Category Archive maswali na majibu

Kuharimishwa ni nini, na kwanini Paulo aombe hivyo?(Warumi 9:2).

Jibu: Ili tuweze kuelewa vizuri tuanzia ule mstari wa kwanza, na tusome mpaka ule wa 5

Warumi 9:1  “Nasema kweli katika Kristo, sisemi uongo, dhamiri yangu ikinishuhudia katika Roho Mtakatifu,

2  ya kwamba nina huzuni nyingi na maumivu yasiyokoma moyoni mwangu.

3  Kwa maana ningeweza kuomba MIMI MWENYEWE NIHARIMISHWE NA KUTENGWA NA KRISTO KWA AJILI YA NDUGU ZANGU, JAMAA ZANGU KWA JINSI YA MWILI;

4  ambao ni Waisraeli, wenye kule kufanywa wana, na ule utukufu, na maagano, na kupewa torati, na ibada ya Mungu, na ahadi zake;

5  ambao mababu ni wao, na katika hao alitoka Kristo kwa jinsi ya mwili. Ndiye aliye juu ya mambo yote, Mungu, mwenye kuhimidiwa milele. Amina”

“Kuharimishwa” maana yake ni “kutengwa mbali na mtu/kitu (kwa ufupi kufanywa haramu)”.

Paulo aliomba kama ingewezekana Aharamishwe kwaajii ya ndugu zake katika mwili (yaani waisraeli), ili waokolewe.

Sasa kwanini aliomba vile, na je jambo hilo linawezekana?

Awali ya yote ili tuelewe vizuri hebu tuweke msingi kwanza kwa kuelewa agenda ya Wokovu ulioletwa na YESU KRISTO.

Wokovu kwamba ulianzia kwa Wayahudi, (soma Yohana 4:22) na baadaye ukahamia kwa watu wa mataifa.

Na kipindi Wokovu (injili) inahubiriwa kwa wayahudi, sisi watu wa mataifa tulikuwa tumeharimishwa, maana yake tulikuwa tumetengwa mbali na injili/neema, na kufanyika watu tusiostahili..

Waefeso 2:11 “Kwa ajili ya hayo kumbukeni ya kwamba zamani ninyi, mlio watu wa Mataifa kwa jinsi ya mwili, mnaoitwa Wasiotahiriwa na wale wanaoitwa Waliotahiriwa, yaani, tohara ya mwilini iliyofanyika kwa mikono;

12  kwamba zamani zile mlikuwa hamna Kristo, MMEFARAKANA NA JAMII YA ISRAELI, wageni wasio wa maagano ya ahadi ile. MLIKUWA HAMNA TUMAINI, HAMNA MUNGU DUNIANI”

Umeona?..kumbe kuna wakati sisi watu wa mataifa hatukuwa na Mungu (neema),Na wakati ulipofika waisraeli (wayahudi) walipomkataa Masihi YESU KRISTO, na kusema yeye siye yule aliyetabiriwa, Ndipo Ikafanya Neema iondoke kwao na kuja kwetu sisi watu wa mataifa, hivyo nao pia WAKAHARIMISHWA ili sisi tupate Neema..

Sasa Utauliza hilo tunalithibitisha vipi kimaandiko..

Warumi 11:30 “ KWA MAANA KAMA NINYI ZAMANI MLIVYOMWASI MUNGU, LAKINI SASA MMEPATA REHEMA KWA KUASI KWAO”

31  KADHALIKA NA HAO WAMEASI SASA, ILI KWA KUPATA REHEMA KWENU WAO NAO WAPATE REHEMA.

Soma pia  Matendo 28:28 na Matendo 13:46,utaona jambo hilo Zaidi.

Sasa Mtume Paulo kwa kulijua hilo kwamba “Neema imewaondokea Wayahudi wengi” na imeenda kwa watu wa MATAIFA, kwa mantiki hiyo hiyo akatamani kama ingewezekana IONDOKE kwake (yaani aharimishwe), ili irudi tena kwa WAISRAELI ndugu zake wapate kuokolewa.

Na neema ikiondoka juu ya mtu/watu maana yake ile nguvu ya kumwamini KRISTO inakuwa haipo tena!, kila kitu kumhusu YESU ni upumbavu kwa mtu huyo au watu hao, (Mfano wa PAULO alivyokuwa kabla ya kuokoka..alikuwa anaona injili ni upuuzi na Zaidi sana alikuwa anawaua wafuasi wa BWANA YESU). (Hiyo yote ni kutokana na neema kutokuwepo juu yake).

Sasa swali ni je! Jambo hilo aliloliomba Paulo linawezekana?..yaani Mungu anaweza kumharimisha yeye ili ndugu zake wapone?

Jibu ni LA! Ni jambo ambalo haliwezekani,..Paulo alisema vile kutokana na huruma na upendo kwa ndugu zake!..Ni sawa na mtu aliye mzima, aone ndugu yake anateseka na ugonjwa mbaya..na aombe ahamishiwe yale maumivu kwake kutokana na kumhurumia yule mgonjwa, na ndivyo Paulo alichokuwa anakiomba.

Kadhalika Mungu hawezi kuihamisha Neema aliyokupa na kuipeleka kwa mtu mwingine kwa wewe kumwomba...(hawezi kukupokonya uzima wa milele ikiwa umestahili uzima wa milele) Neema huwa inaondoka kutoka kwa mtu kwa njia ya matendo yake(kama matendo yake yakiwa hayafai, lakini si kwa kumwomba Mungu aihamishe kutoka kwako.

Je umeokoka?..kama bado unasubiri nini?

Fahamu kuwa tunaishi siku za mwisho na BWANA YESU yupo mlangoni.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MPAKA UTIMILIFU WA MATAIFA UTAKAPOWASILI.

JINSI YA KUITUMIA VYEMA NEEMA YA MUNGU ILIYO JUU YANGU.

SI KWA MATENDO BALI NEEMA.

MAMBO YATAKAYOTOKEA ISRAELI SIKU ZA HIVI KARIBUNI.

Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?

Rudi nyumbani

Print this post

Yahu ni nani? (Wimbo 8:6).

Jibu: Turejee,

Wimbo 8:6 “Nitie kama muhuri moyoni mwako, Kama muhuri juu ya mkono wako; Kwa maana upendo una nguvu kama mauti, Na wivu ni mkali kama ahera. Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni MIALI YA YAHU”.

“YAHU” ni jina lingine la “YAHWE” ambalo ndilo “YEHOVA”.

Kutoka 6:2 “Kisha Mungu akasema na Musa, akamwambia, Mimi ni YEHOVA; 

3 nami nilimtokea Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kama Mungu Mwenyezi, bali kwa jina langu YEHOVA sikujulikana kwao”.

Kwahiyo YAHU, YAHWE na YEHOVA ni jina Moja!

Lakini hapo katika Wimbo 8:6 maandiko yanasema kuwa “upendo una nguvu kama mauti”.. maana yake kama vile mauti ilivyo na nguvu kiasi kwamba wanaokufa ni ngumu kurudia uzima! Vile vile Upendo wa Mungu kwetu ni mkuu kiasi kwamba akitupenda ametupenda!, hakuna wakati atatuchukia, anaweza asipendezwe na sisi lakini si kutuchukia!.

Warumi 8:35 “Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?………

38  Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo,

39  wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Lakini pia anasema wivu ni mkali kuliko Ahera..Ahera ni “Kaburi”, Kwa urefu Zaidi fungua hapa >>>Ahera ni wapi? Kama tunavyosoma katika biblia.

Na miali yake ni miali ya YAHU. Maana yake ni kuwa Mungu ana upendo lakini pia anawivu, huwezi kamwe kutanganisha vitu hivi viwili, UPENDO na WIVU.

Kwahiyo kama Mungu ametupenda, basi hapendi kuona tunaabudu miungu mingine, tukifanya hivyo tunamtia yeye wivu, umbao unaweza kutupeleka kaburini (Ahera).

Kutoka 20:3 “Usiwe na miungu mingine ila mimi.

4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.

5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, NI MUNGU MWENYE WIVU; NAWAPATILIZA WANA MAOVU YA BABA ZAO, HATA KIZAZI CHA TATU NA CHA NNE CHA WANICHUKIAO, 

6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu”.

YAHU atusaidie tusimtie Wivu, lakini tumpende, na vile vile upendo wake utubidiishe katika kuyafanya mapenzi yake.

 

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Maran atha.

Mafundisho Mengine:

Wivu ni nini na kuna aina ngapi za Wivu?

UMETEKWA NA UPENDO WA KRISTO?

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

IJUE HEKIMA YA MUNGU KATIKA KUKUINUA KIMAISHA.

WEKA KUMBUKUMBU YA MAMBO BWANA ANAYOKUFANYIA KWASABABU YATAKUFAA MBELENI.

Rudi Nyumbani:

 

Print this post

Falaki ni elimu gani? (Isaya 47:13).

Falaki ni nini katika biblia?

Jibu: Turejee,

Isaya 47:12 “Simama sasa na uganga wako, na wingi wa uchawi wako, uliojitaabisha nao tangu ujana wako; labda utaweza kupata faida, labda utaweza kushinda. 

13 Umechoka kwa wingi wa mashauri yako; basi, na WASIMAME HAO WAJUAO FALAKI, wazitazamao nyota, watabirio kila mwezi mambo ya mwezi huo, wakakuokoe na mambo yatakayokupata”.

“Falaki” ni “elimu ya nyota na sayari na jua”.

Wanaofanya Falaki, wanaamini kuwa  “mpangilio wa nyota, mwezi na jua na sayari angani, unaathiri tabia ya nchi na tabia ya mtu/watu”. Jambo ambalo kwa sehemu moja ni kweli na sehemu nyingine uongo!.

Ni kweli Mpangilio wa Jua na mwezi, unaweza kuathiri tabia ya nchi, kama  vile vipindi vya mvua, kiangazi, au kipupwe….ipo miezi ambayo mvua inanyesha, na miezi ambayo mvua hainyeshi, ipo miezi ya kiangazi na miezi ya kipupwe…Majira ya mwezi wa 6 na 7 ni Kipindi ambacho jua linakuwa mbali na dunia na kweli nchi inaathirika na baridi kali, katika ukanda wa kusini wa dunia.

Vile vile tabia za mimea zinaathiriwa na majira na nyakati, yanayotokana na mpangilio wa mwezi na jua angani, mfano tabia za miembe kuzaa maembe zinaathiriwa na mwezi wa 12, kwamba yanapofika majira ya mwezi huo wa 12 mpaka wa 1 basi miti yote ya miembe inazaa sana, tofauti na kipindi kingine chote (kwahiyo kwa sehemu ni kweli).

Sasa kwa mantiki hiyo wana-falaki wanaamini kuwa kama mpangilio wa jua, mwezi na nyota angani unaweza kuathiri mazingira na hali ya hewa, basi vile vile mpangilio huo huo unaweza kuathiri tabia za watu, na hisia zao, na maamuzi yao na hata hatima yao!.

Kwamba kila tarehe na mwezi unabeba matukio yake kulingana na mtu na mtu, na pia kulingana na tarehe aliyozaliwa, vile vile mpangilio wa nyota na mwezi unaweza kuelezea ni kitu gani mtu atafanya, au atakitenda, au kitampata, vile vile ni bahati gani ipo mbele yake au hatari gani inamkabili.

Kwahiyo wote waliohitaji kujua mambo yatakayowapata mbeleni waliwatafuta hawa wana-Falaki, au kwa lugha nyingine wanajimu kujua hatima zao.

Lakini swali ni je! Elimu hii ina ukweli wowote na je wakristo ni sahihi kuitafuta, ili kujua hatima zetu kupitia falaki?

Jibu ni LA! Elimu hii haina ukweli wowote, mpangilio wa sayari na nyota, na mwezi hauwezi kuelezea tabia, hisia, maamuzi au hatima ya Mwanadamu!…mpangilio huo unaweza kufaa katika utabiri wa hali ya hewa na misimu ya kupanda na kuvuna (tena kwa sehemu ndogo) lakini hauwezi kutabiri maisha ya mtu.

Maisha ya mtu hayatabiriwi wala kusomwa kwa kutazama jua, au mwezi au nyota au sayari, kama ndivyo kulikuwa hakuna haja ya Kristo kuja, au hata kama angekuja basi angetuhubiria sana hiyo elimu, bali maisha ya mtu yanatabiriwa kwa KULITAZAMA NENO LA MUNGU peke yake!.

Ukitaka kujua kesho yako itakuwaje, isome biblia, itakuambia sio tu kesho utakuwa wapi, bali MILELE UTAKUWA WAPI!!!.

Utauliza vipi wale Mamajusi, mbona walioiona nyota ya Bwana YESU kutoka mashariki?.

Mungu alipenda kutumia ishara ya nyota kuelekeza utukufu wa mwanae alipozaliwa, lakini hakuwa anahubiri elimu ya nyota pale!, ni sawa na alivyotumia ishara ya Nguzo ya wingu au nguzo ya moto juu ya wana wa Israeli walipokuwa jangwani,.. ilikuwa ni kwa lengo la kuelekeza utukufu wa wana wake mahali walipo, lakini hakuwa anahubiri elimu za mawingu na moto, kwamba zikasomwe kwa bidii ili kuelezea utukufu juu ya mtu/watu.

Vile vile leo hii shetani anapenyeza elimu hii ya Nyota(Falaki) ndani ya kanisa kwa kasi sana!. Elimu hii inatoka kwa waganga na inahamia kanisani kwa kasi sana..Watu hawasomi tena biblia wanatafuta kusomewa nyota zao! Hawaombi tena kulingana na Neno wanaombea nyota kwa kurejea elimu ya falaki.

Ndugu usidanganyike!..Elimu ya nyota (Falaki) ni elimu ya shetani asilimia mia.

Kama unataka kusafisha hatima yako itii biblia, wala usitafute maombi ya kutakasiwa nyota!, hiyo ni elimu nyingine!… Vile vile ukitaka kujua kesho yako itakuwaje kasome biblia, usitafute utabiri wa kusomewa nyota kutoka kwa yoyote yule iwe mganga au anayejiita mtumishi wa Mungu.. Biblia pekee ndiyo itakayokuonyesha tabia yako na kukupa utabiri sahihi wa maisha yako ya kesho na ya milele.

Je umemwamini Yesu?, je umebatizwa ubatizo sahihi? Je umepokea Roho Mtakatifu?.

Bwana Yesu anarudi.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MSHIKE SANA ELIMU.

NYOTA ZIPOTEAZO.

Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?

Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.

MIEZI 13 YA KIYAHUDI.

Rudi nyumbani

Print this post

Haki ni Nini katika biblia. Haki ya Mungu ni ipi?

Haki maana yake ni kitu ambacho mtu anastahili kukipata. Kwamfano kuishi ni haki ya Kila mwanadamu, Hakuna mtu anayepaswa kumzuia mwingine kuishi, kisa ni mwanamke au ni mfupi, au ni kichaa, au mlemavu. Maadamu tu amekuwa mwanadamu tayari anayo haki ya kuishi.

Mfano mwingine wa haki, ni mtu aliyesoma  ukahitimu katika shahada Fulani labda tuseme ya utatibu, mtu kama huyo tunasema ana haki ya kuitwa daktari kwasababu amesomea jambo Hilo.

Vivyo hivyo katika Roho. Mungu naye anayo haki yake, katika kutoa vitu vyake.

Mwanzoni ilikuwa Ili kumkaribia Mungu na kupata kibali kwake na mema yote na baraka zote ilikupasa kwanza uishike Sheria yake yote. Hivyo yoyote aliyeweza kufanya hivyo alipatiwa haki hiyo. Soma Kumbukumbu 28

Lakini Kwa bahati mbaya hakukuwa na mtu aliyestahili kumkaribia Mungu kwasababu Hakuna mwanadamu aliyekwenda katika maagizo yote ya Mungu Kwa ukamilifu wote, bila kosa. Kwahiyo tangu zamani hakukuwa na mwanadamu hata mmoja aliyefanikiwa kumkaribia Mungu. Wote walitenda dhambi (Zaburi 14:3)

Hivyo Mungu akabuni mpango mwingine wa kumwokoa mwanadamu ili awe amestahili kupokea mambo yote ya rohoni ya Mungu, ikiwemo uzima wa milele na kumkaribia yeye.

Ndipo akamleta Yesu duniani, Ili Kila amwaminiye asipotee Bali apokee kuhesabiwa haki bure, bila kutegemea Tena matendo ya Sheria. Kwasababu Kwa matendo ya Sheria hakukuonekana aliyestahili.

Hivyo Mimi na wewe tunapomwamini Kristo kama ndiye Bwana na mwokozi pekee wa maisha yetu na kuukubali msamaha wake wa dhambi, basi tunahesabiwa tumestahili kuitwa watakatifu, na hivyo tunamkaribia Mungu katika ukamilifu wote, kumwomba yeye na kupokea vyote kutoka kwake bila sharti. Haleluya!

Warumi 3:21-24

[21]Lakini sasa, haki ya Mungu imedhihirika pasipo sheria; inashuhudiwa na torati na manabii; 

[22]ni haki ya Mungu iliyo kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote waaminio. Maana hakuna tofauti; 

[23]kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; 

[24]wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu; 

Hivyo ikiwa umekombolewa na Yesu Kristo, basi unapaswa uwe na ujasiri wote kumkaribia Mungu, bila kutegemea ukamilifu wako,Bali Kristo tu, na hivyo utapokea mema, yote kutoka Kwa Mungu.

Waebrania 4:16

[16]Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji. 

Hiyo Ndio inaitwa “HAKI itokayo Kwa Mungu” ambayo tunaipata kwa kupitia Yesu Kristo tu peke yake.

Kwa Yesu tunapokea uzima wa milele bure. Kwa Yesu Tunapokea majibu ya mahitaji yetu yote bure. Kwa Yesu tunaitwa watakatifu.

Lakini Swali ni je! Umemwamini Kristo? Kumbuka kamwe huwezi kumpendeza Mungu Kwa matendo yako pekee, Kila mwanadamu chini ya jua anamuhitaji Kristo.

Ikiwa Bado hajaokoka basi mlango upo wazi Leo. Tubu mgeukie Bwana akuponye. Ikiwa upo tayari kupokea msamaha wa dhambi Leo, na kufanywa kiumbe kipya, basi fungua hapa Kwa Mwongozo huo. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Mafundisho mengine

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

SI KWA MATENDO BALI NEEMA.

NJONI, NUNUENI MLE NA MNYWE.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mithali 16:30 Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka; 

SWALI: Nini maana ya Mithali 16:30

Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka;  Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya. 

JIBU: Mstari huo haumaanishi mtu anayefumba macho yake, Huwa anaishia kuwaza mawazo mabaya, hapana kama ni hivyo basi,  tungekuwa tunafanya makosa kufumba macho tunapoomba.

Zaidi sana mtu mwenye hekima huwa anapoona jambo la kutisha ovu, au lenye aibu Ndio anayekuwa wa kwanza kufumba macho yake asiruhusu kuona kinachoendelea.. kama vile walivyofanya watoto wa Nuhu.(Mwanzo 9:23)

Hali kadhalika anaposema mtu aikazaye (aifumbaye), midomo yake. Haimaanishi mtu asiyezungumza-zungumza, Huwa anaishia kuyazungumza maneno yasiyofaa. Kama ni hivyo biblia isingesema;

Mithali 21:23

[23]Mtu azuiaye kinywa chake na ulimi wake, Atajilinda nafsi yake na taabu. 

Lakini je? Vifungu hivyo vilimaanisha Nini?

Hapo anaposema afumbaye macho yake ni kuwaza yaliyopotoka,..alimaanisha afumbaye macho asitazame kweli (ambayo ni Neno la Mungu), linapomfundisha au kumwonya. Mtu huyo lengo lake ni kuendelea katika mawazo yake mabaya ya dhambi. Mfano aambiwapo kuishi na mke ambaye si wako ni uzinzi, na wazinzi sehemu Yao ni Katika ziwa la moto, lakini hataki kuliona au kulisikia Hilo andiko, jibu lake ni kuwa anataka kuendelea katika matendo yake ya giza.

Ndicho kilichokuwa Kwa waliompinga Yesu., Ndio maana akasema  maneno haya; 

Mathayo 13:15 Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema, 

Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya. 

Vilevile anaposema “Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya”

Anamaanisha, aizuiaye midomo yake kusema maneno ya uzima, ya staha, ya kujenga, ya adabu, ya maarifa, ya busara n.k.. Mwisho wake utakuwa ni kunena maneno mabaya tu.

Bwana alisema..

Luka 6:45

[45]Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake. 

Vivyo na hivyo na sisi, hatuna budi tujipime na kujichunguza…macho yetu hutazama Nini, vinywa vyetu vimejawa na maneno gani.? Lakini fahamu kuwa huwezi kushinda jicho lako, au ulimi wako ikiwa Kristo hajaumbika ndani yako.

Je! Unataka msaada Kwa Yesu Kristo? Kama jibu ni Ndio, basi unachopaswa kufanya cha kwanza ni kuyaachilia maisha yako kwake. Ili akusamehe dhambi zako. Ndipo akupe nguvu ya kushinda dhambi.

Hivyo bofya hapa Kwa ajili ya Mwongozo wa Sala ya Toba.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

NI WAKATI UPI UTAUONA USO WA KRISTO?

MWANANGU, NIPE MOYO WAKO;

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya mbingu na nchi zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe? (Mathayo 24:35).

Jibu: Turejee,

Mathayo 24:35  “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe”

Ili tuelewe vizuri, tutafakari kwanza mstari ufuatao…

Waebrania 13:8 “Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele”.

Mpaka maandiko yaseme kuwa “Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele”… Maana yake kuna watu, au vitu ambavyo haviwezi kuwa vile vile jana, leo na hata milele.

Kwa mfano mtu hawezi kuwa na tabia ile ile, au msimamo ule ule jana na leo na hata milele,..ni lazima tu utafika wakati tabia yake itabadilika, mtazamo wake utabadilika, utendaji wake utabadilika au hata msimamo wake!…. lakini KRISTO YESU yeye ni yule yule, kitabia, na kiutendaji, hajawahi kusema jambo halafu akajikosoa.. ni yeye yule na ataendelea kuwa vile vile Milele.

Hali kadhalika, vitu tunavyoviona katika mbingu kama jua, mwezi  na nyota, ijapokuwa tunaona vimedumu kuwa vilevile kwa maelfu ya miaka, lakini biblia inatabiri kuwa siku moja vitatoweshwa vyote…

Ufunuo 6:12 “Nami nikaona, alipoifungua muhuri ya sita, palikuwa na tetemeko kuu la nchi; jua likawa jeusi kama gunia la singa, mwezi wote ukawa kama damu,

13  na NYOTA ZIKAANGUKA juu ya nchi kama vile mtini upukutishavyo mapooza yake, utikiswapo na upepo mwingi.

14  MBINGU ZIKAONDOLEWA KAMA UKURASA ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake”.

Vile vile vitu tunavyoviona katika “NCHI” kama vile milima, na habari ambavyo tunaviona kama zimedumu kwa maelfu ya miaka, lakini bado biblia inatabiri kuwa siku moja vitafutika..

Ufunuo 16:20  “Kila kisiwa kikakimbia, wala milima haikuonekana tena”

Soma pia Ufunuo 21:1..

Lakini wakati ambapo vitu vyote hivi vinaondolewa (maana yake VINAPITA) Bado Kristo atabaki kuwa yeye yule, na maneno yake yatabaki kuwa yale yale, na yana nguvu ile ile katika umilele wote.

Kwamfano maneno ya Yesu anayosema yeye ni ALFA na OMEGA, yaani Mwanzo na Mwisho (katika Ufunuo 21:6 na Ufunuo 22:13) yataendelea kuwa hivyo hivyo Milele, hakuna wakati utafika Kristo ataacha kuwa Alfa na Omega…jua na mwezi na nyota na wanadamu watapita, lakini maneno hayo yataeendelea kuwa halisi hivyo hivyo milele na milele.

>Vile vile maneno yake aliyosema kuwa “Yeye ndio Njia, Kweli na Uzima (Yohana 14:6)” yataendelea kuwa hivyo milele na milele, hakuna wakati utafika ambao Kristo ataacha kuwa Njia, au ataacha kuwa  Kweli au ataacha kuwa Uzima..Kristo YESU sasa ni Uzima, na ataendelea kuwa UZIMA hivyo hivyo milele na milele.

>Vile vile aliposema kuwa yeye ni “Nuru ya Ulimwengu (Yohana 8:12)”…Maneno hayo hautafika wakati ambao yata-expire… Jua na mwezi kuna wakati vitaisha muda wake wa matumizi, jua litaondolewa halitamulika tena, na mwezi utaondolewa hautaangaza tena.. lakini Kristo ataendelea kuwa NURU hata kipindi ambacho jua na mwezi havipo..

Ufunuo 21:23  “Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, KWA MAANA UTUKUFU WA MUNGU HUUTIA NURU, NA TAA YAKE NI MWANA-KONDOO”.

> Vile vile maneno yake mengine yanamtaja yeye kama “Mwaminifu na wa Kweli (katika Ufunuo 3:14, na Ufunuo 19:11)”. Yeye atabaki kuwa hivyo Milele na milele, hakuna wakati ambao atabadilika na kukosa uaminifu!… Sisi wanadamu tunaoishi chini ya jua na juu ya nchi, tutakuwa waaminifu tu kwa kitambo Fulani lakini si milele. Lakini yeye ataendelea kuwa mwaminifu milele na milele hata wakati ambao mbingu zitafutwa, na kuletwa mbingu mpya na nchi mpya, bado ataendelea kuwa mwaminifu.

> Pia alisema wote wamwaminio yeye watakuwa na uzima wa milele, hakuna wakati hilo Neno litabadilika, kwamba awanyime uzima wa milele wale wote waliomwamini na kuishi kwa kuzifuata amri zake.. Majira yatabadilika, vipindi vitabadilika lakini milele na milele hawezi kujisahihisha maneno yake hayo. AKIAHIDI AMEAHIDI!!.. Na milele habadiliki.

Na maneno mengine yote yaliyosalia aliyoyasema BWANA YESU hakuna hata moja litapita!!! , yote yatabaki kuwa vile vile

Je umemwamini huyu Mkuu wa UZIMA asiyeweza KUBADILIKA?, Au Unawatumainia wanadamu ambao leo wapo na kesho hawapo, leo wanaahidi na kesho wamebadilika, leo wanakupenda kesho wanakuchukia.. Ni heri ukaanza kumtumainia yeye asiyeweza kubadilika, YESU KRISTO, MFALME WA WAFALME, na BWANA WA MABWANA.

Mungu akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Mafundisho Mengine

Mbinguni ni sehemu gani?

Kuna Mbingu ngapi?

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

INJILI YA MILELE NI IPI KATIKA BIBLIA?

Je! Sulemani alienda mbinguni?

Rudi Nyumbani:

 

 

Print this post

Gudulia ni nini? (1Samweli 26:11).

Jibu: Tusome,

1Samweli 26:11 “Hasha! Nisiunyoshe mkono wangu juu ya masihi

12 Basi Daudi akalitwaa lile fumo, na lile GUDULIA LA MAJI, kichwani pa Sauli; nao wakaenda zao, wala hapana mtu aliyeliona jambo hili wala kulijua, wala kuamka; maana wote walikuwa wamelala; kwa kuwa usingizi mzito kutoka kwa Bwana umewaangukia”.

Gudulia ni chombo maalumu kilivyotengenezwa kwa lengo la kuhifadhia maji ya kunywa ya watu wachache, kwa lugha ya sasa hivi tunayaita “majagi”

Magudulia/majagi ya zamani yalitengenezwa kwa malighafi tofauti na ya zama hizi. Zamani majagi/magudulia waliyatengeneza kwa kutumia udongo wa (mfinyanzi tazama picha juu), lakini sasa yanayotumika mengi yao yametengenezwa kwa glasi au plastiki.(tazama picha chini).

Gudulia ni nini?

Mistari mingine inayotaja chombo hiki (gudulia) ni pamoja na 1Wafalme 19:6, Yeremia 19:1 na Yeremia 19:10.

Je umemwamini Bwana Yesu?, je unajua kuwa tunaishi katika majira ya kurudi kwa YESU mara ya pili, na wakati wowote unyakuo wa kanisa utatokea?.

Bwana atusaidie.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Shilo ni wapi?

TWEKA MPAKA VILINDINI.

WALA HAKUACHA MTU ACHUKUE CHOMBO KATI YA HEKALU.

Ni nani aliyemshawishi Daudi akawahesabu Israeli? Ni Mungu au shetani?

JINSI YA KUISHINDA HALI YA MSONGO WA MAWAZO.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “SAA INAKUJA” na “SASA IPO” (Yohana 4:23).

Jibu: Turejee,

Yohana 4:19  “Yule mwanamke akamwambia, Bwana, naona ya kuwa u nabii!

20  Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia.

21  Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.

22  Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.

23  Lakini SAA INAKUJA, NAYO SASA IPO, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba KATIKA ROHO NA KWELI. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu”.

Maana ya kumwabudu Baba katika roho na kweli, ni KUMFANYIA MUNGU IBADA, KATIKA ROHO MTAKATIFU NA KATIKA KWELI YA NENO LAKE.

Yohana 16:13 “Lakini yeye atakapokuja, huyo ROHO WA KWELI, ATAWAONGOZA AWATIE KWENYE KWELI YOTE…”

Sasa BWANA YESU aliposema kuwa “SAA INAKUJA”, alimaanisha kuwa kuna kipindi kinakuja  mbeleni, ambacho waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli, na wakati huo si mwingine Zaidi ya ule wa Pentekoste. Kipindi ambacho Roho Mtakatifu atamwagwa juu ya kanisa kwa mara ya kwanza, baada ya BWANA YESU kuondoka!.

Huo ndio uliokuwa mwanzo wa watu kumwabudu Baba katika roho na kweli. (Matendo 2:1-15)

Lakini pia aliposema kuwa..“NA SASA IPO”…. maana yake hata huo wakati tayari Baba ameshaanza kuabudiwa katika roho na kweli. Na aliyekuwa anamwabudu baba katika ROHO NA KWELI ni yeye mwenyewe BWANA YESU KRISTO. Kwasababu tayari alikuwa na Roho Mtakatifu ndani yake, ambaye alipoondoka ndipo akammwaga juu ya kanisa.

Yohana 16:7 “Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu”.

Na hata sasa tupo kipindi ambacho Neema ya Roho Mtakatifu bado ipo duniani kwa kila anayemwitaji sawasawa na Matendo 2:38, Na kumbuka Roho Mtakatifu pekee ndiye funguo za mtu kumwabudu Mungu katika roho na kweli, na pasipo yeye haiwezekani kumwabudu Mungu katika roho.

Kwa somo refu lihusuyo jinsi ya kumwabudu Mungu katika roho na kweli fungua hapa >>Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “Saa yangu haijawadia?”

Ni muda gani Bwana Yesu alisulibiwa. Je! Ni saa 3 au saa 6?

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

UWEZO WA KIPEKEE.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya  Mithali 21:1 Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana;

SWALI: Nini maana ya  Mithali 21:1

“Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana; Kama mifereji ya maji huugeuza po pote apendapo”.


JIBU: Kuna mithali inayosema “maji hufuata mkondo”. Ikiwa na maana, palipo na mfereji kule kule unapoelekea ndipo maji nayo huelekea. Mfano ukielekeza mrefeji shambani mwako, basi maji yale yataelekea huko si kwingineko, ukielekezea mfereji nyumbani mwako, basi maji yatakuja ndani mwako. Kamwe maji  hayajiamulii  pa kuririkia.

Vivyo hivyo na Mungu, ndivyo anavyofananisha mamlaka yake juu ya wafalme na wakuu wa dunia hii. Kwamba mashauri yao, hawajiamulii tu peke yao kwa kujitakia. Kwamfano utakumbuka kuna wakati  Mungu alimnyanyua Moyo Koreshi mtawala wa Uajemi ili awape ruhusu wayahudi warudi katika nchi yao wakamjengee nyumba.

Ezra 1:1 Ikawa katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, ili kwamba neno la Bwana alilolisema kwa kinywa cha Yeremia lipate kutimizwa, Bwana akamwamsha roho yake Koreshi, mfalme wa Uajemi, hata akapiga mbiu katika ufalme wake wote, akaiandika pia, akisema,  2 Koreshi, mfalme wa Uajemi asema hivi;  3 Basi kila mtu katika ninyi nyote mlio watu wake, Bwana, Mungu wake, na awe pamoja naye, na akwee mpaka Yerusalemu, ulioko Yuda, akaijenge nyumba ya Bwana, Mungu wa Israeli, (yeye ndiye Mungu), iliyoko Yerusalemu.  4 Na mtu awaye yote aliyesalia mahali po pote akaapo hali ya ugeni, na asaidiwe na watu wa mahali pake, kwa fedha, na dhahabu, na mali, na wanyama, zaidi ya vitu vitolewavyo kwa hiari ya mtu, kwa ajili ya nyumba ya Mungu, iliyoko Yerusalemu

Mungu huyo  huyo ndiye aliyemfanya mfalme Nebukadreza kuwa na moyo mkatili ili awachukue watu wake utumwani kwasababu ya makosa yao.(Yeremia 27:6, 43:10)

Mungu anaweza kuwatumia watawala kuadhibu taifa, au kuwabariki watu wake. Hii ni kuonyesha kuwa hakuna tawala yoyote katika hii dunia inamilikiwa na fikra za mwanadamu asilimia 100, bali mengi ya mashauri ya wakuu hutoka juu mbinguni, au yameruhusiwa na Mungu. Wao ni kama maji tu yanayofuata mkondo wa kusudi la Mungu.

Ndio jambo ambalo Mungu alimwambia Mfalme Nebukadreza kwamba “aliye juu ndiye anayetawala”(Danieli 5:21) lakini yeye alidhani ni uongo, mpaka siku alipoondolewa kwenye ufalme wake kwa miaka 7, na kurudishwa baadaye.

Hivyo, jambo hili, sio tu la viongozi wa kidunia, lakini pia hata wa kanisani. Ikiwa kanisa ulilopo linasimamia kweli na utakatifu na Kristo Yesu ndio kiini cha fundisho lao, basi waheshimu sana viongozi wako, kwasababu si kila shauri linalotoka kwenye vinywa vyao, ni wao wamefikiria. Wao ni kama maji tu yaliyomwagwa kwenye mfereji, ili kukuongoza wewe. ukishandana nao, au ukipuuzia kuongozwa nao, wakati mwingine unapingana na maamuzi ya Mungu wako bila kujijua.

Waheshimu viongozi wako wanaokulea kiroho, kama vile unavyowaheshimu watawala ya kidunia.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Fahamu maana ya Mithali 29:4 “Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.

Ni kwa namna gani Kristo analitakasa kanisa kwa Maji katika Neno? (Waefeso 5:26)

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

ITAMBUE KARAMA YA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Mabibi wastahiki walikuwa ni watu gani? (Esta 1:18).

(Mada maalumu kwa wanawake)

Jibu: Mabibi Wastahiki ni “wanawake wa heshima”.. kundi hili la wanawake lilihusisha wake za Wafalme, Maliwali au Maakida au Majumbe..

Wakati mfalme Ahasuero alipowafanyia maakida wake na maliwali wake karamu, biblia inatuambia kuwa Malkia Vashti (mke wa mfalme), yeye naye aliwafanyia wanawake (ambao ni wake wa hao maakida na maliwali) karamu.

Esta 1:2 “siku zile mfalme Ahasuero alipoketi katika kiti cha enzi cha ufalme wake, huko Shushani ngomeni;

3 mwaka wa tatu wa kumiliki kwake, ikawa aliwafanyia karamu maakida wake wote na majumbe wake; wakuu wa Uajemi na Umedi, watu wenye cheo na maakida wa majimbo, wakihudhuria mbele zake. 

4 Akawaonyesha utajiri wa ufalme wake mtukufu, na heshima ya enzi yake bora siku nyingi, maana siku mia na themanini……………………..

9 Tena Vashti, malkia, naye akawafanyia karamu WANAWAKE NDANI YA NYUMBA YA KIFALME YA MFALME Ahasuero”.

Sasa hao wanawake waliokuwa wake za “maliwali na maakida” ndio waliojulikana kama “mabibi wastahiki”.. wakiongozwa na Malkia Vashti.

Lakini tunachoweza kujifunza ni kuwa ile karamu ya hawa wanawake haikuwa na utukufu wowote, kwani iliishia kuleta aibu kubwa katika ufalme wote wa Uajemi. Kwani Malkia Vashti alikosa utii kwa Mfalme alipoitwa, na zaidi sana alionyesha dharau hizo mbele ya Mfalme na maliwali wake wote.

Na huenda pia kiburi hicho kilichochewa na jopo la wale wanawake wengine wastahiki waliohudhuria karamu hiyo ya Malkia Vashti. Hiyo ikifunua kuwa hakuna cha maana walichokuwa wanakizungumza au kukipanga katika hiyo karamu Vashti aliyowaandalia, huenda yaliyokuwa yanazungumziwa kule ni UMBEA TU na kusema mapungufu ya waume zao!

Hiyo ikamfanya Vashti apoteze umalkia wake, na hata hao wanawake wengine ambao wastahiki kuzidi kutawaliwa na waume zao.

Esta 1:16 “Basi Memukani akajibu mbele ya mfalme na maakida, Huyu Vashti, malkia, hakumkosa mfalme tu peke yake, ila na maakida wote, na watu wote pia walioko katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero. 

17 Kwa maana tendo hilo la malkia litajulikana na wanawake wote, hata waume zao watadharauliwa machoni pao, itakaponenwa ya kuwa mfalme Ahasuero aliamuru Vashti, malkia, aletwe mbele yake, bali hakuja. 

18 Hata na leo hivi mabibi wastahiki wa Uajemi na Umedi waliokwisha kuzisikia habari za tendo lake malkia watawaambia vivi hivi maakida wote wa mfalme. Hivyo kutatokea dharau nyingi na ghadhabu tele.

 19 Basi mfalme akiona vema, na itoke kwake amri ya kifalme, nayo iandikwe katika sheria za Waajemi na Wamedi isitanguke, ya kwamba Vashti asifike tena mbele ya mfalme Ahasuero; na umalkia wake mfalme ampe mwingine aliye mwema kuliko yeye.

 20 Basi mbiu ya mfalme atakayoipiga itakapotangazwa katika ufalme wake wote, nao ni mkubwa, wake wote watawaheshimu waume zao, wakubwa kwa wadogo.

 21 Basi neno hili likawapendeza mfalme na maakida; naye mfalme akafanya sawasawa na neno lake Memukani.

 22 Kwa maana alipeleka nyaraka katika majimbo yote ya mfalme, kila jimbo kwa mwandiko wake, na kila taifa kwa lugha yake, ya kwamba kila mwanamume atawale nyumbani mwake, na kuitangaza habari hii kwa lugha ya watu wake”.

Tabia kama hii inaendelea mpaka leo kwa baadhi ya wanawake walioolewa!, ambao baada ya kuolewa wanawaona waume zao kama si kitu tena, na hata kupoteza UTII kwao!. Pasipo kujua kuwa kwa kufanya hivyo wanazidi kujipotezea nafasi zao ndani ya familia zao, kwani badala ya kuwa kichwa Mungu anawaweka kuwa wa mwisho.

Neno la Mungu linasema wanawake na wawatii waume zao.

1Petro 3:1 “Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;

2  wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu.

3  Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

4  bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.

5  Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, NA KUWATII WAUME ZAO”

Soma tena Waefeso 5:24 na Tito 2:5 utaona jambo hilo hilo, sasa mwana-mama unatolea wapi kiburi!!!. Badilika, na anza kuwa mtii, ikiwa haupo ndani yako, na hiyo ni kwa faida yako na familia yako. Kitabu cha Esta, huenda kingepaswa kiitwe kitabu cha Vashti, lakini kwa kiburi chake, umalkia wake akapewa Esta.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

ESTA: Mlango wa 5, 6 & 7

LITANIA YA BIKIRA MARIA JE! NI SALA YA KIMAANDIKO?

YESU ANAKWENDA KUIBADILISHA OFISI YAKE.

NI KIJIJI CHA AINA GANI UPO?

MAJESHI YA PEPO WABAYA.

Rudi nyumbani

Print this post