Jibu: Biblia imetuelekeza kufanya kazi za Mikono, ambayo kupitia hiyo Mungu atatupa riziki zetu za kila siku.
1Wathesalonike 4:11 “Tena mjitahidi kutulia, na kutenda shughuli zenu, na kufanya kazi kwa mikono yenu wenyewe, kama tulivyowaagiza;
12 ili mwenende kwa adabu mbele yao walio nje, wala msiwe na haja ya kitu cho chote”
Hivyo ni wajibu wa kila mmoja mwenye uwezo wa kufanya kazi, afanye kazi, aidha za Mikono au za kiutumishi.
Kazi za mikono ni zile zote zinazohusisha kuajiriwa au kujiajiri, na kazi za kiutumishi ni zile zote za Madhabahuni au za kiinjilisti. Mkristo yoyote ni lazima awepo katika kundi mojawapo ya hayo mawili, akikosekana katika yote (na ilihali ni mzima, au hana tatizo lolote lile) basi mtu huyo yupo kinyume na Neno la Mungu, aidha kwa kujua au kutokujua.
Mtume Paulo alisema kwa uongozo wa Roho, kuwa mtu yeyote asiye na shughuli yoyote katika Mwili wa Kristo, yaani asiyefanya kazi yoyote ya Madhabahuni kama Uchungaji, Uinjilisti, au Shemasi, au Mzee wa kanisa au ya Uinjilisti, au mfanya kazi wa kanisani (inayomfanya muda wake mwingi atumie kuhubiri) mtu huyo basi asipewe fungu lolote kutoka kanisani..
1Wathesalonike 3:10 “ Kwa kuwa hata wakati ule tulipokuwapo kwenu tuliwaagiza neno hili, kwamba ikiwa mtu hataki kufanya kazi, basi, asile chakula.
11 Maana twasikia kwamba wako watu kwenu waendao bila utaratibu, hawana shughuli zao wenyewe, lakini wanajishughulisha na mambo ya wengine.
12 Basi twawaagiza hao, na kuwaonya katika Bwana Yesu Kristo, watende kazi kwa utulivu na kula chakula chao wenyewe”
Kumbuka pia unapoamua kufanya kazi za Mikono, basi huwezi kuwa Mchungaji kwa wakati huo huo, kwasababu huwezi kushikilia mambo mawili kwa wakati mmoja.. Ni aidha ushikilia moja uache lingine! Huwezi kuwa mchungaji na huku ni Mbunge, huwezi kuwa Mchungaji na huku ni Mfanya biashara mashuhuri.. jambo hilo haliwezekani!, haijalishi mtu atalilazimisha kiasi gani?.
Mathayo 6:24 “Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali”
Tofauti na inavyodhaniwa na wengi kwamba Mtume Paulo alikuwa anafanya kazi muda wote!, kwamba alikuwa anashona Mahema kila wakati ili kujipatia riziki, nataka nikuambie kuwa haikuwa hivyo, ni sehemu chache sana ndizo alizokuwa anashona mahema, lakini sehemu kubwa ya maisha ya Paulo ilikuwa ni kuhubiri injili, na Mungu alikuwa anamfungulia milango ya riziki kupitia injili hiyo, na alikuwa haombi kwa watu fedha wala mali, (ili awe kielelezo) bali watu walikuwa wanampa kwa kadiri wanavyoguswa.
Tunalithibitisha hilo katika kitabu cha Wafilipi, 4:1-19, (Zingatia Mistari iliyoainishwa kwa herufi kubwa)
Wafilipi 4:14 “Lakini mlifanya vema, mliposhiriki nami katika dhiki yangu.
15 Nanyi pia, ninyi wenyewe mnajua, enyi Wafilipi, ya kuwa katika mwanzo wa Injili, nilipotoka Makedonia, hakuna kanisa lingine lililoshirikiana nami katika HABARI HII YA KUTOA NA KUPOKEA, ila ninyi peke yenu.
16 KWA KUWA HATA HUKO THESALONIKE MLINILETEA MSAADA KWA MAHITAJI YANGU, WALA SI MARA MOJA.
17 Si kwamba nakitamani kile kipawa, bali nayatamani mazao yanayozidi kuwa mengi, katika hesabu yenu.
18 Lakini ninavyo vitu vyote na kuzidi, tena nimejaa tele; NIMEPOKEA KWA MKONO WA EPAFRODITO VITU VILE VILIVYOTOKA KWENU, HARUFU YA MANUKATO, SADAKA YENYE KIBALI, IMPENDEZAYO MUNGU.
19 Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu”
Umeona hapo ? Sio wakati wote Paulo alikuwa anafanya kazi ya kushona, Soma pia 2Wakorintho 8:1-5..
Lakini biblia inatufundisha nini katika hali tulizopo (yaani ya kufanya kazi ya Mikono au ya Madhabahuni)?
Biblia imetufundisha kutumika kwa uaminifu popote pale tunapopatumikia, maana yake kama ni Mtumwa basi tumika ipasavyo kwa Bwana wako (maana yake Boss wako, au Mkubwa wako) kana kwamba unamtumikia Kristo.
Waefeso 6:5 “Enyi watumwa, watiini wao walio bwana zenu kwa jinsi ya mwili, kwa hofu na kutetemeka, kwa unyofu wa moyo, kana kwamba ni kumtii Kristo;
6 wala si kwa utumwa wa macho tu kama wajipendekazao kwa wanadamu bali kama watumwa wa Kristo, mkitenda yampendezayo Mungu kwa moyo;
7 kwa nia njema kama kumtumikia Bwana wala si mwanadamu;
8 mkijua ya kuwa kila neno jema alitendalo mtu atapewa lilo hilo na Bwana kwamba ni mtumwa au kwamba ni huru”.
Vile vile kama tunatumika katika utumishi wowote ule.. Maandiko yanatufundisha KURIDHIKA, Maana yake TUSIJISIKIE VIBAYA kutumika pale tulipopachagua sisi, kwasababu ni mapenzi ya Mungu. Kama ni Mfanyakazi wa kuajiriwa maana yake wewe ni Huru kwa kazi ya Bwana ya madhabahuni, hivyo usijisikie vibaya kuifanya kazi hiyo, kilicho kikubwa na cha muhimu ni wewe kuwa Mwaminifu katika kazi unayoifanya na pia katika kumtolea Bwana, na mwisho wa siku utapokea thawabu kutoka kwa Mungu, vile vile kama wewe ni mtumishi wa Madhabahuni au wa Injili, maana yake wewe ni Huru katika utumishi wa kazi za kidunia, hivyo basi usijisikie vibaya kutumika hivyo, maana ni Mungu kakuita katika hali hiyo, wala usiitamani kazi nyingine zaidi ya hiyo uliyopewa!.
1Wakorintho 7:21 “Je! Uliitwa u mtumwa? Usione ni vibaya lakini kama ukiweza kuwa na uhuru, afadhali kuutumia.
22 Kwa maana yeye aliyeitwa katika Bwana hali ya utumwa, ni huru wa Bwana. Vivyo hivyo yeye naye aliyeitwa hali ya uhuru, ni mtumwa wa Kristo.
23 Mlinunuliwa kwa thamani; msiwe watumwa wa wanadamu”
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.
MAOMBI YA KUFUNGULIWA KIUCHUMI.
Orodha ya mistari ya biblia kuhusu watoto.
Kwanini iwe ni nchi ibubujikayo maziwa na asali?
Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?
Jibu: Tiro na Sidoni ni miji iliyokuwa katika nchi inayoitwa LEBANONI. Tofauti na nchi nyingine ambazo zilibadilika majina baada ya miaka mingi kupita, lakini nchi ya Lebanoni, imeitwa kwa jina hilo hilo tangu nyakati za biblia hata leo.
Tiro na Sidoni ni miji ambayo ipo karibu karibu, (Kusini Mashariki mwa Nchi ya Lebanoni), na miji hii enzi za biblia ilikuwa ni miji ya kibiashara, lakini iliyojaa machukizo mengi.
Kwasasa nchi ya Lebanoni ina miji mikubwa minne, Ambayo ni Beiruti, Tripoli, Sidoni na Tiro. Mji wa Sidoni ni mkubwa kuliko Tiro na katika Lebanoni ndiko ulipokuwepo pia Mji wa Tarshishi, ule ambao Yona aliukimbilia ili apate kujiepusha na uso wa Bwana.
Kwasasa nchi hii ya Lebanoni inakaliwa na Waarabu, na ni nchi ambayo ipo katika upande wa Kaskazini mwa Israeli, Eneo kubwa la Nchi ya Lebanoni, ni misitu na ndio huko Mfalme Sulemani alipotolea Miti aina ya Mierezi kwaajili ya ujenzi wa Hekalu la Mungu.
Nchi ya Lebanoni kwasasa ina uadui mkubwa sana na Nchi ya Israeli. Na unabii unaonyesha katika Ezekieli 38 na 39 kuwa siku za mwisho Lebanoni pamoja na nchi za kando kando zitashirikiana na Nchi ya Urusi kwa lengo la kuifuta Israeli katika uso wa dunia, lakini zitapigwa zote, kwasababu Mungu wakati huo atasimama upande wa watu wake Israeli.
Kwaufupi miji ya Tiro na Sidoni imebeba ufunuo mkubwa katika matukio ndani ya biblia. Kasome Mathayo 11:21-22, Yoeli 3:4, Zekaria 9:1-4, na Matendo 12:20
Lakini lililo kubwa zaidi ni ufunuo mji huo uliobeba, kumhusu shetani.. Biblia inamtaja mkuu wa Mji wa Tiro katika ulimwengu wa roho, kwamba ni shetani mwenyewe.
Ezekieli 28:1 “Neno la Bwana likanijia tena, kusema,
2 Mwanadamu, mwambie mkuu wa Tiro, Bwana MUNGU asema hivi; Kwa kuwa moyo wako umeinuka, nawe umesema, Mimi ni Mungu, nami nimeketi katika kiti cha Mungu, kati ya bahari; lakini u mwanadamu wala si Mungu, ujapokuwa umeweka moyo wako kama moyo wa Mungu……
13 Ulikuwa ndani ya Adeni, bustani ya Mungu; kila jiwe la thamani lilikuwa kifuniko chako, akiki, na yakuti manjano, na almasi, na zabarajadi, na shohamu, na yaspi, na yakuti samawi, na zumaridi, na baharamani, na dhahabu; kazi ya matari yako na filimbi zako ilikuwa ndani yako; katika siku ya kuumbwa kwako zilitengenezwa tayari.
14 Wewe ulikuwa kerubi mwenye kutiwa mafuta afunikaye; nami nalikuweka hata ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu, umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto.
15 Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako”.
Na shetani si mkuu tu wa Tiro, bali biblia imezidi kutupa mwangaza kuwa ni mungu wa ulimwengu mzima (2Wakorintho 4:4).. Yaani mifumo yote ya kishetani iliyopo duniani ni yeye muasisi.
Je umempokea Yesu?
Kumbuka hizi ni siku za mwisho na Kristo yupo Mlangoni.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
Kwanini Herode aliwakasirikia watu wa Tiro na Sidoni? (Matendo 12:20)
JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)
SWALI: Bwana Yesu asifiwe, naomba kufahamu tofauti iliyopo kati ya Imani na ujasiri.
Ujasiri ni ile hali ya kuweza kukabiliana na tatizo au shida, au changamoto Fulani, (uwezo wa kuushinda woga).. Ujasiri unaweza kuonekana kwa kiumbe hai chochote cha Mungu, kwamfano unaweza kuonekana kwa mtu, vilevile unaweza kuonekana kwa Simba, au mbwa, au nyoka. Pia ni hali ambayo mtu/kiumbe kinaweza kuzaliwa nao, tofauti na imani,
Lakini Imani, inatokana na Neno ‘kuamini’.. Maana yake ni kwamba huzalika kwa kutegemea, kuamini kitu kingine (Haisimami yenyewe kama yenyewe)..Na kwa kupitia hicho ndio unapata sasa wa kutenda Neno ambalo mtu ulikuwa huwezi kulifanya. Kwamfano kwanini leo hii ukipishana na kuku barabarani hushtuki, lakini ukipishana na nyoka unaruka na kukimbia, au unachukua hatua ya kupambana naye? Ni kwasababu umeyaamini macho yako yaliyokupa taarifa kule kile ni kiumbe salama na kile ni hatari, lakini kama usingekuwa na macho matendo hayo yasingezalika. Hivyo ujasiri ni zao la imani, lakini imani haiwezi kuwa zao la ujasiri.
Na ndivyo ilivyo kwetu sisi, ili tuweze kupata IMANI timilifu. Hatuna budi tuwe na kitu cha uhakika cha kutegemea. Na hicho si kingine zaidi ya NENO LA MUNGU.. Hapo ndio mwisho wa mambo yote. Hilo ndio jicho letu la ndani tunalopaswa tulifufue, kwasababu ndio litatupa ujasiri wa kufanya mambo yote, na kutenda mambo yote yasiyowezekana kwa namna ya kibinadamu.
Na imani hii, haiji kwa njia nyingine yoyote isipokuwa kwa kulisikia Neno la Mungu biblia inasema hivyo .
Warumi 10:17 “Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo”.
Unaposoma Neno la Mungu, na kuona ndani yake, matendo makuu aliyoyofanya, ndipo unapopata Imani sasa na wewe ya kutenda au kusonga mbele, kwamfano, wewe ni tasa, unaposoma habari za Sara na Ibrahimu, na kuona katika uzee wa miaka 100 ndio wanapata watoto, hapo na wewe utapata nguvu ya kumwamini Mungu ukijua kuwa kama aliweza kufanya kwa Sara atafanya na kwako, kwasababu yeye ni Yule Yule jana na leo na hata milele. Lakini ikiwa huijui hii habari au huitafakari mara kwa mara, imani yako haiwezi kutokea, utabakia kusema mimi ndio basi, tena siwezi kuzaa.
Daudi alipokwenda kushindana na Goliati, alitafakari jinsi Mungu alivyomshindania, akiwa porini anachunga mbuzi na kondoo, jinsi alivyoweza kuua simba na dubu. Akamwesabia Mungu kuwa anaweza pia kumsaidia kwa Yule Goliati mtu wa miraba minne, na kweli ikawa hivyo.. Halikadhalika na wewe ili uweze kutenda mambo makubwa, kufungua mambo ambayo hayawezekani kwa akili za kibinadamu, unahitaji Imani, lakini si imani kwa wanadamu au kwa vitu au kwenye mali, bali imani kwa Mungu, ambalo ndio NENO LAKE.
Penda sana, kusoma Neno, kiwe ndio chakula chako asubuhi, mchana na jioni.
Biblia inasema..
Waebrania 11:24 “Kwa imani Musa alipokuwa mtu mzima, akakataa kuitwa mwana wa binti Farao;
25 akaona ni afadhali kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha katika dhambi kwa kitambo;
26 akihesabu ya kuwa kushutumiwa kwake Kristo ni utajiri mkuu kuliko hazina za Misri; kwa kuwa aliyatazamia hayo malipo.
27 Kwa imani akatoka Misri, asiogope ghadhabu ya mfalme; maana alistahimili kama amwonaye yeye asiyeonekana.
28 Kwa imani akaifanya Pasaka, na kule kunyunyiza damu, ili yule mwenye kuwaangamiza wazaliwa wa kwanza asiwaguse wao.
29 Kwa imani wakapita kati ya Bahari ya Shamu, kama katika nchi kavu; Wamisri walipojaribu kufanya vivyo wakatoswa.
30 Kwa imani kuta za Yeriko zikaanguka, zilipokwisha kuzungukwa siku saba.11.31 Kwa imani Rahabu, yule kahaba, hakuangamia pamoja na hao walioasi; kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi kwa amani.
32 Nami niseme nini tena? Maana wakati usingenitosha kuleta habari za Gideoni na Baraka na Samsoni na Yeftha na Daudi na Samweli na za manabii;
33 ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi, walifunga vinywa vya simba,
34 walizima nguvu za moto, waliokoka na makali ya upanga. Walitiwa nguvu baada ya kuwa dhaifu, walikuwa hodari katika vita, walikimbiza majeshi ya wageni.
35 Wanawake walipokea wafu wao waliofufuliwa. Lakini wengine waliumizwa vibaya hata kuuawa, wasikubali ukombozi, ili wapate ufufuo ulio bora;
36 wengine walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa mafungo, na kwa kutiwa gerezani;
37 walipigwa kwa mawe, walikatwa kwa misumeno, walijaribiwa, waliuawa kwa upanga; walizunguka-zunguka wakivaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi; walikuwa wahitaji, wakiteswa, wakitendwa mabaya;
Hiyo ndio tofauti kati ya imani na ujasiri.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
ENZI NA MAMLAKA AMEZIFANYA KUWA MKOGO
NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?
KWANINI TUNAPASWA KWENDA KUIHUBIRI INJILI KWA UJASIRI WOTE?
Je!Sisi kama wakristo Tunaruhusiwa kuchangia ujenzi wa Imani nyingine?
Agano ni nini? na kuna aina ngapi za maagano?
Atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani? Maana yake nini?
Swali: Katika Mwanzo 3:20 na Mwanzo 4:1 mkewe Adamu ni Hawa. Nmekuwa nikisikia mkewe Adamu pia ni Eva. Je! jina Eva na Hawa ni sawa?
Jibu: Hawa na Eva ni jina moja isipokuwa katika lugha mbili tofauti ni sawa na jina YESU na JESUS; ni jina moja isipokuwa katika lugha mbili tofauti, yaani ya kiingereza na ya kiswahili.
Kadhalika na Eva (au Eve) ni kiingereza na HAWA ni kiswahili chake.
Sasa swali ni kwanini, tafsiri zake zionekane kama mbalimbali, yaani Kutoka Eve mpaka Hawa ni kama hazikaribiani?. Kwanini Eve isingetafsiriwa tu Eva kwa lugha ya kiswahili badala yake ikawa Hawa?
Jibu ni kwamba lugha ya kiswahili sehemu nyingi imeitafsiri herufi “V” kwa “W” katika majina ya watu au vitu. Kwamfano utaona jina “LAWI”, kwa lugha ya kiingereza ni “LEVI”.
Vilevile mji wa “Ninawi” kwa lugha ya kiingereza ni “NINEVEH”n.k
Kwahiyo hata Eva kiswahili chake ni lazima kirudi kwenye herufi “w” na kuwa “Hawa”
Ni kama vile majina yote yanayoanza na herufi “J” yanavyobadilika na kuanza na herufi “Y” yanapokuja katika lugha ya kiswahili…Kwamfano Jina Jesus-Yesu, Jonah-Yona, Joshua-Yoshua, Jezebel- Yezebeli n.k Ndivyo ilivyo kwa majina yote yenye herufi “V”, yalibadilika na kuwa “W” yanapoletwa katika lugha ya kiswahili.
Kwahiyo kwa hitimisho mtu anayetumia Jina Hawa na anayetumia Eva wote wapo sahihi, na wanamlenga mtu mmoja.
Je umempokea Yesu?..je umebatizwa?..je umepokea Roho Mtakatifu?..Kama bado unasubiri nini?. Kumbuka hizi ni nyakati za mwisho na Kristo yupo mlangoni kurudi.
Maran atha!.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!
Je! dhambi zote ni sawa Kuna dhambi kubwa na ndogo?
JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?
Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe;(Mithali 16:2)
Kipaku ni kipele kidogo kinachochipuka kwenye ngozi ya mwanadamu au mnyama. Kipele hichi kinaweza kusababishwa na mabadiliko ya mazingira, au aleji au magonjwa mbalimbali.
Hivyo Neno hili katika biblia linaonekana sehemu nyingi, hususani pale unapotajwa ugonjwa wa ukoma. Kwani ugonjwa huo kabla huujakolea kwenye mwili, huwa unaanza kwanza kama kipeleke kidogo king’aacho kekundu (ndio hicho kipaku). Hivyo katika hatua za awali ilikuwa ni ngumu kukitambua kama ni cha ukoma au cha ugonjwa mwingine wa kawaida. Hivyo ili kuepusha maambukizi zaidi kwa wengine, Mgonjwa Yule alitengwa kwa muda wa siku saba.
Na baada ya siku saba, kuhani huja na kuangalia, kama kipaku kile kimeenea zaidi kwenye mwili na kuzama kwenye ngozi basi ulikuwa ni ugonjwa wa ukoma. Hivyo mtu huyo alitengwa daima, kama hakutakasika.
Walawi 13:1 “Kisha Bwana akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,
2 Mtu atakapokuwa na kivimbe katika ngozi ya mwili wake, au kikoko, au kipaku king’aacho, nalo likawa pigo la ukoma katika ngozi ya mwili wake, ndipo atakapoletwa kwa Haruni kuhani, au kwa wanawe, makuhani mmojawapo;
3 na huyo kuhani ataliangalia hilo pigo lililo katika ngozi ya mwili; na kwamba malaika yaliyo katika hilo pigo yamegeuka kuwa meupe, na hilo pigo kuonekana kwake limeingia ndani kuliko ile ngozi ya mwili wake, ni pigo la ukoma hilo; na kuhani atamwangalia na kusema kuwa yu mwenye unajisi.
4 Na hicho kipaku king’aacho, kwamba ni cheupe katika ngozi ya mwili wake, na kuonekana kwake si shimo la kuingia ndani kuliko ngozi, na malaika hayakugeuka kuwa meupe, ndipo kuhani atamweka mahali muda wa siku saba huyo aliye na hilo pigo;
5 kisha kuhani atamwangalia siku ya saba; naye akiona ya kuwa pigo limeshangaa, na pigo halikwendelea mbele katika ngozi yake, ndipo kuhani atamweka mahali muda wa siku saba tena;
6 kisha siku ya saba kuhani atamwangalia tena; na tazama, ikiwa hilo pigo limeanza kufifia, wala pigo halikwendelea mbele katika ngozi yake, ndipo kuhani atasema kuwa yu safi; ni kikoko; naye atazifua nguo zake, kisha atakuwa yu safi”.
Ni fundisho gani lipo nyuma ya pigo hili la ukoma?
Zamani za agano la kale ukoma uliwakilisha pigo kutoka kwa Mungu,. Na sikuzote Mungu kabla hajaleta mapigo hutanguliza kwanza ishara na dalili, Kama vile KIPAKU tu kidogo.. Lakini baada ya siku SABA, huenea mwili wote.
Kufunua nini?
Yesu alipokuwa duniani alisema tubuni kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia, akasema pia kabla ya ule mwisho wa dunia kufika ambapo Mungu ataleta mapigo makubwa sana juu ya ulimwengu huu wa dhambi..Zitatangulia kwanza dalili na ishara, ambazo yeye aliziita ‘mwanzo wa utungu’..Ndio haya matetemeko, majanga, magonjwa, tetesi za vita, n.k. tuliyoyana tangu enzi za Bwana hadi sasa, (Ndio kipaku chenyewe rohoni, ila ukoma wenyewe kuenea bado).
Lakini aliruhusu kipindi cha neema cha NYAKATI SABA kipite kwanza, ili watu watengeneze mambo yao, watubu dhambi zao, Bwana awaepushe na uharibifu huo. Ndio hii miaka 2000, sasa ambapo ndani yake nyakati saba za kanisa zinapita, na sisi watu wa kizazi hiki ndio tupo katika kanisa la mwisho kabisa la saba, lijulikanalo kama LAODIKIA (Ufunuo 3:14-22).
Hivyo ni kama dalili za ukoma tu, mwisho wa siku saba, uhakika unapatikana. Na ndivyo ilivyosasa, hivi karibuni Unyakuo utapita, Bwana atawaondoa kwanza watu wake ulimwenguni. Na baada ya hapo atatusha laana yake ya mwisho juu ya huu ulimwengu, ndio vile vitasa saba vinavyozungumziwa katika kitabu cha Ufunuo 16.
Jiulize ndugu yangu, je huu ukoma ulioanza ndani yako, kama kipaku, je umeshaupatia tiba? Kumbuka tiba ni Bwana Yesu, usisubiri unyakuo ukupite, au ufe katika dhambi zako, mguekie Masihi akuoshe na kukusafisha.
Maandiko yanasema kipindi cha Elisha, kulikuwa na wakoma wengi, Israeli, lakini hakutumwa kwa mmojawapo wao, ila Naamani mtu wa shamu (Luka 4:27). Kwasababu gani? Kwasababu alikubali kutii maagizo aliyopewa na Elisha kwenda kujichovya mtoni mara saba..Leo hii watu hatutaki kusoma kitabu cha Ufunuo, ambapo ndani yake tutakutana na ujumbe wa makanisa saba na nyakati zao. Ambazo kwa kuzielewa hizo tutaweza kuepukana na ukoma huu wa rohoni ambao Mungu anawapiga watu sasa.. Badala yake tunapenda kusikia habari ya kutabiriwa, na mafanikio ya mwilini.. Hii ni hatari kwasababu tunaweza kujikuta tunaachwa katika unyakuo, kama sio kufa katika dhambi.
Bwana atusaidie tulipende Neno lake.
Maran Atha.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Ukoma wa nyumba ulifunua nini zamani?
Hawa ndege katika Walawi 11:13-19 ndio ndege gani kwasasa?
Je mke wa Musa alikuwa ni Mweusi?
Hawa ndege katika Walawi 11:13-19 ndio ndege gani kwasasa?
Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?
Yakobo 1:13 “Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu”
Hapo Neno linasema kuwa Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, kinyume chake ni kweli kwamba yeye anajaribiwa na MEMA tu!. Maana yake tunapofanya mema hapo tunakuwa tunamweka Mungu kwenye jaribu la kutubariki.. Na hivyo ni lazima aachie baraka kwetu.
Lakini tukienda kinyume na Neno lake na huku tunataka atubariki, hapo maana yake tunamjaribu yeye kwa Maovu.. Mfano wa watu waliomjaribu Mungu kwa maovu ni Wana wa Israeli kipindi wapo jangwani, Walitaka Bwana awashushie chakula kile cha kimiujiza, huku mioyoni mwao wamemwacha Mungu, ni watu wenye viburi, ni watu wa kunung’unika, ni watu wasio na heshima wala staha kwa Mungu na mwishowe wakaangukia hukumu.
Waebrania 3:7 “Kwa hiyo, kama anenavyo Roho Mtakatifu, Leo, kama mtaisikia sauti yake,
8 Msifanye migumu mioyo yenu, Kama wakati wa kukasirisha, Siku ya kujaribiwa katika jangwa,
9 Hapo baba zenu waliponijaribu, wakanipima, Wakaona matendo yangu miaka arobaini.
10 Kwa hiyo nalichukizwa na kizazi hiki, Nikasema, Sikuzote ni watu waliopotoka mioyo hawa; Hawakuzijua njia zangu;
11 Kama nilivyoapa kwa hasira yangu, Hawataingia rahani mwangu”.
Na maandiko yanasema Mungu ni yeye Yule jana na leo na hata milele, alilolikataza miaka elfu 2 iliyopita analitakata hata leo.. Akisema “yeye hajaribiwi na Movu, ni kweli hajaribiwi na hayo”.. Lakini kinyume chake anajaribiwa na Mema yaliyoandikwa katika Neno lake.
Kwamfano unapomtolea Mungu sadaka isiyo na kasoro (Maana yake iliyo sawasawa na Neno lake, na kwa nia njema) Hilo ni jaribu kwa Mungu kukubariki wewe, na hapo utakuwa umemjaribu kwa Mema.
Malaki 3:8 “Je! Mwanadamu atamwibia Mungu? Lakini ninyi mnaniibia mimi. Lakini ninyi mwasema, Tumekuibia kwa namna gani? Mmeniibia zaka na dhabihu.
9 Ninyi mmelaaniwa kwa laana; maana mnaniibia mimi, naam, taifa hili lote.
10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.
11 Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu; wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake katika mashamba, asema Bwana wa majeshi”.
Na mambo mengine yote mema, ambayo tunayafanya yaliyo sawasawa na Neno la Mungu, mambo hayo ni TANZI kwa Mungu, kutumwagia Baraka zake, au kuzungumza na sisi.
Lakini kama moyoni mwako umemwacha Bwana, halafu unatafuta kuisikia sauti yake, unaenda kwa nabii ili usikie Mungu anasema nini kuhusu wewe, hapo unamjaribu Mungu kwa mabaya na hivyo unajitafutia laana badala ya Baraka.
Ezekieli 14:4 “Basi sema nao, uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Kila mtu wa nyumba ya Israeli atwaaye vinyago vyake na kuvitia moyoni mwake, na kuliweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake, na kumwendea nabii; mimi, Bwana, nitamjibu neno lake sawasawa na wingi wa sanamu zake;
5 ili niwakamate nyumba ya Israeli kwa mioyo yao wenyewe, kwa sababu wamefarakana nami kwa vinyago vyao.
6 Kwa sababu hiyo uwaambie nyumba ya Israeli, Bwana MUNGU asema hivi; Rudini ninyi, mkageuke na kuviacha vinyago vyenu; mkageuze nyuso zenu zisielekee machukizo yenu yote.
7 Kwa maana kila mtu wa nyumba ya Israeli, au wa wageni wakaao katika Israeli, ajitengaye nami, na kuvitwaa vinyago vyake na kuvitia moyoni mwake, na kuliweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake, kisha kumwendea nabii, na kuniuliza neno kwa ajili ya nafsi yake; mimi, Bwana, nitamjibu, mimi mwenyewe
8 nami nitaukaza uso wangu juu ya mtu yule, na kumfanya kuwa ajabu, awe ishara na mithali, nami nitamkatilia mbali, asiwe kati ya watu wangu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.”
Bwana Yesu atusaidie.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Je Adamu na Hawa, walikuwa hawafanyi mema kabla ya kula tunda?
DAMU YA YESU INANENAJE MEMA KULIKO YA HABILI?
Jibu: Tusome..
Walawi 22:21 “Na mtu awaye yote atakayemtolea BWANA dhabihu katika sadaka za amani, ili kuondoa nadhiri, au SADAKA YA MOYO WA KUPENDA, katika ng’ombe, au katika kondoo, atakuwa mkamilifu, apate kukubaliwa; pasiwe na kilema ndani yake cho chote”.
Sadaka ya Moyo wa kupenda, ni sadaka ambayo wana wa Israeli walimtolea Mungu wao wenyewe kwa kupenda (yaani pasipo kuagizwa wala masharti).
Zilikuwepo sadaka zilizokuwa na sababu, kwa mfano sadaka ya Shukrani, tayari sadaka hiyo inatolewa kwa lengo la kushukuru, kutokana na mambo fulani ambayo mtu kafanyiwa na Mungu.
Lakini sadaka ya Moyo wa kupenda, haikuwa na sababu yoyote nyuma yake… ni mtu tu anapenda kumtolea Mungu kwasababu amependa tu kufanya hivyo..na wala si kwasababu Mungu kaagiza.
Mfano wa sadaka hiyo ni ile ambayo baadhi ya wana wa Israeli waliipeleka mbele za Bwana wakati wa ujenzi wa Maskani ya Bwana.
Wakati huo Mungu hakuwaagiza wana wa Israeli wachangie gharama za ujenzi huo wa maskani ya Mungu…lakini baadhi ya watu waliguswa na kumtafuta Musa na kudhamiria kubeba gharama za kazi hiyo kwa mapenzi yao wenyewe…
Kutoka 35:29 “Wana wa Israeli WAKALETA SADAKA ZA KUMPA BWANA KWA MOYO WA KUPENDA; wote, waume kwa wake, AMBAO MIOYO YAO ILIWAFANYA KUWA WAPENDA KULETA KWA HIYO KAZI, ambayo BWANA aliamuru ifanywe kwa mkono wa Musa”.
Kutoka 35:21 “Wakaja kila mtu ambaye moyo wake ulimhimiza, na kila mtu ambaye roho yake ilimfanya kuwa apenda, nao wakaleta sadaka za kumpa BWANA, kwa kazi ya hema ya kukutania, na kwa utumishi wake, na kwa hayo mavazi matakatifu”.
Soma pia Kutoka 25:2 na 2Nyakati 29:31.
Swali ni je! katika Agano jipya bado tunazo sadaka kama hizi?..
Jibu ni Ndio! Bado Zipo na ndizo zinazompendeza Bwana, na tunazopaswa kutoa.
Utauliza katika agano jipya tunasoma wapi hayo…??.
2 Wakorintho 9:7 “Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu”.
Umeona sadaka ya Moyo wa kupenda ni sadaka Bwana anayoikubali.
Je na wewe unayo desturi ya kumtolea Bwana kwa moyo wa kupenda au kwa sababu tu ya shinikizo fulani?.
Kamwe usiache kumtolea Mungu, lakini katika kumtolea hakikisha unamtolea kwa Moyo.
Sadaka ya namna hii ni sadaka bora na inayompendeza Mungu
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1
TOA SADAKA ISIYO NA KASORO KWA BWANA.
Mambo yaleyale waliyokuwa wanayafanya wana wa Israeli walipokuwa jangwani, yanafanywa sasa na wana wa Mungu. Ni vizuri tukafahamu asili ya ile ndani jinsi ilivyoundwa, ili tuelewe kwa undani, inavyoundwa sasa mioyoni mwa watu.
Maandiko yanatuonyesha, hawakuwa na rasilimali zozote za kuitengeneza, vilevile hawakuwa na urahisi wowote wa kuifanyia karamu yake, kwasababu pale palikuwa ni jangwani, hakuna namna wataweza kupika vyakula vizuri, pamoja na kupata pombe za kuifurahisha ibada yao.
Lakini cha ajabu ni kuwa, japokuwa changamoto hizo zilikuwepo, lakini vyote hivyo vilipatikana, na mambo yakaenda vizuri kabisa bila shida. Ndama akatengenezwa tena sio wa mawe bali wa dhahabu, vilevile Vinywaji vilipatikana(pombe zote) pamoja na vyakula vya kila namna? Na disco la miziki na vinanda juu vikawekwa.
Kutoka 32:2 “Haruni akawaambia, Zivunjeni pete za dhahabu zilizo katika masikio ya wake zenu, na wana wenu, na binti zenu, mkaniletee. 3 Watu wote wakazivunja pete za dhahabu zilizo katika masikio yao, wakamletea Haruni. 4 Akaipokea mikononi mwao akaitengeneza kwa patasi, akaifanya iwe sanamu ya ndama kwa kuiyeyusha; nao wakasema, Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri. 5 Naye Haruni alipoona jambo hili, akajenga madhabahu mbele yake; Haruni akatangaza akasema, Kesho itakuwa sikukuu kwa Bwana. 6 Wakaondoka asubuhi na mapema, wakatoa dhabihu, wakaleta sadaka za amani, watu wakaketi kula na kunywa, wakaondoka wacheze”.
Utajiuliza vilipatikanaje?
Hii ni kuthibitisha kuwa nafsi ya mtu ikidhamiria kutafuta jambo Fulani, ni lazima itapata tu haijalishi mazingira iliyopo.
Ndicho walichokifanya hawa.. Walipohitaji dhahabu, wakakumbuka kuwa wake zao, wanazo kwenye masikio yao, wanazo kwenye shingo zao.. Hivyo wakazitumia hizo hizo na kuzikusanya, zikawa nyingi, mno, wakampa Haruni akaziyeyusha na matokeo yake ikatokea ndama kubwa iliyong’aa sana.
Biblia haijatuambia pombe na vyakula vizuri walivitolea wapi, lakini ni wazi kuwa, waliagiza watu, waende nje ya jangwa kununua vyakula hivyo na pombe, katika miji ya kandokando huwenda muasisi alikuwa ni Kora au mwingine.. Au pengine wakatoa baadhi ya hizo dhahabu wakanunua. Lakini kwa vyovyote vile, na kwa njia yoyote ile, shughuli ilikamilika.
karamu ilikuwepo, watu walikula, walikunywa walisaza..na zaidi sana Sanamu yenye utukufu ilitengenezwa. Akili hizo hawakuwahi hata sikumoja kuzielekeza kwa Mungu wao aliyewaokoa kwa gharama kubwa sana kutoka kwa watesi wao wamisri, hawakuwahi kufikiria kumfanyia Mungu karama ya shukrani kama hiyo wale na wanywe mbele ya Yehova kwa matendo makuu aliyowatendea..
Hata kufikiria kutengeneza kibanda kidogo tu cha udongo kwa ajili ya Mungu wao kukutana nao, kuliko Musa kupanda huko milimani, na kutoweka muda mrefu,hawakuwahi kufikiri hivyo, wanakuwa wepesi kuwaza kuunda miungu ya dhahabu ambayo haijawahi kuwasaidia kwa chochote..Unadhani Kwa namna hiyo wangeachaje kumtia Mungu wivu?
Mambo kama haya yanaendelea sasa miongoni mwa wakristo..
Tukisikia harusi Fulani inafungwa, tunakuwa wepesi kubuni kila namna ya kuifanya ipendeze, tunaweza kutoa hata michango ya milioni moja, na kutengeneza kamati nzuri za maandalizi, tunatoa mapendekezo haya au yale, mpaka inatokea na kuvutia, hata kama ilikuwa ni ya bajeti ndogo lakini itafanikiwa tu mwisho wa siku..Lakini kwa Mungu aliyetukomboa, aliyetufia msalabani, ambaye kila siku anatupigania usiku na mchana, anatupa pumzi yake bure, hatuna muda naye..Zaidi tunaitazama nyumba yake, au kazi yake, tunaona kabisa ipo katika hali ya unyonge, lakini tunapita tu,kama vipofu, tunasema Mungu mwenyewe atatenda..
Tukiangalia tulivyovichangia katika mambo yasiyo ya msingi ni vingi kuliko tulivyovipeleka kwa Mungu. Ndugu tukiwa watu wa namna hii hapo tuwe na uhakika kuwa tumeunda sanamu za ndama nyingi, na tunaziabudu bila kujua. Na zimemtia sana Mungu wetu wivu sana.
Kukitokea party, au birthday, au tafrija Fulani, ni wepesi sana kuutikia, lakini kwa Mungu ni mpaka tukumbushwe kumbushwe, tuvutwe vutwe.. Hii inasikitisha sana.
Embu hii Ndama ya dhabahu tuivunje.. Hii miungu tuiondoe ndani yetu, mioyo yetu itusute.. Tumpe Mungu kipaumbele cha kwanza, kwasababu yeye ndio anayestahili kuliko hao wengine. Tusiwaone wale ni wajinga sana kuliko sisi. Huwenda wale wanao unafuu mkubwa zaidi ya sisi ambao tumeshaona mifano lakini tunarudia mambo yaleyale.
Tumpende Mungu, tuuthamini na wokovu wake, tuithamini pia na kazi yake.
EFATHA.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Hema ya kukutania ni nini, na ilikuwaje?
Maashera na Maashtorethi ni nini?
Kusubu ni nini? Miungu ya kusubu ni ipi?
Ayala, Paa na Kulungu ni wanyama gani?
HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?
Jibu: Tusome kuanzia ule wa 2 ili tuweze kuelewa vizuri.
Ayubu 24:2 “Wako waziondoao alama za mipaka; Huyachukua makundi kwa jeuri na kuyalisha.
3 Humfukuza punda wake asiye baba, Humtwaa rehani ng’ombe wake mwanamke mjane.”.
Hapa Ayubu anazungumzia juu ya kundi la watu wabaya ambao wanawaonea Mayatima na kuwadhulumu wajane.
Ndio hapo anasema wapo (watu duniani) ambao.
1. Wanaondoa alama za Mipaka, na kuyachukua makundi kwa jeuri na kuyalisha.
Maana yake wanawadhulumu watu mashamba/ardhi kwa kuondoa mipaka iliyokuwepo na kuweka mipaka ya uongo!,..na baada ya kumiliki ardhi kwa dhuluma namna hiyo bado wanalisha mifugo yao juu ya hizo ardhi za dhuluma.
2. Humfukuza punda wake asiye baba,
Maana yake humfukuza Punda wa Yatima, (mtoto asiye na Baba). Punda wake anapoingia mahali kula vichache vilivyosalia katika mashamba yao, wao humfukuza punda Yule, pasipo kuzingatia kuwa Yule ni yatima asiye na uwezo wa kujimudu mwenyewe, asiye na uwezo wa kununulia chakula punda wake, lakini wao hawajali hayo yote, bali wanazifukuza punda zake.
3. Humtwaa rehani ng’ombe wake mwanamke mjane.
Hawa watu pia wanachukua Ng’ombe za wanawake wajane, ambao wamefiwa na waume zao, na hata nguvu za kufanya kazi tena hawana!.. wanachukua Ng’ombe zao na kuwaweka Rehani, kutokana na mikopo wanawake hao waliyoichukua.. Jambo ambalo ambalo si jema machoni pa Mungu..Wangepaswa wawahurumie na kuwapa mikopo bila kuwawekea rehani chochote kwasababu wao hawana tumaini msaada wowote wapo wao kama wao, na umri wao umeshakwenda..
Kumbukumbu 24:17 “Usipotoshe hukumu ya mgeni, wala ya yatima; wala usitwae mavazi ya mjane, yawe rehani;
18 bali kumbuka ya kuwa ulikuwa mtumwa katika Misri, Bwana, Mungu wako, akakukomboa huko; kwa hiyo nakuamuru kutenda neno hili”
Hivyo watu wa namna hii ambao wanawatesa Wajane na Mayatima, Bwana Mungu alitaja hukumu yao katika kitabu cha Kutoka 22:22
Kutoka 22: 22 “Usimtese mjane ye yote aliyefiwa na mumewe, wala mtoto yatima.
23 Ukiwatesa watu hao katika neno lo lote, nao wakanililia mimi, hakika yangu nitasikia kilio chao,
24 na hasira yangu itawaka moto, nami nitawaua ninyi kwa upanga; na wake wenu watakuwa wajane, na watoto wenu mayatima”.
Hivyo na sisi hatuna budi kuwatendea Mema watu hawa, na kuwapenda ili na Bwana atubariki
Shalom
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Mtu asiye na akili ni nani kibiblia?
Kwanini wajane vijana hawakupaswa kuandikwa?
NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?
TENDA AGIZO LA YESU, HILO NDIO LITAKALOKULINDA.
Jina la Bwana na Mwokozi, Mkuu wa Uzima, Yesu Kristo lihimidiwe!..karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu.
Upo wakati ambao TAA ya Mungu itazima!.. Tuitikie wito wa Mungu, kabla ya huo wakati kufika..
1Samweli 3:2 “Ikawa wakati huo, Eli alipokuwa amelala mahali pake (tena macho yake yalikuwa yameanza kupofuka, hata asiweze kuona),
3 NA TAA YA MUNGU ILIKUWA HAIJAZIMIKA BADO, na Samweli alikuwa amelala katika hekalu la Bwana, palipokuwa na sanduku la Mungu;
4 basi, wakati huo Bwana akamwita Samweli; naye akasema, Mimi hapa.”
Sasa ili kuelewa vizuri Taa ya Mungu ni kitu gani, na ilikuwa inazimika wakati gani..hebu turejee ile Hema ambayo Musa aliagizwa aitengeneze, tunasoma Ilikuwa imegawanyika katika Sehemu kuu tatu, Ua wa Ndani, Patakatifu na Patakatifu pa patakatifu.
Na ndani katika Patakatifu, palikuwa na madhabahu ya uvumba, Meza ya mikate ya wonyesho pamoja na KINARA CHA TAA, ambacho kilikuwa na Mirija saba. (Tazama picha juu).
Hiki kinara cha Taa kazi yake ilikuwa ni kutia Nuru ile hema wakati wa USIKU. Kwamba Nyakati zote za usiku ni sharti ndani ya Hema kuwe na Nuru, na amri hiyo ilikuwa ni ya Daima, maana yake ya kila siku!.. haikupaswa hata Usiku mmoja upite bila Kinara hicho kuwashwa ndani ya Hema.
Kutoka 27: 20 “Nawe waamuru wana wa Israeli wakuletee mafuta ya zeituni safi ya kupondwa kwa ajili ya nuru, ili kufanya ile taa kuwaka daima.
21 Ndani ya ile hema ya kukutania, nje ya hilo pazia, lililo mbele ya huo ushuhuda, Haruni na wanawe wataitengeza TANGU JIONI HATA ASUBUHI MBELE YA BWANA; itakuwa ni amri ya milele katika vizazi vyao vyote kwa ajili ya wana wa Israel”
Tusome tena..
Walawi 24:1 “Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
2 Waagize wana wa Israeli kwamba wakuletee mafuta ya zeituni safi ya kupondwa kwa ajili ya ile nuru, ili hiyo taa iwake daima.
3 Hapo nje ya pazia la ushahidi, ndani ya hema ya kukutania, Haruni ataitengeza TANGU JIONI HATA ASUBUHI MBELE ZA BWANA DAIMA; ni amri ya milele katika vizazi vyenu”
Hapo mstari wa 3, unasema ataitengeneza “tangu jioni hata asubuhi” maana yake wataiwasha tangu jioni mpaka asubuhi, na kukiisha pambazuka basi taa ile inazimwa, kwasababu kulikuwa na Nuru ya mwanga wa Nje wa jua iliyokuwa inaingia ndani ya Hema.
Sasa tukirudi katika habari hiyo ya Samweli, maandiko yanasema Samweli alikuwa analala katika Hema karibu na sanduku la BWANA, na wakati ambapo Taa ya Mungu bado haijazimika..Maana yake bado hakujapambazuka, (kwasababu kukisha pambazuka tu, tayari ile taa ilikuwa inazimwa).
Wakati huo ndipo Samweli aliisikia Sauti ya Mungu ikimwita mara 4, na Samweli akaitikia wito wa Mungu.
Lakini ni nini tunajifunza katika hiyo habari?
Upo wakati ambao sauti ya Mungu inaita juu ya Mtu..na wakati huo ni wakati wa giza Nene juu ya maisha ya mtu.. Huo ndio wakati ambapo Mungu anamwita mtu, na anamwita kwa sauti ambayo inakuwa inayofanana na ya watu wa Mungu.. kiasi kwamba mtu anaweza kudhani ni mtu anayemwita/kumshawishi kumbe ni Mungu, ndio maana Samweli alipoitwa alikimbilia kwa Eli akidhani ni Eli anayemwita kumbe ni MUNGU.
Vile vile Mungu anawaita leo watu kutoka katika dhambi, na uvuguvugu lakini watu wanadhani ni wachungaji wao ndio wanaowaita, wengine wanadhani ni wahubiri ndio wanaowatafuta wawe washirika wao, pasipo kujua kuwa ni sauti ya Mungu ndio inayowaita na si watu.
Sasa endapo Samweli asingeitikia ule wito wakati ule ambapo TAA BADO HAIJAZIMIKA, huenda ile sauti ya Mungu asingeisikia tena kwa wakati ule mpaka labda kipindi kingine ambapo Taa hiyo itakuwa inawaka.
Ndugu TAA ya Mungu leo ni NEEMA, Hii Neema kuna wakati itasimama!, na hakutakuwa tena na nafasi ya kumkaribia Mungu, wakati ambao unyakuo wa kanisa utapita, ndio wakati ambao TAA itakuwa imezima, vile vile wakati ambao utaondoka katika haya maisha huo ndio wakati ambao Taa ya Mungu itakuwa imezimika juu yako.
Je umemkabidhi Yesu maisha yako?.. Umebatizwa katika ubatizo sahihi? Umeokoka?.. Kama bado ni vyema ukafanya hivyo sasa kabla Taa haijazimika.
Mhubiri 12:1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo.
Maran atha!
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Hema ya kukutania ni nini, na ilikuwaje?
Kiango na Pishi ni nini (Mathayo 5:15)?
NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA-KONDOO.