Title 2025

Maana ya Mithali 29:9 Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu; Akikasirika au akicheka, pia hapana raha. 

 Mithali 29:9 Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu; Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.


Mstari huo kwa lugha rahisi tunaweza kuuweka kwa namna hii. “Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu, akijibu kwa kicheko au kwa hasira, matokeo ni yaleyale tu hakuna amani au suluhisho”

Unafunua sifa za mpumbavu, kwamba sikuzote mwitikio wake wowote hauwezi kuleta mabadiliko. Kwamfano labda hoja imetolewa na ikamuumiza kiasi cha kumfanya ajibu kwa hasira. Sasa wewe waweza tarajia pengine jambo hilo limemgusa kweli moyo, litambadilisha lakini matokeo yake ni kwamba anakuwa vilevile, Halikadhalika waweza kutoa hoja ikamfanya acheke ukitarajia kitaambatana na  badiliko lolote ndani yake lakini hakuna.

Maana yake mpumbavu, haguswi kwa ukali au kwa wepesi wa maneno ya aina yoyote…Na hivyo ni kuachana naye Tu.

Tukiachia wapumbavu wa kawaida tunaowafahamu..Mpumbavu hasaa ni yule mtu anayeikataa kweli ya Mungu mfano wa wale waandishi na mafarisayo wakati wa Bwana Yesu (Mathayo 23:17), mtu wa namna hii unapomuhubiri injili, hata imchomeje au imchekesheje hawezi kufikiri hata chembe kubadilika, kinyume Chake ni mapambano tu.

Bwana Yesu alitufundisha na kutuambia kuwa si kila mtu ni wa kumtupia lulu zetu, maana yake wanaweza kutugeukia na Kuturarua. Ukiona mtu anaishia kwenye ubishi tu na mashindano, ni kuachana naye na kugeukia waliotayari kupokea.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)

Elewa tafsiri ya Mithali 27:22 Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi kinuni.

KILINDI CHAPIGIA KELELE KILINDI.

Print this post

Theolojia ni nini?. Na je ni sahihi kuisoma?

Theolojia ni elimu ya kujifunza sifa za Mungu na mapenzi yake na jinsi anavyohusiana na wanadamu na ulimwengu  kwa ujumla.

Neno Theolojia limezaliwa kutoka katika maneno mawili ya kigiriki ‘theos’, na ‘logos’

Theos likiwa na maana ya Mungu, na logos ni neno/wazo/elimu/maarifa.

Hivyo tukiunganisha maneno hayo, ni sawa kusema theolojia ni mafundisho au maarifa au elimu kuhusu Mungu.

Ni utafiti kuhusu  Mungu katika mpangilio na mtiririko maalumu. Ukweli ni kwamba theolojia haiwezi kumfafanua Mungu katika ufasaha wote, ikiwa mtu ataitegemea  theolojia tu kumjua Mungu, ukweli ni kwamba amepotea, lakini ikiwa itasomwa vema (si kwa lengo la kitaaluma), bali kwa lengo la kupanua upana wa fikra kuhusu Mungu na maandiko, inafaa sana katika uelewa wa nyanja mbalimbali, hususani kwa wale viongozi na waangalizi kama vile wachungaji, na wahubiri. Si lazima isomwe kwenye vyuo maalumu, mtu yeyote akitia nia kujifunza theolojia anaweza jifunza, kwa kupitia mafundisho mengi, majadiliano na waalimu walio na upeo mpana wa biblia, semina, na kujisomea mwenyewe n.k.

Na Haya ni matawi makuu ya theolojia katika kuichambua biblia.

1) Theolojia ya ki-biblia.

Imejikita katika kutafiti Maudhui au fundisho kuu la biblia, inaangazia jinsi gani vitabu mbalimbali kwenye biblia, vinavyoelezea mpango wa Mungu katika nyakati tofauti tofauti tangu mwanzo hadi mwisho. Mfano kujifunza MAAGANO, katika agano la kale na jipya yalivyotenda kazi na jinsi Yesu alivyoanza kutambulishwa tangu Edeni kama mzao wa mwanamke, hadi nyakati za manabii Isaya 53, hadi wakati wa kutokea kwake duniani Luka 24:27.

Upo umuhimu wa kuijua hii theolojia kwasababu itakupa kujua kiini cha biblia ni nini? Zipo habari nyingi, hadithi nyingi, nyimbo nyingi, mifano mingi, lakini ni vema ujue maudhui zao ni zipi ili usijikute unatoka nje ya shabaha ya imani.

2) Theolojia ya ki-mpangilio/Mada

Inaegemea kujifunza biblia katika migawanyo maalumu ya mada, kwa mfano,

Fundisho la Mungu (theolojia),

Fundisho La Yesu Kristo (Kristolojia),

Fundisho La Roho Mtakatifu (niumatolojia),

Fundisho La wokovu (Soteriolojia),

Fundisho La kanisa,(Ekleziolojia)

La Siku za mwisho.(Esokatolojia)

La mwanadamu (Anthropolojia)

La malaika (Angeolojia)

3) Theolojia ya ki-vitendo

Inajikita kujifunza jinsi maagizo ya kibiblia yanavyoweza kutendewa kazi katika,, huduma kwa mfano kuhubiri na kufundisha , katika uangalizi wa kichungaji, katika umisheni, na katika taratibu za kiibada, na katika kutoa mashauri ya kikristo kama vile kuwaonya wenye matatizo ya kiroho,  kifikra, vifungo n.k.

4) Theolojia ya ki-historia.

Inaangazia jinsi gani imani ya kikristo imekuwa ikipiga hatua katika vipindi mbalimbali vya kihistoria, inaangazia mabaraza mbalimbali ya makanisa yaliyokaa katika kujadili fundisho na misingi ya imani. Kwamfano lile baraza la Nikea (325WK). Mpaka nyakati za matengenezo mfano akina Martin Luther, calvin, na wengine.

Hii inakusaidia kujua historia na chimbuko la imani yetu, na sababu ya ukristo kuonekana katika muundo huu leo.

5) Theolojia ya kimaadili.

Hii inaegemea katika ukristo na jamii, kwamfano mtazamo wa ukristo katika maeneo ya kijamii mfano ndoa, biashara, taratibu za kijamii, haki za kibinadamu, vita,

Zipo theolojia nyingine kama vile theolojia za tafsiri, za kulinganisha, za utetezi, za kifalsafa. n.k. Kwasababu ya upana wa theolojia, haya ni  matawi baadhi tu, kati ya mengi. Hivyo, kama watu wa Mungu, pamoja na kutegemea Bwana kutufunulia mwenyewe maandiko, upo pia wakati ambao hatuna budi kuyamulika maandiko kiundani (Kitheolojia), tukiwa na lengo la kumjua Mungu kwa upana na sio kuwa wasomi, au wanataaluma.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mwanazuoni ni mtu gani kibiblia?

Kwanini kuna tafsiri nyingi za Biblia, na tafsiri ipi ni sahihi?

Yesu anapoitwa mwana wa Azali, maana yake nini?

Print this post

Je tumepewa kujua nyakati na majira ya kurudi kwa Bwana au la?.

Swali: Katika Matendo 1:7, tunaona Bwana anasema si kazi yetu kujua nyakati na majira ya kuja kwake,

Lakini katika 1Wathesalonike 5:1-2 tunasoma Mtume Paulo akisema kuhusu nyakati na majira kuwa hana haja ya kutuandikia kwasababu sisi wenyewe tunajua…je hii imekaaje?..je kuna mkanganyiko hapo?


Jibu: Awali, tuirejee mistari hiyo…

Matendo 1:6 “Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme?

7 Akawaambia, Si kazi yenu kujua NYAKATI WALA MAJIRA, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe”.

Tusome tena habari ya Paulo…

1 Wathesalonike 5:1 “Lakini, ndugu, kwa habari ya NYAKATI NA MAJIRA, hamna haja niwaandikie.

2 Maana ninyi wenyewe MNAJUA yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku”.

Ni muhimu kufahamu kuwa hakuna mkanganyiko wowote kwenye biblia, na wala haijichanganyi,

Sasa Paulo aliposema kuwa “hana haja ya kuandika kuhusu nyakati na majira kwasababu tayari wameshajua”.. hakumaanisha kuwa tayari wameshajua/tumeshajua siku na tarehe za kurudi Bwana YESU, LA! Hakumaanisha hivyo, vinginevyo angekuwa ameenda kinyume na maneno hayo ya Bwana YESU aliyosema kuwa “Si kazi yetu kujua majira na nyakati” na tena aliposema “hakuna ajuaye siku wala saa”.

Sasa ni kitu gani Paulo alichomaanisha kuwa tayari wameshakijua, au tumeshakijua kuhusu nyakati na majira?.

Kitu ambacho tayari Wathesalonike pamoja na sisi tumeshakijua kuhusu Nyakati na Majira ya kurudi kwa YESU sio ile tarehe atakayokuja, hapana!.. bali tulichokijua kuhusu Nyakati na Majira ya kurudi kwa YESU ni kwamba “ATAKUJA KAMA MWIVI”… Hicho ndicho Paulo alichokimaanisha.

Na ni lini tulijua hilo?…tulijua kupitia maneno ya Bwana YESU mwenyewe..
Mathayo 24:40 “Wakati ule watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa;
41 wanawake wawili watakuwa wakisaga; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa.
42 Kesheni basi; kwa maana hamjui ni siku ipi atakayokuja Bwana wenu.
43 Lakini fahamuni neno hili; kama mwenye nyumba angaliijua ile zamu mwivi atakayokuja, angalikesha, wala asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.
44 Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja”

Ndio maana tukiendelea mistari ya mbele kidogo mpaka ule mstari wa tatu tutaona Paulo analielezea zaidi…

1 Wathesalonike 5:1 “Lakini, ndugu, kwa habari ya NYAKATI NA MAJIRA, hamna haja niwaandikie.

2 Maana ninyi wenyewe MNAJUA yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.

3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”.

Kwahiyo biblia haijichanganyi popote, wala Paulo hakusema kitu chochote tofauti na BWANA YESU.

Je umempokea Mwokozi YESU?..Je wajua kuwa dakika yoyote parapanda italia, na watakaonyakuliwa ni wale tu waliojitaka, je utakuwa wapi siku ile ikiwa leo hii hutaki kubadili njia zako?.

Jibu unalo!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Je Paulo, alihimiza kusikiliza nyimbo za kidunia kulingana na Matendo 17:28

Matendo 17:28 Kwa maana ndani yake yeye tunaishi, tunakwenda, na kuwa na uhai wetu. Kama vile mmoja wenu, mtunga mashairi alivyosema, Maana sisi sote tu wazao wake.

29 Basi, kwa kuwa sisi tu wazao wa Mungu, haitupasi kudhani ya kuwa Uungu ni mfano wa dhahabu au fedha au jiwe, vitu vilivyochongwa kwa ustadi na akili za wanadamu.

JIBU: Paulo alipofika Athene, na kuona jinsi mji ule ulivyojaa sanamu nyingi, maandiko yanatuambia moyo wake ulichukizwa sana, hivyo kama ilivyo desturi yake kuhubiri injili, alijua njia mojawapo ya kuwavuta watu ni “kujiungamanisha nao”, kwa kuwagusia kwanza yale mambo mema waliyoyafikiri au kuyatenda.

Ndio maana utaona kabla ya kuwagusia kuhusu huyo mtunga mashairi, aliwaambia kuhusu madhabahu waliyoijenga, ambayo waliipa jina la “MUNGU ASIYEJULIKANA”

Matendo 17:23 Kwa sababu nilipokuwa nikipita huko na huko na kuyaona mambo ya ibada yenu, naliona madhabahu iliyoandikwa maneno haya, KWA MUNGU ASIYEJULIKANA. Basi mimi nawahubirini habari zake yeye ambaye ninyi mnamwabudu bila kumjua.

Paulo akaanza kuwahubiria Kristo kwa kupitia huyo wanayemwabudu kimakosa, Lakini tunajua Paulo, hakuwa na ushirika wowote na mifumo yao ya kipagani, wala hakuwahimiza waendelee kumwabudu Kristo kwa njia yao hiyo hiyo.

Tunaona katika kuendelea kujiungamanisha zaidi ya wenyeji wale wa Athene, Paulo akagusia tena habari nyingine za mtunga mashairi, ambaye alikuwa maarifu katikati yao, nyimbo zake zilivuma na kila mmoja alikuwa anazijua, na ndani ya mashairi yake, aliweka vina vinavyoeleza kuwa sisi sote ni wazao wake, au kusema sisi sote ni watoto wa Mungu.

Hivyo akatumia tena fursa hiyo, kuwaeleza uhai wa Mungu, ikiwa sisi tumezaliwa na yeye, basi haiwezekani Baba yetu akawa mfano wa sanamu, ni lazima tu atakuwa mwenye akili, ufahamu, na uelewa kama sisi na zaidi, na sio kama kipande cha mti.

Kwa njia hiyo Paulo akawapata watu wengi, kwa Kristo.

Lakini hatuoni mahali popote akiwaambia wawe wafuatiliaji au  mashabiki, wa nyimbo za kidunia.Hiyo ilikuwa njia ya kuwapata wapagani, wamjue Kristo.

Kinyume chake Paulo katika nyaraka zake, anahimiza, waamini kutofuatisha namna ya dunia hii (Warumi 12:1). Na kuhimiza uimbaji unaomtukuza Mungu na kutujenga sisi nafsi zetu kwake ndio unaopaswa kwa wakristo.

Waefeso 5:19 mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu;

20 na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo;

Wakolosai 3:16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.

17 Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.

Hivyo hatuoni mahali popote Paulo akikubaliana na usikilizaji wa nyimbo za kidunia, wala sisi kama wakristo, hatupaswi kujikita huko, kwasababu tumeshajua ni nani hasaa wa kumwimbia na kumsifu, na wa kumburudikia.

Mungu akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kuharimishwa ni nini, na kwanini Paulo aombe hivyo?(Warumi 9:2).

Uchambuzi na mwandishi wa kitabu cha Waefeso.

Ni kwa namna gani Bwana YESU alikula Siagi na Maziwa? (Isaya 7:15)

Print this post

Yaya ni nani? (Mwanzo 24:59).

Swali: Huyu yaya aliyeenda na Rebeka ni nani kama tunavyomsoma katika Mwanzo 24:59?

Jibu: Turejee…

Mwanzo 24:59 “Ndipo wakampeleka Rebeka ndugu yao, na YAYA wake, na mtumishi wa Ibrahimu, na watu wake”.

Yaya maana yake ni muuguzi (yaani mwangalizi wa mtu aliye katika udhaifu fulani au ugonjwa)...kwa kiswahili kingine chepesi ni NESI.

Kwahiyo Rebeka wakati anachukuliwa ili apelekwa kwa Isaka…aliambatana na Nesi wake huyo(Yaya).

Sasa biblia haijaelezea kwa undani sababu za kwenda naye, kwamba ni kwasababu za ugonjwa Rebeka aliokuwa nao (ambao pia haujatajwa) au labda kwa dharura endapo angepata shida fulani katika njia anayoiendea basi apate msaidizi kwani safari ile ilikuwa ni ndefu sana….

Au labda alimuhitaji yaya mbeleni katika maisha yake ya ndoa, baada ya kujifungua n.k hakuna anayejua, biblia imesema tu alienda na Yaya wake.

Neno hili pia limeonekana sehemu nyingine katika biblia..

2 Samweli 4:4 “Naye Yonathani, mwana wa Sauli alikuwa na mwana aliyekuwa na kilema cha miguu. Alikuwa amepata miaka mitano, habari za Sauli na Yonathani zilipofika Yezreeli, na yaya wake akamchukua akakimbia ikawa, alipokimbia kwa haraka, huyo mtoto akaanguka, akawa kilema. Na jina lake aliitwa Mefiboshethi”

Soma pia 2Nyakati 22:11 utaona pia  neno hilo.

Naam kiroho YAYA wetu ni YESU KRISTO, tuwapo wadhaifu au katika dhiki au hali za kuishiwa nguvu na kuhitaji msaada, ni YESU KRISTO tu pekee awezaye kututunza na kututoa katika hizo hali.

Lakini Bwana hawezi kuwa mlezi wetu ikiwa hatutamruhusu awe hivyo, lakini tukiruhusu aingie maishani mwetu, na pia tukimheshimu na kuzishika amri zake hakika hatatuacha katika mateso sawasawa na ahadi zake.

Zaburi 41:3 “BWANA atamtegemeza alipo mgonjwa kitandani. Katika ugonjwa wake umemtandikia”

Je unaye YESU moyoni, na je maisha yako yanaakisi wokovu wa kweli?.

Kama bado upo nje ya YESU tafuta msaada mapema kwa YESU kabla mambo hayajaharibika zaidi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Mistari ya biblia kuhusu sadaka

Hii ni mistari ya biblia inayogusia utoaji wa sadaka wa namna mbalimbali.

Sadaka kama ibada na utiifu.

Mithali 3:9 Mheshimu Bwana kwa mali yako, Na kwa malimbuko ya mazao yako yote. 10 Ndipo ghala zako zitakapojazwa kwa wingi, Na mashinikizo yako yatafurika divai mpya.

Mwanzo 4: 3 Ikawa hatimaye Kaini akaleta mazao ya ardhi, sadaka kwa Bwana. 4 Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. Bwana akamtakabali Habili na sadaka yake; 5 bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana.

Sadaka za kupenda:

Kutoka 25:2 Waambie wana wa Israeli kwamba wanitwalie sadaka; kila mtu ambaye moyo wake wampa kupenda mtatwaa kwake sadaka yangu.

2Wakorintho 9:7 Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.

Kumbukumbu 16:17 Kila mtu na atoe kama awezavyo, kwa kadiri ya baraka ya Bwana, Mungu wako, alivyokupa

Kutoka 35:5 Katwaeni kati yenu matoleo kwa Bwana; mtu awaye yote aliye na moyo wa kupenda, ayalete matoleo; dhahabu na fedha na shaba;

2Nyakati 31: 5 Mara ilipotangaa amri, wana wa Israeli wakatoa kwa wingi malimbuko ya nafaka, na divai, na mafuta, na asali, na mazao yote ya mashamba; na zaka za vitu vyote wakazileta nyingi.

Sadaka za kushukuru:

Zaburi 50:14 Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru; Mtimizie Aliye juu nadhiri zako.

Walawi 22: 29 Tena mtakapomchinjia Bwana dhabihu ya shukrani, mtamchinja ili mpate kukubaliwa. 30 Italiwa siku iyo hiyo; msisaze kitu chake hata asubuhi; mimi ndimi Bwana.

Sadaka za Zaka na malimbuko:

Malaki 3:10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.

Walawi 27: 30 Tena zaka yote ya nchi, kama ni mbegu ya nchi, au kama ni matunda ya nchi, ni ya Bwana; ni takatifu kwa Bwana.

Sadaka za kugharimika:

Marko 12:43 Akawaita wanafunzi wake, akawaambia, Amin, nawaambia, Huyu mjane maskini ametia zaidi kuliko wote wanaotia katika sanduku la hazina; 44 maana hao wote walitia baadhi ya mali iliyowazidi; bali huyu katika umaskini wake ametia  vyote alivyokuwa navyo, ndiyo riziki yake yote pia.

Wafilipi 4:18 Lakini ninavyo vitu vyote na kuzidi, tena nimejaa tele; nimepokea kwa mkono wa Epafrodito vitu vile vilivyotoka kwenu, harufu ya manukato, sadaka yenye kibali, impendezayo Mungu.

Luka 6:38 Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.

Sadaka zimpendezazo Mungu:

Yesu Kristo.

Pamoja na kuwa na sadaka za aina nyingi, lazima tufahamu, Sadaka halisi zimpendezazo Mungu. Na ya kwanza ni Yesu Kristo. Yeye alitolewa kwetu kama dhabihu kamilifu kwa ajili ya dhambi zetu. Hivyo mtu yoyote anayeitoa sadaka hii kwa Mungu basi, hukubaliwa na yeye asilimia mia. Na tunaitoa kwa kumpokea mioyoni mwetu kama Bwana na mwokozi wa maisha yetu. Imefanyika bora kuliko dhabihu zote na matoleo yote.

Waebrania 10: 4 Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi. 5 Kwa hiyo ajapo ulimwenguni, asema, Dhabihu na toleo hukutaka, Lakini mwili uliniwekea tayari;

Sambamba na hizo, sadaka nyingine zilizobora kuliko matoleo ni pamoja na kujitoa miili yetu katika utakatifu, kutenda haki, kuonyesha fadhili na rehema, kwa Bwana.

Warumi 12:1 Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.

Hosea 6:6 Maana nataka fadhili wala si sadaka; na kumjua Mungu kuliko sadaka za kuteketezwa.

Mika 6:6 Nimkaribie Bwana na kitu gani, na kuinama mbele za Mungu aliye juu? Je! Nimkaribie na sadaka za kuteketezwa, na ndama za umri wa mwaka mmoja? 7 Je! Bwana atapendezwa na elfu za kondoo waume, au na elfu kumi za mito ya mafuta? Je! Nimtoe

mzaliwa wangu wa kwanza kwa kosa langu, mzao wa mwili wangu kwa dhambi ya roho yangu? 8 Ee mwanadamu, yeye amekuonyesha yaliyo mema; na Bwana anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!

Je! Unatoa sadaka zote hizi? Kwa Bwana?

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

FUKUZA TAI WOTE JUU YA SADAKA YAKO.

NINI NI KILICHOMFANYA IBRAHIMU AKUBALI KUMTOA MWANAWE SADAKA?

Sadaka ya kuinuliwa ni sadaka ya namna gani?

Print this post

Kwanini Mwanadamu hakuumbwa kwa Neno tu kama viumbe wengine?

Swali: Katika kitabu cha Mwanzo tunaona viumbe vyote viliumbwa na Mungu kwa kutamka tu Neno!, lakini kwa mwanadamu haikuwa hivyo, alimwumba kwa mikono yake, je sababu ni nini?


Jibu: Turejee

Mwanzo 1:19 “Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya nne.

 20 MUNGU AKASEMA, Maji na yajawe kwa wingi na kitu kiendacho chenye uhai, na ndege waruke juu ya nchi katika anga la mbingu.

 21 MUNGU AKAUMBA nyangumi wakubwa, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho, ambavyo maji yalijawa navyo kwa wingi kwa jinsi zao, na kila ndege arukaye, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema. 

22 Mungu akavibarikia, akisema, Zaeni, mkaongezeke, mkayajaze maji ya baharini, ndege na wazidi katika nchi. 

23 Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya tano.

24 MUNGU AKASEMA, Nchi na izae kiumbe hai kwa jinsi zake, mnyama wa kufugwa, nacho kitambaacho, na wanyama wa mwitu kwa jinsi zake; ikawa hivyo

25 MUNGU AKAFANYA mnyama wa mwitu kwa jinsi zake, na mnyama wa kufugwa kwa jinsi zake, na kila kitu kitambaacho juu ya nchi kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.”

Hapa tunasoma kwamba MUNGU AKASEMA, na kisha MUNGU AKAFANYA..  Kwahiyo kumbe MUNGU alianza kwanza kwa kusema ndipo “akafanya”..Naam hata wewe unaweza kusema “utajenga nyumba” ikawa ni kauli, na wakati utakapofika ukaanza kukusanya malighafi na kuitengeneza ile nyumba.. Kwahiyo kuna “KUSEMA” na “KUFANYA” ndiyo kanuni Bwana MUNGU aliyoenda nayo pia.

Sasa biblia haijaeleza kwa urefu alifanyaje fanyaje, kwenye huo udongo wakatokea wanyama, na viumbe..Kwamba ile kauli ya kinywa chake ndio ilienda kubadili ule udongo na kuwa Twiga, na Simba, na Tembo, au kwamba baada ya kusema alienda kuchukua udongo kwa vidole vyake na kufanya wanyama wale wote hakuna anayejua, lakini tunachojua ni kwamba wanyama walitokea ardhini kwa neno lake hilo.

Lakini tukiendelea na mstari wa 26 alipomwumba mtu, tunaona jambo jipya.. MUNGU ANASEMA, na kisha ANAUMBA kwa maelezo  marefu zaidi tofauti na ilivyokuwa kwa wanyama.

Mwanzo 1:26 “MUNGU AKASEMA, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. 

27 MUNGU AKAUMBA mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba”.

Soma tena Mwanzo 2:7 na Isaya 45:12 utaona maelezo ya ziada juu ya uumbaji wa mtu.

Kwa wanyama Bwana MUNGU hakuelezea kawaumba kwa mfano wa kitu gani, na kwa sura ya kitu gani, huenda labda waliumbwa kwa mfano wa baadhi ya viumbe vya mbinguni (kwani kuna malaika mbinguni wenye uso kama wa tai, na wengine wenye uso kama wa simba na ndama, na pia mbinguni kumetajwa uwepo wa farasi, soma Ezekieli 1:10, Ufunuo 4:7 na Ufunuo 19:11), lakini hiyo yote biblia haijaeleza, ni makisio tu..

Lakini alipoumbwa mwanadamu, biblia imetoa maelezo ya wazi kabisa ziada kaumbwa kwa mfano wa MUNGU, na kwa sura  ya MUNGU, kuonyesha umaalumu wake na utofauti wake na viumbe vingine vyote.

Na kama jinsi MUNGU alivyo Mkuu mbinguni na tena anatawala mbinguni, hali kadhalika na yule aliyetengenezwa kwa mfano wake duniani, atakuwa na nguvu na utawala kama wa kwake duniani.

Mwanzo 1:27 “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.

28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi”.

Lakini pamoja na kwamba Adamu aliumbwa ili atawale duniani, bado alimwuzia shetani nafasi yake hiyo, lakini habari njema ni kwamba YESU KRISTO alishinda na kuirejesha nafasi ya mwanadamu ya utawala..

Na wote wamwaminio Bwana YESU wanatawala naye si tu duniani, bali hata mbinguni.. kwani tumeketi naye mbinguni katika ulimwengu wa roho.

Waefeso 2:5 “ hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema.

6  Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu”

Lakini ukiwa nje ya Kristo, huna mamlaka yoyote, kwani shetani ndiye anayekutawala..Mpokee leo KRISTO na upande viwango vingine vya kiroho.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Kufuatana na ile habari ya Tajiri na Lazaro, ingewezekanikaje Nabii Samweli kupandishwa juu?

Swali: Katika ile habari ya Tajiri na maskini Lazaro (katika Luka 16: 27-31) tunasoma kuwa haikuwezekana kwa Lazaro kurudishwa duniani kuwahubiria ndugu watano wa yule Tajiri, ijapokuwa yule Tajiri alimsihi sana baba Ibrahimu amtume Lazaro, lakini haikuwezekana…

Lakini tukirudi nyuma katika 1Samweli 28:12-14….. tunasoma kuwa iliwezekana kumrudisha nabii Samweli aliyekuwa amekufa na kusema na Mfame Sauli ambaye alikuwa anaishi..je hii imekaaje, na ili hali tunajua Ibrahimu alikuwepo kabla hata ya Samweli na Sauli?.


Jibu: Awali turejee habari ya maskini Lazaro na Tajiri.

Luka 16:27 “Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu,

28 kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso.

29 Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao.

30 Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu.

31 Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu”

Hapa biblia inaonyesha kuwa ni kweli haikuwezekana Lazaro kutumwa duniani na kusema na ndugu watano wa yule Tajiri…

Lakini tusome tena ile habari ya nabii Samweli na Sauli alipokwenda kwa yule mwanamke mwenye pepo la utambuzi.

1 Samweli 28:12 “Hata yule mwanamke alipomwona Samweli alilia kwa sauti kuu; na yule mwanamke akamwambia Sauli, akasema, Mbona umenidanganya? Kwa kuwa wewe ndiwe Sauli.

13 Mfalme akamwambia Usiogope; waona nini? Yule mwanamke akamwambia Sauli, Naona mungu anatoka katika nchi.

14 Naye akamwuliza, Ni mfano wa nini? Akajibu, Ni mzee anazuka; naye amefunikwa vazi. Basi Sauli akatambua ya kwamba ndiye Samweli mwenyewe, akainama uso wake mpaka nchi, akasujudia

15 Ndipo Samweli akamwambia Sauli, Mbona umenitaabisha mimi, hata kunipandisha juu? Sauli akajibu, Mimi nimetaabika sana; kwa kuwa hao Wafilisti wananifanyia vita, naye Mungu ameniacha; hanijibu tena, wala kwa manabii, wala kwa ndoto; kwa hiyo nimekuita wewe, ili wewe unijulishe nifanyeje”

Hapa tunaona Samweli aliyekufa akipandishwa juu, sasa swali la msingi ni hili; ingewezekanikaje jambo hilo na ilihali ile habari ya Lazaro na Maskini inakataa uwezekano wa jambo hilo?..je biblia inajichanganya?

Jibu ni la! biblia haijichanganyi, kwani maneno yake yote yamethibitika na wala haijakosewa mahali popote..

Sasa iliwezekanikaje nabii Samweli kuzungumza na Sauli aliye hai na ishindikane kwa Lazaro kurudi kuwahubiria walio hai?.

Fumbo lipo kwa huyo mwanamke mwenye pepo, alichokifanya mwanamke mwenye pepo si kumfufua nabii Samweli na kumrudisha juu, hiko kitu kisingewezekana….alichokifanya mwanamke mwenye pepo ni kuwasiliana na wafu.. na kutoa taarifa za wafu na kuwapa walio hai.

Hivyo Sauli hakumwona Samweli kwa macho, ndio maana alimwuliza yule mwanamke; anayezuka anaonekanaje na yule mwanamke akamtajia kuwa ni mzee mwenye mvi, ikimaanisha kuwa Sauli hakuwa anamwona Samweli, bali alikuwa anasubiria taarifa kutoka kwa yule mwanamke.

Kwahiyo kilichokuwa kinaendelea pale ni kwamba Sauli alikuwa anaongea na Samweli kupitia kinywa cha yule mwanamke, (kama tu vile mtu anavyoongea na roho za mapepo, kupitia kinywa cha yule aliyepagawa na pepo).

Lakini katika ile habari ya Luka, yule Tajiri alitaka Lazaro atoke kule kwa wafu (yaani afufuke) arudi katika mwili aseme na walio hai, jambo ambalo lisingewezekana..

Sasa utauliza je mpaka leo inawezekana mtu kuwasiliana na wafu kama huyu mwanamke mwenye pepo alivyofanya?.

Jibu ni La! Baada ya Bwana YESU kufufuka alizitwaa funguo za mauti na kuzimu, na kuwamiki wote walio hai na walio kufa, kwahiyo hakuna yoyote hata shetani mwenye uwezo wa kuwasiliana na mfu, au kutoa habari za wafu.

Mwenye uwezo huo ni BWANA YESU PEKE YAKE!!.

Mapepo yanaweza kujigeuza na kuchukua sauti na umbile la mtu aliyekufa na kuigiza kama yule mtu, na kuwatokea watu yakidai ni watu halisi waliokufa… yanaweza kufanya hivyo kwani maandiko yanathibitisha hilo.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Nabii Samweli hakumtokea Sauli na kusema naye, bali alizungumza naye kupitia kinywa cha yule mwanamke mwenye pepo, na jambo hilo kwasasa haliwezekani tena kwani Kristo ndiye mwenye funguo hizo peke yake.

Kwa urefu kuhusiana na roho za waliokufa na mizimu fungua hapa 》》》Mizimu ni nini?

Bwana akubariki…

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Nini tofauti kati ya kileo na divai ?

1Samweli 1:5 Hana akajibu, akasema, Hasha! Bwana wangu, mimi ni mwanamke mwenye roho ya huzuni, mimi  sikunywa divai wala kileo, ila nimeimimina roho yangu mbele za Bwana.

Divai na kileo ni vinywaji vya kulewesha, na vyote vilitumika zamani katika Israeli, ambavyo hata sasa vinatumika.

Tofauti kati ya Divai na kileo ni hii;

DIVAI:

Divai, ilichachushwa kutoka katika matunda ya zabibu tu.

Kwa wayahudi divai ilikuwa kama kinywaji cha kitamaduni kilichotumika sana sana katika karamu mbalimbali za kijamii,  tunaona mfano wa sherehe ile aliyoalikwa Bwana Yesu kule Kana,  katikati ya sherehe walitindikiwa Divai, ndipo Yesu akaenda kuyageuza yale maji kuwa divai. Kuonyesha kuwa divai ilikuwa ni kinywaji kilichoruhusiwa kitamaduni Israeli, katika karama. (Yohana 2)

 Lakini pia ilikuwa kama kinywaji cha kiibada, katika karamu za kidini, kwa mfano sikukuku za pasaka, wana wa Israeli walikunywa  divai pamoja na mikate isiyotiwa chachu. Tunaona hilo Kristo alilidhihirisha kipindi kile cha pasaka alipoketi na wanafunzi wake akawapa mkate na divai, kama ishara ya mwili wake na damu yake, imwagikayo kwa ajili ya ondoleo la dhambi za watu wengi. (Mathayo 26.27-29)

Lakini pia divai ilisimama kama kiashiria cha furaha, au baraka.

Zaburi 104: 15 Na divai imfurahishe mtu moyo wake. Aung’aze uso wake kwa mafuta, Na mkate umburudishe mtu moyo wake.

MVINYO:

Mvinyo ulitengenezwa kwa  ngano, shayiri, makomamanga, au tende tofauti na divai iliyozalishwa katika zabibu tu.

Mvinyo ulikuwa na kilevi kikali kuliko divai, na matumizi yako hayakuwa rasmi Israeli, Ilitumika sana sana katika karamu za ulafi na ulevi, lakini sio katika shughuli zozote za kijamii au kidini.

Makuhani hawakuruhusiwa kuinywa walipokuwa wakihudumu katika hema (Walawi 10:9)

Lakini maandiko yanasema nini kuhusu ulevi?

Mithali 20:1 Mvinyo hudhihaki, kileo huleta ugomvi; Na akosaye kwa vitu hivyo hana hekima.

Katika andiko hilo tunaona Hana, aliposhutumiwa na Eli kuhusu ulevi, yeye akamwambia mimi sikunywa divai wala kileo. Kuonyesha kuwa alitilia umakini ibada yake na sala zake kwa Mungu.

Hata leo, ni vema tufahamu kuwa hatulewi tena kwa mvinyo, bali kwa Roho Mtakatifu tuliyepewa ndani yetu (Waefeso 5:18), Yeye ndiye divai yetu na mvinyo yetu.

Hivyo ni wajibu wa mwamini yoyote kudumu katika Maombi, kutafakari Neno, na ibada, ili ajazwe vema Roho.

Mungu akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Paulo alimwambia Timotheo atumie mvinyo kidogo kwa ajili ya tumbo lake, Je! tunaruhusiwa na sisi pia kutumia pombe?

Je! mabalasi Bwana Yesu aliyoyatumia kugeuzia maji kuwa divai, yalitumika tu kwa kazi hiyo?

Kwanini Bwana YESU ageuze maji kuwa Divai? Na ni ujumbe gani tunapata?

Print this post

Je Bwana YESU alikuwa na amri ya kumwingiza mtu katika ufalme wa MUNGU au hakuwa nayo?

Swali: Kwenye Mathayo 20:20-25 Mke wa Zebedayo anamwendea YESU na wanawe akimuomba wakae pande zote za YESU na awape mamlaka alizonazo ila YESU akamwambia hana amri juu ya jambo hilo lakini huku kwenye Luka 23:39 anamwambia mmoja wa wale wanyang’anyi leo hii utakuwa na mimi peponi, naomba ufafanuzi wa mwingiliano huo wa maandiko….Je biblia inajichanganya kwa maneno hayo???…

Jibu: Turejee mistari hiyo..

Mathayo 20:20 “Ndipo mama yao wana wa Zebedayo akamwendea pamoja na wanawe, akamsujudia, na kumwomba neno.

21  Akamwambia, Wataka nini? Akamwambia, Agiza kwamba hawa wanangu wawili waketi mmoja mkono wako wa kuume, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika ufalme wako.

22  Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomba. Je! Mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi? Wakamwambia, Twaweza.

23  Akawaambia, Hakika mtakinywea kikombe changu; lakini kuketi mkono wangu wa kuume na mkono wangu wa kushoto, sina amri kuwapa, bali watapewa waliowekewa tayari na Baba yangu.

24  Na wale kumi waliposikia, waliwakasirikia wale ndugu wawili”.

Hapa tunaona Bwana anatamka kuwa “Hana amri ya kuwaketisha vijana hao upande wa kuume na kushoto katika ufalme wake”

Tusome tena Luka 23:39

Luka 23:39 “Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi.

40  Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?

41  Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.

42  Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.

43  YESU AKAMWAMBIA, AMIN, NAKUAMBIA, LEO HIVI UTAKUWA PAMOJA NAMI PEPONI.”

Sasa swali ni kwanini KRISTO awe na amri juu ya huyu mhalifu na asiwe amri juu ya wale Vijana wa Zebedayo?.

Jibu ni kwamba “walichokiomba wana wa Zebedayo ni tofauti na alichokiomba huyu mhalifu”.. Wana wa Zebedayo wenyewe waliomba nafasi za ukubwa ndani ya ufalme wa mbinguni (kwamba watakapofika mbinguni wakawazidi wengine wote ikiwemo akina Petro na mitume wengine na hata sisi watu wa kizazi hiki)…

Lakini huyu Mhalifu yeye hakuomba ukubwa wowote ndani ya ufalme wa mbinguni kwamba akawe nani huko anakokwenda bali aliomba tu nafasi ya kuuingia ule ufalme wa mbinguni, (habari za kwenda kuwa nani huko aendako hilo hakujali, alichokitamani na kuuingia tu ule ufalme).

Na KRISTO alimpa hiyo nafasi kwani hiyo AMRI anayo kwa watu wote watakaokiri makosa yao Ikiwa na kumwamini Bwana YESU kama alivyofanya huyu Mhalifu. (Na KRISTO alimwambia vile kwasababu alijua hatakengeuka tena, kwani maisha yake ndio yalikuwa yanaenda kuisha, alikuwa amebakisha masaa machache tu ya kuishi).

Lakini wana wa Zebedayo, tayari walikuwa wameshajiwekea hakika wa kuuingia ufalme wa mbinguni, kwasababu walishamwamini Bwana YESU na kutubu kitambo kirefu….na hivyo wakaenda mbali zaidi si kuomba kuuingia ufalme wa mbinguni, bali kuomba nafasi za juu katika huo ufalme wa mbinguni watakaouingia… Jambo ambalo KRISTO asingeweza kuwaahidia.

Ni sawasawa na mwanafunzi anayemwomba mwalimu ampe zawadi ya nafasi ya kwanza darasani na ilihali bado hajafanya mtihani.. Ni wazi kuwa mwalimu hawezi kumpa hiyo zawadi, kwani bado hajafanya/kumaliza mtihani…Matokeo yatakapotoka ndio yatakayoeleza kama anastahili hiyo zawadi ya nafasi ya kwanza au la!.

Na KRISTO hakuwa na amri ya kuwapa hizo nafasi walizokuwa wanazitaka kwani vita vya imani bado walikuwa hawajavimaliza, na ule mwisho bado haujafika, ambapo kazi ya kila mtu itakapopimwa na kupewa thawabu,

Siku ile kama watakuwa wamefanya bora kuliko wengine wote watapata hiyo nafasi waliyoiomba (ya kuketi mkono wa kuume na kushoto), lakini kama watatokea wengine watakaofanya vema kuliko wao, basi wataikosa na nafasi hizo watapewa wengine.

Je umeokoka?

Je unajua kuwa YESU KRISTO anarudi!… na dalili za kurudi kwake karibia zote zimeshatimia?..Je unafahamu kuwa kuishi maisha ya uvuguvugu ni laana? Soma Ufunuo 3:14, leo unaenda kanisani kesho unaenda bar, asubuhi unaimba kwaya, jioni miziki ya kidunia, kwenye kabati una nguo za heshima, na nguo za kikahaba.. Huo wote ni uvuguvugu ambao Bwana YESU alisema matokeo yake ni kutapikwa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post