SWALI: Naomba kufahamu maana ya unabii unaozungumzia taifa la Tiro (Isaya 23). Kwamba litafanya ukahaba na falme zote ulimwenguni kisha utajiri wake utakuwa wakfu kwa Bwana. Tafsiri yake ni nini?
Isaya 23:17-18 inasema..
[17]Hata itakuwa mwisho wa miaka sabini, BWANA ataizuru nchi ya Tiro, naye atarudi apate ujira wake, atafanya ukahaba pamoja na falme zote za ulimwengu juu ya uso wa dunia.
18 Na biashara yake na ujira wake utakuwa wakfu kwa BWANA, hautawekwa hazinani wala hautawekwa akiba; bali mapato ya biashara yake yatakuwa mali zao wakaao mbele za BWANA, wapate kula na kushiba, na kuvaa mavazi ya fahari.
JIBU: Ukianza kusoma toka mstari wa kwanza wa hiyo sura ya ishirini na tatu (23), utaona Mungu anazungumzia adhabu, aliyoitoa kwa hilo taifa la Tiro lililokuwa na utajiri na mali nyingi kutokana na biashara zake lilizofanya na dunia nzima. Hata kuyakosesha na mataifa mengine, kwa bidhaa zake. Na jambo hilo Mungu akalihesabu kama ni ukahaba, hivyo akalipiga na kuliangusha kabisa likawa si kitu tena kwa muda wa miaka sabini(70).
Ni mfano tu, mataifa yanayokosesha ulimwengu sasa, kwa kuuza bidhaa ambazo ni machukizo kwa Mungu, utakuta taifa linazalisha nguo za mitindo ya nusu uchi, na kuyauzia mataifa mengine, au linatengeneza sinema zenye maudhui za kizinzi na kuyasambazia mataifa mengine yaliyokuwa na maadili.. Huo ndio mfano wa ukahaba ambao taifa la Tiro lilikuwa linafanya.
Isaya 23:15
[15]Basi, itakuwa katika siku ile, Tiro utasahauliwa miaka sabini, kadiri ya siku za mfalme mmoja; hata mwisho wa miaka sabini, Tiro utakuwa kama vile ulivyo wimbo wa kahaba.
Lakini baadaye Mungu alilirudia tena, na kuruhusu lifanikiwe, kama pale mwanzo. Likajikusanyia tena utajiri mwingi sana kwa biashara zake.. Lakini Kwasababu halikutubu, kitabia Mungu akalipiga kwa namna nyingine kwa kuzuia utajiri wao wasiule au kwa lugha nyingine hazina zao zisitunzwe kwa maendeleo yao, Bali Bwana atazizuia zije kutumika kwa kazi yake yeye mwenyewe na watu wake.
Na unabii huo ulikuja kutimia..
ndio maana ya huo mstari wa 18, unaosema..
[18]Na biashara yake na ujira wake utakuwa wakfu kwa BWANA, hautawekwa hazinani wala hautawekwa akiba; bali mapato ya biashara yake yatakuwa mali zao wakaao mbele za BWANA, wapate kula na kushiba, na kuvaa mavazi ya fahari.
Hii ni kufunua nini?
Kufanikiwa kwake mwovu, kunatimiza makusudi mawili la kwanza ni aidha kwenda kujiangamiza mwenyewe (Mithali 1:32, Zab 92:7), au kumkusanyia mtu mwingine mwenye haki.
biblia inasema..
Mithali 28:8
[8]Yeye azidishaye mali yake kwa riba na faida, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.
Watu wengi wanaofanikiwa isivyo halali,mara nyingi mali zao, hula wengine..Ndicho alichokifanya Mungu kwa taifa la Tiro.
Ni kutufundisha pia fedha na dhahabu ni mali ya Bwana. Yeye ana uwezo wa kuzuia na kuachilia, anauwezo wa kuwapa watu wake hazina za gizani ambazo hawajazisumbukia, kwa ajili ya kazi yake.
Hivyo kumbuka Bwana akufanikishapo, tembea na Kristo, kinyume na hapo, mambo hayo mawili yanaweza kukukuta, aidha mafanikio hayo yazidi kukuangamiza ufe uende kuzimu, au yaliwe na watu wengine kabisa wema usiowajua na kazi yako ikawa bure.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Masomo mengine:
Kwanini Herode aliwakasirikia watu wa Tiro na Sidoni? (Matendo 12:20)
Swali: Sheshaki inayotajwa katika Yeremia 25:26 ilikuwa ni wapi?
Jibu: Turejee..
Yeremia 25:26 “na wafalme wote wa kaskazini, walio mbali na walio karibu, wote pamoja; na wafalme wote wa dunia, wakaao juu ya uso wa dunia; na MFALME WA SHESHAKI atakunywa baada yao.
27 Nawe utawaambia hivi, Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nyweni, na kulewa, na kutapika, na kuanguka msiinuke tena, kwa sababu ya upanga nitakaoupeleka kati yenu”.
“SHESHAKI” ni jina lingine la Taifa la “Babeli”. Kama vile “YESHURUNI” ilivyo jina lingine la Taifa la Israeli.
Kumbukumbu 33:26 “Hapana aliyefanana na Mungu, Ee Yeshuruni, Ajaye amepanda juu ya mbingu ili akusaidie. Na juu ya mawingu katika utukufu wake”.
Soma pia Kumbukumbu 32:15 na Isaya 44:2, utaona Zaidi kuhusu Yeshuruni, na kwa urefu Zaidi fungua hapa >> Yeshuruni ni nani katika biblia?
Na vivyo hivyo na “Babeli”, jina lake lingine aliitwa “Sheshaki”… Majina haya yalitumika mara nyingi kwenye mashairi na methali za kiyahudi. Utalisoma jina hilo tena katika Yeremia 51:41, ambapo imetaja kwa uwazi kuwa ni Babeli.
Yeremia 51:41 “Jinsi Sheshaki alivyotwaliwa! Naye sifa ya dunia yote alivyoshambuliwa! Jinsi Babeli alivyokuwa ukiwa katikati ya mataifa.
42 Bahari imefika juu ya Babeli, Umefunikwa kwa wingi wa mawimbi yake.
43 Miji yake imekuwa maganjo; Nchi ya ukame, na jangwa; Nchi asimokaa mtu ye yote, Wala hapiti mwanadamu huko”.
Je Umeokoka?.. kama bado unasubiri nini?..
Maran atha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Jibu: Turejee..
Walawi 15:1 “Kisha Bwana akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,
2 Haya, semeni na wana wa Israeli, mkawaambie, Mtu ye yote atakapokuwa na kisonono kimtokacho mwilini mwake, atakuwa najisi kwa ajili ya kisonono chake.
3 Na unajisi wake katika kisonono chake ni huu; kama mwili wake unachuruzika kisonono chake, au kama kisonono chake kimezuiwa mwilini mwake, ni unajisi wake.
4 Kitanda cho chote akilaliacho mwenye kisonono kitakuwa najisi; na kitu cho chote ambacho akiketia kitakuwa najisi”.
Moja ya magonjwa yaliyotajwa kwenye biblia ni pamoja na huu wa “kisonono” lakini kisonono hiki ni Zaidi ya hiki tukujuacho ambacho kipo mingoni mwa magonjwa ya zinaa (Maarufu kama Gonorrea).
Mistari mingine iliyotaja ugonjwa huo ni (Walawi 22:14 na Hesabu 5:2)
Kisonono kilichozungumzwa katika biblia ni mjumuiko wa magonjwa yote yanayosababisha kutokwa na uchafu katika njia za haja ndogo (kwa jinsia zote), yawe yanasababishwa na zinaa, au yasiyosababishwa na zinaa….na uchafu huo ni pamoja na (usaha, damu au mchanganyiko).
Kwahiyo katika biblia mtu yeyote aliyetokwa na chochote kati ya hivyo katika viungo vyake vya uzazi alihesabika kuwa na kisonono na alikuwa najisi mpaka atakapopona ugonjwa huo (hawezi kukusanyika katika kusanyiko la Bwana, na alikuwa anatengwa).
Lakini je hata sasa mtu wa namna hii anapaswa kutengwa?
Katika agano jipya hakuna agizo la kuwatenga wagonjwa wa aina yoyote, au wanawake walio katika mzunguko wa hedhi. Wote wanaweza kukusanyika katika nyumba ya Mungu (kwasababu kimtokacho mtu katika mwili hakimtii unajisi, bali kile kimtokacho kutoka moyoni, ndicho kinachomtia mtu unajisi, sawasawa na Marko 7:20-22).
Marko 7:20 “Akasema, Kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi.
21 Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati,
22 wivi, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu.
23 Haya yote yaliyo maovu yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi”.
Ikiwa mtu huyo amejitakasa moyoni kwa viwango vya kustahili kumfanyia Mungu ibada, hata akiwa na maradhi mwilini, bado ibada yake itapokelewa na Bwana.
Ikiwa kisonono mtu alichokipata ni matokeo ya zinaa, huyu mtu anapaswa atubie kwanza zinaa yake aliyoifanya kwa kumaanisha kuacha hiyo dhambi (kwa ufupi aokoke), na baada ya toba akiwa katika hatua za kutafuta uponyaji, anaweza kujumuika na wengine katika majumuiko ya kumwabudu Mungu.
Vile vile ikiwa ameupata kwa njia nyingine isiyohusisha zinaa, atajitakasa nafsi yake kwa toba na rehema kwa makosa mengine na atajiunga na wengine katika kumwabudu Mungu.
Mwisho: Mshahara wa dhambi ni mauti..ikimbie dhambi, na sehemu salama ya kukimbilia ili upate msaada ni msalabani, kwasababu msaada kamili upo msalaban, Kama hujampokea Bwana YESU upo hatarini…na hauwezi kushindana na dhambi.
Ni heri leo ukayasalimisha maisha yako kwake, na yeye atakuokoa.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
FAHAMU ZA WATU HUWA ZINAONDOLEWA NA NINI?
Tatizo la Bawasiri kibiblia
Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?
JINSI UNAJISI UNAVYOMGHARIMU MTU.
Kati ya lugha tatu ambazo zinaonekana katika uandishi wa biblia Kiaramu (Aramaic), ni mojawapo nyingine zikiwemo Kiebrania na kiyunani.
Sehemu kubwa ya agano la kale imeandikwa katika lugha ya Kiebrania na maeneo machache machache sana yalikuwa na maandishi ya kiaramu, (Ezra 4:8 – 6:18, Danieli 2: 4 – 7:28)
Lakini katika agano jipya sehemu kubwa imeandikwa katika lugha ya kiyunani (kigiriki), na mahali pachache pachache kuna maandishi ya kiaramu.
Hivyo lugha hii haipo kwa sehemu kubwa katika biblia
Je chimbuko la hii lugha ni wapi?.
Ni lugha iliyozungumzwa na watu walioitwa Waaramu, ambao lugha yao ilienea kwenye mataifa mbalimbali ambayo kwasasa ni nchi za Lebanoni, Syria, Yordani, Iraq, na Uturuki, na sehemu nyingine za mashariki ya kati. Ni lugha ambayo ilikuwa na nguvu sana zamani za falme kama Ashuru, na ufalme wa Uajemi.
Enzi za Bwana wetu Yesu Kristo, lugha hii ilizungumzwa pia maeneo ya Israeli hususani katika miji ya Galilaya, ambapo Bwana wetu Yesu Kristo alilelewa. Huku kiyahudi ikiwa ni lugha ya asili, kidini na kisiasa.
Hivyo lugha kuu ya Bwana ilikuwa ni hii kiaramu, japokuwa alizungumza pia kiyahudi.
Baadhi ya maneno ya kiaramu ambayo yananukuliwa moja kwa moja kutamkwa na Bwana Yesu ni haya; (japo yapo na pia mengine)
Marko 5:41 “Akamshika mkono kijana, akamwambia, Talitha, kumi; tafsiri yake, Msichana, nakuambia, Inuka”.
Marko 7:34 “akatazama juu mbinguni, akaugua, akamwambia, Efatha, maana yake, Funguka.
Marko 15:34 “Na saa tisa Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Maana yake, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
Maneno mengine ni kama “Hosana” (lenye maana ya okoa sasa), Mathayo 21:9
“Aba” (Marko 14:36), lenye maana ya Baba.
Lakini pia swali la kujiuliza ni nini sababu ya Bwana Yesu, kuipenyeza lugha hii katika baadhi ya matukio?
jibu ni kuwa hakuna jambo la muhimu sana katika hiyo lugha, isipokuwa ni maongozo ya Roho Mtakatifu ndani yake kwa wakati huo. Kama tu sehemu nyingine alipoongozwa kutema mate chini atengeneze tope apake mtu machoni ili apone.
Hivyo Bwana Yesu alikuwa ni mtu aliyetega sikio kuisikia sauti ya Roho. Vivyo hivyo na sisi, misukumo mbalimbali yaweza kuja ndani yetu. Wakati mwingine hutaomba kwa akili, utaomba kwa kunena kwa lugha, utaomba kwa nyimbo, utaomba kwa kuugua na kulia, kwa jinsi Roho atakavyokusukuma ndani.
Ni kutuonyesha kuwa Bwana hakuwa na fomula fulani pekee katika kutenda kazi, alitegemea maongozo ya Roho Mtakatifu.
Vivyo hivyo na sisi tunapojawa Roho vema. Atatugusa kwa namna mbalimbali na hivyo tutatimiza makusudio yake vizuri, katika jina lake kuu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
JE! NI LAZIMA WATU WOTE WANENE KWA LUGHA?
ZIFAHAMU KARAMA 9 ZA ROHO MTAKATIFU NA UTENDAJI KAZI WAKE.
UNYAKUO WA KANISA UMEPITA LEO!!
Swali: Katika Luka 19:26, kwanini Bwana YESU aseme kila mwenye kitu atapewa na yule asiye na kitu atanyang’anywa?, na kwanini isiwe kinyume chake?..kwasababu hilo ni kama jambo la kikatili, kumnyang’anya mtu kile kidogo alicho nacho.
Jibu: Turejee mstari huo..
Luka 19:24 “Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang’anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi.
25 Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi.
26 Nawaambia, KILA ALIYE NA KITU ATAPEWA, BALI YULE ASIYE NA KITU ATANYANG’ANYWA HATA ALICHO NACHO”.
Ni kweli tukisoma kwa tafakari za kawaida (za kimwili) ni kama jambo la kikatili, kumpokonya mtu kile kidogo alichonacho, lakini mstari huo hauhusu mambo ya mwilini bali ya rohoni (kwamba maskini anyang’anywe kidogo alicho nacho na apewe tajiri..La! hiyo sio maana ya huo mstari).
Ili tuelewe vizuri, turejee ule mfano wa Mzabibu katika Yohana 15:1-2, Neno la Mungu linasema..
Yohana 15:1 “Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima.
2 KILA TAWI NDANI YANGU LISILOZAA HULIONDOA; NA KILA TAWI LIZAALO HULISAFISHA, ILI LIZIDI KUZAA”.
Kwa wale wakulima wanaelewa lengo la kuondoa yale matawi yasiyozaa matunda ni nini?.
Kusudi au lengo la kuondoa yale matawi yasiyozaa na kubakisha yale yanayozaa peke yake katika shina la mti ni kudhibiti matumizi mabaya ya chakula yatokayo katika mizizi kulekeka katika matawi.
Chakula kitokacho ardhini, na kupanda katika matawi ya mti, kama matawi yale yapo kumi (10) na kati ya hayo manne (4) ndiyo yenye kuzaa na (6) yaliyosalia hayazai, ni kwamba kile chakula kitokacho kwenye mizizi na kuelekea kwenye matawi hayo, kitajigawanya kulingana na idadi ya matawi yaliyopo.. na hivyo yale matawi manne (4) yazaayo yatapokea chakula kidogo, na yale (6), yatapokea kingi.
Sasa matokeo yake ni kwamba yale matawi manne (4) yazaayo yatazaa kwa kiwango kidogo kwasababu ya kiasi kidogo cha chakula yapokeayo, na yale mengine sita yasiyozaa yatakuwa yanapokea chakula cha bure ambacho hakiyasaidii matawi hayo, hivyo uzalishaji wa ule mti UTAKUWA HAFIFU, endapo ukiendelea kubaki na yale matawi yasiyozaa.. (mti utaonekana una matawi mengi na mkubwa lakini matunda machache).
Sasa kutatua hilo tatizo wakulima, huwa wanayaondoa yale matawi yasiyozaa ili yasiendelee kutumia chakula cha bure, na matokeo ya kuyaondoa kwa kuyakata yale matawi yasiyozaa, na kubakisha yale yazaayo peke yake, ni kwamba kile chakula chote kitokacho ardhini hakitapotea bali kitaenda moja kwa moja kwa yale matawi yazaayo..
Na matokeo yake yale matawi yazaayo yatapokea virutubisho vingi na kusababisha kuzaa Zaidi..Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba uwepo wa matawi yasiyozaa katika shina ni uharibifu kwa yale matawi mengine yazaayo..
Na hiyo ndiyo sababu ya Bwana YESU kusema, “KILA ALIYE NA KITU ATAPEWA, BALI YULE ASIYE NA KITU ATANYANG’ANYWA HATA ALICHO NACHO”.. maana yake KILA TAWI LINALOZAA LITAONGEZEWA NGUVU NA LILE LISILOZAA HATA KILE KIDOGO LIPOKEACHO LITANYANG’ANYWA (LITAKATWA).
Mathayo 3:10 “Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni”.
Ikiwa umepata Neema ya kusikia injili lakini unaichezea, hutaki kuzaa matunda ya haki kuwa makini sana, kuna hatari mbele yako!!
Ikiwa umepata Neema ya kusikia Injili na hutaki kubadilika miaka nenda rudi, uko vile vile, kuwa makini!!
Luka 13:6 “Akanena mfano huu; Mtu mmoja alikuwa na mtini umepandwa katika shamba lake la mizabibu; akaenda akitafuta matunda juu yake, asipate.
7 Akamwambia mtunzaji wa shamba la mizabibu, Tazama, miaka mitatu hii naja nikitafuta matunda juu ya mtini huu, nisipate kitu; uukate, mbona hata nchi unaiharibu?
8 Akajibu akamwambia, Bwana, uuache mwaka huu nao, hata niupalilie, niutilie samadi;
9 nao ukizaa matunda baadaye, vema! La, usipozaa, ndipo uukate”.
Ikiwa umepewa Karama/huduma na hutaki kuitumia, ipo vile vile kuwa makini sana!!.. hiyo Neema itaondolewa kwako na kupewa mtu mwingine ambaye atazaa matunda.
Mathayo 25:24 “Akaja na yule aliyepokea talanta moja, akasema, Bwana, nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda, wakusanya usipotawanya;
25 basi nikaogopa, nikaenda nikaificha talanta yako katika ardhi; tazama, unayo iliyo yako.
26 Bwana wake akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya;
27 basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo yangu na faida yake.
28 Basi, mnyang’anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi.
29 Kwa maana kila mwenye kitu atapewa, na kuongezewa tele; lakini asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang’anywa”.
Bwana akubariki, na Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
TAWI LIZAALO HULISAFISHA ILI LIZIDI KUZAA.
SHIKA SANA ULICHO NACHO, ASIJE MTU AKAITWAA TAJI YAKO.
UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?
Tofauti kati ya zaka na sadaka ni ipi?
Yubile, wengine huiita yubilei, au yubilii.
Ni mwaka wa hamsini (50), katika kalenda ya miaka ya kiyahudi. Mungu aliwaagiza wana wa Israeli, wahesabu miaka saba, kisha waizidishe mara saba, 7×7=49.
Na ule unaofuata wa 50, uliitwa mwaka wa yubile.
Ni mwaka ambao Mungu aliwaagiza wapumzike kabisa, hawakuruhusiwa kupanda wala kuvuna. Kwa miaka miwili mfululizo(yaani mwaka wa 49 na ule wa 50), kwasababu ule wa 49 ni sabato ya kila mwaka wa 7, ndio maana miaka miwili inatokea hapo. Sasa swali la kujiuliza wangewezaje kuishi miaka yote miwili bila kufanya kazi? Jibu ni kwamba Mungu aliwabariki mara dufu katika mwaka wa 48, hivyo wakafanikiwa kukusanya vingi vya kuwatosha miaka yote hiyo miwili ijayo bila kazi.
Lakini pia ulikuwa ni mwaka wa kusamehe madeni sambamba na hilo ulikuwa mwaka pia wa kuwaachilia huru watumwa.
Walawi 25:8 Nawe utajihesabia Sabato saba za miaka, maana, miaka saba mara saba; zitakuwa ni siku za Sabato saba za miaka kwenu, maana miaka arobaini na kenda.
9 Ndipo utakapoipeleka pande zote hiyo baragumu yenye sauti kuu, siku ya kumi ya mwezi wa saba; katika siku hiyo ya upatanisho mtaipeleka baragumu katika nchi yenu yote.
10 Na mwaka wa hamsini mtautakasa, na kupiga mbiu ya kuachwa mahuru katika nchi yote kwa watu wote wanayokaa; itakuwa ni yubile kwenu, nanyi kila mtu atairudia milki yake mwenyewe, nanyi mtarejea kila mtu kwa jamaa yake.
11 Mwaka huo wa hamsini utakuwa ni yubile kwenu; msipande mbegu, wala msivune kitu hicho kimeacho chenyewe, wala msizitunde zabibu za mizabibu isiyopelewa.
12 Kwa kuwa ni yubile; utakuwa mwaka mtakatifu kwenu; mtakula maongeo yake yatokayo shambani. 13 Mwaka huo wa yubile mtairudia kila mtu milki yake.
14 Tena kama ukimwuzia jirani yako cho chote, au kununua cho chote mkononi mwa jirani yako, msidanganyane wenyewe kwa wenyewe;
15 kwa hesabu ya miaka iliyo baada ya yubile, ndivyo utakavyonunua kwa jirani yako, na kama hesabu ya miaka ya mavuno ndivyo atakavyokuuzia wewe
Yubile, ilifunua kazi ya msalaba baadaye. Kwani Bwana wetu Yesu ndiye aliyekuja kutimiza kazi hii rohoni.
Kwanza ndani yake tunapokea pumziko kamili la utumwa wa dhambi. Pili tunasamehewa deni zetu (dhambi zetu), Na Tatu tunafanywa huru, katika vifungo vya shetani. Yaani Magonjwa na mapepo.
Huo ndio mwaka wa Bwana uliokubaliwa, ndio Yubile yetu halisi.
lakini pia sisi kama waamini katika mwenendo wetu, tuna mambo ya kujifunza tuipatazampo Yubile?.
Kwanza ni umuhimu wa kupumzika, kuahirisha mambo yetu kupata muda na Mungu. Si tupate tu siku moja kwa wiki kuwa karibu na Mungu. Wakati mwingine Mungu anataka kipindi kirefu. Wewe kama mfanyakazi, au umejiajiri, jiwekee utaratibu baada ya kipindi fulani uwe na likizo ndefu ambayo unaitenga kwa Mungu wako,kuutafuta uso wake, ni muhimu sana.
pili tunajifunza kusamehe watu madeni yao. Si kila tunayemdai lazima atulipe, fikiria juu ya hilo. Yesu alisema achilieni nanyi mtaachiliwa. Hujui ni wapi na wewe sikumoja utakwama, na utatamani.uachiliwe.
na mwisho kuwapa uhuru watumwa wetu ikiwa wewe ni mwajiri, fikiria kuwa mfanyakazi wako anahitaji pumziko refua, mpatie, bila kumpunguzia mshahara wake. Bwana ataona umeitunza yubilee yake pia kimwili. Na sio kufanya kumbukizi ya ndoa, au kuzaliwa, hiyo sio yubilei.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!
Kitabu cha Matendo ya mitume hakimtaji moja kwa moja mwandishi wake, lakini tunaweza kumtambua, kutokana na utambulisho wake mwanzoni mwa waraka huo, kwamba ni LUKA. Kwasababu waraka huu aliulekeza kwa mtu mmoja aliyeitwa Theofilo, ambaye anamtaja pia alimtumia waraka wa kwanza uliozungumzia habari za Yesu tangu mwanzo hadi siku alipochukuliwa juu, na huu si mwingine zaidi ya waraka wa Luka. Soma Luka. (1:1-3)
Ndio maana inaaminika aliyeandika waraka huu ni Luka.
Matendo 1:1 Kitabu kile cha kwanza nalikiandika, Theofilo, katika habari ya mambo yote aliyoanza Yesu kufanya na kufundisha,
2 hata siku ile alipochukuliwa juu, alipokuwa amekwisha kuwaagiza kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua;
3 wale aliowadhihirishia nafsi yake, kwa dalili nyingi, baada ya kuteswa kwake, ya kwamba yu hai, akiwatokea muda wa siku arobaini, na kuyanena mambo yaliyouhusu ufalme wa Mungu.
Kitabu hichi cha matendo ya mitume, kama jina lake linavyojieleza kinaeleza hasaa jinsi mitume wa Bwana walivyoanza kulitekeleza lile agizo kuu la Yesu alilowaambia wakahubiri injili kwa kila kiumbe. Tangu Yerusalemu, uyahudi, samaria na dunia nzima.
Kinatufundisha jinsi Roho Mtakatifu alivyowaongoza hadi kukamilisha jukumu hilo la injili ulimwenguni mwote kwa mafanikio makubwa.
Na mambo ambayo tunajifunza kwao ni haya:
Umoja: Hawakuwa na nia tofauti tofauti, bali moja ya Kristo, walikubali kudumu katika fundisho la mitume bila shuku yoyote. Walifanya yote kwa ushirikiano kwasababu vitu vyote waligawana kama kila mtu alivyokuwa na hitaji lake.
Matendo 4:32 Na jamii ya watu walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja; wala hapana mmoja aliyesema ya kuwa kitu cho chote alicho nacho ni mali yake mwenyewe; bali walikuwa na vitu vyote shirika.
Mashauri ya pamoja: Hata mahali ambapo hakukueleweka vema, au kutokea kwa mikanganyiko waliweza kukaa katika Baraza la wazee na mitume, kutafakari kwa pamoja ndipo hekima ya Roho ikaamua yawapasayo kutenda.(Matendo 15: 1-21).Ndio maana hawakuwa na madhehebu.
Furaha ya Roho: Kanisa lilifurahia ibada, na imani ndani ya Kristo. Sio la watu ambao walisukumwa kufanya majukumu yao, bali wote waliona ni raha kumfuata Kristo kwa moyo mweupe.
Matendo 2:46 Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe
Maombi: Mara nyingi walidumu katika maombi, hekaluni, na manyumbani mwao (Watendo 1:14)
Upendo: Walipendana, Waliweza kuwa na vitu vyote shirika, hawakubaguana, wala kuwa na ubinafsi kiasi kwamba hakukuwa na yoyote aliyekuwa na mahitaji ndani ya kanisa.
Matendo 2:44 Na wote walioamini walikuwa mahali pamoja, na kuwa na vitu vyote shirika, 45 wakiuza mali zao, na vitu vyao walivyokuwa navyo, na kuwagawia watu wote kama kila mtu alivyokuwa na haja
Uvumilivu: Walipitia dhiki, wengine wapigwa mawe, waliburutwa, lakini hawakuitupilia mbali imani, kinyume chake ndio injili walizidi kuihubiri.
Matendo 8:1,4
1 Siku ile kukatukia adha kuu ya kanisa lililokuwa katika Yerusalemu; wote wakatawanyika katika nchi ya Uyahudi na Samaria, isipokuwa hao mitume…..4 Lakini wale waliotawanyika wakaenda huko na huko wakilihubiri neno.Hivyo hayo ni baadhi ya mambo ambayo na sisi tunaweza kujifunza katika kanisa la mwanzo.
Je! Umeokoka?
Kama bado unasubiri nini? Kumbuka hizi ni siku za mwisho. Tubu dhambi zao leo, mwamini Yesu, ukabatizwe akusamehe dhambi zako, Ikiwa utapenda kupata msaada huo wa kumpokea Kristo, basi fungua hapa kwa mwongozo huo >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
SWALI: Naomba kufahamu maana ya 1Wakorintho 15:24-25 , hususani hapo anaposema ‘hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake. 26 Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti’.
1Wakorintho 15:24 Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu.
25 Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake.
26 Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti.
JIBU: Bwana Yesu alikuja duniani kwa kazi maalumu ya kumkomboa mwanadamu pamoja na kumkamilisha. Na ukombozi huu, aliukamilisha wote siku ile pale msalabani kwa kifo chake. Hivyo tangu wakati ule mwanadamu ambaye atampokea, tayari maadui zake wote wamewekwa chini yake, ikiwemo na mauti yenyewe.
Lakini pia ni muhimu kufahamu, ukamilifu wa ukombozi wetu, sio sasa, kwasababu ijapokuwa tumeokolewa na ndani yetu tuna uzima wa milele, bado tutakufa (ki-mwili), bado tutaugua, bado tutazeeka, bado tutakula kwa taabu, bado tutapitia dhiki na masumbufu, bado tutakutana na uovu kila mahali tuendapo.
Hivyo ‘ukamilifu’ wetu kabisa kabisa bado. Lakini ‘ukombozi’ wetu tayari, tunaokoka tukiwa hapa hapa duniani, tukifa tunakuwa tunaishi. Sasa Ndio maana Yesu alikuja mara ya kwanza kama MWANAKONDOO achukuaye dhambi za ulimwengu, lakini pia atarudi mara ya pili, ambapo safari hii atakuja kama MFALME, Atawalaye kwa mamlaka na nguvu nyingi.
Safari hii atakuja sasa kwa ajili ya huo ukamilifu, kwanza atayahukumu mataifa na falme zao,(Mathayo 25:31-46) vilevile mapepo (Ufunuo 19:20), kisha ataurekebisha huu ulimwengu ulioharibika,(Ufunuo 6:12-17) na kuufanya kuwa zaidi hata ya edeni. Kisha atatawala na watakatifu wake, kwa kipindi cha miaka elfu moja (Ndio ule utawala wa amani wa Kristo wa miaka 1000), Ufunuo 20, hapa hapa duniani, kwa wakati huo dhiki nyingi sana zitaondoka, watu wataishi muda mrefu sana, biblia inasema mtu atakayekufa na miaka mia ataitwa mtoto mchanga,(Isaya 65:20) wanyama hawatakuwa wakali tena, , hakutakuwa na laana ya nchi kutoa miiba, wala kuzaa kwa uchungu. Hichi ni kipindi ambacho dunia itakuwa salama na tulivu sana. Ni wakati wa Raha ambao Yesu amewaandalia watumishi wake.
Lakini wapo baaadhi watakufa (lakini sio sisi tutakaonyakuliwa), kwasababu shetani alikuwa bado hajahukumiwa amefungwa tu, hicho ndio kipindi ambacho Kristo atakwenda kutokomoza mauti ya mwili, hivyo shetani atafunguliwa kwa muda, ajaribu kuwaangusha watakatifu, atashindwa na kutupwa kwenye ziwa la moto pamoja na watu wote waovu (Ufunuo 20:7-10). Hapo ndipo mwisho wa yote, hakuna tena mauti, wala kifo, wala uchungu, wala huzuni,. Yesu atayakamilisha yote, ambapo adui wa mwisho ndio huyo mauti ya mwili.
Ufunuo 21:1 Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.
2 Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe.
3 Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.
4 Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.
5 Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli.
6 Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure
Wakati huo ndio Kristo atakuwa ameikamilisha kazi yake yote, na kumrudishia Baba ufalme wote, kama ilivyokuwa kule mwanzo, ili tumwabudu Mungu, sio katika kukombolewa, au kuchungwa, au katika kuongozwa tena, katika ile mbingu mpya na nchi mpya, Huduma ya Kristo itakuwa imeisha.
Yatakuwa makao yetu milele. Mambo ambayo tumeandaliwa huko ndugu, jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia. Unasubiri nini leo usimpe Bwana maisha yako? Kumbuka tunaishi katika nyakati ambazo Kristo amekaribia sana kurudi. Moja ya hizi siku parapanda italia, tutakwenda mbinguni. Tubu dhambi zako, mwamini Yesu, upokee uzima wa milele.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
SIFA SITA (6), ZINAZOIKAMILISHA ILE SIKU YA BWANA ITISHAYO.
Yeremia 29:12 Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.
13 Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.
14 Nami nitaonekana kwenu, asema Bwana, nami nitawarudisha watu wenu waliofungwa, nami nitawakusanya ninyi, nikiwatoa katika mataifa yote, na katika mahali pote, nilikowafukuza, asema Bwana; nami nitawaleta tena, hata mahali ambapo kutoka hapo naliwafanya mchukuliwe mateka
Huu ni utabiri ambao Mungu aliwaambia Israeli, pindi tu walipochukuliwa utumwani Babeli, akiwaahidia atawarudisha tena kwenye nchi yao baada ya miaka sabini. Na zaidi ya hayo akawapa pia na Neno la ahadi kwamba wakati huo wakimtafuta kwa mioyo yao yote, watamwona, watamwomba atawasikia, na wote watarejeshwa nyumbani ijapokuwa walichukuliwa mbali sana.
Na kweli utabiri huo ulikuja kutumia, kwani mwishoni mwa hiyo miaka sabini, mbiu ilipigwa waisraeli wote warudishwe kwao. Na aliwaonekania sana pindi waliporejea.
Ni neno la ahadi hata kwetu,
Kwamba tukimtafuta yeye kwa mioyo yetu yote, tutamwona. Kumbuka anasema “MIOYO YETU YOTE”. Kosa linatokea pale tunapompenda Mungu kwa sehemu, leo kwake kesho kwa shetani. Ndio Inayopelekea tusimwone Mungu katika ukamilifu wake wote. Mungu anahitaji vyako vyote vielekee kwake, ndipo tumwombe na kumwita ili atuitikie..
Shalom
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine
Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho,
Rudi Nyumbani
Katika mapokeo ya kikristo, moja ya eneo ambalo limezuia mikanganyiko mingi, ni eneo hili linalohusiana na “Uungu wa Mungu” . Migawanyiko ya madhehebu mengi unayoyaona sasa chimbuko kubwa hasaa ni hapa.
Wapo wanaoamini Mungu ni mmoja amegawanyika katika nafsi tatu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu), lakini wapo wanaoamini Mungu ni mmoja mwenye nafsi moja (Hajagawanyika), yaani Yesu ni Yule Yule Yehova aliyekuwa zamani zile, wengine hawaamini kabisa kama Yesu anastahili kuwekwa katika nafasi ya uungu, wengine hawaamini kuwa Roho Mtakatifu ni halisi, bali ni nguvu tu ya Mungu, ni Yesu na Mungu tu basi. Je! Ukweli ni upi? Na Je tunapaswa tusimamie wapi?
Jambo la kwanza kufahamu, ni kuangalia kiini, cha kumjua Mungu? Kama kiini kimeharibika hapo ndipo penye shida kubwa. Tunaposema kiini, tunamaanisha idadi ya miungu. Cha ajabu ni kwamba makundi yote haya yanaamini “Mungu ni mmoja”, sawasawa na maandiko yanavyosema..
Marko 12:29 Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, BWANA MUNGU WETU NI BWANA MMOJA;
30 nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.
Tena kizuri zaidi ni kwamba wote wanaamini kazi ya Kristo ya ukombozi, wanaamini pia kazi za Roho Mtakatifu mioyoni mwetu.
Kinachotofautisha ni kutambua tu, nafasi zao za kiungu. Hilo tu, ambalo kimsingi halina nguvu sana, zaidi ya kuzitambua kazi zao mioyoni mwetu. Ni sawa na watu wawili wanaoshindania kama MUWA, ni jamii gani ya mmea, mmoja anasema ni tunda, mwingine anasema ni aina ya jani. Embu jiweke wewe katika hiyo nafasi, ukiulizwa swali hilo utasema ni nini?. Ni rahisi kusema “muwa” ni tunda, lakini kibaolojia muwa ni jamii ya “jani”, isipokuwa limerefu tu zaidi ya mengine na lina maji matamu, .
Sasa je! Kufahamu kama ni jani, au ni tunda? Maarifa hayo yanaweza kubadili asili yake? Kwamba ukifahamu sukari yake itaongezeka, au itawabadilikia maumbo. Wewe na yeye hamna tofauti, kiladha, isipokuwa kiufahamu tu.
Vivyo hivyo na kwenye uungu wa Mungu, Tunatafuta “UJUZI”. Na ujuzi ni mzuri, lakini mara nyingi tunapoung’ang’ania sana haujengi, bali huleta matengano, Ni upendo tu ndio unaojengwa.
1Wakorintho 8:1b…Twajua ya kuwa sisi sote tuna ujuzi. Ujuzi huleta majivuno, bali upendo hujenga
Ndio maana kwanini hatushangai kuona kanisa la kwanza, liliweza kutembea katika utimilifu wote wa ki-Mungu ijapokuwa hawakuwa na maarifa ya kutosha ya kutambua uungu wa Yesu, vema, isipokuwa baadaye sana katika nyaraka za mitume, ambayo hata hivyo waliita ‘Siri ya Mungu’. Lakini hao hao waliweza kumwabudu Kristo, lakini pia wakamwabudu Baba, bila shida yoyote, wapo waliotambua siri hii, lakini wapo ambao hawakutambua vema.
Kuonyesha kuwa hilo sio jambo la kung’ang’ania sana kana kwamba usipojua utakwenda kuzimu, kama inavyochukuliwa leo, mpaka kutupelekea matengano.
Ukweli ni kwamba Mungu wetu ni Yule Yule mmoja, isipokuwa ametenda kazi kwenye nafasi tatu tofauti kwa lengo la kumkamilisha mwanadamu, na sio yeye. Na sio kana kwamba ni watu watatu wamepatana katika jambo moja. Ni sawa na maji, mvuke na barafu. Vyote vitatu vikiwekwa pamoja vinaweza kuonekana na vitu tofauti tofauti kabisa, lakini ni kitu kile kile kimoja, ambacho ni maji. Ndivyo alivyo Mungu wetu.
Kutembea katika ofisi ya ubaba, na wakati huo huo mwana, na wakati huo huo Roho Mtakatifu, sio shida kwake, amefanya hivyo ili sisi tukamilishwe. Kama mwanadamu asingeanguka hakukuwa na haja ya Mungu kujifunua katika ofisi zote, angebakia katika ubaba wake ule ule mmoja,
Ni sawa na mtu aliyebuni simu, kama kusingekuwa na changamoto ya umbali ya nini mtu kuzungumza kupitia kifaa hicho?. Vivyo hivyo Mungu kuuvaa mwili, ni ili kutuunganisha sisi na yeye, katika mahusiano ambayo tuliyapoteza pale Edeni. Baadaye akaingia kabisa ndani yetu, kwa Roho wake Mtakatifu, kiasi kwamba sasa tunamwabudu Mungu wetu moja kwa moja ndani ya mioyo yetu.
Kwahiyo, Mungu wetu hajagawanyika. Ni Yule Yule mmoja, wala hana nafsi tatu, bali moja. Wala hakuna mahali kwenye maandiko yanathibitisha kuwa Mungu anazo nafsi tatu. Lakini hilo si jambo la kuzozana nalo, kwa wanaoamini Mungu anazo nafsi tatu, maadamu hawaamini miungu mingi. Akimwabudu Baba, ni Yule Yule, akimwambudu Yesu ni yuleyule Mungu, akimwabudu Roho bado haabudu Mungu mwingine zaidi yake yuleyule mmoja. Hilo ni suala tu la kiufahamu ambalo halimwondolei mtu wokovu.
Hivyo ikiwa wewe ni mkristo, umemwamini Kristo kama ni mwokozi wako, na mwenzako pia kampokea kama wewe tu ulivyopokea, lakini haamini kama ni Mungu bali ni mwana wa Mungu. Lakutosha, usishindanie mambo ambayo ni ya ujuzi. Mwombee tu, Mungu ampe ufahamu kamilifu, kwasababu kujua kama utatu mtakatifu ni sahihi au sio sahihi hilo haliwezi kumtenga na Mungu wake, maadamu haubudu nje ya hao. Tukue kiufahamu, tusimpe adui nafasi ya kuleta mtengano yasiyo na maana.
Kwa maarifa ya ndani zaidi kuhusu, mafundisho ya uungu wa Mungu pitia haya masomo >>>
JE UNATAMANI KUMJUA MUNGU, NA HUJUI PA KUANZIA?
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine: