Title March 2023

Nini maana ya kukunguwazwa (Marko 14:27)

Jibu: Tusome,

Marko 14:27  “Yesu akawaambia, Mtakunguwazwa ninyi nyote kwa ajili yangu usiku huu; kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo watatawanyika”.

Kukunguwazwa maana yake ni “kuchukizwa”.. Mtu anapokufanya ukasirike au uchukie maana yake amekukunguwaza, biblia imetoa tafsiri ya neno hilo vizuri katika Mathayo 26:30.

Mathayo 26:30  “Nao walipokwisha kuimba, wakatoka nje kwenda mlima wa Mizeituni.

31  Ndipo Yesu akawaambia, Ninyi nyote MTACHUKIZWA kwa ajili yangu usiku huu kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika”.

Unabii huo alioutoa Bwana ulitimia masaa machache tu mbeleni, pale ambapo kikosi cha Askari wa kirumi kilitokea na kumkamata Bwana Yesu.

Na tunasoma Mitume hawakukifurahia kile kitendo, “WALICHUKIZWA SANA”, hata Petro kufikia hatua ya kutoa upanga na kumkata sikio mtumwa wa kuhani mkuu. Hicho ni kiwango kikubwa sana cha hasira.

Yohana 18:7  “Basi akawauliza tena, Mnamtafuta nani? Wakasema, Yesu Mnazareti.

8  Yesu akajibu, Nimekwisha kuwaambieni ya kwamba ni mimi; basi ikiwa mnanitafuta mimi, waacheni hawa waende zao.

9  Ili litimizwe lile neno alilolisema, Wale ulionipa sikumpoteza hata mmoja wao.

10  Basi Simoni Petro alikuwa na upanga, akaufuta, akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio la kuume. Na yule mtumwa jina lake ni Malko”.

Vile vile na sisi tuliompokea Yesu ni lazima tutapitia tu vipindi vya kuchukizwa kwaajili ya Yesu.

Unapofika mahali na kukuta watu wanalikufuru jina la Yesu ni lazima utachukizwa tu!, unapofika mahali na kukuta watu kwa makusudi kabisa wanahubiri injili nyingine tofauti na ile ya kimaandiko ni lazima utachukizwa tu!.

Unapofika mahali na kukuta unatolewa unabii wa uongo, au kweli ya Mungu inapotoshwa kwa makusudi, ni lazima utachukizwa tu!, Unapofikia hatua ya kusumbuliwa kiimani na watu wengine kwasababu tu umeokoka, au umeamua kwenda katika njia sahihi ni lazima tu utakunguwazwa! hata wakati mwingine kufikia kiwango kama kile cha Petro cha kutamani kumdhuru mtu kabisa.

Lakini sisi hatujapewa ruhusa wala amri ya kumdhuru wengine, hata kama ni waovu au wanatutendea maovu, au hata kama wanamtukana Mungu mbele yetu, kazi tuliyopewa ni kuziokoa roho, na si kuziangamiza, kwasababu kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama bali juu ya majeshi ya mapepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

Lakini siku zote fahamu kuwa, ni lazima tu tutapitia vipindi vya kuchukizwa kwaajili ya Yesu, hilo haliepukiki kwa kila aliyezaliwa mara ya pili.

Yohana 15:20 “Likumbukeni lile neno nililowaambia, Mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake. Ikiwa WALINIUDHI MIMI, WATAWAUDHI NINYI; ikiwa walilishika neno langu watalishika na lenu”.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

Nini tofauti ya Mtumwa, Mjakazi na kijakazi?

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

JINSI YA KUEPUKA KUUMIZWA MOYO KUSIKOKUWA NA SABABU.

Je ni lazima kushiriki Meza ya Bwana?

YEYE ATAWABATIZA KWA ROHO MTAKATIFU NA KWA MOTO.

Rudi nyumbani

Print this post

Kama kuua ni dhambi kwanini Mungu aruhusu mauaji katika Kumbukumbu 13:6-10?

Bwana alisema “Usiue” (Kutoka 20:6) lakini tunaona anawapa wana wa Israeli maagizo ya kuua wale wote wanaoabudu miungu? Je Hii inakaaje? (Kumbukumbu 13:6).

Jibu: Tusome,

Kumbukumbu 13:6 “Atakapokushawishi kwa siri ndugu yako, mwana wa mamaako, au mwana wako, au binti yako, au mke wa kifuani mwako, au rafiki yako aliye kama moyo wako, akikuambia, Twende tukaabudu miungu mingine usiyoijua wewe wala baba zako; 7 katika miungu ya mataifa yaliyo kando-kando yenu karibu nawe au mbali nawe, tokea ncha moja ya dunia hata ncha ya pili ya dunia;8 usimkubalie wala usimsikize; wala jicho lako lisimwonee huruma, wala usimwache, wala usimfiche;9 MWUE KWELI; mkono wako na uwe wa kwanza juu yake katika kumwua, na baadaye mikono ya watu wote.10 NAWE MTUPIE MAWE HATA AFE; kwa kuwa alitaka kukupotoa na Bwana, Mungu wako aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.11 Na Israeli wote watasikia na kuogopa, wasifanye tena uovu mfano wa huo katikati yako”

Ni kweli Mungu alikataza “Kuua” lakini pia kuna mahali pengine aliruhusu “kuua”, sasa ni rahisi kuhisi kuwa biblia inajichanganya, lakini kiuhalisia haijichaganyi.

Katika biblia zilikuwepo sheria za mtu binafsi lakini pia zilikuwepo sheria za Nchi/Taifa. Ikumbukwe kuwa Israeli lilikuwa ni Taifa la kidini, hivyo baadhi ya Amri na sheria zilikuwa ni za kitaifa. Kwahiyo mtu akiivunja sheria Fulani iliyoandikwa kwenye torati basi alikuwa amevunja sheria ya kitaifa.

Ili tuelewe vizuri tuchukue mfano wa mataifa ya sasa, katika mataifa mengi, (karibia yote) kuna sheria ya “kutoua” yaani raia haruhusiwi kumuua mwenzake kwa kosa lolote lile!!, lakini katika Taifa hilo hilo tunaona kuna sheria ya “kunyongwa” endapo mtu akikutwa na hatia iliyo kubwa sana..

Sasa Yule askari aliyetumwa kumweka kitanzi Yule mtuhumiwa, tayari kashafanya tendo la mauaji, lakini kwa kumnyonga Yule mhalifu, bado anakuwa hajavunja sheria ya “kuua”.. Kwasababu yeye kapewa amri ya kuua na mamlaka, lakini haja ua kwa matakwa yake yeye. Lakini kama ingekuwa kajichukulia sheria mkononi ya kuua basi angehesabika ni muuaji, na angekuwa amevunja sheria ya nchi. Na pia Nchi kuweka sheria ya Kuwaua wale waalifu sugu, haijamaanisha kuwa imeruhusu sheria ya watu kuuana huko uraiani.

Vivyo hivyo katika Israeli, Mungu alikataza mtu kujichukulia sheria mkononi za kuua, lakini pia aliruhusu mauaji kwa watu ambao watathibitika kisheria (yaani kitaifa) kuwa wamestahili kifo!.  Na mamlaka hayo aliwapa watu wote, tofauti na sasa ambapo wanapewa tu wale askari walioteuliwa kwa kazi hiyo.

Kwahiyo biblia haijichanganyi, lakini pia tunachoweza kujifunza ni kuwa Lile baya mtu analolifanya litamrudia hata kwa njia nyingine, mtu aliye muuaji naye pia atauawa, mtu anayefanya ubaya ule ubaya utampata na yeye siku za baadae.

Mathayo 26:51  “Na tazama, mmoja wao waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono wake, akaufuta upanga wake, akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.

52  Ndipo Yesu akamwambia, Rudisha upanga wako mahali pake, maana wote waushikao upanga, wataangamia kwa upanga”.

Soma pia Ufunuo 13:10.

Kwahiyo tujihadhari na dhambi tuwafanyiazo watu au tuzifanyazo mbele za Mungu, kwasababu yale tunayoyafanya tutapata malipo yake hapa hapa, kama ni mema au kama ni mabaya.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

MJUMBE WA AGANO.

Je! sheria ilikuwaje dhaifu kwasababu ya mwili? (Warumi 8:3)

Je! Watu ambao hawajawahi kusikia injili kabisa siku ya mwisho watahukumiwa?

IMANI NI KUWA NA UHAKIKA WA MAMBO YATARAJIWAYO.

Rudi nyumbani

Print this post

Kama ndege aendaye huko na huko mbali na kitundu chake;

SWALI: Nini maana ya huu mstari?

Mithali 27:8 “Kama ndege aendaye huko na huko mbali na kitundu chake; Ndivyo alivyo mtu aendaye huko na huko mbali na mahali pake”

JIBU: Hapa Sulemani alikuwa anajaribu kueleza jinsi tabia ya ndege inavyoweza kufananishwa na tabia ya mkristo katika maisha yake hapa duniani. Kwa kawaida ndege anapotoka katika kiota chake, huwa na lengo la aidha kutafuta chakula, au kukiendeleza kiota chake, au kujipumzisha mahali Fulani kwa muda. Hivyo huwa anaenda na kurudi, anaenda na kurudi kwa siku hata mara 10 na zaidi, anaweza kufanya hivyo.

 Lakini wakati huo huo, awapo katika mazingira ya kuzunguka huko na huko, hukutana na hatari nyingi sana. Aidha Maadui au mitego. Hivyo asipokuwa makini anaweza asirudi, kabisa nyumbani kwake.

Hivyo ndivyo alivyo mkristo, ambaye misingi yake ni “biblia na Kanisa”. Ukweli ni kwamba si kila wakati atakuwa katikati ya watakatifu, au atakuwa uweponi akimsifu Mungu na kumwimbia, au akilitafakari Neno la Mungu. Zipo nyakati atatoka kwa muda ataenda kazini, atatoka kwa muda ataenda shambani pengine kujitafutia riziki, ataenda shuleni masomoni na kama si hivyo basi kwa namna moja au nyingine atajihusisha na mambo ya kijamii, kama kutembelea jamaa, na ndugu, majirani n.k.

Sasa awapo katika mazingira haya anafananishwa na ndege atokaye katika kiota chake na kuzunguka huko na huko. Hivyo anapaswa awe na busara kwa sababu huko nje, zipo hatari nyingi sana za yeye kunaswa na adui asipokuwa makini.

Ni lazima ajiwekee mipaka, si kila biashara afanye, si kila jambo la kidunia analoletewa mbele yake ajihusishe nalo, si kila mazungumzo ayaongee. Bali muda wote awapo nje, atambue kuwa makao yake ni KANISANI awezapo kufanya ibada, na kujumuika na watakatifu wenzake. Muda wote atambue usalama  wake ni katika Neno la Mungu basi. Alale katika hilo na aamke katika hilo.

Akitafutacho huko nje ajue ni kwa lengo la kuendeleza tu kiota chake (kazi ya Mungu), na sio vinginevyo. Mtu huyo akizingatia vigezo hivyo atakuwa salama. Lakini watu wengi wamenaswa na ulimwengu. Hata Kanisani hawaonekani tena baada ya kupata kazi, Upendo wao kwa Mungu umepoa pale walipokutana na marafiki Fulani wapya, muda wa maombi wanakosa kisa wapo buzy na mihangaiko ya maisha. Kauli zao zimebadilika, kwasababu muda mwingi wamekaa na watu wenye mizaha, na matusi, hadi na wao wakajifunza lugha zao.

Biblia inatuambia,

Waefeso 5:15  “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; 16  mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu. 17  Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana.

Anasema tena..

Wakolosai 4:5  “Enendeni kwa hekima mbele yao walio nje, mkiukomboa wakati. 6  Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea munyu, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu”.

Hivyo tuwapo nje ya uwepo wa Bwana, tujichunge, tujizuie, tuwe na kiasi, tutakuwa salama. Ili tusijikute tunanaswa katika mitego ya ibilisi.(Mithali 1:17,  7:22)

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

Mambo yale yaliyo mbali, na yale yaendayo chini sana,

Dia ni nini katika biblia? (Mithali 13:8)

Mithali 24:17 inamaana gani kusema Tengeneza kazi yako huko nje?

Nini maana ya “Atamwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake”. (2Wathesalonike 2:8).

Aibusu midomo atoaye jawabu la haki (Mithali 24:26)

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

Marijani ni nini katika biblia(Ayubu 28:18,Mithali 8:11)?

Rudi nyumbani

Print this post

Kupwelewa maana yake nini? (Matendo 27:26).

Tusome,

Matendo 27:25 “Basi, wanaume, changamkeni; kwa sababu namwamini Mungu, ya kwamba yatakuwa vile vile kama nilivyoambiwa.

26 Lakini hatuna budi kupwelewa katika kisiwa kimoja”.

Kupwelewa maana yake ni “kusafiri katika kina kifupi”. Meli au Mashua inaposafiri katika maji yenye kina kifupi, maana yake Meli hiyo au boti hiyo “inapwelewa”.

Katika safari ya Paulo kuelekea Rumi chini ya kikosi cha maaskari, maandiko yanatuonyesha safari ile ilikuwa ni ya misuko-suko mingi baharini, kwasababu wale mahabaria hawakulisikiliza shauri la Paulo ambalo aliwashauri wasing’oe nanga lakini wenyewe hawakusikia hivyo. Mwishowe wakakutana na misuko suko mikuu baharini, mpaka wakakata tamaa ya kuokoka.

Matendo 27:10 “akawaambia, Wanaume, naona kwamba safari hii itakuwa na madhara na hasara nyingi, si ya shehena na merikebu tu, ila na ya maisha yetu pia.
11 Lakini yule akida akawasikiliza nahodha na mwenye merikebu zaidi ya yale aliyoyasema Paulo”.

Wakiwa katika hiyo misukosuko, Paulo alitokewa na Malaika na kuambiwa kuwa hakuna atakayekufa katika safari hiyo, kwani ni lazima Paulo afike salama Rumi ili akalishuhudie Neno la Mungu na kule nako. Na jambo lingine aliloambiwa na Malaika yule ni kwamba Merikebu itapwelewa (yaani itasafiri katika kina kifupi) kando kando ya kisiwa kimoja, mpaka watakapofika kwenye hicho kisiwa.

Na kweli ufunuo huo mahabaria waliuhakiki kwani muda mfupi tu walipoanza kupima kina cha maji waliona kinaanza kupungua kwa jinsi walivyokuwa anaendelea mbele.

Matendo 27:27 “Hata usiku wa kumi na nne ulipofika, tulipokuwa tukichukuliwa huko na huko katika bahari ya Adria, kama usiku wa manane baharia wakadhani ya kuwa wanaikaribia nchi kavu.

28 Wakatupa bildi wakapata pima ishirini, wakaendelea kidogo wakatupa bildi tena, wakapata pima kumi na tano”.

Ni nini tunachoweza kujifunza katika safari hiyo ya Paulo?

1.Mungu atakuwepo na sisi hata katikati ya majaribu
Paulo, alikuwa amefungwa lakini katika kufungwa kwake, bado Mungu alikuwa naye, akimwongoza katika mapito yake, utaona pia wakati akiwa gerezani bado Bwana alikuwa naye, na kila mahali Bwana alikuwa naye, vile vile na sisi tunapokuwa katika majaribu, ambayo tunajua kabisa ni Mungu kayaruhusu basi hatupaswi kuwa na woga wala kukata tamaa, kwasababu Mungu atakuwa Pamoja nasi, na zaidi sana yeye alisema “hawezi kutuacha tujaribiwe kupita tuwezavyo”

2. Wokovu wa Mungu ni hata kwa maadui zetu.

Tunapokuwa katikati ya majaribu ni muhimu kujua kuwa Mungu katuweka pale kwa wokovu wa wengine, Utaona Paulo kafungwa lakini Mungu anamwokoa yeye Pamoja na wale Mabaharia, na wafungwa na watesi wake, anawaokoa na Mauti vile vile na sisi Mungu anapotuweka mahali ni ili tuokoke na wale tulio nao, haijalishi ni maadui zetu au watesi wetu.

Matendo 27:22 “Sasa nawapeni shauri, iweni na moyo mkuu, kwa maana hapana hata nafsi mmoja miongoni mwenu atakayepotea, ila merikebu tu.

23 Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye, alisimama karibu nami,

24 akaniambia, Usiogope, Paulo, huna budi kusimama mbele ya Kaisari; tena, tazama, Mungu amekupa watu wote wanaosafiri pamoja nawe.

25 Basi, wanaume, changamkeni; kwa sababu namwamini Mungu, ya kwamba yatakuwa vile vile kama nilivyoambiwa.

26 Lakini hatuna budi kupwelewa katika kisiwa kimoja”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

Kaanani ni nchi gani kwasasa?

SI KWA MATENDO BALI NEEMA.

Rudi nyumbani

Print this post

Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo; Lakini hukumu zake zote ni za BWANA.

SWALI: Nini maana ya huu mstari?

Mithali 16:33

[33]Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo; Lakini hukumu zake zote ni za BWANA.

JIBU: Kura zilipigwa kwa namna mbalimbali zamani, njia iliyokuwa nyepesi ndio hiyo ambayo kipande cha shuka, au nguo, iliyofumwa vilitumiwa kukusanya kura za watu mbalimbali ambazo ziliandikwa katika vipande vya vibao vidogo vidogo, au mawe kisha hukorogwa, na lile litakalotoka la kwanza au kuchukiliwa humo basi ndio kilichosahihi..

Wengine walitumia makopo, wengine kofia, kisha kuzikoroga kura na ile itakayotoka au kuchaguliwa cha kwanza huko ndio huaminika kuwa chaguo sahihi

Hivyo, zipo nyakati ambazo Mungu aliruhusu baadhi ya mambo yaamuliwe kwa kura kama vile kugawanya nchi n.k.Soma(Hesabu 26:55, Yoshua 18:6-10)Lakini si kila jambo, mengi Mungu alitoa majibu kwa njia ya moja kwa moja, kwa kufunuliwa aidha kwa kupitia manabii au maono au ndoto.

Sasa tukirudi katika mstari huo..

Anaposema..

Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo; Lakini hukumu zake zote ni za BWANA.

Maana yake ni kuwa Japo kuwa kupiga kura ni tendo linaloonekana la kibinadamu lakini ikiwa linafanyika katika Bwana, majibu ya kweli hutoka kwake.

Yule atakayechaguliwa, au kile kitakachopendekezwa, ndio jibu sahihi kutoka kwa Bwana.

Katika Biblia tunaona mtume Mathiya alichaguliwa kwa kura, lakini kabla ya kupiga kura ile, mitume walimtanguliza kwanza Mungu katika uchaguzi wao,waliomba na kumsihi Bwana aingilie uchaguzi wao..kisha kila mmoja akaandika pendekezo lake na jawabu likatoka na ndio likawa kweli jibu sahihi la Mungu.

Matendo 1:23-26

[23]Wakaweka wawili, Yusufu, aitwaye Barsaba, aliyekuwa na jina la pili Yusto, na Mathiya.

[24]Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili,

[25]ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe.

[26]Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja.

Wakati mwingine tunaweza kulaumu, viongozi tuliowachagua, tukasema waliiba kura n.k. lakini kama Mungu asingetaka wawepo pale wasingekuwepo tu, kwasababu yeye ndio anayewamilikisha watawala haijalishi watakuwa ni waovu au wema..

Danieli 2:21

[21]Yeye hubadili majira na nyakati; huuzulu wafalme na kuwamilikisha wafalme; huwapa hekima wenye hekima; huwapa wenye ufahamu maarifa;

Hii ni kuonyesha uhuru wa Mungu wa kuchagua, yapo mambo kwetu tutaona kama tumeamua sisi, au yametokea kwa bahati, lakini kumbe ni Mungu kapanga..kwake yeye vitu havitokei kwa bahati, bali vyote chini ya makusudi yake.Mungu ndiye ayaruhusuyo yote..

Utukufu una yeye milele na milele.

Amina.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?

NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!

kwanini yule kijana aliitupa ile nguo ya kitani chini na kukimbia uchi?

HAKUVAA NGUO SIKU NYINGI.

Ni kura ya aina gani waliipiga wale watu waliosafiri na Yona?

NI WAPI UTAKUTANA NA MALAIKA WA BWANA?

Rudi nyumbani

Print this post

TABIA ZA NJIA YA MUNGU KWA MKRISTO

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo.

Biblia inatuambia Yesu ndiye njia na kweli na uzima. (Yohana 14:6)

Ni kweli wakristo wengi tunamtambua yeye kama njia, lakini hatujui tabia ya hii njia kwa undani jinsi ilivyo kwetu sisi wakristo.

Tofauti na hizi njia tuzijuazo, kwamfano ukitaka kutoka Dar es salaam kwenda Morogoro, ni rahisi kuifuata hiyo barabara, au kuielewa kwasababu daima ipo palepale haibadiliki, watu wote tunaipita hiyo kila siku, tumeshaikariri, tunajua vituo vyake vyote vya njiani,  tunaweza hata kukadiria ni muda gani tutakaoutumia kumaliza safari yetu.

Lakini vipi kuhusu njia ya Mungu kwa wakristo. Je na yenyewe inakaririka, au inazoeleka, au ipo palepale?

Maandiko yanatupa majibu; tusome;

Warumi 11:33

Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! Hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazitafutikani!

Hapo anasema “Njia zake hazitafutikani”

Ndugu Bwana alichotuhakikishia ni , usalama na mwisho mwema wa safari yetu ya wokovu endapo tutaamua kumfuata YESU kwa mioyo mikamilifu. Lakini hakutuhakikishia kuwa njia zetu sote kwa pamoja zitafanana. Kwamba sote tukitoka hapa tutapita pale, kisha tutamalizia na pale.

Ni Mungu ndiye anayemchagulia kila mtu mapito yake kwa jinsi apendavyo yeye. Mwingine akishaokoka Bwana atampitisha mashariki kwenda Magharibi, mwingine ataanza naye kusini kwenda kaskazini, na ndio hapo utaona, mmoja ataanza kwa kupoteza kila kitu, mwingine Mungu atambariki atamfanikisha katika maisha yake atakuwa bilionea, mwingine atakuwa na maisha ya kawaida, mwingine atakuwa na ya chini. Mwingine atakuwa na afya sikuzote, mwingine atakuwa na magonjwa yasiyotibika na Bwana hamwondolei kwa kipindi fulani kirefu.

Lakini katika mapito hayo yote, Kristo atahakikisha kuwa anampa nguvu ya kuweza kukabiliana au kuchukuliana na hayo mazingira  bila kukengeuka au kuona ni mzigo mkubwa sana kwake.

Tatizo kubwa la  watakatifu ni kuwa tunataka njia zetu ziwe kama za mtu fulani pale tunapodhamiria.

Sote tunataka tuwe mabilionea kama Sulemani. Ndugu mawazo ya kumpangia Mungu ni wapi akupitishe yatakugharimu. Kwasababu njia zake hazikaririki, hazitafutikani, wala hazichunguziki. Atakupitisha ajuapo yeye, sio ujuapo wewe.

Kuna mmoja atakuwa kama Yohana mbatizaji, hali wala hanywi anakaa majangwani, kuna mwingine atakuwa kama Bwana Yesu anakula na kunywa..kikubwa ni matokeo ya wito ndicho kitakachoeleza wito wa mtu huyo ni kweli au la. Wote wawili Yohana na Bwana Yesu walikuwa na mafanikio makubwa katika huduma zao, japo mapito tofauti, hivyo kila mmoja wito wake ulikuwa ni wa kweli.

Njia za Mungu kwetu sisi hazichunguziki, kaa katika nafasi yako na wito wako, mwamini Bwana hapo hapo ulipo ikiwa kweli umeokoka na umemanisha kumfuata Yesu, kamwe usijilinganishe na mkristo mwingine, kisa yeye ni tajiri kuliko wewe, au ana uwezo wa kuhubiri sana kuliko wewe.

Mtazame Yesu tembea katika njia yake aliyokupangia, hata kama ni mlemavu, isiwe sababu ya wewe kupoteza uelekeo wa wokovu katika maisha yako.Kila pito la mtu, lina sehemu kubwa mbeleni kulisaidia kanisa la Kristo. Maisha yako ni ushuhuda wa kuwaponya wengine mbeleni. Hujui kwanini Mungu akupitishe katika mapito hayo. Hivyo acha kuzikariri njia za Bwana…

Sulemani alikuwa ni mtu mwenye akili nyingi, ambazo alipewa na Mungu, akili za kuweza kuchunguza kila kitu kilicho duniani, lakini alipofika katika njia za Mungu alikiri kuwa hakuna anayeweza kuzielewa alisema..

Mhubiri 8:17 “basi, niliiona kazi yote ya Mungu, ya kuwa haitafutikani na mwanadamu kazi inayofanyika chini ya jua; kwa sababu mwanadamu na akijisumbua kadiri awezavyo kuitafuta, hata hivyo hataiona; naam, zaidi ya hayo, mwenye hekima ajapodhania ya kuwa ataijua, lakini yeye hataweza kuiona”.

Sasa ni kwa namna gani hazitafitikani?

Ni kwa sababu nyakati nyingine Mungu anakupitisha mahali usipopatarajia, wana wa Israeli hawakujua kuwa wangeelekezwa baharini walipokuwa wanatoka Misri, lakini ndio ilikuwa njia ya Bwana kwao. Unaweza kuelekezwa na Mungu, mahali ambapo hakuna dalili yoyote ya wewe kutoka kumbe ndio Mungu kakusudia upite hapo, aonyeshe maajabu yake.

Pili wakati mwingine Mungu anatabia ya kuvuruga mipango yetu. Kanisa la kwanza lilkuwa linakwenda vizuri, katika raha yote, lakini Mungu akamnyanyua Paulo alitese kanisani mpaka Kifo cha Stefano. Kanisa likaogopa nikaondoka Yerusalemu. Kumbe nyuma ya kutawanyika kule kulikuwa na kusudi la Mungu injili ihubiriwe dunia nzima. Paulo alipomaliza kusudi hilo akageuzwa na yeye moyo akawa mhubiri. Njia za Mungu hazichunguziki.

Hata wewe mambo yako yanaweza kwenda sawa, halafu ghafla Mungu akayavuruga, lakini mwisho wake ukawa mwema. Kupata na kupoteza, nyakati za raha na shida, milima na mabonde..tarajia katika safari hii ya ukristo..Njia za Mungu hazichunguziki.

Lakini katika yote Bwana anasema.. Sisi tulioamua kumfuata yeye kwa mioyo yetu yote kamwe hatutakaa tupotee katika njia hiyo hata  kama tutakuwa hatueleweki, tutakuwa wajinga kiasi gani, hatutakaa tupotee, lakini tutafikia tu mwisho mwema kwasababu njia hiyo ni salama sana na hakika.

Isaya 35:8

[8]Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, Njia ya utakatifu; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; wasafirio, wajapokuwa wajinga, hawatapotea katika njia hiyo.

Anasema pia…

Yeremia 29:11

[11]Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema BWANA, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.

Wote waliomfuata Yesu, waliofaida yake, katika kila pito. Jitwike msalaba wako mfuate Yesu. Kwasababu yeye ndio Njia pekee ya kufika mbinguni na kuumaliza mwendo wako salama.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

MATARAJIO YA KILA MWANADAMU DUNIANI NI YAPI?

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

MBINGUNI YUPO NANI SASA?

Je Mungu ana njia ngapi za kuzungumza?

Dia ni nini katika biblia? (Mithali 13:8)

Mofa ni nini? na inafunua nini kiroho?(1Samweli 28:24).

Kujazi ni nini? (Mathayo 6:4)

Zile Rangi saba za Upinde wa Mvua zinawakilisha nini?

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

Rudi nyumbani

Print this post

IJUE FAIDA YA KUNENA KWA LUGHA MPYA!

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo lihimidiwe daima, karibu tujifunze Biblia Neno la Mungu wetu lililo taa ya miguu yetu na Mwanga wa njia yetu (Zab.119:105).

Maandiko yanatuonyesha kuwa si lazima watu wote wanene kwa lugha (1Wakorintho 12:30 na  14:23), kana kwamba ndio uthibitisho pekee wa mtu kuwa wa kiroho…lakini pia kuna faida kubwa ya kunena kwa lugha ikiwa mtu atajaliwa hilo.

Na pia kunena kwa lugha si jambo  ambalo mtu anaweza kuamua, kwamba sasa naanza kunena, la! Kunena kwa lugha ni msukumo ambao Roho Mtakatifu anaushusha ndani ya mtu pasipo mtu kutaka au kupanga!.. Ni kama mtu anavyopokea unabii, au anavyopokea ndoto au maono.. hakuna mtu anayeweza kupanga unabii au maono au ndoto (labda awe nabii wa uongo)!.. kwani mambo hayo yanakuja tu yenyewe kutoka kwa Mungu, kwajinsi apendavyo Mungu… Na kunena kwa lugha ni hivyo hivyo, si lazima iwe kila siku au kila saa, bali ni wakati maalumu tu ambao Roho atalishusha jambo hilo ndani ya mtu.

Sasa zipo lugha za wanadamu, na vile vile za Malaika (Soma 1Wakorintho 13:1), Zozote kati ya hizo mtu aliyejazwa Roho anaweza kuzinena. Na zote zina faida katika kuzinena… Katika kunena lugha za wanadamu ni pale ambapo mtu haijui lugha Fulani ya jamii fulani ya watu, lakini ghafla anajikuta anaanza kuizungumza ile lugha vizuri sana.. Vile vile katika kunena lugha za malaika, ni pale ambapo anajikuta anazungumza lugha ambayo ni mpya kabisa isiyotumiwa na wanadamu mahali popote.

Na maneno anayoyazungumza yanakuwa aidha ni maneno ya unabii, au maonyo au ya kumsifu Mungu.. kwahiyo kama ni ujumbe kwa kanisa ni lazima awepo mfasiri..

Vile vile kama ni lugha Mpya inayozungumzwa, maana yake ambayo haitumiki na jamii yoyote ya wanadamu, na ni ujumbe kwa kanisa, basi anahitajika pia mfasiri, lakini kama mtu yupo katika maombi yake binafsi na lugha hiyo ikamjia ndani yake, basi hapo hahitaji mfasiri bali anakuwa ananena maneno ya siri na Mungu wake.

Na leo tutaangalia faida moja kubwa  ya kunena lugha mpya, uwapo wewe binafsi katika maombi yako ya faragha.

MAZUNGUMZA YAKO YANAKUWA NI YA SIRI.

Hii ndio faida kuu na ya kwanza. Kikawaida mazungumzo ya siri yanakuwa na upinzani mchache kuliko mazungumzo ya wazi!..  na njia mojawapo ya kuficha mazungumzo ni kutumia lugha nyingine!..

Kwamfano utaona Waarabu wawili, au Wachaga wawili, au wamasai wawili, au wasukuma wawili, wanapokutana mahali Fulani ili waongee kwa uhuru zaidi utaona wanatumia lugha zao  za asili , lengo ni kuficha mazungumzo na pia kuzungumza mambo yao yale mambo ya ndani kwa uhuru zaidi.. watu walio kando kando inakuwa ngumu kuelewa na hivyo wazungumzaji wanakuwa wamefunga milango mingi.

Na  sisi tunapozungumza na Mungu wetu, KUNA WAKATI TUNAHITAJI USIRI.. Maneno yetu tunayoyazungumza si lazima yaeleweke na watu wa kando yetu au na mapepo katika ulimwengu wa roho. Ili kuzuia vita visivyokuwa na msingi.

Shetani asipoelewa kile tunachoomba kwa Mungu, inamwia vigumu kwake kupanga mashambulizi, kwasababu hajui ni nini tunamwomba Mungu kwa wakati huo, hivyo anabaki tu hapo katikati, lakini akisikia unamwomba Mungu akupe Amani, au akupe riziki Fulani, tayari na yeye kashajua ni eneo gani aende kukupiga vita ili usipokee kile ulichomwomba Mungu. Ndio maana Mtume Paulo kwa ufunuo wa roho aliliona hilo na akawaandikia watakatifu..                                                                                                                                                   

1Wakorintho 14:2  “Maana yeye anenaye kwa lugha, hasemi na watu, bali husema na Mungu; maana hakuna asikiaye; lakini anena mambo ya siri katika roho yake”.

Hivyo usijizuie kunena kwa lugha kama umejaliwa hilo.. itakusaidia kuzuia vita vingi katika ulimwengu wa mwili na wa roho.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je kunena kwa Lugha mpya kukoje?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

SEMA KWA LUGHA NYINGINE.

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

USHIRIKA WA ROHO MTAKATIFU UKAE NANYI NYOTE.

Rudi nyumbani

Print this post

Yeremia alikuwa na umri gani alipoitwa?

JIBU: Maandiko hayaweki wazi ni katika umri gani Yeremia aliitwa isipokuwa watafiti wengi ya Biblia wanakadiria Yeremia aliitwa katika umri wa miaka 20, au chini kidogo ya hapo, pengine 17

Biblia inachosema tu..alipoitwa aliitikia kwa kusema mimi ni MTOTO…Ikiwa na maana kuwa alijiona  umri wake ulikuwa bado haujakidhi vigezo vya kumtumikia Mungu..

Yeremia 1:4 “Neno la Bwana lilinijia, kusema,  5 Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.  6 Ndipo niliposema, Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto.  7 Lakini Bwana akaniambia, Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru”.

Na hiyo pengine kwasababu aliona historia ya manabii wengi walioitwa walikuwa tayari ni watu wazima,

Pili Yeremia yeye alizaliwa katika familia ya kikuhani, na alijua umri wa kuhani kutumika Mungu ni kuanzia miaka 25 na kuendelea sawasawa na (Hesabu 8:24). Hivyo huwenda yeye hakuwa katika umri huo, ndio maana akawa na ujasiri wa kumwambia Mungu mimi bado ni mtoto.

Hivyo na sisi tunajifunza nini?

Kwa Bwana hakuna umri maalumu au  wakati maalumu wa kuitwa..Uonapo unavutwa umwamini Yesu, saa hiyo hiyo itikia wito huo, kama Yeremia, neema hiyo haitadumu milele. Ikiwa utapuuzia kwa kusema Aah, Muda bado ngoja kwanza nifikishe umri Fulani, ngoja kwanza nijenge nyumba, ngoja kwanza nipate kazi, ngoja kwanza niondoke kwa wazazi. Fahamu kuwa una dalili kubwa ya kuipoteza neema ya Mungu. Saa ya wokovu ni sasa, wakati uliokubalika ndio huu. Maneno ya Mungu yanapokuchoma, tambua huo ndio wakati wako. Itikia sauti hiyo, badilika, tumika, tii. Na Bwana atayashughulikia hayo yaliyosalia.

Bwana akubariki

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?

Raheli aliwalilia vipi watoto wake?

Matowashi ni wakina nani?

Historia ya wimbo wa tenzi – Ndio dhamana Yesu wangu

Je ni kweli miaka yetu ya kuishi ni 80 tu (kulingana na Zaburi 90:10).

Nabii Elisha alikuwa ana maana gani kulia na kusema”Gari la Israeli na wapanda farasi wake”?

Maswali na Majibu

HISTORIA YA ISRAELI.

Rudi nyumbani

Print this post

SI KWA MATENDO BALI NEEMA.

Ikiwa unafanya matendo mazuri yanayompendeza Mungu, basi mshukuru Mungu kwa hayo lakini USIJISIFU wala kujigamba hata kidogo kwa hayo. Kwasababu wakati unadhani kuwa umefanya 100 yanayompendeza Mungu kwa siku moja, yapo mengine 200 uliyoyafanya yasiyompendeza Mungu, kwa kutokujua.

Laiti tukifunguliwa macho na kuona makosa yetu yote tunayoyafanya bila sisi wenyewe kujua, tusingeendelea kujitamani hata kidogo, tusingeendelea kujivuna, tusingeendelea kujisifia vimema vichache vichache tunavyovitenda kwa siku!!!…Kwaufupi maisha yetu yamejaa makosa mengi kuliko mema!, hata kama tutajiona kama tuna mema mengi kuliko kasoro.. Lakini uhalisia utabakia pale pale kwamba makosa yetu yamezidi mema yetu..

Kwahiyo kama Mungu ni wa haki, basi ni haki yake atulipe mabaya mengi kuliko mema.

Kama ukimlazimisha Mungu akuhesabie haki ya kukubariki kwa sadaka yako uliyotoa  jumapili, vile vile anapaswa akuhesabie haki ya kuadhibiwa kwa mawazo yako ya kutamani na kwa hasira uliyomwonea ndugu yako siku hiyo hiyo ya jumapili. Na maandiko yanasema mtu amwoneaye ndugu yake hasira ni mwuaji, kwahiyo unapaswa uhukumiwe kama mwuaji..

Lakini kama hutaki Mungu atazame udhaifu wako huo na hutaki akuadhibu kwa makosa yako basi usilazimishe akulipe kwa matendo yako mazuri unayomfanyia. Bali kinyume chake nyenyekea!!!.. Fanya tu yakupasayo kufanya sawasawa na Luka 17:10.

Luka 17:10  “Vivyo hivyo nanyi, mtakapokwisha kuyafanya yote mliyoagizwa, semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya”.

Na kama tukiingia mkataba huo na Mungu wa kupokea haki yetu kwa matendo yetu, basi tunazo sababu nyingi za kulipwa mabaya kuliko mema. Kwasababu Mungu siku zote ni  wa haki.

Lakini kama mara nyingi Mungu anatuvumilia kwa mabaya yetu tunayoyafanya sawasawa na Zaburi 130:3  “Bwana, kama Wewe ungehesabu maovu, Ee Bwana, nani angesimama? Lakini kwako kuna msamaha, Ili Wewe uogopwe”…basi na sisi hatuna budi kutoyatumainia mema yetu tunayoyafanya!.

Ndio hapa sasa panazaliwa kitu kinachoitwa NEEMA!... Neema tafsiri yake ni upendeleo maalumu usiokuwa na sababu. Kwamba unapokea tu kitu kutoka kwa Mungu pasipo matendo yako.. Yaani Mungu anapenda tu kukupa si kwasababu wewe ni mtenda mema, au ni mwombaji sana, au ni mfungaji sana, au ni mhubiri mzuri… La!, bali anakutendea tu mema bila kwa upendo wake tu!, na huruma zake na kupenda kwake.

Ndio maana hatuna budi kila siku KUOMBA NEEMA YA MUNGU ije juu yetu. Kwasababu tukiipata hiyo tumepata kila kitu.

Usijivune, bali omba neema kwasababu Mungu huwapinga wenye kiburi na kuwapa wanyenyekevu Neema yake (1Petro 5:5).

Afya uliyonayo ni kwa neema tu, Uzima ulio nao ni kwa Neema tu, karama uliyo nayo ni kwa neema tu, zaidi sana hata Wokovu ulio nao ni kwa Neema tu na wala si kwa matendo yako.

Waefeso 2:8 “Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu;

9  wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu”

Na zaidi ya yote pia Roho Mtakatifu tunampokea kwa Neema..

Wagalatia 3:2 “Nataka kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani”

Omba Neema!!.. omba Neema!, Omba Neema…usitumainie matendo yako..

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

NEEMA YA MUNGU KWA MARIAMU.

FUNDISHO KUU LA NEEMA YA MUNGU KWETU.

Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?

Nini tofauti ya Uwezo na Uweza kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

HISTORIA YA BIBLIA YA KING JAMES, INA FUNZO GANI KWETU?

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Karibu tujifunze biblia, leo tujikumbushe historia fupi ya tafsiri ya biblia ya King James.

King James au kwa Kiswahili “Mfalme Yakobo” wa Uingereza, alikuwa ni mmoja wa wafalme ambao hawakuwa maarufu sana kwa wakati wao. Lakini alikuja kufanya jambo la kishujaa ambalo mpaka leo yupo katika rekodi ya watu maarufu na wakihistoria waliowahi kutokea Uingereza.

Mwaka 1604 baadhi ya wanazuoni wa Kiprotestanti (Wapuriti) walipendekeza kuchapishwa kwa tafsiri mpya ya biblia, kuchukua nafasi ya ile iliyokuwepo ambayo ilijulikana kama tafsiri ya “Geneva”. Tafsiri ya Geneva ndio ilikuwa tafsiri ya kwanza kwa lugha ya kiingereza kuchapichwa huko Ulaya, iliyotumiwa na Waprotestanti.

Upungufu wa tafsiri hiyo ya Geneva, ni kwamba ilikuwa ina “maoni ya ziada” yaliyoongezwa ili kutilia mkazo kile kilichoelezwa katika biblia, na maoni hayo ya mkazo, yalilenga sana kuwakosoa viongozi wa kisiasa na kidini.

Hivyo baadhi ya waprotestanti hao, jamii ya Wapuriti, walitoa mapendekezo yao kuchapiswa biblia nyingine ambayo itaondoa hayo maoni ya watu na kuiacha yenyewe kama yenyewe, pasipo maoni ya watu. Na pia chapisho hilo litalenga pia kuitafsiri biblia nzima katika kingereza kizuri zaidi.

Wapuri hao baada ya kutoa hilo pendekezo, walilifikisha kwa Mfalme ambaye alikuwa anaitwa YAKOBO (King James).

Kikawaida wafalme wengi huwa hawajihusishi na masuala ya kiimani, zaidi sana huwa wanayapinga, lakini ikawa ni kinyume chake kwa huyu King James, badala ya kulipinga au kulikosoa wazo lao, yeye alikubali biblia mpya hiyo ichapishwe na tena akatoa sehemu kubwa ya hazina ya utajiri wake kusaidia zoezi zima la utafsiri mpya.

Tafsiri hiyo mpya ya Biblia hiyo mpya iliandaliwa kwa kipindi cha Miaka 7, na wanazuoni zaidi ya 47 kutoka kila mahali, Uingereza.  Walianza kuitafsiri biblia upya kutoka katika Lugha ya kigiriki kwa agano la kale, na kiaramu kwa agano jipya. Walipomaliza kuitafsiri biblia yote wakaiita biblia hiyo KING JAMES BIBLE, Yaani biblia ya Mfalme Yakobo.

Baada ya kumaliza kutafsiri, kazi ile ilionekana kama dhaifu sana, lakini muujiza ni kwamba ndani ya kipindi kifupi, tafsiri hiyo mpya ya King James, ilianza kupendwa na watu wengi, kwani haikuwa na mchanganyiko wa maoni ya watu, na ilikuwa na kiingereza kikamilifu na haikuongeza neno wala kupunguza Neno.

Kufikika Mwaka 1611, tafsiri ya King James ilikuwa imeshasambaa katika bara la Ulaya yote, na baadaye duniani kote. Na tangu mwaka huo wa 1611 mpaka leo karne ya 21 ndio kitabu kinachoongoza kwa kuuzwa kuliko vitabu vyote duniani, na kumfanya Mfalme James, kuendelea kushika nafasi za juu za watu maarufu waliowahi kutokea.

Ni nini tunajifunza katika Mfalme Yakobo (King James).

Ni Mfalme ambaye alikuwa na hofu ya Mungu, ingawa hakuwa mkamilifu sana, lakini alitii na kuheshimu pendekezo la watu wa Mungu, ambao walimshauri aridhie ombi la kukitakasa kitabu kitakatifu cha Bwana, kwa kuondoa maoni ya watu na kukiacha kisafi kama kilivyo.

King James, aliruhusu pendekezo hilo pasipo kujua kuwa litaenda kuubadilisha ulimwengu. Mpaka Leo hii tafisiri bora ya kiingereza inayosomwa na wengi ni tafsiri hiyo ya King James. Na kwa kufanya hivyo Bwana akampa King James kumbukumbu la daima.

Ni wafalme wengi na mamalkia wengi wamekuja na kupita, wameandika vitabu lakini vitabu vyao vimepita, lakini kazi ya James mpaka leo inadumu na itaendelea kudumu hivyo mpaka Kristo anarudi.

Na sisi tukitaka tupate kumbukumbu la kudumu hatuna budi kumfikiri Mungu kwanza katika maisha yetu, haijalishi ngazi tuliyopo tuwe maskini, matajiri, tuwe wafalme tuwe watu wa kawaida.. tukimjali Bwana kwa mioyo yetu yote, na akili zetu zote na nguvu zetu zote, bali tuna kumbukumbu kubwa mbele zake si tu katika maisha haya, bali hata yale yajayo.

Malaki 3:13 “Maneno yenu yamekuwa magumu juu yangu, asema Bwana. Lakini ninyi mwasema, Tumesema maneno juu yako kwa namna gani?

 14 Mmesema, Kumtumikia Mungu hakuna faida; na, Tumepata faida gani kwa kuyashika maagizo yake, na kwa kwenda kwa huzuni mbele za Bwana wa majeshi? 

15 Na sasa twasema ya kwamba wenye kiburi ndio walio heri; naam, watendao uovu ndio wajengwao; naam, wamjaribuo Mungu ndio waponywao.

 16 Ndipo wale waliomcha Bwana waliposemezana wao kwa wao. Naye Bwana akasikiliza, akasikia; na kitabu cha ukumbusho kikaandikwa mbele zake, kwa ajili ya hao waliomcha Bwana, na kulitafakari jina lake.

 17 Nao watakuwa wangu, asema Bwana wa majeshi, katika siku ile niifanyayo; naam, watakuwa hazina yangu hasa; nami nitawaachilia, kama vile mtu amwachiliavyo mwanawe mwenyewe amtumikiaye”.

Bwana atubariki.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Dina akatoka kuwaona binti za nchi. (Mwanzo 34:1)

Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

WHAT DOES IT MEAN TO BE A CHRISTIAN?

Je ni viatu gani Musa aliambiwa avivue?  Vya mwilini au vya rohoni? (Kutoka 3:5).

NI UTUKUFU WA MUNGU KUFICHA JAMBO.

Rudi nyumbani

Print this post