Title Devis

NG’OMBE MWEKUNDU ALIYEZALIWA ISRAELI, ANAFUNUA NINI?

Utakumbuka tarehe 28/8/2018 kulitokea tukio la kihistoria Israeli la kuzaliwa kwa ng’ombe mke mwekundu. Kulingana na chuo cha kidini kijihusishacho na mambo ya Hekalu kinasema jambo hilo halikuwahi kutokea kwa zaidi ya miaka 2000, tangu kuharibiwa kwa hekalu la pili pale Yerusalemu. Wanaamini tangu wakati wa Musa hadi kuharibiwa kwa hekalu la pili jumla ya ng’ombe tisa tu wa namna hiyo ndio waliotolewa sadaka kwa ajili ya kuwatakasa watu.
 
Tunasoma wakati wana wa Israeli walipokuwa jangwani Mungu alitoa maagizo kwa kuhani mkuu, kwamba atwae ng’ombe mmoja wa kike, mwekundu, asiye na mapungufu ya aina yoyote, yaani asiwe na jeraha au kilema chochote, asiwe na manyoya ya rangi nyingine yaliyochangikana na hayo mekundu hata kama likionekana nyoya moja tu tayari huyo hafai, anapaswa awe hajazaa, pia anapaswa awe bado hajapandwa na mtu yeyote, au hajatumika kwa kazi yoyote ile, hata kama atakuwa ni mwekundu lakini akiwa ameshawahi kuwekewa hata tambara tu la mizigo juu yake au amefungwa nira shingoni mwake huyo tayari hastahili…
 
Sasa hiyo ndio iliyokuwa inamfanya ng’ombe huyu awe adimu, atakayekidhi vigezo vyote hivyo.. ng’ombe huyo alikuwa anatumika kuwasafisha wana wa Israeli, baada ya kuteketezwa nje ya kambi, majivu yake yalikuwa yanachukuliwa na kuchanganywa na maji masafi, kisha mtu yeyote ambaye alikuwa amenajisika aidha kwa kuishika maiti, au kushika kaburi, au kuwa na maiti nyumbani, au alishika maiti ya mnyama aliyekufa au mzoga basi alinyunyiziwa maji hayo yaliyochanganywa na hayo majivu kwanza kwa muda wa siku tatu, kisha siku ya saba anakuwa safi ndipo aruhusiwe kuingia hemani au hekaluni. Hiyo ilikuwa ni sheria mtu yeyote na aliyekiuka amri hiyo ilikuwa adhabu yake ni kifo.
 
Hivyo ng’ombe huyo alikuwa ni wa muhimu sana katika ibada za hekaluni, yaani kwa namna nyingine bila kuwepo ng’ombe huyo hakuna shughuli zozote za hekuluni zinaweza kuendelea.
 
Hesabu 19:1 “Bwana akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,
 
2 Hii ndiyo amri ya sheria Bwana aliyoagiza, akisema, Waambie wana wa Israeli wakuletee ng’ombe mke mwekundu asiye na kipaku, mkamilifu, ambaye hajatiwa nira bado;
 
3 nanyi mtamleta kwa Eleazari kuhani, naye atakwenda naye nje ya kambi, na mtu mmoja atamchinja mbele yake”;
 
Lakini Kama wengi tunavyofahamu ng’ombe huyu katika agano jipya anasimama kama Bwana wetu Yesu Kristo, yeye ndiye dhabihu iliyotolewa isiyokuwa na ila wala mawaa, Bwana Yesu alikuwa mkamilifu sana hakuna asiyejua hilo, alikuwa hana doa la kasoro yoyote katika mwili wake wala katika roho yake, alikuwa ni dhabihu iliyokamili tayari kwa kafara kwa ajili yetu.
 
Ni ng’ombe mwekundu kwasababu ni ng’ombe wa damu, kumfunua Bwana wetu Yesu Kristo kwamba agano atakaloingia na sisi ni damu yake mwenyewe. Na ndio maana hata tukisoma katika ufunuo, tunamwona siku ile atakaporudi mara ya pili atakuwa na vazi jekundu lililochovya katika damu, kufunua ni jinsi gani alivyotukomboa sisi kwa damu yake..
 
Ufunuo 19:11 “Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.
 
12 Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.
 
13 Naye amevikwa VAZI LILILOCHOVYWA KATIKA DAMU, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.”
 
Sasa leo hii kwanini tukio kama hilo limejirudia Israeli?, Kumbuka Wayahudi ni watu wa mwilini, na pale walipo wanajiandaa kwa kuja kwa masihi wao na kwa ujenzi wa hekalu la tatu, ambalo wanaamini kwa kupitia hilo Masihi ndipo atakaposhukia..Na kwa muda mrefu walikuwa wakijiuliza hata hekalu litakapojengwa, tutampata wapi huyu ng’ombe mwekundu wa ajili ya utakaso wa watu watakao najisika kwa zile sababu tulizozitaja hapo juu.
 
Lakini mwaka jana tarehe 28/8/2018 tendo hilo lilitimia, Na hiyo ilikuwa ni Mungu kuwathibitishia kuwa hivi karibuni Hekalu litajengwa, Kumbuka ndugu kwetu sisi wakristo kinaweza kisiwe kitendo cha maana sana kwani sisi tunafahamu kuwa dhabihu halisi ni YESU KRISTO na sio ng’ombe. Lakini wayahudi bado hawajapata neema hiyo, hivyo Mungu pia anasema nao kwa ishara wanazoziamini ili tu kuwathibitishia kuwa wakati wao upo karibu sana..Hata siku ile watakapofumbuliwa macho na kumwamini masihi, ndipo watafahamu kila kitu.
 
Ni wakati gani huu tunaishi? Una habari kuwa neema itahama na kuiendea Israeli? Na ikishahamia Israeli, sisi huku mlango utakuwa umeshafungwa? Ni dhiki kuu ya mpinga kristo itakuwa inaendelea, wakati huo Unyakuo utakuwa umeshapita.. Leo hii unaichezea hii neema laiti ungeona ni wayahudi wangapi wanalia usiku na mchana pale YERUSALEMU kwenye ukuta wa maombolezo, wanamlilia Mungu wao aje kuwaokoa na kuwapigania kama ilivyokuwa katika enzi za kale, ambapo kimsingi ni kweli watarudiwa. halafu sisi huku watu wa Mataifa tunachezea wokovu, siku zimeshakaribia sana, watauona wokovu ambao wanautaabikia sasa.
 
Wayahudi leo hii wanasema ikiwa Mungu hakutuletea ng’ombe huyu kwa muda wa zaidi ya miaka 2000 na amemleta leo, ni ishara kuwa huu ndio wakati aliouandaa wa sisi kumjengea hekalu.
 
Ndugu hatuna mengi ya kuzungumza hapo, huu ni wakati wa kuchagua ni upande upi wa kusimama, Kipindi hichi kifupi tulichobakiwa nacho kitumie vizuri, maana hatujui kesho ni nini kitatokea? tubu dhambi zako zote leo kwa Bwana Yesu kama bado hujafanya hivyo, jitwike msalaba wako umfuate, kisha ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi kwa jina la YESU KRISTO upate ondoleo la dhambi zako, kulingana na Matendo 3:38 ili Mungu akupe Roho wake mtakatifu ambaye atakulinda na kukuongoza katika kuijua kweli yote ya Biblia..Kumbuka pasipo Roho Mtakatifu hakuna Unyakuo..Unasubiri nini?
 
Bwana akubariki.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP



 

Mada Nyinginezo:

WAISRAELI WENGI SANA WANARUDI KWAO SASA.

AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA.

SIKU YA TAABU YA YAKOBO.

NOTI YA UFALME WA MBINGUNI.

SIKU YA BWANA INAYOTISHA YAJA!

UNYAKUO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

HAMJAFAHAMU BADO?

 Moja ya mambo ya muhimu sana ambayo Roho Mtakatifu anayafanya ndani ya mtu baada ya kukata shauri la kumfuata Yesu Kristo, kwa moyo wote ni “KUMWONDOLEA HOFU YA MAISHA HAYA” Karibia kila mwamini katika hatua za kwanza kwanza kabisa, Roho Mtakatifu ni lazima ampitishe katika madarasa ya kumwondolea hofu ya Maisha haya…Kwasababu katika hali ya kawaida wanadamu wote tukishafikisha umri fulani, tayari hofu ya Maisha inakuja yenyewe ndani yetu…Hofu ya Kesho itakuwaje! Mwakani nitaishije! Nitakula nini wiki zijazo, nitaishije ishije! Na mambo mengine mengi…Hofu hii haijalishi wewe ni nani, maadamu umeshaitwa mtu, tena mwenye Akili timamu lazima ije ndani yako…Ni hofu ambayo inamfanya mtu awe mtumwa wa Kesho! Ni hofu ambayo inamfanya mtu asiwe anaridhika na mwisho wa siku anakuwa katika mkandamizo mkubwa wa mawazo..

Sasa Roho Mtakatifu anajua kabisa hatuwezi kumtumikia Mungu katika hali hiyo ya utumwa wa Kesho itakuwaje! Kwasababu hiyo basi ni lazima ampitishe katika kipindi fulani cha madarasa, kuipunguza hiyo hofu ndani ya Mtu ili aweze kuishi kwa furaha akiwa ndani ya Yesu.

Hebu fikiria mwanao, anakaa nyumbani mwako, halafu anakwenda shule huku anamashaka kwamba Kesho anaweza asipate chakula nyumbani, au akiwa na mashaka kwamba atakosa ada! Je! Huyo mtoto atasoma kweli, au atafanya vizuri darasani? Ni wazi kuwa hatasoma bali atakuwa ni mtu tu wa mawazo siku zote! Na itamsababishia kufeli, na hivyo hivyo Mawazo ya Maisha haya na mawazo ya Kesho itakuwaje! Itatusababishia tusimwelewe Mungu na kutusababisha tufeli mitihani mingi ya Maisha yetu ya kikristo.

Kulitatua hilo Bwana Yesu aliwafundisha wanafunzi wake masomo kadhaa, ya kutohofia Kesho, na hivyo kwa masomo hayo pia anatufundisha na sisi…Embu tusome tukio hili moja..

Mathayo 16:5 “Nao wanafunzi wakaenda hata ng’ambo, wakasahau kuchukua mikate.

6 Yesu akawaambia, Angalieni, jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.

7 Wakabishana wao kwa wao, wakisema, Ni kwa sababu hatukuchukua mikate.

8 Naye Yesu akafahamu, akawaambia, Mbona mnabishana ninyi kwa ninyi, enyi wa imani chache, kwa sababu hamna mikate?

9 Hamjafahamu bado, wala hamkumbuki ile mikate mitano kwa wale elfu tano, na vikapu vingapi mlivyoviokota?

10 Wala ile mikate saba kwa watu elfu nne, na makanda mangapi mliyoyaokota?

11 Imekuwaje hamkufahamu ya kuwa si kwa sababu ya mkate naliwaambia? Ila jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.

12 Ndipo walipofahamu ya kuwa hakuwaambia kujilinda na chachu ya mkate, bali na mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo”

Somo hilo Bwana Yesu aliwafundisha wanafunzi baada ya Wanafunzi wake kusahau kubeba mikate ya safari yao..Hivyo walipofika njiani, Bwana Yesu akawaambia wajihadhari na chachu ya mafarisayo, wenyewe wakadhani anawashutumu kwanini hawakubeba mikate katika safari yao..na hivyo hawana kitu cha kula, kwamba Bwana kawakataza wasile chachu ya mafarisayo…(kumbuka chachu ni hamira, na chachu ilikuwa inawekwa kwenye mikate, hivyo mtu akizungumzia chachu ilikuwa inajulikana kwamba anazungumzia mikate yenye Hamira)..

Hivyo wanafunzi wakahuzunika sana, kwasababu watakwenda kukaa na njaa bila chakula huko wanakokwenda…Lakini Bwana Yesu aliwakemea na kuwaambia wana Imani chache…kwasababu wameshasahau jinsi gani Bwana alifanya miujiza ya kutokeza maelfu ya mikate kutoka katika mitano tu na maelfu ya watu wakala na kusaza na kukusanya mabaki mengi tena mara mbili… kama Mungu aliweza kufanya hivyo huko nyuma kwanini asiwafanyie tena hivyo huko mnakokwenda?? Huo ndio ulikuwa ujumbe wa Bwana! Wasianze kutafakari tafakari Kesho wakula nini? Kesho kutwa watavaa nini…wao kazi yao ni kuangalia mbele kuitenda kazi ya Mungu na hayo mengine watazidishiwa…

Tunaona tena mahali pengine Bwana Yesu alizidi kulitilia mkazo jambo hilo katika Mathayo Mlango wa 6

Mathayo 6: 24 “Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.

25 Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?

26 Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Ninyi je! Si bora kupita hao?

27 Ni yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?

28 Na mavazi, ya nini kuyasumbukia? Fikirini maua ya mashamba, jinsi yameavyo; hayafanyi kazi, wala hayasokoti

29 nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo.

30 Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?

31 Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?

32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.

34 Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake”

Unaona! Bwana anatufundisha ni jinsi gani, Kesho yetu ipo mikononi mwake, kwamba haijalishi leo sina chochote lakini Kesho nitakuwa na kitu..Bwana hawezi kutupungukia kabisa ikiwa tu tupo katika kusudi lake, anasema hivyo katika Neno lake (Waebrania 13:5), anajua tuna haja ya chakula, mavazi, malazi, makazi n.k lakini anachotutaka ni sisi kumtafuta kwanza yeye..Tusiwe na hofu ya Kesho..Kwasababu Hofu ni utumwa, hakuna mtu yeyote mwenye hofu, akapiga hatua yoyote mbele, hakuna.

Tatizo lililopo tunataka pindi tu tunapomkaribisha Yesu Maishani mwetu, basi atupe ratiba ya leo, Kesho na miaka mitano au kumi mbele itakuwaje! Tunataka tuone Kesho tutakuwa na shilingi ngapi mifukoni mwetu, uhakika wa kila kitu…Mungu si wakati wote anatenda kazi hivyo, wakati mwingine unaweza kukupitisha katika ukame leo, na huku hujui Kesho utakuwaje na ghafla ukashangaa kafungua mlango Kesho ukapata unayohitaji tena na zaidi ya matarajio yako…

Hivyo yeye anataka tu tumwamini kwamba hatatuacha kabisa! Anafahamu tunayohitaji!

Kama unafanya shughuli yoyote ambayo inakupatia kipato, na ikatokea ukapungukiwa kabisa, anatakiwa umwamini kuwa hajakuacha, na wala hana mpango wa kukuacha!..kumbuka wakati fulani nyuma ambapo ulipitia kupungukiwa na akakufungulia mlango kimiujiza…ukumbuke huo muujiza, na usikie sauti yake leo moyoni mwako ikikuambia…HUJAFAHAMU TU?..Haujafahamu bado?..Siku ile ulipopungukiwa na akakufungulia mlango kimiujiza?..Yatafakari matendo yake ya nyuma kisha Uinyanyue Imani yako kwake..na siku zote utaishi Maisha ya furaha na yasiyo na hofu, ukijua kuwa Baba yako wa Mbinguni, sio Baba wa kambo, ni Baba wa damu kabisa ambaye hapendi kuona utakufa njaa wala kuteseka.

Maombolezo 3:36 “Na kumnyima mtu haki yake, Hayo Bwana hayaridhii kabisa”.

Bwana akubariki.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP



Mada nyinginezo:

CHAKULA CHA ROHONI.

USITAFUTE FAIDA YAKO MWENYEWE BALI YA WENGINE.

YAKUMBUKE YA NYUMA.

SI SHETANI BALI NI WEWE. (CHAGUA MEMA)

MUNGU WANGU,MBONA UMENIACHA?.

LAANA YA YERIKO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNANG’OKA MENO.

Hii ni moja ya ndoto inayootwa na watu wengi, ikiwa na wewe ni mmojawapo na inajirudia rudia  mara kwa mara basi fahamu kuwa lipo jambo ambalo Mungu anataka kukukumbusha, Sikuzote meno yanafanya kazi mbili kuu, ya kwanza ni kumeng’enya na ya pili ni kung’ata,..asilimia kubwa ya viumbe vyote vinatumia meno kwa kazi mojawapo ya hizo, isipokuwa tu mwanadamu inaongezeka nyingine hapo, ambayo ni kuzungumza, mtu usipokuwa na meno huwezi kuzungumza, atatoa sauti tu zisizoeleweka…

Vilevile Mtu Ukipoteza meno huwezi kula vitu vigumu, wala huwezi kung’ata kitu chochote Na ndio maana mtu unapoota meno yake aidha  ya juu au ya chini au magego yanang’oka halafu ghafla ukashtuka saa hiyo hiyo  na kujiona yupo salama huwa anashukuru kweli, anasema afadhali imekuwa ndoto, ni kwasababu unajua thamani iliyo katika meno yake.

Sasa ukiota meno yanatoka Hapo ni Mungu anakukumbusha, kuwa unakaribia kupoteza Meno yako ya rohoni, yenye thamani kubwa zaidi ya haya ya mwilini, ikiwa hujaokoka basi nakushauri  utubu haraka sana, umegukie Mungu wako, kwasababu mara kikipotea hicho basi fahamu kuwa kitapotea milele…Ukishaondolewa  uwezo wako wa kupambanua na kuyaelewa  mambo ya rohoni basi hutakaa uwe nao tena, ukishaondolewa uwezo wako wa kung’ata maadui zako wa rohoni kwa meno makali Mungu aliyokupa basi fahamu utabakia hivyo milele, Vilevile Ukishaondolewa uwezo wa kuzungumza na Mungu wako rohoni basi ndio utabakia hivyo milele na milele hatakaa  akuelewe wewe, hiyo inamaanisha hata ukiomba dua yao hawezi kukusikia…Na hiyo yote ni kwasababu ya dhambi zako unazozitenda sasa hivi.

Zaburi 58:3 “Wasio haki wamejitenga tangu kuzaliwa kwao; Tangu tumboni wamepotea, wakisema uongo.

4 Sumu yao, mfano wake ni sumu ya nyoka; Mfano wao ni fira kiziwi azibaye sikio lake.

5 Asiyeisikiliza sauti ya waganga, Ijapo wanafanya uganga kwa ustadi.

6 Ee Mungu, UYAVUNJE MENO YAO VINYWANI MWAO; Ee Bwana, uyavunje magego ya wana-simba.

7 Na watoweke kama maji yapitayo kwa kasi; Akiielekeza mishale yake, iwe imetiwa ubutu”.

Ndugu Usiipuuzie Injili ya msalaba hata kidogo, inapohubiriwa mbele zako, Mungu ameona jambo hilo kwako na hivyo anakuonya kwasababu anakupenda, mgeukie muumba wako, anza kuzingatia Neno lake kile anachokuambia tii na yeye mwenyewe atakuokoa na kukulinda na kukuongoza hadi unyakuo.

Aidha kama wewe tayari upo ndani ya Kristo, na unaota ndoto za namna hiyo hapo Mungu anakuonyesha pia ni jinsi gani unaelekea kupoteza ule uwezo wako wa thamani uliokuwa nao wa kupambanua  mambo ya rohoni na ukali wako, hivyo simama imara kama ulikuwa umeshaanza kuyumba yumba,  au kupoa simama imara ili usije ukabakia kuwa mbwa bubu tu asiyeweza hata kubweka rohoni (kukemea dhambi )kwa kukosa meno.

Isaya 56:10 “Walinzi wake ni vipofu, wote pia hawana maarifa; wote ni mbwa walio bubu, hawawezi kulia; huota ndoto, hulala, hupenda usingizi.

11 Naam, mbwa hao wana choyo sana, hawashibi kamwe; na hao ni wachungaji wasioweza kufahamu neno; wote pia wamegeuka upande, wazifuate njia zao wenyewe, kila mmoja kwa faida yake, toka pande zote.

12 Husema, Njoni, nitaleta divai, Na tunywe sana kileo; Na kesho itakuwa kama leo, Sikukuu kupita kiasi”.

Zingatia hayo na Bwana hakika atakuwa na wewe katika kila hatua moja unayopiga kwake…Hizi ni siku za mwisho na Unyakuo wa kanisa upo karibuni, tengeneza mambo yako.

Ubarikiwe.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP



Mada Nyinginezo:

KUOTA UNAENDESHA GARI.

KUOTA UPO UCHI.

KUOTA UNAFANYA MTIHANI.

JE! KUBET NI DHAMBI?

JE! NI KWELI KUNA VIUMBE VINAVYOISHI SAYARI NYINGINE (ALIENS)?

UBATILI.


Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNAENDESHA GARI.

Awali ya yote ni vizuri kufahamu kuwa asilimia kubwa ya ndoto tunazoota kila siku au mara kwa mara huwa zinatokana na mawazo yetu wenyewe, naweza kusema hata asilimia 95 ya ndoto zote tuziotazo usiku hutokana na sisi wenyewe, na hizo zinakuja  aidha kwa shughuli tunazozifanya kila siku au mazingira yanayotuzunguka au kitu tunachokiwaza sana…

Hivyo ndoto kama hizi, huwa hazibebi ujumbe wowote wa rohoni, ikitokea umeota  wewe zipuuzie tu vinginevyo utajikuta unachanganyikiwa ukidhani kuwa kila ndoto unayoota ina maana, ikiwa bado hujaweza kuzitofautisha aina za ndoto katika makundi yake basi pitia kwanza somo hili ili upate msingi kisha tuendelee. >>>NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI?

Lakini kama ndoto unayoota haihusiani na mazingira uliyopo, na huwa inajirudia mara kwa mara, basi lipo jambo ambalo Mungu anataka kukuonyesha hapo.

Sasa Kuota unaendesha gari na wakati mwingine umewapakiza watu nyuma,  ni ishara kwamba wewe mwenyewe unayaongoza maisha yako au maisha ya wengine, kukufikisha mahali Fulani au kuwafikisha mahali fulani..Kama wewe umeokoka na unalifanya kusudi la Mungu au unaifanya kazi ya Mungu basi zidisha mwendo katika safari yako kwasababu lengo lako utalifikia, kama hutapunguza mwendo kama alivyofanya Yehu, pale alipokuwa anakwenda kumuua Yule mfalme muasi Yoramu na mama yake Yezebeli waliowakosesha Israeli mpaka kupelekea wakaingia kwenye uchawi na ibada za sanamu, na Kumkasirisha Mungu kwa viwango vya juu sana.

2Wafalme 9:20 Yule mlinzi akatoa habari, akasema, Amewafikilia wala harudi tena; na mwendo huu ni kama mwendo wa Yehu mwana wa Nimshi; MAANA ANALIENDESHA GARI KWA KASI.

Hivyo kama unalo kusudi la Mungu mkononi mwako,litimize bila kuogopa kipingamizi au mitazamo ya watu..

Lakini pia,

unapaswa uwe makini ni gari la aina gani unatumia kuliendesha kusudi la Mungu wakati Fulani mfalme Daudi alikuwa analitoa sanduku la Mungu kutoka kwa Abinadabu kwenda Yerusalemu, lakini alifanya makosa kuwatumia ng’ombe kama usafiri wa kulisafirisha kusudi la Mungu badala ya kutumia watu tena makuhani ambao ndio Mungu aliowaagiza walibebe wakati wote,  wao wakawaweka ng’ombe kama magudurumu ya gari lao na ikapelekea kifo cha mtu mmoja..soma 1Nyakati 13:7

1Nyakati 13:7 “Hivyo Wakalipandisha sanduku la Mungu juu ya gari jipya kutoka nyumba ya Abinadabu; na Uza na Ahio WAKALIENDESHA LILE GARI.

8 Wakacheza Daudi na Israeli wote, mbele za Mungu, kwa nguvu zao zote; na kwa nyimbo na kwa vinubi, na kwa vinanda, na kwa matari, na kwa matoazi, na kwa tarumbeta.

9 Hata walipofika penye uga wa Nakoni, Uza akaunyosha mkono wake alishike sanduku; kwa maana wale ng’ombe walikunguwaa.

10 Ndipo hasira ya Bwana ikawaka juu ya Uza, naye akampiga, kwa sababu alilinyoshea sanduku mkono wake, hata akafa pale pale mbele za Mungu.

Hivyo uwe makini unapolifanya kusudi la Mungu na wale unaowaongoza, zingatia vigezo cha maandiko . Na ndio maana wengine wanaota wanaendesha vyombo tofauti tofauti , wengine wanaota wanaendesha malori, wengine wanaota wanaendesha baiskeli, wengine wanaota wanaendesha pikipiki n.k. Vyovyote vile, kuendesha ni kuendesha tu, hiyo ni kulingana na kusudi Mungu alilokupa cha msingi hapo ni kutimiza kusudi hilo kwa ukamilifu wote, ili uepuke kulaumiwa huko mbeleni.

Lakini kama unajijua wewe bado ni mwovu na hadi sasa upo katika dhambi, Hiyo ni Ishara mbaya sana kwako, Aidha Unajiongoza mwenyewe katika mauti au unawaongoza wengine katika mauti, au vyote viwili kwa pamoja..

2Nyakati 21:12 “Likamjia andiko kutoka kwa Eliya nabii, kusema, Bwana, Mungu wa Daudi baba yako, asema hivi, Kwa sababu hukuziendea njia za Yehoshafati baba yako, wala njia za Asa mfalme wa Yuda;

13 lakini umeiendea njia ya wafalme wa Israeli, UKAWAENDESHA KATIKA UASHERATI Yuda na wenyeji wa Yerusalemu, kama walivyofanya nyumba ya Ahabu; tena umewaua ndugu zako wa nyumba ya baba yako, waliokuwa wema kuliko wewe;

14 tazama, Bwana atawapiga pigo kubwa watu wako, na watoto wako, na wake zako, na mali yako yote;

15 nawe utakuwa na ugonjwa mkuu kwa maradhi ya matumbo, yatakapotokea matumbo yako kwa sababu ya ugonjwa huo siku kwa siku.

Unaona hapo huyu mfalme Yehoramu, alikuwa mtu mwovu, alikuwa ni muuaji, na mwabudu sanamu, akawafanya na Israeli wote wote wawe kama yeye, au kwa lugha nyingine akawaendesha waisraeli mpaka kwenye uasherati wa kiroho, kwa sababu hiyo basi Mungu akampiga kwa mapigo yale..

Hata na wewe, unayaongoza maisha yako sasa ukidhani kuwa upo salama, lakini mwisho wake utakuwa ni mauti kama hutatubu, unawasababishia wengine mauti wale walio chini yako, au wanaokutegemea, au wanaokutazama kwa mwenendo wako na maisha yako..

Hivyo Bwana anakupenda na ndio maana anakuonya Leo hii, Utubu umgeukie yeye, ili uliendeshe gari la maisha yako katika njia sahihi ya kutimiza makusudi ya Mungu na sio makusudio ya Shetani.

Ubarikiwe.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

KUOTA UNAFANYA MTIHANI.

KUOTA UPO UCHI.

KUOTA UNAPAA.

KUOTA UNASAFIRI.

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?

JE! KUBET NI DHAMBI?

AGANO LAKO LINABEBWA NA NANI?.


Rudi Nyumbani:

Print this post

SIKU ZA MWISHO ZA UHAI WANGU.

Kila mwanadamu atafikia ukomo wa siku zake, (yaani siku ya Mauti yake)..Lakini kabla ya siku yenyewe ya kuondoka ulimwenguni haijafika…Kinakuwepo kipindi fulani kifupi ambacho kinaweza kuwa ni miaka 10, au 5 kabla ya kuondoka kwako, au kinaweza kuwa mwaka mmoja au mwezi mmoja au wiki moja….Kipindi hicho kifupi ndicho kinachojilikana kama SIKU ZA MWISHO ZA UHAI WA MTU. 

Katika kipindi hicho, Kuna hali fulani mtu anakuwa anaanza kuipitia, mara nyingi inakuwa ni kumbukumbu ya mambo yaliyopita nyuma, ndio utakuta mtu anaanza kukumbuka mambo yake yote ya nyuma aliyoyapitia na jinsi alivyoyaishi, kipindi hichi sio kipindi kizuri kwa Mtu ambaye hakuwa ndani ya Kristo, kwasababu ni kipindi cha mashaka mazito, mara nyingi kwa mtu ambaye hajampa Kristo maisha yake huko nyuma, ni ngumu sana kushinda hali atakayopitia wakati wa hiki kipindi. Wengi wanaishia kujiua.

Ndio maana Biblia ikasema katika Mhubiri.

Mhubiri 12:1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo”

Umeona hapo? biblia haisemi mkumbuke muumba wako wakati wa siku zilizo mbaya..Hapana! bali inasema mkumbuke muumba wako siku za ujana wako, kabla hazijakaribia siku zilizo mbaya…Siku zilizo mbaya zinazozungumziwa hapo ndio hizi SIKU ZA MWISHO ZA UHAI WAKO.

Siku hizo ni ngumu kumrudia Muumba wako, kama katika siku za ujana wako ulikuwa unaichezea Neema, na kumbuka pia siku za ujana sio tu siku za miaka ya ujana kama vile miaka 15-45 hapana..bali siku za ujana ni siku ambazo ulikuwa unauwezo wa kumgeukia Mungu, na mazingira yote yalikuwa yanakuhimiza kufanya hivyo lakini  hukutaka!

Hivyo huu sio wakati wa kuzunguka huko na huko mitandaoni na mitaani kutafuta mambo ya ulimwengu huu yanayopita, huu ni wakati wa kutafuta wokovu kwa nguvu zote. Biblia inasema Ufalme wa Mbinguni unapatikana kwa nguvu na wenye nguvu ndio wauteka..Je! wewe nguvu zako unazipeleka wapi sasa katika ujana wako? katika ulimwengu au kwa Yesu?..Kama ni katika ulimwengu basi tambua kuwa SIKU ZA KUFA KWAKO ZINAKARIBIA na katika siku hizo, hazitakuwa siku za furaha bali huzuni.

Daudi aliziona siku zake na alikuwa na furaha..akafurahi akamwusia mwanawe kuzifuata njia za Bwana.

1Wafalme 2:1 “Basi siku ya kufa kwake Daudi ikakaribia, akamwusia Sulemani mwanawe, akasema,

2 Mimi naenda njia ya ulimwengu wote; basi uwe hodari, ujionyeshe kuwa mwanamume;

3 uyashike mausia ya Bwana, Mungu wako, uende katika njia zake, uzishike sheria zake, na amri zake, na hukumu zake, na shuhuda zake, sawasawa na ilivyoandikwa katika torati ya Musa, upate kufanikiwa katika kila ufanyalo, na kila utazamako;”

Yakobo naye aliziona siku za kufariki kwake akafurahi, akawabariki wanawe…

Na siku hizo zinakuja kwako mimi na wewe! Umejiandaaje?..je zitakuja na huzuni au furaha kwako?

Tubu mgeukie Kristo sasa, angali mlango wa Neema bado upo..Angali u kijana.Na Kristo atakupa tumaini la maisha ya sasa, na yale yajayo!

Bwana akubariki.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

HUDUMA YA MALAIKA WATAKATIFU.

SIKU ZA MAPATILIZO.

WEWE NI HEKALU LA MUNGU.

JE! BAADA YA ULIMWENGU HUU KUISHA MALAIKA WATAKUWA NA KAZI GANI TENA?

JE! KUNA UBAYA WOWOTE KUWAOMBEA NDUGU ZETU WALIOKUFA KATIKA DHAMBI, MUNGU AWAKUMBUKE KATIKA UFALME WA MBINGUNI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Mtu wa Kwanza kufika mwezini

Hakukuwa na mtu mmoja maalumu aliyefika mwezini, kulingana na Sayansi…Waliofika mwezini ilikuwa ni TEAM ya watu watatu (Neil A. Armstrong, Michael Collins na  Edwin E. Aldrin Jr.) Hao ndio waliokuwa ndani ya chombo cha Kwanza kulichotua mwezini, na wote watatu walikuwa ni wa-Marekani na safari yao iliyojulikana kama Apollo 11. Safari yao ilichukua siku 8 na masaa 3..Kwenda na kurudi, Na hiyo ilikuwa ni Mwaka 1969.

Sasa kumbuka tukio lolote linaloendelea duniani, linafunua tukio fulani linaloendelea katika roho.

Kama wanadamu wamefikia hatua ya kutengeneza chombo ambacho kimewafanya wafike juu zaidi ya mawingu, na kutua Mwezini. Kadhalika kuna kitu pia kinaendelea kutengenezeka  sasa katika roho, ambapo itafikia kipindi kitakamilika, na hicho kitalifanya kanisa kupaa juu sana zaidi ya mawingu na zaidi ya mwezi na kulifanya lifike mahali panapoitwa Mbinguni.

Na kama tunavyoona hiyo safari ya kwenda mwezini ilihusisha watu wachache sana, kadhalika, safari ya kwenda mbinguni itahusisha watu wachache sana, kwasababu biblia inasema mlango ni mwembamba na njia imesonga ielekeayo uzimani..

Hivyo ndugu, huu ni wakati wa kuingia ndani ya Kristo, kwani injili sasa inahubiriwa na teknolojia tunazoziona, Hizi ni zile siku za mwisho ambazo biblia imesema maarifa yataongezeka…Na tunaona jinsi yanavyoongezeka kwa Kasi, na katika roho pia yanaongezeka, watu wa Mungu hivi karibuni watafikia Imani ya kunyakuliwa na hivyo kuondoka kwenda mbinguni kwa Bwana..Je! na wewe utakuwa miongoni mwao?

Jibu unalo, tubu mpe Kristo maisha yako na uishi maisha yanayopatana na Toba yako.

Bwana akuabariki.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA

NYOTA ZIPOTEAZO.

KUONGEZEKA KWA MAARIFA.

ROHO SABA ZA MUNGU NI ZIPI? NA JE ZINATOFAUTIANA NA ROHO MTAKATIFU?


Rudi Nyumbani:

Print this post

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

Upendo ni kitendo cha kuonyesha hisia za tofauti za ndani kwa mtu mwingine, Ni hisia zinazoonyesha pengine umeridhishwa na mtu huyo, au umemkubali, au umemuhurumia, au unataka kumkaribia uwe karibu naye n.k.

Kibiblia kuna upendo wa aina tatu:

UPENDO WA KWANZA NI UPENDO UNAOTOKANA NA HISIA:

Upendo huu unajulikana kama “EROS” Ni upendo unaozaliwa na hisia, Upendo huu ni maarufu sana kwa mke na mume, katika biblia Sulemani alijaribu kuuleza upendo ya namna hii:

Wimbo 1:13 “Mpendwa wangu ni kama mfuko wa manemane Ukilazwa usiku maziwani mwangu.

14 Mpendwa wangu ni kama kishada cha hina, Katika mizabibu huko Engedi.

15 Tazama, u mzuri, mpenzi wangu, U mzuri, macho yako ni kama ya hua.

16 Tazama, u mzuri, mpendwa wangu, Wapendeza, na kitanda chetu ni majani;

17 Nguzo za nyumba yetu ni mierezi, Na viguzo vyetu ni miberoshi”.

Huu ni Upendo ambao hauwezi kufananishwa na upendo kama wa mtu na ndugu yake au Rafiki yake.

AINA YA PILI YA UPENDO NI UPENDO UNAOZALIWA KWA VITU VINAVYOENDANA:

Unajulikana kama “PHILEO”. Upendo huu unazuka kutokana na mahusiano Fulani mtu mmoja alionao na mwenzake, anaweza akawa ni ndugu, au rafiki, au mchezaji mwenzake, au mfanyakazi mwenzake. Ni upendo ambao kusipokuwa na mahusiano Fulani ya karibu au faida Fulani ambayo mtu anaweza kuipata kwa mwenzake, hauwezi kuzaliwa.

Tunapaswa tupendane sisi kwa sisi, biblia inatuambia hivyo katika (1Yohana 2:9-10), vilevile inatuambia tupendane sisi tulio ndugu katika Bwana, lakini upendo wa namna hii haupo tu kwa waaminio bali hata kwa watu waovu pia wanao..Bwana Yesu alisema:

Mathayo 5:46 “Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?

47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo”?

Unaona kwahiyo upendo huu bado hujafikia vile viwango vyenyewe.

AINA YA TATU YA UPENDO NI UPENDO USIO NA MASHARTI. UNAOJULIKANA KAMA “AGAPE” (UPENDO WA KI-MUNGU).

Huu ndio upendo Yesu Kristo aliokuwa anauzungumzia, ni upendo unaompenda mtu bila ya sababu yoyote, Ni upendo wa kiwango cha juu sana, unampenda mtu kwa kutokujali kama na yeye anakupenda au hakupendi, kama anakuchukia au hakuchukii, kama anakusema vibaya au hakusemi vibaya, kama anafaida yoyote kwako au hana faida yoyote kwako.

Upendo huu ndio YESU alikuwa nao kwetu, biblia pale inaposema “alitupenda Upeo”(Yohana 13:1),  ilimaanisha kusema hivyo Alitupenda upeo kweli kweli, sio kwasababu tulikuwa ni watakatifu, au kwasababu tulikuwa waovu…au kwasababu alikuwa anatafuta ukubwa kwetu hapana, alitupenda tu, tena ile wa kutoka moyoni hadi kufikia hatua ya kuutoa uhai wake kwa ajili yetu.

Kama ilivyoelezwa katika makala haya, https://www.swisswatch.is/product-category/tag-heuer/grand-carrera/ unaweza kuvinjari chaguo lako la ofa zinazopatikana kwenye simu mahiri na chapa maarufu na uchunguze mipango ya huduma inayokidhi mahitaji yako.

Na upendo wa aina hii ndio Bwana anataka kila mmoja wetu awe nao, Ni ngumu kuufikia, hususani pale tunapoona mtu Fulani anayetuchukia au anatuzungumzia vibaya halafu huyo huyo ndio tunapaswa tumpende, kuna kama ugumu fulani..Lakini Huo ndio Mungu anataka kuuona kwetu haijalishi tutawapenda wake zetu na waume zetu kiasi gani, au ndugu zetu wengi kiasi gani au rafiki zetu wengi kiasi gani kama hatujaweza bado kuufikia huu upendo wa AGAPE, mbele za Mungu bado hatuna upendo..

Hizi ndizo tabia za upendo wa AGAPE.

1Wakorintho 13:4 “Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;

5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;

6 haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;

7 huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.

8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika”.

Hivyo ili mimi na wewe tuweze kuufikia Upendo wa namna hii hatupaswi kuungojea kama hizo aina mbili juu, bali tunapaswa tuupapalilie kwa kuvumilia, kwa kutokurudisha baya kwa baya, kwa kutokusengenya, kwa kutokuhesabu mabaya ya mtu tu sikuzote, kuwaelewa watu ..n.k.

Tuombe Mungu atusaidie sote tufike hapo, kwasababu hapo ndipo Mungu mwenyewe alipo, na hiyo ndio inayojulikana kama karama iliyo kuu kuliko zote. Ukiwa nayo hiyo wewe ni zaidi ya nabii yoyote, au mwalimu yoyote, au mwinjilisti yoyote, au mtume yoyote duniani. Mungu anakuwa karibu sana na wewe.

Ubarikiwe sana.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

JIRANI YAKO NI NANI?

SAMEHE KUTOKA NDANI YA MOYO WAKO.

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

JE! UNAYO NAFASI MBINGUNI?

HERI, WALE MUNGU ASIOWAHESABIA MAKOSA YAO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

JE UMEOKOKA?

Shalom, mtu wa Mungu karibu tujifunze Biblia pamoja..

Wapo wanaodhani kuwa hakuna kuokoka duniani! lakini nataka nikuambie wokovu ni hapa hapa duniani..Mbinguni ni matokeo ya wokovu wetu.

Biblia inasema kama ilivyokuwa katika siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku za kuja kwake mwana wa Adamu, Na kama ilivyokuwa katika siku za Lutu ndivyo itakavyokuwa katika siku za kuja kwake mwana wa Adamu..Hivyo tukijifunza ni vitu gani vilikuwa vinaendelea muda mchache kabla ya Matukio hayo mawili ya kuangamizwa dunia, tunaweza kuelewa ni mambo gani yatatokea katika siku za kuja kwa Kristo mara ya pili.

Tukio la kipekee tunaloweza kuliona kabla ya Moto kushuka sodoma na gomora ni namna watu walivyookoka…Yapo matukio mengi lakini leo tutalizungumzia hili moja.

Biblia inasema.

Mwanzo 19: 12 “Basi wale watu wakamwambia Lutu, Je! Unaye mtu hapa zaidi? Mkwe, wanao, na binti zako, na wo wote ulio nao katika mji, uwatoe katika mahali hapa;

13 maana tutapaharibu sisi mahali hapa, kwa kuwa kilio chake kimezidi mbele za Bwana; naye Bwana ametupeleka tupaharibu.

14 Lutu akatoka akasema na wakweze, waliowaposa binti zake, akasema, Ondokeni mtoke katika mahali hapa kwa sababu Bwana atauharibu mji huu. LAKINI AKAWA KAMA ACHEZAYE MACHONI PA WAKWEZE.

15 Hata alfajiri ndipo malaika wakamhimiza Lutu, wakisema, Ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili waliopo hapa, usipotee katika maovu ya mji huu”.

Tunasoma hapo, kabla ya gharika, kuna injili ya haraka haraka ilipita…Lutu aliambiwa akawaambie ndugu zake watoke mjini kwasababu mji unakwenda kuangamizwa, na laiti kama hao ndugu zake wangesikia, kila mmoja angeogopa na kwenda mbio kuwaambia ndugu zao wengine wa mahali pengine…na hao ndugu wengine wangewaambia wengine…Hivyo kwa kipindi kifupi watu wengi sana wangeokoka…laiti watu wangekuwa na masikio ya kusikia maonyo na kuwa hofu ya Mungu, hata baada ya hukumu ile kutamkwa bado kungekuwepo na nafasi ya KUOKOKA!..Lakini hata huo mlango mdogo wa Neema watu waliupuuzia na hivyo kusababisha kuangamizwa wote.

Na kama pia ukichunguza wakati wa Gharika, Nuhu hakuokoka peke yake, bali aliambiwa akawakusanye watu wa jamaa yake yote…Ni wazi kuwa naye pia alikwenda kuwaambia mambo yale yale…lakini inawezekana naye pia alionekana kama anacheza! Ndio maana akaishia kuingia safinani yeye na wanawe tu, kama Lutu alivyookoka yeye na wanawe!

Mwanzo 7:1 “Bwana akamwambia Nuhu, Ingia wewe na jamaa yako yote katika safina; kwa maana nimekuona wewe u mwenye haki mbele zangu katika kizazi hiki”.

Mwanzo 7: 5 “Nuhu akafanya kama vile Bwana alivyomwamuru.

6 Naye Nuhu alikuwa mtu wa miaka mia sita hapo hiyo gharika ya maji ilipokuwa juu ya nchi.

7 Nuhu akaingia katika safina, yeye, na wanawe, na mkewe, na wake za wanawe pamoja naye; kwa sababu ya maji ya gharika”

Ndugu nafasi hii ndogo Mungu anayoitoa baada ya hukumu kutamkwa sio ya kwenda kutenda mema, hapana! ni nafasi ya kuokoka!! Hukumu imeshatamkwa..haiwezi kugeuzwa ni lazima ije tu kama ilivyotamkwa! Ni nafasi ya kuukimbia ulimwengu na kuingia safinani, hivyo hivyo kama ulivyo….Ni wakati wa kuikimbia sodoma na gomora ukiwa hivyo hivyo ulivyo…Usiende kumuaga mtu! Wala usiende kumwuliza baba yako au mama yako je! Natakiwa kuokoka? Ondoka sodoma kama ulivyo! Wewe kama wewe…wokovu unaanzia hapo hapo sodoma ulipo! kwasababu hukumu imeshatamkwa…Watoto wa Nuhu haikuhitaji utakatifu mwingi kupata nafasi ya kuingia safinani?..hawakuwa wakamilifu na ndio maana unaona baada ya kutoka safinani, Hamu aliuona uchi wa Baba yake…Lakini walitii injili ndio maana wakaokoka! tu Injili ya Nuhu ya mwisho ya kuokoka! Basi! Kulikuwa hakuna muda tena wa Mungu kusikiliza maombi ya watu…kulikuwa na mambo mawili tu! Aidha kuingia safinani uokoke au kubaki duniani uangamie.

Ukishaingia safinani tayari umeokoka! Hata kama mafuriko hayajaja!

Na siku za mwisho karibia na kuja kwa Yesu ndio injili ndio hiyo inahubiriwa na Roho Mtakatifu, hatuwezi kukaa na kumwomba Mungu kwamba asiiangamize dunia! Alishasema siku ya maangamizi itakuja ni kweli itakuja! Hakuna atakayeweza kubadilisha hilo… Na hivyo zipo chaguzi mbili tu mbele yetu! Kubaki ulimwenguni kuangamia au kuingia safinani kupona! Safina ni Bwana Yesu.

Kama unataka kuokoka na maangamizi..unamfuata Bwana Yesu ukiwa mwenye dhambi kama ulivyo wokovu ni hapa hapa duniani…haihitaji utakatifu kumwamini Yesu…Kwasababu kilichopo mbele ni kifo..Ukimwamini Yesu na kutubu moja kwa moja unapata nafasi ya kuingia safinani..na utakuwa umeokoka na maangamizi, kwasababu huwezi kuokoka mahali ambapo hakuna maangamizi!..Kisha baada ya hapo wewe mwenyewe atakuongoza katika utakatifu na ukamilifu wote,..wewe unachopaswa kufanya ni kuanzia huo wakati kutokuangalia nyuma tu,

Je! Upo safinani?…Umeitii Injili ya Roho Mtakatifu inayotuonya tujiepushe na ulimwengu?

Bwana akubariki

Mada Nyinginezo:

UKIAMINI NA UKIMKIRI YESU KWA KINYWA CHAKO, UTAOKOKA.

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

MATUNDA YAPATANAYO NA TOBA!

NYOTA ZIPOTEAZO.

SAA YA KIAMA.

FREEMASONS NI NINI? NA MTU ATATOKAJE HUKO?


Rudi Nyumbani:

Print this post

JE UNATAMANI KUMJUA MUNGU, NA HUJUI PA KUANZIA?

Ukiwasimamisha watu wawili mbele yako, mmoja daktari na mwingine mtu wa kawaida ambaye hajasoma, halafu ukawaonyesha wote wawili ndege ya kivita inayopaa hewani, kisha ukawauliza swali moja jepesi “ Je! Ile mnayoiona juu ni kazi ya nani”….moja kwa moja Yule mtu ambaye hajasoma atakuambia bila shaka ile ni kazi ya mtu,.. lakini Yule daktari si rahisi kwake kutoa jibu la kiwepesi wepesi hivyo, kulingana na kiwango chake cha elimu kumuhusu mwanadamu, atakuambia “mimi ninaona kazi ya ubongo wa mwanadamu”

Sasa ikiwa wewe ndio umeweka utoe alama hapo, ni nani kapata na nani kakosa, utatoa jibu gani?..Ni wazi kuwa Utagundua kuwa wote wawili wapo sahihi, isipokuwa tu Yule daktari kwa kuwa ameshamsoma sana mwanadamu katika fani yake ya utabibu aliyoipitia na kujua kuwa kilichondani ya mwanadamu ndicho kilichofanya kazi ile, hakuishia tu juu juu kumtaja mtu, bali aliingia ndani zaidi mahali huo uutu wake unaomfanya kuwa mtu unapotokea na hapo si pengine zaidi ya kwenye ubongo..hapo ndipo panapomtofauti kuwa huyu ni nyani na huyu ni mtu.

Vivyo hivyo, kwa mtu wa kawaida tu akiulizwa hii unayoiona duniani ni kazi ya nani, asilimia 99 watakuambia tunaona kazi ya Mungu, lakini ni wachache sana watakuambia tunaona kazi ya Neno la Mungu, ambapo huo ndio ubongo wa Mungu wenyewe. Kwa hilo ulimwengu mzima uliumbwa kwalo.

Webrania 11:3 “Kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo Dhahiri”.

Lakini watu wengi wanachanganyikiwa wakidhani kuwa Neno la Mungu ni tofauti na Mungu..Kwamba ile ni nafsi nyingine ya tatu ya Mungu..Embu turudi pale kwenye ule mstari wa

Yohana 1:1 inaposema:

“1 Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.

2 Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.

3 Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika”.

Sasa embu tumfananishe Yohana na Yule daktari mwenye elimu, ni wazi kuwa angesema maneno yake hivi “tangu zamani ubongo ulikuwepo, na huo ubongo ulikuwepo ndani ya mtu, na huo ubongo ndio mtu mwenyewe, vyote vimefanyika kwa huo, wala pasipo huo hakuna ndege yoyote ya kivita ingeweza kuumbwa au kitu chochote kile”..

Umeona hapo, Ndivyo ilivyo kwa hata katika habari za Neno la Mungu ndio Ubongo wa Mungu, huwezi kulitenga Neno lake na yeye, kwasababu yeye ndio Neno lenyewe..

Tunajua kabisa taarifa zote zimuhusuzo mwanadamu, na ufahamu wake wote upo kwenye ubongo kibaolojia, kwamba ukitaka kujua siri zake basi cheza na ubongo wake, ukitaka kujua uwezo wake wa kufikiri au kufanya mambo, au kuamua, basi cheza na ubongo wake, lakini kama ukijifanya unaweza kumfahamu Mtu kwa kumwangalia tu sura yake au urefu wake, au uzuri wake, au kazi zake, utapotea na usiambulie chochote ..

Vivyo hivyo na leo hii, ili umwelewe Mungu, huna budi kuusoma ubongo wake, na ubongo wake ni Neno lake, hutakaa umjue Mungu kwa vitu alivyoviumba, hutakaa umjue Mungu kwa maajabu anayoyafanya, utamjua Mungu kwa Neno lake tu..basi..

Kama ni hivyo basi? Je hili Neno lake likoje likoje na tutalipata wapi?.

Mungu alijua shida itakuja hapo kwa wanadamu, hivyo akatugawia ofa kubwa sana, ambayo hakuna mtu angeweza kufiki kama Mungu angekaa afanye kitu kama hicho, na ofa hiyo si nyingine zaidi ya kuliundia Neno lake mwili kama ule ule wa binadamu, na kulifanya liishi na wanadamu, liongee, lizungumze nao, liulizwe maswali, litufundishe sisi namna ya kumjua Mungu, na kumfikia yeye..na huo mwili ndio ule ulioitwa YESU KRISTO, mwana wa Mungu aliye hai, Haleluya!! (1Timotheo 3:16)

1Yohana 1:1 “Lile lililokuwako tangu mwanzo, tulilolisikia, tuliloliona kwa macho yetu, tulilolitazama, na mikono yetu ikalipapasa, kwa habari ya Neno la uzima;

2 (na uzima huo ulidhihirika, nasi tumeona, tena twashuhudia, na kuwahubiri ninyi ule uzima wa milele, uliokuwa kwa Baba, ukadhihirika kwetu);”

Sasa unaweza kuona kazi imerahisishwa, tunaweza kujua siri zote na ufahamu wote wa Mungu kama tutaweza kumfahamu vizuri YESU KRISTO na kuyafuata maagizo yake yote aliyotuagiza. Yeye ndio huo Ubongo wa Mungu unaozungumza na sisi kila siku..Tukiyashika maneno yake basi hakuna kitu chochote kitakachoshindikana kwetu.

Hivyo, ikiwa unahitaji kumjua Mungu au kumkaribia na kuzungumza naye, au kuzijua siri zake zote, hatua ya awali kabisa ya kuanzana nayo ni kumwamini YESU KRISTO, na kumpa maisha yako ayaongoze..Na hiyo inakuja kwa kutubu kwanza dhambi zako zote mbele zake kwa kumaanisha kabisa kuziacha, na kutokuzifanya tena, kisha ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi kwa jina la Yesu Kristo kulingana na Matendo 2:38 kama hukuwahi kubatizwa, nawe utakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu. Na kuanzia huo wakati na kuendelea ataanza kukupa uelewa wa kumjua Mungu, kwa namna ambayo hukuwahi kuijua.

Lakini ukitafuta kumjua Mungu kwa nje nyingine mbali na YESU KRISTO,..Hesabu kuwa umepotea. Kwasababu maandiko yanasema katika

Yohana 14:6 “ Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi”

Ubarikiwe sana. Tafadhali “Share” ujumbe huu Na kwa wengine.

Na Bwana atakubariki.

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.

NENO LA MUNGU KATIKA UTIMILIFU WOTE.

MZEITUNI HALISI UTAKAPOPACHIKWA.

SADAKA ILIYOKUBALIKA.

NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

FREEMASONS NI NINI? NA MTU ATATOKAJE HUKO?

Freemason ni nini? nini historia ya freemason?, nani mwanzilishi wa freemason na Je! Freemasons ni wa kuogopwa? Masharti ya freemason ni yapi?

Shalom! Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tuongeze maarifa ya Neno la Mungu.

Leo tutajifunza juu ya kikundi kinachoitwa “Freemasons” na jinsi gani ya kutoka au kuwasaidia ambao tayari wameshaingia humo.

HISTORIA YA FREEMASONS

Kwa kuanzia tujifunze kidogo historia ya kikundi hicho: Freemasons tafsiri yake kwa lugha ya kiswahili ni “wajenzi huru” ingawa hawatambuliki kwa jina hilo, lakini kwa asili ni kikundi cha wajenzi. Kikundi hichi kilianzishwa miaka mingi kinadai tangu wakati wa ujenzi wa hekalu la Mfalme Sulemani, japo umaarufu wake umekuja kuwa mwingi katika karne za hivi karibuni.

NANI MWANZILISHI WA FREEMASONS

Kikundi hichi kinaamini “kulikuwa kuna siri zimefichika ambazo ndizo zilitumika katika ujenzi wa hekalu la Mfalme Sulemani”...Na kama vile wakristo wanavyoamini kuwa Yesu Kristo ndiye Masihi na kiini cha siri zote za Mungu. Vivyo hivyo Na Freemasons wenyewe wanamwamini mtu mmoja anayeitwa HURAMU, Kama Masihi wao, huyu anapatikana katika kitabu cha 1Wafalme 7, ambaye ndiye aliyekuwa mtu wa mji wa Tiro ambao kwa sasa ni maeneo ya nchi ya Lebanoni. Huyu ndio kama Masihi wao, Na Mwanzilishi wa freemasons kulingana na wao.

JE FREEMASONS NI KIKUNDI CHA SIRI?

Sasa kikundi hichi ni cha Siri, tukisema ni cha siri haimaanishi watu wake hawaonekani, au majengo yao hayajulikani..Hapana! Vikundi vya Freemasons vyote vimesajiliwa na serikali zote duniani, na vinalipa kodi, kwahiyo ni watu waliowazi..Kitu pekee ambacho ni siri ni “IBADA ZAO”. Na sheria za dunia zinawalinda kufanya ibada zao kwa siri. Kama vile sheria zinavyolilinda shirika la COCACOLA kuficha formula ya utengenezaji wa vinywaji vyao.Ni watu wachache sana wanafahamu, Na hiyo yote ni kuzuia unakiliji wa bidhaa zao.(www.wingulamashahidi.org)

FREEMASON INA WANACHAMA WANGAPI?

Freemasons ina wanachama zaidi ya milioni 6 duniani kote, miongoni mwao wakiwa, maraisi, wanasiasa, wana uchumi, wanasayansi, madaktari, waalimu, viongozi wa dini, wakulima, n.k…Idadi kubwa ya wanachama hao ipo nchini Uingereza na Wales.

MASHARTI YA FREEMASON

Mshirika kabla ya kujiunga ni lazima awe ana imani ya kuwa kuna “nguvu ya Kiungu”….Hiyo ikifunua kwamba tayari hicho ni “kikundi cha rohoni” kama huamini huwezi kuwa mshirika …Wanaojiunga huko ni watu kutoka dini zote duniani, waislamu, wahindu, wakristo-jina, wabudha n.k..Baada ya mshirika mpya kujiunga anatakiwa kukusanyika na wenzake mara kwa mara katika majengo yao maalumu ya ibada yanayoitwa “Grand Lodges”..Na wanawake hawaruhusiwi kujiunga katika kikundi hicho.

ISHARA/ ALAMA ZA FREEMASONS

Ndani ya Ibada hizo kwenye majengo yao wanatumia ishara ya vitu vingi, katika vidole, mikono, miguu, na pia wana ishara za picha na vito kama pete, mikufu, stika, ribbons, na ishara za vifaa vya ujenzi kama bikari, rula, pembe tatu.n.k na Kila ishara ina maana yake. Kama vile sisi wakristo tunavyokuwa na ishara ya misalaba kanisani mwetu, Inafunua kitu kilichotendeka Kalvari.

Sasa Ibada hizo zinabadilika kulingana na vyeo, wenye vyeo vya chini hawafanyi ibada zinazofanana na wenye vyeo vya juu, na pia wenye vyeo vya chini hawafahamu siri nyingi kama wanazofahamu wenye vyeo vya juu. Hapa ndipo watu wengi wasipojua!…tutakuja kupaelewa vizuri mbele kidogo mwa somo hili…

NGAZI ZA FREEMASONRY

Sasa vyeo hivyo vimegawanyika katika ngazi kuu 33 wanazoziita “shahada” au “degrees”

Mshirika mpya anayejiunga, kuna viapo anaambiwa aape, moja ya viapo hivyo ni kukiri kuwa mwaminifu, na kutokufichua siri yoyote ya chama hicho, na pia ataambiwa akiri kwamba endapo atafichua basi atakufa, na pia anaambiwa aape kwamba atakuwa mwaminifu, na pia atakuwa tayari kushirikiana na wenzake, na kusaidiana na wenzake kwa hali na mali…(www.wingulamashahidi.org)

Na katika hatua za awali, ataambiwa tu hicho ni kikundi cha kijamii!, kinachoamini katika ujenzi, na cha kusaidiana, na wala hataambiwa siri nyingi za kikundi hicho,..Na wala hawatamkataza kurudi kusali katika kanisa lake kama ni mkristo. Ila kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda na anayozidi kupanda vyeo, ndipo ataanza kugundua kuwa sio sehemu ambayo aliambiwa pindi alipokuwa anajiunga.

SHUHUDA ZA WALIOJIUNGA NA KUTOKA FREEMASON

Wengi waliojiunga na kutoka wanasimulia…”kuwa pindi walipojiunga, hawakujua chochote na pia walikuwa wanauhuru wa kuendelea kurudi kwenye makanisa yao kuabudu” na tena walikuwa wanapingana vikali na wale waliokuwa wanakishutumu chama hicho kuwa ni chama cha kishetani” na kinachoamini mauaji.

Wengine wanasema “Nilikuwa mshirika wa chama hicho kwa miaka mingi lakini sikuwahi kujua kuwa ni chama kinachomuabudu shetani” kwasababu wote tuliokuwa ndani ya chama hicho wenye degree ndogo, tulikuwa na upendo, na tulikuwa tunasaidiana, na kupeana fursa..Mpaka nilipofika ngazi za juu ndipo nilipoelewa kuwa sio sehemu salama”..mmoja aliyekuwa na degree ya 2 aliyetolewa huko na Bwana Yesu alihojiwa… je! ulishawahi kumuona shetani ndani ya ibada zenu?…akasema la! hata siku moja, wala sijawahi kuona vitu vya kiroho kama mapepo ndani ya logde! nilikuwa naingia na kutoka tu kama ninavyoingia kanisani…Na wala nilikuwa siamini kwamba ni kikundi kibaya kwa miaka kadhaa…na wala sikuwahi kutoa kafara yeyote ya mtu! mpaka baadaye sana nilipokuja kugundua kuwa hayo yanafanyika na wenye shahada za juu na hawatuambii sisi.

Kuanzia shahada ya 30 na kuendelea ndio wanaotokewa na mapepo na kuzungumza na shetani mwenyewe, na hao ndio wanaojua siri nyingi za chama hicho kuwa ni chama cha kumwabudu shetani moja kwa moja! na agenda kubwa ya chama hicho ni “kuikimbiza dunia katika ustaarabu mpya wa ulimwengu” ambao utakuja kuhasisiwa na Mpinga-kristo, chini ya utawala wa kirumi” katika siku za mwisho, lakini wengine wa shahada za chini hawaelewi sana.(www.wingulamashahidi.org)

Freemasons pamoja na vikundi vingine vya kichawi kama Iluminati, Brotherhood, ku-klax-klan,sisterhood, vinafanya kazi zinazofanana..Vyote ni vikundi vya kumwabudu shetani. Kwahiyo sio wote waliojiunga na freemasons wanaoelewa wapo sehemu gani.

JE! FREEMASONS NI WA KUOGOPWA?

Dhana iliyopo sasa hivi, ambayo hiyo inatokana na kukosa maarifa ni kwamba mtu aliyejiunga na freemasons tayari huyo ni pepo! hapana! hiyo si kweli kama tulivyotangulia kusema wapo wengine hawajui chochote wamedanganyika tu wakidhani kuwa ni kikundi cha kijamii cha kusaidiana kama vikundi vingine, hawaelewi vizuri freemason ni nini..Sasa hao wanahitaji msaada! Kumbuka ni watu kama wewe na mimi, wanapumua, wanasikia maumivu, wana hofu kama wewe na mimi, hivyo ni wa kusaidiwa kutoka huko kabla hawajazama kikabisa kabisa humo…sio wa kuwakimbia…Wanahitaji injili ya Yesu Kristo ya msamaha wa dhambi..wengine hawaelewi wamepelekwa tu na marafiki zao, ni kama tu makahaba waliojiingiza kwenye madanguro sio wote wanaelewa madhara ya kuwa kule, wanahitaji wokovu kama wewe ulioupata.

Ukienda pasipo maarifa kwa mtu ambaye ni freemason na kumwambia wewe ni shetani! unaabudu shetani na unatokewa na shetani kila siku na kuzungumza naye na kuua watu na kuwatoa kafara! na unakunywa damu…kwasababu tu umemwona kavaa pete yenye alama zao…

Ni rahisi sana kumkosa kwasababu hivyo unavyovisema unaweza kuta havifanyi katika levo aliyopo huko…kwasababu wote wanaojiunga huko kwa mara ya kwanza ni lazima wadanganywe… Hivyo huyo ni kumweleza kwa maarifa mwanzo wa chama hicho na mwisho wake.. Na kumweleza Injili ya Yesu Kristo ya msalaba…Lakini ukikutana naye na kuanza tu! kukemea hapo hapo! na kumwogopa!…na kumhakikishia kwamba yeye ni mchawi..atakushangaa sana na hatakuelewa, na pengine atakuchukia na itamfanya azidi kuamini kuwa yupo sehemu salama zaidi. Wengi waliojiunga huko ni kwasababu wamekosa maarifa..Hivyo wanatakiwa waokolewa kwa kupewa maarifa ya Neno la Mungu. Hivyo usikose maarifa ya namna ya kuvua roho za watu!.

Biblia inasema katika

Hosea 4:6 “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa;..”

WATU WANAJIUNGAJE FREEMASON

Na pia jambo lingine watu wasilolijua ni kwamba Freemasons watu hawajiungi kwa kupitia Facebook, wala hawajiungi kwa kupitia vipeperushi huko barabarani, wala vinakala juu ya nguzo za umeme…Huo wote ni utapeli tu ambao watu wanadanganywa…Ni watu wa kawaida ambao wanatafuta kupata pesa za kitapeli. Na pia freemasons ni kitu kidogo sana kwa mtu aliyeokoka haipaswi kukuzwa kiasi hicho mpaka kutengeneza hofu ya kupita pembezoni mwa barabara yenye jengo la freemasons, wala kumsalimia mtu aliyejiunga huko..Hakuna chochote kitakachokupata ukiwa ndani ya Kristo kwasababu shetani ni yule yule, unayeshindana naye kanisani ndio huyo huyo huko freemason! Sasa unachoogopa ni nini? (www.wingulamashahidi.org)

WATU WALIOJIUNGA FREEMASON WANAPATAJE PESA?

Na pia usikose maarifa kuwa freemasons ni mahali watu wanakwenda kupewa pesa!! hawaendi kupewa pesa, waliotoka huko na kumpa Bwana Maisha yao, wanasema “watu wote wanaojiunga huko ni wafanya kazi” na kule hawapewi pesa kana kwamba kuna ATM inayomwaga pesa…hapana! isipokuwa waliopo kule wanapeana fursa wao kwa wao, na ndio moja ya viapo vyao… freemasons wenzao waliopo ngazi za juu katika shughuli za ulimwengu kila mmoja ana jukumu la kumwangalia mwenzake aliye chini..

Kama mmoja yupo ngazi ya juu katika serikali anamnyanyua freemasons mwenzake aliye chini, kama mmoja ni mkurugenzi basi ikitokea nafasi ya kazi anamtafuta freemason mwenzake anamchomeka hapo n.k hiyo ndio maana unaona mtu aliyejiunga anaweza kupata maendeleo ya ghafla, na endapo akijitoa wananyang’anya ile nafasi, ndio maana unaona mtu anaporomoka ghafla. Lakini sio kwamba wanapewa hela za kimajini ambazo zinatokea tu kichawi! Huko ni kukosa maarifa!

UTAJITOAJE FREEMASON KAMA UMEJIUNGA?

Hivyo kama umejiunga huko! Kumbuka kujiunga kunakozungumziwa sio kwa kupitia facebook! Au mtandaoni….Kuna watu nimekutana nao, wanakuja kuomba msaada, wamedanganywa na matapeli facebook na kuambiwa wasipotuma kiasi fulani watakufa! Na hivyo wanaogopa na kutuma pesa! Hao ni matapeli..kujiunga kunakozungumziwa ni kule kuwasili kwenye hayo maukumbi yao, na kupewa viapo na kukutana na washirika wengine. Kama umejiunga kwa namna hiyo, mlango wa kutoka upo wazi.(www.wingulamashahidi.org)

Huko ulipo upo kwenye elimu ya shetani kamili, na nguvu za giza zimekufunika..Unamwabudu shetani sasa bila kujua, lakini ipo siku utamwabudu waziwazi, hivyo unayo nafasi ya kutoka…haijalishi uliapa kiasi gani! Kuwa utakitumikia chama hicho na endapo ukitaka kutoka utakufa! Nataka nikuambie hutakufa! Zaidi ya yote ukiendelea kukaa huko ndio utakufa.

Hapo ulipo fanya jambo moja la kiimani! Tubu! Na uwaambie mimi sio mmoja wenu tena! Watakutishia lakini hakuna kitakachokupata! Kwasababu aliye upande wako ni mkuu kuliko aliye upande wao. Na usiende tena huko, wala usifanye ibada zao, wala ishara zao, choma vito vyao, uniform zao, pamoja na mihamala yao..futa na namba za washirika wenzako. Tafuta kanisa la kiroho linaloamini injili kamili ya YESU KRISTO, dumu huko, Na ukae katika mafundisho ya Kweli ya Kristo Yesu. Au wasiliana nasi kupitia boxi la maoni hapo chini.

Kumbuka washirika wote wa Freemasons watakwenda kuzimu kwasababu wanamwabudu shetani kama wasipotubu! Hivyo kama hutatubu utakwenda kuzimu….Hivyo kwa hitimisho freemason ni nini?…jibu ni kikundi cha kishetani kinachomwabudu shetani.

Bwana akubariki.

Group la whatsapp Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

USIPIGE MATEKE MCHOKOO!

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.

VITA DHIDI YA MAADUI.

UNYAKUO.

JEHANAMU NI NINI?


Rudi Nyumbani:

Print this post