Maisha Mapya ya wokovu yanasukumwa na maombi. Kama Neno ni chakula, basi maombi ni maji. Vilevile huwezi tenganisha maisha ya wokovu na uombaji.
Ni tendo la kuongea na Mungu, lakini pia kumsikia. Maombi sio maneno matupu tu, au utaratibu wa kidini, bali ni mahusiano halisi kati ya sisi na Mungu.
Yeremia 33:3
[3]Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.
Maandiko hayatoi ukomo wa maombi. Zaidi sana yanasisitiza tuombe kila wakati na bila kukoma.
1Wathesalonike 5:17 ombeni bila kukoma;
Waefeso 6:18 kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;
Hivyo Maombi ni tendo endelevu la wakati wote.
Mathayo 26:41 Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.
Luka 3:21 Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu
zilifunuka
Mathayo 17:20 Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.
21 [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]
Wafilipi 4:6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
Zipo aina mbalimbali za maombi, ili kufahamu kwa kina bofya hapa >> KUNA AINA NGAPI ZA MAOMBI?
Ramani kuu ya maombi tulishafundishwa na Bwana Yesu Kristo. Ambayo ndio ile Sala, ijulikanayo kama “Sala ya Bwana”. Hivyo kufahamu namna ya kuiomba fungua hapa >>>> Namna bora ya kuiomba sala ya Bwana
Miongozo mingine itakayokusaidia kutanua upeo wako wa uombaji kwa lengo la ukuaji wa kiroho Bofya hapa >>> MWONGOZO WA MAOMBI YA KUJIKUZA KIROHO.
Haya ni mafundisho, mengine yatakayokusaidia kujua kwa undani kuhusu maombi;
Kuomba katika roho ni kupi? na je nifanye nini ili niweze kuomba hivyo?
MWONGOZO WA MAOMBI YA ASUBUHI.
JINSI YA KUVURUGA MIPANGO YA MUNGU.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Kama tulivyotangulia kuona kuwa kusoma Neno kunazidisha Ujazo wa Roho Mtakatifu Ndani Yetu..lakini pia ndio Chakula kikuu cha Roho zetu. Bila NENO ni sawa na mwili bila chakula, huawezi kuishi.
Mathayo 4:4
[4]Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.
> Kusoma biblia ndiko kunakoweza kukukuza kiroho, (1Petro 2:2,),
> Pia ndipo unapoweza kufanywa upya ufahamu wako (Warumi 12:12).
> Lakini pia Ndani ya biblia kuna unabii wa maisha yako, kuna faraja, Kuna maonyo, kuna mashauri na miongozo (Zaburi 119:105).
Hivyo hakuna Namna mtu atayatenganisha maisha ya wokovu na usomaji Neno.
Sasa unapotaka kuanza kusoma unapaswa ufahamu Kuna usomaji wa aina mbili kuu.
Aina hizi mbili Ni muhimu kuendana nazo. Kuijua biblia yote ni jambo la msingi, kwasababu ili Kuelewa muktadha wa biblia ni lazima kwanza kuzielewa habari mbalimbali zilizo katika biblia.
Hivyo ni lazima Uwe na nidhamu ya kusoma kila siku. Na kama ukifanya Hivyo kwa kusoma sura 6-7 kwa siku, basi ndani ya miezi sita (6), utakuwa umeimaliza biblia yote. Ukimaliza kuisoma rudia tena na tena.
Lakini kusoma kwa muktadha ni kusoma kwa mnyumbuliko, kunahitaji pia mkufunzi Wa kukusaidia kuelewa. Pamoja na utafakariji sana wa Neno, na kwenda taratibu taratibu ili Roho Mtakatifu Akusaidie kuelewa.
1) Hakikisha unakuwa na biblia yako, wewe kama mwanafunzi mpya wa Kristo, yenye agano la kale na lile jipya. Biblia yenye vitabu 66
2) Tenga Muda wa utulivu wa kujisomea kila siku. Ni vema ukawa na mahali pako pa utulivu, ili kuweza kusoma kwa umakini zaidi.
3) Kuwa na daftari Na kalamu, ili Kuandika kila unachojifunza, kwa kumbukumbu zako za baadaye.
4) Omba kwanza kila unapoanza kujisomea biblia ili Mungu Akupe uelewa.
5) Mwisho Hakikisha unakitendea kazi kila unachokisoma.
Kujisomea na wengine pia ni jambo jema la ziada. Uwezavyo kupata rafiki ambaye anapenda biblia, basi kutana naye mara kwa mara, utafakari Naye maandiko. Epuka kampani za watu wasio- na kiu ya Mungu wakati wako huu, tumia muda wako mwingi katika kumtafakari Mungu, ili ukue kiroho kwa haraka, mtoto mchanga huwa ananyonya hata mara saba kwa siku. Kwasababu mwili wake upo katika kukua unahitaji maziwa wakati wote. Vivyo hivyo na wewe hakikisha una muda wa kutosha wa kusoma biblia kila siku.
Vifungu hivi unaweza ukavikariri viwe Kama nanga ya maisha yako ya usomaji Neno.
Zaburi 119:11
[11]Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.
Waebrania 4:12
[12]Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.
Yoshua 1:8
[8]Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.
Bwana akubariki.
Haya ni mafundisho yanayoweza kukusaidia kupata mwongozo wa usomaji biblia mzuri.
MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.
Mtiririko wa vitabu vya biblia kwanini upo vile?
CHAMBUZI ZA VITABU VYA AGANO JIPYA.
NIFANYE NINI ILI NISILALE NINAPOSOMA BIBLIA.
Kwanini kuna tafsiri nyingi za Biblia, na tafsiri ipi ni sahihi?
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Ahadi ya Roho Mtakatifu ni ya kila mwamini. (Matendo 2:39). Ni msaidizi ambaye Mungu alitupa ili kutuwezesha kuishi maisha ya wokovu kwa viwango vya ki-Mungu hapa duniani.
Hivyo siku ile ulipomkubali Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yako. Tayari ulipokea Roho Mtakatifu siku hiyo hiyo.
Isipokuwa Huwezi ukahisi chochote ndani, bali kwa jinsi unavyoendelea kutii kwa kumfuata Bwana utaziona tu kazi zake ndani yako.
Na hizi ndio kazi zake kuu azifanyazo Roho Mtakatifu anapokaa ndani ya mtu;
Yohana 16:13
[13]Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.
Yohana 14:26
[26]Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.
Warumi 8:26 Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
Wagalatia 5:16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana
hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.
Hivyo humfanya aendelee kuishi maisha ya utakatifu (Yohana 16:8)
Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu
1Wakorintho 12:7 Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana.
8 Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo
Roho yeye yule;
9 mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama za kuponya katika Roho yule
mmoja;
10 na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii; na mwingine kupambanua roho;
mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha;
11 lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake
kama apendavyo yeye
Matendo 1:8
Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi
wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.
Hivyo faida zote hizi hudhihirika ndani ya mtu kwa wingi , hutegemea jinsi mtu huyo anavyompa Roho Mtakatifu nafasi ndani yake. Ndio maana ni vema wewe kama mwamini mpya ujue mambo haya ili usije ukajikuta unamzimisha Roho Mtakatifu ndani yako. Ukawa unaisha maisha ya kama mtu ambaye hajaokoka.
Moja ya agizo la Bwana Yesu kwetu sisi, ni kwamba “tujikane nafsi”. Kujikana maana yake ni kuyatakataa matakwa yetu wenyewe ya mwilini na kukubali yale ya Mungu tu. Ulikuwa mlevi unakuwa tayari kukaa mbali na ulevi, ulikuwa ni kahaba unauaga ukahaba wako. n.k.
Kuwekewa mikono kunanyanyua mafuta Ya Roho Mtakatifu ndani ya mtu kwa namna nyingine. Na matokeo yake ni kuwa unaambukizwa pia neema.. Katika maandiko tunaona wapo watu kadha wa kadha waliojazwa Roho kwa namna hii. (Matendo 8:17, Matendo 19:6 , 2 Timotheo 1:6 )
Kiwango cha chini ambacho Bwana alituagiza ni SAA moja. Zaidi Pia katika maombi yako mwambie Bwana nijalie kuomba kwa Roho ( kwa kunena kwa lugha) ikiwa bado kipawa hichi hakijakushukia, Ni muhimu pia.
Zingatia: Katika uombaji wako,jifunze kutoa sauti, pia jiachie mbele zake. Huwezi kunena kwa lugha moyoni.. ni lazima kinywa kihusike hivyo Jifunze kuomba huku kinywa chako kikitoa maneno kabisa. Hiyo ni nidhamu nzuri katika hatua za ujazwaji Roho.
Tunajazwa Roho Kwa kuitambua sauti yake inatuagiza nini. Na sauti yake ni biblia. mahali Pekee penye uwepo wote wa Mungu ni kwenye Neno lake.
Hivyo zingatia sana hilo. Mkristo ambaye hasomi NENO, kamwe hatakaa aweze kumsikia wala kumwelewa Roho Mtakatifu.
Ukizingatia hayo basi, utaona uzuri wa Roho Mtakatifu ndani yako.
Mafundisho ya ziada kuhusu Roho Mtakatifu
YEYE ATAWABATIZA KWA ROHO MTAKATIFU NA KWA MOTO.
NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?
JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.
Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni ipi?
NAMNA YA KUNENA KWA LUGHA MPYA
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Nehemia 8:10 “Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu; maana siku hii ni takatifu kwa Bwana wetu; wala msihuzunike; KWA KUWA FURAHA YA BWANA NI NGUVU ZENU”.
Hapa anaposema “Furaha ya Bwana ni Nguvu zetu” hamaanishi “kufurahi kwa Bwana ndio Nguvu zetu”, hapana bali anamaanisha “Furaha yetu sisi katika Bwana ndiyo Nguvu yetu”.. Maana yake tunapofurahi tukiwa ndani ya MUNGU hiyo ni Nguvu kwetu..
Neno la Mungu linasema katika 1Wathesalonike 5:16 na Wafilipi 4:4 kuwa tufurahi siku zote katika Bwana..
Wafilipi 4:4 “Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini”
Furaha ya Bwana inapokuwa ndani yetu, ndivyo tunazidi kupata NGUVU za mambo yote.. Sasa tunaivutaje Furaha ya MUNGU ndani yetu?..Kwa mambo haya sita (06), furaha ya Mungu itaingia ndani yetu.
1. KUOKOKA
Mwimbaji mmoja wa Tenzi no. 22, (wimbo; Kale nilitembea) alisema hivi katika ubeti mmoja …
“ Hicho ndicho chanzo cha kufurahi kwangu, hapo ndipo mzigo uliponitulia…
usifiwe msalaba, lisifiwe kaburi linalozidi yote, asifiwe Mwokozi”.
Akimaanisha Msalaba ndio chanzo cha kwanza cha Furaha yake, na hiyo ni kweli kabisa.. Mtu aliyemkimbilia YESU huyo kafungua mlango wa kwanza wa mkondo wa Furaha katika maisha.. kwasababu yeye mwenyewe alisema tukienda kwake atatupumzisha na mizigo tuliyotwikwa na shetani na tutapata raha.
Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu”
2. MAOMBI.
Huu ni ufunguo wa pili wa Furaha ya kiMungu.. Bwana YESU alisema tuombe ili furaha yetu iwe timilifu..
Yohana 16:23 “Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu.
24 Hata sasa hamkuomba neno kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu”.
Unapokuwa mwombaji wa mara kwa mara, ukiwa binafsi au katika kikundi cha maombi, kamwe huwezi kupungukiwa Furaha, kwani maombi yanaumba Furaha ya kiMungu yenyewe ndani ya mtu.
3. KULIISHI NENO LA MUNGU.
Huu ni ufunguo wa tatu wa Furaha ya Mungu: Tunapolitenda Neno la Mungu/amri za Mungu moja kwa moja Furaha ya Bwana inaumbika ndani yetu, ambayo ndio chanzo cha nguvu yetu.
Yohana 5:10 “Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu; kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake.
11 Hayo nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu, na FURAHA YENU ITIMIZWE”.
4. KUIFANYA KAZI YA MUNGU.
Huu ni ufunguo wa Nne wa Furaha ya kiMungu ndani.. Unapojishughulisha na kazi yoyote ya Mungu, iwe kuhubiri mitaani, au kufanya huduma kanisani, au kumtolea Mungu sadaka, au shughuli nyingine yoyote ile ya kikanisa au nje ya kanisa inayohusu ufalme wa Mbinguni, hiko ni chanzo kikubwa sana cha Furaha ya kiungu, ambacho ndicho chanzo cha Nguvu za MUNGU.
Watu wenye kumtumikia Mungu kwa nguvu zao au mali zao wamejaa furaha siku zote.. hata kama watapitia vipindi vya huzuni, lakini kwa kipindi kifupi sana Furaha yao inarejea na wanakuwa na nguvu nyingi za rohoni, wanapotazama matunda ya kazi yao katika Mungu furaha yao inaongezeka.
2Wathesalonike 2:19 “Maana tumaini letu, au furaha yetu, au taji ya kujionea fahari, ni nini? Je! Si ninyi, mbele za Bwana wetu Yesu, wakati wa kuja kwake?
20 Maana ninyi ndinyi utukufu wetu, NA FURAHA YETU”.
5. KUMSIFU MUNGU.
Huu ni ufunguo wa tano wa Furaha ya kiMungu, tunapomsifu Mungu katika Roho na Kweli, Furaha ya kiMungu inaumbika ndani yetu.. na matokeo ya Furaha hiyo ni Nguvu ya Mungu..
Zaburi 43:4 “Hivyo nitakwenda madhabahuni kwa Mungu, kwa Mungu aliye furaha yangu na shangwe yangu; Nitakusifu kwa kinubi, Ee MUNGU, Mungu wangu”.
Msifu Mungu kwa vitu unavyoviona, msifu Mungu kwa uumbaji wake, msifu kwa upendo wake, msifu kwa miujiza yake n.k
6. KUSOMA NENO LA MUNGU.
Hiki ni chanzo sita cha Furaha Mungu, Mtu anayesoma Neno la Mungu maisha yake yatatawaliwa na Furaha tu siku zote..
Yeremia 15:16 “Maneno yako yalionekana, nami nikayala; na MANENO YAKO yalikuwa ni FURAHA KWANGU, na shangwe ya moyo wangu; maana nimeitwa kwa jina lako, Ee Bwana, Mungu wa majeshi”.
Ukiwa na Furaha ya Mungu utakuwa na Nguvu ya Kuendelea mbele katika mambo yote, utakuwa na nguvu ya kuomba, utakuwa na nguvu za kusubiri, utakuwa na nguvu ya kuinua wengine nk n.k.
Anza leo kuitafuta Furaha ya Mungu kwani hiyo ndio Nguvu yako, na kama tayari ipo ndani yako basi zidi kuipalilia kwa kufanya mambo hayo sita na mengine yanayofanana na hayo.
Mungu akubariki.
Maran atha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.
IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.
MUNGU HAJARIBIWI NA MAOVU BALI MEMA.
Ubatizo ni agizo la Bwana katika hatua za awali za wokovu. Wapo watu wanaosema Ubatizo hauna maana, ndugu usijaribu kufanya hivyo, unaweza usiwe na maana kwako, lakini unaomaana kwa yule aliyekupa hayo maagizo.
Mathayo 28:19 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
Ikiwa yeye hakuwa na dhambi wala kasoro yoyote alibatizwa, kwanini sisi tusibatizwe?
Mathayo 3:13 Wakati huo Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Yordani kwa Yohana ili abatizwe.
Ubatizo ni ishara ya nje ya kile ulichokiamini, kuwa umekufa kwa habari ya dhambi, kisha ukafufuka katika upya na Kristo.
Warumi 6:3-4
[3]Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?
[4]Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.
Ni yule aliyeamini, yaani kuupokea ujumbe wa injili kwa geuko(toba).
Matendo 2:41
Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa;…
Haraka sana, tangu siku ile alipoamini. Ubatizo sio mpaka umekomaa kiroho au kimafundisho, hapana, bali ulipopokea tu wokovu, wakati huo huo unastahili ubatizo.
Matendo ya Mitume 2:38
[38]Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
Ni ule wa kuzamishwa katika maji tele (Yohana 3:23, Matendo 8:36-38 ),
Na kwa jina la Yesu Kristo.(Ambalo ndio Jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu) [Mathayo 28:19, matendo 8:16, 10:48, 19:5]
Ndio, ili kufuata mkondo sahihi wa kimaandiko, huna budi kubatizwa tena.
Kwakuwa umeokoka, na bado hujapata huduma hiyo basi waweza tafuta Kanisa la kiroho, ambalo linaamini katika ubatizo wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo ili utimize agizo hilo.
Lakini ikiwa utapenda kusaidiwa na sisi. Basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi kwa msaada huo:
+255693036618 / +255789001312
Bwana akubariki.
Mistari ya kusimamia kila ukumbukapo tendo la ubatizo.
Wakolosai 2:12 Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu.
Wagalatia 3:27 Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo.
Bwana akubariki.
Kwa mafundisho zaidi kuhusu ubatizo
MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Dini ni mfumo au utaratibu wa kumwabudu Mungu. Kwamfano ukienda mahali ukaona watu wamekusanyika na kukubaliana kuabudu kitu Fulani, ni lazima utaona tu utaratibu, au mwongozo au miiko wamejiwekea ya kuifuata na kuishika, ili ibada yao iwe na matokeo. Sasa huo utaratibu ndio unaitwa dini.
Hata imani yetu ndani ya Kristo, inasukumwa na dini. Hatumwabudu tu Mungu kama tunavyotaka bali Mungu aliweka utaratibu na njia ya kuifuata.
Lakini Dhehebu, ni “aina ya dini”. Ambayo huzalika ndani ya imani ile ile moja. Kwamfano utaona wakristo imani yao ni moja kwa Kristo Yesu, na msingi wa kuegemea ni biblia ile ile moja takatifu. Lakini ndani yao kuna michipuko mingi tofauti tofauti ya kitaratibu na ufanyaji ibada, kulingana na walivyoielewa biblia. Ndio hapo utaona wengine wanajiita wapentekesto, wengine wakatoliki, wengine wasabato, n.k. Sasa hii yote ni michupuko, ambayo mengine inakaribiana sana na uhalisia, na mengine inakwenda mbali na kweli ya Mungu.
Lakini cha kumshukuru Mungu ni kuwa biblia imeshaeleza asili ya dini ya kweli inapaswa iweje….
Yakobo 1:26 Mtu akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hali akijidanganya moyo wake, dini yake mtu huyo haifai. 27 Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.
Kwamba ni lazima itakuwa ya kimatendo zaidi. Yaani utafunzwa utakatifu, na kujitoa.
Hapana, kwasababu Yesu hakuja kuleta dhehebu jipya duniani. Kwani alipokuja alikuta tayari yapo madhehebu mengi yamesha-zaliwa kama tu ilivyo sasa, mfano Mafarisayo, na masadukayo. Lakini hakuwahi kutetea lolote kati yao. Bali alisisitiza watu kumwamini yeye, kama ndio njia ya kweli na uzima mtu asipofanya hivyo hawezi kumwona Baba (Yohana 14:6).
Ikiwa na maana haijalishi una dhehebu zuri kiasi gani. Ukikosa shabaha ya Ukristo, bado mbinguni huendi. Waamini wengi wanashikilia zaidi dini, jambo ambalo ni jema, lakini dini ni kisaidizi cha imani. Sio imani yenyewe, ni sawa na shule na elimu, tunaweza kusema shule ni kisaidizi cha elimu, lakini sio elimu yenyewe.
Hivyo ni busara kuchukua tahadhari ya dhehebu unalotaka kumwabudia Mungu, kwasababu ukweli ni kwamba madhehebu mengine hayana ubora wa kumfanya mtu awe mkristo kamili.
Kwamfano dhehebu lisilo, patana na imani katika Kristo Yesu tu, au lisilofundisha utakatifu, au lisilo amini juu ya vipawa vya Roho Mtakatifu, au linalochanganya ibada ya Mungu na sanamu, bali linasisitiza mambo ya mwilini tu, hilo halikujengi, bali linakupoteza.
Lifananishe kwanza na biblia yako, huku ukimwomba Roho Mtakatifu akusaidie, kisha ndio ufanye maamuzi.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini kuna tafsiri nyingi za Biblia, na tafsiri ipi ni sahihi?
Swali: Tunajua watoto wachanga hawana dhambi sasa kwanini ile gharika ya Nuhu ilizomba mpaka vichnga?..kwanini Mungu aangamize mpaka watoto wasio na hatia?..napata utata na gharika ile ya Nuhu, na kwenye ile miji ya Sodoma na Gomora je na watoto nao walifanya dhambi ya kustahili kuchomwa na kugharikishwa vile?
Jibu: Ni kweli Biblia inaonyesha ile gharika iliua wote wenye roho ya uhai puani, ikiwemo watoto wachanga na wanyama… na waliosalia ni watu nane tu! Kati ya Dunia iliyokuwa imejaa mabilioni ya watu.
Mwanzo 7:22 “kila kitu chenye pumzi ya roho ya uhai puani mwake kikafa, kila kilichokuwako katika nchi kavu”
Sasa kwanini Mungu aangamize hadi watoto wadogo, na ilihali tunajua kuwa watoto hawana dhambi.
Jibu la swali hili ni kwamba, “mtu anaweza kubeba adhabu ya dhambi ya mwingine lakini asibebe ile dhambi” ili tuelewe vizuri tutafakari huu mfano.. “Mama mjamzito kafanya kosa likamsababishia kifo, ni wazi kuwa na mtoto aliyeko tumboni naye atakufa” kwahiyo adhabu wameshiriki wawili lakini aliyefanya kosa ni mmoja.
Ni hivyo hivyo kipindi cha gharika na kipindi cha Sodoma na Gomora, Watoto walibeba adhabu za wazazi wao ingawa si dhambi!..(wao hawakufanya dhambi yoyote), lakini kutokana na maasi kuwa mengi ikawasababisha nao kushirikishwa katika adhabu hiyo, lakini hiyo haimaanishi kuwa hawataokolewa siku ya mwisho.. huwenda watakaokolewa katika ufufuo wa mwisho kwasababu Mungu ni Mungu wa haki hawezi kumhukumu mtu asiye na kosa.
Lakini kwa wengine (watu wazima) waliosalia ambao ndio waliowasababisha watoto wao kuangamizwa na maovu yao, hao biblia imesema kuwa ipo hukumu nyingine itawapata ya kuhukumiwa kwa mara nyingine na kutupwa katika lile ziwa la moto.
Mathayo 10:15 “Amin, nawaambia, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma na Gomora kustahimili adhabu ya siku ya hukumu, kuliko mji ule”.
Hapo anasema itakuwa rahisi Sodoma na Gomora kustahimili, maana yake ipo adhabu nyingine kwa watu wa Sodoma na Gomora zaidi ya hiyo iliyowapata ya kuteketezwa kwa moto kutoka mbinguni..
Ndio maana Biblia inasema tumwogope yeye awezaye kuuua mwili, na akiisha kuua mwili (kwa moto au maji au kitu kingine) bado anauwezo wa kushughulika na roho tena na kuihukumu katika ziwa la Moto.
Luka 12:5 “Lakini nitawaonya mtakayemwogopa; mwogopeni yule ambaye akiisha kumwua mtu ana uweza wa kumtupa katika Jehanum; naam, nawaambia, Mwogopeni huyo”
Watu wa Sodoma na Gomora, pamoja na watu wa gharika ya Nuhu waliuawa katika mwili, lakini bado tena ipo adhabu nyingine inakuja juu yao, jambo linalotisha sana..
Kwahiyo jambo kuu la kujifunza ni kuwa adhabu inaweza kurithiwa au kushirikishwa na mwingine hata pasipo kufanya kosa, na kinyume chake ni kweli Baraka zinaweza kurithiwa hata pasipo mwingine kufanya mema.. Mzazi unaweza kuwa chanzo cha Baraka au matatizo kwa mtoto wako.
Fahamu kuwa Kama utakuwa mwovu kupindukia basi fahamu pia watoto wako hawatakuwa salama kwa uovu wako, ndicho kilichomtokea Mfalme Daudi baada ya kwenda kulala na mke wa Uria, Biblia inasema mtoto aliyezaliwa alikufa, ijapokuwa mtoto hakufanya kosa lolote… lakini alilazimika kubeba adhabu ya baba yake.
Vile vile kuna mambo mema unaweza kuyafanya yakawa akiba njema kwa watoto wako, au watu wanaokuzunguka wakati wa sasa au wa baadaye.. Kwahiyo ni lazima kumcha Mungu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je gharika ya Nuhu iliangamiza hadi samaki wa baharini na nyangumi?.
JE! NI CHEMCHEMI IPI INATOKA NDANI YAKO, YA MITO AU YA KISIMA?
Je! Adamu na Hawa walizikiwa wapi?
Haya ndio mambo ambayo baada ya kuokoka, wokovu hufanya juu ya maisha ya mtu
Yohana 3:3
[3]Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.
Maana yake ni kwamba pindi tu unapookoka, ni lazima ufahamu si kwamba unarekebisha yale maisha yako ya kale, na kuwa mtu mwema hapana bali unakuwa mtu mwingine kabisa. Kama mtoto mchana aliyekuja duniani, katika mazingira mapya kabisa.
Kwasababu ukristo sio nembo, au kikundi, au mtindo fulani au aina fulani ya dini hapana bali ni ulimwengu mwingine kabisa ambao mtu anaanza kuuishi.
2 Wakorintho 5:17
[17]Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.
Wakolosai 1:13
[13]Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;
Maana yake ni kuwa tunakuwa tayari kutoka chini ya utawala wote wa shetani, yaani kufuatisha mambo Ya kidunia, na anasa, wizi, tunaacha, Kama tulikuwa na vikoba vya kiganga, hirizi, mazindiko Yote hayo tunayaondoa, na kuanza kumtumikia Kristo, mfalme mpya.
Wafilipi 2:12-13
[12]Basi, wapendwa wangu, kama vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.
[13]Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.
Maana yake ni lazima Tujue wokovu ni mwendelezo ijapokuwa tunaokolewa pindi tu tunapookoka, lakini hatuupokei tu, na kusema tayari imekwisha hapana bali unapaswa udumu Moyoni mwetu, na kuhakikisha kila siku tunaweka umakini kwa kuuzalia matunda, kwa kufanya bidii kuishi maisha yampendezayo Mungu.
Hivyo kwa ufupi wokovu sio tu, kipawa cha Mungu Kwetu, lakini pia kukubali maisha mapya, mfalme mpya, na njia mpya.
Maana yake ni nini?
Tangu siku hii ya leo wewe uliyookoka hakikisha unayaweka kando mambo yote ya kale ambayo ulikuwa unayafanya yasiyompendeza Mungu, kwasababu hiyo ndio TOBA pekee, kama ulikuwa mzinzi acha mara moja, ulikuwa mlevi, ulikuwa mwizi, ulikuwa mlanguzi acha, kama alivyofanya Zakayo alipokutana na Kristo. Kisha endelea kuishi maisha ya utakaso kila siku, ili Wokovu wako uzidi kuwa thabiti.
Bofya hapa kurudi kwenye mwongozo mkuu wa mafundisho ya mwongofu mpya. >>
Nini kinafuata? bofya hapa. >>>
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Jina la Mkuu wa Uzima na Mfalme wa haki na pekee, YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu wetu, lililo taa na Mwanga wa Njia yetu (Zab.119:105).
Kama Mkristo ni lazima uzijue alama hizi kuu nne (04), zitakazothibitisha kuwa unaye KRISTO maishani mwako, na alama hizo ni HEKIMA, HAKI, UTAKATIFU na UKOMBOZI.
1Wakorintho 1:30 “Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanywa kwetu hekima itokayo kwa Mungu, na haki, na utakatifu, na ukombozi”
Maana yake kupitia Yesu Kristo tunapata Hekima, Haki, Utakatifu na Ukombozi.
1. HEKIMA YA MUNGU.
Kama Yesu ni hekima ya Mungu kwetu, je hii hekima ni nini na tunaipataje..
Ayubu 28:28 “Kisha akamwambia mwanadamu, Tazama, kumcha Bwana ndiyo hekima, Na kujitenga na uovu ndio ufahamu”.
Kumbe kumcha Bwana ndio hekima, maana yake kumpata Yesu ni kupata kumcha Bwana, na ndio hekima ya Mungu, na pasipo Yesu hakuna kumcha Mungu.
2. HAKI.
Na kama Yesu ni haki ya Mungu, je hii haki inapatikanaje..
Warumi 3:21 “Lakini sasa, haki ya Mungu imedhihirika pasipo sheria; inashuhudiwa na torati na manabii;
22 ni haki ya Mungu iliyo kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote waaminio. Maana hakuna tofauti;
23 kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;
24 wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu”
Tunapomwamini Yesu tunakuwa tumeipata haki ya Mungu, haki ya kupokea kila tuombacho, haki ya kuishi milele, haki ya kumkaribia Mungu, haki ya kuwa na afya, haki ya kuwa amani, haki ya kuwa na furaha n.k
3. UTAKATIFU.
Na kama pia Bwana Yesu ni Utakatifu wa Mungu.. Je huu utakatifu tunaupataje?
Hiki ni kipengele muhimu sana, ambacho kinakwepwa na wengi, kumbuka huwezi kumtenganisha Yesu na UTAKATIFU, Ikiwa umemwamini Yesu ni lazima uishi maisha ya Utakatifu, hiyo ni kanuni. Na utakatifu sio ule wa rohoni tu, bali pia wa mwilini..
2Wakorintho 7:1 “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku TUKITIMIZA UTAKATIFU katika kumcha Mungu”.
Utakatifu unakuja kwa kujitenga na vichocheo vyote vya dhambi, ambavyo vyanzo vyake ni tamaa ya macho na mwili, mfano wa hizo ni maudhui yote machafu yanayopatikana kwenye luninga, Mitandao na Magazeti, vile vile mazungumzo mabaya na makundi mabaya..
4. UKOMBOZI.
Yesu Kristo amefanyika pia ukombozi kwetu, kupitia kifo chake.. Na hii ndio alama ya mwisho inayomtambulisha Yesu, ambayo kimsingi hii ndio inayojulikana sana na wengi!
Wakolosai 1:13 “Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake.
14 ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi”
Ndugu ukimjua Yesu kama mkombozi tu! (yaani anayesamehe dhambi), pasipo kumjua kwamba yeye pia ni “Mtakatifu” na anataka tuwe watakatifu kuna shida katika kuaminini kwako, vile vile ukimjua tu kama ni mtakatifu pasipo kumjua kama ni Hekima ya Mungu na Haki ya Mungu, bado pia kuna kitu kitakuwa hakijakamilika.. Lakini tukimjua katika sifa hizo Nne na kuziishi basi tutakuwa tumemjua hasa, na kufikia ule utimilifu.
Waefeso 4:13 “hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo”
Bwana atusaidie tuweze kufikia cheo cha kimo cha utimilifu wake.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Maana ya Mithali 10:1 Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye;
HEKIMA NANE(8) ZA KIUINJILISTI, KATIKA KUWAVUA WATU KWA KRISTO.
Nini maana ya hekima ya maskini haisikilizwi? (Mhubiri 9:16)
Maana ya Mhubiri 9:18 Hekima ndiyo bora kupita silaha za vita;