Jina kuu la Bwana na Mwokozi wetu Yesu KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze biblia.
Sarepta ulikuwa ni mji mdogo uliokuwepo nje kidogo mwa nchi ya Israeli, katika Taifa la Lebanoni.
Katika biblia tunasoma kipindi Nabii Eliya amefunga Mbingu miaka mitatu na nusu kwa Neno la Bwana, aliongozwa aende mpaka mji huu wa Sarepta ambapo kulikuwepo na Mwanamke ambaye Bwana alikuwa amemwandaa ili amlishe.
Mungu angeweza kumshushia Nabii Eliya mana kutoka mbinguni na akala akashiba, lakini hakufanya hivyo, bali alitumia watu na viumbe kumlisha wakati dunia nzima inapitia njaa. Mara ya kwanza alitumia kunguru (1Wafalme 17:4), na mara ya pili akatumia Mtu (ambaye ndiye huyu mwanamke wa Sarepta).
Sasa huyu mwanamke wa Sarepta alikuwa na tabia ya kipekee ambayo kupitia hiyo tunaweza kuvuna hekima ya mafanikio ya kimwili na kiroho.
Inawezekana mambo yako hayaendi sawa, inawezekana unapitia kipindi kigumu sana cha mbingu kufungwa juu yako, kila mahali unapogusa hapaendi, kila unalojaribu halifanikiwi, kila mahali ni ukame!!
Kama unapitia hii hali, basi usiende kutafuta kuombewa! Bali fanya kama alivyofanya huyu mwanamke wa Sarepta.
Ukifanya kama alivyofanya huyu mwanamke wa Sarepta, basi kipindi ambacho wengine watakuwa wanalia matatizo na dhiki, wewe hutakuwa katika hayo matatizo wala hizo dhiki..
Sasa ni kitu gani alichokifanya huyu mwanamke mpaka kufikia hatua ya yeye kuishi vizuri katikati ya vipindi vya shida na njaa na mauti?
Hebu tusome habari yake kwa ufupi kisha tujifunze tabia aliyokuwa nayo.
1Wafalme 17:7 “Ikawa, baada ya siku kupita, kile kijito kikakatika, kwa sababu mvua haikunyesha katika nchi.
8 Neno la Bwana likamjia, kusema,
9 Ondoka, uende Sarepta, ulio mji wa Sidoni, ukae huko. Tazama, nimemwagiza mwanamke mjane wa huko akulishe
10 Basi, akaondoka, akaenda Sarepta; hata alipofika langoni pa mji, kumbe! Mwanamke mjane alikuwako akiokota kuni; akamwita, akamwambia, Niletee, nakuomba, maji kidogo chomboni nipate kunywa.
11 Alipokuwa akienda kuleta, akamwita akasema, Niletee, nakuomba, kipande cha mkate mkononi mwako.
12 Naye akasema, Kama Bwana, Mungu wako, aishivyo, sina mkate, ila konzi ya unga katika pipa, na mafuta kidogo katika chupa; nami ninaokota kuni mbili ili niingie nijipikie nafsi yangu na mwanangu, tuule tukafe.
13 Eliya akamwambia, Usiogope; enenda ukafanye kama ulivyosema; lakini unifanyie kwanza mkate mdogo ukaniletee; kisha ujifanyie nafsi yako na mwanao.
14 Kwa kuwa Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Lile pipa la unga halitapunguka, wala ile chupa ya mafuta haitaisha, hata siku ile Bwana atakapoleta mvua juu ya nchi.
15 Basi akaenda, akafanya kama alivyosema Eliya; na yeye mwenyewe, na Eliya, na nyumba yake, wakala siku nyingi.
16 Lile pipa la unga halikupunguka, wala ile chupa ya mafuta haikuisha, sawasawa na neno la Bwana alilolinena kwa kinywa cha Eliya”.
Umeona tabia ya huyu mwanamke?.. alikubali kutoa chakula chake kipindi ambacho amebakiwa nacho kidogo!!.. kipindi ambacho hajui kesho itakuwaje.. Alikubali kuweka sababu zake kando ilimradi tu aone Neno la Mungu linazidi kusambaa kupitia mtumishi wake, aliona mtu wa Mungu,au kazi ya Mungu ina thamani mara nyingi zaidi ya kazi zake yeye au uwepo wake yeye na mwanae.
Hivyo akajitoa sadaka maisha yake.. akijua kuwa hata kama atakufa na njaa yeye na mwanae lakini atakuwa na thawabu kubwa mbinguni, atakuwa hajaifanya kazi ya Mungu isimame… Hicho ndicho kilichomfanya Mungu ayaangalie matatizo yake, na kumfungulia Mbingu wakati wengine bado mbingu zimefungwa.
Na Mungu ni yeye Yule jana, leo na hata milele hajabadilika (Waebrania 13:8).. Ukitaka Bwana ayaangalie mambo yako, basi wewe weka kando mambo yako na shida zako, na anza kujishughulisha na mambo yake..
Hii ndio shida kubwa inayowakabili wakristo wengi, huwa wanatanguliza matatizo yao mbele za Mungu na huku hawataki kumjali Mungu katika maisha yao.. wanatafuta kuombewa mambo yao yakae sawa, lakini kutafuta kuyaweka sawa mambo ya Mungu hawataki..
Watamwambia Mungu, tazama mwanangu hajala, mwanangu hana ada ya shule, mwanangu yuko hivi yuko vile, mimi sina chakula, mimi sina kazi, mimi sina hiki au kile..(wanakuwa ni watu wa kujijali wao) na hawana habari na mambo ya Mungu au kazi ya Mungu, wakidhani kuwa kwasababu Mungu ni muweza wa mambo yote, hivyo hahitaji kupewa chochote au kufanyiwa chochote.
Ni kweli yeye ni mweza wa yote, na hahitaji kufanyiwa chochote, lakini wakati mwingine anafanya hivyo kutujaribu upendo wetu kwake,.. angeweza kumshushia Eliya Mana kama alivyowashushiwa wana wa Israeli jangwani lakini hakufanya hivyo kwa Eliya, bali alimpeleka Eliya kwa huyu mwanamke, ili aujaribu upendo wake kwake.
Wengi wetu hatujui kuwa Mungu anafurahiwa sana na matoleo yetu kipindi ambacho hatuna kitu zaidi ya kipindi ambacho tuna kila kitu. Utasema hilo tunalithibitisha vipi kimaandiko?… Rejea ile habari ya Yule mwanamke mjane aliyetoa riziki yake yote katika sanduku la hazina…Utaona baada ya kutoa Bwana Yesu anamsifia, na tena anasema katoa zaidi ya wote, kwasababu hao wengine walitoa katika sehemu zilizowazidi…
Marko 12:41 “Naye akaketi kulielekea sanduku la hazina, akatazama jinsi mkutano watiavyo mapesa katika sanduku. Matajiri wengi wakatia mengi.
42 Akaja mwanamke mmoja, mjane, maskini, akatia senti mbili, kiasi cha nusu pesa.
43 Akawaita wanafunzi wake, akawaambia, Amin, nawaambia, Huyu mjane maskini ametia zaidi kuliko wote wanaotia katika sanduku la hazina;
44 maana hao wote walitia baadhi ya mali iliyowazidi; bali huyu katika umaskini wake ametia vyote alivyokuwa navyo, ndiyo riziki yake yote pia”
Kwaufupi huyu mjane, hakubakiwa na kitu, huenda alijua baada ya kutoa vile atakaa siku kadhaa na njaa… lakini akiwa katika hiyo hali, Bwana Yesu alimsifia.. huenda baada ya pale, alishangaa kwa milango ya Baraka iliyofululiza mbele yake.
Na wewe ukitaka Mbingu zifunguke juu yako, usianze kutoa visababu katika kumtolea Mungu, usianze kusema sijalipa kodi, usianze kusema sina chakula, sijalipa ada, sijafanya hiki, sijafanya kile, ngoja nikusanye kidogo nitakapopata nitatoa.. Ni kweli siku ukipata na kutoa basi Bwana atakubariki, hataacha kukubariki!!!… lakini hujui tarehe wala siku mambo yako yatakapokuwa sawa..
Walikuwepo wanawake wengi sana kipindi cha Eliya wenye matatizo ya chakula kama huyu wa Sarepta, ambao na wenyewe pengine walikuwa wanafunga na kuomba Mungu awape riziki kwasababu ya ukame…lakini Eliya hakutumwa kwao kwasababu hizo hizo, huenda angeenda kwao na kuwaambia wampe yeye kwanza mkate, wangemfukuza kwa mawe, tena wangemtukana…
Wangesema hatuwezi kuona watoto wetu wanakufa njaa halafu tukupe wewe mzee chakula chao, wangetumia hata na maandiko kuthibitisha hilo.. Kwaufupi kila mmoja angeeleza shida zake na sababu zake kwanini asingempa Eliya mkate.. Ndicho Bwana Yesu alichokisema katika Luka 4:25.
Luka 4:25 “Lakini, kwa hakika nawaambia, Palikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli zamani za Eliya, wakati mbingu zilipofungwa miaka mitatu na miezi sita, njaa kuu ikaingia nchi nzima;
26 wala Eliya hakutumwa kwa mmojawapo, ila kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni”.
Na sisi pia tukitaka mbingu zifunguke juu yetu kabla ya wakati wake, hatuna budi kumjali Mungu zaidi ya kujijali sisi, hatuna budi kuyatazama mambo ya Mungu zaidi kuliko mambo yetu. Hii ni moja ya kanuni za Mafanikio.
Bwana Yesu atubariki.
Maran atha.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?
Kwanini wajane vijana hawakupaswa kuandikwa?
NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.
MWANAMKE, BINTI, MAMA. (Sehemu ya 3)
Nini maana ya kumpenda Bwana kwa moyo,roho, akili na nguvu zetu zote?
Makanda ni neno lingine la KAPU.
Ambalo hutumika kuhifadhi au kubebea vitu mbalimbali hususani vyakula au nafaka.
Katika biblia Neno hilo utakutana nalo katika vifungu kadha wa kadha, mfano wapo ni hivyo ni hivi;
Mathayo 15:37
[37]Wakala wote wakashiba; wakayaokota masazo ya vipande vya mikate makanda saba, yamejaa.
Marko 8:8
[8]Wakala, wakashiba, wakakusanya mabaki ya vipande vya mikate makanda saba.
Luka 16:6-7
[6]Akasema, Vipimo mia vya mafuta. Akamwambia, Twaa hati yako, keti upesi, andika hamsini.
[7]Kisha akamwambia mwingine, Na wewe wawiwani? Akasema, Makanda mia ya ngano. Akamwambia, Twaa hati yako, andika themanini.
Luka 16:5-7
[5]Akawaita wadeni wa bwana wake, kila mmoja; akamwambia wa kwanza, Wawiwani na bwana wangu?
[6]Akasema, Vipimo mia vya mafuta. Akamwambia, Twaa hati yako, keti upesi, andika hamsini.
[7]Kisha akamwambia mwingine, Na wewe wawiwani? Akasema, Makanda mia ya ngano. Akamwambia, Twaa hati yako, andika themanini.
Ni nini twapaswa kujua nyuma ya makanda ya mikate waliyoyakusanya wanafunzi wa Yesu ambayo baadaye waliyasahau mpaka wakaanza kulalamikiana na kulaumiana..Hadi Yesu akawakemea..(Marko 8:14-21)
Ni kwamba waliweka mioyo yao katika makapu yao, katika hazina zao, hata waliposahau wakapaniki.
Ni hali iliyopo sasa miongoni mwetu sisi, tuliookolewa. Tunafikiri sana makapu yetu yana nini, kwa miezi 10 mbele, kwa miaka 3 ijayo..na pale tunapopungukiwa hata uhusiano wetu na Mungu unakufa..Lakini Bwana Yesu anatuambia tusiwe wasiwasi, wala tusiyasumbukie hayo..bali tuutafuta kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine atatuzidishia..kwasababu maisha ni zaidi ya chakula.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Ila atapewa mara mia sasa,Ndugu wake(Marko 10:30)
Mtu akizaa watoto mia, lakini nafsi yake haikushiba mema;
MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA- Sehemu ya 2.
WAKINYAMAZA HAWA, MAWE YATAPIGA KELELE.
Ulishawahi kujiuliza ni nini Mungu anafundisha wana wa Israeli nyuma ya agizo hili? Tunalolisoma katika Kumbukumbu 22:6
“Kiota cha ndege kikitukia kuwa mbele yako njiani, katika mti wo wote, au chini, chenye makinda au mayai, naye koo ameatamia juu ya makinda, au juu ya mayai, usimtwae yule koo pamoja na makinda; 7 sharti umwache yule koo aende zake, lakini makinda waweza kuyatwaa uwe nayo; ili upate kufanikiwa, ufanye siku zako kuwa nyingi”.
Bwana aliwapa agizo, endapo mtu yeyote akipita, njiani au karibu na kichaka, kisha akakutana na kiota cha ndege koo kimelala pale karibuni, kinatekeka kirahisi, kiasi kwamba unaweza kuwachukua wote, bila nguvu yoyote.Basi hapo, walipewa sharti, wasiwe na tamaa ya kuwachukua wote, bali wamwache koo aende zake akaendeleze uzao, lakini wale makinda anaweza kuwachukua na kuwafanya wake. Hivyo kwa kitendo hicho tu, mtu anajiongezea siku za kuishi duniani.
Ufunuo wake ni upi Katika Ukristo na katika maisha?
1) Katika Maisha.
Ni mara ngapi tunaona watoto wa jamaa zetu, wamekuwa mayatima, au wazazi wao wapo katika hali ya kutojiweza kupitiliza, mpaka wanashindwa kuwamudu watoto wao, lakini sisi tunapita hatuna muda nao kisa tu sio sisi tuliowazaa . Tunawaona watoto wale wakiangamia pamoja na wazazi wao. Bwana anatushauri, tusifanye hivyo, ni heri tusiwajali wale wazazi, tuwaache, tusiwape kitu chochote, lakini wale watoto tuwahurumie, kwani tukifanya hivyo, Mungu atatubariki na kutuongezea siku za kuishi duniani.
Watu wengi tunadhani, kuwaheshimu tu wazazi, ndio tunapata siku nyingi za kuishi, lakini ukweli ni kwamba, ukiwajali pia watoto wa asiyejiweza, utajiongezea siku pia za kuishi duniani.
2) Katika ukristo.
Vilevile katika ukristo. Ipo mikusanyika mingi, Yapo makanisa mengi, zipo huduma nyingi, ambazo haziwaweki watu katika mstari wa wokovu wa kweli, viongozi wao ni vipofu, hivyo na wale wanaoongozwa pia watakuwa ni vipofu, na mwisho wa siku wote watatumbukia shimoni. Sasa ikiwa wewe ni mchungaji au mkristo, na unaona mwenzako mahali alipo anapotezwa..Usikae kimya, na kusema wale sio washirika wangu, au wale sio wa dhehebu langu, au wale sio wa dini yetu..Bali unapaswa kuwaeleza ukweli, uwavute katika mahali sahihi ili uokoe roho zao..
Yawezekana ikawa ni ngumu kumgeuza kiongozi, hivyo usihangaike naye sana ikiwa utashindwa kumfikia, lakini wale makinda hakikisha unawajuza njia sahihi. Hiyo itakuongezea siku zako za kuishi hapa duniani.
Katika siku hizi za mwisho, watu wengi wamewekwa sehemu za hatari, wengine wameaminishwa katika watu, wengine vitu, wengine katika dini, wengine taasisi..lakini Kristo hayupo kabisa mioyoni mwao. Hawamjui, hawalifahamu Neno, hawajui nyakati wanazoishi, dini walizopo ni za kipagani. Sasa hii ni hatari sana, tunapoona wakiendelea katika kudanganywa na viongozi wao ambao wameshindwa kutimiza wajibu wao. Hivyo sisi tuwe wa kwanza kulihubiria hili kundi la Mungu, litoke huko lirudi kwenye Neno.
Bwana atusaidie shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
KOIKOI ANGANI AJUA NYAKATI ZAKE ZILIZOAMRIWA.
MISTARI YA BIBLIA KUHUSU WATOTO.
NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?
Watu wenye ulemavu wa akili, wataenda mbinguni?
Afadhali mtu akutwe na dubu aliyenyang’anywa watoto wake.
MTEGO HUTEGWA BURE, MBELE YA MACHO YA NDEGE YE YOTE.
Biblia ina Aya ngapi?
Jibu: “Sura, na Mlango” ni Neno moja. Biblia ni mkusanyiko wa vitabu 66, na kila kitabu kina milango yake (sura zake), na kila sura zina aya zake, na kila aya ina mistari yake.
Kwamfano kitabu cha kwanza cha Mwanzo kina Sura hamsini (50), na kila Sura ina mistari yake.. Kwamfano Sura ya kwanza ya kitabu cha Mwanzo ina mistari 31.
Kwahiyo tukiuliza biblia ina Sura ngapi, jibu lake ni kuwa ina sura nyingi kufuatana na Vitabu vyake. Jumla ya sura zilizopo katika vitabu vya Agano la kale ni 929, na sura zilizopo katika vitabu vya Agano jipya ni 260, Hivyo jumla ya milango/sura zote za vitabu vyote vya biblia ni 1,189.
Je unafahamu kuwa huwezi kuielewa biblia kama hujapokea Roho Mtakatifu?.. Ili uielewe biblia ni lazima umpate Roho Mtakatifu na kanuni ya kumpokea Roho Mtakatifu ni kumwamini Yesu Kristo kwanza kama Bwana na Mwokozi wa maisha yako, na kisha kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha kabisa, na baada ya hapo kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana Yesu Kristo na hapo Roho Mtakatifu atakuja juu yako.
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.
40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi”
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?
Nini maana ya tumeumbwa kwa mfano na sura ya Mungu?
Je ni kweli ilikuwa desturi ya Bwana kuishika sabato?(Luka 4:16)
Shalom
Hii ni sehemu ya pili ya maswali na majibu yahusuyo ndoa.. Sehemu ya Kwanza unaweza kuisoma kupitia link hii >> MASWALI-NDOA
SWALI 01: Je Mkristo anaruhusiwa kuoa mtu wa Imani nyingine? Yaani akafunga naye ndoa tu, na kila mmoja akaendelea na imani yake.
Jibu: Ndoa ya kikristo ni ndio inayohusisha Imani moja, Bwana mmoja, Roho mmoja, tumaini moja, Ubatizo mmoja na Mungu mmoja..
Waefeso 4:3 “na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
4 Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.
5 Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja.
6 Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote”
Kwahiyo kabla ya Ndoa ni lazima wawili hao wafikie kuwa na imani moja, na ubatizo mmoja na Roho Mmoja na Mungu mmoja, wasipofikia huo umoja basi hiyo sio ndoa ya kikristo.
Sasa nini cha kufanya endapo ikitokea mmoja si wa imani ya kikristo?, Jibu: Huyo ambaye tayari kashaokoka anapaswa amhubirie mwenzake habari za Wokovu kwanza, na aamini na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu (kwaufupi awe mkristo aliyesimama kweli kweli) na baada ya hapo ndipo wafunge ndoa, lakini kumbuka, si abadilike kwasababu tu anataka kuoa au kuolewa!, hapana bali anapaswa apate badiliko la kweli kiasi kwamba hata kama asipoolewa na huyo basi bado Kristo atabaki kuwa Mwokozi wake siku zote za maisha yake.
SWALI 02: Je kuna umuhimu wowote wa kupima afya kabla ya kufunga Ndoa?
Jibu: Ndio upo umuhimu wa kufanya hivyo kama kuna huo ulazima. Kuhakikisha afya zenu zipo sawa kabla ya kufanya lolote, maandiko hayajakataza kufanya hivyo. Na endapo ikitokea mmoja kakutwa na maradhi ambayo yatawafanya wawili hao wasiweze kukutana kimwili!.. Basi hapo ni uchaguzi wa Yule aliye salama, kama upendo wake ni mwingi kama ule wa Kristo, anaweza kuishi na huyo anayemchagua, lakini kamba si hawezi basi yupo huru kutafuta mwingine aliye chaguo lake hafanyi dhambi.
Lakini kama tayari wameshafunga ndoa na mmoja akapata maambukizi ya maradhi hayo basi Yule aliye salama hapaswi kumwacha huyo aliye na maradhi, wataendelea kubaki pamoja siku zote. Vile vile kama mmojawapo kapata ulemavu ambao utamfanya asiweze kabisa kukutana na mwenzake basi Yule aliye mzima pia hapaswi kumwacha mwenzake aliye na udhaifu, siku zote za maisha yake.
SWALI 03: Je wakristo wanaruhusiwa kutoa Ujauzito (Mimba)?
Jibu: Mkristo haruhusiwi kutoa ujauzito (mimba), kwasababu yoyote ile isipokuwa ya kiafya kwa maelezo ya madaktari:
Kwamfano Ikitokea mtoto kafia tumboni hapo ni lazima ile mimba changa iondolewe ili kuokoa maisha ya mama, vile vile ikitokea itilafu katika tumbo la mama, ambayo ili mama awe salama (asipoteze maisha) na kama mama huyo hana imani ya kutosha ya kuamini kuwa anaweza kuishi bila kuitoa na akawa salama, na hivyo akakubali itolewe kufuatia maelezo hayo ya daktari, mama huyo hafanyi dhambi!, kwasababu ya usalama wake mwenyewe.
Lakini sababu nyingine yoyote ya kutoa mimba tofauti na hiyo ya kiafya, ni dhambi!..Kwamfano mwanamke kapata ujauzito bahati mbaya na alikuwa hana mpango wa kuipata hiyo, hapo hapaswi kuutoa huo ujauzito, au kapata ujauzito kwa njia ya ukahaba, hapo hapaswi kuitoa hiyo mimba, atabaki nao mpaka hatua ya kujifungua.
SWALI 04: Ni nani mtu sahihi wa kumpelekea matatizo ya ndoa? Endapo kukitokea kutokuelewana?
Jibu: Endapo kukitokea kutoelewana, ni vizuri kuomba kwa Bwana suluhisho na kurejea biblia kujua ni nini biblia inasema kuhusu hali hiyo, lakini kama bado mwanandoa anahisi anahitaji msaada zaidi basi anapaswa ayafuate makundi yafuatayo.
1: MCHUNGAJI WA KWELI WA BWANA:
Si wachungaji wote ni waaminifu, lakini pia wapo walio wa kweli na waaminifu, watu hao ni kituo bora cha kupata ushauri wa kiMungu na maombezi.
2. MZAZI:
Kama unaye mzazi aliyeokoka basi hicho pia ni kituo bora sana cha kupokea mashauri bora..na yenye msingi mkubwa.
Kamwe usitafute ushauri kwa marafiki, majirani, ndugu wa mbali, au watu usiowajua kuhusiana na mambo ya kindoa.
SWALI 05: Endapo nikagundua baada ya kufunga ndoa Mwenzangu ana matatizo katika uzazi wake (hana uwezo wa kuzaa au kuzalisha)..Je naweza kwenda kupata mtoto nje na kuendelea kuwa naye?
Jibu: Kama mwanandoa mmoja anamatatizo ya uzazi yanayomfanya asiweze kuwa na mtoto, hapo mwanandoa mwingine asiyekuwa na matatizo hayo hapaswi kumwacha Yule mwenye matatizo, wala kuondoka na kwenda kupata mtoto wa kando, atabaki naye huyo huyo siku zote za maisha yake, huku wakimwomba Bwana awafungue!.
Na kama ni mapenzi ya Bwana wao kuwa na watoto, basi Bwana atawapa mtoto haijalishi ni miaka mingapi itapita (Ibrahimu na Sara walipata watoto katika uzee), na Mungu ni Yule Yule hajabadilika.
Lakini pia kama wanaona ahadi za Mungu bado zipo mbali wanaweza ku-adopt mtoto/watoto na kuwalea kama watoto wao.. Vipo vichanga vingi visivyo na wazazi, na mtu akiwalea hao mbele za Mungu ni zaidi hata ya Yule mwenye watoto 100 waliotoka katika uzazi wake.
SWALI 06: Je mkristo anaruhusiwa kupanga uzazi?
Jibu: Ndio wakristo wanaweza kupanga idadi ya watoto wanaotaka kuwa nao!. Biblia haijatoa amri ya kuzaa idadi ya watoto 10 au 50, ni kila mtu atakavyotaka yeye. Lakini imetoa tu angalizo kuwa tuwe watu wenye uwezo wa kuwatunza wakwetu (1Timotheo 5:8 Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.)
Kwahiyo ni lazima Mkristo awe na uwezo wa kuwatunza watoto wake, hivyo ni lazima awe na uzazi wa mpango.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA-1
MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.
TOFAUTI YA MITUME, MANABII, WAINJILISTI, WACHUNGAJI NA WAALIMU NI IPI?
Je ni viatu gani Musa aliambiwa avivue? Vya mwilini au vya rohoni? (Kutoka 3:5).
SWALI: Naomba kufahamu vifungu hivi tunavyovisoma katika Isaya 24:18-20 vinamaana gani?
Isaya 24:18 “Itakuwa kila akimbiaye sauti ya hofu ataanguka katika shimo; na kila apandaye na kutoka shimoni atanaswa na mtego; kwa maana madirisha yaliyo juu yamewekwa wazi, na misingi ya dunia inatikisika. 19 Dunia kuvunjika, inavunjika sana; dunia kupasuka, imepasuka sana; dunia kutikisika, imetikisika sana. 20 Dunia inalewa-lewa kama mlevi, nayo inawaya-waya kama machela; na mzigo wa dhambi zake utailemea; nayo itaanguka, wala haitainuka tena.”
JIBU: Mstari hiyo inatupa picha ya dunia ilivyosasa katika hali ya roho. Imefananishwa na mlevi ambaye amelewa sana, na hivyo hawezi kujimudu tena.
Kama tunavyofahamu, mlevi kabla ya kudondoka mtaroni na kulala hapo hapo, huwa unayumba yumba sana, anapepesuka sana, hatua moja mbele, kumi nyuma, kwenda kulia, kwenda kushoto, hiyo yote ni anatafuta uwiano lakini anaukosa kwasababu kichwa chote kimeshatiwa uzito, kila kitu kilichombele yake anakiona kama kimeguzwa juu chini..
Hivyo kutembea kwake, hakuhusishi tena ubongo, bali uzoefu, na hatari zaidi pale atakapo jikwaa tu kidogo na kuanguka, basi safari yake inakuwa imeishia hapo, hawezi tena kunyanyuka, mpaka atakapolevu asubuhi.
Ndivyo dunia, ilivyo rohoni, nyakati hizi tulizopo, imelevywa sana kwa dhambi za wanadamu, na hivyo imepoteza muhimili wake, tofauti na ilivyokuwa hapo mwanzo, hatushangai sikuhizi kuona, majangwa mengi, ukame uliopitiliza, matetemeko makubwa ya ajabu, magonjwa ya kutisha kama Korona, Ebola kuzuka, mambo ambayo hapo zamani hayakuwepo. Sasa haya yote hayajajizukia hivi hivi tu, bali ni kuleweshwa kwa dunia kwa dhambi zinazoendelea kuwa nyingi.
Ndugu yangu, tupo katika hatari kubwa; Hatari ya “hofu, mashimo, na mitego”, kama hayo maandiko yanavyosema, Ikiwa na maana kama tupo nje ya Kristo tujiandae, kukutana na mambo haya katika maisha yetu. Mtu ambaye hajaokoka, ni kwa neema za Mungu tu anaishi hadi sasa kwenye dunia hii inayowaya-waya kama machela.
Lakini kama tumeokolewa Bwana ameahidi kutuepusha nayo. Kwasababu unyakuo wa kanisa upo karibuni sana kutokea. Na baada ya hapo, ndipo huu ulimwengu utaanguka kabisa..
Ufunuo 6:12 “Nami nikaona, alipoifungua muhuri ya sita, palikuwa na tetemeko kuu la nchi; jua likawa jeusi kama gunia la singa, mwezi wote ukawa kama damu,
13 na nyota zikaanguka juu ya nchi kama vile mtini upukutishavyo mapooza yake, utikiswapo na upepo mwingi.
14 Mbingu zikaondolewa kama ukurasa ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake.
15 Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na mwungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya milima,
16 wakiiambia milima na miamba, Tuangukieni, tusitirini, mbele za uso wake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na hasira ya Mwana-Kondoo.
17 Kwa maana siku iliyo kuu, ya hasira yao, imekuja; naye ni nani awezaye kusimama?.
Je! Unasubiri nini, usimkaribishe maishani mwako? Je! Unauhakika wa kesho? Vipi ikiwa utakufa leo, au Kristo amerudi ghafla sasa hivi utasema nini rafiki.. Kumbuka mipango yote ya mpinga-Kristo ipo tayari, injili imeshahubiriwa duniani kote, dakika tulizonazo ni za nyongeza tu, wakati wowote, parapanda italia, na hali halisi ilivyo tusidhani tuna miaka mingi mbele, muda umeisha kwelikweli, usipumbazwe na mambo ya ulimwengu ukadhani, Yesu harudi hivi karibuni. Ni kwasababu husomi biblia ndio maana unadhani hivyo. Injili ya sasa sio ya kubembelezwa tena, ni mtu mwenyewe kuona na kugeuka, na kuyasalimisha maisha yako. Sio wakati wa kutanga tanga, na maisha bali ni kumtafuta Mungu.
Bwana atusaidie.
Maranatha.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
TABIA ZITAKAZOMTAMBULISHA MPINGA-KRISTO AJAYE.
Je! Bwana Yesu alikunywa kileo mpaka watu wakasema ni mlafi na mlevi? Kulingana na Mathayo 11:19?
Kiburi ni nini?
Kulingana na biblia kiburi “ni hali ya mtu kujiinua kifikra, na kuamini kuwa hahitaji msaada wowote kutoka kwingine”. Hali hii inaambatana na kudhihirisha tabia nyingine ndogo ndogo kama majivuno, matukano, au kuwadharau wengine, au kuwa na ujasiri kupitiliza na hata kukufuru.
Viburi vimegawanyika katika sehemu mbili (2);KIBURI BINAFSI, na KIBURI CHA UZIMA.
KIBURI BINAFSI:
Kiburi binafsi ni kile kinachomfanya mtu aamini kuwa Mawazo yake, au maamuzi yake, au msimamo wake ni thabiti na hauwezi kubadilishwa na yeyote. Mtu mwenye kiburi binafsi hata aambiwe ukweli kiasi gani, au athibitishiwe jambo kiasi gani bado huwa habadiliki. Tayari anachokiamini, au alichokiamua amekiamua!. Mtu mwenye aina hii ya kiburi anakuwa pia ni mbishi na mtu wa mashindano, na anakuwa anajiona yeye ni bora kuliko wengine wote..
Mithali 13:10 “Kiburi huleta mashindano tu; Bali hekima hukaa nao wanaoshauriana”.
Kiburi binafsi kipo kwa Wakristo na kwa wasio waKristo..
Kwa wakristo ni pale ambapo mtu hataki kuambiwa jambo wala kuelekezwa ndani ya kanisa…yeye mawazo yake ndio bora siku zote, au njia zake ndio bora, na zaidi ya yote anakuwa anapenda kuwa juu ya wote, na anawadharau wengine wote…
WaKristo wenye kiburi cha namna hii Bwana amesema anapingana nao…
1Petro 5: 5 “..ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa SABABU MUNGU HUWAPINGA WENYE KIBURI, lakini huwapa wanyenyekevu neema”.
Mithali 29:23 “Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa”.
Kwa wasio wakristo ni pale ambapo mtu hashauriwi na yeyote, juu ya jambo lolote, hata aambiwe vipi anakuwa yupo vile vile, yeye ni wa kuelekeza tu na sio wa kuelekezwa.
KIBURI CHA UZIMA:
Kiburi cha uzima ni kile kinachozungumziwa katika.. 1 Yohana 2:16
“Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na KIBURI CHA UZIMA, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.”
Kiburi cha Uzima ni kiburi kinachompata mtu kutokana na Vitu alivyonavyo, au anavyotegemea kuwa navyo..
Watu wengi wenye mali wanakuwa na hiki kiburi(japokuwa si wote, bali asilimia kubwa).. Wanaona mtu asiyekuwa na mali kama wao hawezi kuwaambia chochote,..kiburi hiki cha mali kinamfanya mtu aone hata Mungu hana maana, Neno la Mungu kwake ni kama habari zilizopitwa na wakati.
Kulifanyia mizaha Neno la Mungu, ni habari ya kawaida kwao…hata wasikie maonyo ya Mungu kiasi gani, kwao ni habari tu upuuzi.. Mioyo yao imeinuka kutokana na Mali au vitu walivyonavyo, wanaona wanaweza kula hata pasipo kumwomba Mungu, wanaweza kuendeleza maisha yao hata pasipo kupiga magoti.. hivyo hawamhitaji Mungu tena..
Kiburi hiki ndio kibaya kuliko vyote, na ndicho kilichozungumziwa sehemu nyingi katika biblia.. naa watu wote wenye hiki kiburi, biblia imeandika hatima yao..
Isaya 2:12 “Kwa maana kutakuwa siku ya Bwana wa majeshi juu ya watu wote WENYE KIBURI NA MAJIVUNO, na juu ya yote yaliyoinuka; nayo yatashushwa chini.”
Mithali 16:5 “Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa Bwana; Hakika, hatakosa adhabu”.
Mithali 8:13 “Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; Kiburi na majivuno, na njia mbovu, Na kinywa cha ukaidi pia nakichukia.”’
Ayubu 40:12 “Mtazame kila mtu mwenye kiburi ukamshushe, Ukawakanyage waovu hapo wasimamapo”.
Zaburi 119:21 “Umewakemea wenye kiburi, Wamelaaniwa waendao mbali na maagizo yako”.
Soma pia Mithali 21:4, Mithali 16:18, Zaburi 31:18, Zaburi 119:51, Mithali 11:2, na Malaki 4:1 biblia imeelezea zaidi juu ya kiburi na madhara yake..
Tujiepushe na kiburi, tunyenyekee chini ya mkono wa Mungu ulio hodari
Bwana akubariki.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.
SWALI 01: Je wakristo tunaruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja?
Jibu: Kwa mujibu wa biblia, Ndoa ya kikristo ni ya mke mmoja na mume mmoja.
Marko 10:6 “Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke.
7 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe;
8 na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja”.
SWALI 02: Je kama mtu alifunga ndoa ya kiserikali, au kimila ndoa hiyo inatambulika mbinguni?..Yaani Mungu anawatambua kama ni mume na mke kihalali?.
Jibu: Ndio! Mbinguni watu hao wanatambulika kama ni mke na mume, ingawa ndoa yao haitakuwa ndoa takatifu ya kikristo..maana yake kuna mambo hawataweza kuyafanya wakiwa katika hiyo hali, mfano wa mambo hayo ni Uchungaji wa kundi, au Uaskofu au Ushemasi. Kwasababu nafasi hizo ni za kuhubiria wengine njia sahihi, hivyo haiwezekani mtu awahubirie wengine wafunge ndoa takatifu ya kikristo wakati yeye mwenyewe hayupo katika ndoa kama hiyo. (Atakuwa mnafiki).(Tito 1:6-7).
Hivyo ni sharti aibariki ndoa yake hiyo na kuwa ndoa takatifu ya kikristo ili asifungwe na baadhi ya mambo.
Mfano wa ndio hizi ambazo ni za kipagani lakini Mungu alikuwa anazitazama ni kama ile ya Herode ambayo Yohana mbatizaji aliikemea.
Marko 6:17 “Kwa maana Herode mwenyewe alikuwa ametuma watu, akamkamata Yohana, akamfunga gerezani, kwa ajili ya Herodia, mkewe Filipo ndugu yake, kwa kuwa amemwoa;
18 kwa sababu Yohana alimwambia Herode, Si halali kwako kuwa na mke wa nduguyo”.
Herode hakuwa mkristo lakini alipomwacha tu mke wake na kwenda kumchukua wa ndugu yake ikawa ni chukizo mbele za Bwana, na vivyo hivyo ndio zote zilizofungwa ambazo zimehusisha mahari pamoja na makubaliano pande zote, basi ndio hizo Mungu anazitazama na zinapaswa pia ziheshimiwe.
SWALI 03: Je Wakristo tunaruhusiwa kutoa talaka?
Jibu: Wakristo hawaruhusiwi kuachana baada ya kuoana. Kwahiyo talaka hairuhusiwi katika ndoa ya kikristo wala mwanaume haruhusiwi kumwacha mke wake katika hali yoyote ile ya udhaifu wa kimwili.
Luka 16:18 “Kila amwachaye mkewe na kumwoa mke mwingine azini; naye amwoaye yeye aliyeachwa na mumewe azini”
SWALI 04: Je! Kama Mwanamke alikuwa ameolewa na mwanaume ambaye tayari alikuwa na Mke, je anapookoka anapaswa amwache huyo mume wake au aendelee naye?.
Jibu: Kulingana na maandiko anapaswa amwache kwasababu tayari huyo alikuwa ni mume wa mtu, hivyo ili maisha yake yawe na ushuhuda na aishi kulingana na Neno ni lazima amwache huyo na akaolewe na mwanaume mwingine ambaye hajaoa (lakini katika Bwana tu), au akae kama alivyo.
SWALI 05: Kama mwanaume alikuwa ameoa wanawake wawili na kashaishi nao muda mrefu na kuzaa nao watoto, lakini ukafika wakati akaokoka je anapaswa amwache mmoja na kuendelea na mwingine au?
Jibu: Kama mwanaume alikuwa amemwoa mwanamke wa kwanza katika ndoa ya kikristo (yaani iliyofungishwa kanisani), na baada ya ndoa hiyo akaongeza mwingine wa pili…Na baadaye akatubu na kuokoka upya!. Hapo hana budi kumwacha huyo wa pili kwasababu alikuwa anafanya uzinzi kulingana na biblia, haijalishi ameishi na huyo mwanamke kwa miaka mingapi, na amepata naye watoto wangapi..anapaswa amwache na kubaki na mke wake wa kwanza.
Lakini kama alimwoa mke wa kwanza kipagani na kulingana na sheria za kipagani akaongeza wa pili, na akaishi nao muda mrefu na wanawake hao wote wawili bado wanahitaji kukaa naye, hapaswi kuwaacha labda mmoja wapo wa wanawake hao aridhie mwenyewe kumwacha kwa hiari yake..
Lakini kama ataendelea kubaki nao mtu huyo ndoa yake hiyo ya wake wawili haitawezi kubarikiwa kanisani, na pia yeye mwenyewe hataweza kuwa Mchungaji, askofu au Mwinjilisti au shemasi bali atakuwa muumini wa kawaida tu, kwasababu biblia inasema ni lazima Askofu awe mume wa mke mmoja..
Tito 1:6 “ikiwa mtu hakushitakiwa neno, naye ni mume wa mke mmoja, ana watoto waaminio, wasioshitakiwa kuwa ni wafisadi wala wasiotii.
7 Maana imempasa askofu awe mtu asiyeshitakiwa neno, kwa kuwa ni wakili wa Mungu; asiwe mtu wa kujipendeza nafsi yake, asiwe mwepesi wa hasira, asiwe mlevi wala mgomvi, asiwe mpenda mapato ya aibu”.
SWALI 06: Je?.Kujifungua kwa operation au kuzalishwa na wakunga wakiume ni halali kwa mwanandoa wa kikristo?.
Jibu: Operesheni ni njia mbadala ya kukiondoa kiumbe tumboni ili kusalimisha maisha ya mama na mtoto..Hivyo kibibla sio dhambi, kwasababu lengo lake ni kuokoa maisha na si lengo lingine.
Vile vile kuzalishwa na mkunga wa jinsia ya kiume si dhambi, kwasababu lengo ni lile lile kusaidia kuokoa maisha,..Katika eneo la uokozi ni eneo ambalo haliangalii jinsia..
Kwasababu pia zipo operesheni kubwa zaidi hata za kuzalisha ambazo zinahusisha kuondoa au kurekebusha viungo vya ndani kabisa vya uzazi wa mwanamke au mwanaume, ambazo operesheni hizo madaktari wake bingwa wanakuwa ni wa jinsia tofauti na wanaofanyiwa, hivyo hapo kama mtu anataka kupona kwa njia hiyo ya matibabu basi hana uchaguzi, wa atakayemfanyia hiyo operesheni.
Kwahiyo katika mazingira kama hayo, jinsia yoyote itakayotumika kumfanyia matibabu huyo mgonjwa wa kikristo, itakuwa si dhambi kwa mkristo huyo anauefanyiwa hiyo operesheni wala kwa yule anayemfanyia.
Shalom.
Usikose sehemu ya pili…
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)
Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?
Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Ni siku nyingine tena yenye neema za Bwana.
Napenda leo tujifunze, ni nini kwanza Bwana anahitaji kuona kwetu kabla ya yeye kuachilia neema zake katika mambo tumwombayo au tuyatafutayo. Embu tusome habari hii kwa mara nyingine tena..
Luka 5:4 “Hata alipokwisha kunena, alimwambia Simoni, Tweka mpaka kilindini, mkashushe nyavu zenu mvue samaki. 5 Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, TUMEFANYA KAZI YA KUCHOSHA USIKU KUCHA, tusipate kitu; lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu. 6 Basi, walipofanya hivyo walipata samaki wengi mno, nyavu zao zikaanza kukatika; 7 wakawapungia mikono washirika wao waliokuwa katika chombo cha pili, waje kuwasaidia; wakaja, wakavijaza vyombo vyote viwili, hata vikataka kuzama. 8 Simoni Petro alipoona hayo, alianguka magotini pa Yesu, akisema, Ondoka kwangu, kwa kuwa mimi ni mtu mwenye dhambi, Bwana. 9 Maana alishikwa na ushangao, yeye na wote waliokuwa pamoja naye, kwa sababu ya wingi wa samaki walioupata;”
Kumbe Bwana Aliona taabu ya Petro usiku ule ilivyokuwa, aliona kule kutafuta kwake usiku kuchwa pasipo mafanikio kulivyokuwa. Alipokuwa anatupa nyavu hapati, anajaribu tena hapati, anasogea sehemu nyingine avue ndio anakosa kabisa mpaka kunapambazuka, haambulii chochote..
Na ndio maana hatushangai jambo la kwanza Yesu alilomwambia Petro mara baada ya kuhubiri kwake, sio Petro twende shambani kwako nikakubariki, au twende tukahubiri injili, ..Hapana bali tweka vilindini ukavue samaki, nikabariki kwanza kwa kile ulichokuwa unakisumbukia kwa muda mrefu..
Hata sasa Kristo ni Yule Yule, kabla ya kutupigisha hatua yoyote kiroho..Hatuna budi kwanza tufanye kazi ya kuchosha usiku kucha, wakati mwingine bila mafanikio yoyote. Watu wengi wanataka Mungu atembee nao kwa viwango vya juu zaidi, lakini hawapo tayari kutaabika kwanza, hawapo tayari kutumika kwanza, katika utumishi wa Mungu kwa muda mrefu, tena ule ambao hauonyeshi matunda yoyote ya awali, lakini tunataka tulale, tuamke kesho tuwe kama Musa.
Huduma nyingi zimekufa kwa namna hii, pale wanapoona hakuna maendeleo au hatua zozote, mwishowe wanakata tamaa ya kumtumikia Mungu, wanavunjika moyo, wanaghahiri, wanakwenda kutafuta shughuli nyingine.
Ndugu, Hatuna budi kufahamu wakati mwingine ni desturi ya Mungu kutuacha kwanza, kwa kipindi Fulani, atupime uaminifu wetu, lakini pia atutengeneze, si kila wakati mambo yote yatakuja papo kwa papo kama wengi wanavyosema, yaweza kuchukua mwaka kama sio miaka, lakini tukivumilia, siku isiyokuwa na jina tutashangaa vile tulivyovitamani, tunavipata kwa urahisi sana, tena bila kusumbukia, wala kuchukua muda kama ilivyokuwa hapo mwanzo, Hatua kama hiyo ukishaifikia, ujue tayari Kristo ameshaona utumishi wako. Lakini lazima tufanye kazi ya kuchosha usiku kucha.
Waweza kusema, jambo kama hili alilifanya siku hiyo tu ya kwanza alipokutana na Petro, lakini utaona mwishoni kabisa mwa huduma yake kuwa nao, baada ya kufufuka kwake, mitume kwa mara nyingine tena walienda kuvua samaki, lakini usiku ule wote hawakupata kitu, ilipofika asubuhi wakamwona Yesu amesimama pwani, ndipo akawauliza wanangu mna kitoweo? Wakasema hapana, akawaambia watupe jarife upande wa kulia watapata (Yohana 21:1-13)
Na kweli samaki ambapo waliwasumbukia usiku kuchwa, wakawapata kwa dakika tano, tena sio kule vilindini bali pale pale pwani. Unataka Mungu aikuze huduma yako, tumika kwanza kwa Bwana, fanya uinjilisti sana, hata kama huoni mtu yeyote ameokoka leo au kesho, wakati wa Bwana ukifika, utaona maajabu. Lakini ukikata tamaa, ukasema sioni chochote, Kristo atasema hustahili kupokea neema.
Wewe ni mwimbaji wa Injili, imba sana, dumu kwa uaminifu kufanya mazoezi, tunga, jifunze kwa moyo wako wote, nyimbo za utakatifu, na kuponya,bila ulegevu, hata kama utaambiwa hujui kuimba,wewe imba sana, hata kama miaka 10 itapita bila kuona kazi yako inamponya mtu..endelea tu, wakati utafika wa Bwana kuachilia neema yake, ataibariki sauti yako, na kuwa msaada ya maelfu ya watu duniani. Sauti itakuwa ni ileile lakini itajazwa neema na nguvu.
Kuna wakati ambao Yesu alipowalazimisha wanafunzi wake wapande mashuani, waende ng’ambo, usiku ule bahari iliwachafukia, lakini maandiko yanatuambia Yesu aliwaona wakitaabika katika kuvuta makasia, lakini hakufanya chochote, mpaka usiku sana wa manane ndio akawafuata akiwa anatembea juu ya maji. Ndipo akawatulizia dhoruba yao. (Marko 6:45-52).. Katika habari ile utajiuliza ni kwanini Yesu awaache wataabike, muda wote ule bila kuchukua hatua..jibu ni kuwa alikuwa anawajengea ushuhuda. Nasi pia Kabla ya Yesu kuzimisha dhoruba katika maisha yetu, na kutupa amani daima, yatupasa tuwe wastahimilivu sasa katika majaribu mengi na shida kwa ajili ya jina lake.
Luka 6:21 “Heri ninyi mlio na njaa sasa, kwa sababu mtashiba. Heri ninyi mliao sasa, kwa sababu mtacheka”.
Jambo lolote la ki-Mungu unalopenda kulifanya, litende kwasababu Mungu anataka kuona kwanza kiu yako kwenye hilo jambo. Vilevile kama unataka Mungu akubariki, penda kutoa bila kutazamia malipo yoyote sasa, toa tu, hata kama ni kwa miaka, unaona unapata hasara tu, usikate tamaa, malipo yake utayaona wakati Fulani mbeleni, Bwana atakapoachilia neema zake.
Hii ni kanuni ya Ki-Mungu, aliitumia kwa, kwa Ibrahimu, Kwa Yusufu, kwa Musa, hata na kwetu pia anaitumia ikiwa tutakubali kwanza kufanya kazi ya kuchosha isiyokuwa na faida kwa muda mrefu.
Usikate tamaa, Bwana awe nawe.
Shalom
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
RUDIA, TENA NA TENA KUMWOMBA MUNGU USIKATE TAMAA.
Je! Siku ilihesabiwaje kabla ya jua na mwezi kuumbwa?
REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.
USHIRIKA WA ROHO MTAKATIFU UKAE NANYI NYOTE.
Biblia inamaanisha nini iliposema “wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa;?
Swali: Kudhili ni nini, au mtu aliyedhiliwa anakuwaje?
Jibu: Kudhili maana yake ni “kushusha chini” Mtu aliyeshushwa chini maana yake “kadhiliwa”.
Katika biblia, maandiko yanaonesha kuwa Mungu huwadhili watu wote wanaojikweza, na wenye kiburi..na wale wote wanaojishusha (yaani wanaojidhili) basi yeye huwakweza, kwa kuwapandisha juu!!.
Mathayo 23:11 “Naye aliye mkubwa wenu atakuwa mtumishi wenu.
12 Na ye yote atakayejikweza, atadhiliwa; na ye yote atakayejidhili, atakwezwa”
Ayubu 40:11 “Mwaga mafuriko ya hasira zako, Ukamtazame kila mtu mwenye kiburi, ukamdhili”.
Zaburi 75:7 “Bali Mungu ndiye ahukumuye; Humdhili huyu na kumwinua huyu”.
Unaweza kusoma pia juu ya Neno hilo katika Zaburi 107:39, na Wafilipi 4:12.
Hivyo na sisi hatuna budi kujishusha siku zote mbele za Mungu, na mbele za watu ili Bwana atukweze.. Kwasababu Mungu hapendi watu wanaojiinua, na wenye majivuno na wanaojiona wao ni bora kuliko wengine wote.
Luka 18:9 “Akawaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote.
10 Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru.
11 Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang’anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru.
12 Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote.
13 Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi.
14 Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa”
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.
NI MAONO YAPI HAYO UNAYOSUBIRIA?
JE UNA MATUMAINI YA KUPATA TENA KILE ULICHOPOTEZA?
Nini maana ya kuabudu malaika? (Wakolosai 2:18)