Title Devis

Nini tofauti ya haya maneno. 1) KUOKOKA, 2) WOKOVU, 3) KUONGOKA.?

JIBU: Shalom! Maana ya Neno ongoka ni KUGUEUKA.

Hivyo biblia inaposema mtu ni mwongofu inamaanisha kuwa ni mtu aliyegeuka na kuacha mienendo aliyokuwa anaiendea hapo mwanzo. Embu tutazame baadhi ya vifungu kwa kupitia hivyo tutajifunza kwa uelewa mrahisi zaidi:  

Mathayo 18.3 “akasema, Amin, nawaambia, MSIPOONGOKA na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni”.

Hapo Bwana alikuwa anamaanisha MSIPOGEUKA na kuwa kama vitoto, yaani wasipogeuzwa fikra zao na kuwa kama watoto wadogo hawawezi kuuingia katika ufalme wa mbinguni.   Kadhalika tukisoma..

Marko 4: 11 “Akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuijua siri ya ufalme wa Mungu, bali kwa wale walio nje yote hufanywa kwa mifano,

12 ili wakitazama watazame, wasione; Na wakisikia wasikie, wasielewe; Wasije WAKAONGOKA, na kusamehewa.”  

Tunaona hapo Bwana alimaanisha wale watu wasije WAKAGEUKA na kuacha njia zao mbaya, ambapo kama wakifanya hivyo Mungu atawasemehe, na kuwaachilia neema ya kusamehewa dhambi zao.   Tukisoma pia..

1Timotheo 3.6 “Wala asiwe mtu ALIYEONGOKA karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi.”

Hapo Mtume Paulo aliposema mtu aliyeongoka hivi karibuni, alimaanisha kuwa mtu Yule aliyegeuka na kuacha njia zake mbovu, hivi karibuni, asije akapewa kazi ya uaskofu kwasababu mtu kama huyo bado hajaweza kuijua imani vizuri, na kuweza kuzitambua hila za shetani kwani bado ni mchanga wa imani.  

Hivyo ukitazama na vifungu vingine utaliona jambo hilo kwa muda wako unaweza ukavipitia baadhi ninavyokuorodheshea hapa (Mathayo 13:15,Luka 22:32, Matendo 15:3).  

Kwa hiyo tunaweza kusema mtu anaweza akawa ni mwongofu, lakini bado hajaokoka. Tutalitazama hilo kwa undani tutakapojua kwanza maana ya kuokoa pia.

KUOKOKA/WOKOVU.  (Nini Maana ya kuokoka/ kuokoka ni nini?)

Kuokoka na wokovu ni kitu kile kile..Kuokoka ni kitenzi cha nomino Wokovu. Hivyo mtu mpaka awe ameokoka ni lazima kwanza awe amehusishwa na anayemwokoa mwenyewe (yaani mwokozi). Katika ukristo huwezi kusema umeokoka mwenyewe kama Yesu Kristo hajayageuza maisha yako, kama maisha yako hajahusianishwa na Kristo moja kwa moja, basi utakuwa umepokea wokovu mwingine tofauti na ule unaozungumzwa kwenye biblia.  

Biblia inasema.

Warumi 10:9 “ Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, “”utaokoka””.

10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu”.

  Na pia inasema: “AAMINIYE na KUBATIZWA “ataokoka”; asiyeamini, atahukumiwa.(Marko 16:16)”. Zingatia hivyo vifungu viwili vya mistari, vitakuja kutusaidia huko mbeleni. Kwasababu vyote viwili vinahusianishwa na suala la wokovu kwa mwanadamu.   Kama tulivyosema suala la kuokoka ni jambo la kuingia moja kwa moja katika mahusiano ya karibu na Yule anayekuokoa. Upo udanganyifu mkubwa unaoendelea duniani sasahivi, watu wadhaniao kuwa wokovu ni jambo la Kuzungumza tu kwenye kinywa halafu basi wewe tayari utakuwa umeokoka. Hivyo imepelekea kila mtu duniani anasema ameokoka hata kama ni mlevi kisa tu tayari alishakiri yale maneno alipokuwa anaangozwa sala ya toba.  

Watumishi wa Mungu wameyaacha na yale mwengine na kuona kuwa hayana umuhimu wowote. Hii ni kutokana na kwamba Kushindwa kuelewa maana ya Neno KUKIRI, ndiyo inayopelekea wokovu kuonekana ni kitu cha ajabu sasa duniani. Ndiyo inayopelekea watu kutoona nguvu za wokovu zikitenda kazi ndani yako. Wanakiri wameookoa, wameokoka.. lakini ukweli ni kwamba Wapo mbali na wokovu kuliko wao wanavyodhani.   Biblia inaposema kwa kinywa mtu Hukiri “HATA” kupata wokovu..zingatia hilo Neno “HATA”..Ikiwa na maana kuwa ni tendo ENDELEVU. Sio kuzungumza tu siku moja halafu basi, Pia ili neno KIRI liwe na uweza na nguvu ni lazima pia neno KANA liwepo..

Kwa Watakatifu wa kale ilikuwa mtu akionyesha tu kumkiri Yesu kuwa ni mwokozi ilikuwa adhabu yake ni kufa au kutengwa na jamii pamoja na sinagogi. (Soma Yohana 3&9). Hivyo watu wa wakati ule ilikuwa kukiri tu vile, basi wewe ulikuwa umeshajihalalisha si wa kwao, na hivyo unawekwa mbali na watu wote wanamchukia Kristo. Lakini kukiri kwetu sisi mazingira tuliyopo mazingira ya kukana hayapo basi hilo neno halina nguvu kwa kinywa pekee.

Kama ndio hivyo basi sisi tunamkirije Kristo?.

  Tunamkiri Kristo kwa maisha yetu na matendo yetu kuonyesha kuwa ni kweli Kristo alikufa, na kufufuka pamoja na sisi, kwanza kwa kubatizwa katika maji mengi na katika jina la YESU KRISTO kama maandiko yasemavyo pindi tu tuaminipo kama ishara ya kuamini kuwa alikufa akafufuka pamoja na sisi kuuonyesha ulimwengu tumekuwa milki halali ya Bwana. Na Pili ni kukubali kuishi maisha yanayomkiri Kristo kila siku.

  Hapo ndio mtu anakuwa tayari kuingia gharama zote ikiwemo kuwa tayari kutengwa, kuchukiwa, kuachwa, kudharauliwa kwa ajili ya KRISTO, kwa ajili ya kumfuata Kristo.   Sasa hapo ndipo mtu amemkiri Kristo. Na wokovu kwake ni jambo la lazima.   Fananisha maneno hayo na vifungu hivi Bwana Yesu alivyowaambia makutano:  

Mathayo 10:32 “Basi, kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, nami nitamkiri mbele za Baba yangu aliye mbinguni.

33 Bali mtu ye yote atakayenikana mbele ya watu, nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye mbinguni.

34 Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga.

35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu; 36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.

37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.

38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili.”  

Pia ni vizuri kufahamu kuwa wapo watu wanaosema kuwa tukiwa hapa duniani hatuwezi kukoka mpaka tutakapokwenda mbinguni. Huo nao ni uongo. Biblia inasema 2 Wakoritho 6: 2 “Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama SIKU YA WOKOVU NI SASA)”.

  Unaona hapo?

Siku ya wokovu ni sasa. Tunaokolewa tukiwa hapa duniani hivyo mtu kusema nimeokoka ikiwa kweli amezingatia vigezo vyote vilivyotelewa na huyo amwokoaye.

  Hana budi kujithibitishia hilo kuwa tayari ameshaokoka. Na hivyo siku ile ya kwenda mbinguni ni kukamilishwa tu kwa wokovu wake. Kumbuka raha ya wokovu inaanzia hapa hapa duniani pindi tu pale mtu anapomwamini Yesu Kristo, matunda ya wokovu yanaanzia duniani mbinguni ni kukamilishwa tu.   Hivyo, kwa kuhitimisha tunaweza kusema mtu aliyeongoka ni tofauti na aliyeokoka. Japo aliyeokoka tayari alishaongoka ndani yake, lakini aliyeongoka haitupi uhakika kuwa ameokoka, kwasababu Neno lenyewe kuongoka ni KUGEUKA na sio KUOKOLEWA.   Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Ubarikiwe sana.


 

Mada zinazoendana:

JE! UMECHAGULIWA KABLA YA KUWEKWA MISINGI YA ULIMWENGU?

KAMA MHUBIRI NI WOKOVU UPI UNAUPELEKA KWA WATU?

UKIAMINI NA UKIMKIRI YESU KWA KINYWA CHAKO, UTAOKOKA.

MELKIZEDEKI NI NANI?

DANIELI: MLANGO WA 1

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

KANUNI RAHISI YA KUFANIKIWA.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

SWALI: KUFUKIZA UVUMBA ndio kufanyaje? Na tena wana wa Israel walimfukizia uvumba Malkia wa mbinguni, ndio yupi huyo?


JIBU: Uvumba ni aina Fulani ya manukato, yanayotengenezwa kwa viungo mbalimbali ambavyo baada ya kutengenezwa pamoja, huwa yanachomwa na kutoa harufu Fulani iliyo nzuri. Sasa katika biblia (Agano la Kale) wana wa Israeli walipokuwa jangwani kabla ya kufika nchi ya Ahadi, walipewa maagizo na Mungu mwenyewe watengeneze UVUMBA, na makuhani watakuwa wanauchoma huo kila siku ndani ya ile Hema waliyoambiwa waitengeneze..

Na ni makuhani peke yao ndio waliokuwa wanaruhusiwa kufanya hiyo kazi ya kuvukiza uvumba. Hivyo Makuhani waliuchukua huo uvumba na kuuchoma kila siku ndani ya ile hema ya kukutania katika madhabahu ndogo iliyokuwemo kule ndani, Na ilikuwa ni amri ya daima ni lazima wafanye hivyo kila siku..Na Bwana aliwaagiza wana wa Israeli wasitengeneze uvumba wowote kwa viungo hivyo kwa ajili ya mambo yao..Fomula ya kutengeneza huo uvumba ni kwa ajili ya Bwana tu!

 Kutoka 30:34 “Bwana akamwambia Musa, Jitwalie MANUKATO MAZURI, yaani, natafi, na shekelethi, na kelbena; viungo vya manukato vizuri pamoja na ubani safi; vitu hivyo vyote na viwe vya kipimo kimoja;

35 nawe UTAFANYA UVUMBA WA VITU HIVYO, manukato ya kazi ya ustadi wa mtengenazaji manukato, yatakuwa yamekolea, safi, matakatifu;

36 nawe baadhi yake utayaponda sana, na kuyaweka mbele ya ushuhuda ndani ya hema ya kukutania, hapo nitakapokutana nawe; nayo yatakuwa kwenu matakatifu sana.

37 Na uvumba utakaofanya, hamtajifanyia uvumba wenye viungo sawasawa na uvumba huo; utakuwa kwenu mtakatifu kwa ajili ya Bwana”.

Sasa swali ni kwanini Bwana aliwapa hayo maagizo ya kuchoma uvumba ndani ya nyumba yake??

 Jibu ni kwamba kila kitu kilichokuwemo ndani ya ile Hema ya kukutania kilikuwa ni lugha ya picha ya jambo linaloendelea rohoni….kwamfano kile kinara cha taa saba ndani ya nyumba ya Mungu kiliwakilisha makanisa saba katika ufunuo sura ya 2 na ya 3, kadhalika Yule kuhani mkuu anayeingia patakatifu pa patakatifu na Damu ya mwanakondoo ili kufanya upatanisho, anamwakilisha Yesu Kristo, ambaye ndiye kuhani wetu mkuu aliyeingia patakatifu pa patakatifu kwa damu yake mwenyewe mara moja tu! 

Kadhalika na ule UVUMBA, kwa jinsi ulivyokuwa unachomwa ndani ya Nyumba ya Mungu, na moshi wake kukijaza kile chumba, na kupaa juu mbinguni..Jambo lile lilikuwa linafunua jinsi gani maombi ya watakatifu yanavyomfikia Mungu, kwanza yanakuwa yameandaliwa kulingana na Neno lake, pili yanapaa juu kama moshi na kumfikia Mungu mbinguni, kwani tunajua kitu pekee kinachopaa juu chenyewe ni moshi..Hivyo kwasababu yametengenezwa na viungo vinavyoendana na Neno la Mungu, maombi ya watakatifu yanakuwa ni harufu nzuri ya kuvutia mbele za Mungu, yanakuwa kama perfume mbele zake. Na ndio maana Daudi alisema maneno haya..

Zaburi 141: 2 “SALA YANGU IPAE MBELE ZAKO KAMA UVUMBA, Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni.”

Kwasababu hiyo basi katika agano jipya hatuchomi ubani tena, wala hatuvukizi uvumba kwasababu hayo yalikuwa ni mambo ya mwilini yanayofunua mambo ya rohoni, HIVYO UVUMBA WETU NI MAOMBI YETU TUNAYOMWOMBA MUNGU KILA SIKU YANAYOENDANA NA NENO LAKE.Ndio maana pia tunasoma hayo katika kitabu cha Ufunuo..

Ufunuo 5:8 “ Hata alipokitwaa kile kitabu, hao wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele za Mwana-Kondoo, kila mmoja wao ana kinubi, NA VITASA VYA DHAHABU VILIVYOJAA MANUKATO, AMBAYO NI MAOMBI YA WATAKATIFU.”

Ufunuo 8:4 “NA MOSHI WA ULE UVUMBA UKAPANDA MBELE ZA MUNGU PAMOJA NA MAOMBI YA WATAKATIFU, kutoka mkononi mwa malaika.” 

Lakini pamoja na hayo shetani naye huwa anapenda kuiga na kugeuza mambo, na kuwadanganya watu kuwa mambo hayo kwasasa yanapaswa yaendelee kufanyika, kama anavyowadanganya watu kuwa kwasababu agano la kale kondoo na mbuzi walikuwa wanachichwa kwa ajili ya upatanisho, vivyo hivyo na sasa kondoo na mbuzi wanapaswa wachichwe kwa ajili ya kuondoa mikosi katika mtu, au jamii au ukoo, hivyo watu badala wapone ndio wanajiongezea roho juu ya roho..

Vivyo hivyo leo hii Bado shetani anawadanganya watu juu ya kuvukiza uvumba, ndio utasikia watu wanaambiwa wakachome ubani manyumbani mwao kufukuza mapepo, na zaidi hata makanisani watu wanavukiza uvumba, jambo ambalo ni machukizo kwa Mungu wa mbinguni…. Na kuhusu MALKIA WA MBUNGUNI. Hakuna mahali popote biblia imesema kuna malkia mbinguni, isipokuwa imeeleza miungu ya kipagani, inayojulikana kama malkia wa Mbinguni, hivyo biblia ilipotaja malkia wa mbinguni mahali popote ilikuwa inamaanisha miungu ya kipagani inayojulikana na watu kama malkia wa mbinguni, Ni sawa na leo atokee mtu atengeneze kinyago chake halafu akiite Malkia wa mbinguni, kiuhalisia sio kweli kwamba ni malkia wa mbinguni, mbinguni Mungu aliko hapana bali kimeitwa vile kutokana na watu wanakiita chenyewe malkia wa mbinguni. 

Ubarikiwe!


Mada zinazoendana:

ZILE TUNU (DHAHABU, UVUMBA NA MANEMANE) MAMAJUSI WALIZOZITOA KWA BWANA ZILIWAKILISHA NINI?

HUYU AZAZELI NI NANI TUNAYEMSOMA KATIKA(WALAWI 16:8)

JE! SISI NI WAFALME NA MAKUHANI KWA NAMNA GANI?

NADHIRI.

MWANA WA MUNGU.

MCHE MWORORO.

 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mtume Paulo alikuwa na maana gani kusema katika 1Wakorintho 15:31″…NIKAKUFA KILA SIKU?

JIBU: Katika ukristo KUFA kupo kwa namna mbili:  

>Aina ya kwanza ni kufa kwa habari ya dhambi.  

>Aina ya pili ni kufa kwa ajili ya Ndugu: Yaana kuwa tayari kuiponza roho yako, mpaka kufikia hatua ya kuweza kuitoa roho yako kwa ajili ya injili na kwa ajili ya Kristo.  

Ukristo sio wa leo na kesho halafu basi, Tunapokuwa wakristo inamaanisha tunajikana nafsi zetu kila siku, na kumwishia Mungu siku zetu zote zilizobakia na ndio maana Bwana YESU alisema:

Luka 9:23 “ Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake KILA SIKU, anifuate.

24 Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu ndiye atakayeisalimisha.”  

Unaona hapo, ni kuchukua msalaba wako na kumfuata KILA SIKU na sio siku moja au mbili kisha basi. Kwa lugha iliyo rahisi ni kwamba kila siku unapaswa UFE kwa habari ya ulimwengu na uwe hai kwa habari ya Kristo.

Unakufa kila siku kwa habari ya fashion za ulimwengu huu, unakufa kila siku kwa kampani za marafiki wabovu, unakufa kila siku kwa habari ya matusi, kila siku unakufa kwa habari ya uasherati na tama zake kwa kujiweka mbali nazo, unakufa kwa habari ya rushwa, unakufa kwa habari ya usengenyaji, na anasa n.k.  

Kadhalika pia tunapoona ndugu zetu walio wachanga na wanahitaji msaada wa kiroho wa injili kutoka kwetu nasi tunajua kabisa tusipofanya hivyo wataangamia, hapo pia tunagharimika kuwaendea kwa gharama zozote zile bila kujali ni hatari gani tutakumbana nayo huko mbeleni kama vile mtume Paulo alivyokuwa anasema..Bila kujali jamii itakutenga vipi, bila kujali serikali itapingana nawe vipi, bila kujali watu wenye chuki watakuvizia muda wowote kukuua, bila kujali watu wa dini wanakuchuliaje n.k.   Sasa huko ndio KUFA KILA SIKU WA AJILI YA KRISTO.

Lakini ikiwa maisha yetu kila siku yatakuwa hivyo hayana mabadiliko yoyote, kila siku tunaonakena hatuna tofuati na watu wa ulimwengu. Hiyo ni dalili tosha kutuonyesha kuwa bado hatujamfauta Kristo..

  Ubarikiwe.


Mada zinazoendana:

JIKANE NAFSI MTEULE WA MUNGU.

JE! NI KWELI UMEMFUATA YESU?

NJIA YA MSALABA

AGIZO LA UTUME.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

NGURUMO SABA

Rudi Nyumbani:

Print this post

Biblia inasema usiongeze wala usipunguze Neno la Mungu, huko kuongeza na kupunguza kukoje?

JIBU: Hata katika hali ya kawaida mtu anapozungumza maneno mengine ya uongo ambayo wewe hujasema mtu huyo ni sawa na kakuongezea maneno… Kwamfano mtu anapokwenda kutoa ushahidi mahakamani ya kwamba amekusikia ukisema maneno Fulani na angali wewe hujasema hayo maneno,na anafanya vile kwa makusudi mtu huyo atakuwa ni kama amekuongezea maneno, Vivyo hivyo na kwa Mungu mtu anapotoa ushuhuda wa uongo kuhusu Mungu, au anapofundisha jambo la uongo kinyume na Neno la Mungu na anafanya vile makusudi kwa nia ya kupotosha, mtu huyo ni sawa na ameongeza neno katika maneno ya Mungu na Biblia inasema ataongezewa mapigo katika siku ile (Ufunuo 22:18).  

Kwamfano maandiko yanasema “Mtu ameandikiwa kufa mara moja na baada ya kifo ni hukumu Waebrania (9:27)” Lakini inatokea mwalimu au mtumishi analijua hilo andiko na maana yake lakini badala ya kuwafundisha watu hilo, anawapotosha na kuwaambia hakuna hukumu baada ya kufa, au mtu baada ya kufa anakwenda toharani kutakaswa kisha mbinguni baadaye hata kama alikufa katika dhambi, Hivyo anaendelea kuwafariji watu wazidi kudumu katika dhambi zao..huyo ni sawa na ameongeza Neno katika maneno ya Mungu..  

Kadhalika kupunguza maneno inatokea pale mtu anapoujua ukweli na hauhubiri wote kama inavyopaswa, pengine kwa hofu Fulani, au kwasababu anaogopa kutengwa, au kuchukiwa…mtu kama huyo ni sawa na amepunguza Neno kati ya maneno ya Mungu, na hivyo atapunguziwa sehemu yake (yaani thawabu yake) katika ule mti wa Uzima, na katika ule mji Mtakatifu Yerusalemu ya Mungu katika siku ile.(Ufunuo 22:19).

  Kwamfano Maandiko yanasema Mwanamke asivae mavazi yampasayo mwanamume, wala mwanamume asivae mavazi ya mwanamke; KWA MAANA KILA AFANYAYE MAMBO HAYO NI MACHUKIZO KWA BWANA, MUNGU WAKO. (Kumbu.22:5), sasa kwamfano Mwalimu, au muhubiri au mchungaji, akilijua hili na hawafundishi wanafunzi wake , au washirika wake,mambo kama hayo kwa hofu Fulani labda watamchukia, au watamkimbia sasa mtu kama huyu ni sawa na amepunguza Neno katika Maneno ya Mungu na hivyo sehemu yake pia itapunguzwa katika mji ule.

  Kwahiyo tunapaswa tulichukue Neno la Mungu kama lilivyo bila kupunguza makali yake, au kuongeza shuhuda zipinganazo na Neno la Mungu kwa lengo la kuwapotosha watu.  

Ubarikiwe.


Mada zinazoendana:

NENO LA MUNGU KATIKA UTIMILIFU WOTE.

TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.

USIACHE KUJIFUNZA NENO LA MUNGU

MANENO YA MUNGU YANAPINDULIWAJE?

UMEFUNULIWA AKILI?

VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Biblia inasema askofu anapaswa awe mume wa mke mmoja! Je! Wale wasiooa kwa ajili ya injili hawawezi kuwa maaskofu?

1 Timotheo 3:1 Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema.2 Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja,..” 


JIBU: swali zuri, na pia wengi wanachanganyikiwa kuhusu hilo, wakidhani kuwa mtu yeyote anayeitwa askofu ni lazima aoe…lakini unapaswa uelewe kuwa hapo Mtume Paulo alisema hivyo kwa mantiki ipi?, hakuwalenga wale ambao hawajaoa bado hapana, bali aliwalenga wale ambao wanao wake zaidi ya mmoja..kwamba hao ndio hawapaswi kuwa maaskofu, kwasababu ni lazima waonyeshe kielelezo kwanza wao wenyewe katika nyumba zao na ndio waje kuchunga wa nje, sasa kama mtu alikuwa na wake 6 kabla hajaamini na akaingia kwenye ukristo na ukristo unasema mtu anapaswa awe na mke mmoja, sasa unadhani wale atakaowachunga yeye kama askofu atakuwa anacho kielelezo gani? 

Na ndio maana haipaswi mtu yeyote anayeitwa askofu au mchungaji awe na mke zaidi ya mmoja…Lakini haikumaanisha pale kwamba ni lazima kila anayetaka kuwa askofu awe na mke, huo ni uelewa hafifu wa maandiko. Kumbuka mtume Paulo naye hakuwa na mke, lakini alikuwa mwangalizi wa makanisa yote, Kristo naye hakuwa na mke lakini yeye ndiye Askofu wa maaskofu. Hivyo hapo maneno hayo yaliwalenga wale ambao tayari wanao mke zaidi ya mmoja. 

1Wakoritho 7:32 Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;

33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe.

34 Tena iko tofauti hii kati ya mke na mwanamwali. Yeye asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana, apate kuwa mtakatifu mwili na roho. Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mumewe

Ubarikiwe.

Maran atha


Mada zinazoendana:

MATOWASHI NI WAKINA NANI?

JE! NI VIBAYA KUTAJA HUDUMA KWA KUJIPA CHEO? MFANO MIGHTY PROPHET, CHIEF APOSTLE N.K.?

NITAMJUAJE NABII WA UONGO?

MLINZI, NI HABARI GANI ZA USIKU?

BIDII YA MFALME YOSIA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! ni sahihi kwa Mkristo kusherekea siku yake ya kuzaliwa.[Birth day]?

JIBU: Sherehe yoyote ile iwe ni ya kuzaliwa, au mahafali, maadhimisho ya miaka ya ndoa, harusi, kumbukumbu n.k. Biblia haitatoa katazo lolote kufanyika, isipokuwa imetoa katazo tu kwa KARAMU ZA ULAFI.

Tukisema karamu za ulafi tunamaanisha karamu/sherehe zozote zinazovuka mipaka ya Neno la Mungu, kwamfano sherehe zinazochanganyikana na pombe,Disco, miziki ya kidunia, uvaaji mbovu, na mambo yote yafananayo na hayo ambayo ni kunyume na Neno la Mungu, hizo zote ni karamu za ULAFI ambazo biblia imezikataza. Ukisoma..  

1Petro 4: 3 “Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na KARAMU ZA ULAFI, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;”  

Unaona hapo pia ukisoma …  

2 Petro 2: 13 “Wakipatikana na madhara, ambayo ni ujira wa udhalimu wao, wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa; wamekuwa ni mawaa na aibu WAKIFUATA ANASA ZISIZO KIASI KATIKA KARAMU ZAO ZA UPENDO, wafanyapo karamu pamoja nanyi; ”

  Unaona pia hapo karamu/sherehe zenye mambo kama hayo ndani yake ni dhambi kwa mkristo kufanya, lakini ikiwa ni kwa ajili ya kuhitimu, au kuzaliwa, au ndoa, au mahadhimisho unaweza ukasheherekea upendavyo lakini hapo ndio kuzingatia lile neno linalosema Wakolosai 3: 17 “Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”.  

Na ndio maana Bwana YESU alitushauri pale tunapojisikia kufanya karamu au kusheherekea kwa namna yoyote ile tufanye kwa manufaa ya kimbinguni zaidi, yaani kuliko kuwaalika watu wenye cheo, ni vizuri kusheherekea na watu maskini, ili thawabu yetu iwe kubwa mbinguni (Luka 4:12)..Kuliko kukata keki na ndugu zetu au na marafiki zetu tu, ni vema tukaongeza pia kukata na yatima waliokaribu nasi pamoja na wajane.. Ndio karamu yenye harufu nzuri mbele za Mungu.

  Ubarikiwe.


Mada zinazoendana:

JE! SISI KAMA WAKRISTO NI DHAMBI KUSHEHEREKEA KRISMASI?.

JE! NI SAHIHI KWA MKRISTO KUOA/KUOLEWA NA MTU WA IMANI NYINGINE?

NI SAHIHI KUMUITA MARIAMU, MAMA WA MUNGU?

JE! NI SAHIHI KWA MKRISTO KUNING’INIZA PICHA NYUMBANI MWAKO KAMA YA YESU?

USIISHIE KUTAZAMA JUU, ENDELEA MBELE.

KARAMA ILIYO KUU.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! taratibu za kufunga ndoa [yaani harusi] ni agizo la Mungu au ni mapokeo tu ya kibinadamu?

JIBU: Kufunga ndoa ni agizo la Mungu, lakini Harusi ni karamu/sherehe ya Ndoa mpya. Na hizo ni desturi tu ambazo zipo katika mataifa mbalimbali kulingana na chimbuko lao. Hata taifa la Israeli walikuwa na desturi za harusi ukisoma

Yohana 2:1 Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo.
2.2 Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.

Hivyo ikiwa ndoa mpya itaambatana na harusi kwa Mungu hakuna dhambi, wala hakuna maagizo yoyote kwenye biblia kwamba mtu akioa au akiolewa ni lazima afanyiwe harusi au asifanyiwe…Ni jinsi mtu mwenyewe atakavyopenda isipokuwa tu, tumeagizwa lolote tufanyalo kwa Neno au kwa tendo tufanye kwa jina la Yesu Kristo. Ikiwa na maana kuwa hiyo arusi isivuke vigezo vya kikristo.

Ubarikiwe.


Mada zinazoendana:

NDOA NA HARUSI TAKATIFU.

NDOA NA TALAKA:

BIBLIA INAKATAZA KUAPA, LAKINI KATIKA VIFUNGO VYA NDOA?

JE! NI HALALI KUTOA CHETI KWA WAKRISTO WANAOOA?

NINI TOFAUTI KATI YA UZINZI NA UASHERATI?

JE! MBINGUNI KUTAKUWA NA KULA NA KUNYWA?.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! ni halali kwa mtu wa Mungu kutumia njia za uzazi wa mpango,ikiwamo mipira?

JIBU: Biblia haijaeleza moja kwa moja kuhusu suala la uzazi wa mpango aidha utumike au la, kwasababu njia zinazotumika sasa hazikuwepo katikati ya watu wa kale, Lakini ni vizuri kufahamu lengo la kufanya hivyo ni nini, wapo wengine wanafanya hivyo kwasababu ya matatizo ya kiuchumi, wengine kwasababu ya mapungufu ya kimwili, wengine kwasababu ya kuzuia kuathiriwa kwa kazi yake Fulani, na pia wapo wengine ni kwasababu tu za kiasherati/zinaa n.k..

  Hivyo njia nyingi za sasa zitumiwazo kwa uzazi wa mpango zinachukuliwa kwa taswira ya kiasherati kwasababu iko wazi nyingi zinatumiwa hivyo. Lakini ikiwa ni kwa wana ndoa, na dhamira zao zikiwa ni safi mbele za Mungu, na malazi yao ni masafi siku zote, na wanazo sababu za muhimu zinazowalazimu kufanya hivyo labda kwasababu za uleaji wa watoto n.k. Si dhambi wanaweza kutumia. Kwasababu kumbuka pia maandiko yanasema Katika

1Timotheo 5: 8 “Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini”.

  Unaona hapo? Uzaaji wa watoto usio na mpango, hususani pale usipokuwa na uwezo wa kuwalea, ni sawa na umeikana Imani. Hivyo ni vizuri kama wewe ni mwanandoa, ukae chini katika maombi na kumuuliza Mungu, na mapatano na mwenzako, na kisha zitumike.

Lakini mambo hayo hayamuhusu mtu asiye mwana-ndoa.

Ubarikiwe.


Mada zinazoendana:

NDOA NA HARUSI TAKATIFU.

JE! NI HALALI KUTOA CHETI KWA WAKRISTO WANAOOANA?

JE! KUFANYA MASTURBATION (PUNYETO) NI DHAMBI?

MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.

WATU WASIOJIZUIA.

MWANZI ULIOPONDEKA.


Rudi Nyumbani:

 

Print this post

Kunena kwa lugha kukoje?

KUNENA KWA LUGHA. 

Kuna aina nyingi za lugha, zipo lugha za wanadamu na lugha za malaika, lugha za wanadamu ndio kama hizi tunazozifahamu na kuzizungumza; Kiswahili, kingereza, kiarabu, kizulu n.k..Na lugha za malaika nazo zipo nyingi, hatuwezi tukazielewa kwa upeo wetu wa kibinadamu.

 1Wakoritho 13: 1 “Nijaposema kwa LUGHA ZA WANADAMU na ZA MALAIKA, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao”.

 Sasa moja ya ishara kubwa kati ya nyingi ambayo Bwana aliichagua siku ile ya Pentekoste ijidhihirishe kama ushahidi kuwa Roho Mtakatifu amemwagwa juu ya watu wake ni ISHARA YA LUGHA. Kumbuka: angependa kutumia ishara nyingine pia angeweza, kama watu kutabiri, watu kung’aa nyuso zao kama Musa, n.k lakini yeye alipenda kutumia ishara ya lugha, kama tu alivyotumia ishara ya lugha kuwatapanya watu waliokuwa wanaujenga mnara wa Babeli. Sasa kilichotokea siku ile ya Pentekoste baada ya Roho Mtakatifu kushuka juu ya watu, watu kujikuta wanapata msukumo wa ajabu(au uwezo wa ajabu) kuzungumza lugha wasizozijua.

Na lugha hizo hazikuwa lugha za MALAIKA hapana! Bali zilikuwa ni lugha za WANADAMU. Ili tuelewe vizuri tujifunze kwa mfano ufuatao. Petro mwanafunzi wa Yesu alikuwa anaongea ki-galilaya lakini hawezi kuongea kiyunani, Roho aliposhuka juu yake siku ile ya Pentekoste, alisikia uwezo na msukumo wa ajabu ndani yake, na kujikuta anamtukuza Mungu kwa lugha nyingine pasipo kujua ile lugha anayoizungumza ni ya kiyunani. Na kadhalika Mathayo naye lugha yake ya asili ni ki-galilaya lakini nguvu ilipomjia akajikuta anamtukuza Mungu kwa lugha ya kiarabu, pasipo kujua kwamba anaongea kiarabu..na vivyo hivyo kwa wanafunzi wengine wote na wale wote waliokuwepo siku ile ya Pentekoste. 

Sasa wao pasipo kujua kwamba zile lugha wanazoziongea ni lugha halisi, wale watu wa nje ndio waliowasikia wanazungumza kwa lugha zao, labda tuseme kuliwepo na wayunani pale ghafla wanamsikia mtu akimtukuza Mungu huko ghorofani kwa lugha ya kiyunani, na hali anajua kabisa pale mjini wayunani wenzake ni wa kubahatisha, na Kadhalika kama palikuwepo na muarabu kafika pale mjini Yerusalemu kwa biashara yake, ghafla anamsikia mtu huko ghorofani anapaza sauti akimshukuru Mungu kwa lugha yake ya kiarabu, tena kiarabu kile cha ndani kabisa na hali anajua kabisa katika huo mji hakuna waarabu wenzake wengi, na cha ajabu akimtazama mtu anayenena hana hata dalili ya kufahamu tamaduni za kiarabu,ni wazi kabisa ataishia kuduwaa tu!. Sasa ndicho kilichotokea siku ya Pentekoste.

Ni mfano leo usafiri na kwenda Kijiji kimoja huko China, na wakati umefika huko, unamsikia mchina mmoja huko anaongea kichaga kile cha ndani kabisa, wakati unajiuliza hilo ni nini, unasikia mchina mwingine huko anamsifu Mungu kwa kimakonde! Bila shaka utashangaa na kujiuliza hawa wote si ni wachina! Imekuwaje basi mimi kuwasikia wakizungumza kwa lugha zetu za asili za kiafrika?. Sasa hiyo ishara ya lugha Bwana Yesu aliiachia siku ile ya Pentekoste ili watu wote wajue kwamba kuna kitu kipya kimemwagwa duniani (nacho si kingine Zaidi ya Roho Mtakatifu). Lakini Roho Mtakatifu mwenyewe sio lugha, kama tulivyosema hiyo ni ishara Roho Mtakatifu aliyoichagua tu kujidhihirisha yeye, anaweza akatumia ishara nyingine tofauti na hiyo, mtu akishindwa kuelewa hilo, atadhani kuwa asiponena kwa lugha basi hana Roho Mtakatifu ndani yake, Na ndio hapo inapelekea kulazimisha kufanya hivyo na asiponena mwisho wake anaishia kunena kwa akili zake tu, na sio kwa jinsi Roho anavyowajalia.

Kunena kwa lugha ni karama Roho wa Mungu anayoitoa kama yeye apendavyo na sio kila mtu anaweza kuwa nayo. Sasa nini kinatokea Roho Mtakatifu anapoingia ndani ya Mtu?Roho Mtakatifu anapoingia ndani ya mtu, hali atakayoisikia mtu yule kwa mara ya kwanza sio kunena kwa lugha, kwasababu lugha kazi yake ni ishara kwa watu wa nje wasioamini, kuwaonyesha kwamba kuna jambo jipya limeshuka juu ya huyo mtu, lakini kama Roho ameshuka juu ya mtu na yule mtu yupo peke yake, hakuna lugha hapo!.

 Jambo la kwanza atakalolisikia yule mtu ndani yake baada ya Roho Mtakatifu kushuka ni badiliko kubwa ndani ya moyo wake, atajisikia anaichukia dhambi, na maisha yake ya zamani, atajikuta anatamani na anakuwa na kiu ya KUWA MTAKATIFU, na huo ndio uthibitisho wa kwanza na sio kutamani kunena kwa lugha, au kuona maono, au kutabiri.Uthibitisho wa ROHO YA UASHERATI ndani ya mtu ni UASHERATI sio kuzungumza kingereza, vivyo hivyo uthibitisho wa ROHO YA MAUAJI ndani ya mtu ni MAUAJI anayoyafanya na sio elimu yake, huwezi kusema elimu ya mtu ndio uthibitisho wa Roho ya mauaji iliyopo ndani ya huyo mtu, Vivyo hivyo na ROHO MTAKATIFU kama jina lake lilivyo “MTAKATIFU” uthibitisho kwamba mtu yule anaye Roho Mtakatifu ndani yake ni UTAKATIFU ANAOUISHI, na sio lugha anazoziongea, Kwahiyo hizi lugha, ni ISHARA TU na Bwana anachagua nani wa kumpa hii na nani wa kumpa ile.

Hivyo jambo la kwanza mtu akipokea Roho Mtakatifu ni kuanza kuona ile kiu ya kupenda dhambi inakufa, anaanza kupenda kuwa MTAKATIFU na kuishi maisha ya kumcha Mungu, Sasa vya ziada ndio hizo ishara nyingine zinafuatana naye, labda anaona MAONO, lakini haneni kwa lugha, sasa mtu kama huyo anaweza akadhani hajapokea Roho Mtakatifu kwasababu tu hajanena kwa lugha, hajui kwamba Roho Mtakatifu yupo ndani yake, na amemchagulia ishara ya Maono iambatane naye badala ya ishara ya lugha.

Mwingine katubu dhambi na ghafla anaona kiu ya kupenda dhambi inakufa anatamani na anaanza kuishi maisha ya UTAKATIFU, lakini anajigundua kila anapolala anaota ndoto na zile ndoto zinakuja kutokea kama zilivyo, lakini hajanena kwa lugha, naye huyo Roho kapenda kumpa kipawa cha NDOTO badala ya lugha, Vivyo hivyo na wengine watapewa, karama za uponyaji badala ya LUGHA, wengine watapewa karama za unabii badala ya lugha, wengine watapewa karama neno la faraja, wengine karama za neno la maarifa, wengine watapewa uinjilisti badala ya lugha, wengine watapewa lugha badala ya uinjilisti, na maono, wengine waalimu, wengine wachungaji, N.k na wengine watapewa karama mbili mbili, wengine tatu tatu, wengine moja tu n.k Lakini wote hawatenena kwa lugha wala wote hawatakuwa manabii n.k na ndio maana Mtume Paulo ililisema hilo katika.. 

1Wakoritho 12: 28 “ Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha.29 Je! Wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni waalimu? Wote wanatenda miujiza?30 Wote wana karama za kuponya wagonjwa? WOTE WANENA KWA LUGHA? Wote wafasiri?”

Umeona hapo? Sio wote watanena kwa lugha. Hivyo usikazane kutafuta kunena kwa lugha, kama hiyo karama haipo ndani yako,[sisemi kama ukimwomba Mungu hatakupa,] lakini ikiwa haipo ndani yako zidi kujaa Roho Mtakatifu, na baki katika nafasi uliyoitiwa. 

Ubarikiwe.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Print this post

Je! ni vema kwa mkristo kwenda hospitali au kutumia miti shamba anapougua?

JIBU: Kama tukisoma Marko 2: 17 tunaweza kuona Bwana Yesu aliwaambia watoza ushuru na Mafarisayo maneno haya, “…WENYE AFYA HAWAHITAJI TABIBU, BALI WALIO HAWAWEZI; sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.” Bwana alitumia mfano huo wa kidunia kueleza mambo ya rohoni, akimaanisha kuwa ni jambo la kawaida kwa mtu aliye mgonjwa kumtafuta daktari amuhudumie afya yake. Kwasasa tunaweza kusema kwenda hospitali. Hivyo mkristo kuumwa na kwenda hospitali hafanyi kosa lolote, maadamu anafanya tendo ambalo halimwathiri Imani yake.  

Kadhalika pia anaweza kutumia aina zozote za mimea ambazo anaweza kuona zitamsaidia kuimarisha afya ya mwili wake, mwingine anaona kutumia mwarobaini, au alovera ni nafuu zaidi kwake kuliko dawa za hospitalini kwasababu pia dawa nyingi za hospitalini zinatengenezwa kutoka kwenye hiyohiyo mimea ya asili. Lakini la kuzingatia mkristo anapotumia dawa hizo, hapaswi kuzihusisha na ibada zozote za Kiroho isipokuwa kwa Mungu wake.  

Kwamfano mtu anapewa dawa za miti shamba labda mwarobaini, halafu anaambiwa achinje kuku, au aweke uvunguni, au aseme maneno Fulani au afanye kafara kisha ndio anywe, sasa hizo tayari ni ibada za sanamu ambazo ni machukizo makubwa mbele za Mungu. Lakini mtu akiwa na mwarobaini wake nyumbani, akatengeneza akanywa kwa jina la YESU hakuna tatizo lolote. Akizingatia tu lile Neno katika

Wakolosai 3: 17 “Na kila mfanyalo, KWA NENO au KWA TENDO, fanyeni yote KATIKA JINA LA BWANA YESU, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”.

Lakini pia kuna mwingine kwa Imani yake anaamini kuwa Mungu ndiye mponyaji wake kwa asilimia zote pasipo kupitia nyenzo yeyote, hivyo anaposikia kuumwa anaamini kuwa Mungu atamponya pasipo kwenda hospitali, akiliamini lile Neno (Mathayo 8:17 “…Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu, Na kuyachukua magonjwa yetu.” )

hivyo mtu wa namna hii pia hafanyi kosa, Kwasababu Mungu ni yule yule anayeweza kumponya mtu kwa kupitia daktari au pasipo daktari..Hapo ni kulingana na Imani ya mtu kwa Mungu wake.  

Ubarikiwe.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

YESU MPONYAJI.

HADITHI ZA KIZEE.

MADARAKA YA WAKATI MKAMILIFU.

MKUU WA GIZA.

NGUVU ZA ZAMANI ZIJAZO:

PENGINE MUNGU ALISHASEMA NAWE KWA NJIA HII.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post