Biblia inatufundisha kuwa Mazungumzo mabaya ndiyo yanayoharibu tabia njema ya mtu.
1Wakorintho 15:33 “Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema”.
Maandalizi ya dhambi karibia zote yanaanzia katika “mazungumzo”.. wanaopanga kuua wanaanzia na mazungumzo, wanaopanga kuiba wanaanzia katika mazungumzo, hali kadhalika wanaopanga kufanya zinaa na uasherati wanaanza na mazungumzo.
Kwahiyo kama mtu wa Mungu jiangalie sana aina ya mazungumzo yako hali kadhalika na mtu unayezungumza naye.
Yusufu alijua siri ya mazungumzo na hiyo ikamsaidia kushinda dhambi ya “zinaa”. Kwani maandiko yanasema Yusufu hakukubali kulala na mke wa Potifa na hata KUZUNGUMZA NAYE!
Mwanzo 39:7 “Ikawa baada ya mambo hayo, mke wa bwana wake akamtamani Yusufu, akamwambia, Lala nami.
8 Lakini akakataa, akamwambia mke wa bwana wake, Tazama, bwana wangu hajui kitu kilichowekwa kwangu nyumbani, na vyote alivyo navyo amevitia mkononi mwangu.
9 Hakuna mkuu katika nyumba hii kuliko mimi, wala hakunizuilia kitu cho chote ila wewe, kwa kuwa wewe u mkewe. Nifanyeje ubaya huu mkubwa nikamkose Mungu?
10 Akawa akizidi kusema na Yusufu siku baada ya siku, lakini hakumsikia alale naye, WALA AONGEE NAYE”.
Wengi tunaishia hapo kuwa Yusufu alikataa kulala naye.. lakini biblia inatuonyesha kuwa alikataa pia KUONGEA NAYE..
Huu ni mtego ambao shetani anawanasa wengi katika siku hizi za mwisho, utakuta mtu anajisifia hawezi kuanguka, lakini ni mtu aliejaa mazungumzo na jinsia nyingine kwa kiwango kikubwa!, ni mtu wa mizaha na utani na wa maneno maneno…hawezi kukaa bila angalau kuanzisha mazungumzo yasiyo na maana na mwingine, hawezi kutulia asipochati na mtu mwingine..
Hapo ni ngumu kushinda dhambi ya zinaa, au dhambi nyingine yeyote… Kwasababu biblia imeshasema kuwa, mazungumzo mabaya ndiyo yanayoharibu tabia ya mtu! (1Wakorintho 15:33), haihitaji maelezo mengi!
Ni lazima tu utaharibikiwa tabia ukiwa ni mtu wa mazungumzo mazungumzo yasiyo na maana… hususani na watu ambao bado hawajamjua Mungu.. na watu wa jinsia nyingine.
Chunga mdomo wako, kama unaipenda tabia yako!
Maran atha
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
MAZUNGUMZO MABAYA HUHARIBU TABIA NJEMA.
JIHUDHURISHE, ILI AANZISHE MAZUNGUMZO NA WEWE
ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.
NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.
AKAPITA KATIKA LILE SHAMBA AMBALO YAKOBO ALIMPA YUSUFU MWANAWE
Masomo maalumu kwa wanawake.
Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia Neno la Mungu wetu lililo taa na Mwanga wa njia yetu (Zab.119:105).
Je wewe ni mwanamke? Na unapenda upate kibali mbele za watu?..au je wewe ni binti na unatamani upate ndoa, tena iliyo bora na ya Baraka?, au je wewe ni mwanamke uliyeolewa na unatamani ndoa yako Bwana aibariki na pia upate kibali na heshima Zaidi katika ndoa yako?. Kama ndio basi hakikisha unazingatia mapambo!!..
Katika biblia kuna wanawake waliofanya utafiti wa mapambo yaliyo bora na mazuri na yenye mvuto mkubwa, ili kwamba wawe na mvuto wa heshima mbele za watu, wengine ili wapate ndoa nzuri na kibali kwa wenzi wao..na walipoyatumia hayo mapambo wakafanyika kuwa wanawake bora kuliko wote, na wenye kukubalika kuliko wote.
Wanawake hawa hawakutumia mapambo ya kiulimwengu kama kupaka wanja machoni au kupaka rangi mdomoni ili waolewe au waheshimiwe na waume zao, vile vile hawakuvaa nusu uchi ili wavutie mbele ya wanaowatafuta kuoa, wala hawakusuka nywele ili waonekane warembo, wala hawakupaka rangi katika kucha zao, ili wavutie mbele za watu na kupata ndoa, lakini walitumia mapambo ya aina nyingine na hayo hakawapa ndoa wanazozitafuta, yakawapa heshima wanayoitafuta, yakawapa kibali wanachokitaka n.k.
Na mapambo hayo ni yapi…..?
1Petro 3:3 “Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;
4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, ROHO YA UPOLE NA UTULIVU, ILIYO YA THAMANI KUU MBELE ZA MUNGU.
5 MAANA HIVYO NDIVYO WALIVYOJIPAMBA WANAWAKE WATAKATIFU WA ZAMANI, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.
6 Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote”.
Nataka tuuangalie huo mstari wa 5 unaosema “MAANA HIVYO NDIVYO WALIVYOJIPAMBA WANAWAKE WATAKATIFU WA ZAMANI”..
Kwahiyo kumbe zamani kulikuwa na wanawake “watakatifu” na “wasio watakatifu”. Na kila kundi lilikuwa na aina yake ya mapambo ili lipate kibali na kuvutia.
Na hapa biblia inatufundisha wanawake wa zamani waliokuwa watakatifu ijapokuwa katika masomo yao kulikuwa na vipodozi vingi, kulikuwa na rangi nyingi za kucha, na za uso na za mdomoni, lakini wao kwa ufunuo waliokuwa nao hawakuchagua mojawapo wa hayo mapambo, badala yake waliona yana kasoro, hivyo wakachagua mapambo ya ndani ambayo ni UPOLE, HESHIMA, UTII NA UTULIVU.
Wakaona hayo ndio yatakayowafanya waolewe, ndio yatakayowafanya wapendwe na waume zao, ndio yatakayowafanya wapate kibali katika ndoa zao na jamii zao, ndiyo yatakayowafanya waonekane wa thamani, na si kupaka wanja, au kupaka rangi mdomoni, au kujichubua, au kuvaa nusu tupu.
Ndio maana sasa utaona biblia inasema kama vile Sara alivyokuwa mtii kwa Ibrahimu mumewe hata kufikia hatua ya kumwita Ibrahimu “bwana”, Roho hiyo ya unyenyekevu na utii, na utulivu, ndio iliyomfanya Sara awe “mama wa mataifa” na si “wigi kichwani” wala rangi mdomoni, wala hereni sikioni. Kulikuwa na wanawake wengi katika ile nchi, ambao walikuwa wanajiremba na pengine hata kukaribia kufanana na malaika, lakini Ibrahimu hakuwachagua hata mmoja wao!.
Ibrahimu alimchagua Sara kwasababu alikuwa ni mtii, na mtulivu..(alikuwa na mapambo ya ndani)
“5 MAANA HIVYO NDIVYO WALIVYOJIPAMBA WANAWAKE WATAKATIFU WA ZAMANI, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.
6 Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana…”
Vile vile roho ya upole na ya kujisitiri iliyokuwa juu ya Rebeka, ndio iliyomfanya apate kibali kwa Isaka, kiasi kwamba alipofikishwa kwa Isaka, alifunika kichwa chake kwa shela (Mwanzo 24:62-67), ndio iliyomfanya awe mama wa Taifa kuu la Israeli (Yakobo), na si mavazi ya vimini, au ya mgongo wazi,…Na vivyo hivyo wanawake wengine wote watakatifu walitumia mapambo hayo ili kujipatia kibali.
Lakini wale wengine wa kidunia, walitumia mapambo ya nje, yaani.. vipodozi vyote walivyovitaka, waliweka pini katika pua zao, waliweka rangi kwenye kucha na kwenye kope, na midomoni, walipaka wanja machoni, na kupaka hina mwilini na kuweka nywele bandia n.k lakini wengi wa hao waliishia kutamaniwa tu na si kupendwa kama walivyotafuta,
Na wengine waliishia kuonekana kama makahaba, kama Yezebeli, (maana biblia inaonyesha Yezebeli alikuwa ni mwanamke mwenye kupaka uwanja machoni na kupamba kichwa, maana yake kusokota rasta, na kuweka nywele bandia, na ndio maana biblia ikamtaja kama mwanamke kahaba na mchawi soma 2Wafalme 9:22,30, Ufunuo 2:20-22).
Na siku zote mapambo haya mawili hayawezi kwenda pamoja!, ukitumia moja lazima lingine utalikosa…
Ukiwa unapaka uso rangi, unajichubua, unatoboa pua huwezi kuwa na unyenyekevu, utii, utulivu, au mapambo mengine yote ya ndani huwezi kuwa nayo… ni lazima tu utakuwa na kiburi, tamaa, wivu,.
Na vile vile huwezi kuwa mtii, mnyenyekevu, mpole (mapambo yote ya ndani) halafu ukavaa nusu uchi, vimini au nguo za kubana…
Ingekuwa mapambo haya mawili yanaweza kwenda pamoja (yaani ya ndani na ya nje) basi biblia isingesema wanawake wasijipambe kwa “mapambo ya nje”, badala yake ingesema “wasijipambe kwa mavazi ya nje tu pake yake bali pia wajipambe kwa mapambo ya ndani”. Lakini utaona imekosoa moja na kulihakiki lingine, ikiwa na maana kuwa mapambo haya hayawezi kwenda pamoja.
Mama, dada, binti unayetaka kwenda mbinguni?, na unayetaka kupendeza na kupata kibali.. basi zingatia kujipamba kwa mapambo ya ndani na nje jiweke katika hali yako ya asili, uone kama hutapata kazi unayoitafuta, au ndoa, au kibali popote pale uendapo kama ilivyokuwa kwa akina Sara, na wanawake wengine wa kwenye biblia, na Zaidi ya yote pia utaenda mbinguni kwasababu miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, na si midoli ya matangazo ya nguo masokoni.
1Timotheo 2:9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;
10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu”
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 . jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
NJIA NYINGINE YA KUPATA REHEMA NA KIBALI KUTOKA KWA MUNGU.
NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA
Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?
MWANAMKE, BINTI, MAMA. (Sehemu ya 3)
SWALI: Maandiko yanasema tusilaani, je! Paulo aliwalaani wagalatia na wakorintho?
Wagalatia 1:8 Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe. 9 Kama tulivyotangulia kusema, na sasa, nasema tena, mtu awaye yote akiwahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo mliyoipokea, na alaaniwe.
1Wakorintho 16:22 Mtu awaye yote asiyempenda Bwana, na awe amelaaniwa. Maran atha.
Mtume Paulo alipokwenda katika Galatia na kuwakuta baadhi ya watakatifu wa pale wamegeukia injili nyingine, iliyoletwa na wayahudi, inayosema ili mtu ahesabiwe haki ni lazima amwamini Kristo pamoja na sheria ya Musa, zaidi ya vile mtume alivyofundisha kwamba kinachoweza kumwokoa mtu ni Imani tu katika Kristo!. Sasa alipoona wamefikia hatua hiyo mbaya ndipo aliposukumwa kusema maneno hayo makali kwa wagalatia , kwamba “mtu awaye yote akiwahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo waliyoipokea kwake, na alaaniwe”.
Lakini ni vema kufahamu kuwa kauli hii na ile ya 1Wakorintho 16:22 imetumiwa vibaya na baadhi ya wakristo kwa vizazi vingi, kwamba kwa ajili ya injili tunaruhusiwa kuweka laana kwa watu. Lakini je! Paulo aliwaalaani watu wale?
Jibu la! Kwasababu kama angekuwa ameruhusiwa kuwalaani maadui na wanaokwenda kinyume na , yeye basi asingesema tena maneno haya ya kubariki katika Warumi 12:14
Warumi 12:14 Wabarikini wanaowaudhi; barikini, wala msilaani.
Na isitoshe mtume Paulo alikuwa anawaombea sana rehema ndugu zake Wayahudi waliopotoka, mbali na neema (Warumi 10:1)
Kama hakuwalaana Je! Katika vifungu hivyo alimaanisha nini?
Hilo Neno kulaani, tukisoma katika tafsiri ya awali ya biblia ya kigiriki linasomeka kama “Anathema”
Ambalo linamaanisha “mtu aliye chini ya laana/Hukumu ya Mungu”
Hivyo katika vifungu hivyo, Mtume Paulo aliposema “Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe” Alimaanisha Hivi;
Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na awe kama mtu aliye chini ya laana ya Mungu”
Na ndio maana mtume Paulo katika hiyo nyaraka yake mbeleni alieleza kwa mapana zaidi, jinsi gani watu waliokuwa wanategemea sheria ili kuwaokoa walivyokuwa chini ya laana ya hukumu. Soma;
Wagalatia 3:10 Kwa maana wale wote walio wa matendo ya sheria, wako chini ya laana; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati, ayafanye.
Kwa hitimisho ni kuwa, mtume Paulo hakuwalaani wakorintho au wagalatia. Bali aliwaeleza uhalisi, madhara ya kuipotosha injili ya Kristo. sisi kama wakristo hatupaswi kuwalaani watu ambao wanatupinga/ au wanahubiri injili inayopotosha, bali ni kuwaombea rehema, wageuzwe, lakini bila kuwaficha matokea ya kutenda kwao huko, Kwamba wapo chini ya laana ya Mungu na hivyo waogope! Kwasababu hukumu ipo.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Je Musa yupo anawashitaki watu..kulingana na Yohana 5:45?
Je Paulo na Petro walishindania nini? (Wagalatia 2:11).
Kwanini Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasichukue chochote isipokuwa fimbo tu?
Ni lazima tujue namna mbalimbali za kupambana na adui yetu (Ibilisi). Tunajua yeye ni mpinzani wetu, na mpinzani sikuzote huwa si rahisi kukubali kushindwa kirahisi, ni lazima ataleta ukinzani. Na ndio hapo suala la Kukemea linakuja wala hatumbembelezi wala hatumsihi-sihi, bali tunamkemea.
Kukemea maana yake ni kukipinga/ kukifukuza kitu kwa nguvu, kwa mamlaka uliyonayo.
Tunaona sehemu nyingi Yesu akimkemea ibilisi Pamoja na mapepo yake, ambayo yalikuwa yanawatesa watu.
Mathayo 17:18 “Yesu akamkemea pepo, naye akamtoka; yule kijana akapona tangu saa ile”.
Marko 8:33 Akageuka, akawatazama wanafunzi wake, akamkemea Petro, akasema, Nenda nyuma yangu, Shetani; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu
Hivyo na sisi tumepewa mamlaka hiyo, ya kumkemea ibilisi na mapepo yake, na uovu, na magonjwa, na vitu vya asili kwa jina la Yesu na vikatii.
Lakini pia tuna majira si lazima tufanye hivyo, Tutatumia nguvu nyingi sana! Leo tutaona silaha nyingine za Malaika ambayo wanatumia kumshughulikia shetani.. Maandiko yanatuambia wanao uwezo mkuu kuliko sisi lakini hawatumii uwezo wao wakati wote, kufanya hivyo kila wanapokutana na adui yao shetani.
Kwamfano, Wakati Fulani Malaika Mikaeli alipokutana na shetani, wakiushindania mwili wa Musa, maandiko yanasema, hakutumia uwezo wake kumlaumu, bali alisema Bwana na akukemee!.
Yuda 1:9 “Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee”.
Utajiuliza ni kwanini afanye vile? Sio kwasababu alishindwa, lakini alitambua SILAHA kubwa Zaidi itamfutilia mbali adui yake. Kwa namna nyingine Mikaeli alikuwa anamchonganisha shetani kwa Mungu. Na ukikemewa na Mungu unatarajia nini? Kama sio kupotelea mbali kabisa moja kwa moja.
Hivyo shetani anaiogopa vita ya Mungu Zaidi ya ile ya malaika au wanadamu.
Utaona tena jambo kama hili hili alilitenda Malaika mwingine, wakati ule wa Yoshua kuhani mkuu alipokuwa amesimama mbele za Bwana kuomba, na shetani naye amesimama kumpinga. Yule Malaika alimwambia shetani “Bwana na akukemee”.
Zekaria 3:1 “Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, amesimama mbele ya malaika wa Bwana, na Shetani amesimama mkono wake wa kuume ili kushindana naye. 2 Bwana akamwambia Shetani, Bwana na akukemee Ewe Shetani; naam, Bwana, aliyechagua Yerusalemu, na akukemee; je! Hiki si kinga kilichotolewa motoni?”
Umeona? Hivyo si kila wakati unapopishana na adui yako uso kwa uso, ufikirie kurusha makombora, kuvunja, kuharibu na kubomoa ngome, ndio yapo majira utasimama kuomba hivyo lakini pia tulia kwasababu maandiko yanasema VITA NI VYA BWANA. Mkabidhi Bwana yote. Kwamfano shetani amekuletea majaribu ya magonjwa sugu. Mwambie Bwana yaone mateso yangu, UMKEMEE SHETANI. Arudi nyuma yangu.
Sasa Maombi kama haya, usiyaombe juu juu tu,Fahamu kanuni, Ni maombi ya kumwita Mungu aingilie tatizo hilo, amwone mtesi wako, Ili pale anapopatumia kama mlango wa kukusumbua AMKEMEE atoke. Tatizo Lililokutesa kwa muda mrefu Bwana alifutilie mbali, kwa kulikemea.
Ni maombi aliyoyafanya Esta. Alipoona adui yake Hamani, amepanga vita dhidi yake na uzao wake na ndugu zake wauawe. Hakuhangaika, kushindana na Hamani adui yake. Aliona mambo yatakuwa mengi na kuumizana kichwa. Bali alikwenda moja kwa moja kwa mfalme. Akajinyenyekeza mbele zake, akamfanyia karamu kubwa sana, tena akamwomba katika karamu hiyo aje na yule adui yake, washiriki pamoja. ndipo mfalme akamuuliza haja yako ni nini, Lakini tunaona Esta bado hakumwambia tatizo lake kwa haraka,, akamfanyia tena na mara ya pili mfalme na adui yake karamu iliyo kubwa kama ile ya kwanza, akawaalika.. Ndipo Mfalme akamuuliza tena Esta haja yako ni nini?. Ndipo Esta sasa akaeleza akasema, ni HUYU ADUI YANGU HAMANI, amepanga kuniua mimi.
Akamwachia mfalme hukumu yote. Saa ileile Hamani akaenda kutundikwa msalabani, yeye na nyumba yake yote ikauliwa. Na Habari yake ikawa imeisha pale hadi hivi leo. Wala Esta hakuita kikosi, wala hakuchukua upanga, wala hakumwambia mfame muue, mvunje shingo, mchome moto Hamani. Hakusema hayo alichomwomba mfalme ni uhai wake tu (Esta 5).
Na ndivyo Mungu atakavyofanya kwa adui yetu Ibilisi na mapepo yake, pale ambapo tutataka Bwana ashughulike na matatizo yetu, zaidi ya sisi kushughulika nayo kuyakemea. Lakini ni sharti sisi tumkaribie yeye, kwa moyo wa upendo, tumfanyie karamu, ya Kupendeza ndipo tuzikabidhi changamoto zetu kwake.
Hivyo silaha hii ukiitumia vema itakusaidia sana. Jenga ukaribu wako na Mungu, Fanya ibada nyingi, mtolee Bwana sadaka, mwimbie sifa, mtukuze sana, ruka-ruka uweponi mwake, mpendeze moyo wake..( fanya hivi Zaidi ya kurusha makombora, na maombi ya vita) kisha mwishoni ndio mwambie Bwana amkemee adui yako. . Matokeo utayaona makubwa sana, haijalishi tatizo ulilonalo limekusumbua kwa muda mrefu kiasi gani, umepambana nalo kwa muda mrefu kiasi gani, limekuja na kujirudia rudia mara nyingi kiasi gani. Ugonjwa huo hautibiki kwa namna ipi, utakwenda tu.. Safari hii halitarudi kwako tena milele.
Bwana akubariki.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?
USIRUHUSU INZI WATUE JUU YA ROHO YAKO.
Ni kwa namna gani, upendo husitiri wingi wa dhambi? (1Petro 4:8).
(Masomo maalumu yahusuyo mifungo na maombi).
Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze Biblia Neno la Mungu wetu lililo taa ya miguu yetu na Mwanga wa njia yetu (Zab 119:105).
Biblia inatufundisha sehemu kadhaa FAIDA za kufunga (yaani kujizuia kula na kunywa kwa kitambo) kwamba kwa kufanya hivyo tunafungua milango mingi, ambayo isingeweza kufunguka kwa maombi ya kawaida tu.
Mathayo 17:20 “Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.
21 [LAKINI NAMNA HII HAITOKI ILA KWA KUSALI NA KUFUNGA”.
Lakini JE UNAJUA FAIDA ZA KUIFUNGISHA NA MIFUGO YAKO PIA? AU KAZI YAKO, AU BIASHARA YAKO?. Si watu tu wanaopaswa kufunga hata wanyama pia.. Utauliza hilo limekaaje?, hebu turejee biblia kidogo nyakati zile za Nabii Yona alipokwenda kuhubiri katika mji wa Ninawi.
Biblia inaonyesha kuwa Mfalme wa Ninawi alipiga mbiu kuwa wanadamu na wanyama wote walioko Ninawi wafunge wasile wala wasinywe (Zingatia hilo: si wanadamu tu bali hata wanyama wa kufugwa).
Yona 3:6 “Habari ikamfikia mfalme wa Ninawi, naye akaondoka katika kiti chake cha enzi, akavua vazi lake, akajivika nguo za magunia, na kuketi katika majivu.
7 Naye akapiga mbiu, akatangaza habari katika mji wa Ninawi, kwa amri ya mfalme na wakuu wake; kusema, Mwanadamu ASIONJE KITU, WALA MNYAMA WALA MAKUNDI YA NG’OMBE, WALA MAKUNDI YA KONDOO; WASILE, WALA WASINYWE MAJI;
8 bali na wafunikwe nguo za magunia, MWANADAMU NA MNYAMA PIA, nao wakamlilie Mungu kwa nguvu, naam, na wageuke, kila mtu akaache njia yake mbaya, na udhalimu ulio mikononi mwake.
9 Ni nani ajuaye kwamba Mungu hatageuka na kughairi, na kuiacha hasira yake kali, ili msiangamizwe? 10 Mungu akaona matendo yao, ya kuwa wameiacha njia yao mbaya. Basi Mungu akalighairi neno lile baya, ambalo alisema atawatenda; asilitende”.
Unaona alichofanya Mfalme wa Ninawi??…Na matokeo yake tunaona baadaye Mungu anawataja wanyama kuwa wamestahili rehema kwa mfungo huo..Maana yake wanyama nao pia wasingefungishwa huenda wangepona watu tu lakini wanyama wangepigwa (wangekufa!!)..Maana yake uchumi wao watu wa Ninawi ungeharibika, hata baada ya wao kupokea msamaha!!.
Yona 4:10 “Bwana akamwambia, Wewe umeuhurumia mtango, ambao hukuufanyia kazi, wala kuuotesha; uliomea katika usiku mmoja, na kuangamia katika usiku mmoja;
11 na mimi, je! Haikunipasa kuuhurumia Ninawi, mji ule mkubwa; ambao ndani yake wamo watu zaidi YA MIA NA ISHIRINI ELFU, wasioweza kupambanua katika mkono wao wa kulia na mkono wao wa kushoto; TENA WAMO WANYAMA WA KUFUGWA WENGI SANA?”
Nataka uangalie hayo maneno ya mwisho ya Bwana… “TENA WAMO WANYAMA WA KUFUGWA WENGI SANA?”
Kumbe hata wanyama pia wanaweza kuingizwa kwenye mkondo wetu wa BARAKA AU LAANA!.. Mfalme wa Ninawi aliliona hili, alijua siku ile ya gharika ya Nuhu hata wanyama waliangamizwa na dunia, na yeye akajua dhambi zimewachafua si tu watu, bali hata na wanyama wao wa kufugwa, hivyo nao pia ni lazima watakaswe kwa toba na kwa kufunga, na utaona aliwavisha mpaka hao wanyama mavazi ya magunia!.
Ni vizuri kulijua hili ndugu, kuwa unapofunga fanya hivyo pia kwa wanyama wako (inaweza isiwe mara kwa mara lakini weka desturi hiyo)!!!
Unapofunga hebu pia funga pia na shamba lako, usinyeshee chochote siku hiyo, usiweke mboleo siku hiyo, wala usilipalilie, kama unafuga kuku, usiwalishe siku hiyo, usilishe ng’ombe wako siku hiyo, usilishe mbuzi wako siku hiyo, vile vile usifungue biashara yako siku hiyo, fanya hivyo kwa Imani na utaona matokeo makubwa sana baada ya hapo!.
Wengi hawaoni matokeo katika kazi zao kwasababu wanasahau kufunga biashara zao, badala yake wanafunga tu wao, pasipo kujua kuwa vifungo pia havipo tu katika mwili, bali pia katika biashara na mifugo, hivyo nayo pia inapaswa ifungishwe.
Bwana akubariki.
Maran atha
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.
Hakuna namna utautenganisha “Moyo” na “hazina”.. vitu hivi vinaenda pamoja!.(ni sawa na miguu na mwili,..mahali miguu ilipo na mwili upo, miguu haiwezi kuwa mahali pengine na mwili mahali pengine) Vile vile Moyo wa mtu na hazina yake, vinaenda pamoja…Pale mtu alipojiwekea hazina, ni lazima (akili yake yote na fikra zake na hisia zake na mawazo yake yatakuwa huko).
Ndio maana mtu aliyejiwekea hazina kubwa ya mali za kidunia, halafu mali zile zikapotea zote ghafla, ni rahisi mtu huyo kuchanganyikiwa au kupoteza maisha maisha kabisa!.
Kwanini?..Kwasababu Moyo wake wote (fikra, mawazo, akili, malengo, uzima, hadhi) vilikuwepo katika mali zile, na sasa hana tena!, hata maisha kwake yanakuwa hayana maana tena!. Ndivyo ilivyo, kwamba Moyo siku zote unafuata hazina ilipo!, na unaishi kutokana na hazina mtu alizonazo. Ndivyo moyo wa mtu ulivyoumbwa!..
Vile vile mtu anayejiwekea hazina mbinguni, ni lazima fikra zake, mawazo yake, akili yake, malengo yake yote yatakuwa kule mbinguni hazina yake ilipo.
Sasa Bwana Yesu alitufundisha kanuni ya kuielekeza Mioyo yetu mbinguni, kwamba si kwa kuomba tu! Bali kwa kujiwekea hazina kule mbinguni,..kwanini?…kwasababu tutakapojiwekea hazina kule juu mbinguni basi mioyo yetu (yaani fikra, fahamu, akili, mawazo na hisia) zitaelekea kule Mbinguni, bila shuruti!.
Sasa swali, tunajiwekeaje hazina juu mbinguni?.. yeye mwenyewe (Bwana Yesu) alitufundisha kanuni katika Luka 18:18-22
Luka 18:18 “Tena, mtu mkubwa mmoja alimwuliza, akisema, Mwalimu mwema, nifanye nini ili nipate kuurithi uzima wa milele?
19 Yesu akamwambia, Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, naye ndiye Mungu.
20 Wazijua amri; Usizini, Usiue, Usiibe, Usishuhudie uongo, Waheshimu baba yako na mama yako.
21 Akasema, Hayo yote nimeyashika tangu utoto wangu
22 Yesu aliposikia hayo alimwambia, Umepungukiwa na neno moja bado; viuze ulivyo navyo vyote, ukawagawanyie maskini, NAWE UTAKUWA NA HAZINA MBINGUNI; kisha, njoo unifuate”.
Na tena anarudia maneno kama hayo hayo katika Luka 12:32-34…
Luka 12:32 “Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme.
33 Viuzeni mlivyo navyo, mtoe sadaka. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, AKIBA ISIYOPUNGUA katika mbingu, mahali pasipokaribia mwivi, wala nondo haharibu.
34 KWA KUWA HAZINA YENU ILIPO, NDIPO ITAKAPOKUWAPO NA MIOYO YENU”.
Umeona?.. Kumbe kanuni ya kujiwekea hazina mbinguni ni kumtolea Mungu!..
Kwanini?.. Kwasababu tunapomtolea Mungu vile tulivyo navyo, mawazo yetu yatakuwa siku moja kwenda kupata thawabu mbinguni!, fikra zetu zitakuwa siku moja kwenda kuona miji mizuri tuliyoandwaliwa, mawazo yetu yatakuwa siku moja kwenda kuvikwa taji……hivyo muda wote tutakuwa tunafakari tu yaliyo ya juu na huko ndiko mioyo yetu itakapokuwepo!.
Ndio maana utaona watu wanaojitoa kwa Mungu kuanzia miili yao, mpaka mali zao, muda wote wanawaza unyakuo utakuwa lini?, muda wote wanawaza Kristo anakuja lini?.. ni kwanini wanakuwa hivyo?, si kwamba wanajilazimisha kuwa hivyo, ni kwamba tayari mioyo yao ipo mbinguni kwasababu wamejiwekea hazina huko.
Hii ni kanuni rahisi kabisa ya kuhamisha mioyo yetu kutoka kutafakari MAMBO YA CHINI na kuanza kutafakari MAMBO YA JUU!.
Ukitaka uwe mtu wa kutafakari mambo ya mbinguni sana, mtolee Mungu kuanzia muda wako, akili yako, mwili wako, ufahamu wako na hata vitu vyako!.. Hapo moyo wako wenyewe tu utaanza kuelekea mbinguni bila hata kutumia nguvu nyingi!,. Utajikuta tu unaanza kutamani kumwona Yesu, utajikuta unatamani ile siku ya mwisho ifike n.k
Laakini kinyume chake usipofanya hivyo na ukajitumainisha katika kujiwekea hazina katika mambo ya ulimwengu, basi fahamu kuwa moyo wako utaelekea tu katika mambo ya ulimwengu hata kama hupendi!.
Wakolosai 3:2 “Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi”.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Hazina za gizani ni zipi? (Isaya 45:3).
YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.
Nondo ni nini kama tunavyosoma katika biblia?
UKIOKOKA, JIANDAE KUPITISHWA USIPOPATAZAMIA.
Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu libarikiwe.
Karibu tujifunze biblia Neno la Mungu wetu lililo taa ya miguu yetu na mwanga wa njia yetu.
Kuna mambo makuu mawili ambayo yanaweza KUMUUNGANISHA MTU MOJA KWA MOJA NA USHIRIKA WA MAPEPO.
Na mambo hayo ni SADAKA NA UASHERATI. Haya mambo mawili yanaenda pamoja, ndio maana wanaoenda kwa waganga utaona wanaambiwa watoe sadaka, au wafanye zinaa, lengo la zile sadaka si kuimairisha maisha ya wale wanaozitaka (waganga), wala lengo la ile zinaa si kuwafurahisha hao waganga bali ni kumuunganisha yule mtu na madhabahu ile!.
Sasa nataka tuangalie mfano mmoja wa kwenye biblia wa watu waliojiunganisha na madhabahu za mashetani kwa njia hizo mbili; (MATOLEO PAMOJA NA UASHETANI). Na hao si wengine Zaidi ya Wana wa Israeli walipokuwa katika safari yao ya kwenda Kaanani.
Tusome,
Hesabu 25:1 ”Basi Israeli akakaa Shitimu, KISHA WATU WAKAANZA KUZINI PAMOJA NA WANAWAKE WA MOABU;
2 kwa kuwa waliwaalika hao watu WAENDE SADAKANI, sadaka walizowachinjia miungu yao; watu wakala chakula, wakaisujudu hiyo miungu yao.
3 IKAWA ISRAELI KUJIUNGAMANISHA NA BAAL-PEORI; hasira za Bwana zikawaka juu ya Israeli.
4 Kisha Bwana akamwambia Musa, Watwae wakuu wote wa hao watu, ukamtungikie Bwana watu hao mbele ya jua, ili kwamba hizo hasira kali za Bwana ziwaondokee Israeli.
5 Basi Musa akawaambia waamuzi wa Israeli, Waueni kila mtu watu wake waliojiungamanisha na Baalpeori”
Mstari wa 3 hapo unasema hao watu kajiunganisha na “Baali-peori” ambaye ni mungu wa wamoabi, na njia waliojiunganisha nayo ni UASHERATI na SADAKA!
Na adui njama aliyoitumia ni KUALIKA!.. walioalikwa tu! Lakini kumbe walikuwa wameshaandaliwa “wanawake wa kuzini nao” na kwa tamaa zao wakaingia kwa wanawake hao na kuzini, pasipo kujua kuwa kwa kitendo hiko tayari walikuwa wameshajiungamanisha na miungu yao, na hivyo hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli na Mungu akapigo kwa pigo kuu.
Ndugu, (kaka, dada,mama, baba) jihadhari na uasherati, jihadhari na Mialiko isiyo rasmi inayohusisha jinsia mbili tofauti.. Mtego wa shetani si wewe ufanye tu dhambi ya uzinzi, bali lengo lake ni wewe kukuunganisha na miungu na madhabahu ya huyo unayekwenda kuzini naye.
Na madhara ya kuunganishwa na mtu huyo ni kwamba zile “laana” na “hukumu” anazozibeba na wewe unazibeba..Ndicho kilichowatokea wana wa Israeli walipozini na wanawake wa Moabu, Taifa la Moabu lililaaniwa na wote waliozini na wale wanawake walibeba zile laana.
Ndivyo maandiko yanavyosema katika 1Wakorintho 6:15…
1Wakorintho 6:15 “Je! Hamjui ya kuwa miili yenu ni viungo vya Kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha!
16 Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja”.
Sasa inawezekana ulifanya hayo pasipo kujua, na hivyo ulijiungamanisha na madhabahu za kuzimu. Suluhisho la kwanza si kwenda kuombewa!… bali ni wewe kutubu! Kwa kumaanisha kutofanya machukizo hayo tena. Na baada ya kutubu, hatua inayofuata ni ubatizo sahihi na kisha kudumu katika Imani huku ukijitenga na uovu na vichocheo vyake vyote.
1Wakorintho 6:18 “Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe”.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?
Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?
MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.
Chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu ndio kipi? (Matendo 21:25).
Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tena tujifunze maneno ya uzima.
Kulikuwa na aina nne za wito ambao Bwana aliwaitwa mitume wake.
Matendo 1:8 Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi
Sasa nini maana ya kuwa SHAHIDI? Kuwa shahidi maana yake ni kuwa tayari kupitia mateso au kumwaga damu yako kwa ajili ya kumtetea Yule anayekutuma. Hivyo mtu yoyote aliyemwaga damu yake, kwa ajili ya Yesu huyo ni SHAHIDI. Hivyo mitume walijua kabisa hatma yetu ni kumwaga damu tu, huko mbeleni. Na watu kama hawa wanakuwa na nafasi ya juu sana, mbele ya Kristo siku ile watakapofika mbinguni, kwasababu wanakuwa wamepitia sehemu ya mapito yaleyale aliyoyapitia Bwana wao hapa duniani.
Leo tutatazama aina nne(4), za mashahidi wa Kristo. Na wewe pia utajipima upo wapi kati ya hawa na kama haupo popote basi, ufanye bidii uwe katika wingu hili la Mashahidi wa Yesu.
2Wakorintho 11:23 “Wao ni wahudumu wa Kristo? (Nanena kiwazimu), mimi ni zaidi; katika taabu kuzidi sana; katika vifungo kuzidi sana; katika mapigo kupita kiasi; katika mauti mara nyingi. 24 Kwa Wayahudi mara tano nalipata mapigo arobaini kasoro moja. 25 Mara tatu nalipigwa kwa bakora; mara moja nalipigwa kwa mawe; mara tatu nalivunjikiwa jahazi; kuchwa kucha nimepata kukaa kilindini”.
Hata sasa, wapo watu wanateswa kwa namna mbalimbali, wengine wanamwaga damu kwa mapigo, watu kama hawa ni mashahidi wa Bwana. Sawa tu wale mitume wake.
Hili ni kundi la pili ambalo linamwaga damu pia. Ijapokuwa haitaonekana kwa nje lakini rohoni Mungu anawaona kama wamemwaga damu kwa ajili ya ushuhuda wake. Kwamfano tukiangazia kile kisa cha Daudi ambapo wakati Fulani alitamani kunywa maji ya kisima kilichokuwa katikati ya maadui zake wafilisti. Lakini tunaona mashujaa wake watatu waliposikia, waliondoka kisirisiri, wakahatarisha maisha yao, kwenda katika marago ya wafilisti, na kuyachukua yale maji na kumletea Daudi, lakini Daudi hakuyanywa alisema ile ni damu yao na sio maji tena.
2Samweli 23:14 Naye Daudi wakati ule alikuwako ngomeni, na jeshi la Wafilisti wakati ule walikuwako Bethlehemu. 15 Daudi akatamani, akasema, Laiti mtu angeninywesha maji ya kisima cha Bethlehemu, kilicho karibu na lango! 16 Basi hao mashujaa watatu wakapenya jeshi la Wafilisti, wakateka maji kutoka kile kisima cha Bethlehemu, kilicho karibu na lango, wakayachukua, wakamletea Daudi; walakini yeye hakukubali kuyanywa, akayamimina mbele za Bwana. 17 Akasema, Hasha, Bwana, nisifanye hivi; je! Si damu hii ya watu hao waliohatirisha nafsi zao? Kwa hiyo hakukubali kuyanywa. Hayo ndiyo waliyoyafanya wale mashujaa watatu.
Umeona? Maji yamekuwa damu kwasababu ya hatari waliyoingia watu wale. Vivyo hivyo na wewe ujitoapo sadaka kwa ajili ya Bwana, unapohatarisha hata kazi yako, muda wako, ujana wako, ili tu umfanyie Mungu jambo. Ndugu hilo linakuwa sio jambo la kawaida bali ni damu yako unayoimwaga kwake.
Kulikuwa na Yule mwanamke alikwenda kumtolea Bwana sadaka ya senti mbili, lakini maandiko yanasema ndio iliyokuwa riziki yake yote, hajui kama kesho ataiona, pengine hata jana yake hakula. Si ajabu kwanini Bwana aliona ametoa zaidi ya wengine wote. Kwasababu kilichokuwa anakitoa ni uhai wake, na sio sadaka ya kawaida.
Jiulize nguvu zako unazozisumbukia daima unazimalizia kwa nani, je! Ni kwenye kujenga tu, ni kuwekeza, ni kuvaa ni kula? Au ni nini? Vipi kwa Mungu wako, unampa sehemu ndogo tu, ni kweli utapata thawabu? Lakini je! Ulishawahi kufikiria kutenda jambo linalokugharimu wewe kwa Bwana wako? Damu yako unaimwaga wapi?. Watakatifu wa kanisa la kwanza, waliweza kuuza mali zao za thamani na kumtolea Bwana, na sisi tunafanya nini kwa Bwana?.
Hili nalo ni kundi lingine la wanaomwaga damu. Ukisoma Marko 9:43-49, kuna maneno Bwana Yesu alisema, kuhusiana na viungo vyetu. Akasema ikiwa kimojawapo kinakukosesha kikate, ili usikose uzima wa milele. Unajua sikuzote kiungo kikatwapo, ni lazima damu imwagike. Ukiuondoa mguu wako, yapo maumivu, lakini pia ipo damu itakayokutoka.
Viungo vinaweza vikawa ni wazazi, marafiki, ndugu, kazi, mazingira n.k. Ikiwa mzazi anakukosha usisimame vema na Mungu, anakukataza usimwabudu Bwana,au usihubiri huna budi kutomtii kwasababu hiyo, ni kweli utakutana na maumivu, damu itatoka, lakini umemtii Kristo.
Ndicho alichokifanya mfalme mmoja aliyeitwa ASA, yeye alimcha Mungu, na alipoona mama yake anamletea habari za ibada za masanamu, akamwondoa kwenye kiti cha umalkia, japokuwa ni fedheha kubwa alionyesha lakini aliona ni heri kumtii Kristo zaidi ya mwanadamu (1Wafalme 15:11-13)
Hata leo, watu ambao, wameachwa, na viongo vyao vya karibu, au wameviondoa, kwasababu ya Kristo, visiwaghasi, labda ni kazi, ndugu, rohoni wanaonekana kama wamemwaga damu zao kwa ajili ya ushuhuda wa Kristo, na hivyo ni mashahidi wa Bwana. Ndugu usiopoge maumivu, mpende Bwana zaidi ya chochote.
Yesu alipokuwa anaomba, kwa maomboleza na dhiki nyingi kwa ajili yetu muda mfupi kabla ya kusulibiwa, maandiko yanasema jasho lake, likageuka kuwa matone ya damu.
Luka 22:41 “Mwenyewe akajitenga nao kama kiasi cha kutupa jiwe, akapiga magoti akaomba, 42 akisema, Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke. 43 Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu. 44 Naye kwa vile alivyokuwa katika dhiki, akazidi sana kuomba; hari yake ikawa kama matone ya damu yakidondoka nchini.]
Hivyo na wote, waombolezao kwa ajili ya haki, machozi yao si bure, wanaokesha kuliombea kanisa, na kazi ya Mungu, wanaowaombea wengine kwa machozi na huzuni, wanadumu madhabahuni kwa Bwana muda mwingi mfano wa Ana (Luka 2:36). Rohoni wanamwaga damu, japo wanaweza wasilijue hilo. Na hivyo ni mashahidi wa Kristo duniani. Thawabu yao mbinguni ni sawasawa na wale waliokatwa vichwa kwa ajili ya Bwana.
Swali ni je! Mimi na wewe tunasimama wapi? Paulo anasema ninakufa kila siku, je! Na sisi tunafanya hivyo kwa Bwana wetu? Bwana atusaidie tuwe maaskari wake kwelikweli, ili siku ile ajivunie sisi mbele za Mungu na malaika zake.
Fanyika shahidi mwaminifu wa Bwana.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.
VIFO VYA MITUME WA YESU/ JINSI MITUME WALIVYOKUFA.
KAZI ZA ROHO MTAKATIFU
MAMBO YA KUJIFUNZA KWA KLOPA NA MKE WAKE!
Maana Ya Maneno Katika Biblia.
Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo, karibu tuyatafakari maneno ya neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.
Sisi kama wakristo hatuna budi kutambua kuwa yapo majira mbalimbali tutapishana nayo angali tukiwa hapa duniani katika safari yetu ya imani. Leo tutaona mojawapo ya majira ambayo, huna budi kupishana nayo sehemu Fulani katika maisha yako. Na watakatifu wengi wanapofikia hatua hii, huwa wanavunjika moyo, na wengine kudhani Mungu amewaacha. Lakini la! Ni moja ya mapito ambayo Bwana anayaruhusu kwasababu zake maalumu.
Na majira hayo ni ya kuondolewa msaada, au usaidizi, au ukaribu, au faraja ya ndugu, ya marafiki, au ya wapendwa. Yategemea na pito la mtu mwenyewe. Na sio kwamba ni wabaya, hapana, ni Mungu tu peke yake kaamua kufunga milango hiyo. Ili abaki yeye na Mungu wake tu, katika chumba cha siri cha rohoni.
Tujifunze kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Ambaye, alikuwa mashuhuri sana, na kila mahali alipokwenda alizingirwa na makutano mengi, wakati mwingine alijificha ili watu wasimwone, kwasababu walikuwa wanamsonga sana, hata nafasi ya kula ilikosekana, maelfu ya watu walitamfuata popote alipokwenda.
Lakini kuna majira, hata wale waliokuwa karibu naye (yaani mitume) walimkimbia akabaki yeye peke yake, na hilo aliliona mapema akawaambia wanafunzi wake, ili wasije wakajisikia vibaya.
Yohana 16:32 Tazama, saa yaja, naam, imekwisha kuja, ambapo mtatawanyika kila mmoja kwao kwao, na kuniacha mimi peke yangu; walakini mimi si peke yangu, kwa kuwa Baba yupo pamoja nami.
33 Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.
Na ilikuja kutokea hivyo (Soma Marko 14:27-51). Kwasababu ilikuwa ni sehemu ya pito la mwana wa Mungu.
Halikadhalika yupo mtume Paulo, kama tunavyojua yeye ndio alikuwa kama askofu-kiongozi wa makanisa ya mataifa. Alikuwa na marafiki wengi, alikuwa na wapendwa wengi waliomsapoti na kumfariji, katika utumishi wake. Lakini upo wakati alijikuta peke yake. Mpaka akaandika sehemu ya waraka huo na kumtumia Timotheo. Jambo ambalo huwezi dhani linawezekana kwa askofu wa makanisa.
2Timotheo 4:16 “Katika jawabu langu la kwanza hakuna mtu aliyesimama upande wangu, bali wote waliniacha; naomba wasihesabiwe hatia kwa jambo hilo. 17 Lakini Bwana alisimama pamoja nami akanitia nguvu, ili kwa kazi yangu ule ujumbe utangazwe kwa utimilifu, hata wasikie Mataifa yote; nami nikaokolewa katika kinywa cha simba. 18 Bwana ataniokoa na kila neno baya, na kunihifadhi hata nifike ufalme wake wa mbinguni. Utukufu una Yeye milele na milele. Amina”
Hivyo, hii sio bahati mbaya, ijapokuwa tunazungukwa na wapendwa, na familia, na watoto, na marafiki, lakini kuna wakati Bwana atataka ubaki peke yako na yeye. Na hivyo katika kipindi hicho utakachojikuta, upo mbali nao, au huoni msaada wowote kutoka kwao kama ilivyokuwa kule mwanzo, au hawakuulizii tena, huna mtu wa kucheka naye, kuimba naye. Usijione mpweke, bali mtazame Kristo, elekeza mawazo yako kwake, kwasababu kuna jambo anataka kukufundisha.
Na wakati huo ukiisha, utaona tena anakurejeshea, faraja yako, wapendwa wako, rafiki zako, ndugu zako, na safari inaendelea. Kama alivyofanya kwa Ayubu.
Ayubu 42:10 “Kisha Bwana akaugeuza uteka wa Ayubu, hapo alipowaombea rafiki zake; Bwana naye akampa Ayubu mara mbili kuliko hayo aliyokuwa nayo kwanza. 11 Ndipo wakamwendea nduguze wote, waume kwa wake, nao wote waliojuana naye hapo zamani, wakala chakula pamoja naye katika nyumba yake; nao wakamlilia na kumtuza moyo katika habari za huo uovu wote Bwana aliouleta juu yake; kila mtu akampa kipande cha fedha, na pete ya dhahabu kila mmoja”.
Hivyo weka akiba ya wakati huo, kwasababu hutaukwepa ikiwa wewe ni mwana wa Kristo.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
WATAMTAZAMA YEYE AMBAYE WALIMCHOMA; NAO WATAMWOMBOLEZEA.
HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.
NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?
NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.
Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?
Karibu katika mfululizo ya masomo yahusuyo matoleo!
(Ifahamu Nguvu iliyopo katika Sadaka)
Tangu Adamu aanguke ardhi ilianza kulaaniwa; kila siku laana ilikuwa inajiongeza juu ya laana, ndio maana utaona Mungu alimwambia Adamu ardhi imelaaniwa kwaajili yake yeye na uzao wake (Mwanzo 3:17), lakini ukizidi kusoma utaona tena ardhi inalaaniwa mara ya pili kwa Kaini (Mwanzo 4:11).
Na desturi hiyo iliendelea juu ya wanadamu, (Maana yake kila kukicha ardhi ilikuwa inalaaniwa juu ya wanadamu, kutokana na maasi).
Lakini tunasoma alipozaliwa Nuhu maandiko yanamtaja kama mwana wa Faraja, atakayeikomesha laana iliyo juu ya ardhi.
Mwanzo 5:28 “Lameki akaishi miaka mia na themanini na miwili, akazaa mwana.
29 Akamwita jina lake Nuhu, AKINENA, HUYU NDIYE ATAKAYETUFARIJI KWA KAZI YETU NA KWA TAABU YA MIKONO YETU KATIKA NCHI ALIYOILAANI BWANA”
Sasa unaweza kujiuliza ni wakati gani ambao Nuhu alileta faraja katika Nchi aliyoilaani Bwana?
Tusome Mwanzo 8:20-22.
Mwanzo 8:20 Nuhu akamjengea Bwana madhabahu; akatwaa katika kila mnyama aliye safi, na katika kila ndege aliye safi, akavitoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu.
21 Bwana akasikia harufu ya kumridhisha; Bwana akasema moyoni, SITAILAANI NCHI TENA BAADA YA HAYO KWA SABABU YA WANADAMU, MAANA MAWAZO YA MOYO WA MWANADAMU NI MABAYA TANGU UJANA WAKE; WALA SITAPIGA TENA BAADA YA HAYO KILA KILICHO HAI KAMA NILIVYOFANYA.
22 Muda nchi idumupo, majira ya kupanda, na mavuno, wakati wa baridi na wakati wa hari, wakati wa kaskazi na wakati wa kusi, mchana na usiku, havitakoma”
Umeona hapo? Baada ya Nuhu kumjengea Bwana madhabahu na kumtolea Bwana sadaka nzuri na ya kumridhisha, ndipo akaikomesha ile laana yote iliyokuwa inaendelea juu ya ardhi, kukawa hakuna tena kulaaniwa kwa nchi baada ya hapo!, ndio maana mpaka leo tunaona misimu ya mvua ipo, misimu ya kiangazi cha mavuno ipo, majira ya kuvuna na kupanda bado yapo, kama isingelikuwa ile sadaka Nuhu aliyoitoa huenda leo tungekuwa dunia ingekuwa mahali pabaya.
Lakini siri ya KUIKOMESHA HIYO LAANA!, Nuhu alifahamu ni kwa NJIA YA MATOLEO TU!..Na ni kanuni gani Nuhu aliyoitumia kutoa sadaka mpaka kufikia kuvunja misingi ya laana ya ardhi?
1.Alijenga Madhabahu.
Na sisi ni lazima tujenge madhabahu kwanza, na Madhahabu ya sasa, Agano jipya si ile ya mawe bali ni MIOYO YETU, Hiyo inapaswa iwe misafi kabla ya kufikiri kumtolea BWANA sadaka. Kwasababu maandiko yanasema sadaka ya mtu mbaya ni machukizo kwa Bwana (Mithali 15:8).
2. Kutoa vilivyo safi.
Baada ya Nuhu kutoka kwenye safina alitwaa wanyama walio safi tu na kumtolea Mungu, Na sisi ni lazima tumtolee Mungu vitu vilivyo visafi, hatupaswi kumtolea Mungu vitu vilivyopatikana kwa njia haramu kama ukahaba, dhuluma, rushwa, wizi, utapeli, na njia nyingine zote zinazofanana na hizo.
Kumbukumbu 23:18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili.”
3. Kutoa katika KILA kilicho safi!
Hii ni kanuni ya mwisho na ya muhimu sana, Ni lazima kutoa katika “KILA” kilicho safi, na si katika “BAADHI ya vilivyo safi”. Nuhu hakutoa tu Ng’ombe pekee yake kama sadaka, na kuwahifadhi mbuzi kwaajili ya chakula chake na biashara yake, au hakutoa kondoo pekee yake, na kuwaacha kuku na mbuzi…bali alitoa katika vyote vilivyo safi, ikiwemo kondoo, mbuzi, ng’ombe, njiwa, kuku na vinginevyo.. kila kimoja kwa sehemu yake..Hiyo ikafanya sadaka yake kumridhisha Mungu, na hivyo kufuta laana zote zilizokuwepo juu ya nchi, ambapo mpaka leo tunakula matunda yake.
Na wewe una vitu gani vilivyo safi mbele za Mungu?, je katika vyote unavyovifanya huwa unafikiri kumtolea Mungu katika hivyo?, Je katika zawadi unazopewa ulishawahi kufikiri kumtolea Mungu sehemu ndogo katika hiyo?, au unafiki ni sehemu ya mshahara tu ndio Mungu anaitaka?!
Je katika mifugo yako yote ulishawahi kufikiri kumtolea Mungu sehemu ya hiyo? Usimtolee Mungu kuku na kuacha Mbuzi!.. Jaribu siku moja kumtolea mbuzi na kuku kwa pamoja, na uone matokeo yake, (Mungu ameruhusu tumjaribu kwa njia hiyo, Malaki 3:10).
Utaona laana zinavyoondoka juu yako!!.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Sadaka ya Moyo ipoje? (Walawi 22:21).
Chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu ndio kipi? (Matendo 21:25).
Kwanini Nuhu alimlaani Kaanani badala ya mtoto wake Hamu,
UTAYAFIKIAJE MANENO SAFI YA MUNGU?
Biblia inaposema Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, Inamaana gani?