Title May 2023

IPENDE BUSTANI YAKO.(Ilime, itunze)

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze maneno ya uzima.

Ipo tabia ambayo tunapaswa tujifunze kuhusu Mungu. Kama tunavyojua, alipomaliza kuumba vitu vyote ndani ya zile siku saba, zoezi la mwisho kabisa lilikuwa ni Mungu kupanda bustani mashariki mwa Edeni. Tengeneza picha, bustani hiyo ilikuwaje! Bila shaka ilikuwa ni nzuri sana. Mungu alifanya kazi ya kuchukua Ua hili, Ua lile, ukoka huu, ukoka ule, mti huu wa kivuli, mti ule wa matunda kila moja mahali pake stahiki.. Yaani kwa ufupi Edeni ni bustani ambayo iliundwa kwa kila aina ya mmea, lakini katika mpangilio bora. Jambo lililoifanya bustani ile kuwa tofauti na maeneo mengine yote duniani.

Kwani huko kwingine kulijiotea otea, bila mpangilio maalumu. Japo pia napo kulikuwa pazuri lakini sio kama Edeni, kwasababu ile ni bustani iliyopandwa sio kujiotea. Lakini tunaona, asili ya ile Bustani. Ni kwamba ilihitaji kulimwa na matunzo baada ya pale ili iendelee kuwepo vilevile katika ubora wake. Hii ikiwa na maana kama isingetunzwa na kulimwa, ingepotea kabisa, na kufanana tu na sehemu nyingine yoyote ya dunia.

Mwanzo 2:8 “Bwana Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa Edeni, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya…15 Bwana Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza.

Watunza bustani wanaelewa jambo hili, mahali ambapo wanazipanda, huwa ni lazima mara kwa mara, wawepo kung’oa majani-shambulizi yanayojitokeza, wanafyeka ukoka unapozidi kimo, wanatia mbolea panaposua sua, na wanainyeshea bustani kila siku, na wakati mwingine kuiwekea uvuli. Hivyo ni kazi ambayo inamgharimu mtunza bustani kuwepo pale wakati mwingi.

Ndivyo ambavyo Mungu alimpa jukumu hilo Adamu, kwamba aitunze bustani na kuilima, kwasababu hilo halikuwa jukumu lake tena. Tafsiri yake ni kwamba ili aendelee kukaa katika mahali pazuri pa nchi. Hana budi kupalima na kupatunza. Asipofanya hivyo pataendelea kuwa kama sehemu nyingine tu ya dunia.

Lakini Adamu, hakuweza kudumu katika bustani ile kwasababu aliyakaidi maagizo ya Mungu.

Hii ikifunua nini?

Kila mtu ameandaliwa Edeni yake hapa duniani, ambayo atamfurahia Mungu wake katika hiyo. Si kila mazingira Mungu amekuwekea wewe kumfurahia yeye, si kila mahali ni Edeni yako. Ipo sehemu maalumu, ambapo hapo Mungu anakuundia kisha wewe unapatunza baada ya hapo.

Na sehemu yenyewe ni ndani ya Kristo.

 Maana yake ni kuwa ukishaokoka, tayari Mungu amekuwekea mema yako mbeleni. Hivyo kuanzia huo wakati huna budi kuanza kuistawisha bustani yako kwa kuitilia mbolea mara kwa mara, kuinyeshea maji, kuipalilia, kuichonga n.k.. Ndio hapo, linakuja suala la Maombi ya mara kwa mara, mikesha, mifungo, kutafakari Neno, kufanya ibada za sifa,  kutoa sadaka, kujitenga na dhambi, na kushuhudia.

Unapokuwa mtu wa namna hii ndivyo unavyoifanya bustani yako kupendeza siku baada ya siku rohoni, ndivyo inavyojitofautisha na sehemu nyingine za dunia, kwa uzuri wake. Matokeo yake ni kuwa Dunia yako itakuwa ya neema sikuzote yenye furaha, Amani na mafanikio, yenye kububujika maziwa na asali. Lakini ukikaa tu ukasubiri, ukasema Mungu atatenda, huku huyatunzi  maneno ya Mungu ndani yako, sahau kuona mabadaliko yoyote maisha yako yatakuwa hayana tofauti na yale ya kale, kwasababu kazi ya utunzaji sio ya Mungu bali ni yako. Wewe umemsubiria Mungu, wakati Mungu alishamaliza kazi yake.

Litunze sana Neno la Mungu, kwa kuliishi sio kulisikia tu. Kwani wanaofanya hivyo wanafungua milango mingi sana ya kiroho, Kanisa la Filadelfia ndio kanisa pekee lililopendwa na Kristo kwasababu liliyatunza maneno yake, na matokeo yake likafunguliwa mlango wa mafanikio mbele yake.

Ufunuo 3:8  “Nayajua matendo yako. Tazama, nimekupa mlango uliofunguliwa mbele yako, ambao hapana awezaye kuufunga, kwa kuwa unazo nguvu kidogo, nawe UMELITUNZA NENO LANGU, wala hukulikana jina langu”.

Hivyo anza sasa kujibidiisha kulitendea kazi Neno la Mungu. Kwa jinsi unavyolitunza ndivyo utakavyoona mabadiliko yako.

Bwana akubariki.

Je! Umeokoka? Je, unatambua kuwa hizi ni nyakati za mwisho? Tunaishi katika dakika za nyongeza tu? Dalili zote zilizotabiriwa kuhusiana na kurudi kwa pili kwa Yesu zimeshatimia?. Wasubiri nini? Ukifa leo utajibu nini mbele ya kiti cha enzi cha Mungu?  Tubu sasa ukabatizwe, upokee ondoleo la dhambi zako. Ikiwa bado hujafanya hivyo, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi kwa msaada huo; +255693036618/+255789001312

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kuna tofauti gani kati ya  “Edeni” na “Adeni”?

UNAWAZA NINI SASA, JUU YA UFALME WA MBINGUNI?

EDENI YA SHETANI.

SISI TU MANUKATO YA KRISTO.

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

Kwanini Mungu hakumuua Nyoka, akamwacha Hawa ajaribiwe katika bustani ya Edeni?

Kwa jina lake Ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa.

AKAPITA KATIKA LILE SHAMBA AMBALO YAKOBO ALIMPA YUSUFU MWANAWE

Rudi nyumbani

Print this post

AGIZO LA TOBA LINAENDANA NA UBATIZO!.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu, Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia!.

Usipoujua ufunuo umhusuyo Yesu hutaona sababu ya kumwamini wala kumfuata, vile vile usipopata ufunuo wa kutosha uhusuo ubatizo hutaona umuhimu wa kubatizwa! (utaona ni habari tu ya kawaida, kwamba ukibatizwa au usipobatizwa vyote ni sawa tu).

Nataka nikuambie ndugu, ubatizo ni tendo la muhimu sana kuliko wengi tunavyodhani. Na leo nataka tuone ni jinsi gani agizo la Ubatizo lilivyoambata na Toba, kwamba baada ya kutubu ni lazima kubatizwa.

Hebu tuyasome maneno yafuatayo ya Bwana Yesu..

Luka 24:46  “Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu;

47  na kwamba mataifa yote “WATAHUBIRIWA KWA JINA LAKE HABARI YA TOBA NA ONDOLEO LA DHAMBI, kuanza tangu Yerusalemu”.

Nataka tuone na kuutafakari kwa kina huo mstari wa 47 unaosema kuwa mataifa yote watahubiriwa “KWA JINA LAKE HABARI YA TOBA NA ONDOLEO LA DHAMBI”

Hili ni agizo ambalo Bwana Yesu aliwapa wanafunzi wake kwamba watu wote ni lazima wahubiriwe habari ya toba na ondoleo la dhambi kwa jina lake.

Mitume walilisikia hili agizo la Bwana, na walilishika  sasa hebu tuangalie ni kwa namna gani walilitekeleza,..je walikwenda kuwaambia tu watu “watubu waondolewe dhambi zao au kuna la ziada walilifanya ”

Tusome kitabu cha Matendo 2:36-38

Matendo 2:36  “Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo.

37 Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38  Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.

Umeona hapa! Petro anawaambia watu “watubu na kubatizwa kwa jina lake Yesu, wapate ondoleo la dhambi zao”.. na sio tu “Tubuni mpate ondoleo la dhambi”….. sasa linganisha na yale maagizo Bwana aliyowapa akina Petro kuwa “wakawahubirie watu wote kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi”.

Kumbe kuhubiriwa habari ya Toba na ondoleo la dhambi ni pamoja na ubatizo!.. Maana yake ili mtu apate ondoleo kamili la dhambi zake ni lazima pia akabatizwe (Katikati ya Toba na ondoleo la dhambi, kuna ubatizo ambao shetani kawafumba watu macho wasiuone)..Ndio maana ni ngumu leo hii wengi kushinda dhambi, kwasababu mzizi wa dhambi katika maisha yao haujaondolewa, kwasababu wameukosa ubatizo sahihi.

Mitume sehemu zote walihubiri hivi, kwamba watu baada ya kutubu ni lazima wakabatizwe ili dhambi zao ziondolewe… na mitume kamwe wasingeweza kufanya kitu chochote kilicho kinyume na maagizo ya Bwana Yesu…ikiwa na maana kuwa walimwelewa sana Bwana pale aliposema kuwa wakawahubirie mataifa yote kwa jina lake, kwamba ubatizo pia kwa jina lake ni sehemu ya mahubiri yao.

Swali ni je!, na wewe umebatizwa kwa maji mengi na  katika ubatizo sahihi wa jina la Bwana Yesu?.. Kumbuka, kama ulibatizwa utotoni basi fahamu kuwa watoto wachanga hawabatizwi kwasababu bado hawajatubu, (kujitambua hawajajitambua watawezaje kutubu?) ni sharti kwanza wahubiriwe wamwamini Mwokozi na kujijua kuwa wao ni wenye dhambi ndipo watubu na kubatizwa.  Bwana akubariki.

Tafuta ubatizo sahihi kama bado hujabatizwa, na kama utahitaji msaada Zaidi wa namna ya kupata ubatizo karibu na mahali ulipo basi utawasiliana nasi kupitia namba zetu hapa chini.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

LISHIKILIE SANA LILE AGIZO LA KWANZA.

TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU

HUNA SHIRIKA NAMI.

BASI TUENDELEE KUMJUA MUNGU,NAYE ATATUJILIA KAMA MVUA YA VULI.

Rudi nyumbani

Print this post

Wakolosai 3:5 inamaana gani?

SWALI: Wakolosai 3:5 inamaana gani?. Tofauti kati ya tamaa mbaya na kutamani ni ipi?


JIBU: Wakolosai 3:5 Inasema..

  “Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu;”

Hapo anaanza kwa kusema vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi. Ikiwa na maana kuwa kuna viungo vya duniani ambavyo kazi yake kimsingi ni kutimiza mapenzi ya duniani (ya shetani). Tofuati na vile vya ki mbinguni ambavyo vinatimiza mapenzi ya Mungu. Viungo hivi sio mikono, miguu, macho, masikio au pua hapana, bali viungo vya rohoni.

Viungo vya kimbinguni vimeelezwa kwenye mstari wa 12-17. Lakini vya duniani ndio hivi vinavyozungumziwa hapa katika mstari wa 5, ambavyo tunapaswa tuviue. Navyo ni;

1) Uasherati.

Uasherati unajumuisha kitendo chochote cha zinaa nje ya ndoa pamoja na mambo yafanywayo kinyume na asili. Ikiwemo Uzinzi, ufiraji, na ulawiti. Vitu hivi havipaswi vipewe nafasi kwa mtakatifu yoyote.

2) Uchafu

Uchafu ni kinyume na usafi. Mtu mchafu kimsingi anakuwa amebeba takataka katika mwili wake. Vivyo hivyo, mtu ambaye anaruhusu takataka za hii dunia zimtawale ni mchafu kiroho. Mfano wa takatakata hizi ni miziki ya kidunia, anasa, matusi, ulevi, kubeti, mazungumzo yasiyofaa, kutazama vitu visivyojenga mitandaoni, ushabiki n.k. Epuka kujitia unajisi na vitu vya ki-ulimwengu.

3) Tamaa mbaya.

Kuzipa tamaa za mwili nafasi ya kukutawala. Na matokeo ya tamaa hizi mbaya kukutawala ndani yako, utaishia, ni kutazama picha chafu, muda wote kuwa na mazungumzo ya kizinzi, kuchat na jinsia tofauti na wewe kusikokuwa na sababu, kuvaa mavazi ya namna hiyo au kujiwekwa kimwili uvutie uzinzi kwa mwengine. Tabia hizi ndani yako unapaswa uziue.

4) Mawazo mabaya.

Mawazo mabaya ni kinyume cha mawazo mazuri. Mtu mwenye mawazo mazuri huwaza yaliyo mazuri, ya kujenga. Lakini mwenye mawazo mabaya sikuzote ni kubomoa. Mawazo hayo ni pamoja na wivu, rushwa, uongo, wizi, uuaji, unafki, visasi,. Hivi havipaswi kuonekana ndani ya mkristo.

5) Kutamani.

Kutamani kunakozungumziwa hapa sio kule kwa tamaa za mwili, hapana, bali tamaa ya mambo ya kidunia, mfano tamaa ya kuwa na mali, tamaa ya kufanana na watu wa kidunia, wanamiziki, wanamitindo n.k., na hizo ndizo zinazompelekea mtu, kugeuza vitu hivyo kuwa kama mungu wao, kuvitafuta na kuvisumbukia sikuzote .Na ndio maana mwandishi anamalizia kwa kusema “Ndiyo ibada ya sanamu” maana yake rohoni vinaonekana ni miungu kwao. Jiepushe na kutamani.

Hivyo  tukifanikiwa kuviua viungo hivi, basi mwili hauwezi kuwa na matunda yoyote, kwasababu hakuna kiungo chake hata kimoja kina uhai. Lakini pia anasema,

Wakolosai 3:12  Basi, kwa kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu,

13  mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.

14  Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.

15  Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani.

16  Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.

17  Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.

Hivyo ndivyo viungo vya kimbinguni, Tujitahidi vituvae.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Nini maana ya huu mstari “sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje”

WAPENDENI ADUI ZENU, WAOMBEENI WANAOWAUDHI.

Ni nani aliye kipofu, ila mtumishi wangu?

Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?

Rudi nyumbani

Print this post

Birika walilooga Makahaba lilikuwaje?

Swali: Katika kifo cha Ahabu, biblia inasema alikufa na gari lake likaenda kuoshwa katika birika ambalo wanaoga Makahaba, (1Wafalme 22:38)..hili birika walilokuwa wanaoga makahaba lilikuwaje?

Jibu: Turejee.

1Wafalme 22:37 “Hivyo akafa mfalme, akachukuliwa Samaria, wakamzika mfalme huko Samaria. 

38 Wakaliosha gari penye birika la Samaria, na mbwa wakaramba damu yake; (basi ndipo walipooga makahaba); sawasawa na neno la Bwana alilolinena. 

39 Na mambo yote ya Ahabu yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, na nyumba ya pembe aliyoijenga, na miji yote aliyoijenga, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli?”

Ikumbukwe Ahabu alimwua Nabothi Myezreeli na kumdhulumu kiwanja chake, (1Wafalme 21:1-16), na baada ya kumwua ndipo unabii ukaja kupitia Eliya, kumwambia kuwa atakufa na damu yake italambwa na mbwa kama alivyomwua Nabothi (soma 1Wafalme 21:17-27).

Baada ya miaka mitatu, ndipo unabii huo unakuja kutimia, Mfalme Ahabu alikufa alipokuwa vitani na damu yake ikalambwa na mbwa mahali pale pale mbwa walipolamba damu ya Nabothi.

Lakini tunasoma tena jambo lingine lililoambatana na kifo cha Ahabu, kwamba mahali pale gari lake lilipooshwa ni mahali pia Makahaba wanapooga.

Sasa biblia haijaeleza kwa kina hili birika ambalo walikuwa wanaoga makahaba lilikuwaje. Lakini ni wazi kuwa hili halikuwa birika la kiyahudi, Kwani mabirika/ mabwawa ya kiyahudi yalikuwa yanatumika na makuhani na watu wa kawaida katika kuoga(kutawadhia) ili kujitoa unajisi.

Walawi 15: 16 “Na mtu ye yote akitokwa na shahawa yake, ndipo ataoga mwili wake wote majini, naye atakuwa najisi hata jioni”.

Soma pia Walawi 15:13, Kumbukumbu 23:10-11.

Lakini hili Birika/bwana hili ambalo makahaba walikuwa wanaoga, lilikuwa katika mji wa Samaria mtaa wa Yezreeli, ambao ndio ulikuwa kitovu cha ibada zote za mungu baali. Hivyo hili halikuwa bwawa la dini ya kiyahudi, bali lilikuwa ni bwawa la mungu baali. Huenda makahaba walikuwa wanaoga hapo kulingana na desturi zao za kibaali, kwani desturi nyingi za dini ya kibaali zilikuwa zinakaribia kufanana na za dini ya kiyahudi.. (mfano wa hizo utaona ni ile sadaka Ahabu aliyoitoa katika 1Wafalme 18:20-30).

Hivyo huenda nao pia walikuwa na desturi kama hiyo ya wayahudi ya kujiosha katika mabwawa/mabirikia.

Lakini lililo kubwa la kujifunza hapo ni kuwa Neno la Mungu kamwe halipiti.. Alisema Ahabu atakufa na damu yake italambwa na mbwa, na kweli alikufa sawasawa na neno hilo miaka mitatu baadaye, katika kifo cha aibu zaidi hata ya  kile alichomuua Nabothi.

Na vile vile alisema, kuwa atarudi tena pamoja na ujira wake kulimlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo, Neno hilo halitapita, ni lazima litimie na sasa tupo katika siku za kurudi kwake, muda wowote unyakuo unatokea!

Ufunuo 22:12  “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

13  Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.

14  Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake”

Je umeokoka kikweli kweli au bado una uvuguvugu?…Ufunuo 3:16 “Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu”.

Mathayo 24:35 “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Je Mungu anaweza kumdanganya mtu?

BIRIKA LA SILOAMU.

USIMPE NGUVU SHETANI.

Baali alikuwa nani?

Birika ni nini?, na yale Matao matano katika birika la Bethzatha ni nini?.

Rudi nyumbani

Print this post

Chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu ndio kipi? (Matendo 21:25).

Jibu: Turejee,

Matendo 21:25 “Lakini kwa habari za watu wa Mataifa walioamini, tuliandika na kutoa hukumu yetu ya wao kujilinda nafsi zao na vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, na kitu kilichosongolewa, na uasherati”


Vyakula vilivyotolewa sadaka kwa sanamu ni vyakula vyote vinavyotolewa kwa maagizo ya kishetani.
Mfano wa vyakula hivyo ni vile vya kimila au vya waganga wa kienyeji.

Mfano wa vya kimilia ni vile ambavyo mtu anakula au analishwa kwa lengo la kumkinga na madhara fulani ya kiroho kama uchawi au kumpatanisha na roho fulani..


Ndio hapo utakuta mtu anaambiwa alete mbuzi, au kondoo na kisha yule kondoo achinjwe kama sadaka/kafara kwa mizimu na kisha ale sehemu ya nyama ya huyo mnyama aliyetolewa sadaka… Sasa endapo mtu huyo akila hiyo nyama au sehemu ya hiyo nyama tayari anakuwa amekula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu.


Au utakuta mtu anaenda kwa mganga wa kienyeji na yule mganga anamwambia ili tatizo lake litatulike basi alete mnyama fulani aidha mbuzi, au ng’ombe au kuku na achinjwe kama kafara na nyama yake au damu yake inywewe na mhusika.. Mtu anayekula hiyo nyama anakuwa tayari amekula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu.


Au anaweza asiambiwe alete mnyama, bali akaambiwa alete hata nafaka fulani na kisha ile nafaka ikatolewa kwa miungu na mtu akaambiwa ashiriki sehemu ya ile nafaka..sasa mtu huyo endapo akila kile chakula au sehemu ndogo ya kile chake basi anakuwa amekula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu.


Na mtu anayekula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu, anakuwa anajiungamanisha na ile madhabahu ya kishetani..ndivyo biblia inavyosema.


1 Wakorintho 10:19-22 “Basi niseme nini? Ya kwamba kile kilichotolewa sadaka kwa sanamu ni kitu? Au ya kwamba sanamu ni kitu?
20 Sivyo, lakini vitu vile wavitoavyo sadaka wavitoa kwa mashetani, wala si kwa Mungu; nami sipendi ninyi kushirikiana na mashetani. Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana na kikombe cha mashetani.
21 Hamwezi kushirikiana katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani.
22 Au twamtia Bwana wivu? Je! Tuna nguvu zaidi ya yeye?


Hiyo ni tahadhari kwetu kuwa tujiepushe na vyakula vya namna hiyo kwani ni hatari kiroho.
Lakini kama umealikwa mahali na umetengewa chakula ambacho kimetolewa sadaka kwa sanamu na ukala bila kujua kuwa kilikuwa kimetolewa sadaka kwa miungu, hapo hupaswi kuogopa kwasababu lile andiko ya kwamba “tutakula vitu vya kufisha navyo havitatudhuru (Marko16:18)” litatimia juu yako.


Lakini kama umeshajua kuwa chakula hicho ni cha miungu basi hupaswi kula kabisa..


Je umewahi kula au kulishwa chakula cha namna hiyo katika familia yenu au ukoo wenu au kwa waganga wa kienyeji?..Kama ndio basi fahamu kuwa siku ulipokula tayari ulijiungamanisha na hiyo miungu, na hivyo roho za hiyo miungu zitayaongoza maisha yako siku zote.


Hivyo suluhisho ili uweze kufunguka ni wewe kwanza kutubu mbele za Bwana kwa kumaanisha na kisha kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana Yesu Kristo (Matendo 2:38) na mwisho kupokea Roho Mtakatifu..Kwa hatua hizo utakuwa umefunguliwa moja kwa moja.


Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

“Kinga kilichotolewa motoni “Kinafunua nini kibiblia?

Sadaka ya Amani ilikuwaje?

Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?

HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU

Rudi nyumbani

Print this post

NIFANYE NINI ILI NIKUBALIWE NA YESU?

Boazi na Ruthu.

Atukuzwe Yesu Kristo Bwana wetu  na mwokozi wetu, Nakukaribisha tuzidi kuzitafakari siri za ufalme wa mbinguni.

Awali ya yote tukumbuke kuwa mahusiano ambayo Yesu anayatengeneza kwa kila mwaminio sio mahusiano kama ya rafiki na rafiki, au ndugu na ndugu, hapana, bali kama ya Bwana-arusi na Bibi-arusi.

Ni vema hilo ukalifahamu mapema, kwasababu kitakachotufanya tuende mbinguni, ni Ndoa, na sio urafiki. Hivyo yeye kama Mfalme ndio Bwana-arusi, na sisi ni Bibi-arusi wake. Tunapojiunganisha naye, ni lazima tuonyeshe tabia za bibi-arusi wa kweli, vinginevyo hatutapata kibali cha kuwepo katika karamu ya Arusi yake, atakayoifanya mbinguni kwa wateule wake kwa tukio linalojulikana kama Unyakuo.

Mimi na wewe hatua budi kuhakikisha tunakuwa bibi-arusi safi wa Kristo, na sio masuria, ili tupate kibali cha kukubaliwa na yeye siku ile ya mwisho.

Leo wa neema za Bwana, tutajifunza kwa kupitia maisha ya Boazi na Ruthu. Kumbuka hadithi zote unazozisoma katika biblia zina ufunuo wa Kristo na kanisa lake. Hivyo usomapo hakikisha unamwomba Roho Mtakatifu akufunulie, ili biblia kwako isiwe kama vitabu vingine vya hadithi.

Sasa kama wewe ni mwanafunzi wa Biblia utakuwa umeshawahi isoma habari ya Ruthu. (Kama hujasoma nashauri ukakisome kwanza hicho kitabu, ndipo utaelewa vema, kiini cha somo hili, kwasababu hatutakichambua chote).

Utakumbuka, Boazi alikuwa ni shemeji wa yule mwanamke mjane aliyeitwa Naomi. Biblia inasema Boazi alikuwa ni tajiri sana, na mkuu katika mji ule. Lakini huyu Naomi alikuwa pia na mkwe wake aliyeitwa Ruthu.

Ruthu naye alikuwa mjane, kwani alifiwa na mume wake kabla hajapata mtoto. Hivyo wote wawili walikuwa ni wajane yaani Naomi na Ruthu, isipokuwa Ruthu alikuwa bado ni kijana aliyekidhi vigezo vya kuoelewa tena, lakini Naomi alikuwa ameshakuwa mkongwe hawezi kuolewa tena.

Lakini siku moja Naomi, akaona si vema mkwe wake Ruthu abakie kama yeye. Akaanda mazingira ya kumpatia mkwe wake mume mwingine, ndipo akachunguza na kuona kuwa Boazi ndiye amfaaye. Hivyo akaunda mpango aliokuwa na uzoefu nao, akamfundisha Ruthu namna ya kumwingia, na kwa kupitia njia ile basi Ruthu atapata kibali, kwa mtu huyu tajiri na mkuu wa mahali pale.

Embu tuutazame mpango wenyewe, tunaousoma katika ile sura ya 3, kisha tuone kanuni na sisi ya kukubaliwa na Kristo.

Ruthu 3:1 “Kisha Naomi akamwambia mkwewe, Je! Mwanangu, si vizuri nikutafutie raha, ili upate mema?  2 Basi na huyu Boazi, je! Siye wa mbari yetu, ambaye ulikuwapo pamoja na wasichana wake? Tazama, usiku wa leo atakuwa akipepeta shayiri pale ugani. 

3 Basi wewe oga, ujipake mafuta ujivike mavazi yako, kisha uende kwenye uga; walakini usijionyeshe kwake mtu yule, ila atakapokwisha kula na kunywa. 

4 Nayo itakuwa wakati atakapolala, utapaangalia mahali alalapo, nawe uingie, uifunue miguu yake ujilaze hapo; na yeye atakuambia utakalofanya. 

5 Akamwambia, Hayo yote unenayo mimi nitayafanya. 

6 Basi akashuka mpaka ugani; akafanya yote kama vile mkwewe alivyomwagiza”

Ukichunguza hapo utaona, Ruthu anapewa hatua tano za kupitia.

  1. Kuoga
  2. Ajipake mafuta
  3. Ajivike mavazi yake
  4. Aende Ugani kwa siri
  5. Akalale miguuni pake
  1. Kuoga

Naomi alijua uchafu, haupatani na bibi-arusi yoyote. Hakuna mume anayependa mwanamke mchafu, ni sharti awe msafi tena kwelikweli. Ndipo hapo sasa utaona akamwambia Ruthu akaoge kwanza awe safi. Ikifunua kuwa mkristo yoyote kabla ya kukubaliwa na Kristo, ni sharti kwanza awe safi kwa maji, yaani Ubatizo, ambao unaleta ondoleo la dhambi zake. Kama hujabatizwa, ni sharti ubatizwe katika maji ya kuzama, na kwa jina la Yesu Kristo, ili dhambi zako ziondolewe, Ndipo ukidhi hatua ya pili ya kumkaribia Kristo.

2) Kujipaka mafuta

Kuoga tu peke yake haikutosha aliambiwa pia ajipake mafuta, Ikifunua kuwa Mkristo yoyote ni lazima awe na mafuta rohoni mwake. Na mafuta hayo ni Roho Mtakatifu. Ukikosa Roho Mtakatifu kamwe huwezi kukubaliwa na Kristo.

Matendo 2:38  “Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”

3) Avae mavazi mengine.

Ruthu alikuwa na mavazi yake ya kawaida, lakini hapa Naomi anampa shauri avae mavazi mengine yanayofanana na ya bibi-arusi, meupe safi, aonekane tofauti na wanawake wengine, apendeze, avutie machoni pa Boazi atakapoenda kujionyesha kwake.

Maana yake ni kuwa kila mkristo lazima awe na vazi la arusi, na vazi lenyewe ni Utakatifu. Kama tunavyosoma katika Ufunuo 19:8.Ukipoteza utakatifu, kamwe Kristo hawezi kukupokea, haijalishi utasema nimeokoka.

4) Kwenda ugani kwa siri

Ugani ni mahali wanapopepeta nafaka, Hivyo Boazi alikuwa ni mtu wa kazi, muda wote utamkuta yupo kazini kwake, si mtu aliyekuwa mlegevu, Ukitaka kumpata sharti na wewe pia uingie ugani kwake. Hivyo Ruthu ilimpasa aende vilevile, lakini alipewa maagizo kwamba iwe kwa siri, asijulikane na mtu yoyote yule.

Ikifunua kuwa, pamoja na kwamba, utakuwa umeokoka, huna budi kujishughulisha na kazi ya Bwana. Na wewe pia uwepo shambani mwake, lakini ukiwa na vazi lako la thamani(yaani Utakatifu). Na wakati uwapo huihitaji, kutenda kazi yake kama mtu wa mshahara bali kama mtumwa asiyekuwa na faida, uhakikishe upo kama mtu asiyetambulika na Kristo. Unatumika ndipo baadaye yeye mwenyewe aone vema kujifunua kwako.

Luka 17:5  Mitume wakamwambia Bwana, Tuongezee imani.

6  Bwana akasema, Kama mngekuwa na imani kiasi cha chembe ya haradali, mngeuambia mkuyu huu, Ng’oka, ukapandwe baharini, nao ungewatii.

7  Lakini, ni nani kwenu mwenye mtumwa alimaye au achungaye ng’ombe, atakayemwambia mara arudipo kutoka shambani, Njoo upesi, keti, ule chakula?

8  Je! Hatamwambia, Nifanyie tayari chakula, nile; jifunge unitumikie, hata niishe kula na kunywa, ndipo nawe utakapokula na kunywa?

9  Je! Atampa asante yule mtumwa, kwa sababu ameyafanya aliyoagizwa? 10  Vivyo hivyo nanyi, mtakapokwisha kuyafanya yote mliyoagizwa, semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya

5) Kujilazama miguuni pake

Na hatua ya mwisho aliyopewa Ruthu na Naomi  ni  kujilaza miguuni pa Boazi.  Maana yake ni kujivika unyenyekevu, Unakubali kulala kwenye miguu yenye mavumbi ya Bwana wako.  unathamini cha Bwana ambacho kinadharauliwa, unathamini watu wa Mungu, .. Hapo ndipo pawe makazi yako daima, penye unyenyekevu.

Hivyo baada ya kutimiza, hatua zote hizo 5, yaani kuoga, kujipaka mafuta, kuvaa vazi la bibia-arusi, kudumu ugani na kulala chini ya miguu ya Yesu. Fahamu kuwa Kristo atajidhihirisha kwako, kama Boazi wa Ruthu.

Kumbuka maagizo hayo yote, Ruthu hakujiamulia tu, bali aliyapokea, kwa mkwe wake mzoefu aliyeitwa Naomi. Na sisi Naomi wetu ni Mitume na Manabii, yaani Biblia Takatifu. Tukiipenda, kuyashika yaliyoandikwa mule, basi tutakuwa bibi-arusi wa Kristo kwelikweli. Mtume Paulo aliandika hivi;

2Wakorintho 11:2  “Maana nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi.

3  Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo”.

Zingatia:  Kama wewe si bibi-arusi, huwezi kwenda kwenye Unyakuo. Hizi ni siku za mwisho, wakati wowote Yesu anarudi, Je! umejiandaaje? Utajibu nini siku ile, utakapoulizwa kwanini hukuitii injili? Wakati ni mchache sana tunaishi katika dakika za nyongeza tu, Tengeneza maisha yako sasa, huu sio wakati wa kuhubiriwa injili ya kubembelezwa, ni wewe mwenyewe uone uhalisia utubu. Yesu yupo mlangoni.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

KWANINI UNAPASWA UWE BIBI ARUSI NYAKATI HIZI ZA MAJERUHI?

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:

ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.

INAYOENDELEA SASA NI HUDUMA YA RUTHU.

EWE MKE! HESHIMA YAKO IPO KWA WAKWE ZAKO.

KAMA MKRISTO FAHAMU ZIPO HATUA UTAPIGISHWA NA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

KUWA MAKINI, HATUA ZA UNYAKUO ZINAENDELEA.

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tuzidi kuyatafakari maneno ya uzima.

Je! Unahabari kuwa watakaonyakuliwa wameshaanza kuandaliwa?  Je! Wewe upo katika hatua ipi?

Biblia inasema zipo hatua ambazo Bwana atatumia kushuka kabla haijaja siku ile yenyewe ya sisi kutwaliwa kwenda mbinguni. Hivyo haitakuwa tendo la kushtukiza kwa wale ambao tayari yameshaingizwa katika hatua hizo.

Angalia ni nini Bwana anasema hapa..

1Wathesalonike 4:16  “Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na MWALIKO, na SAUTI YA MALAIKA MKUU, na PARAPANDA YA MUNGU; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. 17  Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. 18  Basi, farijianeni kwa maneno hayo.”

 Tafakari kwa makini hayo maneno, Bwana hasemi atashuka na “Parapanda” nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu. Hapana Bali anasema, ataanza kwanza na MWALIKO, kisha SAUTI YA MALAIKA MKUU na ndipo Parapanda ya Mungu mwisho. Tofauti na sisi tunavyofikiri, kuwa ni parapanda tu ndio tutakaoisikia ndipo tunyakuliwe.

Ndugu, tafsiri ya hayo maandiko ni kuwa huwezi kuisikia parapanda ya Mungu, kama hujaitikia hatua ya mwaliko na hatua ya sauti ya malaika mkuu. Hivyo Embu tukautazame huo mwaliko ni upi na hiyo sauti ya malaika mkuu ni ipi?

1) MWALIKO.

Awali ya yote tukumbuke kuwa lengo la kunyakuliwa sisi ni ili kwenda kula karamu ya arusi ya mwanakondoo mbinguni, aliyoiandaa Yesu Kristo kwa ajili yetu, kama alivyosema katika Yohana 14:1-4 na Ufunuo 19:9. Hivyo kama tunavyojua hakuna sherehe yoyote isiyokuwa na mwaliko. Hakuna mtu anayejikuta tu kwenye arusi ya mtu bila kualikwa, hakujawahi kuwa na utaratibu huo. Na ndivyo Yesu naye, kabla ya kutupelekea huko mbinguni alipotuandalia vinono, ni sharti kwanza atualike. Hapo ndipo akatumia mfano mmoja wa Mfalme aliyemfanyia mtoto wake karamu kubwa. Lakini katika kuwaalika watu wake, kukawa na mwitikio tofauti tofauti,

Embu tuisome habari hiyo tupate kuielewa vizuri; (Soma kwa utulivu) kwasababu hapa ndipo palipo na msingi.

Mathayo 22:1  “Yesu akajibu, akawaambia tena kwa mithali, akisema, 2  Ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyemfanyia mwanawe arusi.

3  Akawatuma watumwa wake wawaite walioalikwa kuja arusini; nao wakakataa kuja.

4  Akatuma tena watu kwa wengine, akisema, Waambieni wale walioalikwa, Tazameni, nimeandaa karamu yangu; ng’ombe zangu na vinono vimekwisha kuchinjwa, na vyote vimekuwa tayari, njoni arusini.

5  Lakini hawakujali, wakaenda zao, mmoja shambani kwake, mmoja kwenye biashara yake;

6  nao waliosalia wakawakamata watumwa wake, wakawatenda jeuri, na kuwaua.

7  Basi yule mfalme akaghadhibika; akapeleka majeshi yake, akawaangamiza wauaji wale, akauteketeza mji wao.

8  Kisha akawaambia watumwa wake, Arusi i tayari, lakini wale walioalikwa hawakustahili.

9  Basi enendeni hata njia panda za barabara, na wote mwaonao waiteni arusini.

10  Watumwa wale wakatoka wakaenda njia kuu, wakakusanya wote waliowaona, waovu kwa wema; arusi ikajaa wageni.

11  Lakini alipoingia yule mfalme ili kuwatazama wageni wake, akaona mle mtu mmoja asiyevaa vazi la arusi.

12  Akamwambia, Rafiki, uliingiaje humu nawe huna vazi la arusi? Naye akatekewa.

13  Mfalme akawaambia watumishi, Mfungeni mikono na miguu, mchukueni mkamtupe katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.

14  Kwa maana waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache.

Ukitafakari hapo, utajiuliza, iweje mfalme akualike kwenye sherehe yake halafu usiende?..Ni heri angekuwa mtu wa kawaida, lakini walioalikwa hawakulijali hilo, kwamba yule ni mfalme na sio mtu wa kawaida, hawana budi kuahirisha shughuli zao waende, kwani wamepewa heshima kubwa, lakini  kwao mambo yalikuwa tofauti, wakapuuzia na kibaya zaidi wakawapiga na kuwaua baadhi ya watumwa wake.

Sasa hawa wanalinganishwa na wayahudi, ambao ndio waliokuwa wa kwanza kupewa mwaliko huu ya injili, lakini waliwaangamiza, manabii wengi wa Mungu, mpaka ikafikia hatua ya Kristo akawakataa kabisa, akawakatilia mbali (Soma Mathayo 23:37-39). Hivyo Mungu akahamishia mpango wake wa wokovu kwa watu wa mataifa, ambao ndio mimi na wewe.

Ambao tunalinganishwa sasa na hao waovu, na vilema, waliookotwa huko mabarabarani wakaalikwa kwenye karamu. Maandiko yanatuambia kundi hilo halikukataa mwaliko kama lile la kwanza. Bali lilikubali lote, Lakini sasa ndani ya ukumbi, akaonekana mmoja ambaye alikuwa tofauti na wenzake, yeye hakuwa na “vazi la arusi”. Utajiuliza ni kwanini akose vazi lile? Ni kwanini asifanane na wenzake? Utagundua kuna jambo alilipuuzia, ambalo angepaswa alifanye kabla ili akidhi vigezo vya yeye kuila karamu.

Sasa kabla hatujatazama vazi hilo ni nini? Maana ya mfano huo ni mwaliko wa wokovu ambao tunahubiriwa sisi sote. Ukweli ni kwamba leo hii lipo japo kubwa la watu katika kanisa “wanaokiri wokovu”, wengi wao wamebatizwa, wanashiriki ibada kama kawaida kanisani, wanatoa zaka, wote wanakiri kuwa wanamsubiria Yesu aje kuwanyakua. Lakini je! Ni wote watakaonyakuliwa?  La! Bwana anasema..Siku ile Mmoja atanyakuliwa mmoja ataachwa!(Mathayo 24:40-41) .. Maana yake ni kwamba hupaswi kuridhika tu kuitwa mkristo, lipo jambo la ziada unapaswa ufanye ili ukidhi vigezo vya kuiila karamu ya mwanakondoo mbinguni. Usiridhike tu kusema mimi ni mshirika, mimi ni muumini, acha kabisa hayo mawazo, katika siku hizi za mwisho tunazoishi, yule mtu aliketi kabisa ukumbini, akaona vinono vyote lakini hakula hata kimoja..Sasa embu tuitazame hatua ya pili,

2) SAUTI YA MALAIKA MKUU.

Bwana anasema atashuka na..”Sauti  ya malaika mkuu”. Maana yake ni kwamba kabla ya kuisikia parapanda, ni sharti uisikie hii sauti ya malaika mkuu. Tukirudi katika hiyo habari, ni kwamba yule mtu ambaye hakuwa na mavazi ya arusi, hakuisikia/aliipuzia sauti ya mjumbe aliyesimama pale mlangoni kuwapa maelekezo ya namna ya kukubaliwa katika karamu. Wakati wenzake wanamsikiliza, walipoambiwa wakaoge, wabadili mavazi yao ya kihuni, ya ki-utupu, ya ki-zinzi, ya ki-dunia. Wavae mavazi meupe ya sherehe, yeye akaona ule ni mzigo mzito sana, anamnyima uhuru wake, akataka kwenda kipekee pekee na staili zake, maadamu ameshapewa heshima ya kualikwa na mfalme. Hawezi kuzuiliwa. Hivyo akaendelea kustarehe vilevile pale ukumbini, akimsubiria mfalme, kuja kuwapongeza wageni wake waliomtii.  Lakini alipofika kwake, akidhani, sasa ni wakati wa kupongezwa, akashangaa amebadilikiwa uso, badala ya kupongezwa, ndio kwanza anafungwa Kamba kama vile vibaka, kisha anatupwa nje!

Unajua ni kwanini mpaka biblia inasema ndipo kutakuwa na kilio na kusaga meno, maana yake ni kuwa huyu mtu ambaye alikuwa ameshaweka mawazo yake katika kusheherekea, ghafla anajikuta yupo nje, ni wazi kuwa yeye ndio atakayeumia Zaidi kuliko wale ambao hawakuwahi kualikwa kabisa.

Hivyo kundi hili linafananishwa na watu wote, wanaoitwa wakristo walio kanisani, lakini hawana mavazi ya arusi. Na vazi la Arusi ni UTAKATIFU. Maandiko yanasema hivyo.

Ufunuo 19:7  “Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na mkewe amejiweka tayari.

8  Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni MATENDO YA HAKI YA WATAKATIFU.

9  Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo. Akaniambia, Maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu.

Ndio maana malaika wa kanisani letu la Mwisho lijulikanalo kama Laodikia. Alipewa ujumbe, unaotuhusu sisi. Ambao hautaki tuwe vuguvugu. Kwasababu tukiwa vuguvugu tutatapikwa. Kumbuka kila kipindi cha Kanisa kilikuwa na malaika wake, mtoa ujumbe, na huyo malaika, alisema kigezo cha kila mmojawao kukubaliwa na Kristo. Tangu kanisa la kwanza, hadi sasa tupo kanisa la mwisho la saba, lijulikanalo kama Laodikia.

Huyo ndio malaika wetu mkuu, ambaye kaachiliwa kutushushia ujumbe huo, hatuna budi kuisikia sauti yake. Kwamba tuwe moto tusiwe vuguvugu, vilevile tununue mavazi meupe, kwa Kristo. Yaani  tuishi maisha matakatifu wasiokuwa na madoa, ili tukidhi vigezo vya kunyakuliwa kwasababu tukikosa maisha hayo, kamwe tusijidanganye sisi ni wakristo.

Tuusome ujumbe wetu;

Ufunuo 3:14  “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu.

15  Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. 16  Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

17  Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.

18  Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, NA MAVAZI MEUPE UPATE KUVAA, AIBU YA UCHI WAKO ISIONEKANE, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.

19  Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.

20  Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.

21  Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi.

22  Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa”

Hivyo wewe kama mkristo, Epuka maisha ya uvuguvugu. Sababu ya wale wanawali watano wapumbavu kutoingia karamuni, ilikuwa ni hiyo hiyo ya uvuguvugu, hawana mafuta ya kutosha kuziwasha taa zao (Mathayo 25). Mungu anajua tabia ya kanisa la sasa, halipendi kukemewa dhambi linapenda mwonekano wa nje tu, lakini ndani ya uchafu. Bwana atusaidie roho hii isituvae.

3) PARAPANDA YA MUNGU.

Sasa ukishakidhi vigezo hivyo, maana yake unakuwa umepita kigezo cha “walioitwa” mpaka kuwa “mteule”. Unachongoja wewe ni unyakuo tu, parapanda itakapolia, utapaa mawinguni, na hata ukifa kabla Yesu hajarudi, utafufuliwa siku ile, kwasababu ulitii mwaliko na Sauti ya Malaika wako mkuu.

Lakini ukifa katika ukristo vuguvugu, kisha ukafa leo, siku ile ya unyakuo hutafufuliwa na watakatifu wengine, utaendelea kubaki makaburini mpaka siku ya hukumu. Ndugu, unasubiri nini, usiokoke? Na ikiwa umeokoka, maisha ya uvuguvugu utaendelea nayo mpaka lini? Leo upo kanisani, kesho disco, leo unamsifu Mungu, kesho unasikiliza nyimbo za kidunia, leo unatoa sadaka, kesho unakula rushwa, hayo maisha yatakufikisha wapi? Hujui kuwa tunaishi katika kizazi ambacho yamkini kinaweza shuhudia tukio la Unyakuo, kutokana na kutimia kwa dalili zote za siku za mwisho?

Embu tubu sasa umaanishe kumfuata Yesu, mambo aliyotuandalia Yesu ni mazuri yasiyoelekeza, mambo ambayo jicho haliwahi kuona wala sikio kusikia. Tusiyakose hayo. Kosa kila kitu, Usikose Unyakuo. Ikiwa upo tayari kutubu leo dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha.

Wasiliana nasi kwa namba hizi bure +255693036618/ +255789001312, tukupe mwongozo wa sala ya toba.. Fanya uamuzi wa haraka sasa, kwani kesho si yao.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

KWANINI KUWE NA UTAWALA WA MIAKA 1000

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

BONDE LA KUKATA MANENO.

Kutekewa maana yake nini?(Mathayo 22:12)

JIPE MOYO MKUU.

Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza

Rudi nyumbani

Print this post

JE UMEKUFA PAMOJA NA NANI?

Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu.

Warumi 6:8  “Lakini tukiwa TULIKUFA PAMOJA NA KRISTO, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye”

Kabla ya kujitathmini kama kweli tulikufa pamoja na Kristo hebu kwanza tukitafakari kifo cha Bwana Yesu.

Tunasoma kifo cha Mwokozi wetu hakikuwa cha ugonjwa, au cha uzee, au cha ajali… bali kilikuwa ni kifo cha mateso, Bwana Yesu alibeba msalaba wake mpaka Golgotha, na pale akatundikwa msalabani kwa dhihaka nyingi na  maumivu makali na kwa masaa mengi.

Lakini pamoja na hayo alisema kuwa “mtu yeyote akitaka kumfuata, ajikane mwenyewe ajitwike msalaba wake ndipo amfuate..

Marko 8:34  “Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate”.

Nataka tutafakari kwa undani mambo hayo matatu (3), kujikana, kubeba msalaba na kumfuata Yesu…

1. Ajikane mwenyewe.

Maana ya kujikana, ni kukataa mapenzi yako na kujiachilia kwa mapenzi ya mwingine, hivyo Kristo anataka mtu yeyote anayetaka kumfuata ni lazima ayaache yale anayoyapenda na kuyafuata yale yeye (Kristo) anayoyapenda.

2. Ajitwike Msalaba wake.

Kujitwika msalaba maana yake ni kubeba kitu ambacho utakwenda Kuteswa nacho. Kristo alibeba msalaba wake na akaenda kusulubiwa juu ya huo, na ndivyo sisi nasi tunapaswa tubebe misalaba yetu..

3. Anifuate

Amfuate wapi?…amfuate kila mahali atakapokwenda… na mwisho wa safari ya Yesu ni Golgotha, katika Kifo!….na kifo cha Bwana Yesu kilikuwa juu ya ule msalaba alioubeba, na si juu ya kitu kingine chochote, vile vile na sisi tunaposema tumekufa pamoja na Kristo ni lazima kifo chetu kiwe juu ya misalaba yetu tuliyoibeba na si juu ya kitu kingine chochote.

Je umeubeba msalaba wako?

Kama hukuubeba msalaba wako utasemaje basi ulikufa pamoja Kristo?.. Kama hujajikana nafsi utasemaje kuwa umekufa pamoja na Kristo?, Kama mapenzi ya baba yako yana nguvu kuliko mapenzi ya Mungu utasemaje ulikufa pamoja na Kristo?.. Kama unamwogopa mama yako kuliko kumwogopa Mungu utasemaje ulikufa pamoja na Kristo?… Kama kazi yako ina nguvu kuliko ibada za Kristo utasemaje ulikufa pamoja na Kristo?, kama kumkiri Kristo tu mbele ya watu ni ngumu utasemaje ulikufa pamoja naye?, kama maisha yako yamejaa uchafu wa kila aina utasemaje basi ulikkufa pamoja na Kristo?.. Wengi wamekufa pamoja na Yuda katika roho lakini si pamoja na Kristo, waliokufa pamoja na Kristo ni watu waliobeba misalaba yao..

Luka 14:25  “Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia,

26  Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.

27  MTU YE YOTE ASIYEUCHUKUA MSALABA WAKE NA KUJA NYUMA YANGU, HAWEZI KUWA MWANAFUNZI WANGU”.

Na wote waliokufa pamoja na Kristo na kuzikwa pamoja naye ndio watakaoishi pamoja naye kama maandiko yanavyosema…

Warumi 6:8 “Lakini tukiwa TULIKUFA PAMOJA NA KRISTO, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye”

Je wewe umekufa pamoja na nani?.. na umekufa juu ya nini?….Ishara ya kufa pamoja na Kristo ni msalaba, je wewe unao huo msalaba katika maisha yako?

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

BASI MUNGU ALIMWADHIMISHA MNO.

Je! Bwana Yesu alisulubiwa juu ya msalaba au juu ya mti uliokuwa wima?

UTHAMINI WITO WA PILI WA YESU ZAIDI YA ULE WA KWANZA.

Mtu asiye na akili ni nani kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

MWANAMKE ABIGAILI ANAFUNZO GANI KWA WANAWAKE?

Abigaili.

Huu ni mwendelezo wa mafundisho maalumu yahusuyo wanawake.

Na Leo tutaisikia sauti ya Mungu iliyokuwa nyuma maisha ya huyu mama aliyeitwa Abigaili.

Abigaili ni mwanamke aliyeolewa na mwanaume ambaye halikuwa chaguo la Mungu kwake, ijapokuwa mwanaume huyo alikuwa tajiri, hatujui ni nini kilimsukuma Abigaili katika ujana wake kukubali kuolewa na mwanaume yule, labda pengine Nabali hakuanza vile, alikuja kubadilika baadaye, au pengine wazazi wake walimshurutisha aolewe naye kwasababu ya utajiri aliokuwa nao.

Lakini mwanaume huyo halikuwa chaguo sahihi la Abigaili Kutoka Kwa Mungu, kwani Nabali hakuwajali watu wa chini kabisa, Wala hakuwa mtu wa kurudisha fadhila. Utakumbuka wakati ambapo Daudi anakimbizwa na Sauli, akiwa kule  maporini, alikutana na kundi kubwa la mifugo wa huyu Nabali, hivyo Daudi alichofanya ni kuwapa hifadhi watumwa wake, kuwahakikishia ulinzi, dhidi ya wavamizi wa mifugo ya wachungaji,kwasababu Nabali alikuwa na mifugo mingi sana na kipindi ambacho wanakwenda kuwakata manyoya kondoo wao, waporaji wenye silaha Huwa wanawavamia sana wafugaji..hivyo walidumu na Daudi Kwa muda wote huo mpaka walipomaliza shughuli zao.

Lakini siku moja Daudi alipungukiwa chakula yeye na jeshi lake hivyo wakaona mtu wa karibu atakayeweza kuwasaidia ni huyu Nabali. Ndipo Daudi akatuma wajumbe kwake kumuomba chochote alichonacho awasaidie.Lakini badala ya kupokea fadhili akapokea matusi. Ndipo Daudi akakasirika sana akataka kwenda kumuua Lakini mke wake alipopata habari akafanya kinyume chake akaaanda vyakula na kumpelekea Daudi, ndipo hasira yake ikageuka.

Embu tukisome kisa hichi Kwa ufupi;

1 Samweli 25:9-38

[9]Basi walipofika vijana wake Daudi, wakamwambia Nabali sawasawa na maneno hayo yote kwa jina la Daudi, kisha wakanyamaza.

[10]Naye Nabali akawajibu wale watumishi wa Daudi, akasema, Huyu Daudi ni nani? Na mwana wa Yese ni nani? Siku hizi kuna watumwa wengi wanaomtoroka kila mtu bwana wake!

[11]Basi mimi je! Nitwae mkate wangu, na maji yangu, na machinjo yangu niliyowachinjia hao watu wangu wakatao manyoya kondoo zangu, na kuwapa watu ambao siwajui wametoka wapi?

[12]Basi vijana wake Daudi wakageuka, wakaenda zao, wakarudi, nao wakaja wakamwambia sawasawa na maneno hayo yote.

[13]Kisha Daudi akawaambia watu wake, Haya! Jifungeni kila mtu upanga wake. Nao wakajifunga kila mtu upanga wake; Daudi naye akajifunga upanga wake; nao wakapanda nyuma yake Daudi, wapata kama watu mia nne; na watu mia mbili wakakaa na vyombo vyao.

[14]Lakini kijana mmojawapo alimpasha habari Abigaili, mkewe Nabali, kasema, Tazama, Daudi alituma wajumbe kutoka nyikani waje ili kumsalimu bwana wetu, naye akawatukana.

[15]Walakini watu hawa walitutendea mema sana, wala hatukupata dhara, wala sisi hatukupotewa na kitu cho chote, wakati wote tulipofuatana nao, tulipokuwako mavueni;

[16]watu hao walikuwa boma kwetu usiku na mchana, wakati wote tulipokuwa nao tukiwachunga kondoo.

[17]Basi sasa ujue na kufikiri utakayotenda; kwa sababu yamekusudiwa mabaya juu ya bwana wetu, na juu ya nyumba yake yote; kwa kuwa yeye ni mtu asiyefaa kabisa, hata mtu hawezi kusema naye.

[18]Ndipo Abigaili akafanya haraka, akatwaa mikate mia mbili, na viriba viwili vya divai, na kondoo watano waliofanyizwa tayari, na vipimo vitano vya bisi, na vishada mia vya zabibu, na mikate ya tini mia mbili; akavipakia vitu hivi juu ya punda.

[19]Akawaambia vijana wake, Haya! Tangulieni mbele yangu; angalieni, mimi nawafuata. Ila hakumwambia mumewe, Nabali.

[20]Ikawa, alipokuwa amepanda punda wake, na kutelemka penye sitara ya mlima, tazama, Daudi na watu wake walikuwa wakishuka kumkabili; naye akawakuta.

[21]Basi Daudi alikuwa amesema, Hakika ni bure nilivyokuwa nikilinda nyikani yote aliyo nayo mtu huyu, asipotewe na kitu cho chote cha mali yake yote; naye amenilipa mabaya badala ya mema.

[22]Mungu naye awafanyie hivyo adui za Daudi, na kuzidi, nikimwachia katika wote walio wake hata mtoto mume mmoja, kutakapopambazuka asubuhi.

[23]Ndipo hapo Abigaili alipomwona Daudi, alifanya haraka kushuka juu ya punda wake, akamwangukia Daudi kifulifuli, akainama mpaka nchi.

[24]Akamwangukia miguuni pake, akasema, Juu yangu, bwana wangu, juu yangu mimi na uwe uovu; tafadhali mjakazi wako na anene masikioni mwako, nawe uyasikilize maneno ya mjakazi wako.

[25]Nakusihi, bwana wangu, wewe usimwangalie huyu mtu asiyefaa, yaani, Nabali; kwa maana kama lilivyo jina lake ndivyo alivyo yeye; jina lake ndilo Nabali, na upumbavu anao; lakini mimi, mjakazi wako, sikuwaona hao vijana wa bwana wangu aliowatuma.

[26]Basi sasa, bwana wangu, aishivyo BWANA, na iishivyo nafsi yako, kwa kuwa BWANA amekuzuia usimwage damu, tena usijilipize kisasi mkono wako mwenyewe, basi sasa adui zako, na hao wamtakiao bwana wangu mabaya, wawe kama Nabali.

[27]Na sasa zawadi hii, mjakazi wako aliyomletea bwana wangu, na wapewe vijana wamfuatao bwana wangu.

[28]Nakuomba ulisamehe kosa lake mjakazi wako, kwa kuwa hakika BWANA atamfanyia bwana wangu nyumba iliyo imara, kwa sababu bwana wangu anavipiga vita vya BWANA; tena uovu hautaonekana ndani yako siku zako zote.

[29]Na hata ijapokuwa binadamu angeinuka akuwinde, na kuitafuta nafsi yako, hiyo nafsi ya bwana wangu itafungwa katika furushi ya uhai pamoja na BWANA, Mungu wako; na nafsi za adui zako ndizo atakazozitupa nje, kama kutoka kati ya teo.

[30]Tena itakuwa, hapo BWANA atakapokuwa amemtendea bwana wangu sawasawa na mema yote aliyoyanena juu yako, na kukutawaza juu ya Israeli;

[31]hili halitakuwa kwazo, wala chukizo la moyoni kwa bwana wangu, ama ya kuwa umemwaga damu bure, ama ya kuwa bwana wangu amejilipiza kisasi mwenyewe; tena hapo BWANA atakapokuwa amemtendea bwana wangu mema, ndipo umkumbuke mjakazi wako.

[32]Naye Daudi akamwambia Abigaili, Na ahimidiwe BWANA, Mungu wa Israeli, ambaye amekuleta hivi leo kunilaki;

[33]na ibarikiwe busara yako, na ubarikiwe wewe, uliyenizuia hivi leo nisimwage damu, wala kujilipiza kisasi kwa mkono wangu mwenyewe.

[34]Kwa kuwa ni kweli, aishivyo BWANA, Mungu wa Israeli, aliyenizuia nisikudhuru, kwamba hungefanya haraka kuja kunilaki, hakika huyu Nabali asingaliachiwa hata mtoto mume mmoja, kutakapopambazuka asubuhi.

[35]Basi Daudi akapokea mkononi mwake vitu vile alivyomletea; akamwambia, Haya! Kwea kwa amani kwenda nyumbani kwako; tazama, nimeisikiliza sauti yako, nami nimeukubali uso wako.

[36]Kisha Abigaili alimjia Nabali; na tazama, alikuwa amefanya karamu nyumbani mwake, kama karamu ya kifalme; na moyo wake huyo Nabali ukafurahiwa ndani yake, kwa maana amelewa kabisa. Kwa sababu hiyo hakumwambia neno, dogo wala kubwa, hata kulipopambazuka.

[37]Ikawa asubuhi, divai ilipokuwa imemtoka Nabali, mkewe alimwambia mambo hayo, na moyo wake ukafa ndani yake, akawa kama jiwe.

[38]Tena ikawa, yapata siku kumi baadaye, BWANA alimpiga huyo Nabali, hata akafa.

Ni nini mwanawake wanapaswa wajifunze kuhusiana na maisha ya Abigaili.

  1. Mwanaume Bora si yule mwenye Mali:

Kundi kubwa la wanawake wengi wa sasa wanaotaka kuolewa kigezo wanachokitazama Kwa wanaume ni Mali, wanasahau kuwa hata shetani hutoa Mali. Nabali alimsumbua sana Abigaili katika maisha yake ya ukamilifu, na kama asingekuwa na bidii katika busara yake angeshauliwa mbali na Daudi pamoja na Mali zao. Kufunua kuwa Kristo kama mfalme wetu, Huwa anaziadhibu familia Kwa makosa ya wanandoa wasiowajibika kiroho. Haijalishi wingi wa Mali walizonazo. Wewe kama mwanamke unayekaribia kuolewa kumbuka mwanaume anayemcha Mungu ndio chaguo sahihi kwako, na si vinginevyo.

  1. Pili Abigaili analiwakilisha kundi la wanawake ambao, wameshaingia katika ndoa za watu wasiosahihi.

Wanawake wengi wapo kwenye ndoa, lakini baadaye sana ndio wanakuja kugundua kuwa waume walionao hawakuwa Kutoka Kwa Bwana. Wengine ni wazinzi, wengine ni walevi kama Nabali, wengine hawajali kazi za Mungu Wala Roho zao wenyewe, wengine majambazi, wengine wanawatesa n.k.

Lakini utaona busara ya Abigaili haikuwa kwenda kutafuta mwanaume mwingine aolewe naye, kisa mume wake ni mpumbavu, ila aliendelea kudumu katika haki na ukamilifu, aliendelea kumwombea rehema mume wake hata Kwa maadui zake. Ijapokuwa alikuwa mjinga, lakini hakujaribu kujitenga na mumewe, alimwachia Mungu amfanyie wepesi. Na tunaona Mungu mwenyewe ndio alikuja kushughulika na Nabali akamuua, Kisha Abigaili akawa mke wa Mfalme Daudi. Pumziko la ndoa yake likaja.

Hata sasa wewe kama mwanamke ambaye upo katika ndoa chungu. Huitaji kuizira ndoa hiyo, badala yake omba rehema, na wokovu Kwa mume wako kwa Yesu. Naye ataugeuza moyo wake. Bwana hatatumia njia ya kumuua, lakini ataua uovu na ubaya ulio ndani yake. Na atakuwa tu mume Bora, lakini  usichoke kuomba ukasema nimeomba sana sijaona mabadiliko.yoyote… wewe endelea kuomba hata kama itapita miaka 20, ujue Mungu anaona na kusikia maombi Yako tu, atatenda jambo. Huyo atakuwa mume Bora zaidi ya unavyodhani, usipozimia moyo.Hivyo iga busara ya Abigaili.

Anza sasa kuijenga ndoa Yako. Bwana akubariki.

Shalom.

Je! Umeokoka? Je unafahamu kuwa hizi ni nyakati za mwisho na Mlango wa neema unakaribia kufungwa? Unasubiri nini usiokoke? Itakufaidia nini uupate ulimwengu wote halafu upate hasara ya nafsi Yako? Ikiwa upo tayari kumkabidhi Leo Bwana Yesu maisha Yako. Basi wasiliana nasi Kwa namba zetu hizi Kwa ajili ya mwongozo huo Bure.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MASOMO MAALUMU KWA WANAWAKE.

NI KITU GANI TUNAJIFUNZA KWA RISPA, BINTI AYA?

Je! kuna mwanamke mwingine aliyempaka Bwana marhamu (manukato) zaidi ya Mariamu ndugu yake Lazaro?

Maneno ya mchongezi ni kama vitoweo; Nayo hushukia pande za ndani za tumbo

Na ulimi laini huvunja mfupa.(Mithali 25:15)

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?

MISTARI YA BIBLIA YA FARAJA.

Rudi nyumbani

Print this post

Tu uzao wake Ibrahimu, wala hatujawa watumwa wa mtu.

SWALI: Kwanini wayahudi walimwambia Yesu kuwa hawajawahi kuwa watumwa wa mtu yeyote angali tunajua kuwa walishawahi kuwa watumwa kule Misri kwa miaka 400?


JIBU: Tusome;

Yohana 8:31  “Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli; 32  tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru. 33  Wakamjibu, Sisi tu uzao wake Ibrahimu, wala hatujawa watumwa wa mtu wakati wo wote; nawe wasemaje, Mtawekwa huru? 34  Yesu akawajibu, Amin, amin, nawaambia, Kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi. 35  Wala mtumwa hakai nyumbani sikuzote; mwana hukaa sikuzote. 36  Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli”.

Kauli ya hawa wayahudi haikuwa kauli ya kweli bali ya uongo uliowazi, Na lengo la majibu yao halikuwa kutafakari Yesu anayoyasema bali kumpinga tu, Na ndio maana hawakuona shida kuzungumza uongo wa wazi, kwani vitabu vyao vinaeleza walishawahi kuwa watumwa Misri,Babeli, Ashuru na sehemu kadha wa kadha walishawahi kutumikishwa na mataifa hata wakiwa katika taifa lao wenyewe.

 Lakini Yesu hakulenga utumwa wa mwilini kama wao walivyodhani, bali ule wa rohoni, wa dhambi, yaani tamaa, wivu, uongo, mawazo mabaya, hasira n.k. Mambo ambayo walikuwa hawana.Lakini kwasababu lengo lao lilikuwa ni kumpinga waliendelea bado kusema uongo hata juu yake..Kwamfano ukisoma vifungu vinavyofuata katika mazungumzo yao, ule mstari wa 48  utaona wanasema kwamba yeye ni msamaria tena ana pepo. Jambo ambalo ni uongo mwingine wa makusudi.  Kwani Walijua kabisa Yesu ni myahudi, na wazazi wake Yusufu, na ndugu zake wote wapo nao, mpaka kazi yao ya useremala waliyoifanya waliijua, tena wakamwita Rabi sehemu nyingine,  lakini kwasababu wapo kibishi wakazusha uongo na kusema yeye ni msamaria, tena mwenye pepo.

Na ndio maana Bwana Yesu katika mazungumzo hayo hayo (Mstari wa 44) akawaeleza wazi kuwa wao ni wa Baba yao ibilisi kwasababu “hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo ”. kwasababu ya uongo wao.

Hii ni kutufundisha nini?

Tuipende kweli, Kwasababu tusipolipenda Neno la Mungu, shetani atatutumia kulipinga Neno hilo hilo kwa kushuhudia habari za uongo uliowazi na wala hututaona shida, kama ilivyokuwa kwa wayahudi hawa.

Je! Umeokoka, je! Unahakika wa maisha yako ya milele baada ya kifo? Je! Unatambua  kuwa hizi ni siku za mwisho, na roho ya mpinga-Kristo inatenda kazi ndani ya watu ambao hawajaokolewa leo? Unasubiri nini usimgeukie muumba wako, tamaa za dunia zitakufikisha wapi?umefungwa Rohoni upo chini ya Utumwa wa dhambi, anayeweza kukuweka huru ni Yesu tu peke yake. Ikiwa upo tayari kuokoka leo, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618 / +255789001312, kwa ajili ya mwongozo huo bure.

Bwana akubariki.         

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Ni kosa gani lililowafanya wana wa israeli wawe watumwa miaka 400 Misri?.(

WANA WA MAJOKA.

EPUKA MUHURI WA SHETANI

YULE JOKA WA ZAMANI.

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)

Je! Mwendo wa Sabato ulikuwaje kibiblia?(Matendo 1:12)

Rudi nyumbani

Print this post