Fahamu Maana ya;
Mithali 18:18 Kura hukomesha mashindano; Hukata maneno ya wakuu.
Kupiga kura ni Moja ya njia ambayo ilitumika kuleta suluhisho lenye utata, na wakati mwingine kuchagua viongozi/wamiliki. Pitia hapa ujue zaidi kuhusu kura zilivyopigwa zamani za biblia…>> Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo;
Na Mungu wakati mwingine aliingilia kati na kuleta majibu yake sahihi kwa kupitia njia hiyo. Kwamfano wakati ule Yona anamkimbia Mungu, Hali ilipochafuka kule baharini, utaona wale watu walipiga kura, ili kujua sababu ya mambo yale ni nani na Ile kura ikamwangukia Yona.
Mitume wa Bwana baada ya kuomba, kuhusu mrithi wa nafasi ya Yuda wakapiga kura katika ya wale wanafunzi wawili, nayo ikamwangukia Mathiya, na likawa kweli ni chaguo la Mungu.(Matendo 1:15-19),
Hata wakati wa nchi ya Israeli kugawanywa . Kura zilitumika kuamua nani akae wapi, na nani arithi wapi (Hesabu 26:55).
Hivyo kupiga kura ilikuwa ni mojawapo ya njia kuleta jibu lisilokuwa na upendeleo. Au lililoegemea upande Fulani mmoja. Na kwa kufanya hivyo malalamiko mengii yalikomeshwa kwasababu maamuzi hayakuamuliwa na upande wowote ule.
Ndio maana ya hili andiko
Mithali 18:18
[18]Kura hukomesha mashindano; Hukata maneno ya wakuu.
Hata kipindi Cha sasa njia ambayo hutumiwa kuchagua viongozi wengi ulimwenguni Huwa ni ya kura. Isipokuwa hii siyo ya kurusha SHILINGI, au kete angani inayomwangukia mmojawapo ndio anakuwa kiongozi..hapana Bali ni kuruhusu Kila mmoja kutia maoni yake..Kisha zinahesabiwa na yule mwenye nyingi hupewa. Na hivyo hakuna malalamiko.
Tofauti na Ile mtu atawadhwe tu Moja Kwa moja kuwa kiongozi, Hiyo huleta ukakasi mwingi.
Hivyo ni kutufundisha kua Bwana anaouwezo wa kuingilia kura zipigwazo na kuleta majibu yake sahihi..hususani pale anaposhirikwa Kwa maombi, na kama hakusema Kwa njia nyingine ya Moja Kwa moja.
Bwana akubariki
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?
Mzushi ni nani kibiblia? (Tito 3:10).
Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?
Biblia inakataza kuapa kabisa, lakini kwanini watu wanaapa mahakamani na katika vifungo vya ndoa?
Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake
Nini maana ya Mithali 27:21 inaposema “mtu hujaribiwa kwa sifa zake?”
Swali: Biblia inatufundisha katika Wagalatia 5:23 kuwa “tuwe wapole kiasi”, sasa napenda kujua mtu utakuwaje mpole kiasi.
Jibu: Tusome,
Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
23 UPOLE, KIASI; juu ya mambo kama hayo hakuna sharia”.
Hapa biblia haisemi kuwa tunda la Roho Mtakitifu kuwa ni “Upole kiasi” kana kwamba “upole unapaswa uwe na kiasi”…. La! Bali inasema tunda la Roho ni “Upole”, halafu “Kiasi”… hayo ni maneno mawili yaliyotengenishwa na alama ya mkato.
Maana yake “Upole” ni kitu kingine na “Kiasi” ni kitu kingine. Ikiwa na maana kuwa Tunda la Roho “Upole ulio wote” na sio upole kiasi.
Biblia inatufundisha tuwe watu wapole kama Hua (Njiwa).
Mathayo 10:16 “Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwa-mwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua”
Hua ni ndege mpole sana ndio maana Roho Mtakatifu alitumia umbile la Hua kushuka juu ya Bwana Yesu wakati ule alipobatizwa (Mathayo 3:16)... Na maandiko yanazidi kutufundisha kuwa Bwana Yesu ni Mpole..
Mathayo 21:5 “Mwambieni binti Sayuni Tazama, mfalme wako anakuja kwako, MPOLE, naye amepanda punda, Na mwana-punda, mtoto wa punda”.
Soma pia, Mathayo 11:29, utaona sifa hiyo ya Bwana ya upole ikitajwa..
Na sisi pia ni lazima tuwe na sifa hiyo ya “Upole” kama ishara mojawapo ya kuwa na Roho Mtakatifu ndani yetu… shetani kaligeuze Neno hili la Upole na kuweka “Upole kiasi” ili kuchochea ubaya ndani ya watu.. Kwamba ni vizuri kuwa wapole lakini tusiwe wapole sana, tuwe wapole tu kiasi!. Huo ni uongo wa adui!.
Na kumbuka kuna tofauti ya “upole” na “unyonge”. Biblia haitufundishi kuwa wanyonge, bali kuwa wapole, Mtu mpole ni yule ambaye ana uwezo wote wa kutumia ukali lakini hautumii!, kama alivyokuwa Bwana Yesu… Lakini mnyonge ni yule anayekuwa analazimika kuwa hivyo mpole kutokana tu na mazingira..na akitoka katika hayo mazingira basi tabia yake ya ubaya na ukali usio na maana na vurugu inajidhihirisha.
Bwana atusaidie .
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
BWANA UNIJULISHE MWISHO WANGU.
Je Paulo na Petro walishindania nini? (Wagalatia 2:11).
Jibu: Tusome kuanzia mstari wa 5..
Zaburi 91:5 “Hutaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana,
6 Wala tauni ipitayo gizani, Wala uele uharibuo adhuhuri”.
“Uele” ni janga linaloleta mauti linaloweza kumpata mtu.. ajali ya gari ni mfano wa Uele, Ajali ya kuzama kwenye maji ni mfano wa “Uele”, janga la kuungua moto mpaka kufa ni mfano wa “Uele”.
Maandiko yanatufundisha kuwa wote wamtumainio Bwana, na kumkimbilia na kumfanya kuwa ngome na msaada, hawatakuwa na hofu na majanga hayo, kwani Mungu ni ngome ya wote wanaomcha, naye ndiye awaokoaye na majanga.
Zaburi 121:4 “Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi, Yeye aliye mlinzi wa Israeli.
5 BWANA ndiye mlinzi wako; BWANA ni uvuli mkono wako wa kuume.
6 Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku.
7 BWANA atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako.
8 BWANA atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele”.
Je una hofu na UELE?..Mpokee Yesu kwa kutubu dhambi na kujazwa Roho Mtakatifu, naye atakupa furaha nawe utaishi maisha ya raha na ya utulivu.
Zaburi 127:2 “……Yeye humpa mpenzi wake usingizi”
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
KUOTA AJALI, KUNAMAANISHA NINI?
Je! Mungu anasababisha ajali au Majanga?
MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.
Kaniki ni nini katika biblia? (Yeremia 8:21).
Fahamu Maana ya Mithali 19:15 “Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; Na nafsi yake mvivu itaona njaa”.
Mara nyingi Sulemani kwa hekima ya Roho aliongozwa kuona uhusiano uliopo kati ya uvivu na umaskini. Kama tu kinyume chake, sehemu nyingine alivyoweka uhusiano kati ya bidii na utajiri(Mithali 10:4). Vivyo hivyo uvivu na umaskini havipishani.
Na kama anavyosema hapo, uvivu humpeleka mtu katika usingizi, lakini sio usingizi tu bali ule mzito, Kwasababu gani? Ni kwasababu mwili haupo katika hali ya kujishughulisha, na hivyo utalala tu, na Bado utaendelea kulala siku baada ya siku.. Na matokeo yake kutokuzalisha chochote kinachoonekana, hatimaye, umaskini unaingia.
Hivyo mstari huo unalenga Nyanja mbili. Ya kwanza ni ule uvivu wa mwilini, na ya pili ni ule uvivu wa rohoni.
Mungu katuumbia kufanya kazi, watu wote (ikiwemo watakatifu). Maana yake ni kuwa ikiwa huna huduma yoyote ya madhabahuni Bwana amekuitia, ambayo inakufanya utumike muda wote hapo. Ni sharti ufanye kazi. Mtume Paulo alilionya kanisa juu ya watu ambao hawafanyi kazi kwamba ni sharti wajishughulishe ili wapate na kitu cha kuwagawia na wengine (2Wathesalonike 3:10)
Lakini pia Uvuvi wa rohoni. Mtakatifu anapokuwa mvivu, kusoma Neno, yaani muda wa Neno anakwenda kutazama filamu, anakwenda kijiweni kucheza drafti,.Anakuwa mvivu kuomba, Unapofika huo muda tu anaona usingizi ni bora kuliko kuomba,.Au Mtakatifu hataki kushuhudia habari za Kristo kwa wengine, anasema jua kali. Sasa mtu huyo anajiandaa kuwa maskini kiroho. Yaani atakuwa katika wokovu usiokuwa na matunda, ukuaji wake wa kiroho utakuwa hafifu, Neema ya Mungu haitatenda kazi kwa wingi juu yake, na hivyo atakosa mema mengi ya Mungu katika safari yake wa wokovu hapa duniani.
Uvuvi wowote, una hasara, kwahiyo tuuweke katika orodha ya maadui zetu wa imani.
Bwana atusaidie.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Kwanini kila nikitaka kusali naingiwa na uvivu?
Amwimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.
WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.
Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni ipi?
SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!
SWALI: Nini maana ya Mithali 24:11 Uwaokoe wanaochukuliwa ili wauawe; Nao walio tayari kuchinjwa uwaopoe.
JIBU: Mstari huu una maana mbili,
Mana ya kwanza ni uhai kama ‘uhai’ alionao mwanadamu yoyote,
Maana yake ni kuwa uonapo, mtu asiyekuwa na hatia, amepangiwa njama za kuuliwa, au ndio anakaribia kufa, na wewe unaowezo wa kumsaidia huna budi kufanya hivyo wala usijifanye kama hiyo sio biashara yako.
Ni mfano wa Yule mtu aliyevamiwa na wanyang’anyi ambaye Bwana Yesu alimtolea mfano, akasema mlawi alimpomwona akapita kando, kuhani naye alipomwona akapita kando, lakini Yule msamaria akamuhurumia, akamtibu, akaokoa uhai wake. Na Yesu akasema huo ndio Upendo.(Luka 10:25-37)
Ni sawa na wakati ule Paulo amepangiwa njama na wayahudi wamvizie auawe, lakini mjomba wake alipogundua alikwenda kumjuza akida wa kikosi (Matendo 23:12-22). Huyo amemwopoa aliyekaribu na kuchinjwa.
Ni sawa na Mordekai alichofanya kwa Mfalme, Ahusuero, wale watu walipopanga njama ya kumuua akaenda kuwasemelea (Esta 6:1-12),. Ni sawa na Yonathani, alivyomtunza Daudi dhidi ya upanga wa baba yake Sauli ili asiuliwe. Hivyo hawa wote, walilitambua andiko hili, na wala hawakuogopa kutoa siri, za wale waliokusudia mabaya juu ya maisha ya wengine.
Hata leo, vifo vingi vya kikatili, vingeweza kuzuilika kwa sehemu kubwa, endapo baadhi ya wanaojua matukio hayo wangetoa taarifa mapema. Kwamfano utaona mtu anawekewa sumu kwenye chakula, wewe unayejua, ni wajibu wako kutoboa siri hiyo, ili uutunze uhai wa mtu. Utaona mwizi anapigwa, huna budi kuripoti polisi mapema maadamu jambo hilo lipo ndani ya uwezo wako, ili askari waje kumkamata wampe wao adhabu stahiki, lakini ukipita ukasema hainihusu, atachomwa moto. Lakini kumbuka uhai unathamani, hata wa mtu aliye mbaya, unathamani nyingi.
Lakini ukisema hainuhusu, Utakuwa unajipunguzia pia rehema nyingi kwa Mungu, ndio maana mstari unaofuata unasema;
Mithali 24:11 “Uwaokoe wanaochukuliwa ili wauawe; Nao walio tayari kuchinjwa uwaopoe. 12 Ukisema, Sisi hatukujua hayo; Je! Yeye aipimaye mioyo siye afahamuye? Naye ailindaye nafsi yako siye ajuaye? Je! Hatamlipa kila mtu sawasawa na kazi yake?”
Hivyo penda uhai, pia tunza uhai wa watu, popote pale uonapo unahatarishwa. Usiwe mzito kusaidia.
Lakini maana ya pili ya mstari huu ni ule Uhai wa rohoni.
Wapo watu ambao ibilisi, anakaribia kuwameza, na ukiwaacha ndani ya kipindi kifupi hakika wataangamia kabisa kiroho. Wengine wanakaribia kufa kwasababu ya huzuni mioyoni mwao, kukata tamaa, kwasababu ya dhiki na magonjwa, wengine wanakaribia kuzama katika ushirikina, wengine kwenye imani potofu ambazo zinakwenda kuwaua roho zao n.k. Hivyo makundi kama haya, unapoyaona, mwelekeo wao wewe kama mkristo uliyesimama huna budi kuwasaidia ili waokoke, wasipotelee katika mauti ya roho zao, na kwenye minaso ya adui mfano wa Yuda. Wala usisime hiyo sio shughuli yangu.
Yuda 1:22 “Wahurumieni wengine walio na shaka, 23 na wengine waokoeni kwa kuwanyakua katika moto; na wengine wahurumieni kwa hofu, mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili.
Hivyo tutunze Uhai, wa mwili na Roho za watu wa Mungu, naye Bwana atatunza na wetu.
Bwana akubariki
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?
“Kinga kilichotolewa motoni “Kinafunua nini kibiblia?
Biblia inamaanisha nini inaposema “Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake”?
Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?
Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?
Zaburi 34:15 Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake hukielekea kilio chao. 16 Uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya, Aliondoe kumbukumbu lao duniani.
JIBU: Andiko hili lilinukuliwa tena na mtume Petro katika 1Petro 3:12-13 linasema;
“12 Kwa kuwa macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake husikiliza maombi yao; Bali uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya. 13 Naye ni nani atakayewadhuru, mkiwa wenye juhudi katika mema?
Kama tunavyojua Macho kazi yake ni kutazama, lakini uso, ni kueleza taswira ya mtu/ kitu fulani.
Na kimsingi macho huona vyote, vilivyo vyema na vilivyo vibaya. Isipokuwa jicho lolote hupendelea zaidi kutazama vilivyo vyema zaidi ya vile vibaya. Ndivyo ilivyo kwa Mungu wetu pia, anaona yote, maandiko yanasema hivyo katika;
Mithali 15:3 “Macho ya Bwana yako kila mahali; Yakimchunguza mbaya na mwema”.
lakini zaidi anaelekeza macho yake zaidi kwa walio wema ili awape mema.
Na ndio maana ya hiyo sehemu ya kwanza ya andiko hilo inayosema ‘Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake hukielekea kilio chao’ Lakini haimaanishi kuwa macho yake pia hayawaoni watenda mabaya.
Vivyo hivyo katika sehemu ya pili inayoeleza juu ya Uso wa Bwana. Kama tulivyoona Uso kazi yake ni kueleza taswira ya mtu. Kwa mfano mtu akifurahi, au akiwa na huzuni au akiwa na hasira ni rahisi kumtambua kwa kuutazama uso wake. Na Vivyo hivyo, kwa Mungu wetu ukiitambua tabia yake, basi ni sawa na umeuona uso wake.
Sasa uso wake pia upo katika pande mbili; 1) Wa Rehema, 2) na wa Hasira (Nahumu 1:2-3)
Maana yake ni kuwa ukimtafuta Bwana, na kumpenda, utaona uso wake mwema, utaona upendo wake, utaona fadhili zake, utaona ukarimu wake, huruma yake, na rehema zake sikuzote. Na ndio maana maandiko yanatuasa tupende kuutafuta Uso wa Bwana. Ili tuujue uzuri wake.
Zaburi 105:4 ‘Mtakeni Bwana na nguvu zake, Utafuteni uso wake sikuzote’.
Zaburi 143:7 “Ee Bwana, unijibu hima, roho yangu imelegea; Usinifiche uso wako, Nisifanane nao washukao shimoni’
Lakini pia kinyume chake ni kweli ukiwa mwovu, ukiwa mkaidi, ukiwa mbaya, unajiandaa kuuna uso wa Mungu wenye ghadhabu,na hasira, na mapigo na matokeo yake utakumbana na adhabu kali kutoka kwake. Ndio hapo, anasema.
‘Uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya, Aliondoe kumbukumbu lao duniani’.
Hivyo kwa ufupisho ni kwamba jicho la Mungu linaona wote, waovu na wema, vilevile uso wa Bwana unawaelekea wote waovu na wema. Lakini katika vifungu hivyo, na vingine baadhi, vinapozungumzia macho ya Bwana huwa vinalenga sana sana kwa wema. Na vinaposema Uso wa Bwana, huwa vinalenga sana sana kwa upande wa waovu.
Kwahiyo usichanganyikiwe, bali fahamu muktadha, wa habari hiyo katika sehemu husika. Ili ujue alimaanisha nini hapo, kwa msaada wa Roho wa Mungu. Kwasababu hutumika kotekote
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
UNAVYOZIDI KUWA MWENYE HAKI, NDIVYO KUJITAMBUA KWAKO KUNAVYOPUNGUA.
ANDALIZI LA MWISHO LA UJIO WA MPINGA KRISTO.
JIFUNZE KUDUMU UWEPONI MWA MUNGU.
Biblia inaposema Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, Inamaana gani?
Ni kweli hakuna mtu aliyewahi kuuona uso wa Mungu Zaidi ya Bwana Yesu?
Je Paulo na Petro walishindania nini? (Wagalatia 2:11).
Kwa utamaduni wa sasa mtu anapokufa, huwa anafukiwa chini ardhini, na juu huwekewa kiashirio Fulani cha kawaida kuonesha eneo hilo lipo kaburi. Lakini watu wengine hupenda kuyapa thamani makaburi ya watu wao, hivyo kwa juu hujengea, kichumba Fulani kinachopambwa kwa vito au mawe ya thamani , wengine wanaweka mnara Fulani n.k. Sasa vitu hivi vyote vinavyojengewa juu ndio huitwa Maziara.
Kwamfano katika picha hii, ni mfano wa Ziara ambalo lilijengwa na wenyeji wa Marekani kama kumuenzi raisi wao wa kwanza wa taifa hilo aliyeitwa George Washington.
Hata katika agano la kale, enzi za biblia, yapo makaburi yaliyokuwa ya kawaida, lakini pia yapo yaliyokuwa yamejengewa maziara. Na hayo yalikuwa hususani ya wafalme na manabii wakubwa waliotokea Israeli, ambao waliuliwa kikatili mfano wa hao ni Zekaria, Hagai na Malaki. Na waliohusika sana kutengeneza maziara haya walikuwa ni hawa waandishi na mafarisayo(Watu wa kidini). Wakidai kuwa wanawa-enzi manabii wao, lakini tunaona Yesu akiwakemea kwa dhambi ya unafki waliyokuwa wanaifanya kwa tendo hilo.
Tusome.
Mathayo 23:29 Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnayajenga makaburi ya manabii, na kuyapamba maziara ya wenye haki, 30 na kusema, Kama sisi tungalikuwako zamani za baba zetu, hatungalishirikiana nao katika damu ya manabii. 31 Hivi mwajishuhudia wenyewe, ya kwamba ninyi ni wana wao waliowaua manabii. 32 Kijazeni basi kipimo cha baba zenu. 33 Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum? 34 Kwa sababu hiyo, angalieni, mimi natuma kwenu manabii na wenye hekima na waandishi; na wengine wao ninyi mtawaua na kuwasulibisha, na wengine wao mtawapiga katika masinagogi yenu, na kuwafukuza mji kwa mji; 35 hivyo ije juu yenu damu yote ya haki iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habili, yule mwenye haki, hata damu ya Zakaria bin Barakia, mliyemwua kati ya patakatifu na madhabahu. 36 Amin, nawaambieni, Mambo hayo yote yatakuja juu ya kizazi hiki.
Soma pia (Luka 11:47-48).
Jibu ni hapana, Bali walichokuwa wanakifanya nje, hakikuendana na kile kilichokuwa mioyoni mwao na ndio maana akawaita wanafiki. Kwasababu walikuwepo pia manabii wa Mungu na watu wenye haki wakati wao, mfano wa Yohana, pamoja na yeye mwenyewe lakini walikuwa wanataka kuwaua. Na ndivyo walivyokuja kufanya kwa Bwana, pamoja na mitume wako na watakatifu wa kanisa la kwanza kama vile wakina Stefano.
Jibu ni la, Endapo tu hatutashirikisha ibada yoyote ya wafu mahali pale. Lakini kama ni kwa kumbukumbu, au kumu-enzi marehemu wako, hakuna shida kuweka ziara (kupamba kaburi lako kwa jinsi upendavyo). Lakini fahamu tu hilo halitakuongezea jambo lolote rohoni. Wala halimfaidii kwa lolote Yule marehemu kule alipo.
Kutunza kaburi lolote, yaani kulisafisha, kulirepea, kulipandia bustani, kulilinda.. Si kosa kibiblia, kwasababu tunaona katika biblia makaburi yalitunzwa kwa bustani, soma (Yohana 20:15), pia yalilindwa, Na zaidi yalihifadhiwa yasiharibiwe. Soma
2Wafalme 23:16 Naye Yosia alipogeuka, aliyaona makaburi yale yaliyokuwako huko, juu ya mlima; akatuma watu, akaitoa ile mifupa katika yale makaburi, akaiteketeza juu ya madhabahu, akainajisi, sawasawa na lile neno la Bwana, alilolinena yule mtu wa Mungu, aliyetamka mambo hayo. 17 Kisha akasema, Ni kumbukumbu la nani, hili ninaloliona? Na watu wa mji wakamwambia, Ni kaburi la yule mtu wa Mungu, aliyetoka Yuda, akayanena mambo hayo uliyoyatenda wewe juu ya madhabahu ya Betheli. 18 Akasema, Mwacheni; mtu awaye yote asiiondoe mifupa yake. Basi wakaiacha mifupa yake, pamoja na mifupa ya yule nabii aliyetoka Samaria.
Hivyo, upendapo kutunza kaburi la mpendwa wako, aliyefariki hufanyi kosa.
Zipo ibada za wafu, ambazo ndizo zinazofanyika mara nyingi katika makaburi ya marehemu, ibadani hizo, zinahusianisha kuwaombea wafu hao, n.k. Ibada hizi ni za kipagani, na mkristo hapaswi kuzifanya ni ibada za miungu. Au wengine wanakwenda kuzungumza na kaburi wakiamini Yule mtu yupo pale makaburini anawasikia. Huo ni uchawi.
Hivyo hakuna mahusiano yoyote ya kiibada katika makaburi. Endapo imetokea unakwenda kufanya maziara (yaani kukarabati au kupamba), basi unachofanya ni kufungua kwa maombi na kufunga kwa maombi, kisha mnaendelea na kazi yenu, ili kutimiza hili andiko
Wakolosai 3:17 “Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”.
Na kama mmeguswa kutafakari maneno ya Mungu mahali pale, kama mfanyapo sehemu nyingine zozote, mfano kazini, shuleni, chini ya mwembe n.k.. Basi iwe ni kwa Mungu na sio kwasababu ya makaburi. Epuka Ibada za wafu.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Pango la Makpela ni lipi, je lina umuhimu wowote kwetu?
MAKABURI YAKAFUNUKA; IKAINUKA MIILI MINGI YA WATAKATIFU WALIOLALA;
MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.
Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani?
Praitorio ni nini? Na Kwanini ilikuwa ni najisi kwa wayahudi kuingia humo? (Yohana 18:28)
Mithali 29:21 “Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto, Mwisho wake atakuwa ni mwanawe”.
Kutundua ni kujali mtu kupita kiasi, au kuonyesha wema uliopitiliza.
Hivyo hapo anaposema amtunduiaye mtumwa wake tangu utotoni, mwisho wake atakuwa ni mwanawe. Anamaanisha amjalie mtumwa wake, kupita kiasi, yaani kuishi naye kama sio mtumwa kwake, (kumdekeza), na kama mfano ikiendelea hivyo kwa kipindi kirefu, mwisho wake utakuwa ni kumfanya mwanawe, yaani mrithi.
Zamani enzi za biblia, watu walikuwa aidha wananunua watumwa, au wanawazalisha majumbani kwao, ikiwa na maana kama mtu huyo alikuwa na mtumwa, kisha mtumwa Yule akazaa, sasa wale watoto wanakuwa pia ni watumwa wa Yule bwana.
Na kulikuwa na sheria kwamba kila baada ya miaka 7, mbiu ilipigwa ya kuwafanya watumwa wote huru, hivyo waliotaka kuondoka waliondoka, lakini waliotaka kuendelea, basi waliendelea kwa mkataba mwingine wa miaka saba. Na hivyo mtumwa huyo aliwajibika kutumika ipasavyo muda wote huo wa mkataba wake (Kumbukumbu 15:1-18).
Sasa hapa, biblia inaeleza tabia ya bwana ambaye moyo wake ni wa kitofauti. Bwana ambaye, anatabia ya kumjali sana mtumwa wake kuliko uhalisia, huwenda anamuhurumia, kumwona anafanya kazi nyingi, hivyo anampa kidogo tu, au anapokwenda kwenye sherehe hamwachi nyumbani anakwenda naye pia, hata akiwa nyumbani majukumu anapewa machache sana, anakaa naye mezani pamoja wanacheka n.k… Sasa katika hali kama hiyo, ikiwa mtumwa huyo, atadumu kubaki kwa bwana wake, kwa kipindi kirefu, Yule bwana, atamfanya tu kuwa kama mmojawapo wa mwanawe, maana yake siku atakapotoa urithi, na huyu lazima apewe, kwasababu ameishi kama mtoto wake kwa kipindi kirefu.
Na hii ni kweli, hata katika kipindi hichi, labda mfanyakazi kaajiriwa kwenye nyumba fulani, kisha mwenye nyumba akampenda, akawa naye kwa kipindi cha miaka mingi, mwishowe, atamfanya tu kama mwanafamilia, na hatimaye atapata kitu kama mmojawapo wa watoto wake.
Hii ni Tabia aliyokuwa nayo Mungu kwetu sisi watu wa mataifa.
Tulipokwenda kwake, hatukuwa wana wake, au warithi, bali warithi walikuwa ni wayahudi tu, lakini kwa ukarimu wake, akatutoa katika utumwa na kutufanya WANA, jambo ambalo si kawaida kwa bwana yoyote, kutenda kwa kijakazi aliyezaliwa kusikojulikana. Ndicho alichokuja kukifanya Yesu;
Yohana 15:15 Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki; kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu.
Yohana 8:35 “Wala mtumwa hakai nyumbani sikuzote; mwana hukaa sikuzote. 36 Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli”.
Hivyo mimi na wewe tunafanyika, WANA na WARITHI, wa Mungu kwa njia ya Bwana Yesu. Haleluya. Utukufu na heshima ni kwa Bwana wetu Yesu!! milele na milele.
Ni kukubali tu kudumu katika nyumba yake. Kama vile mtumwa Yule ambaye aliamua kudumu tangu UTOTONI. Hivyo na wewe umepewa neema, dumu katika neema, dumu katika wokovu, acha kutanga tanga huku na kule. Mungu akaghahiri mema kwako. Ulimwengu hauwezi kukupa unafuu wowote, ni kwa Kristo tu ndio utapata raha nafsini, Hakuna mateso kwa Kristo, Utumwa wake ni mwepesi sana alisema hivyo. Soma (Mathayo 11:28-30).
Ikiwa hujaokoka unasubiri nini sasa? Embu fanya uamuzi wa haraka sana umgeukie Kristo akuokoe. Hizi ni siku za mwisho, anakaribia kurudi kuwanyakua wateule wake. Kama upo tayari kutubu leo dhambi zako, basi fungua hapa kwa ajili ya mwongozo wa sala ya toba.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Nini tofauti ya Mtumwa, Mjakazi na kijakazi?
Maana ya Mithali 9:17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu, Na mkate ulioliwa kwa siri hupendeza”
Miimo ni nini na kizingiti ni nini?
Ni kwa namna gani haki huinua taifa? (Mithali 14:34)
AKAPITA KATIKA LILE SHAMBA AMBALO YAKOBO ALIMPA YUSUFU MWANAWE
Nini maana ya Mithali 27:6 “Jeraha utiwazo na rafiki ni amini;
Jibu: Tuanze kusoma kuanzia mstari wa 7..
Kutoka 21:7 “Mtu akimwuza binti yake awe kijakazi, hatatoka yeye kama watumwa wa kiume watokavyo.
8 Kwamba bwana wake hakupendezewa naye, akiwa amemposa, ndipo atakubali akombolewe; hana amri yeye kumwuza aende kwa watu wageni maana amemtenda kwa udanganyifu.
9 Kwamba amposa mwanawe, atamtendea kama desturi zipasazo binti zake.
10 Kwamba ajitwalia mke mwingine, chakula chake huyo, na nguo zake, na ngono yake, hatampunguzia. 11 Kwamba hamfanyii mambo haya matatu, ndipo atatoka aende bure, pasipo kutolewa mali”.
Jibu: Kwa desturi za kiyahudi mtumwa wa kiume au wa kike anapaswa amtumikie bwana wake kwa muda wa miaka 6 tu, ukifika mwaka wa 7 anakuwa yupo huru kuondoka.,
Kumbukumbu 15:12 “Ikiwa nduguyo, mume wa Kiebrania, au mwanamke wa Kiebrania, akiuzwa kwako, naye amekutumikia miaka sita; basi mwaka wa saba mwache huru aondoke kwako.
13 Nawe utakapomwacha huru aondoke kwako, usimwache aende zake mikono mitupu”
Ikiwa mtumwa wa kiume aliingia na mke wake basi utakapofika mwaka wa 7 ataondoka na mke wake huyo, (Kutoka 21:1-3) lakini kama aliingia bila mke na akaozwa mke kutoka katika familia ya bwana wake, basi utakapofika mwaka wa 7 atatoka yeye kama yeye, lakini mke na watoto watabaki kwa baba wa mke wake, hana amri ya kuondoka nao, lakini kama hataki kumwacha mke wake na watoto wake basi atamtumikie bwana wake huyo daima kwa agano la kutobolewa sikio kwa uma.
Kutoka 21:5 “Lakini huyo mtumwa akisema waziwazi, Mimi nampenda bwana wangu, na mke wangu na watoto wangu; sitaki mimi kutoka niwe huru;
6 ndipo hapo huyo bwana wake atamleta mbele ya Mungu na kumleta mlangoni, au penye mwimo wa mlango; na bwana wake ATALITOBOA SIKIO LAKE KWA UMA; ndipo atamtumikia sikuzote”.
Hivyo ishara ya kutobolewa sikio ilikuwa ni ishara ya mtumwa kukataa uhuru wake.
Lakini kwa upande wa mtumwa wa kike (yaani kijakazi) ilikuwa ni tofauti kidogo. Kama kijakazi aliingia bila kuolewa na baadaye kijana wa bwana wake akampenda na kumwoa, kama mke wa kwanza basi famila ya kijana inapaswa kumfanya kama binti yao.
Lakini kama ameolewa kama mke wa pili, na bado ni kijakazi, na bwana wake hamtaki tena awe mke wake au suria wake, basi utakapofika mwaka wa 7, wakati wa maachilio, yeye hatamwachilia kama mabinti wengine wajakazi wanaoachiwa huru, bali kinyume chake ataachiliwa kwa gharama (maana yake atakombolewa).
Hivyo yule baba wa mtoto wa kiume aliyemwoa huyo binti, atamwuza kwa mojawapo wa ndugu aliye karibu, na si kwa mgeni (yaani mtu kutoka taifa lingine tofauti na Israeli), na asipopatikana wa kumnunua ndipo yule kijana ataendelea kuishi naye huku akimtimizia haki yote ya ndoa, ikiwemo CHAKULA, MAVAZI NA HAKI YA NDOA (Ngono).
Vitu hivyo vitatu ni sheria avitimize, si kwasababu hamtaki tena na kakosa mtu wa kumnunua basi aanze kumnyanyasa kwa kumnyima chakula chake na mavazi pamoja na haki ya ndoa ambayo imenenenwa na mtume Paulo kwa uongozo wa Roho katika 1Wakorintho 7:5. Na ikitokea kashindwa kumtimizia hayo mambo matatu basi atamwacha aende zake huru, bila gharama zozote za kumkomboa.
Kutoka 21: 10 “Kwamba ajitwalia mke mwingine, chakula chake huyo, na nguo zake, na ngono yake, hatampunguzia.
11 Kwamba hamfanyii mambo haya matatu, ndipo atatoka aende bure, pasipo kutolewa mali”.
Mambo gani tunajifunza?
1.Kutoboa masikio si ishara nzuri.
Asili ya kutoboa sikio na kuweka hereni haikuwa nzuri, watu waliotobolewa masikio enzi za zamani ni watu waliokataa uhuru wao, hali kadhalika roho hiyo hiyo inatembea mpaka leo, kibiblia mwanamke au mwanaume hapaswi kutoboa masiko yake. Huenda ulitobolewa enzi hujaokoka, sasa umeshaokoka usiweke hereni baki katika uhalisia wako.
Wengi wanaosumbuliwa na nguvu za giza ni kutokana na vitu wanavyoviweka katika miili yao, na hawajui kuwa hivyo ndio vyanzo vya roho zinazowasumbua.
2. Ni lazima kutimiza haki ya Ndoa
Mtu aliyeoa au aliyeolewa ni sharti amtimizie mwenzie haki zote za ndoa ikiwemo upendo, na ukaribu wakati wowote unapohitajika. Maandiko yanasema mume hana amri juu ya mwili wake kadhalika mke.
1Wakorintho 7:2 “Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe.
3 Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.
4 Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.
5 Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu”.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.
TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.
JIBU: Picha nyingi zinazochorwa kumweleza Yesu, takribani nyingi ya hizo zinamwonyesha ni mtu mwenye nywele ndefu. Lakini Je uhalisia wake ni upi, ni kweli alikuwa na nywele ndefu au fupi?
Maandiko yanaeleza utamaduni wa wayahudi, kwa wanaume ilikuwa kuacha nywele zirefuke kama zile za mwanamke ni aibu kwa mtu huyo. Anajivunjia heshima kubwa.
1Wakorintho 11:14 “Je! Hayo maumbile yenyewe hayawafundishi ya kwamba mwanamume akiwa na nywele ndefu ni aibu kwake? 15 Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni fahari kwake. Kwa sababu amepewa zile nywele ndefu ili ziwe badala ya mavazi”
Hivyo hakukuwa na mtu aliyekuwa na nywele ndefu isipokuwa tu mtu aliyeitwa mnadhiri wa Mungu.
Lakini Je! Yesu alikuwa ni Mnadhiri ?
Kabla ya kufahamu kama Yesu alikuwa mnadhiri au la! Tufahamu kwanza mnadhiri alikuwa ni nani, na sheria ya mnadhiri ilikuwaje
Mnadhiri ni mtu aliyetengwa au aliyejitenga mwenyewe/ aliyejitoa wakfu kwa Mungu, kufuata na sababu binafsi, aidha kwa sababu ya shukrani yake ya kutendewa jambo Fulani kama vile kuponywa ugonjwa, au kupatiwa mtoto, au kupata kitu Fulani kwa Mungu alichokuwa anamwomba. Hivyo katika agano la kale, kulikuwa na sheria ya mnadhiri. Na mnadhiri alikuwa yoyote Yule aidha mwanamke au mwanaume.
Kulingana na Hesabu 6:1-8
Matendo 18:18 “Baada ya hayo Paulo akazidi kukaa huko siku nyingi, kisha akaagana na ndugu akaabiri kwenda Shamu; na Prisila na Akila wakaenda pamoja naye, alipokwisha kunyoa kichwa chake huko Kenkrea; maana alikuwa ana nadhiri”
Sasa tukirudi kwa Bwana Yesu.
Je! Na Yeye alikuwa ni mnadhiri?
Jibu ni hapana, kwasababu Bwana alikunywa mzao wa mzabibu.
Mathayo 26:29 Lakini nawaambieni, Sitakunywa kabisa tangu sasa uzao huu wa mzabibu, hata siku ile nitakapokunywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.
Kuonyesha kuwa hapo kabla alikuwa anakunywa.
Soma pia Mathayo 11:19, Na Yohana 2:1-12, inatupa picha alitumia mzao wa mzabibu. Halikadhalika aligusa maiti, (Marko 5:41), na zaidi ya yote Bwana hakufungwa na sheria za torati.
Hivyo kwa kifupisho ni kwamba Bwana Yesu hakuwa na nywele ndefu, yawezekana alikuwa na nywele nyingi lakini hazikuwa ndefu kama za mwanamke, mfano wa aonekanavyo kwenye baadhi ya picha zinazochorwa.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
JE! NYWELE ZAKO ZINAOTA AU ZIMESIMAMA?
Je! sheria ilikuwaje dhaifu kwasababu ya mwili? (Warumi 8:3)
MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.
Nini maana ya Kucheka kwenu na kugeuzwe kuwa kuomboleza (Yakobo 4:9)