Category Archive maswali na majibu

Kwanini Mungu alimkataa Sauli? (1Samweli 15:23)

Swali: Kwanini Mungu alimkataa Mfalme Sauli na tunapata funzo gani?


Jibu: Sauli alikataliwa na Mungu kwasababu ya mambo makuu mawili, 1) UASI na 2) UKAIDI WA MOYO.

Hayo ndio mambo mawili yaliyomkosesha Sauli, na biblia imeweka wazi..

1Samweli 15:22 “Naye Samweli akasema, je! Bwana huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu Sawasawa na kuitii sauti ya Bwana? Angalia, kutii ni bora kuliko dhabihu, Na kusikia kuliko mafuta ya beberu.

23 Kwani KUASI ni kama dhambi ya uchawi, Na UKAIDI ni kama ukafiri na vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la Bwana, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme”.

     1. KUASI

Kuasi maana yake ni kuondoka katika njia sahihi na kuwa adui wa hiyo njia. Ndicho kilichomtokea Sauli, Moyo wake ulianza kuondoka kwa MUNGU kidogo kidogo, na akaanza KWENDA KINYUME na sheria ya MUNGU huku akijua kabisa kuwa anachokifanya si sawa.

     2. UKAIDI

Dhambi ya pili ya Sauli ni “Ukaidi”. Mkaidi ni mtu asiyeshaurika wala hakubali kubadili mawazo yake…anachokiamini amekiamini!!,…anachokishikilia amekishikilia!..

Na Mfalme Sauli alikuwa mkaidi kwa BWANA!, Kwani utaona alipofanya kosa la kwanza la kutoa dhabihu kinyume na sheria ya Mungu katika 1Samweli 13:18 na kukemewa na Bwana, lakini utaona anakuja kurudia kosa linalofanana na hilo katika 1Samweli 15:14 pale alipoleta dhabihu haramu kutoka kwa waamaleki na kutaka kuzitoa kwa Bwana.

Alileta kondoo na Ng’ombe (walionona) kutoka Taifa la Amaleki, ili amtolee Mungu dhabihu… Kwa jicho la Haraka inaweza kuonekana kuwa alifanya jambo la busara…lakini kwa jicho la ndani SAULI alifanya machukizo makubwa sana.

Kwani kitendo cha kutwaa Ng’ombe za watu wanaoabudu miungu, ambao wanaitolea miungu yao, na tena hajui hizo ng’ombe zina historia gani..na kuzichukua hizo kisa tu zimenona kisha kumtolea Mungu, ilikuwa ni kitendo cha dharau kubwa sana (1Samweli 15:14-15)!!.. Ni sawa tu na kutwaa msharaha wa kahaba na kumletea Bwana ule alioukataza katika Kumbukumbu 23:18..

Kumbukumbu 23:18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili”.

Hivyo Sauli alikuwa mkaidi kwa  Mungu.. kwani sheria inasema Usimchinjie Bwana Ng’ombe wala kondoo aliye na kilema au MWENYE NENO OVU! (Kumbukumbu 17:1)..Na hapa Sauli analeta Ng’ombe walionona lakini waliojaa maovu ya Waamaleki kama sadaka kwa Bwana. (1Samweli 15:14-15)!!.. Huo ni UKAIDI MKUU..

Na hata leo, Mambo haya mawili (UASI na UKAIDI) yanamchukiza Mungu.

Yeremia 5:22 “Je! Hamniogopi mimi? Asema Bwana; hamtatetemeka mbele za uso wangu; mimi niliyeweka mchanga kuwa mpaka wa bahari, kwa amri ya daima, isiweze kuupita? Mawimbi yake yajapoumuka-umuka, hayawezi kushinda nguvu; yajapovuma sana, hayawezi kuupita.

23 Lakini watu hawa wana moyo wa KUASI NA UKAIDI; wameasi, wamekwenda zao.

24 Wala hawasemi mioyoni mwao, Basi, na tumche Bwana, Mungu wetu, aletaye mvua, mvua ya mwaka, na mvua ya vuli, kwa wakati wake; na kutuwekea juma za mavuno zilizoamriwa.

25 Maovu yenu yameyageuza haya, na dhambi zenu zimewazuilia mema msiyapate”.

Maran atha!

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

ROHO MBAYA KUTOKA KWA BWANA.

DHABIHU ZA ROHO NI ZIPI? (1Petro 2:5)

Dhabihu ni nini?

Gudulia ni nini? (1Samweli 26:11).

Habari ile ya Pilato kuchanganya zile damu za wayahudi na pamoja na dhabihu zao,(Luka 13) ilihusu nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Mungu alituumba?

Swali: Kwanini Mungu ametuumba? Na Sababu ya sisi kuwepo ni ipi?.. Na kwanini mmoja aumbwe hivi mwingine vile? kwa ujumla kwanini Mungu aliiumba dunia?


Jibu: Mungu katuumba sisi kwa “Kupenda kwake yeye (Mapenzi yake)”… Ili yeye afurahi kuwa pamoja nasi na sisi tufurahi kuwa pamoja naye!.

Ufunuo 4:11 “Umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na KWA SABABU YA MAPENZI YAKO VILIKUWAKO, navyo vikaumbwa”.

Kwetu kuumbwa ni “faida kubwa”…kwasababu hakuna faida yoyote ya “kutokuwepo”.. tengeneza picha haupo au hatupo!..je ni faida gani unapata au tunapata?..Lakini kama tukiwepo na tukaishi maisha ya milele na furaha basi ni heri sana!.

Na Mungu mwenyewe ametuahidia uzima wa milele kupitia mwanae YESU KRISTO.

Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”

Lakini kama mtu hatapenda kuishi, na wala hataki maisha basi njia ya kupoteza maisha ni kumkataa YESU.

1Yohana 5:12  “Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima”

swali la pili; kwanini mmoja aumbwe hivi mwingine vile?

Jibu rahisi ni kwasababu ndivyo ilivyompendeza yeye ili kututofautisha sisi kwa sisi (hajapenda wote tufanane kama sisimizi)…na hatuwezi kuhoji Zaidi!.

Warumi 9:20  “La! Sivyo, Ee binadamu; wewe u nani umjibuye Mungu? Je! Kitu kilichoumbwa kimwambie yeye aliyekiumba, Kwani kuniumba hivi?

21  Au mfinyanzi je! Hana amri juu ya udongo, kwa fungu moja la udongo kuumba chombo kimoja kiwe cha heshima, na kimoja kiwe hakina heshima?”

Lakini kwa vyovyote vile tulivyoumbwa tunapaswa tuutafute uzima wa milele na pia ni muhimu kufahamu kuwa kwa Mungu hakuna upendeleo wa mmoja Zaidi ya mwingine, wote tupo sawa mbele zake, pasipo kuangalia mwonekano, wala kimo, wala umri, wala jinsia.. Wote tunapendwa sawa, na tunapimwa sawa mbele zake .

Je unao uzima wa milele ndani yako?..Kumbuka uzima wa Milele upo kwa mmoja tu! YESU KRISTO!, Ikiwa bado hujampokea na unahitaji msaada katika kumpokea basi  waweza wasiliana nasi kwa namba zetu..

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

NUNUA MAJI YA UZIMA.

UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.

FAHAMU VIASHIRIA VYA MTU ALIYESAMEHEWA DHAMBI ZAKE.

Kwanini Yakobo alimshinda Mungu, Je! Mungu huwa anashindwa na wanadamu?

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Kuota unakabwa, mara kwa mara ni ishara ya nini?

SWALI: Mimi kila nikilala, huwa kuna kitu kinanikaba koo, nakosa pumzi, kinanikandamiza naona kama nakwenda kufa au wakati mwingine ninaganda muda mrefu siwezi kusogea. Hata nikijaribu kukemea, natumia kushindana sana, baadaye kinaniachia, Je hili ni jinamizi?. Jambo hili limekuwa likijirudia mara kwa mara. Nimejaribu kufunga na kuomba zinaweza pita tu  siku kadhaa halafu kikajirudia tena. Naomba msaada nifanye nini?


JIBU: Hayo ni mashambulizi ya adui ndotoni. Tufahamu kuwa adui hashambulii tu katika mwili, lakini wakati mwingine pia katika ndoto. Wapo watu wanaosumbuliwa na shetani husasani katika maeneo ya ndoto.

Utakuta kila anapolala, ni mfululizo tu wa ndoto za kipepo, labda anafukuzwa-fukuzwa, au anazini-zini na mapepo hayo, au yupo makaburini, anafanya mambo ya kichawi, zaidi wengine zinakuwa ni mwendelezo, yaani pale alipoishia jana, leo anaendelea nazo sehemu ya pili, kila anapolala hana raha, kwasababu anajua vitisho ni vilevile anakwenda kukutana navyo. Wengine mpaka inazidi wanasikia sauti kabisa za mapepo, zikiwasemesha, au wanaona vitu vya ajabu vikipita mbele yao, na hiyo yote hutokea pindi tu wanapopitiwa na usingizi kidogo, haijalishi mchana au usiku. Kundi lingine ndio hili ambalo wanaona kama wananaswa, na kitu Fulani pumzi haitoki, wanaishia kutaabika. N.k.

Sasa, unapokutana na mojawapo ya shida, hizo au mashambulizi hayo ndotoni. Jambo la kwanza ‘hupaswi kuogopa’ Fahamu suluhisho ni moja tu nalo ni YESU KRISTO. Lakini wengi hawajui ni kwa namna gani.

Mambo haya matatu (3), yaelewe yatakusaidia..

1) Tumia jina la Yesu.

Unapojikuta kwenye mashambulizi hayo, usiwe tu bubu. Hakikisha unalitumia jina la YESU kukemea. Kuyadhibiti hayo mapepo na kazi zao. Kwasababu mamlaka hiyo umepewa.

Mathayo 10:19  Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.

Lakini ukiona unasumbuliwa na hizo ndoto, halafu unapambana mwenyewe mwenyewe, huna silaha yoyote mkononi mwako, jiandae kukugeuza wewe  kuwa ndio kijiwe chao. Vaa silaha za vita. Jina la Yesu ndio silaha yetu kuu, kutiisha nguvu zote za Yule mwovu.

2) Jiweke vema nafsini, kabla hujalala.

Penda kuwa mwombaji kabla hujalala, usilale tu bila kumkabidhi Bwana usiku wako. Lakini pia hakikisha moyoni mwako, huna makunyanzi ambayo shetani atapata sababu ya kukushitaki. Unajua ni kwanini biblia inasema maneno haya?

Waefeso 4:26  Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka; 27  wala msimpe Ibilisi nafasi

Ni kwasababu shetani hupenda mipenyo kama hiyo, kwamfano moyoni mwako una vinyongo na wenzako, una hasira na jirani zao, mambo kama hayo, husababisha adui kukushambulia kwa njia yoyote nyakati za usiku. Hivyo ukabidhi moyo wako kwa Bwana.

3) Zidisha Imani.

Ikiwa mambo hayo mawili unayafanya, lakini bado unaona mashambulizi, yanaendelea. Basi tatizo kubwa kwako lipo kwenye IMANI.  Imani yako ni chache. Upo wakati mitume walipambana na mapepo wakashindwa kuyatoa. Baadaye wakamuuliza Bwana mbona sisi tulishindwa? Yesu akawaambia ni kwasababu ya upungufu wa imani yenu. Hata leo hii ukiona mkristo unasumbuliwa sana na vibwengo, na vipepo. Ujue pia imani yake bado haijawa imara.

Kwa namna gani?

Bado hujaamini vya kutosha nguvu iliyopo ndani ya JINA LA YESU. Na ushindi ulipoupata kupitia Kristo Yesu moyoni mwako. Unachopaswa kufanya ni kumwamini Yesu asilimia mia alimaliza yote msalabani, uwe jasiri, ondoa hofu, vipepo ni vinyago tu, havina chochote cha kukubabaisha wewe. Ukiona hiyo hali inakuja wewe kuwa  ujasiri na Imani yote, usiope kitu. Kemea. “Sema wewe pepo, mimi nimekombolewa na Yesu, huna uwezo wa kushindana na Roho Mtakatifu aliye ndani. Na sasa nisikilize, kuanzia sasa hili sio hekalu lako. Kwa mamlaka ya kifalme iliyo ndani ya jina la Yesu Kristo mwokozi wangu, nakuamuru toka na kwamwe usirudi hapa tena”.

Ukiwa na ujasiri unaotokana na imani ya Bwana unayemtumikia. Nakuambia pepo hilo litabadili uelekeo mara moja, hata likija kujaribu mara nyingine likakukuta na msimamo wako huo huo, hakuna hofu ndani yako. Ndio bye! bye! Halitakaa lirudi tena itakuwa ni historia.

Kumbuka Samsoni alipokutana na Yule Simba, yeye alimwona kama ni “mzinga” tu uliomletea asali. Hivyo akalirarua, na ndio maana baadaye akaja akakuta asali ndani yake akala akaondoka. Kwasababu alijua nguvu zilizo ndani yake, zinatuliza pepo na bahari, na milima  simbuse hichi kisimba-mbarara kinachonguruma hapa mbele yangu.

Na wewe vivyo hivyo, usiishi kinyonge-nyonge tu, unakubali kunyanyaswa nyanyaswa na hivyo vipepo ambavyo havina kitu kwako kama vile huna mtetezi hapa duniani.. KEMEA! KWA IMANI, na Ujasiri. KAZI ITAKUWA IMEISHA!. Wala usitafute maombezi.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine

IMANI “MAMA” NI IPI?

MAMBO (2) YATAKAYOKUTENGA NA IMANI SIKU HIZI ZA MWISHO.

KUOTA UPO MAKABURINI.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini tunafunga na kuomba?

Kanuni ya kufunga na kuomba inafananishwa na kanuni ya Kuku kuyaatamia mayai yake mpaka kufikia hatua ya kutotoa vifaranga.

Ili mayai yaweze kuanguliwa na vifaranga kutokea ni lazima Kuku ayaatamie mayai kwa siku 21, na ili aweze kuyaatamia kwa mafanikio, basi hana budi kujizuia kula kwa kipindi kirefu ili asipoteze joto la mayai yale. Ndio hapo utaona itampasa atoke mara chache chache kwenda kutafuta chakula kisha kuyarudia mayai yake, na atafanya hivyo kwa siku zote 21.

Maana yake kama kuku hatajiingiza katika hiyo adhabu ya kuutesa mwili wake na kujizuia na milo kwa siku 21, hawezi kupata vifaranga!.

Vile vile kuna mambo ambayo yanahitaji “Joto la kiroho” kwa siku kadhaa za MIFUNGO na MAOMBI na KUJITESA. Ili tuweze kuyapata…Vinginevyo hayatatokea kabisa haijalishi tutayatamani kiasi gani!.

Bwana YESU alisema mambo mengine hayatoki pasipo Maombi na Mifungo..

Mathayo 17:21  “[Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]”

> Ukiona umejaribu kutafuta kitu na hujakipata, ingia kwenye mfungo!

> Ikiwa umeomba na bado hujapata, ongezea na mfungo juu yake!.

> Ikiwa umetafuta na hujapata ongezea na mfungo wa maombi juu yake!.

> Ikiwa unataka Amani, Furaha, au Nguvu za kuendelea mbele, usikwepe mfungo! N.k

Ukiwa ni mtu wa kuomba pamoja na kufunga, utakuwa ni mtu wa mafanikio kiroho na kimwili. Utaangua vingi kwa wakati.. Lakini ukiwa ni mtu wa kukwepa mifungo basi utatumia nguvu nyingi sana kupata baadhi ya mambo.

Danieli 9:2 “katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danielii, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini.

3 Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka KWA MAOMBI, na dua, PAMOJA NA KUFUNGA, na kuvaa nguo za magunia na majivu.……………………….

21 naam, nilipokuwa nikinena katika kuomba, mtu yule, Gabrieli, niliyemwona katika njozi hapo kwanza, akirushwa upesi, alinigusa panapo wakati wa dhabihu ya jioni.

22 Akaniagiza, akaongea nami, akasema, Ee Danielii, nimetokea sasa, ili nikupe akili upate kufahamu.

23 Mwanzo wa maombi yako ilitolewa amri, nami nimekuja kukupasha habari; maana wewe unapendwa sana; basi itafakari habari hii, na kuyafahamu maono haya”.

Na kuna Toba nyingine zinahitaji Mfungo kabisa ili mtu aweze kufunguliwa.

Yoeli 2:12 “Lakini hata sasa, asema Bwana, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, na kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuombolea;

13 rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie Bwana, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi mabaya”.

Usikwepe mifungo!

Shalom.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?

HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.

Kuomba katika roho ni kupi? na je nifanye nini ili niweze kuomba hivyo?

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

IJUE FAIDA YA KUFUNGA PAMOJA NA WANYAMA WAKO.

Rudi nyumbani

Print this post

Ni mtu yupi aliyeishi miaka mingi kwenye biblia?

Swali: Je mtu aliyeishi miaka mingi kwenye biblia alikuwa nani?..na Mtu aliyeishi miaka mingi duniani ni nani?.


Jibu: Katika biblia mtu aliyeishi miaka mingi kuliko wote, ni METHUSELA, mwana wa Henoko aliyetwaliwa na Mungu..Biblia inasema huyu Methusela aliishi miaka 969, na hakuna mwingine aliyerekodiwa kuishi miaka mingi kuliko yeye.

Mwanzo 5:25 “Methusela akaishi miaka mia na themanini na saba, akamzaa Lameki.

26 Methusela akaishi baada ya kumzaa Lameki miaka mia saba na themanini na miwili, akazaa wana, waume na wake.

27 Siku zote za Methusela ni miaka MIA KENDA NA SITINI NA KENDA, AKAFA”.

Wengine walioishi miaka mingi katika biblia ni pamoja na;

  1. Yaredi, aliishi miaka 962, (Soma Mwanzo 5:20).
  2. Nuhu, Miaka 950 (Soma Mwanzo 9:29)
  3. Adamu, Miaka 930 (Soma Mwanzo 5:5)
  4. Sethi, Miaka 912 (Soma Mwanzo 5:8)
  5. Kenani, Miaka 910 (Soma Mwanzo 5:14)
  6. Enoshi, Miaka 905 (Soma Mwanzo 5:11)
  7. Mahalaleli, Miaka 895 (Soma Mwanzo 5:17)
  8. Lameki, Miaka 777 (Soma Mwanzo 5:31)
  9. Henoko, Miaka 365 (Soma Mwanzo 5:18-24)

Baada ya “Gharika ya Nuhu” miaka ya wanadamu ilishushwa mpaka kufikia miaka 120.. Ambapo ni wachache sana walivuka miaka hiyo, wengi waliishi chini ya hiyo..

Mwanzo 6:3 “Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini”.

Lakini kwajinsi siku zinavyozidi kwenda Miaka ya mwanadamu kuishi duniani ilizidi kushuka.. kutoka 120 mpaka 80

Zaburi 90:9 “Maana siku zetu zote zimepita katika hasira yako, Tumetowesha miaka yetu kama kite.

10 Siku za miaka yetu ni MIAKA SABINI, NA IKIWA TUNA NGUVU MIAKA THEMANINI; Na kiburi chake ni taabu na ubatili, Maana chapita upesi tukatokomea mara”.

Lakini swali kuu ni hili; kwanini miaka ya wanadamu inazidi kupungua siku baada ya siku? Je ni kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa au mabadiliko ya vyakula?

Jibu rahisi ni kwasababu ya “kuongezeka kwa Maasi”. Wala si mabadiliko ya hali ya hewa! Bali ni DHAMBI!.. Kitu cha kwanza kilichopunguza miaka ya Adamu na Hawa kutoka kuishi MILELE mpaka kufikia kuishi miaka 930 si kingine Zaidi ya DHAMBI!.. wala si kwasababu walikuwa hawazingatii mazoezi au milo kamili!..La!! bali ni dhambi!..

Na kanuni hiyo hiyo ndiyo inayopunguza maisha ya mwanadamu inaendelea mpaka sasa… Na wakati huo huo upande wa pili shetani anajaribu kuwaaminisha watu kuwa ni “Milo wanayokula ndiyo inayopunguza miaka” kwamba wapunguze ulaji wa nyama, na mafuta, na wazingatie mazoezi wataishi miaka mingi.

Mambo hayo ni mazuri, na yanafaa..lakini hayafai katika kuongeza UREFU WA MAISHA YA MTU, Kwani kuna wengi ambao wamezingatia hayo yote lakini wamewahi kuondoka duniani!.. na kuna ambao hawajazingatia hayo yote lakini wanayo miaka mingi duniani.

Kanuni ya kuishi miaka mingi na ya heri NI KUMCHA MUNGU NA KUEPUKANA NA UOVU, hiyo tu… Zishike Amri, fanya mapenzi ya Mungu, maisha yako yatakuwa marefu, hapa na katika ulimwengu ujao.

Kutoka 20: 12 “Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako”.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Je! mwanadamu wa kwanza kuumbwa ni yupi?

MAANA YA KUISHI NA MKE KWA AKILI.

NIFANYE NINI ILI NISILALE NINAPOSOMA BIBLIA.

MWONGOZO WA MAOMBI YA WAHUDUMU/ WASIMAMAO MADHABAHUNI.

Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Je Farao alikufa kwenye maji pamoja na jeshi lake au alipona?

Maandiko hayaelezi moja kwa moja kifo cha Farao. Lakini baadhi ya hivi vifungu vinatuonyesha Farao alizama na jeshi lake katika bahari ya shamu.

Zaburi 136:15

[15]Akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu;  Kwa maana fadhili zake ni za milele. 

Kuonyesha kwamba sio tu jeshi lake, lakini pia pamoja na yeye..walizamishwa baharini.

Pia vifungu hivi…

Kutoka 14:28

[28]Yale maji yakarudi yakafunikiza magari na wapanda farasi, hata jeshi lote la Farao lililoingia katika bahari nyuma yao; hakusalia hata mtu mmoja. 

Maandiko hayo, hapo mwishoni yanasema hakusalia hata “mtu mmoja”. Ikiwa na maana hata Farao mwenyewe alikwenda na maji.

Lakini pia andiko linaendelea kusema zaidi…

Kutoka 15:19

[19]Kwa maana farasi za Farao na magari yake na wapanda farasi wake waliingia ndani ya bahari, BWANA akayarudisha maji ya bahari juu yao; bali wana wa Israeli walikwenda katika nchi kavu katikati ya bahari. 

Maana yake ikiwa kama magari yake mwenyewe yalizama baharini, ni uthibitisho kuwa hata na yeye mwenyewe alikuwa juu ya gari lake. Haiwezekani yeye kama mfalme aruhusu gari lake liende halafu abakie kwa miguu.

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba Farao alikufa katika bahari ile, pamoja na jeshi lake. Na Mungu ilimpasa awahakikishie wokovu kamili watu wake. Kwa kumwangamiza aliye kichwa cha adui zao. Kwasababu tangu mwanzo, masumbufu yote yalishinikizwa na Farao, hivyo alikuwa hana budi kuondolewa na yeye. Ili Israeli waufurahie wokovu mkuu wa Mungu.

Bwana akubariki.

Kutufundisha nini?

Mungu huwa anawahakikishia wokovu kamili watu wake, hata sasa tunao ukombozi mkamilifu ndani ya Yesu Kristo kwa kumwimini yeye, adui yetu shetani na mapepo yake yanafukuzwa,mbali na sisi. Lakini yatupasa tusiwe watu wa kutokuamini kama wana wa Israeli jangwani kwa kuishi kama wapagani, kwasababu ijapokuwa Mungu aliwaahidia nchi nzuri iliyobubujika maziwa na asali, lakini hakuna hata mmoja aliyeweza kuiingia isipokuwa wawili. Vivyo hivyo na sisi hatuna budi kuishindania Imani yetu. Ili tusionekane tumekosa kuingia kwenye ufalme wa Mungu wetu.

Shalom.Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

YONA: Mlango 1

Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?

USIMWABUDU SHETANI!

Rudi nyumbani

Print this post

Rubani ni nani katika biblia? (Ezekieli 27:8)

Swali: Je zamani marubani wanaoendesha ndege walikuwepo kama tunavyosoma katika Ezekieli 27:8?


Jibu: Turejee mstari huo..

Ezekieli 27:8 “Wakaao Sidoni na Arvadi ndio waliovuta makasia yako; wana wako wenye akili, Ee Tiro, walikuwa ndani yako, ndio WALIOKUWA RUBANI ZAKE”.

“Marubani” wanaozungumziwa hapo si Marubani wanaorusha ndege kwamaana kipindi hicho ndege zilikuwa hazijavumbuliwa…bali marubani wanaozungumziwa hapo ni wana-maji (manahodha)..Kwasababu asili ya neno hilo rubani si mwana-anga, bali ni mwana-maji.

Isipokuwa kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda na kumavumbuzi mengi kuibuka, basi maneno mengi yanakuwa yanapata maana Zaidi ya moja.

Kwamfano katika biblia yametajwa magari (Mwanzo 45:21)..sasa magari ya zamani si sawa na haya sasahivi, ingawa yote ni magari… vile vile katika biblia kuna mahali pametajwa “Risasi” (Kutoka 15:10) lakini Risasi hiyo si sawa na hii inayojulikana sasa.. Vile vile pametajwa neno “Ufisadi“ (2Petro 2:7).. Lakini ufisadi huo wa biblia ni tofauti kabisa na huu unaofahamika sasa. N.k

Kwahiyo tukirudi katika Rubani, anayetajwa hapo katika Ezekieli 27:8, ni rubani mwana-maji, na si mwana-anga. Ndio maana ukiendelea mbele Zaidi katika mstari wa 29 utaona biblia imeweka sawa…

Ezekieli 27:29 “Na wote wavutao kasia, wana-maji, na RUBANI ZOTE WA BAHARINI, watashuka katika merikebu zao, na kusimama katika nchi kavu”.

Hapo anasema “Rubani zote za baharini” ikiashiria kuwa ni wana-maji na si wana-anga.

Shalom.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Risasi inayotajwa kwenye Ezekieli 27:12 ni ya namna gani?

Ufisadi una maanisha nini katika biblia?

EZEKIELI, ITABIRIE MIFUPA MIKAVU.

Mashonde ni nini? (Ezekieli 4:15).

Kalafati ni nini? (Ezekieli 27:9)

Rudi nyumbani

Print this post

Ubani ni nini?.. Na je wakristo tunaruhusiwa kuchoma ubani?

Swali: Je kuna ubani katika biblia?.. Na kazi ya Ubani ni nini?


Jibu: Ubani ni moja ya viungo vilivyotumika zamani kutengenezea manukato matakatifu yaliyoitwa “Uvumba”..

Viungo hivi (ubani) vinatokana na utomvu unaozalishwa na mmea ujulikanao kama “Boswelia” (Tazama picha juu). Mti wa Boswelia unaanza kutoa utomvu kati ya miaka 8 mpaka 10 baada ya kupandwa kwake, miti hii pia inastawi Zaidi sehemu zenye ukame.

Katika biblia “ubani” ulichanganywa pamoja na viungo vingine vitatu (3) ambavyo ni NATAFI, SHEKELETHI na KELBENA, kutengeneza Manukato matakatifu yaliyoitwa Uvumba ambapo Kuhani mkuu aliyachoma pamoja na kisha kuvukiza moshi ndani ya ile Hema kabla ya kufanya shughuli za upatanisho.

ubani katika biblia

Na uvumba wa aina hiyo, haukuruhusiwa kutengenezwa mfano wa huo kwa matumizi yoyote yale tofauti na hayo ya nyumba ya Mungu.. (maana yake haikuruhusiwa mtu kutengeneza kwa fomula hiyo na kufanya kama marashi nyumbani kwake, au ibada nyumbani kwake, ilikuwa ni kosa).

Kutoka 30:34 “Bwana akamwambia Musa, Jitwalie manukato mazuri, yaani, natafi, na shekelethi, na kelbena; viungo vya manukato vizuri pamoja na ubani safi; vitu hivyo vyote na viwe vya kipimo kimoja;

35 nawe utafanya uvumba wa vitu hivyo, manukato ya kazi ya ustadi wa mtengenazaji manukato, yatakuwa yamekolea, safi, matakatifu;

36 nawe baadhi yake utayaponda sana, na kuyaweka mbele ya ushuhuda ndani ya hema ya kukutania, hapo nitakapokutana nawe; nayo yatakuwa kwenu matakatifu sana.

37 Na uvumba utakaofanya, hamtajifanyia uvumba wenye viungo sawasawa na uvumba huo; utakuwa kwenu mtakatifu kwa ajili ya Bwana.

38 Mtu ye yote atakayefanya mfano wa huo, ili kuunusa, mtu huyo atakatiliwa mbali na watu wake”

Sasa kuelewa kwa upana Zaidi kuhusu “Uvumba” na maana yake kiroho basi fungua hapa >>KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

Lakini swali ni je! Sisi wakristo tunaruhusiwa kuchoma Ubani katika ibada au manyumbani mwetu?

Jibu ni La!.. Wakristo hatujapewa maagizo yoyote ya kuchoma ubani wala kujishughulisha nao. Manukato ya Ubani yalitumika katika agano la kale katika hema ya kukutania, na baada ya agano jipya kuanza, mambo hayo yakawa ni ya KIROHO na si ya kimwili tena, hivyo hakuna Uvumba, wala ubani wala hivyo viungo vingine unaopaswa kuhusishwa na ibada yoyote katika agano hili jipya.

Kwanini Ibada hizo za Kuvukiza uvumba na ubani hazipo tena sasa?

Ni kwasababu ile ile za kuondoka ibada za kafara za wanyama.. Hatuwezi sasa kutumia Ng’ombe au kondoo kwaajili ya utakaso wa dhambi zetu, na wakati kuna damu ya YESU, ambayo inatusafisha sasa katika ulimwengu wa roho.

Vile vile hatuwezi kuchoma ubani, na kuvukiza uvumba kama njia ya kuvuta uwepo wa Mungu na wakati tunaweza kufanya hivyo kwa njia ya sala na maombi.

Zaburi 141:2 “Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba, Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni”

Sasa Kafara za wanyama (Ng’ombe, mbuzi, kondoo na njiwa) na kuchoma ubani zimebaki kuwa ibada za miungu!… Wote wanaofanya hizo, wanavuta uwepo wa mapepo na si wa Mungu! Hivyo ni muhimu kuwa makini.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

SISI TU MANUKATO YA KRISTO.

MADHABAHU NI NINI?

Chetezo ni nini katika biblia? (Walawi 10:1)

NAFASI YAKO NI IPI KATIKA MWILI WA KRISTO?

Rudi nyumbani

Print this post

Dhamiri ni nini kibiblia?

Dhamiri au Dhamira ni nini kibiblia?


“Dhamiri” au kwa lugha nyingine “Dhamira” ni hisia ya ndani ya mtu (ya asili) inayompa kupambanua lililo jema na lililo baya, lililo zuri na lisilo zuri, linalofaa na lisilofaa. Hisia hii kila mtu anayo na haitokani na mafundisho au maelekezo, bali mtu anakuwa anazaliwa nayo.

Dhamiri ni kama mtu mwingine wa pili, aliyeko ndani yako ambaye anasahihisha hisia zako au maamuzi yako, kabla hujayafanya au baada ya kuyafanya. Kama jambo halipo sawa basi dhamiri inakushuhudia aidha kwa kukosa Amani au raha au ujasiri..

Vile vile kama jambo lipo sawa basi dhamiri yako ya ndani inakushuhudia kwamba kile ufanyacho ni chema, aidha kwa kupata furaha Fulani au Amani au ujasiri.

Kwamfano mtu anapofikiri “kuua/ kumwaga damu” au “kuiba”.. kabla ya kufanya kile kitu “dhamiri” ya ndani itamshuhudia kuwa kile kitu si sawa! Pasipo hata kuambiwa na mtu au kuhubiriwa, kuna kitu tu ndani yake kinamwambia hicho si sawa!.. Na kama ni mtu wa kujali basi haraka sana atahairisha maamuzi yake hayo.

Katika biblia neno Dhamiri limeonekana mara kadhaa.

Sehemu ya kwanza maarufu ni ule wakati ambao baadhi ya Waandishi na Mafarisayo walimletea Bwana YESU mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, kwa lengo la kutaka kumwua lakini pia kumjaribu Bwana. Lakini maandiko yanasema walipopewa ruhusa ya kumtupia mawe, wote walichomwa dhamiri zao na hakuna aliyemhukumu.

Yohana 8:3  “Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, wakamweka katikati.

4  Wakamwambia, Mwalimu, mwanamke huyu amefumaniwa alipokuwa akizini.

5  Basi katika torati, Musa alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake namna hii; nawe wasemaje?

6  Nao wakasema neno hilo wakimjaribu, ili wapate sababu ya kumshitaki. Lakini Yesu akainama, akaandika kwa kidole chake katika nchi.

7  Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe.

8  Akainama tena, akaandika kwa kidole chake katika nchi.

9  Nao waliposikia, WAKASHITAKIWA NA DHAMIRI ZAO, wakatoka mmoja mmoja, wakianzia tangu wazee hata wa mwisho wao; akabaki Yesu peke yake, na yule mwanamke amesimama katikati.

10  Yesu akajiinua asimwone mtu ila yule mwanamke, akamwambia, Mwanamke, wako wapi wale washitaki wako? Je! Hakuna aliyekuhukumu kuwa na hatia?

11  Akamwambia, Hakuna, Bwana. Yesu akamwambia, Wala mimi sikuhukumu. Enenda zako; wala usitende dhambi tena.]”

Vile vile biblia inatabiri kuwa katika siku za mwisho, watatokea watu ambao watasema uongo ijapokuwa dhamiri zao zinawashuhudia, lakini hawatazisikiliza, na watu hawa watawafundisha watu mafundisho ya mashetani.

1Timotheo 4:1  “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;

2  kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe;

3  wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli”

Mistari mingine ihusuyo dhamiri ni pamoja na Matendo 23:1, Warumi 2:15, Warumi 9:1, Warumi 13:5, na 1Timotheo 1:9.

Ikiwa ndani yako unahisi “Dhamiri yako imekufa” au “imepungua nguvu”… maana yake husikii chochote kikikuzuia au kukuhukumu unapofanya jambo lisilo sawa, basi fahamu kuwa adui kaharibu utu wako wa ndani, na hivyo unamhitaji Bwana YESU akuhuishe utu wako wa ndani kwa damu yake.

Unapompokea BWANA YESU, na kubatizwa na kujazwa na Roho wake mtakatifu, ule utu wako wa ndani uliokufa au uliofifia yeye (Bwana YESU) anauhuisha upya…na hivyo Dhamiri yako inafufuka na inakuwa safi. Hivyo fanya maamuzi leo ya kumsogelea yeye karibu na imarisha mahusiano yako naye.

Waebrania 9:14  “basi si zaidi damu yake Kristo, ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa, itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate kumwabudu Mungu aliye hai?”

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

Nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.

IKO NJIA IONEKANAYO KUWA SAWA MACHONI PA MTU.

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

Manabii walisema “Neno la Mungu likanijia” ..Maana ya hili neno ni nini?.

Rudi nyumbani

Print this post

Ulimwengu wa Roho ni nini? Na mtu anawezaje kuwa wa rohoni?

Kwa tafsiri za kiulimwengu, ulimwengu wa roho Ni ulimwengu usioonekana kwa macho ambao unasadikika viumbe kama malaika, mapepo, au roho za wafu huishi na kutenda kazi. Na kwamba vyenyewe ndio vinavyoyaathiri maisha ya ulimwengu huu unaoonekana.

Na kwamba ili mtu aweze kutembea vizuri hapa duniani hana budi kufahamu au kuwasiliana navyo, ili viwape taarifa, au kushindana navyo pale vinapokinzana nao, kwa kuzingatia misingi Fulani maalumu ya kiroho. Na wengine wanaamini kuwa ni mahali ambapo pana mifumo kama hii ya kidunia, mfano  majumba, magari, falme na mamlaka, isipokuwa tu hapaonekani kwa macho n.k. ipo mitazamo mingi.

Lakini kibiblia Mungu anataka tufahamu kwa picha ipi juu ya huu ulimwengu wa Roho?

Awali ya yote biblia inatuambia ulimwengu wa roho upo. Na hauonekani kwa macho.

Waebrania 11:3  Kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo dhahiri.

Umeona, kumbe vitu vyote tunavyoviona kwa macho vilitokea mahali ambapo hapaonekani. Na huko si pengine zaidi ya rohoni.

Lakini jinsi unavyotazamwa kiulimwengu ni tofauti na jinsi Mungu anavyotaka sisi tuutazame.

Mungu anataka tutambue kuwa ulimwengu wa Roho, ni mahali ambapo sisi tunakutana na yeye kuwasiliana, pia kumwabudu, na kumiliki, na kutawala, na kubarikiwa, kuumba, kujenga, kufunga na kufungua, na kupokea mahitaji yetu yote kutoka kwake. Kwasababu yeye ni Roho,  zaidi ya kufikiri ni mahali ambapo tunakwenda kupambana na wachawi na mapepo au kuona vibwengo na mizimu.

Alisema..

Yohana 4:23  Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu. 24  Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.

Hivyo, pale tu mtu anapoonyesha Nia ya kutaka kumjua Mungu (asiyeonekana), muumba wa mbingu na nchi. Tayari hapo anaanza hatua ya kuingia katika ulimwengu wa roho ambao Mungu aliuumba kwa ajili yake, na si kitu kingine.

Ndipo hapo sasa anapofahamu kuwa anauhitaji wokovu ili aweze kumkaribia Mungu.  Anaanza kumwamini Yesu, anapokea msamaha wa dhambi, kisha Roho Mtakatifu, na baada ya hapo anaishi kwa kulifuata Neno la Mungu aliloliamini. Sasa huyu mtu ambaye Ameokoka, anaitwa mtu wa rohoni, lakini Yule ambaye anaishi katika Neno la Mungu kwa kulitii, huyu sasa ndiye anayetembea rohoni.

Hivyo haijalishi kama alishawahi kuona malaika, au pepo, au kusikia sauti, au kuona maono. Maadamu analiamini Neno la Mungu, na nguvu zake, na kuliishi. Huyo yupo katika ulimwengu wa Roho tena katika viwango vya juu sana. Kwasababu maandiko yanasema kwa kupitia hilo (NENO), vitu vyote viliumbwa.

Kuishi katika Neno ndio kuishi rohoni. Maana yake ni kuwa  unaishi kwenye ulimwengu wa Neno.

Sasa utauliza, na haya mashetani sehemu yao ni ipi katika ulimwengu wa roho?

Haya nayo yanaingia rohoni, kwa lengo moja tu kuwapinga wale watu ambao wanatembea katika ulimwengu wa roho (yaani ulimwengu wa Neno). Hivyo yanajiundia mikakati, falme, ngome, na milki, ili tu yakuangushe wewe, uache kumwamini Mungu na Neno lake, na mpango wake wa wokovu kupitia Yesu Kristo. Uendelee kuwa mtu wa mwilini.

Ndio hapo sasa Bwana anatutahadharisha kuwa yatupasa tuwapo rohoni tusiwe hivi hivi tu. Bali tuhakikishe kweli silaha zote tumezivaa, kwasababu, mashetani haya pamoja na wajumbe wake wapo kwa lengo la kutuondoa kwenye Neno la Mungu.

Waefeso 6:10  Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.

11  Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.

12  Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya KATIKA ULIMWENGU WA ROHO.

13  Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.

14  Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

15  na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;

16  zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

17  Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;

18  kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa unapookoka, wewe tayari ni mtu wa rohoni. Ni mlango wa wewe kuonana na Mungu. Umeshaingia ulimwengu wa roho. Hivyo ili uweze kuona matunda yote ya Mungu, ni sharti uliishi kwa kuliamini Neno lake na ahadi zake, maisha yako yote yawe hivyo. Uwe mtu wa Neno. Lakini mtazamo wa kwamba siku unaona maono na malaika, au kusikia sauti ya Mungu kwenye masikio yako, au wachawi na mapepo ndio mara ya kwanza umeingia rohoni,. Si kweli. Bali Uanzapo kuliamini na kulitendea kazi Neno la Mungu.

Bwana akubariki.

Hivyo ni vifungu baadhi ambavyo utakutana na hilo neno, kwenye maandiko, vitakavyokusaidia kuelewa vema.

Waefeso 1:3  Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ULIMWENGU WA ROHO, ndani yake Kristo;

Waefeso 1:17  “Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awape ninyi roho ya hekima na ya ufunuo katika kumjua yeye;18  macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo; 19  na ubora wa ukuu wa uweza wake ndani yetu tuaminio jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa nguvu za uweza wake; 20  aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ULIMWENGU WA ROHO”

Soma pia Waefeso 2:6,  3:10

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NITAONGEZAJE NGUVU ZANGU ZA ROHONI?

CHAKULA CHA ROHONI.

ITAMBUE KARAMA YA MUNGU.

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

Rudi nyumbani

Print this post