Category Archive Uncategorized @sw-tz

MGAWANYIKO WA ISHARA ZA UJIO WA BWANA YESU KRISTO.

Ujio wa BWANA YESU duniani umegawanyika katika sehemu kuu Tatu (3).

Sehemu ya Kwanza: Ni kuzaliwa kwake kupitia bikira Mariamu.

Luka 1:30 “Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.

31 Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu.

32 Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake”

Sehemu ya Pili: Unyakuo wa kanisa.

Luka 17:34 “Nawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa katika kitanda kimoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.

35 Wanawake wawili watakuwa wakisaga pamoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.

36 Watu wawili watakuwa shambani, mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.

Unyakuo wa kanisa utakapotokea si kila mtu atajua, na si kila mtu atamwona BWANA YESU, isipokuwa wale tu watakaonyakuliwa na wafu waliokufa katika Bwana… wengine wataendelea na shughuli zao, na biashara zao, na usingizi na wengine waliokufa nje ya Kristo wataendelea katika mauti zao. Na Hatua hii ndiyo tunayoingojea sasa, na hata mmoja wetu hapaswi kuikosa!.

Sehemu ya Tatu: Ujio wa utawala wa miaka elfu moja ambapo kila jicho litamwona.

Ufunuo 1:7 “Tazama, yuaja na mawingu; na kila jicho litamwona, na hao waliomchoma; na kabila zote za dunia wataomboleza kwa ajili yake. Naam. Amina”

Hiki ni kipindi ambacho, wale wote waliosalia kwasababu ya kuukosa unyakuo, na wakabaki kuipokea ile chapa ya mnyama, baadhi yao watakufa katika ile hukumu ya mataifa, na wachache watakaosalia basi watamwona BWANA YESU mawinguni akija kwa nguvu nyingi, na utukufu mwingi, kama umeme wa radi, na wataangamia kwa mwako wake. Na Lengo la KRISTO kuja ni kwaajili ya ule utawala wa miaka elfu unaotajwa katika Ufunuo 20.

> Sasa ZIPO ISHARA ZILIZOTANGULIA KUJA KWA KWANZA KWA KRISTO (yaani kipindi Bwana YESU anazaliwa).

> Na pia ZIPO ISHARA ZINAZOTANGULIA KUJA KWA PILI KWA KRISTO (yaani kipindi cha unyakuo wa kanisa).

> Na pia ZIPO ISHARA ZINAZOTANGULIA KUJA KWA TATU WA KRISTO (yaani kipindi cha utawala wa miaka Elfu, ambapo kila jicho la watakaokuwepo duniani litamwona.)

Kwa ufupi sana tuzitazame ishara hizo au dalili hizo.

1. Ishara za kuja kwa kwanza: Kuzaliwa kwa Bwana.

Ishara kuu ya kuja kwa kwanza, au kukaribia kutokea kwa Bwana duniani ni UJIO WA ELIYA, kwani maandiko yalitabiri kwamba kabla ya kuzaliwa kwa Masihi basi Bwana Mungu atamtuma kwanza mjumbe atakayetangulia kumtengenezea njia, ambaye huyo atakuwa na roho ya Eliya ndani yake, na huyo hakuwa mwingine Zaidi ya Yohana Mbatizaji.

Luka 1:13 “Lakini yule malaika akamwambia, Usiogope, Zakaria, maana dua yako imesikiwa, na mkeo Elisabeti atakuzalia mtoto mwanamume, na jina lake utamwita Yohana.

14 Nawe utakuwa na furaha na shangwe, na watu wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.

15 Kwa sababu atakuwa mkuu mbele za Bwana; hatakunywa divai wala kileo; naye atajazwa Roho Mtakatifu hata tangu tumboni mwa mamaye.

16 Na wengi katika Waisraeli atawarejeza kwa Bwana Mungu wao.

17 NAYE ATATANGULIA MBELE ZAKE KATIKA ROHO YA ELIYA, na nguvu zake, ili kuigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto, na kuwatilia waasi akili za wenye haki, na kumwekea Bwana tayari watu waliotengenezwa”

Soma pia Mathayo 11:10 na Mathayo 17:10-13, utaona ishara ya ujio wa Yohana mbatizaji kama Eliya.

Hivyo Yohana Mbatizaji alikuwa ni ishara ya kuja kwa Bwana dunia kwa mara ya kwanza kupitia kuzaliwa katika tumbo la bikira.

Na wote walioweza kumwelewa Yohana kiufunuo, walijua kuwa Masihi amekaribia kutokea au hata tayari kashatokea yupo duniani.

2. Ishara ya kuja kwa Pili: Yaani Unyakuo wa kanisa.

Kabla ya kanisa kunyakuliwa yapo mambo yatakayotangulia kutokea yatakayotambulisha kuwa ule wakati umekaribia au umeshafika, na mambo hayo ni baadhi ya yale yaliyotajwa katika Mathayo 24, na Luka 21 na Marko 13, ambayo ni Tetesi za vita, upendo wa wengi kupoa, maasi kuongezeka na kuzuka kwa manabii wa uongo, ambao watadanganya hata yamkini walio wateule.

Mathayo 24:4 “Yesu akajibu, akawaambia, Angalieni, mtu asiwadanganye.

5 Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ni Kristo; nao watadanganya wengi.

6 Nanyi mtasikia habari za vita na matetesi ya vita; angalieni, msitishwe; maana hayo hayana budi kutukia; lakini ule mwisho bado.

7 Kwa maana taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali.

8 Hayo yote ndiyo mwanzo wa utungu”.

Ishara hizi hata sasa zimeshatokea, hivyo tumeukaribia sana unyakuo.

Hivyo kwa walio na macho ya rohoni, wakiziona hizo wanatambua kuwa wapo katika siku za kurudi kwa YESU kwa pili na wakati wowote unyakuo unatokea.

3. Ishara ya kutokea kwa tatu kwa Bwana: Kila jicho litamwona.

Huu ni wakati ambao kanisa limeshanyakuliwa, na dhiki kuu imepita, na KRISTO anarejea kwaajili ya utawala wa miaka elfu (na atarejea pamoja na watakatifu walionyakuliwa) sawasawa na ufunuo wa Yuda 1:14.

Na atakaporudi basi wale waliomchoma mkuki ubavuni (wakiwakilisha wale wote waliomkataa, waliopo duniani) wataomboleza na kulia, na wataharibiwa kwa mwako wa ujio wake.

Sasa zipo ishara zitakazotangulia kabla ya yeye kutokea mawinguni, na hizi kanisa hawataziona kwani tayari walishanyakuliwa, bali watakaoziona ni wale watakaokuwa wamesalia dunia na kuipokea chapa ya mnyama.

Luka 21:25 “ Tena, kutakuwa na ishara katika jua, na mwezi, na nyota; na katika nchi dhiki ya mataifa wakishangaa kwa uvumi wa bahari na msukosuko wake;

26 watu wakivunjika mioyo kwa hofu, na kwa kutazamia mambo yatakayoupata ulimwengu. Kwa kuwa nguvu za mbinguni zitatikisika.

27 Hapo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika wingu pamoja na nguvu na utukufu mwingi”.

Na moja ya ishara hizo, zitakazotangulia ambazo zitawafanya watu wa mataifa wavunjike mioyo na kuwaza ni nini kitaukumba dunia, ni jua kuzima (kuwa jeusi) pamoja na mwezi kuwa damu na nyota kuanguka.

Mathayo 24:29 “Lakini mara, baada ya dhiki ya siku zile, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka mbinguni, na nguvu za mbinguni zitatikisika;

30 ndipo itakapoonekana ishara yake Mwana wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa yote ya ulimwengu watakapoomboleza, nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi.

31 Naye atawatuma malaika zake pamoja na sauti kuu ya parapanda, nao watawakusanya wateule wake toka pepo nne, toka mwisho huu wa mbingu mpaka mwisho huu”.

Soma pia Isaya 13:9-12 na Ufunuo 6:12-17 utaona unabii wa ishara hiyo na hofu ya mataifa.

Kumbuka tena: Kanisa litakalokwenda kwenye unyakuo halitaona ishara hii ya jua kutiwa giza, na mwezi kuwa damu na nyota kuanguka, kwani ishara hizi zitatokea baada ya dhiki kuu, ambapo kanisa litakuwa halipo, limeenda kwenye unyakuo.

Ndio zaweza kuonekana ishara chache chache mfano wa hizo kama ile iliyotokea katika sehemu za Ulaya mwaka 1780, ambapo giza lilionekana katika sehemu za uingereza, lakini kwa habari ya jua lote kuwa giza, na nyota kuanguka, ni jambo ambao kanisa halitalishuhudia.

Je umempokea YESU na unao uhakika kwamba akirudi leo utaenda naye kwenye unyakuo?.. Kama huna uhakika huo, basi utafute kwa bidii sana.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

FAHAMU KURUDI KWA YESU KUKO KWA NAMNA NGAPI?

MFANYE BWANA YESU MWENYEJI MAISHANI MWAKO.

Je kuwashwa mkono ni ishara ya kupata pesa?

UNYAKUO WA KANISA UMEPITA LEO!!

Bwana Yesu alikuwa anamaanisha nini kusema Marko 2:19″walioalikwa harusini wawezaje kufunga maadamu bwana-arusi yupo pamoja nao?”

Rudi Nyumbani

Print this post

Je! ndoa ni lazima ifungwe kanisani? kama ndio, imeandikwa wapi?

SWALI: Je! tunalisoma wapi kwenye maandiko panasema ndoa inapaswa ifungwe kanisani. Utaratibu huo upoje?


JIBU: Ili kujibu swali hili tuanzie mbali kidogo.

kufahamu ndoa ni nini? aina za ndoa, kisha mahali sahihi pa kufungia ndoa ni wapi?.

Ndoa ni nini?

Ndoa ni muunganiko kati ya watu wawili(mwanaume na mwanamke ) unaotambulika na kuheshika kijamii, au kisheria.

Pale mwanaume anapomwona mwanamke na kupatana naye waishi pamoja kama mume na mke, kwa kufuata taratibu husika za kijamii, labda kukutanishwa kwanza wazazi, au walezi, wazee wa ukoo, kupokea mahari, kisha kuidhinisha jambo hilo, au serikali kuidhinisha, hiyo tayari inaitwa ndoa.

Aina mbili za ndoa.

  1. Ndoa za wapagani
  2. Ndoa za kikristo.

Ndoa za wapagani. Hizi ni ndoa lakini hazijadhibitiwa na kanuni timilifu za Mungu. Mfano wa hizi, ndio hizo kama za kijamii, na kiserikali, au za dini nyingine zote mfano wa ki-hindu, kiislamu, ki-budha n.k. zote hizi ni ndoa za wapagani.

Zingatia: (Hapa hatumaanishi zile za mashetani, kama za jinsia moja, au za wanadamu na wanyama hapana kwasababu hizo sio ndoa, bali tunazungumzia hizi za kawaida kabisa za asili).

Kiuhalisia mtu anaweza akawa katika mojawapo ya ndoa hizi, na asihesabike kuwa ni mkosaji kwasababu ndoa hasa ni jambo la kiutamaduni, ambalo huusisha wanadamu wote, bila kuchagua dini, rangi, au kabila.

Hivyo si sawa kudhani kuwa kwasababu watu fulani hawajafungishwa ndoa kikristo(kanisani) basi, zote hizo sio ndoa kwamba ni sawa tu hata kwenda kuoa tena hapo, au kuivuruga, wasiishi pamoja. Ukifanya hivyo Mungu atakuwajibisha kwa kuzivuruga ndoa za watu wengine. 

Aina ya pili ya ndoa ni ndoa ya kikristo.

Hii ni ndoa inayofungwa katika kanuni timilifu za Mungu alizozikusudia tangu mwanzo.

Kanuni zenyewe ni hizi

    i) Wote wawe waamini.

(1Wakorintho 7:39, 1Wakorintho 9:5, 2Wakorintho 6:14 – 16)

Kuamini si lazima muwe katika viwango sawa kiroho, lakini wote muwe upande mmoja wa Kristo, (Kwasababu hayo mengine yanaweza rekebika). Lakini mmoja ni mganga wa kienyeji, mwingine mkristo,.au mmoja ni muislamu mwingine mkristo. Hilo si sawa ni sharti wote wawe wakristo. Kwasababu hakuna ushirika wowote kati ya nuru na giza.

Kwasababu Ndoa ya kikristo ni lazima iwe katika jina la Bwana, vinginevyo, itaangukia katika lile kundi lingine.

      ii) Mume mmoja, mke mmoja.

Tofauti na ndoa za wapagani. Ambazo kwao unaweza kuwa na mke zaidi ya mmoja, lakini mtu anayetaka ndoa yake itimilike mbele za Kristo, basi mume/mke atambue kuwa hana ruhusa ya kuongoza mwenza mwingine. 

Mathayo 19:4-5

[4]Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke, 

[5]akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja? a

      iii) Malazi yawe safi:

Waebrania 13:4

[4]Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu. 

Malazi kuwa safi maana yake ni nidhamu ya kiasi, katika kukutana kimwili. Mkristo hapaswi kuwa mtu wa hulka ambaye wakati wote anawaza zinaa, mpaka anakosa muda wa kujishughulisha na mambo ya rohoni.

1 Wakorintho 7:5

[5]Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu. 

Vilevile viitendo kama kuingiliana kinyume na maumbile haviruhusiwi ndani ya ndoa (1Wakorintho 6:9).

      iv) Hakuna talaka. 

Tofauti na ndoa za wapagani, mtu anaweza kuacha/kuachwa kwa sababu yoyote, labda mfano wamechokana, au wameudhiana, lakini katika ukristo hilo jambo halipo mtaendelea kuishi pamoja mpaka kifo kitakapowatenganisha. 

Bwana alitoa ruhusa hiyo katika eneo la uasherati tu lakini ukumbuke, alisema pia ‘samehe mara saba sabini’. Hivyo kwa kauli hiyo hakuna popote tunaona wigo wa wanandoa kuachana kwa sababu yoyote ile.(1Wakorintho 7:39-40)

      V) Mume ni sharti ampende mkewe. 

Mume kumpenda mkewe ni amri ya kindoa, anawajibu wa kumtunza na kumuhudumia na kujitoa kwa ajili yake, kama Kristo alivyolipenda kanisa.(Waefeso 5:25-31)

     Vi) Mke ni sharti amtii mumewe.

Ni amri mke amtii mumewe kwa agizo atakaloambiwa/ elekezwa. Tofauti na ndoa za wapagani ambazo hili linaweza lisiwe la muhimu. Kwenye ukristo, ni lazima utii wa mwanamke uonekane kwa mumewe.

Waefeso 5:22

[22]Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu. 

Sasa vigezo hivi wakivikidhi hawa wakristo ambao wameokoka na wanatarajia kuishi kama mke na mume. Basi hiyo huitwa  ndoa ya Kikristo iliyokidhi vigezo vitimilifu vya Mungu,.haijalishi imefungwa kanisani au kwenye familia, .

Swali ni je? kwanini watu wafungie kanisani? Na  Je ni takwa? 

Mkristo ambaye anathamini ukamilifu wote wa ki-Mungu, katika maeneo yake yote ya kiroho na kimwili, kufungia ndoa yake kanisani itakuwa ndio chaguo lake bora. Kwanini iwe hivyo?

Hizi ndio faida za ndoa kufungiwa kanisani

  1.  Kanisa ni mahakama ya wakristo

Biblia inatueleza mashtaka yetu, hayapaswi kutatuliwa na watu wa ulimwengu, bali ndani ya kanisa. Kwasababu kanisa ni zaidi ya mahakama yoyote, ambayo Mungu ameiheshimu mpaka akaamua malaika zake wahukumiwe katika hiyo.

Hivyo endapo kuna migogoro, au kutoelewana, au kupatiwa misaada, au mashauri, au maonyo, au maongozi,  basi kanisa, limewekwa na Mungu kwa ajili yako kukusaidia katika hayo yote. 

Lakini ikiwa hukuifungia ndoa yako kanisani. Fahamu kuna mambo kama hayo yatakupita, au yatakuwa magumu kwetu kutatulika.

1 Wakorintho 6:1-3

[1]Je! Mtu wa kwenu akiwa ana daawa juu ya mwenzake athubutu kushitaki mbele ya wasio haki, wala si mbele ya watakatifu? 

[2]Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo? 

[3]Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya? 

    2) Ushuhuda mwema.

Mungu anapenda mambo mema atufanyiayo tumtukuze mbele ya kusanyiko la watakatifu. Tunajua Ndoa ni kitu chema, hivyo tunapoweka wazi mbele za Bwana,  na mbele ya kanisa lake, yeye hutukuzwa lakini pia tunapokea baraka za kanisa, Ikiwa tunapoumwa na kuponywa hatuoni sawa kukaa na shuhuda zetu ndani, tunakwenda kushuhudia mbele ya kanisa, si zaidi ndoa zetu?, ni ushuhuda mkubwa, ambao utawafariji wengine, lakini pia utaihubiri injili ya Kristo.

Zaburi 35:18

[18]Nitakushukuru katika kusanyiko kubwa; 

Nitakusifu kati ya watu wengi. 

Hivyo, kwa maelezo hayo tunaweza kusema hakuna sababu ya Mkristo yoyote kuifungia ndoa yake, mbali na kanisa. 

Lakini hiyo haimaanishi kuwa usipofungia kanisani, ndoa yake haitambuliwi na Mungu. Maadamu umekidhi vigezo “mama”, tulivyoviorodhesha juu. Hiyo ni ndoa.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAFUNDISHO YA NDOA.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

Je! Ni sahihi kuoa/kuolewa na mtu uliyemzidi umri?

Rudi Nyumbani

Print this post

Je ni YESU au JESUS au YESHUA?

Ni YESU au JESUS au YESHUA

Swali: Je tunapaswa kutumia jina lipi katika maombi na utumishi?..Je tutume YESU (kwa lugha ya kiswahili) au JESUS (kwa lugha ya kingereza) au YESHUA (kiyahudi)?.

Jibu: Moja ya mafundisho yaliyogeuzwa na adui ni pamoja na matumizi ya jina la YESU?.

Lipo kundi linaloamini kuwa jina la “Masihi” linapaswa litamkwe vile vile kama Malaika Gabrieli alitamka kwa  Bikira Mariamu, ambalo ni “Yeshua” (ישוע) kiebrania.

Na lipo kundi linaloamini kuwa jina la Masihi linaweza kutafsiriwa katika lugha mbalimbali na kuwa na matokeo yale yale.

Na mfano wa tafsiri hizo mbalimbali ni kama “JESUS” (ambayo ni lugha ya kiingereza)…nyingine ni “YESU” (ambayo ni lugha yetu ya kiswahili).. Na katika lugha nyingine pia jina hilo linatafsirika katika namna nyingine…ambapo likisikika haliwi mbali na ile lile la asili “ Malaika Gabrieli alilomwambia Mariamu Yeshua”.

Sasa swali ni je! Ni sahihi kulitafsiri jina hilo kutoka kiebrania kwenda katika lugha nyingine ikiwemo kiswahili, kama hivi tunavyosema leo YESU?.

Jibu ni Ndio!.. Ni sahihi kabisa na matokeo ya jina hilo yanabaki kuwa yale yale Mungu aliyoyakusudia, ikiwa na maana kuwa mtu anayetaja jina la YESHUA, na yule anayetaja JESUS na yule anayetaja YESU, wote wa wapo sawa…(hakuna ambaye anakosea)…Hapo ni suala la lugha tu!

Sasa utauliza tunalithibitisha vipi hilo kibiblia?.

Tunasoma siku ile ya Pentekoste, Roho Mtakatifu alivyoshuka kwa mara ya kwanza juu ya kanisa, kilichotokea ni watu kusikika wakisema kwa lugha nyingine.

Sasa zile lugha walizokuwa wanazungumza hazikuwa za kimbinguni bali za duniani, (ambazo zinazungumza na jamii mbalimbali za watu) soma Matendo 2:7-11.

Hali kadhalika na maneno yaliyokuwa yanazungumzwa sio makelele, (yasiyo na maana) kwamba mtu akisikiliza haelewi ni kitu gani kinazungumzwa.

Bali ni maneno ya kumwadhimisha na kumtukuza Mungu, kama Roho alivyowajalia….jambo kama hilo pia lilitokea katika nyumba ya Kornelio, soma Matendo  10:46.

Kwahiyo wale waliojaliwa kuzungumza kiyunani, maana yake lugha yao yote ilibadilika na kuwa kiyunani ikiwemo na majina ya Mungu, wasingeweza kuzungumza kiyunani halafu jina “MUNGU” au “YESU” liendelee  kubaki vile vile kiebrania, (maana yake vyote vilibadilika, kuanzia maneno mpaka majina).

Vile vile waliojaliwa kusema kirumi siku ile ya Pentekoste na maneno yao yote yalibadilika na kuwa kirumi, ikiwemo jina la Mungu na Yesu.

Na kama kiswahili kingekuwepo pale basi hata jina la YESU lingetajwa na Mungu pia

Hiyo ni kufunua nini?

Ni kufunua kwamba katika agano jipya Bwana Mungu anazikubali lugha zote, na katika mataifa yote jina lake litatajwa na injili itahubiriwa kila Taifa, na kila lugha na kila kabila.

Zaburi 86:9 “Mataifa yote uliowafanya watakuja; Watakusujudia Wewe, Bwana, Watalitukuza jina lako”.

Na hiyo ndio sababu pasipo hata kujua kiebrania, bado pepo wakisikia jina la YESU kwa lugha yetu hii hii ya kiswahili wanaondoka…

Vile vile wakisikia jina la YESU kwa lugha ya kiyunani wanatoka, au kwa lugha ya kingereza JESUS wanahama.

Kwahiyo suala sio tafsiri ya jina suala ni Imani katika hilo jina.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Biblia inasema nini kuhusu sayari, je ni kweli zipo tisa?

SWALI:  Shuleni tumefundishwa sayari zipi Tisa Lakini je maandiko yanasemaje kuhusu hili, je zipo kweli kwa idadi hiyo?


JIBU: Biblia si kitabu cha kisayansi, au cha taaluma yoyote, kwasababu lengo lake sio uvumbuzi na utafiti wa mambo ya ulimwenguni. Bali ni kumrejesha mwanadamu kwa muumba wake. Ni kitabu chenye msingi wa IMANI. Mambo yasiyothibitika kwa macho bali rohoni. Ni kitabu kielezacho njia ya ukombozi wa mwanadamu inayopatikana kupitia YESU KRISTO  mwokozi wa ulimwengu.

Ijapokuwa vipo vifungu vichache vichache vinavyoelezea uhalisia wa elimu za duniani, lakini isidhaniwe kuwa lengo lake kuu ni kutoa taarifa za kila kitu kwenye hii dunia, bali mara nyingi huwa ni kuelezea vema habari husika ya rohoni iliyokuwa inazungumziwa hapo.

Tukirudi kwenye swali linalouliza kuhusu sayari, kwamba sayansi inatuambia zipo tisa, je biblia nayo inazitaja ngapi?

Kama tulivyotangulia kusema biblia haielezi kila kitu kuhusu dunia hii, bali inaeleza kila kitu kuhusu wajibu wa mwanadamu kwa muumba wake.

kuhusu Sayari biblia inazitaja  bila shaka kwamba yeye ndio aliziumba, na magimba yote angali, ambayo yamejumuishwa katika neno jeshi la mbinguni .

Katika biblia sayari zimejatwa kwenye vifungu  hivi;

Ayubu 38:32

[32]Je! Waweza kuziongoza Sayari kwa wakati wake? Au waweza kuongoza Dubu na watoto wake?

2 Wafalme 23:5

[5]Akawaondosha wale makuhuni walioabudu sanamu, ambao wafalme wa Yuda waliwaweka ili kufukiza uvumba katika mahali pa juu, ndani ya miji ya Yuda, na katika kila mahali, pande zote za Yerusalemu; na hao pia waliomfukizia uvumba Baali, na jua, na mwezi, na sayari, na jeshi lote la mbinguni.

Lakini biblia Haijatoa idadi, kama ni tisa, au mia au elfu Mungu alizoziumba,  bila shaka ni nyingi, kwani turudipo kwenye sayansi, ndio tunathibitisha kuwa zipo mabilioni kwa mabilioni kwa mabilioni, hizi tisa walizoziona ni ambazo zipo tu kwenye mfumo wa jua letu..lakini huko angani kuna ma-jua mengi yasiyo hesabika na yote hayo yana sayari zake. Hata hivyo husema hizi nyota zote tuzionazo angani ni ma-jua kama hili letu isipokuwa tu yapo mbali sana.

Kwahiyo wanasayansi hututhbitishia zaidi uweza wa ajabu wa Mungu. Mambo yasiyoelezeka kwa ukuu na maarifa. Utukufu una yeye milele na milele. Amina.

Lakini Je! umempokea huyu Mungu aliyeumba mambo haya ya ajabu? kumbuka kumpokea yeye ni kumwamini Yesu. Kuaminije? . Ni kuamini ile kwa ile kazi yake kamilifu ya ukombozi wetu aliyotutenda sisi kwa kifo chake pale msalabani, iletao ondoleo la dhambi.

Ikiwa upo tayari leo kumpokea huyu mwokozi basi bofya hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba  >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mtu wa Kwanza kufika mwezini

Je! dunia Ni duara, tufe au ipo kama sahani?biblia inasemaje?

ACHENI MJUE YA KUWA MIMI NI MUNGU.

Print this post

Je! dunia Ni duara, tufe au ipo kama sahani?biblia inasemaje?

SWALI: Naomba kufahamu Je! dunia Ni duara, tufe au ipo kama sahani imefunikwa na glasi kwa juu?.


JIBU: Jambo la msingi kufahamu kuhusu biblia ni kwamba, Biblia si kitabu cha kisayansi, au cha taaluma nyingine yoyote, kana kwamba unaweza vumbua elimu ya kidunia kupitia hicho. ukitegemea biblia ikupe majibu ya kitaaluma,  kwa bahati mbaya unaweza usifikie lengo lako, kwasababu hakikuandikwa na Roho Mtakatifu kwa dhumuni hilo.

Biblia ni kitabu kinachoeleza sifa na tabia za Mungu, na jinsi mwanadamu anavyopaswa aoane nazo ili aweze tembea kama Mungu mwenyewe atakavyo. Ni kitabu kinachomrejesha mtu kwa muumba wake.  Kwa hiyo mtaala wake ni tofauti kabisa na elimu za ulimwengu huu na mavumbuzi yake.

Ni ajabu kuona mkristo analazimishia kutafuta kanuni za kibiashara kwenye biblia. Huwezi ona huko “demand and supply” au “cash flow” au masoko ya hisa. Nenda tu darasani utafundishwa vema kanuni za uwekezaji na utafanya vema.

Vivyo hivyo na kwenye sayansi, huwezi ona  aina za atomu au miamba, au mionzi, au chembe hai nyeupe za seli, au asprin huko  . Nenda tu darasani utafundishwa vema yote hayo.

Ndio, hatuwezi kukataa zipo  sehemu chache chache sana, zinazozungumzia elimu ya ulimwengu huu, lakini sio kwa lengo la kutufundisha kanuni zake, bali kwa lengo la kuelezea kwa undani jambo la kiroho katika tukio husika.

kwasababu biblia yenyewe inasema, hekima ya huu ilimwengu ni upumbavu mbele za Mungu, vilevile hekima ya Mungu ni upumbavu kwa ulimwengu. haviingiliani

1 Wakorintho 1:20

[20]Yu wapi mwenye hekima? Yu wapi mwandishi? Yu wapi mlete hoja wa zamani hizi? Je! Mungu hakuifanya hekima ya dunia kuwa ni upumbavu?

Kuhusu mapinduzi yote ya kiteknolojia ya wanadamu ambayo tunayaona  sasa, na hata yatakayokuja huwezi yapata kwenye biblia, huwezi ona facebook, internet, vikizungumziwa kwenye biblia, sio kwamba Mungu hakuyaona au kuyajua, aliyajua sana, lakini yote hayo yamejumuishwa katika neno moja kuwa “maarifa kuongezeka” (Danieli 12:4)

Sasa tukirudi kwenye swali, ambalo linauliza je dunia ni tufe, duara au kama sahani imefunikwa na glass juu. Jibu ni lile lile hakuna taarifa za kutosha kwenye biblia zinazofafanua juu ya hilo lakini haya ni maandiko machache yanayotuambia kuhusu uhalisia wa dunia..

Isaya 40:22

[22]Yeye ndiye anayeketi juu ya duara ya dunia, na hao wanaokaa ndani yake huwa kama panzi; yeye ndiye azitandazaye mbingu kama pazia na kuzikunjua kama hema ya kukaliwa;

Kwa andiko hili, tunaonyeshwa kuwa dunia ipo katika duara, aidha kama tufe au mpira. lakini ni mzunguko, na sio kama sahani yenye glasi juu.

Hivyo tukirudi katika sayansi, ukisoma huko ndio utaelewa vizuri zaidi kuwa dunia ni mfano wa tufe, na sisi tukiwa tumenata-nata juu yake sio ndani yake.

Lakini tukumbuke kuwa haya ni maarifa ya mwanadamu, aliyopewa na Mungu ya kutafiti, na maarifa yake yanatabia ya kuboreka na kupinduka. Lakini kwa upeo wao wameweza kuthibitisha hilo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MUNGU WETU, JINSI LILIVYO TUKUFU JINA LAKO DUNIANI MWOTE!

Heshima ni nini kibiblia?

NYOTA ZIPOTEAZO.

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya neno kumwamba (Zaburi 78:19)

Zaburi 78:18-19

[18]Wakamjaribu Mungu mioyoni mwao Kwa kutaka chakula kwa tamaa zao. [19]Naam, walimwamba Mungu, wakasema, Je! Mungu aweza kuandika meza jangwani? 

Kumwamba kama ilivyotumika hapo ni “kuzungumza kinyume”

Hivyo hapo anaposema 

“Naam, walimwamba Mungu, wakasema, Je! Mungu aweza kuandika meza jangwani?”

Ni sawa na kusema..

Naam, walizungumza kinyume na Mungu, wakisema Je! Mungu aweza kuandika meza jangwani?

Wana wa Israeli kule jangwani, vinywa vyao havikuwa vya shukrani au vya kuomba, bali vivywa vya kumjaribu Mungu na manung’uniko, ijapokuwa walijua uweza wake wote, lakini walijifanya kama Mungu wao hawezi kuwaokoa, wakawa wanauliza maswali yaliyoonekana magumu, kumbe nafsini mwao wanajua yote yanawezekana, wanafanya tu makusudi ili waone Yehova atafanya nini. Na ndio sababu iliyomfanya Mungu asipendezwe nao.

Na sisi pia tusiwe watu wa kumwamba Mungu, kwa kusema maneno ya kutoamini.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

Kama Musa aliandika vitabu vya torati, Je! kifo chake alikiandikaje mule?

BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.

Biblia inamaana gani kusema “vipo sita, naam saba”?

Rudi Nyumbani

Print this post

JIFUNZE KWA SHUJAA YAELI.

(Ukarimu na maziwa)

Nakusalimu katika jina la Yesu Kristo mwokozi wetu. Karibu tujifunze maneno ya uzima. Haya ni mafunzo maalumu kwa ajili ya wanawake. Ikiwa utatamani kupata mengine mengi basi fungua link hii.. uweze yasoma..

https://wingulamashahidi.org/2021/07/21/masomo-maalumu-kwa-wanawake/

Kama wewe ni msomaji mzuri wa biblia, utakumbuka ile habari ya Debora na Baraka katika kitabu cha waamuzi.

Habari ile inaeleza jinsi Israeli ilivyo nyanyaswa na kutumikishwa  na maadui zao wakaanani kwa muda wa miaka ishirini, chini ya mfalme mmoja aliyeitwa Yabini, na jemedari wake mkali aliyeitwa Sisera.(Waamuzi 4)

Watu hawa walikuwa wameendelea sana kivita, hivyo Israeli hawakuweza kufanya lolote isipokuwa kukubali mateso, ndipo wakamlilia Bwana sana. Naye akawasikia akawainulia mtetezi. Ndio huyu Debora nabii pamoja na baraka shujaa wa Israeli.

Sasa huyu Sisera alikuwa ni jemedari kwelikweli, hata Neno la Mungu lilipomjilia Debora, kumwagiza Baraka jemedari wa Israeli, akapange vita nao, bado alisita, na alichofanya ni kuomba Debora aende naye vitani..

Ni jambo ambalo ni kinyume na asili, wanawake kuhusishwa kwenye vita, kwasababu hiyo Debora akapewa Neno na Bwana kwa Baraka..kufuatana na wazo lake la kutaka.mwanamke aende naye vitani..kuwa ushindi huo hautakuwa mkononi mwake bali mkononi mwa mwanamke.

Waamuzi 4:8-9

[8]Baraka akamwambia, Kama utakwenda pamoja nami ndipo nitakwenda; bali kama huendi pamoja nami, mimi siendi. 

[9]Basi akasema, Hakika nitakwenda pamoja nawe, lakini safari utakayoiendea haitakupatia heshima wewe; maana BWANA atamwuza Sisera katika mkono wa mwanamke. Debora akainuka, akaenda pamoja na Baraka mpaka Kedeshi. 

Na kweli tunaona walipokwenda vitani kupigana nao. Yule Sisera jemedari wao, alifanikiwa kutoroka..Alipokuwa anakimbia alimwona mwanamke mmoja aliyeitwa Yaeli. Mwanamke huyo alimkaribisha kwake kwa ukarimu wa hali ya juu sana. Akampeleka sehemu ya maficho kabisa mahali ambapo si rahisi kugundulika, tena akamfunika ili kumuhakikishia ulinzi wote, 

Jambo lile la ukarimu usio wa kawaida lilimtuliza moyo Sisera, akajihisi kama amepona, ndipo akamwomba yule mwanamke maji kidogo anywe. Lakini yule mwanamke bado akaendelea kuonyesha ukarimu wa hali wa juu sana, akaenda kumletea MAZIWA badala ya MAJI.. Pengine akamwambia aah! bwana wangu, maji si mazuri ukiwa umefunguka tangu asubuhi, tena kwenye mbio na pilika pilika za vita, kutumia maji si vizuri kiafya,  kunywa kwanza maziwa haya, mwili uchangamke, upate nguvu, ndipo baadaye nitakupa maji unywe.  

Sisera kuona vile akaendelea ku-relax, zaidi kuona ukarimu wa ajabu wa yule mwanamke, akafanya kosa akanywa yale maziwa, yakamlewesha kwa haraka mpaka akapotelea usingizini akasahau kabisa kwamba yupo vitani anatafutwa.

Lakini mwanamke Yaeli alipoona shujaa Sisera amelala fofofo, akasema nimempata adui yetu, sasa  ninakwenda kumuua kirahisi kabisa.Akaenda kuchukua msumari mrefu, na nyundo. akavielekezea kichwani, akaupigilia ukaingia wote kichwani. Na mwisho wake ukawa umefikia pale pale.

Hata baadaye Baraka anakuja akakuta tayari mtu ameshakuwa marehemu.

Waamuzi 4:17-21

[17]Lakini Sisera akakimbia kwa miguu, akaifikilia hema ya Yaeli mkewe Heberi, Mkeni; kwa maana palikuwa na amani kati ya Yabini, mfalme wa Hazori, na nyumba ya Heberi, Mkeni. 

[18]Yaeli akatoka kwenda kumlaki Sisera, akamwambia, Karibu Bwana wangu, karibu kwangu; usiogope. Akakaribia kwake hemani, naye akamfunika kwa bushuti. 

[19]Akamwambia, Tafadhali nipe maji kidogo ninywe; maana nina kiu. Akafungua chupa ya maziwa, akampa kunywa, akamfunika. 

[20]Naye akamwambia, Simama mlangoni pa hema; kisha itakuwa mtu awaye yote akija na kukuuliza, akisema, Je! Yupo mtu hapa, basi, mjibu, La, hapana. 

[21]Ndipo Yaeli, mkewe Heberi, akatwaa kigingi cha hema, akashika nyundo mkononi mwake, akamwendea polepole, akamtia kile kigingi katika kipaji chake, nacho kikapenya, hata kuingia mchangani; kwa maana usingizi mzito ulikuwa umemshika; basi akazimia, akafa. 

Ni nini Kristo anataka wanawake wafahamu kwa ushujaa wa Yaeli? (Ni ukarimu na Maziwa)

Kumbuka vita vyetu sisi si juu ya damu na nyama, bali dhidi ya wakuu wa giza hili na ibilisi. Na mtu yeyote ambaye anahubiri injili, mtu huyo ni askari wa Bwana. Mfano wa akina Debora, na Baraka. Haijalishi jinsia yake ni ipi, wote ni watendakazi katika shamba la Bwana.

Lakini kama tunavyojua Mungu ameweka majukumu mbalimbali ndani ya mwili wa Kristo, wewe kama mwanamke hujaitwa kuwa mchungaji, au askofu, lakini umeitwa kuwa shujaa wa kumwangamiza adui kwa karama uliyopewa.  Debora na Yaeli hakuwa kama Baraka, maumbile yao hayakuumbwa kusimama na mikuki na ngao, na kukimbizana maporini usiku na mchana na maadui. Hapana.. bali ni kuwa katika utulivu. Na utulivu ukitumiwa vizuri huleta mlipuko mkubwa kuliko wingi wa makombora ya vita.

Aliyemuua shujaa Sisera alikuwa mwanamke, aliyekuwa nabii wa Israeli alikuwa mwanamke. Ushindi ulipatikana kwa mikono ya wanawake. Lakini bila kuvaa suruali, na mitutu vya vita.

Hata leo, ikiwa mwanamke ataitambua vema kazi ya injili kwa kufuata kanuni za kibiblia anaouwezo wa kuwavua watu wengi kwa Kristo zaidi hata ya mhubiri wa kusimama kwenye majukwaa makubwa.

Ukarimu, kwa wenye dhambi, upendo wa waliotekwa na mwovu, pamoja na maziwa (Ndio Neno la Mungu) ni Njia hii ya YAELI, ukiitumia itakufanya uwavute wale watu kwa Kristo wengi, na hatimaye kanisa la Kristo kukua na kuongezeka.

Ni watu wangapi unaweza wafadhili kichakula huku unawahubiria injili, unaweza wapelekea mavazi huku unawafundisha habari za Kristo, unaweza wafadhili kwa chochote huku unawaalika kanisani..kidogo.kidogo, upo kazini kwako, unazungumza nao kwa ukarimu, unawasaidia majukumu ambayo wangepaswa wayafanye wao wenyewe lakini wewe unawasaidia, lengo lako ni uwavute katika imani, huku ukihakikisha unawapa na maziwa, yaani maneno ya faraja ya Mungu,(1Wakorintho 3:2, 1Petro 2:2).

Wewe ni mamantilie, wateja wako, unawapa zaidi ya huduma, huku unawafundisha habari za Kristo, unawaeleza uzuri wa kukusanyika kanisani, n.k.

Ukiendelea hivyo baada ya kipindi fulani utashangaa watu hao wanavutika kwako, na kwa Kristo. Hata yule mpinga-kristo aliyekuwa na moyo mgumu kuliko wote anaokoka, yule boss wako ambaye alikuwa hataki kusikia masuala ya Mungu anaokoka. Wale ambao walirudi nyuma, wanaamka tena.

Onyesha tu ukarimu, lakini usiwe ukarimu wa bure, huo hautazaa chochote bali wenye injili nyuma yake.

Hivyo wewe kama mwanamke/binti wa kikristo simama katika eneo la utulivu, kiasi, kujisitiri, ni ukweli utaziangusha ngome sugu za adui.

1 Petro 3:1-5

[1]Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno; 

[2]wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu. 

[3]Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi; 

[4]bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu. 

[5]Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao. 

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

Maziwa yasiyoghoshiwa ni nini? Kwanini biblia inatumia mfano huo?

Maana ya Mithali 30:33 Kwa maana kupiga maziwa huleta siagi

Rudi Nyumbani

Print this post

msalaba ni nini.

Msalaba ni kipande cha mti, kilichochongwa kwa kupishanishwa na kingine kwa juu. chenye lengo la kumuulia mwanadamu kwa kifo cha mateso.

Tofauti na sasa, ambapo adhabu nyingi za kifo kwa mataifa mbalimbali huwa ni kunyongwa, au kupigwa risasi, au kuwekwa kwenye kiti cha umeme, n.k.. Lakini katika falme za zamani watu waovu kupita kiasi, kwamfano wauaji, au wenye makosa ya uhaini, adhabu yao, ilikuwa ni kutundikwa au kugongelewa pale msalabani mpaka ufe. Ni mateso ambayo utataabika hapo kwa saa nyingi sana kabla ya kufa, hata siku mbili.

Hivyo kwa lugha rahisi tunaweza kusema msalaba ni chombo cha kuulia mtu.

Kwetu sisi tuliomwamini Kristo. Msalaba ni ishara kuu ya ukombozi tulioupata kwa kifo cha mwokozi wetu. Kufahamu kwa undani ni kwanini fungua link hizi; usome..

AMELAANIWA AANGIKWAYE MSALABANI.

Nini maana ya sulubu/ sulubisha?

nini maana ya kujikana nafsi na kujitwika msalaba?

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> 

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.


Mafundisho mengine:

Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?

Je! msalaba kaburini una umuhimu wowote?

Print this post

LAANA NI NINI KIBIBLIA?

Kibiblia  Neno laana linatafsiri kwa namna mbili.

Namna ya kwanza, ni Kupoteza sifa ya kukubaliwa na Mungu kwa jambo lolote lile. Na hii chanzo chake ni lile anguko la mwanadamu tangu mwanzo.

Namna ya pili, ni apizo alitoalo mtu kwa mwenzake au alitoalo Mungu mwenyewe, kwa mwanadamu ili wafikiwe na ubaya fulani, au wakasifikiwe na Mema waliyokusudiwa.

 

LAANA YA KWANZA:

Sasa laana hii ya kwanza, inazalika kwasababu ya  asili yetu, ambayo ilionekana tangu Adamu, kuhasi maagizo ya Mungu, ambayo hata sisi sote tuliopo leo, asili hiyo ipo ndani yetu. Ni sawa na unavyomwona mdudu kama mende, ukimtazama tu tangu akiwa mtoto, utamchukia hata kabla hajaonyesha hali yake ya kupenda uchafu, kwasababu unajua asili hiyo ipo ndani yake. Atakuja kuwa mchafu tu.

 

Ndivyo ilivyo kwetu sisi, tayari Mungu alishaona tangu tunazaliwa tutamwasi tu yeye, mfano wa baba yetu Adamu.

Na ndio maana akaandaa mpango wa kuzaliwa upya mara ya pili, kupitia Yesu Kristo. Hivyo mtu yeyote anayezaliwa mara ya pili, anaondolewa katika laana hiyo ya kukataliwa na Mungu, na anakuwa mwana wa Baraka. Laana hii haiwezi kuondoka bila damu ya Yesu.

 

Hiyo ndio sababu kwanini maandiko yanasema Yesu alifanyika laana kwa ajili yetu. Maana yake, tunapokombolewa na yeye tunafanywa kuwa watu wengine kabisa wenye asili nyingine wasio na laana, wenye kukubaliwa na kupendwa na Mungu.

 

Wagalatia 3:13  Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;

14  ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani.

 

Hivyo wewe uliyeokoka, na kupokea Roho Mtakatifu unaitwa, mbarikiwa, unaitwa mungu duniani, mtoto wa Mungu kwelikweli.

LAANA YA PILI

Lakini laana ya pili, kama tulivyoona ipo katika maapizo ambayo huyatoa Mungu au mwanadamu mwenyewe.

a) Tukianzana na zile zinazonenwa na Mungu

Mungu anaweza kukutamkia laana, hata kama utakuwa umekombolewa na yeye. Unaweza kushiriki mabaya. Laana hizi zinaweza kukufanya usipoteze wokovu wako, lakini zikakukosesha mambo mengi sana duniani.

 

Mfano wa hizi ndio zile alizowaambia wana wa Israeli, kwamba watakapoacha sheria zake, basi watatawanywa katika mataifa yote, watakuwa mikia na sio vichwa, nchi itazuliwa Baraka zake, wataondokeshewa adui zao N.k. (Kumbukumbu 28)

 

Mfano pia wa hizi, ndio kama ile aliyoilaani nchi, na nyoka pale Edeni. Akasema itatoa miiba, na nyoka atakwenda kwa tumbo (Mwanzo 3:17). Vilevile ndio ile aliyomwambia Kaini kuwa atakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani (Mwanzo 4:12).

 

Hata sasa wapo wengi wanaokutana na maapizo hayo ya Mungu kwa kufanya dhambi au makosa ya makusudi. Namna ya kueupuka laana hizi ni kutii agizo la Mungu.

Kwasababu unapozizoelea zitakufanya uangukie kabisa kwenye kundi lile la kwanza la kukataliwa kabisa..la watu ambao hawajaokoka.

 

Waebrania 6:4  Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,5  na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,

6  wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.

7  Maana nchi inayoinywa mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuzaa mboga zenye manufaa kwa hao ambao kwa ajili yao yalimwa, hushiriki baraka zitokazo kwa Mungu; 8  bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa.

 

Kinyume cha laana ni Baraka, unapotii amri za Mungu, umejiwekea mazingira mazuri ya kupokea Baraka.

 

b) Lakini pia zipo laana  zinazonenwa na  mwanadamu.

Hizi nazo zimegawanyika katika makundi mawili.

 

i) Kundi la kwanza ni la watu wa Mungu/wenye haki.

Kwamfano Utakumbuka Hamu alipoona uchi wa baba yake. Nuhu aliulaani uzao wake, Hivyo watu wa Mungu wamepewa mamlaka hiyo, hata sasa, ndio maana Bwana Yesu alisema mtakalolifunga duniani, limefungwa mbinguni, na akatusihi pia tuwe watu wa kubariki kuliko  kulaani. (1Petro 3:9)

Unapokosewa na mwenye dhambi epuka kutoa neno la madhara kwake, kwasababu hakika jambo hilo litampata na kumwangamiza kabisa. Ndicho alichokifanya Elisha kwa wale vijana arobaini na wawili waliomdhihaki.

 

ii) Kundi la pili ni laana zitokazo kwa watu waovu.

 

Husasani wachawi, nao pia huweza kusema jambo likatokea, Utakumbuka kisa cha Balaamu mchawi, alipoajiriwa na Balaki kwenda kuwalaani Israeli wa Mungu, lakini alishindwa akajikuta anawabariki badala ya kuwalaani.

Akasema hakuna uchawi (Hesabu 23:23).

Ikiwa wewe umeokoka, huna haja ya kuogopa laana za hawa, kwasababu haziwezi kukupata, kwasababu unalindwa na nguvu za Mungu, hizi huwa zinawapata watu ambao wapo nje ya Kristo YESU.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NUHU WA SASA.

MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.

KUVUNJA MAAGANO YA UKOO.

Rudi Nyumbani

Print this post

Fahamu Mwandishi wa kitabu cha Waebrania ni nani.

Mwandishi wa kitabu cha Waebrania ni nani?

Kitabu cha Waebrania ni moja ya nyaraka ambazo waandishi wake hawajajitambulisha aidha ndani au mwanzoni  au mwishoni mwa nyaraka hizo. Lakini kwa kutathimini baadhi ya nukuu za mwandishi, huwenda alikuwa ni mtume Paulo aliyeuandika. Kufuata na kumtaja Timotheo kwenye waraka huo, na tunajua Timotheo alikuwa chini ya utume wa Paulo, kwani  ndiye aliyeongozana naye na kumtaja sana katika nyaraka zake nyingi.

Waebrania 13:23  Jueni ya kuwa ndugu yetu Timotheo amekwisha kufunguliwa; ambaye, akija upesi, nitaonana nanyi pamoja naye.

Na pia jinsi mwandishi alivyomalizia waraka wake,  kwa kusema “neema na iwe nanyi nyote”.  Ni salamu inafanana na nyaraka zote za mtume Paulo, kila alipomaliza alihitimisha na  baraka hizo.

Japo wengine wanasema namna ya uandishi haifanani na mtume Paulo, yawezekana alikuwa ni Apolo, au Barnaba, au sila au mtu mwingine tofauti na Paulo.

Lakini kwa vyovyote vile kumtambua mwandishi, si lengo la uandishi, lengo ni kufahamu kilichoandikwa ndani humo.

Maelezo mafupi ya kitabu hichi.

Kwa ufupi, kama kitabu hichi kinavyoanza kujitambulisha,  kinasema

WARAKA KWA WAEBRANIA.

Maana yake ni kitabu kilichoelekezwa kwa wayahudi-wakristo waliokuwa katika kanisa wakati ule. Ndio maana kwa jinsi ulivyoandikwa waraka huu, mwandishi anazungumza na mtu ambaye mwenye uelewa wa dini ya kiyahudi na taratibu zake za kiibada.

Dhumuni kuu ni kueleza UKUU WA YESU JUU YA WATU WOTE, NA MAMBO YOTE YA AGANO LA KALE.

Kwamfano anaeleza Yesu alikuwa mkuu juu ya;

  1. Manabii wa agano la kale

Waebrania 1:1  Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, 2  mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu. 3  Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu

  1. Alikuwa mkuu zaidi ya malaika: Soma Waebrania 1:13-2:18

Waebrania 1:13  Je! Yuko malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako chini ya nyayo zako? 14  Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?

  1. Alikuwa mkuu zaidi ya Musa, Yoshua na Haruni. (Soma, Waebrania 3:1-19, 4:1-13, 4:14-10:18)
  2. Alikuwa mkuu zaidi ya kafara za agano la kale. (Soma, Waebrania 10:11-14).

Waebrania 10:11  Na kila kuhani husimama kila siku akifanya ibada, na kutoa dhabihu zile zile mara nyingi; ambazo haziwezi kabisa kuondoa dhambi.

12  Lakini huyu, alipokwisha kutoa kwa ajili ya dhambi dhabihu moja idumuyo hata milele, aliketi mkono wa kuume wa Mungu;

13  tangu hapo akingojea hata adui zake wawekwe kuwa chini ya miguu yake. 14  Maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa.

Hivyo kitabu hichi kinamfafanua Kristo kwa undani, jinsi alivyo na ukuu zaidi ya mambo yote ya agano la kale. Na kwamba watu wote tangu Adamu mpaka Ibrahimu wasingeweza kukamilishwa bila Kristo. Waliishi wa ahadi hiyo ya kuja mkombozi, wakiingojea kwa shauku na hamu (Waebrania 11).

Lakini pia kitabu hichi  kinatoa angalizo kwa wayahudi wasirudi nyuma kwasababu ya dhiki na mateso yanayowapata kwa ajili ya imani ya Yesu Kristo. (Waebrania 12:1-13, 10:26-31), Bali wamtazame Kristo kama kielelezo chao, jinsi alivyostahimili mashutumu makuu namna ile.  Hii ni kutuhamasisha na sisi kuwa tunapopitia dhiki leo basi nasi tumtazame Kristo aliyestahili, mapingamizi yale, wala hakuutupa ujasiri wake.

Waebrania 12:1  Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,

2  tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mwandishi wa kitabu cha Matendo ya mitume.

Ielewe kwa kina Waebrania 13:5 maana yake.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

Je ni Mungu au Malaika?

Rudi Nyumbani

Print this post