Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia Neno la Mungu wetu, lililo Taa ya miguu yetu na Mwanga wa njia yetu.
Kuna jambo la muhimu la kujifunza juu ya safari ya Wana wa Israeli kutoka Misri kuelekea Kaanani. Maandiko yanaonesha kuwa wana wa Israeli hawakutoka wenyewe Misri, bali walitoka na Kundi lingine lililochanganyikana.
Hebu tusome..
Kutoka 12:35 “Wana wa Israeli wakasafiri kutoka Ramesesi mpaka Sukothi, walipata hesabu yao kama watu sita mia elfu watu waume waliokwenda kwa miguu, bila kuhesabu watoto.
38 NA KUNDI KUBWA LA WATU WALIOCHANGAMANA MNO WAKAKWEA PAMOJA NAO; na kondoo na ng’ombe, wanyama wengi sana”
Umeona hapo?.. Kulikuwa na watu wengine tofauti na Waisraeli walioondoka Misri pamoja na wana wa Israeli.
Sasa swali ni je! kundi hilo lilikuwa ni kundi gani?.
Kundi hilo lilijumuisha baadhi ya Wamisri ambao huenda walikuwa hawataki kuendelea kuishi Misri, labda kutokana na aina ya Maisha ya Misri, pamoja na Wamisri ambao walioana na Waisraeli, maana yake huenda (mwanamke wa kimisri aliolewa na Mwisraeli) hivyo ni lazima aondoke na mumewe, au mwanamke wa kiisraeli aliolewa na Mmisri, na hivyo huyo Mmisri, hataki kumwacha mke wake huyo na akawa radhi kuondoka naye, na kwenda na wana wa Israeli. Hivyo lilikuwa ni kundi kubwa sana!!..
Sehemu nyingine iliyotaja kundi hili lililochanganyikana ni mchanganyiko katika kile kitabu cha Mambo ya Walawi 24:10-16. (Kisa cha Yule mwana wa kiMisri, aliyechanganyikana).
Walawi 24:10 “Ikawa mwana wa mwanamke wa Kiisraeli, ambaye babaye alikuwa Mmisri, akatokea kati ya wana wa Israeli; na huyo mwana wa mwanamke wa Kiisraeli, na Mwisraeli mmoja, wakapigana pamoja ndani ya marago;
11 kisha huyo mwana wa mwanamke wa Kiisraeli akalikufuru hilo Jina, na kuapiza; nao wakamleta kwa Musa. Na jina la mamaye alikuwa akiitwa Shelomithi, binti ya Dibri, wa kabila ya Dani.
12 Nao wakamtia kifungoni, ili wapate kuambiwa neno litakalotoka kinywani pa Bwana.
13 Na Bwana akasema na Musa, na kumwambia,
14 Mtoe huyo aliyeapiza nje ya marago; na wale wote waliomsikia na waweke mikono yao kichwani mwake, kisha mkutano wote na wamwue kwa kumpiga kwa mawe.
15 Nawe nena na wana wa Israeli na kuwaambia, Mtu awaye yote atakayemlaani Mungu wake atachukua dhambi yake.
16 Na yeye atakayelikufuru jina la Bwana hakika atauawa; mkutano wote watamwua kwa kumpiga kwa mawe; kama ni mgeni, kama ni mzalia, hapo atakapolikufuru jina la Bwana atauawa”.
Sasa tukirudi katika habari ya Huu Mkutano uliochanganyika, huenda mkutano huu ukaonekana kama ulikuwa ni mwema, lakini kinyume chake ulikuja kuwa mwiba mkubwa kwa wana wa Israeli, kwani uliwakosesha sana mbele za Mungu wao.
Katika biblia tunasoma kwamba sio wana wa Israeli walioanza kumlalamikia Mungu kuhusu kutaka Nyama jangwani, bali tunasoma ni hili kundi lililochanganyikana ndilo lililoanza kunung’unika na hatimaye kushawishi mkutano mzima hadi wa wana wa Israeli kunung’unika, na kusababisha kuwa dhambi kubwa sana kwa wana wa Israeli.. Hebu tusome habari hiyo…
Hesabu 11:4 “Kisha MKUTANO WA WAFUASI WALIOKUWA KATI YAO, wakashikwa na tamaa; wana wa Israeli nao wakalia tena, wakasema, N’nani atakayetupa nyama tule?
5 Twakumbuka samaki tuliokula huko Misri bure; na yale matango, na matikiti, na mboga, na vitunguu, na vitunguu saumu”
Umeona tena hapo?.. maandiko yanasema “MKUTANO WA WAFUATI WALIOKUWA KATI YAO” ndio walioanza kushikwa na tamaa..wakata nyama..na ndipo Israeli wote nao wakaingiwa na tamaa.
Maandiko yanasema, agano la kale ni kivuli cha agano jipya..Safari ya wana wa Israeli kutoka Misri kuelekea Kaanani , inafananishwa na safari yetu ya kutoka katika utumwa wa dhambi, hapa duniani na kuelekea mbinguni.. Hivyo basi tunapokuwa katika safari hii, hatuna budi kujihadhari na watu waliochanganyikana, (yaani watu waliovuguvugu katika imani), kwasababu kwa nje wanaweza kuonekana hawana madhara yoyote, lakini tukijifunga Nira nao, na kutembea nao huko mbeleni watatukosesha na Mungu wetu na kuturudisha nyuma pakubwa sana, kama hawa walivyowakosesha wana wa Israeli.. Ndivyo maandiko yanavyosema..
2 Wakorintho 6:14 “Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?
15 Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini?
16 Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
17 Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.
18 Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike”
Unapoanza safari ya Wokovu, ni Mungu kakuita wewe, na si wewe pamoja na rafiki yako au mfanyakazi mwenzako.. kama bado yeye hajaokoka hupaswi kujifunganisha naye Nira, maana yake ni kwamba kama mlikuwa mmezoea kwenda bar pamoja unaacha!, (wewe unapaswa umhubirie wokovu kuanzia huo wakati na kuendelea na si kujishikamanisha naye tena), kama mlikuwa mnaketi kuwasengenya watu, unaacha!, unajitenga naye katika hilo eneo.. Na mambo mengine yote mabaya hupaswi kuambatana naye, mpaka na yeye atakapobadilika na kuwa kama wewe.
Lakini usipoamua kujiachanisha naye katika utu wenu wa kale..basi tambua kuwa atakuja kuwa kikwazo kwako kumaliza safari yako salama ya Imani, (atakuwa ni lango la shetani kumtumia kukurudisha wewe nyuma) kama alivyolitumia lile kundi liliochanganyikana kuwarudisha Israeli nyuma kiimani.
Bwana atusaidie katika safari yetu ya Imani.
Maran atha.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
KWA MIOYO YAO WAKAREJEA MISRI.
Hema ya kukutania ni nini, na ilikuwaje?
JINSI MUNGU ANAVYOIPIGA NA KUIPONYA AFRIKA.
KUOTA UMECHOMWA KISU/KUOTA UMEPIGWA RISASI.
Sala ya Bwana ni sala ambayo Bwana wetu Yesu Kristo aliwafundisha wanafunzi wake, kabla ya kuondoka kwake. Na kwa kupita sala ile, hakuwafundisha tu wanafunzi wake bali alitufundisha na sisi pia, maana yake ni kwamba, nasi pia tunapaswa tuombe kama vile Bwana alivyowaelekeza wanafunzi wake.
Lakini ni muhimu kuielewa sala hii kwa mapana, ili kusudi tuisikose shabaha tunapoomba.. Kwa maana tusipoielewa vizuri basi tutajikuta tunaifanya kama Mashairi (kwa kuirudia rudia kama watu wa mataifa, wanavyofanya wanapoiomba miungu yao).. Sisi biblia imetuambia tusifanane na hao.(Mathayo 6:7).
Sasa sala ya Bwana Imegawanyika katika vipengele vikuu nane (8).. Na vipengele hivyo sio sala yenyewe bali ni kama “maelekezo ya sala”. Sala yenyewe hatuwezi kuandikiwa, bali tunaomba kila mtu kulingana na anavyoongozwa au kujaliwa na Roho Mtakatifu.
Ni sawa mtu akupe vipengele saba vya kuombea, akakuambia ombea Familia, ombea Taifa, ombea Kanisa, ombea Marafiki.. Sasa kwa kukwambia hivyo huwezi kwenda kupiga magoti na kusema naombea Taifa, kanisa, ndugu na marafiki halafu basi uwe umemaliza!, Huwezi kufanya hivyo.. bali utakachofanya ni kuzama ndani kwa kila kipengele kukiombea..
Kwamfano Katika kipengele cha kuombea Taifa utaombea Viongozi wote na Hali, na hali ya Taifa, na ya Imani kwa ujumla katika Taifa zima, jambo ambalo linaweza kuchukua dakika kadhaa au masaa kadhaa, vile vile katika Familia, na katika kanisa utafanya hivyo hivyo..zitahitajika dakika nyingi kwasababu kuna watu wengi katika familia, na kuna matatizo mengi ambayo ukianza kuyataja mbele za Mungu, huenda yakachukua dakika nyingi au masaa mengi.. Hivyo kwa vipengele tu hivyo vichache unaweza kujikuta unasali hata masaa 6.
Vile vile katika sala ya Bwana, ni hivyo hivyo, vile alivyoviorodhesha Bwana ni vipengele tu, na sio sala yenyewe, maana yake Mitume hawakuchukua hiyo sala na kuikariri kama shairi na kisha kuirudia rudia kila wakati kabla na baada ya kulala, kama inavyozoeleka leo kufanyika hivyo.
Sasa hebu tuisome sala yenyewe na kisha tutazame kipengele kimoja baada ya kingine.
Mathayo 6:7 “Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke, kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi.
8 Basi msifanane na hao; maana BABA YENU ANAJUA MNAYOHITAJI KABLA NINYI HAMJAMWOMBA.
9 BASI NINYI SALINI HIVI; BABA YETU ULIYE MBINGUNI, JINA LAKO LITUKUZWE, UFALME WAKO UJE,
10 MAPENZI YAKO YATIMIZWE, HAPA DUNIANI KAMA HUKO MBINGUNI.
11 UTUPE LEO RIZIKI YETU.
12 UTUSAMEHE DENI ZETU, KAMA SISI NASI TUWASAMEHEVYO WADENI WETU.
13 NA USITUTIE MAJARIBUNI, LAKINI UTUOKOE NA YULE MWOVU. [KWA KUWA UFALME NI WAKO, NA NGUVU, NA UTUKUFU, HATA MILELE. AMINA.]”
1.BABA YETU ULIYE MBINGUNI
Hiki ni kipengele cha kwanza, ambacho Bwana anatuelekeza tuanze nacho katika sala zetu. Kwamba maombi yetu tuyaelekeze kwa Baba aliye mbinguni, kwamba tumwite Baba asikie maombi yetu na haja zetu, na yeye ni mwaminifu atatupa kama tutakavyomwomba, ikiwa tutaomba sawasawa na mapenzi yake.
Na jambo la kuzingatia hapo ni kwamba Bwana Yesu anatufundisha kuomba kwa “Baba” na sio kwa “Mungu”. Sasa Baba ndio huyo huyo Mungu, lakini cheo cha ubaba kinahubiri mahusiano mazuri zaidi kwetu na aliyetuumba kuliko cheo cha UMUNGU. Viumbe vyote vinamwona muumba kama Mungu, lakini kwetu sisi wanadamu tumepewa heshima ya kipekee kwamba tumwite Mungu, Baba yetu (1Yohana 3:1).
Kwahiyo tunapoingia kwenye sala/ maombi ni vizuri sana kuomba kwa kumwita muumba wako Baba kuliko Mungu, kwasababu wewe ni zaidi ya kiumbe chake bali ni mtoto wake.
Luka 11:11 “Maana ni yupi kwenu aliye baba, ambaye mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe au samaki, badala ya samaki atampa nyoka?
12 Au akimwomba yai, atampa nge?
13 Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?”
2. JINA LAKO LITAKASWE/ LITUKUZWE
Baada ya kumwita Baba aliye mbinguni kwamba atege sikio lake na kusikia maombi yetu sisi watoto wake, Hoja ya kwanza tunayopaswa tumpelekee ni kwamba JINA LAKE LITAKASWE au LITUKUZWE. Wengi hawajui kuwa jina la Mungu linachafuliwa kila siku kutokana na maovu watu wa Mungu wanayoyafanya..
Warumi 2:22 “Wewe usemaye kwamba mtu asizini, wazini mwenyewe? Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu?
23 Wewe ujisifuye katika torati, wamvunjia Mungu heshima kwa kuiasi torati?
24 KWA MAANA JINA LA MUNGU LATUKANWA KATIKA MATAIFA KWA AJILI YENU, kama ilivyoandikwa”.
Madhara ya jina la Mungu kutukanwa katika mataifa, ni watu wengi kupotea na kuifanya thamani ya msalaba isionekane.. Hivyo basi mwenye uwezo wa kulitakasa jina lake ni Mungu tu, (yeye mwenye jina), hivyo tunapochukua nafasi hiyo ya kuomba kwamba Bwana alitakase jina lake, maana yake tunaomba Mungu alete utukufu katika Injili yake.. Kwamba Bwana ajalie watu kuliogopa jina lake, kwa kuonyesha matendo makuu na ya ajabu, na hivyo wengi kutubu na kumrudishia yeye utukufu.
Kwahiyo hii inapaswa iwe sehemu ya sala kwa kila mkristo kila mahali..
3. UFALME WAKO UJE.
Siku ambayo Ufalme wa Mungu utakuja duniani ni siku ambayo Mateso yatakuwa yameisha, tabu zitakuwa zimeisha, huzuni zitakuwa zimeisha, na maumivu yatakuwa yameisha.. (hakika huo ni wakati mzuri sana). Dunia ya sasa imejaa tabu na mahangaiko na majaribu mengi.. hivyo kila siku hatuna budi kuomba kwa Baba kwamba aharakishe kuileta ile siku ambayo tutapata pumziko la hakika, dhidi ya haya majaribu mengi ya ulimwengu.
Kwa mtu ambaye anatamani kuondokana na haya maisha na kutamani kukaa na Mungu milele, basi atatumia muda wa kutosha kumwomba Bwana aulete ufalme wake. Na kwa kuomba hivi maana yake, tunaomba pia watu wengi waokolewe, kwasababu ile siku haitakuja mpaka kondoo wa mwisho aliyekusudiwa uzima wa milele, aingie ndani ya zizi.. Hivyo basi kwa kuomba ufalme wake uje basi moja kwa moja pia tutakuwa tumeomba Bwana aharakishe kuwavuta watu wake ndani ya Neema.
4. MAPENZI YAKO YATIMIZWE.
Baada ya kuomba kwamba ufalme wake uje, basi hatua inayofuata ni kuomba kwamba Mapenzi yake yatimizwe.. Tunayo mapenzi yetu (yaani matakwa yetu), lakini pia yapo mapenzi ya Mungu ambayo huwenda sisi hatuyafahamu.. Bwana Yesu kabla ya kuteswa alimwomba Baba na kusema, “kikombe hiki kiniepuka lakini si kama nitakavyo mimi bali utakavyo wewe soma Mathayo 6:39.
Na sisi hatuna budi kuomba kuwa mapenzi ya Mungu yatimizwe hapa duniani, katika shughuli zetu, katika utendaji kazi wetu, na katika mambo yote yanayoendelea, mapenzi yake yakatimizwe kama yanavyotimizwa huko mbinguni, mahali malaika walipo..
5. UTUPE LEO RIZIKI ZETU.
Baada ya kuomba mapenzi yake yatimizwe, sasa ni wakati wa sisi kupeleka haja zetu, kama chakula, mavazi, makazi, fedha, na mambo yote tunayoyahitaji katika mwili na katika roho, Baba akatupatie.. Na Mungu anayesikia maombi atatupa kama ni fedha, au chakula au makazi au malazi, vile vile katika kipengele hiki ndicho kipengele pia cha kuwaombea wengine Bwana awape pia riziki, hivyo kinaweza kuchukua muda mrefu, kulingana na haja mtu alizonazo.
6. UTUSAMEHE DENI ZETU.
Ipo tofauti ya Deni na dhambi, Mtu anaweza kusamehewa dhambi lakini Deni la adhabu lipo palepale, Daudi alisamehewa dhambi yake ya kumtwaa mke wa Uria, lakini deni la kuadhibiwa yeye na mtoto wake halikuondoka, na hapa sala ya Bwana inatuelekeza kwamba tumwombe Bwana atusamehe Deni zetu, huenda tumemkosa Mungu na tukamwomba msamaha na yeye akatusamehe lakini adhabu bado hajaiondoa.. hivyo hatuna budi kumwomba Mungu kwa kuugua sana kwamba atuondolee dhambi zetu pamoja na madeni yetu,
Hapa mtu anaweza kutumia muda mrefu, kujiombea mwenyewe na kuwaombea wengine. Lakini tunapoomba tusamehewe madeni ni sharti kwamba na sisi tuwasamehe wadeni wetu, tusipowasamehe wadeni wetu na Baba yetu aliye mbinguni hatatusamehe sisi.
7. USITUTIE MAJARIBUNI, BALI UTUOKOE NA YULE MWOVU.
Shetani anatutafuta usiku na mchana ili atuingize katika kukosa, sasa hila zote za shetani ili kutuangusha sisi ndio “majaribu yanayozungumziwa hapo”
Bwana anatufundisha kumwomba Baba, atuepushe na mitego hiyo ya mwovu, ambayo kaiweka kila mahali ili kutuangusha, na mitego hiyo shetani kaiweka makanisani, mashuleni, makazini na kila mahali.. hivyo lazima kuomba kwa muda mrefu kwaajili ya mahali ulipo, au unapokwenda ili kusudi usianguke katika mitego ya ibilisi. Na pia unapaswa uwaombee na wengine. (Wagalatia 6:2).
8. KWA KUWA UFALME NI WAKO, na Nguvu na Utukufu
Hii ni hatua ya mwisho ya kumtukuza Mungu na kumwadhimisha, na kumshukuru..hapa mtu anaweza kupaza Sauti yake kama Daudi kwa nyimbo au kwa kinywa na kusema Bwana ni mwenye Nguvu, asikiaye maombi , ajibuye maombi..Bwana ni mwenye haki, Bwana ni mwenye enzi na mamlaka..utukufu una yeye milele na milele.
Tukisali kwa namna hiyo, au kwa ufunuo huo basi tutakuwa tumeomba sawa sawa na mapenzi yake.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Kuna tofauti gani kati ya SALA na DUA?
SALA YA UPONYAJI/MAOMBI YA UPONYAJI.
NITAJUAJE KAMA MAOMBI YANGU YAMEFIKA (YAMEJITOSHELEZA)?.
(Masomo maalumu kwa wanawake)
Wanawake waombolezaji maana yake nini?, Na je hadi leo wapo?, au wanapaswa kuwepo?.
Kabla ya kuingia ndani kuhusiana na wanawake waombolezaji, hebu tujue kwanza maana ya neno kuomboleza.
Kuomboleza maana yake “ni kuingia katika sikitiko kuu, kutokana na tukio ambalo limetokea au litakalotokea!”.. Sikitiko hili linaambatana na Toba, na Majuto.
Kwamfano mtu anayeomboleza kutokana na msiba alioupata anakuwa katika hali ya huzuni kuu, akitafakari kwa undani tukio lililotokea huku akiomba rehema na msamaha kwa Mungu, na huku akiomba Mungu amponye majeraha yake na pia akiomba jambo kama hilo lisijirudie tena, (huyo ndio mtu anayeomboleza kibiblia kutokana na tukio lililotokea).Na mtu anayeomboleza kwajili ya tukio lijalo pia anakuwa katika hali hiyohiyo.
Hebu tuangalie mifano ya watu walioomboleza kabla ya tukio Fulani/msiba Fulani kutokea na watu walioomboleza baada ya Tukio kutokea.
1.KABLA YA TUKIO.
Mfano wa watu waolioomboleza kabla ya Msiba kutokea ni wana wa Israeli kipindi cha Malkia Esta, wakati ambapo waraka wa kuuawa wayahudi uliposomwa katika majimbo yote ya Mfalme Ahasuero, ambapo uliasisiwa na Hamani, aliyekuwa adui wa wayahudi.
Lakini tunasoma mara baada tu ya waraka ule kutolewa, Wayahudi wote wakiongozwa na Mordekai walifunga, kwa kulia na kuomboleza.
Esta 4:1 “Basi Mordeikai alipojua mambo yote yaliyofanyika, alizirarua nguo zake, akajivika gunia pamoja na majivu, akatoka hata kufika katikati ya mji, akalia kwa sauti kuu ya uchungu.
2 Pia akafika hata mbele ya mlango wa mfalme; maana hakuna awezaye kuingia ndani ya mlango wa mfalme hali amevaa magunia.
3 Na katika kila jimbo, ambako amri ya mfalme na mbiu yake imewasili, PALIKUWAKO MSIBA MKUU KWA WAYAHUDI, NA KUFUNGA, NA KULIA, NA KUOMBOLEZA; hata na wengi wakalala juu ya gunia na majivu”
Na matokeo ya maombolezo haya ni USHINDI KWA WAYAHUDI, na Mauti kwa maadui zao.
2. BAADA YA TUKIO.
Mfano wa maombolezo ambayo yalifanyika baada ya tukio Fulani/msiba Fulani kutokea ni yale ya NABII YEREMIA.
Baada ya wana wa Israeli, kuuawa kikatili na Mfalme Nebukadreza na baadhi yao kuchukuliwa mateka mpaka Babeli, tukio hilo lilikuwa ni tukio baya ambalo halikuwahi kutokea kama hilo katika Israeli, kwani wanawake wajawazito walipasuliwa matumbo yao, na vijana na wazee walichichwa kikatili pale Yerusalemu, na zaidi sana kundi dogo lililosalia lilipelekwa utumwani kwa aibu, kwani walikuwa uchi kabisa na wengine nusu uchi. Na wachache sana ambao walikuwa ni maskini na walemavu ndio waliobakishwa Israeli ili wayatunze mashamba.
Sasa miongoni mwa waliobaki alikuwa ni Yeremia, yeye hakuwa maskini wala mlemavu, lakini Mungu alimlinda na maangamizi hayo kwasababu alikuwa anamcha yeye, Kwasababu hiyo basi YEREMIA, baada ya kulishuhudia tukio hilo, alilia kwa machozi mengi na kuomboleza siku nyingi.. (na ndio akaandika maombolezo yake katika kitabu, ambacho ndio sisi leo tunakisoma kama kitabu cha Maombolezo).
Maombolezo 3:47 “Hofu imetujilia na shimo, Ukiwa na uharibifu.
48 Jicho langu lachuruzika mito ya maji Kwa ajili ya uvunjifu wa binti ya watu wangu.
49 Jicho langu latoka machozi lisikome, Wala haliachi;
50 Hata Bwana atakapoangalia Na kutazama toka mbinguni.
51 Jicho langu lanitia huzuni nafsini mwangu, Kwa sababu ya binti zote za mji wangu.
52 Walio adui zangu bila sababu Wameniwinda sana kama ndege”
Sasa ni Maombolezo gani kati ya hayo mawili, Mungu anayotaka sisi tuyafanye??
Jibu ni “Maombolezo ya kabla ya tukio”. Mungu hataki tuomboleze baada ya tukio, bali anataka tuomboleze kabla ya tukio..
Leo hii dunia tayari imeshatamkiwa hukumu na Mungu, huenda Taifa lako limeshatamkiwa hukumu, huenda familia yako imeshatamkiwa hukumu na Mungu, huenda Nyumba yako imeshaandikiwa hukumu na Mungu, kutokana na mambo yanayoendelea humo yasiyompendeza yeye.
Huenda Kanisa lako limeshaandikiwa hukumu, washirika wenzako wameshaandikiwa hukumu, mchungaji wako kashaandikiwa na kashakusudiwa kuadhibiwa na Mungu hapa hapa duniani kabla hata hajaondoka..Hivyo kabla hukumu hizo hazitimia, Bwana Mungu anataka tuwe na jicho la kuona na KULIA NA KUOMBOLEZA KWA TOBA NA MSAMAHA, NA KWA KUTAKA REHEMA kwa Mungu ili Mabaya haya yasitokee, Kama Akina Esta, Mordekai na Wayahudi wote walivyofanya kipindi cha Hamani.
Sasa pamoja na hayo, lipo kundi moja la Watu, ambalo ni rahisi kuzama katika Maombolezo na hata kuvuta rehema za Mungu, na fadhili za Mungu upesi.
Na kundi hilo si lingine zaidi ya kundi la Wanawake.. Mwanamke anapoomba kwa hisia (iliyo ya kiMungu), basi ni rahisi maombi yake kufika kwa Baba mbinguni zaidi ya wanaume.. Hivyo biblia imewataja wanawake kama viungo vifaavyo kusimama katika hii nafasi ya kuomboleza.
Hebu tulithibitishe hili kimaandiko…
Yeremia 9:17 “Bwana wa majeshi asema hivi, Fikirini ninyi, mkawaite wanawake waombolezao, ili waje; mkatume na kuwaita wanawake wenye ustadi, ili waje;
18 na wafanye haraka na kutuombolezea, ili macho yetu yachuruzike machozi, na kope zetu zibubujike maji.
19 Maana sauti ya maombolezo imesikiwa toka Sayuni, Jinsi tulivyotekwa! tulivyofadhaika sana! Kwa sababu tumeiacha nchi, kwa kuwa wameangusha makao yetu”.
Umeona Nafasi yako wewe mwanamke?..Wewe umewekwa na Mungu katika hilo kanisa ili ulie na kuomboleza kwaajili ya Uovu, ili Bwana akumbuke rehema, wewe umewekwa katika hilo Taifa ili ulie na kuomboleza Bwana aachilie neema na rehema.. Hiyo ndio nafasi yako ambapo usipoitumia siku ile utakwenda kuulizwa!!.
Biblia haijashindwa kuwaweka hapo wanaume, na kusema wao ndio waomboleze!!.. lakini imewaweka pembeni na kuwapa vipaumbele wanawake!..Sasa sio kwamba ina upendeleo haina upendeleo..bali ni kutokana na jinsi wanawake walivyoumbwa!.. Kadhalika mwanamke usikimbilie kuwa mchungaji, hiyo ni nafasi ya wanaume..(kasome 1Wakorintho 14:34). Kwahiyo biblia imetoa majukumu kwa kila jinsia..
Je umewahi kulia na kuomboleza kwaajili ya Nyumba yako, au kanisa lako au Taifa lako? Kama bado halafu wewe ni mwanamke unayesema umeokoka, basi badilika leo.. Litii Neno na lifuate hilo, usijiamulie utumishi au usijitwike wito ambao hujawekewa juu yako.. kaa katika nafasi yako hiyo na Mungu atakutumia.
Na baada ya kujua nafasi yako hii basi wafundishe na wanawake wengine kuwa kama wewe (mwombolezaji)..ndivyo biblia inavyoelekeza..
Yeremia 9:20 “Lakini lisikieni neno la Bwana, enyi wanawake, Na masikio yenu yapokee neno la kinywa chake; Mkawafundishe binti zenu kuomboleza, Na kila mmoja jirani yake kulia.
21 Kwa maana mauti imepandia madirishani mwetu, imeingia majumbani mwetu; Ipate kuwakatilia mbali watoto walio nje, na vijana katika njia kuu”.
Bwana akubariki.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
TUKIO LA MUSA NA ELIYA KUMTOKEA BWANA, LIMEBEBA UJUMBE GANI?
NAFASI YAKO NI IPI KATIKA MWILI WA KRISTO?
Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?
Karibu tujifunze biblia..
Daudi anasema..
Zaburi 39:4 “Bwana, unijulishe mwisho wangu, Na kiasi cha siku zangu ni kiasi gani……..”
Hapa si kwamba Daudi anataka aijue siku ya kufa kwake!, Hapana!, Mungu hajawahi kumwahidia mwanadamu hayo maarifa..(Hakuna maombi ya mtu kufunuliwa siku yake ya kufa). Bali hapo Daudi anaomba Mungu ampe KUZIJUA SIKU ZAKE DUNIANI KWAMBA SI NYINGI, Kwamba siku za mwanadamu ni kama maua! Si wa kudumu (Zaburi 103:15).
Hivyo Daudi alijua Mungu akimpa moyo wa kuelewa kuwa “Yeye ni kama mpitaji tu hapa duniani, na siku zake si nyingi”.. basi atakuwa mnyenyekevu zaidi, na ataishi maisha ya kumtafuta Mungu, kumcha Mungu na kuishi kwa hekima duniani..
Zaburi 90:12 “Basi, utujulishe kuzihesabu siku zetu, Tujipatie moyo wa hekima”.
Na sio tu yeye aliyepaswa kuomba maombi kama haya, bali hata sisi pia watu wa siku za Mwisho, ni lazima tumwombe Mungu atujulishe siku zetu! (Yaani atupe mioyo ya hekima kujua kuwa sisi ni wapitaji tu, na siku zetu za kuishi si nyingi).
Faida ya kuomba Moyo huu kutoka kwa Mungu, ni kwamba tutakuwa watu wa kutazama maisha yajayo zaidi kuliko maisha haya ya hapa duniani ya kitambo!.. Kwasababu ndani ya akili zetu tutajua kuwa siku zetu si nyingi!..kwamba siku yoyote safari ya maisha yetu itafikia mwisho.
Watu wengi wenye huu moyo, utaona ndio watu wenye mioyo ya kumtafuta Mungu kwa kujikana nafsi kwelikweli…ndio watu wenye mioyo ya kusaidia wengine, ndio watu wenye mioyo ya kuwahubiria wengine mwisho wa maisha haya.
Na watu kama hawa, hata kama wakiambiwa kuwa watapewa miaka elfu moja ya kuishi duniani, bado tu!, watajiona kuwa siku zao ni chache, kwasababu tayari ndani yao wamepewa mioyo ya “kuzihesabu siku zao na kujijua kuwa wao si kitu, ni kama maua tu, yaliyopo leo na kesho kutupwa kwenye tanuru” hivyo maisha yao yatakuwa ni yale yale siku zote ya kutafuta kutengeneza maisha yajayo ya umilele.
Shetani hapendi watu wawe na moyo huu, anataka watu wawe na moyo wa kufikiri kwamba wataishi milele katika hii dunia, hataki watu wajue kwamba siku yoyote safari ya maisha yao itafikia ukingoni, kwasababu anajua watu wakilijua hilo, basi watatengeneza maisha yao hapa kwaajili ya huko waendako, na hivyo atawapoteza wengi. Na yeye (shetani) hataki kumpoteza mtu hata mmoja, anataka wote waende katika ziwa la moto kama yeye!!.
Kwahiyo kila siku ni muhimu sana kuomba Bwana atupe huu moyo.. “Atujulishe miisho yetu, na siku zetu za kuishi” ili tufahamu kuwa “sisi ni wapitaji tu”.
Moyo huu utaupata kwa kufanya mambo yafuatayo matatu (3)
1.Kwa kuomba
Majibu ya mambo yote tunayapata katika maombi, kama vile Sulemani alivyoomba kwa Mungu apewe moyo wa hekima na Mungu akamsikia, vile vile pia Moyo wa kujua kuwa wewe ni mpitaji tu, unatoka kwa Bwana, ndio maana hata hapo Daudi anaonekana kama anaomba.. “Bwana nijulishe”..Na wewe siku zote sema “Bwana nijulishe”
2. Kwa kutafakari matukio ya vifo yanayotokea.
Unapotenga muda wa kutafakari matukio ya Ajali yanayotokea, au unapotazama wagonjwa mahututi, au unapokwenda kwenye nyumba za misiba..sehemu hizo ni sehemu ambazo Mungu anaitengeneza mioyo ya wengi.. Hivyo na wewe huna budi kuhudhuria misiba, au kufuatilia matukio (Wengi hawapendi kufuatilia haya), kwasababu hawataki kuumia moyo, lakini ndani ya mioyo yao wana viburi vya maisha, wanajiona kama wao wataishi milele.. Biblia inatufundisha pia tuhudhurie sehemu za Misiba, sio kwenye karamu tu, ili tukajifunze huko..
Mhubiri 7:2 “Heri kuiendea nyumba ya matanga, Kuliko kuiendea nyumba ya karamu. Kwa maana huo ndio mwisho wa wanadamu wote, naye aliye hai atautia moyoni mwake.
3 Huzuni ni afadhali kuliko kicheko, Maana simanzi ya uso ni faida ya moyo”.
3. Kwa kusoma Neno.
Unaposoma Biblia, huko ndiko utakapopata Maarifa kamili ya Neno la Mungu, na maneno ya kuunyenyekeza moyo wako, biblia ndio kioo kamili cha kujijua wewe ni nani?.. ukitaka kujijua wewe ni mtu wa namna gani, basi soma Biblia.
Bwana atubariki.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?
KWA MIOYO YAO WAKAREJEA MISRI.
Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?
REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.
Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?
Yakobo 1:13 “Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu”
Hapo Neno linasema kuwa Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, kinyume chake ni kweli kwamba yeye anajaribiwa na MEMA tu!. Maana yake tunapofanya mema hapo tunakuwa tunamweka Mungu kwenye jaribu la kutubariki.. Na hivyo ni lazima aachie baraka kwetu.
Lakini tukienda kinyume na Neno lake na huku tunataka atubariki, hapo maana yake tunamjaribu yeye kwa Maovu.. Mfano wa watu waliomjaribu Mungu kwa maovu ni Wana wa Israeli kipindi wapo jangwani, Walitaka Bwana awashushie chakula kile cha kimiujiza, huku mioyoni mwao wamemwacha Mungu, ni watu wenye viburi, ni watu wa kunung’unika, ni watu wasio na heshima wala staha kwa Mungu na mwishowe wakaangukia hukumu.
Waebrania 3:7 “Kwa hiyo, kama anenavyo Roho Mtakatifu, Leo, kama mtaisikia sauti yake,
8 Msifanye migumu mioyo yenu, Kama wakati wa kukasirisha, Siku ya kujaribiwa katika jangwa,
9 Hapo baba zenu waliponijaribu, wakanipima, Wakaona matendo yangu miaka arobaini.
10 Kwa hiyo nalichukizwa na kizazi hiki, Nikasema, Sikuzote ni watu waliopotoka mioyo hawa; Hawakuzijua njia zangu;
11 Kama nilivyoapa kwa hasira yangu, Hawataingia rahani mwangu”.
Na maandiko yanasema Mungu ni yeye Yule jana na leo na hata milele, alilolikataza miaka elfu 2 iliyopita analitakata hata leo.. Akisema “yeye hajaribiwi na Movu, ni kweli hajaribiwi na hayo”.. Lakini kinyume chake anajaribiwa na Mema yaliyoandikwa katika Neno lake.
Kwamfano unapomtolea Mungu sadaka isiyo na kasoro (Maana yake iliyo sawasawa na Neno lake, na kwa nia njema) Hilo ni jaribu kwa Mungu kukubariki wewe, na hapo utakuwa umemjaribu kwa Mema.
Malaki 3:8 “Je! Mwanadamu atamwibia Mungu? Lakini ninyi mnaniibia mimi. Lakini ninyi mwasema, Tumekuibia kwa namna gani? Mmeniibia zaka na dhabihu.
9 Ninyi mmelaaniwa kwa laana; maana mnaniibia mimi, naam, taifa hili lote.
10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.
11 Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu; wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake katika mashamba, asema Bwana wa majeshi”.
Na mambo mengine yote mema, ambayo tunayafanya yaliyo sawasawa na Neno la Mungu, mambo hayo ni TANZI kwa Mungu, kutumwagia Baraka zake, au kuzungumza na sisi.
Lakini kama moyoni mwako umemwacha Bwana, halafu unatafuta kuisikia sauti yake, unaenda kwa nabii ili usikie Mungu anasema nini kuhusu wewe, hapo unamjaribu Mungu kwa mabaya na hivyo unajitafutia laana badala ya Baraka.
Ezekieli 14:4 “Basi sema nao, uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Kila mtu wa nyumba ya Israeli atwaaye vinyago vyake na kuvitia moyoni mwake, na kuliweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake, na kumwendea nabii; mimi, Bwana, nitamjibu neno lake sawasawa na wingi wa sanamu zake;
5 ili niwakamate nyumba ya Israeli kwa mioyo yao wenyewe, kwa sababu wamefarakana nami kwa vinyago vyao.
6 Kwa sababu hiyo uwaambie nyumba ya Israeli, Bwana MUNGU asema hivi; Rudini ninyi, mkageuke na kuviacha vinyago vyenu; mkageuze nyuso zenu zisielekee machukizo yenu yote.
7 Kwa maana kila mtu wa nyumba ya Israeli, au wa wageni wakaao katika Israeli, ajitengaye nami, na kuvitwaa vinyago vyake na kuvitia moyoni mwake, na kuliweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake, kisha kumwendea nabii, na kuniuliza neno kwa ajili ya nafsi yake; mimi, Bwana, nitamjibu, mimi mwenyewe
8 nami nitaukaza uso wangu juu ya mtu yule, na kumfanya kuwa ajabu, awe ishara na mithali, nami nitamkatilia mbali, asiwe kati ya watu wangu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.”
Bwana Yesu atusaidie.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Je Adamu na Hawa, walikuwa hawafanyi mema kabla ya kula tunda?
DAMU YA YESU INANENAJE MEMA KULIKO YA HABILI?
Jina la Bwana na Mwokozi, Mkuu wa Uzima, Yesu Kristo lihimidiwe!..karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu.
Upo wakati ambao TAA ya Mungu itazima!.. Tuitikie wito wa Mungu, kabla ya huo wakati kufika..
1Samweli 3:2 “Ikawa wakati huo, Eli alipokuwa amelala mahali pake (tena macho yake yalikuwa yameanza kupofuka, hata asiweze kuona),
3 NA TAA YA MUNGU ILIKUWA HAIJAZIMIKA BADO, na Samweli alikuwa amelala katika hekalu la Bwana, palipokuwa na sanduku la Mungu;
4 basi, wakati huo Bwana akamwita Samweli; naye akasema, Mimi hapa.”
Sasa ili kuelewa vizuri Taa ya Mungu ni kitu gani, na ilikuwa inazimika wakati gani..hebu turejee ile Hema ambayo Musa aliagizwa aitengeneze, tunasoma Ilikuwa imegawanyika katika Sehemu kuu tatu, Ua wa Ndani, Patakatifu na Patakatifu pa patakatifu.
Na ndani katika Patakatifu, palikuwa na madhabahu ya uvumba, Meza ya mikate ya wonyesho pamoja na KINARA CHA TAA, ambacho kilikuwa na Mirija saba. (Tazama picha juu).
Hiki kinara cha Taa kazi yake ilikuwa ni kutia Nuru ile hema wakati wa USIKU. Kwamba Nyakati zote za usiku ni sharti ndani ya Hema kuwe na Nuru, na amri hiyo ilikuwa ni ya Daima, maana yake ya kila siku!.. haikupaswa hata Usiku mmoja upite bila Kinara hicho kuwashwa ndani ya Hema.
Kutoka 27: 20 “Nawe waamuru wana wa Israeli wakuletee mafuta ya zeituni safi ya kupondwa kwa ajili ya nuru, ili kufanya ile taa kuwaka daima.
21 Ndani ya ile hema ya kukutania, nje ya hilo pazia, lililo mbele ya huo ushuhuda, Haruni na wanawe wataitengeza TANGU JIONI HATA ASUBUHI MBELE YA BWANA; itakuwa ni amri ya milele katika vizazi vyao vyote kwa ajili ya wana wa Israel”
Tusome tena..
Walawi 24:1 “Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
2 Waagize wana wa Israeli kwamba wakuletee mafuta ya zeituni safi ya kupondwa kwa ajili ya ile nuru, ili hiyo taa iwake daima.
3 Hapo nje ya pazia la ushahidi, ndani ya hema ya kukutania, Haruni ataitengeza TANGU JIONI HATA ASUBUHI MBELE ZA BWANA DAIMA; ni amri ya milele katika vizazi vyenu”
Hapo mstari wa 3, unasema ataitengeneza “tangu jioni hata asubuhi” maana yake wataiwasha tangu jioni mpaka asubuhi, na kukiisha pambazuka basi taa ile inazimwa, kwasababu kulikuwa na Nuru ya mwanga wa Nje wa jua iliyokuwa inaingia ndani ya Hema.
Sasa tukirudi katika habari hiyo ya Samweli, maandiko yanasema Samweli alikuwa analala katika Hema karibu na sanduku la BWANA, na wakati ambapo Taa ya Mungu bado haijazimika..Maana yake bado hakujapambazuka, (kwasababu kukisha pambazuka tu, tayari ile taa ilikuwa inazimwa).
Wakati huo ndipo Samweli aliisikia Sauti ya Mungu ikimwita mara 4, na Samweli akaitikia wito wa Mungu.
Lakini ni nini tunajifunza katika hiyo habari?
Upo wakati ambao sauti ya Mungu inaita juu ya Mtu..na wakati huo ni wakati wa giza Nene juu ya maisha ya mtu.. Huo ndio wakati ambapo Mungu anamwita mtu, na anamwita kwa sauti ambayo inakuwa inayofanana na ya watu wa Mungu.. kiasi kwamba mtu anaweza kudhani ni mtu anayemwita/kumshawishi kumbe ni Mungu, ndio maana Samweli alipoitwa alikimbilia kwa Eli akidhani ni Eli anayemwita kumbe ni MUNGU.
Vile vile Mungu anawaita leo watu kutoka katika dhambi, na uvuguvugu lakini watu wanadhani ni wachungaji wao ndio wanaowaita, wengine wanadhani ni wahubiri ndio wanaowatafuta wawe washirika wao, pasipo kujua kuwa ni sauti ya Mungu ndio inayowaita na si watu.
Sasa endapo Samweli asingeitikia ule wito wakati ule ambapo TAA BADO HAIJAZIMIKA, huenda ile sauti ya Mungu asingeisikia tena kwa wakati ule mpaka labda kipindi kingine ambapo Taa hiyo itakuwa inawaka.
Ndugu TAA ya Mungu leo ni NEEMA, Hii Neema kuna wakati itasimama!, na hakutakuwa tena na nafasi ya kumkaribia Mungu, wakati ambao unyakuo wa kanisa utapita, ndio wakati ambao TAA itakuwa imezima, vile vile wakati ambao utaondoka katika haya maisha huo ndio wakati ambao Taa ya Mungu itakuwa imezimika juu yako.
Je umemkabidhi Yesu maisha yako?.. Umebatizwa katika ubatizo sahihi? Umeokoka?.. Kama bado ni vyema ukafanya hivyo sasa kabla Taa haijazimika.
Mhubiri 12:1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo.
Maran atha!
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Hema ya kukutania ni nini, na ilikuwaje?
Kiango na Pishi ni nini (Mathayo 5:15)?
NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA-KONDOO.
Thenashara ni neno la kiebrania linalomaanisha namba “kumi na mbili” (12). Kwahiyo badala ya kusema watu 12, ni sahihi kabisa kusema “watu Thenashara”, au badala ya kusema “miezi 12” ni sahihi kusema “miezi Thenashara”…badala ya kusema makabila 12 ni sawa na kusema “Makabila thenashara” n.k
Biblia imelitumia Neno hilo Thenashara kuwakilisha wale Wanafunzi 12 wa Bwana Yesu, ambao baadaye waliitwa Mitume.
Marko 3:16 “Akawaweka wale Thenashara; na Simoni akampa jina la Petro;
17 na Yakobo, mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye Yakobo, akawapa jina la Boanerge, maana yake, wana wa ngurumo;
18 na Andrea, na Filipo, na Bartholomayo, na Mathayo, na Tomaso, na Yakobo wa Alfayo, na Thadayo, na Simoni Mkananayo,
19 na Yuda Iskariote, ndiye aliyemsaliti. Kisha akaingia nyumbani”
Na ni kwanini wanafunzi hawa 12, watenganishwe kwa kuitwa hivyo Thenashara?.. Ni kwasababu Bwana Yesu alikuwa anao wanafunzi wengine wengi zaidi ya 70,
Luka 10:1 “Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.”
hivyo ili kuwatofautisha hawa wanafunzi 70 na wale 12 aliowateua kwanza kndio likatumika hilo neno “Thenashara”
Unaweza kulisoma neno hilo pia katika Mathayo 26:14-16, Marko 4:10, Marko 9:35, na Yohana 20:24
Je umefanyika kuwa Mwanafunzi wa Yesu? kwa kutubu dhambi zako zote, na kumaanisha kuziacha na vile vile kuchukua msalaba wako na kumfuata yeye?
Luka 14:27 “Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Wahuni ni watu gani katika biblia?
Jibu: Kutoka 40:20 “Akautwaa ule ushuhuda, akautia ndani ya sanduku, akaiweka miti ya kuchukulia juu ya sanduku, akakiweka kiti cha rehema juu ya sanduku”.
Kiti cha Rehema kilichokuwa juu ya Sanduku la Agano hakikuwa “kiti” kama viti hivi tuvijuavyo, vyenye miguu minne, na vyenye nafasi ya Mtu kuketi.. Bali neno “kiti” kama lilivyotumika hapo limemaanisha “Nafasi ya wazi”.
Kwahiyo juu ya sanduku la Agano hakukuwa na Kitu Fulani mfano wa “Stuli” juu yake, hapana! bali palikuwa na nafasi wazi ambayo ndiyo iliyoitwa “kiti cha rehema”. Nafasi hiyo ilikuwa ipo katikati ya wale Makerubi wawili wa dhahabu ambao walikuwa wanatazamana, na mbawa zao kukutana kwa juu na kuifunika hiyo sehemu ya wazi (yaani kiti cha rehema).
Nafasi hiyo haikuwa kubwa sana, na pia ilikuwa ni sehemu ya mfuniko wa Sanduku zima (maana yake wale Makerubi wawili pamoja na kile kiti cha rehema vilikuwa vimeungana, na kwa pamoja kufanya mfuniko wa sanduku), na ndani ya sanduku kulikuwa na Mana, zile Mbao za mawe zenye amri kumi pamoja na ile fimbo ya Haruni iliyochipuka. (Tazama picha juu).
Hivyo ulipofika muda wa Upatanisho, Kuhani Mkuu aliingia na damu Ng’ombe na kwenda kuinyunyiza juu ya kiti cha rehema mara saba, na damu hiyo inakuwa ni upatanisho kwa wana wa Israeli, dhidi ya dhambi zao.
Walawi 16: 14 “Kisha atatwaa baadhi ya damu ya yule ng’ombe, na kuinyunyiza kwa kidole chake juu ya kiti cha rehema upande wa mashariki; na mbele ya kiti cha rehema atainyunyiza ile damu kwa kidole chake mara saba”.
Katika Agano la kale, Israeli walikitazama hicho kiti cha Rehema kama kitovu chao cha kwenda kupata msamaha, kupitia kuhani mkuu wao aliyeteuliwa kwa wakati huo.
Lakini kiti hicho cha rehema kilikuwa na mapungufu yake, kwasababu watu hawakuwa wanapata msamaha wa dhambi, bali dhambi zao zilikuwa zinafunikwa tu!, na kulikuwa na kumbukumbu la dhambi kila mwaka….kwamaana damu za Ng’ombe na Kondoo haziwezi kuondoa dhambi za mtu, vile vile Makuhani wa kibinadamu ambao nao pia wamejaa kasoro hawawezi kuwapatanisha wanadamu na Mungu, kwasababu wao pia ni wakosaji!.. Na pia kiti cha rehema ambacho kipo duniani, kilichotengenezwa na mikono ya wanadamu hakiwezi kufanya utakaso mkamilifu wa dhambi, kwasababu na chenyewe kimetengenezwa na mikono ya watu wenye dhambi..
Hivyo ni lazima kiihitajike kiti kingine cha Rehema kilicho kikamilifu ambacho hakijatengenezwa na mikono ya wanadamu, na vile vile ni lazima ipatikane damu kamilifu ya Mwanadamu asiye na kasoro, na hali kadhalika ni lazima apatikane kuhani Mkuu ambaye hana dhambi..Ndipo UTAKASO na UPATANISHO WA MWANADAMU UWE KAMILI.
Na kiti hicho cha Rehema kipo Mbinguni sasa, na kuhani Mkuu mkamilifu tayari tumepewa, ambaye si mwingine zaidi ya YESU, na damu kamilifu isiyo na kasoro imeshamwagwa kwaajili yetu, na damu hiyo si NYINGINE ZAIDI YA DAMU YA YESU. Hivyo Msamaha mkamilifu unapatikana sasa, na upatanisho mkamilifu unapatikana sasa kupitia Damu ya YESU, kwa kila aaminiye.
Waebrania 9:11 “Lakini Kristo akiisha kuja, ALIYE KUHANI MKUU wa mambo mema yatakayokuwapo, kwa HEMA ILIYO KUBWA NA KAMILIFU ZAIDI, isiyofanyika kwa mikono, maana yake, isiyo ya ulimwengu huu
12 wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali KWA DAMU YAKE MWENYEWE aliingia mara moja tu katika Patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele”.
Je umemwamini Yesu na kuoshwa dhambi zako? Na kupata ukombozi mkamilifu?. Kama Bado unasubiri nini? Kiti cha Rehema kipo wazi sasa, lakini hakitakuwa hivyo siku zote, siku si nyingi baada ya unyakuo kupita mlango wa Neema utafungwa.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
NJIA NYINGINE YA KUPATA REHEMA NA KIBALI KUTOKA KWA MUNGU.
Jibu: Tusome kuanzia mstari wa kwanza..
Matendo 23:1 “Paulo akawakazia macho watu; wa baraza, akasema, Ndugu zangu, mimi kwa dhamiri safi kabisa nimeishi mbele za Mungu hata leo hivi.
2 Kuhani Mkuu Anania akawaamuru wale waliosimama karibu naye wampige kinywa chake.
3 Ndipo Paulo akamwambia, Mungu atakupiga wewe, UKUTA ULIOPAKWA CHOKAA. Wewe umeketi kunihukumu sawasawa na sheria, nawe unaamuru nipigwe kinyume cha sheria?”
Makaburi ya zamani sio kama ya zama hizi.. Haya ya wakati yanachimbwa kuelekea chini, na mtu anawekwa kwenye jeneza na kisha kufukiwa chini, lakini makaburi ya zamani hayakuwa hivyo.. Bali yalikuwa katika mfumo wa pango, ambayo linafunguliwa na watu wanawekwa ndani ya hayo mapango, na kisha kwa nje yanarembwa kwa kupakwa chokaa au rangi nyingine ya kuvutia.
Sasa Bwana Yesu alitumia mfano wa makaburi hayo yaliyopakwa chokaa, ambayo kwa nje yanaonekana ni mazuri na kuvutia kana kwamba kuna kitu cha thamani ndani, kumbe ndani yake ni mifupa tu imejaa. Alitumia mfano huo kuwalinganisha na watu ambao kwa mwonekano wa nje wanaonekana wanafaa, wanaonekana na wacha Mungu, wanaonekana ni Watumishi wazuri, wanaonekana ni waimbaji wazuri, ni wakristo wa zuri, kumbe ndani yao ni MIFUPA TU!.. Ni wanafiki.. Bwana alisema Ole wa hao!!.
Mathayo 23;27 ‘Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mmefanana na MAKABURI YALIYOPAKWA CHOKAA, nayo kwa nje yaonekana kuwa mazuri, bali ndani yamejaa MIFUPA YA WAFU, na uchafu wote.
28 Vivyo hivyo ninyi nanyi, kwa nje mwaonekana na watu kuwa wenye haki, bali ndani MMEJAA UNAFIKI NA MAASI’.
Hizo ndizo tabia walizokuwa nazo makuhani na mafarisayo wa wakati huo, walikuwa wamejaa unafiki ndani yao, na wana maasi mengi ingawa kwa nje wanasifiwa na watu wote!!.
Na katika siku hizi zetu tunazoishi, mambo haya haya yanajirudia katikati ya watu wa Mungu.. tunaonekana kwa nje ni wakristo wazuri, ni wahubiri wazuri, ni waimbaji wazuri…lakini ndani tuna unafiki uliopitiliza.. Ndani tumejaa viburi, uongo, kutokusamehe, vinyongo, visasi na kila aina ya uchafu!
Bwana Yesu atusaidie tusiwe kuta zilizopakwa chokaa, bali tuwe wakamilifu nje na ndani..
1Wathesalonike 5:22 “jitengeni na ubaya wa kila namna.
23 Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi NAFSI ZENU NA ROHO ZENU NA MIILI YENU mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo”.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
MAKABURI YAKAFUNUKA; IKAINUKA MIILI MINGI YA WATAKATIFU WALIOLALA;
HAPAKUWA NA NAFASI YA KUPITA KWA YULE MNYAMA ALIYEKUWA CHINI YANGU.
EZEKIELI, ITABIRIE MIFUPA MIKAVU.
Wakati ni “kipindi cha Muda” kwa kusudi Fulani, Kwamfano ukipanga kesho saa 7 mchana uende sokoni kununua bidhaa.. sasa huo muda wa “Saa 7 mchana” ndio unaoitwa “wakati wa kwenda kununua bidhaa”
Lakini “Majira” ni kipindi cha Muda ambacho ni cha “Msimu” Kwamfano Msimu wa mvua za masika hayo ni “majira ya masika”..msimu wa matunda ya maembe “hayo ni majira ya maembe”.. Msimu wa baridi, unaitwa “Majira ya baridi”.. Msimu wa joto huo unaitwa “majira ya joto”.
Mwanzo 8:22 “Muda nchi idumupo, MAJIRA YA KUPANDA, na mavuno, wakati wa baridi na wakati wa hari, wakati wa kaskazi na wakati wa kusi, mchana na usiku, havitakoma”
Sulemani alizidi kuliweka hili vizuri kitabu cha Mhubiri..
Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna MAJIRA YAKE, Na WAKATI kwa kila kusudi chini ya mbingu.
2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa;
3 Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;
4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza”
Unaweza kusoma zaidi juu ya Majira na Nyakati katika Mwanzo 7:21, Zaburi 1:3, Walawi 15:25, na Ayubu 39:1.
Lakini pia yapo majira na nyakati katika makusudi ya Mungu. Na kusudi kuu ambalo ni muhimu kulijua majira yake ya kurudi kwa BWANA YESU MARA YA PILI!.. Hatuwezi kujua “Wakati” lakini “majira” ya kurudi kwake, tunaweza kuyajua… Ni kama vile hatuwezi kujua siku au wakati mvua itanyesha, lakini tunajua msimu, kuwa tukishaufikia huo msimu basi tunajua siku yoyote mvua itaanza kunyesha.
Vile vile Bwana Yesu hakutoa wakati wa kurudi kwake, lakini alitoa “MAJIRA” Kwamba tuyafikiapo hayo majira basi tutajua kuwa WAKATI wowote atatokea mawinguni.
Marko 13:32 “Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba.
33 Angalieni, kesheni, [ombeni], kwa kuwa hamjui WAKATI ule utakapokuwapo”
Sasa Majira ya kurudi kwake ni yapi, ambayo tukiyatazama tutajua kuwa yupo mlangoni?.
Si mengine zaidi ya yale tunayoyasoma katika Mathayo 24, Luka 21 na Marko 13... kwamba kutatokea “Tauni” mahali na mahali, kutasikika tetesi za vita mahali na mahali, kutatokea na magonjwa mfano wa Tauni mahali na mahali, vile vile kutatokea na manabii wengi wa uongo ambao watawadanganya wengi na upendo wa wengi utapoa na maasi yataongezeka.
Hivyo tukishaona hizo dalili basi tunajua kuwa tayari tumeingia katika MAJIRA YA KURUDI KWAKE…na kwamba wakati wowote atatokea mawinguni, na hivyo tunapaswa tuchukue tahadhari… Na majira yenyewe ndio haya tuliyopo mimi na wewe..
Ndugu yangu Yesu anarudi wakati wowote!!, na yeye mwenyewe alituonya tuwe macho!, tukeshe katika roho kila siku, ili siku ile isije ikatujia ghafla..
Lakini tukifumba macho yetu na kukataa kuyatazama haya majira na kuchukua tahadhari.. basi tutaangukia katika like kundi la wanafiki Bwana Yesu alilolitaja katika Luka 12:54-56 na siku ile itatujia ghafla na hatutapona.
Luka 12:54 “Akawaambia makutano pia, Kila mwonapo wingu likizuka pande za magharibi mara husema, Mvua inakuja; ikawa hivyo.
55 Na kila ivumapo kaskazi, husema, Kutakuwa na joto; na ndivyo ilivyo.
56 Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa nchi na mbingu; imekuwaje, BASI, KUWA HAMJUI KUTAMBUA MAJIRA HAYA?”
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
WAKATI ULIOKUBALIKA NALIKUSIKIA
Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?
KUNA NGUVU YA ZIADA KATIKA KULING’ANG’ANIA KUSUDI LA MUNGU.