Category Archive Home

Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.

Zaburi 147:3 Huwaponya waliopondeka moyo, Na kuziganga jeraha zao.  4 Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.  5 Bwana wetu ni mkuu na mwingi wa nguvu, Akili zake hazina mpaka.

Ukitazama juu unaona nyota nyingi sana zisizo na idadi, mbali na hizo zilizo ndani ya upeo wa macho yetu, lakini pia zipo nyingine tusizoziona ambazo idadi yake ni mabilioni kwa mabilioni, matrilioni kwa matrilioni,..

Lakini hapa Mungu anatupa siri ya uweza wake, anasema zote hizo amezihesabu na kuzipa majina,..

Sasa Kwanini atuambie jambo kama hilo?

Ni kutuaminisha kuwa ikiwa anazifahamu  nyota zote zilizo mbali, nje-ndani, atashindwaje kutufahamu sisi? Atashindwaje kuziona taabu zetu na shida zetu, atashindwaje kuyaona mateso yetu na majeraha yetu?

Hivyo hapo anaposema ‘Huwaponya waliopondeka moyo, Na kuziganga jeraha zao’. Anamaanisha, huweza kutufanya upya, endapo tutamkaribia.

1Petro 5:7  ‘huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu’.

Mkaribie Kristo akuponye kwasababu yeye yupo karibu sana na wewe zaidi ya nyota za angani.

Utukufu na uweza vina yeye milele na milele amina.

Maombi Yangu:

“Baba mwema, tumeona uweza wako, juu ya ulimwengu wako uliouumba, kwamba hakuna lolote usilolijua,wala usiloliweza, na sasa ninakukaribia Baba wa Upendo, kama ulivyoahidi kwenye Neno lako kwamba utaziganga jeraha zangu, Naomba sasa niponye moyo wangu, na mwili wangu, nifanye upya tena, nisimame mbele zako, nikutumikie. Ni katika jina la Yesu naomba nikuamini. Amen.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NYOTA ZIPOTEAZO.

UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?

Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?

MUNGU WETU, JINSI LILIVYO TUKUFU JINA LAKO DUNIANI MWOTE!

UNAMCHUKULIA YESU KWAKO KAMA NANI?

Agano ni nini? na kuna aina ngapi za maagano?

Mofa ni nini? na inafunua nini kiroho?(1Samweli 28:24).

NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.

Rudi nyumbani

Print this post

Ni kosa gani alilolifanya Eli, ilihali aliwaonya watoto wake?

SWALI: Kwanini Mungu alimuadhibu Eli kwa kosa la kutowaonya watoto wake, angali tunasoma katika maandiko aliwaonya hapo kabla?

Tusome;

1Samweli 2:22 Basi Eli alikuwa mzee sana; naye alisikia habari za mambo yote ambayo wanawe waliwatenda Waisraeli; na jinsi walivyolala na wanawake waliokuwa wakitumika mlangoni pa hema ya kukutania. 

23 Akawaambia, Mbona mnatenda mambo kama hayo? Maana nasikia habari za matendo yenu mabaya kwa watu hawa wote.  24 Sivyo hivyo, wanangu, kwa maana habari hii ninayoisikia si habari njema; mnawakosesha watu wa Bwana. 

25 Mtu mmoja akimkosa mwenzake, Mungu atamhukumu; lakini mtu akimkosa Bwana, ni nani atakayemtetea? Lakini hawakuisikia sauti ya baba yao, kwa sababu Bwana amekusudia kuwaua.

Lakini Hapa Mungu anasema…

1Samweli 3:12 Siku hiyo nitayatimiza maneno yale yote niliyoyasema juu ya Eli katika habari za nyumba yake, tangu mwanzo hata mwisho. 

13 Kwa maana nimemwambia ya kwamba nitaihukumu nyumba yake milele, kwa ajili ya ule uovu alioujua; kwa kuwa wanawe walijiletea laana, wala yeye HAKUWAZUIA. 

14 Na kwa hiyo nimeapa juu ya nyumba ya Eli, ya kwamba uovu wa nyumba ya Eli hautasafika kwa dhabihu wala kwa sadaka hata milele.


JIBU: Kibiblia “Kuonya” sio tu kusema kwa mdomo, bali pia kuchukua hatua stahiki, endapo maonyo hayatatekelezwa. Eli ni kweli aliwaonya watoto wake, kwa dhambi walizokuwa wanazifanya madhabahuni pa Mungu, lakini aliendelea kuwaangalia, wakifanya mambo yao maovu bila kuwaondoa katika nafasi zao. Ndio maana hapo kwenye 2Samweli3:13 Mungu anamwambia Samweli, kwamba HAKUWAZUIA. Hakuwaondoa katika kazi ya utumishi, Pengine kwasababu ni watoto wake, warithi wake, akawastahi zaidi ya  Mungu. Hivyo wakati wa adhabu ulipofika yeye naye alishiriki adhabu ile.

Hili ni funzo, pia kwa viongozi wote wa imani, nyakati hizi tunazoishi, kanisa limegeuzwa kama mahali pa kila mtu kujiamulia jambo lake, na viongozi wanaona wanafumbia macho. Utakuta mchungaji ni mzinzi, lakini askofu akipata taarifa, badala wamwondoe katika ofisi ile, wanamwonya tu, kisha wanamuhamisha dayosisi, wanamstahi, na akifika kule anaendelea na maovu yake, anahamishwa tena dayosisi.

Utakuta watoto wa wachungaji, ni walevi, hawana maadili, lakini wanaendelea kubaki katika nafasi za wazee wa kanisa au waimbaji kwaya. Mchungaji akiambiwa, anachokifanya ni kuwaonya tu, lakini bado wanaendelea kushika nafasi hizo za madhabahuni. Hii ni hatari. Mungu anataka hatua stahiki zifuatane na maonyo kama hakuna mabadiliko.

Hivyo kama wewe ni kiongozi, kumbuka maonyo yako ni lazima yaambatane na vitendo.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwanini Kuhani wa Mungu Eli alikufa kwa kuvunjika shingo?

IKABODI MAANA YAKE NI NINI?

NA NENO LA BWANA LILIKUWA ADIMU SIKU ZILE.

NI NINI KINATOKA KINYWANI MWA MTOTO WAKO?

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?

Rudi nyumbani

Print this post

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU BARAKA

Baraka ni karama ya Mungu, na kila mmoja wetu aliyekombolewa na Yesu, ahadi hiyo ni yake. Baraka zimegawanyika mara mbili, zipo baraka za mwilini, na baraka za rohoni. Lakini kubwa zaidi ni zile za rohoni. Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyoeleza Baraka za Mungu. Lakini pia ikiwa utapenda kupata vifungu mbalimbali, pamoja na mafundisho mazuri ya Neno la Mungu, bofya link hii uweze kujiunga na kundi letu la Whatsapp>>> WHATSAPP GROUP

Wafilipi 4:19  “Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu”

Yakobo 1:17  “Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka”.

Hesabu 6: 24 “Bwana akubarikie, na kukulinda;  25 Bwana akuangazie nuru za uso wake, na kukufadhili;  26 Bwana akuinulie uso wake, na kukupa amani”

3Yohana 1:2  “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo”

2Wakorintho 9:8  “Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema;”

Kumbukumbu 28:2 “na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako.  3 Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.  4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako.  5 Litabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga.  6 Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo”.

Waefeso 1:3 ” Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo;”

Mathayo 6:30 ” Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba? 31  Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini? 32  Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote. 33  Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa. 34  Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake”

Malaki  3:10 “Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la”.

Zaburi 20:4 “Akujalie kwa kadiri ya haja ya moyo wako, Na kuyatimiza mashauri yako yote”.

Mathayo 5:6  “Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa”.

Mithali 16:3 “Mkabidhi Bwana kazi zako, Na mawazo yako yatathibitika”

Yeremia 17:7 “Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake”

Pia Kwa wokovu/ maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU WATOTO.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU KIFO.

MISTARI YA BIBLIA YA FARAJA.

MISTARI YA BIBLIA YA UPONYAJI.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU UPENDO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

Dina akatoka kuwaona binti za nchi. (Mwanzo 34:1)

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, Huu ni mfululizo wa masomo maalumu kwa ajili ya wanawake: Ikiwa hukupata chambuzi nyingine za nyuma basi fungua link hii  uweze kuzipitia >>>   MAFUNDISHO KWA WANAWAKE

Mwanzo 34:1-3 Inasema..

“Basi Dina, binti Lea, ambaye Lea alimzalia Yakobo, AKATOKA KUWAONA BINTI ZA NCHI.  2 Shekemu, mwana wa Hamori, Mhivi, mkuu wa nchi, akamwona akamtwaa, akalala naye, akambikiri.  3 Moyo wake ukaambatana na Dina binti Yakobo, akampenda huyu msichana, akasema na huyu msichana kwa maneno mazuri”

Dina alikuwa ni binti wa Yakobo, aliyejitunza na kujiheshimu, alikaa chini ya Mama zake akifundishwa desturi za uzao wa Ibrahimu unavyopaswa uwe. Akafahamu kuwa uzao wao haupaswi kuchanganywa na uzao wa ukoo mwingine, Ili Baraka ya Ibrahimu aliyoahidiwa kwa uzao wake isiingiliwe na doa.

Lakini Tunaona, jambo moja alilolifanya Dina, ambalo pengine hakujua mwisho wake utampelekea pabaya. Na jambo lenyewe “ni yeye kutoka na kwenda kuonana na mabinti wa nchi”. Kama msichana alipoona mabinti wa mataifa mengine, wanaishi maisha ya kidunia, maisha ya anasa, maisha ya ukisasa. Na yeye naye akatamani kwenda kuunga urafiki nao, bila kujua mwisho wake utakuwaje.

Hivyo kidogo kidogo, akaanza kuchukuliwa na desturi za wanawake wa kidunia, akaanza kujichanganya, siku ya kwanza, siku ya pili, wiki ya kwanza wiki ya pili, mwezi wa kwanza, mwezi wa pili. Kidogo kidogo wale mabinti wa kidunia waanza kumfundisha tabia mbaya..Pengine wakaanza kumwambia “Mbona wewe ni mrembo, hadi sasa huna boyfriend”..Mbona una shepu zuri, embu vaa hizi nguo fupi uonekane na wanaume..Embu twende leo disco, tukakutane na vijana wenzetu, tule maisha, ujana maji ya moto..

Akawa anawasikiliza, na huko ndipo akakutana na huyo Shekemu, akamlaghai, kisha akambikiri..Taarifa zikawafikia ndugu zake, wakakasirika sana Simeoni na Lawi, hadi kufikia kitendo cha kwenda kuwaua watu wote wa huo ukoo. Kwasababu waliona tendo alilofanya Dina, ni chukizo kubwa sana kwa jamii yao. Kuuchafua uzao uliobarikiwa, kuvunja maagano ya Mungu.

Nini Bwana anataka mabinti na wanawake wajifunze?

Kabla ya kuanguka katika dhambi, ushawihi huwa unaanza kwanza kwa marafiki wanaokuzunguka.  Angalia ni watu wa namna gani uliozoena nao, au uliounga urafiki nao, au unaokaa nao muda mrefu. Mabinti wengi waliookoka, hawajafundishwa kuvaa vibaya na wanaume wazinzi, bali na mabinti wenzao, hawajafundishwa kwenda disco au kunywa pombe na wanaume, bali mabinti wenzao. Hawajafundishwa kwenda kwa waganga na kaka zao, bali wanawake wenzao, hawajafundishwa kusengenya na jamii, bali ni wanawake wenzao wanaokutana nao masaluni na mabarazani.

Hawa ndio maadui wa kwanza. Dina hakutoka kwenda kumtafuta Shekemu, alitoka kuwatazama mabinti  tu wa kidunia na huko huko wakamuunganishia Shekemu. Laiti angetulia nyumbani akakaa na wale wabinti wenzake wa ukoo mmoja hata kama ni washamba, angekuwa salama.

Wewe kama mwanamke usipende kuunga urafiki na wanawake ambao hawajaokoka, ambao hawana habari na Mambo ya ufalme wa mbinguni, upo chuo, upo shuleni, upo kazini, ni heri ubaki kivyako vyako, kuliko kujiingiza hatarini. Siku zote uangamivu unavyokuja huwa unaanzia mbali sana, hivyo kuwa makini, tafuta watu waliodhamiria kuishi maisha matakatifu, hao ndio wawe marafiki zako wa karibu, washauri wako, uige tabia zao, kataa kampani za kipepo, acha wakuone mshamba, lakini roho yako ipo salama, acha upitwe na fashion, acha upitwe na uzuri lakini jina lako lipo katika kitabu cha uzima.

Majira tunayoishi ni ya kung’ang’ania kwa nguvu wokovu tuliopewa, ni kuwa siriazi kweli kweli, kwasababu maelfu kwa maelfu ya watu wanaangamia, wanashindwa kumaliza mwendo wao salama hapa duniani wanaponzwa na marafiki, Unadhani na sisi tukiwa walegevu, tunadhiria kila kitu tu kinachokuja mbele yetu, tutawezaje kupona. Njia imesonga, mlango ni mwembamba, tunajiingiza kwa nguvu, isitoshe muda tuliobakiwa nao ni mchache. Hivyo hatupaswi kuwapa nafasi watu wakidunia katika maisha yetu.

Tujifunze kwa Dina. Tuwe salama. Kataa, kampani za kipepo!

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

MAFUNDISHO KWA WANAWAKE

FUNGUO WALIZOKUWA NAZO MABINTI WATANO WA SELOFEHADI!

MAZUNGUMZO MABAYA HUHARIBU TABIA NJEMA.

Nondo ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Nifanyeje niwe mwombaji mzuri, wa masafa marefu?

Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima; (Mithali 11:16)

Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?

Rudi nyumbani

Print this post

KAMA MTUMISHI WA MUNGU, TAFUTA MAARIFA KWA BIDII.

Huu ni mfululizo wa Masomo maalumu kwa Watumishi wa Mungu (Wahubiri wa Injili, Wachungaji, Wainjilisti, Waalimu, Manabii na Waimbaji wote).

Hosea 4:6 “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe, usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako, mimi nami nitawasahau watoto wako”.

Tunaona hapa Bwana anaanza  kama kwa kulaumu!.. sasa anamlaumu nani? Si wana wa Israeli bali anawalaumu  MAKUHANI wake! (Yaani watu waliowekwa kwa lengo la kuwafundisha wana wa Israeli njia ya kumcha Bwana)… ambao kwasasa wanafananishwa na (Wachungaji, Wainjilisti, Waalimu, Mitume, Manabii na wahubiri wote)

Watu hawa Bwana anawalaumu kwa kuwa “wameyakataa maarifa” (maana yake hawataki kujishughulisha kutafuta maarifa yatakayowasaidia wao pamoja na wengine), na hivyo kusababisha Israeli yote kukosa maarifa.. kwasababu laiti wakiyapata maarifa hayo ya kiMungu ya kutosha, basi wangeweza kuwafundisha Israeli nzima na hivyo Israeli yote ingeponyeka..

Lakini kinyume chake, Makuhani hawa hawayataki maarifa!, wanaridhika kukaa katika ujinga, hawataki kusoma maandiko,  na hivyo kusababisha Israeli yote kukosa maarifa na kuangamia, jambo ambalo ni DHAMBI KUBWA SANA MBELE ZA MUNGU!, Kwasababu wao ndio chanzo cha Israeli yote kukosa maarifa..

Na tunaona madhara yake ni nini… Bwana AKAWAKATAA wasiendelee kuwa makuhani, na akawakataa na WATOTO WAO pia.

Ni jambo baya sana, Bwana kukukataa kuwa KUHANI.. kwani unakuwa Umenyang’anywa Neema yote iliyokuwa juu yako.. utalazimisha kuendelea na Mungu, lakini yeye atakuwa yupo mbali na wewe kama ilivyokuwa kwa Sauli..

1Samweli 15:23 “Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la Bwana, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme”

Hili ni jambo baya sana na linaloendelea sasa miongoni mwa watumishi.. Ni heri tukataliwe na wanadamu wote, lakini tusikataliwe na Mungu..

Kama mtumishi wa Mungu tafuta maarifa!!!… kwasababu utumishi wako unapimwa!.. Bwana anategemea kuona watu wake wanajaa maarifa ya kumjua yeye pindi wanapokuja katika kanisa unalohudumu, wanapokuja katika maskani unayo hudumu…. hataki kuona watu wake wanaangamizwa kwa kukosa maarifa, ili hali wewe (unayejiita mtumishi wa Mungu) ndiye ambaye ungepaswa uwape hayo maarifa.!

Bwana akiona watu wake wanaangamia kwa kukosa maarifa, usidhani wewe utabaki salama!.. Bwana atakukataa wewe na pia atawakataa watoto wako..

Usifurahie kuona watu walio chini yako, hawaelewi kanuni ya Imani, wanatanga tanga huku na kule kutafuta  maji, au mafuta au kuufananisha ukristo na uganga wa kienyeji…

Chukua jukumu la kujifunza biblia kwa kina ili ujae maarifa yatakayokusaidia wewe na ukawasaidie na watu wako!!!!!…soma, tafiti, chunguza maandiko kila siku, hakiki mambo yote, acha kutafuta umaarufu na sifa zisizokuwa na maaana kutoka kwa watu wako…. hiyo itathaminisha utumishi wako mbele za Mungu.. wape watu Maarifa ya kiMungu, hayo ndiyo yatakayowalinda wasije wakaangamia!… Kumbuka siku zote kuwa Bwana hataki watu wake waangamizwe kwa kuyakosa hayo!.

Kama unaona uvivu kutafuta maarifa na kuwapa watu hayo, acha hiyo kazi ya kuhubiri, sio wito wako!, nenda katafuta kazi nyingine, kafanye biashara na Mungu atakubariki huko!, lakini usiwaongoze watu katika njia ya upotevu, kwa kuwajaza elimu za mambo ya ulimwengu huu na elimu za kichawi badala ya kuwapa elimu na maarifa ya ufalme wa mbinguni.. utajitafutia laana badala ya Baraka!.

Bwana Yesu na atusaidie sana.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TAFUTA KWA BIDII KUWA MTAKATIFU.

NJAA ILIYOPO SASA.

Je! Mungu anaupendeleo kwa wanaume zaidi ya wanawake?

UFANYE WEMA WAKO KATIKA MAARIFA.

Tofauti kati ya Hekima, ufahamu na maarifa, ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya andiko hili  “Sauti yake hamkuisikia wakati wo wote, wala sura yake hamkuiona.(Yohana 5:37)”

Jibu: Tusome,

Yohana 5:37  “Naye Baba aliyenipeleka amenishuhudia. SAUTI YAKE HAMKUISIKIA WAKATI WO WOTE, WALA SURA YAKE HAMKUIONA.

38  Wala neno lake hamnalo likikaa ndani yenu, kwa kuwa ninyi hammwamini yule aliyetumwa na yeye.”

Hapa Bwana Yesu hamaanishi kwa Wayahudi hawajawahi kuisikia sauti ya Mungu, wala kuliona umbile lake!. Hapana bali andiko hilo linamaansha kuwa Mungu alijidhihirisha kwao kimaumbile lakini hawakumwona na vile vile alijidhihirisha kwao kisauti lakini hawakumsikia.

Sawasawa kabisa na alivyosema katika Kitabu cha Isaya

Isaya 50:2 “Basi, NILIPOKUJA, MBONA HAPAKUWA NA MTU? NILIPOITA, MBONA HAPAKUWA NA MTU ALIYENIJIBU? Je! Mkono wangu ni mfupi, hata nisiweze kukomboa? Au je! Mimi sina nguvu za kuponya? Tazama, kwa kukemea kwangu naikausha bahari, mito ya maji naifanya kuwa jangwa; samaki wao wanuka kwa sababu hapana maji, nao wafa kwa kiu”.

Umeona hapo?.. kumbe kuna wakati Bwana anatujia kimaumbile lakini hatumwoni?… Sasa utauliza ni wakati gani anatujia hatumwoni, na ni wakati gani anapaza sauti yake hatuisikii??

Kupitia watumishi wake wa kweli, wanapotujia kama wageni na kutuletea habari njema, ujio wao unafananishwa kabisa na ujio wa Kristo kwetu kimaumbile, haihitaji yeye Mungu atutokee ndio ihesabike kuwa tumeliona umbile lake, bali watumishi wake tu kutujia tayari hao ni umbile lake…… utasema hilo tunalithibitisha vipi kimaandiko??

Mathayo 25:41 “Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;

42  kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe;

43  nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama.

44 Ndipo hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie?

45  Naye atawajibu, akisema, Amin, nawaambia, KADIRI MSIVYOMTENDEA MMOJAWAPO WA HAO WALIO WADOGO, HAMKUNITENDEA MIMI.

46  Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele”.

Umeona?.. Vile vile tusiposikiliza sauti za watumishi wake, ni sawa na hatujaisikiliza sauti yake!.. Ndio maana hapo katika Isaya 52:2 anasema “nilipoita mbona hamkuitika?”.. maana yake ni kwamba wenyewe walidhani sauti wanayoisikia ni ya mwanadamu kumbe ni ya Mungu.. vile vile walidhani umbile walionalo mbele yao ni la mwanadamu kumbe ndio umbile la Mungu, kwahiyo wakayadharau maneno ya Mungu aliyoyazungumza kupitia watumishi wake..

Na hapa Kristo anarudia tena maneno hayo hayo ya Isaya na kusema… “Naye Baba aliyenipeleka amenishuhudia. SAUTI YAKE HAMKUISIKIA WAKATI WO WOTE, WALA SURA YAKE HAMKUIONA.”.. Maana yake Mungu alizungumza nao mara nyingi, na kuonekana kwao mara nyingi lakini hawakuwahi kumsikia wala kumwelewa wala kumfahamu hata mara moja, kwasababu mioyo yao ilikuwa mbali naye.

Na sisi tunajifunza kuwa sauti ya Mungu haiji kwetu kama sisi tunavyotaka au tunavyopanga, wala Mungu hatujii kimaumbile kama sisi tunavyotaka!..

Ni wengi sana wanafunga na kukesha ili kwamba Mungu awatokee, na waisikie sauti ya Mungu kama vile redio,..kama unafanya hivyo nataka nikuambie kuwa “unapoteza muda wako”.. kwasababu hiyo sio Njia ya MUNGU kuzungumza na sisi, hizo ni njia zetu sisi wanadamu za kuwasiliana..Mungu yeye anazo njia zake, ni lazima tuzijue hizo, tusilazimishe atumie zetu… “atafanya hivyo akipenda”, lakini si kanuni yake!.

Ukitaka kuisikia sauti ya Mungu vizuri, soma Neno na kulitafakari, Sikiliza mahubiri ya watumishi wa Mungu wa kweli, na ishi maisha matakatifu. Hapo utamwona Mungu sana katika maisha yako na utamsikia sana.

Bwana atusaidie na kutubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

WAKAKAA KWAKE SIKU ILE. NAYO ILIKUWA YAPATA SAA KUMI.

Je Mungu ana njia ngapi za kuzungumza?

Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana?

FAHAMU JINSI MUNGU NA SHETANI WANAVYOZUNGUMZA NA WATU.

Rudi nyumbani

Print this post

Pande zote twadhikika, bali hatusongwi;(2Wakorintho 4:8)

Unaweza kushushwa chini, lakini simama usivunjike moyo.

2Wakorintho 4:8  “Pande zote twadhikika, bali hatusongwi; twaona shaka, bali hatukati tamaa; 9  twaudhiwa, bali hatuachwi; twatupwa chini, bali hatuangamizwi”

Kwa kuwa bado tupo duniani, dhiki, mateso, manyanyaso hayaepukiki katika baadhi ya vipindi, Kiongozi wetu Yesu alituweka wazi, kwamba “duniani mnayo dhiki, lakini jipeni moyo mimi nimeushinda ulimwengu”(Yohana 16:33)

Utaudhiwa na mume/mke/baba/mtoto, kwasababu ya imani, utapigwa bila sababu, utatishiwa kufukuzwa kazi, utakuwa na mashaka pande zote, mwingine hujui kesho utaamkaje, ule nini, magonjwa hayana mwisho..Lakini katika yote, bado neema ya Mungu itatushika na kutusaidia, hatutasongwa kiasi hicho mpaka kuicha imani, hatutakata tamaa, hata turudi nyuma, Bwana atakuwa upande wetu.

Mambo hayo ni ya kitambo tu, hata kama tutauawa, bado tunao uzima wa milele, hata kama tutapoteza kila kitu bado mwenye vitu vyote yupo ndani yetu. Tutadhikika pande zote, tutasongwa kila mahali lakini hatutakata tamaa. Tukumbuke tu,  Kila pito linasababu yake, lakini katika yote, tujue Bwana anatuwazia mawazo mema, tukishakwisha kukamilishwa tutatoka kama dhahabu.

Yakobo 1:2  “Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali; 3  mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi. 4  Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno”.

Bado maandiko yanasema..

1Petro 1:6  “Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali;

7  ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo”.

Bwana awe nawe.

Maombi yangu:

“Baba mwema, nakushukuru kwa neema ya wokovu uliyonipa, Najua kama sio wewe nisingefika hata hapa nilipo, nakuomba Mungu wangu unione katika dhiki zangu, uyaone machozi yangu, uniondoe katika mateso yangu. Lakini zaidi unipe nguvu ya kuweza kukabiliana na dhiki zote za ulimwenguni, nisirudi nyuma wala kukata tamaa. Nikutumikie wewe katika mazingira yote. Upendo wako usipunguke ndani yangu. Ninaomba nikiamini katika jina la Yesu Kristo. Amen”.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

MISTARI YA BIBLIA YA FARAJA.

UYATIE MACHOZI YANGU KATIKA CHUPA YAKO EE! BWANA.

Furaha ni nini?

Unyenyekevu ni nini?

JE! UTATOA HESABU YA NINI KATIKA SIKU ILE?

Nini maana ya kumpenda Bwana kwa moyo,roho, akili na nguvu zetu zote?

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

Ni kosa gani lililowafanya wana wa israeli wawe watumwa miaka 400 Misri?.

Swali: Kwanini Mungu aliwapeleka wana wa Israeli Misri kwa miaka 400, Ni kosa gani kubwa walilolifanya mpaka Mungu kuwauza kwa Farao miaka yote hiyo?

Jibu: Hakuna kosa lolote walilolifanya mpaka kufikia hatua hiyo ya kupelekwa Misri katika nyumba ya utumwa. Bali Mungu aliruhusu iwe hivyo, kwa makusudi maalumu. Ni kama tu Yusufu alivyoenda kuuzwa kwa Misri kwa Potifa, maandiko hayaonyeshi kuwa Yusufu alifanya kosa lolote lililompelekea kwenda kuuzwa kama mtumwa kwa Potifa, lakini maandiko yanaonyesha kuwa Mungu alimpeleka Misri kwa lengo la kuwaokoa watu wengi siku za mbeleni, tunalisoma hilo katika Mwanzo 45:4-8

Mwanzo 45:4 “Yusufu akawaambia ndugu zake, Karibuni kwangu; basi, wakakaribia. Akasema, Mimi ni Yusufu, ndugu yenu, ambaye mliniuza kwenda Misri. 

5 Basi sasa, msihuzunike, wala msiudhike nafsi zenu, kwa kuniuza huku; MAANA MUNGU ALINIPELEKA MBELE YENU KUHIFADHI MAISHA YA WATU.

 6 MAANA MIAKA HII MIWILI NJAA IMEKUWA KATIKA NCHI, NA IKO TENA MIAKA MITANO ISIYO NA KULIMA WALA KUVUNA. 

7 MUNGU ALINIPELEKA MBELE YENU KUWAHIFADHIA MASAZO KATIKA NCHI, NA KUWAOKOA NINYI KWA WOKOVU MKUU

8 Basi si ninyi mlionipeleka huku, ila Mungu; naye ameniweka kama baba kwa Farao, na bwana katika nyumba yake yote, na mtawala katika nchi yote ya Misri”.

Hali kadhalika Mungu aliwapeleka wana wa Israeli Misri na kuwafanya kuwa watumwa, kwa malengo makuu mawili.. ambayo yanafanana na yale ya Yusufu.

1.MUNGU KUTANGAZA UKUU WAKE.

Kupitia wokovu wa Israeli kutoka Misri kwa mapigo yale 10 aliyompiga nayo Farao, na kwa kupitia ishara za ajabu alizozofanya jangwani kama kushusha Mana, kuleta Kware, kudhihirisha Nguzo ya Wingu na Moto n.k, ulimwengu umeweza kumjua Mungu wa Ibrahimu kuwa ni Mungu mkuu na wa haki na mwenye nguvu nyingi na maajabu mengi.

Kwahiyo ijapokuwa Israeli waliteswa Misri lakini maisha yao baadaye yalikuja kuwa mahubiri makubwa sana kwa ulimwengu kumjua Mungu wa kweli, pengine wasingepitia hiyo njia ya mateso tusingemjua Mungu kwa kiwango hicho.

2. KUTANGAZA NJIA YA WOKOVU

Lengo la pili la wana wa Israeli kupitia yale maisha ni kutangaza njia ya Wokovu. Maisha yao kuanzia Misri mpaka Kaanani, ni ufunuo kamili wa maisha ya Wokovu kutoka Dhambini(Misri), kueleka mbinguni (Kaanani) mji wa raha.

Tunapomwamini Bwana Yesu na kutubu dhambi zetu, katika roho ni kama tumetoka Misri..na hivyo Kristo anatuweka huru mbali na vifungo vyote vya dhambi, kwasababu maandiko yanasema “atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi (Yohana 8:34)”.

Hii inatufundisha nini?.. Si kila mateso tunayoyapitia yanatokana na makosa tuliyoyafanya?.. Yusufu hakuna kosa alilolifanya mpaka kufikia kuuzwa Misri kwa Potifa na hata kufungwa gerezani, vile vile wana wa Israeli hakuna kosa walilolifanya mpaka kufikia kuwa watumwa kwa muda ule, bali Mungu aliruhusu hayo yatokee ili mwisho wake aonyeshe utukufu wake!..

Kwahiyo hatutakiwi kukata tamaa tunapopitia shida, maadamu tuna uhakika tupo sawa na Mungu (yaani tunaishi maisha yanayompendeza yeye), vile vile tunapopitia magonjwa ya muda mrefu hatupaswi kukata tamaa wala kulaumu, bali tunapaswa kushukuru na kuendelea kuomba na kuishi maisha yanayompendeza, kwasababu Mungu anataka kufanya maisha yetu kuwa ushuhuda..

Hata Kristo maisha yake yalikuwa ni ya ushuhuda, alikuwa kama namna ya mtumwa (Wafilipi 2:7-8), lakini alijua mwisho wake utakavyokuja kuwa, na sisi hatuna budi kuwa watu wa namna hiyo hiyo, kwasababu mwisho wetu utakuwa mzuri hata kama mwanzo wetu umekuwa mbaya na wa kukatisha tamaa, maadamu tupo katika Neno lake na amri zake, basi hatuna haja ya kuwa na hofu, ni suala la muda tu.

Maran atha!.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWA MIOYO YAO WAKAREJEA MISRI.

MAJARIBU 10 WANA WA ISRAELI WALIYOMJARIBU MUNGU.

JIHADHARI NA MKUTANO WA WATU WALIOCHANGANYIKANA.

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

Nini tofauti ya Mtumwa, Mjakazi na kijakazi?

Rudi nyumbani

Print this post

UNAFAHAMU KUWA YESU HUWA ANAJITENGA NA BAADHI YA WATU?

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo, utukufu na heshima vina yeye milele na milele amina.

Zipo tabia kadhaa za Yesu ambazo watu wengi huwa hatuzitambui. Kwamfano utakumbuka wakati ule, anakwenda Yerusalemu kwenye sikukuu, biblia inasema alipita mahali penye birika Fulani iliyojulikana kama Bethzatha, Birika hii kuna kipindi ilitoa uponyaji, hivyo, watu wengi maelfu kwa maelfu walikuwa wakikusanyika, kungojea bahati zao, ambayo ilitokea kwa nadra sana pengine mara moja kwa mwaka.

Lakini hapa tunamwona Bwana Yesu, akiingia katikati ya mkusanyiko huo, na kumponya Yule mtu aliyekuwa amepooza, Cha kushangaza ni kwamba Yesu hakuendelea kubaki mule mule kuwaponya watu wengine kama ilivyo desturi yake, bali aliondoka mara moja, kwa haraka ambayo hata aliyeponywa hakuweza kumkariri.

Hata baadaye makuhani walipomuuliza, ni nani kakupa amri hiyo ya kujitwika godoro lako uende, Yule aliyepooza hakuweza kumtambua,.

Lakini ni nini kilichompelekea Yesu aondoke pale?

Tusome kidogo;

Yohana 5:12  “Basi wakamwuliza, Yule aliyekuambia, Jitwike, uende, ni nani?

13  Lakini yule mtu aliyeponywa hakumjua ni nani; MAANA YESU ALIKUWA AMEJITENGA, KWA SABABU PALIKUWA NA WATU WENGI MAHALI PALE.

14  Baada ya hayo Yesu akamkuta ndani ya HEKALU, akamwambia, Angalia, umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi.

15  Yule mtu akaenda zake, akawapasha habari Wayahudi ya kwamba ni Yesu aliyemfanya kuwa mzima.

Sababu ya kujitenga maandiko yanasema ni kwamba palikuwa na watu wengi.. Watu wengi ambao wanatafuta miujiza na uponyaji wa miili yao, na sio roho zao. Na ndio maana Yesu hakuweza kustahimili kuendelea kuwepo pale muda mrefu, akaondoa mara..

Mpaka Yule mtu alipopata akili, akaona pale sio sehemu yake, akaenda zake HEKALUNI kutulia uweponi mwa Bwana, kukaa kusali na kujifunza sheria za Mungu, Ndipo Yesu akajidhihirisha kwake alipokuwa kule hekaluni,..akamwambia “usitende dhambi tena!”, “usitende dhambi tena!”, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi”. Akampa siri ya matatizo yake, na suluhisho la kudumu.

Lakini kama mtu Yule asingekwenda hekaluni, badala yake akaendelea kumtafuta  Yesu kila siku pale birikani, kamwe asingekaa amwone, na ugonjwa wake ungemrudia muda si mrefu, kwasababu, angeenda kurudia dhambi yake ile ile aliyoitenda.

Ni nini Bwana anataka tufahamu.

Hii ni picha kamili ya kinachoendelea sasa katika ulimwengu wa wakristo. Kinachowakimbiza kwa Mungu ni ishara na miujiza, na uponyaji, Hivyo wanayaacha makanisa yanayowafundisha Njia za wokovu, na kujitenga na dhambi, wanakimbilia kwenye vituo vya maombi na maombezi, huko ndipo walipojazana, wakisikia kuna mafuta ya upako, wanamiminika mpaka wanakanyagana, Lakini ukweli ni kwamba sio wote wanaopokea uponyaji, bali ni wachache sana..na tena hao wachache ni Yesu ndiye anayewafuata huko kwa huruma zake, na kuwadhihirishia uponyaji wake.. Lakini huko hayupo..Utasubiri sana, na kulia sana, na kungoja sana.

Huwezi kuliacha Hekalu lake, ukakimbilia mikusanyiko ya miujiza na uponyaji, ambayo hukemewi dhambi, hufundishwi kusali, hufundishwi habari za kwenda mbinguni, hufundishwi utakatifu, ukadhani utamwona Yesu..Ataendelea tu kujitenga nawe kwasababu yeye hakai katika mikusanyiko ya watu wa namna hiyo.

Wanaoponywa wanakuwa wanarudiwa matatizo yaleyale, baada ya muda, kwasababu hawafundishwi chanzo cha matatizo yao, kwamba ni dhambi, Bali wanamgeuza Mungu mganga wa kienyeji, anayetoa tu dawa, hajali kujua machafu yako.

Embu leo tubu na ugeuke, ondoka huko, Usikae mahali ambapo Yesu hayupo, hata kama kuna utiriri wa watu, Yesu hapokei umati wa watu,kama tulivyoona hapo anapokea watu waliotayari kumwabudu katika roho na kweli haijalishi watakuwa wawili au watatu.

Epuka upepo wa watu, asilimia kubwa Yesu hayupo huko.

Tubu dhambi zako, maanisha kwa moyo wako wote, kumfuata Yesu. Kumbuka hizi ni siku za mwisho,  majira yale ya  makristo na manabii wa uongo ndio haya Yesu aliyoyatabiri, Kaa katika Kristo Yesu, hakikisha umejitwika msalaba wako na kumfuata Yeye. Parapanda inakaribia kulia, Hukumu ipo karibu, umejiwekaje na Kristo wako?.

Bwana akubariki

Amen.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

KUNA WAKATI YESU ATAPITA NA WATU HAWATAJUA.

JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI, TUNAPOMWOMBA BWANA ATUGUSE MARA YA PILI.

USIJARIBU KUMGEUZA MUNGU MGANGA WA KIENYEJI,UTAKUFA.

Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)

Usimwache mwanamke mchawi kuishi! Biblia ilimaanisha nini?

Afadhali mtu akutwe na dubu aliyenyang’anywa watoto wake.

Rudi nyumbani

Print this post

WANNE WALIO WAONGO.

Biblia imetuonya imetutahadharisha vitu vitatu vilivyo na udanganyifu kuliko vitu vyote.

1.MOYO

Moyo wa mtu ndio kitu kilicho kidanganyifu kuliko vyote..

Yeremia 17:9 “Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?”

Hakukuwa na shetani mwingine mbinguni aliyemdanganya shetani, bali kilichomdanganya shetani ni moyo wake mwenyewe… Moyo wake ulimtuma kuamini kuwa anaweza kuwa kama Mungu. Na hivyo akaufuata moyo wake na mwisho akaangukia upotevuni.

Na mioyo yetu sisi wanadamu ni midanganyifu sana, na mara nyingi inatuongoza pabaya…Mithali 16:2 “Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe…” Na maandiko yanatufundisha kulinda mioyo yetu kuliko vyote tulindavyo, kwasababu huko ndiko zinakotoka chemchemi za uzima (Mithali 4:23).

Na tunailinda kwa kuangalia yale tunayoyasikia au tunayojifunza, na biblia ndio kitabu pekee cha kutusaidia kupima mambo yote.

2. DHAMBI.

Dhambi ni adui wa pili wa kumwongopa kuliko “shetani”. Na dhambi siku zote inadanganya, (inavutia kwa nje lakini mwisho wake ni Mauti, Warumi 6:23). Ulevi unaonekana kama unavutia lakini mwisho wake ni Mauti, Anasa zinaonekana kama zinavutia, lakini mwisho wake ni Mauti, Vivyo hivyo na Zinaa, na usengenyaji, na wizi, na rushwa n.k Vyote hivyo vinavutia kwa nje lakini ndani yake ni Mauti.

Waebrania 3:13 “Lakini mwonyane kila siku, maadamu iitwapo leo; ili mmoja wenu asifanywe mgumu kwa UDANGANYIFU WA DHAMBI”.

3. SHETANI.

Maandiko yanasema wazi kuwa shetani ni baba wa Uongo.

Shetani atakuambia kuabudu sanamu si dhambi, kunywa pombe si dhambi, kuupenda ulimwengu si dhambi, kujiburudisha kwa anasa si dhambi n.k  Na kumbe anasema Uongo, kwasababu yeye ni baba wa huo, ndivyo alivyomdanganya Hawa na ndivyo anavyoendelea kudanganya watu mpaka leo.

Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo”

4. MALI

Maandiko pia yanasema kuwa Mali zinadanganya!.. Mali zinasema ukizipata utaheshimika, ukizipata utapendwa, ukizipata utaishi vizuri.. jambo ambalo si kweli, Kristo pekee ndiye ukimpata mambo yote, yatakuwa sawa hata pasipo hizo mali… Kama alisema “mtu hataishi kwa mkate tu, bali Neno la Mungu”…si zaidi Mali???.

Lakini Mali zenyewe zinatuhubiria kinyume chake kuwa pasipo hizo, maisha yetu hayawezi kwenda au yatakuwa ya shida, maisha yetu yatakuwa ya tabu na mateso…

kwahiyo kama hatutaongeza umakini katika kumjua Mungu na uweza wake tutadanganyika na udanganyifu huo ambao Mali zinauhubiri.. tutajikuta tunatumia muda mwingi kuzisaka na kutumia muda mchache kumtafuta Mungu.. na hivyo kupotea..

Mathayo 13:22  “Naye aliyepandwa penye miiba, huyo ndiye alisikiaye lile neno; na shughuli za dunia, na UDANGANYIFU WA MALI hulisonga lile neno; likawa halizai”.

Mali zisikudanganye na kukupotezea muda wako mwingi, Mali zisikuambie kuwa usipoenda kuzisaka siku ya jumapili utakufa njaa!!, mali zisikudanganye kuwa usipotumia usipotumia muda mwingi kuzisaka basi zitakukimbia!!..  Jihadhari na udanganyifu huo.

Bwana atubariki na kutusaidia.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MBINGUNI YUPO NANI SASA?

Kwanini Paulo aungane na wale watu wanne wenye nadhiri?

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

KWA WALE WALIO NJE “YOTE” HUFANYWA KWA MIFANO.

Sadaka ya Moyo ipoje? (Walawi 22:21).

Rudi nyumbani

Print this post