa Uajemi na Umedi waliokwisha kuzisikia habari za tendo lake malkia watawaambia vivi hivi maakida wote wa mfalme. Hivyo kutatokea dharau nyingi na ghadhabu tele.

 19 Basi mfalme akiona vema, na itoke kwake amri ya kifalme, nayo iandikwe katika sheria za Waajemi na Wamedi isitanguke, ya kwamba Vashti asifike tena mbele ya mfalme Ahasuero; na umalkia wake mfalme ampe mwingine aliye mwema kuliko yeye.

 20 Basi mbiu ya mfalme atakayoipiga itakapotangazwa katika ufalme wake wote, nao ni mkubwa, wake wote watawaheshimu waume zao, wakubwa kwa wadogo.

 21 Basi neno hili likawapendeza mfalme na maakida; naye mfalme akafanya sawasawa na neno lake Memukani.

 22 Kwa maana alipeleka nyaraka katika majimbo yote ya mfalme, kila jimbo kwa mwandiko wake, na kila taifa kwa lugha yake, ya kwamba kila mwanamume atawale nyumbani mwake, na kuitangaza habari hii kwa lugha ya watu wake”.

Tabia kama hii inaendelea mpaka leo kwa baadhi ya wanawake walioolewa!, ambao baada ya kuolewa wanawaona waume zao kama si kitu tena, na hata kupoteza UTII kwao!. Pasipo kujua kuwa kwa kufanya hivyo wanazidi kujipotezea nafasi zao ndani ya familia zao, kwani badala ya kuwa kichwa Mungu anawaweka kuwa wa mwisho.

Neno la Mungu linasema wanawake na wawatii waume zao.

1Petro 3:1 “Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;

2  wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu.

3  Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

4  bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.

5  Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, NA KUWATII WAUME ZAO”

Soma tena Waefeso 5:24 na Tito 2:5 utaona jambo hilo hilo, sasa mwana-mama unatolea wapi kiburi!!!. Badilika, na anza kuwa mtii, ikiwa haupo ndani yako, na hiyo ni kwa faida yako na familia yako. Kitabu cha Esta, huenda kingepaswa kiitwe kitabu cha Vashti, lakini kwa kiburi chake, umalkia wake akapewa Esta.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

ESTA: Mlango wa 5, 6 & 7

LITANIA YA BIKIRA MARIA JE! NI SALA YA KIMAANDIKO?

YESU ANAKWENDA KUIBADILISHA OFISI YAKE.

NI KIJIJI CHA AINA GANI UPO?

MAJESHI YA PEPO WABAYA.

Rudi nyumbani

Print this post

Kipuli ni nini, na kimebeba ujumbe gani?.(Mithali 25:12).

Jibu: Turejee,

Mithali 25:12 “KIPULI CHA DHAHABU, na pambo la dhahabu safi; Ndivyo alivyo mwonyaji mwenye hekima kwa sikio lisikialo”

“Kipuli” ni jina lingine la “hereni za masikioni”.

Neno hili limeonekana mara moja tu katika biblia, katika kitabu cha Mithali 25:12.

Na mwandishi wa Mithali (Sulemani) kwa hekima ya roho alipata kuelewa vipuli (hereni) sahihi wanazopaswa wavae watu, tofauti na hizi tuzijuazo.

Anasema… “KIPULI CHA DHAHABU, na pambo la dhahabu safi; Ndivyo alivyo MWONYAJI MWENYE HEKIMA KWA SIKIO LISIKIALO”.

Maana yake ni kuwa sikio linalosikia hekima kutoka kwa wenye hekima, linafananishwa na sikio lililovishwa hereni ya dhahabu au pambo la dhahabu.

Kwa lugha nyingine ni kwamba, kama tukitaka kupamba masikio yetu kwa vitu vya thamani, basi tuwe wasikilizaji wa maneno ya hekima. (Kwani maneno hayo yataonekana kama mapambo ya thamani katika masikio yetu).

Na maneno ya hekima hatuyapati pengine isipokuwa katika biblia takatifu (Humo ndimo tutakapopata lulu na mapambo ya thamani ya masikio yetu)..

Mithali 2:1 “Mwanangu, kama ukiyakubali maneno yangu, Na kuyaweka akiba maagizo yangu;

2 HATA UKATEGA SIKIO LAKO KUSIKIA HEKIMA, UKAUELEKEZA MOYO WAKO UPATE KUFAHAMU;

3 Naam, ukiita busara, Na kupaza sauti yako upate ufahamu;

4 Ukiutafuta kama fedha, Na kuutafutia kama hazina iliyositirika;

5 Ndipo utakapofahamu kumcha Bwana, Na kupata kumjua Mungu”

Soma tena  Mithali 4:20, Mithali 5:1, na  Mithali 22:17 utaona maneno yanayopatana na hayo..

Mithali hizi zinalingana kabisa na ujumbe wa Roho Mtakatifu tunaousoma katika kitabu cha 1Petro 3:3. Na 1 Timotheo 2:9.

1 Petro 3:3 “Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

4 BALI KUWE UTU WA MOYONI USIOONEKANA, KATIKA MAPAMBO YASIYOHARIBIKA; YAANI, ROHO YA UPOLE NA UTULIVU, ILIYO YA THAMANI KUU MBELE ZA MUNGU.

5 Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.

6 Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote”.

Mstari wa 4 unasema… “ BALI KUWE UTU WA MOYONI USIOONEKANA, KATIKA MAPAMBO YASIYOHARIBIKA; YAANI, ROHO YA UPOLE NA UTULIVU, ILIYO YA THAMANI KUU MBELE ZA MUNGU”.

Je ni vipuli gani vipo masikioni mwako?…vya chuma au vya maneno ya hekima?.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Rudi nyumbani

Print this post

Mashonde ni nini? (Ezekieli 4:15).

Swali: Mashonde ni kitu gani kama tunavyosoma katika Ezekieli 4:15, na yamebeba ufunuo gani?

Jibu: Turejee..

Ezekieli 4:12“Nawe utakila kama mkate wa shayiri, nawe utakioka mbele ya macho yao juu ya MASHONDE YATOKAYO KATIKA MWANADAMU”.

“Mashonde” ni jina lingine la “kinyesi kikavu” aidha cha mwanadamu au mnyama.

Zamani na hata sasa katika maeneo baadhi, kinyesi kikavu kimetumika kama chanzo cha nishati, kwasababu kinawaka kwa haraka zaidi hata ya kuni, Hivyo kinaweza kutumika kama mbadala wa kuni kama kikiwa kwa wingi.

Katika maeneo ya mashariki ya kati, vinyesi vikavu vya ngamia na ng’ombe vilitumika kwa sana kama chanzo cha nishati, na nyakati chache chache sana (hususani vipindi vya ukame na dhiki), na vilitumika hata vya wanadamu lakini vyote vilikuwa ni vikavu….lakini sasa vinatumika hata vibichi kutokana na kukuwa kwa teknolojia.

Sasa tukirejea katika biblia, tunasoma Nabii Ezekieli akipewa maagizo na Mungu kuwa aoke mkate aina ya shayiri juu ya Mashonde (yaani kinyesi) cha mwanadamu, maana yake atumie kinyesi cha mwanadamu kama chanzo cha nishati, badala ya cha Wanyama. Sasa changamoto ya kutumia vinyesi, aidha vya mwanadamu au mnyama kama nishati ni “harufu”.

Maana yake kile kitakachopikwa juu ya mashonde (kinyesi) fulani kitabeba harufu ya kile kinyesi husika, kwahiyo kama mkate utaokwa juu ya kinyesi cha ngamia, basi ule mkate kwa sehemu utatoa harufu ya kinyesi cha ngamia, vile vile kama umeokwa juu ya kinyesi cha mwanadamu basi utatoa harufu ya kinyesi cha mwanadamu.

Hivyo Mungu alimwambia Ezekieli atumie kinyesi cha Mtu, kutengeneza huo mkate na kisha aule!.. Lengo la kumwambia vile si kumwadhibu Ezekieli, la! Kwani Ezekieli alikuwa ni nabii wa Mungu mwaminifu sana, hivyo aliambiwa afanye vile ili awe ishara kwa Taifa la Israeli kama Hosea alivyokuwa ishara kwa Taifa la Israeli alipoambia akaoe mwanamke wa uzinzi.

Maana yake kwa Ezekieli kula mkate uliookwa juu ya kinyesi cha mtu, ni ujumbe kwa wana wa Israeli kuwa na wao watakwenda utumwani mahali pa dhiki nyingi, na watapitia shida na njaa kali hata kufikia hatua ya kukosa chanzo bora cha nishati na hivyo kuona hata kinyesi chao wenyewe chaweza kufaa kwa nishati ya kuokea mikate ili tu waweze kuzishibisha nafsi zao wasife kwa njaa.

Hivyo Bwana Mungu alimchagulia Ezekieli hiyo ishara, lakini tunasoma Ezekieli alimsihi Bwana ambadilishie hiyo ishara kwani hakuwahi kula kitu najisi tangu amezaliwa, (kwasababu kulingana na desturi za kiyahudi kitu chochote kilichookwa juu ya kinyesi ni najisi), Hivyo akamsikia kwa ombi hilo, na Bwana Mungu akambadilishia, badala ya kutumia kinyesi cha mtu, basi atumie cha Ng’ombe, na ndivyo Ezekieli alivyofanya kama tunavyosoma…

Ezekieli 4:13 “Bwana akasema, Hivyo ndivyo wana wa Israeli watakavyokula chakula chao, hali kimetiwa unajisi, kati ya mataifa nitakakowafukuza

14 Ndipo nikasema, Ee Bwana MUNGU, tazama, roho yangu haikutiwa unajisi; maana tangu ujana wangu hata sasa sijala nyamafu, wala iliyoraruliwa na hayawani; wala nyama ichukizayo haikuingia kinywani mwangu.

15 Ndipo akaniambia, Tazama, NIMEKUPA MASHONDE YA NG’OMBE badala ya mashonde ya mwanadamu, nawe utakipika chakula chako juu ya hayo.

16 Tena akaniambia, Mwanadamu, tazama, nitalivunja tegemeo la chakula katika Yerusalemu; nao watakula mkate kwa kuupima, na kwa kuutunza sana; nao watakunywa maji kwa kuyapima, na kwa kushangaa;

17 wapate kupungukiwa na mkate na maji, na kustaajabiana, na kukonda kwa sababu ya uovu wao”.

Ni nini tunajifunza katika Habari hiyo?

Kikubwa tunachoweza kujifunza ni kuwa “tunapomwacha Mungu na kufuata mambo yetu, tunajiweka katika hatari ya kuharibu Maisha yetu kuanzia ya rohoni mpaka ya mwilini”.  Wana wa Israeli hapa walimwacha Mungu na matokeo yake Maisha yao yaliharibika kwa njaa na umasikini na utumwa mpaka kufikia hatua ya kula mikate iliyookwa juu ya vinyesi vyao wenyewe, na ni hivyo hivyo hata leo, (kwasababu Mungu ni yule yule hajabadilika)… kama tukigeuka na kufuata mambo yetu, basi Maisha yetu yataharibika hata zaidi ya hayo ya wana wa Israeli nyakati hizo.

Je umempokea YESU KRISTO, kama Bwana na Mwokozi wa Maisha yako?

Bwana atusaidie.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

EZEKIELI, ITABIRIE MIFUPA MIKAVU.

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

Roho Mtakatifu ni nani?.

Kuna tofauti gani kati ya  “Edeni” na “Adeni”?

Bawa la mbuni hufurahi; Lakini mabawa yake na manyoya yake, je! Yana huruma? 

Rudi nyumbani

Print this post

Bwana alimaanisha nini kusema “atazamaye mwanamke kwa kumtamani” amezini naye?

Je! Kutamani kwa namna yoyote hakufai?

Mathayo 5:27  Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini; 28  lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.

JIBU: Ukitafakari hapo utaona mazingira Bwana anayoyazungumzia hapo ni ya uzinzi. Uzinzi ni kitendo cha kutoka nje ya mpango wa ki-ndoa katika eneo la kukutanika kimwili. ambao chanzo chake ni tamaa.

Sasa Bwana anaweka wazi kuwa uzinzi huanzia ndani kwenye mawazo ya mtu, moyoni mwake, tofauti na vile inavyodhaniwa kuwa mpaka wakutane dhahiri.

Lakini swali linaloulizwa je! Hatupaswi kutamani kabisa? Na kama tukitamani tutakuwa tunafanya kosa.

Kila kitu Mungu amekiweka katika utaratibu wake. Ni sawa na kusema kwanini ulafi ni dhambi, wakati Mungu ametuwekea ndani yetu hamu ya kula. Au kwanini nisile udongo wakati, najisikia hamu ya kuula mimi kama mjamzito, Au kwanini nisinywe pombe wakati ninajiona kabisa nina kiu nayo?. Kama Mungu angekuwa hapendi kwanini ameniwekea kiu hiyo?

Lakini unajua kabisa ukizidisha kula kuna madhara mwilini, pia ukila/ukinywa kitu kisichopasa utajisababishia madhara mwenyewe.

Vivyo hivyo katika tamaa. Haijawekwa, iwe ni “kutamani-tamani”, kila kitu kinachokatiza mbele. Bali Mungu aliiumba hiyo mahususi kwa wanandoa. Hivyo ikiwa upo humo huna budi kuzielekeza kwa mkeo/mumeo tu, na kama bado hujaingia humo, unapaswa uweze kuzitawala. Na hiyo inawezekana kabisa, usipozitengenezea mazingira, haziwezi kuamka na kukusumbua. Kwasababu maandiko yanasema moto hufa kwa kukosa kuni.

Ufanyeje.

Ni kujiepusha na mazingira yote, yatakayoweza kukupelekea kulipuka tamaa. Kwamfano, mazungumzo-zungumzo yasiyokuwa na maana na mtu wa jinsia nyingine, (kuchati), na kutazama video au picha zenye maudhui ya kizinzi, kuzungumza-zungumza habari hizo na marafiki zako, kuwa katika mazingira yasiyo ya kujishughulisha, kwamfano upo tu huna kazi yoyote umekaa, ni rahisi kupelekwa kwenye mawazo hayo na adui. Lakini pia kuwa msomaji wa Neno na mwombaji. Vitakusaidia sana kuwa mtu asiyetawaliwa na tamaa.

Na hivyo hata adui akitaka kukupeleka kwenye hali ya kutamani, kujengea picha, kutafakari,  basi unaweza kuyakataa hayo mawazo haraka, na ukaendelea kuwa salama, bila ya kuzini moyoni mwako. Kwasababu umevidhibiti.

Pia kumbuka jambo hili, si la wanaume tu, bali kwa jinsia zote. Hatupaswi kuishi maisha ya tamaa.

Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO

Nini Tofauti kati ya uzinzi na uasherati ?

WAANDAA MEZA MBELE YANGU, MACHONI PA WATESI WANGU

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Yesu alipopaa juu aliteka mateka, Kauli hiyo ina maana gani?

SWALI: Ni mateka yapi hayo aliyoyateka..na ni vipawa gani alivyowapa wanadamu.?

Waefeso 4:8 Hivyo husema, Alipopaa juu aliteka mateka, Akawapa wanadamu vipawa. 


JIBU: Ufalme wa Mbinguni umefananishwa na ngome Fulani, yenye hazina kubwa sana ambayo hupiganiwa na watu wengi kumilikiwa.

Na Ndio maana Bwana Yesu aliyasema maneno haya; 

Mathayo 11:12 Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka. 

Umeona unafananishwa na kitu cha kutekwa, sio kitu cha kuombwa, au kubembelezwa Fulani. Inahitaji kupambania.

Hivyo Kwa  maneno hayo utaelewa kuwa hata Bwana wetu Yesu Kristo, alikuwa katika operesheni hiyo ya kuuteka huo ufalme.

Na hiyo ilikuja kutimia siku ile aliposhinda pale Kalvari Kwa kifo chake na kufufuka katika wafu aliweza kumiliki vyote vya mbinguni na vya duniani…vyote viliwekwa chini yake.

Waefeso 1:20-23 aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho;  [21]juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia;  [22]akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo  [23]ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote. 

Sasa kwasababu ameteka Kila kitu cha mbinguni, aliteka pia na ‘uweza wote wa kiungu’ na kutupa sisi wanadamu, ndio vipawa au karama za Roho Mtakatifu, alizozitoa Kwa lengo la kuujenga mwili wa Kristo, kuhubiri injili, na kuhudumu.

Ndio hapo akawafanya wengine kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine wainjilisti, wengine, wachungaji na wengine waalimu.(Waefeso 4:11)

Pamoja na karama zile 9, tunazozisoma katika 1Wakorintho 12.

1 Wakorintho 12:8 Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo Roho yeye yule; [9]mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama za kuponya katika Roho yule mmoja;  [10]na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii; na mwingine kupambanua roho; mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha;  [11]lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye. 

Mambo ambayo hayakuwahi kuonekana zamani, hata za manabii..lakini Sasa twaziona zikidhihirika katika kanisa la Kristo.

Hivyo kumbuka Yesu hajateka mateka tu mbinguni. ni mpaka duniani. Maana yake ni kuwa sisi tuliomwamini hatuna budi pia kuwa watekaji. Hivyo popote pale uendapo kuhubiri injili, usiogope Wala usiwe mnyonge, vamia, hubiri Kwa ujasiri na hakika watu watabadilika kwasababu nguvu hizo tumepewa katika Kristo Yesu

2 Wakorintho 10:4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)  tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo; 

Bwana akubariki

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Wakaldayo ni watu gani?

TUNA JUKUMU LA KWENDA KUTEKA MATEKA.

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

TABIA ZA NJIA YA MUNGU KWA MKRISTO

MBINGUNI YUPO NANI SASA?

Rudi nyumbani

Print this post

Makonde ni nini? (Marko 14:65)

Swali: Yale Makonde Bwana Yesu aliyopigwa yalikuwaje?.

Jibu: Turejee..

Marko 14:65 “Wengine wakaanza kumtemea mate, wakamfunika uso, na KUMPIGA MAKONDE, na kumwambia, tabiri. Hata watumishi nao wakampiga makofi”.

“Makonde” ni kiswahili kingine cha “Ngumi”. Je umewahi kuwaza kuwa Bwana wetu YESU aliwahi kupigwa ngumi?.

Ndio!..Alipigwa mijeledi (Yohana 19:1) na alitemewa mate (Marko 15:19) lakini pia alipigwa ngumi nyingi na wale askari kwaajili ya makosa yetu sisi..

Mapigo Bwana Yesu aliyoyapata kabla na baada ya kupandishwa msalabani yalimbasilisha kabisa mwonekano wa uso wake na mwili wake wote kwa ujumla, na kumfanya kuwa mtu aiyeharibika uso na mwili kuliko watu wote waliowahi kutokea duniani.

Isaya 52:13 “Tazama, mtumishi wangu atatenda kwa busara, atatukuzwa, na kuinuliwa juu, naye atakuwa juu sana.

14 Kama vile wengi walivyokustaajabia, (USO WAKE ULIKUWA UMEHARIBIWA SANA ZAIDI YA MTU YE YOTE, NA UMBO LAKE ZAIDI YA WANADAMU)”.

Umeona?..Mapigo aliyoyapata Bwana Yesu ni zaidi ya yanayoigizwa katika Filamu.. ya kwenye filamu yamepunguzwa makali sana, na pia ni agenda ya shetani kuurahisisha msalaba na kuwaaminisha wanadamu kuwa jambo lililomtokea Bwana lilikuwa la kawaida tu na si zito sana.

Shetani hataki tujue kuwa tumeokolewa kwa thamani na gharama kubwa sawasawa na 1Wakorintho 6:20, Lengo lake ni ili tusijikane nafsi wala tusiuthamini msalaba.

Lakini kama tukijua kwa uhalisia gharama Bwana Yesu alizoingia pale msalabani kwaajili ya dhambi zetu, tutalia kwa machozi na hatutabaki kama tulivyo zoea kufanya mchezo na dhambi.
Madhara ya kudharau kazi ya msalaba ni makubwa kuliko kitu kingine chochote.

Waebrania 10:29 “Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?”

Ikiwa bado hujaokoka, ni vyema ukafanya hivyo leo!.. Na si kwasababu tu ya kuepuka hukumu, bali kasababu ya kupata uzima wa milele.

Utajisikiaje ukiukosa uzima wa milele, hata kama tu ziwa la moto lisingekuwepo???..huoni ni hasara kubwa kufutwa kabisa kwenye kumbukumbu zakichwa cha Mungu milele??.
Ni heri ukampokea Kristo leo!.

Ikiwa utahitaji kufanya hivyo basi waweza kuwasliana nasi inbox tutakusaidia.

Bwana akubariki

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Ni kweli hakuna mtu aliyewahi kuuona uso wa Mungu Zaidi ya Bwana Yesu?

Kuna tofauti gani kati ya uso wa Bwana na macho ya Bwana?

Biblia inaposema Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, Inamaana gani?

MBINGUNI YUPO NANI SASA?

Je! dhambi zote ni sawa Kuna dhambi kubwa na ndogo?

Rudi nyumbani

Print this post