Category Archive Home

KONDE LA DAMU (Akeldama).

Shalom, karibu tujifunze biblia.

Leo napenda tujifunze juu ya lile Konde Yuda alilolinunua.. Biblia inaliita kuwa ni “konde la Damu”. Tafsiri na konde ni “shamba/kiwanja”.. Hivyo Konde lolote lililopatikana au kununuliwa kwa fedha za mauaji lilijulikana kama “konde la damu”.

Na maandiko yanaonyesha kuwa Yuda alilinunua shamba kwa fedha/kima cha mauaji.. Na hakulinunua kwa matakwa yake, bali Maukuhani ndio waliokwenda kulinunua, lakini hati ya kile kiwanja ikaandikwa kwa jina la YUDA!.. kwasababu ni fedha zake ndizo zilizonunulia kiwanja hicho..

Sasa tendo walilolifanya makuhani kwenda kununua mahali pa kuzika wageni lilikuwa ni tendo la heshima na lenye kugusa hisia za wengi, kwani katika desturi za wayahudi ilikuwa wageni na Wayahudi hawazikwi mahali pamoja, sasa ilikuwepo changamoto ya wageni kutoka mbali wanaokuja Yerusalemu na kufia huko, changamoto ya mahali pa kuwazika ilikuwa kubwa, kwahiyo hawa makuhani kitu walichofanya kilikuwa ni cha kiungwana.. Hivyo wakaenda kununua sehemu ya gharama ya juu, katikati ya Yerusalemu karibu na bonde la mwana wa Hinomu.

Lakini sasa watu walipoulizia ni nani kanunua konde lile na kiasi kilichotolewa, siri ikajulikana kuwa kiwanja kile kilinunuliwa na mtu mmoja (marehemu) aliyeitwa Yuda kwa fedha iliyotokana na kumsaliti Bwana Yesu. Kwahiyo kila aliyepita karibu na kiwanja hicho na kuulizia habari za kiwanja hicho na mmiliki, basi alisimuliwa habari ya Yuda.. Hivyo kiwanja kile kikawa na sifa mbaya kutokana na tukio la Yuda.

Ni sawa sasahivi upite mahali uone jengo limejengwa na linatoa huduma Fulani nzuri…halafu unaambiwa jengo lile limejengwa kwa fedha za ujambazi/mauaji yaani mmiliki wa jengo aliua watu Fulani ili kupata fedha za kujenga hilo jengo. Bila shaka, hata kama lile jengo linafanya kazi nzuri kiasi gani, bado sifa yake itabaki kuwa mbaya. Ndivyo na konde alilolinunua Yuda.

Mathayo 27:3 “Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, alipoona ya kuwa amekwisha kuhukumiwa, alijuta, akawarudishia wakuu wa makuhani na wazee vile vipande thelathini vya fedha, akasema, Nalikosa nilipoisaliti damu isiyo na hatia.

4  Wakasema, Basi, haya yatupasani sisi? Yaangalie haya wewe mwenyewe.

5  Akavitupa vile vipande vya fedha katika hekalu, akaondoka; akaenda, akajinyonga.

6  Wakuu wa makuhani wakavitwaa vile vipande vya fedha, wakasema, Si halali kuviweka katika sanduku ya sadaka, kwa kuwa ni kima cha damu.

7  Wakafanya shauri, wakavitumia kwa kununua konde la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.

8  Kwa hiyo konde lile huitwa konde la damu hata leo”.

Habari hii tunaweza kuisoma tena vizuri katika Matendo 1:16-19.

Matendo 1:16 “ Ndugu, ilipasa andiko litimizwe, alilolinena Roho Mtakatifu zamani kwa kinywa cha Daudi, katika habari za Yuda aliyewaongoza wao waliomkamata Yesu;

17  kwa sababu alikuwa amehesabiwa pamoja na sisi, akapata sehemu ya huduma hii.

18  (Basi mtu huyu alinunua konde kwa ijara ya udhalimu; akaanguka kwa kasi akapasuka matumbo yake yote yakatoka.

19  Ikajulikana na watu wote wakaao Yerusalemu; hata konde lile likaitwa kwa lugha yao Akeldama, maana yake, konde la damu.)”

Ni nini tunajifunza katika habari hii?

1. Ukifanya jambo baya litakuja kujulikana tu hata baada ya kufa kwako!.

Yuda alimsaliti Bwana mbele ya wanafunzi wake 12 tu!, pengine wale wanafunzi wangeshuhudia kuwa Yuda ni msaliti wasingeaminika, lakini LILE KONDE lilikuja kumtangaza Yuda kwa watu wote, hata ambao walikuwa hawamjui walimjua kupitia konde lile. Vile vile Daudi alimfanyia ubaya Uria, kwa kumwua na kumchukua mke wake, jambo lile alilifanya kwa siri, lakini Mungu alikuja kulitangaza mbele ya jua, mpaka leo tunalisoma tukio lile.

2. Mali ya dhuluma ni lazima iishie kuwa na sifa mbaya.

Haijalishi mali ya dhuluma itadumu kuwa na heshima kwa muda gani, utafika wakati heshima yake itapotea na itabaki aibu!!.. Kama umepata nyumba kwa dhuluma mwisho wake utakuwa ni aibu, kama umepata shamba kwa dhuluma mwisho wake utakuwa ni aibu, na kitu kingine chochote kama ni cha dhuluma mwisho wake ni aibu.

Vile vile kama umemwibia Bwana kwa matoleo yako, na ukatumia matoleo yale kufanya mambo yako ikiwemo kununua shamba kama Yuda, basi utaishi kuwa kama Yuda.

Vile vile kama unamsaliti Bwana na injili yake kwa kazi yako, au uzuri wako, au hadhi yako, au fedha zako au kwa chochote kile, basi fahamu kuwa unaelekea mahali pabaya.

Bwana Yesu atusaidie tuishi maisha ya uangalifu.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UNAWAZA NINI SASA, JUU YA UFALME WA MBINGUNI?

LISHIKILIE SANA LILE AGIZO LA KWANZA.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

Je Mtu anaweza kusema uongo, Na Mungu akambariki?

Paulo alikuwa na maana gani aliposema “nimeaminiwa uwakili”

Rudi nyumbani

Print this post

KAZI YA MALAIKA MIKAELI KWA WATU WA MUNGU.

Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe, karibu tuongeze maarifa ya Neno la Mungu.

Leo tutajifunza juu ya Malaika Mikaeli.

Mbinguni kuna aina kuu tatu za Malaika. Wapo malaika wa sifa ambao ndio wale Maserafi na Makerubi, pia wapo malaika wa Ujumbe ambaye ndio kundi la Gabrieli (aliyemletea Mariamu taarifa za kumzaa Bwana Yesu na pia aliyemletea ujumbe Danieli)

Pia wapo malaika wa Vita, ambao kazi yao ni kupambana na nguvu zote za adui zinazoshindana na watu wa Mungu, na hapa ndipo kundi la Mikaeli na wenzake linapotokea.

Sasa inaaminika na baadhi ya watu kuwa Mikaeli ni jina lingine linalomwakilisha Bwana Yesu..lakini kulingana na maandiko hilo jambo si kweli..

Sasa ni kwa namna gani Mikaeli sio Bwana Yesu kulingana na maandiko unaweza kufungua hapa na kusoma >>>Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?

Sasa maswali mawili ya kujiuliza ni je Mikaeli anampigania nani, na anapiganaje?

1. Anampigania nani?

Mikaeli ni malaika wa vita aliyewekwa na Mungu kulipigania Taifa la Israeli na kanisa la Mungu.

Tunalithibitisha hilo kipindi kile ambacho Danieli analetewa ujumbe na Malaika Gabrieli, na kumtaja Mikaeli kuwa amewekwa kusimama upande watu wa Danieli (yaani waisraeli)”.

Danieli12:1 “Wakati huo Mikaeli atasimama, jemadari mkuu, asimamaye upande wa wana wa watu wako…”

Pia unaweza kusoma Danieli 10:21,utaona Mikaeli anatajwa kama Mkuu wa watu wa Danieli

Hivyo Mikaeli ni malaika wa vita kwa ajili ya Taifa la Israeli kwa jinsi ya mwili, na Israeli ya roho ambayo ni kanisa (yaani sisi tuliompokea Yesu).

2. Mikaeli anapiganaje?

Vita vya Mikaeli dhidi ya roho zitufuatiliazo si za kurusha mikuki au mapanga..bali ni za hoja.

Maandiko yanasema shetani anatushitaki usiku na mchana mbele za Mungu (Ufunuo 12:10)..na zaidi sana tafsiri ya jina shetani ni “mshitaki / mchongezi”..hiyo ndio tafsiri ya jina shetani.

Kwahiyo shetani anachokifanya usiku na mchana na kuchukua taarifa zetu mbaya na kuzifikisha mbele za Mungu kama mashitaka, hata kama hataona dosari katika maisha yetu bado tu atafika Kwa Mungu kutuchongea kama alivyofanya kwa Ayubu.

Lakini sasa Mikaeli pamoja na wenzake wanachokifanya ni kupeleka hoja zetu nzuri mbele za Mungu, kamwe hawapeleki mashitaka..Na hoja za Mikaeli zikishinda dhidi ya hoja za shetani juu yetu ndipo hapo tunapata yale yote tuliyomwomba Mungu.

Lakini hoja za shetani zikishinda dhidi ya zile za Mikaeli bali tunakabidhiwa shetani, na hivyo tunawekwa katika mikono ya shetani na kupata madhara…kwasababu Mungu ni Mungu wa haki na hana upendeleo!…Ndio maana Adamu alipoasi Mungu hakumpendelea Adamu na bali aliruhusu shetani ayachukue mamlaka yake, kwasababu ni kweli kayapata kihalali kutoka kwa Adamu.

Kwahiyo vita kati ya shetani na malaika watakatifu si vingine zaidi ya hivyo vya hoja, kila upande unapamba kuvuna watu.

Tunaweza kupata picha zaidi tunaposoma ufunuo alioonyeshwa Yuda ambao alioonyesha kuhusu mwili wa Musa.

Yuda (sio yule aliyemsaliti Bwana) alifunuliwa katika roho jambo ambalo shetani alikuwa analifanya baada tu ya Musa kufa.

Alionyeshwa baada ya Musa kufa kumbe shetani alimfuata Mungu na kuutaka mwili wake, na lengo la kuutaka mwili wake ni wazi kuwa si lingine zaidi ya kutaka kuuweka uabudiwe na watu.

Na alipofika mbele za Mungu, alikuwa na hoja kwanini anautaka ule mwili, na pengine hoja ambayo alikuwa nayo ni lile kosa Musa alilolifanya lililompelekea yeye kufa (la kutompa Mungu utukufu).

Hivyo shetani alikuwa na kila sababu za yeye kuumiliki mwili wa Musa, lakini tunaona kitu cha kipekee ni kwamba wakati anapeleka hayo mashitaka Mikaeli aliyewekwa kwaajili ya kuwatetea Israeli alisimama kumpinga hoja zake hizo, na Mikaeli akatoa hoja zenye nguvu juu ya Musa, na hivyo Mikaeli akashinda na shetani hakukabidhiwa mwili wa Musa, ndio maana mpaka leo hakuna mtu anajua mifupa ya Musa ilipo.(Ni Mungu mwenyewe ndiye  aliyemzika).

Lakini endapo shetani angeshinda hoja mbele ya Mikaeli basi huenda Musa angekufa hemani na watu wangeikusanya mifupa yake na kuiabudu na ufalme wa giza ungestawi zaidi.

Yuda 1:9 “Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee”.

Ndugu mpendwa Ikiwa unasema umeshampokea Yesu halafu bado unafanya uzinzi, basi fahamu kuwa shetani anapeleka mashaka hayo mbele za Mungu mchana na usiku…akidai haki ya kukumiliki wewe.

Lakini matendo yako yakiwa sawasawa na biblia, basi shetani anakosa alama za kukushitaki mbele za Mungu, na kinyume chake Malaika wa Bwana, Mikaeli na kundi lake wanasimama kuyataja mambo yako mazuri mbele za Mungu, wanautazama uso wa Baba na kutaja mema yako kama maandiko yasemavyo..

Mathayo 18:10 “Angalieni msidharau mmojawapo wadogo hawa; kwa maana nawaambia ya kwamba malaika wao mbinguni siku zote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni”

Na kamwe malaika hawapeleki mashtaka mabaya mbele za Mungu kwaajili yetu.

2 Petro 2:11 “Wenye ushupavu, wenye kujikinai, hawatetemeki wakiyatukana matukufu; ijapokuwa malaika ambao ni wakuu zaidi kwa uwezo na nguvu, hawaleti mashitaka mabaya juu yao mbele za Bwana”.

Je umetubu kwa kumaanisha kuacha dhambi?..umeacha wizi?, umeacha usengenyaji?, umeacha ulevi, umeacha uasherati?, umeacha uuaji na hasira?.

Kama bado hujaacha hivyo vyote basi fahamu kuwa ndivyo vinavyokushitaki mbele za Mungu.

Marana tha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?

AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!

Je Musa yupo anawashitaki watu..kulingana na Yohana 5:45?

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

UFUNUO: Mlango wa 14

Rudi nyumbani

Print this post

MAUMIVU  NYUMA-YA-HUDUMA.

Mtu yeyote aliyeokoka (Kwa kumaanisha kabisa), ni lazima Bwana ataweka huduma ndani yake, anaweza akawa mchungaji, au mwinjilisti, au mwalimu, au mwimbaji, shemasi, lakini pia anaweza akawa  mwandishi, mtunza bustani, mratibu wa vipindi, mwasibu wa kanisa,  n.k. maadamu tu zinafanya kazi ya kulihudumia kanisa  la Mungu, na si vinginevyo.

Licha ya kuwa utaifurahia kazi yako na kupata thawabu, lakini uhalisia wake ni kwamba, huduma yoyote Mungu anayokupa haitakuwa nyepesi kama wewe unavyoweza kudhani, yaliyowakuta mitume wakati fulani, yatakukuta na wewe, lakini yatamkuta hata na Yule ambaye atakuja kutumika baadaye.

Haya ni baadhi ya maumivu utakayokutana nayo;

KUACHWA:

2Timotheo 4:10  “Maana Dema aliniacha, akiupenda ulimwengu huu wa sasa, akasafiri kwenda Thesalonike; Kreske amekwenda Galatia; Tito amekwenda Dalmatia”

Tengeneza picha, Wakati ambapo mtume Paulo yupo katika kilele cha utumishi, halafu mtendakazi mwenzake mpendwa, anageuka ghafla, na kumwachwa alijisikiaje. Ni heri angemwacha na kwenda kutumika mahali pengine, lakini anamwacha na kuurudia ulimwengu. Ni maumivu makali  kiasi gani? Ni kuvunjwa moyo kiasi gani?

Mwaka 2016-2018, tulikuwa na rafiki yetu mmoja, hatukudhani kama siku moja tungekaa tutengane, kwasababu tulikuwa tumeshajiwekea malengo mengi makubwa ya kumtumikia Mungu, tuliishi kama Daudi na Yonathani, lakini tulipoanza kupiga hatua tu ya kutekeleza malengo yetu, ghafla alikatisha mawasiliano na sisi, akawa hapokei simu zetu, na baadaye kutu-block kabisa, akaurudia ulimwengu, hadi leo.

Tuyahifadhi haya ili yatakapotokea tusivunjike moyo tukaacha utumishi. Wakina Dema unaweza kupishana nao katika huduma Mungu aliyoweka ndani yako, ila usivunjike moyo.

UPWEKE:

Pale pale Mtume Paulo anamsihi Timotheo asikawie kumfuata, kwasababu Kreske, amekwenda Galatia, Tito, Dalmatia..

2Timotheo 4:9  “Jitahidi kuja kwangu upesi. 10  Maana Dema aliniacha, akiupenda ulimwengu huu wa sasa, akasafiri kwenda Thesalonike; Kreske amekwenda Galatia; Tito amekwenda Dalmatia. 11  Luka peke yake yupo hapa pamoja nami. Umtwae Marko, umlete pamoja nawe, maana anifaa kwa utumishi. 12  Lakini Tikiko nalimpeleka Efeso.

Kundi hili halikuondoka, kwasababu ya kuupenda ulimwengu kama Dema, hapana bali kwasababu ya huduma, hivyo mtume Paulo akabaki peke yake. Kuna wakati alikuwa na kundi kubwa la watenda kazi pamoja naye, lakini upo wakati alibaki peke na Luka tu.. Anamhizi Timotheo afike  pamoja na Marko, ili afarijike katika huduma, hali ya upweke imwache.

Kama mhudumu wa Kristo, zipo nyakati utakuwa peke yako, Hivyo usife moyo, ni vipindi tu vya Muda.

KUACHANA:

Moja ya ziara za mtume Paulo iliyokuwa na mafanikio makubwa sana, basi ni ile ziara ya kwanza. Ni kwasababu gani? Ni kwasababu alikuwa na Barnaba. Wote wawili walikuwa na nia ya Kristo, hawakuwa na fikra za kiulimwengu au kimaisha. Lakini cha kusikitisha hilo halikuendelea sana.. Walipishana kauli, kutokana na kwamba kila mmoja aliona uchaguzi wake ni bora kuliko wa mwingine.. Paulo alitaka kwenda Sila, lakini Barnaba kwenda na Marko. Lakini kama wangetoa tofauti zao, na kuwachukua wote, naamini huduma ingekuwa na mafanikio makubwa zaidi, lakini hilo lilikuwa halina budi kutokea.

Matendo 15:36 “ Baada ya siku kadha wa kadha Paulo akamwambia Barnaba, Haya! Mrejee sasa tukawaangalie hao ndugu katika kila mji tulipolihubiri neno la Bwana, wa hali gani.

37  Barnaba akaazimu kumchukua Yohana aliyeitwa Marko pamoja nao.

38  Bali Paulo hakuona vema kumchukua huyo aliyewaacha huko Pamfilia, asiende nao kazini.

39  Basi palitokea mashindano baina yao hata wakatengana. Barnaba akamchukua Marko akatweka kwenda Kipro”.

Nyakati za kupoteza kiungo chako muhimu katika huduma utapishana nacho.

KUFANYIWA UBAYA:

2Timotheo 4:13  “Lile joho nililoliacha kwa Karpo huko Troa, ujapo ulilete, na vile vitabu, hasa vile vya ngozi. 14  Iskanda, mfua shaba, alionyesha ubaya mwingi kwangu; Bwana atamlipa sawasawa na matendo yake. 15  Nawe ujihadhari na huyo, kwa sababu aliyapinga sana maneno yetu”.

Haijalishi, utampendeza mtu kiasi gani, utafanya wema mwingi namna gani, bado wapo watakaokupinga tu utumishi wako, na zaidi watakuwa ni kama maadui zako. Ni jambo ambalo mtume Paulo hakulitarajia lakini alikumbana nalo baadaye, kutoka kwa Iskanda.. Yaliyomkuta Kristo Bwana wetu kutoka kwa mafarisayo yakamakuta na yeye. Na huwenda yatakukuta na wewe wakati Fulani mbele. Usirudi nyuma.

KUDHANIWA VINGINE:

Watu wengi wanaweza kuchukizwa na wewe kwasababu matarajio yao kwako ni tofauti na walivyokutegemea, hili lilianza tangu wakati wa Bwana alipokuwa duniani. Watu wengi waliosikia habari zake, ikiwemo Yohana mbatizaji, walimtazamia Bwana angekuja kama mfalme Daudi, akipambana na utawala sugu wa kirumi, akivaa nguo za kifalme, akiogopwa na kila mtu. Lakini aliposikia analala kwenye milima ya mizeituni, anaongozana na wavuvi, anakaa na wenye dhambi..Imani ya Yohana ikatetereka kidogo na kutuma watu ili kuulizia kama yeye kweli ndiye, au wamtazamie mwingine..Lakini maneno ya Bwana Yesu yalikuwa ni haya;

“Naye heri awaye yote asiyechukizwa nami” (Mathayo 11:6).

Vivyo hivyo na mtume Paulo, alitarajiwa na wengi kuwa atakuwa ni mtu mkuu kimwonekano, mwenye mavazi ya kikuhani kama waandishi, kutoka na sifa zake, na nyaraka zake, kuvuma duniani kote..lakini walipokutana naye walimwona kama kituko Fulani hivi;

2Wakorintho 10:10  “Maana wasema, Nyaraka zake ni nzito, hodari; bali akiwapo mwenyewe mwilini ni dhaifu, na maneno yake si kitu.

11  Mtu kama huyo na afikiri hivi, ya kwamba jinsi tulivyo kwa maneno katika nyaraka tusipokuwapo, ndivyo tulivyo kwa matendo tukiwapo”

Hivyo si kila mtu atapendezwa na jinsi atakavyokukuta, wengine watakuacha au hawatakuamini kwasababu umekuja nje ya matarajio yao.

KUPUNGUKIWA:

Japokuwa vipo vipindi vyingi vya mafanikio, lakini pia vipo vipindi vya kupungukiwa kabisa. Paulo anamwagiza Timotheo pindi amfuatapo makedonia ambebe joho(Koti) lake, kwa ajili ya ule wakati wa baridi. Kama angekuwa na fedha ya kutosha wakati huo, kulikuwa hakuna haja ya kumwagiza, angenunua lingine tu alipokuwepo.

Mungu hawezi kukuacha, wala kukupungukia kabisa, atakupa, na kukufanikisha, lakini pia vipindi kama hivi utapishana navyo mara kwa mara na ni Mungu mwenyewe anaruhusu. Hivyo usitetereke.

Wafilipi 4:11  “Si kwamba nasema haya kwa kuwa nina mahitaji; maana nimejifunza kuwa radhi na hali yo yote niliyo nayo.

12  Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa. 13  Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”

KUUGUA:

Ukiwa mtumishi, haimaanishi wewe ni malaika, umejitenga na mateso ya hii dunia, Kazi hii itakufanya uumwe wakati mwingine, Timotheo alikuwa anaumwa mara kwa mara tumbo, kwasababu ya mifungo, kuhubiri sana, hivyo akashauriwa na Paulo atumie mvinyo kidogo kwa ajili ya kuweka tumbo lake sawa. Alikuwepo Epafrodito mtume, naye kwasababu ya injili, aliumwa sana, karibu na kufa lakini baadaye Bwana akamponya( Wafilipi 2:25). Elisha alikufa na ugonjwa wake.

Upitiapo vipindi vya magonjwa, usitetereke ukaacha utumishi bali jifariji kwa kupitia mashujaa hawa.

Hivyo, tukiyahifadhi haya moyoni, basi utumishi wetu hautakuwa wa manung’uniko au wa kuvunjika moyo, mara kwa mara. Kwasababu ndio njia ya wote. Hivyo tukaze mwendo katika kumtumikia Bwana, kwasababu malipo yake ni makubwa kuliko mateso tunayopishana nayo. Thawabu za utumishi ni nyingi sana,

Ufunuo 3:11  “Naja upesi. Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako”.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

GHARAMA YA UFALME WA MBINGUNI.

Je Musa yupo anawashitaki watu..kulingana na Yohana 5:45?

Tofauti kati ya mtume na mwanafunzi ni ipi kibiblia?

Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma.

Je mbinguni itakuwa ni kuimba tu wakati wote?

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

KAMA MHUBIRI USIWE MFANO WA DIOTREFE.

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Siku ilihesabiwaje kabla ya jua na mwezi kuumbwa?

Swali: Katika kitabu cha Mwanzo tunasoma jua na mwezi viliumbwa katika siku ya 4 , sasa napenda kujua kabla ya hapo siku zilihesabiwaje, maana jua ndilo linalotenga mchana na usiku…na maandiko yanatuonyesha kuwa lilikuja kuumbwa siku ya 4?

Jibu: Ni kweli jua na mwezi viliumbwa siku ya 4, tena baada ya miti na miche ya kondeni kuumbwa (Mwanzo 1:14).

Lakini ukisoma kuanzia mstari wa pili katika kitabu hiko cha Mwanzo, utaona Mungu tayari alikuwa ameshaumba mchana na usiku na ameshatenga giza na nuru.

Mwanzo 1:1 “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.

2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.

3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru.

4 Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; MUNGU AKATENGA NURU NA GIZA.

5 MUNGU AKAIITA NURU MCHANA, NA GIZA AKALIITA USIKU. IKAWA JIONI IKAWA ASUBUHI, SIKU MOJA”.

Umeona?..kumbe tayari Mungu alikuwa ameshaumba mchana na usiku kabla hata ya kuumba jua. Maana yake hata kama asingeumba jua bado majira na mchana na usiku yangekuwepo kwasababu yeye mwenyewe ndio Nuru ya ulimwengu (mwilini na rohoni).

Yohana 8:12 “Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima”.

Ndio maana katika ile mbingu mpya na nchi mpya hakutakuwepo  na jua na bado Nuru itakuwepo.

Ufunuo 21:23 “Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, kwa maana utukufu wa Mungu huutia nuru, na taa yake ni Mwana-Kondoo”.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kuwa Mungu aliumba mchana na usiku, kabla ya kuliumba jua..na hiyo ni kuonyesha utukufu wake yeye, na pia kuonyesha kuwa yeye ndiye Nuru halisi Na ndio chanzo cha Nuru yote.

Je umempokea Bwana Yesu aliye Nuru ya kweli? Kama bado fahamu kuwa bado upo gizani ijapokuwa jua linakumulika…kwahiyo ni vyema ukafanya maamuzi thabiti leo ya kumpokea na kuokoka.

Yohana 12:46 “Mimi nimekuja ili niwe nuru ya ulimwengu, ili kila mtu aniaminiye mimi asikae gizani”

Soma pia Yohana 9:5 na Yohana 11:9.

Bwana Yesu akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je! mwanadamu wa kwanza kuumbwa ni yupi?

HAMA KUTOKA GIZANI

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

Biblia inamaanisha nini iliposema “wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa;?

Je mke wa Musa alikuwa ni Mweusi?

Rudi nyumbani

Print this post

KWA WINGI WA WASHAURI HUJA WOKOVU.

Nakusalimu katika jina kuu lenye uweza la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze maneno ya Mungu ambayo ndio uzima wetu.

Mungu ana njia nyingi za kuzungumza, anaweza kutumia ufunuo wa roho, anaweza kutumia Neno, anaweza kutumia maono anaweza kutumia mambo ya asili au matukio. Lakini si wakati wote Mungu ataleta majibu kwa kupitia njia hizo. Haijalishi utakuwa ni wa kiroho kiasi gani. Ipo njia nyingine ambayo Mungu huitumia na hiyo tusipoifahamu vema, tutapata hasara ya mambo mengi kama sio kupotea kabisa. Na njia yenyewe ni kupitia mashauri yetu sisi wenyewe tunapokuwa wengi pamoja..

Kwamfano embu tafakari hivi vifungu;

Mithali 11: 14 “Pasipo mashauri taifa huanguka; Bali kwa wingi wa washauri huja wokovu”

Maana yake ni nini? Kwamba taifa linapokataa maoni, mapendekezo, mawazo mbalimbali, kutoka kwa wananchi wake, kamwe taifa hilo haliwezi kufanikiwa,

Maandiko bado yanasema..

Mithali 15: 22 “Pasipo mashauri makusudi hubatilika; Bali kwa wingi wa washauri huthibithika”.

Mithali 24:6 “Maana kwa mashauri ya akili utafanya vita; Na kwa wingi wa washauri huja wokovu”.

Maana yake ni nini? Kwamba palipo na vita, ni lazima yawepo maono ya askari wengi, ni jinsi gani watapambana na adui yao, huyu anasema hivi, Yule vile, na mwisho wa siku linatoka jawabu moja madhubuti ambalo litaleta mafanikio makubwa, lakini ikiwa pendekezo linatoka kwa mmoja tu yaani yule mkuu wa kikosi, ni dhahiri kuwa jeshi, litakuwa dhaifu, na matokeo yake ni kupigwa..

Amen.

Hili ni jambo la muhimu sana kwa sisi tulio wakristo. Bwana Yesu aliposema tuwe na umoja, tunie mamoja, alijua kabisa atatumia njia hiyo kuleta majibu ya mambo mengi pasipo hata kusubiria mafunuo au maono.

Utauliza jambo hili lilifanyika wapi katika kanisa kwenye agano jipya.

Utakumbuka, Paulo na Barnaba walipokwenda kuhubiri injili kwa watu wa mataifa, walitokea wayahudi kadha wa kadha, wakaanza kuwaambia mataifa kuwa msipotahiriwa ninyi hamwezi kuokoka()..Hivyo jambo hilo likaleta mkanganyiko mkubwa sana, ikawabidi hadi Paulo na Barnaba warudi Yerusalemu wakasikilize mitume na wazee wanasema nini juu ya hilo.

Hivyo walipofika Yerusalemu, akina Petro na wazee, waliitisha baraza, na kuanza kulitathimini jambo hilo. Je ni sawa watahiriwe na kuishika torati ya Musa au sio sawa.. Sasa maandiko yanatuambia walihojiana sana, huyu anasema hivi, yule vile (Lakini katika amani na upendo, na sio katika mashindano).. na matokeo yake Roho wa hekima akaingia ndani yao, likapatikana shauri moja thabiti. Na kwa kupitia hilo kanisa la mataifa likathibitika sana kwa waraka waliowaandikia, likaenenda katika furaha ya Roho Mtakatifu daima.

Embu tusome pale kidogo, litusaidie…

Matendo 15:7  “NA BAADA YA HOJA nyingi Petro akasimama, akawaambia, Ndugu zangu, ninyi mnajua ya kuwa tangu siku za kwanza Mungu alichagua miongoni mwenu ya kwamba Mataifa walisikie neno la Injili kwa kinywa changu, na kuliamini.

8  Na Mungu, ajuaye mioyo ya watu, akawashuhudia, akiwapa Roho Mtakatifu vile vile kama alivyotupa sisi;

9  wala hakufanya tofauti kati yetu sisi na wao, akiwasafisha mioyo yao kwa imani…..

13  Na hao walipokwisha kunyamaza Yakobo akajibu, akisema, Ndugu zangu, nisikilizeni.

14  Simeoni ametueleza jinsi Mungu hapo kwanza alivyowaangalia Mataifa ili achague watu katika hao kwa ajili ya jina lake.

15  Na maneno ya manabii yapatana na hayo, kama ilivyoandikwa, 16  Baada ya mambo haya nitarejea, Nami nitaijenga tena nyumba ya Daudi iliyoanguka. Nitajenga tena maanguko yake, Nami nitaisimamisha;”

Kwa muda wako isome habari yote katika kitabu hicho cha Matendo ya mitume sura ya kumi na tano (15),

NINI BWANA ANATAKA SISI TUJUE  KAMA KANISA?

Lazima  tujifunze wakati mwingine tuwe watu wa Hoja nyingi, mapendekezo mengi, (lakini katika upendo na amani), ili kanisa lijengwe, ili injili ihubiriwe katika ufasaha wote. Kama tulivyosoma hapo juu inavyosema.. “kwa mashauri ya akili utafanya vita; Na kwa wingi wa washauri huja wokovu.” Hatutaweza kushindana na shetani kama tutakuwa hatuna mikakati, na mipango ya mara kwa mara,.

Kila kiungo katika mwili wa Kristo, kina nafasi ya kuchagia mashauri mema. Hivyo tujifunze njia hii, ili Mungu azungumze na sisi. Lakini tukikosa mapatano, “Taifa huangamia”..Sisi hatutaangamia kwa kutii agizo hili.

Bwana alibariki kanisa lake.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

Ni kwa namna gani, upendo husitiri wingi wa dhambi? (1Petro 4:8)

Na ulimi laini huvunja mfupa.(Mithali 25:15)

JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?

MITHALI AU METHALI ZA BIBLIA

Rudi nyumbani

Print this post

NAYAJUA MATENDO YAKO.

Mara kadhaa, Bwana Yesu kabla hajasema Neno lolote alianza kwanza na kauli hii “Nayajua matendo yako” Kwamfano Soma vifungu hivi uone alivyosema, (Ufunuo 2:2, 2:19, 3:1, 3:8).

Nikwanini aanze kwa kusema hivyo? Ni kwasababu anataka hilo tuliweke akilini, tufahamu kuwa yupo karibu sana na hatua zetu kuliko tunavyoweza kudhani, hususani zile ambazo tunafikiri kuwa yeye hazijui, au hazioni.  Tutawaficha wanadamu lakini yeye kamwe hatuwezi kumficha chochote.

Wewe ni mchungaji, unazini na washirika, unazungumza lugha za mizaha na wake za watu, unadhani Kristo hajui nia yako, halafu unasimama madhabahuni unahubiri habari za wokovu..Bwana anakupa onyo, tena kali sana, anayajua matendo yako, na hasira yake ipo juu yako.

Wewe ni mkristo, unasema umeokoka, umebatizwa, unashiriki meza ya Bwana, lakini kwa siri unatazama picha za ngono, unafanya uasherati..Ukija kanisani unasema Bwana Asifiwe! Tena bila aibu unasimama na madhabahuni kuimba..utamficha mchungaji, utawaficha washirika wote, utamficha hata na shetani..Lakini Yesu anayajua matendo yako nje-ndani..Anajua mnapokutania, mnapotekelezea mipango yenu miovu, anajua ni nini unachofanya unapokuwa chumbani mwenyewe.

Wewe ni mwanandoa, unaigiza kwamba unampenda mwenzi wako, muwapo pamoja, lakini akisafiri kidogo tu, mkiwa mbali, unachepuka, mke umetoa mimba nyingi, na huko nje wewe mume umezaa watoto, hata mkeo haujui, unadhani unamficha  nani rafiki? .

Leo hii lipo kundi kubwa la washirikina  miongoni mwa watakatifu, tukiachilia mbali wachawi, lakini cha ajabu hujawahi kumsikia hata mmoja akijivunia kazi yake hiyo au akijitangaza? Wameficha hirizi chini ya biashara zao, wana mazindiko kwenye nyumba zao, wanajifanya wana maadili na hodari wa kusema AMEEN!!..Lakini hawajui kuwa Bwana anayajua matendo yao.

Ufunuo 3:1  “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Sardi andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye na hizo Roho saba za Mungu, na zile nyota saba. NAYAJUA MATENDO YAKO, ya kuwa una jina la kuwa hai, nawe umekufa.

2  Uwe mwenye kukesha, ukayaimarishe mambo yaliyosalia, yanayotaka kufa. Maana sikuona matendo yako kuwa yametimilika mbele za Mungu wangu.

3  Basi kumbuka jinsi ulivyopokea, na jinsi ulivyosikia; yashike hayo na kutubu. Walakini usipokesha, nitakuja kama mwivi, wala hutaijua saa nitakayokuja kwako”

Ndugu ni heri ukatubu, uwe na amani na Kristo katika nyakazi hizi za hatari, kwasababu ukiendelea na hali hiyo hiyo utakufa na kwenda kuzimu, na adhabu yako itakuwa ni kubwa sana.

Bwana anasema…

“Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema”. (Mithali 28:13)

Leo hii ziungame dhambi zako, usiyafiche moyoni hayo unayoyafanya, wala usione aibu, wakati ndio sasa, hata kama umeshindwa kuacha, au hujui cha kufanya kwa uliyoyatenda, embu mfuate kiongozi wako wa kiroho mshirikishe akupe ushauri,.aombe pamoja na wewe,  Ili Bwana akusamehe makosa hayo uliyoyofanya.

Unachopaswa kufanya ni kutubu tu kwa kumaanisha..Ukiwa na nia kweli ya kuacha, ili Bwana atakusamehe na kukusaidia kuyashinda, lakini ukiwa upo vuguvugu, hueleweki, bado unayo hatia ya dhambi..kwasababu anayajua matendo yako.

Ufunuo 3:15  “NAYAJUA MATENDO YAKO, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

16  Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa change”.

Jimimine kwelikweli kwa YESU akusaidie..Wakati wa Yesu kuyahukumu mambo yote ya sirini, umekaribia sana, Hukumu ipo karibu. Jiepushe nayo. (Warumi 2:16, 1Wakor 4:5). Ni wakati wa lala-salama.

Ikiwa utapenda kupata msaada huo wa kumkaribisha tena Kristo upya maishani mwako. Basi waweza wasiliana nasi kwa namba hizi kwa ajili ya mwongozo huo bure. +255693036618 / +255789001312.

Bwana akubariki.

Shalom. (Bwana Yesu anarudi).

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KUONGOZWA SALA YA TOBA

NINI MAANA YA KUTUBU

TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU

SEMA KWA LUGHA NYINGINE.

Kupiga ramli ni nini katika biblia?

Kumwambia mtu mwenye dhambi kuwa atakwenda kuzimu asipotubu Je! ni kuhukumu?

Rudi nyumbani

Print this post

NI UTUKUFU WA MUNGU KUFICHA JAMBO.

Jina la Mkuu wa Uzima, Simba wa kabila la Yuda na Mungu katika mwili, YESU KRISTO libarikiwe!.

Kuna mambo ambayo ni muhimu kuyajua sisi kama watu wa Mungu ili tuende sawa na Mungu na pia ili tuwe na amani kama maandiko ya avyotuelekeza katika Ayubu 22:21.

Ayubu 22:21 “Mjue sana Mungu, ili uwe na amani; Ndivyo mema yatakavyokujia”

Ipo tabia moja ya Mungu ambayo ni muhimu kuijua ili tuishi kwa amani.

Na tabia yenyewe ni kuficha jambo/mambo. Biblia inasema hivyo katika…Mithali 25:2

Mithali 25:2 “Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo…”.

Mpaka mwenyewe anasema kuwa ni utukufu wake kuficha jambo…maana yake ni kuwa hiyo ni fahari yake yeye kufanya hivyo, hatuwezi kumbadilisha…

Kwahiyo ukiona ni kwanini kakuficha jambo fulani usilijue au usilipate kwa wakati fulani unaotoka wewe ni kwasababu ndivyo ilivyompendeza, anafanya hivyo kwa utukufu wake.. Na anafanya hivyo kwa watu wote wala hana upendeleo.. Wala usijione unayo mikosi unapojikuta hujui kitu au kinapokuwa ni kigumu kukipata.

Ukiona ni kwanini humwoni Mungu sasa kwa sura na mwonekano…ni kwasababu ni utukufu wake yeye kufanya hivyo..

Sasa ni nini anachotaka kwetu kutokana na hiyo tabia yake.

Anachotaka kutoka kwetu ni sisi TUTAFUTE KWA BIDII MPAKA TUPATE.

Luka 11:9 “Nami nawaambia, Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa”

Ukitaka kumjua Mungu kwa viwango vya juu, haiwezi kuwa ni jambo la kulala na kuamka tu!..hapana! Inahitajika bidii sana katika kumtafuta..

Yeremia 29:12 “Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.

13 Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote”.

Vile vile ukitaka kuwa Mkamilifu si suala la kufumba na kufumbua tu, bali inahitajika bidii sana kuutafuta utakatifu na ukamilifu..kujazwa na Roho Mtakatifu ni hatua ya awali, baada ya hapo ni kuongeza juhudi kila siku, ndivyo maandiko yanavyosema katika Waebrania 12:14.

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”

Na mambo mengine yote ya KiMungu yaliyo mazuri yamefichwa na Mungu mwenyewe Na hayapatikani kwa njia nyingine yoyote isipokuwa kwa kutafuta kwa bidii.

Na hatuwezi kumwuliza kwanini ayafiche hivyo!…ni fahari yake yeye na kwa utukufu wake

Tukitaka kuyavumbua basi ni sharti tuyatafute.

Dada/kaka anza leo kumtafuta Mungu kwa bidii sana, kwasababu anapatikana..adhimia kumtafuta kama Daudi…..

Zaburi 27:8 “Uliposema, Nitafuteni uso wangu, Moyo wangu umekuambia, BWANA, uso wako nitautafuta”

Tumia muda mwingi katika kutafuta kuliko kungoja, tumia muda mwingi katika kutafuta kuliko kunung’unika. Na Bwana atakufunulia.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TAFUTA KWA BIDII KUWA MTAKATIFU.

Kwanini Eliya alijulikana kama “Eliya Mtishbi”?

Sadaka ya Amani ilikuwaje?

Je Mungu ana njia ngapi za kuzungumza?

Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake

Rudi nyumbani

Print this post

Paulo alikuwa na maana gani aliposema “nimeaminiwa uwakili”

SWALI: Mtume Paulo alikuwa na maana gani aliposema “nimeaminiwa uwakili”?

1Wakorintho 9:16  “Maana, ijapokuwa naihubiri Injili, sina la kujisifia; maana nimewekewa sharti; tena ole wangu nisipoihubiri Injili! 17  Maana nikiitenda kazi hii kwa hiari yangu nina thawabu; ila ikiwa si kwa hiari yangu, nimeaminiwa uwakili”.


JIBU: Mtume Paulo aliifanya kazi ya Mungu, kana kwamba ni muajiwa/kibarua aliyepewa dhamana ya kusimamia kazi zote alizowekewa chini yake kwa uangalifu, kana kwamba akipoteza chochote au akileta hasara ya jambo lolote atawajibishwa, na boss wake utakapofika muda wa mahesabu.

Tofauti na mtu aliyejitolea tu kazi, kama kusaidia, mtu wa namna hiyo hata akiacha wakati wowote, hawezi kuwajibishwa zaidi sana atapewa shukrani, kwa kutoa mchango wake katika shughuli hiyo, na kupewa viposho.

Ndio maana ya hiyo kauli, “nimeaminiwa uwakili”..kwa lugha nyepesi “nimeamiwa kazi ya mtu mwingine niisimamie kama kijakazi” Na hiyo ndiyo iliyompelekea Mtume Paulo, kusema mimi ni ‘mtumwa na mfungwa’ wa Yesu Kristo (Warumi 1:1,Waefeso 3:1).. Kwasababu hiyo akaitenda kazi ya Mungu kwa uaminifu wote, na kwa umakini wote, hata zaidi ya mitume wengine.

Ni funzo gani tunalipata.

Nasi pia tukiichukulia kazi ya Mungu kama sio jambo la hiari, au la kujitolea tu, bali kama ndio sehemu ya kazi yetu tuliyoajiriwa na Mungu hapa duniani, na kwamba tusipoifanya kwa uaminifu tukaleta hasara, tutatolea hesabu yake siku ya mwisho,..

Yaani tukimtumikia Mungu kama vile tuzitumikiavyo kazi zetu maofisi, bila kuwa na udhuru wowote.

basi tutajifunza kuitenda bila ulegevu Na mwisho wake utakuwa ni kupewa thawabu kubwa na kutukuzwa sana na Bwana Yesu  tutakapofika kule mbinguni.

Lakini kama tutajitoa kwa Mungu pale tunapojisikia tu, au tunapokuwa na nafasi, au tunapokumbushwa, au tunapofanikiwa sisi si watumwa au wafungwa wa Yesu Kristo, bali ni watumishi wake tu. Hatujafikia hatua hiyo ya kuitwa watumwa wake.

Bwana atujalie utumishi bora, kama huo, wa kuaminiwa uwakili

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JIFANYIE RAFIKI KWA MALI YA UDHALIMU.

Mungu alikuwa anaongea na nani aliposema na “Tumfanye mtu kwa mfano wetu”

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

Pesa za bindoni ni nini?(Marko 6:8)

Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.

UTAMBUE UJUMBE WA SAA UNAYOISHI.

Rudi nyumbani

Print this post

KAMA MHUBIRI USIWE MFANO WA DIOTREFE.

Je! Unamjua Diotrefe katika biblia?

Diotrefe alikuwa ni kiongozi katika kanisa moja ambalo mtu wa Mungu ,Gayo alikuwa akishiriki. Kiongozi huyu alianza vizuri na Bwana lakini mwisho wake ulikuwa mbaya.. mpaka Mtume Yohana anamwandikia Gayo waraka juu yake,  ili asiziige tabia zake..

Hebu tumsome huyu Diotrefe jinsi alivyokuwa na tabia zake..

3Yohana 1:8 “Basi imetupasa sisi kuwakaribisha watu kama hao, ili tuwe watenda kazi pamoja na kweli.

9  Naliliandikia kanisa neno, lakini Diotrefe, apendaye kuwa wa kwanza kati yao, hatukubali.

10  Kwa hiyo, nikija, nitayakumbuka matendo yake atendayo, atoavyo upuzi juu yetu kwa maneno maovu; wala hatoshwi na hayo, ila yeye mwenyewe hawakaribishi hao ndugu, na wale watakao kuwakaribisha, huwazuia, na kuwatoa katika kanisa”.

Sasa hebu tuzitazame hizi tabia 4 Diotrefe alizokuwa nazo.

1: ANAPENDA KUWA WA KWANZA:

 Hii ni tabia ya kwanza Diotrefe aliyokuwa nayo;  Sasa Kupenda kuwa wa kwanza si jambo baya, lakini mtu anapotaka kuwa wa kwanza kwa lengo la kutukuzwa na watu, au kwa lengo la kuwatawala wa wengine, au kwa lengo la kutumikiwa.. hususani ndani ya kanisa, basi hiyo ni mbaya sana na ni kinyume na Neno la Mungu..

Kwasababu Bwana Yesu alisema..

Mathayo 20:25  “Lakini Yesu akawaita, akasema, Mwajua ya kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha.

26  LAKINI HAITAKUWA HIVYO KWENU; BALI MTU YE YOTE ANAYETAKA KUWA MKUBWA KWENU, NA AWE MTUMISHI WENU;

27  NA MTU YE YOTE ANAYETAKA KUWA WA KWANZA KWENU NA AWE MTUMWA WENU;

28  kama vile Mwana wa Adamu asivyokuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi”.

Kwahiyo kama Mhubiri wa Injili: Katika nafasi yoyote uliyopo aidha ni Mchungaji, au Mwalimu, au Nabii, au Mtume au Mwimbaji kumbuka kuwa unapaswa uwe Mtumwa wa wote!, kama unataka kuwa wa Kwanza, lakini kamwe usijiinue wala usitafute utukufu wa wanadamu kama huyu Diotrefe. Ni hatari kubwa!

2. ANANENA MANENO YA UPUUZI  JUU YA MITUME

Hii ni tabia ya pili Diotrefe aliyokuwa nayo.. Alikuwa anawachafua Mitume wa Bwana Yesu (Ikiwemo Yohana, Mtume wa Yesu ambaye alipendwa sana na Bwana Yesu). Ijapokuwa aliwajua kuwa wamechaguliwa na Bwana lakini yeye aliwachafua kwa maneno mabaya na kuwafanya waonekane si kitu mbele ya kanisa la Mungu…Na hiyo yote ni kutokana na wivu.

Roho hii pia ipo kwa baadhi ya watu, ambao kutokana na Wivu, basi wapo radhi hata kuwachafua watumishi wa kweli wa Mungu, na huku mioyoni wakishuhudiwa kuwa wanawachafua ni watumishi wa kweli wa Mungu, lakini kutokana na wivu wanaendelea tu kuwachafua!,.. Hili ni jambo la kuzingatia sana  wewe kama Mwimbaji, au Mchungaji, au Mtume au Nabii au Mwinjilisti.

3. HAWAKARIBISHI NDUGU

Hii ni tabia ya tatu ambayo Diotrefe alikuwa anaionyesha katika kanisa… Yeye alikuwa ni kiongozi lakini kamwe hakutaka kupokea Watumishi wengine waliokuja kuhubiri katika mitaa yake, au mji wake, au waliokuwa wakipita njia yake kuelekea sehemu nyingine kuhubiri. Na sababu ya kufanya hivyo ni ile ile ya wivu na kutaka kuwa wa kwanza..

 Aliona kama mtu mwingine akija kuhubiri katika mji wake basi yeye hadhi yake, au heshima yake itashuka, na Yule alitakayekuja atatukuzwa zaidi..Hivyo hiyo roho ikampelekea mpaka kukataa kupokea wahubiri walio wageni.

Vile vile na sisi hatuna budi kuikataa hiyo roho kwasababu ni roho kutoka kwa Yule adui, siku zote hatuna budi kuwakubali na kuwakaribisha Watumishi wengine wanaotaka kuja kuhubiri maeneo tuliyopo, maadamu tumewahakiki kuwa kweli ni watumishi wa Mungu kwa Neno la Mungu, na wamekuja kwa nia ya kuhubiri injili.

4. ALIWAZUIA WATU WENGINE WASIWAKARIBISHE NDUGU

Hii ni tabia ya mwisho aliyoionyesha huyu Diotrefe.. Hakuridhika tu kuwakataa Mitume waliokuja kuhubiri pande zake, bali pia aliwakataza washirika wa kanisa lile wasimpokee mtumishi mwingine yoyote atakayekuja kuomba hifadhi kwao, kwaajili ya kuhubiri injili.. Na hakuishia hapo, bali aliendelea na kuwafukuza katika kanisa wale wote waliodhubutu kuwakaribisha Mitume. (Uone jinsi hii roho ilivyoenda mbali).

Lakini huyu Diotrefe hakuanza hivi.. Alianza vizuri tu!, ndio maana hata akafikia hatua ya kuwa kiongozi wa Makanisa (Huenda alikuwa Askofu).  Lakini roho nyingine ya kujiinua ilimwingia na ya kupenda kutukuzwa na watu na kuinuliwa, na akaipalilia mwishowe ikawa ni roho ya uadui mbaya sana na iliyoiharibu kanisa.

Na sisi hatuna budi kujifunza katika haya, ili tusijikute tunaangukia katika makosa hayo hayo ya Diotrefe (Ndio maana Mungu karuhusu kisa cha Diotrefe kiwepo katika biblia hata kama kwa ufupi sana). Ili tujifunze na tujihadhari na roho ya kujiinua, na kupenda utukufu wa wanadamu zaidi ya utukufu wa Mungu, na tama nyingine zote za kiulimwengu.

Bwana atusaidie tuwe kama Mzee Gayo aliyekubali kupokea mashauri hayo.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?

MJUMBE ASIYEKUWA NA UJUMBE.

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

Ni sahihi kusema sikuitiwa kuhubiri ubatizo kama Paulo alivyosema (1Wakorintho 1:17)?.

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

Rudi nyumbani

Print this post

EPUSHA WIVU KATIKA NDOA:

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WANANDOA: Epusha Wivu katika ndoa:

Sehemu ya kwanza: Upande wa Mwanamke.

Huu ni mfululizo wa mafundisho maalumu yawahusuyo wanandoa: Ikiwa hukupata sehemu za nyuma, basi waweza kututumia ujumbe kwa namba zetu zilizo chini ya somo hili, tukutumie;

Leo tutaona  jinsi wivu unavyoweza kuathiri kwa sehemu kubwa mahusiano ya wanandoa.

Kibiblia wivu upo wa aina mbili:

1)  Wivu wa kipepo: Ni ule wa kumuonea mtu kijicho, yaani kutotaka, mwenzako kufanikiwa kwasababu wewe hukufanikiwa kama yeye alivyofanikiwa, kutaka kile ambacho mwenzako anacho uwe nacho wewe huku hutaki yeye awe nacho. Biblia imetuonya sana dhidi ya wivu huu, kwasababu ni zao la shetani. Ndio walikuwa nao masadukayo na makuhani kwa Bwana wetu Yesu na mitume wake, pale walipoona neema ya Mungu ipo juu yao kubwa lakini kwao haipo, (Matendo 5:17, Warumi 13:13)

2)  Wivu wa kimahusiano: Wanandoa, Huu ni wivu ambao ni wa asili, Mungu kauweka ndani ya mtu, huu upo katika mahusiano ya kindoa,au maagano Na ndio Wivu ambao Mungu amekiri pia mwenyewe anao.(Kutoka 20:5)..Huu ni wa kuulinda sana, hususani pale unapoingia kwenye ndoa, kwasababu madhara yake ni makubwa zaidi hata ya hasira, au ghadhabu. Biblia inasema hivyo katika..

Mithali 27:4 “Ghadhabu ni kali, na hasira ni gharika; Lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu”.

Huu ndio umesababisha watu, kugombana, kuchukiana, kusalitiana  na hata wakati mwingine kuuana, na kuwasababishia matatizo na wengine ambao hata hawahusiki.

Leo  tutatazama, ni kwa namna gani, kinywa cha mwanamke, kinaweza kuwasha wivu mbaya sana, kwa upande wa pili. Na somo linalofuata tutaona tabia ambazo mwanaume anapaswa ajiepushe nazo, kuepukana na madhara ya wivu kwenye ndoa yake.

 hii itakusaida, kuishi kwa amani na utulivu na kuinusuru ndoa yako, .

Sasa embu tusome kisa hichi tunachokiona katika 1Samweli 18:7. Si kisa cha kindoa lakini ni kisa kimuhusucho Daudi na Sauli, Wengi wetu tunajua sababu iliyomfanya Sauli amchukie Daudi, ambaye hapo mwanzo alimpenda ilikuwa ni Wivu. Lakini wachache sana, wanafahamu CHANZO cha wivu huo, kilikuwa ni nini?

Biblia inatupa majibu, kilikuwa ni wanawake, waliotoka na kutoa sifa zao, mahali pasipostahili kwa wakati ule. Embu Tusome.

1Samweli 18:5 “Basi Daudi akatoka kwenda kila mahali alikotumwa na Sauli, akatenda kwa akili; SAULI AKAMWEKA JUU YA WATU WA VITA; jambo hili likawa jema machoni pa watu wote, na machoni pa watumishi wa Sauli pia.

6 Hata ikawa, walipokuwa wakienda, hapo Daudi aliporudi baada ya kumwua yule Mfilisti, wanawake wakatoka katika miji yote ya Israeli, kwa kuimba na kucheza, ili kumlaki mfalme Sauli; wakatoka na matari, na shangwe, na vinanda.

7 NAO WALE WANAWAKE WAKAITIKIANA WAKICHEZA, WAKASEMA, SAULI AMEWAUA ELFU ZAKE, NA DAUDI MAKUMI ELFU YAKE.

8 Basi Sauli akaghadhibika sana, na maneno haya yakamchukiza; akasema, Wamempa Daudi makumi elfu, na mimi wamenipa elfu tu; kuna nini tena awezayo kupata, isipokuwa ni ufalme?

9 Sauli akamwonea Daudi wivu tangu siku ile”.

Hicho ndicho kilichokuwa chanzo, cha vita vya Daudi na anguko la Sauli,. Wanawake wale walikuwa wanasema kweli, kwa waliyoyaona, lakini hawakutumia busara kuimba mbele ya mfalme, kwa wakati ule.. Huwenda hata Daudi, alitamani wakae kimya, wasimsifie yeye zaidi ya mfalme wake, mbele ya umati.. Lakini wale wanawake hilo halikuwa akilini mwao. Hawakujua kuwa kumbe nyimbo zao, sifa zao, maneno yao, ni panga ndani ya mioyo ya wakuu wao.

Ndio ikawa sababu ya Sauli kughahiri, hata vyeo vyote alivyompa Daudi, akampokonya na kumfukuza na kutaka kumuua kabisa, kwa kosa tu la wale wanawake.  Lakini kama wale wanawake wangetumia busara, kumwimbia mfalme zaidi, basi Daudi angeendelea kustarehe na kudumishwa katika ufalme ule.

Maana yake ni nini?

Maneno yoyote ya sifa yanayotoka kinywani mwako wewe kama mwanamke, yana matokeo makubwa sana kwa upande wa pili. Sasa tukirudi katika upande wa ndoa, Wivu unatokea pale ambapo unathamini, au unasifia wanaume wengine zaidi ya mume wako. Ukiwa umeolewa tambua kuwa mume wako ndio,bora kuliko wanaume wote ulimwenguni, ndio mwenye sifa zote kuliko wanaume wote ulimwenguni.Hata kama wale wengine wamemzidi yeye kwa kiwango kikubwa kiasi gani, acha kuwazungumza zungumza mbele ya mume wako.

Hii ni kwa faida yako, na kwa wengine. Wanaume wengi wanagombana na marafiki zao vipenzi, kisa tu wake zao,wanapowasifia, wanakuwa mpaka maadui kwa sababu ndogo ndogo tu kama hizi,..Labda utasikia mmoja anasema, “mume wangu,rafiki yako huwa anapendezaga uvaaji wake, yaani navitiwa nao”..Kauli kama hizi ziepuke kinywani mwako, ili kunusuru, urafiki au ujirani wenu.

Kwa ufupi kauli zozote za sifa, zichungumze mara mbili mbili; Unaweza usione shida yoyote, au ukadhani ni jambo dogo tu, lakini upokee huu ushauri utakufaa kwa siku za mbeleni, , hilo jambo linamuathiri sana mwanaume. Usimzungumze zungumze mwanaume mwingine mbele ya mumeo, isipokuwa kwa kiasi, hata wale unaowaona kwenye tv, au unaowasiliana nao kwenye simu. Kumbuka wivu unawashwa na mambo madogo sana.

Bwana akubariki.

Je! Umeokoka? Je! Unauhakika wa maisha yako ya milele baada ya kifo? Kumbuka Kristo yupo mlangoni kurudi, dalili zote zimeshatimia, Huu si wakati wa kumbelezewa tena wokovu, ni wakati wa kujitahidi kuingia ndani ya Safina(Yesu Kristo) kwa nguvu zote, maana muda umekwisha.. Tubu dhambi zako, ukabatizwe mgeukie Bwana akupe uzima wa milele.

Maran Atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)

WANA-NDOA: Baba Mkwe, Na mama Mkwe.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

Ndoa ya serikali ni halali?

Rudi nyumbani

Print this post