SWALI: Naomba kufahamu maana ya 1Wakorintho 15:24-25 , hususani hapo anaposema ‘hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake. 26 Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti’.
1Wakorintho 15:24 Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu. 25 Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake. 26 Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti.
1Wakorintho 15:24 Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu.
25 Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake.
26 Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti.
JIBU: Bwana Yesu alikuja duniani kwa kazi maalumu ya kumkomboa mwanadamu pamoja na kumkamilisha. Na ukombozi huu, aliukamilisha wote siku ile pale msalabani kwa kifo chake. Hivyo tangu wakati ule mwanadamu ambaye atampokea, tayari maadui zake wote wamewekwa chini yake, ikiwemo na mauti yenyewe.
Lakini pia ni muhimu kufahamu, ukamilifu wa ukombozi wetu, sio sasa, kwasababu ijapokuwa tumeokolewa na ndani yetu tuna uzima wa milele, bado tutakufa (ki-mwili), bado tutaugua, bado tutazeeka, bado tutakula kwa taabu, bado tutapitia dhiki na masumbufu, bado tutakutana na uovu kila mahali tuendapo.
Hivyo ‘ukamilifu’ wetu kabisa kabisa bado. Lakini ‘ukombozi’ wetu tayari, tunaokoka tukiwa hapa hapa duniani, tukifa tunakuwa tunaishi. Sasa Ndio maana Yesu alikuja mara ya kwanza kama MWANAKONDOO achukuaye dhambi za ulimwengu, lakini pia atarudi mara ya pili, ambapo safari hii atakuja kama MFALME, Atawalaye kwa mamlaka na nguvu nyingi.
Safari hii atakuja sasa kwa ajili ya huo ukamilifu, kwanza atayahukumu mataifa na falme zao,(Mathayo 25:31-46) vilevile mapepo (Ufunuo 19:20), kisha ataurekebisha huu ulimwengu ulioharibika,(Ufunuo 6:12-17) na kuufanya kuwa zaidi hata ya edeni. Kisha atatawala na watakatifu wake, kwa kipindi cha miaka elfu moja (Ndio ule utawala wa amani wa Kristo wa miaka 1000), Ufunuo 20, hapa hapa duniani, kwa wakati huo dhiki nyingi sana zitaondoka, watu wataishi muda mrefu sana, biblia inasema mtu atakayekufa na miaka mia ataitwa mtoto mchanga,(Isaya 65:20) wanyama hawatakuwa wakali tena, , hakutakuwa na laana ya nchi kutoa miiba, wala kuzaa kwa uchungu. Hichi ni kipindi ambacho dunia itakuwa salama na tulivu sana. Ni wakati wa Raha ambao Yesu amewaandalia watumishi wake.
Lakini wapo baaadhi watakufa (lakini sio sisi tutakaonyakuliwa), kwasababu shetani alikuwa bado hajahukumiwa amefungwa tu, hicho ndio kipindi ambacho Kristo atakwenda kutokomoza mauti ya mwili, hivyo shetani atafunguliwa kwa muda, ajaribu kuwaangusha watakatifu, atashindwa na kutupwa kwenye ziwa la moto pamoja na watu wote waovu (Ufunuo 20:7-10). Hapo ndipo mwisho wa yote, hakuna tena mauti, wala kifo, wala uchungu, wala huzuni,. Yesu atayakamilisha yote, ambapo adui wa mwisho ndio huyo mauti ya mwili.
Ufunuo 21:1 Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena. 2 Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe. 3 Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. 4 Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita. 5 Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli. 6 Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure
Ufunuo 21:1 Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.
2 Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe.
3 Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.
4 Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.
5 Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli.
6 Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure
Wakati huo ndio Kristo atakuwa ameikamilisha kazi yake yote, na kumrudishia Baba ufalme wote, kama ilivyokuwa kule mwanzo, ili tumwabudu Mungu, sio katika kukombolewa, au kuchungwa, au katika kuongozwa tena, katika ile mbingu mpya na nchi mpya, Huduma ya Kristo itakuwa imeisha.
Yatakuwa makao yetu milele. Mambo ambayo tumeandaliwa huko ndugu, jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia. Unasubiri nini leo usimpe Bwana maisha yako? Kumbuka tunaishi katika nyakati ambazo Kristo amekaribia sana kurudi. Moja ya hizi siku parapanda italia, tutakwenda mbinguni. Tubu dhambi zako, mwamini Yesu, upokee uzima wa milele.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
KWANINI KUWE NA UTAWALA WA MIAKA 1000
SIFA SITA (6), ZINAZOIKAMILISHA ILE SIKU YA BWANA ITISHAYO.
ILI TUONEKANE WAKAMILIFU MBELE ZA MUNGU.
Rudi Nyumbani
Print this post
Zaburi 42:7
[7]Kilindi chapigia kelele kilindi kwa sauti ya maboromoko ya maji yako, Gharika zako zote na mawimbi yako yote yamepita juu yangu.
Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tutafakari pamoja Neno la Mungu.
Biblia inatuambia kila jambo tunalolifanya lina matokeo sawa rohoni. Ikiwa wewe ni mwizi malipo ya wizi utayapata rohoni, ikiwa wewe ni muuaji, malipo ya uuwaji utayapokea vilevile rohoni, mito ya maji inapoelekea huko huko ndipo inaporudia.
Ufunuo 13:10
Mtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hapa ndipo penye subira na imani ya watakatifu.
Sasa hapo tumeona katika eneo la ubaya, je vipi katika upande wa Mema?
Maandiko hayo hayo yanatuambia kwamba Kilindi hupigia kelele kilindi.
maana yake ni nini?
kilindi ni mahali pa katikati kabisa mwa bahari. Sasa mwandishi wa zaburi anatumia mifano ya kitu halisi kana kwamba kinaongea… anasema Kinaita chapigia kelele kilindi. Na cha kushangaza ni kwamba hakiiti eneo lingine lolote la maji labda ufukweni.. au kwenye rasi, au ghuba.. hapana bali kinapigia kelele kilindi chenzake.
Kilindi chapigia kelele kilindi
Maana yake ni nini?
Tukitaka mambo ya ndani ya Mungu, mambo ya vilindini, lazima na sisi tuwe vilindini. Ni muunganiko wa ki-Mungu. kila kiwango kina sauti yake. kamwe hizo sauti haziingiliani, ni sawa na mbwa amwite tai kwa sauti yake ya kubweka, haiwezekani kuja inahitaji, ajifunze sauti yake ili yule tai aelewe, vinginevyo atakuwa anapiga kelele tu.
Na sisi vivyo hivyo kwa Mungu, wengi tunatamani tumwone Mungu kwa undani katika maisha yetu, lakini hatutaki tuzame ndani yake.
Mwandishi wa Zaburi mwanzoni kabisa kabla hajasema maneno hayo kwenye hiyo sura 42 anasema
Zaburi 42:2-3
[2]Nafsi yangu inamwonea kiu MUNGU, Mungu aliye hai, Lini nitakapokuja nionekane mbele za Mungu? [3]Machozi yangu yamekuwa chakula changu mchana na usiku, Pindi wanaponiambia mchana kutwa, Yuko wapi Mungu wako.
[2]Nafsi yangu inamwonea kiu MUNGU, Mungu aliye hai, Lini nitakapokuja nionekane mbele za Mungu?
[3]Machozi yangu yamekuwa chakula changu mchana na usiku, Pindi wanaponiambia mchana kutwa, Yuko wapi Mungu wako.
Kuonyesha ni mtu ambaye alimtamani sana Mungu wake.
Sehemu nyingine Daudi anasema..
Zaburi 63:1-8
[1]Ee MUNGU, Mungu wangu, nitakutafuta mapema, Nafsi yangu inakuonea kiu, Mwili wangu wakuonea shauku, Katika nchi kame na uchovu, isiyo na maji. [2]Ndivyo nilivyokutazama katika patakatifu, Nizione nguvu zako na utukufu wako. [3]Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai; Midomo yangu itakusifu. [4]Ndivyo nitakavyokubariki maadamu ni hai; Kwa jina lako nitaiinua mikono yangu. [5]Nafsi yangu itakinai kama kushiba mafuta na vinono; Kinywa changu kitakusifu kwa midomo ya furaha. [6]Ninapokukumbuka kitandani mwangu, Nakutafakari Wewe makesha yote ya usiku. [7]Maana Wewe umekuwa msaada wangu, Na uvulini mwa mbawa zako nitashangilia. [8]Nafsi yangu inakuandama sana; Mkono wako wa kuume unanitegemeza.
[1]Ee MUNGU, Mungu wangu, nitakutafuta mapema,
Nafsi yangu inakuonea kiu, Mwili wangu wakuonea shauku, Katika nchi kame na uchovu, isiyo na maji.
[2]Ndivyo nilivyokutazama katika patakatifu, Nizione nguvu zako na utukufu wako.
[3]Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai; Midomo yangu itakusifu.
[4]Ndivyo nitakavyokubariki maadamu ni hai; Kwa jina lako nitaiinua mikono yangu.
[5]Nafsi yangu itakinai kama kushiba mafuta na vinono; Kinywa changu kitakusifu kwa midomo ya furaha.
[6]Ninapokukumbuka kitandani mwangu, Nakutafakari Wewe makesha yote ya usiku.
[7]Maana Wewe umekuwa msaada wangu, Na uvulini mwa mbawa zako nitashangilia.
[8]Nafsi yangu inakuandama sana; Mkono wako wa kuume unanitegemeza.
Umeona, usiku kucha, anamtafakari Mungu, kuonyesha ni mtu ambaye moyo wake upo kwa Mungu asilimia mia..unategemea vipi mtu kama huyo Mungu asijifunue kwake kwa viwango vile?
Nafasi hii pia mimi na wewe tunayo. Tumfuate Mungu wetu vilindini, ili ajifunue kwetu katika viwango vingine..
Na hiyo inakuja kwa kile Bwana Yesu alichosema..Tujitwike misalaba yetu tumfuate, tuwe tayari kuacha vyote visivyompendeza yeye na kumtii. Na kwa kufanya hivyo rohoni tunatafsirika kuwa tunamwita Mungu wa vilindini.
Anza sasa.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
WAKINYAMAZA HAWA, MAWE YATAPIGA KELELE.
Ni kelele gani zinazozungumziwa hapo katika Waefeso 4:31.
NIONDOLEENI KELELE ZA NYIMBO ZENU (Amosi 5:23)
Nini maana ya Mithali 9:13 Mwanamke mpumbavu hupiga kelele, Ni mjinga, hajui kitu?
Katika mapokeo ya kikristo, moja ya eneo ambalo limezuia mikanganyiko mingi, ni eneo hili linalohusiana na “Uungu wa Mungu” . Migawanyiko ya madhehebu mengi unayoyaona sasa chimbuko kubwa hasaa ni hapa.
Wapo wanaoamini Mungu ni mmoja amegawanyika katika nafsi tatu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu), lakini wapo wanaoamini Mungu ni mmoja mwenye nafsi moja (Hajagawanyika), yaani Yesu ni Yule Yule Yehova aliyekuwa zamani zile, wengine hawaamini kabisa kama Yesu anastahili kuwekwa katika nafasi ya uungu, wengine hawaamini kuwa Roho Mtakatifu ni halisi, bali ni nguvu tu ya Mungu, ni Yesu na Mungu tu basi. Je! Ukweli ni upi? Na Je tunapaswa tusimamie wapi?
Jambo la kwanza kufahamu, ni kuangalia kiini, cha kumjua Mungu? Kama kiini kimeharibika hapo ndipo penye shida kubwa. Tunaposema kiini, tunamaanisha idadi ya miungu. Cha ajabu ni kwamba makundi yote haya yanaamini “Mungu ni mmoja”, sawasawa na maandiko yanavyosema..
Marko 12:29 Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, BWANA MUNGU WETU NI BWANA MMOJA; 30 nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.
Marko 12:29 Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, BWANA MUNGU WETU NI BWANA MMOJA;
30 nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.
Tena kizuri zaidi ni kwamba wote wanaamini kazi ya Kristo ya ukombozi, wanaamini pia kazi za Roho Mtakatifu mioyoni mwetu.
Kinachotofautisha ni kutambua tu, nafasi zao za kiungu. Hilo tu, ambalo kimsingi halina nguvu sana, zaidi ya kuzitambua kazi zao mioyoni mwetu. Ni sawa na watu wawili wanaoshindania kama MUWA, ni jamii gani ya mmea, mmoja anasema ni tunda, mwingine anasema ni aina ya jani. Embu jiweke wewe katika hiyo nafasi, ukiulizwa swali hilo utasema ni nini?. Ni rahisi kusema “muwa” ni tunda, lakini kibaolojia muwa ni jamii ya “jani”, isipokuwa limerefu tu zaidi ya mengine na lina maji matamu, .
Sasa je! Kufahamu kama ni jani, au ni tunda? Maarifa hayo yanaweza kubadili asili yake? Kwamba ukifahamu sukari yake itaongezeka, au itawabadilikia maumbo. Wewe na yeye hamna tofauti, kiladha, isipokuwa kiufahamu tu.
Vivyo hivyo na kwenye uungu wa Mungu, Tunatafuta “UJUZI”. Na ujuzi ni mzuri, lakini mara nyingi tunapoung’ang’ania sana haujengi, bali huleta matengano, Ni upendo tu ndio unaojengwa.
1Wakorintho 8:1b…Twajua ya kuwa sisi sote tuna ujuzi. Ujuzi huleta majivuno, bali upendo hujenga
Ndio maana kwanini hatushangai kuona kanisa la kwanza, liliweza kutembea katika utimilifu wote wa ki-Mungu ijapokuwa hawakuwa na maarifa ya kutosha ya kutambua uungu wa Yesu, vema, isipokuwa baadaye sana katika nyaraka za mitume, ambayo hata hivyo waliita ‘Siri ya Mungu’. Lakini hao hao waliweza kumwabudu Kristo, lakini pia wakamwabudu Baba, bila shida yoyote, wapo waliotambua siri hii, lakini wapo ambao hawakutambua vema.
Kuonyesha kuwa hilo sio jambo la kung’ang’ania sana kana kwamba usipojua utakwenda kuzimu, kama inavyochukuliwa leo, mpaka kutupelekea matengano.
Ukweli ni kwamba Mungu wetu ni Yule Yule mmoja, isipokuwa ametenda kazi kwenye nafasi tatu tofauti kwa lengo la kumkamilisha mwanadamu, na sio yeye. Na sio kana kwamba ni watu watatu wamepatana katika jambo moja. Ni sawa na maji, mvuke na barafu. Vyote vitatu vikiwekwa pamoja vinaweza kuonekana na vitu tofauti tofauti kabisa, lakini ni kitu kile kile kimoja, ambacho ni maji. Ndivyo alivyo Mungu wetu.
Kutembea katika ofisi ya ubaba, na wakati huo huo mwana, na wakati huo huo Roho Mtakatifu, sio shida kwake, amefanya hivyo ili sisi tukamilishwe. Kama mwanadamu asingeanguka hakukuwa na haja ya Mungu kujifunua katika ofisi zote, angebakia katika ubaba wake ule ule mmoja,
Ni sawa na mtu aliyebuni simu, kama kusingekuwa na changamoto ya umbali ya nini mtu kuzungumza kupitia kifaa hicho?. Vivyo hivyo Mungu kuuvaa mwili, ni ili kutuunganisha sisi na yeye, katika mahusiano ambayo tuliyapoteza pale Edeni. Baadaye akaingia kabisa ndani yetu, kwa Roho wake Mtakatifu, kiasi kwamba sasa tunamwabudu Mungu wetu moja kwa moja ndani ya mioyo yetu.
Kwahiyo, Mungu wetu hajagawanyika. Ni Yule Yule mmoja, wala hana nafsi tatu, bali moja. Wala hakuna mahali kwenye maandiko yanathibitisha kuwa Mungu anazo nafsi tatu. Lakini hilo si jambo la kuzozana nalo, kwa wanaoamini Mungu anazo nafsi tatu, maadamu hawaamini miungu mingi. Akimwabudu Baba, ni Yule Yule, akimwambudu Yesu ni yuleyule Mungu, akimwabudu Roho bado haabudu Mungu mwingine zaidi yake yuleyule mmoja. Hilo ni suala tu la kiufahamu ambalo halimwondolei mtu wokovu.
Hivyo ikiwa wewe ni mkristo, umemwamini Kristo kama ni mwokozi wako, na mwenzako pia kampokea kama wewe tu ulivyopokea, lakini haamini kama ni Mungu bali ni mwana wa Mungu. Lakutosha, usishindanie mambo ambayo ni ya ujuzi. Mwombee tu, Mungu ampe ufahamu kamilifu, kwasababu kujua kama utatu mtakatifu ni sahihi au sio sahihi hilo haliwezi kumtenga na Mungu wake, maadamu haubudu nje ya hao. Tukue kiufahamu, tusimpe adui nafasi ya kuleta mtengano yasiyo na maana.
Kwa maarifa ya ndani zaidi kuhusu, mafundisho ya uungu wa Mungu pitia haya masomo >>>
JE UNATAMANI KUMJUA MUNGU, NA HUJUI PA KUANZIA?
Je Yesu ni Mungu au Nabii?
MADHIHIRISHO MATATU YA MUNGU.
UUNGU NI NINI? (1Petro 1:3-4)
JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOKUJA JUU YA MTU.
Roho Mtakatifu ni nani?.
Hilo ndio jambo la kwanza. Kamwe huwezi kumshinda shetani ikiwa upo nje ya Kristo, Ndicho kilichowakuta wale wana wa Skewa, walipotaka kutoa pepo kwa jina la Yesu. Lakini Yule pepo akawaambia Yesu namjua, na Paulo namfahamu, lakini je ninyi ni akina nani?
Matendo 19:13 Baadhi ya Wayahudi wenye kutanga-tanga, nao ni wapunga pepo, wakajaribu kutaja jina la Bwana Yesu juu yao waliopagawa na pepo wachafu, wakisema, Nawaapisha kwa Yesu, yule anayehubiriwa na Paulo. 14 Walikuwako wana saba wa mtu mmoja Skewa, Myahudi, kuhani mkuu, waliofanya hivyo. 15 Yule pepo mchafu akawajibu, akawaambia, Yesu namjua na Paulo namfahamu, lakini ninyi ni nani? 16 Na yule mtu aliyepagawa na pepo mchafu akawarukia wawili, akawaweza, akawashinda, hata wakatoka mbio katika nyumba ile hali wa uchi na kujeruhiwa.
Matendo 19:13 Baadhi ya Wayahudi wenye kutanga-tanga, nao ni wapunga pepo, wakajaribu kutaja jina la Bwana Yesu juu yao waliopagawa na pepo wachafu, wakisema, Nawaapisha kwa Yesu, yule anayehubiriwa na Paulo.
14 Walikuwako wana saba wa mtu mmoja Skewa, Myahudi, kuhani mkuu, waliofanya hivyo.
15 Yule pepo mchafu akawajibu, akawaambia, Yesu namjua na Paulo namfahamu, lakini ninyi ni nani? 16 Na yule mtu aliyepagawa na pepo mchafu akawarukia wawili, akawaweza, akawashinda, hata wakatoka mbio katika nyumba ile hali wa uchi na kujeruhiwa.
Wokovu, ni Kristo ndani yako, na kwa huo nguvu za adui zote huyeyuka mara moja. Mtu aliyempokea Yesu, shetani kamwe hamwezi, kwasababu anamwona Kristo ndani yake.
Unaweza ukawa umeokoka, lakini shetani akapata nguvu za kukusumbua kwa majaribu, kwasababu unashindwa kutumiza baadhi ya wajibu wako kwa mwamini, Yesu alisema..
Mathayo 26:41 Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.
Yesu ijapokuwa alikuwa ni mkamilifu hana dhambi, alijaribiwa na adui, wewe ni nani usikutane na hayo? Usipokuwa mwombaji, uvivu ukakumeza, unaona shida kuomba kila siku, kuhudhuria mikesha ujue tayari upo majaribuni. Hata kama utajiona upo sawa, fahamu tu hapo ulipo kuna eneo Fulani adui anakusumbua, utakuja kugundua pindi utakapoanza kuwa mwombaji. Na ndio maana maisha ya wokovu hayatengwi na maombi. Shetani akimwangalia mwombaji anaona moto umemzunguka mkali, hawezi jiamulia tu kufanya analotaka kwake.
Warumi 16:19 Maana utii wenu umewafikilia watu wote; basi nafurahi kwa ajili yenu, lakini nataka ninyi kuwa wenye hekima katika mambo mema, na wajinga katika mambo mabaya. 20 Naye Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi. [Amina.]
Hapo anasema tuwe wajinga katika mambo mabaya. Ni nafasi kubwa kwa Mungu kumweka shetani chini ya miguu yetu. Kwamfano, unapokuwa hujui kuhusu mitindo mipya ya kidunia, sio mfuatiliaji wa miziki ya kidunia, muvi mpya mpya zilizotoka duniani, yaani kwa ufupi unapitwa na mambo ya kidunia yasiyokuwa na maana kwako, kinyume chake, unakuwa na ujuzi na hekima katika mambo ya rohoni jua hapo umemshinda shetani kwa sehemu kubwa. Hana kitu kwako, kwasababu bidhaa zake, huna mpango nazo, hununui chochote kwake. Kuipenda dunia ni kuwa adui wa Mungu, na rafiki wa shetani.
Kuweka Neno sio, kukariri vifungu vingi vya biblia, hapana, bali ni kufahamu “ukweli” (ufunuo) wa kila Neno unaloliweka moyoni mwako. Pale jangwani, Yesu alipokutana na shetani, alimjaribu kwa Neno hilo hilo,lakini Yesu akamwambia kweli yote ipoje.
Mathayo 4:6 akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe. 7 Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.
Ni muhimu ukalifahamu Neno la Mungu katika kweli yake, na hiyo huchangiwa na kufundishwa kwa ufasaha Neno la Mungu na waalimu, kwasababu Roho Mtakatifu atasema na wewe kupitia wao. Lakini pia kumpa Roho Mtakatifu nafasi ya moja kwa moja kukufundisha. Vinginevyo adui atakudanganya sana, hususani kupitia manabii wa uongo, kwasababu hulijui Neno vema.
Kulifahamu Neno, na kuijua kweli, ni jambo muhimu lakini bado shetani anaweza pata mianya ya kukunasa endapo hutaweza kulitii Neno. Penda utakatifu, penda kutendea kazi kile unachofundishwa. Yesu alisema, wapo watu wasikiao tu, lakini wapo wasikiao na kuyatendea kazi. Wote hujaribiwa kwa pepo, mafuriko na mvua za shetani. Sasa Yule aliyejijenga juu ya fundisho tu, na sio kutendea kazi fundisho, ndio huyo anayechukuliwa na mafuriko.
Mathayo 7:26 Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga; 27 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.
Mathayo 7:26 Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;
27 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.
Mateso mengine huwapata watu kwasababu ya dhambi. Kuishi maisha matakatifu, humnyima adui mlango wa kukushambulia kwa namna yoyote. Liishi Neno.
Watu wengi hudharau ushuhudiaji. Tunapokuwa na moyo mmoja wa kuitenda kazi ya Mungu, adui hawezi kukaa juu ya anga hili, kutupinga. Tunalisoma wapi hilo? Utakumbuka wakati ule Bwana alipowatuma wanafunzi wake wawili wawili kuhubiri, waliporudi kwa furaha, huku wakimwambia Bwana hata mapepo yanawatii. Yesu akawaambia nalimwona shetani akianguka kutoka juu kama umeme. Kuonyesha kuwa kitendo cha wao kuhubiri adui alikuwa anaporomoka kwa kasi sana.
Mathayo 10:17 Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako. 18 Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.
Hivyo ukizingatia mambo hayo sita (6), Utakuwa sio tu umemdhibiti adui kila Nyanja, bali pia umemteka. Ni wajibu wako mimi na wewe kuboresha mahali ambapo hapako sawa, ili kwa pamoja tukaujenge ufalme wa Mungu na kuziangusha kazi za shetani.
Yakobo 4:7 Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.
ZIFAHAMU KAZI KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.
YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.
USIWE ADUI WA BWANA
SWALI: Kwenye 2Wakorintho 8:18, Mtume Paulo anamtaja ndugu ambaye jina lake hajaliweka wazi. Ni kwanini afanye hivi tofauti na alivyozoea kufanya katika nyaraka zake nyingine, kuwataja aliowatuma?
2Wakorintho 8:18 Na pamoja naye tukamtuma ndugu yule ambaye sifa zake katika Injili zimeenea makanisani mwote.19 Wala si hivyo tu, bali alichaguliwa na makanisa asafiri pamoja nasi katika jambo la neema hii, tunayoitumikia, ili Bwana atukuzwe, ukadhihirike utayari wetu.
JIBU: Katika waraka huu, tunaona Paulo akiwaandikia kanisa la Korintho, suala la changizo kwa ajili ya watakatifu maskini waliokuwa Yerusalemu. Hivyo akawatuma pia na watatu ili kulifanikisha jambo hilo. Wa kwanza ni Tito, Ukisoma mstari wa 16-17, katika sura hiyo hiyo ya 8, anatajwa, wa pili ndio huyu ambaye sifa zake za injili zilivuma kwenye makanisa, na watatu ni ndugu mwingine ambaye pia hajatajwa jina, isipokuwa Paulo alimwita kama ‘ndugu yetu’ ambaye tunamsoma kwenye mstari wa 22
2Wakorintho 8:22 Nasi pamoja nao tumemtuma ndugu yetu tuliyemwona mara nyingi katika mambo mengi kuwa ana bidii, na sasa ana bidii zaidi sana kwa sababu ya tumaini kuu alilo nalo kwenu.
Watu hawa watatu ndio waliotumwa kwa ajili ya huduma hiyo ya changizo kwa wakorintho. Lakini swali huulizwa huyu ndugu wa pili ni nani hasaa?
Wengine husema ni Luka, wengine Barnaba, wengine Apolo, wengine Marko, Aristako. Kutokana na kwamba wengi wa hawa walisifika kwa usambazi injili, lakini pia walikuwa na Paulo mara nyingi kwenye huduma.
Lakini Hayo ni makisio tu, anaweza akawa miongoni mwa hawa, lakini pia asilimia kubwa anaonekana sio kabisa miongoni mwao, waliowahi kutajwa na Paulo.
Jambo la muhimu ambalo, linalengwa hapo, kufichwa kwa jina lake. Sio kwamba Mungu anataka tumchunguze ni nani? Hapana Lakini alipenda kutuonyesha kwamba SIFA, hujitambulisha zaidi kuliko jina.
Ukichunguza hapo, utaona Paulo anasema sifa zake zimeenea kwenye “makanisa yote”. Ikiwa na maana kuanzia huko Akaya mpaka Makedonia. Alijulikana kuwa mhubiri mwenye juhudi na mwenye kuthamini injili. Na si hivyo tu, walimchagua mwenyewe kusafiri pamoja na Paulo. Hivyo Paulo kuandika waraka huo, kwa kueleza sifa zake, aliona hilo latosha tu, kumtambulisha bila hata ya jina. Kwasababu hakuna mwingine zaidi yake. Yaani kwa namna nyingine Paulo anasema, “Mpaka hapo mmeshamtambua ni nani”.
Sikuzote wanaotambulishwa kwa majina huwa ni watu wasiojulikana, au wasio na sifa za kutosha kwenye jamii husika.
Ndivyo ilivyokuwa pia kwa Yule mtu wa tatu ambaye Paulo alimwita kama “NDUGU YETU”. Kulikuwa hakuna haja ya kumtambulisha kwa jina kwasababu walikuwa wanamwona wakati wote akiwa na akina Paulo katika ziara zake na huduma. Hivyo kumtafaja tu ndugu yetu ilitosha, alijua kila mmoja alielewa ni nani aliyekuwa anazungumziwa, kwasababu mitume hawakuwa na ndugu mwingine zaidi ya huyo, aliyekuwa karibu nao.
Hata leo, Bwana anapenda sisi tutambuliwe kwa SIFA zetu, zaidi ya MAJINA yetu. Kiasi kwamba kazi itakayoonekana kwa ajili ya Kristo, itutambulishe sisi, sio sisi tuyatambulishe majina yetu katikati ya watu.
Utaona baadhi ya wahubiri wanachokifanya, ni kutumia nguvu kubwa kutangaza majina yao, na sura zao, ili wajulikane, lakini kazi zao hazitambuliki. Hilo sio lengo la mhubiri, au Mtumishi wa Mungu. Bwana wetu Yesu Kristo alipokuwa duniani, haikuwa na muda wa kujitangaza, wakati mwingine hakutaka mambo yake yadhihirishwe kiwepesi, mpaka atakapomaliza kazi yake, Na sisi pia tupende aina hii ya utumishi.
Shalom.
Epafrodito ni nani kwenye biblia?
Epafra ni nani katika biblia? (Wakolosai 1:7)
Je ni sawa kuukubali udhaifu kama mtume Paulo alivyojisifia kwa huo? (2Wakorintho 12:9-10)
Jibu ni ndio.
Lakini sio njia zote zinaweza kutibu ugonjwa huo. Ni kweli madaktari hufanya kwa sehemu yao. Lakini Mungu hufanya zaidi, kwake yote hutibika.
Uvimbe wa aina yoyote ile, uwe ule wa kwenye mfuko wa uzazi, au kibofu, au kwenye koo, au kichwa, au tumboni. Popote pale, maadamu ni uvimbe, haijalishi ukubwa wake, unaponyeka huo.
Na anayeweza kufanya hivyo ni YESU TU.
Tafsiri ya jina lake ni MWOKOZI. Ndiye aliyetumwa na Mungu mahususi kuwaokoa wanadamu na dhambi zao, pamoja na shida zao na magonjwa yao, alizaliwa kwa kusudi hilo tu moja. Hivyo maadamu yeye yupo huna haja ya kuwa na hofu.
Isaya 53:4 Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa. 5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona
Huo ugonjwa alishauchukua zamani sana, kabla ya wewe kuzaliwa. Alimponya Lazaro aliyekufa na ugonjwa, na kuzikwa na kuoza. Atakuponya na wewe, ambaye hata bado hujafa kwa ugonjwa huo. Ni kumwamini tu, basi,
Lakini hatua ya kwanza ni wewe kumpokea maishani mwako. Kukubali neema yake, kwa kutubu dhambi zako, kwa kumaanisha kabisa kuziacha, kisha yeye mwenyewe atakupa ondoleo la dhambi hizo, na utakuwa umeupokea uzima wa milele, Wala hatazikumbuka tena kuanzia siku hii ya leo na kuendelea.
Ikiwa upo tayari kupokea wokovu huu bure basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Ikiwa sasa tayari umeokoka. Basi unahitaji msaada ya kimaombi.
Piga namba uzionazo chini ya chapisho hili nasi tutakuombea (bure) na kwa imani utapokea uponyaji wako.
KANSA/SARATANI INATIBIKA.
SALA YA UPONYAJI/MAOMBI YA UPONYAJI.
UPONYAJI WA YESU.
JE! UKIMWI UNATIBIKA?
Yapo matatizo ya kimwili ambayo kwa tiba hutatulika, Ukiona unahisi vitu vinatembea mwilini kama vile wadudu, na kukusababishia madhara fulani mwilini lada kuchoka, mwili kuuma, ni vema ukaenda kwanza kuangalia afya yako kwa daktari, utashuariwa na kupewa tiba, Ukiona limetatulika basi ilikuwa ni shida ya kimwili.
Lakini ukiona tiba, haitatui haeleti majibu yoyote. Unahitaji msaada wa kiroho. Mara nyingi wanaokumbana na hali hii ya kuhisi vitu vinatembea mwilini, au sindano zipita zinachoma-choma, au kuhisi kitu kinatembea tumboni, au mgongoni, mikononi na miguuni, huwa ni dalili za mapepo kuwapo ndani yao.
Angalia, je, hali hiyo inapokutokea unakuwa katika mazingira gani? Je, kwenye maombi ndio huzidi? Je! Unapojaribu kusikiliza, au kusoma biblia? Ukiona hiyo hali inakujia halafu inaambatana na mambo kama kupoteza kumbukumbu, au unakuwa na hasira, au hofu, au ufanisi wako unapungua. Hizo ni dalili za mapepo. Hivyo hayana budi kuondolewa ndani yako.
Kumbuka mtu anafunguliwa kwanza kuwa kumkumbali Yule ambaye atamwokoa yaani YESU KRISTO. Hivyo jambo la kwanza ni wewe kumpokea moyoni mwako. Kwa msaada huo waweza fungua hapa, upata wokovu >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Lakini kwa msaada wa ki-maombi (bure), wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini mwa makala hii, na Bwana atakufanya huru kwelikweli.
DALILI TISA (9) ZA PEPO KUWEPO NDANI YA MTU.
Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni ipi?
ITAMBUE KARAMA YA MUNGU.
WhatsApp
SWALI: Nini maana ya vifungu tunavyovisoma katika Wakolosai 2:18,
‘Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu, kwa kunyenyekea kwa mapenzi yake mwenyewe tu, na kuabudu malaika, akijitia katika maono yake na kujivuna bure, kwa akili zake za kimwili;
JIBU: Tukianzia mistari ya juu anasema..
16 Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato; 17 mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo. 18 Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu, kwa kunyenyekea kwa mapenzi yake mwenyewe tu, na kuabudu malaika, akijitia katika maono yake na kujivuna bure, kwa akili zake za kimwili;
16 Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;
17 mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo. 18 Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu, kwa kunyenyekea kwa mapenzi yake mwenyewe tu, na kuabudu malaika, akijitia katika maono yake na kujivuna bure, kwa akili zake za kimwili;
Katika vifungu hivyo, Mtume Paulo anaanza kwa kuwaambia ‘mtu asiwanyang’anye thawabu yenu’. Akiwafananisha na wana-michezo ambao wanashiriki katika mashindano Fulani, ambao hujitahidi kwa kila namna kujizuia, na kujichunga ili wafanye vema katika mashindano hayo wachukue tuzo.
Sasa Paulo, anatoa angalizo, akirejea mfano wa washindani hao, yawezekana mwingine akamfanyia hila mwenzake, ili asiwe na ufanisi, kwenye michezo hiyo akashindwa kushiriki vema na kuchukua tuzo, kwamfano anaweza kumpa kinywaji Fulani ambacho kitadhoofisha uchezaji wake, au atamdanganya afanya zoezi Fulani, ambalo anajua kabisa halina manufaa kwake, kwamfano labda mchezaji ni mwana-riadha, utaona Yule mwingine anamwambia akanyanyue vyuma vizito atakuwa mwepesi kukimbia. Kumbe kukimbia hakuhusiani na misuli mikubwa bali pumzi.
Vivyo hivyo Paulo aliona kuwa kuna waalimu wa uongo, viongozi wa uongo,watakaozuka, kuwadanganya watu waiache njia sahihi, ya kukubaliwa na Mungu. Na ndio hapo anataja mambo matatu ambayo watakuwa nayo;
Jambo la kwanza,
Watachukua thawabu yao kwa kunyenyekea kwa mapenzi yao wenyewe tu,
Kunyenyekea sio kubaya, ni tunda la Roho Mtakatifu ndani ya mtu, na wakristo wote, tunasukumwa katika unyenyekevu. Lakini angalia hapo anasema kunyenyekea KWA MAPENZI YAKE MWENYEWE. Maana yake, ni kuwa hanyenyekei kwa mapenzi ya Mungu, bali yake. Na hiyo ni mbaya, kwasababu watu wa kidini leo hii ndio kanuni yao, hubuni njia zao za kumwabudu Mungu, na hiyo huwavutia watu wengi, waone kama ni Mungu kweli anaabudiwa, kwa unyenyekevu na heshima, nao wanaingia kwenye mkondo huo. Wanasahau kuwa ibada lazima ifanyike kwanza katika Roho na Kweli.
Mambo kama kusujudia, kuvaa mavazi Fulani meupe, kutawadha mwili, kuvua viatu katika nyumba za ibada, kuomba kwa sauti ya kuvuta sana, ya upole, huku umeinamisha kichwa chini, unaibusu biblia. Hudhanikuwa kuwa ndio hicho Mungu anakitaka, Lakini ndani, kinywa chake kina matusi, akitoka hapo anakwenda kuishi maisha kishirikina, na ulevi. Huo ni udanganyifu mkubwa sana.
Ndicho Paulo alichokiona kwa kanisa la Kolosai, kulitokea watu wanawaambia usile kambale ni chukizo kwa Mungu, shika siku ya sabato, inatosha.. Yote hayo yakifanyika kimwili. Lakini wasifundishe kwamba unyenyekevu wa ki-Mungu hutoka rohoni, ukisukumwa na neema katika Roho Mtakatifu, Ambapo mtu kupaswa kukubali wokovu kwanza, na kutii kwa kumfuata Kristo anayeweza kumfanya mtu kiumbe kipya, na sio jambo la kufanya kimwili tu, akidhani atampendeza Mungu.
Jambo la pili
wanaweza kuwanyang’anya thawabu yao kwa mafundisho ya kuabudu malaika.
Tangu zamani, kulikuwa na watu waliowaweka malaika katika nafasi ya Mungu. Na kuvuka ile mipaka ya kutuhudumia tu sisi (Waebrania 1:14). Hivyo ikiwa mtu alikuwa na karama Fulani ya maono, ambapo mengine huletwa kwa mikono ya malaika, tunaliona hilo mara nyingi tangu Musa, na wana wa Israeli jangwani, pamoja na mitume mpaka Yohana kule Patmo. Mungu aliwatumia malaika kwa sehemu kubwa kutufikishia sisi jumbe zake, kwasababu waliwekwa kutuhudumia sisi.
Lakini dini na imani zikazuka kuanzia hapo, kwa baadhi ya watu wakaanza kuwafanyia ibada, jambo ambalo ni chukizo kwa Bwana. Hata leo utaona zipo sala za malaika na watakatifu kuwataka wawaombee. Au wawasaidie vitani. Ikiwa wewe ni mtoto wa Mungu umeokoka, kuwa makini na ibada hizo, taabu yako kwa Mungu yaweza kuwa bure, kwasababu unamudhi Mungu. Ibada za namna hiyo hazina tofauti na ibada za majini. Usiabudu mwanadamu, wala kiumbe chochote kilicho mbinguni wala duniani.
Jambo la tatu
Na mwisho anasema wakijivuna bure kwa akili zao za mwili.
Kujivuna, maana yake kusifia vitu vya mwilini mfano vipaji vyao, wengine ujuzi wa kuongea vizuri, na kupangalia maneno, werevu, elimu za falsafa, mambo ambayo Paulo aliyaona, yakiwavuta wengi, na kuacha njia kamilifu ya Kristo iliyo katika neema, upendo, Imani na nguvu za Mungu. (2Wakorintho 11:18-20).
Injili inabadilishwa inakuwa vichekesho, na kanuni za ki-ujasiriamali,
Hata leo mimi na wewe ni kuwa makini, bidii yako katika Kristo isichukuliwe na udini, bali Neno, isichukuliwe na maono na karama, na ibada za malaika bali Mungu, isichukuliwe na falsafa za kibinadamu, na mwonekano, bali, Roho Mtakatifu na kweli, katika neema.
mtu asichukue taji lako
JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)
JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 2)
Nini maana ya kikombe cha maji ya baridi(Mathayo 10:42)?
Matendo 11:25
Kisha akatoka akaenda Tarso kumtafuta Sauli;
Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo, napenda leo tujifunza jambo moja ambalo huwenda linasahaulika miongoni mwetu kama watendakazi shambani mwa Bwana.
Hatuna budi kufahamu ,ufuatiliaji huenda sambamba na uinjilisti. Twaweza hubiria watu wakaokoka, wakamjua Kristo, wakati mwingine wakaweza hata kujisimamia wenyewe, lakini tusipojijengea tabia ya kuwafuatilia na kukaa nao, kuwaimarisha, basi kazi yetu yaweza kuwa bure, au isiwe na matunda mazuri kama ipasavyo.
tunajifunza kwa mtu mmoja aliyeitwa Barnaba, aliyejulikana pia kama mwana wa faraja. Huyu aliithamini huduma hii. Baada ya kusikia kuwa Paulo, amegeuka na kuwa mkristo, lakini akaenda mahali panaitwa Tarso, mbali kidogo na kanisa, Barnaba aliona si vema amwache huko. Ikabidi afunge safari yeye mwenyewe kutoka Antiokia aende kumtafuta.
Hatujui safari yake ilichukua siku ngapi, wiki ngapi, miezi mingapi. Lakini hatimaye akampata ..Alipomwona huwenda hakuridhishwa na mazingira ya kihuduma aliyokuwa nayo, hakuridhishwa na hali ya kiroho aliyokuwa nayo. Kwasababu hata mtume Paulo kuondoka Yerusalemu ilikuwa si kupenda kwake ni kutokana pia na kukataliwa na kanisa, na hatari ya kuuliwa na wayahudi.
Lakini Barnaba alipomuona. Akamchukua amlete mahali bora zaidi, ambapo kanisa lipo hai. Akafika akaendelea na huduma, akaanza kuwa moto tena na kutokea hapo ndipo Mungu alipomfanya mhubiri wa kimataifa.
Leo hii tunasoma ushujaa wa Paulo, lakini kusimama kwake kulichangiwa na nguvu ya kufuatiliwa kwa waliomtangulia kiroho.
Je na sisi tumejiwekea desturi hii? kuwafuatilia mara kwa mara tunaowashuhudia injili?
Kamwe usimdharau mwongofu mpya, hata kama atakuwa anasua-sua, au mdhaifu sasa. Fahamu kuwa huyo ndio Paulo wa baadaye. Usihubiri tu ukaacha, ukadhani atajikuza mwenyewe. Shughulika naye, omba naye, mfuate alipo, mfundishe, ikiwezekana mwamishe eneo alilopo ikiwa linamfanya asisimame kiroho. Na kazi yako itazaa matunda, usichoke.
FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.
MAUMIVU NYUMA-YA-HUDUMA.
MAMBO NANE (8), AMBAYO WEWE KAMA KIONGOZI UTAIGWA.
SWALI: Maandiko yanaposema Habili ijapokuwa amekufa angali akinena, je! Ananenaje, wakati yeye ni marehemu. Je! Hiyo inamaana wazee wetu wa zamani wanaweza kunena na sisi?
Waebrani 11:4 Kwa imani Habili alimtolea Mungu dhabihu iliyo bora kuliko Kaini; kwa hiyo alishuhudiwa kuwa ana haki; Mungu akazishuhudia sadaka zake, na kwa hiyo, ijapokuwa amekufa, angali akinena
JIBU: Kibiblia ni kweli kabisa watakatifu waliokufa kale hunena nasi. Lakini kunena kwao ni tofauti na huku kunakodhaniwa, kwamba mzimu unakutokea kwenye ndoto, au unasikia sauti ya petro makaburini ikizungumza na wewe, Hapana, ukiona hivyo ujue huzungumzi na huyo mtu, bali ni pepo.
Sasa watakatifu waliokufa wanazungumzaje na sisi?
Ni kwa ushuhuda waliouacha. Maisha yao na maagizo yao, ndio huzungumza nasi, sikuzote, kana kwamba tupo nao sasa, kwa mafundisho yao yaliyopo mpaka sasa kana kwamba tunawaona wenyewe kumbe wamekufa.
Ndio maana ile habari ya Yule tajiri wa Lazaro, tunaambiwa alipofika kule kuzimu akaomba mtu atolewe kwa wafu awahubirie injili, akakataliwa, kuonyesha kuwa hakuna mtu aliyekufa mwenye uwezo wa kuja tena kuzungumza na sisi, nafasi hiyo haipo kwao. Lakini waliambiwa WANAO MUSA NA MANABII, WAWASIKILIZE.
Luka 16:29 Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao.
Maana yake ni kuwa sio kwamba Musa kweli alikuwepo duniani, au manabii wa kale kama Isaya walikuwa duniani kwa wakati huo, anaambiwa hayo maneno. Lakini shuhuda zao na mahubiri yao, huwawakilisha wao. Tunaweza kusema “ijapokuwa wamekufa wangali wakinena”
Ndivyo ilivyo kwa Habili, ijapokuwa aliuliwa na ndugu yake, lakini IMANI yake inasema nasi mpaka leo. Mitume wa Kristo ijapokuwa hawapo duniani lakini sauti zao tunazisikia hadi sasa.
Lakini pia kuna mahali pengine biblia inasema damu ya Yesu hunena mema kuliko ya Habili (Waebrania 12:24). Kufahamu kwa kina damu ya mtakatifu hunenaje? Pitia somo hili. >>> DAMU YA ZAKARI BIN BARAKIA.
JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?
KUOTA MTU AMEKUFA/NDUGU AMEKUFA.
ALIPOKUWA ANGALI MBALI, BABA YAKE ALIMWONA.