Category Archive maswali na majibu

Rhema ni nini, katika biblia?

SWALI: Nimesikia hili neni Rhema, likitajwa sana Kwa watumishi na sehemu mbalimbali, naomba nifahamishwe maana yake Nini, mbona silioni kwenye biblia?


JIBU: Ni vema kutambua kuwa Biblia, katika eneo la agano jipya sehemu kubwa imeandikwa kwa lugha ya kiyunani. Hivyo Kuna baadhi ya maandishi ambayo tukiyasoma katika lugha nyingine mfano kwenye yetu hii ya kiswahili, tunaweza kuona yalimaanisha jambo lile lile moja lakini tukirudi kwenye lugha ya asili ya kiyunani yalimaanisha maana zaidi ya Moja.

Kwamfano, tunapokutana na hili Neno “NENO”. kwenye tafsiri yetu ya kiswahili, Mahali pote limeandikwa hivyo hivyo tu “Neno” likimaanisha Neno la Mungu.

Lakini tukirudi  kwenye lugha ya asili ya kiyunani zipo sehemu limelitajwa kama “Logos”na sehemu nyingine kama “Rhema”

Logos ikiwa na maana Neno la Mungu la Daima/ wazo la Mungu/mpango wa Mungu ulioandikwa  na pia kama Yesu Kristo mwenyewe, ambaye ndio Neno lililofanyika mwili.

Lakini ‘Rhema’: maana yake ni “Neno lililosemwa na Mungu” . Ni neno la wakati husika, sio la daima.

Mfano wa maandiko yanayolitaja Neno kama Logos ni haya: Yohana 1:1-18, Yakobo 1:22, Waebrania 4:12. N.k

Na mfano wa maandiko yanayolitaja Neno la Mungu kama Rhema ni haya;

Mathayo 4:3-4

[3]Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate. [4]Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.

Hapo Bwana aliposema, “ila Kwa Kila Neno litokalo katika kinywa Cha Bwana”..alimaanisha Neno lisemwalo na Bwana.. mfano wa Eliya alipomwambia yule mwanamke mjane, Bwana asema hivi; “lile pipa la unga halitapinguka, Wala Ile chupa ya mafuta haitaisha”. (1Wafalme 17:14). Halikuwa Neno ambalo lilitumika Kwa wakati wote, ambalo hata sasa tunaweza litumia sisi, Bali la wakati ule ule tu, amefunuliwa, akalisema na ikiwa hivyo.

Lakini ‘Rhema’ ni yaliyonenwa Kwa wakati huo tu..tofauti ya Yale yaliyokuwa Daima.

Neno lingine ambalo linasomeka kama Rhema katika biblia,. Ni wakati ule mitume wamehangaika usiku kucha kutafuta samaki, lakini kulipokucha Yesu akawaambia watweke.mpaka vilindini wakavue. Petro akasema maneno haya;

Luka 5:5

[5]Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu; lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu.

Aliliamini Neno lililosemwa na Bwana (na ikiwa vile).

Ili kuelewa vizuri tunaweza kusema  “logos” ni BIBLIA TAKATIFU, na Rhema’ ni Neno mtu analofunuliwa Kwa kipindi Fulani.

JE! MUNGU ANASEMA NA SISI HATA SASA KAMA RHEMA?

Ni kweli Mungu ameshatupa njia yake kuu ya kusema na sisi, ambayo ni Kwa kupitia Biblia. Lakini pia bado Mungu anasema nasi, na kutushushia Neno lake Kwa wakati husikia litufae.

Tuwapo katika kanisa. Mungu hutumia karama mbalimbali, kusema nasi, au kutupa ujumbe wake. Anasema kutumia unabii au fundisho, au Neno la hekima, au maono, au ndoto, kutuwasilishia Neno lake.

Lakini pia ni lazima tujue kuwa Neno hilo lililofunuliwa ni sharti lisikinzane na Neno lake lililoandikwa. Vyote viwili vikichanganyikana huleta matokeo makamilifu na kutufanya tumwone Mungu katika uhalisia wake zaidi katika maisha yetu, kwasababu yeye Yu hai.

Lakini ipo hatari kubwa sana. Kwani katika siku hizi za mwisho wapo baadhi ya watu wanalichukua Neno liliokuwa kama Rhema, na kulifanya logos yao. Ndio hapo wanaposoma Bwana Yesu alitema mate chini akachanganya na udongo, akampaka mtu machoni akaona, hivyo na wenyewe wanafanya hivyo Kwa kisingizio kuwa andiko limeruhusu. Au wanapomsoma mtume Paulo anatoa leso yake, Kisha watu wanapona kupitia Ile, na wenyewe wanafanya hivyo hivyo, wakisema andiko limeruhusu. Hawajui kuwa ulikuwa ni ufunuo wa wakati ule ambao si agizo kuu, ni Rhema’. 

Na madhara ya jambo hili ndio linageuka kuwa ibada ya sanamu. Tunayo mifano kadhaa katika biblia ya watu ambao waligeuza Rhema kuwa Logos, ikawapelekea kuingia katika laana. Kipindi Wana wa Israeli wakiwa jangwani, walipomkosea  Mungu alimwagiza Musa aunde nyoka wa shaba, ili Kila amtazamaye apone. Na kweli ilikuwa vile. Lakini baada ya pale haikuwa sheria mama kama vile torati, kana kwamba waendelee kufanya vile.  lakini tunaona baadhi ya watu walikuja kuifanya kama ndio sehemu Yao ya ibada ya uponyaji Kwa Mungu,.mpaka Mungu akachukizwa ikawapelekea kupelekwa tena utumwani Babeli, ikiwa kama mojawapo ya sababu.(2Wafalme 18:4)

Agizo letu la wakati wote ni JINA LA YESU TU! ndio logos yetu Bwana aliyotuagiza tutumie, wakati wote. Ikiwa hujafunuliwa kutumia kisaidizi/kiambatanishi kingine basi usifanye kwani huyo sio Mungu nyuma yake. Tegemea Biblia zaidi.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?

UUNGU NI NINI? (1Petro 1:3-4)

Shekina ni nini? Na Je! Utukufu wa shekina unamaana gani?

NENO LA MUNGU KATIKA UTIMILIFU WOTE.

Miimo ni nini na kizingiti ni nini?

Maziara ni nini? Je! Na Tunaruhusiwa kuyajenga kwenye makaburi yetu?

Maswali na Majibu

Rudi nyumbani

Print this post

JE YESU ALINENA KWA LUGHA?

Katika maandiko hakuna vifungu vya Moja Kwa Moja vinavyorekodi tukio la Bwana Yesu kunena Kwa lugha.

Lakini Kwa ufahamu wa Rohoni tuliopewa twajua kuwa ni wazi Yesu alinena Kwa lugha. Kutokurekodiwa Kwa tukio hilo hakumaanishi kuwa hakuwahi kunena Kwa lugha, kwasababu maandiko yanasema yapo mambo mengi aliyoyafanya Yesu kama yangeandikwa hata vitabu vyote duniani visingeweza kutosha, Kwa wingi wa habari zake.(Yohana 21:25)

Hivyo si Kila tukio la Bwana Yesu limeandikwa  kwenye biblia.

Halikadhalika Ifahamike kuwa taaarifa za kunena Kwa lugha aliyezieleza kwa mara ya kwanza Kwa mitume ni Bwana Yesu.(Hawakufunuliwa baadaye)   Hivyo hawezi kuwaambia watu jambo ambalo yeye mwenyewe halipo ndani yake, au hajawahi kulifanya.

Marko 16:17-18

[17]Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;

[18]watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.

Vilevile Yesu ndiye mwanadamu pekee aliyetiwa mafuta mengi na Roho kuliko mtu yeyote aliyewahi kutokea duniani, (Waebrania 1:9). Zile karama zote za Roho zilikuwepo ndani yake, alikuwa ni nabii, mwalimu, mwinjilisti, mchungaji, mtume, n.k. na karama za uponyaji, miujiza, upambanuzi alikuwa nazo, hivyo hatuwezi kushangaa pia na hii kunena Kwa lugha kuwemo ndani yake.

Kwa kuhitimisha ni wazi kuwa Bwana Yesu alinena Kwa lugha. Hivyo akampendeza kukimwaga  kipawa hicho na kwetu pia.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Je kunena kwa Lugha mpya kukoje?

WANAWAKE WAOMBOLEZAJI

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

IJUE FAIDA YA KUNENA KWA LUGHA MPYA!

YEYE ATAWABATIZA KWA ROHO MTAKATIFU NA KWA MOTO.

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOKUJA JUU YA MTU.

Rudi nyumbani

Print this post

Ipi tofauti kati ya matoleo na sadaka?

Jibu: Jina la Bwana Yesu Kristo lisifiwe daima.

Matoleo ni Neno la ujumla linalomaanisha aidha sadaka, au michango.

Neno Matoleo linatokana na neno “Kutoa” Hivyo chochote kile mtu anachokitoa kwa Mungu wake kinaitwa Matoleo.

Lakini sadaka ni toleo rasmi ambalo linalenga moja kwa moja madhabahu, na matoleo ya sadaka tofauti na matoleo mengine kama michango ni kwamba sadaka inakuwa ni siri lakini michango mengine inaweza isiwe Siri,

Kwamfano yale matoleo Anania na Safira mkewe waliyoyatoa ya kuuza viwanja na kuleta thamani yake chini ya miguu ya mitume, hayakuwa siri, bali lilikuwa ni jambo linalowekwa wazi kwa wote.

Lakini sadaka haipaswi kuwa kitu cha kuonyesha mbele za watu, bali kinapaswa kiwe siri ya mtu na Mungu wake…kama Bwana wetu Yesu alivyotufundisha.

Mathayo 6:2 “Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu”.

3 Amin, nawaambieni, Wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe utoapo sadaka, hata mkono wako wa kushoto usijue ufanyalo mkono wako wa kuume;

4 sadaka yako iwe kwa siri; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.

Na Matoleo yote (iwe changizo au sadaka). Yana thawabu kubwa mbele za Mungu kama yakitolewa kwa nia njema na dhamiri njema na kulingana na Neno la Mungu,na Mungu anayaangalia sana.

Ukiahidi au ukipanga kumtolea Mungu kitu, basi hakiksha unatimiza kama ulivyoahidi au ulivyopanga pasipo kupunguza hata kidogo, ili isiwe kwako dhambi kama ilivyokuwa kwa Anania na Safira mkewe, ambao waimdanganya Roho Mtakatifu kwa matoleo yao.(Matendo 5:1-11).

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +25569303661

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

KUWA MAKINI, HATUA ZA UNYAKUO ZINAENDELEA.

Sadaka ya Amani ilikuwaje?

Sadaka ya Moyo ipoje? (Walawi 22:21).

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

Fahamu maana ya Mithali 28:20 Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele;

Rudi nyumbani

Print this post

UUNGU NI NINI? (1Petro 1:3-4)

2 Petro 1:3  Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe

4 Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa.

Uungu ni Ile Hali ya kuwa kama Mungu.

Kwamfano mtu anayefanya vitendo viovu kama vya  uuaji, utoaji mimba, uchawi, ushoga tunasema anafanya “Ushetani”.. Kwasababu anatenda kazi za shetani. 

Vivyo hivyo tunaposema “Uungu”. Tunamaanisha kuwa kama Mungu, au kufanya kazi kama za Mungu, au kuwa na sifa za Mungu ndani yako.

Na Tabia ya Mungu ndani ya Mtu. Si Kila mtu anazo. Bali ni wale tu waliozaliwa na yeye. Yaani waliokoka

Hizi ni baadhi ya Tabia za kiungu.

1. Uzima wa milele:

Kitu ambacho Mungu anawakiria watu wake waliompokea ni uzima wa milele. Ambao upo ndani yake. Mwanadamu wa Tabia ya asili Hana uzima wa milele ndani yake. Akifa Hana Tumaini la kuishi. Lakini aliyezaliwa mara ya pili. Huishi milele. Kwasababu uungu upo ndani yake.

Yohana 10:34  “Yesu akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, Ndinyi miungu?”

Ukiwa kama mwana wa Mungu sifa hii ni lazima itaonekana ndani yako. Hakikisho la uzima wa milele, mwovu hana uzima wa milele.

2. Matunda ya Roho

Pili mtu mwenye uungu ndani yake, anatoa tabia za Mungu ndani yake, ndio zile tabia za Roho tunazozisoma katika Wagalatia 5:22, kama vile Upendo, , fadhili, uaminifu, utakatifu n.k.

Wagalatia 5:22-25

[22]Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, [23]upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria. [24]Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake. [25]Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.

Mambo ambayo huwezi kuyaona kwa mtu mwenye tabia ya asili. Yeye huwa kinyume chake, au akijaribu kufanya basi ni kwa unafki, kwasababu havipo moyoni mwake.

3. KUSHINDA DHAMBI:

Na pia mtu mwenye tabia ya uungu unakuwa na uwezo wa kuushinda ulimwengu(yaani dhambi) kama vile Kristo alivyoushinda ulimwengu..

1 Yohana 3:9

[9]Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu.

Maana yake,dhambi inakuwa haina nguvu ndani yake. Maandiko yanasema hata wao wenyewe wakishangaa tunawezaje kuishi  maisha ya mbali na dhambi (1Petro 4:4). Hawajui  Ni kwasababu sisi tuna tabia za uungu ndani yetu.

Maandiko mengine yanayoeleza Neno uungu. Ni haya  (Matendo 17:29, Warumi 1:20).

Bwana akubariki.

Je! Na wewe utatamani uwe na tabia za Ki-Mungu ndani yako?. Ni wazi kuwa hii ni kiu ya kila mmoja wetu. Kama ni hivyo basi, hauwezi kwa akili yako au nguvu zako, bali kwa Roho wa Mungu. Kwasababu biblia inasema wote waliompokea aliwapa UWEZO wa kufanyika wana wa Mungu (Yohana 1:12). Hivyo huu ni uwezo utokao kwa Mungu mwenyewe, na sio kwa mwanadamu. Na tunaupata kwa kutubu dhambi zetu kwa kumaanisha kabisa kuziacha, kwa kumkiri Yesu, na kumfanya kama Bwana na mwokozi wa maisha yetu. kisha kumpa nafasi ya kuyatawala maisha yetu.

Hivyo basi ikiwa upo tayari siku ya leo kutubu dhambi zako, ili Bwana akufanye kiumbe kipya. Basi fungua hapa kwa ajili ya mwongozo wa Sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

Uzima wa milele ni nini?

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

DANIELI: Mlango wa 12.

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

Ni kosa gani alilolifanya Eli, ilihali aliwaonya watoto wake?

Rudi nyumbani

Print this post

Dinari ni nini na Rupia ni nini (Mathayo 20:2,Ufunuo 6:6)

Dinari ilikuwa ni sarafu ya kirumi yenye thamani ya (utumishi wa kibarua wa siku nzima)..Kwamfano leo hii tuseme kibaru atalipwa kwa siku shilingi elfu 20, na ukawa ndio utaratibu wa nchi nzima, kuwalipa vibarua kiasi hiko kwa siku kama mshahara, basi kiasi hiko cha fedha kingekuwa na thamani sawa na Dinari kwa wakati huo.

Tutalithibitisha hilo Zaidi katika ule mfano Bwana alioutoa wakulima walioajiriwa katika shamba la mizabibu..

Mathayo 20:1  “Kwa maana ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu

2 Naye alipokwisha kupatana na wakulima KUWAPA KUTWA DINARI, aliwapeleka katika shamba lake la mizabibu”.

Kwahiyo “ malipo ya utumishi wa kutwa nzima wa kibarua” ndiyo yaliyokuwa na uthamani wa “Dinari”  na uzito wa sarafu ya Dirani ulikuwa ni “gramu 3.85”,

Kwa urefu kuhusiana na vipimo hivyo fungua hapa  >>>VIPIMO VYA KIBIBLIA

Lakini tukirudi katika “Rupia”.. tunaisoma sehemu moja tu katika kitabu cha Ufunuo 6:6

Ufunuo 6:5  “Na alipoifungua muhuri ya tatu, nikamsikia yule wa tatu mwenye uhai akisema, Njoo! Nikaona, na tazama, farasi mweusi, na yeye aliyempanda ana mizani mkononi mwake.

6  Nikasikia kama sauti katikati ya hao wenye uhai wanne, ikisema, Kibaba cha ngano kwa NUSU RUPIA, na vibaba vitatu vya shayiri kwa nusu RUPIA, wala usiyadhuru mafuta wala divai”.

“Rupia” ni sarafu nyingine yenye thamani sawa na “Dinari”.. ambayo ilikuwa inatumiwa zaidi namataifa mengine tofauti na Rumi (uthamani wake ulikuwa ni sawa na mshahara wa kibarua wa kutwa)… Na mpaka sasa bado baadhi ya mataifa yanatumia Rupia!.

Lakini ni somo gani tunalolipata kutoka katika thamani hii ya fedha (Dinari na Rupia)?

Somo kubwa tunalolipata si lingine Zaidi ya lile tunalolisoma katika Mathayo 20:1-16, kuwa thawabu za Mungu hazichunguziki.

Kwa urefu unaweza kusoma hapa >>KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

AINA TATU ZA WAKRISTO.

GHARAMA YA UFALME WA MBINGUNI.

SHAMBA HUWA HALIMTAMBUI WALA KUMSUBIRIA MKULIMA.

Je! Ni sawa kuingia katika shamba la mtu mwingine na kula jinsi utakavyo?

Rudi nyumbani

Print this post

Kuba ni nini (Ayubu 22:14)?

Jibu: Tusome,

Ayubu 22:12 “Je! Mungu hayuko mbinguni juu? Tena tazama umbali wa nyota, jinsi zilivyo juu!

13 Nawe wasema, Mungu anajua nini? Je! Aweza kuamua kati ya giza kuu?

14 Mawingu mazito ni kifuniko chake, hata asione; Naye yuatembea juu ya KUBA YA MBINGU. 

15 Je! Utaiandama njia ya zamani Waliyoikanyaga watu waovu?”

Kuba ni mzunguko wa Anga, Ukitazama juu utaona ncha za mbingu ni kama duara, ndio maana jua wakati wa asuhuhi ni kama “linachomoza kutoka chini upande wa mashariki” na wakati wa mchana linaonekana lipo juu kabisa (utosini) lakini inapofika  jioni “linazama tena chini upande wa magharibi”..

Sasa huo mduara wa anga ndio unaoitwa “KUBA” na maandiko yanasema Bwana anatembea juu ya mduara huo, kuonyesha utukufu wake.

Ayubu 22:14 “Mawingu mazito ni kifuniko chake, hata asione; Naye yuatembea juu ya KUBA YA MBINGU”. 

Hivyo andiko hili linaonyesha utukufu na ukuu wa Mungu, kuwa yuko juu sana na mwingi wa uweza.

Je umemrudia yeye aliyezifanya Nyota na Mwezi, na anga na viumbe vyote?..

Mhubiri 12:1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo.

 2 Kabla jua, na nuru, na mwezi, Na nyota, havijatiwa giza; Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

MKUU WA ANGA.

NYOTA ZIPOTEAZO.

Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?

Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.

Mbinguni ni sehemu gani?

Rudi nyumbani

Print this post

JE! TUNAPASWA TUOMBE MARA NGAPI KWA SIKU?

Biblia haijatoa ‘fomula’, ya idadi ya nyakati tunazopaswa kuomba kwa siku. Ila imesema ‘tuombe kila wakati’ na sehemu nyingine imesema ‘tuombe bila kukoma’. Hiyo ni kutupa uelewa kwamba maombi yanapaswa yawe ni endelevu lakini pia yawe ya wakati wote. Na hakuna mahali maandiko yanatoa nafasi ya mwaminio kutokuomba kabisa.

Waefeso 6:18  “kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;”

1Wathesalonike 5:17  “ombeni bila kukoma”

Hivyo ni sisi kutazama, watakatifu walikuwa na desturi gani, na nidhamu gani waliyojijengea katika kuomba. Je! Walitumia vipindi vingapi kwa siku? Vilevile tutaona Bwana Yesu anasemaje kuhusiana na hilo pia. Ili na sisi tuige vielelezo vyao katika  utaratibu wetu wa kusali.

DAUDI

Daudi aliomba mara tatu(3) kwa siku . Asubuhi, adhuhuri na jioni.

Zaburi 55:17 Jioni, asubuhi, na adhuhuri nitalalama na kuugua, Naye ataisikia sauti yangu.

DANIELI

Danieli pia aliomba mara tatu (3), kwa siku.

Danieli 6:10 Hata Danieli, alipojua ya kuwa yale maandiko yamekwisha kutiwa sahihi, akaingia nyumbani mwake, (na madirisha katika chumba chake yalikuwa yamefunguliwa kukabili Yerusalemu;) akapiga magoti mara tatu kila siku, akasali, akashukuru mbele za Mungu wake, kama alivyokuwa akifanya tokea hapo.

Hivyo hii ni kutuonyesha kuwa ilikuwa ni desturi ya watakatifu wa kale, kwenda magotini walau mara 3 kwa siku. Na maombi waliyoyaomba hayakuwa ‘sala’ za dakika tano (kama zile za kuombea chakula).  Bali ni maombi ambayo huwenda yalizidi saa moja, kwasababu maombi  ya kulalama, na kuugua, (mfano wa hayo ya Daudi) sio ya dakika chache.

YESU KRISTO.

Bwana Yesu aliomba alfajiri na usiku, na majira mengi nyakati za adhuhuri aliahirisha huduma na kwenda mahali pa utulivu kusali.

Marko 1:35  “Hata alfajiri na mapema sana akaondoka, akatoka akaenda zake mahali pasipokuwa na watu, akaomba huko”

Na usiku

Mathayo 26:40  “Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja? 41  Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu”.

Adhuhuri

Luka 5:16  “Lakini yeye alikuwa akijiepua, akaenda mahali pasipokuwa na watu, akaomba”

Hivyo tunaona pia Bwana aliomba nyakati zote. Alipopata nafasi.

Hivyo kiwango cha chini kabisa cha nyakati za kuomba kwa siku kwa sisi wakristo ni MARA MBILI. Yaani asubuhi na jioni.  Unapoanza siku huna budi kuanza na Bwana kwa kumshukuru na kumwomba mwongozo wa siku hiyo, vilevile unapomaliza siku wapaswa ufanye hivyo hivyo.

Na ndio maana Bwana alisema maneno haya, kwa watu wake wanaoomba alisema;

Luka 18:7  Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?

Kumbe usiku na mchana tunapaswa tuombe. Walau mara mbili kwa siku. Alisema, Yeye ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho. Kufunua kuwa yupo katika mwanzo wetu na mwisho wetu. Hakikisha uanzapo siku unatenga muda wa kutosha wa kuingia uweponi, na umalizapo siku unafanya hivyo hivyo. Utakuwa imara sana kiroho.

Lakini zaidi sana Bwana anataka tuwe watu wa kuomba siku zote kufikia hata kukesha. Hivyo ikizidi hapo ni vema sana, kwasababu utajiwekea akiba ya maombi kwa wakati ambao utakuwa na nguvu chache.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.

HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA

Fahamu Namna ya Kuomba.

NITAJUAJE KAMA MAOMBI YANGU YAMEFIKA (YAMEJITOSHELEZA)?.

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Adamu na Hawa walizikiwa wapi?

JIBU: Ipo mitazamo mingi, ihusuyo eneo halisi la makaburi ya wazazi wetu wa kwanza, Kwamfano kwa mujibu wa hadithi za kiyahudi, wao wanaamini kuwa Adamu na Hawa walizikwa pale Israeli, mahali palipoitwa Hebroni katika pango lijulikanalo kama pango la  Makpela. Ambalo baadaye Ibrahimu na Sara walikuja kulinunua likawa ni eneo la maziko yao ya kifamilia, (Mwanzo 49:29-31)  kwa  urefu wa habari hiyo fungua hapa usome >>> Pango la Makpela ni lipi,

Wengine, wanaamini kuwa pale Kristo  aliposulubiwa Golgota, ndipo palipokuwa kaburi la Adamu, wakiamini kuwa kama Kristo alivyoitwa Adamu wa pili, maana yake ni alikuja kurudisha kile kitu ambacho Adamu wa kwanza alikipoteza, yaani uzima. Hivyo kama Adamu alileta kifo, Kristo alileta uzima kwa msalaba wake, na aliyafanya hayo  juu ya kaburi la Adamu.

Lakini je! kuna usahihi kwa mitazamo hiyo.

Kwasababu biblia haijaeleza chochote, kuhusiana na kaburi la Adamu na Hawa, hii yote ni mitazamo, ambayo yaweza kuwa ukweli au uongo, tusiweke imani yetu moja kwa moja katika mitazamo. Kwasababu gharika ilipokuja ilivuruga ramani yote ya ulimwengu, isingekuwa rahisi kupatambua mahali sahihi alipozikwa Adamu, isipokuwa kwa ufunuo.

Na habari hiyo kutoandikwa ni kutuonyesha kuwa hakuna umuhimu sana wa kujua Adamu alizikiwa wapi. Ushindi tulioupata kwa kifo cha Kristo, na kufufuka kwake, ni habari tosha tunayopaswa tuitafakari usiku na mchana, zaidi ya kaburi la Adamu.

Lakini swali ni Je! Yesu amefufuka ndani yako? Fahamu kuwa  Ikiwa bado hujazaliwa mara ya pili, kifo kina nguvu juu yako, ukifa hakuna maisha kwako, ni mateso katika moto wa jehanamu. Lakini ukizaliwa mara ya pili uzima wa milele unao na hata ukifa, utakuwa unaendelea kuishi.

Yohana 11:25  “Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; 26  naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo?

Unasubiri nini? Usiokoke leo.

Saa ya wokovu ni sasa, ni pale tu unapotubu kwa kumaanisha kuacha dhambi, na kumwita Yesu ayatawale maisha yako, kisha kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu. Hapo unakuwa tayari umezaliwa mara ya pili. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo sasa, basi fungua hapa kwa mwongozo wa Sala hiyo ya toba.>>>KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

Maziara ni nini? Je! Na Tunaruhusiwa kuyajenga kwenye makaburi yetu?

JINA LAKO NI LA NANI?

Kuhimidi ni nini?(Zaburi 31:21)

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?

Rudi Nyumbani

Print this post

Tofauti kati ya mwonaji na Nabii ni ipi?

Katika biblia mtu ambaye alipokea taarifa iliyofichwa kutoka Kwa Mungu na kuiwasilisha Kwa watu aliitwa mwonaji. Alipokea aidha kupitia, maono, ndoto, au kufunuliwa dhahiri, Mfano wa Hawa alikuwa ni Samweli…

1 Samweli 9:9-12

[9](Hapo zamani katika Israeli, mtu alipokwenda kuuliza neno kwa Mungu, husema hivi, Haya! Twende kwa mwonaji; maana mtu aitwaye sasa Nabii hapo zamani aliitwa Mwonaji.)

[10]Basi Sauli akamwambia mtumishi wake, Umesema vema; haya! Twende. Wakaenda mpaka mji ule aliokuwamo mtu wa Mungu.

[11]Hata walipokwea kwenda mjini, wakakutana na wasichana, wanatoka kwenda kuteka maji; wakawaambia, Je! Mwonaji yuko?

[12]Nao wakawajibu, wakasema, Yuko; tazama, yuko huko mbele yako; fanyeni haraka sasa, maana hivi leo amekuja mjini; kwa sababu watu wana dhabihu leo katika mahali pa juu;

Lakini baadaye watu Hawa walikuja pia kuitwa Manabii kama tunavyosoma kwenye vifungu hivyo

Isipokuwa Maana ya Nabii ni Pana zaidi sio tu kupokea taarifa kutoka Kwa Mungu na kuiwasilisha Bali pia alisimama kufundisha na kuwarejesha watu, katika Sheria ya Mungu.ikiwemo kukaripia na kukemea, na kuonya. Mfano wa Hawa ni Isaya, Yeremia, Ezekieli, Yona, Hosea, Mika, Hagai, Malaki na wengine.

Hivyo nabii ni lazima pia awe mwonaji, kwamba apokee pia taaarifa za Moja Kwa Moja kutoka Kwa Mungu, na kufichua Siri zilizositirika lakini mwonaji haikuwa lazima afanye kazi ya kinabii,  Bali ni kusema tu kile anachoelezwa, au kufichua Siri zilizojificha, au kuomba mwongozo wa  Roho wa Mungu, Kwa ajili ya jambo/tatizo Fulani.

Hivyo kuhitimisha ni kwamba Kuna maandiko mengine yanawataja waonaji, lakini yalimaanisha pia ni manabii, na mengine yanabakia kumaanisha walewale tu waonaji.

Mfano wake ni Samweli, ambaye alikuwa ni mwonaji lakini pia ni Nabii.

1 Mambo ya Nyakati 29:29

[29]Basi habari za mfalme Daudi, mwanzo na mwisho, angalia, zimeandikwa katika tarehe ya Samweli, mwonaji, na katika tarehe ya Nathani, nabii, na katika tarehe ya Gadi, mwonaji;

Soma pia vifungu hivi, kufahamu zaidi.

(2Samweli 24:11, 2Nyakati 16:7, 29:30,)

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.

NA TAA YA MUNGU ILIKUWA BADO HAIJAZIMIKA.

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?

NA TAA YA MUNGU ILIKUWA BADO HAIJAZIMIKA

Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Fahamu Maana ya Mithali 18:13 Yeye ajibuye kabla hajasikia, Ni upumbavu na aibu kwake.

Maelezo ya Mithali 18:13 Yeye ajibuye kabla hajasikia,  Ni upumbavu na aibu kwake.


Hekima inatufundisha tusiwe watu wa kujibu au kuzungumza kabla hatujasikia habari yote au taaarifa yote na kuitafakari kwanza..Kwamfano mwenzako anazungumza jambo Kisha wewe ukaingilia kati na kutaka kujibu, hoja ambayo haijakamilika..Matokeo yake hapo ni Nini kama sio kutoa majibu yasiyosahihi?. Au ambayo hayajakamilika?

Ndio hapo anasema ni upumbavu na aibu kwake. 

Hii imeathiri hata kusambaa Kwa taaarifa za uongo. Mtu atasikia jambo, kwasababu Hana taaarifa nalo vizuri, atatoka muda huo huo na kwenda kumpasha mwingine, na yule mwingine atampasha mwingine..Hivyo taaarifa za uongo huzagaa Kwa upesi sana. Ndivyo ambavyo hata waandishi wa habari ambao hawawi makini wanavyosambaza habari ambazo bado hawajazifanyia uchambuzi yakinifu. Na matokeo yake husababisha matatizo makubwa katika jamii. 

Mafarisayo na wayahudi walimpinga Yesu kwasababu walikuwa ni watu wa kupokea tu taaarifa ambazo hawazitafiti, walisikia Yesu anatokea Nazareti, wakahitimisha amezaliwa Nazareti, wengine wakamwita Msamaria. Lakini kama wangesubiri kutuatilia Kwa ukaribu mawazo Yao yangebadilika, na wasingekuwa wapumbavu kama tunavyowasoma kwenye biblia.

Hata wakati alipokuwa anazungumza nao, hawakutaka kusikiliza mpaka mwisho ni Nini Bwana anataka kuwaambia, kwamfano Kuna wakati aliwaambia, mtu akilishika Neno lake hataonja mauti milele. Lakini wao Hawakutaka ufafanuzi alimaanisha Nini.. hapo hapo wakarukia na kumwita ana Pepo;Kwa kauli Ile.

Yohana 8:52-53

[52]Basi Wayahudi wakamwambia, Sasa tumeng’amua ya kuwa una pepo. Ibrahimu amekufa, na manabii wamekufa; nawe wasema, Mtu akilishika neno langu, hataonja mauti milele.

[53]Wewe u mkuu kuliko baba yetu Ibrahimu, ambaye amekufa? Nao manabii wamekufa. Wajifanya u nani?

Wakati mwingine aliwaambia livunjeni hili hekalu,nami nitalisimamisha baada ya siku tatu. Wakairukia hiyo kauli bila kusubiria maelezo  yake , ndio ikawa habari ya mji mzima Kuna mtu kasema anaweza kulijenga Kwa siku 3 hekalu lililojengwa Kwa miaka 46. Kumbe hawakujua Kristo anazungumzia habari ya mwili wake.(Yohana 2:20)

Biblia inatuasa tuwe wepesi wa kusikia, na si wa kusema; Ina faida nyingi.

Yakobo 1:19

[19]Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika;

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

HAUWEZI KURUKA MADARASA YA MUNGU!

KUOTA UPO UCHI.

FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Maana ya Mithali 19:15 ‘Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito;

Rudi nyumbani

Print this post