Category Archive Uncategorized @sw-tz

JITAHIDI KUJA KABLA YA WAKATI WA BARIDI.

2Timotheo 4:21  “Jitahidi kuja kabla ya wakati wa baridi. Eubulo akusalimu, na Pude, na Lino, na Klaudia, na ndugu wote pia”

Mtume Paulo ni mtu aliyetambua kuwa kustawi kwa huduma yake kunategemea sana sapoti ya watendazi wenzake wengine wenye ni moja na yeye. Hivyo tunasoma wakati akiwa Rumi kama mfungwa, alimwandikia waraka mwanawe Timotheo, aiharakishe huduma yake, ili amfuate kule Rumi wasaidiane katika huduma kabla ya wakati wa bariki kuanza.

“Jitahidi kuja kabla ya wakati wa baridi”.

Paulo alijua mazingira yanaweza kukawiisha kusudi la Mungu. Hivyo alitambua kuwa mtu akiongeza jitihada anaweza kukamilisha mambo yake mapema kabla mazingira Fulani hayajamuathiri kutenda kusudi lingine la Mungu.

Kwa ukanda waliokuwa, ilikuwa ni ngumu sana, meli kusafiri nyakati za baridi kwasababu ya barafu baharini, hivyo safari zote za majini zilisitishwa kwa miezi kadhaa mpaka baridi itakapoisha ndipo safari zianze tena, Paulo aliliona hilo akatambua ni jambo la asili haliwezi kuepukika kwa kufunga na kuomba, isipokuwa kwa kupangilia tu ratiba vizuri.

Hii ni kutufundisha sisi, tufahamu kuwa mazingira Fulani, au nyakati Fulani zisizo rafiki sana huwa zinapita, au zitakuja mbele yetu ambazo zinaweza zikawa ni kikwazo cha utumishi kwa sehemu Fulani.

Kwamfano wakati wa baridi kwako, unaweza kuwa ni wakati wa ndoa. Kama wewe ni kijana hujaoa/ hujaolewa, unanafasi sasa ya kumtumikia Mungu kwa uhuru wote. Titahidi sana kufanya hivyo sasa, kwasababu nafasi hiyo inaweza ikapungua kwa sehemu uingiapo katika majukumu ya kindoa. Usipojitahidi sasa kujiwekea msingi mzuri kwa Mungu wako, utataabika sana kuujenga huo uwapo kwenye ndoa.

Wakati wa baridi unaweza ukawa ni kipindi cha kazini au masomoni. Ikiwa bado hujapata kazi, au upo likizo kazini au shuleni, embu tumia vema wakati wako, kuongeza kitu kikubwa katika ufalme wa Mungu, kwasababu shughuli zitakapokulemea, kuujenga tena huo msingi itakuwia ngumu sana, na kama ikiwezekana yaweza kukuchukua wakati mrefu. Uwapo ‘free’ usilale, bali tumia sasa kuongeza mikesha, maombi ya masafa marefu, kusoma biblia yote.

Wakati wa baridi waweza kuwa uzee. Kwa jinsi umri unavyokwenda ndivyo uwezo wa mwili wako unavyopungua, Hivyo utengenezapo mambo yako mapema na Bwana, basi wakati huo ukikukuta hautakuathiri sana, kwasababu tayari yale ya msingi uliyopaswa uyafanye umeshayafanya mapema, uzeeni ni kumalizia tu.

Zipo nyakati nyingi za baridi. Chunguza tu maisha yako ujue wakati wako wa baridi unafika lini na ni upi, kisha jitahidi sana, kuwekeza kwa Mungu sasa, kimaombi, kiusomaji Neno, na kiuinjilisti.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MCHE MWORORO.(Opens in a new browser tab)

Nini maana ya kikombe cha maji ya baridi(Mathayo 10:42)?

Je ni wakina nani ambao hawataonja mauti mpaka siku ya kuja Bwana?

(Opens in a new browser tab)Fahamu maana ya Mithali 25:13 Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno;(Opens in a new browser tab)

(Opens in a new browser tab)Rudi Nyumbani

Print this post

MAMBO SITA, AMBAYO MUNGU HUTUMIA KUONDOA UOVU NDANI YA MTU.

Nakusalimu katika jina kuu la mwokozi wetu Yesu Kristo, karibu katika kujifunza Neno la Mungu. Leo tutaona mambo Makuu sita (6), ambayo Mungu anatumia kuondoa uovu ndani ya mtu, na kumfanya awe mtakatifu kabisa kama yeye alivyo. Ikiwa wewe umemfuata Kristo basi tarajia mambo haya matano atayatumia katika maisha yako, kukukamilisha.

  1. Damu
  2. Maji
  3. Moto
  4. Fimbo
  5. Pepeto
  6. Dawa

Tukianza na

DAMU:

Kumbuka sisi sote tulizaliwa na deni la dhambi. Hivyo tulistahili hukumu ya mauti, (Warumi 6:23), Lakini deni hilo lilikuja kulipwa na Bwana wetu Yesu kwa kifo chake pale msalabani (Warumi 5:8). Kumwagika kwa damu yake, sote tumepokea “msamaha wa dhambi” bure kwa neema. Hakuna mwanadamu yoyote anayeweza kukubaliwa na Mungu, kwa uweza wake mwenyewe. Kwahiyo damu ya Yesu imekuwa hatua ya kwanza ya sisi kukubaliwa na Mungu.

Sasa tunaweza kupokea msamaha kweli, tukasemehewa, lakini dhambi bado ikawepo ndani yetu. Na hilo sio kusudu la Mungu atusemehe tu, halafu atuache tuendelee kuwa watumwa wa dhambi ndani kwa ndani. Si lengo la Mungu, hata mtu mwenye upendo wa dhati wa Yule aliyekosewa naye, anapoona amemsamehe, huwa hamwachi tena kesho arudie kosa lile lile ili, amsamehe, hapana, bali humwonyesha njia ya kuepuka makosa ili yeye mwenyewe aweze kusimama kwa ujasiri mbele zake. Na ndivyo ilivyo kwa Mungu mara baada ya kupokea msamaha wa dhambi, huyo mtu anaanza hatua ya utakaso wa Mungu ambao sasa hufanywa na Roho Mtakatifu aliyeingia ndani yake, Ndio hapo inakuja hatua ya pili,

NENO:

Biblia inasema Neno ni kama maji, ambayo yanasafisha.

Waefeso 5:26  ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno; 27  apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa.

Umeona, Kristo hulisafisha kanisa lake, kwa Neno, ndio maana wewe kama mtu uliyempokea Yesu, Ni lazima uwe na juhudu nyingi sana za kusoma Neno la Mungu kila siku, usikie maonyo, fundisho, agizo,  njia, (2Timotheo 3:16), Na kwa jinsi unavyojifunza sana, ndivyo unavyosafishwa moyo wako na roho yako, hatimaye unaanza kujiona mtu ambaye huna hatia ndani yako. Na hapo ndipo unapojikuta unaacha baadhi ya mambo uliyokuwa unafanya huko nyuma. Kumbuka biblia uliyonayo sio kitambulisho cha mkristo au pambo la mkoba, bali ni maji hayo ya kukusafisha, hivyo oga kila siku, uwe msafi. Kwasababu usipofanya hivyo utakuwa mchafu tu sikuzote.

MOTO:

Kwa kawaida sio kila uchafu hutoka kwa maji, mwingine huitaji moto ili kuundoa. Kwamfano ukiupata mwamba wenye dhahabu ndani yake ukipitisha maji huwezi toa uchafu uliogandamana nao,hivyo wale wafuaji, wanaupitisha kwenye moto, kisha unayeyuka na baada ya hapo uchafu na dhahabu hujitenga kisha wanaikusanya dhahabu. Ndivyo ilivyo na Mungu kwa watoto wake. Upo moto ambao wewe kama mwana wa Mungu ni lazima tu utapitishwa hata iweje, kuondoa mambo sugu yaliyogandamana na wewe yasiyoweza kutoka kwa Neno tu bali kwa hatua ya kimaisha, ndio huo unaoitwa “ubatizo wa moto”. Mfano wa huu ndio ule uliompata mfalme Nebukadreza (Danieli 4), kukaa miaka saba maporini kula majani ili tu aondolewe kiburi ndani yake. Ni aina Fulani ya maisha ambayo kwako yatakuwa kama moto, lakini mwisho wake hukuletea faida ya roho yako.

1Petro 1:6  Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali;7  ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo.

FIMBO:

Zipo tabia nyingine ambazo Mungu anaona mwanawe anakuwa nazo kwa ujinga tu, hivyo, ili kuundoa ujinga huo, haihitaji maji wala moto, bali kiboko. Anapoona unafanya jambo Fulani kwa makusudi na alishakukataza hapo awali fahamu pia kiboko kitapita juu yako.

Waebrania 12:6  Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, Naye humpiga kila mwana amkubaliye.

7  Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye?

8  Basi kama mkiwa hamna kurudiwa, ambako ni fungu la wote, ndipo mmekuwa wana wa haramu ninyi, wala si wana wa halali. 9  Na pamoja na hayo tulikuwa na baba zetu wa mwili walioturudi, nasi tukawastahi; basi si afadhali sana kujitia chini ya Baba wa roho zetu na kuishi?

10  Maana ni hakika, hao kwa siku chache waliturudi kama walivyoona vema wenyewe; bali yeye kwa faida yetu, ili tuushiriki utakatifu wake.

Biblia inasema pia..

Mithali 22:15 Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali.

PEPETO:

Yohana mbatizaji kwa uvuvio wa Roho aliandika maneno haya kuhusu  Bwana Yesu..

Mathayo 3:11  Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.

12  Ambaye pepeto lake li mkononi mwake, naye atausafisha sana uwanda wake; na kuikusanya ngano yake ghalani, bali makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.

Yesu akija kwako, fahamu kuwa mkononi ameshika pepeto pia, na wewe utawekwa juu yake, Anajua kabisa ulipo wewe makapi pia yapo, uliyotoka nayo huko shambani (ulimwenguni), hivyo ili kukutenga nayo, ataanza kukupepeta, kama vile ngano, utarushwa juu, utashushwa chini, utarushwa juu utashushwa chini, huwezi kuachwa utulie, lengo ni kuhakikisha makapi yote yanapeperushwa na upepo, iwe ni watu, vitu, utaona tu unapelekwa mbele, unarudishwa nyuma..baadaye akishaona ni ngano tu imebakia chini, hapo ndipo anapokuacha, unaanza kuona ushwari. Hii ilimkuta Ibrahimu, Bwana anamtoa Uru, anampeleka kaanani, mara anakimbilia Misri, mara anarudisha, lakini baadaye Mungu alimpa pumziko, baada ya kuona wote waliokuwa wameshikamana naye hawapo naye.

Usishangae kutokuwa na utulivu katika nyakati fulani za maisha yako wokovu, wakati Fulani unafanikiwa, halafu unarudi chini, wakati Fulani unapata amani kotekote, gafla inaondoka, unapata, ghafla tena unapoteza, tulia tu, kuwa na amani ndani ya Kristo, utakuwa tu, imara, wala hiyo misukosuko haitakuwepo tena, ni kwanini iwe hivyo? Ni kwasababu makapi yanapeperushwa na upepo.

DAWA:

Kaa ukifahamu Yesu anajulikana pia kama tabibu,(Marko 2:17) na anajua maovu mengine unayoyafanya yanatokana na magonjwa na majeraha ya rohoni, anajua hali yako ilivyo hivyo anachokifanya ni kukutibu yeye mwenyewe, ndio hapo unashangaa tu mwingine anatokwa na mapepo yaliyokuwa yanamsumbua na kumpelekea kutenda dhambi mwingine anapona udhaifu fulani, uliokuwa unamfanya amkosee Mungu, mwingine anapokea faraja, amani, utulivu usio wa kawaida, anashangaa kuona tofauti kubwa  ya sasa na hapo kabla. Hili nalo mtu aliyempokea Kristo ataliona kwenye maisha yake. Na atimaye anakuwa mwema yeye tu mwenyewe, asukumwi tena na presha ya dhambi fulani. Kwasababu tabibu mkuu ameshamponya, ambaye akikuweka huru, unakuwa huru kwelikweli.

Ufunuo 3:18

Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na DAWA ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.

Hivyo, wewe kama mwana wa Mungu, tambua yote hayo yatapita katika sehemu Fulani ya maisha yako. Usidhani kusafishwa tu na damu ya Yesu ndio basi, utatakaswa na hiyo ni katika maisha yako yote. Haiwezekani mtu aliyeokoka ambaye amepokea Roho maisha yake yote awe Yule Yule wa zamani, hizo sio kanuni za wokovu, wala sio kusudi la Mungu. Ukubali utakaso, au usiwe mkristo kabisa. Kwasababu hivi viwili huenda sambamba wala haviwezi kutenganishwa. Huo ndio upendo wa Mungu.

Utukufu na heshima ni vyake  milele na milele.

Bwana akubariki.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> hhttps://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

(Opens in a new browser tab)UTAKASO NI SEHEMU YA MAISHA YA MKRISTO YA KILA SIKU.

Ipi tofuati kati ya UTAKATIFU na UKAMILIFU?

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 21:30 Hapana hekima, wala ufahamu, Wala shauri,  juu ya Bwana.

SWALI: Nini maana ya Mithali 21:30 Hapana hekima, wala ufahamu, Wala shauri,  juu ya Bwana ?


JIBU: Mstari huo unaweza ukasemwa hivi; “Hapana hekima, wala ufahamu, wala shauri linaloweza kufanikiwa/kusimama kinyume na Mungu”.

Ikiwa na maana iwe ni mwanadamu au malaika, atumie uwezo wake wote, kufanya jambo la hila kinyume na yeye haliwezi kufichika kwasababu yeye ni mkuu zaidi ya vyote. Mpango wa shetani kuliharibu kanisa huawezi kufanikiwa hata azidishe kufanya kazi mara elfu zaidi ya mwanzo hilo haliwezekani kama lilivyoshindikana mbinguni.

Mambo yote yanayotokea hayafiki kwake ghafla tu bila hodi, kama ilivyo kwetu sisi wanadamu. Elimu ya darasani haiwezi pindua ukweli wake wa uungu, wajaposema mwanadamu ametokana na nyani, mwishoni wanarudia kule kule kwenye ukweli wa uumbaji wa kiungu, kwasababu atabakia kusimama kuwa Mungu wa daima, na ataabudiwa vizazi vyote haijalishi dunia itaelimika kiasi gani.

Mungu Anajua mawazo yetu yote tokea mbali, wewe kama mwanadamu huwezi mficha dhambi zako, ukajifanya  mbele zake umesahau, au ulikuwa hujui, hata utumie hekima nyingi kiasi gani kuficha ukweli bado anatambua nia ya mioyo yetu.

Anasema;

Zaburi 50:17 Maana wewe umechukia maonyo, Na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.  18 Ulipomwona mwivi ulikuwa radhi naye, Ukashirikiana na wazinzi.

19 Umekiachia kinywa chako kinene mabaya, Na ulimi wako watunga hila.  20 Umekaa na kumsengenya ndugu yako, Na mwana wa mama yako umemsingizia.

21 NDIVYO ULIVYOFANYA, NAMI NIKANYAMAZA; UKADHANI YA KUWA MIMI NI KAMA WEWE. Walakini nitakukemea; Nitayapanga hayo mbele ya macho yako.

22 Yafahamuni hayo, Ninyi mnaomsahau Mungu, Nisije nikawararueni, Asipatikane mwenye kuwaponya.

Pale tunapomwona Mungu ni kama sisi ndio unakuwa mwanzo wa kuto-mhofu  yeye. Unapokuwa na udhuru wa kuifanya kazi yake halafu unasingizia sina muda, lakini una muda wa kufanya mambo yako, ukidhani yeye hajui nia yako ya ndani, unajidanganya mwenyewe. Unapoepuka maombi, kwa kisingizio umechoka, na bado unataka Mungu akuhudumie, fahamu Mungu anakuelewa vizuri sana, atakuonyesha ambao wanachoka zaidi yako, lakini hawana udhuru. Jambo lolote tulifanyalo, tutambue kwanza kwa Mungu halifichiki.

Kwasababu Hapana hekima, wala ufahamu, wala shauri litakalosimama kinyume cha Mungu

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya Mithali 19:21Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.(Opens in a new browser tab)

Je shauri la kuipepeleza Kanaani lilitoka kwa wana wa Israeli au kwa BWANA?(Opens in a new browser tab)

Tofauti kati ya Hekima, ufahamu na maarifa, ni ipi?

(Opens in a new browser tab)Maana ya Mithali 11:17 Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 21:17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini;

SWALI: Nini maana ya  Mithali 21:17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini; Apendaye mvinyo na mafuta hatakuwa tajiri.


JIBU: Mstari huo unamaana mbili.

Maana ya kwanza ni ya mwilini, ni ukweli watu wanaopenda maisha ya anasa, mwisho wao huwa ni kutofanikiwa. Kwasababu kile wanachokipata ambacho kingepaswa kiwekwe akiba kwa wakati wa baadaye au kiwekezwe kizalishe zaidi, wao hutumia chote katika starehe mfano wa pombe, uasherati, na kununua vitu vya gharama kubwa, lengo tu asionekane amepitwa na wakati, au aonekane wa kisasa.

Hapo anaposema apendaye mvinyo na mafuta, hayo mafuta yanayozungumziwa hapo ni marashi ya gharama ambayo zamani waliokuwa wananunua ni matajiri. Ni sawa na leo labda mwajiriwa analipwa mshahara wa laki tatu (3) kwa mwezi, halafu anakwenda kununua perfume (marashi), ya  laki 2, ili tu aonekane wa kisasa, hiyo ni anasa, na mwisho wake ni umaskini.

Anasa ni tunda la majivuno, na kukosa adabu. Hivyo biblia inamfundisha mwanadamu yoyote kuwa, anasa ni kinyume cha mafanikio.

Lakini pia rohoni, anasa ni zao la ufukara wa ki-Mungu. Mtu wa anasa, hutumia muda wake vibaya, kwasababu nyakati zake za ziada huishia kwenye starehe za kimwili na sio kwenye mambo ki-Mungu.

Bwana alisema;

Luka 8:14  Na zilizoanguka penye miiba ni wale waliosikia, na katika kuenenda kwao husongwa na shughuli na mali, na anasa za maisha haya, wasiivishe lo lote.

Umeona? Anasa husonga mbegu ya Mungu ndani yako.

Katika kizazi cha sasa anasa ni pamoja na kushinda kwenye tv kutazama muvi kila kukicha, ni pamoja na kushinda mitandaoni kufuatilia vipindi vinavyokupa raha za kimwili na kihisia lakini havikujengi rohoni,  ni kuwekeza muda wako katika matanuzi ya mijini na kwenye sherehe-sherehe za kila mara ambazo hazina mpangalio. Muda wote akili yako ipo katika kile kitu wanachosema “ku-party weekend” na marafiki. Ushikapo simu yako, usiku wote ni kuchat, na wale wanaowaita ma-boyfriend na ma-girlfriend. Muda ambao ungepaswa kusoma Neno na kuomba.

Sasa ikiwa wewe umeokoka, na una mwenendo huo wa maisha, usitazamie hapo utazalisha kitu. Utabakia kuwa Yule Yule milele. Biblia inasema ni heri kuona kwa macho kuliko kutangatanga kwa tamaa(Mhubiri 6:9). Sio kila taarifa uifuatilie, sio kila kitu ukitende, viache vingine vikupite, ili upate nafasi ya kuwa karibu na Mungu wako, uwe mtu wa matunda. Komboa wakati.

Shalom..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa.

(Opens in a new browser tab)APENDAYE FEDHA HASHIBI FEDHA.

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 4)(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

MAMBO NANE (8), AMBAYO WEWE KAMA KIONGOZI UTAIGWA.

Uwapo katika nafasi yoyote ya uongozi, katika kanisa au kwenye huduma, labda mchungaji, mwalimu, mtume, nabii, shemasi, askofu, mzee wa kanisa. Na una watu walio chini yako, fahamu mambo ambayo utaigwa, Na hivyo kuwa makini sana katika maeneo hayo uyajenge.

Mtume Paulo aliyaona kwa mwanawe Timotheo, akayaandika;

2 Timotheo 3:10-11

[10]BALI WEWE UMEYAFUATA mafundisho yangu, na mwenendo wangu, na makusudi yangu, na imani, na uvumilivu, 

[11]na upendo, na saburi; tena na adha zangu na mateso, mambo yaliyonipata katika Antiokia, katika Ikonio, na katika Listra, kila namna ya adha niliyoistahimili, naye Bwana aliniokoa katika hayo yote. 

Paulo ametaja mambo saba ambayo Timotheo aliyaona kwake akayaiga, ni kama yafuatayo;.

la kwanza ni 

1) Mafundisho yake:

Wewe kama kiongozi kumbuka unachofundisha ndicho watakachofundisha wafuasi wako, ikiwa injili yako ni ya mafanikio, hicho hicho watakifuata na kukifundisha, ikiwa ni mafundisho ya wokovu watakifundisha hicho hicho, ikiwa ni shuhuda za wachawi nao pia watakuwa nazo hizo hizo kama kiini cha injili yao. Hivyo kuwa makini na fundisho lako vinginevyo utajikuta  unapotosha jamii yako ya waaminio, na utatoa hesabu juu ya hilo, mbele za Bwana siku ile.

2) Mwenendo wake:

Ukiwa ni mtu wa kidunia, usitazamie utazaa watu wa rohoni, uvaaji wako, unawafundisha wafuasi wako, kauli zako zitazungumzwa hizo hizo na washirika wako, ukiwa na tabia ya maombi, wanaokufuata nao pia wataiga mwenendo huo wa maombi, ukiwa ni mtakatifu nao pia watakuwa hivyo hivyo. Jichunge mwenendo wako, wewe ni kioo unaigwa mpaka hatua zako. Hivyo usifanye mambo kiwepesi wepesi, ukidhani wote wamekomaa wanaweza kujiamulia tu mienendo bila kukuangalia wewe. Liondoe hilo kichwani.

3) Makusudio yake:

Makusudi ya mtume Paulo, yalikuwa ni kuhubiri injili kwa mataifa kotekote wamjue Mungu (2Wakorintho 1:15-20). Hakuwa na kusudio la umaarufu, fedha, kuheshimiwa na wanadamu, hapana, bali kuhubiri injili tu peke yake, bila kujali dhiki, au kupungukiwa, ilimradi watu waokoke. Hivyo Timotheo naye alipoliona kusudi hilo akaiga, naye pia akawa mhubiri tu wa injili, asiyetafuta vya kwake ndani ya kazi ya Mungu. Halidhalika na wewe pia, nia yako hutakumbulikana mahali ulipo, Je! Unachokifanya ni injili ya Mungu kweli au una lengo lingine. Ikiwa ni Yesu wa mikate, basi ujue watu wako pia watakuwa hapo kumtafuta Mungu huyo huyo wa kwako. Kuwa na kusudi la Kristo ambalo aliliweka pia ndani ya mitume wake, yaani kulitumikia na kulichunga kundi, kama mtendakazi asiyekuwa na faida. Ukijua kuwa thawabu yako ipo mbinguni, usiwe na makusudio mengine, kwasababu wewe ni kioo.

4) Imani yake:

Imani, katika mambo yote, wewe kama kiongozi ukiwa ni mtu wa mashaka juu ya mambo ya rohoni.  Ikiwa huamini uponyaji wa ki-ungu, na wale pia watakuwa hivyo hivyo, huamini miujiza, na karama za Roho, vivyo hivyo na washirika wako watakuiga, ikiwa huamini katika mifungo, ikiwa huamini kuwa duniani kuna watakatifu, au mtu hawezi kuwa mtakatifu, vivyo hivyo watu wako nao watakuwa hivyo, Ikiwa unaamini katika ibada za sanamu, watakuwa kama wewe.  Jenga imani yako kwenye neno la Mungu tu, kuwa mtu wa imani usiwe Sadukayo. Fahamu kuwa mtumishi wa Mungu tafsiri yake ni kuwa mtu wa Imani.

5) Uvumilivu wake:

Kama kiongozi ni ukweli usiopingika utapitia vipindi mbalimbali vya kushinda na kushindwa, vipindi vya kukatishwa tamaa, kusemwa vibaya,  vipindi vya kuachwa peke yako n.k. Mtume Paulo alipitia vipindi vyote, na wanafunzi wake wakawa wanamwangalia, wakaiga mwenendo ule walipoona mafanikio yake yalipotanguliwa na vipindi vingi vya kuvunjwa moyo lakini akastahimili. Hivyo na wewe pia kama kiongozi wa wengine, simama imara, uvumilivu wako ni funzo kubwa kwa wengine. Wakati mwingine Mungu anaruhusu uyapitie hayo ili kuwaimarisha wengine katika dhiki zao, wakuonapo wewe unasimama katika changamoto, na wao pia hupokea nguvu ya kushindana na changamoto zao.

6) Upendo wake:

Kama kiongozi, upendo ni sehemu, kubwa sana, ambalo mtume Paulo alifanya bidii kulionyesha kwa wanafunzi wake na kanisa.  Unapolipenda kundi lako, vivyo hivyo na wale wataiga tabia hiyo na kuidhihirisha kwa wengine. Unapoonyesha chuki, nao pia watakuwa watu wa chuki, unapowajali nao pia watawajali wengine. Unapowasikiliza, tafsiri yake ni kuwa unawafundisha kuwasikiliza na wengine. Hivyo ni kuangalia sana na kuongeza bidii katika eneo hilo, uwe kielelezo.

7) Saburi yake:

Saburi ni kitendo cha kungojea ahadi za Mungu hata katika mambo magumu yanayokinzana na wewe, bado unasubiria tu. Kama kiongozi watu watatazamia jinsi unavyoyashikilia maono yako, bila kuyumbishwa, waige, na wenyewe kushikilia ya kwao. Kamwe usiwe mtu wa kusita-sita, utawavunja moyo wengi, na hatimaye watashindwa kusimama aidha pamoja na wewe, au wao wenyewe. Ijenge saburi yako, wala usiidharau, ni nguvu kwa mwingine aliye chini yako. Leo unaona jinsi gani saburi ya Ayubu ilivyo na fundisho kubwa kwetu. Vivyo hivyo na yako ujue ni darasa kwa wengine.

8) Adha na mateso yake:

Ukweli ni kwamba watu watatamani kusikia ushuhuda wa mapito yako au kuyaona mapito yako hususani yale magumu sana. Lakini waweza kudhani, haliwafahi sana kiroho, lakini wengine pia wakaiiga njia hiyo ya mateso kama yako, kwasababu wameona mwisho wake ulivyo mzuri. Hivyo usiogope kupitia mateso kwa ajili ya Bwana wala usione haya wakati mwingine kueleza shida ulizopitia kwa wengine, hilo nalo huigwa, Leo hii tunaposoma mapito ya mtume Paulo ni wazi kuwa yanatutia nguvu na sisi, kuwa tusonge mbele.

Hivyo, zingatia mambo hayo saba, kwa faida yako na wale walio chini yako. Kwasababu ndicho Paulo alichokiona kwa watoto wake.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

Fahamu maana ya Mithali 29:4 “Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.

IMANI “MAMA” NI IPI?

Bwana alimaanisha nini kusema “Mwanafunzi hawi mkuu kuliko mwalimu wake”?

Rudi Nyumbani

Print this post

Fahamu maana ya Mithali 18:22 Apataye mke apata kitu chema

SWALI: Je andiko hili humaanisha nini? kupata mke ni kujipatia kibali cha kumkaribia Mungu tofauti na  hapo mwanzo?

Mithali 18:22

Apataye mke apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa BWANA. 

JIBU: Andiko hili hutafsiriwa vibaya na watu wengi, wakiamini kuwa pale mtu anapoingia kwenye ndoa basi ndio amejizidishia kibali cha kukubaliwa na Mungu katika maisha yake. Jibu ni hapana, kibali kwa Mungu sio ndoa, kibali kwa Mungu ni “kufanya vema mapenzi ya Mungu” .

Mungu alimwambia kaini maneno haya

Mwanzo 4:7

[7]Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde. 

Zaidi pia, maandiko yanaeleza ipo nafasi kubwa kwa mtu  kumkaribia Mungu anapokuwa hajaoa/kuolewa kuliko yule aliyeoa au kuolewa.Kwasababu ambaye hajaoa/ olewa hupata nafasi ya kutosha kumtafuta Bwana na kumfikiria yeye ampendezeje.

1 Wakorintho 7:32-33

[32]Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana; 

[33]bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe. 

Lakini je! andiko hilo humaanisha kibali gani?

“Apataye mke apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa BWANA”. 

Tafsiri ya Neno hilo ni kuwa Mungu analikubali jambo hilo(Ndoa), analibariki, na pia analiona ni jema. Hivyo mtu asidhani kuwa aingiapo katika ndoa atamkosea Mungu, au Mungu atapunguza ukaribu naye. Hapana, kinyume chake atapata kibali tu. Hivyo awe na furaha na amani afanyavyo hivyo.

Makala Yanayofadhiliwa Tafuta kitu kwa kila mtu katika mkusanyiko wetu wa soksi za rangi, http://www.swisswatch.is best replica watches angavu na maridadi. Nunua kibinafsi au kwa vifurushi ili kuongeza rangi kwenye droo yako!

kwasababu pia zipo faida zinazoambata na mtu aliyeoa, mojawapo ni kujiongezea heshima kwa jamii lakini pia kuaminiwa zaidi. Na hilo ni jema husasani katika utumishi & huduma.

Lakini haimaanishi kuwa unapooa ndio Mungu anakukubali zaidi ya ule wakati ambao ulikuwa hujaoa/kuoelewa, au zaidi ya yule mtu ambaye hafikirii kuoa.

Mtume Paulo, Barnaba hawakuoa na zaidi mwokozi wetu Yesu Kristo hakuoa lakini tunaona ni jinsi gani walivyojirahisishia nafasi zao  kwa Mungu. 

kwa mafundisho zaidi kuhusu ndoa pitia masomo chini;

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAFUNDISHO YA NDOA.

MWANAMKE UKITAKA KIBALI, USIWE MTU WA KUPENDA VITU. (Esta 2:17)

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Fahamu maana ya Mithali 10:5 Akusanyaye wakati wa hari ni mwana mwenye hekima; 

SWALI: Nini maana ya;

Mithali 10:5 Akusanyaye wakati wa hari ni mwana mwenye hekima; Bali asinziaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha. 

JIBU: Kwa kawaida kipindi cha hari ( kiangazi), huwa ndio kipindi cha mavuno mengi. kwasababu mavuno yanakuwa yameshakomaa na kukauka.

Hivyo wakulima wengi kwa nyakati hizo wanakuwa mashambani kuvuna, kama vile tu walivyokuwa wakati wa masika walipokuwa wanapanda..

Na ni kipindi ambacho mkulima hufurahi pia kwasababu anakwenda kuona matunda ya kazi yake wakati si mwingi.

Lakini ni ajabu kuona, mtu ambaye hajasumbukia kupanda, halafu anaambiwa tu yeye akavune, tena kwa faida yake mwenyewe akauze, anaona uvivu kwenda kuvuna, hataki kabisa kwenda kujishughulisha na kazi hiyo, mpaka msimu mwingine unakuja, mazao yanaharibikia yote shambani. Mtu kama huyo utamchukuliaje? Ni sawa tu akiitwa  “mwana mwenye kuaibisha”, Kwasasababu ni uvivu wa makusudi.

Sasa jambo kama hili kwasasa lipo pia rohoni.

Na lipo kwa namna mbili.

1.) Katika kazi ya Mungu.

Bwana Yesu alisema..

Yohana 4:35-38

[35]Hamsemi ninyi, Bado miezi minne, ndipo yaja mavuno? Tazama, mimi nawaambieni, Inueni macho yenu myatazame mashamba, ya kuwa yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno. 

[36]Naye avunaye hupokea mshahara, na kukusanya matunda kwa uzima wa milele, ili yeye apandaye na yeye avunaye wapate kufurahi pamoja. 

[37]Kwa maana hapo neno hilo huwa kweli, Mmoja hupanda akavuna mwingine. 

[38]Mimi naliwatuma myavune yale msiyoyataabikia; wengine walitaabika, nanyi mmeingia katika taabu yao. 

Umeona? Kufuatana na vifungu hivyo Bwana anatuonyesha kuwa tupo wakati wa mavuno sasa, wakati wa hari, wa kiangazi, mashamba yamekwisha kuwa meupe,  Hivyo sote kwa pamoja kwa moyo mmoja yatupasa tutoke tuanze kuifanya kazi ya Mungu bila ulegevu kwasababu Yesu alishatupa agizo kuu kuwa tutoke tuenende ulimwenguni kote kuwafanya mataifa kuwa wanafunzi.

Lakini ukilala na kusema huu si wakati, ndugu ni sawasawa na hilo neno unakuwa mwana mwenye kuaibisha. Kila mmoja wetu ameitwa kuwahubiria wengine habari njema za wokovu wa Yesu Kristo, haijalishi upo ofisini, shuleni, ugenini, jeshini, una wajibu wa kuvuna. Shika mundu yako washuhudie wengine habari njema, kwasababu huu ni wakati  sahihi, na hautadumu milele.Hivyo tumia muda vizuri.

2) Katika kipindi cha maisha ulichopo.

Neno la Mungu linasema..

Mhubiri 12:1

[1]Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya,  Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo. 

na pia linasema..

1 Yohana 2:14

[14]Nimewaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.

Katika umri wako wa ujana ambao una nguvu ndio wakati wa kwenda shambani kumtumikia Bwana wako. ndio wakati wako wa hari, lakini unapokuwa mlegevu, hujishughulishi na Mungu wako, unachowaza ni anasa, starehe, mihangaiko, unasema nitamtumikia Mungu uzeeni, fahamu kuwa wewe ni sawa na mwana mwenye kuaibisha, kwasababu wakati huo utakuwa umeshapita.

Komboa wakati wako, thamini majira uliyopo, etende kazi ya Bwana.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

Maana ya Mithali 25:25 Kama vile maji ya baridi kwa mtu mwenye kiu 

Nini maana ya Mithali 16:30 Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka;

Rudi Nyumbani

Print this post

Hadhari ni nini kibiblia? (Mithali 1:4)

Hadhari ni nomino ya kitenzi tahadhari. Neno Lenye maana ya “uangalifu”.

>Kwamfano mwalimu anayesahisha mitihani ya wanafunzi tunasema huwa na hadhari kubwa katika usahishaji.

  • Kula bila hadhari ya usafi huweza sababisha magonjwa.

Katika biblia neno hili utalisoma kwenye vifungu hivi;

Danieli  2:13 Basi ile amri ikatangazwa, na hao wenye hekima walikuwa karibu na kuuawa; watu wakamtafuta Danielii na wenzake ili wauawe.  14 Ndipo Danieli kwa busara na HADHARI akamjibu Arioko, akida wa walinzi wa mfalme, aliyekuwa ametoka ili kuwaua wenye hekima wa Babeli;  15 alijibu, akamwambia Arioko, akida wa walinzi wa mfalme, Mbona amri hii ya mfalme ina ukali namna hii? Ndipo Arioko akamwarifu Danielii habari ile

Mithali 1: 1 Mithali za Sulemani, mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli.  2 Kujua hekima na adabu; kutambua maneno ya ufahamu;  3 kufundishwa matendo ya busara, katika haki na hukumu na adili.  4 Kuwapa wajinga werevu, na kijana maarifa na HADHARI;

Yoshua 22:24 au kama sisi tumefanya jambo hili kwa HADHARI sana, tena makusudi, huku tukisema, Katika siku zijazo wana wenu yamkini wakanena na wana wetu, na kusema, Ninyi mna nini na Bwana, yeye Mungu wa Israeli?

Sisi pia kama watakatifu, tuwe na hadhari, katika maisha ya ulimwenguni. Tunaishi ulimwenguni lakini hatupaswi kufungwa nira na huo kwa jinsi isivyo sawasawa. Kwasababu watu wanaokosa jambo hili husongwa na anasa, udanganyifu wa mali na shughuli za ulimwengu huu, na tamaa ya mambo mengine hatimaye hawazalishi kitu.

Shalom.

Je! Umeokoka? Unatamani leo kupokea msamaha wa dhambi? Ikiwa jibu ni ndio basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya kumkaribisha Yesu moyoni mwako.>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Akida ni nani kibiblia, na kazi yake ni ipi? (Mathayo 8:5)

NGUVU YA HEKIMA NA AKILI

AGANO LA MOYO LENYE NGUVU

JE! WEWE NI MWANA WA IBRAHIMU?

Rudi Nyumbani

Print this post

Adabu ni nini biblia?

Adabu, ni kitendo cha kuonyesha staha, kufuata miiko, kuonyeshaAdabu ni nini biblia? ustaarabu mzuri kwa wengine.

Adabu huonyeshwa kwa Mungu, lakini pia kwa wanadamu.

Adabu kwa Mungu.

> Ni pamoja na mwonekano wako uwapo ibadani.

Yesu alipomwona Petro akiwa uchi alijivika vazi lake kwasababu alitambua anahitaji kuonyesha adabu kwa Mungu wake. (Yohana 21:7).

 >Ni pamoja na kuwa mtulivu: Uwapo ibadani, mazungumzo ya ovyo, yasiyo ya kiibada yaepuke, minong’ono madhabahuni kwa Mungu acha, kuchati, mizunguko zunguko, kutafuna tafutana.havihitajiki,

Adabu kwa wanadamu:

>Ni pamoja na Kuwasalimia wengine. Yesu alisema.

Mathayo 5:47  Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo? 48  Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.

>Vilevile ni pamoja na kuwasikiliza wengine, kuzuia kinywa chako kunena zaidi ya wastani (Kiasi), kuonyesha upole, kuonyesha kujali, kuonyesha maadili, na kutojishughulisha na mambo ya wengine.

Maandiko yanatufundisha tunda mojawapo la upendo ni adabu.

1Wakorintho 13:4  Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; 5  HAUKOSI KUWA NA ADABU; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya.

>Vilevile Imetoa agizo kwa wanawake wacha Mungu,kwamba pambo lao mojawapo liwe ni adabu nzuri (1Timotheo 2:9). Ambapo huusisha pia Uvaaji wako kilemba uwapo ibadani ni adabu kwa Mungu wako kwasababu maandiko yameagiza hivyo. (1Wakorintho 11:5). Kujisitiri kwako ni adabu pia.

Lakini zaidi sana imetoa  agizo kwa watawakatifu wote, tuenende kwa adabu kwa wale walio nje (1Wathesalonike 4:12).

Hivyo, sote kwa pamoja tuipe adabu nafasi maishani mwetu,ili tujengwe.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima; (Mithali 11:16)

Chamchela ni nini kwenye biblia?(Zaburi 58:9, Amosi 1:14)

UMETEKWA NA UPENDO WA KRISTO?

Rudi Nyumbani

Print this post

Heshima ni nini kibiblia?

Heshima ni kitendo cha kumpa mtu hadhi yake, au uthamani wake anaostahili. Kwa kawaida kila mwanadamu anastahili heshima. Na hivyo kama mwamini huna budi kujua jinsi ya kuigawanya heshima kulingana na mtu husika. Kwasababu ukosefu wa heshimu, kwanza ni zao la kiburi (Mithali 15:33), lakini pia hukuondolea Baraka na kibali  popote pale uendapo. Lakini pia ukitoa heshima isiyompa mtu ni kosa pia.

Warumi 13:7  Wapeni wote haki zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahiliye hofu, hofu; astahiliye heshima, heshima

Heshima kwa Mungu ipo wapi?

  1. Ipo katika kuliamini na kuliishi Neno lake: Si katika kulipamba jina lake, na huku hufanyi anayokuambia. Alisema. Luka 6:46  Na kwa nini mnaniita, Bwana, Bwana, walakini hamyatendi nisemayo? 47  Kila mtu ajaye kwangu, na kuyasikia maneno yangu na kuyatenda, nitawaonyesha mfano wake.
  2. Ipo katika uaminifu katika  utoaji: Mithali 3:9 Mheshimu Bwana kwa mali yako, Na kwa malimbuko ya mazao yako yote
  3. Ipo katika ibada :  Anayestahili kuabudiwa, kusujudiwa, kupigiwa magoti, kuhimidiwa ni Mungu tu peke yake, na wala si mwanadamu au kiumbe kingine pamoja naye, heshima hii inamuhusu yeye peke yake. Ufunuo 4:11 “ Umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo vikaumbwa”

Heshima kwa Wazazi ipo wapi?

  1. Kuwasaidia. Biblia inasema kuwaheshimu wazazi ni pamoja na kuwasaidia kimahitaji (Mathayo 15:1-7)
  2. Kuwasikiliza na kushika maagizo yao: Mithali 1: 8 Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,

Heshima kwa Viongozi wako wa kiroho ipo wapi?

Kutii maelekezo yao.

Waebrania 13:17  Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.

Heshima kwa watoto ipo wapi?.

Kutowakwaza,

Waefeso 6:4  Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana.

Heshima kwa Viongozi wa nchi.

Kutenda agizo lao.

Warumi 13:1  Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu. 2  Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu

Heshima kwa Mabwana ipo wapi?

Kuwatumikia kwa uaminifu na adabu. (Waefeso 6:5-8)

Hivyo kwa hitimisho, ni kwamba kila mwanadamu anastahili heshima, haijalishi, tajiri, au maskini, mrefu au mfupi, mgonjwa au mzima, mwenye elimu au asiye na elimu, bwana au mtumwa, ameokoka au hajaokoka. Wote ni agizo tuheshimiane.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?

CHUJIO HILI NI LA AJABU SANA!

JIWE LILILO HAI.

Rudi Nyumbani

Print this post