Title Devis

Je! hizi roho saba za Mungu ni zipi? na je zinatofautiana na Roho Mtakatifu?

Swali ambalo ni wajibu wetu sote kulijua ni juu ya Roho saba za Mungu, kwamba zenyewe ni nini na zinatendaje kazi. Na pia ni muhimu kufahamu juu ya makanisa saba

JIBU: Tukisoma mandiko yanatuambia kuwa Mungu ni mmoja, agano la kale linatuthibitishia hilo, (Kumb 6:4), vile vile agano jipya linatuthibitishia hilo, tukisoma katika (Marko 12:29) pale Bwana Yesu alipofuatwa na Yule mwandishi na kuulizwa ni amri ipi iliyo ya kwanza alijibu..


“….Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja; 30 nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.”

Hivyo maagano yote mawili yanathibitisha kuwa Mungu ni mmoja, lakini sasa kwanini tunamwona YESU kama Mungu, kwanini tunamwona Roho kama Mungu, tena tukiendelea kusoma tunaziona kuna Roho nyingine saba za Mungu, swali ni je! hawa wote wametokea wapi, ikiwa Mungu ni mmoja?.Hili ni moja ya swali lililoleta migawanyiko mikubwa sana sio tu katika ukristo, bali hata kwa wale wasioamini limewafanya wazidi kwenda mbali zaidi kwa kushindwa kuelewa utendaji kazi wa Mungu.

Tukiweza kujua kuwa kitu kinachoitwa Dhambi na kutengwa mbali na uso wa Mungu ndicho chanzo kilichopelekea tumwone Mungu katika taswira nyingi tofauti tofauti, tukilifahamu hilo basi hatutashindwa kumwelewa Mungu katika nafasi yake ya Uungu.. Na ameamua kufanya hivyo makusudi kwa lengo la kuturejesha sisi asingefanya hivyo leo hii tungekuwa makapi sisi. Laiti kama tusingeanguka katika dhambi, tungemwona Mungu na kuzungmza na Mungu kama yeye tu tusingejua kitu kingine cha ziada kumuhusu yeye, tabia zake zilivyo.

Kwamfano kulikuwa hakuna sababu ya Mungu kuutafuta mwili na kuiweka Roho yake mwenyewe ndani yake aje asulubiwe ili atupatanishe sisi na yeye kama tusingepotea katika dhambi, vile vile kulikuwa hakuna haja ya Roho Mtakatifu kuwa msaidizi wetu kama tungekuwa tunazungumza na Mungu uso kwa uso kama ilivyokuwa pale Edeni Adamu alipokuwa anazungumza na Mungu..

Ni sawa tu ni kifaa kinachoitwa simu, kama sio suala la umbali kati ya mtu mmoja na mwingine, simu isingehitajika katika jamii, kusingekuwa na haja ya wewe kuisikia sauti yangu kwenye kifaa kinachoitwa simu..Lakini je! Fikiria pia siku ile uliposikia mimi ninazungumza ndani ya kifaa kile, je ulisema nimegawanyika?, na kuwa wawili, kwamba mimi unayeniona tukizungumza uso kwa uso ni tofauti na Yule unayenisikia kwenye kifaa-simu? Ukweli ni kuwa utasema ni kifaa tu lakini mimi ni Yule Yule..Na ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana Yesu kuja kwake duniani, ..yule ni Mungu yule yule kauvaa mwili lakini sio MUNGU wa pili katika UUNGU, kama wengi wanavyodhani…YESU na Mungu BABA, sio Mtu na Mtu mwenzake, Ni Mungu yule Yule mmoja isipokuwa amekuja kwetu katika vazi lingine.
Kwa maelezo marefu ya kufahamu kwanini Yesu alikuja duniani, tutumie ujumbe inbox tukutumie somo lake..

Vivyo hivyo na Roho wake Mtakatifu, Yule sio Nafsi ya Tatu katika uungu bali ni ofisi ya tatu ya Mungu Yule Yule mmoja katika hatua zake za kuturejesha sisi katika mstari wake wa ukamilifu..Kama tusingekuwa katika hali ya dhambi na kumsahau Mungu, basi hakukuwa na haja ya sisi kupewa msaidizi, lakini Mungu aliona ajitoe sehemu ya nafsi yake iliyo moja aje kwetu kama Roho Mtakatifu ili atukumbushe yale yote Bwana Yesu aliyotuagiza.(Yohana 14:26).

Vile vile Roho Mtakatifu alipoachiwa pale Pentekoste, hakuachiwa kwa mtu mmoja mmoja tu peke yake kama wengi wanavyodhani, bali aliachiwa pia na kwa kanisa kwa ujumla..Hivyo kulikuwa na makanisa tofauti tofauti kulingana na wakati na majira..Sasa Roho huyu huyu aliyetenda pia kazi tofauti tofauti kulingana na kanisa husika..Ndio yale makanisa saba tunayoyasoma katika kitabu cha ufunuo sura ya 2&3, ..


Ufunuo 1:4 Yohana, kwa yale makanisa saba yaliyoko Asia; Neema na iwe kwenu na amani, zitokazo kwake yeye aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja; na zitokazo kwa roho saba walioko mbele ya kiti chake cha enzi;

makanisa saba

Sasa biblia inaposema Roho saba za Mungu nadhani utakuwa umeelewa kuwa hakuna tena Roho nyingine 7 zilizo mbele za Mungu, bali ni Roho Yule Yule mmoja akitenda kazi katika yale makanisa saba, Biblia inasema pia ndio macho 7 ya Mungu (Ufunuo 5:6), Na Taa 7 za moto (Ufunuo 4:5).
Kwa maelezo marefu juu ya nyakati saba za Kanisa,pia tutumie ujumbe inbox tukutumie somo lake..

Hivyo hizo zote ni hatua za Mungu za utendaji kazi lakini ni yeye Yule Yule, Mungu mmoja, hajagawanyika..


Lakini Swali lingine mtu anaweza kuuliza je! Tunafanya makosa kumwabudu YESU au Roho Mtakatifu? Jibu ni hapana, unapomwabudu Bwana YESU umemwabudu Mungu Yule Yule mmoja, Unapomwabudu Roho Umemwabudu Mungu Yule Yule mmoja, ni ofisi tu imebadilika, lakini Mungu ni Yule Yule umwabuduye..

Hivyo YESU ni Mungu mwenyewe katika mwili (1Timotheo 3:16), Roho Mtakatifu ni Mungu mwenyewe katika roho, vile vile zile Roho 7 za Mungu ndio Yule Yule Roho mmoja na ndio Mungu mwenyewe YEHOVA muumba wa mbingu na nchi, Hana mwanzo wala hana mwisho, ALFA NA OMEGA. Haleluya!

Je unampenda kwa moyo wako wote? Jibu unalo.


Ubarikiwe.Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Washirikishe na wengine habari hizi

 


Mada zinazoendana:

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

JINA LA MUNGU NI LIPI?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

ACHENI MJUE YA KUWA MIMI NI MUNGU.

MJUE SANA YESU KRISTO.

MUNGU KUSEMA NA WEWE PEKEE, HAITOSHI KUKUPA USHINDI.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Huyu Azazeli ni nani tunayemsoma katika(Walawi 16:8)

SWALI: Huyu AZAZELI ni nani? Kwa sababu ukisoma maandiko naye aikuwa anapewa kafara? (Walawi 16:8).



JIBU: Neno Azazeli linaonekana likitajwa mara moja tu katika kitabu cha Mambo ya Walawi sura ya 16, Azazeli sio mtu au kuhani bali ni mbuzi aliyetengwa kwa ajili ya upatanisho wa dhambi za Wana wa Israeli ndiye aliyejulikana kwa jina hilo, ambaye yeye hakuwa anachinjwa kwa ajili ya dhambi kama mbuzi wengine hapana bali yeye alikuwa anachukuliwa akiwa hai mpaka jangwani na kutelekezwa huko.


Maagizo hayo Mungu aliwapa wana wa Israeli, wayafanye katika siku ile kuu ya Upatanisho ambayo ilikuwa inafanyika mara moja tu kwa mwaka, tarehe 10 mwezi wa 7 wa kalenda ya Kiyahudi, wakati huo ndio ule Kuhani Mkuu anakwenda kufanya upatanisho kwa ajili ya dhambi za wayahudi wote siku hiyo kila mtu alipaswa asifanye kazi yoyote, bali unatulia nyumbani kwake ukiitesa nafsi yake kwa dhambi zake.


Sasa katika siku hii Kuhani Mkuu kwanza anawajibika kufanya upatanisho kwanza kwa ajili ya nafsi yake yeye mwenyewe na ya watu wake (wa nyumbani kwake), kisha ndio aende kufanya upatanisho wa dhambi za watu wengine, vinginevyo atakufa. Sasa katika kufanya upatanisho wa wana wa Israeli aliagizwa atwae mbuzi wawili kutoka katika mkusanyiko wa Wayahudi kwa sadaka ya dhambi na kondoo mmoja mume kwa sadaka ya kuteketezwa (Walawi 16:5), baada ya hapo kuhani mkuu anasimama mbele ya hema na kupiga kura kati ya wale mbuzi wawili.

Walawi 16:7 “Kisha atawatwaa wale mbuzi wawili na kuwaweka mbele za Bwana mlangoni pa hema ya kukutania.

8 Na Haruni atapiga kura juu ya wale mbuzi wawili; kura moja kwa ajili ya Bwana; na kura ya pili kwa ajili ya Azazeli.”

Akishamaliza mmoja anachukuliwa kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa dhambi za watu wote,
kisha damu yake inachukuliwa na kwenda kunyunyizwa katika hema ya kukutania na madhabahu, na yule wa pili hauliwi bali kuhani mkuu anamchukua na kuweka mikono yake yote miwili juu ya pembe za Yule mbuzi ambaye ndio anaitwa Azazeli kisha kuhani anaungama makosa yote na dhambi zote za wana wa Waisraeli walizozifanya juu ya mbuzi Yule,..baada ya hapo mbuzi huyo anakabidhiwa kwa mtu mmojawapo kisha anapelekwa jangwani mbali kabisa na makazi ya watu na kutelekezwa huko. Ndipo ouvu wa Israeli unafunikwa.


Walawi 16:21 “Na Haruni ataweka mikono yake miwili juu ya kichwa cha yule mbuzi aliye hai, na kuungama juu yake uovu wote wa wana wa Israeli, na makosa yao, naam, dhambi zao zote; naye ataziweka juu ya kichwa chake yule mbuzi, kisha atampeleka aende jangwani kwa mkono wa mtu aliye tayari.

22 Na yule mbuzi atachukua juu yake uovu wao wote, mpaka nchi isiyo watu; naye atamwacha mbuzi jangwani.”


Ni picha kamili tunayoiona katika agano jipya, Kristo akiwa kama Azazeli wetu alichukua dhambi zetu na mashutumu yetu yote, akasulibiwa nje ya mji, alihesabiwa kuwa si Kitu kwa ajili yetu.. Na kwa kupitia yeye dhambi zetu zinaondolewa moja kwa moja, tofauti na mbuzi Yule ambaye ikifika mwakani anapaswa atolewe mwingine…Ni raha kiasi gani ukikombolewa na Kristo,.Ukisamehewa dhambi zako, umesamehewa milele. Haleluya.


Ubarikiwe.


Mada Nyinginezo:

KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?

SANDUKU LA AGANO LILIKUWA LINAWAKILISHA NINI KATIKA AGANO JIPYA?

NAOMBA KUJUA WATAKAOENDA MBINGUNI JE! NI WENGI AU WACHACHE?

UNYAKUO.

SIKU YA TAABU YA YAKOBO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?

JIBU: Ndoto ni mfululizo wa picha na mawazo na hisia zinazokuja wakati mtu amelala, Na hizo zinakuja pasipo hiyari ya mtu, kwamba mtu hapangi au haamui ni nini cha kuota! zinakuwa zinajitengeneza zenyewe tu!..Na ndoto zinaweza kuathiriwa na shughuli zetu tunazozifanya kila siku au mazingira yanayotuzunguka au yaliyokuwa yanatuzunguka kipindi kifupi nyuma (Mhubiri 5:3, Isaya 29:8),

Na kuna ndoto zinatokana na shetani na nyingine zinazotokana na Mungu (Mwanzo 28:12, 37:5-10).


Na Maono hayana tofauti sana na ndoto, Maono ni mawazo ya picha na hisia yanayokuja wakati mtu akiwa hajalala…Na haya vile vile hayaji kama atakavyo mtu, wala mtu haamui ni aina gani ya maono ayaone wala huwezi kuyavuta kama mtu anavyovuta usingizi…. anajikuta tu ghafla anaona kitu ambacho sio cha kawaida au cha kawaida, au unakuta anaona tukio Fulani kama vile anaota, na anaporudi anajikuta alikuwa hajalala, pengine alikuwa anatembea au amesimama au alikuwa anaongea na mtu na analikumbuka lile tukio aliloliona kwenye hilo ono.

Na maono yapo yanayotokana na shughuli nyingi, hususani watu ambao wana msongo mkubwa wa mawazo na walioathirika na matumizi ya madawa makali, kadhalika yapo yanayoletwa na shetani haya yanawatokea wengi ambao ni wachawi au wenye roho za mapepo..na yapo yanayoletwa na Mungu.

Tofauti na inavyoaminiwa na wengi kuwa ni lazima kila mtu aliyezaliwa mara ya pili aone maono ya kiMungu, ukweli ni kwamba sio lazima kila mtu aone maono, mtu anaweza akazaliwa mara ya pili na hadi anakufa akawa hajawahi kuona ono hata moja na akaenda mbinguni..Kwasababu suala la kuona maono au kutabiri hivyo ni vipawa vya Roho Mtakatifu, na anapanga nani ampe na nani asimpe, ambaye hajapewa basi atakuwa amepewa kipawa kingine cha kipekee tofauti na hicho, na aliyepewa atakuwa amenyimwa vipawa vingine vya Roho. Haiwezekani watu wote wafanane au wawe na karama zinazofanana na haiwezekani mtu mmoja akawa na karama zote yeye peke yake (1 Wakorintho 12:29-31).


Jambo la muhimu ni kuzaliwa mara ya pili na kuwa kiumbe kipya,(Wagalatia 6:15) na kuishi kulingana na Neno, kuona maono au kutabiri au kufundisha hivyo sio vipimo vya utakatifu au tiketi za kwenda mbinguni (Mathayo 7:22).


Bwana akubariki.

Kwa mawasiliano/mafundisho zaidi kwa njia ya whatsapp, tutumie ujumbe kwenye
namba hizi: +255789001312/ +255693036618

 
 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mana zinazoendana:

NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI?

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

VIUNO VYENU VIWE VIMEFUNGWA NA TAA ZENU ZIWE ZINAWAKA.

TUSIPOUTHAMINI WOKOVU TUTAPATAJE KUPONA?

NI TAMAA IPI HIYO HAWA ALIAMBIWA ITAKUWA KWA MUMEWE?

JE! ASKARI MAGEREZA AKIAMURIWA KUMNYONGA MTU ANATENDA DHAMBI?

 


Rudi Nyumbani:

Print this post

Tunaposema tuishi kwa Neno, Inamaanisha tuishi maisha ya namna gani?


JIBU: Kuishi kwa Neno ni sawa mtu aseme ishi Kwa sheria au katiba ya nchi.Sasa unaishije kwa sheria ya nchi?, kwanza ni lazima uzijue sheria zenyewe kisha uziishi bila kuzivunja kwa namna yeyote ile, sheria ya nchi inasema usiibe mali ya mwingine, usiue, usile rushwa, usifanye biashara isiyo halali n.k unapozitii hapo ni sawa na kusema unaishi kwa sheria za nchi.

Na maana ya pili ya kuishi kwa sheria za nchi ni kuitumia sheria hiyo hiyo kupata haki yako..Kwamfano mtu haruhusiwi kukutesa, kwasababu sheria inakataza hilo, hivyo unatumia sheria kumshitaki au kumwonya, mtu anayetaka kukudhulu haki yako, kukudhalilisha, kukutapeli, au kukuua, au kukuibia unatumia sheria hiyo hiyo kujilinda…Kwasababu usipoijua haki yako utaonewa.
Na kwenye Neno la Mungu ni hivyo hivyo, unaishi kwanza kwa kulitii Neno la Mungu, Neno linaposema usizini, unapaswa usizini, linaposema mwanamke avae mavazi ya kujisitiri unapaswa ujisitiri, usiabudu sanamu, mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, nguvu zako zote na akili zako zote na jirani yako kama nafsi yako..Yote hayo unapaswa uyatii bila shuruti, Na hapo utakuwa umeishi kwa Neno. Hiyo ni namna ya kwanza.


Namna ya pili pia unalitumia Neno hilo hilo kujilinda dhidi ya yule mwovu, na kudai haki yako… mwovu akija na kusema utakufa wewe unasema Neno linasema sitakufa bali nitaishi (Zaburi 118:17), akija tena na kusema hutapona wewe unasema Neno linasema “kwa kupigwa kwake sisi tumepona (Isaya 53:5)”, unapopita katika bonde la mauti na misukosuko na dhoruba unasema Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu n.k. hivyo tu!..Kwa kufanya hivyo utaishi na wala hakutakuwa na jambo lolote litakalokushinda hapa duniani.
Hiyo ndio maana ya kuishi kwa Neno.


Ubarikiwe!


Mada Nyinginezo:

BIBLIA INASEMA USIONGEZE WALA USIPUNGUZE NENO LA MUNGU, HUKO KUONGEZA NA KUPUNGUZA KUKOJE?

AYUBU ALIJARIBIWA KWA MUDA GANI?

WAPUNGA PEPO WANAOZUNGUMZIWA KWENYE BIBLIA NI WATU WA NAMNA GANI?

NINI MAANA YA KIPAIMARA?..NA JE! NI JAMBO LA KIMAANDIKO?

VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.

NYOTA YA ASUBUHI.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya huu mstari ” Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;”?(2Timotheo 4:7)

JIBU: Vita vipo vya aina mbili, 1) Vita vya kuishindania Imani …na 2) Vita vya kuishindania Injili,

 Vita vya kuishindania Imani Tunasoma katika

Yuda 1:3 “Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, naliona imenilazimu kuwaandikia, ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu.

4 Kwa maana kuna watu waliojiingiza kwa siri, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, makafiri, wabadilio neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi, nao humkana yeye aliye peke yake Mola, na Bwana wetu Yesu Kristo.” 

Na hii ndio vita dhidi ya mafundisho potofu ambayo ambayo yanapindua imani zetu na dhidi ya dhambi ambayo inatenda kazi katika viungo vyetu …Wagalatia 5:17 “Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka”.

Waebrania 12:4 “Hamjafanya vita hata kumwagika damu, mkishindana na dhambi;”… 

Na kila mtu aliyezaliwa mara ya pili anapambana kwenye hii vita. 2. Aina ya pili ya Vita ni vita vya kuipigania injili, na hivi ndivyo Mtume Paulo alivyokuwa anavizungumziwa hapo katika hiyo 2 Timeotheo 4:7 , si vita vya kimwili bali ni vita katika safari yake ya kuhubiri injili, akipambana na majaribu na nguvu zote za yule mwovu katika kuwaleta watu kwa Kristo,

….. 2 Wakorintho 10:3 “Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili;

4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)

5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo”; 

Kazi ya kuhubiri Injili, siku zote shetani haifurahii hata kidogo, atanyanyua vikwazo vingi, na kuleta majaribu mengi..hivyo kusababisha vita vikali vya mapambano visivyoisha, ndio maana utaona Mtume Paulo alipitia kufungwa magerezani, kuchapwa bakora, kupigwa mawe kusalitiwa na kukumbwa na kila hatari katika safari yake ya kuhubiri injili.…

2 Wakorintho 11:3 “……. mimi ni zaidi; katika taabu kuzidi sana; katika vifungo kuzidi sana; katika mapigo kupita kiasi; katika mauti mara nyingi.

24 Kwa Wayahudi mara tano nalipata mapigo arobaini kasoro moja.

25 Mara tatu nalipigwa kwa bakora; mara moja nalipigwa kwa mawe; mara tatu nalivunjikiwa jahazi; kuchwa kucha nimepata kukaa kilindini;

26 katika kusafiri mara nyingi; hatari za mito; hatari za wanyang’anyi; hatari kwa taifa langu; hatari kwa mataifa mengine; hatari za mjini; hatari za jangwani; hatari za baharini; hatari kwa ndugu za uongo;

27 katika taabu na masumbufu; katika kukesha mara nyingi; katika njaa na kiu; katika kufunga mara nyingi; katika baridi na kuwa uchi”. 

Kwahiyo hapo aliposema amevipiga vita vizuri anamaanisha, “kuwa Ameishindania injili ipasavyo” hakuacha kuishindania kwasababu ya mateso amevumilia na kuvuta wengi kwa Kristo, na ndio maana juu kidogo mstari wa 5 utaona anamwambia Timotheo naye ashindanie Injili vivyo hivyo. Na kila mtu ambaye atakwenda kuhubiri Injili ni lazima akutane na hivyo vita na lazima apambane, na kushinda na kuhakikisha kwa gharama yoyote, anakwenda kuzivua roho za watu..Bwana Yesu alisema

 Mathayo 10:16 “Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwa-mwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua.

17 Jihadharini na wanadamu; kwa maana watawapeleka mabarazani, na katika masinagogi yao watawapiga;18 nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa”. 

2) Nitailindaje imani maana mimi nahitaji kulindwa na Mungu.

Ni vipi mkristo wa leo atailea na kuilinda imani?Utailinda Imani, kwa kuishika Imani…Na unaishika Imani kwa kukaa na kudumu katika Neno la Mungu..kila siku ukihakiki ni lipi limpendezalo Bwana,(Waefeso 5:10) na kujiepusha na Ulimwengu…Na jukumu la kuilinda Imani ni la mwanadamu si la Mungu, sisi ndio tunajukumu la kushika kile tulichonacho asije mtu akaitwa taji yetu Biblia inasema hivyo…

soma Ufunuo 3:11 na 1 Wakorintho 10:12. 3).je! kunao Mwendo wa kuumaliza, ni upi? Maandishi haya yamekua maarufu sana kwa mazishi, nisaidie tafadhali.Mwendo unaozungumziwa hapo, ni mwendo wa riadha, Safari yetu ya kwenda mbinguni inafananishwa na mashindano ya kukimbia mbio ndefu…tunapompa Kristo Maisha yetu ndio tunaanza mbio, na tunapoondoka duniani ndio tunakuwa tumeumaliza mwendo, kwahiyo hapo Mtume Paulo aliposema Mwendo ameumaliza, alikuwa yupo karibu sana na wakati wa kufariki kwake, Roho Mtakatifu alimshuhudia kuwa muda wake wa kuishi uliobakia sio mwingi…

Ukisoma juu kidogo mstari wa 6, utaona jambo hilo. Na maandishi haya yamekuwa yakiandikwa kwenye makaburi ya wapendwa wetu kuwafariji wafiwa, lakini kimsingi kama Maisha ya aliyekufa hayakuwa ya kikristo, wala hakupigana vita vyoyote vya kuitetea injili wala kushindana na dhambi, basi maneno hayo ni hewa tu! Hayana msaada wowote kwa aliyekufa. 

Bwana akubariki.

Mada Nyinginezo:

TUZO UTAPEWA KULINGANA NA NAFASI YAKO.

LULU YA THAMANI.

BEI YA UFALME WA MBINGUNI:

BARUA INAYOSOMWA

KISASI NI JUU YA BWANA.

BADO KITAMBO KIDOGO HAMNIONI

ZIFAHAMU NAMBA KATIKA BIBLIA NA MAANA ZAKE.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini kabila la Dani na Efraimu hayaonekani yakiorodheshwa miongoni mwa yale makabila 12 ya Israeli katika Ufunuo 7?

SWALI: Yakobo aliyeitwa ISRAELI:Alikuwa na wana 12 (Benyamini,Yusufu,Yuda,Lawi,Asheri,Isakari,Gadi,DANI,Zabuloni,Naftali,Reubeni,&Simeoni) Ambao kabila za Taifa la Israeli ziliitwa kwa majina ya hao wana 12 wa Israeli. Wana wawili wa Yusufu, Benyamini na Manase nao pia wanatajwa kuwa miongoni mwa makabila ya ISRAEL..Hivyo wana wa watoto wakiume wa Yakobo (WALIOFICHWA KUTAJWA KAMA KABILA ZA ISRAEL.Mfano wa Manase & Efraimu) nao pia wakitajwa kama kabila za Israel, hilo ni ono tosha kwamba Nchi ya ISRAELI imeundwa na zaidi ya KABILA 12 hivi? (SWALI:Bwana Mungu anapoenda kuupachika mzeituni halisi kwenye shina lake kulingana na Warumi 11} tunafunuliwa watakaopata hii neema ya mzeituni halisi kupachikwa ni KABILA12 tu za ISRAELI tunazizoma kwenye Ufunuo7:

Swali hapo ni kwanini hapo KABILA LA DANI na lile la Efraimu Yamenyimwa hiyo Neema (hayajatajwa hapo) kwenye hiyo ufunuo mlango wa 7?


JIBU: Shalom ndugu.. Makabila ya Israeli ni 12 tu, Efraimu na Manase, walihesabiwa tu miongoni mwa makabila 12 kwa upendeleo wa Yusufu kutoka kwa baba yake lakini makabila halisi yaani watoto wa Yakobo ni 12 tu, ambao wanatambulika kuliunda taifa la Israeli…na ndio wale ambao majina yao yanaonekana katika milango ya kuta za mji ule Yerusalemu mpya..(Ufunuo 21:12)..

Hao ni wale watoto halisi 12 wa Yakobo, kama tu vile misingi ya mji ule ilivyokuwa 12 kufunua wale mitume 12 wa Bwana… Sasa ni kwanini Efraimu na Dani, hawaonekani pale kwenye Ufunuo 7…Sasa kitu cha kutazama hapo ni kwamba kiuhalisi ni kabila moja tu halipo pale, nalo ni kabila la DANI, lakini kabila la Efraimu lipo, ndio lile kabila la Yusufu lililotajwa pale…Ikumbukwe kuwa Yusufu aligawanyika mara 2, Manase na Efraimu, Haiwezekani liwepo kabila la Yusufu halafu tena liwepo kabila la manase na Efraimu kwa mpigo, hapo basi Yusufu angepaswa awe na watoto wengine tofuati na hao wawili ili atengeneze kabila lake mwenyewe, lakini kama wale ni watoto wake, basi Kabila lake lazima ligawanyike tu,..

Hivyo unapoona Biblia inasema Kabila la manase halafu tena inasema kabila Yusufu ujue basi alimaanisha kabila la manase na kabila la Efraimu, vile vile unapoona mahali biblia inasema Kabila la Yusufu halafu tena kabila la Efraimu, basi ujue linamaanisha kabila la Manase na kabila la Efraimu…

Soma (Hesabu 1:32, 13:11)   Lakini tukirudi kwenye kabila la Dani ambalo tunaona limeondolewa, biblia haijatoa sababu ya moja kwa moja kwanini limetolewa, lakini tukirudi nyuma, tunaweza tukahisi sababu moja, kumbuka Mungu huwa hapendezwi na mambo maovu hususani uabuduji sanamu,..Na ukirudi kwenye agano la kale utaona ni kabila moja tu la Dani ndio lililokuwa ovu kiasi cha kutokumwogopa Mungu hadi kwenda kunyanyua sanamu na kuiweka katika mji wao (soma Waamuzi 18)..Hilo likawa chukizo kufikia hatua ya Mungu kuwaondoa katika neema ya wokovu aliokusudia kuuleta baadaye juu ya Israeli,..Hiyo inaweza kuwa ni sababu mojawapo zinaweza kuwepo sababu nyingine tusizozijua, pengine hadi hapo Mungu atakapotufunulia..

Lakini katika ulimwengu ujao Dani atakuwepo, Efraimu na Manase watarudi chini ya viuno vya Baba yao Yusufu na kuhesabiwa kuwa kabila moja.  

Ubarikiwe sana.


 

Mada Nyinginezo:

UFUNUO: MLANGO WA 7 & 11

UFUNUO: MLANGO WA 14

MPAKA UTIMILIFU WA MATAIFA UTAKAPOWASILI.

CHAKULA CHA ROHONI.

SWALI LA KUJIULIZA!

USILITAJE BURE JINA LA BWANA!


Rudi Nyumbani:

Print this post

Ni laana ipi hiyo Mungu alimaanisha ataipiga dunia nayo katika Malaki 4:5-6?

SWALI: Malaki 4: 5”Angalieni,nitawatumia Eliya nabii,kabla siku ile ya BWANA,iliyo kuu na ya kuogofya haijafika.Naye ataigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto wao,na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, ILI NISIJE NIKAIPIGA DUNIA KWA ‘Laana’…Hapo anamaanisha [LAANA kwa namna gani] au LAANA Ipi?.


JIBU: Mahali popote Mungu anapozungumzia kuipiga dunia, anamaanisha kwa mapigo kama yale yaliyotokea wakati wa Nuhu, na ule wakati wa Sodoma na Gomora,..

Kumbuka wakati ule wa Nuhu, watu walikuwa sio wa kujizuia na hiyo ikasababisha watu kujisahau kupindukia na hiyo yote ni kwasababu hakukuwa na manabii wa kutosha wa kuwaonya..Vile vile hata wakati wa utawala wa Mfalme ahabu, kama Eliya asingetumwa na Mungu kuwageuza watu mioyo iwaelekee Mungu, katika kipindi kile cha kilele cha maovu Israeli ambapo ibada za sanamu na miungu ilikuwa ni jambo la kawaida vikiongozwa na Yezebeli, walikuwa wamebakiwa na muda mchache sana kabla ya kuangamizwa kwao..Lakini kwasababu Mungu alilihurumia Taifa lake teule na viapo alivyomuapia Ibrahimu, basi alikuwa akiwatumia manabii wake wengi wawe wanawaonya mara kwa mara. 

Vivyo hivyo katika agano jipya, kama Mungu asingeachia Roho wake mtakatifu, na asingepeleka watumishi wake mitume na manabii kuhubiri duniani kote kuwaonya watu wamgeukie Mungu, dunia hii isingekuwepo mpaka leo hii..Tunaona tokea kipindi cha kanisa la kwanza Mungu amekuwa akiwatuma watumishi wake kwa Roho ile ile ya Eliya kuwarejesha watu wamegukie Mungu.. 

Hadi kanisa hili la mwisho la Laodikia tulilopo sasa tunaona aliwatuma watumishi wake wengi, akiwemo William Branham kwa ujumbe wa kuwarejesha watu wamgeukie Mungu..Na hata sasa bado anaendelea kuwatuma wengine wengi kwa huduma hiyo….. ikiwa utapenda kufahamu kuwa urefu juu ya huduma ya Eliya jinsi inavyotenda kazi katika agano jipya, nitumie ujumbe inbox nikutumie somo lake kwa urefu kwasababu hapa hatuwezi kuliandika lote.. Lakini ipo siku Injili hii ya kuonywa na kukumbushwa itakoma..Wala Mungu hataipeleka Roho yake tena juu ya watumishi wake kuigeuza mioyo ya watu imwelekee Mungu..Wakati huo ukifika basi ndio KIAMA chenyewe..

Hasira ya Mungu au LAANA ya Mungu itaakwenda kuachiliwa juu ya dunia nzima.. Kama Mtume Petro alivyoandika.. 

2 Petro 3:9 “Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.

10 Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.

11 Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,

12 mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka?”.

Bwana akubariki.

HOME

Print this post

Nitajuaje kama ndoto ni ya Mungu au ya Shetani?

JIBU: Maarifa yanayohusiana na ndoto ni mapana kidogo, lakini kwa ufupi, zipo ndoto za aina tatu,  

1) Ndoto zinazotokana na shughuli (Mhubiri 5:3): hizi ndio mara nyingi zinamjia mtu, kwamfano mtu alikuwa anafanya shughuli fulani siku nzima na usiku anapolala bado anaota anaifanya ile shughuli au anaota mambo yanayoendana na jambo ambalo amekuwa akijishughulisha nalo mara kwa mara. Sasa Kutokana na shughuli ile kuchukua sehemu kubwa ya siku yake au maisha yake, inapelekea pia kuchukua nafasi kubwa katika ulimwengu wa ndoto zake. Ndoto hizi ni mwili ndio unaozitengeneza, hazitokani na Mungu wala shetani.  

2) Ndoto zinazotokana na yule mwovu. Hizi zinatengenezwa na yule mwovu na kutumwa ndani ya mtu, Hizi ni ndoto zote zenye maudhui ya kumfanya mtu aikane au aiache IMANI, au zinampelekea mtu aende mbali na mpango wa Mungu, au kutenda dhambi na huwa zinaambatana na ushawishi fulani mkubwa sana mara baada ya kuamka.  

kwamfano mtu anaota kaachana na mume/mke wake na kupata mke/mume mwingine ambaye ni mzuri kuliko yule aliyekuwa naye, na anapoamka asubuhi anajikuta anaanza kuona kero ya kuishi na mke wake au mume wake kama ilivyokuwa hapo mwanzo. Au anashawishika kuamua kumwacha mumewe au mkewe.  

Au mtu anaota mzazi wake mmoja ni mchawi na hamtakii mema, na ile ndoto inamtaka ajitenge na huyo mzazi, au amchukie awe naye mbali. Au mwingine anaota anafanya uzinzi/uasherati na mtu asiyemjua au anayemfahamu, na anajikuta akiamka asubuhi ile roho ya tamaa bado inakuwa ndani yake kwa nguvu zaidi, tofauti na alivyokuwa jana.  

Au mtu anaota kapata utajiri kwa kumwibia mwajiri wake, au kwa kucheza kamari , na baada ya kuamka anajisikia msukumo ndani yake wa kwenda kufanya jambo lile na wakati mwingine mazingira aliyoyaona kwenye ndoto ndio hayo hayo anayaona akiwa nje ya ndoto kana kwamba ni unabii unatimia..  

Au wakati mwingine mtu anaota ndoto ameenda kwa mganga, akafanikiwa na anapoamka anashawishika kufanya mambo yale, au mtu anajikuta anaota kuna sanamu mahali fulani au kuna mti mahali fulani umebeba mafanikio yake (pengine uani kwake) na kwenye ndoto anaona ameukata ule mti na mambo yote yakaharibika, na anapoamka anajikuta anaogopa kuukata ule mti akijua ndio mafanikio yake yapo pale.  

Au wakati mwingine mtu anaota, ametenda dhambi na amejaribu kumwomba Mungu, na Mungu hataki kumsamehe, na anapoamka asubuhi anashawishika kuamini kuwa Mungu hataki kumsamehe na anamchukia.   Au ndoto nyingine mtu anaota amekufa baada ya kujaribu kuwa mkristo au kumpa Kristo maisha yake. N,k…

Sasa ndoto zote kama hizi zinatoka kwa yule mwovu kwasababu zina maudhui ya kumlazimisha mtu asilitii Neno la Mungu au aende kinyume na maagizo ya Mungu, zinampeleka mtu katika kutenda dhambi zaidi kuliko kumfanya kuwa mtakatifu, nyingine zinamfanya mtu awe mwoga zaidi na kumchukia Mungu kuliko kumpenda! N.k  

Namna ya kuzidhibiti hizi ndoto ni kuamua kuishi maisha masafi yampendezayo Mungu na kujifunza kwa kina Neno la Mungu ili shetani anapoleta mawimbi yake kama bahari uwe na uwezo wa kuyadhibiti, Kadhalika na kudumu katika maombi. kwamfano mtu anayeoota kafanya kosa na hasamehewi, hiyo ni mishale ya shetani kutaka kukuvunja moyo usitake kuendelea kumtafuta Mungu, kwahiyo kama Neno halipo ndani yako linalosema

“1Yohana 1: 9 “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote. ” hutaweza kumshinda shetani.  

Au ndoto inapokuja umegombana na mke wako na umeachana naye na kupata mwingine bora kuliko huyo, utajua imetoka kwa yule mwovu kwasababu Neno la Mungu limekaa ndani yako linalosema

“Luka 16:18 Kila amwachaye mkewe na kumwoa mke mwingine azini; naye amwoaye yeye aliyeachwa na mumewe azini. ”

Hivyo unajua ni ndoto iliyotoka kwa yule mwovu kukutaka wewe kutoka nje ya kusudi la Mungu na kutenda dhambi.   Au unapoota umebeti na umekuwa tajiri ghafla, utajua kabisa ni ndoto kutoka kwa yule mwovu kwasababu Neno la Mungu limekaa ndani yako linalosema “11 Mali iliyopatikana kwa haraka itapunguka; Bali yeye achumaye kidogo kidogo atazidishiwa. (Mithali 13:11)” Kwahiyo utajua ni yule mwovu anataka kukupeleka kwenye kazi iliyolaaniwa.  

Kadhalika na ndoto nyingine zote zinazofanana na hizo utazipima kwa Neno la Mungu tu! na utaweza kuzishinda na kuzifahamu kama Neno la Mungu linakaa ndani yako. Na pia kusali kabla ya kulala ni muhimu sana..Hiyo itasaidia kufunga mipenyo yote ya yule mwovu anayoweza kuitumia kukujaribu katika ndoto.  

3)Aina ya tatu ya ndoto ni ndoto zinazotoka kwa Mungu. Hizi ni zile zinazomjia mtu kutoka kwa Mungu kwa maudhui ya kumwonya mtu au kumuimarisha katika imani, na hizi haziwi kwa wingi kama zile zinazotokana na shughuli nyingi. Mfano wa ndoto hizi ni pale mtu anapoota kakutana na mtu/muhubiri kamshuhudia na kumwonya juu ya maisha yake maovu na anapoamka asubuhi anajikuta anahukumiwa na maisha ya dhambi anayoishi na kushawishika kutubu. Na mfano mwingine wa hizi ndoto ni pale mtu anaota unyakuo umepita na kaachwa, na anapoamka asubuhi anashawishika kujikagua maisha yake, nyingine mtu anaota kafa na kaenda kuzimu na anapoamka asubuhi anagundua ilikuwa ni ndoto tu.  

Nyingine ni zile mtu anaota kafanyiwa jambo baya sana la kumuumiza, na anapaamka asubuhi anajikuta yeye ndiye kamtendea mtu hilo jambo, hivyo anashawishika kujirekebisha na kutubu,   Nyingine unakuta mtu anaota kabeti, au kaenda kwa waganga, au kufanya uasherati, au kaiba, au kamtukana mtu, au kachukua mke au mume wa mtu, au kamsengenya mtu, au kaua na baada ya kufanya hivyo mambo yake yote yakaharibika, akajikuta kafilisika, au kafungwa, au kahukumiwa kufa, na anapoamka asubuhi anashawishika kutokufanya moja wapo ya mambo hayo ili yasimpate hayo mabaya. Hizo ni ndoto kutoka kwa Mungu, zinalenga kumuonya mtu   Na nyingine unakuta mtu anaota yupo shuleni anasoma, na kumbe alishamaliza muda mrefu sana, na anajiona anapambana kusoma na bado anafeli, ndoto ya namna hii unajua kabisa ni kutoka kwa Mungu kwasababu inayokuonyesha aina ya maisha unayoishi kwamba mwendo wako ni wa taratibu katika kumtafuta Mungu na bado upo nyuma ya wakati.  

Kwahiyo kwa ufupi ndoto zote zinazotokana na Mungu utazijua pia kama Neno la Mungu linalo kaa ndani yako, ndoto yoyote inayokupeleka kumtafuta Mungu zaidi, kutubu, au kukuonya tabia uliyonayo ambayo sio nzuri unajua kabisa ndoto hiyo inatoka kwa Mungu , au uichukie imani au ujitenge na kweli basi hiyo utajua moja kwa moja ni ya shetani.  

Ayubu 33:14 Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali.

15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani;

16 Ndipo huyafunua masikio ya watu, Na kuyatia muhuri mafundisho yao,

17 Ili amwondoe mtu katika makusudio yake, Na kumfichia mtu kiburi;

18 Yeye huizuia nafsi yake isiende shimoni, Na uhai wake usiangamie kwa upanga.

19 Yeye hutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, Na kwa mashindano yaendeleayo daima mifupani mwake;

Ubarikiwe sana.

 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?

NJONI, NUNUENI MLE NA MNYWE.

TULICHUNGUZE UMBO LA YESU NA MWENENDO WAKE.

MADHARA YA KUTAFUTA ISHARA.

NGUVU YA HEKIMA NA AKILI.

WANA WA MAJOKA.

UBATILI.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! mwanadamu wa kwanza kuumbwa ni yupi?

Je! mwanadamu wa kwanza kuumbwa ni yupi Mzungu, mwafrika au Mchina na kama ni mmojawapo kati ya hao je hao wengine wametoka wapi?

JIBU: Ni muhimu kufahamu kuwa Mungu aliiumba jamii moja tu ya watu..Hakuumba jamii nyingi za watu pale Edeni na hii jamii tunaipata kutoka kwa Adamu na Hawa

(Mwanzo 1: 27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba ).

Watu Hawa wawili ndio Mungu aliowaumba kwa ukamilifu wote bila kasoro kubwa wala ndogo,sasa Adamu na mke wake hawakuwa wazungu hapo mwanzo, kama wengi wanavyodhani, au waafrika au wachina au wahindi au jamii nyingine yeyote ya watu tunayoiona leo. la! Adamu na Hawa walikuwa ni watu wenye upekee wao ambao leo hii hatuwezi kuuona kwa mtu yeyote aliyeko duniani, wala hakuna mfano wa kulinganishwa nao kwa uzuri na mvuto waliokuwa nao kwasababu Mungu aliwaumba wakamilifu sana pasipo mapungufu yeyote. Lakini baada ya wao kumkosea Mungu na kuasi ule ndipo utukufu waliokuwa nao ukaanza kuondoka kidogo kidogo na mauti kuingia ndani yao.Siku baada ya siku wakaanza kubadilika mionekano yao ikaanza kuwa kama yetu sisi tunavyoonekana sasa hivi.

Hivyo miili yao ikaanza kubadilika ghafla kutokana na kwamba Utukufu wa Mungu umewaondokea, ardhi ikalaaniwa kama tunavyosoma, jua likaanza kuwa kali, mimea ikaanza kukauka baadhi ya maeneo, na kusababisha majagwa kutokea duniani, jasho likaanza kuwatoka kutokana na jua kuwa kali, ngozi zikazidi kubadilika, makovu yakaanza kutokea..Watu wakaanza kuzaliana kwa kasi na baada ya gharika dunia ilipozidi kuharibika zaidi na kupoteza taswira iliyokuwa nayo kwanza, tunakuja kuona watu wakaanza kuweka tena ustaarabu mpya duniani wakaanza kujenga ule mnara wa Babeli ili wamfikie Mungu..Lakini Mungu alipoona matendo yao ndipo akawatawanya waende katika pembe zote za dunia..

Mwanzo 11:1 Nchi yote ilikuwa na lugha moja na usemi mmoja.

2 Ikawa watu waliposafiri pande za mashariki waliona nchi tambarare katika nchi ya Shinari; wakakaa huko.

3 Wakaambiana, Haya, na tufanye matofali tukayachome moto. Walikuwa na matofali badala ya mawe, na lami badala ya chokaa.

4 Wakasema, Haya, na tujijengee mji, na mnara, na kilele chake kifike mbinguni, tujifanyie jina; ili tusipate kutawanyika usoni pa nchi yote.

5 Bwana akashuka ili auone mji na mnara waliokuwa wakiujenga wanadamu.

6 Bwana akasema, Tazama, watu hawa ni taifa moja, na lugha yao ni moja; na haya ndiyo wanayoanza kuyafanya, wala sasa hawatazuiliwa neno wanalokusudia kulifanya.

7 Haya, na tushuke huko, tuwachafulie usemi wao ili wasisikilizane maneno wao kwa wao.

8 Basi Bwana akawatawanya kutoka huko waende usoni pa nchi yote; wakaacha kuujenga ule mji.

9 Kwa sababu hiyo jina lake likaitwa Babeli; maana hapo ndipo Bwana alipoichafua lugha ya dunia yote; na kutoka huko Bwana akawatawanya waende usoni pa nchi yote.

Sasa kuanzia hapo jamii ya watu walikwenda zile sehemu zenye majangwa, wakakaa huko, wengine walikimbilia nchi za baridi, wakaa kaa huko, wengine sehemu za barafu, wengine visiwani, wengine misituni n.k…Hivyo walipoendelea kukaa kwa muda mrefu kutokana na mazingira waliyopo, wakaanza kuendana na yale mazingira, ndipo watu wakaonekana tofuati zao kulingana na mahali walipotokea.. Kwa mfano watu waliokuja pande za Afrika, mazingira ya huku tunafahamu ni ya joto, hivyo ni dhahiri kuwa ngozi ikipigwa na jua kwa muda mrefu inakuwa nyeusi, na pia nywele zinapungua..

kwahiyo hatushangai kuona watu wa Afrika ni weusi, kadhalika na watu waliopo nchi za baridi miili yao kwa kawaida itahitaji joto, hivyo nywele zitalazimika kukua na kuwa ndefu huko ndipo tunapowaona watu jamii ya wazungu, ukitazama nchi kama ya India, wahindi waliopo pande za kaskazini za baridi kama DELHI n.k utaona ngozi yao ni nyeupe, kadhalika waliopo pande za kusini(mf. Sri Lanka) ambako kuna joto kali utaone ngozi yao umefifia kidogo(inakuwa nyeusi) n.k.

Na kumbuka hii sio tu kwa wanadamu..bali hata kwa wanyama..Kama ukichunguza wanyama kama kondoo,ng’ombe au mbuzi mwitu, au farasi,mbwa,tembo n.k wanaotoka nchi za baridi utawaona wana manyoya mengi zaidi, kuliko wale wanaotokea nchi za joto.

Hivyo kwa ufupi mazingira ndiyo yaliyowabadilisha watu, na si kingine.

Shalom.

 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

JE! ADAMU ALIWASALIANA NA MUNGU KWA LUGHA IPI PALE BUSTANINI?

JE! NGOZI NYEUSI ILILAANIWA ?

MNARA WA BABELI

DAMU YA ZAKARI BIN BARAKIA.

 KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.

HUYU AZAZELI NI NANI TUNAYEMSOMA KATIKA(WALAWI 16:8)


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! baada ya ulimwengu huu kuisha malaika watakuwa na kazi gani tena?

SWALI: Moja ya kazi ya Malaika ni kumlinda Binadamu na Mapepo, Sasa baada ya hukumu kazi ya malaika itakuwa ipi kama shetani atakuwa kashatupwa na mwanadamu kainuliwa kiwango cha juu sana?. ( Inamaana Malaika watapotezwa au wataachishwa kazi zao?).


JIBU: Kama ulivyosema “MOJA” ya kazi ya malaika ni kutulinda sisi…kumbe hiyo ni mojawapo ya kazi zao, ikiwa na maana kuwa pia zipo kazi nyingine nyingi wanazozifanya…Ikumbukwe kuwa Malaika ni sehemu ya familia ya Mungu na Mungu aliwaumba wale miaka mingi kabla yetu sisi, Mungu hakungoja kutuumba sisi kwanza kisha awaumbe wao ili wapate kazi ya kufanya hapana..  

Mbinguni kuna shughuli nyingi sana zinazoendelea biblia haujatueleza kwa urefu mambo ya mbinguni yahusianayo na kazi za malaika kwa Mungu, tunachojua tu ni kwamba kuna wakati Bwana Yesu alitaka kutufunulia walau kwa sehemu mambo yanayoendelea mbinguni lakini aliacha hakutuambia na hiyo yote ilikuwa ni sababu ya kutokuamini kwetu.. Tunalithibitisha hilo katika  

Yohana 3:12 “Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani, wala hamsadiki, mtasadiki wapi niwaambiapo mambo ya mbinguni?”  

Hivyo fahamu tu malaika wanazo kazi nyingine nyingi mbele za Mungu tusizozijua sisi…Tukifika huko tutazifahamu..Sisi tumeishia tu kwenye hizo mbili zilizoandikwa kwenye biblia moja kwa moja yaani ile ya kutuhudumia sisi wanadamu (Waebrania 1:14), na nyingine ni kumsifu Mungu(Luka 2:13-14, Ufunuo 4:8), zaidi ya hapo hatujui…(Ikiwa utependa kujifunza kuwa upana somo lihusulo huduma ya malaika watakatifu kwetu sisi wanadamu, tutumie ujumbe inbox tutakutumia somo lake..)   Tunachopaswa kufanya sasa ni kuwa waaminifu na kutii kwanza haya tuliyopewa kuyaamini yahusuyo wokovu wetu, ili tukishashinda sasa, siku ile tutakapofika mbinguni tufunuliwe zaidi..   Na ndio maana mtume Paulo alisema:  

1Wakoritho 13:12 “Maana wakati wa sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana.”  

Hivyo malaika hawatatoweshwa, na wala hawatakosa kazi ya kufanya kwani hadi sasa zipo shughuli wanazozifanya ambazo hazina uhusiano wowote na sisi wanadamu.  

Ubarikiwe.


Mada Nyinginezo:

HUDUMU YA MALAIKA WATAKATIFU.

KUNDI LA MALAIKA WALETAO MABAYA.

JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI, AU KUTOA TALAKA?

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI:

JIWE LA KUKWAZA.

NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?


Rudi Nyumbani:

Print this post