Title Devis

Mashonde ni nini? (Ezekieli 4:15).

Swali: Mashonde ni kitu gani kama tunavyosoma katika Ezekieli 4:15, na yamebeba ufunuo gani?

Jibu: Turejee..

Ezekieli 4:12“Nawe utakila kama mkate wa shayiri, nawe utakioka mbele ya macho yao juu ya MASHONDE YATOKAYO KATIKA MWANADAMU”.

“Mashonde” ni jina lingine la “kinyesi kikavu” aidha cha mwanadamu au mnyama.

Zamani na hata sasa katika maeneo baadhi, kinyesi kikavu kimetumika kama chanzo cha nishati, kwasababu kinawaka kwa haraka zaidi hata ya kuni, Hivyo kinaweza kutumika kama mbadala wa kuni kama kikiwa kwa wingi.

Katika maeneo ya mashariki ya kati, vinyesi vikavu vya ngamia na ng’ombe vilitumika kwa sana kama chanzo cha nishati, na nyakati chache chache sana (hususani vipindi vya ukame na dhiki), na vilitumika hata vya wanadamu lakini vyote vilikuwa ni vikavu….lakini sasa vinatumika hata vibichi kutokana na kukuwa kwa teknolojia.

Sasa tukirejea katika biblia, tunasoma Nabii Ezekieli akipewa maagizo na Mungu kuwa aoke mkate aina ya shayiri juu ya Mashonde (yaani kinyesi) cha mwanadamu, maana yake atumie kinyesi cha mwanadamu kama chanzo cha nishati, badala ya cha Wanyama. Sasa changamoto ya kutumia vinyesi, aidha vya mwanadamu au mnyama kama nishati ni “harufu”.

Maana yake kile kitakachopikwa juu ya mashonde (kinyesi) fulani kitabeba harufu ya kile kinyesi husika, kwahiyo kama mkate utaokwa juu ya kinyesi cha ngamia, basi ule mkate kwa sehemu utatoa harufu ya kinyesi cha ngamia, vile vile kama umeokwa juu ya kinyesi cha mwanadamu basi utatoa harufu ya kinyesi cha mwanadamu.

Hivyo Mungu alimwambia Ezekieli atumie kinyesi cha Mtu, kutengeneza huo mkate na kisha aule!.. Lengo la kumwambia vile si kumwadhibu Ezekieli, la! Kwani Ezekieli alikuwa ni nabii wa Mungu mwaminifu sana, hivyo aliambiwa afanye vile ili awe ishara kwa Taifa la Israeli kama Hosea alivyokuwa ishara kwa Taifa la Israeli alipoambia akaoe mwanamke wa uzinzi.

Maana yake kwa Ezekieli kula mkate uliookwa juu ya kinyesi cha mtu, ni ujumbe kwa wana wa Israeli kuwa na wao watakwenda utumwani mahali pa dhiki nyingi, na watapitia shida na njaa kali hata kufikia hatua ya kukosa chanzo bora cha nishati na hivyo kuona hata kinyesi chao wenyewe chaweza kufaa kwa nishati ya kuokea mikate ili tu waweze kuzishibisha nafsi zao wasife kwa njaa.

Hivyo Bwana Mungu alimchagulia Ezekieli hiyo ishara, lakini tunasoma Ezekieli alimsihi Bwana ambadilishie hiyo ishara kwani hakuwahi kula kitu najisi tangu amezaliwa, (kwasababu kulingana na desturi za kiyahudi kitu chochote kilichookwa juu ya kinyesi ni najisi), Hivyo akamsikia kwa ombi hilo, na Bwana Mungu akambadilishia, badala ya kutumia kinyesi cha mtu, basi atumie cha Ng’ombe, na ndivyo Ezekieli alivyofanya kama tunavyosoma…

Ezekieli 4:13 “Bwana akasema, Hivyo ndivyo wana wa Israeli watakavyokula chakula chao, hali kimetiwa unajisi, kati ya mataifa nitakakowafukuza

14 Ndipo nikasema, Ee Bwana MUNGU, tazama, roho yangu haikutiwa unajisi; maana tangu ujana wangu hata sasa sijala nyamafu, wala iliyoraruliwa na hayawani; wala nyama ichukizayo haikuingia kinywani mwangu.

15 Ndipo akaniambia, Tazama, NIMEKUPA MASHONDE YA NG’OMBE badala ya mashonde ya mwanadamu, nawe utakipika chakula chako juu ya hayo.

16 Tena akaniambia, Mwanadamu, tazama, nitalivunja tegemeo la chakula katika Yerusalemu; nao watakula mkate kwa kuupima, na kwa kuutunza sana; nao watakunywa maji kwa kuyapima, na kwa kushangaa;

17 wapate kupungukiwa na mkate na maji, na kustaajabiana, na kukonda kwa sababu ya uovu wao”.

Ni nini tunajifunza katika Habari hiyo?

Kikubwa tunachoweza kujifunza ni kuwa “tunapomwacha Mungu na kufuata mambo yetu, tunajiweka katika hatari ya kuharibu Maisha yetu kuanzia ya rohoni mpaka ya mwilini”.  Wana wa Israeli hapa walimwacha Mungu na matokeo yake Maisha yao yaliharibika kwa njaa na umasikini na utumwa mpaka kufikia hatua ya kula mikate iliyookwa juu ya vinyesi vyao wenyewe, na ni hivyo hivyo hata leo, (kwasababu Mungu ni yule yule hajabadilika)… kama tukigeuka na kufuata mambo yetu, basi Maisha yetu yataharibika hata zaidi ya hayo ya wana wa Israeli nyakati hizo.

Je umempokea YESU KRISTO, kama Bwana na Mwokozi wa Maisha yako?

Bwana atusaidie.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

EZEKIELI, ITABIRIE MIFUPA MIKAVU.

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

Roho Mtakatifu ni nani?.

Kuna tofauti gani kati ya  “Edeni” na “Adeni”?

Bawa la mbuni hufurahi; Lakini mabawa yake na manyoya yake, je! Yana huruma? 

Rudi nyumbani

Print this post

Bwana alimaanisha nini kusema “atazamaye mwanamke kwa kumtamani” amezini naye?

Je! Kutamani kwa namna yoyote hakufai?

Mathayo 5:27  Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini; 28  lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.

JIBU: Ukitafakari hapo utaona mazingira Bwana anayoyazungumzia hapo ni ya uzinzi. Uzinzi ni kitendo cha kutoka nje ya mpango wa ki-ndoa katika eneo la kukutanika kimwili. ambao chanzo chake ni tamaa.

Sasa Bwana anaweka wazi kuwa uzinzi huanzia ndani kwenye mawazo ya mtu, moyoni mwake, tofauti na vile inavyodhaniwa kuwa mpaka wakutane dhahiri.

Lakini swali linaloulizwa je! Hatupaswi kutamani kabisa? Na kama tukitamani tutakuwa tunafanya kosa.

Kila kitu Mungu amekiweka katika utaratibu wake. Ni sawa na kusema kwanini ulafi ni dhambi, wakati Mungu ametuwekea ndani yetu hamu ya kula. Au kwanini nisile udongo wakati, najisikia hamu ya kuula mimi kama mjamzito, Au kwanini nisinywe pombe wakati ninajiona kabisa nina kiu nayo?. Kama Mungu angekuwa hapendi kwanini ameniwekea kiu hiyo?

Lakini unajua kabisa ukizidisha kula kuna madhara mwilini, pia ukila/ukinywa kitu kisichopasa utajisababishia madhara mwenyewe.

Vivyo hivyo katika tamaa. Haijawekwa, iwe ni “kutamani-tamani”, kila kitu kinachokatiza mbele. Bali Mungu aliiumba hiyo mahususi kwa wanandoa. Hivyo ikiwa upo humo huna budi kuzielekeza kwa mkeo/mumeo tu, na kama bado hujaingia humo, unapaswa uweze kuzitawala. Na hiyo inawezekana kabisa, usipozitengenezea mazingira, haziwezi kuamka na kukusumbua. Kwasababu maandiko yanasema moto hufa kwa kukosa kuni.

Ufanyeje.

Ni kujiepusha na mazingira yote, yatakayoweza kukupelekea kulipuka tamaa. Kwamfano, mazungumzo-zungumzo yasiyokuwa na maana na mtu wa jinsia nyingine, (kuchati), na kutazama video au picha zenye maudhui ya kizinzi, kuzungumza-zungumza habari hizo na marafiki zako, kuwa katika mazingira yasiyo ya kujishughulisha, kwamfano upo tu huna kazi yoyote umekaa, ni rahisi kupelekwa kwenye mawazo hayo na adui. Lakini pia kuwa msomaji wa Neno na mwombaji. Vitakusaidia sana kuwa mtu asiyetawaliwa na tamaa.

Na hivyo hata adui akitaka kukupeleka kwenye hali ya kutamani, kujengea picha, kutafakari,  basi unaweza kuyakataa hayo mawazo haraka, na ukaendelea kuwa salama, bila ya kuzini moyoni mwako. Kwasababu umevidhibiti.

Pia kumbuka jambo hili, si la wanaume tu, bali kwa jinsia zote. Hatupaswi kuishi maisha ya tamaa.

Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO

Nini Tofauti kati ya uzinzi na uasherati ?

WAANDAA MEZA MBELE YANGU, MACHONI PA WATESI WANGU

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Yesu alipopaa juu aliteka mateka, Kauli hiyo ina maana gani?

SWALI: Ni mateka yapi hayo aliyoyateka..na ni vipawa gani alivyowapa wanadamu.?

Waefeso 4:8 Hivyo husema, Alipopaa juu aliteka mateka, Akawapa wanadamu vipawa. 


JIBU: Ufalme wa Mbinguni umefananishwa na ngome Fulani, yenye hazina kubwa sana ambayo hupiganiwa na watu wengi kumilikiwa.

Na Ndio maana Bwana Yesu aliyasema maneno haya; 

Mathayo 11:12 Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka. 

Umeona unafananishwa na kitu cha kutekwa, sio kitu cha kuombwa, au kubembelezwa Fulani. Inahitaji kupambania.

Hivyo Kwa  maneno hayo utaelewa kuwa hata Bwana wetu Yesu Kristo, alikuwa katika operesheni hiyo ya kuuteka huo ufalme.

Na hiyo ilikuja kutimia siku ile aliposhinda pale Kalvari Kwa kifo chake na kufufuka katika wafu aliweza kumiliki vyote vya mbinguni na vya duniani…vyote viliwekwa chini yake.

Waefeso 1:20-23 aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho;  [21]juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia;  [22]akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo  [23]ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote. 

Sasa kwasababu ameteka Kila kitu cha mbinguni, aliteka pia na ‘uweza wote wa kiungu’ na kutupa sisi wanadamu, ndio vipawa au karama za Roho Mtakatifu, alizozitoa Kwa lengo la kuujenga mwili wa Kristo, kuhubiri injili, na kuhudumu.

Ndio hapo akawafanya wengine kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine wainjilisti, wengine, wachungaji na wengine waalimu.(Waefeso 4:11)

Pamoja na karama zile 9, tunazozisoma katika 1Wakorintho 12.

1 Wakorintho 12:8 Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo Roho yeye yule; [9]mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama za kuponya katika Roho yule mmoja;  [10]na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii; na mwingine kupambanua roho; mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha;  [11]lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye. 

Mambo ambayo hayakuwahi kuonekana zamani, hata za manabii..lakini Sasa twaziona zikidhihirika katika kanisa la Kristo.

Hivyo kumbuka Yesu hajateka mateka tu mbinguni. ni mpaka duniani. Maana yake ni kuwa sisi tuliomwamini hatuna budi pia kuwa watekaji. Hivyo popote pale uendapo kuhubiri injili, usiogope Wala usiwe mnyonge, vamia, hubiri Kwa ujasiri na hakika watu watabadilika kwasababu nguvu hizo tumepewa katika Kristo Yesu

2 Wakorintho 10:4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)  tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo; 

Bwana akubariki

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Wakaldayo ni watu gani?

TUNA JUKUMU LA KWENDA KUTEKA MATEKA.

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

TABIA ZA NJIA YA MUNGU KWA MKRISTO

MBINGUNI YUPO NANI SASA?

Rudi nyumbani

Print this post

Makonde ni nini? (Marko 14:65)

Swali: Yale Makonde Bwana Yesu aliyopigwa yalikuwaje?.

Jibu: Turejee..

Marko 14:65 “Wengine wakaanza kumtemea mate, wakamfunika uso, na KUMPIGA MAKONDE, na kumwambia, tabiri. Hata watumishi nao wakampiga makofi”.

“Makonde” ni kiswahili kingine cha “Ngumi”. Je umewahi kuwaza kuwa Bwana wetu YESU aliwahi kupigwa ngumi?.

Ndio!..Alipigwa mijeledi (Yohana 19:1) na alitemewa mate (Marko 15:19) lakini pia alipigwa ngumi nyingi na wale askari kwaajili ya makosa yetu sisi..

Mapigo Bwana Yesu aliyoyapata kabla na baada ya kupandishwa msalabani yalimbasilisha kabisa mwonekano wa uso wake na mwili wake wote kwa ujumla, na kumfanya kuwa mtu aiyeharibika uso na mwili kuliko watu wote waliowahi kutokea duniani.

Isaya 52:13 “Tazama, mtumishi wangu atatenda kwa busara, atatukuzwa, na kuinuliwa juu, naye atakuwa juu sana.

14 Kama vile wengi walivyokustaajabia, (USO WAKE ULIKUWA UMEHARIBIWA SANA ZAIDI YA MTU YE YOTE, NA UMBO LAKE ZAIDI YA WANADAMU)”.

Umeona?..Mapigo aliyoyapata Bwana Yesu ni zaidi ya yanayoigizwa katika Filamu.. ya kwenye filamu yamepunguzwa makali sana, na pia ni agenda ya shetani kuurahisisha msalaba na kuwaaminisha wanadamu kuwa jambo lililomtokea Bwana lilikuwa la kawaida tu na si zito sana.

Shetani hataki tujue kuwa tumeokolewa kwa thamani na gharama kubwa sawasawa na 1Wakorintho 6:20, Lengo lake ni ili tusijikane nafsi wala tusiuthamini msalaba.

Lakini kama tukijua kwa uhalisia gharama Bwana Yesu alizoingia pale msalabani kwaajili ya dhambi zetu, tutalia kwa machozi na hatutabaki kama tulivyo zoea kufanya mchezo na dhambi.
Madhara ya kudharau kazi ya msalaba ni makubwa kuliko kitu kingine chochote.

Waebrania 10:29 “Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?”

Ikiwa bado hujaokoka, ni vyema ukafanya hivyo leo!.. Na si kwasababu tu ya kuepuka hukumu, bali kasababu ya kupata uzima wa milele.

Utajisikiaje ukiukosa uzima wa milele, hata kama tu ziwa la moto lisingekuwepo???..huoni ni hasara kubwa kufutwa kabisa kwenye kumbukumbu zakichwa cha Mungu milele??.
Ni heri ukampokea Kristo leo!.

Ikiwa utahitaji kufanya hivyo basi waweza kuwasliana nasi inbox tutakusaidia.

Bwana akubariki

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Ni kweli hakuna mtu aliyewahi kuuona uso wa Mungu Zaidi ya Bwana Yesu?

Kuna tofauti gani kati ya uso wa Bwana na macho ya Bwana?

Biblia inaposema Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, Inamaana gani?

MBINGUNI YUPO NANI SASA?

Je! dhambi zote ni sawa Kuna dhambi kubwa na ndogo?

Rudi nyumbani

Print this post

TENGENEZA MAMBO YA NYUMBA YAKO.

Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu katika mafundisho ya Neno la Mungu.

Ni vema tukafahamu tarajio la Mungu kwa kila mwanadamu ni lipi kabla ya kumaliza mwendo wake hapa duniani. Utaona kipindi kile kabla mfalme Hezekia hajafa, Neno la Mungu lilimjia kwa kinywa cha Nabii Isaya na kumwambia, atengeneze mambo yake, kwasababu kifo chake kimekaribia.

Isaya 38:1 Siku hizo Hezekia aliugua, akawa katika hatari ya kufa; na Isaya nabii, mwana wa Amozi, akaenda kwa mfalme, akamwambia, Bwana asema hivi, Tengeneza mambo ya nyumba yako; maana utakufa, wala hutapona

Kwanini Mungu hakumwambia, “pumzika sasa usihangaike-hangaike” kwasababu kipindi si kirefu utaenda kufa? Lakini anamwambia “TENGENEZA”, mambo yako.

Mungu alijua kabisa  nyenzo pekee ya kuwa salama kule ng’ambo ya pili ni kutengeneza sasa mambo yako angali unaishi.

Inasikitisha kuona, watu wengi, wanaishi tu hohe-hahe, wakihubiriwa habari za wokovu, wanakuwa wepesi kusema, ‘siku moja nitaokoka!’ . Wakidhani kuwa mbinguni ni kuingia kama vile mtu aingiavyo kwenye basi/daladala, ambapo siku hiyo hiyo atakata tiketi, na siku hiyo hiyo utasafiri.

Mbingu ina maandalizi. Na maandalizi yake ni hapa duniani, ukiyakamilisha hayo utaonekana umestahili kuingia mule. Bwana anatazamia si tu Uokoke, halafu basi.  anatazamia pia Uache Urithi wa rohoni kwa vizazi vingine, huko ndiko kutengeneza mambo ya nyumbani mwako.  Kama vile tu mtu mwenye busara ambaye anajua anapokaribia kufa ni sharti aache urithi kwa watoto wake. Lakini kama hana urithi atawaachia nini?.

Lazima ujue umewekwa na Mungu pia umzalie matunda. Kwahiyo usiwe na amani kuondoka duniani, kienyeji-enyeji tu, anza kutengeneza wokovu wako leo, uwe na faida kwenye ufalme wa mbinguni. Hata utakapofika kule Bwana aone, ile talanta aliyokupa walau imeongeza jambo Fulani katika ufalme wa Mungu duniani.

Mathayo 25:20  Akaja yule aliyepokea talanta tano, akaleta talanta nyingine tano, akisema, Bwana, uliweka kwangu talanta tano; tazama, talanta nyingine tano nilizopata faida. 21  Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako. 22  Akaja na yule aliyepokea talanta mbili, akasema, Bwana, uliweka kwangu talanta mbili; tazama, talanta nyingine mbili nilizopata faida. 23  Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako. 24  Akaja na yule aliyepokea talanta moja, akasema, Bwana, nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda, wakusanya usipotawanya; 25  basi nikaogopa, nikaenda nikaificha talanta yako katika ardhi; tazama, unayo iliyo yako. 26  Bwana wake akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya; 27  basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo yangu na faida yake. 28  Basi, mnyang’anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi. 29  Kwa maana kila mwenye kitu atapewa, na kuongezewa tele; lakini asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang’anywa. 30  Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno

Je! Mali zako, vitu ulivyo navyo, elimu yako, ujuzi wako, karama yako, vina sehemu gani katika kuundeleza ufalme wa Mungu?.  Kama mtu uliyeokoka Je! Moyo wako kimaombi upo wapi?, Usomaji wako wa Neno umeufichia wapi?. Ukuaji wako wa kiroho umekwama wapi. Tusijione salama katika hayo mazingira na angali muda unakwenda. Ipo hatari, tusipoyatengeneza maisha yetu ya kiroho. Upo wa kusimama mbele ya kiti cha enzi cha hukumu, ambapo kila mmoja atatoa hesabu ya mambo yake mwenyewe.

Hivyo huu ni wakati wetu kila mmoja kujitathimini ndani, kwasababu hapa duniani ni wapitaji tu, hatuna maisha marefu, hujui ni lini utaondoka, au Bwana atarudi lini. Tufahamu tu huko tuendako kama hatujajitengeneza vema sasa, kuingia haiwezekani.

Bwana atupigishe hatua.

Shalom.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Mithali 24:17 inamaana gani kusema Tengeneza kazi yako huko nje?

ANGALIA JINSI USIKIAVYO:

TENGENEZA  NYAVU ZAKO, OSHA NYAVU ZAKO.

BASI NIKAOGOPA, NIKAENDA NIKAIFICHA TALANTA YAKO.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 14 (Yoeli, na Obadia).

Rudi nyumbani

Print this post

Yesu anapoitwa mwana wa Azali, maana yake nini?

Azali ni neno linalomaanisha milele, isiyokuwa na mwanzo, wala mwisho.

Hivyo, watu wanaposema Yesu mwana wa Azali wa Mungu, wanamaanisha Yesu mwana Mungu asiyekuwa na mwanzo.

Neno hili utalisikia sana katika, ukiri wa Imani ya Nikea, (kwa makanisa ya kiprotestanti), Imani ya Nikea imetokana na baraza la maaskofu wa kidini waliokaa chini mwaka 325, ili kuunda kanuni moja mama ya imani, ambayo watatembea nayo wakristo wote duniani.

Na huu ndio ukiri wenyewe unavyosema;

“Twamwamini Mungu mmoja, Baba Mwenyezi, Muumba mbingu na nchi na vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana. Twamwamini Bwana mmoja, Yesu Kristo, Mwana wa pekee wa Mungu, Mwana wa Azali wa Baba: yu Mungu kutoka Mungu, yu Nuru kutoka Nuru, yu Mungu kweli kutoka Mungu kweli; Mwana wa Azali asiyeumbwa, mwenye uungu mmoja na Baba: Kwa Yeye huyu vitu vyote viliumbwa. Aliyeshuka kutoka mbinguni kwa ajili yetu wanadamu na kwa wokovu wetu;  akatwaa mwili kwa uweza wa Roho Mtakatifu katika Bikira Mariamu, akawa mwanadamu: Akasulibiwa kwaajili yetu zamani za Pontio Pilato; aliteswa, akafa, akazikwa. Siku ya tatu akafufuka kama yanenavyo Maandiko Matakatifu: Akapaa mbinguni; ameketi mkono wa kuume wa Baba: Naye atakuja tena kwa utukufu kuwahukumu walio hai na wafu. Na ufalme wake hauna mwisho; Twamwamini Roho Mtakatifu Bwana mtoa uzima, atokaye katika Baba na Mwana, anayeabudiwa na kutukuzwa pamoja na Baba na Mwana, aliyenena kwa vinywa vya manabii; Twaamini Kanisa moja, takatifu, la Kikristo la ulimwengu wote na la kimitume. Twakiri ubatizo mmoja kwa ondoleo la dhambi, Twatazamia kufufuliwa kwa wafu, na uzima wa ulimwengu ujao. Amen”

Je! Ni kweli Kristo ni mwana wa Azali wa Mungu?

Jibu ni  ndio. Yeye hana mwanzo wa siku wala mwisho wa Siku. Amefananishwa na Melkizedeki kama maandiko yanavyosema (Waebrania 7:3). Yesu ndio Yehova, na ndio Elohimu katika umbile la kibinadamu. Wala hana tofauti yoyote na Mungu. Ni ofisi tu tofauti za utendaji kazi wa Mungu, lakini ni yeye Yule milele na milele. Wala si Miungu mitatu, katika umoja. Bali ni mmoja katika utendaji kazi wa aina tatu tofauti. Alikuja akakaa kwetu ili kutufundisha namna ambavyo sisi tunavyoweza kuwa wana kamili wa Mungu.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618


Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?

Huyu Azazeli ni nani tunayemsoma katika(Walawi 16:8)

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

MJUE SANA YESU KRISTO.

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

JINA LA MUNGU NI LIPI?

Rudi nyumbani

Print this post

Vyemba ni nini kama tunavyosoma katika 2Samweli 18:14

Vyemba kama lilivyotumika hapo ni mkuki.

Absalomu mwana wa Daudi alipomwasi baba yake, na kusababisha vita vikubwa katika Israeli, Tunasoma, alipokuwa vitani, akiwa amepanda mnyama wake, alipita chini  ya mti mmojawapo akanaswa, mnyama alipoendelea mbele yeye akabaki ananing’inia pale pale, pasipo mafanikio yoyote ya kujinasua, baadhi ya askari wa Daudi walipomwona waliogopa kumuua, kufuatana na kiapo cha Daudi alichowaagiza wasimuue. Lakini jemedari wa mfalme aliyeitwa Yoabu yeye alikaidi amri, na kwenda kumwua kumpiga hivyo vyemba vitatu, moyoni. Kisha akamaliziwa na wasaidizi wake.

2Samweli 18:14 Ndipo Yoabu akasema, Siwezi kungoja na kusema nawe hivi. Akachukua vyemba vitatu mkononi mwake, akamchoma Absalomu moyoni, alipokuwa akali hai katikati ya ule mwaloni.  15 Kisha vijana kumi, waliomchukulia Yoabu silaha zake wakamzunguka, wakampiga Absalomu, na kumwua

Hivyo Yoabu alimchoma mikuki mitatu Absalomu kifuani mwake.

Lakini katika habari hii tunajifunza nini?

Upendo wa Daudi kwa mwanae ni sawa na Upendo wa Mungu kwetu sisi. Ijapokuwa Absalomu alimuudhi sana baba yake mpaka kumvunjia heshima ya kulala na wake zake, na kuuasi ufalme wake mtukufu, Daudi bado moyo wake ulikuwa kwa Absalomu kutaka atubu. Lakini Absalomu mwenyewe hakutaka, na hivyo alikutana na majeshi yakamwangamiza kwa tabia zake za uasi ulioendelea.  Laiti angekuwa mtoto mtii, asingekufa kwasababu baba yake angeweza kumlinda.

Tunapomwasi Mungu, tunajitenga na rehema zetu wenyewe, Kama vile Yona alivyosema katika (Yona 2:8),. Kamwe usimwasi Mungu ndugu, tembea katika njia zake, kwasababu hakika huko unapokimbilia kifo kipo. Na utakapovamiwa na adui yako ibilisi Mungu hataweza kukutetea kwa lolote. Utakufa na kuangamia milele kwa vyemba hivyo rohoni.

Nje ya Kristo hakuna usalama. Mrudie Mungu wako, kwa kumfuata Bwana Yesu, Tubu dhambi zako leo, ubatizwe, upokee ondoleo la dhambi zako. Uishi maisha ya neema siku zote ndani ya pendo lake. Acha uasi, neema haitadumu kwako daima kukulinda katika hiyo mitego adui anayokutegea kila siku akuue.

Je ungependa kuupokea wokovu leo? Kwa Yesu kuwa mwokozi wako na mtetezi? Kama ni ndio basi fungua hapa kwa mwongozo huo wa Sala ya Toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki. Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

ANGALIA UZURI WAKO, USIGEUKE KUWA KITANZI CHAKO.

UVUMILIVU NA MIKAKATI YA ABSALOMU, INA FUNZO NYUMA YAKE.

MJUMBE ASIYEKUWA NA UJUMBE.

NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?

Je idadi ya askari waliohesabiwa katika 1Nyakati 21:5 na 2Samweli 24:9 inajichanganya?.

Rudi nyumbani

Print this post

SI KILA KILICHO HALALI KINAFAA.

(Jihadhari na Marashi)

Si mambo yote yanayokubalika katika jamii basi yanafaa kwa mkristo.. Si mambo yote yanayokubaliwa na wengi basi yanafaa..ni muhimu kuchuja kila tunaloambiwa au tunayokutana nalo, kabla ya kulikubali, ndivyo biblia inavyotufundisha.

1Wakorintho 10:23  “Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo”.

Mojawapo ya jambo ambalo ni muhimu kuchukua nalo tahadhari ni “Matumizi makali ya marashi”. Unapojipulizia marashi ambayo mtu aliye mita 10 mbali nawe anayasikia, basi fahamu kuwa upo katika hatari kubwa sana.

Utauliza kivipi au kwa namna gani? Hebu turejee katika maandiko kidogo..

Utakumbuka ile habari ya yule mwanamke aliyemmiminia Bwana marhamu ya thamani nyingi mwilini mwake, na maneno Bwana Yesu aliyoyasema kuhusu kazi ya ile marhamu aliyomiminiwa?. Biblia inasema marhamu ile ilikuwa ni ya thamani kubwa, maana yake yenye kunukia sana na kwa eneo kubwa, kiasi kwamba mtu aliye mbali anaweza kuisikia harufu ya marhamu ile.

Tusome

Marko 14:3 “Naye alipokuwapo Bethania, nyumbani mwa Simoni mkoma, ameketi chakulani, alikuja mwanamke mwenye KIBWETA CHA MARHAMU YA NARDO SAFI YA THAMANI NYINGI; akakivunja kibweta akaimimina kichwani pake.

4  Palikuwa na watu waliochukizwa katika nafsi zao wakisema, Kwani kupoteza marhamu namna hii?

5  Maana marhamu hii ingaliweza kuuzwa kwa dinari mia tatu na kuzidi, wakapewa maskini. Wakamnung’unikia sana yule mwanamke.

6  Yesu akasema, Mwacheni; mbona mnamtaabisha? Amenitendea kazi njema;

7  maana sikuzote mnao maskini pamoja nanyi, na kila mpendapo mwaweza kuwatendea mema; lakini mimi hamnami sikuzote.

8  Ametenda alivyoweza; ametangulia kuupaka mwili wangu MARHAMU KWA AJILI YA MAZIKO”.

Umeona hapo?.. wakati huyu mwanamke anadhani Marhamu ile ingeweza kumfanya Bwana anukie vizuri mbele za watu na aonekane mtanashati.. lakini Bwana aliyaona yale manukato tofauti na mwanamke alivyoyaona, Bwana Yesu aliona hayafai kwa utanashati, bali kwa MAZIKO!.

Lakini kwasababu mwanamke alikuwa na nia njema ya kutubu na kumthaminisha Bwana ndio maana akapata kibali kwa muda ule, lakini Ujumbe tayari tumeachiwa, “kuwa marhamu kama hizo ni kwaajili ya maziko” so kwaajili ya utanashati.

Hiyo ikimaanisha kuwa kumbe kuna vitu tunaweza kuvipaka mwilini, au kuvivaa, na kumbe ni malighafi za MAUTI, Na KIFO!!. Ijapokuwa kwa nje tunaweza kuonekana watanashati na tunaovutia, lakini kumbe tumejipaka au tumekivaa kifo!.

Bwana Yesu angeweza kuwaambia wale watu kuwa marhamu ile amepakwa kwa kuwekwa tayari kukutana na mkutano ili kwamba wasikie harufu nzuri itokayo mwilini mwake, kwani bado alikuwa na siku kadhaa za kuhubiri mbele za watu kabla ya kufa, lakini wala yeye hakuziona hizo siku bali aliona marhamu ile inafaa kwa matumizi ya MAZIKO! Na si utanashati kama wengine wote walivyotazamia.

Mama/dada jiulize hayo marashi unayojipulizia mwilini mwako je unajiweka tayari kwa nini?..je kwaajili ya maziko yako??..

Na asilimia kubwa ya watu wanaotumia marashi makali ni lazima wanakuwa wanasumbuliwa na roho za mauti au uasherati… hivyo ni muhimu kuchukua tahadhari ya kiroho! Na si kila kitu kuiga kwasababu tu, tumeona ni kitu chenye kukubalika kila mahali.

Mama/dada Kama unatamani kujipamba basi jipambe kwa mapambo ya kibiblia, ambayo ndiyo yale yanayotajwa katika 1Timotheo 2:9 na 1Petro 3:3.

1Petro 3:3 “Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

4  bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; YAANI, ROHO YA UPOLE NA UTULIVU, ILIYO YA THAMANI KUU MBELE ZA MUNGU.

5  Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.

6  Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada zinazoendana:

Mafundisho mengine:

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI, AU KUTOA TALAKA?

SISI TU MANUKATO YA KRISTO.

Mawaa ni nini? Kama tunavyosoma katika biblia?

EPUKA KUCHELEWA IBADA.

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI YA KUISHINDA HALI YA MSONGO WA MAWAZO.

Msongo wa mawazo ni nini? Ni shinikizo au mfadhaiko wa kiakili, unaomkumba mwanadamu, pale anapokutana  na  matatizo, au taabu, au dhiki au shida Fulani. Hivyo inapotokea mtu huyu anashindwa kuzitatua changamoto hizo, ndipo msongo huo huja.

Kwamfano labda mtu amegundulika, ana ugonjwa usiotubika, na kaambiwa na daktari hawezi kupona, mtu kama huyu ni rahisi kukumbwa na msongo wa mawazo,

Au labda mwingine  hana kazi na akiangalia familia inamtegemea, na bado hajafikia malengo yake kulinganisha na umri alionao, moja kwa moja mtu kama huyu ni rahisi kukumbwa pia na msongo wa mawazo. N.k.

Na kama tiba isipopatikana matokeo yake yanaweza kuwa mtu huyo, kupata matatizo ya kiafya, wengine kuchanganyikiwa, wengine kujitenga na watu, wengine kujifungia ndani kulia tu usiku kucha, wengine kutenda vitendo viovu,hata kujiua.

Je! Mkristo anaweza kuwa na msongo wa kimawazo? Jibu ni ndio anaweza kuwa nao. Lakini tiba imeshatolewa. Tutaona katika somo hili kwa namna gani, kwasababu yawezekana wewe ni mmoja wapo ambaye unakutana na hali hii na hujui cha kufanya.

Embu tuone kwanza baadhi ya watu katika maandiko ambao walipitia misongo ya mawazo

1) Eliya:

Eliya wakati amemaliza kuwaua manabii wa Baali, akatazama huku na huku na kujiona kama ni yeye peke yake ndiye nabii wa Mungu aliyebaki, hivyo ikampelekea ajitenge, na kukimbilia jangwani, akae huko mpaka afe.  Lakini Mungu alikuja kumtokea baada ya siku 40, akampa majibu ya faraja, kwamba asidhani yupo peke yake kuna wengine 7,000 amejisazia, rudi Israeli, kanitumikie.(1Wafalme 18-19)

2) Mfalme Daudi.

Alikumbwa mara nyingi na msongo wa mawazo katika maficho yake alipokuwa anawindwa na mfalme Sauli. Mara nyingi alifikia hatua ya kukata tamaa ya maisha. Embu tafakari haya maneno aliyoyasema Daudi.

Zaburi 69:1 Ee Mungu, uniokoe, Maana maji yamefika mpaka nafsini mwangu.  2 Ninazama katika matope mengi, Pasipowezekana kusimama. Nimefika penye maji ya vilindi, Mkondo wa maji unanigharikisha.  3 Nimechoka kwa kulia kwangu, Koo yangu imekauka. Macho yangu yamedhoofu Kwa kumngoja Mungu wangu.  4 Wanaonichukia bure ni wengi Kuliko nywele za kichwa changu. Watakao kunikatilia mbali wamekuwa hodari, Adui zangu kwa sababu isiyo kweli. Hata mimi nalilipishwa kwa nguvu Vitu nisivyovichukua.  5 Ee Mungu, unajua upumbavu wangu, Wala hukufichwa dhambi yangu

3) Ayubu

Baada ya kupotelewa na mali zake, na watoto wake, hadi mwili wake kubaki mifupa tu. Mkandamizo ulimjia. Ayubu anasema;

Ayubu6:2 Laiti uchungu wangu ungepimwa, Na msiba wangu kutiwa katika mizani pamoja!  3 Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa bahari; Kwa hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka

 Mpaka akanza kusema maneno magumu, ya kulaana siku aliyozaliwa. Mtu kama huyu alikuwa katika hali mbaya sana kifikra na kiakili.

4) Petro

Petro na Yuda walipitia jambo moja, kukana na kusaliti, ni dhambi pacha. Isipokuwa Yuda alikwenda kujinyonga kwasababu msongo wa mawazo ulimshinda, lakini Petro hakujinyonga. Yeye alikwenda kujificha na kulia sana kwa “majonzi”.  Tengeneza picha ni wewe unamkana Mungu wako, tena kwa maneno ya dhihaka mbele za watu. Hali hiyo unadhani itakufanya ujionaje kama sio mateso ya kiakili baada ya hapo?. Wengine wanapitia hali kama hizi, wanapojiona wamemtenda Mungu dhambi kubwa sana, isiyosameheka, wakidhani kuwa Mungu hawajali tena, hawathamini.(Mathayo 26:75)

5) Mitume 11.

Baada ya Bwana Yesu kufa, hofu ya wayahudi ikawavaa mitume, wakiona kuwa wao ndio wanaofuata kuuliwa baada ya kiongozi wao kufa.. Hivyo hiyo ikawapelekea kujifungia ndani, wasitoke. Msongo mkubwa sana wa mawazo uliwavaa, kutoka kwa wayahudi.(Yohana 20:19-29)

Itoshe tu kutumia mifano hiyo michache, kwani wapo wengine wengi sana katika biblia waliopitia hali kama hizi, mfano ni Musa, Yusufu, Yeremia, Nebukadreza, Hana(mamaye Samweli),  Danieli, Mtume Paulo wote hawa ukisoma habari zao katika biblia utayathibitisha hayo.

Lakini Je! Waliwezaje kuzishinda hizo hali.

Utagundua, walipopotia taabu zao, walilikumbuka TUMANI la Mungu. Ndilo lililowapa nguvu ya kuweza kuvuka nyakati hizo mbaya walizozipitia.  Waliyazingatia haya maneno;

1Petro 5:6  Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake; 7  HUKU MKIMTWIKA YEYE FADHAA ZENU ZOTE, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.

Na lile alolilisema Yesu..

Mathayo 11:28  Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha

Pale akili zilipogoma, fikra kuzima, moyo kuwa baridi, walijifunza kumtwika Mungu, huzuni zao, mateso yao, shida zao. Hata pale ambapo hazikutatulika kwa wakati walioutarajia, lakini waliendelea na mwisho wa siku Bwana alikuja kuyaweka yote sawa. Kwasababu yeye mwenyewe alisema.

Yeremia 29:11 Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi TUMAINI siku zenu za mwisho

Hivyo ndugu, ikiwa na wewe upo katika hali hii ya msongo wa kimawazo, katika eneo lolote lile, iwe la kiroho, kihuduma, kifamilia, kikazi, kiafya, kimaendeleo. Umeshindwa kuendelea mbele, Usiogope. Kwa Mungu lipo TUMAINI, zaidi ya Matumaini yote ya kibinadamu.

Haijalishi msongo huo, umekupata kutokana na dhambi zako, au kutokana na hali zilizo nje ya uwezo wako. Usiogope. Mponyaji, mfajiri, mtatuaji wa matatizo yupo. Huyu si mwingine zaidi ya YESU KRISTO mwokozi.

Mungu akikupa tumaini, ujue ni lazima litokee, lakini mwanadamu akikupa tumaini, ni kusudi tu kukufariji, lakini tatizo linaweza kubaki palepale.  Yesu hayupo hivyo. Mtazame tu yeye. Wakati wa shida, ndio wakati wa kukimbilia chini ya mbawa zake, sio kuwakimbilia wanadamu.

JE! UFANYEJE?

  1. Katika hali hiyo, Usiache kuomba sana  & Kumsifu Mungu & Kushukuru, siku zote za maisha yako. Ongeza kiwango chako katika eneo hili.
  2. Soma sana Biblia: Utapata faraja ya Roho katika uwezo wa Mungu aliowatendea wengine.
  3. Usiwe mtu wa kutanga-tanga sana. Tuliza akili zako, si lazima utafute ushauri kwa kila mtu, jiachie kama vile huna tatizo lolote, ukimkabidhi Bwana yote, ukijua yeye yupo kazini.
  4. Kila wakati Jiambie, “Mungu wangu atayaweka yote sawa mwisho wa siku”.
  5. Mawazo ya kushindwa/kujihukumu yanapokuja yapinge.  Sema “Bwana ndiye boma langu na ngome yangu, na mwamba wangu sitatikisika”.

Na hakika, katika muda fulani, utaona Mungu anakuvusha, anakuponya, anakufariji, anakuondolea huo mzigo. Huo ni uhakika sio makisio. Usiache tu kuendelea na Bwana..

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Mafundisho Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mafundisho mengine:

TUMAINI NI NINI?

UKIOKOKA,HIZI FIKRA ZIKIJA NDANI YAKO, ZIKATAE.

VITA VYA KIFIKRA BAADA YA KUZALIWA MARA YA PILI

TUUTAFUTE UMOJA WA ROHO.

Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?

Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Mwanamke aliyepotelewa na sarafu yake.

Huu ni mwendelezo wa Mafundisho maalumu yawahusuyo wanawake.

Mwanamke aliyepoteza shilingi moja.

Luka 15:8  Au kuna mwanamke gani mwenye shilingi kumi, akipotewa na moja, asiyewasha taa na kufagia nyumba, na kutafuta kwa bidii hata aione? 9  Na akiisha kuiona, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimeipata tena shilingi ile iliyonipotea.

Bwana Yesu alipenda kutumia mifano halisi ya kimaisha kutufundisha habari za rohoni. Kwamfano katika habari hiyo tunafahamu mfano huo ulikuwa analenga mambo ya ufalme wa mbinguni, jinsi Mungu anavyomthamini mtu wake mmoja aliyepotea katika dhambi, pindi atubupo na kurejea. Kwamba tendo  hilo linamfanya yeye pamoja na malaika zake mbinguni kufurahi sana.

Lakini leo nataka tujifunze kuhusu mfano huo katika uhalisia wake wa kimaisha kama ulivyoandikwa. Kuna maswali lazima ujiulize kwanini amtaje mwanamke na sio mwanaume. Kisha aipoteze shilingi yake pale NYUMBANI kwake, na sio sehemu nyingine, labda barabarani au sokoni? Tofauti na mfano uliotangulia ambao unamzungumzia Yule mtu aliyepotelewa na kondoo mmoja akawaacha wale 99 akaenda kumtafuta Yule mmoja huko maporini.

Na hatua ambazo alitumia kuitafuta shilingi ile hadi kuipata, kuna funzo gani pia?.

Kumbuka kimaandiko aliyekabidhiwa nyumba aisimamie ni mwanamke, ndio maana biblia inasema,

Mithali 14:1 Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.

Na hazina yake inapatikana humo, lakini pia ikipotea, basi hupotelea humo humo.

Tukisema nyumba hatumaanishi, gorofa, na sebule na jiko. Hapana, bali tunamaanisha wale waliomo mule. Hao ndio hazina yake hasaa.

Sasa katika mfano huo mwanamke huyu alikuwa na shilingi 10, labda tuseme hao ni watoto 10, au ndugu 10, lakini mmoja akapotea, huwenda akawa mtundu, au mwizi, au kibaka, au shoga, au jambazi n.k.  Lakini Mwanamke huyu hakukata tamaa na kukaa chini na kusema, Ahh! Ninao hawa 9, wenye kujitambua na wenye nidhani. Embu ngoja niachane na Yule pasua kichwa mtukutu, mwenye kiburi, asinipe presha, nifarijiwe na hawa wanangu 9 wazuri. Hapana, bali alilazimika kufanya jambo ili kuhakikisha amempata na Yule.

Hivyo kama tunavyosoma, hakukaa tu hivi hivi, na kuzungumza. Bali alichukua hatua fulani, na hatua zenyewe ndio hizi tatu.

  1. Kuwasha taa
  2. Kufagia nyumba
  3. Kuitafuta kwa bidii

Hii ikiwa na maana gani? mpaka anafikia hatua ya kuwasha tamaa, maana yake ni kuwa chumba hicho kilikuwa na giza, hivyo asingeweza kuipata shilingi yake katika mazingira yale. Tafsiri yake ni nini? Alimkaribisha Kristo. Ambaye ndio Nuru ya ulimwengu katika nyumba yake.

Hivyo hatua ya kwanza katika kutatua tatizo lake, alimtambua Kristo kwenye nyumba yake. Na sasa Nuru ilipomulika ndipo akatambua kuwa nyumba ilikuwa chafu. Kama asingewasha taa, kamwe asingeweza kugundua kuwa Vitu havipo katika mpangalio wake. Hivyo ikampasa aanze kwanza kuifagia nyumba ile, aipangilie vizuri. Makombo yaliyodondoka sakafuni ayafagie, vikombe na vijiko vilivyokaa hoe hae, aviweke mahali pake, nguo ambazo hazijakunjwa aziweke kabatini, uwazi uwepo. Hakukimbilia kuitafuta shilingi yake katika hatua hiyo. alijua hawezi kuipata katika mazingira yale, machafu, imejificha sana.

Hivyo ikamchukua muda Fulani mrefu kuisafisha nyumba yake, mpaka hatimaye, pengine baada ya saa 6, ikawa safi. Kila kitu kikawa katika mpangilio wake.

Ndipo sasa akaenda katika hatua ya mwisho ya “kuitafuta kwa bidii ile shilingi”.  Akaanza kupita eneo moja baada ya lingine, hakutoka nje ya nyumba kwenda kuitafuta barabarani, hapana bali pale pale ndani kwasababu alijua fedha zake hazijawahi kutoka nje ya nyumba.

Na hatimaye akaipata. Na mwisho wa siku akawaalika na marafiki zake, wakafurahi pamoja. Kwasababu ilimgharimu kuipata tena.

Hii ni kufunua nini?

Wanawake wengi wanapoona aidha ndugu zao nyumbani, au watoto wao, au ndoa zao zimeharibika,. Wengine wanakimbilia kwa waganga ili wasaidike, hapo umepotea, wengine wanakimbilia kwa washauri wa kijamii, bado hujapata suluhisho. Suluhisho pekee ni Nuru ya ulimwengu. Yesu Kristo, aimulikie kwanza nyumba yako.

Na Yesu anachokifanya ni kukuonyesha madhaifu uliyokuwa nayo, uchafu uliomo nyumbani mwako, ili urekebishe (ndio ufagie). Sasa wengine wanapofikia hatua hii, wanapoona wanahubiriwa waishi maisha ya utakatifu, wawe watu wa ibada majumbani mwao, wawe waombaji, wafungaji, wafukuze tabia zisiojenga majumbani  mwao, waweke mipaka Fulani kwenye familia zao. Wanaona kama wanatwikwa mzigo juu ya mzigo. Wanamkimbia Kristo, wanabakia kulia tu, na kuhuzunika..

Wanachofikiria tu, ni utatuzi wa tatizo, mume aache pombe (aokoke), watoto wawe wasikivu, nyuma iwe na amani, n.k.  lakini hawataki wao wenyewe kurekebisha baadhi ya mambo makwao. Hapo ndugu ukikwepa hatua hii, sahau kukipata unachokitafuta. Hata upewe bahari nzima ya mafuta ya upako, na pipa la chumvi. Unapoteza muda, hutatui jambo lolote.

Kristo anataka usafi kwanza, ndipo akupe jicho la kuiona shilingi yako iliyopotea. Sasa ikiwa utatimiza mambo hayo mawili yaani KRISTO ndani yako, na usafi wako. Kinachofuata ni kutafuta ulichokipoteza.

Hii ndio hatua sasa ya kumuhubiria, kumshauri, kumwonya, kumvuta kwa Bwana. Sasa ukiendelea hivyo hivyo, muda si mwingi utampata kiwepesi sana haijalishi alikuwa amepotea kiasi gani, au alikuwa sugu namna gani. Hakuna linaloweza kujificha mbele ya Nuru. Tatizo lolote sugu unalolijua wewe la kifamilia, kwa kufuata kanuni hizo litatatulika tu.

Hivyo wewe kama mwanamke, itambue huduma hii iliyopewa na Bwana, laiti kama wanawake wote, wangekuwa ni wa kujiwajibisha kwa namna hii, jamii zetu na familia zetu zisingekuwa na migogoro mingi,wala injili isingekuwa ngumu sana kuihubiri kwasababu tayari walishatangulia walioweka misingi bora nyuma. Hii ni huduma kubwa sana kwa mwanamke na Bwana anaithamini sana.

Simama katika nafasi yako wewe kama mama, wewe kama Dada, nyumba au familia itasimama, endapo wewe utasimama.

Bwana akubariki

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mafundisho mengine:

MAFUNDISHO KWA WANAWAKE

MWANAMKE ABIGAILI ANAFUNZO GANI KWA WANAWAKE?

Je mwanamke Fibi, alikuwa ni askofu wa makanisa, kama mitume?

BADO TUTAHITAJI TU KUSAIDIANA.

Je Mungu anaketi katika giza? (1Wafalme 8:12)

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

Rudi nyumbani

Print this post