Category Archive Mafundisho

Kuota upo uwanjani (uwandani)

Nini maana ya kuota upo uwanjani/uwandani?

Jibu: Kiroho uwanja au uwanda unawakilisha mahali pa mapambano.Wanamichezo wote wanaoshindania tuzo, huwa mashindano hayo yanafanyikia viwandani/uwandani.

Kwahiyo unapoota kuwa upo Uwandani na shughuli zako hazihusiani na viwanja, basi fahamu kuwa upo katika mapambano. Na mapambano hayo yanaweza kuwa mazuri au mabaya.
Mapambano Mazuri:

Mapambano mazuri ni yale ya imani, hivyo kama umeokoka vizuri na umesimama kisawasawa na ukapata ndoto au ono unashindana na watu wengi au wachache katika uwanja/uwanda basi fahamu kuwa huenda Mungu anakuonyesha, au kukukumbush vita vya kiimani vilivyopo mbele yako. Hivyo huna budi kupiga mbio..sawasawa na kile kitabu cha Waebrania 12:1

Waebrania 12:1”Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu”.

Soma pia Wafilipi 1:30, Wafilipi 1:27, na 1Wakorintho 9:24.

Lakini kama umejiona upo uwandani peke yako, basi kuna jambo la lingine Mungu anataka kusema nawe. Na hilo huenda ni jambo la tahadhari.

Na tahadhari yenyewe ni kama ile ya Kaini.

Wakati Kaini alipotaka kumwua Habili, alimtenga na kumpeleka uwandani. Na hiyo ni kanuni ya adui anapotaka kumdhuru mtu, anampeleka kwanza uwandani, mahali ambapo hapana watu, wala msaada wa kitu chochote..

Hivyo unapojiona upo uwandani/uwanjani peke yako, au upo na mtu mmoja, basi fahamu kuwa adui anatafuta kukuharibu au kuharibu mambo yako ya kiroho na kimwili.

Mwanzo 4:8 “Kaini akamwambia Habili nduguye, [Twende uwandani].
Ikawa walipokuwapo uwandani, Kaini akamwinukia Habili nduguye, akamwua”.

Kwahiyo uotapo ndoto hiyo, kama hujaokoka zingatia kuokoka, na pia kama una wokovu usio thabiti (maana yake wewe ni vuguvugu) basi zingatia kuwa moto, ili adui asipate nafasi ya kukumaiza.

Lakini kama tayari upo dhani ya wokovu ulio thabiti, basi zingatia Maombi, omba maombi ya kuharibu hila zote na njama za adui, na kutakuwa shwari.
Bwana akubariki.

Tafadhalishea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

KUOTA UPO UCHI.

Kuota unasubiriwa mahali fulani uhutubie, halafu unachelewa.

Kuota mbwa kunamaanisha nini?

UZAO WA NYOKA.

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Rudi nyumbani

Print this post

USILIPIZE KISASI.

Kwanini hatupaswi kujilipiza kisasi?… Kwasababu maandiko yanatufundisha kuwa kisasi ni juu yake yeye atalipa.

Warumi 12:19 “Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, KISASI NI JUU YANGU MIMI; MIMI NITALIPA, ANENA BWANA.

20 Lakini, Adui yako akiwa na njaa, mlishe; akiwa na kiu, mnyweshe; maana ufanyapo hivyo, utampalia makaa ya moto kichwani pake”.

Tabia ya kujilipiza kisasa Bwana Mungu aliikataa tangu Mwanzo na Bwana Yesu akaja kuithibitisha tena katika Mathayo 5.

Tunaona baada ya Kaini kumwua ndugu yake Habili kwasababu ya wivu, Mungu alimlaani Kaini kwa kosa lile..

Lakini Mungu hakumwua Kaini bali alimlaani juu ya ardhi kwamba ataendelea kuishi lakini ardhi itamkataa… Kila kilimo atakachokifanya juu ya ardhi hakitafanikiwa, ndio maana baada ya pale hatuoni Kaini na uzao wake wakiendelea na kazi yake ya ukulima badala yake tunasoma wanaanza kutengeneza vyuma, na wapiga filimbi (Mwanzo 4:17-22).

Sasa baada ya Bwana Mungu kumlaani Kaini alijua kabisa kuna watu watakuja kusikia habari zake kwamba ni mwuaji, na pia kalaaniwa na Mungu, hivyo watataka wajichukulie hukumu aidha ya kumwua au kumnyanyasa…

Sasa Mungu kwa kulijua hilo, akamwekea Kaini alama, ili kila mtu atakayemwona asimguse…

Na alama hiyo ikaendelea kuwepo juu ya Kaini na uzao wake, iliyowatofautisha uzao wa Kaini na uzao mwingine.

Na Bwana akasema mtu atakayemwua Kaini, basi atalipwa kisasi mara 7,

Mwanzo 4:13 “Kaini akamwambia BWANA, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.

14 Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; hata itakuwa kila anionaye ataniua.

15 BWANA akamwambia, Kwa sababu hiyo ye yote atakayemwua Kaini atalipizwa kisasi mara saba. BWANA akamtia Kaini alama, mtu amwonaye asije akampiga”

Hivyo watu walivyosikia hivyo wakaogopa kumnyooshea mikono yao Kaini, kwasababu walijua kuna adhabu kubwa sana katika kufanya hayo…

Umeona?..Kumbe kisasi na hasira ndani ya maisha ya mtu ni machukizo makubwa sana mbele za Mungu..
Ndivyo maandiko yanasema…

Mithali 24:17 “Usifurahi, adui yako aangukapo; Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;

18 BWANA asije akaliona hilo, likamkasirisha; Akageuzia mbali naye hasira yake”.

Ikiwa na maana kuwa kama adui yako amekutenda mabaya na wewe usimrudishie yale mabaya, mwombee Bwana ambadilishe, itakuwa heri kwako…na utasikia ule mzigo umeondoka ndani yako…

Lakini kama ukifikiri kwamba njia ya kuondoa mzigo (uchungu) ndani yako ni wewe kujilipiza kisasi, nataka nikuambie kuwa ndio utauongeza badala ya kuupunguza, kwasababu utakayemlipa kisasi utakuwa umeweka uadui naye hivyo shetani anaweza kumtumia tena kufanya jambo lingine kwa wakati mwingine kwa njia nyingine…lakini lililo baya zaidi ni kwamba utakuwa umekosana na Mungu pia.

Sasa nini kifanyike ili kuishinda nguvu ya kisasi ndani yako?

1. Wokovu.

Wokovu ndio mlango wa Imani. Ni lazima kumwamini Yesu na kumkiri.


2. Maombi (yanayoambatana na mifungo).

Baada ya kuokoka ni lazima uwe mtu wa maombi. Maombi yatakufanya uwe na nguvu za kiroho ambazo zitakusaidia wewe kushinda dhambi.

3 .Kusoma Neno.

Neno la Mungu (biblia) litakusaidia kukujenga utu wako wa ndani. Kwamfano Neno lifuatalo ukilijua litakusaidia wewe kutolipiza kisasi.

Mhubiri 7:21 “Tena, usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa; usije ukamsikia mtumwa wako mwenyewe ali anakutukana.

22 Kwa kuwa mara nyingi moyo wako pia unajua ya kwamba wewe mwenyewe umewatukana watu wengine”.

Mambo haya matatu ukiyazingatia sana basi Nguvu ya kisasi haiwezi kufanya kazi ndani yako, utakuwa mtu wa kusamehe na kuombea wanaokuudhi, na mengine kumwachia Bwana, na hivyo utu wako wa ndani utajengeka sana.

Maran atha!.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Biblia inaposema Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, Inamaana gani?

KISASI NI JUU YA BWANA.

Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?

SADAKA INAKOMESHA LAANA!

JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?

Rudi nyumbani

Print this post

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

Safari ya wokovu ya mkristo inafananishwa na safari ya Wana wa Israeli kutoka Misri kwenda Kanaani. 

Na kama vile maandiko yanavyotuonyesha walikombolewa wote Kwa damu ya Mwana kondoo, Kisha Wakabatizwa katika bahari ya Shamu, wakawa chini ya wingu la Roho Mtakatifu kule jangwani,.. Lakini katika hayo yote bado tunaambiwa wengi wao hawakuweza kuiona Ile nchi ya ahadi. Isipokuwa wawili tu, (yaani Yoshua na Kalebu), waliotoka nchi ya Misri.

Biblia inatuonyesha walipishana na majaribu 5, ambayo yaliwafanya waangamie jangwani. Na majaribu yenyewe tunayasoma katika 1Wakorintho 10:1

1 Wakorintho 10:1-12

[1]Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari; [2]wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari;

[3]wote wakala chakula kile kile cha roho; [4]wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo. [5]Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani.

[6]Basi mambo hayo yalikuwa mifano kwetu, kusudi sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya, kama wale nao walivyotamani. [7]Wala msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa; kama ilivyoandikwa, Watu waliketi kula na kunywa, kisha wakasimama wacheze.

[8]Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu. [9]Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka.

[10]Wala msinung’unike, kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu. [11]Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani. [12]Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.

Kama tunavyosoma hapo. Makosa hayo yalikuwa ni haya;

  1. Kutamani mabaya
  2. Kuabudu sanamu
  3. Kufanya uasherati
  4. Kumjaribu Mungu
  5. Kunung’unika

1) Kutamani mabaya

Mungu aliwapa MANA kama chakula pekee ambacho wangekula jangwani, wao na mifugo Yao, lakini, baadaye waliikinai wakataka NYAMA, na vyakula vingine (Hesabu 11:4-35), matokeo yake ikiwa Mungu kuwaua, wengi wao.

Kama wakristo tuliookoka MANA yetu ni NENO LA MUNGU, Hatupaswi kulikinai, tukakimbilia chakula kingine kisicho Cha kiMungu. Tukataka tuongozwe na mifumo ya kidunia. Ndugu ni hatari mbaya sana. Kumbuka Ile mana ijapokuwa kilikuwa ni chakula Cha aina Moja, lakini hawakuwahi kuumwa, Wala kudhoofika, Wala miguu yao kupasuka, tofauti na walivyokuwa Misri penye vyakula vingi, lakini vimegubikwa na magonjwa. 

Ndugu Lipokee Neno la Mungu, ishi Kwa hilo, hata kama halitavutia (kidunia), lakini limebeba virutubisho vyote vya kimwili na kiroho. Wanaotembea Kwa Neno la Mungu, hawatikisiki hustawi milele.

2) kuabudu sanamu:

Walipomwona Musa amekawia mlimani, na Mungu hazungumzi chochote Kwa wakati ule  wakajiundia sanamu zao za ndama waziabudu. Wakacheza, wakala na kinywa (Kutoka 32). Hii ni kuonesha kuwa kitu chochote kinachokufanya ushangilie  tofauti na Mungu wako, ni ibada ya sanamu.

Rafiki kuwa makini Kwa wakati wa Leo mkristo kushabikia mipira, kwenda Disko, kutumikia Mali, kufuatilia vipindi vya sinema kulikopitiliza, chattings, kupenda anasa. Ni ibada za sanamu waziwazi.

 Kwasababu gani?. Kwasababu ndio bubujiko lako la roho lilipo kama ilivyokuwa Kwa Wana wa Israeli, Kwa sanamu zile. Ikapelekea watu wengi kufa siku Ile. Ibada Yako iwe Kwa Bwana. Mungu ni mwenye wivu. Mpira ukichukua nafasi zaidi ya Mungu wako ni kosa.

3) Kufanya uasherati

Walipokuwa jangwani Mungu aliwakataza wasitangamane na wageni, kwasababu watawageuza mioyo na kuiabudu miungu Yao. Lakini wao walipowaona wanawake wa taifa la Moabu, wakaenda kuzini nao, Kisha wakageuzwa mioyo wakaabudu miungu Yao. Hiyo ikawa sababu ya Mungu kuwaua waisraeli wengi sana idadi yake 23,000.

Na sisi kama wakristo tulishapewa tahadhari kwenye maandiko. Tusifungwe nira na wasioamini isivyo sawasawa (2Korintho 6:14-18). Kwasababu hakuna ushirika kati ya Nuru na Giza. Hivyo hatuna budi kuwa makini na ulimwengu, tushirikiane nao kwenye mambo ya kijamii na ya msingi, pale inapokuwa na ulazima, lakini ya kiroho, hatupaswi hata kidogo kuwa na urafiki nao kwasababu ni rahisi kugeuzwa moyo na kuambatana nao kitabia, na matokeo yake tukamwasi Mungu.

Sulemani aligeuzwa moyo, Wana wa Mungu tunaosoma kwenye Mwanzo 6 nao pia waligeuzwa mioyo Kwa jinsi hiyo hiyo, na wewe pia usipojiwekea mipaka na watu ambao ni wa kidunia, Unaweza kupoteza taji lako. Pendelea zaidi kuwa na kampani ya waliookoka. Ni Kwa usalama wako. Usijikute unafanya uasherati wa kiroho.

4) Kumjaribu Bwana

Wana wa Israeli walimjaribu Bwana, wakati Fulani wakamnun’gunikia Mungu na Musa, wakisema chakula hiki dhaifu, wakitaka Kwa makusudi Bwana awafanyie Tena muujiza mwingine, Mungu akakasirishwa nao, akawaangamiza Kwa nyoka (Hesabu 21:4-9).

Kama mkristo tambua kuwa Mungu haendeshwi kama “robot”. Kwamba ni lazima afanye jambo Fulani Kila tutakapo ndio tuthibitishe yeye yupo na sisi. Ndugu ukristo wa hivi ni hatari, wengi wameishia kuanguka kwasababu hii. Jaribu kama hili aliletewa Bwana Yesu na shetani jangwani. Ajitupe kutoka kinarani, kwasababu maandiko yanasema Mungu atamuagizia malaika wake wamchukue salama. lakini Bwana Yesu alimwambia shetani usimjaribu Bwana Mungu wako.

Kamwe usimwendeshe Mungu, mwache yeye ayaendeshe maisha Yako. Tuwe na hofu na Mungu wetu.

5) Kunung’unika.

Wana wa Israeli tangu mwanzo wa safari Yao Hadi karibia na mwisho, waligubikwa na manung’uniko tu,(Kutoka 23:20-21) wengi wao hawakuwa watu wa shukrani. Ijapokuwa walilishwa mana, waliouna utukufu wa Mungu Kwa wingi. Lakini bado manung’uniko yalizidi shukrani.

Biblia inatuasa sisi tuliookoka tuwe watu wa Shukrani (Wakolosai 3:15), Kwa kazi aliyoimaliza Yesu pale msalabani ya kuondolewa dhambi ni fadhili tosha zaidi hata ya wale Wana wa Israeli kule jangwani. Hata tukikosa Kila kitu, maadamu tumeahidiwa uzima wa milele. Hatuhitaji kuwa na hofu na jambo lolote. Wokovu wetu ndio uwe faraja.

Epuka Maisha ya manung’uniko.

Bwana akubariki.

Ikiwa tutashinda majaribu haya MATANO katika safari yetu ya wokovu. Basi tutalipokea taji timilifu Kwa Bwana  siku Ile mfano wa Yoshua na Kalebu.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

Wale Nyoka wa Moto jangwani, walikuwa ni wa namna gani?

Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

NI KWA NAMNA GANI TUTASHINDA MAJARIBU?

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

TUUTAFUTE UMOJA WA ROHO.

Umoja wa Roho Mtakatifu upo katika vifungo 7, ambavyo kama kanisa ni lazima tujifunge katika vifungo hivyo.

Lakini kabla ya kuvitazama hivi vifungo 7 vya Roho Mtakatifu, ni vizuri tuweke msingi kidogo kumhusu Roho Mtakatifu.

Biblia inatufundisha kuwa kuna Roho 7 za Mungu, ambazo ndizo zinazotajwa kama Macho 7 ya Mungu.

Ufunuo 5:6  “Nikaona katikati ya kile kiti cha enzi na wale wenye uhai wanne, na katikati ya wale wazee, Mwana-Kondoo amesimama, alikuwa kana kwamba amechinjwa, mwenye pembe saba na macho saba, AMBAZO NI ROHO SABA ZA MUNGU zilizotumwa katika dunia yote”

Vile vile inazitaja Roho hizi 7 kama TAA SABA ZA MUNGU, ikiwa na Maana kuwa hizo ndizo mwanga mbele ya kiti cha Enzi.

Ufunuo 4:5 “Na katika kile kiti cha enzi kunatoka umeme na sauti na ngurumo. NA TAA SABA ZA MOTO ZILIKIWAKA MBELE YA KILE KITI CHA ENZI, NDIZO ROHO SABA ZA MUNGU”.

Hii yote ikimaanisha kuwa Roho Mtakatifu anatenda kazi katika Nafasi zake 7, au hatua zake 7 katika kuwakamilisha watu wake, lakini haina maana kuwa Roho Mtakatifu wapo 7.

Kwa msingi huo basi twende tukazitazame jinsi anavyolikamilisha kanisa katika kifungo cha UMOJA katika hatua zake saba.

Tusome,

Waefeso 4:3 “ na kujitahidi kuuhifadhi UMOJA WA ROHO katika kifungo cha amani.

MWILI MMOJA, na ROHO MMOJA, kama na mlivyoitwa katika TUMAINI MOJA la wito wenu.

BWANA MMOJA, IMANI MOJA, UBATIZO MMOJA.

MUNGU MMOJA, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote”.

Tutazame moja baada ya nyingine:

1.MWILI MMOJA.

Mwili unaozungumziwa hapa ni Mwili wa Yesu, (Soma Waefeso 4:12 na Wakolosai 3:15), na Mwili huu unajengwa kupitia Vipawa na Karama ambazo Roho Mtakatifu ameziweka ndani yetu, ambapo kila mmoja ni kiungo ndani ya mwili huo.. Hivyo ili tuufikie umoja wa Roho kama kanisa ni lazima tuenende katika msingi huu kwamba kanisa linaongozwa katika karama za Roho Mtakatifu, na si itikadi, mapokeo au siasa.

1Wakorintho 12:13  “Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi, au kwamba tu Wayunani; ikiwa tu watumwa au ikiwa tu huru; nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.

14  Kwa maana mwili si kiungo kimoja, bali ni vingi”.

2. ROHO MMOJA.

Anaposema Roho mmoja, zipo roho nyingi, hata shetani naye ni roho.. ikiwa na maana kuwa ndani ya kanisa ni lazima tuwe na Roho mmoja anayezaa matunda yanayofanana kwa wote. Na matunda ya Roho ni yale yanayotajwa katika Wagalatia 5:22, kupitia hayo, tutakuwa tumekamilka katika kifungo cha pili cha Roho. Ndio maana biblia inatufundisha kuzichunguza roho, kwamaana zipo roho nyingi..

2Wakorintho 11:4 “Maana yeye ajaye akihubiri Yesu mwingine ambaye sisi hatukumhubiri, au mkipokea ROHO NYINGINE MSIYOIPOKEA, au injili nyingine msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye”

3. TUMAINI MOJA

Tumaini linalozungumziwa hapa ni “Tumaini la Utukufu ujao”.. Kwamba kila aliyeokoka analo tumaini la kuingia katika utukufu wa Mungu ujao,(Mbingu mpya na nchi mpya). Hili ni tumaini ambalo Kanisa lazima liufikie, na si kila mmoja anaamini analoliamini, kwasababu wapo wengine wanaosema hakuna ufufuo, mtu akifa amekufa!, jambo ambalo ni kinyume kabisa na maandiko. Ufufuo upo, na watakatifu watafufuliwa na kuingia katika utukufu wa milele.

Wakolosai 1:26  “siri ile iliyofichwa tangu zamani zote na tangu vizazi vyote, bali sasa imefunuliwa kwa watakatifu wake;

27  ambao Mungu alipenda kuwajulisha jinsi ulivyo utajiri wa utukufu wa siri hii katika Mataifa, NAO NI KRISTO NDANI YENU, TUMAINI LA UTUKUFU”

4. BWANA MMOJA

Yupo Bwana mwingine (yesu mwingine), anayehubiriwa tofauti na yule wa kwenye maandiko matakatifu.

2Wakorintho 11:4 “Maana yeye AJAYE AKIHUBIRI YESU MWINGINE ambaye sisi hatukumhubiri, au mkipokea roho nyingine msiyoipokea, au injili nyingine msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye”.

Yesu mwingine ni yule anayesema Mungu haangalii mwili anaangalia Roho, ni yule anayesema mchukie adui yako, n.k. Lakini yule halisi anasema Mwombee adui yako, waombeeni wale wanaowaudhi, na wasameheni wale wanaowaudhi (Mathayo 5:43).

5. IMANI MOJA

Imani moja ni sahihi ni ile inayosema mpatanishi kati ya Mungu na mwanadamu ni mmoja (naye ni YESU KRISTO), Lakini Imani nyingine inasema “watakatifu waliokufa pia wanaweza kuwa wapatanishi” hivyo wanaweza kutuombea…

1Timotheo 2:5  “Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu”.

Vile vile inasema, mwombezi wetu kwa Baba ni yeye mmoja Yesu Kristo ( 1Yohana 2:1) na wala hakuna mwingine, lakini Imani nyingine inasema waombezi wanaweza kuwa wengi mbinguni. Hivyo kanisa ni lazima lifikie umoja wa Imani ya kweli ya kwenye biblia, kwamba mpatanishi ni mmoja na mwombezi ni mmoja, ambaye ni Yesu Kristo, na wala hakuna mwingine wa kumsaidia.

6. UBATIZO MMOJA.

Ubatizo mmoja wa kimaandiko ni ule wa Maji mengi (Yohana 3:23) na kwa jina la Bwana Yesu Kristo (Matendo 2:38, Matendo 10:48, Matendo 19:5). Ni lazima kanisa lifikie huu umoja, na si kila mmoja kuamini ubatizo wake.

7. MUNGU MMOJA.

Mungu mmoja wa kweli  ni yule aliyeumba mbingu na nchi, ambaye ni Baba wa yote, aliyeko juu mbinguni na si sanamu, wala miti, wala wanadamu. Hivyo ni lazima ndani ya mwili wa Kristo wote tufikie umoja huu wa kumwamini na kumwabudu Mungu mmoja, na kuchanganya ibada na miungu mingine au sanamu.

Adui anafanya kazi kwa nguvu, kuuvunja UMOJA HUU WA ROHO, kwasababu anajua ndio NGUVU YA KANISA, anataka kuweka umoja wake mwingine wa kidunia ndani ya kanisa, na kuutafsiri kama ndio umoja wa roho. Hivyo hatuna budi kuwa makini na kuyaishi maandiko.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

JE UNAMHUBIRI KRISTO KATIKA KWELI YOTE?.

Roho Mtakatifu ni nani?.

NI KWASABABU YA YESU KRISTO.

TUMAINI NI NINI?

Dinari ni nini na Rupia ni nini (Mathayo 20:2,Ufunuo 6:6)

Rudi nyumbani

Print this post

IFAHAMU FAIDA YA KUMKIRI KRISTO UKIWA HAPA DUNIANI.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia,

Bwana wetu Yesu alisema maneno yafuatayo…

Mathayo 10:32  “BASI, KILA MTU ATAKAYENIKIRI MBELE YA WATU, nami nitamkiri mbele za Baba yangu aliye mbinguni..”

Tunapomkiri Bwana Yesu hapa duniani tuna ahadi ya yeye kwenda kutukiri mbinguni mbele za Baba na Malaika lakini pia kuna faida ambayo tutaipata tukiwa hapa duniani kabla hatujafika kule mbinguni. Na moja ya faida hiyo ni ndio kama ile aliyoipata Mtume Petro, alipomkiri Bwana YESU katika usahihi wote mbele ya wote.

Tusome,

Mathayo 16:15  “Akawaambia, NANYI MWANINENA MIMI KUWA NI NANI?

16 Simoni Petro akajibu akasema, WEWE NDIWE KRISTO, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.

17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.

18 Nami nakuambia, WEWE NDIWE PETRO, NA JUU YA MWAMBA HUU NITALIJENGA KANISA LANGU; WALA MILANGO YA KUZIMU HAITALISHINDA.

19 Nami nitakupa WEWE FUNGUO ZA UFALME WA MBINGUNI; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni”.

Umeona?.. Kabla tu ya Bwana Yesu kwenda kumkiri Petro mbele za Malaika watakatifu mbinguni, tayari alianza kumkiri akiwa hapa hapa duniani kabla ya kufika kule, kwamba..“YEYE NDIYE PETRO,… NA AKAMPA FUNGUO ZA UFALME WA MUNGU”…kila atakalolifunga duniani litakuwa limefungwa mbinguni na atakalolifungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.

Na sisi tunapomkiri Yesu kisahihi mbele za watu, tunaanza kuvuna matunda yake tukiwa hapa hapa duniani,….vile vile tunaposhuhudia habari zake kisahihi mbele za watu, na kumtangaza kama jinsi anavyotaka, faida yake tunaanza kuipata tukiwa hapa hapa duniani kabla ya kufika kule mbinguni,.. majina yetu yanabadilishwa katika ulimwengu wa roho tukiwa hapa hapa duniani, tunapewa mamlaka nyingine ya kipekee, na funguo za mambo mengi.

Je! Umemkiri Yesu katika maisha yako? (Kumbuka Kristo hatumkiri kwa moyo, bali kwa Kinywa).. Ikiwa na maana kuwa ni lazima tuhusishe vinywa vyetu na sauti zetu katika kumkiri yeye.

Warumi 10:10 “Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na KWA KINYWA HUKIRI HATA KUPATA WOKOVU”.

Je unamtangaza Bwana Yesu mbele za watu?..

Kama bado hujafanya hayo yote, ni vizuri ukafanya maamuzi leo, kwa faida yako mwenyewe ya hapa duniani na katika ulimwengu ujao…Lakini ukimwonea haya naye pia atakuonea haya kuanzia hapa hapa duniani, kabla ya kufika kule mbinguni.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

USIISHIE TU KUPATA HAKI, BALI PATA NA WOKOVU.

MFALME ANAKUJA.

BADO UPO YERUSALEMU TU..GALILAYA HUTAKI KWENDA?

NJIA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Rudi nyumbani

Print this post

UTAIKUZAJE IMANI NDANI YAKO?

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, lihimidiwe daima.

Karibu katika darasa hili fupi la biblia?

Je unajua imani inafananishwa na nini? Na je unajua ni kitu gani kinachoikuza Imani?.

Majibu ya maswali haya tutayapata ndani ya biblia…

Bwana Yesu aliifananisha imani na chembe ndogo ya Haradali, Chembe ya Haradali au kwa lugha nyingine punje ya Haradali ni mbegu inayotoa mmea unaoitwa Haradali.

Luka 17:6 “Bwana akasema, Kama mngekuwa na imani KIASI CHA CHEMBE YA HARADALI, mngeuambia mkuyu huu, Ng’oka, ukapandwe baharini, nao ungewatii”

Hapa Bwana anaifananisha imani na chembe ya Haradali, na anasema mtu akiwa nayo kwa kiasi hicho tu!, Tayari anaweza kufanya makubwa.

Sasa mtu anawezaje kufanya makubwa akiwa na chembe hiyo ya Haradali?. Hilo ndio swali la kujiuliza.

Wengi tunaishia kuitafakari tu ile chembe ya Haradali kwa udogo wake basi na si kwa upana wake,
Lakini hebu leo hebu tutafakari kwa undani hii chembe ya Haradai na muujiza uliopo ndani yake.

Lakini awali ya yote tuweke msingi kwa kuutafakari mfano ufuatao…Tengeneza picha mkulima anakwambia ukiwa na punje moja ya indi, waweza kulisha watu mia.. Je kwa kusema hivyo atakuwa amemaanisha lile indi moja laweza kushibisha watu wote hao?.

Jibu ni la! Ni wazi kuwa indi moja haliwezi kushibisha umati wa watu mia, bali atakua amemaanisha kuwa endapo ukiiichukua ile mbegu moja ya indi, ukaipanda yaweza kuzaa mahindi mengi ambayo yaweza kushibisha umati mkubwa wa watu.

Vivyo hivyo Bwana Yesu aliposema “Imani kama chembe ya Haradali yaweza kuhamisha milima na mikuyu” ..hakumaanisha ile mbegu kama mbegu bali matokeo ya ile mbegu, ndio maana hakuifananisha imani na chembe ya mchanga isiyozaa bali chembe ya Haradali iliyo hai na inayozaa..

Sasa ili tuelewe vizuri, tusome maandiko yafuatayo…

Marko 4:30 “Akasema, Tuulinganishe na nini ufalme wa Mungu? Au tuutie katika mfano gani?

31 NI KAMA PUNJE YA HARADALI, ambayo ipandwapo katika nchi, ingawa ni ndogo kuliko mbegu zote zilizo katika nchi,

32 lakini ikiisha kupandwa hukua, ikawa kubwa kuliko miti yote ya mboga, ikafanya matawi makubwa; hata ndege wa angani waweza kukaa chini ya uvuli wake”.

Umeona muujiza uliopo ndani ya punje ya Haradali?…kwamba inaanza kama mbegu ndogo tena dhaifu na kisha inapokua kubwa huzidi mboga zote na miti yote na kufanya matawi makubwa ambayo ndege waweza kukaa chini yake.

Kwahiyo kumbe Imani inayofananishwa na chembe ya Haradali, inahitajika kupandwa kwanza katika nchi, na kupaliliwa na kumwagiwa maji, ili iweze kuwa mti mkubwa utakaoweza kutoa matunda na hata kuwa tegemezi kwa viumbe wengine, lakini ikibaki katika hali ile ile haizai kitu, ni sawa na imekufa..kama maandiko yanavyosema…

Yakobo 2:17 “Vivyo hivyo na imani, isipokuwa ina matendo, imekufa nafsini mwake”.

Sasa swali Imani inapaliliwaje na inamwagiwaje maji, ili ikue na kuleta matokeo makubwa.

Tusome Mathayo 17:20-21.

Mathayo 17:20 ” Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.

21 [LAKINI NAMNA HII HAITOKI ILA KWA KUSALI NA KUFUNGA.]

Umeona mwisho hapo?.. anasema, namna hii haitoki isipokuwa kwa KUSALI na KUFUNGA.

Kumbe KUSALI na KUFUNGA ndio kanuni ya kukuza Imani,…..kumbe Kufunga na kusali ndiko kuipalilia na kuinyeshea Imani ili Ikue, na mtu akiendelea kwa kanuni hiyo, kwa kitambo fulani basi ile imani ndani yake itakua yenyewe na baadaye atatoa matokeo makubwa kwa kila anachokihitaji.

Mtu aliyeipalilia imani yake hatatumia nguvu nyingi kupata jambo, kwa maana Imani yake ni imara na thabiti.. Ile punje ya Haradali ndani yake imegeuka kuwa mti mkubwa usiotikisika.

Ndio maana watu waliojaa maombi na mifungo, wachawi hawawatesi wala hawana hofu na hatari yoyote, kwanini??..Kwasababu tayari imani yao imejengeka ndani yao.

Je na wewe unataka imani yako ikue?…basi usikwepe Mifungo, vile vile usikwepe maombi..Ikiwa utahitaji mwongozo wa maombi ya kukua kiroho ya kila wiki basi wasiliana nasi inbox na tutakusaidia kwa hilo, na vile vile kama utapenda kuungana nasi katika ratiba zetu za mifungo waweza kuwasiliana nasi inbox ili tuweze kukupa utaratibu.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

MSHAHARA WA DHAMBI:

UTAONA MAMBO MAKUBWA KULIKO HAYA.

MKAMCHUKUE SALAMA.

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

NGUVU YA UPENDO WA KRISTO.

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Habari iliyo katika 1Nyakati 21:25, na 2Samweli 24:24, ya Daudi kununua kiwanja  inajichanganya?

SWALI:  Ni ipi gharama sahihi ambayo Daudi aliilipia, kununulia shamba la Arauna, kwa ajili ya kumjengea Mungu hekalu. Je! Ni shekeli 600, au shekeli 50?. Je! Biblia inajichanganya.

JIBU:  Tusome,

2Samweli 24: 24 Lakini mfalme akamwambia Arauna, La, sivyo; lakini kweli nitavinunua kwako kwa thamani yake; wala sitamtolea Bwana, Mungu wangu, sadaka za kuteketezwa nisizozigharimia. Hivyo Daudi akakinunua hicho kiwanja cha kupuria na wale ng’ombe kwa shekeli hamsini za fedha.  25 Naye Daudi akamjengea Bwana madhabahu huko, akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Basi Bwana aliiridhia nchi, na tauni ikazuiliwa katika Israeli.

1Nyakati 21:25 “Basi Daudi akampimia Arauna thamani ya mahali pale shekeli mia sita za dhahabu kwa uzani  26 Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu huko, akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, akamlingana Bwana; naye akamwitikia kutoka mbinguni kwa moto juu ya madhabahu hiyo ya sadaka ya kuteketezwa”

Vifungu hivyo havijichanganyi,  vyote vipo sahihi. Mwandishi wa kitabu cha Samweli anaeleza lile eneo ambalo lilikuwa ni la kupuria tu, pamoja na wale ng’ombe gharama zake jumla ndio shekeli hamsini, lakini sio eneo lote la kiwanja. Tukirudi kwenye 1Nyakati mwandishi anaeleza sasa eneo lote, anatumia neno “mahali pale”. Kwamba jumla yake yote ni shekeli mia sita. Gharama zote za mahali pale zilikuwa ni shekeli 600

Kwamfano wewe unaweza ukawa umelenga kupanunua mahali Fulani kwa ajili ya shughuli zako za kimaendeleo. Lakini ikakugharimu ununue sehemu yote ili uweze kupamiliki vizuri na pale. Hivyo kama eneo lile tu moja gharama yake ilikuwa milioni 1, Lakini kwasababu ya kulipia fidia kwa watu kando kando kuwahamisha, na kodi, na ukarabati n.k. unajikuta unaenda mpaka milioni 20.

Ndicho kilichomkuta Daudi.

Kwahitimisho ni kuwa vifungu hivyo vipo sahihi havijichanganyi.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Swali: Je idadi ya askari waliohesabiwa katika 1Nyakati 21:5 na 2Samweli 24:9 inajichanganya?.

Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

NI KWANINI WATU WENGI WANASHINDWA KUMWELEWA MUNGU?

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.

Je! Wamwona mtu mwenye bidii katika kazi zake?

Novena ni nini? Na je ipo kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

VUNJA AGANO LA MAUTI.

Mtu anaingiaje agano na mauti?

“Agano” kwa jina lingine ni “Mkataba”

Mtu anapoingia mkataba na mtu mwingine ni sawa na kaingia agano na mtu huyo.

Sasa mwanadamu pia anaweza kuingia Agano na Mauti, Ndivyo biblia inavyotufundisha kuwa mtu anaweza kuingia agano na Mauti na kuingia katika mapatano na kuzimu.

Isaya 28:18 “Na agano lenu mliloagana na mauti litabatilika, tena mapatano yenu mliyopatana na kuzimu hayatasimama; pigo lifurikalo litakapopita, ndipo ninyi mtakapokanyagwa nalo”.

Na kama mtu ameingia Agano na Mauti ni lazima mauti itakuwa na nguvu juu yake,itamwandama popote anapokwenda na itampata..hivyo ni lazima hilo agano livunjwe ili mtu huyo abaki huru, na uzima utawale ndani yake,

Sasa kinachomwingiza mtu katika agano la Mauti ni nini?..je ni ndoto anazoziota?, Au ni wachawi?, Au wanadamu?..

Jibu: Si wanadamu, wala wachawi, wala ndoto mtu anazoota bali ni “dhambi ndani ya mtu”…Biblia inasema “Mshahara wa dhambi ni Mauti”.

Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Sasa hapo hasemi “matokeo ya dhambi ni mauti” bali “mshahara wa dhambi ni mauti”.

Maana yake mtu anayefanya dhambi ni sawa na mtu anayefanya kazi za kumpatia mshahara..Kwamba ni lazima atakuwa na mkataba wa kazi (yaani agano la kazi) ili apokee mshahara.

Halikadhalika na mtu anayefanya dhambi, anakuwa kwanza ameingia agano na hiyo dhambi na ndipo anapokea mshahara wake baada ya kuitendea kazi, na mshahara wake ndio “Mauti”.

Kwahiyo kumbe Agano la Mauti ni “dhambi”..Ikiwa na maana kuwa mtu akiondoa dhambi katika maisha basi atakuwa amelivunja hilo agano la Mauti lililo ndani yake!.

Kumbe mtu anayeabudu sanamu tayari yupo katika agano na mauti, kumbe mtu anayezini tayari kashaingia agano/mkataba na mauti, Kumbe mtu anayeiba tayari yupo katika agano na mauti?, Na kwamba siku yeyote atakumbana na Mauti ya mwili na roho, na hatimaye kutupwa katika ziwa la moto ambako huko kuna mauti ya pili. (Ufunuo 20:14 na 21:8)

Sasa hili agano la Mauti tunalivunjaje?…je ni kwa kuwekewa mikono na watumishi?, Au kwa kunywa maji na mafuta yajulikanayo kuwa ya upako?, Au kwenda kukemea hayo maagano?

Jibu la swali hili hatulipati pengine popote isipokuwa kwenye biblia.

Matendo 2:38 “Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.

Umeona kanuni ya Kuondoa dhambi?…si kwa kupakwa mafuta, au kuwekewa mikono kichwani…bali ni kwa KUTUBU NA KUBATIZWA.

Unapotubu kwa kumaanisha kabisa kuacha dhambi basi unapokea msamaha na papo hapo na lile agano la Mauti linavunjika!..sawasawa na maandiko hayo ya Isaya 28:18,

Isaya 28:18 “Na agano lenu mliloagana na mauti litabatilika, tena mapatano yenu mliyopatana na kuzimu hayatasimama; pigo lifurikalo litakapopita, ndipo ninyi mtakapokanyagwa nalo”.

Lakini kama hakuna toba halisi na ubatizo basi agano la mauti bado lipo palepale..halijavunjika! Haijalishi mtu huyo atawekewa mikono na watumishi wangapi, au ataombewa na watu wangapi, au anaabudu dhehebu kubwa kiasi gani..kama bado hataki kuacha dhambi, zinazotajwa katika Wagalatia 5:19…basi Mauti bado ipo pale pale.

Tubu leo na Agano la Mauti litabatilika juu yako, kile kifo ambacho ulikuwa umekiona kimekukaribia kitapelekwa mbali nawe.. Na hakikisha toba yako inaendana na matendo, kama umetubia wizi, au uzinzi, au uchawi au jambo lingine lolote hakikisha kuanzia siku hiyo hurudii tena hayo..(Unafanyika kiumbe kipya).

Bwana atusaidie.
Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Je Adamu na Hawa, walikuwa hawafanyi mema kabla ya kula tunda?

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

DHAMBI YA MAUTI

MSHAHARA WA DHAMBI

Wote wanaokumbwa na mauti sasa ni kutokana na dhambi zao?

Rudi nyumbani

Print this post

Je maombi ya mlimani yana ulazima wowote kwa mkristo?

Swali: Je sisi watu wa agano jipya ni lazima kuwa na vipindi vya kuombea mlimani?. Na je huko mlimani Mungu ndioko anakosikia Zaidi maombi kuliko chini?.. msaada!

Jibu: Hakuna agizo lolote katika biblia la mahali rasmi pa kuombea!, kama ni  mlimani au kama ni chini.. Lakini tunaweza kujifunza kupitia watu kadhaa katika biblia jinsi walivyoomba na kisha tunaweza kujifunga kitu.

BWANA YESU MWENYEWE.

Mathayo 14:22 “ Mara akawalazimisha wanafunzi wake wapande chomboni na kutangulia mbele yake kwenda ng’ambo, wakati yeye alipokuwa akiwaaga mkutano.

23  Naye alipokwisha kuwaaga makutano, ALIPANDA MLIMANI FARAGHANI, KWENDA KUOMBA. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake”.

Na pia…

Luka 6:12  “Ikawa siku zile aliondoka AKAENDA MLIMANI ILI KUOMBA, akakesha usiku kucha katika kumwomba Mungu”.

Soma pia Marko 6:46 na Yohana 6:15, utaona jambo hilo hilo la Bwana kupanda mlimani kuomba, na pia utaona sehemu nyingine alipanda na wanafunzi wake, soma Luka 9:28.

Umeona?.. Kama Bwana Yesu kuna nyakati alikuwa akienda mlimani kuomba, yeye pamoja na wanafunzi wake maana yake si bure!.. Kuna kitu cha ziada katika milima.

Na kitu hiko si kingine Zaidi ya UWEPO WA MUNGU. Milimani kunakuwa na Uwepo wa Mungu zaidi ya mabondeni?. Na kwanini milimani kunakuwa na Uwepo wa Mungu Zaidi ya sehemu nyingine nyingi?.

Ni kwasababu kule juu kunakuwa na utulivu,.. na siku zote utulivu unavuta uwepo wa Mungu, na milimani ni sehemu ambazo hazina usumbufu hivyo ni rahisi mtu kuzama katika roho kuliko akiwa chini penye masumbufu mengi na mwingiliano wa Sauti nyingi.

Umewahi kujiuliza ni kwanini minara ya simu huwa inapelekwa juu katika milima na haiwekwi mabondeni?.. Ni kwasababu kule juu network inapatikana vizuri Zaidi ya chini, kwasababu hakuna vizuizi vingi vya kuzuia mawimbi kusafiri. Sasa kama wanadamu wameiona hiyo siri iliyopo juu ya milima, vipi kwetu sisi wakristo?

Si kwamba Mungu hatakusikia ukiomba mabondeni, atakausikia lakini ule uwepo wa Mungu kwako unaweza usiupate vizuri kuliko kama ungeenda kuomba sehemu iliyoinuka (Milimani). Ndio maana utaona mtu anakuwa mzito kuomba, pasipo kujua chanzo ni nini?.. Wakati mwingine si mapepo!, bali ni mazingira tu!… Badili mazingira na utaona jinsi utakavyozama katika roho na maombi!.

Kwahiyo kama wakristo ambao pia ni mwanafunzi wa biblia, ni lazima tuwe na vipindi vya kupanda mlimani kuomba!. Kama mahali ulipo hapana milima, basi linaweza lisiwe jambo la lazima sana, lakini kama ipo basi tenga muda wa kufanya hivyo mara chache chache na utaona matokeo makubwa sana na vile vile utaona utofauti na utafungua mlango mpana sana wa kupokea mafunuo kutoka kwa Baba.

Bwana akubariki.

Marana tha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

UTAONA MAMBO MAKUBWA KULIKO HAYA.

AKIJUA YA KUWA ANA WAKATI MCHACHE TU”.

Fahamu Namna ya Kuomba.

KUNA AINA NGAPI ZA MAOMBI?

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Bwana Yesu aikabidhi roho yake mikononi mwa Baba (Luka 23:46)?

Jibu: Tusome kuanzia mstari wa 43..

Luka 23:44  “Hapo ilikuwa yapata saa sita, kukawa giza juu ya nchi yote hata saa kenda,

45  jua limepungua nuru yake; pazia la hekalu likapasuka katikati.

46  Yesu akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Baba, MIKONONI MWAKO NAIWEKA ROHO YANGU.

47  Alipokwisha kusema hayo alikata roho. Yule akida alipoona yaliyotukia, alimtukuza Mungu, akisema, Hakika yake, mtu huyu alikuwa mwenye haki”.

“Mikononi mwako naiweka roho yangu”… haya yalikuwa ni maneno ya Mwisho ya Mwokozi wetu Yesu Kristo alipokuwa pale msalabani?.. lakini swali? Ni kwanini aseme hivyo? Je kulikuwa na ulazima wowote  wa yeye kusema vile, na sisi je tunafundishwa kusema maneno kama hayo tunapokaribia hatua za kumalizia safari zetu za maisha?

Kabla ya kujibu, ni muhimu kufahamu kuwa kabla ya Bwana Yesu kufa na kushuka kuzimu na kupewa zile funguo za Mauti, sehemu ya wafu haikuwa salama (maana yake roho za watatakatifu bado hazikuwa salama hata baada ya kufa).

Ndio maana utaona hata Nabii Samweli ambaye alikuwa ni mtu wa haki sana mbele za Mungu, lakini baada ya kufa kwake, yule mwanamke wa Endori aliyekuwa mganga aliweza kumtoa kuzimu na kumpandisha juu kichawi.

1Samweli 28:7 “Ndipo Sauli akawaambia watumishi wake, Nitafutieni mwanamke mwenye pepo wa utambuzi, nipate kumwendea na kuuliza kwake. Watumishi wake wakamwambia, Tazama, yuko mwanamke mwenye pepo wa utambuzi huko Endori. 

8 Basi Sauli akajigeuza, na kuvaa mavazi mengine, kisha akaenda, yeye na watu wawili pamoja naye, wakamfikilia yule mwanamke usiku; akasema, Tafadhali unibashirie kwa utambuzi, ukanipandishie yeye nitakayemtaja kwako. 

9 Yule mwanamke akamwambia, Angalia, unajua alivyofanya Sauli, jinsi alivyowakatilia mbali hao wenye pepo wa utambuzi na wachawi katika nchi; mbona basi wanitegea tanzi uhai wangu, ili kuniua?

10 Naye Sauli akamwapia kwa Bwana, akasema, Aishivyo Bwana, haitakupata adhabu yo yote kwa jambo hili. 

11 Ndipo yule mwanamke aliposema, Je! Ni nani nitakayekupandishia? NAYE AKASEMA, NIPANDISHIE SAMWELI”.

Umeona hapa? roho ya nabii Samweli inataabishwa na wachawi hata baada ya kufa kwake.. Ndio maana utaona Samweli baada ya kupandishwa juu alimlalamikia Sauli kwanini anamtaabisha.

1Samweli 28:15 “Ndipo Samweli akamwambia Sauli, Mbona umenitaabisha mimi, hata kunipandisha juu?….”

Kwasababu hiyo ndio maana Bwana Yesu akaikabidhi roho yake kwa Baba, kama tu alivyokuwa anazikabidhi kazi zake na safari zake kwa Baba kipindi akiwa hai, vivyo hivyo alifahamu kuwa kuna umuhimu wa kufanya hivyo pia kwaajili ya roho yake baada ya kufa.

Lakini tunaona alipokufa, Baba alimpa funguo za KUZIMU na MAUTI sawasawa na Ufunuo 1:17

Ufunuo 1:17 “Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,

18  na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU”

Maana yake kuwa kuanzia wakati wake mpaka mwisho wa dunia, shetani hatakuwa na uwezo tena wa kuzitaabisha roho za watakatifu waliokufa, hivyo Bwana Yesu sasa ndiye mwenye mamlaka hayo juu ya roho zote za waliokufa na walio hai.

Warumi 14:8 “Kwa maana kama tukiishi, twaishi kwa Bwana, au kama tukifa, twafa kwa Bwana. Basi kama tukiishi au kama tukifa, tu mali ya Bwana.

9 Maana Kristo alikufa akawa hai tena KWA SABABU HII, AWAMILIKI WALIOKUFA NA WALIO HAI PIA”.

Kwahiyo kwasasa hatuna hofu tena ya kwamba baada ya kifo roho zetu zitataabishwa, bali tukifa basi uhai wetu (roho zetu) zinafichwa mbali na adui. Na sehemu hiyo ya maficho ambayo shetani hawezi kuifikia ni Paradiso, mahali pa mangojeo na raha, huku tukiingoja ile siku ya ahadi, ya unyakuo wa kwenda mbinguni. Haleluya!.

Kwahiyo kwasasa hatuna maombi ya kuzikabidhi roho zetu kwa baba wakati wa kufa, kwasababu tayari Kristo anazo funguo za mauti na kuzimu, bali tunapaswa wakati huu sasa tulio hai tuyakabidhi maisha yetu kwake, na kuishi maisha ya kumpendeza,  ili tutakapomaliza safari ya maisha yetu basi tujikute tupo sehemu salama, kwasababu hatujui ni saa ipi tutaimaliza safari yetu ya maisha hapa duniani.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

JIWE LILILO HAI.

ORODHA YA IMANI POTOFU- Sehemu ya 1.

Je Lutu alikwenda kuwahukumu watu wa Sodoma na Gomora? Kulingana na Mwanzo 19:9?

Kwanini Bwana Yesu alisema pale msalabani naona kiu?

Rudi nyumbani

Print this post