Title September 2023

Fahamu Maana ya Mithali 18:13 Yeye ajibuye kabla hajasikia, Ni upumbavu na aibu kwake.

Maelezo ya Mithali 18:13 Yeye ajibuye kabla hajasikia,  Ni upumbavu na aibu kwake.


Hekima inatufundisha tusiwe watu wa kujibu au kuzungumza kabla hatujasikia habari yote au taaarifa yote na kuitafakari kwanza..Kwamfano mwenzako anazungumza jambo Kisha wewe ukaingilia kati na kutaka kujibu, hoja ambayo haijakamilika..Matokeo yake hapo ni Nini kama sio kutoa majibu yasiyosahihi?. Au ambayo hayajakamilika?

Ndio hapo anasema ni upumbavu na aibu kwake. 

Hii imeathiri hata kusambaa Kwa taaarifa za uongo. Mtu atasikia jambo, kwasababu Hana taaarifa nalo vizuri, atatoka muda huo huo na kwenda kumpasha mwingine, na yule mwingine atampasha mwingine..Hivyo taaarifa za uongo huzagaa Kwa upesi sana. Ndivyo ambavyo hata waandishi wa habari ambao hawawi makini wanavyosambaza habari ambazo bado hawajazifanyia uchambuzi yakinifu. Na matokeo yake husababisha matatizo makubwa katika jamii. 

Mafarisayo na wayahudi walimpinga Yesu kwasababu walikuwa ni watu wa kupokea tu taaarifa ambazo hawazitafiti, walisikia Yesu anatokea Nazareti, wakahitimisha amezaliwa Nazareti, wengine wakamwita Msamaria. Lakini kama wangesubiri kutuatilia Kwa ukaribu mawazo Yao yangebadilika, na wasingekuwa wapumbavu kama tunavyowasoma kwenye biblia.

Hata wakati alipokuwa anazungumza nao, hawakutaka kusikiliza mpaka mwisho ni Nini Bwana anataka kuwaambia, kwamfano Kuna wakati aliwaambia, mtu akilishika Neno lake hataonja mauti milele. Lakini wao Hawakutaka ufafanuzi alimaanisha Nini.. hapo hapo wakarukia na kumwita ana Pepo;Kwa kauli Ile.

Yohana 8:52-53

[52]Basi Wayahudi wakamwambia, Sasa tumeng’amua ya kuwa una pepo. Ibrahimu amekufa, na manabii wamekufa; nawe wasema, Mtu akilishika neno langu, hataonja mauti milele.

[53]Wewe u mkuu kuliko baba yetu Ibrahimu, ambaye amekufa? Nao manabii wamekufa. Wajifanya u nani?

Wakati mwingine aliwaambia livunjeni hili hekalu,nami nitalisimamisha baada ya siku tatu. Wakairukia hiyo kauli bila kusubiria maelezo  yake , ndio ikawa habari ya mji mzima Kuna mtu kasema anaweza kulijenga Kwa siku 3 hekalu lililojengwa Kwa miaka 46. Kumbe hawakujua Kristo anazungumzia habari ya mwili wake.(Yohana 2:20)

Biblia inatuasa tuwe wepesi wa kusikia, na si wa kusema; Ina faida nyingi.

Yakobo 1:19

[19]Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika;

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

HAUWEZI KURUKA MADARASA YA MUNGU!

KUOTA UPO UCHI.

FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Maana ya Mithali 19:15 ‘Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito;

Rudi nyumbani

Print this post

Hii ni Maana ya Mithali 18:18 Kura hukomesha mashindano;

Fahamu Maana ya;

Mithali 18:18 Kura hukomesha mashindano;  Hukata maneno ya wakuu.


Kupiga kura ni Moja ya njia ambayo ilitumika kuleta suluhisho lenye utata, na wakati mwingine kuchagua viongozi/wamiliki. Pitia hapa ujue zaidi kuhusu kura zilivyopigwa zamani za biblia…>> Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo;

Na Mungu wakati mwingine aliingilia kati na kuleta majibu yake sahihi kwa kupitia njia hiyo. Kwamfano wakati ule Yona anamkimbia Mungu, Hali ilipochafuka kule baharini, utaona wale watu walipiga kura, ili kujua sababu ya mambo yale ni nani na Ile kura ikamwangukia Yona.

Mitume wa Bwana baada ya kuomba, kuhusu mrithi wa nafasi ya Yuda wakapiga kura katika ya wale wanafunzi wawili, nayo ikamwangukia Mathiya, na likawa kweli ni chaguo la Mungu.(Matendo 1:15-19),

Hata wakati wa nchi ya Israeli kugawanywa . Kura zilitumika kuamua nani akae wapi, na nani arithi wapi (Hesabu 26:55).

Hivyo kupiga kura ilikuwa ni mojawapo ya njia kuleta jibu lisilokuwa na upendeleo. Au lililoegemea upande Fulani mmoja. Na kwa kufanya hivyo malalamiko mengii yalikomeshwa kwasababu maamuzi hayakuamuliwa na upande wowote ule.

Ndio maana ya hili andiko

Mithali 18:18

[18]Kura hukomesha mashindano;  Hukata maneno ya wakuu.

Hata kipindi Cha sasa njia ambayo hutumiwa kuchagua viongozi wengi ulimwenguni Huwa ni ya  kura.  Isipokuwa hii siyo ya kurusha SHILINGI, au kete angani  inayomwangukia mmojawapo ndio anakuwa kiongozi..hapana Bali ni kuruhusu Kila mmoja kutia maoni yake..Kisha zinahesabiwa na yule mwenye nyingi hupewa. Na hivyo hakuna malalamiko. 

Tofauti na Ile mtu atawadhwe tu Moja Kwa moja kuwa kiongozi, Hiyo huleta ukakasi mwingi.

Hivyo ni kutufundisha kua Bwana anaouwezo wa kuingilia kura zipigwazo na kuleta majibu yake sahihi..hususani pale anaposhirikwa Kwa maombi, na kama hakusema Kwa njia nyingine ya Moja Kwa moja.

Bwana akubariki

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?

MKUU WA ANGA.

Mzushi ni nani kibiblia? (Tito 3:10).

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

Biblia inakataza kuapa kabisa, lakini kwanini watu wanaapa mahakamani na katika vifungo vya ndoa?

Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake

Nini maana ya Mithali 27:21  inaposema “mtu hujaribiwa kwa sifa zake?”

Rudi nyumbani

Print this post

HAZINA YAKO ILIPO, NDIPO UTAKAPOKUWAPO NA MOYO WAKO.

Hakuna namna utautenganisha “Moyo” na “hazina”.. vitu hivi vinaenda pamoja!.(ni sawa na miguu na mwili,..mahali miguu ilipo na mwili upo, miguu haiwezi kuwa mahali pengine na mwili mahali pengine) Vile vile Moyo wa mtu na hazina yake, vinaenda pamoja…Pale mtu alipojiwekea hazina, ni lazima (akili yake yote na fikra zake na hisia zake na mawazo yake yatakuwa huko).

Ndio maana mtu aliyejiwekea hazina kubwa ya mali za kidunia, halafu mali zile zikapotea zote ghafla, ni rahisi mtu huyo kuchanganyikiwa au kupoteza maisha maisha kabisa!.

Kwanini?..Kwasababu Moyo wake wote (fikra, mawazo, akili, malengo, uzima, hadhi) vilikuwepo katika mali zile, na sasa hana tena!, hata maisha kwake yanakuwa hayana maana tena!. Ndivyo ilivyo, kwamba Moyo siku zote unafuata hazina ilipo!, na unaishi kutokana na hazina mtu alizonazo. Ndivyo moyo wa mtu ulivyoumbwa!..

Vile vile mtu anayejiwekea hazina mbinguni, ni lazima fikra zake, mawazo yake, akili yake, malengo yake yote yatakuwa kule mbinguni hazina yake ilipo.

Sasa Bwana Yesu alitufundisha kanuni ya kuielekeza Mioyo yetu mbinguni, kwamba si kwa kuomba tu! Bali kwa kujiwekea hazina kule mbinguni,..kwanini?…kwasababu tutakapojiwekea hazina kule juu mbinguni basi mioyo yetu (yaani fikra, fahamu, akili, mawazo na hisia) zitaelekea kule Mbinguni, bila shuruti!.

Sasa swali, tunajiwekeaje hazina juu mbinguni?.. yeye mwenyewe (Bwana Yesu) alitufundisha kanuni katika Luka 18:18-22

Luka 18:18 “Tena, mtu mkubwa mmoja alimwuliza, akisema, Mwalimu mwema, nifanye nini ili nipate kuurithi uzima wa milele?

19  Yesu akamwambia, Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, naye ndiye Mungu.

20  Wazijua amri; Usizini, Usiue, Usiibe, Usishuhudie uongo, Waheshimu baba yako na mama yako.

21  Akasema, Hayo yote nimeyashika tangu utoto wangu

22 Yesu aliposikia hayo alimwambia, Umepungukiwa na neno moja bado; viuze ulivyo navyo vyote, ukawagawanyie maskini, NAWE UTAKUWA NA HAZINA MBINGUNI; kisha, njoo unifuate”.

Na tena anarudia maneno kama hayo hayo katika Luka 12:32-34

Luka 12:32  “Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme.

33  Viuzeni mlivyo navyo, mtoe sadaka. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, AKIBA ISIYOPUNGUA katika mbingu, mahali pasipokaribia mwivi, wala nondo haharibu.

34  KWA KUWA HAZINA YENU ILIPO, NDIPO ITAKAPOKUWAPO NA MIOYO YENU”.

Umeona?.. Kumbe kanuni ya kujiwekea hazina mbinguni ni kumtolea Mungu!..

Kwanini?.. Kwasababu tunapomtolea Mungu vile tulivyo navyo, mawazo yetu yatakuwa siku moja kwenda kupata thawabu mbinguni!, fikra zetu zitakuwa siku moja kwenda kuona miji mizuri tuliyoandwaliwa, mawazo yetu yatakuwa siku moja kwenda kuvikwa taji……hivyo muda wote tutakuwa tunafakari tu yaliyo ya juu na huko ndiko mioyo yetu itakapokuwepo!.

Ndio maana utaona watu wanaojitoa kwa Mungu kuanzia miili yao, mpaka mali zao, muda wote wanawaza unyakuo utakuwa lini?, muda wote wanawaza Kristo anakuja lini?.. ni kwanini wanakuwa hivyo?, si kwamba wanajilazimisha kuwa hivyo, ni kwamba tayari mioyo yao ipo mbinguni kwasababu wamejiwekea hazina huko.

Hii ni kanuni rahisi kabisa ya kuhamisha mioyo yetu kutoka kutafakari MAMBO YA CHINI na kuanza kutafakari MAMBO YA JUU!.

Ukitaka uwe mtu wa kutafakari mambo ya mbinguni sana, mtolee Mungu kuanzia muda wako, akili yako, mwili wako, ufahamu wako na hata vitu vyako!.. Hapo moyo wako wenyewe tu utaanza kuelekea mbinguni bila hata kutumia nguvu nyingi!,. Utajikuta tu unaanza kutamani kumwona Yesu, utajikuta unatamani ile siku ya mwisho ifike n.k

Laakini kinyume chake usipofanya hivyo na ukajitumainisha katika kujiwekea hazina katika mambo ya ulimwengu, basi fahamu kuwa moyo wako utaelekea tu katika mambo ya ulimwengu hata kama hupendi!.

Wakolosai 3:2 “Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Hazina za gizani ni zipi? (Isaya 45:3).

YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.

Nondo ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

UKIOKOKA, JIANDAE KUPITISHWA USIPOPATAZAMIA.

Yeshuruni ni nani katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Je biblia inatufundisha tuwe wapole kiasi? (Wagalatia 5:22-23)

Swali: Biblia inatufundisha katika Wagalatia 5:23  kuwa “tuwe wapole kiasi”, sasa napenda kujua mtu utakuwaje mpole kiasi.

Jibu: Tusome,

Wagalatia 5:22  “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,

23  UPOLE, KIASI; juu ya mambo kama hayo hakuna sharia”.

Hapa biblia haisemi kuwa tunda la Roho Mtakitifu kuwa ni “Upole kiasi” kana kwamba “upole unapaswa uwe na kiasi”…. La! Bali inasema tunda la Roho ni “Upole”, halafu “Kiasi”… hayo ni maneno mawili yaliyotengenishwa na alama ya mkato.

Maana yake “Upole” ni kitu kingine na “Kiasi” ni kitu kingine. Ikiwa na maana kuwa Tunda la Roho “Upole ulio wote” na sio upole kiasi.

Biblia inatufundisha tuwe watu wapole kama Hua (Njiwa).

Mathayo 10:16  “Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwa-mwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua

Hua ni ndege mpole sana ndio maana Roho Mtakatifu alitumia umbile la Hua kushuka juu ya Bwana Yesu wakati ule alipobatizwa (Mathayo 3:16)... Na maandiko yanazidi kutufundisha kuwa Bwana Yesu ni Mpole..

Mathayo 21:5 “Mwambieni binti Sayuni Tazama, mfalme wako anakuja kwako, MPOLE, naye amepanda punda, Na mwana-punda, mtoto wa punda”.

Soma pia, Mathayo 11:29, utaona sifa hiyo ya Bwana ya upole ikitajwa..

Na sisi pia ni lazima tuwe na sifa hiyo ya “Upole” kama ishara mojawapo ya kuwa na Roho Mtakatifu ndani yetu… shetani kaligeuze Neno hili la Upole na kuweka “Upole kiasi” ili kuchochea ubaya ndani ya watu.. Kwamba ni vizuri kuwa wapole lakini tusiwe wapole sana, tuwe wapole tu kiasi!. Huo ni uongo wa adui!.

Na kumbuka kuna tofauti ya “upole” na “unyonge”. Biblia haitufundishi kuwa wanyonge, bali kuwa wapole, Mtu mpole ni yule ambaye ana uwezo wote wa kutumia ukali lakini hautumii!, kama alivyokuwa Bwana Yesu… Lakini mnyonge ni yule anayekuwa analazimika kuwa hivyo mpole kutokana tu na mazingira..na akitoka katika hayo mazingira basi tabia yake ya ubaya na ukali usio na maana na vurugu inajidhihirisha.

Bwana atusaidie .

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Upole ni nini?

KIASI NI NINI KATIKA UKRISTO?

BWANA UNIJULISHE MWISHO WANGU.

Je Paulo na Petro walishindania nini? (Wagalatia 2:11).

Je ni kweli Musa alikuwa mtu mpole kuliko wote duniani?

Rudi nyumbani

Print this post

Uele ni nini katika biblia? (Zaburi 91:6)

Jibu: Tusome kuanzia mstari wa 5..

Zaburi 91:5 “Hutaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana,

6 Wala tauni ipitayo gizani, Wala uele uharibuo adhuhuri”.

“Uele” ni janga linaloleta mauti linaloweza kumpata mtu.. ajali ya gari ni mfano wa Uele, Ajali ya kuzama kwenye maji ni mfano wa “Uele”, janga la kuungua moto mpaka kufa ni mfano wa “Uele”.

Maandiko yanatufundisha kuwa wote wamtumainio Bwana, na kumkimbilia na kumfanya kuwa ngome na msaada, hawatakuwa na hofu na majanga hayo, kwani Mungu ni ngome ya wote wanaomcha, naye ndiye awaokoaye na majanga.

Zaburi 121:4 “Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi, Yeye aliye mlinzi wa Israeli.

5 BWANA ndiye mlinzi wako; BWANA ni uvuli mkono wako wa kuume.

6 Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku.

7 BWANA atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako.

8 BWANA atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele”.

Je una hofu na UELE?..Mpokee Yesu kwa kutubu dhambi na kujazwa Roho Mtakatifu, naye atakupa furaha nawe utaishi maisha ya raha na ya utulivu.

Zaburi 127:2 “……Yeye humpa mpenzi wake usingizi”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

KUOTA AJALI, KUNAMAANISHA NINI?

Je! Mungu anasababisha ajali au Majanga?

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Kaniki ni nini katika biblia? (Yeremia 8:21).

JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?

Rudi nyumbani

Print this post

Maganjo kibiblia? (Walawi 26:31)

Jibu: Tusome,

Ganjo” ni mahali palipoharibika.. Jengo lililoharibika linaitwa “Ganjo” yakiwa mengi yanaitwa “maganjo”, mji ulioharibiwa aidha kwa vita au kwa janga fulani pia unaitwa “Ganjo”.

Katika biblia neno hili limeonekana mara kadhaa..

Walawi 26:30 “Nami nitapaharibu mahali penu palipoinuka, na kuziangusha sanamu zenu za jua, nami nitaitupa mizoga yenu juu ya mizoga ya sanamu zenu; na roho yangu itawachukia. 

31 Nami nitaifanya MIJI YENU IWE MAGANJO, na mahali penu patakatifu nitapatia ukiwa; wala sitasikia harufu ya manukato yenu yapendezayo. 

32 Nami nitaitia hiyo nchi ukiwa; na adui zenu watakaokaa huko wataistaajabia”

Tusome pia…

Ezekieli 29:12 “Nami nitaifanya nchi ya Misri kuwa ukiwa, kati ya nchi zilizo ukiwa, na miji yake, kati ya miji iliyoharibika, ITAKUWA MAGANJO muda wa miaka arobaini; nami nitawatawanya Wamisri kati ya mataifa, nami nitawatapanya kati ya nchi mbalimbali.”

Neno hili pia unaweza kulisoma katika mistari ifuatayo likiwa na maana hiyo hiyo..Walawi 26:33, 2Nyakati 34:6, Ayubu 3:14, Isaya 6:11, 7:19, Yeremia 4:7, Ezekieli 6:14, 36:38, na Amosi 9:14.

Vile vile hii dunia siku moja itafanyika kuwa “GANJO”, kutokana na dhambi!.. Bwana ataiharibu kwa moto kama alivyoiharibu nyakati za Nuhu, kwa maji.

2Petro 3:6 “kwa hayo dunia ile ya wakati ule iligharikishwa na maji, ikaangamia.

7 Lakini mbingu za sasa na nchi zimewekwa akiba kwa moto, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu”.

Je umeokoka? Kama bado, saa ya wokovu ni sasa, tupo mwisho wa nyakati.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Agano ni nini? na kuna aina ngapi za maagano?

Miji ya Tiro na Sidoni ni miji gani kwasasa?

Kama Malkia Esta alijipamba je! Kuna ubaya gani wanawake wa wakikristo wa leo kujipamba?.

TAA YA MWILI NI JICHO,

VICHEKESHO NA UTANI MADHABAHUNI

Rudi nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 19:15 ‘Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito;

Fahamu Maana ya Mithali 19:15 “Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; Na nafsi yake mvivu itaona njaa”.


Mara nyingi Sulemani kwa hekima ya Roho aliongozwa kuona uhusiano uliopo kati ya uvivu na umaskini. Kama tu kinyume chake, sehemu nyingine alivyoweka uhusiano kati ya bidii na utajiri(Mithali 10:4). Vivyo hivyo uvivu na umaskini havipishani.

Na kama anavyosema hapo, uvivu humpeleka mtu katika usingizi, lakini sio usingizi tu bali ule mzito, Kwasababu gani? Ni kwasababu mwili haupo katika hali ya kujishughulisha, na hivyo utalala tu, na Bado utaendelea kulala siku baada ya siku.. Na matokeo yake kutokuzalisha chochote kinachoonekana, hatimaye, umaskini unaingia.

Hivyo mstari huo unalenga Nyanja mbili. Ya kwanza ni ule uvivu wa mwilini, na ya pili ni ule uvivu wa rohoni.

Uvivu wa mwilini:

Mungu katuumbia kufanya kazi, watu wote (ikiwemo watakatifu). Maana yake ni kuwa ikiwa huna huduma yoyote ya madhabahuni Bwana amekuitia, ambayo inakufanya utumike muda wote hapo. Ni sharti ufanye kazi. Mtume Paulo alilionya kanisa juu ya watu ambao hawafanyi kazi kwamba ni sharti wajishughulishe ili wapate na kitu cha kuwagawia na wengine (2Wathesalonike 3:10)

Uvuvu wa rohoni:

Lakini pia Uvuvi wa rohoni. Mtakatifu anapokuwa mvivu, kusoma Neno, yaani muda wa Neno anakwenda kutazama filamu, anakwenda kijiweni kucheza drafti,.Anakuwa  mvivu kuomba, Unapofika huo muda tu anaona usingizi ni bora kuliko kuomba,.Au Mtakatifu hataki kushuhudia habari za Kristo kwa wengine, anasema jua kali. Sasa mtu huyo anajiandaa kuwa maskini kiroho. Yaani atakuwa katika wokovu usiokuwa na matunda, ukuaji wake wa kiroho utakuwa hafifu, Neema ya Mungu haitatenda kazi kwa wingi juu yake, na hivyo atakosa mema mengi ya Mungu katika safari yake wa wokovu hapa duniani.

Uvuvi wowote, una hasara, kwahiyo tuuweke katika orodha ya maadui zetu wa imani.

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Kwanini kila nikitaka kusali naingiwa na uvivu?

Amwimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Mtu asiye na akili ni nani kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 19:11 Busara ya mtu huiahirisha hasira yake.

Fahamu Maana ya;

Mithali 19:11 Busara ya mtu huiahirisha hasira yake; Nayo ni fahari yake kusamehe makosa.


Mstari huo unatufundisha mtu aliyejaa  “Busara” moyoni ni mtu wa namna gani..

Anaeleza ni Yule ambaye anaouwezo wa kughahiri hasira yake, na pia kupenda kusemehe makosa. Ambayo ndio sifa ya Mungu, Aliyonayo, soma;

Kutoka 34:6 Bwana akapita mbele yake, akatangaza, Bwana, Bwana, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli;  7 mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba zao, na wana wa wana wao pia, hata kizazi cha tatu na cha nne.

Hivyo na sisi hatuna budi kutokuwa watu wa kukasirika haraka, mpaka ikaleta athari nje, kwamfano umeumizwa na mke/mume wako, tunapaswa tujifunze kuachilia mara moja, lakini pia kusamehe, sio kuweka kinyongo, au uchungu moyoni. Au mtu amefanya kosa la kukuudhi ambalo anastahili adhabu, si vema kuwa wepesi wa kuadhibu bali kuahirisha hasira hizo kwasababu Mungu naye anatusamehe makosa yetu, hatuadhibu kila kosa.

Bwana alisema kusamehe kwetu hakupaswi kuwe na ukomo, alitumia lugha ya hata ‘saba mara sabini’ kwa siku(Mathayo 18:22). Kuonyesha kuwa kusamehe kwetu kunapaswa kuwe endelevu. Ili  tufikie hatua ya Kuona ‘fahari’ katika uwezo wa kusamehe, zaidi ya kuona fahari katika uwezo wa ‘kupata vitu’. Yaani tuhesabu ni watu wangapi tumewasamehe, hapo ndio iwe furaha yetu. Na kwamba tuipime busara yetu kwa kiwango cha kuiharisha hasira zaidi ya uwezo wa ‘kuwa na maneno mengi ya hekima’.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

NIFANYE NINI NIWEZE KUDHIBITI HASIRA?

Mungu anatufundisha kusamehe mara saba sabini, ila Kwanini yeye hakumsamehe Adamu alipoasi?

TAFUTA HEKIMA, MAARIFA, UFAHAMU NA BUSARA.

BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, LAKINI BWANA NI MWINGI WA HASIRA.

KWANINI TUWE WENYE BUSARA KAMA NYOKA?

SIKU YA HASIRA YA BWANA.

Wivu ni nini na kuna aina ngapi za Wivu?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mithali 24:11 Uwaokoe wanaochukuliwa ili wauawe?

SWALI: Nini maana ya Mithali 24:11 Uwaokoe wanaochukuliwa ili wauawe; Nao walio tayari kuchinjwa uwaopoe.

JIBU:  Mstari huu una maana mbili,

Mana ya kwanza ni uhai kama ‘uhai’ alionao mwanadamu yoyote,

Maana yake ni kuwa uonapo, mtu asiyekuwa na hatia, amepangiwa njama za kuuliwa, au ndio anakaribia kufa, na wewe unaowezo wa kumsaidia huna budi kufanya hivyo wala usijifanye kama hiyo sio biashara yako.

Ni mfano wa Yule mtu aliyevamiwa na wanyang’anyi ambaye Bwana Yesu alimtolea mfano, akasema mlawi alimpomwona akapita kando, kuhani naye alipomwona akapita kando, lakini Yule msamaria akamuhurumia, akamtibu, akaokoa uhai wake. Na Yesu akasema huo ndio Upendo.(Luka 10:25-37)

Ni sawa na wakati ule Paulo amepangiwa njama na wayahudi wamvizie auawe, lakini mjomba wake alipogundua alikwenda kumjuza akida wa kikosi (Matendo 23:12-22). Huyo amemwopoa aliyekaribu na kuchinjwa.

Ni sawa na Mordekai alichofanya kwa Mfalme, Ahusuero, wale watu walipopanga njama ya kumuua akaenda kuwasemelea (Esta 6:1-12),. Ni sawa na Yonathani, alivyomtunza Daudi dhidi ya upanga wa baba yake Sauli ili asiuliwe. Hivyo hawa wote, walilitambua andiko hili, na wala hawakuogopa kutoa siri, za wale waliokusudia mabaya juu ya maisha ya wengine.

Hata leo, vifo vingi vya kikatili, vingeweza kuzuilika kwa sehemu kubwa, endapo baadhi ya wanaojua matukio hayo wangetoa taarifa mapema. Kwamfano utaona mtu anawekewa sumu kwenye chakula, wewe unayejua, ni wajibu wako kutoboa siri hiyo, ili uutunze uhai wa mtu. Utaona mwizi anapigwa, huna budi kuripoti polisi mapema maadamu jambo hilo lipo ndani ya uwezo wako, ili askari waje kumkamata wampe wao adhabu stahiki, lakini ukipita ukasema hainihusu, atachomwa moto. Lakini kumbuka uhai unathamani, hata wa mtu aliye mbaya, unathamani nyingi.

Lakini ukisema hainuhusu, Utakuwa unajipunguzia pia rehema nyingi kwa Mungu,  ndio maana mstari unaofuata unasema;

Mithali 24:11 “Uwaokoe wanaochukuliwa ili wauawe; Nao walio tayari kuchinjwa uwaopoe.  12 Ukisema, Sisi hatukujua hayo; Je! Yeye aipimaye mioyo siye afahamuye? Naye ailindaye nafsi yako siye ajuaye? Je! Hatamlipa kila mtu sawasawa na kazi yake?”

Hivyo penda uhai, pia tunza uhai wa watu, popote pale uonapo unahatarishwa. Usiwe mzito kusaidia.

Lakini  maana ya pili ya mstari huu  ni ule Uhai wa rohoni.

Wapo watu ambao ibilisi, anakaribia kuwameza, na ukiwaacha ndani ya kipindi kifupi hakika wataangamia kabisa kiroho. Wengine wanakaribia kufa kwasababu ya huzuni mioyoni mwao, kukata tamaa, kwasababu ya dhiki na magonjwa, wengine wanakaribia kuzama katika ushirikina, wengine kwenye imani potofu ambazo zinakwenda kuwaua roho zao n.k. Hivyo makundi kama haya, unapoyaona, mwelekeo wao wewe kama mkristo uliyesimama huna budi kuwasaidia ili waokoke, wasipotelee katika mauti ya roho zao, na kwenye minaso ya adui mfano wa Yuda. Wala usisime hiyo sio shughuli yangu.

Yuda 1:22  “Wahurumieni wengine walio na shaka, 23  na wengine waokoeni kwa kuwanyakua katika moto; na wengine wahurumieni kwa hofu, mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili.

Hivyo tutunze Uhai, wa mwili na Roho za watu wa Mungu, naye Bwana atatunza na wetu.

Bwana akubariki

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

“Kinga kilichotolewa motoni “Kinafunua nini kibiblia?

Biblia inamaanisha nini inaposema “Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake”?

Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

HAKUNA MTU ANIONDOLEAYE, BALI MIMI NAUTOA MWENYEWE

Rudi nyumbani

Print this post

UKIMBIE UASHERATI (USIJIUNGAMANISHE NA miungu)

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu libarikiwe.

Karibu tujifunze biblia Neno la Mungu wetu lililo taa ya miguu yetu na mwanga wa njia yetu.

Kuna mambo makuu mawili ambayo yanaweza KUMUUNGANISHA MTU MOJA KWA MOJA NA USHIRIKA WA MAPEPO.

Na mambo hayo ni SADAKA NA UASHERATI. Haya mambo mawili yanaenda pamoja, ndio maana wanaoenda kwa waganga utaona wanaambiwa watoe sadaka, au wafanye zinaa, lengo la zile sadaka si kuimairisha maisha ya wale wanaozitaka (waganga), wala lengo la ile zinaa si kuwafurahisha hao waganga bali ni kumuunganisha yule mtu na madhabahu ile!.  

Sasa nataka tuangalie mfano mmoja wa kwenye biblia wa watu waliojiunganisha na madhabahu za mashetani kwa njia hizo mbili; (MATOLEO PAMOJA NA UASHETANI). Na hao si wengine Zaidi ya Wana wa Israeli walipokuwa katika safari yao ya kwenda Kaanani.

Tusome,

Hesabu 25:1 ”Basi Israeli akakaa Shitimu, KISHA WATU WAKAANZA KUZINI PAMOJA NA WANAWAKE WA MOABU; 

2 kwa kuwa waliwaalika hao watu WAENDE SADAKANI, sadaka walizowachinjia miungu yao; watu wakala chakula, wakaisujudu hiyo miungu yao. 

3 IKAWA ISRAELI KUJIUNGAMANISHA NA BAAL-PEORI; hasira za Bwana zikawaka juu ya Israeli.

4 Kisha Bwana akamwambia Musa, Watwae wakuu wote wa hao watu, ukamtungikie Bwana watu hao mbele ya jua, ili kwamba hizo hasira kali za Bwana ziwaondokee Israeli.

 5 Basi Musa akawaambia waamuzi wa Israeli, Waueni kila mtu watu wake waliojiungamanisha na Baalpeori”

Mstari wa 3 hapo unasema hao watu kajiunganisha na “Baali-peori” ambaye ni mungu wa wamoabi, na njia waliojiunganisha nayo ni UASHERATI na SADAKA!

Na adui njama aliyoitumia ni KUALIKA!.. walioalikwa tu! Lakini kumbe walikuwa wameshaandaliwa “wanawake wa kuzini nao” na kwa tamaa zao wakaingia kwa wanawake hao na kuzini, pasipo kujua kuwa kwa kitendo hiko tayari walikuwa wameshajiungamanisha na miungu yao, na hivyo hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli na Mungu akapigo kwa pigo kuu.

Ndugu, (kaka, dada,mama, baba) jihadhari na uasherati, jihadhari na Mialiko isiyo rasmi inayohusisha jinsia mbili tofauti.. Mtego wa shetani si wewe ufanye tu dhambi ya uzinzi, bali lengo lake ni wewe kukuunganisha na miungu na madhabahu ya huyo unayekwenda kuzini naye.

Na madhara ya kuunganishwa na mtu huyo ni kwamba zile “laana” na “hukumu” anazozibeba na wewe unazibeba..Ndicho kilichowatokea wana wa Israeli walipozini na wanawake wa Moabu, Taifa la Moabu lililaaniwa na wote waliozini na wale wanawake walibeba zile laana.

Ndivyo maandiko yanavyosema katika 1Wakorintho 6:15…

1Wakorintho 6:15  “Je! Hamjui ya kuwa miili yenu ni viungo vya Kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha!

16  Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja”.

Sasa inawezekana ulifanya hayo pasipo kujua, na hivyo ulijiungamanisha na madhabahu za kuzimu. Suluhisho la kwanza si kwenda kuombewa!… bali ni wewe kutubu! Kwa kumaanisha kutofanya machukizo hayo tena. Na baada ya kutubu, hatua inayofuata ni ubatizo sahihi na kisha kudumu katika Imani huku ukijitenga na uovu na vichocheo vyake vyote.

1Wakorintho 6:18 “Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

Sadaka ya Amani ilikuwaje?

MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.

Chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu ndio kipi? (Matendo 21:25).

Rudi nyumbani

Print this post