Category Archive Home

KUACHA KUVUTA SIGARA.

Unaweza ukawa umezunguka huku na huko, umejaribu hiki na kile kwa bidii zako ili kuacha kuvuta sigara lakini imeshindikana, ni uwazi usiopingika kwamba vitu vyote vyenye addiction (yaani ulevi ndani yake) ni ngumu sana kuviacha, sio pombe, sio ugoro, sio bangi, sio madawa ya kulevya sio sigara, sio mirungi vyote hivyo kwa bidii za mtu binafsi ni ngumu leo anaweza akaacha kwa muda tu lakini kikipita kipindi Fulani kifupi ile hamu ikimzidia anarudia tena , Ni utumwa mgumu sana ambao kwa bidii za kibinadamu ni kama haiwezekani, ..Lakini nataka leo nikupe habari njema nazo ni hizi:

Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli.(Yohana 8:36).  

Mamia kwa mamia kama sio maelfu kwa maelfu ya watu duniani wanaacha kuvuta sigara, kwa kumruhusu tu YESU atende kazi maishani mwao. Sio tu kwa wavuta sigara bali pia hata na kwako wewe mnywaji pombe na mtumiaji wa ugoro na madawa ya kulevya, Kwasababu kwake yeye hakuna linaloshindikana, akikufungua habakishi hata chembe moja ndani yako, haijalishi wewe ni mtumwa wa hicho kitu kwa kiwango gani, hakuna utumwa ulio mkubwa zaidi ya utumwa wa DHAMBI lakini huo aliukomesha pale msalabani, si zaidi sigara ambayo ni kitawi kidogo sana cha dhambi yenyewe?.

Ikiwa umekusudia kweli na unataka kuacha leo basi, tiba ipo kwa YESU, Hatuhitaji kusema maneno mengi  Unachopaswa kufanya ni kuanzia sasa umgeukie tu yeye..Utubu dhambi zako kwanza kwa kumaanisha kuziacha, na kisha yeye mwenyewe atakuvika huo uwezo wa kuacha kuvuta sigara, ataiondoa hiyo kiu ya sigara ndani yako moja kwa moja..Lakini Ikiwa tu umemaanisha kuwa kiumbe kipya. Kama upo tayari basi nataka ufuatishe sala hii, lakini tafuta kwanza mahali pa utulivu kisha fuatisha sala hii kwa IMANI..Kwasababu yeye yupo hapo hapo ulipo kukuhudumia hauhitaji mchungaji, au mhubiri aje kukuombea, wewe mwenyewe hapo ulipo anakusikia, kwasababu sio mchungaji anayekuponya au mhubiri bali ni yeye huyo YESU MWOKOZI ndiye anayekwenda kushughulika na shida yako…

Sema maneno haya kwa sauti:

EE! BWANA YESU, NAJA MBELE ZAKO, NINAJIJUA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NIMEKUKOSEA KWA MAMBO MENGI, NA MOJAWAPO NDIO HILI LA KULIHARIBU HEKALU LAKO KWA KULIVUTISHA SIGARA, LEO HII NINAJUTA NA NINATUBU MBELE ZAKO KWA KUMAANISHA KABISA KUWA SITAKI KUVUTA SIGARA TENA, NA NIMEMAANISHA  KUACHANA NA MAISHA YA DHAMBI. NJOO NDANI YANGU BWANA YESU, UNIBADILISHE UNIFANYE KUWA UPYA NIFANANE NA WEWE, MIMI KWA NGUVU ZANGU NIMESHINDWA KUACHA SIGARA LAKINI WEWE ULISEMA KATIKA MATHAYO 11:28 KWAMBA TUJE KWAKO SISI WOTE TUNAOSUMBUKA NA KULEMEWA NA MIZIGO YA DHAMBI, NAWE UTATUPUMZISHA, NAWE UTATUPA RAHA NAFSINI MWETU NA LEO HII KWA UNYENYEKEVU WOTE NIMEKUJA KWAKO BWANA YESU ILI UNIFUNGUE  KATIKA VIFUNGO HIVI VYA DHAMBI NA MAUTI. NINAKIRI KUWA WEWE NDIO BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, NA KWAMBA ULIKUFA NA UKAFUFUKA, NA SASA UPO HAI KUNISIKIA, HIVYO KUANZIA LEO NAAHIDI KUKUTUMIKIA NA KUKUISHIA WEWE DAIMA.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNISAMEHE NA KUNIPONYA NA SHIDA YANGU YOTE AMEN.

Ikiwa umesali sala hii kwa imani, basi fahamu kuwa Mungu amekusikia na kukusamehe dhambi zako zote sio hiyo ya sigara tu bali na nyingine zote, , hivyo unachopaswa kufanya ni kutupa sigara zote ziweke mbali nawe wakati Bwana YESU anaendelea kushughulika na hiyo kiu ya sigara ndani yako, Hivyo hakikisha, unatafuta  kanisa la kiroho, lililokaribu nawe  ili kukusaidia kukua kiroho, au wasiliana nasi kwa namba hizi 0789001312 ikiwa utahitaji msaada wetu.

Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

 

Mada Nyinginezo:

WEWE NI HEKALU LA MUNGU.

YESU NI NANI?

FREEMASONS NI NINI? NA MTU ATATOKAJE HUKO?

JE! KUBET NI DHAMBI?

WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU.

NI KWASABABU YA YESU KRISTO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

KUJIPAMBA NI DHAMBI?

Ni Muhimu kufahamu kama Je kujipamba ni dhambi? au  kujichubua ngozi ni dhambi? kama kuchonga nyusi ni dhambi, kupaka lipstick ni dhambi na kama kupaka wanja ni dhambi?

Kiuhalisia Kujipamba kunahusisha kupaka rangi uso, kujichubua ngozi, kuchonga nyusi, kupaka lipstick, kupaka wanja, kupaka hina,kusuka nywele, kuvaa hereni, bangili, na mikufu, kuweka kucha za bandia, kuweka nywele za bandia (wigi), kujipulizia  marashi makali.

Watu wengi hususani wanawake hawapendi kuambiwa ukweli, kutokana na kwamba wanahofia wataonekana wamepitwa na wakati. Lakini ukweli ni kwamba kujipamba ni DHAMBI, Tena ni dhambi ambayo inawapeleka wanawake wengi kuzimu, na wanaume baadhi wanaofanya hayo..

Katika Biblia kulikuwepo na mwanamke mmoja tu ambaye alikuwa anajipamba…Na huyo si mwingine zaidi ya mwanamke Yezebeli..

Ambaye tunamsoma katika kitabu cha Wafalme

2Wafalme 9:30 “Hata Yehu alipofika Yezreeli, Yezebeli akapata habari; akatia uwanja machoni mwake, akapamba kichwa chake, akachungulia dirishani”.

Mwanamke huyu biblia inasema alikuwa mchawi…na aliwakosesha sana wana wa Israeli na alimsumbua sana Nabii Eliya. Na alienda kuzimu! kwasababu anaonekana tena katika kitabu cha Ufunuo kutajwa kama Nabii wa Uongo, na Manaabii wa Uongo pamoja na wachawi, na waabudu sanamu wote biblia imesema sehemu yao ni katika lile ziwa la moto. Kasome (Ufunuo 2:20)

Na biblia inasema miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, hivyo hatuwezi kulifanya hekalu la Mungu kuwa nyumba inayofanana na nyumba za makahaba. Na Neno linasema mtu akiliharibu hekalu la Roho Mtakatifu, Mungu naye atamharibu mtu huyo.

Vivyo hivyo Biblia imezungumza katika Agano jipya.

1Timotheo 2:9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;

10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu”. 

Hivyo kujipamba kwa aina yoyote ile ni dhambi..  kusuka nywele ni dhambi, kujichubua ngozi ni dhambi, kuchonga nyusi ni dhambi, kupaka lipstick ni dhambi, kupaka wanja ni dhambi nk Mwanamke anapaswa ajiweke katika hali yake ya asili, kadhalika na wanamume pia..Ni wajibu  wetu wote kujiweka safi na nadhifu, lakini si kuharibu uhalisia.

Mungu akubariki.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789 001312.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

WEWE NI HEKALU LA MUNGU.

NI KWA JINSI GANI MUNGU ANAPATILIZA MAOVU YA BABA ZETU SAWASAWA NA KUTOKA 20:5-6?

AMPOKEAYE NABII KWA KUWA NI NABII, ATAPATA THAWABU YA NABII; MSTARI HUU UNAMAANA GANI?.

SHETANI ANATOLEA WAPI FEDHA, ANGALI TUNAJUA FEDHA NA DHAHABU NI MALI YA BWANA?

ASKOFU MKUU NA MCHUNGAJI MKUU NI NANI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

NILIMWONA SHETANI, AKIANGUKA KUTOKA MBINGUNI.

Tunasoma mara baada ya Bwana Yesu kuwatuma wanafunzi wake wengine 70 wawili wawili wamtangulie kila mahali alipotaka kwenda, na kuwapa amri ya kufanya ishara zote alizokuwa anafanya yeye, walipotii na kwenda kuhubiri kwa furaha na kurudi kumpa Bwana ripoti ya mambo yote yaliyotendeka huko…Wao Hawakujua ni kitu gani Bwana Yesu alikuwa anaona huku nyuma, pengine wao kwa nje walikuwa wanaona ni jambo la kawaida tu, wanatimiza wajibu wao uwapasao kufanya, lakini Bwana Yesu aliwafumbulia alichokuwa anakiona aliwaambia maneno haya:

Luka 10:17 “Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako.

18 Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.

19 Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru”.

Unaona yaani kwa jinsi walivyokuwa wanalisambaza lile Neno la Mungu na kuiangaza nuru ya injili kila mahali, huku Nyuma shetani alikuwa anaanguka kwa kasi ya ajabu sana mfano wa Umeme/radi, hakuna kitu kinachosafiri kwa kasi zaidi ya umeme, hivyo hapo Bwana alipokuwa anasema nilimwona shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme, alimaanisha ni anguko ambalo halikuwa na kipingamizi chochote kile (flawless). Leo hii shetani anaweza kuleta vipingamizi katika maombi, anaweza ukaomba lakini bado shetani akabakia pale pale ameshikilia..Lakini kwa pamoja tunapoamka na kwenda kuhubiri injili ya Kristo kila mahali, anajua hawezi kubaki pale pale, ni lazima aanguke tu, na ndio maana jambo kubwa ambalo shetani analipiga vita kuhubiri injili.

Kumbuka kibiblia mbinguni sio tu, kule Mungu alipo, mbinguni inaweza ikawa nafasi ya juu sana, ambayo kimsingi ndio inayompasa Mungu peke yake aikalie, lakini wanadamu au shetani wanaweza kutafuta nafasi hiyo kwa nguvu na kuketi hapo, na hivyo rohoni wakaonekana kama wamefika mbinguni. Soma Danieli 4:9-37, soma pia:

Isaya 14:13 “Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini.

14Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu.

15 Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo.

16 Wao wakuonao watakukazia macho, Watakuangalia sana, wakisema, Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia, Huyu ndiye aliyetikisa falme;

17 Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake; Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao?

18 Wafalme wote wa mataifa wamezikwa wote kwa heshima, Kila mmoja ndani ya nyumba yake mwenyewe;”

Ikiwa wewe umeokoka na umekaa katika hali hiyo kwa miezi sasa, au miaka, na hutaki kuangaza nuru ya injili kwa wengine ili na wenyewe waokoke kama wewe, hutaki kuitumia karama Mungu aliyoiweka ndani yako kumtangaza yeye na huku unamwomba Mungu watu waokolewe nataka nikuambie shetani atendelea kuwatesa tu..Usitegemee kuwa shetani ataondoka kwenye jamii unayoishi, usitegemee huyo mkuu wa giza ataacha aliye katika eneo lako ataacha kuwapufusha watu macho wasiiamini Injili..Ataendelea sana kuziangusha roho za wengi…

Unadhani mapepo hayo yatadondoka kwa maombi tu?…Bwana Yesu hakuwaambia kauli ile walipotoka kusali, lakini aliwaambia kauli ile walipotoka kuhubiri..Vivyo hivyo na wewe, leo hii usipozaa matunda utafika wakati Bwana atakukata, unaposikia injili Mungu anatazamia na wengine waisikie hiyo hiyo uliyoisikia kwa kupitia wewe..Lakini kama wewe utakuwa ni kupokea tu hutaki kutoa ili na wengine waokolewe, wakati utafiki utakatwa.

Popote pale ulipo unaweza kuwahubiria wengine injili, iwe ni kazini, iwe ni shuleni, iwe ni mtaani, iwe ni nyumbani, iwe ni mitandaoni, iwe ni safarini, iwe barabarani..Kwa karama Mungu aliyokupa na mlango aliokufungulia itumie hiyo hiyo kumletea Kristo faida..Tukishirikiana kwa pamoja, hakuna nguvu yoyote ya shetani itakayoweza kuzuia watu wasimjue Mungu, yeye kazi yake itakuwa ni moja tu, kila sekunde ni kuanguka huko aliko kwa kasi ya umeme. Kuhubiri Injili ni moja ya zile silaha zilizotajwa katika..

Waefeso 6: 13 “Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.

14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani”

Unapowahubiria wengine wokovu, unammaliza shetani na upande wa pili.

Ni maombi yangu utafanya hivyo kuanzia huu wakati. Bwana akubariki…

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP




Mada Nyinginezo:

TUZO UTAPEWA KULINGANA NA NAFASI YAKO.

NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.

ALIYE MKUU KATIKA UFALME WA MBINGUNI.

ANGUKO LA UFALME WA SHETANI:

INJILI YA MILELE.


Rudi Nyumbani:

Print this post

UKITAKA KUMFUATA YESU NI SHARTI UACHE VYOTE!

Luka 14: 25 “Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia,

26 Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.

27 Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.

28 Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia?

29 Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki,

30 wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza.

31 Au kuna mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, asiyeketi kwanza na kufanya shauri, kwamba yeye pamoja na watu elfu kumi ataweza kukutana na yule anayekuja juu yake na watu elfu ishirini?

32 Na kama akiona hawezi, hutuma ujumbe kutaka sharti za amani, mtu yule akali mbali.

33 Basi, KADHALIKA KILA MMOJA WENU ASIYEACHA VYOTE ALIVYO NAVYO, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”

Bwana Yesu alisema katika mstari wa 26 kuwa asiyemchukia Baba yake na Mama yake, mke wake, mwanawe, na ndugu zake wakiume na wake hawezi kuwa mwanafunzi wake..

Chuki inayozungumziwa hapo sio chuki ile ya dhambi, kwamba umchukie Baba yako au mama yako kwa nia ya kumdhuru, au kumdharau, au kumshushia heshima hapana! Bali chuki inayozungumziwa hapo ni “kuyachukia mapenzi yake ambayo ni kinyume na mapenzi ya Mungu”…Baba anakuambia mwanangu tunapaswa tuende kwa waganga na wewe hali unajua kuwa hayo ni machukizo kwa Mungu, hapo unapaswa uyachukie hayo mapenzi ya Baba yako na kumwambia wazi kwa ujasiri kuwa “Baba mimi siwezi kwenda huko, kwasababu ni Mkristo, namwabudu Mungu aliye mbinguni”..

Mama yako anakwambia ukajiuze tupate pesa, wewe unatakiwa umwambie wazi kuwa “mimi siwezi kufanya hivyo kwasababu ni Mkristo”..Mume wako anakuambia ufanye mambo machafu ambayo ni machukizo kwa Mungu, na anakulazimisha, kutenda dhambi.. hapo unapaswa kumweleza wazi msimamo wako kwamba wewe ni Mkristo, na kama hataki kuishi na wewe, basi anayoruhusa ya kuondoka!…Biblia imeruhusu matengano Katika mazingira kama hayo (soma 1Wakorintho 7:15).

Kuna mtu mmoja alikuwa anazungumza na mimi anasema alikuwa ameokoka tu vizuri yeye na mchumba wake, tena walikuwa wamesimama ipasavyo katika imani, lakini siku ya kwenda kutambulishwa kwao, mama yake Yule mwanamume akamwambia kama hutaacha huo wokovu wako, mimi sio mama yako, na nitakuachia laana..Sasa Yule mwanamume kwa kuwa alikuwa anampenda mama yake zaidi ya Kristo, akaamua kuacha wokovu anakamshawishi na mke wake wote wakaucha wokovu, wakaanza kuwa watu wa ajabu, Yule mwanamume akawa mzinzi na mtu wa kidunia kishinda hata walipokuwa hapo mwanzo..Sasa watu wa namna hiyo Kristo anasema hawafai kwake, na aliposema hawafai alimaanisha kusema kweli hawafai..

Na jambo lingine Bwana alilolisema ni kwamba 33…KADHALIKA KILA MMOJA WENU ASIYEACHA VYOTE ALIVYO NAVYO, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”

Pia mtu asiyeacha vyote alivyonavyo…Maana ya kuacha vyote ulivyo navyo ni kuvitoa vile vitu ndani ya moyo wako…kila mtu anafahamu namna ya kukitoa kitu moyoni, hakuna haja ya kuelezea… “unapotoa kitu moyoni, unakuwa unakifuta ndani yako, kinakuwa sio kitu tena kinachokupa raha, kiwepo kisiwepo ni sawa tu” Wakati mwingine hiyo hali inaweza kuambatana na kuviacha vitu kwa nje kabisa wazi wazi…

Ulikuwa ni Tajiri unauacha utajiri wako unamfuata Yesu, maana yake…Hata mali zote zikipukutika katika safari yako ya kumfuata YESU hilo hujali, kwasababu hazipo tena moyoni mwako, Unamhisi Yesu moyoni kuliko utajiri ulionao…Na pia unakuwa humfuati Yesu ili akupe mali au azilinde mali zako, unamfuata kwasababu Moyoni mwako unaona una haja naye…Kuna upendo fulani ambao unamiminika ndani yako ambao hauwezi kuuelezea, Unajikuta tu unampenda tu Yesu bila sababu kama yeye anavyokupenda wewe bila sababu yoyote.

Kadhalika Ulikuwa ni MASKINI, unauacha Umaskini wako unamfuata YESU. Unauondoa umaskini moyoni mwako….Usimfuate Yesu kwasababu hauna gari! Au kwasababu umaskini unakutesa na kukuumiza… Hapo hujajikana nafsi ndugu! Usimfuate Yesu kwasababu unataka utajiri, au unataka heshima katika jamii, au kwasababu unataka kuwakomesha maadui..Unatakiwa Uuache umaskini wako ndipo unamfuata Yesu kiasi kwamba hata katika safari yako ya Imani, ukiongezekewa na kuwa Tajiri wa mambo ya kimwili, hilo kwako halina maana sana!…mali zikiongezeka ni kama vile moyoni mwako hakuna kilichoongezeka…lakini uhusiano wako na Yesu unapoimarika ndipo unajihisi uchangamfu wa Ajabu unakuvaa….Inafikia mahali umasikini na Utajiri kwako ni sawasawa tu! Kama Ayubu, ilifika wakati hata mali zilipoongezeka hakufurahia (Soma Ayubu 31:25)..

Wapo watu ni maskini lakini hata katika huo umaskini wao, hawajawahi kumwomba Mungu katika sala zao utajiri, wameridhika na wana amani ya Ajabu mioyoni mwao..wawe nacho wasiwe nacho, hilo kwao halijalishi maadamu wanaye Yesu, hilo kwao ndio linalojalisha, huo ndio utajiri mkubwa kwao. Hivyo ni lazima kabla ya kumfuata Yesu kuuacha umaskini! Na kumfuata yeye wewe kama wewe.

Na pia baada ya kuacha vyote namna hiyo, kitakachofuatia ni kuchukiwa, kutengwa, kuonekana umerukwa na Akili, kuonekana mjinga katika jamii na kuonekana hufai…Na hivyo pia unapaswa uwe navyo tayari! Bwana Yesu hakutuficha kabisa alituambia ili tukikutana nayo tusiseme mbona hivi mbona vile..Upige gharama kabisa kabla ya kuanza kujenga Mnara! Usije ukafika katikati ukashindwa kumalizia…

Ndivyo ilivyo kwa Bwana Yesu kabla ya kumfuata, piga hesabu kuwa kuna kuchekwa huko mbele, kuna kudharaulika, kuna kupungukiwa wakati mwingine hata kwa kipindi kirefu sana, wakati mwingine hata miaka kadhaa, hata miaka 5, au 10, hata 15, lakini haitadumu hivyo hata milele, kuna kutengwa na kuonekana mjinga, hata kwa miaka kadhaa…piga gharama zote hizo..Kama haupo tayari! Kuonekana mshamba kwa muda mrefu hivyo, au kuonekana mjinga kwa miaka kadhaa, au kudharaulika kwa miaka kadhaa, au kama haupo tayari kukosana na mama yako kuhusiana na Imani yako, au kukosana na Baba yako, au Watoto wako, au mke wako..kama unajua yatakushinda huko mbeleni…Biblia inasema tafuta sharti ya Amani mapema!…Usijiingize mahali ambapo hujajua yatakayokupata mbeleni, ukaja ukakutana na ambayo hukutegemea ukaanza kujuta na kulalamika.

Kwasababu Bwana Yesu anasema:

Luka 12: 51 “Je! Mwadhani ya kwamba nimekuja kuleta amani duniani? Nawaambia, La, sivyo, bali mafarakano.

52 Kwa kuwa tokea sasa katika nyumba moja watakuwamo watu watano wamefarakana, watatu kwa wawili, wawili kwa watatu.

53 Watafarakana baba na mwanawe, na mwana na babaye; mama na binti yake, na binti na mamaye; mkwe mtu na mkwewe, mkwe na mkwe mtu”.

Je! Umejikana nafsi?..Umejitwika msalaba wako na kumfuata Yesu? Fahamu kubwa mtu yeyote anayeingia gharama kubwa kama hizo, Sio bure bure tu, Huyo anapelekwa katika viwango vya juu zaidi vya kuwa karibu na Kristo zaidi ya watu wengine wote, anafanyika kuwa mwanafunzi wake, na zaidi ya yote Bwana atakuja kumpa mara mia, na siku ile ataketi pamoja naye katika kiti chake cha enzi akiwahukumu mataifa..(Mathayo 19:27-30)

Bwana akubariki.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP



Mada Nyinginezo:

NJIA YA MSALABA.

NI KWANINI MUNGU HAONEKANI?

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA JIKANE MWENYEWE?(MATHAYO 6:24)

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

JE? NI HATUA ZIPI MUHIMU ZA KUFUATA BAADA YA KUBATIZWA?

MTI WA MLOZI ALIOONYESHWA NABII YEREMIA 1:12 TAFSIRI YAKE NI NINI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

NG’OMBE MWEKUNDU ALIYEZALIWA ISRAELI, ANAFUNUA NINI?

Utakumbuka tarehe 28/8/2018 kulitokea tukio la kihistoria Israeli la kuzaliwa kwa ng’ombe mke mwekundu. Kulingana na chuo cha kidini kijihusishacho na mambo ya Hekalu kinasema jambo hilo halikuwahi kutokea kwa zaidi ya miaka 2000, tangu kuharibiwa kwa hekalu la pili pale Yerusalemu. Wanaamini tangu wakati wa Musa hadi kuharibiwa kwa hekalu la pili jumla ya ng’ombe tisa tu wa namna hiyo ndio waliotolewa sadaka kwa ajili ya kuwatakasa watu.
 
Tunasoma wakati wana wa Israeli walipokuwa jangwani Mungu alitoa maagizo kwa kuhani mkuu, kwamba atwae ng’ombe mmoja wa kike, mwekundu, asiye na mapungufu ya aina yoyote, yaani asiwe na jeraha au kilema chochote, asiwe na manyoya ya rangi nyingine yaliyochangikana na hayo mekundu hata kama likionekana nyoya moja tu tayari huyo hafai, anapaswa awe hajazaa, pia anapaswa awe bado hajapandwa na mtu yeyote, au hajatumika kwa kazi yoyote ile, hata kama atakuwa ni mwekundu lakini akiwa ameshawahi kuwekewa hata tambara tu la mizigo juu yake au amefungwa nira shingoni mwake huyo tayari hastahili…
 
Sasa hiyo ndio iliyokuwa inamfanya ng’ombe huyu awe adimu, atakayekidhi vigezo vyote hivyo.. ng’ombe huyo alikuwa anatumika kuwasafisha wana wa Israeli, baada ya kuteketezwa nje ya kambi, majivu yake yalikuwa yanachukuliwa na kuchanganywa na maji masafi, kisha mtu yeyote ambaye alikuwa amenajisika aidha kwa kuishika maiti, au kushika kaburi, au kuwa na maiti nyumbani, au alishika maiti ya mnyama aliyekufa au mzoga basi alinyunyiziwa maji hayo yaliyochanganywa na hayo majivu kwanza kwa muda wa siku tatu, kisha siku ya saba anakuwa safi ndipo aruhusiwe kuingia hemani au hekaluni. Hiyo ilikuwa ni sheria mtu yeyote na aliyekiuka amri hiyo ilikuwa adhabu yake ni kifo.
 
Hivyo ng’ombe huyo alikuwa ni wa muhimu sana katika ibada za hekaluni, yaani kwa namna nyingine bila kuwepo ng’ombe huyo hakuna shughuli zozote za hekuluni zinaweza kuendelea.
 
Hesabu 19:1 “Bwana akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,
 
2 Hii ndiyo amri ya sheria Bwana aliyoagiza, akisema, Waambie wana wa Israeli wakuletee ng’ombe mke mwekundu asiye na kipaku, mkamilifu, ambaye hajatiwa nira bado;
 
3 nanyi mtamleta kwa Eleazari kuhani, naye atakwenda naye nje ya kambi, na mtu mmoja atamchinja mbele yake”;
 
Lakini Kama wengi tunavyofahamu ng’ombe huyu katika agano jipya anasimama kama Bwana wetu Yesu Kristo, yeye ndiye dhabihu iliyotolewa isiyokuwa na ila wala mawaa, Bwana Yesu alikuwa mkamilifu sana hakuna asiyejua hilo, alikuwa hana doa la kasoro yoyote katika mwili wake wala katika roho yake, alikuwa ni dhabihu iliyokamili tayari kwa kafara kwa ajili yetu.
 
Ni ng’ombe mwekundu kwasababu ni ng’ombe wa damu, kumfunua Bwana wetu Yesu Kristo kwamba agano atakaloingia na sisi ni damu yake mwenyewe. Na ndio maana hata tukisoma katika ufunuo, tunamwona siku ile atakaporudi mara ya pili atakuwa na vazi jekundu lililochovya katika damu, kufunua ni jinsi gani alivyotukomboa sisi kwa damu yake..
 
Ufunuo 19:11 “Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.
 
12 Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.
 
13 Naye amevikwa VAZI LILILOCHOVYWA KATIKA DAMU, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.”
 
Sasa leo hii kwanini tukio kama hilo limejirudia Israeli?, Kumbuka Wayahudi ni watu wa mwilini, na pale walipo wanajiandaa kwa kuja kwa masihi wao na kwa ujenzi wa hekalu la tatu, ambalo wanaamini kwa kupitia hilo Masihi ndipo atakaposhukia..Na kwa muda mrefu walikuwa wakijiuliza hata hekalu litakapojengwa, tutampata wapi huyu ng’ombe mwekundu wa ajili ya utakaso wa watu watakao najisika kwa zile sababu tulizozitaja hapo juu.
 
Lakini mwaka jana tarehe 28/8/2018 tendo hilo lilitimia, Na hiyo ilikuwa ni Mungu kuwathibitishia kuwa hivi karibuni Hekalu litajengwa, Kumbuka ndugu kwetu sisi wakristo kinaweza kisiwe kitendo cha maana sana kwani sisi tunafahamu kuwa dhabihu halisi ni YESU KRISTO na sio ng’ombe. Lakini wayahudi bado hawajapata neema hiyo, hivyo Mungu pia anasema nao kwa ishara wanazoziamini ili tu kuwathibitishia kuwa wakati wao upo karibu sana..Hata siku ile watakapofumbuliwa macho na kumwamini masihi, ndipo watafahamu kila kitu.
 
Ni wakati gani huu tunaishi? Una habari kuwa neema itahama na kuiendea Israeli? Na ikishahamia Israeli, sisi huku mlango utakuwa umeshafungwa? Ni dhiki kuu ya mpinga kristo itakuwa inaendelea, wakati huo Unyakuo utakuwa umeshapita.. Leo hii unaichezea hii neema laiti ungeona ni wayahudi wangapi wanalia usiku na mchana pale YERUSALEMU kwenye ukuta wa maombolezo, wanamlilia Mungu wao aje kuwaokoa na kuwapigania kama ilivyokuwa katika enzi za kale, ambapo kimsingi ni kweli watarudiwa. halafu sisi huku watu wa Mataifa tunachezea wokovu, siku zimeshakaribia sana, watauona wokovu ambao wanautaabikia sasa.
 
Wayahudi leo hii wanasema ikiwa Mungu hakutuletea ng’ombe huyu kwa muda wa zaidi ya miaka 2000 na amemleta leo, ni ishara kuwa huu ndio wakati aliouandaa wa sisi kumjengea hekalu.
 
Ndugu hatuna mengi ya kuzungumza hapo, huu ni wakati wa kuchagua ni upande upi wa kusimama, Kipindi hichi kifupi tulichobakiwa nacho kitumie vizuri, maana hatujui kesho ni nini kitatokea? tubu dhambi zako zote leo kwa Bwana Yesu kama bado hujafanya hivyo, jitwike msalaba wako umfuate, kisha ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi kwa jina la YESU KRISTO upate ondoleo la dhambi zako, kulingana na Matendo 3:38 ili Mungu akupe Roho wake mtakatifu ambaye atakulinda na kukuongoza katika kuijua kweli yote ya Biblia..Kumbuka pasipo Roho Mtakatifu hakuna Unyakuo..Unasubiri nini?
 
Bwana akubariki.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP



 

Mada Nyinginezo:

WAISRAELI WENGI SANA WANARUDI KWAO SASA.

AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA.

SIKU YA TAABU YA YAKOBO.

NOTI YA UFALME WA MBINGUNI.

SIKU YA BWANA INAYOTISHA YAJA!

UNYAKUO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

HAMJAFAHAMU BADO?

 Moja ya mambo ya muhimu sana ambayo Roho Mtakatifu anayafanya ndani ya mtu baada ya kukata shauri la kumfuata Yesu Kristo, kwa moyo wote ni “KUMWONDOLEA HOFU YA MAISHA HAYA” Karibia kila mwamini katika hatua za kwanza kwanza kabisa, Roho Mtakatifu ni lazima ampitishe katika madarasa ya kumwondolea hofu ya Maisha haya…Kwasababu katika hali ya kawaida wanadamu wote tukishafikisha umri fulani, tayari hofu ya Maisha inakuja yenyewe ndani yetu…Hofu ya Kesho itakuwaje! Mwakani nitaishije! Nitakula nini wiki zijazo, nitaishije ishije! Na mambo mengine mengi…Hofu hii haijalishi wewe ni nani, maadamu umeshaitwa mtu, tena mwenye Akili timamu lazima ije ndani yako…Ni hofu ambayo inamfanya mtu awe mtumwa wa Kesho! Ni hofu ambayo inamfanya mtu asiwe anaridhika na mwisho wa siku anakuwa katika mkandamizo mkubwa wa mawazo..

Sasa Roho Mtakatifu anajua kabisa hatuwezi kumtumikia Mungu katika hali hiyo ya utumwa wa Kesho itakuwaje! Kwasababu hiyo basi ni lazima ampitishe katika kipindi fulani cha madarasa, kuipunguza hiyo hofu ndani ya Mtu ili aweze kuishi kwa furaha akiwa ndani ya Yesu.

Hebu fikiria mwanao, anakaa nyumbani mwako, halafu anakwenda shule huku anamashaka kwamba Kesho anaweza asipate chakula nyumbani, au akiwa na mashaka kwamba atakosa ada! Je! Huyo mtoto atasoma kweli, au atafanya vizuri darasani? Ni wazi kuwa hatasoma bali atakuwa ni mtu tu wa mawazo siku zote! Na itamsababishia kufeli, na hivyo hivyo Mawazo ya Maisha haya na mawazo ya Kesho itakuwaje! Itatusababishia tusimwelewe Mungu na kutusababisha tufeli mitihani mingi ya Maisha yetu ya kikristo.

Kulitatua hilo Bwana Yesu aliwafundisha wanafunzi wake masomo kadhaa, ya kutohofia Kesho, na hivyo kwa masomo hayo pia anatufundisha na sisi…Embu tusome tukio hili moja..

Mathayo 16:5 “Nao wanafunzi wakaenda hata ng’ambo, wakasahau kuchukua mikate.

6 Yesu akawaambia, Angalieni, jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.

7 Wakabishana wao kwa wao, wakisema, Ni kwa sababu hatukuchukua mikate.

8 Naye Yesu akafahamu, akawaambia, Mbona mnabishana ninyi kwa ninyi, enyi wa imani chache, kwa sababu hamna mikate?

9 Hamjafahamu bado, wala hamkumbuki ile mikate mitano kwa wale elfu tano, na vikapu vingapi mlivyoviokota?

10 Wala ile mikate saba kwa watu elfu nne, na makanda mangapi mliyoyaokota?

11 Imekuwaje hamkufahamu ya kuwa si kwa sababu ya mkate naliwaambia? Ila jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.

12 Ndipo walipofahamu ya kuwa hakuwaambia kujilinda na chachu ya mkate, bali na mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo”

Somo hilo Bwana Yesu aliwafundisha wanafunzi baada ya Wanafunzi wake kusahau kubeba mikate ya safari yao..Hivyo walipofika njiani, Bwana Yesu akawaambia wajihadhari na chachu ya mafarisayo, wenyewe wakadhani anawashutumu kwanini hawakubeba mikate katika safari yao..na hivyo hawana kitu cha kula, kwamba Bwana kawakataza wasile chachu ya mafarisayo…(kumbuka chachu ni hamira, na chachu ilikuwa inawekwa kwenye mikate, hivyo mtu akizungumzia chachu ilikuwa inajulikana kwamba anazungumzia mikate yenye Hamira)..

Hivyo wanafunzi wakahuzunika sana, kwasababu watakwenda kukaa na njaa bila chakula huko wanakokwenda…Lakini Bwana Yesu aliwakemea na kuwaambia wana Imani chache…kwasababu wameshasahau jinsi gani Bwana alifanya miujiza ya kutokeza maelfu ya mikate kutoka katika mitano tu na maelfu ya watu wakala na kusaza na kukusanya mabaki mengi tena mara mbili… kama Mungu aliweza kufanya hivyo huko nyuma kwanini asiwafanyie tena hivyo huko mnakokwenda?? Huo ndio ulikuwa ujumbe wa Bwana! Wasianze kutafakari tafakari Kesho wakula nini? Kesho kutwa watavaa nini…wao kazi yao ni kuangalia mbele kuitenda kazi ya Mungu na hayo mengine watazidishiwa…

Tunaona tena mahali pengine Bwana Yesu alizidi kulitilia mkazo jambo hilo katika Mathayo Mlango wa 6

Mathayo 6: 24 “Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.

25 Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?

26 Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Ninyi je! Si bora kupita hao?

27 Ni yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?

28 Na mavazi, ya nini kuyasumbukia? Fikirini maua ya mashamba, jinsi yameavyo; hayafanyi kazi, wala hayasokoti

29 nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo.

30 Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?

31 Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?

32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.

34 Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake”

Unaona! Bwana anatufundisha ni jinsi gani, Kesho yetu ipo mikononi mwake, kwamba haijalishi leo sina chochote lakini Kesho nitakuwa na kitu..Bwana hawezi kutupungukia kabisa ikiwa tu tupo katika kusudi lake, anasema hivyo katika Neno lake (Waebrania 13:5), anajua tuna haja ya chakula, mavazi, malazi, makazi n.k lakini anachotutaka ni sisi kumtafuta kwanza yeye..Tusiwe na hofu ya Kesho..Kwasababu Hofu ni utumwa, hakuna mtu yeyote mwenye hofu, akapiga hatua yoyote mbele, hakuna.

Tatizo lililopo tunataka pindi tu tunapomkaribisha Yesu Maishani mwetu, basi atupe ratiba ya leo, Kesho na miaka mitano au kumi mbele itakuwaje! Tunataka tuone Kesho tutakuwa na shilingi ngapi mifukoni mwetu, uhakika wa kila kitu…Mungu si wakati wote anatenda kazi hivyo, wakati mwingine unaweza kukupitisha katika ukame leo, na huku hujui Kesho utakuwaje na ghafla ukashangaa kafungua mlango Kesho ukapata unayohitaji tena na zaidi ya matarajio yako…

Hivyo yeye anataka tu tumwamini kwamba hatatuacha kabisa! Anafahamu tunayohitaji!

Kama unafanya shughuli yoyote ambayo inakupatia kipato, na ikatokea ukapungukiwa kabisa, anatakiwa umwamini kuwa hajakuacha, na wala hana mpango wa kukuacha!..kumbuka wakati fulani nyuma ambapo ulipitia kupungukiwa na akakufungulia mlango kimiujiza…ukumbuke huo muujiza, na usikie sauti yake leo moyoni mwako ikikuambia…HUJAFAHAMU TU?..Haujafahamu bado?..Siku ile ulipopungukiwa na akakufungulia mlango kimiujiza?..Yatafakari matendo yake ya nyuma kisha Uinyanyue Imani yako kwake..na siku zote utaishi Maisha ya furaha na yasiyo na hofu, ukijua kuwa Baba yako wa Mbinguni, sio Baba wa kambo, ni Baba wa damu kabisa ambaye hapendi kuona utakufa njaa wala kuteseka.

Maombolezo 3:36 “Na kumnyima mtu haki yake, Hayo Bwana hayaridhii kabisa”.

Bwana akubariki.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP



Mada nyinginezo:

CHAKULA CHA ROHONI.

USITAFUTE FAIDA YAKO MWENYEWE BALI YA WENGINE.

YAKUMBUKE YA NYUMA.

SI SHETANI BALI NI WEWE. (CHAGUA MEMA)

MUNGU WANGU,MBONA UMENIACHA?.

LAANA YA YERIKO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNANG’OKA MENO.

Hii ni moja ya ndoto inayootwa na watu wengi, ikiwa na wewe ni mmojawapo na inajirudia rudia  mara kwa mara basi fahamu kuwa lipo jambo ambalo Mungu anataka kukukumbusha, Sikuzote meno yanafanya kazi mbili kuu, ya kwanza ni kumeng’enya na ya pili ni kung’ata,..asilimia kubwa ya viumbe vyote vinatumia meno kwa kazi mojawapo ya hizo, isipokuwa tu mwanadamu inaongezeka nyingine hapo, ambayo ni kuzungumza, mtu usipokuwa na meno huwezi kuzungumza, atatoa sauti tu zisizoeleweka…

Vilevile Mtu Ukipoteza meno huwezi kula vitu vigumu, wala huwezi kung’ata kitu chochote Na ndio maana mtu unapoota meno yake aidha  ya juu au ya chini au magego yanang’oka halafu ghafla ukashtuka saa hiyo hiyo  na kujiona yupo salama huwa anashukuru kweli, anasema afadhali imekuwa ndoto, ni kwasababu unajua thamani iliyo katika meno yake.

Sasa ukiota meno yanatoka Hapo ni Mungu anakukumbusha, kuwa unakaribia kupoteza Meno yako ya rohoni, yenye thamani kubwa zaidi ya haya ya mwilini, ikiwa hujaokoka basi nakushauri  utubu haraka sana, umegukie Mungu wako, kwasababu mara kikipotea hicho basi fahamu kuwa kitapotea milele…Ukishaondolewa  uwezo wako wa kupambanua na kuyaelewa  mambo ya rohoni basi hutakaa uwe nao tena, ukishaondolewa uwezo wako wa kung’ata maadui zako wa rohoni kwa meno makali Mungu aliyokupa basi fahamu utabakia hivyo milele, Vilevile Ukishaondolewa uwezo wa kuzungumza na Mungu wako rohoni basi ndio utabakia hivyo milele na milele hatakaa  akuelewe wewe, hiyo inamaanisha hata ukiomba dua yao hawezi kukusikia…Na hiyo yote ni kwasababu ya dhambi zako unazozitenda sasa hivi.

Zaburi 58:3 “Wasio haki wamejitenga tangu kuzaliwa kwao; Tangu tumboni wamepotea, wakisema uongo.

4 Sumu yao, mfano wake ni sumu ya nyoka; Mfano wao ni fira kiziwi azibaye sikio lake.

5 Asiyeisikiliza sauti ya waganga, Ijapo wanafanya uganga kwa ustadi.

6 Ee Mungu, UYAVUNJE MENO YAO VINYWANI MWAO; Ee Bwana, uyavunje magego ya wana-simba.

7 Na watoweke kama maji yapitayo kwa kasi; Akiielekeza mishale yake, iwe imetiwa ubutu”.

Ndugu Usiipuuzie Injili ya msalaba hata kidogo, inapohubiriwa mbele zako, Mungu ameona jambo hilo kwako na hivyo anakuonya kwasababu anakupenda, mgeukie muumba wako, anza kuzingatia Neno lake kile anachokuambia tii na yeye mwenyewe atakuokoa na kukulinda na kukuongoza hadi unyakuo.

Aidha kama wewe tayari upo ndani ya Kristo, na unaota ndoto za namna hiyo hapo Mungu anakuonyesha pia ni jinsi gani unaelekea kupoteza ule uwezo wako wa thamani uliokuwa nao wa kupambanua  mambo ya rohoni na ukali wako, hivyo simama imara kama ulikuwa umeshaanza kuyumba yumba,  au kupoa simama imara ili usije ukabakia kuwa mbwa bubu tu asiyeweza hata kubweka rohoni (kukemea dhambi )kwa kukosa meno.

Isaya 56:10 “Walinzi wake ni vipofu, wote pia hawana maarifa; wote ni mbwa walio bubu, hawawezi kulia; huota ndoto, hulala, hupenda usingizi.

11 Naam, mbwa hao wana choyo sana, hawashibi kamwe; na hao ni wachungaji wasioweza kufahamu neno; wote pia wamegeuka upande, wazifuate njia zao wenyewe, kila mmoja kwa faida yake, toka pande zote.

12 Husema, Njoni, nitaleta divai, Na tunywe sana kileo; Na kesho itakuwa kama leo, Sikukuu kupita kiasi”.

Zingatia hayo na Bwana hakika atakuwa na wewe katika kila hatua moja unayopiga kwake…Hizi ni siku za mwisho na Unyakuo wa kanisa upo karibuni, tengeneza mambo yako.

Ubarikiwe.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP



Mada Nyinginezo:

KUOTA UNAENDESHA GARI.

KUOTA UPO UCHI.

KUOTA UNAFANYA MTIHANI.

JE! KUBET NI DHAMBI?

JE! NI KWELI KUNA VIUMBE VINAVYOISHI SAYARI NYINGINE (ALIENS)?

UBATILI.


Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNAENDESHA GARI.

Awali ya yote ni vizuri kufahamu kuwa asilimia kubwa ya ndoto tunazoota kila siku au mara kwa mara huwa zinatokana na mawazo yetu wenyewe, naweza kusema hata asilimia 95 ya ndoto zote tuziotazo usiku hutokana na sisi wenyewe, na hizo zinakuja  aidha kwa shughuli tunazozifanya kila siku au mazingira yanayotuzunguka au kitu tunachokiwaza sana…

Hivyo ndoto kama hizi, huwa hazibebi ujumbe wowote wa rohoni, ikitokea umeota  wewe zipuuzie tu vinginevyo utajikuta unachanganyikiwa ukidhani kuwa kila ndoto unayoota ina maana, ikiwa bado hujaweza kuzitofautisha aina za ndoto katika makundi yake basi pitia kwanza somo hili ili upate msingi kisha tuendelee. >>>NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI?

Lakini kama ndoto unayoota haihusiani na mazingira uliyopo, na huwa inajirudia mara kwa mara, basi lipo jambo ambalo Mungu anataka kukuonyesha hapo.

Sasa Kuota unaendesha gari na wakati mwingine umewapakiza watu nyuma,  ni ishara kwamba wewe mwenyewe unayaongoza maisha yako au maisha ya wengine, kukufikisha mahali Fulani au kuwafikisha mahali fulani..Kama wewe umeokoka na unalifanya kusudi la Mungu au unaifanya kazi ya Mungu basi zidisha mwendo katika safari yako kwasababu lengo lako utalifikia, kama hutapunguza mwendo kama alivyofanya Yehu, pale alipokuwa anakwenda kumuua Yule mfalme muasi Yoramu na mama yake Yezebeli waliowakosesha Israeli mpaka kupelekea wakaingia kwenye uchawi na ibada za sanamu, na Kumkasirisha Mungu kwa viwango vya juu sana.

2Wafalme 9:20 Yule mlinzi akatoa habari, akasema, Amewafikilia wala harudi tena; na mwendo huu ni kama mwendo wa Yehu mwana wa Nimshi; MAANA ANALIENDESHA GARI KWA KASI.

Hivyo kama unalo kusudi la Mungu mkononi mwako,litimize bila kuogopa kipingamizi au mitazamo ya watu..

Lakini pia,

unapaswa uwe makini ni gari la aina gani unatumia kuliendesha kusudi la Mungu wakati Fulani mfalme Daudi alikuwa analitoa sanduku la Mungu kutoka kwa Abinadabu kwenda Yerusalemu, lakini alifanya makosa kuwatumia ng’ombe kama usafiri wa kulisafirisha kusudi la Mungu badala ya kutumia watu tena makuhani ambao ndio Mungu aliowaagiza walibebe wakati wote,  wao wakawaweka ng’ombe kama magudurumu ya gari lao na ikapelekea kifo cha mtu mmoja..soma 1Nyakati 13:7

1Nyakati 13:7 “Hivyo Wakalipandisha sanduku la Mungu juu ya gari jipya kutoka nyumba ya Abinadabu; na Uza na Ahio WAKALIENDESHA LILE GARI.

8 Wakacheza Daudi na Israeli wote, mbele za Mungu, kwa nguvu zao zote; na kwa nyimbo na kwa vinubi, na kwa vinanda, na kwa matari, na kwa matoazi, na kwa tarumbeta.

9 Hata walipofika penye uga wa Nakoni, Uza akaunyosha mkono wake alishike sanduku; kwa maana wale ng’ombe walikunguwaa.

10 Ndipo hasira ya Bwana ikawaka juu ya Uza, naye akampiga, kwa sababu alilinyoshea sanduku mkono wake, hata akafa pale pale mbele za Mungu.

Hivyo uwe makini unapolifanya kusudi la Mungu na wale unaowaongoza, zingatia vigezo cha maandiko . Na ndio maana wengine wanaota wanaendesha vyombo tofauti tofauti , wengine wanaota wanaendesha malori, wengine wanaota wanaendesha baiskeli, wengine wanaota wanaendesha pikipiki n.k. Vyovyote vile, kuendesha ni kuendesha tu, hiyo ni kulingana na kusudi Mungu alilokupa cha msingi hapo ni kutimiza kusudi hilo kwa ukamilifu wote, ili uepuke kulaumiwa huko mbeleni.

Lakini kama unajijua wewe bado ni mwovu na hadi sasa upo katika dhambi, Hiyo ni Ishara mbaya sana kwako, Aidha Unajiongoza mwenyewe katika mauti au unawaongoza wengine katika mauti, au vyote viwili kwa pamoja..

2Nyakati 21:12 “Likamjia andiko kutoka kwa Eliya nabii, kusema, Bwana, Mungu wa Daudi baba yako, asema hivi, Kwa sababu hukuziendea njia za Yehoshafati baba yako, wala njia za Asa mfalme wa Yuda;

13 lakini umeiendea njia ya wafalme wa Israeli, UKAWAENDESHA KATIKA UASHERATI Yuda na wenyeji wa Yerusalemu, kama walivyofanya nyumba ya Ahabu; tena umewaua ndugu zako wa nyumba ya baba yako, waliokuwa wema kuliko wewe;

14 tazama, Bwana atawapiga pigo kubwa watu wako, na watoto wako, na wake zako, na mali yako yote;

15 nawe utakuwa na ugonjwa mkuu kwa maradhi ya matumbo, yatakapotokea matumbo yako kwa sababu ya ugonjwa huo siku kwa siku.

Unaona hapo huyu mfalme Yehoramu, alikuwa mtu mwovu, alikuwa ni muuaji, na mwabudu sanamu, akawafanya na Israeli wote wote wawe kama yeye, au kwa lugha nyingine akawaendesha waisraeli mpaka kwenye uasherati wa kiroho, kwa sababu hiyo basi Mungu akampiga kwa mapigo yale..

Hata na wewe, unayaongoza maisha yako sasa ukidhani kuwa upo salama, lakini mwisho wake utakuwa ni mauti kama hutatubu, unawasababishia wengine mauti wale walio chini yako, au wanaokutegemea, au wanaokutazama kwa mwenendo wako na maisha yako..

Hivyo Bwana anakupenda na ndio maana anakuonya Leo hii, Utubu umgeukie yeye, ili uliendeshe gari la maisha yako katika njia sahihi ya kutimiza makusudi ya Mungu na sio makusudio ya Shetani.

Ubarikiwe.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

KUOTA UNAFANYA MTIHANI.

KUOTA UPO UCHI.

KUOTA UNAPAA.

KUOTA UNASAFIRI.

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?

JE! KUBET NI DHAMBI?

AGANO LAKO LINABEBWA NA NANI?.


Rudi Nyumbani:

Print this post

SIKU ZA MWISHO ZA UHAI WANGU.

Kila mwanadamu atafikia ukomo wa siku zake, (yaani siku ya Mauti yake)..Lakini kabla ya siku yenyewe ya kuondoka ulimwenguni haijafika…Kinakuwepo kipindi fulani kifupi ambacho kinaweza kuwa ni miaka 10, au 5 kabla ya kuondoka kwako, au kinaweza kuwa mwaka mmoja au mwezi mmoja au wiki moja….Kipindi hicho kifupi ndicho kinachojilikana kama SIKU ZA MWISHO ZA UHAI WA MTU. 

Katika kipindi hicho, Kuna hali fulani mtu anakuwa anaanza kuipitia, mara nyingi inakuwa ni kumbukumbu ya mambo yaliyopita nyuma, ndio utakuta mtu anaanza kukumbuka mambo yake yote ya nyuma aliyoyapitia na jinsi alivyoyaishi, kipindi hichi sio kipindi kizuri kwa Mtu ambaye hakuwa ndani ya Kristo, kwasababu ni kipindi cha mashaka mazito, mara nyingi kwa mtu ambaye hajampa Kristo maisha yake huko nyuma, ni ngumu sana kushinda hali atakayopitia wakati wa hiki kipindi. Wengi wanaishia kujiua.

Ndio maana Biblia ikasema katika Mhubiri.

Mhubiri 12:1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo”

Umeona hapo? biblia haisemi mkumbuke muumba wako wakati wa siku zilizo mbaya..Hapana! bali inasema mkumbuke muumba wako siku za ujana wako, kabla hazijakaribia siku zilizo mbaya…Siku zilizo mbaya zinazozungumziwa hapo ndio hizi SIKU ZA MWISHO ZA UHAI WAKO.

Siku hizo ni ngumu kumrudia Muumba wako, kama katika siku za ujana wako ulikuwa unaichezea Neema, na kumbuka pia siku za ujana sio tu siku za miaka ya ujana kama vile miaka 15-45 hapana..bali siku za ujana ni siku ambazo ulikuwa unauwezo wa kumgeukia Mungu, na mazingira yote yalikuwa yanakuhimiza kufanya hivyo lakini  hukutaka!

Hivyo huu sio wakati wa kuzunguka huko na huko mitandaoni na mitaani kutafuta mambo ya ulimwengu huu yanayopita, huu ni wakati wa kutafuta wokovu kwa nguvu zote. Biblia inasema Ufalme wa Mbinguni unapatikana kwa nguvu na wenye nguvu ndio wauteka..Je! wewe nguvu zako unazipeleka wapi sasa katika ujana wako? katika ulimwengu au kwa Yesu?..Kama ni katika ulimwengu basi tambua kuwa SIKU ZA KUFA KWAKO ZINAKARIBIA na katika siku hizo, hazitakuwa siku za furaha bali huzuni.

Daudi aliziona siku zake na alikuwa na furaha..akafurahi akamwusia mwanawe kuzifuata njia za Bwana.

1Wafalme 2:1 “Basi siku ya kufa kwake Daudi ikakaribia, akamwusia Sulemani mwanawe, akasema,

2 Mimi naenda njia ya ulimwengu wote; basi uwe hodari, ujionyeshe kuwa mwanamume;

3 uyashike mausia ya Bwana, Mungu wako, uende katika njia zake, uzishike sheria zake, na amri zake, na hukumu zake, na shuhuda zake, sawasawa na ilivyoandikwa katika torati ya Musa, upate kufanikiwa katika kila ufanyalo, na kila utazamako;”

Yakobo naye aliziona siku za kufariki kwake akafurahi, akawabariki wanawe…

Na siku hizo zinakuja kwako mimi na wewe! Umejiandaaje?..je zitakuja na huzuni au furaha kwako?

Tubu mgeukie Kristo sasa, angali mlango wa Neema bado upo..Angali u kijana.Na Kristo atakupa tumaini la maisha ya sasa, na yale yajayo!

Bwana akubariki.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

HUDUMA YA MALAIKA WATAKATIFU.

SIKU ZA MAPATILIZO.

WEWE NI HEKALU LA MUNGU.

JE! BAADA YA ULIMWENGU HUU KUISHA MALAIKA WATAKUWA NA KAZI GANI TENA?

JE! KUNA UBAYA WOWOTE KUWAOMBEA NDUGU ZETU WALIOKUFA KATIKA DHAMBI, MUNGU AWAKUMBUKE KATIKA UFALME WA MBINGUNI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Mtu wa Kwanza kufika mwezini

Hakukuwa na mtu mmoja maalumu aliyefika mwezini, kulingana na Sayansi…Waliofika mwezini ilikuwa ni TEAM ya watu watatu (Neil A. Armstrong, Michael Collins na  Edwin E. Aldrin Jr.) Hao ndio waliokuwa ndani ya chombo cha Kwanza kulichotua mwezini, na wote watatu walikuwa ni wa-Marekani na safari yao iliyojulikana kama Apollo 11. Safari yao ilichukua siku 8 na masaa 3..Kwenda na kurudi, Na hiyo ilikuwa ni Mwaka 1969.

Sasa kumbuka tukio lolote linaloendelea duniani, linafunua tukio fulani linaloendelea katika roho.

Kama wanadamu wamefikia hatua ya kutengeneza chombo ambacho kimewafanya wafike juu zaidi ya mawingu, na kutua Mwezini. Kadhalika kuna kitu pia kinaendelea kutengenezeka  sasa katika roho, ambapo itafikia kipindi kitakamilika, na hicho kitalifanya kanisa kupaa juu sana zaidi ya mawingu na zaidi ya mwezi na kulifanya lifike mahali panapoitwa Mbinguni.

Na kama tunavyoona hiyo safari ya kwenda mwezini ilihusisha watu wachache sana, kadhalika, safari ya kwenda mbinguni itahusisha watu wachache sana, kwasababu biblia inasema mlango ni mwembamba na njia imesonga ielekeayo uzimani..

Hivyo ndugu, huu ni wakati wa kuingia ndani ya Kristo, kwani injili sasa inahubiriwa na teknolojia tunazoziona, Hizi ni zile siku za mwisho ambazo biblia imesema maarifa yataongezeka…Na tunaona jinsi yanavyoongezeka kwa Kasi, na katika roho pia yanaongezeka, watu wa Mungu hivi karibuni watafikia Imani ya kunyakuliwa na hivyo kuondoka kwenda mbinguni kwa Bwana..Je! na wewe utakuwa miongoni mwao?

Jibu unalo, tubu mpe Kristo maisha yako na uishi maisha yanayopatana na Toba yako.

Bwana akuabariki.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA

NYOTA ZIPOTEAZO.

KUONGEZEKA KWA MAARIFA.

ROHO SABA ZA MUNGU NI ZIPI? NA JE ZINATOFAUTIANA NA ROHO MTAKATIFU?


Rudi Nyumbani:

Print this post