SWALI: Nini maana ya Waefeso 6:24, pale inaposema “katika hali ya kutoharibika”?
[24]Neema na iwe pamoja na wote wampendao Bwana wetu Yesu Kristo katika hali ya kutokuharibika.
JIBU: Mtume Paulo alipokuwa anahitimisha ujumbe wa waraka wake kwa waefeso, alimalizia kwa kuwatamkia neno la heri watu watu wale akiwaambia ‘NEEMA ikae pamoja nao.
Lakini tunaona hapo hakukusudia tamko hilo kwa watu wote, bali anasema ikae kwa wale wampendao Bwana, lakini bado sio tu kwa wampendao Bwana.. Bali wampendao katika “hali ya kutokuharibika”.
Yaani kwa ufupi upendo usio poa.. Ndio upendo usio haribika.
Ndio ule unaozungumziwa kwenye 1Wakoritho 13. Kwamba hustahimili yote, huvumilia yote, huamini yote, haupungui Neno wakati wowote.
Ni kuonyesha kuwa Bwana wetu Yesu Kristo anastahili kupendwa daima, zaidi ya vitu vyote, kwasababu ya upendo wake mkuu aliotuonyesha sisi wa kuacha vyote mbinguni kwa ajili yetu, ili tukombolewe. Na kwa rehema zake akatupa na vipawa kabisa, na uwezo wa kuitwa wana wa Mungu, kwa nguvu za Roho wake Mtakatifu aliyetupa . Hakika anastahili kupendwa sana bila ukomo.
Zingatia: Waraka huu sio wa waefeso tu, bali ni wetu pia sote tumeandikiwa. Hivyo tutaongezewa neema ikiwa tutampenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa upendo usio haribika. Sio njaa itufanye tumwache, au ufukara, au mke, au kazi, au uzuri, au ubaya, au ndugu, au mali, au afya, au ugonjwa.. au kitu chochote, Bali kila wakati sisi shauku yetu kwa Kristo iwe ni ile ile. Kuomba ni kule-kule, kumtafuta Mungu ni kule-kule. Amen
Neema ya Bwana iwe nasi.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
JE! SISI KAMA WAKRISTO NI DHAMBI KUSHEHEREKEA KRISMASI?.
TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.
Lalama kwa uhai wa watoto wako wachanga wazimiao kwa njaa(Maombolezo 2:19)
Rudi Nyumbani
Print this post
Mithali 13:20 Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.
Tulipokuwa watoto wazazi wetu walitufundisha kubagua baadhi ya marafiki tuliokuwa nao, na cha ajabu vigezo walivyotumia havikuwa hata rangi zao, au kimo chao, au afya zao, bali tabia zao na akili zao. Wale watoto waliokuwa na nidhani, na akili shuleni wazazi wetu walitushurutisha sana kukaa nao karibu, kwasababu waligundua kuwa na sisi tutaambukizwa tabia zao, lakini wale waliokuwa watukutu, hata tulipokutwa tunacheza nao tu, tuliadhibiwa, sisi tuliona kama ni uonevu usio kuwa na tija, lakini baadaye tulipokuwa watu wazima, na kuona hatma ya wale watoto, ndio tulijua ni nini wazazi wetu walikuwa wanakiona.
Vivyo hivyo katika maisha ya rohoni, tunaambiwa.
Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.
Ni watu waliookoka, wenye hofu ya Mungu ndani yao.
Mtu yeyote aliyemwamini Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yake, huku akiendelea katika kumcha Mungu kwelikweli, huyo ni wa kukaa karibu naye sana. Kwasababu na wewe utajifunza njia za wokovu, utaambukizwa kuomba, utaambukizwa mifungo, utaambukizwa upendo wa ki-Mungu, lakini pia na maarifa ya Neno la Mungu, pamoja na uinjilisti.
Watu hawafahamu kuwa hata hekima ya mwokozi wetu Yesu haikuja tu kwa kutegemea hekima kutoka juu kwa baba yake, hapana, ilichangiwa pia na watu aliowachagua kukaa nao karibu, tangu alipokuwa mdogo, tunalithibitisha hilo pindi alipokuwa amekwenda Yerusalemu na wazazi wake kwa ajili ya kuila sikukuu, kama kijana angeweza kukaa na wenzake, kujifunza uchezaji wa kamari, au kutembea mitaani kutafuta wasichana, au kwenda kwenye dansi na sinema, na kujiunga na makundi ya wavuta bangi. Lakini, haikuwa hivyo kwake, yeye alichagua watu ambao wangekuwa ni wa muhimu kwake, ndio wale viongozi wa imani na waalimu waliotwa marabi, akawa akiwasikiliza hao na kuwauliza maswali, na ghafla akaambukizwa tabia zao, mpaka akawa yeye ndio RABI wao mkuu.
Luka 2:40 Yule mtoto akakua, akaongezeka nguvu, amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake. 41 Basi, wazee wake huenda Yerusalemu kila mwaka, wakati wa sikukuu ya Pasaka. 42 Na alipopata umri wake miaka kumi na miwili, walipanda kama ilivyokuwa desturi ya sikukuu; 43 na walipokwisha kuzitimiza siku, wakati wa kurudi kwao, yule mtoto Yesu alibaki nyuma huko Yerusalemu, na wazee wake walikuwa hawana habari. 44 Nao wakadhani ya kuwa yumo katika msafara; wakaenenda mwendo wa kutwa, wakawa wakimtafuta katika jamaa zao na wenzao; 45 na walipomkosa, wakarejea Yerusalemu, huku wakimtafuta. 46 Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, AMEKETI KATIKATI YA WAALIMU, AKIWASIKILIZA NA KUWAULIZA MASWALI. 47 Nao wote waliomsikia walistaajabia fahamu zake na majibu yake. 48 Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni. 49 Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu? 50 Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia
Luka 2:40 Yule mtoto akakua, akaongezeka nguvu, amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake. 41 Basi, wazee wake huenda Yerusalemu kila mwaka, wakati wa sikukuu ya Pasaka.
42 Na alipopata umri wake miaka kumi na miwili, walipanda kama ilivyokuwa desturi ya sikukuu;
43 na walipokwisha kuzitimiza siku, wakati wa kurudi kwao, yule mtoto Yesu alibaki nyuma huko Yerusalemu, na wazee wake walikuwa hawana habari.
44 Nao wakadhani ya kuwa yumo katika msafara; wakaenenda mwendo wa kutwa, wakawa wakimtafuta katika jamaa zao na wenzao;
45 na walipomkosa, wakarejea Yerusalemu, huku wakimtafuta. 46 Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, AMEKETI KATIKATI YA WAALIMU, AKIWASIKILIZA NA KUWAULIZA MASWALI.
47 Nao wote waliomsikia walistaajabia fahamu zake na majibu yake. 48 Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni.
49 Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu? 50 Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia
Mambo mengine hutaweza kuyaacha, au tabia nyingine hutaweza kuziondoa ndani yako. Kama hutaweka machaguzi ya watu sahihi wa kuongozana nao. Utakuta ni mkristo analalamika ni mzito wa kuomba, au kushuhudia, au kufunga. Ukiangalia kampani ya watu wake muda wote, ni wafanyakazi wenzake wa ofisini, ni marafiki zake wa chuo, ni majirani zake hapo mtaani. Lakini wapendwa, au watumishi wa Mungu waaminifu, ni jumapili tu kukutana nao kanisani, hata anapotafutwa, kukumbushwa wajibu wake kiroho, anawakwepa. Na wakati huo huo anatumainia awe moto kiroho. Hapo ni kujidanganya.
Tunahitaji kupashana moto, kamwe huwezi simama kipeke yako, haijalishi wewe ni nani, au unamjua Mungu kwa ukubwa kiasi gani. Tembea na waombaji ili uwe mwombaji, tembea na washuhudiaji ili uweze kushuhudia, kaa na waalimu ili uwe mwalimu. Nje ya hapo utageuzwa na ulimwengu,.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Usimwache rafiki yako mwenyewe, wala rafiki ya baba yako.
NGUVU YA HEKIMA NA AKILI
IVUMBUE INJILI YA KRISTO KUTOKA KATIKA KILA JAMBO.
SWALI: Nini maana ya hii Mithali 10:25
Kisulisuli kikiisha pita asiye haki hayuko tena; Bali mwenye haki ni msingi wa milele.
JIBU: Mstari huo unajifafanua vizuri kwenye ule mfano Bwana Yesu aliutoa kuhusiana na watu wanaoyasikia maneno yake, halafu hawayatendi. Tusome.
Mathayo 7:24 Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba; 25 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba. 26 Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga; 27 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.
Mathayo 7:24 Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;
25 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba.
26 Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;
27 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.
Hivyo tukirejea katika vifungu vile vya kwenye mithali. Unaweza kuelewa mtu asiye haki hasaa ni nani?
Ni Yule ambaye anaisikia injili, halafu hatii. Mtu Yule anayesema ameokoka, lakini zao la wokovu halionekana ndani yake. Rohoni anaonekana hana tofauti na yule ambaye hajamjua Mungu kabisa. Wote hao huitwa wasio haki. Bado wapo dhambini, hawajakombolewa na damu ya Yesu Kristo.
Hawa wataonekana kwa nje kama vile ni watakatifu. Lakini kinapokuja tu kisulisuli aidha cha majaribu, shida, dhiki, udhia,au mapigo kwa ajili ya Kristo, mara ghafla wanarudi nyuma, wanakuwa kama watu ambao hawajawahi kumjua Mungu kabisa, kwasababu hakujikita katika mwamba. Wengine sio majaribu ya shida, bali yale ya mafanikio makubwa, ndio hapo anasa zinawazidi wanamsahau Mungu, wanaiaga imani, kwani walimfuata Yesu kwasababu ya shida tu. Wengine ndoa, elimu, vyeo wakishavipata, huwaoni tena kwa Yesu.
Lakini mtu anayeyasikia maneno ya Kristo na kuyatii, ni kinyume chake, huitwa msingi wa milele. Huyo hatikiswi na wimbi, kisulisuli au dhoruba yoyote. Kwasababu yupo juu ya mwamba.
Okoka, upokee msamaha wa dhambi, kisha ishi kufuata na toba yako, ili uhakika wa kusimama uwe nao wakati wote.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
MWAMBA WETU.
Mtu asiye na akili ni nani kibiblia?
WhatsApp
SWALI: Nini maana ya Mithali 27:15 Kutona-tona daima siku ya mvua nyingi, Na mwanamke mgomvi ni sawasawa;
JIBU: Neno Kutona-tona kama lilivyotumika hapo, ni “maji yanayovuja darini”.
Hivyo anaposema Kutona-tona daima siku ya mvua nyingi. Anamaanisha kitendo cha kuvuja sana kwa dari siku ya mvua nyingi, na kitendo cha kukaa na mwanamke mgomvi ndani ni sawasawa.
Kwa namna gani?
Tunajua ukikaa kwenye nyumba ambayo dari lake halikujengwa vizuri, mvua kubwa inaponyesha maji mengi huchuruzika na kuingia ndani. Wakati umelala utashangaa maji yanakudondekea kitandani mwako, yanachuruzikia kwenye makochi, yanakwenda mpaka kwenye makapeti, jambo ambalo litakufanya usitulie hata kidogo humo ndani utakuwa tu bize, kusogoza vitu ovyo ovyo visilowe, na mbaya ni pale mvua inapokuwa kubwa, na maji kuongezeka ndani, mwisho huwa ni kutoka kabisa nje na kuiacha nyumba.
Ikiwa umeshawahi kupitia changamoto kama hiyo ya kuvujiwa nyumba, unaelewa ni kero kiasi gani.
Ndivyo anavyofananisha kutendo hicho na kuishi na mwanamke mgomvi. Ikilenga hasaa wanandoa. Kumbuka aliyeandika mithali hizi ni Sulemani, alikuwa anatambua anachokisema, kwasababu aliishi na wanawake elfu moja(1000) kama wake zake, na alijua masumbufu yao. Alikutana na changamoto za baadhi yao.
Mwanamke mgomvi, kibiblia ni Yule asimheshimu mumewe, ni Yule anayemwendesha mumewe, anayemkaripia, asiyekuwa msikivu, kila jambo analolifanya mumewe ni kulikosoa tu, mwenye kiburi na mwenye maneno mengi, asiye na staha.
Wanawake wa namna hii, huwataabisha waume zao sana, na hatimaye wengine huwafanya wahame kabisa nyumba, kukaa mbali na familia zao. Ni dari linalovuja utawezaje kukaa kwenye nyumba hiyo?
Andiko hilo limerudiwa pia katika;
Mithali 19:13 Mwana mpumbavu ni msiba kwa babaye; Na ugomvi wa mke kama kutona-tona daima.
Uonapo familia zenye migogoro ya namna hii ni kuziombea sana Bwana aziponye.
Maandiko hayo yamewekwa sio kuonyesha mabaya kwa jinsia ya kike, hapana, bali imetoa tahadhari ili yasitokee kwa wanawake wa kikristo.
Biblia imetoa mwenendo wa mwanamke halisi wa kikristo, inasema awe ni wa kumtii mume wake. Awe ni mwenye kiasi, na MPOLE, na adabu. Akifanya hivyo atasimama vema kwenye nyumba yake, badala ya kuiharibu kinyume chake ataijenga.
1Timotheo 2:9 Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani; 10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu. 11 Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna.
1Timotheo 2:9 Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;
10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.
11 Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna.
Soma pia.
1Petro 3:1 Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno; 2 wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu. 3 Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi; 4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, ROHO YA UPOLE NA UTULIVU, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu. 5 Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao. 6 Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote.
1Petro 3:1 Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;
2 wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu. 3 Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;
4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, ROHO YA UPOLE NA UTULIVU, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.
5 Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.
6 Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote.
Hivyo wewe kama mwanamke ukitembea katika hayo, utakuwa katika upande salama wa Mungu.
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Wokovu wa milele/ Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?
HUIJUI KAZI YA MUNGU, AFANYAYE MAMBO YOTE.
ALIJARIBIWA SAWASAWA NA SISI KATIKA MAMBO YOTE.
Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo, Tukijua kuwa ule mwisho unakaribia, hatuna budi siku baada ya siku tujichunguze je! Tumekamilika vema? ili siku ile tusionekane na mawaa mbele zake. Tulipokee taji timilifu tuliloandaliwa mbinguni na mwokozi wetu Yesu Kristo kwa neema zake.
Leo, napenda tufahamu juu ya wimbo mpya. Kama wewe ni msomaji mzuri wa kitabu cha Ufunuo. Utagundua zimetajwa nyimbo kuu tatu.
Swali ni je! Hizi nyimbo ni zipi na zinatimiaje?
Wimbo wa Musa na wa mwanakondoo tunazisoma, katika Ufunuo 15:2-3
Ufunuo 15:2 Tena nikaona kitu kama mfano wa bahari ya kioo iliyochangamana na moto, na wale wenye kushinda, watokao kwa yule mnyama, na sanamu yake, na kwa hesabu ya jina lake, walikuwa wamesimama kando-kando ya hiyo bahari ya kioo, wenye vinubi vya Mungu. 3 Nao WAUIMBA WIMBO WA MUSA, MTUMWA WA MUNGU, NA WIMBO WA MWANA-KONDOO, wakisema, Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa
Ufunuo 15:2 Tena nikaona kitu kama mfano wa bahari ya kioo iliyochangamana na moto, na wale wenye kushinda, watokao kwa yule mnyama, na sanamu yake, na kwa hesabu ya jina lake, walikuwa wamesimama kando-kando ya hiyo bahari ya kioo, wenye vinubi vya Mungu.
3 Nao WAUIMBA WIMBO WA MUSA, MTUMWA WA MUNGU, NA WIMBO WA MWANA-KONDOO, wakisema, Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa
Wimbo wa Musa, ni injili ya Musa, ambayo iliwafanya watu wa kale, kutembea katika hiyo ili wamkaribie Mungu, ndiyo ile torati, ambayo wale waliokuwa katika agano la Ibrahimu kwa uzao, walirithi neema hiyo. Hivyo wana wa Israeli wote walikuwa wanauimba wimbo wa Musa. Yoyote ambaye hakuwa hana wimbo huo, basi wokovu au kumkaribia Mungu hakukuwezekana kwake.
Lakini wimbo wa Musa haukuwa na ukamilifu wote kwasababu ulikuwa ni wa mwilini, na wa kutarajia ahadi ya mwokozi mbeleni. Hivyo Mungu akaleta wimbo mwingine mpya kwa wanadamu wote. Ndio huo wimbo wa mwana-kondoo.
Ambayo ni injili ya neema iliyoletwa na Bwana wetu Yesu Kristo na kuhubiriwa na mitume wake. Kwa ufupi sisi wote tuliomwamini Yesu Kristo katika agano hili jipya, kwa pamoja tunauimba wimbo wa mwana-kondoo. Ndio maana kiini cha imani, na wokovu wetu ni Yesu Kristo. Mtu yeyote ambaye hajaoshwa dhambi zake kwa damu ya Yesu, hawezi kumwona Mungu, wala kamwe hataweza kumwelewa, haijalishi ataonyesha bidii zake nyingi kiasi gani. Kwasababu ndio utimilifu wote.
Lakini upo wimbo mwingine wa Tatu ndio huo wimbo mpya.
Wimbo huu, si wote watakaoweza kuuimba, lakini watakaoweza kuuimba watakuwa karibu sana na mwana-kondoo (Yesu Kristo), baada ya maisha haya. Ndio wale washindao, Ndio wale Yesu aliosema atawakiri mbele ya Baba na malaika zake, ndio wale watakaoketi pamoja naye katika viti vya enzi, ndio wale watakaotoka mashariki, magharibi, kaskazini na kusini, kula mkate naye mezani pake. Na vigezo amevianisha pale. Anasema..
Ufunuo 14:1 Kisha nikaona, na tazama, huyo Mwana-Kondoo amesimama juu ya mlima Sayuni, na watu mia na arobaini na nne elfu pamoja naye, wenye jina lake na jina la Baba yake limeandikwa katika vipaji vya nyuso zao. 2 Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni, kama sauti ya maji mengi, na kama sauti ya radi kuu. Na hiyo sauti niliyoisikia ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi, wakivipiga vinubi vyao; 3 na KUIMBA WIMBO MPYA mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele ya wale wenye uhai wanne, na wale wazee; WALA HAPANA MTU ALIYEWEZA KUJIFUNZA WIMBO ULE, ila wale mia na arobaini na nne elfu, WALIONUNULIWA KATIKA NCHI. 4 HAWA NDIO WASIOTIWA UNAJISI PAMOJA NA WANAWAKE, KWA MAANA NI BIKIRA. Hawa ndio wamfuatao Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamenunuliwa katika wanadamu, malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo. 5 NA KATIKA VINYWA VYAO HAUKUONEKANA UONGO. MAANA HAWANA MAWAA
Ufunuo 14:1 Kisha nikaona, na tazama, huyo Mwana-Kondoo amesimama juu ya mlima Sayuni, na watu mia na arobaini na nne elfu pamoja naye, wenye jina lake na jina la Baba yake limeandikwa katika vipaji vya nyuso zao.
2 Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni, kama sauti ya maji mengi, na kama sauti ya radi kuu. Na hiyo sauti niliyoisikia ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi, wakivipiga vinubi vyao;
3 na KUIMBA WIMBO MPYA mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele ya wale wenye uhai wanne, na wale wazee; WALA HAPANA MTU ALIYEWEZA KUJIFUNZA WIMBO ULE, ila wale mia na arobaini na nne elfu, WALIONUNULIWA KATIKA NCHI.
4 HAWA NDIO WASIOTIWA UNAJISI PAMOJA NA WANAWAKE, KWA MAANA NI BIKIRA. Hawa ndio wamfuatao Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamenunuliwa katika wanadamu, malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.
5 NA KATIKA VINYWA VYAO HAUKUONEKANA UONGO. MAANA HAWANA MAWAA
Kama tunavyoweza kuona hapo tabia za wale walioweza kuuimba wimbo huo ni mbili;
Hapo hamaanishi kuwa hawakuwa wazinzi, hapana, (ni kweli uzinzi sio jambo lao) bali anamaanisha hasaa uzinzi wa rohoni, yaani Kumwabudu Mungu pamoja na sanamu. Na sanamu kwa wakati wetu si tu vile vinyago vya kuchonga tu, bali pia ni kitu chochote kinachochukua nafasi ya Mungu wako moyoni. Wengine mali, wengine tv, wengine mipira, wengine elimu, wengine ma-magemu, wengine ushirikina, wengine udhehebu. Hizo ni sanamu, unapozidhibiti wewe kama mkristo hiyo ni hatua mojawapo ya kuweza kuuimba wimbo huo mpya.
Lakini anasema..
Ni watu walionena kweli yote ya Mungu (injili ya Kristo), wala hawakuibatilisha kwa ajili ya fedha, au maslahi, au cheo, au unafki au wafuasi. Bali waliitetea kweli yote ya Mungu na kuiishi pia, . Maana yake mimi na wewe tukiinena kweli ya Kristo na kuiishi, basi vinywani mwetu tunakuwa hatuna uongo.
Na matokeo ya mtu wa jinsi hii, ni kwamba anakuwa nafasi maalumu sana mbinguni(Ufunuo 5:8-9), Ni sawa na leo unajisikiaje unapoitwa uishi ikulu na raisi wako? Unajisikiaje kila mahali aendapo na msafara wake wewe upo pamoja naye. Anapopokea heshimu, na wewe unapokea naye.
Hivyo bidii ina malipo. Nyakati tulizonazo sio kusema nimeokoka hiyo inatosha!.. Ni nyakati za kujifunza wimbo huu mpya kwa bidii. Kutijahidi kumpendeza Bwana. Na yeye mwenyewe ameahidi neema yake itatusaidia.
KARAMU YA MWANA-KONDOO.
JE! NI DHAMBI KUIMBA WIMBO WA TAIFA?
Nanyi mtamweka hata siku ya kumi na nne ya mwezi ule ule(Kutoka 12:4)
Huu ni mwongozo wa maombi maalumu kwa ajili ya familia yako. Kama watakatifu, ni wajibu wetu kuziombea familia, Lakini sio kuziombea tu, bali kufahamu maeneo muhimu ya kugusia kwenye maombi hayo. Huu ni mwongozo maalumu wa maombi ya familia. Bofya juu ufungue chapisho hilo (pdf)
Pia Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
MISTARI YA KUOMBEA AMANI YA FAMILIA.
MWONGOZO WA MAOMBI YA ASUBUHI.
TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi
Je unajua UTAKASO hauji tu kufumba na kufumbua????…
Nguvu ya utakaso (yaani Roho Mtakatifu) unaweza kuipokea kufumba na kufumbua, lakini mpaka ule mzizi wa dhambi uondoke ndani yako inachukua muda kidogo (inahitaji juhudi).
Ulikuwa ni mzinzi, siku umepokea ujazo wa Roho sio mwisho wa vita,
Sasa ili upokee utakaso mkamilifu, utakaoondoa mzizi wa dhambi kama usherati, kujichua, kuua, kuiba, kusengenya n.k ni lazima uvitoe viungo vyako vitumike katika haki.
Maana yake ule mdomo uliokuwa unautumia kusengenya sasa utumie kuhubiri, ule ulimi uliokuwa unautumia kutukana sasa unaanza kujizoeza kuutumia kuomba..
Kile kinywa kilichokuwa kinatumika kuimba nyimbo za kidunia, sasa unautumia kumwimbia Mungu sifa.
Yale macho yako uliyokuwa unayatumia kutazama picha za tupu mitandaoni, na kusoma makala za uzinzi… sasa unayatumia kusoma Neno la Mungu.
Ule mwili wako ulikuwa unauchosha kwa ulevi sasa unabadilisha matumizi kwa kuanza kufunga na kuomba.
Kama ulikuwa unafanya uzinzi na ukahaba sasa unautumia mwili wako kuhubiri injili nyumba kwa nyumba na mtaa kwa mtaa..
Kwa kufanya hivyo, UTAKASO utaingia ndani yako. Kwasababu sasa VIUNGO vyako unavitumia kufanya haki…ndivyo biblia inavyotufundisha..
Warumi 6:19 “Nasema kwa jinsi ya kibinadamu kwa sababu ya udhaifu wa miili yenu. Kwa kuwa kama mlivyovitoa viungo vyenu vitumiwe na uchafu na uasi mpate kuasi, vivyo hivyo sasa vitoeni viungo vyenu vitumiwe na haki mpate kutakaswa”.
Umeona??..kwa kuvitoa viungo vyako vitumiwe na Haki unapata UTAKASO…Maana yake ule uzinzi uliokuwa unaona ni mgumu kuuacha, utaona umeondoka ndani yako.
Ule usengenyaji uliokuwa unaona ni mgumu kuacha, utaona unapotea ndani yako na tabia nyingine zote ni hivyo hivyo…
Lakini kama ukipokea Roho Mtakatifu halafu viungo vyako huvizoezi kufanya haki, ni ngumu kutakasika!!!!…utapambana na uasherati miaka na miaka hutauacha, utapambana na ulevi miaka na miaka, hutaona badiliko lolote, hata kama ulibatizwa ubatizo ulio sahihi, na kujazwa Roho siku ile…bado hutaona badiliko lolote.
Jizoeze kuomba (bila kushurutishwa) ndugu uliyempokea Kristo, jizoeze kuhubiri ndugu, jizoeze kumwimbia Mungu, jizoeze kusoma Neno, jizoeze kuutumia mwili wako kufanya mambo yote ya kiungu na utaupokea utakaso (hiyo ni Biblia).
Warumi 6:22 “Lakini sasa mkiisha kuwekwa huru, na kuwa mbali na dhambi, na kufanywa watumwa wa Mungu, mnayo faida yenu, ndiyo kutakaswa, na mwisho wake ni uzima wa milele”
KIJITO CHA UTAKASO.
ZIDI KUTAFUTA UTAKASO WA MWILI.
KILA KIUNGO LAZIMA KISHUGHULIKE.
NAFASI YAKO NI IPI KATIKA MWILI WA KRISTO?
JE UNAZAA MATUNDA NA KUWAPONYA MATAIFA?
SWALI: Naomba kufahamu tafsiri ya Yakobo 1:13-17, hususani pale anaposema “Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu”
Yakobo 1:13-17,
[13]Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu. [14]Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa. [15]Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti. [16]Ndugu zangu wapenzi, msidanganyike. [17]Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka.
[13]Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu.
[14]Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.
[15]Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.
[16]Ndugu zangu wapenzi, msidanganyike.
[17]Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka.
JIBU: Katika hiyo mistari ya juu kabisa, tunasoma mtume Yakobo akitoa ufafanuzi wa mawazo ya watu kuhusu Mungu ambayo sio sahihi. Wakidhani kuwa majaribu yampatayo mtu hutolewa na Mungu, kwasababu chanzo chake ni Mungu.
Chukulia mfano labda mpendwa kabarikiwa na Mungu kwa shamba la mizabibu, likawa linasitawi sana, hata kumfanya afungue kiwanda chake cha juisi na kuuza na kupata faida nyingi..Sasa baada muda fulani watu wakamfuata na kuulizia bidhaa ya mvinyo, mwanzoni alikataa, lakini baadaye alipopiga hesabu na kuona faida itakuja mara nne,.akaingiwa na tamaa akaanza kutengeneza divai akauza na yeye mwenyewe akaanza kuwa mlevi, hatimaye maisha yake ya wokovu yakaporomoka akawa amekufa kabisa kiroho. Mwishowe akaanza kumlaumu Mungu amemletea jaribu la kumpa shamba la mzabibu na kumbariki sana, ndio maana akawa mlevu. Sasa mtu wa jinsi hii Mtume Yakobo anasema asiseme amejaribiwa na Mungu.
Ni sawa na tamaa za mwili,.Mungu aliziweka mahususi kwa ajili ya furaha ya wanandoa lakini imebadilika na kuwa uzinzi, na watu hutumia kisingizio kuwa Mungu ameziweka kama jaribu kwao. kumbe Mungu alichowapa ni chema isipokuwa wao wenyewe wamekigeuza kuwa uovu.
ndo maana sasa ya vifungu vinavyofuata vinasema. “kila kutoa kuliko kwema na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu. Kwa lugha rahisi anamaanisha chochote kitolewacho kilicho chema hutoka kwa Mungu, lakini tu sio kilicho chema bali pia chochote kilicho kikamilifu, hutoka juu kwa Baba yetu.
Mungu sikuzote hutupa sisi vitu vizuri. Na si vizuri tu bali pia vilivyo vikamilifu hutoka kwake. tujengwe na tufurahie, isipokuwa sisi huvipindua na kuvitumia kwa tamaa zetu.
Pesa ni kitu kizuri, chakula ni kitu kizuri, usingizi ni kitu kizuri, ndoa ni kitu kizuri, kazi ni kitu kizuri, muziki ni kitu chema.
Lakini watu wanapovitumia kinyume ndio huzaa uzinzi, anasa, ulevi, uvivu, ufisadi.n.k.
Vitu vyote vyema vimetoka kwa Mungu na hajatupa ili kutujaribu..anaendelea kusema..
“hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka”.
Baba wa mianga, akijifananisha na jua ambalo huangaza kotekote, isipokuwa yeye amelizidi jua, hana misimu wala majira ya kuangaza, yeye wakati wote hutoa vilivyo vyema, hifadhili majira yote kwa watu wake.
Hata leo, uonapo Mungu amekupa kitu chema, halafu baadaye kikakuletea matatizo makubwa.. Tafakari hapo kuna mahali ulimpa nafasi shetani kukujaribu. Kwasababu Mungu hawezi kumpa mtu jiwe aliyemwomba mkate.
“kila kutoa kuliko kwema na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu.
Ubarikiwe.
YAFAHAMU MAPENZI KAMILI YA MUNGU KWA MAADUI ZAKO.
EPUKA KUTOA UDHURU.
SI KILA KILICHO HALALI KINAFAA.
SWALI: Katika Yakobo 1:5 inasema tuombapo Mungu hakemei, maana yake ni nini.
JIBU:
Yakobo 1:5
[5]Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.
Kabla ya kuona maana hilo neno “wala hakemei naye atapewa”. Tuone kwanza tafsiri ya kifungu chote.
Hapa mtume Yakobo kwa uongozo wa Roho, anandika juu ya suluhisho la kupungukiwa kwa jambo muhimu sana ndani ya mwanadamu. Nalo ni Hekima.
Haandiki ikiwa mtu amepungukiwa na mali, au na umaarifu au na fursa, au watoto…hapana bali na hekima, na aombe dua.
Lakini hekima aisemayo sio hekima ya duniani, bali hekima ya ki- Mungu. Ambayo ni ufahamu wa Ki-Mungu unaoingia moyoni mwa mtu kumsaidia aweze kupambanua vema mambo yote, katika ufasaha wote ili kuleta matokeo aliyoyatarajia.
Hivyo sisi wote tunaihitaji hekima katika yote tuyatendayo. Vinginevyo hatutaweza kuzalisha chochote.
Lakini bado anatoa kanuni ya kuipata, hasemi tukae chini tuwaze, au tukahubiri, au tukatoe sadaka, au tuende kwenye shule za biblia. Hapana anasema na tuombe dua kwa Mungu.
Tunaipata kwa kuomba. Kwa kuchukua muda kupiga magoti na kuomba. Sio kuomba dakika mbili, na kusema Amen au yale maombi ya kumalizia siku unapokwenda kulala. Hapana bali ni maombi yaliyochanganyikana na kiu ya dhati kupata hekima ya Ki-Mungu katika eneo fulani, unalotaka Bwana akusaidie.
Vilevile hatupaswi kuomba bila dira. Kwamfano kusema.. “Mungu naomba unipe hekima”.. Hapana tunaomba tukielekeza eneo ambalo tunataka Bwana atusaidie kupata hiyo hekima ya kupambanua.
Kwamfano hekima katika kuyaelewa maandiko, hekima katika kuhubiri, hekima katika kufundisha, katika kuombea wagonjwa, katika kufanya biashara, katika kuimba. n.k.
Na hapo ndipo Mungu mwenyewe anaongeza ufahamu wake juu ya hicho unachokiomba na hatimaye utaona tu, mabadiliko, au njia ya kitu hicho unachotaka akusaidie.
Sasa tukirudi kwenye swali, pale anaposema
“awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa”
Maana yake, kwasababu Mungu ana ukarimu, basi hachagui wa kumpa, anawapa wote. Hii ahadi yake kuwa kila aombaye humpa. Haleluya.
Na tena anasema “hakemei”. Tofauti na sisi wanadamu
Kwamfano sisi tuwafuatapo wazazi wetu na kuwaomba kitu, wakati mwingine, hutugombeza, au huwa wakali, au kutaka utoe kwanza hesabu ya kile cha nyuma ulikitumiaje, kabla ya kukupa hichi kingine. Na ndio maana ulikuwa na hofu, kujifikiria mara mbili mbili hicho unachotaka kwenda kuomba, ukiulizwa hivi, ujibu vipi. Sio tu kwa wazazi, lakini kwa wanadamu wote, sifa hiyo wanayo tuwafuatapo kuwaomba kitu, si kivyepesi vyepesi kama tunavyodhani.
Lakini kwa Mungu wetu sio, hakemei, haangaali ya nyuma kukushutumu, hakuuliza makosa yako. Anakupa tu, bila sharti lolote.
Ni furaha iliyoje. Mimi na wewe tuliomwamini tunapokwenda kumwomba Mungu hekima, hatushutumiwi kwa lolote, au kwa madhaifu yetu. Bali kinachohitajika tu ni kumwamini yeye asilimia mia, bila kutia shaka katika hilo unaloomba, kwasababu ukitia shaka, maombi hayo hayaendi kwake bali kwa mungu mwingine asiyeweza yote.
ndio maana anataka tumfuatapo tusiwe na shaka ya kutojibiwa, ili maombi yetu yafike kwake kwelikweli, yeye aliyemweza wa yote.
Anasema hivyo katika vifungu vya mbeleni.
Yakobo 1:6-8
[6]Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku. [7]Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana. [8]Mtu wa nia mbili husita-sita katika njia zake zote.
[6]Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku.
[7]Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana.
[8]Mtu wa nia mbili husita-sita katika njia zake zote.
Je Elisha alimdanganya Ben-hadadi kuwa hatakufa kwa ugonjwa wake?
Swali: Kile KIWI, kilichomwangukia yule Elima mchawi ni kitu gani?.
Jibu: Tuanzie ule mstari wa nane (8) ili tuelewe vizuri..
Matendo 13:8 “Lakini Elima, yule mchawi (maana ndiyo tafsiri ya jina lake), akashindana nao, akitaka kumtia yule liwali moyo wa kuiacha ile imani. 9 Lakini Sauli, ambaye ndiye Paulo, akijaa Roho Mtakatifu, akamkazia macho, 10 akasema, Ewe mwenye kujaa hila na uovu wote, mwana wa Ibilisi, adui wa haki yote, huachi kuzipotoa njia za Bwana zilizonyoka? 11 Basi, angalia, mkono wa Bwana u juu yako, nawe utakuwa kipofu, usilione jua kwa muda. MARA KIWI kikamwangukia na giza, akazunguka-zunguka na kumtafuta mtu wa kumshika mkono na kumwongoza”.
Matendo 13:8 “Lakini Elima, yule mchawi (maana ndiyo tafsiri ya jina lake), akashindana nao, akitaka kumtia yule liwali moyo wa kuiacha ile imani.
9 Lakini Sauli, ambaye ndiye Paulo, akijaa Roho Mtakatifu, akamkazia macho,
10 akasema, Ewe mwenye kujaa hila na uovu wote, mwana wa Ibilisi, adui wa haki yote, huachi kuzipotoa njia za Bwana zilizonyoka?
11 Basi, angalia, mkono wa Bwana u juu yako, nawe utakuwa kipofu, usilione jua kwa muda. MARA KIWI kikamwangukia na giza, akazunguka-zunguka na kumtafuta mtu wa kumshika mkono na kumwongoza”.
Kiwi kinachozungumziwa hapo si rangi ya viatu bali ni “ukungu mweusi” unaotokea katika macho, aidha kutokana na ugonjwa au mwanga mkali unapomulika macho kwa ghafla!.
Ukungu huu unapompata mtu unamfanya asione kwa muda au moja kwa moja.
Mfano kwa watu waliopatwa na kiwi ndiye huyo Elima mchawi aliyekuwa anashindana na kweli ya Mungu, na huku akitaka kumtia yule liwali Sergio moyo wa kuiacha ile imani.
Vile vile mtu mwigine aliyeangukiwa na “KIWI” ni Paulo mwenyewe alipokuwa anaelekea Dameski, akipokutana na Bwana na mwanga ule mkali wa Bwana, ukatia macho yake KIWI kama ilivyomtokea huyu Elima, mchawi….na Sauli (ambaye ndiye Paulo) akawa kipofu kwa muda wa siku tatu.
Matendo 9:8 “Sauli akainuka katika nchi, na macho yake yalipofumbuka, hakuona kitu; wakamshika mkono wakamleta mpaka Dameski. 9 Akawa siku tatu haoni; hali, wala hanywi”.
Matendo 9:8 “Sauli akainuka katika nchi, na macho yake yalipofumbuka, hakuona kitu; wakamshika mkono wakamleta mpaka Dameski.
9 Akawa siku tatu haoni; hali, wala hanywi”.
Mistari mingine ya biblia inayozungumzia “KIWI” ni pamoja na Ayubu 17:5, Ayubu 31:16, Isaya 32:3, Isaya 58:10 na Zekaria 14:6.
Vile vile na leo kuna watu wanashukiwa na Kiwi cha kiroho wanapoenda kinyume na Mwanga wa Neno la Mungu.
Inapopingana na kweli, maana yake inakabiliana na Nuru na hivyo itakupofusha macho.
Ayubu 11:20 “Lakini macho ya waovu yataingia kiwi, Nao hawatakuwa na njia ya kukimbilia, Na matumaini yao yatakuwa ni kutoa roho”
Na hiyo ndio sababu ya Bwana YESU kusema..
Yohana 9:39 “Yesu akasema, Mimi nimekuja ulimwenguni humu kwa hukumu, ili wao wasioona waone, nao wanaoona wawe vipofu”.
Sasa wanaoona na kufanywa vipofu ni jamii ya hao watu waendao kinyume na nuru, na wale wasioona wapewe kuona ni wale wanaotembea katika uelekeo wa nuru inapomulika.
Kwa urefu kuhusiana maneno hayo basi fungua hapa 》》》Ni kwa namna gani Bwana amekuja kuwafanya wanaoona wawe vipofu?
Je umempokea Bwana YESU?…Je unaenda katika Nuru yake au kinyume na Nuru.
Kama bado hujaokoka, ni vyema ukafanya maamuzi leo kabla ule mlango wa Neema kufungwa.
Kama utahitaji msaada huo wa kjmpokea Bwana YESU maishani mwako basi wasiliana nasi kwa namba zetu..
ELIMA MCHAWI, ANAFANYA KAZI HADI SASA.
BUSTANI YA NEEMA.
UJUE UCHAWI WA MANABII WA UONGO?.
Usimwache mwanamke mchawi kuishi! Biblia ilimaanisha nini?
MAMBO MANNE(4) YAFANYAYO NENO LA MUNGU.