Title Devis

Kutoka 21:10 ina maana gani?.

Jibu: Tuanze kusoma  kuanzia mstari wa 7..

Kutoka 21:7 “Mtu akimwuza binti yake awe kijakazi, hatatoka yeye kama watumwa wa kiume watokavyo. 

8 Kwamba bwana wake hakupendezewa naye, akiwa amemposa, ndipo atakubali akombolewe; hana amri yeye kumwuza aende kwa watu wageni maana amemtenda kwa udanganyifu. 

9 Kwamba amposa mwanawe, atamtendea kama desturi zipasazo binti zake. 

10 Kwamba ajitwalia mke mwingine, chakula chake huyo, na nguo zake, na ngono yake, hatampunguzia.  11 Kwamba hamfanyii mambo haya matatu, ndipo atatoka aende bure, pasipo kutolewa mali”.

Jibu: Kwa desturi za kiyahudi mtumwa wa kiume au wa kike anapaswa amtumikie bwana wake kwa muda wa miaka 6 tu, ukifika mwaka wa 7 anakuwa yupo huru kuondoka.,

Kumbukumbu 15:12 “Ikiwa nduguyo, mume wa Kiebrania, au mwanamke wa Kiebrania, akiuzwa kwako, naye amekutumikia miaka sita; basi mwaka wa saba mwache huru aondoke kwako.

 13 Nawe utakapomwacha huru aondoke kwako, usimwache aende zake mikono mitupu”

Ikiwa mtumwa wa kiume aliingia na mke wake basi utakapofika mwaka wa 7 ataondoka na mke wake huyo, (Kutoka 21:1-3) lakini kama aliingia bila mke na akaozwa mke kutoka katika familia ya bwana wake, basi utakapofika mwaka wa 7 atatoka yeye kama yeye, lakini mke na watoto watabaki kwa baba wa mke wake, hana amri ya kuondoka nao, lakini kama hataki kumwacha mke wake na watoto wake basi atamtumikie bwana wake huyo daima kwa agano la kutobolewa sikio kwa uma.

Kutoka 21:5 “Lakini huyo mtumwa akisema waziwazi, Mimi nampenda bwana wangu, na mke wangu na watoto wangu; sitaki mimi kutoka niwe huru; 

6 ndipo hapo huyo bwana wake atamleta mbele ya Mungu na kumleta mlangoni, au penye mwimo wa mlango; na bwana wake ATALITOBOA SIKIO LAKE KWA UMA; ndipo atamtumikia sikuzote”.

Hivyo ishara ya kutobolewa sikio ilikuwa ni ishara ya mtumwa kukataa uhuru wake.

Lakini kwa upande wa mtumwa wa kike (yaani kijakazi) ilikuwa ni tofauti kidogo. Kama kijakazi aliingia bila kuolewa na baadaye kijana wa bwana wake akampenda na kumwoa, kama mke wa kwanza basi famila ya kijana inapaswa kumfanya kama binti yao.

Lakini kama ameolewa kama mke wa pili, na bado ni kijakazi, na bwana wake hamtaki tena awe mke wake au suria wake, basi utakapofika mwaka wa 7, wakati wa maachilio, yeye hatamwachilia kama mabinti wengine wajakazi wanaoachiwa huru, bali kinyume chake ataachiliwa kwa gharama (maana yake atakombolewa).

Hivyo yule baba wa mtoto wa kiume aliyemwoa huyo binti, atamwuza kwa mojawapo wa ndugu aliye karibu, na si kwa mgeni (yaani mtu kutoka taifa lingine tofauti na Israeli), na asipopatikana wa kumnunua ndipo yule kijana ataendelea kuishi naye huku akimtimizia haki yote ya ndoa, ikiwemo CHAKULA, MAVAZI NA HAKI YA NDOA (Ngono).

Vitu hivyo vitatu ni sheria avitimize, si kwasababu hamtaki tena na kakosa mtu wa kumnunua basi aanze kumnyanyasa kwa kumnyima chakula chake na mavazi pamoja na haki ya ndoa ambayo imenenenwa na mtume Paulo kwa uongozo wa Roho katika 1Wakorintho 7:5. Na ikitokea kashindwa kumtimizia hayo mambo matatu basi atamwacha aende zake huru, bila gharama zozote za kumkomboa.

Kutoka 21: 10 “Kwamba ajitwalia mke mwingine, chakula chake huyo, na nguo zake, na ngono yake, hatampunguzia. 

11 Kwamba hamfanyii mambo haya matatu, ndipo atatoka aende bure, pasipo kutolewa mali”.

Mambo gani tunajifunza?

1.Kutoboa masikio si ishara nzuri.

Asili ya kutoboa sikio na kuweka hereni haikuwa nzuri, watu waliotobolewa masikio enzi za zamani ni watu waliokataa uhuru wao, hali kadhalika roho hiyo hiyo inatembea mpaka leo, kibiblia mwanamke au mwanaume hapaswi kutoboa masiko yake. Huenda ulitobolewa enzi hujaokoka, sasa umeshaokoka usiweke hereni baki katika uhalisia wako.

Wengi wanaosumbuliwa na nguvu za giza ni kutokana na vitu wanavyoviweka katika miili yao, na hawajui kuwa hivyo ndio vyanzo vya roho zinazowasumbua.

2. Ni lazima kutimiza haki ya Ndoa

Mtu aliyeoa au aliyeolewa ni sharti amtimizie mwenzie haki zote za ndoa ikiwemo upendo, na ukaribu wakati wowote unapohitajika. Maandiko yanasema mume hana amri juu ya mwili wake kadhalika mke.

1Wakorintho 7:2  “Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe.

3  Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.

4  Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.

5  Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

EPUKA MUHURI WA SHETANI

USIMPE NGUVU SHETANI.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

Tu uzao wake Ibrahimu, wala hatujawa watumwa wa mtu.

Rudi nyumbani

Print this post

Je Bwana Yesu alikuwa na nywele ndefu?

JIBU: Picha nyingi zinazochorwa kumweleza Yesu, takribani nyingi ya hizo  zinamwonyesha ni mtu mwenye nywele ndefu. Lakini Je uhalisia wake ni upi, ni kweli alikuwa na nywele ndefu au fupi?

Maandiko yanaeleza utamaduni wa wayahudi, kwa wanaume ilikuwa kuacha nywele zirefuke kama zile za mwanamke ni aibu kwa mtu huyo. Anajivunjia heshima kubwa.

1Wakorintho 11:14  “Je! Hayo maumbile yenyewe hayawafundishi ya kwamba mwanamume akiwa na nywele ndefu ni aibu kwake? 15  Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni fahari kwake. Kwa sababu amepewa zile nywele ndefu ili ziwe badala ya mavazi”

Hivyo hakukuwa na mtu aliyekuwa na nywele ndefu isipokuwa tu mtu aliyeitwa mnadhiri wa Mungu.

Lakini Je! Yesu alikuwa ni Mnadhiri ?

Kabla ya kufahamu kama Yesu alikuwa mnadhiri au la! Tufahamu kwanza mnadhiri alikuwa ni nani, na sheria ya mnadhiri ilikuwaje

Mnadhiri ni mtu aliyetengwa au aliyejitenga mwenyewe/ aliyejitoa wakfu kwa Mungu, kufuata na sababu binafsi, aidha kwa sababu ya shukrani yake ya kutendewa jambo Fulani kama vile kuponywa ugonjwa, au  kupatiwa mtoto, au kupata kitu Fulani kwa Mungu alichokuwa anamwomba. Hivyo katika agano la kale, kulikuwa na sheria ya mnadhiri. Na mnadhiri alikuwa yoyote Yule aidha mwanamke au mwanaume.

Sheria za mnadhiri ni zipi?

Kulingana na Hesabu 6:1-8

  1. Hakuruhusiwa kunywa divai, wala zabibu, wala juisi ya zabibu,  wala mbegu zake. Yaani kwa ufupi kitu chochote kilichomzao wa zabibu hakuruhusiwa kunywa
  2. Hakuruhusiwa kukata nywele zake, tangu siku hiyo aliyomwekea Mungu nadhiri mpaka atakapoitoa
  3. Hakuruhusiwa kugusa maiti. Hata kama ni ndugu yake wa karibu amekufa, baba yake au dada yake. Hakuruhisiwa  kufanya hivyo
  4. Ni lazima awe mtakatifu kwa Bwana; Maana yake ajitenge na mambo yote yaliyo najisi kipindi chote awapo katika kiapo chake.

Katika biblia, kulikuwa na makundi mawili ya wanadhiri

  1. Wanadhiri wa daima: Hawa ni waliotengwa tangu tumboni mwa mama zao: Mfano wao alikuwa  ni Samsoni, Samweli, Yohana Mbatizaji.. Hawakukatwa nywele zao, lakini pia hawakunywa divai maisha yao yote.
  2. Wanadhiri wa muda: Hawa ni aidha waliamua wenyewe katika kipindi Fulani katika maisha yao waingie kwenye viapo hivyo kwa Mungu, yaani wamtumikie yeye daima mpaka kufa kwao, au waliokuwa na nadhiri za muda, ambapo pengine baada ya miezi miwili, au mwaka mmoja wanaiondoa na kwenda kunyoa nywele zao, na kuendelea kutumia mizabibu nk. Mfano wa Hawa alikuwa ni mtume Paulo, ambaye kipindi Fulani anashuhudia naye alikuwa na nadhiri hiyo.

Matendo 18:18  “Baada ya hayo Paulo akazidi kukaa huko siku nyingi, kisha akaagana na ndugu akaabiri kwenda Shamu; na Prisila na Akila wakaenda pamoja naye, alipokwisha kunyoa kichwa chake huko Kenkrea; maana alikuwa ana nadhiri”

Sasa tukirudi kwa Bwana Yesu.

Je! Na Yeye alikuwa ni mnadhiri?

Jibu ni hapana, kwasababu Bwana alikunywa mzao wa mzabibu.

Mathayo 26:29  Lakini nawaambieni, Sitakunywa kabisa tangu sasa uzao huu wa mzabibu, hata siku ile nitakapokunywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.

Kuonyesha kuwa hapo kabla alikuwa anakunywa.

Soma pia  Mathayo 11:19, Na Yohana 2:1-12, inatupa picha alitumia mzao wa mzabibu. Halikadhalika aligusa maiti, (Marko 5:41), na zaidi ya yote Bwana hakufungwa na sheria za torati.

Hivyo kwa kifupisho ni kwamba Bwana Yesu hakuwa na nywele ndefu, yawezekana alikuwa na nywele nyingi lakini hazikuwa ndefu kama za mwanamke, mfano wa aonekanavyo kwenye baadhi ya picha zinazochorwa.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JE! NYWELE ZAKO ZINAOTA AU ZIMESIMAMA?

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

Je! sheria ilikuwaje dhaifu kwasababu ya mwili? (Warumi 8:3)

NGUVU YA MNADHIRI WA BWANA.

MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.

Nini maana ya Kucheka kwenu na kugeuzwe kuwa kuomboleza (Yakobo 4:9)

Fahamu maana ya Mithali 29:4 “Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni nyaraka zipi mtume Paulo aliziandikia gerezani?

Kati ya nyaraka kumi na tatu (13) alizoziandika mtume Paulo, Nne (4) kati ya hizo, aliziandika akiwa gerezani. Alipokuwa Rumi, ambapo maandiko yanatuonyesha  alipelekwa na kuwekwa chini ya kifungo maalumu ambacho aliruhusiwa watu kumtembelea lakini pia kuwahubiria injili akiwa katika kifungo hicho cha nyumba.

Matendo 28:16  “Tulipoingia Rumi Paulo alipewa ruhusa kukaa kwake mwenyewe pamoja na askari aliyemlinda…. 30  Akakaa muda wa miaka miwili mizima katika nyumba yake aliyokuwa ameipanga, akawakaribisha watu wote waliokuwa wakimwendea, 28.31  akihubiri habari za ufalme wa Mungu, na kuyafundisha mambo ya Bwana Yesu Kristo, kwa ujasiri mwingi, asikatazwe na mtu”.

Hivyo huko ndipo panaaminika aliandika nyaraka hizi nne. Ambazo ni

  1. Waefeso,
  2. Wafilipi,
  3. Wakolosai,
  4. Filemoni.

Sasa ni kwanini Nyaraka hizi na si nyingine?

Ni kwasababu ya habari za kufungwa kwake, alizozitaja katika nyaraka hizo; Ambazo zinaonyesha mazingira hayo alikuwa kifungoni.

Kwamfano ukisoma vifungu hivi, utaona,

Waefeso 3:1,4:1, Wafilipi 1:13, Wakolosai 4:3, Filemoni 1:10.

Je Ni nini cha kujifunza, katika vifungo vya mtume Paulo?

Yamkini Paulo alitamani awe huru kwa wakati ule ili aendelee kuihubiri injili kwa mataifa yote. Lakini hakujua mpango wa Mungu kwa nyaraka zake. Hakujua kuwa  Mungu atazihifadhi kwa mamia ya miaka, ili ziwe injili kwa vizazi vijavyo. Na matokeo yake ni kuwa nyaraka hizo zimehubiri injili kuliko hata wakati alipokuwa anazunguka mwenyewe kwenye mataifa akiwa huru.

Kwamfano mafunzo yaliyo katika kitabu cha Waefeso, yanatoa mwongozo mzuri kuanzia Viongozi wa kanisa, watakatifu hadi ngazi za kifamilia. Na jinsi gani mtakatifu anavyopaswa avae silaha za haki ili aweze kumpinga adui yake shetani (Waefeso 6:11-18)

Hii ni kuthibitisha maneno yale ya maandiko yanayosema kwamba injili  haifungiki.

2Timotheo 2:9  “Nami katika hiyo nimeteswa hata kufungwa kama mtenda mabaya; lakini neno la Mungu halifungwi

Na wewe pia ujionapo upo katika mazingira yanayokubana kuitangaza injili ya Bwana, usiwe na mawazo ya kukata tamaa, hapo hapo tazama upenyo wowote uutumie, kwasababu wewe umefungwa lakini sauti ya Mungu iliyo ndani yako, inauwezo wa kufika duniani kote, kwa vizazi vyote, hata kama umefungiwa kwenye chumba cha giza, namna gani, injili ya Kristo, inaangusha ngome popote.

Nyanyuka sasa, fanya jambo kwa Bwana, iamini nguvu ya msalaba.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je! Mtume Paulo alikuwa ni Mrumi, Myahudi au raia wa Tarso?

Je Paulo na Petro walishindania nini? (Wagalatia 2:11).

Tarishi au Matarishi ni akina nani  kwenye biblia?

Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)

SIRI YA KUFANIKIWA KWA MTUME PAULO.

Paulo alikuwa na maana gani aliposema “nimeaminiwa uwakili”

Rudi nyumbani

Print this post

Je Paulo na Petro walishindania nini? (Wagalatia 2:11).

Swali: Kwanini Petro na Paulo walishindana na pia tunajifunza nini katika kushindana kwao?.

Jibu: Tusome,

Wagalatia 2:11 “Lakini Kefa alipokuja Antiokia, nalishindana naye uso kwa uso, kwa sababu alistahili hukumu”

Kushindana kunakozungumziwa hapo si kushindana kwa maneno ya dini kule kunakozungumziwa katika 1Timotheo 6:4, 2Timitheo 2:14 na Wafilipi 2:14, kwamba tutende mambo yote pasipo mashindano wala manung’uniko.

Wala si mashindano ya Imani, yale yanayozungumziwa katika Wafilipi 1:30 na Waebrania 12:1 ambayo tunapaswa tuwe nayo, (yaani kushindana dhidi ya nguvu za giza na kuishikilia imani).

Bali neno “mashindano” kama lilivyotumiwa hapo na Paulo lilimaanisha “kukabiliana”. Maana yake Paulo alipofika Antiokia na kukutana na Petro alikabiliana naye uso kwa uso na kumwonya kuhusiana na tabia aliyoonesha ya uvuguvugu juu ya desturi za wayahudi katika kula.

Maana yake Petro alipokuwa ameketi na wayahudi aliungana nao kwa kutokula vyakula vilivyo najisi kwa hofu ya wayahudi…lakini mahali alipoketi katika chakula pamoja na watu wa mataifa, alishirikiana nao katika vyakula hivyo vilivyo najisi kwa wayahudi.

Sasa tabia hiyo haikuwa sawa, ndipo Paulo alipoona na kumkabili na kumwambia dhahiri kuwa anachokifanya sio sawa.

Wagalatia 2:11 “Lakini Kefa alipokuja Antiokia, nalishindana naye uso kwa uso, kwa sababu alistahili hukumu

12 Kwa maana kabla hawajaja watu kadha wa kadha waliotoka kwa Yakobo, alikuwa akila pamoja na watu wa Mataifa; lakini walipokuja wao, akarudi nyuma akajitenga, huku akiwaogopa waliotahiriwa.

13 Na hao Wayahudi wengine wakajigeuza pamoja naye, hata na Barnaba pia akachukuliwa na unafiki wao.

14 Walakini, nilipoona ya kuwa njia yao haiendi sawasawa na ile kweli ya Injili, nalimwambia Kefa mbele ya wote, Ikiwa wewe uliye Myahudi wafuata desturi za Mataifa, wala si za Wayahudi, kwa nini unawashurutisha Mataifa kufuata desturi za Wayahudi?”.

Tunachoweza kujifunza kwa Paulo ni ujasiri wa kusimama kuitangaza kweli pasipo kujali cheo cha mtu wala heshima ya mtu, ikiwa na maana kwamba ikiwa yeyote ananyanyuka na kwenda kinyume na kweli basi anapaswa akabiliwe na kuonywa pasipo kujali cheo chake wala umaarufu wake lakini kwa nia ya upendo.

Vile vile tunachojifunza kwa Mtume Petro ni unyenyekevu, kwani baada ya kuonywa na Paulo alitubu na huoni popote akimkasirikia Paulo zaidi sana utaona anakuja kuwaelekeza watu kwenye nyaraka za Paulo kwamba wazisome..

2 Petro 3:15 “Nanyi uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu, kama vile na ndugu yetu mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima aliyopewa

16 vile vile kama katika nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo; katika nyaraka hizo yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo; na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa, kama vile wayapotoavyo na maandiko mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe”.

Na sisi hatuna budi kuiga ujasiri wa Paulo na unyenyekevu wa Petro, huo ndio ukristo!!!..Lakini si kuona dhambi na kuzifumbia macho au kuambiwa ukweli na kukasirika badala ya kujifunza na kubadilika.

Bwana atusaidie katika hayo yote.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Yesu aliwezaje kuchukuliwa na shetani juu ya kinara cha hekalu kujaribiwa?

SWALI: Wakati shetani anamjaribu Yesu, biblia inasema alimchukua na kumpandisha kwenye kinara cha hekalu, swali ni je! Alikuwa anachukuliwaje mahali pale ni njia gani ilikuwa inatumika?


JIBU: Awali ya yote ni lazima tufahamu kuwa Bwana Yesu hakupelekwa sehemu nyingine yoyote ili kujaribiwa zaidi ya pale jangwani. Hii ikiwa na maana majaribu yake yote yalimtokea akiwa palepale jangwani.

Mathayo 4:1  “Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ili ajaribiwe na Ibilisi,2  Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa”

Sasa kama ni hivyo iweje, shetani amtoe pale na kumpeleka kwenye kinara cha Hekalu na wakati huo huo amwonyeshe milki zote za ulimwenguni? Je! Aliondokaje pale? Au alichukuliwa kimazingara?

Mathayo 4:5  “Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu 6  akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe. 7  Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako. 8  Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake, 9  akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia. 10  Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake. 11  Kisha Ibilisi akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia”

Jibu ni kwamba majaribu yale yalikuwa katika roho, na sio katika mwili, Kwa ufupi yalikuwa ni mfano wa maono. Na kikawaida maono yanapokuja ikiwa ni ya kukuonyesha tukio husika utashangaa waweza kujiona kama upo pale pale eneo lenyewe, lakini sio. Kama tu vile ndoto. Unaota upo kijijini kwenu, unashughulika, unaongea na ndugu, lakini kiuhalisia kumbe umelala palepale kitandani.

Ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana Yesu, alikuwa palepale jangwani, wala hakutoka, isipokuwa alikuwa katika roho, akayaona hayo yote, aliyoonyeshwa na shetani.

Bwana akubariki.

Lakini pia ni vizuri, kutambua maana ya majaribu yale, Kwasababu hayo pia ndio shetani anayotumia kumjaribu kila mtakatifu aliyepo duniani. Kwa upana wa habari hiyo waweza fungua link hii >>> MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

DAKIKA MOJA TU, INAKUFANYA UMWAMINI SHETANI?

Tofauti kati ya ufunuo, unabii na maono ni ipi?

NI KWA NAMNA GANI TUTASHINDA MAJARIBU?

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

UFUNUO: Mlango wa 11

DALILI TISA (9) ZA PEPO KUWEPO NDANI YA MTU.

KWA WINGI WA WASHAURI HUJA WOKOVU.

Rudi nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 9:17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu, Na mkate ulioliwa kwa siri hupendeza”

SWALI: Je! mstari huu unaelewekaje? Mithali 9:17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu, Na mkate ulioliwa kwa siri hupendeza”


JIBU: Mstari huo unamfunua mtu mwenye asili ya dhambi, jinsi vitu vilivyo kinyume na mapenzi ya Mungu vinavyoweza kupendeza mbele yake zaidi ya vile ambavyo ni sahihi kwake kuvifanya.

Kwamfano katika habari hiyo ukianzia vifungu vya juu utaona vinamweleza mwanamke kahaba, anavyowateka watu kuzini naye. Na mtu mjinga ataona ni sahihi kwenda kwake, lakini mwisho wake ni mbaya. Watu wengi wanaacha ndoa zao nakwenda kuzini nje! Kwasababu wanaona kile wanachokipata huko nje, kina uzuri kuliko kile walichokizoea ndani, wengine wanafanya uasherati, kwasababu wanaona wakingojea mpaka wakati wa ndoa, watakosa mambo mengi. Hao ndio wanaotembea katika usemi huo  “Maji yaliyoibiwa ni matamu, Na mkate ulioliwa kwa siri hupendeza”

Wengine wanaona wakitumia njia ya udanganyifu, ndio zitawafikisha katika malengo yao kwa haraka, kuliko njia za halali, hivyo hujiingiza katika wizi, na magendo.

Lakini ukizidi kusoma mstari unaofuata anasema..

.  Lakini huyo hajui ya kuwa wafu wamo humo; Ya kuwa wageni wake wamo chini kuzimuni.

Maana yake ni kuwa wote wafanyao mambo kama hayo, mwisho wao unakuwa ni kifo, na kuishia kuzimu kabisa. Dumu katika ndoa yako, kataa vya wengine, epuka mambo ya sirini. Yusufu hakukubali kuzini na mke wa boss wake. Lakini Daudi alidanganyika akazini na mke wa kijakazi wake, matokeo yake yakawa na yeye kunajisiwa wake zake vilevile, mtoto wake kufa, na ufalme wake kutikiswa na mwana wake mwenyewe aliyeitwa Absalomu, lakini zaidi sana kupoteza furaha ya wokovu kwa miaka mingi sana. Daudi alijutia makosa yake kwa muda mrefu sana.

Hivyo usipumbazwe na vivutio vyovyote vya dhambi vitakugharimu sana.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya Mithali 27:21  inaposema “mtu hujaribiwa kwa sifa zake?”

Fahamu maana ya Mithali 29:4 “Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

Jicho ni  nini (Yakobo 3:11)

NI NINI BWANA ANATAZAMIA KILA TUNAPOSHIRIKI MEZA YAKE.

KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni lazima nibadili jina baada ya kuokoka?

SWALI: Je ni lazima nibadili jina baada ya kuokoka, na kama ni hivyo ni mazingira gani yaliyo sahihi kufanya hivyo?


JIBU: Nakusalimu katika jina la Bwana Yesu Kristo.

Unapookoka, ni vema kufahamu Kristo akishakukomboa umekombolewa kweli kweli, Huwezi kukosa mbingu kwasababu ya jina lako, hata kama lina maana mbaya, kwasababu wapo watu waliokuwa na majina mabaya, mmojawapo ni Yabesi ambaye jina lake lilimaanisha “huzuni”, kwasababu alizaliwa katika kipindi cha huzuni, na wazazi wake wakamwita hivyo lakini alimlingana na Mungu na Mungu akambariki na kumtukuza sana (1Nyakati 4:9-10).Lakini walikuwepo pia watu wenye majina mazuri mmojawapo Yuda, lakini tabia zake hazikuendana na jina lake.

Hivyo ikiwa jina lako si zuri sana, na huoni shida kuendelea nalo, huwezi kumkosa Mungu kwasababu ya hilo. Lakini pia, yapo mazingira ambayo, inampasa mkristo abadili jina endapo kuna ulazima wa kufanya hivyo. Na mazingira yenyewe ni kama haya;

  1. Umefunuliwa na Mungu mwenyewe: Wakati mwingine Mungu anaamua kumwambia mtu abadili jina, sio kwasababu jina lile ni baya, hapana, bali kwasababu ya kusudi alilowekewa mbele yake kulifanya. Kwamfano Mungu alimbadili jina Abramu, akamwita Ibrahimu, na tafsiri yake ni ‘Baba wa mataifa mengi’, hivyo huduma yake ya kuwa baba wa wengi, ilimpasa iendane na jina lake. Na ndivyo  ilivyokuwa kwa Sara na baadhi ya mitume.
  2. Jina lenye tafsiri ya imani nyingine/ au miungu: Yapo majina ambayo, ukiitwa mtu atatambua wewe ni wa dini nyingine, sasa hapa ni amani tu ya Kristo itawale ndani yako, ukiona ni vema ubadili, ni sawa, ili injili au ushuhuda wako usiwe na kikwazo kwa wengine mbeleni. Lakini bado hilo halikufanyi Mungu asikutumie, utatumiwa tu. Katika biblia tunaona Danieli, aliitwa jina la kipagani na Nebukadreza, Belteshaza (Danieli 1:7), Lakini hakuling’ang’ania hili jina, badala yake aliendelea kujiita Danieli, na mbingu pia ilimtambua hivyo. Japokuwa mfalme alimuita Belteshaza kufuatana na jina la miungu yake. Kwahiyo ikiwa jina lako halikaribiani na imani, ukiona vema kubadilisha hutendi dhambi.
  3. Maisha mapya:  Wakati mwingine historia yako ya nyuma, inaacha sifa mbaya katika jina lako. Kwamfano, ulikuwa ni mtu jambazi na mwizi, na unajulikana kwenye jamii kama ‘Yule Fulani kibaka’. Sasa wengi wanapookoka, wanasukumwa kabisa kubadilisha na majina yao, wawe wapya kote kote. Mfano mmojawapo wa hawa ni mtume Paulo, alikuwa mwuaji, na alikuwa anaitwa Sauli. Lakini alipomgeukia Mungu na jina lake pia akalibadili.
  4. Jina lisilo na tafsiri nzuri: Kumbuka pia wapo wengine wanakwazwa na tafsiri za majina yao. Labda anaitwa majuto, au shida, au msiba, au masumbuko. Hivyo anapookoka anapendelea ajiite majina ya ushindi au yenye Baraka. Hivyo anayechagua hili ni vizuri zaidi.

Kwahiyo hivyo ndio vigezo vya mtu kusukumwa abadili jina. Lakini usibadili kwasababu ya shinikizo la mtu, ikiwa huoni kikwazo chochote kuitwa jina hilo lako. Kwasababu wokovu wako, hauwezi kuzuiwa na jina. Hilo ulifahamu.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINA LAKO NI LA NANI?

MAANA YA MAJINA NA TAFSIRI ZAKE.

Kula uzao wa tumbo lako maana yake nini? (Kumbukumbu 28:53)

Majina mbalimbali ya Mungu na maana zake.

Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.

KWA WINGI WA WASHAURI HUJA WOKOVU.

UPEPO WA KUSI HULETA MVUA;

Rudi nyumbani

Print this post

Fahamu maana ya Zaburi 125:3 “ Kwa maana fimbo ya udhalimu Haitakaa juu ya fungu la wenye haki.

SWALI: Nini maana ya Zaburi 125:3 “ Kwa maana fimbo ya udhalimu Haitakaa juu ya fungu la wenye haki; Wenye haki wasije wakainyosha Mikono yao kwenye upotovu”.


JIBU: Mstari huo unatuonyesha jinsi Mungu anavyowatenga watu wake na adhabu ambazo zinawahusu waovu. Kwamba kamwe fimbo ya adhabu haiwezi kuwahusu watu wa Mungu, Ndio maana ya hilo neno ‘Kwa maana fimbo ya udhalimu Haitakaa juu ya fungu la wenye haki;.. Ni mfano tu wa wana wa Israeli wakati ule walipokuwa Misri, Mungu aliwatenga na wamisri na kuwaweka kule Gosheni, na mpigo yote yalipokuja hayakuwakuta wana wa Israeli, bali wamisri tu. Hata baadaye alipotaka kuliadhibu taifa zima, bado aliwaficha  watu wake ndani ya nyumba, na Yule malaika aliyeshushwa kuwauwa watu, hakupita katika nyumba zao. Kuonyesha kuwa fimbo za makosa Mungu hana desturi ya kuzijumuisha na watu wake, isipokuwa tu wamekataa wenyewe. Ndivyo ilivyokuwa kwa Nuhu, na Lutu.

Na anafanya hivyo kwasababu gani? Ndio hapo anasema ili “Wenye haki wasije wakainyosha Mikono yao kwenye upotovu”. Kwamba anawataadharisha watu wake wasidiriki kufanya makosa kama hayo hayo ya waovu kwasababu na wenyewe adhabu inaweza kuwakuta vilevile. Na kweli ndivyo ilivyokuwa kwa wana wa Israeli baadaye, walimwacha Mungu wakaanza kuitumikia miungu, na matokeo yake Mungu akawarudisha tena utumwani, na miji yao kubomolewa.

Hivyo, ni kutuonya kuwa sisi tuliokoka, kamwe tusijichanganye na maovu kwasababu adhabu ya makosa yaweza kutupata na sisi pia, kwasababu Mungu hatazami uso wa mwanadamu, bali ulekevu wako kwake.

Shalom.

Kwa maana nyingine ya mistari mbalimbali ya biblia tembelea website yetu hii >>> www.wingulamashahidi.org.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kulabu ni nini katika biblia?(2Wafalme 19:27)

Miimo ni nini na kizingiti ni nini?

Tirshatha ni nini? (Ezra 2:63)

Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma.

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

Je Bwana Yesu aliruhusu wanafunzi wake kubeba Fimbo au hakuwaruhusu? (Marko 6:8 na Mathayo 10:10).

Tofauti kati ya zaka na sadaka ni ipi?

UTARATIBU WA KUTOA FUNGU LA 10 UPOJE?.

Rudi nyumbani

Print this post

DHABIHU ZA ROHO NI ZIPI? (1Petro 2:5)

SWALI: Dhabibu za roho ni zipi, zinazotajwa kwenye maandiko haya?

1Petro 2:5  “Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo”.

Dhabihu ni sadaka za kuteketezwa zilizokuwa zinatolewa katika agano la kale. Hizi zilikuwa na lengo la kufanya upatanisho wa makosa ya watu, kwamfano  alipochinjwa mwanakondoo, au ng’ombe au mbuzi, au njiwa (Walawi 1:3-16) na kuteketezwa kisha ule moshi wake ukapanda juu basi huo ndio unakuwa  uthibitisho wa sadaka yake kukubaliwa. Na mtu huyo makosa yake yanakuwa yamefunikwa kwa muda.

Hivyo katika agano jipya pia tunayo dhabihu yetu, ambayo kwa kupitia hiyo tunapokea upatanisho wa makosa yetu, na dhabihu yenyewe ni YESU KRISTO mwokozi wetu ambaye yeye kama mwanakondoo alichinjwa kwa ajili yetu ili sisi tupokee ondoleo la dhambi, hivyo yoyote ambaye yupo sasa ndani ya Kristo Yesu tayari ameshamtolea Mungu dhabihu ya upatanisho wake.

Lakini tunapokuwa ndani ya Kristo, hatuna budi kuonyesha kuwa tumekombolewa na yeye, kwa matendo yetu. Hivyo ni lazima tutaonyesha tabia kama za mtu anayekwenda kutoa dhabihu mbele za Bwana, na sio kama za mtu aliyejiamulia tu. Na tabia zenyewe ndio hizo zinazojulikana  kama dhabihu za roho ambazo sisi tunazitoa.

Zifuatazo ndio dhabihu za roho  zenyewe.

1) Shukrani

Zaburi 50:14 Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru; Mtimizie Aliye juu nadhiri zako.

Zaburi 50:23 Atoaye dhabihu za kushukuru, Ndiye anayenitukuza. Naye autengenezaye mwenendo wake, Nitamwonyesha wokovu wa Mungu.

Ukiwa mtu wa shukrani kwa Mungu, Ni kuonyesha kuwa umetambua kazi ya msalaba ndani yako. Na shukrani hizi ni lazima ziwe katika Sifa za kinywa chako, pamoja na matoleo kwa kile Mungu anachokubariki. Ni muhimu sana wewe kama mkristo kuwa mtu na namna hii. Wote waliokwenda kutoa sadaka za namna hii mioyo yao ilijaa shukrani kwa Mungu wao, hawakwenda hivi hivi tu.

2) Moyo uliopondeka

Zaburi 51:16 Maana hupendezwi na dhabihu, au ningeitoa, Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa.  17 Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka, Ee Mungu, hutaudharau.

Moyo uliopondeka ni moyo wa toba, wa majuto ya dhambi, ambao unakufanya utaabike moyoni mwako kwasababu ya makosa yaliyotendeka, na hivyo unakufanya uwe mnyenyekevu sana mbele za Mungu.

Mtu mwenye moyo huu, mbele za Mungu anaonekana kama amejitambua yeye ni mkosaji, na hivyo Yesu amefanyika upatanisho kwa ajili yake, tofauti na mtu ambaye mambo yote kwake ni sawa, hata baada ya kuona kosa bado anaukaza moyo wake, kujifanya kama hana hatia yoyote mbele za Mungu. Yatupasa wakati wote tuwe watu wa kujinyenyekeza mbele za Mungu. Watu wa kutaka rehema zake.

3) Kuitoa miili yetu;

Warumi 12:1  “Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana. 2  Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.

Unapoutunza mwili wako mbali na mambo ya kidunia, kisha ukaufanya utumike kwa ajili ya kazi ya Mungu, hapo ni sawa na unamtolea Mungu dhabihu yenye kupendeza, yaani unaenda mbele za Mungu na badiliko, unasema msalaba mbele, udunia nyuma. Lakini ukiwa unavaa ovyo ovyo, unazini, unatumia mikorogo, unajichora mwili wako, unakunywa pombe, unavuta sigara, unatoa mimba, hapo hufanyi ibada yoyote mbele za Mungu. Kwasababu lazima ufahamu kuwa miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu (1Wakorintho 3:16).

Hivyo, wewe ambaye umeokoka, zangatia mambo hayo matatu, SHUKRANI, MOYO ULIOPONDEKA, NA KUUTOA MWILI WAKO. Wokovu wako utakuwa na maana sana mbele za Mungu.

Bwana akubariki.

Je! Umeshaokoka?. Kama bado wasubiri nini? Unatambua kuwa haya ni majira ya siku za mwisho, na Kristo amekaribia kurudi?.  Dalili zote zimeshatimia, Embu tubu sasa mgeukie Kristo akuokoe uwe upande salama. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi waweza fungua hapa kwa ajili ya mwongozo was ala hiyo.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Dhabihu ni nini?

KUTII NI BORA KULIKO DHABIHU.

Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?

Swali: Kurushwa upesi kunakozungumziwa katika Danieli 9:21 ndio kupi?

Mnanaa, Bizari na Jira ni viungo gani? (Mathayo 23:23)

Sadaka ya Moyo ipoje? (Walawi 22:21).

Kwanini samaki wasio na mapezi na magamba hawakuruhusiwa kuliwa?

Rudi nyumbani

Print this post

NIFANYE NINI ILI NISILALE NINAPOSOMA BIBLIA.

Mara nyingi tunapojikuta tumelala tunaposoma biblia, huwa moja kwa moja tunamsingizia shetani. Lakini ukweli ni kwamba shetani anahusika kwa sehemu ndogo, sehemu kubwa ni hali zetu za kimwili ndio zinakuwa adui katika jambo hili. Mazingira ambayo ni mashambulizi kutoka kwa adui mfano wake yanakuwa ni  kama haya; pengine mtu akianza tu kusoma biblia anasikia maumivu makali kwenye kichwa, au mwili, lakini akiacha tu kusoma hali yake inarudia kama kawaida, au anaona giza au vitu kama mianga mianga kwenye macho na hivyo inamfanya asiweze kuisoma biblia, au kila anapotaka kusoma anapoteza hapo hapo kumbukumbu zote kwamba alikuwa anasoma biblia, na hatimaye anajikuta yupo usingizini, au anafanya mambo mengine kabisa, hiyo ndio mfano ya mashambulizi.. Na inahitaji kuombewa, au kushindana na hiyo roho hadi ikutoke.

Lakini ukijiona unaposoma biblia usingizi mzito umekukamata, unasinzia sinzia, unapiga piga miayo, huyo sio adui huo ni mwili wako, usiopenda mambo ya rohoni. Hivyo ni lazima uushinde huo.

Wagalatia 5:17  “Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka”

Hivyo hizi ni njia ambazo zitakusaidia usilale pale unaposoma biblia.

1) Omba kabla ya kusoma biblia

Usipende kufungua biblia kama kitabu cha riwaya, unasoma tu utakavyo. Kumbuka yale ni maneno ya ROHO, na hivyo inahitaji umkaribishe Roho akusaidie. Hivyo  usiwe mvivu wa kuomba, pata dakika, kadhaa za kufanya hivyo. Ni jambo ambalo nimejifunza sana, wakati nasoma biblia bila kuomba, na pale ninapoomba kisha nikaisoma, kuna tofauti kubwa sana ya kiuelewa na kiutulivu. Maombi pia yanasaidia kama kuna mashambulizi yoyote, basi yanatowekea hapo.

2) Pata muda wa kupumzika.

Ikiwa umechoka sana, si lazima usome biblia muda huo huo. Pendelea kuruhusu mwili wako upumzike vizuri, kwamfano umetoka kazini, umeshughulika kutwa nzima, ni rahisi sana kukabwa na usingizi muda huo huo usomapo biblia peke yako. Hivyo tumia busara, wahi kulala, kisha amka usiku. Ukilala hata masaa 3, mwili unapokea taarifa kuwa huyu mtu tayari alishapumzika. Hivyo ukiamka ukajimwagia maji, ukaketi utajiona unafuu mkubwa, na utapata kitu kikubwa kuliko kulizimisha mwili wakati umechoka.

3) Usipende kusomea biblia kitandani:

Tafuta meza ukae, mwili wako uwe kama mtu aliye darasani, sio kama aliye hospitalini mgonjwa unasubiriwa kuhudumiwa. Kaa kwenye meza, kisha ndio usome biblia yako

Luka 12:35  Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka

4) Kuwa na daftari na kalamu.

Kusoma kwa kuandika na kwa sauti, huwa kuna matokeo makubwa kuliko, kutumia tu macho yako. Hivyo andiko vifungu unavyovisoma, na ufunuo unaopata, itakuongezea umakini katika usomaji wako, na hivyo Roho Mtakatifu atapata nafasi ya kukufindisha kwa urahisi zaidi.

5) Soma na wengine.

Ukiona huwezi kujiwekea ustaarabu wa kuzingatia ratiba yako ya usomaji, pendelea kujifunza na wengine. Kaa na familia yako, au ndugu zako, au rafiki yako katika Bwana jiwekeeni ratiba ya usomaji wa biblia pamoja, kisha mnachambua kile mlichojifunza, kwa namna hiyo itakusaidia sana kuielewa ..

Mathayo 18:20  “Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao”

 6) Soma kwa vituo.

Kusoma biblia sio mashindano kwamba ni lazima uimalize yote kwa siku moja, soma vifungu kadhaa, kisha tumia muda mwingi, kuvitafakari hivyo vilimaanisha nini. Roho Mtakatifu anapenda kutufundisha taratibu sana, hataki tuvuke madarasa ya juu wakati ya chini bado hatujayamaliza. Hivyo zingatia kusoma kwa muktadha wa kuelemishwa na Roho Mtakatifu, sio kumaliza silabasi. Kusoma vifungu vitano kwa dakika mbili, kisha ukavifakari kwa masaa 2, ni bora kuliko kusoma vifungu elfu kwa saa2, halafu hakuna tafakari yoyote.

7) Mifungo

Mfungo ni jambo zuri ambalo huupa mwili wepesi, kwasababu mwili unapotaabika kwa kunyimwa haja zake kwa kawaida roho yako huwa inakuja juu. Hivyo ukiwa katika kipindi cha mfungo, utaona wepesi Fulani wa kuisoma biblia kwa masafa marefu kidogo, kuliko kipindi kingine. Fungu mara kwa mara, au ukiwa unatamani wiki hiyo kuitumia vizuri usiku katika kusoma Biblia, basi hakikisha wiki hiyo yote unafunga, utajiona mwepesi sana hususani wakati wa usiku unapotulia.

8) Mshirikishe mkufunzi wako

Si kila jambo utaweza kulitatua tu peke yako mengine, utahitaji msaada, hivyo hakikisha maendeleo yako ya kiusomaji, kiongozi wako anayafahamu, hatua zako unamshirikisha mchungaji wako, itakusaidia sana, kupata ushauri au maombi , au ushuhuda kwa yale ambayo pengine usingeyafahamu uwapo peke yako. Na hiyo itakupa hamasa zaidi na shauku ya kusoma.

Bwana akubariki.

Hakikisha unasoma BIBLIA kila siku.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Jinsi ya kuandaa Somo la kufundisha

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Tirshatha ni nini? (Ezra 2:63)

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

UFUNUO NI NINI, NA NITAPOKEAJE UFUNUO KUTOKA KWA MUNGU?

Biblia inamaana gani inaposema tutoapo unabii tutoe kwa kadiri ya imani?

Rudi nyumbani

Print this post