Title Devis

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

SWALI: Biblia inaposema “Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao. (Mathayo 5:3)”je hatuna ruhusa ya kuwa matajiri katika roho?.

JIBU: Maskini ni mtu ambaye yupo katika hali ya kutojitosheleza, Sasa Bwana aliposema “heri walio maskini wa roho maana ufalme wa mbinguni ni wao”, hakumaanisha kuwa HERI wale wasio na maarifa yoyote au ufahamu wa mambo ya rohoni (yaani watu wasiomjua Mungu), hapana bali alimaanisha heri wale ambao kila siku wapo katika hali ya uhitaji wa kufahamu mambo ya ufalme wa mbinguni, watu ambao hawajajikinai, watu ambao kila siku wanatamani kuongeza kitu kipya katika maisha yao ya rohoni, watu wenye kiu na njaa ya kumjua Mungu kila siku…

Hao ndio Mungu anawaona ni maskini wa roho ambao kila siku wanamlilia yeye BABA, tupe! Tupe! Chakula cha rohoni..Lakini kuna wengine hawana haja tena ya kujua zaidi mambo ya rohoni, tayari wameshahitimu, pengine labda kwa kuwa walipitia vyuo vya biblia, au wameshasoma sana maandiko, hivyo wanajiona sasa wanajua kila kitu, hawana haja tena ya kujifunza, hata wakiletewa habari ya mpya wanadharau moyoni mwao wanaona kwamba hakuna chochote huyu mtu anaweza kuniongezea? Ndivyo ilivyokuwa kwa wale waandishi na mafarisayo.

Hawakutaka kukaa chini kuyasikiliza maneno ya YESU walimdharau na kumwona si kitu tofauti na yale makutano walimsikiliza kwasababu ndani yao kulikuwa na kiu na njaa na shauku ya kumjua Mungu zaidi na zaidi, na ndio maana Bwana Yesu akazungumza maneno yale.Ikiwa wewe unajiona hapo katika dhehebu lako ndio umefika, na hivyo huna haja ya kuambiwa chochote hata kama kinatoka kwenye maandiko basi fahamu kabisa kuwa upo mbali sana na ufalme wa mbinguni.

Ufunuo 3:17 “Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.

18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.”

Mtume Paulo mpaka anafikia uzee wake, anakaribia kufa pamoja na kwamba Mungu alimfanya kuwa askofu wa mataifa yote, mwenye heshima duniani kote katikati ya waaminio, mtu ambaye Mungu alimpa mafunuo makubwa ambaye hata sasa nyaraka zake tunazitumia kama mwongozo lakini mpaka dakika ya mwisho anamwagiza Timotheo kwamba siku akimfuata vifungoni mwake asiache kumpelekea vile vitabu vya ngozi ili azidi kujifunze zaidi,(2Timotheo 4:13) inatupasaje sisi?…

Huo ni mfano mzuri wa mtu aliye maskini wa roho, haridhiki sehemu alipo, haridhiki na kile alichonacho au alichopewa katika dhehebu lake au dini yake, kila siku anataka zaidi na zaidi amjue Mungu…Sio ajabu mtume Paulo aliandika hivi:1Wakorintho 8:2 “Mtu akidhani ya kuwa anajua neno, hajui neno lo lote bado, kama impasavyo kujua.”Hivyo tupende kila siku kutamani kupiga hatua moja zaidi rohoni, na hiyo inakuja kwa kutokukinai kujifunza Neno la Mungu kila siku.

Ubarikiwe sana.

Mada Nyinginezo:

UFALME WA MUNGU HAUPATIKANI KIRAHISI.

NOTI YA UFALME WA MBINGUNI

UPONYAJI WA YESU.

NI NANI ANAYEUFUNGA MLANGO WA MAARIFA?

LULU YA THAMANI.

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! vitabu vya biblia viliwezaje kukusanywa pamoja?

SWALI: Ninafahamu kwamba, watu waliokua wanakusanya vitabu/maandiko matakatifu kwa lengo la kuandaa BIBLIA, walikua wakiongozwa na ROHO MTAKATIFU Mwenyewe. Ili kitabu au maandishi yachaguliwe, waliangalia vigezo gani?-sababu na sikia, kuna baadhi ya vitabu havikuchukuliwa -Mfano Injili ya petro , na ya Tomaso.


JIBU: Hiyo ipo wazi kabisa kila kitabu cha biblia cha mwandishi yoyote tunayemsoma kimevuviwa na Roho Mtakatifu, hali kadhalika pia kuwepo kwa idadi ya vitabu 66 katika biblia hilo nalo ni tendo lililovuviwa na Roho Mtakatifu na wala sio wazo la kibinadamu kama wale ambao sio-wakristo wanavyofikiri. Ni mpango ambao Mungu alishaupanga kabla hata ya kuwekwa misingi ya dunia. Lakini siku zote Mungu huwa anamtumia “mtu” kutenda kazi japo sio kwamba hawezi kutenda pasipo hao hapana bali huo ni utaratibu wake tu aliojiwekea yeye(ndivyo ilivyompedeza).

Sasa tukirudi katika agano la kale, kukusanywa vitabu vile vyote 39, Mungu alitia hekima kwa wayahudi washindania Imani wakati ule,waliomcha Mungu, waliokuwa wasomi na wafuatiliaji wazuri wa unabii na historia ya taifa la Israeli kwa ujumla, hivyo kwao haikuwa kazi kubwa, kuvihakiki vitabu vya manabii waliowatangulia, Hivyo wale waliokubalika na habari zao zilithibitika kuja kutokea kweli,.Kwamfano vitabu vya torati ya Musa, ni vitabu ambavyo havikuwa na tashwishwi yoyote kwa wayahudi kwani ni vitabu vinavyoeleza chimbuko lao na vimepita kizazi hadi kizazi havijapotea tangu siku vilipoandikwa.. Vile vile Ukiangalia vitabu kama Esta,Ruthu,Wafalme, n.k. ni vitabu vya historia ambavyo vinaeleza habari zilizohalisi kabisa, vile vile vitabu vya manabii kama Isaya, Yeremia,Danieli vyote hivyo ni vitabu vilivyothibitika kuwa ni Vitabu vya wakati wote, na unabii wake ni thabiti ambao watu walikuwa wanawaona. Na kwa kuzingatia hayo ndio vikapatikana vile vitabu 39 vya Agano la kale. Lakini katika agano jipya, utaona kulikuwa pia kuna vitabu ambavyo vilishakubalika tangu kanisa la kwanza.

Kwamfano nyaraka za mtume Paulo zilikuwa zinatumiwa tayari na watakatifu wa makanisa yote yaliyokuwa Asia wakati ule kabla hata yeye hajaondoka, nyaraka zake zilikuwa zinazungushwa toka kanisa hadi kanisa..tunasoma hilo katika

Wakolosai 4:16 “Waraka huu ukiisha kusomwa kwenu fanyeni kwamba usomwe katika kanisa la Walaodikia pia; na ule wa Laodikia usomwe na ninyi

Kwahiyo haikuwa ngumu kuendeleza utaratibu huo mpaka kwa makanisa ya mbeleni. Vile vile utaona mtume Paulo, pia akirejea baadhi ya vifungo ambavyo vilikuwa katika vitabu vya Injili mfano Injili ile ya Luka, soma (1Timotheo 5:18b,linganisha na Luka 10:7) utalibitisha hilo kuwa kumbe hata Paulo alishapokea vitabu vya Injili kama sehemu ya maandiko matakatifu ya kurejea hiyo ni kuonyesha kuwa vitabu vya Injili vilikuwa tayari vimeshapokewa kama sehemu ya maandiko matakatifu ya wakati wote tangu kanisa la kwanza. Sasa baadaye watu kama wakina Klementi wa Rumi , Ignatusi wa Antiokia na Polikapi na wengine wakaja kutaja vitabu vingine. Na baadaye tena mabaraza kadhaa yaliitishwa ili kuthibitisha Uvuvio wa vitabu hivyo Na vigezo walivyokuwa wanatumia, ni kama vifuatavyo..

1) cha kwanza je! Mwandishi wa kitabu husika alikuwa ni mtume au alikuwa na uhusiano wa karibu na mitume.

2) Je! Kitabu husika kinakubalika na kanisa kwa ujumla.

3) Je! Kitabu kinabeba mafundisho halisi na ya msingi (kumtambua Yesu Kristo kama kiini cha Imani)?

4) Je! Kitabu hakivunji miiko na kanuni za rohoni ambazo zinathibitishwa na kazi ya Roho Mtakatifu mwenyewe?.

5) Kitabu lazima kiwe kwa sehemu Fulani kimenukuu vitabu vingine vya agano la kale..Kwamfano unaona nyaraka za Paulo nyingi zilinukuu vitabu vya Zaburi,Ayubu na Mwanzo.. Hivyo baraza la mwisho ambalo lilihitimisha kuwepo kwa vitabu 66 vya Biblia vilivyovuviwa, lilifanyika mwaka 397WK. Na ndio vitabu tulivyonavyo sasa. Lakini kumbuka kama tulivyosema kazi ya vitabu vya biblia kuwa 66 sio mwanadamu alipanga, hata ingekuwaje, kwa namna yoyote ile, kwa kupitia hatua hizo au nyingine zozote biblia ingetufikia tu kwa ukamilifu wake wote.

Ubarikiwe.


Mada Nyinginezo:

KITABU CHA YASHARI KINACHOZUNGUMZIWA KATIKA 2SAMWELI 1:17-18, NI KITABU GANI?

VITABU VYA BIBLIA: SEHEMU YA 1

NI KWA NAMNA GANI TUTASHINDA MAJARIBU?

NJIA MUNGU ALIYOIWEKA KWA KILA JAMBO:

UNAMCHUKULIA YESU KWAKO KAMA NANI?

UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Bwana alimaanisha nini kusema “waache wafu wazike wafu wao.(Mathayo 8:21)?

JIBU: Ili kufahamu vizuri hii habari turudi kidogo kwenye historia ya Wayahudi katika shughuli zao za mazishi, Kumbuka Waisraeli walivyozika zamani sio kama wanavyozika leo, leo hii mtu akifa wanamvisha sanda,(katika baadhi ya tamaduni) kisha wanamfukia chini bila jeneza, na shughuli inakuwa imeisha, lakini zamani, haikuwa hivyo katika tamaduni zao, kwanza makaburi yalikuwa sio ya kuchimbwa chini futi 6 kama yanayotumika sasa hivi hapana, bali yalikuwa yanachongwa kwenye mwamba, au pango lililotokea lenyewe asilia, na yalikuwa sio ya kuzikia mtu mmoja mmoja hapana bali yalikuwa ni ya familia, na kulikuwa kuna kuzikwa “kwa kwanza” na “kuzikwa kwa pili”, tofauti na tamaduni karibu zote tulizonazo sasahivi.

 Kwa mfano imetokea mshirika wa familia amekufa, mwili wake ukishaoshwa na kuvishwa sanda, ulikuwa unapelekwa kwenye kaburi hilo la familia, wakifika huko wanamweka sehemu yake maalumu peke yake,kwenye shelfu ambalo litakuwa limechongwa ndani ya kaburi hilo na huko wanaoruhusiwa kuingia ni wanafamilia tu, Hivyo wakishamlaza jambo linalofuata wanalifunga kaburi kwa jiwe kubwa kisha wanalisakafia, kisha wanarudi nyumbani kuendelea na maombolezo ambayo hayo yanadumu kwa muda wa siku kadhaa ikiwa aliyefariki ni mtoto katika familia, lakini kama ni mzazi iwe ni baba au mama siku za kuomboleza zinaendelea kwa muda wa mwaka mzima..Kisha baadaye mwaka ukishaisha wanafamilia wote na ndugu wanakusanyika tena kwa ajili ya maziko ya pili. 

Hapa ndipo mifupa ya Yule marehemu inatolewa, pale alipolazwa mara ya kwanza na kupelekwa kwenye shelfu lingine lenye mifupa ya wanafamilia wote waliokufa kabla yake, na mifupa yake inalazwa pamoja na ya kwao, kisha habari ya mazishi inakuwa imeisha rasmi, na ndio maana kama ulishawahi kusikia, pale biblia “inaposema akafa akakusanywa pamoja na watu wake”, hilo lilikuwa ni tendo la mwilini ambalo lilifunua tendo la rohoni, (Soma Mwanzo 49:29-33, Hesabu 20:24, Waamuzi 2:10 n.k.)…Kuna kukusanywa katika mwili na katika roho pia. Lakini hatutaenda huko sana. Sasa turudi kwenye swali, kwanini Bwana alimwambia Yule mtu vile..tusome:

Mathayo 8:21 ‘Mwingine katika wanafunzi wake akamwambia, Bwana, nipe ruhusa kwanza, niende nikamzike baba yangu.

22 Lakini Yesu akamwambia, Nifuate; waache wafu wazike wafu wao’.

Tumekwisha kuona jambo la kumzika Baba, halikuwa jambo jepesi la kwenda na kurudi kuchukua siku mbili au tatu, ni jambo linalochukua mwaka..Lisingekuwa jambo kubwa kwa Bwana kumwambia nenda urudi, Kama ni hivyo hata Bwana Yesu asingekaa kuhudhuria msiba wowote lakini tuona aliposikia habari za msiba wa Lazaro pamoja na umbali wote ule na hatari zote zile za kutaka kuuliwa.(Yohana 11),lakini alifunga safari kwenda kumponya. Lakini utaona huyu mtu alikuwa anajaribu kutafuta njia za kuikwepa kazi ya Kristo. 

Ndugu fahamu kuwa ili uwe mwanafunzi wa Yesu, ipo gharama ya kuingia, yeye mwenyewe alisema apendaye Baba au Mama kuliko mimi hanistahili. Pale Mungu anapokuambia sasa ni wakati wa wewe kunitumikia, usiwe ni wakati wa wewe kusema ngoja kwanza nikamalizie kufanya biashara zangu msimu huu ukiisha nitakutumikia, Mungu hataki udhuru. Na ndio maana akamwambia Yule mtu waache wafu wawazike wafu wao, ikimaanisha kuwa mtu yeyote aliye mbali na Kristo, ni mfu tayari katika roho japo atakuwa anatembea, lakini mauti ipo ndani yake na siku akifa wafu wenzake ambao bado hawajafa ndio watakaokwenda kumzika, Mauti inaanzia tukiwa tunapumua kadhalika wokovu unaanzia tukiwa bado tunapumua hapa hapa duniani..ndio maana hatuokoki tukishafika kule, wokovu unaanzia hapa hapa duniani, tunaokoka hapa, kule ni hitimisho la wokovu wetu. hivyo sisi tunaonywa pia tusitoe udhuru kwa vitu tuvipendavyo pale Yesu anapotuchagua tumfuate. 

Bwana akikuita umtumikie, na amekuambia acha kitu Fulani, usianze kutazama ni jinsi gani utawaachia wengine hiyo fursa wewe waachie wanaokifanya hicho kitu waendelee kukifanya wewe nenda kamtumikie Mungu, ikiwa leo hii amekuambie acha biashara haramu nifuate, usianze kumwambia Mungu ngoja kwanza nimalizie kuuza hizi zilizopo kisha nitaanza kufanya biashara halali. Mungu hapendi kuwekwa wa mwisho. 

Na ndio maana YESU akawaambia wanafunzi wake. ‘’Mtu aliyetia mkono wake kulima, kisha akaangalia nyuma, hafai kwa ufalme wa Mungu’’.(Luka 9:62). Ukristo unayo gharama. Ni kujikana na kupiga gharama kweli kweli.

Ubarikiwe.


Mada Nyinginezo:

JE! NI KWELI UMEMFUATA YESU?

JIKANE NAFSI MTEULE WA MUNGU.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

UKOMA NA UJANE ULIO NDANI YAKO, UMEUPATIA TIBA?

LENGO LA SHETANI KWA WATOTO WA KIZAZI HIKI.

JINSI ITAKAVYOKUWA KATIKA SIKU ILE


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Kushiriki au kujihusisha kwenye michezo ni dhambi?..

SWALI: Kama vile kutazama mpira (simba na yanga), au kucheza mipira ya kikapu n.k?

JIBU: Kwanza ni muhimu kufahamu kuwa vimtokavyo mtu ndani ya moyo ndivyo vinavyomfanya kuwa najisi..Chochote mtu anachokifanya, au anachojihusisha nacho kinachomsababishia moyoni mwake kutoke ugomvi, ubishi, mashindano, hasira,matusi kitu hicho tayari ni najisi kwake…Biblia inasema.

Wafilipi 2: 3 “Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake’’.

Swali je! Kuna mchezo wowote ambao ukiufuatilia haukupeleki kwenye mashindano(malumbano)?…kushindana mpaka wakati mwingine kutukana na kufanyiana mizaha. Kama upo basi huo sio najisi kwako. Biblia pia inasema… 

Wafilipi 2: 14 ‘’Yatendeni mambo yote pasipo manung’uniko wala mashindano, 

15 mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu’’. 

Jiulize kuna mchezo wowote ambao ukishaisha haukupeleki kwenye manung’uniko?..yaani kuwanung’unikia wahusika wa huo mchezo, au kumnung’unikia mwenzako? Neno linasema hapo, ‘’ambao kati yao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu’’…sasa ni mwanga gani utakaoonesha endapo ukiwa ni mshabiki, au mtu wa manung’uniko, au mtu wa mizaha, au mbishi, na mtu wa mashindano? Ni kitu gani hapo kitakachomfanya mtu asiyeamini avutiwe na Imani yako?…

Jiulize tangu uanze kuwa mshabiki wa mpira kuna mtu yeyote alishawahi kuokoka alipokutazama wewe wakati unaangalia mpira, au wakati wa wewe kumaliza kuangalia mpira? Au wakati magoli yanapofungwa?..kama ulishawahi kumbadilisha mtu kwa njia hiyo, basi kwako michezo sio najisi…Lakini kama bado ujue kuwa ni dhambi kujihusisha nayo. Hebu fikiria endapo Bwana Yesu yupo duniani angekuwa ni mshabiki wa mchezo Fulani, akishamaliza kuhubiria makutano anakwenda viwanjani kutazama michezo na akitoka hapo anashindana na wanafunzi wake kuhusu ule mchezo, tungewezaje kumwelewa?..angekuwa anatuchanganya…

Na sisi hatupaswi kuwachanganya watu walio nje ya Imani yetu. Wanapaswa wavutiwe na mienendo yetu ili watoke huko na kuja huku tuliko (2 Timotheo 2:24). Swali la mwisho kabisa la kujiuliza, ni juu ya muda unaotumia katika kushabikia au kuangalia hiyo michezo, jitathimini muda unaotumia kutazama hiyo michezo, ulinganishe na muda unaotumia kusali au kuomba au kusoma Neno. Kama unatumia dakika 10 kuangalia michezo na unatumia masaa matano au Zaidi kusoma Neno, basi ni wazi kuwa Michezo sio kitu kilichochukua nafasi moyoni mwako, na kinaweza kisiwe na madhara kwako, lakini kama unatumia masaa mawili kutazama michezo na Neno la Mungu au sala unatumia dakika tano au husali kabisa Hiyo ni Ashera ndani ya moyo wako, hivyo unaishi Maisha ya dhambi.

Kama kwenye ibada unasinzia halafu kwenye michezo unachangamka hilo Ashera kwako, Kama kwenye michezo unaouwezo wa kupiga kelele kwa nguvu kwa ujasiri wote, mpaka mtaa wa pili wanasikia halafu, ibadani kumsifu Mungu unaona aibu unanong’ona kwa sauti ya chini, ni machukizo mbele za Mungu. Kwahiyo kwa ujumbla michezo yote inayozaa magomvi, chuki, matusi, hasira, uchungu,mizaha,mafarakano, utani mbaya, vinyongo, manung’uniko, mashindano,visasi, vita, makwazo, tamaa, ulevi,wizi n.k..Yote ni kutoka kwa yule Adui kwahiyo ni dhambi kujihusisha nayo.

 Ubarikiwe.

Kwa mawasiliano/mafundisho zaidi kwa njia ya whatsapp, tutumie ujumbe kwenye
namba hizi: +255789001312/ +255693036618


Mada Nyinginezo:

KUCHEZA KARATA NI SAHIHI KWA MTU ALIYE MKRITO?

JE! UMEYABATILISHA MAMBO YA KITOTO?

INJILI YA MILELE.

KITABU CHA UKUMBUSHO

KWANINI USIICHAGUE TUZO ISIYOHARIBIKA?

KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Adamu aliwasaliana na Mungu kwa lugha ipi pale bustanini?

JIBU: Biblia haijataja lugha gani ilikuwa inatumika pale Edeni, Lakini ni wazi kuwa kulikuwa na lugha Fulani iliyotumika, kwasababu Mungu ametuumba sisi wanadamu tuwe tunawasiliana kwa njia ya kuzungumza, na hatuwezi kuzungumza bila lugha.   Sasa Mwanadamu wa kwanza Adamu alivyoumbwa ni tofauti na wengine tuliofuata..sisi wengine safari yetu ilianzia katika matumbo ya mama zetu lakini sio Adamu. Adamu Mungu alimwumba mkamilifu, maana ya mkamilifu ni kwamba hajazaliwa wala hajarithi, wala hajafundishwa, yaani ameumbwa tayari ana maarifa kichwani mwake. Tofauti na sisi, tunapozaliwa itatuchukua muda mrefu sana maarifa yaingie kichwani mwetu, mpaka tuweze kuelewa hichi na kile…inachukua miaka mingi….

Ndio maana Mungu alipomtengeneza Adamu alimletea wanyama aangalie atawaitaje..Adamu akawapa majina wote pale pale…hakuhitaji kujifunza kwanza herufi na matamshi..pale pale alianza kuzungumza…Huo ni uwezo wa kipekee sana.   Kwahiyo Adamu aliumbwa na lugha tayari kichwani ambayo kwa kupitia hiyo angeweza kuwasiliana na mkewe, wanawe pamoja na Mungu..(Ingawa Mungu ana uwezo wa kuzungumza na sisi pasipo lugha na tukamwelewa).   Na lugha hiyo Adamu aliyoumbwa nayo ni wazi kuwa iliendelea kutumika kwa vizazi na vizazi mpaka wakati wa Babeli..ambapo lugha nyingi ndipo zilipozaliwa..(Mwanzo 11). Kwahiyo kuitambua lugha yenyewe hasaa ni ipi, ni ngumu inawezekana ni moja ya lugha tunazotumia sasahivi, au ilishamezwa ndani ya lugha nyingine na kupotea kabisa..  

Ubarikiwe.


Mada Nyinginezo:

JINSI EDENI ILIVYOKUWA.

MTU MWENYE KUSITA-SITA KATIKA MAWAZO MAWILI.

ALIYE MKUU KATIKA UFALME WA MBINGUNI.

DHAMBI YA MAUTI

BEI YA UFALME WA MBINGUNI:

FUVU LA KICHWA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Ni dhambi kwa kijana aliyeokoka kuvaa suruali za kubana (model), kunyoa mitindo (mfano kiduku), ?

JIBU: Kumbuka mavazi tangu zamani licha tu ya kuwa na matumizi ya kujisitiri yalitumika pia kueleza hali ya mtu rohoni jinsi ilivyo. Kwamfano kwenye biblia utaona kulikuwa na mavazi ya kifalme (2Nyakati 18:9, Esta 6:8), Ni mavazi yaliyoweza kumtofautisha mfalme na watu wengine wa kawaida.Kulikuwa na nguo za magunia, tunalithibitisha hilo sehemu nyingi katika biblia, mtu akionekana amevaa mavazi ya magunia iliashiria kuwa yupo katika majonzi na maombolezo makubwa ya rohoni, pengine kwa kufiwa au kuomba toba mbele za Mungu…

Pia biblia inataja kuwa kuna mavazi ya kikahaba, (Mwanzo 38:14 ) ukisoma Mithali 7:10 inasema “Na tazama, mwanamke akamkuta, Ana mavazi ya kikahaba, mwerevu wa moyo;…mtu yeyote aliyekuwa ameonekana ameyavaa hayo” Kulikuwa na mavazi ya kikuhani pia ambayo yakivaliwa, yanamjulisha Yule ni Kuhani nk. yote hayo mtu alipokuwa akivaa yalikuwa yaashiria kitu Fulani rohoni.

Vivyo hivyo hata sasa, mavazi yanabeba tafsiri Fulani ya mtu rohoni. Kama binti wa kike anatembea barabarani kava kimini, au suruali, au top, au nguo nyepesi inayoonyesha maungo yake ya ndani, huyo tayari ni kahaba, kwasababu mavazi hayo yanavaliwa na wale makahaba wa KASINO na DISCO, ndio kitambulisho chao kule., mfano leo hii ukikutana na gari linye kibao juu kimeandikwa TAXI, huhitaji mpaka lisimame na kuliuliza kama kweli ni TAXI, moja kwa moja tokea likuwa kule mbali utalipunga mkono, lisimame kisha utapanda, kwani kibao chenyewe kinajieleza juu kwa gari lile ni la umma,

halidhadhalika ukimwona binti anatembea na nguo hizo hauhitaji kumthibitisha kama yeye ni kahaba tayari mbinguni na duniani anaonekana kama ni kahaba. Sasa kwa kijana wa kiume, suruali za milegezo, suruali za kubana (zinazojulikana kama utumbo wa kuku), hizo zinajulikana ni za wasanii wa kidunia na wanamtindo wa ulimwengu huu ambao hata habari na Mungu hawana…Lengo lao kubwa ni kuitangaza miili yao na mitindo yao.. Sasa Jiulize wewe kijana wa kikristo unayesema umeokoka unavaa milegezo,na suruali za kubana n.k. mbinguni na ulimwenguniunadhani unaonekanaje?, wewe na wanamuziki wa ulimwengu huu ni kitu kimoja hata kama utakana, ndivyo ulivyo..

Halidhadhalika unanyoa viduku, na kusuka, na kufuga rasta mtu akipita barabarani akakuita kama mmoja wapo wa wasanii wa ulimwengu wanaofanya hivyo au akikuita Bob Marley mvuta bangi utakwazika?.

Biblia inasema.

Warumi 12:1 “Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.

2 Wala msiifuatishe NAMNA YA DUNIA HII; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu”.

Hilo neno hapo juu NAMNA YA DUNIA HII, linamana ya FASHION. Kabla haujafikiria kuvaa suruali ya kubana, embu mvishe kwanza Yesu, kabla hujafikiria kunyoa kiduku mnyoe kwanza Yesu, ukiona hizo nguo hawezi hata kuzitazama mara mbili , inakupasaje wewe kama hayo mambo hayamstahili Mungu, wewe unayavaa ya nini?. Hivyo ni DHAMBI kwako..

Ubarikiwe.


Mada Nyinginezo:

FASHION! NI DHAMBI KWA BINTI ZA MUNGU.

MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.

UMUHIMU WA KUZALIWA MARA YA PILI.

JE! WEWE NI MWANA WA IBRAHIMU?.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

HUDUMA YA (ELIFAZI, BILDADI, NA SOFARI).


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! kuchora tattoo ni dhambi?

JIBU: Biblia inasema katika kitabu cha Mambo ya

Walawi 19: 28 “Msichanje chale yo yote katika nyama ya miili yenu kwa ajili ya wafu, wala MSIANDIKE ALAMA MIILINI MWENU; mimi ndimi Bwana”.

Bwana alikataza watu kuchanjwa chale kwasababu chale zote zinahusiana na ibada za wafu, au ushirikina, Bwana hajawahi kuwaagiza wana wa Israeli wanapopatwa na matatizo fulani au wanapohitaji kinga ya jambo Fulani wachanjwe chale..Hizo zilikuwa ni ibada za kipagani ambazo tunaona hapa Bwana anawaagiza wana wa Israeli wasizifuate hizo desturi…Bwana aliwaagiza kuwa tiba ya magonjwa yao ni kuzishika sheria zake basi na sio kwenda kujichanja mwilini.  

Lakini pia aliwaagiza wasiandike alama zozote katika miili yao (tattoo). Sasa wengi hawajui asili ya tattoo…watu wa zamani walikuwa hawachori tattoo kwa lengo la urembo kama sasahivi, watu wa zamani walikuwa wanachora tattoo kwenye miili yao kwa lengo hilo hilo kama la kuchanja chale, (kwa lengo la ibada) ilikuwa ni ibada za miungu, na walikuwa wanafanya hivyo kufuata maagizo ya miungu yao kuwa wanapotaka wapate jambo Fulani, au wajikinge na hatari Fulani, ni lazima wachore alama hizo katika miili yao..  

Hivyo zinaweza kuwa ni michoro ya aina Fulani ya wanyama kama vile nyoka, ndege, au wakati mwingine majina Fulani ya lugha zisizoeleweka, au alama za jua, au mwezi n.k. Na kwasababu shetani ndiye aliyekuwa nyuma ya mambo hayo basi kila aliyefanya hivyo alikuwa ananufaika kwa sehemu Fulani kwa masuala ya kishetani..ni kama tu mtu aliyechanjwa chale au anayetembea na hirizi leo, anakuwa anatembea na pepo Fulani linalomkinga dhidi ya mambo Fulani yanayohusiana na anachokiamini.   Lakini miaka ilipokwenda mbele watu waliwaona watu wanaojichora tattoo kuwa wanapendeza, hivyo pasipo kuchunguza asili la lile jambo ni ipi nao pia wakaenda kuiga mioyoni mwao wakidhani kuwa wanaweka urembo tu kwenye miili yao kumbe wanaweka uchawi na mapepo kwenye miili yao pasipo wao kujijua..wanajiongezea roho Fulani za yule adui katika maisha yao.   Kwahiyo mwili wowote wenye tattoo tayari una pepo fulani ndani yake, kwasababu asili ya tattoo au chale sio urembo bali kinga Fulani za kichawi..

Na Biblia imetuonya kuwa miili yetu inapaswa iwe hekalu la Roho Mtakatifu.  

1Wakorintho 6: 19 “Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;

20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu”.  

Kumbuka hapo biblia haijasema miili yetu sisi tuliomwamini Bwana YESU kuwa ni NYUMBA YA KAWAIDA, bali ni HEKALU, hekalu ni tofauti na nyumba za kawaida, kuna nyumba za aina nyingi, zipo za kulala wageni(guest house), nyumba za kuhifandhia mizigo, nyumba za kiofisi nk lakini HEKALU ni nyumba maalumu kwa ajili ya Ibada tu!!..sasa nyumba yenye chale au yenye tattoo itakuwaje hekalu la Mungu,?..Unaona?

kwahiyo kuchora tattoo ya aina yoyote ile sio sahihi.   Kama ulijichora tattoo huko zamani, au ulichanjwa chale udogoni na sasa umempa Bwana maisha yako hiyo ni vizuri sana, ile roho nyuma ya hiyo tattoo imeondoka lakini shetani bado atakuwa na visababu vichache vichache vya kukushitaki mbele za Mungu, hivyo chukua uamuzi wa kwenda kuvifuta hivyo vitu ili shetani asipate sababu yoyote ya kukushitaki..na pia mwili wako usitumike kuitangaza kazi za shetani, kwasababu usipofuta ni sawa na kampuni fulani la matangazo..   Hivyo futa tattoo zote mwilini mwako, uuwekwe mwili wako wakfu kwa Mungu sasa ili autumie..  

Ubarikiwe.

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

JE! KUBET NI DHAMBI?

JE! KUSHIRIKI AU KUJIHUSISHA KWENYE MICHEZO NI DHAMBI?

JE! KUFANYA MASTURBATION (PUNYETO) NI DHAMBI?

AMPOKEAYE NABII KWA KUWA NI NABII, ATAPATA THAWABU YA NABII; MSTARI HUU UNAMAANA GANI?

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

JE! SISI NI WAFALME NA MAKUHANI KWA NAMNA GANI?

UNYAKUO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Mbinguni Kutakuwa na kula na kunywa?.

JIBU: Biblia haijaeleza kwa mapana na marefu mambo yatakayokuwa yanaendelea mbinguni baada ya unyakuo kupita, na ndio maana mtume Paulo anasema katika 1Wakorintho 13:9 “Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu;..”

Hivyo kuhusu kama watakatifu watakula au hawatakula na kunywa biblia haijatoa jibu la moja kwa moja lakini tunaweza kutazama baadhi ya mistari inaweza kutusaidia kupata picha fulani. Tukisoma:

Marko 14.23 “Akatwaa kikombe, akashukuru, akawapa; wakakinywea wote.

24 Akawaambia, Hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi.

25 Amin, nawaambia ninyi, Sitakunywa tena kabisa uzao wa mzabibu, hata siku ile nitakapounywa mpya katika ufalme wa Mungu.

26 Nao walipokwisha kuimba walitoka kwenda mlima wa Mizeituni”. 

Tunaona katika habari hiyo hapo, Yesu akiwaagiza mitume wake kwa habari ya kunywa katika ufalme wa mbinguni, Lakini pia tukimtazama Bwana baada ya kufufuka kwake alikuwa na mwili wa umilele wa utukufu usioweza kufa tena, wala kuugua, mwili ambao uliweza kufanya mambo makubwa zaidi yasiyoweza kufanywa na mwili wowote wa asili, ule mwili uliweza kupotea na kutokea mahali popote, uliweza kuchukua sura tofauti tofauti, uliweza kupaa, na mpaka sasa unaishi n.k. Na kumbuka pia biblia inatuambia “siku atakapodhihirishwa tutafanana naye (1Yohana 3:2)”..Sasa jambo ambalo utaliona pale alipowatokea mitume wake baada ya kufufuka kwake aliwaambia wampe chakula chochote ale.

Luka 24.41 “Basi walipokuwa hawajaamini kwa furaha, huku wakistaajabu, aliwaambia, Mna chakula cho chote hapa?

42 Wakampa kipande cha samaki wa kuokwa.43 Akakitwaa, akala mbele yao”. 

Hiyo inatupa picha kwa sehemu jinsi miili hii ya utukufu itakavyokuwa, haitakuwa na mipaka Fulani kwamba kwasababu ni ya umilele haitaweza kula wala kunywa. Ni kweli kabisa uzima wa hiyo miili hautakuwa tena katika vyakula, inaweza kuendelea kuishi bila ya njaa wala chakula wala kutegemea chochote kile,kwasababu asili yake ni ya kimbinguni lakini hiyo haimaanishi kuwa haitaweza kunywa wala kula. Pia kumbuka Adamu kwa asili kabla ya kuasi alikuwa mtu wa umilele, asiyeweza kufa, wala kuugua, wala kuzeeka, lakini pamoja na ukamilifu wake Mungu bado alimuumbia ndani yake kula na kunywa katika ile bustani ya Edeni. Hivyo tusubiri tuone, tukifika huko tutajua zaidi, kikubwa tu tunachopaswa kufanya sasahivi ni kujitahidi kuishi maisha ya ushindi yampendezayo Mungu ili siku ile itakapofika tusikose kuyaonja hayo mambo mazuri Mungu aliyotuandalia ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia.

Ubarikiwe.

Mada Nyinginezo:

JE! MBINGUNI KUNA MALAIKA WA KIKE?

CHAGUA NI JIWE LIPI LITAKALO KUFAA KWA UJENZI.

ALAMA KATIKA VIPAJI VYA NYUSO.

USIONDOE ALAMA YA MPAKA ILIYOWEKWA NA MABABA.

JIHADHARI NA ROHO ZIDANGANYAZO.

UMUHIMU WA KUISHI MAISHA YAMPENDEZAYO MUNGU SASA.

MPENDE JIRANI YAKO KAMA NAFSI YAKO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?

SWALI: Maana unanipa utata je! Ni kwamba Nisiwabariki watu asubuhi?.


JIBU: Kumbuka Neno kubariki katika biblia ni Neno pana, licha tu ya kuwa na maana ya kutoa Baraka kwa mtu lakini pia linaweza kumaanisha kushukuru, kutukuza, kusifia, kusujudia, au kuhimidi..inategemea na mahali lilipotumika.   Kwamfano mstari kama huu

Zaburi 96:2 “Mwimbieni Bwana, libarikini jina lake, Tangazeni wokovu wake siku kwa siku”

Haimaanishi tu tulibariki (kwa kulitakia mema jina lake), hapana bali pia linamaanisha litukuzeni, lihimidini jina lake takatifu.   Sasa tukirudi kwenye huo mstari hapo juu, Tunaweza kuona kuna mambo mawili ambayo yamesababisha Baraka za huyu mtu zibadilishwa na kuwa laana. Jambo la kwanza ni kitendo cha yeye kumbariki mwenzake kwa SAUTI KUU. Na jambo la pili ni kufanya hilo tukio ASUBUHI NA MAPEMA.

  Mpaka mtu amsifie mwenzake kwa sauti kuu, kumbuka sio sauti tu ya kawaida hapana bali kwa sauti KUU ni wazi kuwa mtu huyo lengo lake ni asikiwe au aonekane na watu kitu anachokifanya na siku zote sifa za namna hiyo huwa zinakuwa si za kweli bali ni za kinafki. Na ndio hapo zinageuzwa na kuwa laana, mfano wake ndio ule Bwana Yesu alioutoa katika..  

Mathayo 6:5 “Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.6 Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.”

Unaona mtu huyu, kama angekuwa na nia kweli ya kubariki angemwombea yeye mwenyewe kwa siri au kwenda kuzungumza naye kawaida tu, na sio mpaka apige panda mbele.  

Pili kitendo cha mtu huyu kufanya hivyo asubuhi na mpema katika roho kuna maana kubwa sana. Sikuzote asubuhi na mapema ni wakati mtulivu ndio mwanzo wa siku, ambao mtu analazima kukatiza usingizi wake kwa ajili ya mambo ya muhimu sana. Na jambo la kwanza kabisa mtu akiamka asubuhi anachopaswa kufanya ni Kumbariki Mungu wake (kwa kumshukuru, kumwimbia na kumsifu). Ndege wakiamka asubuhi jambo la kwanza wanalolifanya ni kumsifu Mungu kwa sauti kuu ya shangwe, utawasikia kila mahali kwenye viota vyao kabla hata hawajaenda popote huko ndani wanamsifu Mungu.   Daudi aliamka ALFAJIRI na kumbariki Mungu kwa vinanda na vinubi kwa sauti Kuu sana.  

Zaburi 57:7 “Ee Mungu, moyo wangu u thabiti, Moyo wangu u thabiti. Nitaimba, nitaimba zaburi, 8 Amka, utukufu wangu. Amka, kinanda na kinubi, NITAAMKA ALFAJIRI. 9 Ee Bwana, nitakushukuru kati ya watu, Nitakuimbia zaburi kati ya mataifa. 10 Maana fadhili zako ni kubwa hata mbinguni, Na uaminifu wako hata mawinguni. 11 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako”.  

Halikadhalika Mungu aliwaamsha Manabii wake, asubuhi na mapema wawpeleke habari njema za wokovu kwa watu wake(Yeremia 44:4)

Unaona Alfajiri siku zote ni ya Mungu..Ukiamka na Bwana, basi siku yako yote itakuwa ni ya Baraka.   Lakini huyu anaamka asubuhi na mpema jambo la kwanza ni kumpa mwanadamu utukufu, tena kwa sauti kubwa kana kwamba yeye ndio aliyemfanya aamke asubuhi. Hivyo mbele za Mungu kwake inakuwa ni laana. Mambo kama hayo yanajirudia hata sasa hivi ikiwa utamka asubuhi jambo la kwanza ni kukimbila SMARTPHONE yako uangalie message zote jana zilizotumwa whatsapp na facebook. Jambo la kwanza ni kuchati na kupiga simu za biashara zako, jambo la kwanza ni kuamka na kuwatukuza wanadamu badala ya muumba wake, Jambo la kwanza ni kuongea na mpenzi wako ambaye hata si mke wako/mume wako.Basi fahamu kuwa hata siku yako nzima umeiharibu mwenyewe.

Mika 1: 1 “Ole wao wakusudiao mambo maovu, na kutenda mabaya vitandani mwao! Kunapopambazuka asubuhi huyafanya, kwa sababu ya katika uwezo wa mikono yao”.  

Isaya 5:11 “Ole wao waamkao asubuhi na mapema, wapate kufuata kileo; wakishinda sana hata usiku wa manane mpaka mvinyo imewaka kama moto ndani yao!”.

Hivyo Ujumbe mkuu hapo tuopaswa kuufahamu ni kuwa kitendo cha kusumbukia kitu kingine asubuhi na mapema tena kwa sauti kubwa kabisa, basi hicho kitu ni wazi kabisa kimekuwa ni KINGA yako, na biblia imeweka wazi kuwa amelaaniwa mtu Yule amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake. (Yeremia 17:5).   Alfajiri ikiwa ni ya Bwana, basi yaliyosalia nayo yatabarikiwa.

Warumi 11:16 “Tena malimbuko yakiwa matakatifu, kadhalika na donge lote; na shina likiwa takatifu, matawi nayo kadhalika”

Ubarikiwe.

Print this post

Kitabu cha YASHARI kinachozungumziwa katika 2Samweli 1:17-18, ni kitabu gani?

SWALI: 2 Samweli1:17-18. Inasema: Daudi akamwomboleza Sauli,na Yonathani, mwanawe,…”(Kama ilivyoandikwa katika KITABU CHA YASHARI’).Hicho kitabu cha Yashari ni kipi?


JIBU: Kumbuka Biblia sio kitabu cha kinabii tu kutabiri mambo yajayo peke yake, hapana bali pia ni kitabu kilichorekodi historia ya mambo yaliyopita, Na hiyo yote ni ili kutufundisha na kutuonya sisi kwa mifano iliyo hai ambayo ilishawahi kutokea huko nyuma,tuamini na kugeuka,

Hivyo sikuzote ili historia iweze kukubalika kuwa ni kweli ipo wazi kuwa ni lazima iwe imetibitishwa kwa ushahidi zaidi ya mmoja,   Kwa mfano haiwezekani historia ya vita vya Kagera ijulikane na watanzania tu peke yao watu wengine duniani wasiifahamu, yaani tujitangaze duniani kote sisi tulipigana vita na Uganda, lakini hakuna taifa hata moja lililoona hilo na kuthibitisha habari hiyo, kwa namna moja au nyingine zinaweza zikawa ni habari za kuzusha tu, lakini kama jirani zetu wakenya walishuhudia ni kweli, waganda walishuhudia ni kweli tulipigana nao, na Waafrika wote waliokuwepo kipindi kile watashuhudia jinsi walivyoshirikiana na sisi katika vita vile, basi hiyo vita kwa asilimia zote itakuwa ni ya ukweli na ilishawahi kupiganwa na hata kwa vizazi 100 vijavyo havitaweza kukana kwa ushahidi huo.  

Vivyo hivyo biblia nayo, ilivyoandika habari, kwa kuwathibitishia watu kuwa hayo yote ni kweli ikiwa kama mtu atatokea hatoamini kilichoandikwa, basi vipo vitabu vingine ambavyo vimerekodi habari za matukio hayo hayo biblia iliyoyarekodi, na mojawapo ndio hichi kitabu cha YASHARI ambacho tunaona kimeandika maombolezo ya mashujaa na sehemu nyingine matendo makuu yaliyofanywa na mashujaa wa Israeli.   Sasa tafsiri ya hilo Neno Yashari “NI MTU MWEMA AU MTU MTU WA HAKI”, hili ni Neno la Kiyahudi, hivyo kitabu cha Yashari ni kitabu cha mtu mwema, au mtu wa haki, na kitabu hichi katika biblia hakijazungumziwa hapa tu tunakisoma pia katika kitabu cha Yoshua :

Yoshua 10:12 “Ndipo Yoshua akanena na Bwana katika siku hiyo ambayo Bwana aliwatoa Waamori mbele ya wana wa Israeli; akasema mbele ya macho ya Israeli, Wewe Jua, simama kimya juu ya Gibeoni; Na wewe Mwezi, simama katika bonde la Aiyaloni.

13 Ndipo jua likasimama, na mwezi ukatulia, Hata hilo taifa lilipokuwa limekwisha jipatiliza juu ya adui zao. Hayo, Je! Hayakuandikwa ndani ya kitabu cha YASHARI? Basi jua likasimama kimya katikati ya mbingu, wala halikufanya haraka kuchwa kama muda wa siku nzima”.


Unaona, vipo pia vitabu vingine vinatajwa mbali na hii biblia yetu, ukisoma Hesabu 21:14, utaona kimoja kinaitwa kitabu cha VITA VYA BWANA. Ukisoma pia (1Nyakati 29:29), Utaona kulikuwa na kitabu kinachojulikana kama KITABU CHA TAREHE CHA SAMWELI MWONAJI, kulikuwa na kitabu cha tarehe ya Nathani nabii, na pia kulikuwa na kitabu cha tarehe ya Gadi mwonaji; Pia kulikuwa na kitabu cha tarehe cha wafalme wa Yuda, ukisoma (1Wafalme 14:29), utaliona hilo:..

1Wafalme 14:29 “Na mambo yake Rehoboamu yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Yuda?”

Unaona vyote hivyo vilinakili matukio ambayo biblia ilirekodi pia. Lakini sasa hiyo haimaanishi kuwa ni vitabu vilivyovuviwa na Roho Mtakatifu kwamba vitumike kuwa mbadala wa Biblia hapana, Hivyo vipo kuithitisha kuwa Biblia ni kweli na sio biblia kuthibitisha kuwa vitabu hivyo ni kweli.   Halikadhalika leo hii, utasema mimi siiamini kuwa biblia ina habari za ukweli, wala siamini kama YESU alizaliwa na bikiria kwa uweza wa Roho Mtakatifu, wala siamini kama alipaa, hizo ni hadithi za kutunga tu, zilibuniwa tu na watu Fulani Rumi, lakini nataka nikuambie vipo vitabu vingi vya historia na vya kidini mbali na hiyo biblia unayoitilia mashaka na vyote vinathibitisha ujio wa kwanza wa Yesu Kristo kuwa ni yeye pekee ndiye aliyezaliwa na bikiria kadhalika vinathibitisha ujio wake wa pili duniani kuwa atakuja kuuhukumu ulimwengu wote. na mojawapo wa vitabu hivyo ni QURAN!..

Sasa sio kwamba Qurani ni kitabu cha kweli cha Mungu hapana, kina mambo mengi sana yasiyo ya ukweli, lakini ndani yake kibebea chembechembe ndogo za ukweli kwamba ni kweli alishawahi kutokea Mtu wa kipekee aliyezaliwa bila dhambi na kuishi duniani anayeitwa YESU, na huyo atarudi tena mara ya Pili.   JE! Mambo yote Yesu aliyoyafanya tangu kuzaliwa kwake mpaka kufa kwake, na kurudi kwake hayakuandikwa katika kitabu cha waislamu Quran?. Ni uthitisho gani tena unahitaji?   Utakwenda wapi uukimbie uso wa Mungu, na ukweli uliopo katika Kristo Yesu?. Tubu leo YESU ndiye Njia kweli na uzima, NA YUPO MLANGONI KURUDI TENA, Hakuna tumaini nje ya yeye. Wala siku ile hakutakuwa na cha kujitetea.  

Ubarikiwe.


Mada Nyinginezo:

JE! VITABU VYA BIBLIA VILIWEZAJE KUKUSANYWA PAMOJA?

VITABU VYA BIBLIA: SEHEMU YA 1

TUZO UTAPEWA KULINGANA NA NAFASI YAKO.

INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA

HUYU AZAZELI NI NANI TUNAYEMSOMA KATIKA(WALAWI 16:8)

SHETANI ANATOLEA WAPI FEDHA, ANGALI TUNAJUA FEDHA NA DHAHABU NI MALI YA BWANA?

WITO WA MUNGU

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:


Rudi Nyumbani:

Print this post