Category Archive maswali na majibu

Ulimwengu wa Roho ni nini? Na mtu anawezaje kuwa wa rohoni?

Kwa tafsiri za kiulimwengu, ulimwengu wa roho Ni ulimwengu usioonekana kwa macho ambao unasadikika viumbe kama malaika, mapepo, au roho za wafu huishi na kutenda kazi. Na kwamba vyenyewe ndio vinavyoyaathiri maisha ya ulimwengu huu unaoonekana.

Na kwamba ili mtu aweze kutembea vizuri hapa duniani hana budi kufahamu au kuwasiliana navyo, ili viwape taarifa, au kushindana navyo pale vinapokinzana nao, kwa kuzingatia misingi Fulani maalumu ya kiroho. Na wengine wanaamini kuwa ni mahali ambapo pana mifumo kama hii ya kidunia, mfano  majumba, magari, falme na mamlaka, isipokuwa tu hapaonekani kwa macho n.k. ipo mitazamo mingi.

Lakini kibiblia Mungu anataka tufahamu kwa picha ipi juu ya huu ulimwengu wa Roho?

Awali ya yote biblia inatuambia ulimwengu wa roho upo. Na hauonekani kwa macho.

Waebrania 11:3  Kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo dhahiri.

Umeona, kumbe vitu vyote tunavyoviona kwa macho vilitokea mahali ambapo hapaonekani. Na huko si pengine zaidi ya rohoni.

Lakini jinsi unavyotazamwa kiulimwengu ni tofauti na jinsi Mungu anavyotaka sisi tuutazame.

Mungu anataka tutambue kuwa ulimwengu wa Roho, ni mahali ambapo sisi tunakutana na yeye kuwasiliana, pia kumwabudu, na kumiliki, na kutawala, na kubarikiwa, kuumba, kujenga, kufunga na kufungua, na kupokea mahitaji yetu yote kutoka kwake. Kwasababu yeye ni Roho,  zaidi ya kufikiri ni mahali ambapo tunakwenda kupambana na wachawi na mapepo au kuona vibwengo na mizimu.

Alisema..

Yohana 4:23  Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu. 24  Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.

Hivyo, pale tu mtu anapoonyesha Nia ya kutaka kumjua Mungu (asiyeonekana), muumba wa mbingu na nchi. Tayari hapo anaanza hatua ya kuingia katika ulimwengu wa roho ambao Mungu aliuumba kwa ajili yake, na si kitu kingine.

Ndipo hapo sasa anapofahamu kuwa anauhitaji wokovu ili aweze kumkaribia Mungu.  Anaanza kumwamini Yesu, anapokea msamaha wa dhambi, kisha Roho Mtakatifu, na baada ya hapo anaishi kwa kulifuata Neno la Mungu aliloliamini. Sasa huyu mtu ambaye Ameokoka, anaitwa mtu wa rohoni, lakini Yule ambaye anaishi katika Neno la Mungu kwa kulitii, huyu sasa ndiye anayetembea rohoni.

Hivyo haijalishi kama alishawahi kuona malaika, au pepo, au kusikia sauti, au kuona maono. Maadamu analiamini Neno la Mungu, na nguvu zake, na kuliishi. Huyo yupo katika ulimwengu wa Roho tena katika viwango vya juu sana. Kwasababu maandiko yanasema kwa kupitia hilo (NENO), vitu vyote viliumbwa.

Kuishi katika Neno ndio kuishi rohoni. Maana yake ni kuwa  unaishi kwenye ulimwengu wa Neno.

Sasa utauliza, na haya mashetani sehemu yao ni ipi katika ulimwengu wa roho?

Haya nayo yanaingia rohoni, kwa lengo moja tu kuwapinga wale watu ambao wanatembea katika ulimwengu wa roho (yaani ulimwengu wa Neno). Hivyo yanajiundia mikakati, falme, ngome, na milki, ili tu yakuangushe wewe, uache kumwamini Mungu na Neno lake, na mpango wake wa wokovu kupitia Yesu Kristo. Uendelee kuwa mtu wa mwilini.

Ndio hapo sasa Bwana anatutahadharisha kuwa yatupasa tuwapo rohoni tusiwe hivi hivi tu. Bali tuhakikishe kweli silaha zote tumezivaa, kwasababu, mashetani haya pamoja na wajumbe wake wapo kwa lengo la kutuondoa kwenye Neno la Mungu.

Waefeso 6:10  Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.

11  Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.

12  Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya KATIKA ULIMWENGU WA ROHO.

13  Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.

14  Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

15  na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;

16  zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

17  Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;

18  kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa unapookoka, wewe tayari ni mtu wa rohoni. Ni mlango wa wewe kuonana na Mungu. Umeshaingia ulimwengu wa roho. Hivyo ili uweze kuona matunda yote ya Mungu, ni sharti uliishi kwa kuliamini Neno lake na ahadi zake, maisha yako yote yawe hivyo. Uwe mtu wa Neno. Lakini mtazamo wa kwamba siku unaona maono na malaika, au kusikia sauti ya Mungu kwenye masikio yako, au wachawi na mapepo ndio mara ya kwanza umeingia rohoni,. Si kweli. Bali Uanzapo kuliamini na kulitendea kazi Neno la Mungu.

Bwana akubariki.

Hivyo ni vifungu baadhi ambavyo utakutana na hilo neno, kwenye maandiko, vitakavyokusaidia kuelewa vema.

Waefeso 1:3  Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ULIMWENGU WA ROHO, ndani yake Kristo;

Waefeso 1:17  “Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awape ninyi roho ya hekima na ya ufunuo katika kumjua yeye;18  macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo; 19  na ubora wa ukuu wa uweza wake ndani yetu tuaminio jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa nguvu za uweza wake; 20  aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ULIMWENGU WA ROHO”

Soma pia Waefeso 2:6,  3:10

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NITAONGEZAJE NGUVU ZANGU ZA ROHONI?

CHAKULA CHA ROHONI.

ITAMBUE KARAMA YA MUNGU.

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni halali kwa mkristo kufanya biashara ya Forex?

SWALI: Je! ni sahihi kwa mkristo kufanya biashara za kifedha mitandaoni kama vile Forex, na crypto-currency mfano wa bitcons?


JIBU: Ni vema kufahamu biashara za kifedha mitandaoni kama forex ni nini?

Ni biashara ya ubadilishaji wa fedha za kigeni katika soko la dunia. Yaani ununuaji na uuzaji wa fedha za kigeni, sawa tu ile tuliyowahi kuisikia, ijulikanayo kama Bureau de change, ambayo watu wanakwenda kununua/kuuza pesa za kigeni, isipokuwa hii hufanyika mitandaoni, tofauti na bureau ambayo hufanyika kwa makarati ndani ya ofisi Fulani maalumu. Biashara hii ya forex na nyinginezo Mara nyingi hufanywa na taasisi kubwa za kifedha kama mabenki na makampuni, lakini pia hata watu binafsi.

Ni biashara ya bahati nasibu, inayofanana na michezo ya kubahatisha kitabia.. Lakini ni tofauti kabisa kimaudhui.

Biashara  hii ni ya uwekezaji, ambayo imehalalishwa ki-ulimwengu, japokuwa hatusemi kuwa kila biashara iliyohalalishwa na taifa kuwa ni halali kwa mkristo kufanya, hapana mfano zipo pombe zimehalalishwa kitaifa lakini kwa mkristo sio sawa kufanya biashara kama hizo.

Lakini, biashara hii, haihusishi katika kumdhulumu mtu, au kumlaghai mtu kiakili, apoteze kitu Fulani ili wewe ujilimbikizie fedha zake ambazo hazina mzungumko wowote wa kimaendeleo. Mfano wa hizo ni kama vile “Betting na kamari”. Kwa mkristo kushiriki katika biashara hizo za betting na kamari sio sawa. Kwa urefu wa somo lake pitia link hii >>>JE! KUBET NI DHAMBI?

Lakini Forex na nyinginezo zijulikanazo kama biashara za uwekezaji, zinahitajika sana, kwasababu kama zikikosekana, basi mzunguko wa fedha za kigeni, ungekuwa mgumu sana, na hivyo kupunguza kasi ya ukuaji uchumi, katika ulimwengu wa sasa wa teknolojia.

Hivyo tukirudi kwa mkristo, je kufanya biashara hii ni dhambi?

Kimsingi ikiwa anafanya kwa lengo la uwekezaji wake, huku akijua pia ni kwa faida ya uchumi, na hamdhulumu au kumlaghai mtu. Hafanyi kosa. Lakini akiwa na fikra za kikamari, kama vile afanyavyo kwenye betting, Kwake itakuwa ni kosa, kwasababu dhamiri yake inamshuhudia, ameigeuza kama kamari moyoni mwake.

Ndio hapo hili andiko linakuja.

Warumi 14:22  Ile imani uliyo nayo uwe nayo nafsini mwako mbele za Mungu. Heri mtu yule asiyejihukumu nafsi yake katika neno lile analolikubali.

23  Lakini aliye na shaka, kama akila, amehukumiwa kuwa ana hatia, kwa maana hakula kwa imani. NA KILA TENDO LISILOTOKA KATIKA IMANI NI DHAMBI.

Maana yake ni kuwa ukiwa na mashaka moyoni mwako kuifanya kazi hii, basi ni heri usifanye kabisa, kwasababu mashaka yoyote ni dhambi. Lakini kimsingi biashara hii sio kosa kwa mkristo, ambaye ana maarifa/elimu ya kutosha juu ya biashara za kifedha katika ulimwengu wa sasa.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Kalafati ni nini? (Ezekieli 27:9)

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

Tarshishi ni mji gani kwasasa?

NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

Rudi nyumbani

Print this post

Toba ni nini?

Swali: Toba maana yake nini?.. na je ina umuhimu gani kwetu?


Jibu: Neno “Toba” liinatokana na neno “kutubu”. Mtu anayetubu maana yake kafanya “TOBA”. Na kutubu maana yake ni “kugeuka, kutoka katika njia uliyokuwa unaiendea”.. Maana yake kama mtu ameshawishika kugeuka kutoka katika njia au mwenendo aliyokuwa anauendea kwa njia ya majuto na maombi ya kuomba msamaha kama njia hiyo ilikuwa ni kwanzo kwa mwingine, mtu huyo anakuwa ametubu, au amefanya TOBA.

Kibiblia mtu aliyegeuka na kuiacha njia ya dhambi aliyokuwa anaiende na kuomba msamaha kwa Mungu wake aliyemkosea, basi mtu huyo anakuwa amefanya TOBA, na ndio hatua ya kwanza kabisa ya Mtu kumsogelea MUNGU, hakuna njia nyingine tofauti na hiyo!.

Injili ya Yohana Mbatizaji na ya BWANA YESU (Mjumbe wa Agano jipya) ilianza na Toba.

Yohana 3:1  “Siku zile aliondokea Yohana Mbatizaji akihubiri katika nyika ya Uyahudi, na kusema,

TUBUNI; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia”.

Mathayo 4:17 “Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, TUBUNI; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia”.

Maana yake watu waageuke na kuacha maisha ya kuabudu sanamu, waache maisha ya mauaji, waache maisha ya uzinzi na uasherati, waache maisha ya ulevi na utukanaji n.k.. kwasababu Ufalme wa mbinguni hautawapokea watu wa namna hiyo.

Lakini pia si kutubu tu, bali ni pamoja na “KUZAA MATUNDA YAPATANAYO NA HIYO TOBA”.. Maana yake baada ya kugeuka na kuacha dhambi, basi mwongofu huyo anapaswa ajifunze kuishi maisha yanayoendana na toba yake hiyo, maana yake asirudie tena machafu ya nyuma yatawale maisha yake.

Luka 3:8 “Basi, toeni matunda yapatanayo na toba; wala msianze kusema mioyoni mwenu, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba katika mawe haya Mungu aweza kumwinulia Ibrahimu watoto”.

Je na wewe umetubia dhambi zako na kumkaribisha YESU maishani mwako? Kama bado basi fungua hapa ufuatilize sala hii ya TOBA na KRISTO YESU ataingia maishani mwako kwa Imani >>>KUONGOZWA SALA YA TOBA

Maran atha!

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Ni lazima mtu aongozwe sala ya toba ili awe ameokoka?

AGIZO LA TOBA LINAENDANA NA UBATIZO!.

ALIPOKUWA ANGALI MBALI, BABA YAKE ALIMWONA.

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

KAMA MTUMISHI WA MUNGU, TAFUTA MAARIFA KWA BIDII.

Rudi nyumbani

Print this post

Je watu waliookoka wanaruhusiwa kukopa?

Swali: Je wakristo tunaruhusiwa kukopa benki au kutoka kwa watu?..kama ni ndio, kwanini maandiko yaseme mtakopesha wala hamtakopa? (Kumbukumbu 15:6).


Jibu: Turejee..

Kumbukumbu 15:6 “Kwani Bwana, Mungu wako, atakubarikia, kama alivyokuahidi; nawe utakopesha mataifa mengi, lakini hutakopa; tena utayatawala mataifa mengi, usitawaliwe na wao”

Kuna kukupa kwa aina mbili; 1) KWA AJILI YA KUTATUA TATIZO/JANGA…. 2) KWAAJILI YA KUJITANUA.

    1. KUKOPA KWAJILI YA KUTATUA MATATIZO.

Kukopa kwa namna hii ni ile hali ambayo, mtu anapatwa na baa Fulani au janga, hivyo ili kujikimu au kujikidhi anakwenda kutafuta msaada kwa njia ya kukopa!.. Sasa kukopa kwa namna hii ndiko kunakozungumziwa hapo katika Kumbukumbu 15:6 (kwamba tutakopesha wala hatutakopa).

Na kwanini tutakuwa watu wa namna hiyo (ya kutokukopa)?.. ni kwasababu Mungu ni msaada wetu ambaye hataruhusu tupate matatizo hayo pasipo kuwa na sababu yoyote. Hivyo tutabaki katika usalama wake ambao utatuhifadhi dhidi ya madhara yote ya yule adui.

Hivyo kama mkristo ukiona unapitia vipindi vya mfululizo vya kukopa ili kukidhi mahitaji yako ikiwemo chakula, basi jaribu kulitazama jambo hilo kiroho Zaidi, na Bwana atakusaidia kukutoa hapo!.

       2. KUKOPA KWAAJILI YA KUJITANUA.

Hii ni aina ya pili ya UKOPAJI, ambayo biblia haijaikataza!.. Inapotokea huna janga lolote, huna baa lolote, na unaishi vizuri kwa katika neema ya Mungu, kiasi kwamba ukipatacho kinakidhi hali ya kutokuwa na haja ya kukopa!.. Lakini ukapenda kujitanua Zaidi ya hapo kifedha au kibiashara au kimiradi kama mtu wa Mungu, na ukaamua kwenda kukopa ili kuongeza labda ule mtaji ulio nao ili kutanua kazi au biashara..

Kukopa kwa namna hii “hakujakatazwa kwa mkristo” na wala hakumaanishi kuwa wewe ni maskini, kwasababu hata watu wengi walio matajiri sana pia wanakopa!!.. lengo lao la kukopa si kukidhi mahitaji (kwamba wana janga fulani au baa fulani, hivyo wasipopata huo mkopo wanaweza kudhurika) bali mara nyingi ni kwa lengo la kutanua biashara zao wazifanyazo au miradi yao.

Na Mkristo anapofikia mahali anahitaji kutanuka Zaidi anaweza kuchukua mkopo, na isiwe na tafsiri yoyote kwamba ni maskini au muhitaji, na kwamba pasipo huo hawezi kuishi.

Kanuni ya KUKOPA ni sawa na ile ya KUUZA tu!… Mtu anayeuza shamba kwaajili ya matatizo, ni tofauti na yule anayeuza shamba kama biashara!..kadhalika mtu anayekopa kwaajili ya kutatua matatizo/au janga Fulani ni tofauti na yule anayekopa kwaajili ya kujitanua.

Bwana atusaidie katika yote.

Maran atha!

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

WENGINE WANAKESHA KWAAJILI YAKO.

Rehani ni nini katika biblia?

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Kaniki ni nini katika biblia? (Yeremia 8:21).

JINSI YA KUITUMIA VYEMA NEEMA YA MUNGU ILIYO JUU YANGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Rehani ni nini katika biblia?

Rehani ni nini kibiblia?, na je sisi wakristo tunaruhusiwa kuweka kitu rehani?


Rehani ni mali iliyowekwa kama dhamana kwa mkopo uliochukuliwa, maana yake mkopo usipolipwa basi mali ile inachukuliwa ili kufidia ule mkopo.

Katika biblia (Agano la kale), Rehani iliruhusiwa lakini kwa kuiangalia hali ya mtu. Kama mtu alikuwa ni tajiri mwenye uwezo basi alipokopa alipaswa aweke rehani mali itakayosimama badala ya ule mkopo endapo atashindwa kuulipa.

Lakini kama mtu alikuwa ni maskini sana, na hana kitu isipokuwa jiwe la kusagia tu na mavazi, basi hakupaswa kutozwa rehani katika hivyo alivyo navyo, ilikuwa ni dhambi kubwa kutwaa jiwe la kusagia la maskini au mavazi yake kama Rehani.

Kumbukumbu 28: 6 “Mtu awaye yote asitwae jiwe la kusagia, la juu wala la chini, kuwa rehani; kwani hivi ni kutwaa maisha ya mtu kuwa rehani”.

Kumbukumbu 24:17 “Usipotoshe hukumu ya mgeni, wala ya yatima; wala usitwae mavazi ya mjane, yawe rehani;

18 bali kumbuka ya kuwa ulikuwa mtumwa katika Misri, Bwana, Mungu wako, akakukomboa huko; kwa hiyo nakuamuru kutenda neno hili”.

Kwa urefu kwanini si sawa kutwaa jiwe la kusagia la maskini kama rehani waweza kufungua hapa >>>Kwanini jiwe la kusagia Mungu alikataza lisiwekwe rehani? (Kumbukumbu 24:6).

Sasa swali je na sisi wakristo ni sahihi kuweka kitu rehani au kupokea rehani kutoka kwa mtu tuliyemkopesha?

Jibu: Rehani haijakatazwa katika biblia, kama umemkopesha mtu kitu cha thamani, na mtu huyo si ndugu yako katika Imani (yaani mpendwa mwenzako) au si ndugu yako katika mwili (yaani mwanafamilia) waweza kupokea Rehani, ili kumhamasisha kurejesha lile deni, (ikiwa lengo lako si kumkandamiza bali kumhamasisha na kama mtu huyo uwezo huo anao). 

Lakini kama ni maskini na kaja kukopa kwako, si vizuri kuchukua rehani. Waweza kumkopa bila rehani yoyote, ni itakuwa baraka kwako.

Lakini kama ni ndugu yako katika Imani na katika damu, si vyema kumtoza rehani,  wala riba, katika mazingira yoyote yale, awe tajiri au maskini,  waweza kumkopa ukitumai kuwa atakulipa tu pasipo kutaka dhamana.

Lakini pia kama wewe ni mkopaji, (maana yake unakopa kutoka kwa mtu/taasisi kwaajili ya shughuli fulani) si dhambi kusimamisha kitu kama rehani itakayosimama kwaajili ya mkopo wako (kama mtu huyo au taasisi hiyo inahitaji hayo yote).

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

“Humfukuza punda wake asiye baba”, nini maana ya mstari huu? (Ayubu 24:3)

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

LIONDOE JIWE.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

Rudi nyumbani

Print this post

Rahabu kwenye biblia.

Rahabu ni nani?

Jina “Rahabu” limeonekana mara kadhaa katika biblia likiwa na maana Zaidi ya moja. Maana ya kwanza ni linamwakilisha Mwanamke wa kikanaani aliyekuwa kahaba, aliyewahifadhi wapelelezi wa kiisraeli walioingia kuipeleleza Yeriko, na maana ya pili Taifa la Misri.

Kama tu vile neno “Mharabu” katika biblia linamaanisha Jamii ya watu wa Arabia, lakini pia linamaanisha “Mtu au Malaika anayeharibu Vivyo hivyo na jina Rahabu lina maana Zaidi ya moja.

     1.RAHABU (Kahaba).

Habari ya Rahabu aliywakuwa kahaba tunaipata katika kitabu cha Yoshua mlango wa 2 na wa 6. Mwanamke huyu aliwahifadhi wapelelezi wa kiisraeli walioingia Yeriko kuipeleleza nchi ile.

Yoshua 2:1 “Yoshua, mwana wa Nuni, akawatuma watu wawili kutoka Shitimu kwa siri, ili kupeleleza, akawaambia, Enendeni mkaitazame nchi hii, na Yeriko. Wakaenda wakafika nyumbani kwa kahaba mmoja jina lake aliitwa Rahabu, wakalala huko.

2 Mfalme wa Yeriko akaambiwa, kusema, Tazama, watu wawili wa wana wa Israeli wameingia humu leo usiku, ili kuipeleleza nchi.

3 Mfalme wa Yeriko akatuma watu kwa Rahabu, akasema, Watoe watu wale waliokuja kwako, walioingia ndani ya nyumba yako, maana wamekuja ili kuipeleleza nchi.

4 Yule mwanamke akawatwaa wale watu wawili, akawaficha, akasema, Naam, wale watu walikuja kwangu, lakini sikujua walikotoka”

       2.TAIFA LA MISRI.

Jina Rahabu pia katika biblia limetumika kuwakilisha Joka kubwa la baharini ambalo ufunuo wake ni Taifa la Misri.

Isaya 30:7 “Kwa maana Misri huwasaidia bure, bila faida; Kwa hiyo nimemwita, Rahabu aketiye kimya”

Isaya 51:10 “Si wewe uliyemkata-kata Rahabu? Uliyemchoma yule joka? Si wewe uliyeikausha bahari, Na maji ya vilindi vikuu; Uliyevifanya vilindi kuwa njia, Ili wapite watu waliokombolewa?”

Zaburi 87: 4 “Nitataja Rahabu na Babeli Miongoni mwao wanaonijua. Tazama Filisti, na Tiro, na Kushi; Huyu alizaliwa humo”

Soma pia Ayubu 26:12, na Zaburi 89:10..

Jambo kubwa na kuu tunaloweza kujifunza kwa RAHABU (Aliyekuwa Kahaba) ni IMANI.

Alikuwa na Imani juu ya mambo yatarajiwayo sawasawa na Waebrani 11:1. Aliziamini nguvu za MUNGU wa Israeli, hivyo akajua yatakayofuata baadaye kuwa ni anguko la Yeriko, hivyo akatafuta njia ya kujinusuru yeye na familia yake kwa kujiungamanisha na jamii ya Israeli.

Waebrania 11:31  “Kwa imani Rahabu, yule kahaba, hakuangamia pamoja na hao walioasi; kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi kwa amani”.

Yakobo 2:25 “Vivyo hivyo na Rahabu, yule kahaba naye, je! Hakuhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo, hapo alipowakaribisha wajumbe, akawatoa nje kwa njia nyingine?

26  Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa”.

Maran atha.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

RAHABU.

LAANA YA YERIKO.

Kwa maana kahaba ni shimo refu; Na malaya ni rima jembamba.

Je! Daudi hakuwa mtoto wa ndoa wa Yese? (Zab 51:5)

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

Rudi nyumbani

Print this post

Machukizo ni nini?

Machukizo au Chukizo ni nini? kama tunavyosoma katika biblia?


Machukizo linatokana na neno “chukizo” na chukizo ni kitu kinachosababisha chuki/hasira. Kwa Mungu kitu chochote kinachoipandisha ghadhabu yake kinaitwa “chukizo”.

Na vitu vifuatavyo ndivyo vilivyokuwa machukizo kwa MUNGU.

   1. Ibada ya Sanamu.

Sanamu ya aina yoyote ile ilikuwa ni machukizo kwa Mungu na hicho ndicho kitu cha kwanza kilichokuwa kinaletea wivu kwa Mungu.

Kumbukumbu 27:15 “Na alaaniwe mtu afanyaye sanamu ya kuchonga, au ya kusubu, machukizo kwa Bwana, kazi ya mikono ya fundi, akaisimamisha kwa siri. Na watu wote wajibu, waseme, Amina”.

Kumbukumbu 32:16 “Wakamtia wivu kwa miungu migeni, Wakamkasirisha kwa machukizo.

17 Walitoa sadaka kwa pepo, si Mungu, Kwa miungu wasiyoijua, Kwa miungu mipya iliyotokea siku zilizo karibu, Ambayo baba zenu hawakuiogopa”.

Soma pia Kumbukumbu 27:15, na 2Wafalme 23:24

   2. Uasherati na ulawiti.

Walawi 18: 22 “Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni machukizo”.

Soma tena Mambo ya Walawi 20:13

   3. Mavazi yasiyopasa.

Kumbukumbu 22:5 “Mwanamke asivae mavazi yampasayo mwanamume, wala mwanamume asivae mavazi ya mwanamke; kwa maana kila afanyaye mambo hayo ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako”

Mfano wa mavazi yasiyopasa, ni suruali kwa mwanamke, na nguo mfano wa magauni kwa wanaume.

   4. Sadaka yenye kasoro.

Kumbukumbu 23:18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili”.

Kumbukumbu 17:1 “Usimchinjie Bwana, Mungu wako, ng’ombe wala kondoo aliye na kilema, wala neno ovu lo lote; kwa kuwa hayo ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako”.

Na yapo machukizo mengine mengi!.

Lakini pia lipo chukizo moja KUU na KUBWA ambalo litatokea kule YERUSALEMU, ambalo ni CHUKIZO LA UHARIBIFU, linalomhusu Mpinga-kristo.

Kwa upana juu ya CHUKIZO LA UHARIBIFU, basi fungua hapa >>CHUKIZO LA UHARIBIFU

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.

VIPIMO MBALIMBALI VYA KIBIBLIA.

Kemoshi ni nani? (Yeremia 48:46)

Kwanini kuwe na kitabu Cha kumbukumbu la Torati na kwanini kiitwe vile?

Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?

Rudi nyumbani

Print this post

Kemoshi ni nani? (Yeremia 48:46)

Swali: Huyu Kemoshi alikuwa nani, na nini tunajifunza kutoka kwake?


Jibu: Turejee,

Yeremia 48:46 “Ole wako! Ee Moabu, Watu wa Kemoshi wamepotea; Maana wana wako wamechukuliwa mateka, Na binti zako wamekwenda utumwani”.

“kemoshi” hakuwa mtu bali alikuwa ni “mungu” wa watu wa Moabu. Kumbuka kila taifa lilikuwa na mungu wake; Israeli walikuwa na MUNGU wao ambaye ni YEHOVA, Muumba wa mbingu na nchi, Tiro walikuwa na mungu wao anayeitwa “baali”, Sidoni walikuwa na mungu wao anayeitwa “ashtoreti”, wana wa Amoni walikuwa na mungu wao anayeitwa “milkomu”. N.k na hawa wana wa Moabu mungu wao ndio anayekuwa anaitwa “kemoshi” ambaye kiuhalisia ni “pepo”.

Sasa utaona Mungu aliwakataza wana wa Israeli wasiabudu miungu mingine tofauti na yeye…lakini wapo waliotii na wapo waliokaidi na kuamua kuifuata miungu hiyo ya mataifa mengine na kuiabudu na kuisujudia. Na Mfalme Sulemani alikuwa miongoni mwa waliokengeuka dakika za mwisho kwa kuifuata miungu hiyo ya mataifa, ingawa baadaye alikuja kutubu.

2Wafalme 23:13 “Na mahali pa juu palipokuwapo mbele ya Yerusalemu, palipokuwa upande wa kuume wa mlima wa uharibifu, alipopajenga Sulemani, MFALME WA ISRAELI, KWA ASHTORETHI, CHUKIZO LA WASIDONI, NA KEMOSHI, CHUKIZO LA MOABU, NA MILKOMU, CHUKIZO LA WANA WA AMONI, mfalme akapanajisi”.

Hii miungu hata leo inaabudiwa katika sehemu mbalimbali ikiwemo Africa, isipokuwa katika majina mengine tofauti na hayo.

Mila nyingi za kiafrica asili yake ni miungu hii, kwamfano mungu wa wasidoni aliyeitwa Ashtorethi alikuwa ni mtu wenye kuchongwa maumbile ya mtu, na kusujudiwa, na kufanyiwa matambiko..na sasa jamii nyingi na makabila mengi (ikiwemo na wakristo) wanafanya hayo hayo wanapokutanika katika vijiji vyao, pasipo kujua kuwa ni ibada za sanamu kama zile zile tu ambazo mataifa wasiomjua Mungu walikuwa wanazifanya.

Bwana atusaidie tuepukane na ibada hizo za sanamu.

Mistari mingine inayomtaja huyo mungu “kemoshi” ni pamoja na Hesabu 21:9, Waamuzi 11:24, 1Wafalme 11:7, 1Wafalme 11:33, Yeremia 48:7, na Yeremia 48:13.

Maran atha.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Moabu ni nchi gani kwasasa?

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UNAMFAHAMU MUNGU WA KWELI?

MNGOJEE BWANA

USIJITUMAINISHE JUU YA SIRA YAKO ANGALI UPO KATIKA DHAMBI.

Rudi nyumbani

Print this post

Antiokia ni wapi kwasasa?

Antiokia ipo nchi gani kwa sasa? Na nini tunaweza kujifunza kupitia mji huo?


Jibu: Antiokia ni mji uliopo kusini mwa Taifa la UTURUKI na Kaskazini mwa Taifa la SIRIA.

Mji huu una historia kubwa sana ya kanisa, kwani ndicho kitovu cha jina “Ukristo”. Maandiko yanasema Wanafunzi (yaani watu waliomwamini YESU na kumfuata) waliitwa “wakristo” kwanza hapo Antiokia na si Yerusalemu kanisa lilipoanzia.

Matendo 11:26  “hata alipokwisha kumwona akamleta Antiokia. Ikawa kwa muda wa mwaka mzima wakakusanyika pamoja na kanisa na kuwafundisha watu wengi. NA WANAFUNZI WALIITWA WAKRISTO KWANZA HAPO ANTIOKIA.

27  Siku zizo hizo manabii walitelemka kutoka Yerusalemu hata Antiokia”.

Antiokia ni mji uliomiminiwa uliokuwa na Neema ya Ukristo kuliko miji mingi, lililojaa Mitume, manabii na waalimu.. kwani hata Mtume Paulo safari yake ya kuanza kuhubiri injili ilianzia pale.

Matendo 13:1 “Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na Sauli.

2  Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia.

3  Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao.

4  Basi watu hao, wakiisha kupelekwa na Roho Mtakatifu wakatelemkia Seleukia, na kutoka huko wakasafiri baharini hata Kipro”.

Matendo 14:26 “Na kutoka huko wakaabiri kwenda Antiokia. Huko ndiko walikoombewa neema ya Mungu kwa ile kazi waliyokwisha kuitimiza”.

Mji wa Antiokia kwasasa umejaa wa Islamu kutokana na Taifa hilo la Uturuki kuwa la kiislamu, ingawa kuna asilimia ndogo ya wakristo wanaoishi humo. Mahali ambapo uamsho mkubwa wa injili ulianzia sasa adui kapateka na kupafanya kuwa mji wa kipagani… Na miji mingine imenyanyuka yenye uamsho kuliko huo, sawasawa na Neno lile..

Marko 10:31 “Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho; na wa mwisho watakuwa wa kwanza”

Hivyo hiyo ni tahadhari hata kwetu, “Tushike tulicho nacho, mpaka mwisho adui asije akatupokonya taji yetu”.

Mji wa Antiokia mwaka 2023, Februari 6 kulitokea tetemeko kubwa sana lililoua watu elfu 55, na kuharibu makazi mengi sana.

Bwana atusaidie tuwe na mwisho mwema.

Shalom.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Yerusalemu ni nini?

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

MJI WENYE MISINGI.

Babeli ni nchi gani kwasasa?

DANIELI: Mlango wa 8

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni Mungu au Malaika?

Swali: Je biblia inajichanganya katika Zaburi 8:4-5 na Waebrania 2:6-7. Maana sehemu moja inataja ‘Mungu’, na sehemu nyingine ‘Malaika’.


Jibu: Turejee.

Zaburi 8:4 “Mtu ni kitu gani hata umkumbuke, Na binadamu hata umwangalie?

5 Umemfanya mdogo punde KULIKO MUNGU; Umemvika taji ya utukufu na heshima”.

Tusome tena Waebrania 2:6-7..

Waebrania 2:6 “Mwanadamu ni nini hata umkumbuke, Ama mwana wa binadamu, hata umwangalie?

7  Umemfanya mdogo punde kuliko MALAIKA, Umemvika taji ya utukufu na heshima, Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako”.

Katika Waebrania mwandishi ana nukuu maneno kutoka katika Zaburi, lakini ni kama ana nukuu kitu tofauti na kilichoandikwa kule, kwamaana yeye anataja Malaika na wakati mwandishi wa Zaburi alitaja Mungu.. Sasa swali biblia inajichanganya?.

Jibu ni La! Biblia haijichanganyi wala haijakosewa.. Isipokuwa fahamu zetu na pambanuzi zetu ndizo zinazojichanganya.

Sasa ili tuelewe ni vizuri kuzielewa kwanza lugha za kibiblia..

Si kila mahali panapotajwa Mungu, panamaanisha Mungu-muumba, La! Sehemu nyingine panamaanisha Ufalme wa Mungu (yaani jeshi la Mbinguni yaani Malaika na vyote vilivyopo kule)…Na sehemu mojawapo ambayo iliyotajwa Mungu ikimaanisha Jeshi la Mbinguni ni hii Zaburi 8:5 “…Umemfanya mdogo punde KULIKO MUNGU”.

Mungu inayotajwa hapo inamaanisha Ufalme wa Mungu (yaani jeshi la Malaika) na si MUNGU aliye Muumbaji, ambaye ni MMOJA.

Ni sawa na jina ISRAELI katika biblia,…kuna mahali linamaanisha mtu mmoja (ambaye ni Yakobo mwana wa Isaka, Mwanzo 35:10).. Lakini pia jina hili kuna mahali linamaanisha TAIFA (Ufalme, Kutoka 5:2).

Au “Yuda”, kuna mahali anatajwa kama Mtu (Mwana wa Yakobo), lakini pia kama Taifa.

Vivyo hivyo na Mungu, cheo hicho kinaweza kufunua “Ufalme” au nafasi ya MUNGU MWENYEWE kama Muumba.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba mwandishi wa kitabu cha Waebrania hajapishana na mwandishi wa Zaburi.

Kujua kwa mapana ni ufunuo uliopo nyuma ya andiko hili.. “Amefanyika bora kuliko Malaika” basi fungua hapa >>>AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Ielewe kwa kina Waebrania 13:5 maana yake.

MUNGU MWENYE HAKI.

UTAJI ULIOKUWA JUU YA USO WA MUSA.

JE! UNA MHESHIMU MUNGU?

Mwandishi wa kitabu cha Zaburi ni nani?

Rudi nyumbani

Print this post