Jibu: Turejee,
Mithali 25:12 “KIPULI CHA DHAHABU, na pambo la dhahabu safi; Ndivyo alivyo mwonyaji mwenye hekima kwa sikio lisikialo”
“Kipuli” ni jina lingine la “hereni za masikioni”.
Neno hili limeonekana mara moja tu katika biblia, katika kitabu cha Mithali 25:12.
Na mwandishi wa Mithali (Sulemani) kwa hekima ya roho alipata kuelewa vipuli (hereni) sahihi wanazopaswa wavae watu, tofauti na hizi tuzijuazo.
Anasema… “KIPULI CHA DHAHABU, na pambo la dhahabu safi; Ndivyo alivyo MWONYAJI MWENYE HEKIMA KWA SIKIO LISIKIALO”.
Maana yake ni kuwa sikio linalosikia hekima kutoka kwa wenye hekima, linafananishwa na sikio lililovishwa hereni ya dhahabu au pambo la dhahabu.
Kwa lugha nyingine ni kwamba, kama tukitaka kupamba masikio yetu kwa vitu vya thamani, basi tuwe wasikilizaji wa maneno ya hekima. (Kwani maneno hayo yataonekana kama mapambo ya thamani katika masikio yetu).
Na maneno ya hekima hatuyapati pengine isipokuwa katika biblia takatifu (Humo ndimo tutakapopata lulu na mapambo ya thamani ya masikio yetu)..
Mithali 2:1 “Mwanangu, kama ukiyakubali maneno yangu, Na kuyaweka akiba maagizo yangu;
2 HATA UKATEGA SIKIO LAKO KUSIKIA HEKIMA, UKAUELEKEZA MOYO WAKO UPATE KUFAHAMU;
3 Naam, ukiita busara, Na kupaza sauti yako upate ufahamu;
4 Ukiutafuta kama fedha, Na kuutafutia kama hazina iliyositirika;
5 Ndipo utakapofahamu kumcha Bwana, Na kupata kumjua Mungu”
Soma tena Mithali 4:20, Mithali 5:1, na Mithali 22:17 utaona maneno yanayopatana na hayo..
Mithali hizi zinalingana kabisa na ujumbe wa Roho Mtakatifu tunaousoma katika kitabu cha 1Petro 3:3. Na 1 Timotheo 2:9.
1 Petro 3:3 “Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;
4 BALI KUWE UTU WA MOYONI USIOONEKANA, KATIKA MAPAMBO YASIYOHARIBIKA; YAANI, ROHO YA UPOLE NA UTULIVU, ILIYO YA THAMANI KUU MBELE ZA MUNGU.
5 Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.
6 Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote”.
Mstari wa 4 unasema… “ BALI KUWE UTU WA MOYONI USIOONEKANA, KATIKA MAPAMBO YASIYOHARIBIKA; YAANI, ROHO YA UPOLE NA UTULIVU, ILIYO YA THAMANI KUU MBELE ZA MUNGU”.
Je ni vipuli gani vipo masikioni mwako?…vya chuma au vya maneno ya hekima?.
Bwana atusaidie.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Rudi nyumbani
Swali: Mashonde ni kitu gani kama tunavyosoma katika Ezekieli 4:15, na yamebeba ufunuo gani?
Jibu: Turejee..
Ezekieli 4:12“Nawe utakila kama mkate wa shayiri, nawe utakioka mbele ya macho yao juu ya MASHONDE YATOKAYO KATIKA MWANADAMU”.
“Mashonde” ni jina lingine la “kinyesi kikavu” aidha cha mwanadamu au mnyama.
Zamani na hata sasa katika maeneo baadhi, kinyesi kikavu kimetumika kama chanzo cha nishati, kwasababu kinawaka kwa haraka zaidi hata ya kuni, Hivyo kinaweza kutumika kama mbadala wa kuni kama kikiwa kwa wingi.
Katika maeneo ya mashariki ya kati, vinyesi vikavu vya ngamia na ng’ombe vilitumika kwa sana kama chanzo cha nishati, na nyakati chache chache sana (hususani vipindi vya ukame na dhiki), na vilitumika hata vya wanadamu lakini vyote vilikuwa ni vikavu….lakini sasa vinatumika hata vibichi kutokana na kukuwa kwa teknolojia.
Sasa tukirejea katika biblia, tunasoma Nabii Ezekieli akipewa maagizo na Mungu kuwa aoke mkate aina ya shayiri juu ya Mashonde (yaani kinyesi) cha mwanadamu, maana yake atumie kinyesi cha mwanadamu kama chanzo cha nishati, badala ya cha Wanyama. Sasa changamoto ya kutumia vinyesi, aidha vya mwanadamu au mnyama kama nishati ni “harufu”.
Maana yake kile kitakachopikwa juu ya mashonde (kinyesi) fulani kitabeba harufu ya kile kinyesi husika, kwahiyo kama mkate utaokwa juu ya kinyesi cha ngamia, basi ule mkate kwa sehemu utatoa harufu ya kinyesi cha ngamia, vile vile kama umeokwa juu ya kinyesi cha mwanadamu basi utatoa harufu ya kinyesi cha mwanadamu.
Hivyo Mungu alimwambia Ezekieli atumie kinyesi cha Mtu, kutengeneza huo mkate na kisha aule!.. Lengo la kumwambia vile si kumwadhibu Ezekieli, la! Kwani Ezekieli alikuwa ni nabii wa Mungu mwaminifu sana, hivyo aliambiwa afanye vile ili awe ishara kwa Taifa la Israeli kama Hosea alivyokuwa ishara kwa Taifa la Israeli alipoambia akaoe mwanamke wa uzinzi.
Maana yake kwa Ezekieli kula mkate uliookwa juu ya kinyesi cha mtu, ni ujumbe kwa wana wa Israeli kuwa na wao watakwenda utumwani mahali pa dhiki nyingi, na watapitia shida na njaa kali hata kufikia hatua ya kukosa chanzo bora cha nishati na hivyo kuona hata kinyesi chao wenyewe chaweza kufaa kwa nishati ya kuokea mikate ili tu waweze kuzishibisha nafsi zao wasife kwa njaa.
Hivyo Bwana Mungu alimchagulia Ezekieli hiyo ishara, lakini tunasoma Ezekieli alimsihi Bwana ambadilishie hiyo ishara kwani hakuwahi kula kitu najisi tangu amezaliwa, (kwasababu kulingana na desturi za kiyahudi kitu chochote kilichookwa juu ya kinyesi ni najisi), Hivyo akamsikia kwa ombi hilo, na Bwana Mungu akambadilishia, badala ya kutumia kinyesi cha mtu, basi atumie cha Ng’ombe, na ndivyo Ezekieli alivyofanya kama tunavyosoma…
Ezekieli 4:13 “Bwana akasema, Hivyo ndivyo wana wa Israeli watakavyokula chakula chao, hali kimetiwa unajisi, kati ya mataifa nitakakowafukuza
14 Ndipo nikasema, Ee Bwana MUNGU, tazama, roho yangu haikutiwa unajisi; maana tangu ujana wangu hata sasa sijala nyamafu, wala iliyoraruliwa na hayawani; wala nyama ichukizayo haikuingia kinywani mwangu.
15 Ndipo akaniambia, Tazama, NIMEKUPA MASHONDE YA NG’OMBE badala ya mashonde ya mwanadamu, nawe utakipika chakula chako juu ya hayo.
16 Tena akaniambia, Mwanadamu, tazama, nitalivunja tegemeo la chakula katika Yerusalemu; nao watakula mkate kwa kuupima, na kwa kuutunza sana; nao watakunywa maji kwa kuyapima, na kwa kushangaa;
17 wapate kupungukiwa na mkate na maji, na kustaajabiana, na kukonda kwa sababu ya uovu wao”.
Ni nini tunajifunza katika Habari hiyo?
Kikubwa tunachoweza kujifunza ni kuwa “tunapomwacha Mungu na kufuata mambo yetu, tunajiweka katika hatari ya kuharibu Maisha yetu kuanzia ya rohoni mpaka ya mwilini”. Wana wa Israeli hapa walimwacha Mungu na matokeo yake Maisha yao yaliharibika kwa njaa na umasikini na utumwa mpaka kufikia hatua ya kula mikate iliyookwa juu ya vinyesi vyao wenyewe, na ni hivyo hivyo hata leo, (kwasababu Mungu ni yule yule hajabadilika)… kama tukigeuka na kufuata mambo yetu, basi Maisha yetu yataharibika hata zaidi ya hayo ya wana wa Israeli nyakati hizo.
Je umempokea YESU KRISTO, kama Bwana na Mwokozi wa Maisha yako?
Bwana atusaidie.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
EZEKIELI, ITABIRIE MIFUPA MIKAVU.
HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.
Kuna tofauti gani kati ya “Edeni” na “Adeni”?
Bawa la mbuni hufurahi; Lakini mabawa yake na manyoya yake, je! Yana huruma?
Je! Kutamani kwa namna yoyote hakufai?
Mathayo 5:27 Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini; 28 lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.
JIBU: Ukitafakari hapo utaona mazingira Bwana anayoyazungumzia hapo ni ya uzinzi. Uzinzi ni kitendo cha kutoka nje ya mpango wa ki-ndoa katika eneo la kukutanika kimwili. ambao chanzo chake ni tamaa.
Sasa Bwana anaweka wazi kuwa uzinzi huanzia ndani kwenye mawazo ya mtu, moyoni mwake, tofauti na vile inavyodhaniwa kuwa mpaka wakutane dhahiri.
Lakini swali linaloulizwa je! Hatupaswi kutamani kabisa? Na kama tukitamani tutakuwa tunafanya kosa.
Kila kitu Mungu amekiweka katika utaratibu wake. Ni sawa na kusema kwanini ulafi ni dhambi, wakati Mungu ametuwekea ndani yetu hamu ya kula. Au kwanini nisile udongo wakati, najisikia hamu ya kuula mimi kama mjamzito, Au kwanini nisinywe pombe wakati ninajiona kabisa nina kiu nayo?. Kama Mungu angekuwa hapendi kwanini ameniwekea kiu hiyo?
Lakini unajua kabisa ukizidisha kula kuna madhara mwilini, pia ukila/ukinywa kitu kisichopasa utajisababishia madhara mwenyewe.
Vivyo hivyo katika tamaa. Haijawekwa, iwe ni “kutamani-tamani”, kila kitu kinachokatiza mbele. Bali Mungu aliiumba hiyo mahususi kwa wanandoa. Hivyo ikiwa upo humo huna budi kuzielekeza kwa mkeo/mumeo tu, na kama bado hujaingia humo, unapaswa uweze kuzitawala. Na hiyo inawezekana kabisa, usipozitengenezea mazingira, haziwezi kuamka na kukusumbua. Kwasababu maandiko yanasema moto hufa kwa kukosa kuni.
Ufanyeje.
Ni kujiepusha na mazingira yote, yatakayoweza kukupelekea kulipuka tamaa. Kwamfano, mazungumzo-zungumzo yasiyokuwa na maana na mtu wa jinsia nyingine, (kuchati), na kutazama video au picha zenye maudhui ya kizinzi, kuzungumza-zungumza habari hizo na marafiki zako, kuwa katika mazingira yasiyo ya kujishughulisha, kwamfano upo tu huna kazi yoyote umekaa, ni rahisi kupelekwa kwenye mawazo hayo na adui. Lakini pia kuwa msomaji wa Neno na mwombaji. Vitakusaidia sana kuwa mtu asiyetawaliwa na tamaa.
Na hivyo hata adui akitaka kukupeleka kwenye hali ya kutamani, kujengea picha, kutafakari, basi unaweza kuyakataa hayo mawazo haraka, na ukaendelea kuwa salama, bila ya kuzini moyoni mwako. Kwasababu umevidhibiti.
Pia kumbuka jambo hili, si la wanaume tu, bali kwa jinsia zote. Hatupaswi kuishi maisha ya tamaa.
Bwana akubariki.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO
Nini Tofauti kati ya uzinzi na uasherati ?
WAANDAA MEZA MBELE YANGU, MACHONI PA WATESI WANGU
Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?
SWALI: Ni mateka yapi hayo aliyoyateka..na ni vipawa gani alivyowapa wanadamu.?
Waefeso 4:8 Hivyo husema, Alipopaa juu aliteka mateka, Akawapa wanadamu vipawa.
JIBU: Ufalme wa Mbinguni umefananishwa na ngome Fulani, yenye hazina kubwa sana ambayo hupiganiwa na watu wengi kumilikiwa.
Na Ndio maana Bwana Yesu aliyasema maneno haya;
Mathayo 11:12 Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.
Umeona unafananishwa na kitu cha kutekwa, sio kitu cha kuombwa, au kubembelezwa Fulani. Inahitaji kupambania.
Hivyo Kwa maneno hayo utaelewa kuwa hata Bwana wetu Yesu Kristo, alikuwa katika operesheni hiyo ya kuuteka huo ufalme.
Na hiyo ilikuja kutimia siku ile aliposhinda pale Kalvari Kwa kifo chake na kufufuka katika wafu aliweza kumiliki vyote vya mbinguni na vya duniani…vyote viliwekwa chini yake.
Waefeso 1:20-23 aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; [21]juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; [22]akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo [23]ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.
Sasa kwasababu ameteka Kila kitu cha mbinguni, aliteka pia na ‘uweza wote wa kiungu’ na kutupa sisi wanadamu, ndio vipawa au karama za Roho Mtakatifu, alizozitoa Kwa lengo la kuujenga mwili wa Kristo, kuhubiri injili, na kuhudumu.
Ndio hapo akawafanya wengine kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine wainjilisti, wengine, wachungaji na wengine waalimu.(Waefeso 4:11)
Pamoja na karama zile 9, tunazozisoma katika 1Wakorintho 12.
1 Wakorintho 12:8 Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo Roho yeye yule; [9]mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama za kuponya katika Roho yule mmoja; [10]na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii; na mwingine kupambanua roho; mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha; [11]lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye.
Mambo ambayo hayakuwahi kuonekana zamani, hata za manabii..lakini Sasa twaziona zikidhihirika katika kanisa la Kristo.
Hivyo kumbuka Yesu hajateka mateka tu mbinguni. ni mpaka duniani. Maana yake ni kuwa sisi tuliomwamini hatuna budi pia kuwa watekaji. Hivyo popote pale uendapo kuhubiri injili, usiogope Wala usiwe mnyonge, vamia, hubiri Kwa ujasiri na hakika watu watabadilika kwasababu nguvu hizo tumepewa katika Kristo Yesu
2 Wakorintho 10:4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;
Bwana akubariki
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
TUNA JUKUMU LA KWENDA KUTEKA MATEKA.
MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.
Swali: Yale Makonde Bwana Yesu aliyopigwa yalikuwaje?.
Jibu: Turejee..
Marko 14:65 “Wengine wakaanza kumtemea mate, wakamfunika uso, na KUMPIGA MAKONDE, na kumwambia, tabiri. Hata watumishi nao wakampiga makofi”.
“Makonde” ni kiswahili kingine cha “Ngumi”. Je umewahi kuwaza kuwa Bwana wetu YESU aliwahi kupigwa ngumi?.
Ndio!..Alipigwa mijeledi (Yohana 19:1) na alitemewa mate (Marko 15:19) lakini pia alipigwa ngumi nyingi na wale askari kwaajili ya makosa yetu sisi..
Mapigo Bwana Yesu aliyoyapata kabla na baada ya kupandishwa msalabani yalimbasilisha kabisa mwonekano wa uso wake na mwili wake wote kwa ujumla, na kumfanya kuwa mtu aiyeharibika uso na mwili kuliko watu wote waliowahi kutokea duniani.
Isaya 52:13 “Tazama, mtumishi wangu atatenda kwa busara, atatukuzwa, na kuinuliwa juu, naye atakuwa juu sana.
14 Kama vile wengi walivyokustaajabia, (USO WAKE ULIKUWA UMEHARIBIWA SANA ZAIDI YA MTU YE YOTE, NA UMBO LAKE ZAIDI YA WANADAMU)”.
Umeona?..Mapigo aliyoyapata Bwana Yesu ni zaidi ya yanayoigizwa katika Filamu.. ya kwenye filamu yamepunguzwa makali sana, na pia ni agenda ya shetani kuurahisisha msalaba na kuwaaminisha wanadamu kuwa jambo lililomtokea Bwana lilikuwa la kawaida tu na si zito sana.
Shetani hataki tujue kuwa tumeokolewa kwa thamani na gharama kubwa sawasawa na 1Wakorintho 6:20, Lengo lake ni ili tusijikane nafsi wala tusiuthamini msalaba.
Lakini kama tukijua kwa uhalisia gharama Bwana Yesu alizoingia pale msalabani kwaajili ya dhambi zetu, tutalia kwa machozi na hatutabaki kama tulivyo zoea kufanya mchezo na dhambi.
Madhara ya kudharau kazi ya msalaba ni makubwa kuliko kitu kingine chochote.
Waebrania 10:29 “Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?”
Ikiwa bado hujaokoka, ni vyema ukafanya hivyo leo!.. Na si kwasababu tu ya kuepuka hukumu, bali kasababu ya kupata uzima wa milele.
Utajisikiaje ukiukosa uzima wa milele, hata kama tu ziwa la moto lisingekuwepo???..huoni ni hasara kubwa kufutwa kabisa kwenye kumbukumbu zakichwa cha Mungu milele??.
Ni heri ukampokea Kristo leo!.
Ikiwa utahitaji kufanya hivyo basi waweza kuwasliana nasi inbox tutakusaidia.
Bwana akubariki
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Ni kweli hakuna mtu aliyewahi kuuona uso wa Mungu Zaidi ya Bwana Yesu?
Kuna tofauti gani kati ya uso wa Bwana na macho ya Bwana?
Biblia inaposema Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, Inamaana gani?
Makwazo ni mambo yanayozuia mwendelezo wa jambo Fulani lililokuwa limekwisha anza, au linalotaka kuanza. Kwamfano ulikuwa unasafiri lakini ghafla kwenye safari yako unakutana na mto mpana, unaokufanya ushindwe kuvuka, hicho kinaitwa kikwazo. Au ulikuwa unapika chakula chako, halafu ghafla gesi ikaishia katikati na chakula bado hakijaiva, hicho kinatiwa kikwazo.
Na rohoni pia vivyo hivyo yapo makwazo ambayo yanamzuia mtu asimalize mwendo wake wa imani, au asiendelee mbele tena katika kumtafuta Mungu. Na muhimu sana kuyajua na kujiepusha nayo.
Kibiblia makwazo yamegawanyika katika sehemu kuu tatu.
Tukianzana na hilo kundi la kwanza, wapendwa tunaowazungumzia hapa ni wale ambao hawajasimama vema katika kweli. Ndio hawa ambayo Bwana Yesu anawazungumzia katika vifungu hivi;
Luka 17:1 Akawaambia wanafunzi wake, Makwazo hayana budi kuja, lakini ole wake mtu yule ambaye yaja kwa sababu yake! 2 Ingemfaa zaidi mtu huyo jiwe la kusagia lifungwe shingoni mwake, akatupwe baharini, kuliko kumkosesha mmojawapo wa wadogo hawa. 3 Jilindeni; kama ndugu yako akikosa, mwonye; akitubu msamehe. 4 Na kama akikukosa mara saba katika siku moja, na kurudi kwako mara saba, akisema, Nimetubu, msamehe.
Kwa namna gani hawa wanaweza kumkosesha ndugu. Kwamfano ni pale, Mpendwa mwezako anaposikia umemsengenya, Sasa Kama ni mdhaifu kiimani Hili linaweza kuwa ni kwazo kubwa sana kwake ambalo likamfanya hata nguvu yake ya kuendelea kudumu katika kusanyiko ikapoa. Zipo shuhuda nyingi sana za wapendwa ambao wamerudi nyuma kiwokovu kwasababu ya maisha haya. Hivyo kama mwanaminio hakikisha, kinywa chako, unakichunga. Jifunze kuwa na kiasi na uvumilivu. Jifunze kujiepusha na mambo mabaya Kwa wapendwa wenzio.
Kwazo hili linaweza pia kuwa katika ufahamu wa kiroho .
Utakumbuka Ayubu, alipopitia majaribu yake mazito, hakuna mahali popote alinena maneno yasiyo faa, lakini wale marafiki zake watatu, yaani Sofari, Elifazi na Bildadi, (ambao wanawawakilisha watumishi wa Mungu), walipofika, walitumia ujuzi wao wa kibinadamu kumuhukumu Ayubu, kwamba ni kwasababu alitenda dhambi, hiyo ikampelekea Ayubu kunena hata maneno yasiyofaa.
Kama mtumishi wa Mungu, epuka hukumu ya macho,ukiletewa tatizo la mtu/ watu, usiangalie kwa jicho la nje, mwingine ni Mungu mwenyewe anampitisha katika madarasa yake, ukajikuta badala ya kutatua tatizo ndio unaongeza tatizo juu yake. Usianze kuhukumu matukio, bali kuwa katika Roho, tegemea zaidi uongozo wa Roho Mtakatifu. Hekima itakusaidia.
Pia lipo katika ujuzi.
Ukisoma Warumi 14, maandiko yanaeleza kwa upana jinsi ujuzi wetu unaweza kuwa kwazo kwa wengine wadhaifu was imani, kwamfano wewe ukipewa chakula ambacho umesikia kimepitishwa kwenye matambiko, ukashukuru, ukakila, ukijua kabisa chakula hakiwezi kukuondoa kwenye mpango wa Mungu. Lakini kwa ujuzi huo mwingine mwenye imani haba akakuona, na yeye akaanza kula vyakula vya kimatambiko na mila, akajikuta anashirikiana na uganga na mizimu, utakuwa umemsababishia kwazo kubwa kwa Mungu.
Lolote tunalolifanya, lazima tuangalie wengine wanaiga nini kwetu sisi wenye ujuzi. Uvaaji wako, wewe kama mkristo, unaweza ukajiona hauna shida kwako, lakini wengine wakaona ni sawa, hata kuvaa mavazi hayo ambayo hayana utukufu mbele za Mungu, utakuwa umefanyika kwazo kwao
Wapagani wanaweza kuzuia injili, isihubiriwe mahali, wakawapiga au wakawafunga watu wa Mungu n.k. Utaona Herode alimpinga Yohana akamweka gerezani hakuweza tena kuhubiri injili, wapagani waliwapinga watakatifu wengi. Hata mitume katika ziara zao walikutana na vikwazo vingi kutoka kwa watu wa mataifa, mahali pengine hawakuweza kuhubiri kwa utulivu (1Wakorintho 15:32, 1Wathesalonike 2:2).
Watu ambao hawajakamilika katika imani. Kwamfano ni mpendwa lakini mzinzi, sasa wale watu wa nje, ambao walikuwa wanakaribia kuvutwa katika imani, wanapoona matendo ya watu kama hawa, wanasema kama ukristo wenyewe ndio huu ni heri niendelee kuwa mpagani. Hayo ni makwazo. Au unakuta mwingine ni tapeli, mwingine ni mtukanaji, mambo kama haya hufanyika kwazo kubwa sana kwa wapagani kuihubiri injili.
2Wakorintho 6:3 Tusiwe kwazo la namna yo yote katika jambo lo lote, ili utumishi wetu usilaumiwe; 4 bali katika kila neno tujipatie sifa njema, kama watumishi wa Mungu; katika saburi nyingi, katika dhiki, katika misiba, katika shida;
Hitimisho:
Hivyo wewe kama ni mkristo jitahidi sana kuyaepuka makwazo kwa waaminio wenzako au kwa wapagani. Lakini pia kama ulikwazwa na ndugu yako, basi, suluhisho sio kuvunjika moyo au kuuacha wokovu, bali ni kunyanyuka tena na kuendelea mbele. Biblia inasema;
Mithali 24:16 Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena; Bali wasio haki hukwazwa na mabaya.
Amka tena, mtumikie Bwana, kwasababu alishatujuza tangu mwanzo kwamba hayana budi kuja, hivyo hilo liwe ni jambo la kawaida kwako, jitie nguvu uendelee mbele.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mafundisho mengine:
USIMLAANI KIZIWI, WALA USITIE KWAZO MBELE YA KIPOFU.
Biblia inasema tusiwe kwazo kwa yeyote, je! inawezekanikaje kwa dunia hii ya sasa?(2Wakorintho 6:3).
MIMI SIOMBI KWAMBA UWATOE KATIKA ULIMWENGU.
HISIA YA MUNGU ILIYO MBAYA KULIKO ZOTE.
Jibu: Tusome,
1 Wafalme 9:12 “Naye Hiramu akatoka Tiro kuitazama hiyo miji Sulemani aliyompa; wala haikumpendeza.
13 Akasema, Miji gani hii uliyonipa, ndugu yangu? Akaiita NCHI YA KABULI, hata leo”.
Nchi hiyo iliitwa “Nchi ya Kabuli” na sio “Nchi ya Kaburi”.Kuna tofauti ya “Kabuli” na “Kaburi”.
Maana ya “kaburi” ni shimo la kuzikia mtu aliyekufa, lakini “Kabuli” maana yake ni “isiyofaa kitu”. Kwahiyo hapo inaposema Nchi ya Kabuli, maana yake ni nchi isiyofaa kitu.
Sasa kwanini nchi hiyo iliitwa hivyo na huyu Hiramu?. Na ni funzo gani tunapata?.
Kipindi Sulemani anaijenga nyumba ya Mungu pamoja na nyumba yake mwenyewe, aliingia makubaliano na Mfalme wa Tiro kwamba Mfalme wa Tiro atampa Sulemani Malighafi za ujenzi (Miti ya Mierezi na mawe pamoja na malighafi nyingine baadhi, 1Wafalme 5:17-18), kwa makubaliano ya kwamba Mfalme Sulemani atampa Hirimu, mfalme wa Tiro ardhi kama malipo.
Sasa baada ya Sulemani kukamilisha ujenzi wa nyumba hizo mbili, ambapo alitumia miaka 20 (1Wafalme 9:10), aliazimu kumlipa Hirimu malipo yake.
Hivyo Sulemani akaamua kumpa Mfalme wa Tiro miji 20, (maana yake kila mji mmoja kwa mwaka mmoja aliotumikiwa). Zaidi ya hayo Sulemani alimpa Hiramu mwaka kwa mwaka kori nyingi za mafuta na ngano.
1Wafalme 5:10 “Basi Hiramu akampa Sulemani miti ya mierezi na miti ya miberoshi kadiri alivyotaka.
11 Sulemani akampa Hiramu kori ishirini elfu za ngano, chakula cha watu wake, na kori ishirini za mafuta safi. Ndizo Sulemani alizompa Hiramu mwaka kwa mwaka”.
Lakini tunasoma Hiramu, Mfalme wa Tiro hakupendezwa na miji hiyo 20 iliyokuwa kaskazini mwa Israeli (Galilaya, mpakani na Tiro), na biblia haijataja sababu za yeye kutopendezwa na miji hiyo, huenda pengine aliona si mizuri na yeye alitegemea kupewa miji mingine mizuri yenye kupendeza, ambayo huenda ipo katikati ya Israeli.
Na kwasababu hakupendezwa nayo, aliipokea tu hivyo hivyo, na kuiita “miji isiyo na faida” yaani “Kabuli”
Lakini yote katika yote biblia haijaelezea kwa kina sababu ya Sulemani kufanya vile, au sababu ya Hiramu, Mfalme wa Tiro kutopendezwa nayo na hata kuiita nchi ya Kabuli (Maana yake isiyofaa kitu).
Ni nini tujajifunza kupitia habari hiyo na miji hiyo?.
Tunachoweza kujifunza ni kuwa tunapotenda wema “tusitegemee malipo kutoka kwa wanadamu, bali kutoka kwa Mungu”. Malipo ya wanadamu siku zote yana mapungufu mengi.
Mfalme huyu wa Tiro, alikuwa ni mtu mwema sana kuliko wafalme wote waliowahi kutokea Tiro, na zaidi sana alikuwa ni rafiki yake Mfalme Daudi, baba yake Sulemani, na hata alivyosikia kuwa Sulemani anataka kumjengea Mungu nyumba alifurahi sana na kumtukuza Mungu wa Israeli, (1Wafalme 5:7) hivyo akamtia nguvu Sulemani kwa sehemu kubwa sana, lakini pamoja na hayo alitazamia kupewa thawabu nyingi (malipo mengi) kutoka kwa Sulemani, kwasababu alijua Sulemani alikuwa Tajiri sana, Zaidi ya wafalme wote duniani, lakini kinyume chake akapewa vichache tofauti na alivyotegemea, hivyo moyo wake ukauma!, lakini Laiti kama angetegemea vichache ni wazi kuwa asingeumia kwa vile alivyopewa badala yake angeshukuru na thawabu yake ingezidi kuwa kubwa mbele za Mungu.
Hivyo na sisi hatupaswi kutegemea malipo kutoka kwa watu, pale tunapotenda wema bali tunapaswa tuwe na nia ya kiasi, ili wakati wa Bwana ukifika tupate thawabu kulingana na kile tulichokitenda.
Bwana atubariki.
Maran atha.
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mafundisho mengine:
Miji ya Tiro na Sidoni ni miji gani kwasasa?
Kwanini Herode aliwakasirikia watu wa Tiro na Sidoni? (Matendo 12:20)
Je! Sulemani alienda mbinguni?
Je Mungu anaketi katika giza? (1Wafalme 8:12)
Neno hilo utalisoma katika andiko hili;
Yohana 19:13 Basi Pilato, aliposikia maneno hayo, akamleta Yesu nje, akaketi juu ya kiti cha hukumu, mahali paitwapo Sakafu ya Mawe, au kwa Kiebrania, Gabatha
Maana ya Gabatha ni “eneo lililoinuka”. Ni sehemu iliyojengwa mbele ya jumba la kifalme la Pilato ambapo hukumu zake alizitolea hapo. Kama biblia inavyosema paliitwa sakafu ya mawe. Maana yake palikuwa ni eneo la sakafu iliyojengwa kwa mawe. (Tazama picha juu).
Hapo ndipo hukumu ya Bwana wetu Yesu Kristo ilipotolewa ya yeye kusulibiwa.
Lakini jambo ambalo unapaswa utafakari kuhusiana na tukio hilo, ni kuwa Mungu, ambaye ndiye muhukumu wa wanadamu wote, anasimama mbele ya kiti cha hukumu cha wanadamu kuhukumiwa. Mungu kukubali kuhukumiwa Ni ishara ya unyenyekevu usiokuwa wa kawaida. Na hapo tunathibitisha kuwa hukumu za wanadamu hazitendi haki. Lakini utafika wakati na yeye mhukumu mkuu ataketi katika kiti chake cha enzi kuwahukumu wanadamu wote. Ambapo kwa haki kila mtu atalipwa sawasawa na matendo yake.
Jiulize wakati huo utakuwa upande upi?. Kwake hakuna upendeleo wa kibinadamu kama alivyofanya Pilato kwa wayahudi, kwake hakuna rushwa, kwake hakuna siri, yote yatamulikwa na kuwekwa wazi, na kama jina lako halipo katika kitabu cha uzima, utatupwa katika lile ziwa la moto, ambapo utateketea huko usiku na mchana.
Ufunuo 20:11 Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. 12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. 13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. 15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.
Je! Umejiandaaje kukutana na mhukumu wa haki? Kumbuka huwezi kuokoka, ikiwa bado upo nje ya Kristo Yesu. Unachopaswa kufanya ni kutubu leo, ili upate ondoleo la dhambi zako. Ndipo kuanzia huo wakati na kuendelea uwe na amani na Mungu wako,. Hakuna ukombozi kwa yoyote Yule zaidi ya Yesu Kristo.Huwezi kuokoka kwa nguvu zako mwenyewe. Yesu alikufa tayari kwa dhambi zako, ili aziondoe, akuhesabie sio mkosaji.
Ikiwa upo tayari leo kumkabidhi Bwana maisha yako ayaokoe na kuyaongoza, Basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mafundisho mengine:
Kiti cha Rehema kilikuwaje? (Kutoka 40:20)
Uga ni nini? Na kazi yake ni ipi kibiblia?
MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.
Wote wanaokumbwa na mauti sasa ni kutokana na dhambi zao?
Chetezo ni nini katika biblia? (Walawi 10:1)
Mungu mara nyingi huwa anatumia lugha ya picha au maumbo, ili kutupa sisi uelewa mzuri kuhusiana na mambo ya rohoni. Kama tunavyojua inapotokea mtawala, labda raisi amekualika uketi pamoja naye meza moja ule chakula, ni wazi kuwa kwa tendo hilo litakuwa limekupandisha hadhi sana.
Sasa zamani, za wafalme ilikuwa mtu aliyepewa heshima kubwa aliwekewa kiti chake kidogo pembeni mwa mfalme upande wake wa kuume. Na hiyo ilikuwa inamaana kubwa zaidi ya heshima peke yake, bali pia ilimaanisha kupewa mamlaka.
Hivyo katika biblia unapokutana na “mkono wa kuume” Mungu ametumia picha hiyo kumaanisha aidha mambo haya makuu matatu;
1. HESHIMA.
Maandiko kutuambia Kristo, ameketi mkono wa kuume wa Mungu, ni kutuonyesha, hadhi na ukuu alionao sasa. Mbinguni wapo malaika wengi wenye nguvu, wapo wenye uhai wanne, wapo maserafi na mamilioni ya malaika, lakini hakuna hata mmoja alipewa hadhi ya kuwa karibu/sawa na Mungu zaidi ya Kristo, Bwana wetu.
Waebrania 1:13 Je! Yuko malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako chini ya nyayo zako? 14 Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?
Kwahiyo, aliyepokea heshima, ya juu zaidi ya viumbe vyote ni Kristo Yesu Bwana wetu. Na ndio maana tunamwabudu na kumtukuza. Na heshima zote na shukrani zinamwelekea yeye tu peke yake. Ndiye Mfalme wa Wafalme, na Bwana wa Mabwana. Hafananishwi na mwanadamu yoyote duniani, au malaika yoyote mbinguni.
2. MAMLAKA.
Lakini pia mkono wa kuume sio tu heshima bali pia huwakilisha mamlaka, Kuketi kwake kule, ni kuonyesha mamlaka ya kumiliki na kutenda jambo lolote na kutiisha vitu vyote chini yake anayo.
Waefeso 1:20 aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; 21 juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; 22 akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo 23 ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote
> Vilevile anayo mamlaka ya kutuombea na kutuondolea dhambi, kama kuhani mkuu,
Warumi 8:34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea.
>Mamlaka ya kutumwagia vipawa vya rohoni na nguvu ya kushuhudia habari njema.
Matendo 2:33 Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia,
Luka 16:19 Basi Bwana Yesu, baada ya kusema nao, akachukuliwa juu mbinguni, akaketi mkono wa kuume wa Mungu. 20 Nao wale wakatoka, wakahubiri kotekote, Bwana akitenda kazi pamoja nao, na kulithibitisha lile neno kwa ishara zilizofuatana nalo
3. ULINZI.
Uwapo karibu na mfalme, maana yake upo salama, chini ya mfumo wa ulinzi wake. Hivyo Mungu kumweka Kristo kuumeni mwake ni kutuonyesha sisi,ufalme wa Kristo hauhasiki. Na wanaompinga kazi yao ni bure. Na Mungu atawaweka maadui zake chini ya miguu yake.
Zaburi 110:1 Neno la Bwana kwa Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwafanyapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako.
Lakini jambo ambalo watu wengi hawajua ni kwamba Bwana anataka na sisi tumweke yeye mkono wetu wa kuume, maana yake tumpe heshima yake, katika mambo yetu, na yeye, atatuheshimisha, atatuinua, na atatulinda.
Matendo 2:25 Maana Daudi ataja habari zake, Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote, Kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike.
Usiweke Mali kuumeni kwako, usiweke elimu, au mwanadamu kuumeni kwako. Bali Kristo tu peke yake.
Unaweza pia kupitia vifungu hivi Kwa maarifa zaidi; Mathayo 22:44 , Matendo 7:55, Wakolosai 3:1, Waebrania 1:3,13, 10:12, 1Petro 3:22.
Bwana akubariki.
Je! Kristo yupo kuumeni kwako? Fahamu tu ili Kristo awe pembeni yako, na wewe pembeni yake wakati wote, ni sharti uwe umeokoka. Na wokovu unakuja kwanza kwa kutubu (, yaani kukubali kuacha njia mbaya), na hapo hapo unaupokea msamaha wa dhambi, kisha Kristo anaingia moyoni mwako. Na baada ya hapo unaitimiza haki yote kwa kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi, wa maji mengi na kwa jina la Bwana Yesu, na Roho atakuwa tayari ameshakuja ndani yako kuanzia huo wakati na kuendelea. Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu leo akusamehe dhambi zako, basi fungua hapa kwa mwongozo mfupi wa sala ya toba>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Ubarikiwe.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Moyo wake mwenye hekima upo upande wa kuume, maana yake nini?
Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?
Nini maana ya.. “Utoapo sadaka mkono wako wa kuume usijue ufanyalo mkono wako wa kushoto”
KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?
SWALI: Siku ya kwanza Mungu aliumba Nuru, Je ilitokea wapi wakati Tunafahamu jua ambalo ndio lenye kutoa Nuru liliumbwa siku ya Nne?(Mwanzo 1:14-19)
Mwanzo 1:3-5
[3]Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru. [4]Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza. [5]Mungu akaiita nuru Mchana, na giza akaliita Usiku. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku moja.
JIBU: Mungu si kama sisi wanadamu ambao tukitaka kuunda jambo ni lazima tuwe na chanzo Fulani husika. Kwamfano hatuwezi kumleta mtu duniani Kwa kumchukua mwanamke na kumfungia ndani tu peke yake bila mwanaume tukitarajia baadaye ajifungue .
Lakini Mungu ni tofauti anaweza kumpa uzao pasipo kumkutanisha na mwanaume. Tunaona alifanya Kwa Mariamu. Lakini ameamua kuunda njia rasmi ya sisi kuzaliana, ambayo ndio hiyo ya watu wawili kukutana.
Vivyo hivyo na pale mwanzo Mungu kutanguliza Nuru, SI jambo la kushangaza kwake. Yeye ni mweza wa yote, Dunia hii ingeweza kumulika sikuzote Daima pasipo kutegemea jua Wala mwezi Wala nyote.
Lakini aliamua aviundie na chanzo chake, Kwa lengo la kutenganisha majira.
Lakini pia ni vema tukapata ufunuo, wa tukio lile, Nuru Ile ilimwakilisha nani. SI mwingine zaidi ya Yesu. Kumbuka Yesu katika agano la kale alijifunua katika maumbo. Lakini katika agano jipya waziwazi. Hivyo ilihitaji Nuru iwepo ili shughuli zote za uumbaji ziendelee.
Yohana 1:1-5
[1]Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.[2]Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. [3]Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika. [4]Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. [5]Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza.
Je! Kristo Ameangaza ndani Yako? Tambua kuwa pasipo Kristo hakuna maisha, hakuna uhai, Tubu Leo mgeukie Kristo Akusamehe dhambi zako.Ili uumbwe upya na Mungu. Hivyo Ikiwa upo tayari kufanya hivyo sasa fungua hapa Kwa mwongozo wa Sala ya Toba>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.
Je! Siku ilihesabiwaje kabla ya jua na mwezi kuumbwa?
JE! KUNA UMUHIMU WOWOTE WA KULIPA ZAKA?