Category Archive Uncategorized @sw-tz

Theolojia ni nini?. Na je ni sahihi kuisoma?

Theolojia ni elimu ya kujifunza sifa za Mungu na mapenzi yake na jinsi anavyohusiana na wanadamu na ulimwengu  kwa ujumla.

Neno Theolojia limezaliwa kutoka katika maneno mawili ya kigiriki ‘theos’, na ‘logos’

Theos likiwa na maana ya Mungu, na logos ni neno/wazo/elimu/maarifa.

Hivyo tukiunganisha maneno hayo, ni sawa kusema theolojia ni mafundisho au maarifa au elimu kuhusu Mungu.

Ni utafiti kuhusu  Mungu katika mpangilio na mtiririko maalumu. Ukweli ni kwamba theolojia haiwezi kumfafanua Mungu katika ufasaha wote, ikiwa mtu ataitegemea  theolojia tu kumjua Mungu, ukweli ni kwamba amepotea, lakini ikiwa itasomwa vema (si kwa lengo la kitaaluma), bali kwa lengo la kupanua upana wa fikra kuhusu Mungu na maandiko, inafaa sana katika uelewa wa nyanja mbalimbali, hususani kwa wale viongozi na waangalizi kama vile wachungaji, na wahubiri. Si lazima isomwe kwenye vyuo maalumu, mtu yeyote akitia nia kujifunza theolojia anaweza jifunza, kwa kupitia mafundisho mengi, majadiliano na waalimu walio na upeo mpana wa biblia, semina, na kujisomea mwenyewe n.k.

Na Haya ni matawi makuu ya theolojia katika kuichambua biblia.

1) Theolojia ya ki-biblia.

Imejikita katika kutafiti Maudhui au fundisho kuu la biblia, inaangazia jinsi gani vitabu mbalimbali kwenye biblia, vinavyoelezea mpango wa Mungu katika nyakati tofauti tofauti tangu mwanzo hadi mwisho. Mfano kujifunza MAAGANO, katika agano la kale na jipya yalivyotenda kazi na jinsi Yesu alivyoanza kutambulishwa tangu Edeni kama mzao wa mwanamke, hadi nyakati za manabii Isaya 53, hadi wakati wa kutokea kwake duniani Luka 24:27.

Upo umuhimu wa kuijua hii theolojia kwasababu itakupa kujua kiini cha biblia ni nini? Zipo habari nyingi, hadithi nyingi, nyimbo nyingi, mifano mingi, lakini ni vema ujue maudhui zao ni zipi ili usijikute unatoka nje ya shabaha ya imani.

2) Theolojia ya ki-mpangilio/Mada

Inaegemea kujifunza biblia katika migawanyo maalumu ya mada, kwa mfano,

Fundisho la Mungu (theolojia),

Fundisho La Yesu Kristo (Kristolojia),

Fundisho La Roho Mtakatifu (niumatolojia),

Fundisho La wokovu (Soteriolojia),

Fundisho La kanisa,(Ekleziolojia)

La Siku za mwisho.(Esokatolojia)

La mwanadamu (Anthropolojia)

La malaika (Angeolojia)

3) Theolojia ya ki-vitendo

Inajikita kujifunza jinsi maagizo ya kibiblia yanavyoweza kutendewa kazi katika,, huduma kwa mfano kuhubiri na kufundisha , katika uangalizi wa kichungaji, katika umisheni, na katika taratibu za kiibada, na katika kutoa mashauri ya kikristo kama vile kuwaonya wenye matatizo ya kiroho,  kifikra, vifungo n.k.

4) Theolojia ya ki-historia.

Inaangazia jinsi gani imani ya kikristo imekuwa ikipiga hatua katika vipindi mbalimbali vya kihistoria, inaangazia mabaraza mbalimbali ya makanisa yaliyokaa katika kujadili fundisho na misingi ya imani. Kwamfano lile baraza la Nikea (325WK). Mpaka nyakati za matengenezo mfano akina Martin Luther, calvin, na wengine.

Hii inakusaidia kujua historia na chimbuko la imani yetu, na sababu ya ukristo kuonekana katika muundo huu leo.

5) Theolojia ya kimaadili.

Hii inaegemea katika ukristo na jamii, kwamfano mtazamo wa ukristo katika maeneo ya kijamii mfano ndoa, biashara, taratibu za kijamii, haki za kibinadamu, vita,

Zipo theolojia nyingine kama vile theolojia za tafsiri, za kulinganisha, za utetezi, za kifalsafa. n.k. Kwasababu ya upana wa theolojia, haya ni  matawi baadhi tu, kati ya mengi. Hivyo, kama watu wa Mungu, pamoja na kutegemea Bwana kutufunulia mwenyewe maandiko, upo pia wakati ambao hatuna budi kuyamulika maandiko kiundani (Kitheolojia), tukiwa na lengo la kumjua Mungu kwa upana na sio kuwa wasomi, au wanataaluma.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mwanazuoni ni mtu gani kibiblia?

Kwanini kuna tafsiri nyingi za Biblia, na tafsiri ipi ni sahihi?

Yesu anapoitwa mwana wa Azali, maana yake nini?

Print this post

Je Paulo, alihimiza kusikiliza nyimbo za kidunia kulingana na Matendo 17:28

Matendo 17:28 Kwa maana ndani yake yeye tunaishi, tunakwenda, na kuwa na uhai wetu. Kama vile mmoja wenu, mtunga mashairi alivyosema, Maana sisi sote tu wazao wake.

29 Basi, kwa kuwa sisi tu wazao wa Mungu, haitupasi kudhani ya kuwa Uungu ni mfano wa dhahabu au fedha au jiwe, vitu vilivyochongwa kwa ustadi na akili za wanadamu.

JIBU: Paulo alipofika Athene, na kuona jinsi mji ule ulivyojaa sanamu nyingi, maandiko yanatuambia moyo wake ulichukizwa sana, hivyo kama ilivyo desturi yake kuhubiri injili, alijua njia mojawapo ya kuwavuta watu ni “kujiungamanisha nao”, kwa kuwagusia kwanza yale mambo mema waliyoyafikiri au kuyatenda.

Ndio maana utaona kabla ya kuwagusia kuhusu huyo mtunga mashairi, aliwaambia kuhusu madhabahu waliyoijenga, ambayo waliipa jina la “MUNGU ASIYEJULIKANA”

Matendo 17:23 Kwa sababu nilipokuwa nikipita huko na huko na kuyaona mambo ya ibada yenu, naliona madhabahu iliyoandikwa maneno haya, KWA MUNGU ASIYEJULIKANA. Basi mimi nawahubirini habari zake yeye ambaye ninyi mnamwabudu bila kumjua.

Paulo akaanza kuwahubiria Kristo kwa kupitia huyo wanayemwabudu kimakosa, Lakini tunajua Paulo, hakuwa na ushirika wowote na mifumo yao ya kipagani, wala hakuwahimiza waendelee kumwabudu Kristo kwa njia yao hiyo hiyo.

Tunaona katika kuendelea kujiungamanisha zaidi ya wenyeji wale wa Athene, Paulo akagusia tena habari nyingine za mtunga mashairi, ambaye alikuwa maarifu katikati yao, nyimbo zake zilivuma na kila mmoja alikuwa anazijua, na ndani ya mashairi yake, aliweka vina vinavyoeleza kuwa sisi sote ni wazao wake, au kusema sisi sote ni watoto wa Mungu.

Hivyo akatumia tena fursa hiyo, kuwaeleza uhai wa Mungu, ikiwa sisi tumezaliwa na yeye, basi haiwezekani Baba yetu akawa mfano wa sanamu, ni lazima tu atakuwa mwenye akili, ufahamu, na uelewa kama sisi na zaidi, na sio kama kipande cha mti.

Kwa njia hiyo Paulo akawapata watu wengi, kwa Kristo.

Lakini hatuoni mahali popote akiwaambia wawe wafuatiliaji au  mashabiki, wa nyimbo za kidunia.Hiyo ilikuwa njia ya kuwapata wapagani, wamjue Kristo.

Kinyume chake Paulo katika nyaraka zake, anahimiza, waamini kutofuatisha namna ya dunia hii (Warumi 12:1). Na kuhimiza uimbaji unaomtukuza Mungu na kutujenga sisi nafsi zetu kwake ndio unaopaswa kwa wakristo.

Waefeso 5:19 mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu;

20 na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo;

Wakolosai 3:16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.

17 Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.

Hivyo hatuoni mahali popote Paulo akikubaliana na usikilizaji wa nyimbo za kidunia, wala sisi kama wakristo, hatupaswi kujikita huko, kwasababu tumeshajua ni nani hasaa wa kumwimbia na kumsifu, na wa kumburudikia.

Mungu akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kuharimishwa ni nini, na kwanini Paulo aombe hivyo?(Warumi 9:2).

Uchambuzi na mwandishi wa kitabu cha Waefeso.

Ni kwa namna gani Bwana YESU alikula Siagi na Maziwa? (Isaya 7:15)

Print this post

Mistari ya biblia kuhusu sadaka

Hii ni mistari ya biblia inayogusia utoaji wa sadaka wa namna mbalimbali.

Sadaka kama ibada na utiifu.

Mithali 3:9 Mheshimu Bwana kwa mali yako, Na kwa malimbuko ya mazao yako yote. 10 Ndipo ghala zako zitakapojazwa kwa wingi, Na mashinikizo yako yatafurika divai mpya.

Mwanzo 4: 3 Ikawa hatimaye Kaini akaleta mazao ya ardhi, sadaka kwa Bwana. 4 Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. Bwana akamtakabali Habili na sadaka yake; 5 bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana.

Sadaka za kupenda:

Kutoka 25:2 Waambie wana wa Israeli kwamba wanitwalie sadaka; kila mtu ambaye moyo wake wampa kupenda mtatwaa kwake sadaka yangu.

2Wakorintho 9:7 Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.

Kumbukumbu 16:17 Kila mtu na atoe kama awezavyo, kwa kadiri ya baraka ya Bwana, Mungu wako, alivyokupa

Kutoka 35:5 Katwaeni kati yenu matoleo kwa Bwana; mtu awaye yote aliye na moyo wa kupenda, ayalete matoleo; dhahabu na fedha na shaba;

2Nyakati 31: 5 Mara ilipotangaa amri, wana wa Israeli wakatoa kwa wingi malimbuko ya nafaka, na divai, na mafuta, na asali, na mazao yote ya mashamba; na zaka za vitu vyote wakazileta nyingi.

Sadaka za kushukuru:

Zaburi 50:14 Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru; Mtimizie Aliye juu nadhiri zako.

Walawi 22: 29 Tena mtakapomchinjia Bwana dhabihu ya shukrani, mtamchinja ili mpate kukubaliwa. 30 Italiwa siku iyo hiyo; msisaze kitu chake hata asubuhi; mimi ndimi Bwana.

Sadaka za Zaka na malimbuko:

Malaki 3:10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.

Walawi 27: 30 Tena zaka yote ya nchi, kama ni mbegu ya nchi, au kama ni matunda ya nchi, ni ya Bwana; ni takatifu kwa Bwana.

Sadaka za kugharimika:

Marko 12:43 Akawaita wanafunzi wake, akawaambia, Amin, nawaambia, Huyu mjane maskini ametia zaidi kuliko wote wanaotia katika sanduku la hazina; 44 maana hao wote walitia baadhi ya mali iliyowazidi; bali huyu katika umaskini wake ametia  vyote alivyokuwa navyo, ndiyo riziki yake yote pia.

Wafilipi 4:18 Lakini ninavyo vitu vyote na kuzidi, tena nimejaa tele; nimepokea kwa mkono wa Epafrodito vitu vile vilivyotoka kwenu, harufu ya manukato, sadaka yenye kibali, impendezayo Mungu.

Luka 6:38 Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.

Sadaka zimpendezazo Mungu:

Yesu Kristo.

Pamoja na kuwa na sadaka za aina nyingi, lazima tufahamu, Sadaka halisi zimpendezazo Mungu. Na ya kwanza ni Yesu Kristo. Yeye alitolewa kwetu kama dhabihu kamilifu kwa ajili ya dhambi zetu. Hivyo mtu yoyote anayeitoa sadaka hii kwa Mungu basi, hukubaliwa na yeye asilimia mia. Na tunaitoa kwa kumpokea mioyoni mwetu kama Bwana na mwokozi wa maisha yetu. Imefanyika bora kuliko dhabihu zote na matoleo yote.

Waebrania 10: 4 Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi. 5 Kwa hiyo ajapo ulimwenguni, asema, Dhabihu na toleo hukutaka, Lakini mwili uliniwekea tayari;

Sambamba na hizo, sadaka nyingine zilizobora kuliko matoleo ni pamoja na kujitoa miili yetu katika utakatifu, kutenda haki, kuonyesha fadhili na rehema, kwa Bwana.

Warumi 12:1 Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.

Hosea 6:6 Maana nataka fadhili wala si sadaka; na kumjua Mungu kuliko sadaka za kuteketezwa.

Mika 6:6 Nimkaribie Bwana na kitu gani, na kuinama mbele za Mungu aliye juu? Je! Nimkaribie na sadaka za kuteketezwa, na ndama za umri wa mwaka mmoja? 7 Je! Bwana atapendezwa na elfu za kondoo waume, au na elfu kumi za mito ya mafuta? Je! Nimtoe

mzaliwa wangu wa kwanza kwa kosa langu, mzao wa mwili wangu kwa dhambi ya roho yangu? 8 Ee mwanadamu, yeye amekuonyesha yaliyo mema; na Bwana anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!

Je! Unatoa sadaka zote hizi? Kwa Bwana?

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

FUKUZA TAI WOTE JUU YA SADAKA YAKO.

NINI NI KILICHOMFANYA IBRAHIMU AKUBALI KUMTOA MWANAWE SADAKA?

Sadaka ya kuinuliwa ni sadaka ya namna gani?

Print this post

Je yale Makabila kumi na mawili ya Israeli, kila kabla lilikuwa na kazi gani maalumu?

Wana kumi na mbili wa Yakobo ndio waliozaa makabila 12 ya Israeli. Majina yao ni kama yafuatavyo;

  1. Reubeni
  2. Simeoni
  3. Lawi
  4. Yuda
  5. Dani
  6. Natali
  7. Gadi
  8. Asheri
  9. Isakari
  10. Zabuloni
  11. Yusufu (Manase & Efraimu)
  12. Benyamini

Zipo kazi au majukumu ambayo makabila yote yaliwajibika kuyatekeleza mfano wa hayo ni kama kumwabudu Mungu, kuihudumia hema, ambayo baadaye ikawa hekalu, ulinzi kwa taifa (msaada wa kijeshi), kuendeleza Sheria ya Mungu kwa vizazi vyote.

Lakini pamoja na hayo, yapo majukumu ambayo yalitekelezwa Zaidi na kabila husuka kuliko mengine. ambapo mengine yaliagizwa na Mungu Moja kwa moja na mengine yalikuja Kama kipawa, walichokirimiwa . Na hatimaye yakawa ni majukumu yao.

  1. Reubeni

Reubeni alipaswa kuwa na jukumu la kiuongozi, kama mzaliwa wa kwanza, lile kusudi lote la ukuhani lingepaswa liwe la lake lakini kwasababu alizini na mke wa Baba yake, akapoteza haki ya mzaliwa wa kwanza akaondolewa nafasi hiyo (mwanzo 35:22, 49:3-4).

Ijapokuwa alishushwa daraja lake. Bado alibakia kutimiza kusudi la kiulinzi upande wa mashariki mwa Israeli kwani jeshi lake, lilikiwa na watu hodari, lakini hawakuwa viongozi wa kijeshi.

  1. Simeoni

Kabila la Simeoni nalo lingepaswa lichukue nafasi kuu katika Israeli, lakini lilishushwa chini kwasababu ya ukatili wao pamoja na Lawi, walipokwenda kuwaua wale washekemu ambao hawakustahili Kufanyiwa mauaji yale, kwa kosa la kumnajisi dada yao.(Mwanzo 34)

Hivyo kabila hili halikuwa na uongozi wowote wa kiroho katika Israeli, zaidi lilimezwa katika kabila la Yuda, kutimiza unabii wa Baba yao (Mwanzo 49:5-7),  likabakia kuwa mchango kwenye eneo la kijeshi Israeli.

  1. Lawi

Lawi lilichukua nafasi ya kikuhani, lilihudumu katika hema na Hekalu, kufanya Upatanisho kwa wana wa Israeli, kwa sadaka mbalimbali pamoja Kufundisha Torati. (Kutoka 32:26-29).

Lawi hawakuwa urithi Israeli, bali walisambazwa katika makabila yote ya Israeli, kama Simeoni, kutimiza unabii wa Baba yao juu ya hasira walioionyesha Isiyo na huruma.(Mwanzo 49:5-7)

  1. Yuda

Kabila la Yuda lilisimama Kama kabila la Kifalme, na la kikuhani halisi wa milele (2Samuel 7:16)

Ndilo lililoandaa njia ya masihi kuja Duniani,(Mwanzo  49:10).Yuda lilichukua nafasi zote za juu, kutokana na kuwa Reubeni, Lawi na Simeoni kupoteza uwezo wa kuzishika, kwa matendo yao yasiyofaa.

Kabila Hili lilikuwa pia na askari hodari wa vita, na likasimama Kama kitovu cha kiutalawa, kivita na kiibada katika Israeli. Halikadhalika Yuda ilisimama kutunza urithi wa Israeli kwa vizazi vingi baada ya kutawanywa Kwenye mataifa yote, ndio  lenyewe tu lililoweza kurudi Israeli.(Mwanzo 49:9-12)

  1. Dani

Kabila la Dani lilikuwa na jukumu la kimahakama katika Israeli, (Mwanzo 49:16-18). Lilikuwa ninasimama katika nafasi ya maamuzi. Kuhakikisha Sheria na taratibu zake zinafuatwa ipasavyo.

Lakini pia lilisimama kusaidia Israeli, mahali popote walipoweka marago na kuondoka lilihusika kukusanya vitu vyote muhimu, na kuhakikisha watu wasiojiweza wanatembea Na kundi. (Hesabu 10:25).

Pamoja na hilo lilisimama kama mashujaa wa nyuma wa jeshi la Israeli, pale linapokwenda vitani lilisimama kulinda dhidi ya wavamizi wa nyuma.

lakini baadaye lilikuja kupoteza sifa yake ya kiuamuzi, kwasababu ya kwenda kusimamisha miungu ya kigeni na kuiabudu (Waamuzi 18).

  1. Naftali

Kabila la hekima na nguvu.

Ni kabila Ambalo lilikuwa na mchango mkubwa Katika eneo la kivita. Tunaweza kuona katika kipindi cha waamuzi kabila hili kwa uongozi wa  Debora na Baraka (Waamuzi 4:6), lilimshinda Sisera.

Lakini lilisimama Kama washauri wa kiroho kwa Israeli.

Mwanzo 49:21

[21]Naftali ni ayala aliyefunguliwa; Anatoa maneno mazuri.

Katika wakati wa Kristo, eneo La wanaftali ambalo lilikuwa sehemu ya Galilaya lilidharauliwa sana, na kuonekana nyonge,(Yohana 1:46,7:52) si tu kimaendeleo lakini pia kuwa na wapagani wengi, lakini ndio mahali Ambapo palikuwa mji wa makazi ya Masihi Yesu Kristo, sawasawa na unabii alioutoa Isaya.(Mathayo 4:13-16).

  1. Gadi

Gadi lilikuwa hodari katika vita, lisilojisalimisha kirahisi kwa maadui, lilisimama Kama Walinzi wa lango la mashariki la taifa la Israeli, pembezoni mwa Reubeni.

Mwanzo 49:19

[19]Gadi, jeshi litamsonga, Lakini atawasonga wao mpaka visigino.

  1. Asheri

Ni kabila ambalo halikujikita Sana katika mchango Wa kijeshi. Bali Lilikuwa ni kabila la kibiashara Tajiri, lenye kulinda uchumi wa nchi.

Mwanzo 49:20

[20]Asheri, chakula chake kitakuwa kinono, Naye atatoa tunu za kifalme.

  1. Isakari

Ni kabila Lilipewa neema katika kutambua Nyakati na kutoa mashauri sahihi ya kufanya. lilisimama kama washauri Wa taifa.

1 Mambo ya Nyakati 12:32

[32]Na wa wana wa Isakari, watu wenye akili za kujua nyakati, kuyajua yawapasayo Israeli wayatende; vichwa vyao walikuwa watu mia mbili na ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao.

  1. Zabuloni

Walichangia maaskari wa vita, kwasababu walikaa katika fukwe, iliwafanya wawe hodari katika biashara na uchuuzi.

Mwanzo 49:13 Zabuloni atakaa pwani ya bahari, Naye atakuwa kama pwani za kuegesha merikebu, Na mpaka wake utakuwa kando ya Sidoni.

  1. Yusufu(Efraimu na Manase)

Ni kabila lililopewa nguvu, kiutawala na kijeshi  , lilitimiza kusudi la kulisimamisha taifa la Israeli, hata wakati Israeli ilipogawanyika, makao makuu ya kabila zile 10, yalikuwa Ni samaria mji wa Efraimu. (Mwanzo 49: 22-26)

  1. Benyamini

Ni kabila Lililokirimiwa watu hodari wa vita watumiao mashoto (Waamuzi 20:16), ambao walisimama vema katika vita, ijapokuwa lilikuwa dogo, lililojichanganya katika kabila la Yuda ndio kabila la kwanza kutoa mfano Israeli (Sauli), na baadaye mtume Paulo.

La kujifunza: Kuwa mdogo haimaanishi kuwa utakuwa wa mwisho. Bwana anasema walio wa mwisho Watakuwa wa kwanza na wa kwanza watakuwa wamwisho.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini kabila la Dani na Efraimu hayaonekani yakiorodheshwa miongoni mwa yale makabila 12 ya Israeli katika Ufunuo 7?

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

Yakobo alimaanisha nini kusema ‘ndipo BWANA atakuwa Mungu wangu’ Mwanzo 28:21

WEWE U MWALIMU WA ISRAELI,NA MAMBO HAYA HUYAFAHAMU?

Print this post

Je mtu anaweza akawa hajaokoka akaombea mtu na Pepo likamtoka,

SWALI: Je mtu anaweza akawa hajaokoka akaombea mtu na Pepo likamtoka, na pia mtu anaweza akawa ameokoka akaombea mtu na pepo lisitoke ?


JIBU: Kuhusu swali la kwanza linalosema je mtu anaweza akawa hajaokoka kisha akaenda kuombea mtu mwenye pepo na hatimaye likamtoka?

Jibu ni la!,  haiwezekani mtu ambaye hajaokoka, akawa na uwezo wa kutoa pepo, kwasababu pale alipo yupo chini ya vifungo vya ibilisi, haiwezekani akaenda kumfungua mtu ambaye ni mfungwa mwenzake, inahitaji mtu aliye huru ndio aweze kufanya hivyo.

Bwana Yesu alisema…

Marko 3:23-27

[23]Akawaita, akawaambia kwa mifano, Awezaje Shetani kumtoa Shetani?

[24]Na ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, ufalme huo hauwezi kusimama;

[25]na nyumba ikifitinika juu ya nafsi yake, nyumba hiyo haiwezi kusimama.

[26]Na kama Shetani ameondoka juu ya nafsi yake, akafitinika, hawezi kusimama, bali huwa na kikomo.

[27]Hawezi mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu, na kuviteka vitu vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu; ndipo atakapoiteka nyumba yake.

Ni hatari huyo mtu akijaribu kufanya hivyo, kwasababu anaweza kukutana na madhara kama yaliyowakuta wale wana wa Skewa.(Matendo 19:13-16).

Kuhusu swali la pili linalouliza Je mtu ambaye ameokoka  anaweza akaombea na pepo lisitoke?

Jibu ni ndio Ikiwa mtu huyo anakiwango kidogo cha imani, si mapepo yote yanaweza yakatoka, kwasababu mashetani yanatofautiana kimadaraja (Mathayo 12:43-45), yapo yenye nguvu kubwa ya ukinzani, mengine huitwa wakuu wa giza, mengine wafalme na wenye mamlaka. (Waefeso 6:12)

Hivyo inahitaji nguvu zaidi za kiimani ambazo zinakuja kwa njia ya mifungo na maombi.

Ndio maana mitume kuna mahali walitoa kweli pepo wengi lakini kuna mahali hawakuweza kwasababu ya uhaba wa maombi. (Mathayo 17:14-21)

Lakini uhalisia ni kuwa mtu yeyote aliyeokoka, haijalishi amedumu sana katika wokovu au ni mchanga. Anayo mamlaka ndani yake ya kutoa pepo lolote lile, isipokuwa anahitaji pia na maombi ile mengine yasishindikane kwake.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAPEPO YANATAFUTA HIFADHI NDANI YAKO KWA BIDII SANA.

MWANAMKE, USIFUNGUE MLANGO WA MAPEPO KUKUINGIA!.

MAPEPO NI NINI?

Print this post

Kwanini Musa alisita kuitikia mwito wa Mungu alipoitwa mlimani?

Musa alikuwa na sababu kadha wa kadha za yeye kufanye vile, ikiwemo

  1.  Alijiona hastahili

Kutoka 3:11

[11]Musa akamwambia Mungu, Mimi ni nani, hata niende kwa Farao, nikawatoe wana wa Israeli watoke Misri?

  1. Kutolijua jina lake.

Musa aliogopa, kwenda kuwahubiria watu juu ya Mungu Ambaye hakulijua jina lake, kwani zamani zile, miungu yote ilifahamika kwa majina, hivyo alijiona kama kwenda kuwaambia watu habari za Mungu asiyejulikana jina lake, ni kama anawafedhehi.

Kutoka 3:13 Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n’nani? Niwaambie nini?

  1. Kujidhania kuwa watu hawatamwamini.

Kutoka 4:1

[1]Musa akajibu akasema, Lakini, tazama, hawataniamini, wala hawataisikia sauti yangu; maana watasema, BWANA hakukutokea.

 Kwasababu alikuwa hana ishara yoyote ya ki-Mungu ndani yake. 

  1. Kutokuwa na ujuzi wa kuongea

Kutoka 4:10

[10]Musa akamwambia BWANA Ee Bwana, mimi si msemaji, tokea zamani, wala tokea hapo uliposema na mtumishi wako; maana mimi si mwepesi wa kusema, na ulimi wangu ni mzito.

Pamoja na Mungu kumwakikishia kuwa atakuwa naye na kumsaidia lakini Musa bado akakataa, ndipo Mungu akaghadhibika na kumletea nduguye Haruni, kama msaidizi wake.

Jambo ambalo halikuwa mpango wa awali wa Mungu, kwani uongozi wa Haruni hakuwa kusudi kamilifu la  Bwana. Sababu kadha wa kadha zilizowapelekea wana wa Israeli kupata adhabu, zilikuwa ni pamoja na uongozi dhaifu wa Haruni. Utakumbuka wakati Musa amepanda juu mlimani kuchukua zile mbao mbili za amri  10, Haruni aliachiwa uongozi kwa muda, watu walipomfuata Kwa ajili ya hatma zao, akasikiliza mapendekezo yao akawaundia sanamu ya ndama ili waiabudu, ikapelekea Mungu kuwaangamiza wana wa Israeli wengi sana, (Kutoka 32:1-6) mzizi huo ni kutokana na kutokutii kwa Musa, halikadhalika sababu ya Musa kutoiona nchi ya ahadi ilichangiwa pia na uongozi hafifu wa Haruni, kwani kule Meriba kosa alilofinya Musa la kuchukua utukufu wa Mungu, alihusika na Haruni pia. (Hesabu 20:10-12)

Hivyo ni wazi kama angekuwa na imani na Mungu, mengi yasingetokea mbeleni. Hata wakati huu wa sasa, wengi wetu tumejikuta katika machaguzi ya pili ya Mungu kwasababu tu, ya kumpotezea imani, kuwa anaweza kutenda  kusudi lake lote hata katika Madhaifu yetu.

Mwamini Mungu mtegemee yeye tu.

Shikilia vifungu hivi vikusaidie.

Mithali 3:5

[5]Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe;

Isaya 6:8

[8]Kisha nikaisikia sauti ya Bwana, akisema, Nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo niliposema, Mimi hapa, nitume mimi.

2 Timotheo 1:7

[7]Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini Mungu alimchagua Musa, na si mtu mwingine?

Je ni sala gani inahitajika kabla ya kumchinja mnyama katika ukristo?

Je maombi ya mlimani yana ulazima wowote kwa mkristo?

Print this post

Nini maana ya kizazi cha Nne kitarudi hapa? (Mwanzo 15:16)

Jibu: Turejee..

Mwanzo 15:16 “Na kizazi cha nne kitarudi hapa, maana haujatimia uovu wa Waamori bado”.

Ili tuelewe vizuri tuanzie ule mstari wa 13..

Mwanzo 15:13 “Bwana akamwambia Abramu, Ujue hakika ya kwamba uzao wako utakuwa mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia watu wale, nao watateswa muda wa miaka mia nne.

14 Hata na taifa lile, watakaowatumikia, nitawahukumu; baadaye watatoka na mali mengi.

15 Lakini wewe utakwenda kwa baba zako kwa amani, utazikwa katika uzee mwema.

16 NA KIZAZI CHA NNE KITARUDI HAPA, MAANA haujatimia uovu wa Waamori bado”

Katika mistari hiyo Bwana MUNGU anamwambia Abramu kuhusiana na uzao wake kwamba utaenda utumwani katika nchi isiyo yake (ambayo ni nchi ya  Misri) na utamtumikia Farao kwa muda wa miaka 400, na baada ya miaka hiyo watatoka Misri.

Sasa wakati Bwana anamwambia Abramu hayo maneno, Abramu alikuwa tayari yupo katika nchi hiyo ya ahadi, isipokuwa bado alikuwa hajaimiliki kwani uzao wake ulikuwa bado mdogo na ilikuwa ni sharti uende kwanza Misri, ukaongezeke huko na kukua,  ndio maana  Mungu anamwambia kuwa utapelekwa utumwani na kisha utarudi tena katika hiyo nchi Abramu aliyopo muda huo, na itawaondoa wenyeji wa nchi hiyo.

Sasa swali nini maana ya “Kizazi cha Nne kitarudi”..

Jibu: Zamani kizazi kimoja kilihesabika kwa miaka 100, hiko ni kizazi kimoja, kwahiyo vizazi vinne maana yake ni miaka 400.. na mwisho wa hiyo miaka 400 ndio wana wa Israeli walitoka Misri.

Lakini swali lingine ni hili: Ni kwasababu gani uzao wa Abramu ukae Misri miaka muda mwingi hivyo? (400).. Jibu tunalipata katika ule mstari wa 16 unasema..“Na kizazi cha nne kitarudi hapa, maana haujatimia uovu wa Waamori bado”

Kumbe ilihitajika UOVU WA WAAMORI UTIMIE!!..Na hiyo yote ni kuonyesha huruma za MUNGU, kwamba si mwepezi wa hasira, mpaka aachilie ghadhabu yake maana yake ni kwamba kiwango cha maasi kimezidi sana..kile kikombe cha ghadhabu kinakuwa kimejaa..

Kwahiyo hapo aliposema haujatimia uovu wa Waamori, maana yake kiwango cha maasi cha Waamori bado hakikuwa kingi kiasi cha kupigwa na MUNGU..  Lakini baada ya miaka 400 kile kiwango cha maovu na maasi ya Waamori, na ya watu wengine waliokuwa wanaishi Kanaani kilifika kilele, na ndipo MUNGU akaachilia hukumu yake kwa kuwaondoa.

Utazidi kuona MUNGU anawakumbusha wana wa Israeli kuwa sababu ya wenyeji wa Kanaani kuondolewa katika ile nchi, si kwasababu ya utakatifu wa wana wa Israeli, bali ni kwasababu ya maasi ya waliokuwa wanaikalia ile nchi.

Kumbukumbu 9:3 “Basi jua siku hii ya leo kuwa Bwana, Mungu wako, ndiye atanguliaye kuvuka mbele yako kama moto uteketezao; atawaangamiza, tena atawaangusha mbele yako; ndivyo utakavyowafukuza na kuwapoteza upesi, kama alivyokuambia Bwana.

4 USISEME MOYONI MWAKO, BWANA, MUNGU WAKO, ATAKAPOKWISHA KUWASUKUMIA NJE MBELE YAKO, UKASEMA, NI KWA HAKI YANGU ALIVYONITIA BWANA NIIMILIKI NCHI HII; KWANI NI KWA AJILI YA UOVU WA MATAIFA HAYA BWANA AWAFUKUZA NJE MBELE YAKO.

5 Si kwa haki yako, wala kwa unyofu wa moyo wako, hivi uingiavyo kuimiliki nchi yao; lakini ni kwa uovu wa mataifa haya Bwana, Mungu wako, awafukuza nje mbele yako; tena apate kuliweka imara hilo neno Bwana alilowaapia baba zako Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo.

6 Basi jua ya kuwa Bwana, Mungu wako, hakupi nchi hii nzuri uimiliki kwa ajili ya haki yako, kwa maana u taifa lenye shingo ngumu”.

Umeona?… Na MUNGU ni yule yule hajabadilika, kama alivyowavumilia Waamori, na waanaki na Wahiti waliokuwa wanaikalia ile nchi ya ahadi kwa miaka 400, anatuvumilia hata sasa, lakini uvumilivu wake ni ili  sisi tutubu, kwasababu hapendi hata mmoja apotee..

Warumi 2:4  “Au waudharau wingi wa wema wake na ustahimili wake na uvumilivu wake, usijue ya kuwa wema wa Mungu wakuvuta upate kutubu?

5  Bali kwa kadiri ya ugumu wako, na kwa moyo wako usio na toba, wajiwekea akiba ya hasira kwa siku ile ya hasira na ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu”.

Je umeitikia wito wa YESU?, Kama bado hujageuka na kumfuata YESU basi usipoteze muda Zaidi, huu ndio wakati, duniani imefikia kilele kabisa cha maovu na maasi, muda wowote parapanda italia na kile kikombe cha ghadhabu ya MUNGU kitamiminwa duniani.

Bwana atusaidie tusiwe miongoni mwa watakaokabiliana na mkono wa BWANA.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha kwanza cha Petro.(1Petro)

Kichwa cha kitabu hichi kinasema “Waraka wa kwanza wa Petro kwa watu wote” Kutuonyesha kuwa Petro Ndiye mwandishi.

Waraka huu mfupi aliuelekeza kwa watakatifu wote waliotawanyika, na kuishi kama wageni maeneo ya Asia ndogo ambayo kwasasa ni nchi ya Uturuki.

Maudhui makuu ya waraka huu tunaweza kuyagawanya katika sehemu kuu nne(4):

1) Ni kuwafariji watakatifu kwa kuwaeleza juu ya utukufu walioandaliwa mbinguni utakaofunuliwa siku ya mwisho. Na kwamba kwa kulitambua hilo basi wafurahi Katika majaribu mbalimbali ya imani, yaliyo ya kitambo tu.

2) Lakini pia unalenga kuwahimiza kuishi maisha ya utakatifu ya kumpendeza Mungu katika wakati wao wa kuishi hapa duniani.

3) Vilevile wajibu wakuishi maisha ya nidhamu katika Jamii ya wasioamini inayowazunguka.

4) Halikadhalika wajibu wa viongozi kulichunga kundi la Kristo kwa uaminifu wotena wajibu wa kanisa lote kumpinga shetani.

Haya ni maelezo mafupi juu ya kila kipengele:

1) Faraja katika dhiki mbalimbali.

Petro anawahimiza watakatifu kwamba wafurahi katika majaribu mbalimbali (kuliko kuhuzunika) kwa sababu ya uthamani mkuu wa imani yao itakayolipwa siku ile ya mwisho ambayo Yesu atafunuliwa kwetu.

1 Petro 1:6-7

[6]Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali;

[7]ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo.

> Petro Anahimiza kuiga kielelezo cha Kristo ambaye yeye alikubali kuteswa ijapokuwa hakutenda Dhambi, hata alipotukanwa hakurudisha majibu. Vivyo hivyo na sisi tukubali teso lolote kwa ajili yake katika upole wote, uvumilivu na ustahimilivu.

1 Petro 2:19-21

[19]Maana huu ndio wema hasa, mtu akivumilia huzuni kwa kumkumbuka Mungu, pale ateswapo isivyo haki.

[20]Kwa maana ni sifa gani kustahimili, mtendapo dhambi na kupigwa makofi? Lakini kustahimili, mtendapo mema na kupata mateso, huu ndio wema hasa mbele za Mungu.

[21]Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake.

1 Petro 4:12-16

[12]Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho.

[13]Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.

[14]Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia.

[15]Maana mtu wa kwenu asiteswe kama mwuaji, au mwivi, au mtenda mabaya, au kama mtu ajishughulishaye na mambo ya watu wengine.

[16]Lakini ikiwa kwa sababu ni Mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu katika jina hilo.

2) Wito wa kuishi maisha matakatifu.

Sehemu hii ya pili Mtume Petro anawahimiza watakatifu, kuwa kwasababu wanatazamia neema itakayofunuliwa siku ya mwisho ya kuja kwake Yesu Kristo (1:13), hivyo hawana budi kuishi maisha ya kiasi na utakatifu hapa duniani.

1 Petro 1:13-16

[13]Kwa hiyo vifungeni viuno vya nia zenu, na kuwa na kiasi; mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika ufunuo wake Yesu Kristo.

[14]Kama watoto wa kutii msijifananishe na tamaa zenu za kwanza za ujinga wenu;

[15]bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;

[16]kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.

1 Petro 2:1-2

[1]Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote.

[2]Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu;

> Petro anaendelea kuwasihi watakatifu waishi kama wapitaji duniani, kwa kuziepuka tamaa za mwili.

1 Petro 2:11

[11]Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho.

1 Petro 4:2-3

[2]Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.

[3]Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;

> Anaeleza pia Wajibu wa kupendana kuhurumiana, kunyenyekeana, tuwe watu wasiolipa baya kwa baya, bali wenye kubariki(3:8-12, 4:7)

> Kadhalika pia anaeleza wajibu wa wanandoa. Kwamba wake wawatii Waume zao, na kujipamba kwao kunapaswa kuwe kwa mapambo ya rohoni, Lakini pia waume kuishi na wake zao kwa akili. (3:1-7)

3) Mwenendo wa nidhamu kwa watu walio nje

Katika sehemu hii ya tatu anahimiza watakatifu kuwa na mwenendo unaopasa kwa watu wasioamini, ili wakose nafasi ya kutushitaki au kutulaumu kwa lolote.

> Anagusia katika eneo la watumwa Kwamba wawatii bwana zao, si wale tu wapole bali pia wale wakali.(2:18)

> Lakini pia Watakatifu waitii kila kilichoamriwa na mamlaka.

1 Petro 2:13-15

[13]Tiini kila kiamriwacho na watu, kwa ajili ya Bwana; ikiwa ni mfalme, kama mwenye cheo kikubwa;

[14]ikiwa ni wakubwa, kama wanaotumwa naye ili kuwalipiza kisasi watenda mabaya na kuwasifu watenda mema.

[15]Kwa sababu ndiyo mapenzi ya Mungu, kwamba kwa kutenda mema mzibe vinywa vya ujinga vya watu wapumbavu;

> Lakini pia anahimiza watakatifu wawaheshimu watu wote(2:17)

4) Wito kwa viongozo wa kanisa.

Mwishoni Petro anatoa wito wa waangalizi wa kanisa la Mungu (wazee), kwamba walichunge kundi kwa hiari, sio kwa kulazimishwa au kutazamia malipo ya kifedha, bali kwa moyo.

1 Petro 5:1-3

[1]Nawasihi wazee walio kwenu, mimi niliye mzee, mwenzi wao, na shahidi wa mateso ya Kristo, na mshirika wa utukufu utakaofunuliwa baadaye;

[2]lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo.

[3]Wala si kama wajifanyao mabwana juu ya mitaa yao, bali kwa kujifanya vielelezo kwa lile kundi.

> Pamoja na hayo anasisitiza watakatifu wote wawe na kiasi na kukesha, kwasababu adui yetu ibilisi ni mfano wa simba angurumaye akitafuta mtu ammeze, hivyo wana wajibu wa kumpinga sikuzote.(5:8-9)

Hitimisho: 

Hivyo kwa maelezo machache ni kwamba Petro analihimiza kanisa kutembea katika uvumilivu wote na uthabiti Wa imani, pamoja na utakatifu, na kutimiza wajibu wao katika utakatifu na adabu kwa wanadamu wote, katika wakati ambao kanisa linasubiria neema kuu itakayofunuliwa siku ya mwisho Yesu atakaporudi.

Na ndivyo ambavyo sote tunapaswa tuishi hivyo sasa.

Kama mkristo je unaendelea kufurahi katika majaribu? Unaishi maisha matakatifu? Unaishi vema na jamii yako? unaifanya kazi ya Mungu? Unampinga shetani kwa kudumu katika sala?

Ikiwa hayo, unayazingatia basi, wewe ni mshirika wa neema hiyo kuu ya Mungu itakayofunuliwa siku ya mwisho.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakolosai

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)

MAANA YA KUISHI NA MKE KWA AKILI.

JINSI ITAKAVYOKUWA KATIKA SIKU ILE

Print this post

USIRUDI NYUMA KATIKA IMANI

Tukiwa bado tupo mwanzo wa mwaka, ni wakati wa kushika sana vile tulivyo navyo na kuendelea mbele, wala si wakati wa kurudi nyuma kabisa.

Usiyarudie mambo ya kale uliyoyaacha, usiyatamani mambo ya kale uliyoyakimbia, usiirudie njia  ya kale uliyoikataa…

Ulikuwa upo mbali na anasa mwaka jana, basi huu si mwaka wa kuzirudia tena, usirudie ulevi uliouacha miaka ya nyuma, usirudie uzinzi ulioushinda miaka ya nyuma, usirudie kujichua ulikokuacha miaka ya nyuma,

Usirudie mavazi yasiyo na staha uliyoyaacha miaka ya nyuma, usirudie wala kuitamani mitindo ya kidunia uliyoiacha mwaka jana.

Usirudie starehe za kidunia, mwanzo huu wa mwaka ni wakati ambao shetani anafanya kazi kubwa sana kuwarudisha watu nyuma kiroho, na atashambulia mambo yafuatayo ili kuhakikisha mwamini anarudi nyuma kiroho.

    1. Afya.

Atajaribu kukuletea mashambulizi katika eneo la afya, kwa kuitikisa afya yako au ya watu wako wa karibu, ikiwemo pia afya ya uzazi.. Simama endelea mbele usirudi nyuma!.

     2. Uchumi.

Atajaribu kutikisa uchumi wako lakini, hawezi kuondoa baraka zako za mwaka, hivyo usitishwe na vimitikisiko vya uchumi vya ibilisi vya hapa na pale, ni vya muda tu wewe endelea mbele usirudie biashara haramu wala tamaa za mali ulizoziacha huko nyuma endelea mbele kwani Bwana anakujua.

     3. Ndoa.

Atakuletea vimitikisiko vya kifamilia vya hapa na pale, pia visikutishe kwani ni kawaida yake kutishia, lakini wewe endelea mbele na imani usirudie magomvi uliyoyaacha miaka ya nyuma, usirudie anasa za kupunguza mawazo ulizoziacha huko nyuma…yapo mambo mazuri mbele yako kwaajili ya huu mwaka.

Pia ondoa hofu ya kesho…kwamba itakuwaje kesho, itakuwaje disemba…ndio usijizuie kutafakari yajayo, lakini usiufanye moyo wako kuwa mzito kwaajili ya hayo, kwani huo pia ni mlango mwingine wa ibilisi kumrudisha mtu nyuma.

Ukiwa ndani ya Kristo fahamu kuwa mambo yote yatakuwa sawa, haijalishi itachukua muda gani au mambo yanaanzaje…kushinda ni lazima! na ni AMRI.

Usirudi nyuma Baba, usirudi nyuma Mama, usirudi nyuma kaka, usirudi nyuma dada, usirudi nyuma mtoto…kwani matokeo ya kurudi nyuma ni kumfadhaisha Bwana.

1 Samweli 15:11”Najuta kwa sababu nimemtawaza Sauli awe mfalme; maana amerudi nyuma, asinifuate, wala hakufanya nilivyomwamuru. Samweli akasikitika, akamlilia BWANA usiku kucha”.

Utakapofika mwisho wa mwaka tena uwe na sababu ya kumshukuru Bwana kama amekulinda hujarudi nyuma.

Ayubu 23:12 “Sikurudi nyuma kuiacha amri ya midomo yake; Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu”.

Lakini kama ulikuwa umeshaanza kurudi nyuma, bado hujachelewa hebu kataa hiyo njia na leo mwombe Bwana rehema na kuziacha hizo njia utaona maajabu ya Bwana, kwani atakutia nguvu na utaendelea mbele kwa mbio kubwa, Bwana atakurehemu na utamfurahia.

Hosea 14:4 “Mimi nitawaponya kurudi nyuma kwao; nitawapenda kwa ukunjufu wa moyo; kwa maana hasira yangu imemwacha”.

Isaya 50:5 “Bwana MUNGU amenizibua sikio langu, wala sikuwa mkaidi, wala sikurudi nyuma

Lakini usipojali na kuendelea katika njia hiyo ya kurudi nyuma, ipo hatari mbele yako..

Mithali 1:32  “Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua,

Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza”

USIRUDI NYUMA! USIRUDI NYUMA!…USIRUDI NYUMA!.

Ukiwa utahitaji msaada wa maombezi ili uzidi kusimama, basi piga namba hizi 0789001312.

Bwana anakupenda, na Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

USIRUDI NYUMA KWA KUITUMAINIA HAKI YAKO.

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

NI LAZIMA KUISHIKILIA IMANI MPAKA MWISHO.

SHIKA SANA ULICHO NACHO, ASIJE MTU AKAITWAA TAJI YAKO.

USIIGE TABIA YA NAAMANI

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha Wafilipi.

Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha wafilipi

Kama pale mwanzo kinavyojitambulisha “Waraka wa Paulo mtume kwa wafilipi”.

Paulo ndiye mwandishi wa kitabu hiki. Ni moja ya nyaraka ambazo Paulo aliziandika akiwa kama mfungwa, aidha kule Rumi.

Maudhui makuu ya waraka huu mfupi wenye sura nne(4) yalikuwa ni kuwatia moyo watakatifu na kuwahimiza waiendeleze furaha ya Mungu ndani yao,bila kukwamishwa na dhiki za aina yoyote, lakini pia sehemu ya pili ni kuwataka wapige hatua katika mwenendo wao ndani ya injili waliyoipokea.

Tukianza na hiyo sehemu ya kwanza:

1) Furaha ndani ya Kristo

Paulo anahimiza watakatifu kufurahi katika dhiki zote, ikizingatiwa kuwa Kanisa hili lilishuhudia vifungo na mapigo mengi ya Paulo. Kama tunavyosoma kwenye Matendo 16:16-40, Kule ambapo Paulo na Sila walipigwa sana na kutupwa gerezani, biblia inatuambia kulikuwa ni huku Filipi. Lakini hata katika waraka huu bado anashuhudia kuwa dhiki zake, zimekuwa wazi kwa maaskari, na watu wote wa huko (1:12-13).

Hivyo Paulo alijua watu wa Filipi huwenda wakawa na huzuni nyingi juu yake, au juu ya injili, kutokana na dhiki nyingi walizoziona kupitia yeye.

Lakini hapa anawaeleza kuwa yeye anafuraha sikuzote katika Kristo.

> Anaendelea kueleza furaha yake haiathiriwi na watu wanaomzushia fitna ili apitie mateso, maadamu anayeathirika ni yeye si Kristo. Basi bado anafurahi..(1:17-18)

> Anasema hata akihukumiwa kifo kwa ajili ya watakatifu, bado furaha yake itazidi zaidi wala haiwezi kuathiriwa..

Wafilipi 2:17-18

[17]Naam, hata nikimiminwa juu ya dhabihu na ibada ya imani yenu, nafurahi; tena nafurahi pamoja nanyi nyote.

[18]Nanyi vivyo hivyo furahini, tena furahini pamoja nami.

Hivyo anawahimiza pia na wafilipi wafurahi kama yeye, wala wasione huzuni kwasababu ya dhiki hizi, kwasababu tumewekewa kuwa sehemu yetu katika ushuhuda wa injili.

Wafilipi 1:29

[29]Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake;

Hizi ni sehemu nyingine kadha wa kadha Paulo akihimiza jambo hilo hilo,

Wafilipi 3:1

[1]Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana.

Wafilipi 4:4

[4]Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.

Sehemu ya Pili:

2) Mwenendo upasao injili

Katika sehemu ya pili Paulo anahimiza watakatifu kuwa na mwenendo unaipasa injili waliyopokea. Na hiyo ni ili wasiwe na ila na lawama,na udanganyifu. Kuonyesha kuwa injili, inayo na taratibu zake..Sio kuamini tu na kusema nimeokoka…bali pia kutii agizo lake.

Wafilipi 1:27

[27]Lakini mwenendo wenu na uwe kama inavyoipasa Injili ya Kristo, ili, nikija na kuwaona ninyi, au nisipokuwapo, niyasikie mambo yenu, kama mnasimama imara katika roho moja, kwa moyo mmoja mkiishindania imani ya Injili;

Anaendelea kusema watakatifu wana wajibu wa kunia mamoja, kutenda mambo yote bila majivuno,wala manung’uniko, wala mashindano, wanapaswa kutenda yote bila ubinafsi bali na ya wengine..

Anasisitiza watakatifu wanapaswa wawe wanyenyekevu, wenye nia ya Kristo..ambaye yeye hapo mwanzo alikuwa kama Mungu lakini alijishusha kwa kukubali kuachia nafasi yake, akawa kama mtumwa, akajinyenyekeza mpaka mauti ya msalaba,lakini Mungu akamkweza zaidi ya vitu vyote..Na sisi tulioipokea injili tunapaswa tuwe na nia hiyo hiyo ya unyenyekevu.(2:1-16)

Anasisitiza zaidi Wakristo wanapaswa wawe wapole, pia wawe waombaji na wenye shukrani.(4:5)

Halikadhalika ni wajibu wetu sote kuutumiza wokovu tulioupokea kwa kuogopa na kutetemeka, kwasababu ndiye Mungu atendaye kazi ndani yetu.(2:12-13)

Pamoja na hayo Watakatifu wana wajibu pia wa kuyahakiki mambo yote yaliyo mazuri na kuyaiga, (2:1-2)

Wafilipi 4:8

[8]Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.

Lakini pia anawatahadharisha kujiepusha na wahubiri wa uongo akianzana na wayahudi (watu wa tohara), ambao wanahubiri wokovu kwa njia ya torati zaidi ya ile tuipatayo ndani ya Kristo Yesu kwa njia ya imani. (3:1–16,)

Pamoja watumishi ambao fundisho lao ni la mambo ya duniani tu, na sio yale ya kumwelekeza mtu mbinguni (3:17-21).

Mwisho, Paulo anatoa salamu zake, na shukrani kwa huduma ya utoaji kanisa hilo lililomfanyia, na linaloendelea kumfanyia.

Hivyo kwa hitimisho, waraka huu maudhui kuu ni kuwafariji watakatifu wafurahi katika mambo yote, tukizingatia tunda la Roho ni furaha. Yesu alisema tufurahi na kushangalia pale tunapoudhiwa, kwa ajili ya jina lake. Hivyo, hakuna eneo lolote furaha ya Mungu ndani yetu ,inastahili kukatishwa. Tupitiapo magonjwa kama Epafrodito(2:25-30), shida, njaa, tumefundishwa kuyaweza yote ndani ya Kristo(4:12-3). Hivyo furaha yetu haiwezi kuathiriwa..Ilinde furaha yako.

Lakini anahimiza mwenendo upasao injili. Kwamba huo utaweza kufanikiwa pale tunapokubali kuwa na nia kama ile ya Kristo, ya unyenyekevu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Watu wa nyumbani mwa Kaisari ni watu gani? (Wafilipi 4:22).

Epafrodito ni nani kwenye biblia?

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakolosai

Uchambuzi na mwandishi wa kitabu cha Waefeso.

Rudi Nyumbani

Print this post