Biblia inasema katika kitabu cha Mwanzo.
Mwanzo 4:1 Adamu akamjua Hawa mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Kaini, akasema, Nimepata mtoto mwanamume kwa Bwana.
2 Akaongeza akamzaa ndugu yake, Habili. Habili alikuwa mchunga kondoo, na Kaini alikuwa mkulima ardhi”
Mtoto mwingine aliyezaliwa na Adamu na Hawa alikuwa ni Sethi.
Mwanzo 5:1 “Hiki ndicho kitabu cha vizazi vya Adamu. Siku ile Mungu alipoumba mtu, kwa sura ya Mungu alimfanya;
2 mwanamume na mwanamke aliwaumba, akawabariki akawaita jina lao Adamu, siku ile walipoumbwa.
3 Adamu akaishi miaka mia na thelathini, akazaa mwana kwa sura yake, kwa mfano wake, akamwita jina lake Sethi”
Lakini pia Biblia haiishi hapo, inasema Adamu alizaa watoto wengine wakiume na wakike baada ya kumzaa Sethi.
Mwanzo 5:4 “Siku za Adamu baada ya kumzaa Sethi zilikuwa miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake”.
Na hao watoto wakike waliozaliwa ndio waliokuja kuwa wake wa hao watoto wengine wa kiume wa Adamu.
Hivyo Biblia haitoi idadi kamili ya watoto wa Adamu, pengine walikuwa 5 au 10 au 20 au 30, hatujui lakini zaidi ya Sethi, walikuwapo pia watoto wengine wa Adamu ambao habari zao hazikuandikwa katika biblia.
ADAMU ALIISHI MIAKA MINGAPI?
Jibu tunalipata katika Mstari wa 5
Mwanzo 5:5 “Siku zote za Adamu alizoishi ni miaka mia kenda na thelathini, naye akafa.”
Kwahiyo siku zote za Adamu ilikuwa ni miaka 980, akafa
Mada Nyinginezo:
JE! ADAMU ALIWASALIANA NA MUNGU KWA LUGHA IPI PALE BUSTANINI?
MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA NI UPI?.
Biblia haijataja kuna idadi gani ya Malaika walioko mbinguni…Lakini tukisoma Biblia tunaweza kujua au kupata picha kuwa kuna idadi kubwa kiasi gani ya Malaika walioko mbinguni..
Kama maandiko yanasema katika…
Mathayo 18:10 “Angalieni msidharau mmojawapo wadogo hawa; kwa maana nawaambia ya kwamba malaika wao mbinguni siku zote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni”.
Mstari huo unatuonesha kwamba kila mtu aliyezaliwa mara ya Pili, anaye malaika wake akimlinda, akipeleka habari zake njema mbele za Mungu, na akimsaidia katika Kuishikilia Imani.
Sasa hebu fikiri endapo watu wote wangempa Kristo maisha yao, ina maana kila mtu angekuwa na angalau malaika mmoja.
Hivyo mbingu haiwezi kuwa na watenda kazi wachache wa kutuhudumia sisi kiasi kwamba kuna wanadamu wanaweza kukosa Malaika wa kuwahudumia. (Malaika wa Mungu watakaa mbali nasi endapo tu tutakuwa tunajitia unajisi na dhambi), lakini sio kwamba kuna idadi ndogo….Kwahiyo kama wanadamu duniani leo tupo Bilioni 7, basi Malaika ni wengi zaidi ya hiyo idadi…Hivyo unaweza kuona ni jeshi kubwa kiasi gani lililopo mbinguni.
Na Biblia pia inaonesha wazi kwamba inawezekana mtu kutembea na Malaika zaidi ya mmoja.. Soma (2Wafalme 6:16-17).
Mada Nyinginezo:
KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.
KUNDI LA MALAIKA WALETAO MABAYA.
JE! MBINGUNI KUNA MALAIKA WA KIKE?. NA JE! TUKIFIKA MBINGUNI TUTAFANANA WOTE?
Jibu la swali hili tunalipata katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati 34,
Kumbukumbu 34:1 “Musa akapanda kutoka uwanda wa Moabu mpaka mlima Nebo, hata kilele cha Pisga kukabili Yeriko. Bwana akamwonyesha nchi yote ya Gileadi hata Dani;
2 na Naftali yote, na nchi ya Efraimu na Manase, na nchi yote ya Yuda, mpaka bahari ya magharibi;
3 na Negebu, na uwanja wa bonde la Yeriko, mji wa mitende, hata mpaka Soari.
4 Bwana akamwambia, Hii ndiyo nchi niliyowaapia Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, nikisema, Nitawapa wazao wako. Basi nimekuonyesha kwa macho yako, lakini hutavuka huko.
5 Basi Musa, mtumishi wa Bwana, akafa huko, katika nchi ya Moabu, kwa neno la Bwana.
6 Akamzika bondeni, katika nchi ya Moabu, kukabili Beth-peori; lakini hapana mtu ajuaye kaburi lake hata leo”.
Moabu kwa sasa ni maeneo ya Magharibi mwa Nchi ya JORDANI, Na Mungu alificha kaburi la Musa, ili watu wasipagueze mahali pale mahali pa ibada, na kufanya ibada za sanamu na kufanya machukizo mbele za Mungu.
Mada Nyinginezo:
JE! MWANADAMU WA KWANZA KUUMBWA NI YUPI MZUNGU MWAFRIKA AU MCHINA?
NI RAHISI KWA NGAMIA KUPENYA KATIKA TUNDU LA SINDANO, JE! NI SINDANO IPI HIYO INAYOZUNGUMZIWA?
Ndoto yoyote ni lazima idondoke kati ya mojawapo ya haya makundi matatu: Kundi la kwanza ni ndoto zinazotoka na Mungu, kundi la pili ni ndoto zinazotoka kwa shetani na kundi la tatu ni ndoto zinazotoka kwa mtu mwenyewe..
Hivyo ukiweza kuelewa jinsi ya kuzigawanya ndoto zako katika makundi haya basi itakuwa ni rahisi kwako kuitafsiri ndoto hiyo bila hata kutegemea msaada kutoka kwa watumishi yeyote wa Mungu.
Kwa mfano, ndoto nyingi tunazoota sisi wanadamu, zinaangukia katika kundi hilo la tatu, yaani ndoto zinazotoka ndani yetu wenyewe, hizi zinakuja kutokana na shughuli mtu anazozifanya mara kwa mara au mazingira yanayomzunguka, kwamfano kama mtu kazi yake ni kuranda mbao siku zote, moja kwa moja atajikuta ndoto anazoota mara kwa mara zinahusiana na urandaji mbao, au labda mazingira yanayomzunguka ni ya wafugaji, hivyo kujiona na yeye anachunga ng’ombe si jambo la kushangaza..
Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi;…..”
Au utakuta mwingine kabla hajalala labda alikuwa anasikia njaa au kiu, hivyo ni jambo la kawaida katika ndoto za usiku huo kujiona anakula hashibi, au anakunywa maji halafu kiu hakikati, au mwingine mkojo umembana sana usiku , sasa kuota unakoja kitandani hakuepukiki.
Isaya 29:8 “Tena itakuwa kama mtu mwenye njaa aotapo, kumbe, anakula; lakini aamkapo, nafsi yake haina kitu; na kama mtu mwenye kiu aotapo, kumbe, anakunywa; lakini aamkapo, kumbe, anazimia, na nafsi yake inatamani;…….”
Hivyo ikiwa hujahamu bado jinsi ya kujua ndoto yako inaangukia kati ya kundi lipi, fungua kwanza somo hili ulipitie kisha tuendelee..>> NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI?
Sasa ndoto hii kwa sehemu kubwa inaangukia katika lile kundi la tatu yaani ndoto zinazotokana na sisi wenyewe, kwamfano, ikiwa umefiwa na mtu wako wa karibu labda tuseme baba au mama au kaka, au mjomba au hata rafiki, hawa ni watu ambao muda mwingi umekuwa nao katika maisha yako, wengine wamekulelea kwa muda mrefu wengine hata miaka 10 au 20 au zaidi, hivyo wanapokufa ghafla, si jambo la kushangaza sana kuendelea kuwaona katika ndoto zako mara kwa mara, kuota unaongea na mtu aliyefariki, na hiyo haitokani na Mungu au shetani..bali ni wewe mwenyewe..inaweza kuendelea hivyo hivyo pengine hata hadi wakati wa kufa kwako, hivyo ukiona ndoto za namna hiyo usiogope, ipuuzie tu,
Lakini pale inapotokea ndoto ya namna hiyo inaambata na vitisho, au unapewa maagizo Fulani, au unalishwa vitu Fulani usivyovijua, au unapelekwa mahali usipopafahamu basi fahamu kuwa hiyo ndoto ni ya kutoka kwa adui, Hivyo hapo unapaswa unapoamka kemea hiyo roho kwa jina la YESU KRISTO, mara moja na mambo hayo yataisha.
Lakini pia wakati mwingine ndoto hizi zinatoka kwa Mungu mwenyewe.. Mungu anakuonyesha kuwa kuna maisha baada ya kifo, na kwamba kama mpendwa wako alikuwa ni mtakatifu basi hajafa bali yupo hai sehemu nyingine anaishi..Lakini sio kwamba Yule unayemwona unaongea naye kwenye ndoto ndiye mwenyewe hapana, ile ni lugha tu ya ndoto Mungu anaitumia kukufikishia ujumbe unaoweza kuuelewa juu ya ndugu zako waliolala katika Kristo.
1Wathesalonike 4:13 “Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.
14 Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.”
Vilevile kama upo nje ya Kristo, bado Mungu anakuonyesha kuwa kifo cha hapa duniani sio safari ya mwisho, kwamba ipo ng’ambo nawe siku moja utafika huko utakutana na wale waliokutangulia, Sasa kama utaendelea kuwa mwovu basi sehemu yako itakuwa na wale waovu Jehanum, lakini kama utataka kuwa mtakatifu basi pia sehemu yako nawe itakuwa na wale watakatifu walio paradiso wakingojea ufufuo siku ile ya Unyakuo waende na Bwana Yesu mawinguni..
Hivyo kama bado upo nje ya Kristo unasubiri nini?. Tubu leo mgeukie yeye..Ndoto za namna hiyo ni kuonyesha kuwa Mungu anataka umalize safari yako salama hapa duniani, ufikie mwisho mzuri…Siku ile ukutane na watakatifu wengine kwa pamoja mkaishi milele na Mungu.
Ubarikiwe sana..
Jiunge na Group letu ya whatsapp, la masomo ya kila siku kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Mada Nyinginezo:
TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?
NI JAMBO GANI LINALOMTAMANISHA SANA BWANA TUMWOMBE BILA KUKATA TAMAA?
NITAIFAHAMU VIPI KARAMA YANGU?
Shalom, mtu Mungu nakukaribisha tujikumbushe tena Neno la Mungu kwa yale ambayo tulishawahi kujifunza huko nyuma lakini leo tutaangalia kwa upana zaidi, na naamini utaongeza kitu kipya katika ukristo wako(Wafilipi 3:1), Biblia inaufananisha utendaji kazi wa Mungu na vitu viwili cha kwanza ni Moto na cha pili ni Upepo. Bwana Yesu alipomuhubiria Nikodemo habari za kuzaliwa mara ya pili kwa Roho Mtakatifu, Nekodemu alistaajabia sana na kusema inawezekanikaje mtu kuzaliwa mara ya pili lakini Bwana Yesu akamwambia maneno haya:
Yohana 3:7 “Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili.
8 Upepo huvuma upendako, na sauti yake waisikia, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda; kadhalika na hali yake kila mtu aliyezaliwa kwa Roho’’.
Sasa kama ukiichunguza tabia ya Upepo, wataalamu wanasema kuwa Upepo hauna sauti yoyote, Na Kama ni hivyo basi kile tunachokisikia ni nini?, wakati mwingine upepo ukivuma utasikia kama mluzi Fulani hivi unajipiga, au maporomoko Fulani au vitu Fulani vidogo vidogo vinadondoka,n.k. jibu ni kuwa ule upepo wakati unapovuma unakutana na vitu vingi katika safari yake, sasa pale unaposuguana na vitu hivyo inasababisha kutokee sauti fulani, au ule upepo ukisukuma vile vitu inasababisha vile vitu kugongana vyenyewe kwa vyenyewe na kusababisha sauti pia, kwamfano upepo ukikutana na mti, ukipita katikati yake unasababisha matawi kugongana gongana yenyewe kwa yenyewe na hapo hapo kelele ya matawi inasikika, vivyo hivyo unapokutana na vipande vidogo vidogo vya mawe na uchafu, vinapogongana gongana ndio sauti hapo hapo inatokea na hapo ndipo mtu anapogundua kuwa eneo hilo lina upepo mkali au mdogo..Lakini kama upepo ukiwa unapita tu hewani na haukutani na kizuizi au kipingamizi chochote basi kamwe hutakaa usikie au ujue kama kuna upepo wowote unapita hapo iwe ni mkali au mdogo..Eneo hilo litakuwa kimya na tulivu kuliko hata kitu chochote ulichowahi kukisikia.
Na ndiyo maana Bwana Yesu alimfananisha Roho Mtakatifu kama Upepo uvumao ndani ya mtu aliyezaliwa mara ya pili..Hawezi kumwona Roho jinsi anavyokuja juu yake wala huwezi kumchunguza jinsi anavyofanya kazi ndani yake, lakini kitu kitakachomtambulisha kama anavuma juu yake au la ni ile sauti anayoitoa yeye mwenyewe.. Na sauti hiyo ni tabia yako na mwenendo wako baada ya kuzaliwa mara ya pili.
Kwa jinsi utakavyoanza kuonyesha tabia nyingine ghafla, ulimwengu utajiuliza mtu huyu ni kitu gani kimemkumba kinachomfanya aishi hivi, au onyeshe tabia za namna hii, lakini kwamwe hawatapata jibu wala kukiona..Kwasababu Roho Mtakatifu ni kama upepo hautambuliki na ulimwengu, wala ulimwengu hauwezi kumtambua.
Yohana 14:16 “Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele;
17 ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu”.
1Wakorintho 2:14 “Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni.”
Hivyo ikiwa wewe umezaliwa mara ya pili kweli kweli kuna mambo utagundua Mungu ameyageuza ndani yako, utashangaa ile kiu ya kutamani mambo maovu imekufa ndani yako, utashangaa unapenda kila wakati kujifunza Neno la Mungu jambo ambalo hapo kwanza ulikuwa huwezi, utajikuta hupendi tena kukaa karibu na watu wabaya au waovu au zile kampani mbaya ulizokuwa nazo hapo nyuma, watu wataanza kukushangaa umekuwaje au umeingiliwa na nini. Sasa ukishaona hivyo ujue ni upepo wa Roho unavuma ndani yako, usihangaike kuwathibitishia kuwa huyo ni Mungu hawatakuelewa, ni rahisi wao kukutafsiri umedanganywa na walokole, au umepotoshwa…usiwasikilize hapo fahamu kuwa ni Roho Mtakatifu anatenda kazi ndani yako, wewe itii tu, usiichunguze sana, kwasababu hata wewe ukiichunguza ni ngumu kujua chanzo chake ni wapi na mwisho wake ni wapi, lakini wewe itii hiyo na uifuate maadamu inakupeleka kumpenda na kumtafuta Mungu zaidi..
Na ndio maana tunasema, mtu hawezi kudai amezaliwa mara ya pili na huku nyuma bado maisha yake kwa nje yapo vile vile hayajabadilika, ni wazi kuwa Roho Mtakatifu bado hajaanza kupita juu ya huyo mtu.
Tabia nyingine ya Roho Mtakafu ni Moto, Kama vile biblia inavyosema..
Mathayo 3:11 “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto”.
Moto nao vile vile unatabia kama ya upepo huwa hautoi sauti, sauti yake huwa inakuja kutoka katika vile vitu unavyovichoma, kichaka kikiwashwa moto hapo nje, hata kama upo ndani utajua tu nje kuna moto unawaka kwa jinsi kile kichaka kitakavyokuwa kinatoa kelele zake. Na sauti inaweza kuwa kubwa kulingana na kitu kinachochomwa, kwamfano kama inachomwa nazi pale inapopasuka utasikia inapasuka inatoa mlimo mkubwa kama bomu tofauti na karatasi.. lakini pia tabia nyingine ya moto ni kwamba sio vitu vyote inaviteketeza, kwa mfano ukiweka karatasi na dhahabu pamoja, halafu vyote ukavichoma, mwisho wa siku utagundua lile karatasi limeteketea lote lakini ile dhahabu imezidi kuwa mpya ziadi.
Na ndivyo ilivyo Roho Mtakatifu anavyombatiza mtu kwa moto, ni ngumu kumwona, lakini kazi zake utaziona, vile vitu vyote dhaifu ambavyo ni uovu vilivyokuwa ndani yake ataviteketeza mara moja, lakini vile vitu imara na vizuri ndani ya mtu ni kama dhahabu hivyo vinazidi kuwa imara.
Vile vile Roho Makatifu hawabatizi tu watu wema, bali pia na watu waovu, biblia inasema hivyo katika Mathayo 5:45 “kwamba huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki”. lakini kwao inakuwa ni kinyume chake, badala ya kuimarishwa wanateketezwa, biblia inasema..
Waebrania 12:29 “maana Mungu wetu ni moto ulao.”
Na kibaya zaidi moto huu unapowateketeza hawajui kama unawateketeza kwasababu huwa hautoi sauti, utajua tu unawateketeza kwa kule kulalamika kwao na kutaabika kwao kiroho huo ndio uthibisho kuwa moto wa Mungu unapita juu yao kuwala. Na moto huo huo hauishii hapa duniani ndio ule unaoendelea mpaka kwenye ziwa la moto.
Usiulaumu moto na kuuona kuwa ni mbaya kwasababu ulikuchomea nyumba yako, ukasahau kuwa moto huo huo ndio unaokupikia chakula kila siku, ndio unaotumia kuchome taka, ndio unaokupa nishati kila siku, unaweza kukufanya kutazama tv,radio, unaoweza kukufanya kuchaji simu yako na kusoma ujumbe huu, unaweza kupigia pasi nguo zako ukawa mtanashaji, unaweza kusafiri kwa kutumia chombo chako cha moto n.k..
Vivyo hivyo usilaumu kwanini watu waovu watateketezwa kwa moto, kikubwa tu ni kujiepusha na ghadhabu na hasira ya Mungu kwasababu ni kawaida ukienda kinyume na sheria ya moto, utakuunguza hata wewe mwenyewe, moto unahitaji umakini wa hali ya juu kuendana nao. Kadhalika Moto wa Roho Mtakatifu unahitaji umakini wa hali ya juu kuendana nao vinginevyo ni rahisi kujikuta tunajipeleka wenyewe jehanamu ya moto.
Ukiyajua hayo na huku bado upo nje ya Kristo hakuna sababu ya wewe kuendelea kuwa hivyo,..Kwanini usimruhusu Roho Mtakatifu ayaumbe maisha yako upya?, kwanini usiruhusu moto wake na upepo wake uanzee kupita juu yako na kukuimarisha na kukupeleka kule atakapo? Jambo hilo la heri na neema ni bure kabisa.. Tubu hapo ulipo kwa kumaanisha kabisa kuacha dhambi zako zote, kumbuka kutubu ni kugeuka, na kuacha kile ulichokuwa unakifanya ambacho sio sahihi.. Na Bwana akishaona umedhamiria kabisa kwa moyo wako wote wote kugeuka basi yeye ataanza jukumu la moja kwa moja kukugeuza, na bila kuchelewa nenda katafute mahali ubatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi kwa jina la Yesu Kristo kukamilisha wokovu wako, naye atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu, kulingana na Matendo 2:38..Na kuanzia huo wakati na kuendelea utakuwa umehesabiwa kuwa mojawapo wa kondoo wa Bwana unayestahili uzima wa milele, na kuhesabiwa haki bure kwa Imani yako.
Bwana akubariki sana. Tafadhali “Share” Ujumbe huu na kwa wengine. Na Bwana atakubariki.
Mada Nyinginezo:
Jina la Bwana libarikiwe. Karibu tujifunze Biblia..
Hatari kubwa iliyopo katika siku hizi za mwisho ni Kunyanyuka kwa jopo kubwa la Manabii wa Uongo…Sasa biblia inapotaja uwepo wa manabii wa uongo, haimaanishi tu manabii bali hata waalimu, wainjilisti, mitume, wachungaji, maaskofu, mashemasi(2Petro 2:1) n.k…Yaani kwa ufupi kila karama ina waongo wake…Sasa watumishi wote hao wa uongo biblia imewapa jina moja la ujumla ambalo ndio hilo MANABII WA UONGO.
Kwahiyo akitokea mwalimu anafundisha uongo huyo ni Nabii wa Uongo wa siku za mwisho, kadhalika akitokea mchungaji anafundisha uongo huyo pia ni Nabii wa uongo kulingana na Biblia.
Sasa katika siku hizi za mwisho wameongezeka sana…Ni sababu gani imewafanya waongezeke kwa kasi kiasi hicho?? NI KWASABABU HIZI NI SIKU ZA MWISHO! HILO TU!..Hawajataka wenyewe kunyanyuka kwa nguvu zao hapana! bali kuna nguvu ya siku hizi za mwisho ndio zinazowanyanyua.
Umewahi kujiuliza kwanini karibia na mstari wa mwisho wa riadha, ndio watu wanongeza spidi? Na kelele za mashabiki ndio zinaongezeka?.. umewahi kujiuliza kwanini karibia na goli ndio nguvu za wachezaji zinajiongeza mara mbili?, na kelele zinakuwa nyingi uwanjani?..tofauti na mpira ukiwa katikati ya uwanja?…..ni kwasababu mpira unakaribia mwisho wa uwanja ambapo ni golini.…. karibia na mwisho kuna kitu kinawasukuma wamalizie kwa nguvu ili wafunge goli, na pia kama ukichunguza dakika 5 kabla mpira au mchezo wowote kuisha ndio kelele zinaongezeka uwanjani na wachezaji wanacheza kwa nguvu zaidi? Ni kwasababu mwisho umekaribia….kadhalika mstari wa siku za mwisho tunaoukaribia ndio unaoharakisha mambo kama tunavyoona….kama sio huo mstari wa siku za mwisho tunaoukaribia kuwa karibu na sisi, nguvu hii ya kuwasukuma watu kuzimu isingekuwa kubwa kiasi hiki…Kwasababu muda ungekuwa bado sana
Ndugu ipo nguvu kubwa ya upotevu katika hizi siku za mwisho, imeachiwa, ili imalizie kwa nguvu kuwapeleka watu upotevuni…Na pia kuna nguvu ya Mungu imeachiliwa kwa watu wa Mungu itakayowapeleka kwa nguvu uzimani. Hizo nguvu mbili ndio zinazotenda kazi sasa.
Wale wasiompenda Mungu, hii nguvu ya upotevu inawavaa…Sasa inawavaa vipi?
Mtu alikuwa anapenda ulevi, na haipendi injili inayomwambia aache pombe na hataki kutubu…Mungu anamletewa mhubiri wa uongo atakayemuhakikishia kwa maandiko kitu anachokifanya ni sawa mbele za Mungu..atahubiriwa pombe ni sawa kulingana na maandiko, na atatoka amesafishika akiamini anachokifanya ni sahihi, kumbe kasafishiwa Zaidi njia yake ya kwenda upotevuni…
Na ndio hivyo hivyo siku za mwisho Mungu atawaruhusu manabii wengi wa uongo, watimize kusudi lake, ingawa manabii hao watakuwa wametumwa na shetani.
2Timotheo 3:13 “Lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika”.
2Wathesalonike 2:10 “na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.
11 Kwa hiyo Mungu awaletea nguvu ya upotevu, wauamini uongo;
12 ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu”.
1 Wathesalonike 5: 3 “Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”.
Unaambiwa leo, uvaaji mbaya ni dhambi, uvaaji wa mawigi, vimini, na suruali kwa wanawake ni dhambi lakini hutaki kusikia..Utaletewa mhubiri, aliyesomea chuo cha Biblia kabisa, atakuhakikishia kwa maandiko kwamba vimini, mawingi, suruali, uwanja, lipstiki, sio dhambi…atakupa na vifungu vya biblia na atakuombea kabisa na utapokea hata uponyaji…
Na wewe utatoka umeamini kuwa upo sawa, kumbe tayari umepokea nguvu itakayokufanya kuendelea kufanya dhambi pasipo kuwa na mashaka yoyote..kwasababu mashaka ndio yanayomfanya mtu awe hapo katikati… na mtu aliye katikati anaonekana bado hajakomaa vizuri, hivyo ni ngumu kujua kama ni ngano au gugu…ili kujua ni ngano au gugu ndio inaachiliwa nguvu hiyo juu yake..ikishaachiliwa hiyo nguvu ndio inamfanya achague upande mmoja pasipo kuwa na mashaka…Hivyo ndivyo magugu na ngano vinavyotengwa.
Kadhalika Leo hii unaambiwa Ulimwengu na fahari zake unapita, na usijiwekee hazina duniani mahali ambapo nondo na kutu vinaharibu, unaambiwa usiupende ulimwengu, kwasababu kuwa Rafiki wa ulimwengu ni kuwa adui wa Mungu (Yakobo 4:4) na tena hivi karibuni dunia itafikia mwisho, kila kitu kitaharibiwa na waovu wote wataondolewa na hivyo kila kitu kitakuwa ni kazi bure.…lakini wewe hutaki kusikia hilo, unataka kulazimisha kuwa mambo ya ulimwengu huu yamekubaliwa na Mungu, na kwamba dunia haitaharibiwa kutaendelea kuwa na amani hivi hivi siku zote…. hata wakati mwingine unakejeli na kudharau wanaoukataa ulimwengu na kumtafuta Mungu…
Nataka nikuambie ukweli, ukweli kabisa wa dhati!! nguvu ya upotevu itaachiliwa juu yako…au pengine imeshaanza kuachiliwa ni hujui tu…Mungu atakuletea mhubiri, tena inawezekana akawa ni mhubiri maarufu sana, huyo atakuambia kwa kutumia maandiko matakatifu kuwa bado sana dunia iishe! Atakupa na historia ndefu yenye kutumia akili nyingi, atakuaminisha kuwa bado kuna miaka mingi ya hii dunia kuendelea kuwepo, hakutatokea vita wala matetemeko…hivyo usiogope! Endelea na shughuli zako, Mungu atafuata baadaye.
Ndugu yangu! Hao ni manabii wa Uongo, walioruhusiwa watokee siku hizi za mwisho..wanafanya kazi yao ya kupotosha ulimwengu mzima na wakishamaliza wataenda kuhukumiwa..
Tubu leo, ipende kweli na Itii Injili pasipo kuipunguza, Epuka kusikiliza injili hizi za manabii wa uongo, wanaokufariji katika dhambi, lakini hawakuambii ukweli kuwa, ukiendelea na Maisha ya dhambi unayoishi utakwenda kuzimu. Manabii hao ni asili yao ni kuzimu, na siku ile watu wengi sana watashangaa kuwaona Jehanamu.
Bwana anasema..
Yeremia 23: 15 “Basi Bwana wa majeshi asema hivi, katika habari ya manabii, Tazama, nitawalisha pakanga, nitawanywesha maji ya uchungu; kwa kuwa kutoka kwa manabii hao wa Yerusalemu kukufuru kumeingia katika nchi yote.
16 Bwana wa majeshi asema hivi, Msisikilize maneno ya manabii wakiwatabiria; huwafundisha ubatili; hunena maono ya mioyo yao wenyewe; hayakutoka katika kinywa cha Bwana.
17 Daima huwaambia wao wanaonidharau, Bwana amesema, MTAKUWA NA AMANI; nao humwambia kila mtu aendaye kwa ukaidi wa moyo wake, Hamtapatwa na ubaya wo wote.
18 Maana, ni nani aliyesimama katika baraza la Bwana, hata akalifahamu neno lake na kulisikia? Ni nani aliyelitia moyoni neno langu, na kulisikia?
19 Tazama, tufani ya Bwana, yaani, ghadhabu yake, imetokea; ni dhoruba ya kisulisuli; itapasuka, na kuwaangukia waovu vichwani.
20 Hasira ya Bwana haitarudi, hata atakapokwisha kuyatimiza makusudi ya moyo wake; katika siku za mwisho mtalifahamu neno hili kabisa.
21 Mimi sikuwatuma manabii hao, lakini walikwenda mbio; sikusema nao, lakini walitabiri”.
Kama hujayakabidhi Maisha yako kwa Kristo, unangoja nini?..Kama hujabatizwa ubatizo sahihi wa kuzama mwili wote na kwa Jina la Yesu ni nini unasubiri?..Mlango wa Neema upo wazi sasa, ila hautakuwa hivyo siku zote.
Bwana akubariki.
Mada Nyinginezo:
TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.
JE! MUNGU ATAIANGAMIZA DUNIA TENA BAADA YA GHARIKA YA NUHU?
MANENO HAYA YANA MAANA GANI? “..KWA SABABU HAMTOI ROHO KWA KIPIMO. (YOHANA3:34)”
Wagalatia 6:7 “Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.
8 Maana yeye apandaye kwa mwili wake, katika mwili wake atavuna uharibifu; bali yeye apandaye kwa Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele”.
Hapo inasema “chochote” ikiwa na maana kuwa hata vitu visivyokuwa na maana vikipandwa vinaleta majibu.
Na chochote kinachopandwa huwa kinapandwa kama mbegu…na kinapovunwa kinavunwa kama tunda…embe linapandwa kama mbegu, lakini linavunwa kama tunda..
Mtu akipanda mbegu ya dhambi yoyote moyoni mwake leo, akaipalilia hiyo tabia moyoni mwake, baada ya muda fulani, atavuna matunda ya dhambi hiyo..Na matunda yake ni ya aina mbili…MAUTI YA MWILI, na MAUTI YA ROHO…
Mauti ya Mwili, inaweza kuja kutokana aidha Ugonjwa unaotokana dhambi hiyo au janga fulani kwamfano dhambi ya uasherati mauti yake ya kimwili inaweza kutokana na ugonjwa fulani kama HIV, GONOREA au kaswende au inaweza kuja kupitia chanel nyingine yeyote tofauti na hiyo..Wengi hawajui kuwa vifo vingi vya ghafla vinatokana na matokeo ya dhambi…hususani dhambi ya uasherati…
Aina ya pili ya tunda la dhambi ni Mauti ya kiroho. Hii ni ile hali mtu anakufa katika kuisikia Injili na kuiamini, upo usemi unaosema “sikio la kufa halisikii dawa” kadhalika, roho iliyokufa haiwezi kuisikia Injili tena, na mwisho wake ni ziwa la moto.
Jiepushe na uasherati kwasababu apandacho mtu ndicho atakachovuna, jiepushe na ushirikina, ulevi, anasa, ushoga, ulawiti, usagaji, utazamaji wa picha na video chafu, ulaji rushwa n.k kwasababu mambo hayo yote matunda yake ni kifo.
Kwasababu biblia inasema Mshahara wa dhambi ni Mauti.
Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.
Bwana akubariki.
Mada Nyinginezo:
JE! KUNENA KWA LUGHA MPYA KUKOJE?
JE! KUOMBA KWA BIDII KAMA ELIYA NI KUOMBA KWA NAMNA GANI?
JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOKUJA JUU YA MTU.
USITAFUTE FAIDA YAKO MWENYEWE BALI YA WENGINE.
Ufunuo 12:17 “Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari.”
Timotheo 1:4 “Nami natamani sana kukuona, nikiyakumbuka machozi yako, ili nijae furaha;
5 nikiikumbuka imani uliyo nayo isiyo na unafiki, ambayo ilikaa kwanza katika bibi yako Loisi, na katika mama yako Eunike, nami nasadiki wewe nawe unayo.”
2Yohana 1:4 “Nalifurahi mno kwa kuwa nimewaona baadhi ya watoto wako wanaenenda katika kweli, kama vile tulivyopokea amri kwa Baba.
5 Na sasa mama, nakuomba, si kwamba nakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo, kwamba tupendane.
Mithali 14:1 “Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.”
Mada Nyinginezo:
NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA.
MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.
JIFANYIE RAFIKI KWA MALI YA UDHALIMU.
Awali ya yote ili upate ufasaha wa ndoto yako, na kuepuka kudanganywa na kila aina ya tafsiri mtu yeyote anayoweza kukuletea, awali ya yote unapaswa ufahamu ndoto yako inaangukia katika kundi lipi,
Yapo makundi makuu matatu (3) ya ndoto:
Ndoto zinazoangukia katika kundi hili la tatu ndizo zinazootwa na watu mara kwa mara kila siku na kama mtu asipoweza kuzitambua atajikuta anahangaika nazo, na huku hazina maana yoyote ya kumsaidia, kwasababu ni ndoto zinazokuja kutokana na shughuli anazozifanya kila siku au mazingira yanayomzungumka muda wote hivyo hizi huwa hazibebi ujumbe wowote..
Kwahiyo ni rahisi ubongo wake kuchukua yale matukio anayoyofanya kila siku na kuyatengenezea matukio yanayofanana na hayo katika ndoto usiku na kuota, ukijiona unaota hivyo basi puuzia ndoto hizo
Ikiwa unahitaji kufahamu kwa undani juu ya makundi haya basi pitia somo hili kwanza >>>> NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI? kisha ndio tuendelee,
Kwamfano ndoto za namna hii za kujiona unapewa pesa, utakuta mtu mmoja kazi yake kila siku ipo kwenye pesa kama vile benki au mfanyabiashara ambaye muda wote analipa na kulipwa pesa, hivyo kuota anapewa pesa linaweza kuwa ni jambo la kawaida kwake kutokea katika ndoto zake za kila siku, kwasababu ubongo ulishajiengenezea ulimwengu kama huo.
Lakini ikitokea umeota ndoto katika mazingira, ambayo hayaendani na wewe kupewa pesa, au umeota ndoto hiyo na ukaiona si ndoto ya kawaida, au ulikuwa katika maombi ya kumwomba Mungu kitu Fulani na imekuja na uzito Fulani hivi, au amani Fulani hivi, basi fahamu kuwa upo ujumbe unapaswa kujifunza ndani yake.
Kumbuka kibiblia Fedha inawakilisha chombo cha kuletea jawabu.
Mhubiri 10:19 “Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko, Na divai huyafurahisha maisha; Na fedha huleta jawabu la mambo yote”.
Hivyo Mungu kukuonyesha katika ndoto, unapewa fedha, ni ishara kuwa amekupa jawabu la ombi lako, na hivi karibuni utapata haja yako..Ila tilia maanani kitu kimoja hapo biblia inaposema, fedha huleta jawabu la mambo yote haimaanishi kuwa inaleta majibu mpaka kwenye mambo ya rohoni hapana, fedha haiwezi kuleta uzima ndani ya mtu wala haiwezi kununua upendo..lakini kama ukichunguza hapo utaona mistari hiyo inalenga mambo ya ki mwilini..kama vile shughuli za karamu, nguo, chakula, nyumba, gari, biashara, ambavyo hivi kimsingi vinahudumiwa na fedha..
Pia tazama..
Lakini tukirudi kwenye hiyo ndoto ya pesa vile vile usitegemee sana kuwa atatumia njia hiyo hiyo uliyoiona kwamba kweli kuna mtu atakujana kukupa wewe fedha hapana, inaweza ikawa hivyo au isiwe hivyo, anaweza kutumia njia pengine ya kuirutubisha kazi yako unayoifanya sasa hivi ,au ukapata kibali mahali Fulani pengine kazini kwako, ambapo boss wako atakulipa vizuri zaidi kuliko sasa hivi, au ukapata mkopo wa kufanya biashara yako n.k.Na kama ukijiangalia ndio utagundua vitu vya aina hiyo hiyo ndio ulivyokuwa unamwomba Mungu…
Hivyo ametumia ndoto ya fedha kama ishara ya kukuonyesha kuwa maombi yako ameyasikia,..Lakini usitazamie kuwa mtu anayemwomba Mungu mambo ya rohoni kama vile uzima wa milele, au Roho Mtakatifu, au nguvu za Mungu, ataonyeshwa ndoto za namna hiyo kama jibu la maombi yake hapana.. Mungu atamwonyesha Maono ya rohoni, pengine usishangae mtu kama huyo kuona maono ya mbinguni, au kukutana na malaika ndotoni, au kuisikia sauti ya Mungu ikisema naye, au kuota anahubiri au anafundishwa biblia n.k…
Hivyo kaa katika matarajio huku ukiulinda ukamilifu na utakatifu katika kazi yako, ndipo Mungu ataitimiza ahadi yake juu yako. Lakini kama wewe upo nje ya Kristo ukaota ndoto kama hiyo, fahamu kuwa ni ishara mbaya nayo ni ishara ya upotevu zaidi..utakwenda kufanikiwa lakini ni ili upotee..
Mithali 1:32 “Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua, Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza”.
Usisibirie udanganyifu wa mali au mafanikio vikuangamize..Mrudi Muumba wako mapema, tubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha, ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi kwa Jina la YESU KRISTO ikiwa bado hukubatizwa kisha anza kumwangalia Mungu ili yeye atembee pamoja na wewe katika njia zako zote.
Ubarikiwe.
Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Mithali 1:32
kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza.
Mada Nyinginezo:
TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?
Mahusiano yoyote yale yanayohusisha watu wa jinsia moja ni machukizo mbele za Mungu..Biblia imeweka wazi katika kitabu cha Mambo ya Walawi
Walawi 18:22 “Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni machukizo”.
Walawi 20:13 “Tena mtu mume akilala pamoja na mtu mume, kama alalavyo na mtu mke, wote wawili wamefanya machukizo; hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao”
Kutokana na anguko Ipo asili ya dhambi ambayo mtu anazaliwa nayo… inafanya kazi ndani ya mtu, tangu akiwa tumboni mwa mama yake…hiyo inamfanya mtu anazaliwa na tabia fulani fulani ambazo asili yake ni dhambi…mfano wa tabia hizo ni kama hasira zisizokuwa na sababu, kiburi, uchungu usiokuwa na sababu, ukorofu, utundu, tamaa ya uasherati n.k vyote hivyo vinatokana na ile asili ya dhambi mtu anayozaliwa nayo.
Lakini pamoja na hayo, kuna dhambi ambazo Mungu aliziweka mbali sana na mwanadamu kuzifikia, na hizo hazimo miongoni mwa dhambi za asili..Ni dhambi lakini mtu anakuwa hazaliwi nazo… Mtu mwenyewe kwa mapenzi yake anapokuwa mtu mzima anaweza kuzipachika ndani yake na kuzifanya.
Na moja ya dhambi hizo ni dhambi za kumtamani mtu wa jinsia moja na ya kwako. Hiyo tamaa ya namna hiyo haipo ndani ya mtu tangu anazaliwa. Mwanamke kumtamani mwanamke mwenzake au mwanamume kumtamani mwanamume mwenzake…
Dhambi hii ni moja ya dhambi mbaya sana kuliko nyingi kwasababu ipo kinyume na UHAI na UZIMA.
Hebu tafakari endapo Adamu angekuwa na Adamu mwenzake sisi tungetokea wapi? Au wakina Hawa wangeumbwa wawili, sisi tungetokea wapi leo?.. Neno la Bwana linalosema zaeni mkaongezeke lingekuwa wapi?…Hebu fikiri Wanyama wangekuwa wote wa jinsia moja..hii mifugo tuliyonayo leo ingekuwa wapi?…Maziwa tunayokunywa yangetokea wapi? Nyama tunazokula nazo zingetokea wapi, asali tunayoifurahia ingetoka wapi? Endapo nyuki wote wangekuwa wakike au wakiume?
Hata chakula tusingekuwa nacho, kwasababu hata mimea ina sehemu ya kike na ya kiume…sasa kama mimea yote ingekuwa na sehemu ya kiume tu, au ya kike tu…hiyo ngano tunayokula kila siku ingetokea wapi? Mboga tunazokula zingetokea wapi?..Kwahiyo dunia isingekuwa dunia wala Maisha yasingekuwepo endapo kungekuwa na jinsia moja tu duniani.
Kwahiyo dhambi ya mahusiano ya jinsia moja ni dhambi ya KIFO, Kwasababu ipo kinyume na UHAI…Chochote ambacho kipo kinyume na Uhai ni Kifo. Na yeyote afanyaye dhambi ya kifo atakufa.
Kaa mbali na ushoga ni dhambi, kaa mbali na usagaji, wapo wengi wanafanya dhambi hizi kwa siri, pasipo kujua madhara ya dhambi hiyo, Ni dhambi zinazoivuta ghadhabu ya Mungu kwa haraka sana….Dhambi zilizoifanya sodoma na ghomora ziteketezwe ni dhambi hizo za mahusiano ya jinsia moja. Na dhambi hizi hazina cha kujitetea kwasababu ni dhambi za makusudi..Mtu anazipandikiza ndani yake akiwa na akili timamu kabisa, hazina ushawishi wowote..hakuna mazingira yoyote yanayomshawishi mtu kumtamani mtu wa jinsia moja na yeye, ni mtu mwenyewe anazitengeneza ndani yake kwa msaada wa roho za mapepo.
Warumi 1:26 “Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili;
27 wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.
28 Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa”
Tubu, kama wewe ni mmojawapo, kisha uanze uanze kutafuta kuyafanya mapenzi wa Bwana. Naye atakuangazia neema zake.
Shalom.
Mada Nyinginezo:
NINI TOFAUTI KATI YA DHAMBI, UOVU NA KOSA KIBIBLIA?
LILE TUMAINI LILILO NDANI YETU LINAPOULIZIWA.
CHACHU YA MAFARISAYO NA CHACHU YA HERODE.
NIFANYE NINI ILI NIIKWEPE HUKUMU.