SWALI: Wale wachawi walikuwa na maana gani waliposema..”Miungu wasio na kikao pamoja na wenye mwili”?.
Danieli 2:11
[11]Ni neno la ajabu, hili analolitaka mfalme, wala hapana mwingine awezaye kumwonyesha mfalme neno hilo, ila miungu, wasio na kikao pamoja na wenye mwili.
JIBU: Hiyo ni baada ya Mfalme Nebukadneza kutoa mtihani mzito wa kukumbushwa na kupewa tafsiri wa ndoto aliyoiota,..lakini tunaona wale wachawi wote walishindwa kupokea taarifa yoyote kutoka kwa miungu yao..ndipo wakakiri wazi kuwa fumbo hilo, si kila aina na mungu ilimradi mungu tu anaweza kulifichua, bali ni miungu wengine isiyofanya kikao na wanadamu.
Sasa hawa wachawi walitumia neno “miungu”..kwasababu waliamini katika miungu mingi, ndio màana utaona wanatumia neno miungu na sio Mungu asiyefanya kikao na wanadamu…lakini walimaanisha Mungu mmoja ( ambaye ni Yehova) yeye peke yake, ambaye huwa hafanyi vikao na wanadamu.
Sasa aliposema…asiyefanya vikao na wanadamu” maana yake ni kuwa asiyeishi pamoja na wanadamu..yaani Mungu ambaye makazi yake si duniani, bali ni mbinguni.
Miungu yote ya kipagani, makao yao ni hapa duniani, mizimu, mapepo, vibwengo, majini, n.k. vyote hivyo vinaishi katikati ya watu, na vinawategemea watu kutenda kazi zao..vinazurura zurura huku duniani kukusanya taarifa za matukio mbalimbali…havina kitu cha ziada zaidi ya kupeleleza peleleza, kama baba yao shetani (Ayubu 1:7)..
Haviwezi kujua mambo yajayo, haviwezi kutambua siri za ndani za mioyo ya watu..wakati mwingine hata vikitaka taarifa fulani ya mtu vitakuambia niletee kwanza unyayo, au nywele, jinsi gani vilivyo vidhaifu, havijui, wala havipo kila mahali..na ndio maana wale wachawi walitaka kwanza wasimuliwe ile ndoto..ndio walau wakisie kisie tafsiri yake..
Lakini Yehova peke yake ndiye ambaye hategemei, mwanadamu, au kiumbe chake chochote kufahamu au kutenda jambo alitakalo,
Hii ni kutuonyesha kuwa Mungu pekee(Yehova) ndio tumaini la kweli, shetani au vipepo haviwezi kueleza hatma ya mtu. Unapotazama utabiri wa nyota, ujue kuwa umedanganyika, unapokwenda kwa waganga ujue kuwa ndio umekwenda kujitafutia matatizo, unapofanya mila na kuamsha mzimu, ujue unajifungulia milango mwenyewe wa kupelekwa kuzimu.
Zaburi 115:3-9
[3]Lakini Mungu wetu yuko mbinguni, Alitakalo lote amelitenda.
[4]Sanamu zao ni fedha na dhahabu,
Kazi ya mikono ya wanadamu.
[5]Zina vinywa lakini hazisemi, Zina macho lakini hazioni,
[6]Zina masikio lakini hazisikii, Zina pua lakini hazisikii harufu,
[7]Mikono lakini hazishiki, miguu lakini haziendi, Wala hazitoi sauti kwa koo zake.
[8]Wazifanyao watafanana nazo, Kila mmoja anayezitumainia.
[9]Enyi Israeli, mtumainini BWANA; Yeye ni msaada wao na ngao yao.
Amen.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?
JE! PAKA KULIA USIKU NI ISHARA YA UCHAWI?
Kuwiwa maana yake nini katika biblia?
Wasamaria walikuwa ni watu gani?
Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia Neno la Mungu wetu…
Yakobo baada ya kuondoka kwa Labani, alipokuwa njiani maandiko yanasema alikutana na Jeshi la Malaika wa Bwana…
Mwanzo 32:1 “Yakobo akashika njia yake na malaika wa Mungu wakakutana naye.
2 Naye Yakobo alipowaona, alisema, Hili ni jeshi la Mungu. Akapaita mahali pale, MAHANAIMU”.
Maana ya Neno “Mahanaimu” ni “Kambi mbili”…Yakobo alipaita mahali pale kwa jina hilo, kwasababu kaliona jeshi la Bwana likiwa pamoja naye.. Na hivyo kufanya jumla ya majeshi Mawili; jeshi lake yeye mwenyewe (yaani yeye na watumishi wake na watu wake wote) na la Bwana (malaika watakatifu).
Baada ya kuona jeshi hilo la Mbinguni likifuatana naye, ndipo alipojua kuwa hayupo mwenyewe, hivyo nguvu mpya na hofu yote ikamwondoka, Na hofu ya kwanza ambayo ilikuwa inamsumbua kwa muda mrefu ni ile ya kukutana na ndugu yake Esau, maana alikiri kabisa mwenyewe kuwa anamwogopa ndugu yake Esau (Mwanzo 32:11).
Lakini baada ya kujua kuwa lipo Jeshi lingine kubwa la mbinguni linamzungukan na kufuatana naye, ndipo akapata ujasiri mpya na kuamua kumtafuta ndugu yake..
Mwanzo 32:1 “Yakobo akashika njia yake na malaika wa Mungu wakakutana naye.
2 Naye Yakobo alipowaona, alisema, Hili ni jeshi la Mungu. Akapaita mahali pale, Mahanaimu.
3 Basi, Yakobo akapeleka wajumbe mbele yake kwenda kwa Esau nduguye mpaka nchi ya Seiri katika nyika ya Edomu
4 Akawaagiza akisema, Mwambieni hivi bwana wangu, Esau, Hivi ndivyo asemavyo mtumwa wako, Yakobo; Nimekaa ugenini kwa Labani, na kukawia huko hata sasa,
5 nami nina ng’ombe, na punda, na kondoo, na watumwa, na vijakazi; nami nimepeleka watu nimpashe bwana wangu habari, nipate neema machoni pako.
6 Wale wajumbe wakarudi kwa Yakobo wakisema, Tulifika kwa ndugu yako, Esau, naye anakuja kukulaki, na watu mia nne pamoja naye”.
Jambo kama hilo hilo lilitokea pia kwa Elisha, kipindi Mfalme wa Shamu alipotuma majeshi kwenda kumkamata Elisha pamoja na mtumishi wake, walipoamka asubuhi Elisha na mtumishi wake waliona jeshi la Washami limezunguka lile eneo lote.. Na Yule mtumishi wa Elisha akaishiwa nguvu kwa hofu, lakini Bwana akamfumbua macho na kuona jeshi kubwa la Malaika wa mbinguni, lililo kubwa kuliko jeshi la Washami limezunguka kile kilima chote..
2Wafalme 6:15 “Hata asubuhi na mapema mtumishi wake yule mtu wa Mungu alipoondoka, na kwenda nje, kumbe! Pana jeshi la watu, na farasi na magari, wameuzingira mji ule. Mtumishi wake akamwambia, Ole wetu! Bwana wangu, tufanyeje?
16 Akamjibu, Usiogope; maana walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.
17 Elisha akaomba, akasema, Ee Bwana, nakusihi, mfumbue macho yake, apate kuona. Bwana akamfumbua macho yule mtumishi; naye akaona; na tazama, kile kilima kilikuwa kimejaa farasi na magari ya moto yaliyomzunguka Elisha pande zote”.
Jeshi hilo hilo pia limewazunguka leo watu wa Mungu(Waliompokea Yesu), wakati mwingine unaweza kuwa na hofu na kudhani Mungu hayupo na wewe, hata Yakobo alidhani hivyo, hata Mtumishi wa Elisha alidhani hivyo.. Lakini hawakujua kuwa lilikuwepo jeshi lingine kubwa la mbinguni lililofuatana nao, kuhakikisha kuwa wanafanikiwa katika njia zao.
Leo hii unaweza usifumbuliwe macho kama Mtumishi wa Elisha au kama Yakobo, lakini amini kuwa lipo jeshi lingine kubwa sana la mbinguni limekuzunguka.. hivyo usiogope siku zote kuendelea mbele, wala usiogope maadui…
Yakobo alimwogopa ndugu yake Esau kwa miaka mingi, lakini siku alipotambua kuwa Lipo jeshi la pili pamoja naye (Mahanaimu)..alisonga mbele kwa ujasiri na Bwana akampatanisha na Adui yake, Yule Yule adui yake akageuka kuwa kipenzi chake.. Vile vile yale majeshi yaliyotumwa kumkamata Elisha na Mtumishi wake, yaligeuka kuwa marafiki wa Elisha..(kwani baada ya lile tukio hayakurudi tena Israeli kwa kipindi kirefu sana 2Wafalme 6:23).
Na wewe kama umeokoka, songa mbele usikwamishwe na vitisho vya shetani, kwasababu walio upande wako ni wengi kuliko walio upande wa adui.
Bwana akubariki.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.
SINA PESA SASA, YESU ATANISAIDIA NINI?
Je Elisha alimdanganya Ben-hadadi kuwa hatakufa kwa ugonjwa wake?
SWALI: Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa? Kwani kunaendelea mabishano baina ya wakristo baadhi, wengine wanasema kwasasa huduma hizo hazitendi kazi tena kufuatana na andiko la Paulo katika
Waefeso 2:20 linalosema;
[20]Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni.
…Lakini wengine wanasema huduma hizo hadi sasa zipo katika kanisa. Je ukweli ni upi?
JIBU: Kabla hatujafahamu kwanza kama huduma za mitume na manabii zinaendelea hadi sasa au la!…tutazame kwanza aina za manabii wa mwanzo, na mitume wa mwanzo walikuwaje..
1)Manabii wa kutia msingi wa wakati wote
2)Manabii wa kuthibitisha misingi.
1 ) Hawa manabii wa kutia misingi; Ndio wote waliotiwa mafuta na Mungu kaandika biblia takatifu…mfano wa hawa ndio kama Yeremia, Isaya, Nahumu, Malaki, Yoeli, Yona, Habakuki..n.k. Kwamba nabii zao zisimame kama msingi na mwongozo wa daima wa kuliongoza kanisa la Mungu wakati wote..
2 ) Manabii wa kuthibitisha: Hawa Mungu aliwanyanyua kutoa mwongozo wa wakati fulani tu mahususi.. Walikuwa wanasema Neno la Mungu lakini la wakati fulani tu ambapo ukishapita basi, unabii huo hauna umuhimu tena kwa vizazi vijavyo.
Mfano wa hawa utawasoma wengi sana..wakina Mikaya, Aguri, Odedi, Azuri, Ahiya, pia katika agano jipya walikuwepo wakina sila, agabo..n.k
Vivyo hivyo tukirudi na katika Mitume wa Kristo.
Wapo ambao waliotiwa mafuta kwa lengo la kuweka misingi ya daima. Hawa ndio wote tunaosoma nyaraka zao katika maandiko..mfano Paulo, Petro, Yakobo, Yohana, Yuda, Mathayo, Luka.
Na wapo waliowekwa kwa ajili ya kutihibitisha / kutia misingi midogo.midogo. Mfano wa hawa ni Epafrodito Wafilipi 2:25..
Sasa tukishafahamu…hilo…tunaporudi katika lile andiko linalosema..mmejengwa juu ya misingi ya mitume na manabii tunaweza kuelewa
Tusome;
Waefeso 2:20
[20]Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni.
Maana yake ni kuwa sisi kama kanisa tumejengwa juu ya mafunuo ya manabii watangulizi na mitume watangulizi wale waliochaguliwa kuweka misingi ya daima..(Yaani kwa lugha rahisi tumejengwa juu ya BIBLIA TAKATIFU)…
Hakuna namna tutajengwa juu ya misingi mingine mipya zaidi ya hiyo yao.. Hivyo kwasasa hatuna manabii na mitume kama wale watangulizi, ambao walipokea mafunuo ya moja kwa moja ya namna ya kulijenga kanisa la Kristo..ni sawa na kusema hatuna mitume mfano wa Paulo au Petro au manabii mfano wa Yeremia au Isaya, kwasasa.
Lakini wapo mitume na manabii wa nyakati ndogo ndogo, ambao wanafanya kazi za kuthibitisha misingi ambayo tayari ipo lakini sio wa kuleta jambo jipya duniani..
Kwamfano kazi mojawapo ya mitume ilikuwa ni kwenda kupanda makanisani mapya maeneo mapya..hivyo, mtu yeyote mwenye huduma.hii ndani yake, ni mtume lakini kazi yake itakuwa ni kutembea katika mstari ule ule wa mitume wa kwanza..hapaswi kuja na jambo lake jipya..anapaswa ahubiri kilekile mitume walichokifundisha, hapo atakuwa amekidhi kuitwa mtume.
Ni sawa na mtu anayejenga nyumba ya gorofa..msingi mkuu ni mmoja..ule uliopo chini…lakini akitaka aweke nyumba juu yake ni sharti afuata ramani ya msingi wa chini….
Ndivyo ilivyo kwa huduma hizi za kitume na kinabii.. Ni lazima zirejee katika biblia takatifu chochote kitolewacho lazima kionekane katika biblia sio katika maono yao wenyewe wanayojitungia.
Paulo aliandika maneno haya;
1 Wakorintho 3:10-15
[10]Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake.
[11]Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo.
[12]Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri.
[13]Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani.
[14]Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu.
[15]Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto.
Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa tofauti ya wale na hawa ni kwamba wote kazi yao ni moja ya upandaji wa kanisa la Kristo,mahali na mahali, isipokuwa wasasa hawaleti fundisho jipya, au maono mapya isipokuwa yale ambayo tayari yameshaanzishwa na mitume.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Nitamjuaje nabii wa Uongo?
Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?
Hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.
JINSI MTUME PAULO ALIVYOUTHAMINI WITO WAKE, JUU YA WENYE VYEO.
SWALI: Huu mstari una maana gani?
Mithali 19:14 “Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye; Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana”.
JIBU: Mstari huo unatupa picha kuwa, kumbe vipo vitu vya kurithishwa, lakini pia kuna vitu ambavyo hatuvipati kwa kurithishwa..
Kwamfano, hapo anasema mali; kama nyumba, magari, kazi, hivi vitu mtu anaweza kuvipata kutoka kwa wazazi wake,..Lakini linapokuja suala la MKE MWENYE BUSARA. Sio jambo la kurithishwa, au kutafutiwa na wazazi, au kupatwa kwa njia ya mali, au kwa uzuri, au kwa cheo, au kwa nguvu..Hapana, bali mke mwenye busara anatoka kwa Mungu tu! Na si sehemu nyingine.
Kumbuka hapo anasema ‘mke mwenye busara’..Sio ‘mke’…ikiwa na maana, ‘mke’ anaweza kupatikana popote tu pale, hata bar, kazini, barabarani, disco, vyuoni, mtaani, n.k. utampata.. Lakini mwenye busara, hatoki pengine isipokuwa kwa Bwana tu.
Ndio kama huyu aliyezungumziwa katika Mithali 31:10-31..Ambaye sifa zake ni; Kumcha Bwana siku zote, kuwahurumia maskini na wahitaji, Kuishi vyema na watumwa wake, kuwa msaidizi kwa mumewe, asiye mvivu n.k. Biblia pia inasema katika 1Petro 3:1-6 mke mwenye busara ni Ni mtiifu kwa mumewe, mpole, mtulivu, ajisitiriye, aitunzaye nyumba yake.
Hivyo kumpata huyu, wala usijichoshe kwa njia za vitu au mali. Bali nenda mbele za Bwana, mwombe, mshirikishe, mpango wako, kisha yeye mwenyewe atamsogeza kwako, na utamfurahia.
Kumbuka: Kinyume chake pia ni kweli. Mume mwenye busara, hapatikani pengine popote isipokuwa kwa Bwana tu. Mume mwenye busara, ni Yule amchaye Bwana, ampendaye mke wake, kama nafsi yake mwenyewe, ailindaye familia yake, aihudumiaye nyumba yake.(Waefeso 5:25). Hivyo yakupasa umwombe Bwana, kabla ya kuchukua maamuzi ya kutafuta mke/mume.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI.
WANA-NDOA: Baba Mkwe, Na mama Mkwe.
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)
Je! taratibu za kufunga ndoa [yaani harusi] ni agizo la Mungu au ni mapokeo tu ya kibinadamu?
Biblia inakataza kuapa kabisa, lakini kwanini watu wanaapa mahakamani na katika vifungo vya ndoa?
MAMBO MANNE,YANAYODHOOFISHA UOMBAJI WAKO.
Katika maisha bila shaka kuna siku ambazo uliwahi kuamka asubuhi na kuona siku yako inakwenda vizuri sana, una furaha, unafanikiwa, au unautulivu, au unapokea taarifa nzuri mahali Fulani, kazini kwako, kwenye familia n,k. Lakini kuna siku ambazo unaamka huoni uzuri wowote, aidha unaumwa, unaudhiwa na watu, unapata hasara kazini, unapokea taarifa za msiba, unaibiwa, unapigwa, unapata ajali Fulani, n.k.
Ukiwa kama mwanadamu, nyakati hizi za raha na masumbufu ni lazima ukumbukane nazo, haijalishi utakuwa ni mkamilifu kiasi gani.. Na Mungu ameruhusu iwe hivyo, ili kutaka sisi tukue vema katika hali anayoitaka yeye..
Embu tafakari maandiko haya;
Mhubiri 7:14 “Siku ya kufanikiwa ufurahi, Na siku ya mabaya ufikiri. Mungu ameifanya hiyo moja kwenda sambamba na hiyo ya pili, ili mwanadamu asipate kulijua neno lo lote litakalofuata baada yake”.
Mungu ameyaweka hayo yaende sambamba, kwamba hili lisimuache Yule, wala Yule lisimwache huyu..Haiwezekani kila siku utakayoamka asubuhi tu iwe ya furaha,..au iwe ya huzuni tu..hapana,
Sasa kwanini afanye hivyo?
Sababu zipo tatu (3)
Mungu anapenda kutupa furaha, hivyo zipo nyakati utaburudishwa tu na Mungu, hata kama sio sasa wakati huo utafika tu katika maisha yako. Atakufajiri tu kwa njia zake mwenyewe anazozijua. Atakatiza furaha katika siku Fulani Fulani, au katika kipindi Fulani cha maisha, Hivyo Jifunze kumfurahia Mungu wako wakati unafanikiwa, kwa kumshukuru sana..(Yakobo 5:13)
Sikuzote mtu huwa anafikiri vizuri anapokuwa katika shida au mateso Fulani, anapopitia kuumwa kidogo, analazwa, hapo ndipo anapojitambua kuwa yeye sio kitu, hawezi kutenda jambo lolote kwa nguvu zake, au kwa mafanikio yake, hivyo hiyo inamfanya sikuzote tumaini lake alielekeze kwa Mungu. Kwahiyo basi ujifunze kufikiri sana unapokuwa katika matatizo au masumbufu fulani, kwasababu ndicho Mungu anachokitaka hapo, zidi kuwa mwombaji, jifunze Biblia, kaa uweponi, ukishindwa kulielewa hilo utakuwa ni mtu wa kulaumu laumu, kunung’unika nung’unika ovyo sikuzote uingiapo katika vipindi hivi.(Wakorintho 8:1-10 )
Mungu anataka uhai wetu wote, tuumimine mikononi mwake, anataka kila jambo tunalolifanya tuseme BWANA akipenda, (Yakobo 4:13-16 ), anataka tukiamka asubuhi tumwombe kibali cha siku mpya, tunapomaliza siku tumshukuru..Tunapoanza mwezi mpya tumwombe, tunapomaliza tumshukuru, tunapoongeza umri mwingine wa maisha tupeleke shukrani zetu kwake.
Ndivyo Mungu alivyokusudia tuishi. Ni vizuri tuyatambue haya mapema ili tusiwe watu wa kutokuzielewa njia za Mungu wakati mwingine. Tuendelee kumcha Mungu katika majira tuyapitiayo kwa wakati huo,
Anasema pale mema au mabaya yanapokuja tu ghafla, kwa kutokujua mwenyewe..Hiyo inakupa sababu ya kujinyenyekeza, mbele za Mungu, na kumkabidhi Mungu mambo yako yote. Kwasababu hujui kama kesho utakufa au utaendelea kuishi..Ndio maana pale anasema “ili mwanadamu asipate kulijua neno lo lote litakalofuata baada yake”
Kwa kumalizia tafakari tena maandiko haya;
Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.
2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa;
3 Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;
4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;
5 Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe; Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;
6 Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza; Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;
7 Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;
8 Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia; Wakati wa vita, na wakati wa amani”.
Bwana atusaidie.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.
Nyakati za kuburudishwa ni zipi? (Matendo 3:19).
NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?
Na ulimi laini huvunja mfupa.(Mithali 25:15)
Nini maana ya kilichotarajiwa kikikawia kuja moyo huugua (Mithali 13:12)?.
Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia..
Vipo vipindi viwili vya Bwana Yesu kutuita katika maisha yetu.
Hebu tujifunze namna alivyowaita wanafunzi wake mara ya kwanza na mara ya pili, ili itusaidie na sisi kujua jinsi wito wa Mungu ulivyo..
Mara ya kwanza Bwana Yesu aliwaita wanafunzi wake kipindi wapo katika shughuli zao, ndio hapo utaona anamfuata Petro na Adrea kuwaambia wamfuate (Mathayo 4:19), baadaye tena anamfuata Mathayo katika shughuli yake ya utoza ushuru na kumwambia nifuate (Mathayo 9:9). Lakini katika wito wote wake huo, hakuwapa masharti yoyote magumu wanafunzi wake.. wengi wao aliwapa maneno ya faraja tu kuwa “watakuwa wavuvi wa watu badala ya samaki”.. wengine waliambiwa wataona mbingu zikifunguka na malaika wakishuka na kupanda juu ya Mwana wa Adamu (Yohana 1:51).
Kwahiyo wito wa kwanza kwa ufupi ulikuwa ni wito wa faraja na wa matumaini, haukuwa wito wa Masharti..
Lakini tunapokuja katika wito wa pili, tunaona Bwana Yesu akizungumza maneno mengine ambayo ni magumu kidogo… Tunaona anawaita tena kwa mara ya pili: Na wakati huu hawabagui tena kama alivyofanya hapo kwanza.. kwamba anakwenda mahali Fulani na kumtafuta Petro na Adrea peke yao!, na kuacha watu wengine, au anakwenda Forodhani na kumchagua Mathayo peke yake !, na kuacha watoza ushuru wengine..
Bali tunaona wakati huu wa pili, anawaita watu wote kwa pamoja, bila kubagua yule ni wanafunzi wake au sio wanafunzi wake, na kuwaambia maneno mengine mapya.. Na maneno hayo tunayasoma katika mstari ufuatao…
Marko 8:34 “Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate”
Mara ya kwanza Bwana Yesu hakutoa uhuru wa mtu yeyote kumfuata, yeye ndio alikwenda kuwatafuta akina Petro, na kuwachagua watembee naye.. Lakini mara hii ya pili, ANATOA NAFASI KWA WOTE! (wakike au wa kiume, awe mdogo au mkubwa, awe mlemavu au mzima).. na anawaambia wote (Mitume pamoja na Makutano). Kuwa mtu yeyote akitaka kumfuata, “AJIKANE MWENYEWE, AJITWIKE MSALABA WAKE AMFUATE”.
Wito huu wa pili ni kama unaufanya ule wito wa kwanza usiwe na nguvu tena!!.. Kwasababu hapa Bwana Yesu anawaita wote(wanafunzi wake pamoja na watu wa mataifa).. Pengine wakina Petro walingetemea maneno hayo waambiwe wakutano tu!, lakini wanashangaa na wao wanajumuishwa huko huko..
Wote wanapewa agizo moja! Bila upendeleo.. Maana yake ni kwamba pia alitoa mlango wa mtu yeyote kuondoka kama anataka kuondoka, haijalishi tayari alikuwa ameshaitwa hapo kwanza, haijalishi kama alikuwa tayari ameshapewa ahadi na Bwana…
Tunaweza kulithibitisha hilo katika…
Yohana 6:66 “Kwa ajili ya hayo wengi miongoni mwa wanafunzi wake wakarejea nyuma, wasiandamane naye tena.
67 Basi Yesu akawaambia wale Thenashara, JE! NINYI NANYI MWATAKA KUONDOKA?
68 Basi Simoni Petro akamjibu, Bwana! Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele.
69 Nasi tumesadiki, tena tumejua, ya kuwa wewe ndiwe Mtakatifu wa Mungu”
Umeona hapo?.. Yule Petro ambaye aliitwa hapo kwanza kwa wito wa faraja, safari hii Bwana anamwuliza “JE UNATAKA NA WEWE UNATAKA KUONDOKA??”, anamwuliza pia na Nadhanieli ambaye aliambiwa ataona malaika wakipanda na kushuka juu ya mwana wa Adamu, “JE UNATAKA NA WEWE UNATAKA KUONDOKA??”, maana yake ni kwamba kama wangetaka kuondoka, basi mlango upo wazi Bwana angewaruhusu wala asingembembeleza… Na ahadi zile alizowaahidiwa Bwana angewapa wale waliokuwa tayari. (Hii inaogopesha sana!!).
Ndugu inawezekana kipindi unasikia wito wa Mungu kukuita ulikuwa unapokea maneno ya faraja kutoka kwa Bwana Yesu, na kujiona wewe ni wa kipekee sana…huenda Bwana Yesu alikwambia wazi kabisa kuwa utakuwa mtumishi wake na utawavuta wengi kwake na utakuwa Baraka kwa maelfu ya watu..
lakini nataka nikuambia kuwa “usibweteke na wito huo wa kwanza wa faraja”…”utendee kazi wito wa pili” Kwasababu hata Petro na Yohana waliambiwa hivyo hivyo, hata Nadhanieli mara ya kwanza aliambia maneno ya faraja kama yako!..lakini baadaye Bwana Yesu aliwageukia na kuwaambia kuwa “Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate”…Na Bwana Yesu aliwaweka kundi moja na makutano kana kwamba hakuwahi kuwaita huko nyuma.. Kana kwamba siku hiyo ndio aliyokuwa anawaita kwa mara ya kwanza.
Ndugu yangu, huenda ulishausikia wito wa Kwanza, na sasa upo katika wito wa pili, Amua leo kumfuata YESU upya kwa kujikana nafsi!!.. Wakina Petro, baada ya kusikia hayo maneno ndipo walipojijua kuwa wanapaswa wahakiki wito wao upya!.. Ndipo wakaamua kujikana nafsi kweli kweli na kumfuata Yesu.
Na wewe leo, achana na ukristo vuguvugu wa kujisifia maono au karama, anza kujikana nafsi na kubeba msalaba wako, kaa mbali na dhambi na ulimwengu, kwa kadiri uwezavyo, weka chini fasheni za kidunia ambazo hazimpi Mungu utukufu, acha kuvaa kikahaba, acha kuweka wigi kichwani, acha kuweka hereni na mikufu, na kuvaa nguo za kubana..ni machukizo kwa Mungu (1Timotheo 2:9), acha kuabudu sanamu, acha kufanana na watu wa ulimwengu huu….hata kama dunia nzima itakuona umerukwa na akili, hata kama ndugu na wanadamu watakwona umechanganyikiwa.. wewe mfuate Yesu, na udunia uweke nyuma, na siku ile utapokea Taji ya uzima.
Kumbuka siku zote kuwa “waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache”(Mathayo 22:14).
Tujitahidi tuwe wateule wa Bwana Yesu.
Bwana akubariki.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
JINSI MTUME PAULO ALIVYOUTHAMINI WITO WAKE, JUU YA WENYE VYEO.
AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!
NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?
MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.
Swali: Pale Forodhani, Mathayo alipokuwa ameketi ndio mahali gani? (Mathayo 9:9).
Jibu: Tusome,
Mathayo 9:9 “Naye Yesu alipokuwa akipita kutoka huko aliona MTU AMEKETI FORODHANI, aitwaye Mathayo, akamwambia, Nifuate. Akaondoka, akamfuata”
“Forodha” ni “Nyumba au kijumba kidogo” kinachotumika kukusanyia mapato.. Kwamfano watu wanaofanya kazi benki, huwa wanaketi ndani ya madirisha Fulani maalumu ya kupokea au kutoa fedha, sasa vyumba vile walivyopo ndivyo vinavyoitwa “forodha” ( kwa lugha nyingine).
Hali kadhalika watu wanaofanya kazi katika mashirika ya kukusanya mapato, huwa wanaketi katika chumba maalumu chenye dirisha ambapo wanapokea fedha na kutoa risiti. Vyumba hivyo ambavyo vimetengenezwa mahususi kwaajili ya kupokea wateja na kodi zao, au ada zao, au ushuru wao ndivyo vinavyoitwa Forodha.
Katika siku hizi Forodha pia zinatengenezwa na wafanya biashara, kutokana na kutanuka kwa wigo wa kibiashara, kwamfano watu wanaofanya kazi za uwakala wa mitandao ya simu mf. Mpesa n.k huwa wanatengeneza Viforodha vidogo, kwaajili ya shughuli zao hizo za kutoa na kupokea fedha.
Lakini ni funzo gani tunalipata kwa Mathayo aliyeketi Forodhani?..
Mathayo alipoitwa na Bwana Yesu, muda ule ule aliitikia wito!, hakungoja kesho, wala baadaye, badala yake muda ule ule alimfuata Bwana YESU.. Ijapokuwa alikuwa yupo katika mazingira magumu ya kumfuata Bwana Yesu, lakini ilimgharimu kuacha vyote na kumfuata Yesu!. Na faida ya kumfuata Yesu, Mathayo pamoja na wenzake waliyoipata, ni kwamba walikuja kupata mara mia kwa vile vyote walivyovipoteza, na zaidi sana walipata ahadi ya uzima wa milele.
Mathayo 19:27 “Ndipo Petro akajibu, akamwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata; tutapata nini basi?
28 Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli”.
Je ni kazi yako ndio kikwazo cha wewe kumfuata Yesu?, je ni watoto wako au mke wako au wazazi wako ndio kikwazo cha wewe kumfuata Yesu kwa moyo wako wote na nguvu zako zote?.. kama kazi yako ndio kikwazo, basi nataka leo umkumbuke Mathayo, yeye kazi yake aliona si kitu zaidi ya wito wa Mungu!. Na mwishowe leo hii tunasoma waraka wake huu.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Katika (Mathayo 25:8 na Marko 16:8) Wale wanawake walitangaza kufufuka kwa Bwana au walikaa kimya?
REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.
Nakusalimu katika jina kuu la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze maneno ya uzima.
Nehemia ni mtu aliyekusudia kutoka katika moyo wake, kwenda kuukarabati ukuta wa Yerusalemu uliokuwa umebomoka, mtu huyu hakuwa nabii, wala kuhani, wala hakujulikana popote, lakini kwa kuguswa kwake moyoni kwa habari alizozisikia kuhusiana na uharibifu ule, aliumia sana, ndipo akajitia nguvu, kumwomba Mungu kibali na baadaye akapewa, na kuweza kwenda Yerusalemu kwa ajili ya kazi hiyo ya kuukarabati. Sasa hatuna muda wa kueleza historia yote, kwa muda wako waweza kusoma habari yake tangu mwanzo hadi mwisho katika kitabu hicho.
Hivyo naamini kwa kuyatazama mapito yake, utapata funzo, hata na wewe ambaye, anataka kuingia katika kazi ya kusimama “mahali palipobomoka” ili upakarabati.
Sasa wakati Nehemia anafika Yerusalemu, ili kuanza operasheni yake ya kuujenga tena ukuta ule, ilimbidi kwanza, atembee, katika malango yote, na sehemu zote za ukuta huo ili atathimini, uharibifu uliotokea, pamoja na nguvu na gharama zitakazotumika kuukarabati tena..
Biblia inatuambia, aliondoka, usiku wakati ambapo watu wamelala, akaanza kuuzunguka ukuta ule wa mji ambao ulikuwa ni mrefu sana, Kuonyesha kuwa mpango bora wa kukarabati kusudi la Mungu, huwa hashirikishwi kila mtu, bali watu wachache sana tena, waaminifu, ambao wanaweza kuchukua mzigo wako..Tusome
Nehemia 2:11 “Basi nikafika Yerusalemu, nikakaa huko muda wa siku tatu.
12 Kisha nikaondoka usiku, mimi na watu wachache pamoja nami; wala sikumwambia mtu neno hili alilolitia Mungu wangu moyoni mwangu, nilitende kwa ajili ya Yerusalemu; wala hapakuwa na mnyama pamoja nami, ila mnyama yule niliyempanda mwenyewe”.
Anaendelea kusema…
13 Nikatoka nje usiku, kwa njia ya lango la bondeni, nikashika njia iendayo kisima cha joka, na lango la jaa; nikazitazama kuta za Yerusalemu, zilizokuwa zimebomoka; na malango yake yameteketezwa kwa moto. 14 Kisha nikaendelea mpaka lango la chemchemi, na ziwa la mfalme; LAKINI HAPAKUWA NA NAFASI YA KUPITA KWA YULE MNYAMA ALIYEKUWA CHINI YANGU.
15 Kisha nikapanda usiku kando ya kijito, nikautazama ukuta; kisha nikarudi nyuma, nikaingia kwa lango la bondeni, nikarejea hivyo.
16 Wala mashehe hawakujua nilikokwenda, wala nilivyotenda; wala sijawaambia Wayahudi, wala makuhani, wala wakuu, wala mashehe, wala watu wengine waliokuwa wakiifanya kazi hiyo. 17 Kisha nikawaambia, Mnaona hali hii dhaifu tuliyo nayo, jinsi Yerusalemu ulivyo hali ya ukiwa, na malango yake yalivyoteketezwa kwa moto; haya! Na tuujenge tena ukuta wa Yerusalemu, ili tusiwe shutumu tena.
Hapo mwanzo alipoanza safari,alikuwa na mnyama wake, Ambaye ni farasi/punda.. Mnyama Yule alimsaidia sehemu baadhi tu kufika,na kuona uharibifu uliotokea katika kuta, lakini alifika mahali, ambapo mnyama asingeweza kupita katika penyo zile, bali ni mtu tu! Hapo ndipo ikabidi amwache mnyama Yule, atembee yeye kama yeye, mguu kwa mguu, kutazama sehemu za ukuta, ndogo ndogo, za mafichoni, zilizokuwa zimeharibiwa vibaya sana na maadui zao. Asingefanya hivyo, ukarabati wake ungeishia pale pale punda alipoishia, asingekarabati kote.
Ndipo alipomaliza ziara hiyo, akarejea mjini, na kuwaambia makuhani na wahusika wote, hali ilivyokuwa.
Bwana anasema..
Ezekieli 22:30 “Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka, kwa ajili ya nchi, nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu”.
Sikuzote kusimama mahali palipomoboka si rahisi, Mungu anatafuta watu hao mfano wa Nehemia hawaoni,,ni lazima tufahamu kuwa zipo gharama kubwa sana, za kukarabati, waweza kudhani, utakwenda na taasisi, au utakwenda na ushirika, au utakwenda na kiwango Fulani cha pesa kwenye akaunti yako.. Hapana vyote hivyo vinaweza kukusaidia kwa muda tu, bali utafika wakati hivyo vyote havitakusaidia, bali itakubidi usimame wewe kama wewe, kama ni kuomba, kama ni kuhubiri, kama ni kukemea dhambi, kama ni kuanzisha jambo..
Mnyama aliye chini yako, hataweza kuvuka nawe, ndugu zako hawataweza kutembea na wewe,katika maono hayo Mungu aliyokupa juu ya kusudi lake, .. Bali ni wewe kama wewe.
Ilimpasa Nehemia afanye hivi, japokuwa alipitia changamoto nyingi, mpaka mbeleni wakawa wanamdhihaki na kumwambia, ukuta unaoujenga jinsi ulivyo dhaifu, hata mbweha wakipita juu yake utaanguka.(Nehemia 4:3), Lakini hakuvunjika moyo, yeye aliendelea kusimama mpaka mwisho ..
Walipokuwa wanaujenga, mkono mmoja ulishika silaha, na mwingine tofali, waliujenga katika hofu, usiku kucha, Lakini mwishoni ulikamilika, katika utukufu mwingi. Na faida yake ni kwamba hadi sasa tunaisoma habari ya Mtu huyu Nehemia, na kumbukumbu lake lipo hadi leo.(Nehemia 4: 17-23)
Ndugu zipo kuta nyingi sana zilizobomolewa na ibilisi, hadi sasa Bwana anatafuta watu watakaosimama, makanisani kujenga nyumba yake, watakaosimama kwa vijana, kuwaweka kwenye misingi ya imani, watakaosimama kwa familia na watoto kuwafundisha kumcha Bwana. Watakaosimama katika Neno la Mungu, kufundisha injili ya kweli isiyoghoshiwa, na kukemea mafundisho potofu..
Swali ni Je! Sisi tutaweza kusimama na kujenga upya?
Kama ni hivyo basi tuwe tayari hata wakati mwingine kusimama peke yetu, kama Nehemia, pale ambapo hatuona sapoti, uwe ndio wakati wa kusonga mbele, na kuitenda kazi ya Mungu, pale ambapo tunaona vita, na dhihaka, tusife moyo bali uwe ndio tuifanye kazi, usivunjike moyo wala usikate tamaa..Kwasababu Kujenga kuna gharama. Lakini faida zake ni kubwa sana mwishoni.
Bwana atusaidie.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)
Wana wa Asafu ni akina nani katika biblia?
Mlango uitwao “Mzuri” Unaozungumziwa katika Matendo 3:2 ndio upi?
Pango la Makpela ni lipi, je lina umuhimu wowote kwetu?
SWALI: Naomba kufahamu mstari huu unamaana gani?
Mhubiri 4:4 “Tena nikafikiri amali zote, na kila kazi ya ustadi, ya kwamba inatoka katika mtu kupingana na mwenzake. Hayo nayo ni ubatili na kujilisha upepo”.
JIBU: Sulemani ni mtu ambaye alipewa na Mungu uwezo wa kutambua hekima ya mambo yote yanayotendeka huku duniani.. Na moja ya jambo ambalo aliliona na kutolea habari zake ni kuhusiana na chanzo cha mafanikio mengi ya watu ni nini?.. Na ndio hapo anasema..
“Tena nikafikiri amali zote, na kila kazi ya ustadi, ya kwamba inatoka katika mtu kupingana na mwenzake”.
Kwamba kila utajiri, au kazi za ustadi, yaani nyumba nzuri, magari mazuri, mavazi mazuri, hatua zote za mafanikio, asilimia kubwa hutokana na mtu kupingana na mwenzake, kwa tafsiri iliyo nzuri ni kwamba hutokea mtu kushindana na mwingine..ambacho chanzo chake ni wivu.
Kwamfano, mtu atasema mbona Fulani amenunua gari, mimi sijanunua, ngoja nikakope pesa nifanye kazi juu chini na mimi mwaka huu ninunue la kwangu zuri kuliko lile.. Sasa mtu kama huyu atapata gari kweli, lakini chanzo cha gari lake sio malengo yake, bali ni kwasababu wenzake wanayo magari yeye hana.
Hata mashirika makubwa, kufanikiwa kwao ni kwa mashindano, utaona kampuni moja la simu limetoa ofa hii, kesho lingine linaiga ofa ile ile na zaidi, ili lisipoteze wateja.. Hivyo yamefanikiwa kwa njia hizo hizo, za mashindano.
Tajiri mmoja atashindana na tajiri mwenzake ili awe namba moja, hivyo atafanya kazi kwa bidii usiku kucha, ili asishindwe na mwenzake, watashindana kibidhaa n.k.. Mchungaji mmoja atashindana na mchungaji mwingine kwa wingi wa washirika, au kwa ukubwa wa kanisa,
Sasa hayo yote Sulemani ameyaona na kusema ni ubatili, ni sawa na kujilisha(kuufuata) Upepo. Maana yake ni kuwa mafanikio yanayokuja kutoka katika wivu, au mashindano, hayana afya yoyote kiroho.
Hii inatufundisha nini?
Wafilipi 2:14-15 inasema..
“14 Yatendeni mambo yote pasipo manung’uniko wala mashindano,
15 mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu”
Kama watakatifu, hatupaswi kutafuta kitu chochote kwa kushindana, utasema mwenzangu ana neema kubwa kama ile, ngoja na mimi nikafunge na kuomba nimpite,. Hapana, bali tunapaswa tuishi kwa kumtazama Mungu,kila mmoja katika nafasi yake aliyopewa na Mungu, na kuitendea bidii hiyo, kwasababu kwa kupitia hiyo ndio Mungu atatufanikisha, na sio kwa neema za wengine..
Bwana atubariki.
mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Shalom.
Tafadhali share na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Nini maana ya “Amali” na “Ijara” katika biblia?
Na alaaniwe ampigaye mwenzake kwa siri.
Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe;(Mithali 16:2)
Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)
Biblia inatufundisha kuomba bila kukoma…
Wathesalonike 5:17 “ombeni bila kukoma”
Leo tutatazama ishara chache ambazo zitatutambulisha kuwa kiwango cha maombi yetu kimejitosheleza au kimemfikia Baba yetu.
1.MZIGO KUPUNGUA NDANI YAKO.
Hii ni ishara ya kwanza itakayokutambulisha kuwa maombi yako yamefika kwa Bwana.
Unapoomba na kuona mzigo wa kile unachokiombea umepungua ndani yako, basi hiyo ni ishara kuwa kiwango chako cha maombi kimefikia kilele kwa muda huo.
Sasa swali utauliza utajuaje kuwa mzigo umepungua ndani yako?. Tuchukue mfano rahisi, Ulikuwa una jambo la muhimu au la siri ambalo ulikuwa umepanga kumweleza mtu Fulani (labda rafiki yako), na hujapata nafasi, ila unaitafuta kwa bidii, kiasi kwamba huwezi kutulia mpaka umemweleza jambo hilo, au umpe taarifa hiyo, sasa kipindi utakapokutana naye na kumweleza yote ya moyoni mwako, kuna hali Fulani unajiona mwepesi baada ya hapo, (unajiona kama huna deni tena, umeutua mzigo), unaona amani inarudi, na unakuwa huru.. Sasa hiyo hali unayoisikia baada ya kufikisha ujumbe kwa uliyemtarajia ndio kwa lugha nyingine ya (Mzigo kupungua ndani yako).
Kwahiyo hata sisi tunapoomba, yaani tunapopeleka hoja zetu mbele za Mungu, kabla ya kuzipeleka tunakuwa na mzigo mzito ndani yetu, lakini tunapokaa katika hali ya utulivu na kusema na Mungu kwa unyenyekevu mambo yetu na hoja zetu, basi kuna hali/hisia fulani ambayo Bwana Yesu anaiachia ndani yetu, inayotupa wepesi katika roho zetu, na kupunguza ule mzigo, kiasi kwamba, kama ulikuwa unamwombea Mtu, kuna hali Fulani inakuja ndani yako kuwa maombi yako yamemfikia Mungu, na hivyo amani ya kipekee inashuka ndani yako, na unajikuta ile hamu ya kuendelea kuombea hilo jambo inaisha, badala yake inakuja hali nyingine ya kumshukuru Mungu na kumshangilia na kumfurahia.
2. ANDIKO KUKUJIA au KUMBUKUMBU YA JAMBO FULANI.
Hii ni ishara ya pili ya maombi yetu kumfikia Baba..
Unapokuwa katika maombi, halafu ghafla likaja andiko katika ufahamu wako, na andiko hilo linauhusiano mkubwa na kile ulichokuwa unakiombea.. basi fahamu kuwa maombi yako yamefika, na hivyo Bwana anakuthibitishia kwa kukupa hilo andiko. Au unaweza kuwa unaomba halafu ghafla ukaletewa kumbukumbu Fulani ya kisa Fulani katika biblia, ambapo kupitia kisa hiko imani yako ikanyanyuka na kujikuta unapata amani au furaha kubwa.. basi hiyo ni ishara kuwa maombi yako yamefika, na hivyo katika hiyo hatua na kuendelea ni wakati wa kumshukuru Mungu na kuutafakari ukuu wake, kwasababu Bwana kashajibu na kusikia.
Vile vile unapokuwa katika maombi na moyoni una mzigo mkubwa kwa kile unachokiombea, halafu ghafla ikaja kumbukumbu Fulani ya kipindi Fulani cha maisha ambacho Mungu alikupigania ukauona mkono wake, au ukaja ushuhuda Fulani kichwani mwako wa mtu mwingine, na ghafla ukajiona umepata nguvu nyingine basi hiyo ni ishara kuwa hoja zako zimefika mbele zake na hivyo Bwana amekuthibitishia kwa kukukumbusha uweza wake na mkono wake.
3. NGUVU MPYA.
Unaweza usisikie chochote unapokuwa katika maombi, (yaani usisikie mzigo kupungua ndani yako) au usiletewe andiko lolote, lakini ukajikuta unapata nguvu ya kuendelea mbele zaidi….
Maana yake kabla ya maombi ulikuwa umekata tamaa, hata nguvu ya kuendelea mbele ulikuwa huna, lakini baada ya maombi..unaona kuna ujasiri umeongezeka ndani yako, kuna nguvu ya kuendelea mbele imekuja ndani yako, ingawa moyoni mzigo bado hujapungua..
Sasa hiyo hali ya kutiwa nguvu kabla ya kupokea majibu ya maombi yako ni ishara kuwa Maombi yako YAMEMFIKIA BWANA, ila wakati wa kupokea majibu yako bado!…Hivyo Bwana anakutia nguvu ili usije ukazimia kabisa, au ukaanguka kabisa…wakati huo zidi kujisogeza mbele zake kwa maombi ya shukrani…
Kwamfano unaweza kuwa unasumbuliwa na ugonjwa ambao ni mbaya sana, na umemwomba Mungu kwa muda mrefu, akuponye na hapo ulipo upo katika hali ya mauti uti, lakini ukajikuta unapata unafuu mkubwa sana, na hata kuendelea na shughuli zako kana kwamba huumwi kabisa.. lakini ule ugonjwa bado haujaondoka!.. sasa hiyo hali ya kupata unafuu baada ya maombi, ni ishara kuwa Bwana alishasikia maombi yako, ila siku kamili ya muujiza mkuu bado!, (na itafika tu)..lakini amekutia nguvu ili kukuonyesha kuwa yupo pamoja na wewe na ili usije ukazimia kabisa..
Vile vile unaweza kumwomba Bwana akupe kazi fulani nzuri ambayo kupitia hiyo utayafanya mapenzi yake, lakini badala ya kukupa hiyo shughuli unayoiomba muda ule uliomwomba, yeye anakupa riziki za kukutosha tu wakati huo.. (ulitegemea upewe kazi lakini yeye anakupa riziki tu)…Ukiona hivyo jua ni ishara ya kuwa maombi yako yameshamfikia yeye, Ndio maana anakutia nguvu…ni suala la muda tu!, mambo yote yatakaa sawa..
Isaya 40:27 “Mbona unasema, Ee Yakobo, mbona unanena, Ee Israeli, Njia yangu imefichwa, Bwana asiione, na hukumu yangu imempita Mungu wangu asiiangalie?
28 Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, Bwana, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki.
29 Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo
30 Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka;
31 bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.”.
Zipo ishara za kutambulisha kuwa maombi yetu yamemfikia Baba yetu, lakini kwa hizi chache itoshe kusema kuwa Bwana Mungu wetu anatupenda na anatujali na anasikia maombi yetu. Lakini kumbuka kuwa kama bado hujampokea Yesu, (yaani hujaokoka), basi fahamu kuwa Mungu hasikilizi maombi yako wala hajibu. (Yohana 9:31)
Sasa ni kwanini hajibu, wala hasikilizi maombi ya watu ambao hawajampokea?.. Ni kwasababu mtu wa namna hiyo hawezi kuomba sawasawa na mapenzi yake, (kwasababu yeye mwenyewe alisema kuwa mafanikio ya mpumbavu yatamwangamiza, Mithali 1:32) na Mungu hapendi mtu yeyote aangamie wala apotee, bali wote wafikie toba na wafanikiwe..Hivyo atahakikisha kwanza unapata wokovu ndipo mengine yafuate..
Kwahiyo suala la kwanza ni wokovu kabla ya mambo mengine yote.. Kama hujampokea Yesu, kwa kutubu dhambi zako, na kubatizwa katika ubatizo sahihi, basi ni vizuri ukafanya hivyo mapema iwezekanavyo, ili uwe mshirika wa Baraka za Mungu.
Lakini kama tayari umeshampokea Yesu na umesimama vizuri katika imani, basi fahamu kuwa yote unayomwomba Mungu atakupatia sawasawa na ahadi zake, hivyo zidi kumwamini na wala usiishiwe nguvu.
Bwana akubariki
mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU