SWALI: Biblia inaposema “Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake”, ina maana gani?
Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.
JIBU: Ili kuelewa neno hilo, wazia mfano huu; Mtu mmoja ameshitakiwa na mahakama kwa kosa la uchafuzi wa mazingira, hivyo, akapewa adhabu ya kulipa faini ya sh. Milioni 5 ndani ya wiki 3, au jela miaka 3. Sasa ikatokea mtu huyu akawa hana cha kulipa,.. Unadhani atakuwa katika hali gani? Ni wazi kuwa atapoteza amani yote, hawezi kuwa katika furaha, hawezi kuwa katika raha wakati wote huo kwasababu anajua hukumu ya kifungo ipo mbele.. Ili amani yake irudi, hana budi apate kiwango hicho alipe. Lakini akatokea mtu, akasema mimi nitakuchukua adhabu hiyo nitamlipia deni lake. Bila shaka furaha na amani ya yule mdaiwa itarejea tena.
Hivyo tunaweza kusema, ili kuirejesha ile amani yake ya mwanzo, alikuwa hana budi kutumikia adhabu kwanza..
Sasa tukirudi katika huo mstari ..biblia inaposema;
Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.
Huyo ni Bwana Yesu anayezungumziwa hapo, sasa anaposema, Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”. Ni kwamba ili sisi kuipokea Amani yetu, tuliyoipoteza tangu kule edeni, ilitupasa kwanza tutumikie adhabu ya makosa.. Lakini ashukuruwe Kristo kwasababu alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, akapigwa na kuteswa ili sisi tupone. Adhabu ya amani yetu aliichukua yeye.
Na ndio maana Warumi 8:1 inasema; “Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu”.
Ukiwa ndani yake, amani yako inarejeshwa bila kulipa gharama yoyote. Lakini inastaajabisha kuona bado wapo watu hawataki kulipiwa deni zao. Wakidhani kuwa wataweza kustahimili hukumu ya Mungu siku ile. Ndugu ikiwa upo nje ya Kristo huna tumaini lolote. Ukifa ni moja kwa moja jehanamu kwenye ziwa la moto. Adhabu yako ni Mauti katika lile ziwa la moto milele.
Hiyo ndio sababu kwanini unamuhitaji Yesu Kristo leo, kwasababu ukishakufa leo hakuna tumaini, wala huna matendo yoyote ya kumshawishi Mungu, afute dhambi zako. Wasubiri nini, usimgeukie Bwana Yesu akusafishe Maisha yako angali ukiwa hai? Tubu sasa mpokee yeye. Muda ni mchache.
Maran Atha.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
KAMA SI YESU, HABARI YETU INGEKUWA IMEISHA ZAMANI SANA.
BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?
Je Mungu ana njia ngapi za kuzungumza?
Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?
SWALI: Naomba kufahamu maudhui ya mstari huu,
1Timotheo 1:20 “Katika hao wamo Himenayo na Iskanda, ambao nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu”.
JIBU: Awali ya yote, kabla ya kufahamu ni kwanini Mtume Paulo anatoa hukumu kali kama hiyo tuangalie mistari ya juu yake ambayo inaeleza sifa, za hao watu.
Ukisoma mstari wa 19, Paulo anamuasa Timotheo, awe ni mtu mwenye Imani, lakini sio Imani tu, bali pia “dhamiri njema”.. Ni vitu vinavyokwenda sambamba.
1Timotheo 1:19 “uwe mwenye imani na dhamiri njema, ambayo wengine wameisukumia mbali, wakaangamia kwa habari ya Imani.
20 Katika hao wamo Himenayo na Iskanda, ambao nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.”
Dhamiri ni kile kitu cha ndani kinachomshuhudia mtu kwamba anachokifanya ni sahihi au sio sahihi. Hivyo pale mtu anapokuwa na dhamiri njema, maana yake ni kuwa, anaitii nafsi yake, inapofanya kosa, pale inaposuta, anakuwa tayari kugeuka. Hivyo mtu kama huyu huwa anaishi kwa kujichunga, na kuwahurumia na kwa kuogopa hukumu pale anapojaribu kuwapotosha watu.. Kwasababu dhamiri yake njema inamshitaki.
Lakini mtu ambaye hana dhamiri njema, ni kwamba, hata anapoona jambo Fulani alifanyalo ni baya, anastahili hukumu, yeye hajali, bali anafanya atakalo, kwa maslahi yake. Atakuwa tayari kuwafundisha watu mafundisho potofu kwa makusudi kabisa akijua kabisa alifanyalo ni upotevu, lakini yeye ataendelea kufanya, kwa furaha kabisa..
Sasa ndio hapo mtume Paulo, anawatolea mfano watu hao, waliokosa dhamiri njema. Ambao ni Himenayo, na Iskanda. Watu hawa walikuwa ni wabaya, kwasababu walikuwa wanapindua Imani za watu kwa makusudi, wala sio kwa bahati mbaya wakiwafundisha kinyume na mafundisho ya mitume,.
Kwamfano huyu Himenayo, tunasoma tena, Paulo akieleza mafundisho yake potofu, ya kuwaambia watu Ufufuo wa wafu tayari umeshatokea.. Hivyo watu wengi wakaiacha Imani na kumgeukia yeye.
2Timotheo 2:16 “Jiepushe na maneno yasiyo na maana, ambayo si ya dini; kwa kuwa wataendelea zaidi katika maovu,
17 na neno lao litaenea kama donda-ndugu. Miongoni mwa hao wamo Himenayo na Fileto,
18 walioikosa ile kweli, wakisema ya kwamba kiyama imekwisha kuwapo, hata kuipindua imani ya watu kadha wa kadha”.
Na mwezake Iskanda, ambaye wengi wanaamini ndio huyu aliyezungumziwa katika vifungu hivi; Ambaye alimpinga sana Paulo katika kazi zake za kihuduma.
2Timotheo 4:14 “Iskanda, mfua shaba, alionyesha ubaya mwingi kwangu; Bwana atamlipa sawasawa na matendo yake.
15 Nawe ujihadhari na huyo, kwa sababu aliyapinga sana maneno yetu”.
Hivyo, makundi haya, Mtume Paulo hakushughulika nayo kabisa, bali kwa mamlaka aliyopewa, aliwaacha mikoni mwa shetani, ili wafundishwe wasimtukane Mungu. Maana yake ni kuwa, ulinzi wa Mungu uliondolewa juu yao, ili shetani apate nafasi ya kuwashughulikia, ili yamkini watubu.
Aidha walikumbwa na magonjwa, au mapigo, au hata vifo hatujui.. Lakini kuwekwa mikoni mwa shetani, adhabu kali kama hizo utakumbana nazo.(Tunaona kwa ayubu pale alivyoondolewa wigo wa ulinzi na Mungu, jinsi majangwa makali yalivyompata)..Ndivyo ilivyokuwa kwa hawa wakina Himenayo na mwenzake.
Yapo mamlaka ambayo Watakatifu wamepewa, kwa watu ambao wanauchezea ukristo, Ikiwa unafanya dhambi kwa makusudi, angali unaujua ukweli, na upo ndani ya mwili wa Kristo, kuwa makini sana, kwasababu hukumu yoyote itakayotolewa juu yako na wao lazima ikupate.. Na kama utakuwa unafanya kwa siri, kanisa halitajua, lakini Mungu atajua.. Na yeye mwenyewe atakuweka mikononi mwa ibilisi, upigwe. Ukishafikia hatua hii, waweza hata poteza Maisha yako.
Soma;
1Wakorintho 5:1 “Yakini habari imeenea ya kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika Mataifa, kwamba mtu awe na mke wa babaye.
2 Nanyi mwajivuna, wala hamkusikitika, ili kwamba aondolewe miongoni mwenu huyo aliyetenda jambo hilo.
3 Kwa maana kweli, nisipokuwapo kwa mwili, lakini nikiwapo kwa roho, mimi mwenyewe nimekwisha kumhukumu yeye aliyetenda jambo hilo, kana kwamba nikiwapo.
4 Katika jina la Bwana wetu Yesu, ninyi mkiwa mmekusanyika pamoja na roho yangu, pamoja na uweza wa Bwana wetu Yesu;
5 kumtolea Shetani mtu huyo, ili mwili uadhibiwe, ili na roho iokolewe katika siku ya Bwana Yesu”.
Bwana atupe Imani ya kweli na dhamiri safi.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni ipi?
MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.
MAZUNGUMZO MABAYA HUHARIBU TABIA NJEMA.
NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?
KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.
Jina la Bwana na Mwokozi Yesu libarikiwe. Karibu tujifunze biblia.
Je kuna utofauti wowote ya Ubatizo wa Yohana na ule wa Bwana Yesu?,
Jibu ni kwamba hakuna utofauti wowote, ubatizo ni ule ule mmoja wa toba, lakini kinachoutofautisha ule wa Yohana na ule wa Bwana Yesu ni “jina” Lakini ubatizo ni ule ule.
Kumbuka kabla ya Bwana Yesu kuja watu walikuwa wanasali, walikuwa wanafanya maombezi, na vitu vingine lakini walikuwa hawalitumii jina lolote, kwasababu hawakupewa maagizo hayo na Mungu. Hali kadhalika na Yohana alipokuja na ufunuo mpya wa ubatizo, alibatiza pasipo kuhusisha jina lolote. Maana yake baada ya watu kutubu kwa kumaanisha kuziacha dhambi zao, ishara ya mwisho ya wao kutakasika ilikuwa ni “kuzamishwa katika maji, na kuibuka juu” pasipo kutaja jina lolote.
Lakini Bwana Yesu alipokuja, mambo yalibadilika.. Kila kitu cha KIMungu ni lazima kifanyike kwa jina lake yeye..
Wakolosai 3:17 “Na kila mfanyalo, KWA NENO AU KWA TENDO, FANYENI YOTE KATIKA JINA LA BWANA YESU, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”.
Kutokana na maagizo hayo, Mitume na wanafunzi wengine wa Bwana Yesu, walianza kulitumia jina la Yesu katika mambo yote yote ya kiMungu watakayoyafanya kwa NENO na kwa MATENDO.
Mfano wa MANENO ambayo walianza kutamka kwa jina la Yesu ni SALA zote NA MAOMBI NA MAHUBIRI …ndio maana utaona walipokwenda kutoa pepo, na kuombea watu wenye magonjwa na madhaifu mbali mbali walitumia jina la Yesu,..
Luka 16:17 “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; KWA JINA LANGU watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya”.
Vile vile utaona walipoenda kuhubiri na kufundisha, walifundisha kwa jina la Yesu..
Luka 24:46 “Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu;
47 na kwamba mataifa yote watahubiriwa KWA JINA LAKE habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu”.
Soma pia Matendo 4:18
Mfano wa matendo hayo yalikuwa ni ubatizo!..
Hayo yalikuwa ni Maneno, sasa utauliza vipi kuhusu Matendo..je! kuna matendo yoyote ambayo yalikuwa yanafanywa kwa jina la Yesu?.. Jibu ni ndio!
Kumbuka ubatizo si yohana peke yake aliyekuwa anafanya, bali na wanafunzi wake pia walikuwa wanawabatiza watu..kwasababu Yohana aliwafundisha hivyo, na zaidi sana utaona pia Adrea kabla ya kuwa Mwanafunzi wa Bwana Yesu alikuwa ni mwanafunzi wa Yohana. Hivyo alikuwa anaujua ubatizo vizuri na alikuwa akibatiza, kabla hata ya Bwana Yesu.
Lakini baada ya Bwana YESU kuja, na kufahamu kuwa mambo yote, ni lazima yafanyike kwa jina la Bwana Yesu, ikiwemo ubatizo pia, ndipo wote wakaacha kubatiza kama Yohana, kwa kuzamisha bila kutaja jina lolote, na wakaanza kubatiza kwa jina la Yesu.
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
38 Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.
Umeona?.. kumbe hata ubatizo, ni lazima uwe kwa jina la Bwana Yesu ili ulete matokeo.. Ndio maana Mtume Paulo, alipokutana na wale watu kipindi wapo Efeso, aliwaambia wakabatizwe upya kwa jina la Yesu, ijapokuwa tayari walikuwa wameshabatizwa kwa ubatizo wa Yohana.
Matendo 19:1 “Ikawa, Apolo alipokuwa Korintho, Paulo, akiisha kupita kati ya nchi za juu, akafika Efeso; akakutana na wanafunzi kadha wa kadha huko;
2 akawauliza, Je! Mlipokea Roho Mtakatifu mlipoamini? Wakamjibu, La, hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatukusikia.
3 AKAWAULIZA, BASI MLIBATIZWA KWA UBATIZO GANI? Wakasema, Kwa ubatizo wa Yohana.
4 Paulo akasema, Yohana alibatiza kwa ubatizo wa toba, akiwaambia watu wamwamini yeye atakayekuja nyuma yake, yaani, Yesu
5 WALIPOSIKIA HAYA WAKABATIZWA KWA JINA LA BWANA YESU.
6 Na Paulo, alipokwisha kuweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akaja juu yao; wakaanza kunena kwa lugha, na kutabiri.”
Ndugu unayesoma ujumbe huu, fahamu kuwa kama hutabatizwa katika ubatizo sahihi, baada ya kuujua ukweli, utakuwa umemkataa Mungu moja kwa moja!!!.. na kuna madhara makubwa sana ya kutokubatizwa kwa jina la Bwana Yesu, (siku zote usilisahau hilo kichwani mwako).
Ikiwa bado hujampokea Yesu, kumbuka hizi ni siku za Mwisho, Kristo anarudi hivyo ni vizuri ukayatengeneza maisha yako kabla nyakati za hatari hazijafika.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?
MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.
Je ni viatu gani Musa aliambiwa avivue? Vya mwilini au vya rohoni? (Kutoka 3:5).
SWALI: Nini maana ya huu mstari;
Mithali 28:8 “Yeye azidishaye mali yake kwa riba na faida, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.
JIBU: Huyo anayezungumziwa azidishiye mali zake kwa riba na faida ni mtu ajipatiaye mali kwa njia zisizo za haki, kuwadhulumu wanyonge.
Kwamfano katika biblia Mungu aliwaangiza wana wa Israeli, wasiwatoze riba maskini, pindi wawakopeshapo, na pia wasichukue faida kutoka kwa ndugu zao, isipokuwa kwa wageni tu.
Kutoka 22:25
“Ukimkopesha mtu aliye maskini, katika watu wangu walio pamoja nawe; usiwe kwake mfano wa mwenye kumdai; wala hutamwandikia faida”.
Soma pia, Walawi 25: 35-37, kumb 23
Hivyo kulikuwa na kundi kubwa la matajiri walioihasi hii sheria ya Mungu, wakawa wanawatoza riba na kujipatia faida isivyo haki, Matokeo yake Wakafanikiwa kujikusanyia mali nyingi kama mavumbi ya ardhini.
(Ayubu 27: 13-16 )
Lakini bado maandiko, yanatoa matokeo au hatma ya watu kama hawa. Mwisho wa siku Mungu anawapokonya na kuligawia kundi lingine la watu lenye kuwahurumia maskini.
Utajiuliza inawezekanikaje..biblia inasema mali ina mbawa, inaweza kupaa ghafla, au ikatumiwa kwa matumizi yasiyo ya muhimu ikapukutika yote, au wewe ukafa ukamwachia mwingine. Lakini kule inapoelekea, sio popote tu ilimradi, hapana, bali ni kwa mtu yule ambaye anawahurumia maskini.
Ndio Mungu anaweza kufanya hivyo..usipoitumia talanta yako vema. Anasema mnyanganyeni yule mwenye moja mkampe yule mwenye 10 (Mathayo 25:28),.Bwana anaweza kukunyang’anya ulichonacho.
Tukiwa watu wa kutenda haki na kuwahurumia maskini, kwa kuwapa vitu, basi tujue kuwa tayari kuna watu wameshaandaliwa kwa ajili ya kutuletea hazina hizo, na watu wenyewe ndio hao waovu, wanaojilimbikizia mabilioni ya pesa katika akaunti zao za benki kwa dhuluma, na hila, na biashara haramu, na sio kwa njia halali.
Hii ni kuonyesha kuwa watu wanaopenda kuwapa wengine vitu, wanayo hazina kubwa sana hapa dunia.
Bwana atusaidie kuzifahamu hekima hizi tupende kuwasaidia watu wanyonge.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.
Kiburi cha Uzima ni nini? (1Yohana 2:16)
Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?
Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?
Utawanyiko wa Wayunani unaozungumziwa katika Yohana 7:35 ulikuwaje?
Jibu: Tuanzie kusoma mstari wa 31, ili tupate maana kamili..
Yohana 7:31 “Na watu wengi katika mkutano wakamwamini; wakasema, Atakapokuja Kristo, je! Atafanya ishara nyingi zaidi kuliko hizi alizozifanya huyu?
32 Mafarisayo wakawasikia mkutano wakinung’unika hivi juu yake; basi wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakatuma watumishi ili wamkamate.
33 Basi Yesu akasema, Bado kitambo kidogo nipo pamoja nanyi; kisha naenda zangu kwake yeye aliyenipeleka.
34 Mtanitafuta wala hamtaniona; nami nilipo ninyi hamwezi kuja.
35 Basi Wayahudi wakasemezana, Huyu atakwenda wapi hata sisi tusimwone? ATI! ATAKWENDA KWA UTAWANYIKO WA WAYUNANI, NA KUWAFUNDISHA WAYUNANI?
36 Ni neno gani hilo alilolisema, Mtanitafuta wala hamtaniona; nami nilipo ninyi hamwezi kuja?”
Kabla ya kujua Utawanyko wa Wayunani ni kitu gani, ni vizuri kwanza kujua Wayunani walikuwa ni watu gani?.. Kujua Wayunani walikuwa ni watu gani unaweza kusoma hapa >>>>Nawiwa na Wayunani na wasio Wayunani.
Sasa tukirudi kwenye swali; “Utawanyiko wa Wayunani ulikuwaje”?.
Jibu ni kwamba, Utawanyiko wa Wayunani halikuwa tukio Fulani lililowatawanya Wayunani, Bali ni lugha iliyotumika kuwatambulisha Wayahudi waliotawanyika na kuishi katika nchi ya Wayunani, iliyokuwa nchi ya watu wa Mataifa.
Kumbuka si Wayahudi wote walikuwa wanaishi katika nchi ya Israeli, walikuwepo wengi waliokuwa wanaishi nchi nyingine za mbali, kama Rumi, Galatia, Misri, Babeli na ikiwemo hii ya Uyunani. Mfano wa hao utaona ni Mtume Paulo, yeye alikuwa ni Muisraeli kwa asili lakini hakuzaliwa Israeli bali katika mji wa Tarso, ambao ulikuwa upo mbali kabisa na nchi ya Israeli.
Na wengine ni wale waliomfuata Filipo na kumwomba awaonyeshe Bwana Yesu..
Yohana 12:20 “ Palikuwa na Wayunani kadha wa kadha miongoni mwa watu waliokwea kwenda kuabudu kwenye sikukuu.
21 Basi hao walimwendea Filipo, mtu wa Bethsaida ya Galilaya, wakamwomba, wakisema, Bwana, sisi tunataka kumwona Yesu”.
Na wakiwa katika hayo mataifa ya ugenini, wengi wao walikuwa bado wanashika dini yao ya kiyahudi, na hata huko walipokuwepo walijenga masinagogi yao ya ibada. (Matendo 13:43). Ni sawasawa na watu wa asili ya India, wanaoishi Tanzania leo, wakiwa huku bado wanajenga mahekalu yao na kuendeleza dini zao, na wayahudi walikuwa hivyo hivyo, walipokuwa huko katika nchi za ugenini. Walijenga mahekalu na kuendeleza desturi zao, kana kwamba wapo Israeli. Ndio maana utaona Petro anaandika waraka mmoja na kuwapelekea Wayahudi hao waliopo sehemu mbali mbali walizotawanyikia..
1Petro 1: 1 “Petro, mtume wa Yesu Kristo, kwa wateule wa Utawanyiko, wakaao hali ya ugeni katika Ponto, na Galatia, na Kapadokia, na Asia, na Bithinia”
Na zipo sababu kuu mbili zilizowafanya Wayahudi baadhi wawepo katika hizo nchi za mataifa.
1.Kuchukuliwa utumwani.
Utumwa wa Babeli, na Ashuru ndio ulikuwa sababu ya kwanza kuwafanya Israeli wabakie katika hizo nchi.. Kwani mbiu ilipotolewa ya Wayahudi warudi nchini kwao, si wote walirejea nyumbani, wengi walisalia katika nchi walizochukuliwa mateka.. na huko wakaendelea na maisha yao kama kawaida.
2. Biashara
Baadhi ya Wayahudi walikuwa wanasafiri kwenda kufanya biashara katika nchi za mbali, hivyo wengi wao walikuwa wanaanza maisha katika hiyo miji waliokuwa wanaiendea.
Kwahiyo sasa, Utawanyiko wa Wayunani tafsiri yake ni “utawanyiko wa Wayahudi waliopo katika nchi ya Uyunani”
Kwahiyo Bwana Yesu alipowaambia Mafarisayo “kwamba mtanitafuta wala hamtaniona”….wenyewe walidhani Bwana ataenda Uyunani kuwahubiria na Wayunani, kwasababu wao wamekataa kumsikiliza.
Lakini Bwana hakumaanisha hivyo, bali alimaanisha kuwa “atakwenda zake kwa Baba (yaani mbinguni)” na “watamtafuta lakini hawatamwona”, na zaidi ya yote wao hawawezi kwenda kule aliko, kwasababu wamemkataa yeye.
Hiyo ikitufundisha kuwa na sisi tukimkataa sasa Bwana Yesu, utafika wakati “tutamtafuta lakini hatutamwona” na kule aliko “sisi hatutaweza kufika”.
Yohana 7:33 “Basi Yesu akasema, Bado kitambo kidogo nipo pamoja nanyi; kisha naenda zangu kwake yeye aliyenipeleka.
34 Mtanitafuta wala hamtaniona; nami nilipo ninyi hamwezi kuja”
Kaka/Dada ambaye bado hujaokoka, ambaye bado unaipuuzia injili kama hawa Mafarisayo, Bwana Yesu anakuambia leo “bado kitambo kidogo nipo na wewe”…. bado anakuvumilia sasa, lakini bado kitambo kidogo atakuacha… za baada ya kukuacha anasema “kule aliko wewe hutaweza kwenda”.
Ni jambo baya sana kuachwa na Mungu!..
Na mtu anaachwaje na Mungu?.. Ni pale anapoisikia injili kwa muda mrefu bila kubadilika!!.. Kikawaida Mungu ni Mungu wa uhuru, huwa hatulazimishi kufanya jambo, anachokifanya yeye kwa ule moyo mgumu, usio na toba, ni kuuacha tu!.. Utauliza hilo tunalisoma wapi katika biblia??.
Warumi 1:28 “Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, MUNGU ALIWAACHA WAFUATE AKILI ZAO ZISIZOFAA, WAYAFANYE YASIYOWAPASA.
29 Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya,
30 wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao,
31 wasio na ufahamu, wenye kuvunja maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema;
32 ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao”.
Tubu dhambi leo kwa kumaanisha kuziacha..na tafuta ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu, kukamilisha wokovu wako na Roho Mtakatifu atakuongoza kule anakotaka yeye uende.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Ni wayahudi wa aina gani wanaotajwa kuwa sinagogi la shetani? (Ufunuo 2:9, Ufunuo 3:9)
Je! wayahudi wote wataokolewa kulingana na Warumi 11:26?
Nini maana ya wokovu watoka kwa Wayahudi? (Yohana 4:22)
Bwana Yesu asifiwe, karibu tena tujifunze maneno ya uzima. Leo nataka tuone jambo ambalo, wengi wetu tuliookoka hatulifahamu kuhusiana na tabia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
Ili tuelewe vema kiini cha somo, naomba tusome hivi vifungu vitatu, kwa umakini sana;
Marko 2:1
Akaingia Kapernaumu tena, baada ya siku kadha wa kadha, ikasikiwa ya kwamba yumo nyumbani.
Mathayo 13:1 “Siku ile Yesu akatoka nyumbani, akaketi kando ya bahari.
2 Wakamkusanyikia makutano mengi, hata akapanda chomboni, akaketi; na ule mkutano wote wakasimama pwani”.
Mathayo 14:13 “Naye Yesu aliposikia; hayo, aliondoka huko katika chombo, akaenda mahali pasipo watu, faraghani. Na makutano waliposikia, walimfuata kwa miguu kutoka mijini mwao.
14 Yesu akatoka, akaona mkutano mkuu, akawahurumia, akawaponya wagonjwa wao”.
Kama tunavyosoma hapo, kuna wakati Bwana Yesu alikaa nyumbani kwake, mahali ambapo panajulikana, kwamfano kama mtu angemuulizia angeambiwa anakaa pale kwenye kaya ile namba Fulani..Utamkuta ameketi kwenye kochi lake, sebuleni kwake, au yupo jikoni kwake anajipikia chai, atakukaribisha na mtazungumza mengi tu.
Soma,
Yohan1:37 “Wale wanafunzi wawili wakamsikia akinena, wakamfuata Yesu.
38 Yesu aligeuka, akawaona wakimfuata, akawaambia, Mnatafuta nini? Wakamwambia, Rabi, (maana yake, Mwalimu), unakaa wapi?
39 Akawaambia, Njoni, nanyi mtaona. Wakaenda, wakaona akaapo, wakakaa kwake siku ile. Nayo ilikuwa yapata saa kumi”.
Lakini upo wakati aliondoka hapo, akaenda katika mazingira ambayo yana watu, lakini hayana nyumba ndio hapo unamwona anatoka nyumbani kwake anakwenda kuketi kando ya bahari.. Sasa kumpata hapa, si kurahisi kama ilivyokuwa nyumbani, Leo hii ni rahisi mtu kukwambia tuonane hoteli Fulani, au nyumba Fulani, kuliko kukwambia tuonane fukweni, wavuvi walipo. Ni ngumu kwasababu hakuna ofisi au makazi pale.
Lakini kama hiyo haitoshi, aliondoka tena huko fukweni ambapo alikuwa anakwenda mara kwa mara kuwafundisha watu, akakaa sehemu isiyokuwa na watu kabisa, maana yake nyikani/ jangwani. Huku ndiko kubaya kabisa, kwasababu hakuna upatikanaji wa mahitaji yoyote ya kijamii. Hakuna maji wala chakula, wala kivuli, ni jua tu, na vumbi..
Lakini katika sehemu zote hizi, watu waliokuwa na shida kwelikweli walimfuata, isipokuwa ni kwa ugumu sana, kwasababu iliwabidi watembee kwa miguu umbali mrefu, kama tunavyosoma hapo juu, waende mahali ambapo hawajui kama watarudi salama, au mizoga.
Na ndio maana kule nyikani, ilifikia hatua wanawafunzi wake wakamwambia Bwana awaage makutano, waende kujitafutia chakula kwasababu wamekaa naye siku tatu, usiku na mchana, bila chochote, watazimia,…Lakini Yesu alijua ni nini anakitengeneza ndani yao.
Mathayo 14:15 “Hata kulipokuwa jioni, wanafunzi wake walimwendea, wakasema, Mahali hapa ni nyika tupu, na saa imekwisha pita; uwaage makutano, waende zao vijijini, wakajinunulie vyakula”.
Ndugu yangu, pindi unapookoka, ni sawa na ile hatua ya kwanza ya Yesu kukaa nyumbani kwake. Wakati huu Kristo anakuwa karibu sana na wewe, mda wowote utampata, itakuwa ni rahisi yeye kuchukuliana na wewe kwa hali zako zote.. Lakini jambo hilo halitaendelea sana..
Ataondoka nyumbani kwake na kwenda ufukweni.. Hapo ndipo itabidi umfuate. Ukikaa katika mazingira yale yale, miezi inaenda miezi inarudi, huonyeshi bidii yoyote kwa Kristo, wewe mwenyewe utashuhudia tu ukame utakaouna moyoni mwako. Utadhani kwamba Kristo amekuacha, kwasababu ile raha uliyokuwa mwanzo, au vile vitu alivyokuwa anakuonyesha mwanzo vimekata. Ukishaona hivyo, hapo ndipo unapaswa ujiongeze, zidisha bidii yako, kufanya ibada, kuomba, kusoma Neno na kujitenga na uovu. Ukizingatia hayo, utaanza kumwona tena akikufundisha..
Lakini hapo napo hatadumu kwa muda mrefu sana kama unavyodhani.. Atapiga hatua nyingine na kwenda nyikani, pasipokuwa na kitu/watu. Na huko nako huna budi kumfuata.. Hapo ndipo inapokugharimu, kuuaga ulimwengu, inapokugharimu, kupoteza nafsi yako kwa ajili yake,. Unamfuata Yesu hujui kesho yako utakula nini, hujui hatma ya maisha yako itakuwaje, unakubali kupukutika naye pale nyikani, huku ukimsikiliza tu,
Wakati huu usijijali sana, ikiwa unahaja kweli na Yesu.. Kwasababu hatua hii ya kujikana nafsi, inafikiwa na wachache, lakini huku ndipo Kristo anajifunua kwa mtu kwa viwango vingine kabisa. Utaona wale makutano walioweza kustahimili naye, siku tatu kule nyikani, bila kitu chochote, walipata faida mbili, ya kwanza ni kupokea uzima wa milele, na ya pili, ni kugawanyiwa mikate, ambayo waliila na kusaza. Sasa mikate pale inafunua, [rizki zao], maana yake ni kuwa Kristo aliwabariki, rizki zao, kule waliporudi, walipata vingi, kupita kiasi mpaka wakasaza, Kama kulikuwa na muuza genge alipata wateja mara mbili zaidi n.k..yaani kwa ufupi uchumi wao ulirekebishwa na Bwana.(Mathayo 14:19-21)
Lakini hiyo yote ilitokana na nini?
Ni kuwa radhi, kujitwika msalaba wako na kumfata Yesu. Hili haliepukiki kwa mtu yeyote anayemaanisha kumfuata Bwana Yesu. Ikiwa hauwi tayari binti kutupa vimini na suruali, na maurembo ya kidunia, kuukana ulimwengu kweli kweli, huwezi kumwona Bwana katika viwango vingine, ikiwa kijana, upo nusu nusu, vuguvugu, mizaha, na matusi, miziki ya kidunia, kubeti, mipira, punyeto, pamoja na udunia vimekutawala, hapo usiseme nimemwona Bwana.
Marko 8:34 “Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate.
35 Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha.
36 Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake?
37 Ama mtu atoe nini badala ya nafsi yake?”
Tukizijua tabia hizi za Bwana Yesu, basi tutajifunza kuwa watu wa kupiga hatua kila siku, kumfikia yeye. Kwasababu Bwana hayupo sehemu moja. Tukatae ukristo mgando.
Bwana atusaidie.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
KUNA WAKATI YESU ATAPITA NA WATU HAWATAJUA.
JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.
LEO WOKOVU UMEFIKA NYUMBANI HUMU
Je! ni sahihi kuning’iniza picha nyumbani mwako kama ya Yesu?
“Bonde la vilio” ni nini katika biblia?(Zaburi 84:6)
Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?
Karibu tujifunze hekima, zilizo katika Neno la Mungu, Tukisoma Mithali 4:30-34 inasema..
30 “Nalipita karibu na shamba la mvivu, Na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili.
31 KUMBE! LOTE PIA LIMEMEA MIIBA; Uso wake ulifunikwa kwa viwawi; Na ukuta wake wa mawe umebomoka.
32 Ndipo nilipoangalia na kufikiri sana; Naliona, nikapata mafundisho.
33 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, Bado kukunja mikono upate usingizi!
34 Hivyo, umaskini wako huja kama mnyang’anyi, Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha”.
Sulemani anaeleza, tukio alilokutana nalo katika shamba la huyu mtu ambaye alimtambua kama mvivu, Na tukio lenyewe lilimtafakarisha sana.. Yeye alidhani, kwa kulala kwake, na kuchelewa kwake kulilima shamba lake, basi ndio litabakia vilevile, bila chochote kuwepo juu yake. Lakini kilichomstaajabisha ni kuona mazao mengi sana, tena makubwa yaliyostawi, lakini hayakuwa yale aliyoyapanda bali ni miiba.
Kuonyesha kuwa shamba halimsubirii wala halimtabui mkulima, kazi yake ni kuchepusha chochote kile kinachokuja kupandwa juu yake.. Kama ni mchicha, kama ni gugu, kama ni mwiba, kama ni mbigili, kama ni bangi, kama ni tumbaku, haijali kipandacho, hiyo ndio tabia ya shamba lolote Maandiko yanasema hivyo katika (Marko 4:26-29)
Hivyo mtu asipowajibika mwenyewe, kusafisha shamba lake, na kuhakikisha, anayatoa yale yasiyostahili, au analipalilia mara kwa mara, ajue kuwa ataangukia hasara, na mwisho wa siku kazi yake inakuwa bure. Sikuzote kazi nzito ya ukulima ipo katika kupalilia na kulitunza shamba, dhiki ya wavamizi, na magugu, na sio katika kupanda. Kwasababu kupanda kunaweza kuchukua siku moja au mbili basi. Lakini kulitunza shamba ni jambo lingine, linalomgharimu mkulima, kila siku awe anaamka asubuhi na mapema, na mara kwa mara kulitembelea shamba lake, kulitazama na kulipalilia.
Mioyo yetu ni mashamba..Chochote kinachopandwa iwe na Mungu, au ibilisi, au mwanadamu, ni lazima kimee tu, tupende tusipende.. Hapo ndipo umakini unapohitajika sana, Hii ndio sababu kwanini maandiko yanasema, tuilinde mioyo yetu kuliko yote tuyalindayo (Mithali 4:23). Kwasababu chochote kile kinamea.
Hivyo, ikiwa huna tabia ya kuutazama tazama moyo wako, basi rohoni unatafsirika kama mvivu wa hali ya juu, unalala, pale unaposema, aaa, kesho nitasoma Neno, wiki ijayo, nitakwenda Ibadani, hujui kuwa shamba lako (moyo wako), unamea miiba usiyoijua wewe na viwavi kila siku…
Ndugu kusema nimeokoka tu, hakutoshi, ni lazima kila siku uhakikishe umeongeza jambo jipya katika maisha yako ya kiroho, jiulize, je! Lile Neno ulilohubiriwa au ulilolisoma, umeliishi vipi katika siku yako, au wiki yako yote. Ni lazima ufanye hivyo kila siku. Usijisahau, ukawa unaikumbuka roho yako, jumapili kwa jumapili, hiyo ni hatari kubwa sana,..Hata hiyo ibada haiwezi kukusaidia chochote, kwasababu magugu ni mengi kuliko ngano, hivyo utalemewa tu, ukristo wako utakuwa ni mzito sana..
Kama hujui kila inapoitwa leo shetani anaturushia mbegu zake mioyoni mwetu, unapopita barabarani na kusikia miziki ya kidunia, unapokuwa ofisini na kusikia lugha za mizaha kwa wafanyakazi wenzako, hizo ni mbegu, unapokuwa shuleni na kusikia matusi kwa wenzako, unapofungua tv, internet, whatsapp, youtube, na kuona mambo yasiyokuwa na maadili, zote hizo ni mbegu, ambazo kama usipozushughulikia mapema ndani ya siku, zitamea tu, haijalishi wewe ni nani…
Hivyo tunazishughulikia , kwa kusali kila siku, kutafakari maneno ya uzima, kujitenga na uovu, kukaa katika utulivu, kuomba rehema, na kujizuia sana. Tukizingatia haya kila siku. Basi mbegu halisi za Mungu tu, ndio zitakazokuwa zinamea mioyoni mwetu. Na matokeo yake tutakuja kula matunda yake baadaye.
Hivyo tusiwe watu, wa kukumbushwa kumbushwa habari za maisha yetu ya kiroho, tuamke usingizini, tuondoe uvivu, tukayatazame mashamba yetu kila siku. Anza sasa kuwajibika kwa kila kitu kinachoukaribia moyo wako, ikiwa hakimpendezi Mungu, hakikisha unashughulika nacho, hadi kiondoke.
Waefeso 5:14 “Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza.
15 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;
16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.
17 Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana”.
Bwana atusaidie.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
NI NANI ATAKAYEUCHUKUA MSALABA WA YESU?
MWENGE WAKO WA UHURU UPO WAPI?
Kwanini Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasichukue chochote isipokuwa fimbo tu?
UTENDAJI KAZI MWINGINE WA ROHO MTAKATIFU USIOUFAHAMU.
Wakati wakina Shadraka wanatupwa katika tanuru la moto, Danieli alikuwa wapi?
Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu..
Je umewahi kujua kuwa mazungumzo mabaya, yanaharibu tabia njema?..
Biblia inasema katika.
1Wakorintho 15:33 “Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema”.
Hapo haisemi, “mazungumzo mabaya yanachochea tabia mbaya”.. La!, bali anasema “yanaharibu tabia njema”. Maana yake mtu mwenye tabia njema, na nzuri na inayovutia, anapoketi kuzungumza, au kusikiliza mazungumzo mabaya, kidogo kidogo anaanza kuiharibu ile tabia yake njema. Haijalishi, hatashiriki hayo mazungumzo, lakini hata kile kitendo cha kusikiliza tu!, tayari tabia yake itaanza kuathiriki.
Ndio maana biblia inatuonya hapo tukae mbali na mazungumzo yote mabaya!..
Na mazungumzo mabaya ni yapi?, ni mazungumzo yote yenye maudhui ya kizinzi, au usengenyaji, umbea, au wizi, au anasa na starehe za kidunia n.k, na mazungumzo haya mabaya yanapatikana katika sehemu zifuatazo.
1.Kwenye Vijiwe.
Vijiwe ni sehemu yoyote watu wanapokutana kujifurahisha kwa maneno, au michezo.. kwamfano vijiwe vya watu wanaocheza michezo ya draft, au bao, wanaobashiri, au mipira n.k..
2. Kwenye mitandao
Unapotumia muda mwingi kukaa kwenye mitandao kama facebook, au whatsapp na unapojiunga kwenye makundi yasiyo ya neno la Mungu, au yasiyo ya na maana, hata kama huchangii chochote katika mijadala inayozungumziwa kule, wewe ni msomaji tu!, fahamu kuwa unaiharibu tabia yako njema.
3. Televisheni.
Unapotazama tamthilia za kidunia, pamoja na vipindi vingine vya kidunia na mijadala na midahalo mbali mbali katika luninga, ambayo maudhui yake ni ya kidunia, fahamu kuwa unaiharibu tabia yako njema, hata kama wewe huchangii chochote, ni mtazamaji tu!.. bado tabia yako inaharibika.
4. Vitabu vya simulizi.
Unapoketi na kusoma vitabu vya simulizi za kidunia, ambazo ni tungo za watu..ambazo nyingi maudhui zake ni kuchochea anasa, uasherati, na wakati mwingine kuamini uchawi.. Vitabu hivyo vinaharibu tabia njema uliyokuwa nayo, vinaharibu tabia nzuri, ambayo pengine Roho Mtakatifu alikuwa ameshaanza kuiimba ndani yako.
Hivyo ukitaka tabia yako isiharibike jihadhari na mambo hayo.. Kama ni mwanaume kaa mbali na kampani mbaya, nenda katika vijiwe kuhubiri injili, lakini si kusikiliza mambo yanayoendelea pale, au kushiriki mijadala yao…kama ni mwanamke au binti, nenda vijiweni kuhubiri lakini si kwenye kusikiliza wala kushiriki mazungumzo yao.
Hebu tujifunze mfano mmoja kwenye biblia ya Binti mmoja aliyekuwa na tabia nzuri, kuliko wenzake wote katika familia yake, lakini siku alipotoka na kwenda kukutana na mabinti wengine wa kidunia, akajikuta kabadilika tabia na kuwa mwingine.
Na msichana huyo si mwingine zaidi ya Yule binti wa Yakobo, aliyeitwa Dina, Hebu tusome habari yake kidogo.
Mwanzo 34:1 “Basi Dina, binti Lea, ambaye Lea alimzalia Yakobo, AKATOKA KUWAONA BINTI ZA NCHI.
2 Shekemu, mwana wa Hamori, Mhivi, mkuu wa nchi, AKAMWONA AKAMTWAA, AKALALA NAYE, AKAMBIKIRI. ”
Umeona chanzo cha Dina kuharibika tabia??.. Si nyingine zaidi ya kutoka na “kwenda kukutana na mabinti wa kidunia”, ambao stori zao ni huenda ni kuzungumzia wanaume tu, na hadhi zao, na Dina akiwa katika kusikiliza akajikuta kashawishika na kujikuta anazini na binti wa mfalme wa nchi, ambaye alikuwa ni mpagani!…Jambo ambalo ni baya sana, mbele za Mungu na mbele ya baba yake Yakobo!
Sasa kujua Dina alikuwa ni binti wa tabia gani hapo kwanza.. hebu tusome tena mstari ufuatao..
Mwanzo 34:19 “Na yule kijana hakukawia kulifanya neno lile, maana amependezewa na binti Yakobo, naye alikuwa MWENYE HESHIMA KULIKO WOTE NYUMBANI MWA BABAYE”.
Umeona?, Dina alikuwa ni mwenye heshima kuliko wote.. lakini ndiye aliye haribika kuliko wote..jambo linalohuzunisha sana!.. Sasa kama mwana wa Yakobo, mrithi wa ahadi za Mungu kaharibiwa.. wewe ni nani usiharibike??..
Kamwe usijivunie tabia yako, na kusema hakuna mtu anayeweza kukubadilisha wala hakuna chochote kitakachoweza kukubadilisha (na huku ni mtu wa kuzunguka katika vijiwe na mitandao).. fahamu kuwa Neno la Mungu ni thabiti.. limesema “tukae mbali na mazungumzo mabaya ili tusiharibu tabia zetu”... wewe na mimi hatuwezi kulisahihisha na kusema “si mazungumzo yanayoweza kumbadilisha mtu, bali ni mtu mwenyewe ndio anayeweza kujibadilisha”.
Watu wengi wanaorudi nyuma katika siku hizi za mwisho ni kwasababu hiyo.. wanazama katika kusikiliza na kushiriki mazungumzo mabaya na hatimaye wanajikuta tayari wameshapoa na kuikana imani kabisa.
Ndugu Kaa mbali na mazungumzo yote mabaya, na kinyume chake, tafuta mazungumzo mazuri ili ujenge tabia yako, na mazungumzo mazuri, utayapata kanisani, na kwenye biblia, na kwenye vipindi au makala za Neno la Mungu.
Bwana Yesu akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
JIHUDHURISHE, ILI AANZISHE MAZUNGUMZO NA WEWE
KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.
NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.
SWALI: Naomba kufahamu biblia inaposema wenye kuhadaa roho zisizo imara ina maana gani? (2Petro 14)
JIBU: Tusome;
2Petro 2:14 “wenye macho yajaayo uzinzi, watu wasiokoma kutenda dhambi, WENYE KUHADAA ROHO ZISIZO IMARA, wenye mioyo iliyozoezwa kutamani, wana wa laana;
15 wakiiacha njia iliyonyoka, wakapotea, wakiifuata njia ya Balaamu, mwana wa Beori, aliyependa ujira wa udhalimu;
16 lakini alikaripiwa kwa uhalifu wake mwenyewe; punda, asiyeweza kusema, akinena kwa sauti ya kibinadamu, aliuzuia wazimu wa nabii yule.
17 Hawa ni visima visivyo na maji, na mawingu yachukuliwayo na tufani, ambao weusi wa giza ni akiba waliyowekewa”.
Katika siku za mwisho biblia inatabiri kuwa litatokea kundi Fulani la watu mahususi, lenye kazi ya “kuhadaa roho za watu watu”.
Kuhadaa ni kudanganya, Lakini biblia bado haisemi kundi hili litahadaa kila mtu tu, hapana bali inasema, litahadaa watu “wenye roho zisizo imara”.
Kwa kawaida kitu kisicho imara ni kitu kisichoweza kudumu kwa muda mrefu, kisichoweza kustahimili mazingira ya mtikisiko, au mazingira magumu kwa muda mrefu kwasababu kimeundwa chini ya ubora. Kwamfano, ukinunua kiatu cha ngozi, na mwingine akanunua kile cha plastiki, mkavitembelea wote kwa pamoja, utaona baada ya muda mfupi kile cha plastiki, kinachakaa na kuisha kabisa, lakini kile cha ngozi kinaendelea kudumu, Kwasababu gani? Ni kwasababu kiatu kile cha plastiki sio imara.
Vivyo hivyo katika roho siku hizi za mwisho, Kuna wakristo walio imara, na wengine ambao sio imara, kuna wenye nguvu ya kudumu katika wokovu haijalishi ni mitikisiko mingapi inawakumba kwasababu hapo mwanzo walimaanisha kweli kweli kumfuata Kristo.. Hawa wana heri sana, ibilisi hawezi kuwahadaa.
Lakini kundi lililo hatarini ni hili ambalo leo linaokoka kwa Bwana, kesho linarudi nyuma, leo ni moto kesho ni vuguvugu, leo linahudhuria mikesha, kesho linasahau, leo linaeleweka, kesho halieleweki, leo lipo ibadani wiki ijayo halifiki kabisa, likiwa na wapendwa linazungumza habari za Mungu, lakini likikaa na watu wa kidunia, linabadilika rangi, linafanana na wao. Lipo hapo katikati, Kudondoka kiwepesi katika dhambi ni jambo la kawaida kwao, ukiliuliza mbona umefanya hivi litakuambia nimepitiwa tu na shetani.
Sasa watu kama hawa ni lazima shetani atawahadaa tu,kwa hila zake, Na watakapodanganywa hawawezi kufahamu kwasababu wao ni roho zisizo imara. Kama Balaamu alipowahadaa wana wa Israeli, kwa kuwashawishi wazini, na mwisho wa siku Mungu akawapiga kule jangwani, Pale Edeni Hawa alipodanganywa na nyoka hakujua chochote, kwasababu moyo wake haukuwa imara kwa Mungu.
Ndugu kama na wewe ni mmojawapo tubu dhambi mgeukie Bwana, kisha maanisha kabisa kumfuata Yesu kwa gharama zozote, Kumbuka hizi ni nyakati za mwisho. Watu waliovuguvugu Bwana ameahidi kuwatapika, na wewe angalia usitapikwe. Au kudanganywa na ibilisi. Simama imara kwa Bwana. Kataa ukristo feki, au wa juu juu usioingia gharama.
1Wakorintho 16:13 “Kesheni, simameni imara katika Imani, fanyeni kiume, mkawe hodari”.
1Wathesalonike 3:12 “Bwana na awaongeze na kuwazidisha katika upendo, ninyi kwa ninyi, na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tulivyo kwenu;
13 apate kuifanya imara mioyo yenu iwe bila lawama katika utakatifu mbele za Mungu, Baba yetu, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu pamoja na watakatifu wake wote”.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
kwanini yule kijana aliitupa ile nguo ya kitani chini na kukimbia uchi?
Ni mlima gani Yule Mwanamke Msamaria aliokuwa anaumaanisha? (Yohana 4:19)
Ni wayahudi wa aina gani wanaotajwa kuwa sinagogi la shetani? (Ufunuo 2:9, Ufunuo 3:9)
Nini maana ya siku moja kwa Bwana ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja? (2Petro 3:8)
SWALI: Nini maana ya huu mstari? Hapo anaposema yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.
Mhubiri 10:8
[8]Mwenye kuchimba shimo atatumbukia ndani yake; Na yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.
JIBU: Mistari hiyo inawazumgumzia watu ambao wanasababisha matatizo kwa wenzao. Au watu wanaowakosesha wengine waliokuwa tayari katika njia sahihi.
Na ndio maana hapo anaanza kwa kusema mwenye kuchimba shimo atatumbukia ndani yake..Akiwa na maana kuwa dhara lile unalolipanga kwa mwingine limpate ndilo hilo hilo litakupata wewe.
Mfano wa watu kama hawa katika biblia ni Hamani, ambaye alikua adui wa Mordekai na wayahudi wote, mpaka akafikia hatua ya kumtengenezea msalaba Mordekai, lakini kinyume chake msalaba ule ndio ukamtundika yeye mwenyewe.
Lakini kwenye hicho kipengele cha pili anasema Na yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.. Maana yake ni kuwa maboma sikuzote hujengwa kwa lengo la kudhibiti maadui, tukiachilia mbali wanadamu, lakini pia wanyama wakali kama fisi, mbweha na nyoka wasivamie mifugo.
Hivyo anaposema abomoaye boma..anamaanisha aondoaye ulinzi wa mwenzake ili maadui kama nyoka wapite, wawadhuru, kinyume chake atadhurika yeye.
Hii ikifunua nini?
Wapo watu leo hii, wanaoondoa maboma ya watu wengine kwa hila zao. Na maboma yanayomaanishwa hapo si mengine zaidi ya YESU KRISTO. Yeye ndio boma letu, Biblia inasema hivyo..
Zaburi 18:2
[2]BWANA ni jabali langu, na boma langu, na mwokozi wangu, Mungu wangu, mwamba wangu ninayemkimbilia, Ngao yangu, na pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu.
Hivyo watu watu wanawakosesha kwa kuwalaghai ili ibilisi awameze, wanawazuia wasimwabudu Mungu sawasawa na mapenzi yake, wanawazuia wasimwombe Mungu wao, ili wapoe..lakini kinyume chake wao ndio watamezwa. Na Bwana atawaponya watu wake.
Mfano wa watu kama hawa,ni wale maliwali wa Umedi waliompangia visa Danieli, ili asimwombe Mungu wake, kutwa mara tatu. Wakidhani kuwa ndio atapotelea mbali kwenye tundu la simba. Lakini kinyume chake wao ndio walimezwa na ibilisi.
Hivyo kamwe usijaribu kumkosesha mtu wa Mungu, wala usijaribu kumwondolea boma lake (Yesu Kristo), ukadhani ndio tayari atarudi nyuma. Wewe ndio utarudishwa nyuma na shetani.
Tusiwe watu wa kusababisha mabaya/madhara kwa wengine. Ndio kiini cha mistari hiyo.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Wale Nyoka wa Moto jangwani, walikuwa ni wa namna gani?
JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.
Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?
Mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili