Title September 2023

MWAGA DAMU YAKO KWA AJILI YA BWANA.

Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tena tujifunze maneno ya uzima.

Kulikuwa na aina nne za wito ambao Bwana aliwaitwa mitume wake.

  1. Wito wa kawaida: Ambapo Bwana alipowaona mitume aliwaambia nifuate. Lakini hakukuwa na vigezo vyovyote, nyuma yake, au majumu Fulani ya lazima ya kuyafanya.(Yohana 1:35-51)
  2. Wito wa uanafunzi: Baadaye akaja kuwafanya kuwa wanafunzi wake, hapo ndipo aliwakuta na kuwaambia waache vyote kisha wamfuate, na akatoa na vigezo vyake, kwa wale wote waliotaka kuwa wanafunzi wake (Luka 14:25-35), Hivyo Bwana alikuwa nao wengi zaidi ya wale 12
  3. Wito wa kitume: Baadaye akawachagua mitume kati ya wanafunzi wake wengi. Yaani watu ambao atawatuma kwa kazi maalumu. Ndio hapo wakapatikana 12
  4. Wito wa mashahidi: Lakini mwisho akawachagua mashahidi wake, Huu ndio wito wa juu sana na wa mwisho, ambao Bwana aliwakusudia mitume wake, akawapa siku ile aliyokuwa anapaa.

Matendo 1:8  Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi

Sasa nini maana ya kuwa SHAHIDI? Kuwa shahidi maana yake ni kuwa tayari kupitia mateso au kumwaga damu yako kwa ajili ya kumtetea Yule anayekutuma. Hivyo mtu yoyote aliyemwaga damu yake, kwa ajili ya Yesu huyo ni SHAHIDI. Hivyo mitume walijua kabisa hatma yetu ni kumwaga damu tu, huko mbeleni. Na watu kama hawa wanakuwa na nafasi ya juu sana, mbele ya Kristo siku ile watakapofika mbinguni, kwasababu wanakuwa wamepitia sehemu ya mapito yaleyale aliyoyapitia Bwana wao hapa duniani.

Leo tutatazama aina nne(4), za mashahidi wa Kristo. Na wewe pia utajipima upo wapi kati ya hawa na kama haupo popote basi, ufanye bidii uwe katika wingu hili la Mashahidi wa Yesu.

Aina nne (4), za Mashahidi wa Yesu.

1) Wanaoteswa na kupigwa na kuuliwa kwa ajili ya Bwana au injili:

2Wakorintho 11:23  “Wao ni wahudumu wa Kristo? (Nanena kiwazimu), mimi ni zaidi; katika taabu kuzidi sana; katika vifungo kuzidi sana; katika mapigo kupita kiasi; katika mauti mara nyingi. 24  Kwa Wayahudi mara tano nalipata mapigo arobaini kasoro moja. 25  Mara tatu nalipigwa kwa bakora; mara moja nalipigwa kwa mawe; mara tatu nalivunjikiwa jahazi; kuchwa kucha nimepata kukaa kilindini”.

Hata sasa, wapo watu wanateswa kwa namna mbalimbali, wengine wanamwaga damu kwa mapigo, watu kama hawa ni mashahidi wa Bwana. Sawa tu wale mitume wake.

2) Wanaooponza/ wanaohatarisha maisha yao kwa ajili ya Bwana au injili.

Hili ni kundi la pili ambalo linamwaga damu pia. Ijapokuwa haitaonekana kwa nje lakini rohoni Mungu anawaona kama wamemwaga damu kwa ajili ya ushuhuda wake. Kwamfano tukiangazia kile kisa cha Daudi ambapo wakati Fulani alitamani kunywa maji ya kisima kilichokuwa katikati ya maadui zake wafilisti. Lakini tunaona mashujaa wake watatu waliposikia, waliondoka kisirisiri, wakahatarisha maisha yao, kwenda katika marago ya wafilisti, na kuyachukua yale maji na kumletea Daudi, lakini Daudi hakuyanywa alisema ile ni damu yao na sio maji tena.

2Samweli 23:14 Naye Daudi wakati ule alikuwako ngomeni, na jeshi la Wafilisti wakati ule walikuwako Bethlehemu.  15 Daudi akatamani, akasema, Laiti mtu angeninywesha maji ya kisima cha Bethlehemu, kilicho karibu na lango!  16 Basi hao mashujaa watatu wakapenya jeshi la Wafilisti, wakateka maji kutoka kile kisima cha Bethlehemu, kilicho karibu na lango, wakayachukua, wakamletea Daudi; walakini yeye hakukubali kuyanywa, akayamimina mbele za Bwana.  17 Akasema, Hasha, Bwana, nisifanye hivi; je! Si damu hii ya watu hao waliohatirisha nafsi zao? Kwa hiyo hakukubali kuyanywa. Hayo ndiyo waliyoyafanya wale mashujaa watatu.

Umeona? Maji yamekuwa damu kwasababu ya hatari waliyoingia watu wale. Vivyo hivyo na wewe ujitoapo sadaka kwa ajili ya Bwana, unapohatarisha hata kazi yako, muda wako, ujana wako, ili tu umfanyie Mungu jambo. Ndugu hilo linakuwa sio jambo la kawaida bali ni damu yako unayoimwaga kwake.

Kulikuwa na Yule mwanamke alikwenda kumtolea Bwana sadaka ya senti mbili, lakini maandiko yanasema ndio iliyokuwa riziki yake yote, hajui kama kesho ataiona, pengine hata jana yake hakula. Si ajabu kwanini Bwana aliona ametoa zaidi ya wengine wote. Kwasababu kilichokuwa anakitoa ni uhai wake, na sio sadaka ya kawaida.

Jiulize nguvu zako unazozisumbukia daima unazimalizia kwa nani, je! Ni kwenye kujenga tu, ni  kuwekeza, ni kuvaa ni kula? Au ni nini? Vipi kwa Mungu wako, unampa sehemu ndogo tu, ni kweli utapata thawabu? Lakini je! Ulishawahi kufikiria kutenda jambo linalokugharimu wewe kwa Bwana wako? Damu yako unaimwaga wapi?. Watakatifu wa kanisa la kwanza, waliweza kuuza mali zao za thamani na kumtolea Bwana, na sisi tunafanya nini kwa Bwana?.

3) Wanaoondoa viungo vyao vinavyowakosesha kwa ajili ya Kristo.

Hili nalo ni kundi lingine la wanaomwaga damu. Ukisoma Marko 9:43-49, kuna maneno Bwana Yesu alisema, kuhusiana na viungo vyetu. Akasema ikiwa kimojawapo kinakukosesha kikate, ili usikose uzima wa milele. Unajua sikuzote kiungo kikatwapo, ni lazima damu imwagike. Ukiuondoa mguu wako, yapo maumivu, lakini pia ipo damu itakayokutoka.

Viungo vinaweza vikawa ni wazazi, marafiki, ndugu, kazi, mazingira n.k. Ikiwa mzazi anakukosha usisimame vema na Mungu, anakukataza usimwabudu Bwana,au usihubiri huna budi kutomtii kwasababu hiyo, ni kweli utakutana na maumivu, damu itatoka, lakini umemtii Kristo.

Ndicho alichokifanya mfalme mmoja aliyeitwa ASA, yeye alimcha Mungu, na alipoona mama yake anamletea habari za ibada za masanamu, akamwondoa kwenye kiti cha umalkia, japokuwa ni fedheha kubwa alionyesha lakini aliona ni heri kumtii Kristo zaidi ya mwanadamu (1Wafalme 15:11-13)

Hata leo, watu ambao, wameachwa, na viongo vyao vya karibu, au wameviondoa, kwasababu ya Kristo, visiwaghasi, labda ni kazi, ndugu, rohoni wanaonekana kama wamemwaga damu zao kwa ajili ya ushuhuda wa Kristo, na hivyo ni mashahidi wa Bwana. Ndugu usiopoge maumivu, mpende Bwana zaidi ya chochote.

4) Wanaoomboleza kwa ajili ya kanisa, na injili.

Yesu alipokuwa anaomba, kwa maomboleza na dhiki nyingi kwa ajili yetu muda mfupi kabla ya kusulibiwa, maandiko yanasema jasho lake, likageuka kuwa matone ya damu.

Luka 22:41  “Mwenyewe akajitenga nao kama kiasi cha kutupa jiwe, akapiga magoti akaomba, 42  akisema, Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke. 43  Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu. 44  Naye kwa vile alivyokuwa katika dhiki, akazidi sana kuomba; hari yake ikawa kama matone ya damu yakidondoka nchini.]

Hivyo na wote, waombolezao kwa ajili ya haki, machozi yao si bure, wanaokesha kuliombea kanisa, na kazi ya Mungu, wanaowaombea wengine kwa machozi na huzuni, wanadumu madhabahuni kwa Bwana muda mwingi mfano wa Ana (Luka 2:36). Rohoni wanamwaga damu, japo wanaweza wasilijue hilo. Na hivyo ni mashahidi wa Kristo duniani. Thawabu yao mbinguni ni sawasawa na wale waliokatwa vichwa kwa ajili ya Bwana.

Swali ni je! Mimi na wewe tunasimama wapi? Paulo anasema ninakufa kila siku, je! Na sisi tunafanya hivyo kwa Bwana wetu? Bwana atusaidie tuwe maaskari wake kwelikweli, ili siku ile ajivunie sisi mbele za Mungu na malaika zake.

Fanyika shahidi mwaminifu wa Bwana.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.

VIFO VYA MITUME WA YESU/ JINSI MITUME WALIVYOKUFA.

KAZI ZA ROHO MTAKATIFU

MAMBO YA KUJIFUNZA KWA KLOPA NA MKE WAKE!

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA-KONDOO.

Rudi nyumbani

Print this post

UMEJIANDAAJE KWA NYAKATI ZA KUWA PEKE YAKO?

Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo, karibu tuyatafakari maneno ya neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.

Sisi kama wakristo hatuna budi kutambua kuwa yapo majira mbalimbali tutapishana nayo angali tukiwa hapa duniani katika safari yetu ya imani. Leo tutaona mojawapo ya majira ambayo, huna budi kupishana nayo sehemu Fulani katika maisha yako. Na watakatifu wengi wanapofikia hatua hii, huwa wanavunjika moyo, na wengine kudhani Mungu amewaacha. Lakini la! Ni moja ya mapito ambayo Bwana anayaruhusu kwasababu zake maalumu.

Na majira hayo ni ya kuondolewa msaada, au usaidizi, au ukaribu, au faraja ya  ndugu, ya marafiki, au ya wapendwa. Yategemea na pito la mtu mwenyewe. Na sio kwamba ni wabaya, hapana, ni Mungu tu peke yake kaamua kufunga milango hiyo. Ili abaki yeye na Mungu wake tu, katika chumba cha siri cha rohoni.

Tujifunze kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Ambaye, alikuwa mashuhuri sana, na kila mahali alipokwenda alizingirwa na makutano mengi, wakati mwingine alijificha ili watu wasimwone, kwasababu walikuwa wanamsonga sana, hata nafasi ya kula ilikosekana, maelfu ya watu walitamfuata popote alipokwenda.

Lakini kuna majira, hata wale waliokuwa karibu naye (yaani mitume) walimkimbia akabaki yeye peke yake, na hilo aliliona mapema akawaambia wanafunzi wake, ili wasije wakajisikia vibaya.

Yohana 16:32  Tazama, saa yaja, naam, imekwisha kuja, ambapo mtatawanyika kila mmoja kwao kwao, na kuniacha mimi peke yangu; walakini mimi si peke yangu, kwa kuwa Baba yupo pamoja nami.

33  Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.

Na ilikuja kutokea hivyo (Soma Marko 14:27-51). Kwasababu ilikuwa ni sehemu ya pito la mwana wa Mungu.

Halikadhalika yupo mtume Paulo, kama tunavyojua yeye ndio alikuwa kama askofu-kiongozi wa makanisa ya mataifa. Alikuwa na marafiki wengi, alikuwa na wapendwa wengi waliomsapoti na kumfariji, katika utumishi wake. Lakini upo wakati alijikuta peke yake. Mpaka akaandika sehemu ya waraka huo na kumtumia Timotheo. Jambo ambalo huwezi dhani linawezekana kwa askofu wa makanisa.

2Timotheo 4:16  “Katika jawabu langu la kwanza hakuna mtu aliyesimama upande wangu, bali wote waliniacha; naomba wasihesabiwe hatia kwa jambo hilo. 17  Lakini Bwana alisimama pamoja nami akanitia nguvu, ili kwa kazi yangu ule ujumbe utangazwe kwa utimilifu, hata wasikie Mataifa yote; nami nikaokolewa katika kinywa cha simba. 18  Bwana ataniokoa na kila neno baya, na kunihifadhi hata nifike ufalme wake wa mbinguni. Utukufu una Yeye milele na milele. Amina”

Hivyo, hii sio bahati mbaya, ijapokuwa tunazungukwa na wapendwa, na familia, na watoto, na marafiki, lakini kuna wakati Bwana atataka ubaki peke yako na yeye. Na hivyo katika kipindi hicho utakachojikuta, upo mbali nao, au huoni msaada wowote kutoka kwao kama ilivyokuwa kule mwanzo, au hawakuulizii tena, huna mtu wa kucheka naye, kuimba naye. Usijione mpweke, bali mtazame Kristo, elekeza mawazo yako kwake, kwasababu kuna jambo anataka kukufundisha.

Na wakati huo ukiisha, utaona tena anakurejeshea, faraja yako, wapendwa wako, rafiki zako, ndugu zako, na safari inaendelea. Kama alivyofanya kwa Ayubu.

Ayubu 42:10 “Kisha Bwana akaugeuza uteka wa Ayubu, hapo alipowaombea rafiki zake; Bwana naye akampa Ayubu mara mbili kuliko hayo aliyokuwa nayo kwanza.  11 Ndipo wakamwendea nduguze wote, waume kwa wake, nao wote waliojuana naye hapo zamani, wakala chakula pamoja naye katika nyumba yake; nao wakamlilia na kumtuza moyo katika habari za huo uovu wote Bwana aliouleta juu yake; kila mtu akampa kipande cha fedha, na pete ya dhahabu kila mmoja”.

Hivyo weka akiba ya wakati huo, kwasababu hutaukwepa ikiwa wewe ni mwana wa Kristo.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

WATAMTAZAMA YEYE AMBAYE WALIMCHOMA; NAO WATAMWOMBOLEZEA.

RABI, UNAKAA WAPI?

HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.

NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?

JE UTII WAKO KWA MUNGU UMETIMIA?.

Rudi nyumbani

Print this post

NI WAPI PA KUONGOZWA NA ROHO, NA WAPI NI WAJIBU WANGU?

Fahamu mambo ambayo ni wajibu wako kufanya, na yale ambayo unapaswa umsubiri kwanza Roho Mtakatifu akuongoze.

Kama mkristo ni vizuri kuweza kutofautisha mambo ambayo ni wajibu wako kuyafanya, na mambo ambayo utahitaji kwanza uongozwe na Roho Mtakatifu kuyafanya. Ukishindwa kutambua yaliyo wajibu wako, kisha ukasubiri Roho akuongoze, utapotea, halikadhalika ukishindwa kutambua yale ambayo utapaswa usubiri Roho akuongozwe ukayafanya kwa matakwa yako,vilevile utajikuta unapata hasara.

Hivyo haya ni baadhi ya mambo ambayo Mungu anaona ni wajibu wako, na unapaswa uyafanye, na haya usitazamie Bwana atakufunulia uyafanye.  Ni mfano tu wa baadhi ya mambo ya mwilini, kwa mfano hakuna mtu anayeweza kusubiri afuatwe na Mungu na kuambiwa ale chakula ndio ale, au anywe maji ndipo anywe, hapana, ni wewe tu mwenyewe utaona unahisi njaa, na hivyo utatafuta kila namna ya kupata chakula na utakula, wala hutamlaumu Mungu kwanini hakumfunulia juu ya chakula . Vivyo hivyo na baadhi ya mambo ya kiroho.

Haya ni mambo ya kuzingatia kuyafanya pindi tu uokokapo kwa maendeleo yako bora ya kiroho.

Kuomba: Maombi hayaepukiki kwa mwamini yoyote, wapo watu wanasema siwezi kuomba bila kuongozwa na Mungu. Ndugu Maombi hayahitaji kuongozwa, yanahitaji kujiongoza kwanza. Kuomba ni lazima iwe desturi yako kila siku, na kiwango cha chini Bwana alichotoa kwa kila mwaminio ni SAA 1.

Mathayo 26:40  Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja? 41  Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.

Hivyo tangu sasa zingatia kujiwekea utaratibu huu, vinginevyo maisha yako ya wokovu yatakuwa ni mazito sana kuyaishi.

1) Kusoma Neno: Neno ndio chakula chetu cha rohoni, kwasababu Bwana alisema, mtu hataishi kwa mkate tu, bali kwa Neno lake. Kama hutajiwekea ustaarabu ya kutenga muda wako kila siku wa kuyatafakari maandiko, ukasubiri ipo siku Bwana ataanza kukufunulia uanze kusoma kitabu gani, na gani..Utapotea ndugu yangu. Hii njaa ya kiroho tuliyonayo siku hizi za mwisho, tutasubiri kweli, tuletewe chakula mdomoni?. Ni sisi wenyewe kuchangamka kusoma biblia daima, haijalishi wewe ni mchungaji umesoma biblia yote mara saba, au umeokoka leo,wote tunapaswa tuwe watu wa kusoma na kujifunza Biblia.

2) Mifungo ya mara kwa mara: Tunaposema mifungo ya mara kwa mara tunamaanisha ile mifungo ambayo, kila mmoja anaweza kuistahimili, ya saa 24, au siku mbili, au tatu, bila kula. Mifungo inakurahisishia wigo wako wa kimaombi, na kuivuta roho yako juu, ili iweze kukutana na uso wa Mungu kirahisi. Kwahiyo usingoje, kusikia sauti Fulani ikuambie anza kufunga. Anza kujijengea utaratibu huo wewe mwenyewe, walau kila mwezi uhesabu kuna siku kadhaa umefunga.

3) Ibada: Halikadhalika ukikoka, usisubiri Bwana akuambie nenda kanisani ukaniabudu. Au anza kuniimbia sifa. Ni wajibu wako, ‘kumvukizia’ Mungu wako uvumba wa shukrani, sifa, matoleo, nyimbo, ushirika wa  meza yake n.k. mara nyingi kwa jinsi uwezavyo. Wengine watasema ipo changamoto ya makanisa, ndio hiyo isiwe sababu ya kutulia tu nyumbani, nenda kwingine, pakiwa pabaya tafuta kwingine, hatimaye Mungu ataiona nia yako, na kukupa mahali sahihi pa kutuliza moyo wako. Maana kila atafutaye huona.

4) Kushuhudia habari za Yesu kwa wengine: Kuwaeleza wengine Habari za Yesu, ni wajibu wetu sote, aidha umeokoka leo, au umekomaa kiroho.  Kushuhudia haihitaji ujuzi mwingi wa kimaandiko kama wengi wanavyodhani, hata kueleza uzuri wa Kristo na ushuhuda wako kwa mwingine tayari ni injili hiyo.. Paulo alipookoka, tu baada ya kubatizwa hapo hapo akaanza kuwaeleza wengine habari za Yesu na uchanga wake wote.

Matendo 9:18 “ Mara vikaanguka machoni pake vitu kama magamba, akapata kuona, akasimama, akabatizwa;19  akala chakula, na kupata nguvu. Akawa huko siku kadha wa kadha pamoja na wanafunzi walioko Dameski.20  Mara akamhubiri Yesu katika masinagogi, kwamba yeye ni Mwana wa Mungu.21  Na wote waliosikia wakashangaa, wakasema, Siye huyu aliyewaharibu walioliitia Jina hili huko Yerusalemu? Na hapa alikuwa amekuja kwa kusudi hilo, awafunge na kuwapeleka kwa wakuu wa makuhani?”

HAYA NI MAMBO AMBAYO UNAPASWA USUBIRI, UONGOZWE NA ROHO

1) Kuanza huduma: Huduma ni kama kituo rasmi cha kuwasaidia watu kiroho, kwa ule wito uliowekewa na Mungu ndani yako. Na hapa, ni kuwa makini sana, kwasababu mtu akishaona amekoka, au anayo-karama Fulani, anachowaza ni kwenda kuanza kanisa, au akishajiona anao-ushawishi Fulani wa kuwakusanya watu anakwenda kuanza huduma. Ndugu hiyo ni hatari. Chukua mfano rahisi, leo hii wapo watu ambao wanaujuzi Fulani, labda tuseme wajenzi, lakini kama hawana elimu ya shuleni iliyothibitishwa hawawezi kupewa usimamizi wa majengo makubwa wayasimamie, kwasababu wanajua hata kama watakuwa wanaelewa aina nyingi za michanga na matofali, lakini bado kuna mambo watayakosa tu, ya ndani yahusuyo ujenzi, ambayo yanapatikana darasani tu, na hivyo kuna hatari ya kupata hasara kubwa mbeleni kwa mtu kama huyo kupewa usimamizi.

Halikadhalika, Mungu kumuita mtu katika huduma, si jambo atakalolikurupukia, bali atakuandaa, kwa kipindi Fulani katika shule yake ya Roho Mtakatifu (hatulengi shule ya vyuo vya biblia). Na hivyo, mwishoni kabisa ndio atakuita ufanye jambo ili isiwe hasara kwa watu wake.  Kwahiyo usiwe mwepesi wa kutaka kuanza jambo, kuwa mshuhudiaji, huku ukiwa chini ya uangalizi . Mtume Paulo japokuwa alikuwa anashuhudia habari za Kristo kwa ushujaa mwingi lakini alisubiri kwanza mpaka wakati wa Bwana.

Matendo 13:2  “Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia. 3  Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao. 4  Basi watu hao, wakiisha kupelekwa na Roho Mtakatifu wakatelemkia Seleukia, na kutoka huko wakasafiri baharini hata Kipro”

2) Mifungo mirefu: Ipo mifungo ya kutokula na kunywa kwa kipindi kirefu kama wiki 2, mwezi, siku 40 n.k. Katika hali kama hizi, usijiamulie tu mwenyewe kwa akili yako kuiingia. Unawezi  kupata matatizo au kifo kabisa. Kwasababu hiyo inahitaji ROHO wa Mungu kukuongoza. Ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana Yesu.. aliongozwa na Roho, hakujiamulia tu kuanza mifungo hiyo.

Luka 4:1  “Na Yesu, hali amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Yordani, akaongozwa na Roho muda wa siku arobaini nyikani, 2  akijaribiwa na Ibilisi. Na siku hizo alikuwa hali kitu; hata zilipotimia, aliona njaa”

Hivyo zingatia haya, na Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

3) Unayefanya naye mapatano, au maagano: Maagano/mapatano yapo ya namna mbalimbali, yapo ya kipindi kifupi na mengine ya maisha, mfano, unapotaka kuingia katika ndoa, huna budi kumshirikisha Roho Mtakatifu, akupe mwongozo wake, ndio hapo inakugharimu utangulize maombi. Unapochagua viongozi wa kusimamia kundi, hupaswi kuwaza kwa akili zako, bali jipe muda wa Roho Mtakatifu kukufunulia. Ilimpasa Bwana afunge usiku kucha kuomba mwongozo wa wanafunzi wa kutembea nao. Unapotaka kutumika na mtu, usiyemjua chukua muda wa kumuuliza Roho Mtakatifu. kwasababu yapo makosa mengi ambayo hata katika maandiko yalitokea kwa kukosa kumshirikisha Mungu kwanza. Wakati fulani mfalme Yehoshafati alitaka kutumika na mfalme Ahabu, na ilikuwa nusu afe, kwasababu alifanya mapatano na mfalme mwovu.(2Nyakati 18:1-25)

Yoshua aliingia katika mapatano na maadui zake, ambao Bwana alimwambia awaangamize, na ndio hao wakaja kuwa mwiba kwa wayahudi baadaye. Hiyo yote ni kwasababu hawakuwa tayari kumsikiliza kwanza Roho Mtakatifu. Hivyo jambo lolote la kiroho, ambao unaona linahitaji umakini mkubwa, subiri kwanza uongozo wa Roho Mtakatifu. Usiangalie, zawadi, uzuri, utajiri, au chochote. (Yoshua 9:1-27)

Bwana akubariki.

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

ANDALIZI LA MWISHO LA UJIO WA MPINGA KRISTO.

Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?

Aina za dhambi

AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

Roho Mtakatifu ni nani?.

IMESALIA RAHA YA SABATO KWA WATU WA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Kuna tofauti gani kati ya uso wa Bwana na macho ya Bwana?

Zaburi 34:15 Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake hukielekea kilio chao.  16 Uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya, Aliondoe kumbukumbu lao duniani.

JIBU: Andiko hili lilinukuliwa tena na mtume Petro katika 1Petro 3:12-13  linasema;

 “12 Kwa kuwa macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake husikiliza maombi yao; Bali uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya. 13  Naye ni nani atakayewadhuru, mkiwa wenye juhudi katika mema?

Kama tunavyojua Macho kazi yake ni kutazama, lakini uso, ni kueleza taswira ya mtu/ kitu fulani.

Na  kimsingi macho huona vyote, vilivyo vyema na vilivyo vibaya. Isipokuwa jicho lolote hupendelea zaidi kutazama vilivyo vyema zaidi ya vile vibaya. Ndivyo ilivyo kwa Mungu wetu pia, anaona yote, maandiko yanasema hivyo katika;

Mithali 15:3 “Macho ya Bwana yako kila mahali; Yakimchunguza mbaya na mwema”.

 lakini zaidi anaelekeza macho yake zaidi kwa walio wema ili awape mema.

Na ndio maana ya hiyo sehemu ya kwanza ya andiko hilo inayosema ‘Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake hukielekea kilio chao’ Lakini haimaanishi kuwa macho yake pia hayawaoni watenda mabaya.

Vivyo hivyo katika sehemu ya pili inayoeleza juu ya Uso wa Bwana. Kama tulivyoona Uso kazi yake ni kueleza taswira ya mtu. Kwa mfano mtu akifurahi, au akiwa na huzuni au akiwa na hasira ni rahisi kumtambua kwa kuutazama uso wake. Na Vivyo hivyo, kwa Mungu wetu ukiitambua tabia yake, basi ni sawa na umeuona uso wake.

Sasa uso wake pia upo katika pande mbili; 1) Wa Rehema, 2) na wa Hasira (Nahumu 1:2-3)

Maana yake ni kuwa ukimtafuta Bwana, na kumpenda, utaona uso wake mwema, utaona upendo wake, utaona fadhili zake, utaona ukarimu wake, huruma yake, na rehema zake sikuzote. Na ndio maana maandiko yanatuasa tupende kuutafuta Uso wa Bwana. Ili tuujue uzuri wake.

Zaburi 105:4 ‘Mtakeni Bwana na nguvu zake, Utafuteni uso wake sikuzote’.

Zaburi 143:7 “Ee Bwana, unijibu hima, roho yangu imelegea; Usinifiche uso wako, Nisifanane nao washukao shimoni’

Lakini pia kinyume chake ni kweli ukiwa mwovu, ukiwa mkaidi, ukiwa mbaya, unajiandaa kuuna uso wa Mungu wenye ghadhabu,na hasira, na mapigo na matokeo yake utakumbana na adhabu kali kutoka kwake. Ndio hapo, anasema.

‘Uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya, Aliondoe kumbukumbu lao duniani’.

Hivyo kwa ufupisho ni kwamba jicho la Mungu linaona wote, waovu na wema, vilevile uso wa Bwana unawaelekea wote waovu na wema. Lakini katika vifungu hivyo, na vingine baadhi, vinapozungumzia macho ya Bwana huwa vinalenga sana sana kwa wema. Na vinaposema Uso wa Bwana, huwa vinalenga sana sana kwa  upande wa waovu.

Kwahiyo usichanganyikiwe, bali fahamu muktadha, wa habari hiyo katika sehemu husika. Ili ujue alimaanisha nini hapo, kwa msaada wa Roho wa Mungu. Kwasababu hutumika kotekote

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

UNAVYOZIDI KUWA MWENYE HAKI, NDIVYO KUJITAMBUA KWAKO KUNAVYOPUNGUA.

ANDALIZI LA MWISHO LA UJIO WA MPINGA KRISTO.

JIFUNZE KUDUMU UWEPONI MWA MUNGU.

Biblia inaposema Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, Inamaana gani?

Ni kweli hakuna mtu aliyewahi kuuona uso wa Mungu Zaidi ya Bwana Yesu?

Je Paulo na Petro walishindania nini? (Wagalatia 2:11).

TABIA ZA NJIA YA MUNGU KWA MKRISTO

Rudi nyumbani

Print this post

SADAKA INAKOMESHA LAANA!

Karibu katika mfululizo ya masomo yahusuyo matoleo!

(Ifahamu Nguvu iliyopo katika Sadaka)

Tangu Adamu aanguke ardhi ilianza kulaaniwa; kila siku laana ilikuwa inajiongeza juu ya laana, ndio maana utaona Mungu alimwambia Adamu ardhi imelaaniwa kwaajili yake yeye na uzao wake (Mwanzo 3:17), lakini ukizidi kusoma utaona tena ardhi inalaaniwa mara ya pili kwa Kaini (Mwanzo 4:11).

Na desturi hiyo iliendelea juu ya wanadamu, (Maana yake kila kukicha ardhi ilikuwa inalaaniwa juu ya wanadamu, kutokana na maasi).

Lakini tunasoma alipozaliwa Nuhu maandiko yanamtaja kama mwana wa Faraja, atakayeikomesha laana iliyo juu ya ardhi.

Mwanzo 5:28 “Lameki akaishi miaka mia na themanini na miwili, akazaa mwana. 

29 Akamwita jina lake Nuhu, AKINENA, HUYU NDIYE ATAKAYETUFARIJI KWA KAZI YETU NA KWA TAABU YA MIKONO YETU KATIKA NCHI ALIYOILAANI BWANA”

Sasa unaweza kujiuliza ni wakati gani ambao Nuhu alileta faraja katika Nchi aliyoilaani Bwana?

Tusome Mwanzo 8:20-22.

Mwanzo 8:20 Nuhu akamjengea Bwana madhabahu; akatwaa katika kila mnyama aliye safi, na katika kila ndege aliye safi, akavitoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu. 

21 Bwana akasikia harufu ya kumridhisha; Bwana akasema moyoni, SITAILAANI NCHI TENA BAADA YA HAYO KWA SABABU YA WANADAMU, MAANA MAWAZO YA MOYO WA MWANADAMU NI MABAYA TANGU UJANA WAKE; WALA SITAPIGA TENA BAADA YA HAYO KILA KILICHO HAI KAMA NILIVYOFANYA. 

22 Muda nchi idumupo, majira ya kupanda, na mavuno, wakati wa baridi na wakati wa hari, wakati wa kaskazi na wakati wa kusi, mchana na usiku, havitakoma”

Umeona hapo? Baada ya Nuhu kumjengea Bwana madhabahu na kumtolea Bwana sadaka nzuri na ya kumridhisha, ndipo akaikomesha ile laana yote iliyokuwa inaendelea juu ya ardhi, kukawa hakuna tena kulaaniwa kwa nchi baada ya hapo!, ndio maana mpaka leo tunaona misimu ya mvua ipo, misimu ya kiangazi cha mavuno ipo, majira ya kuvuna na kupanda bado yapo, kama isingelikuwa ile sadaka Nuhu aliyoitoa huenda leo tungekuwa dunia ingekuwa mahali pabaya.

Lakini siri ya KUIKOMESHA HIYO LAANA!, Nuhu alifahamu ni kwa NJIA YA MATOLEO TU!..Na ni kanuni gani Nuhu aliyoitumia kutoa sadaka mpaka kufikia kuvunja misingi ya laana ya ardhi?

1.Alijenga Madhabahu.

Na sisi ni lazima tujenge madhabahu kwanza, na Madhahabu ya sasa, Agano jipya si ile ya mawe bali ni MIOYO YETU, Hiyo inapaswa iwe misafi kabla ya kufikiri kumtolea BWANA sadaka. Kwasababu maandiko yanasema sadaka ya mtu mbaya ni machukizo kwa Bwana (Mithali 15:8).

2. Kutoa vilivyo safi.

Baada ya Nuhu kutoka kwenye safina alitwaa wanyama walio safi tu na kumtolea Mungu, Na sisi ni lazima tumtolee Mungu vitu vilivyo visafi, hatupaswi kumtolea Mungu vitu vilivyopatikana kwa njia haramu kama ukahaba, dhuluma, rushwa, wizi, utapeli, na njia nyingine zote zinazofanana na hizo.

Kumbukumbu 23:18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili.”

3. Kutoa katika KILA kilicho safi!

Hii ni kanuni ya mwisho na ya muhimu sana, Ni lazima kutoa katika “KILA” kilicho safi, na si katika “BAADHI ya vilivyo safi”. Nuhu hakutoa tu Ng’ombe pekee yake kama sadaka, na kuwahifadhi mbuzi kwaajili ya chakula chake na biashara yake,  au hakutoa kondoo pekee yake, na kuwaacha kuku na mbuzi…bali alitoa katika vyote vilivyo safi, ikiwemo kondoo, mbuzi, ng’ombe, njiwa, kuku na vinginevyo.. kila kimoja kwa sehemu yake..Hiyo ikafanya sadaka yake kumridhisha Mungu, na hivyo kufuta laana zote zilizokuwepo juu ya nchi, ambapo mpaka leo tunakula matunda yake.

Na wewe una vitu gani vilivyo safi mbele za Mungu?, je katika vyote unavyovifanya huwa unafikiri kumtolea Mungu katika hivyo?, Je katika zawadi unazopewa ulishawahi kufikiri kumtolea Mungu sehemu ndogo katika hiyo?, au unafiki ni sehemu ya mshahara tu ndio Mungu anaitaka?!

Je katika mifugo yako yote ulishawahi kufikiri kumtolea Mungu sehemu ya hiyo? Usimtolee Mungu kuku na kuacha Mbuzi!.. Jaribu siku moja kumtolea mbuzi na kuku kwa pamoja, na uone matokeo yake, (Mungu ameruhusu tumjaribu kwa njia hiyo, Malaki 3:10).

Utaona laana zinavyoondoka juu yako!!.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Sadaka ya Moyo ipoje? (Walawi 22:21).

Chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu ndio kipi? (Matendo 21:25).

Kwanini Nuhu alimlaani Kaanani badala ya mtoto wake Hamu,

UTAYAFIKIAJE MANENO SAFI YA MUNGU?

Biblia inaposema Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, Inamaana gani?

Rudi nyumbani

Print this post

UWE KIKOMBE SAFI 

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tuyasikilize maagizo ya Mungu.

Kuna wakati Bwana alipokutana na mafarisayo alisema maneno haya;

Mathayo 23:25-26

[25]Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnasafisha nje ya kikombe na chano, na ndani yake vimejaa unyang’anyi na kutokuwa na kiasi.

[26]Ewe Farisayo kipofu, safisha kwanza ndani ya kikombe, ili nje yake nayo ipate kuwa safi.

Tengeneza picha ya kikombe. Kiuhalisia ili kifae Kwa matumizi ni lazima kiwe kisafi pande zote, yaani nje na ndani. Huwezi kutumia kikombe ambacho nje ni kisafi lakini ndani kina matope, vilevile huwezi tumia kikombe ambacho ndani ni kisafi lakini nje kina matope,. Bado uchafu ni ule ule..Hivyo ili kifae Kwa matumizi hakina budi kisafishwe kotekote ndani na nje.

Leo hii tunakosa shabaha kudhani, ni upande mmoja tu Mungu anautazama. Ndivyo walivyofanya mafarisayo Kwa nje walionekana wanyenyekevu, wafanya ibada, Wana staha, waalimu wazuri wa torati lakini ndani walijaa wivu, mashindani, majivuno, tamaa n.k.

Lakini vilevile wapo watu ambao Kwa ndani wanadai Wana upole, Upendo, amani, lakini Kwa nje, hawana ushuhuda wowote, Hawa ndio wale ambao wanasema Mungu anaangalia vya rohoni haangalii vya nje.

Ndugu ili utumiwe na Bwana, safisha kikombe kotekote. Rohoni na Mwilini 

Sasa haya ni baadhi ya mambo ambayo unapaswa uyafanye kotekote. Tukiangazia mifano kwa Bwana Yesu.

1) KUMPENDEZA MUNGU.

Yesu aliishi maisha ya kumpendeza Mungu, lakini alijua kwamba kabla ya kumpendeza Mungu ni lazima niwapendeze kwanza wanadamu. Hivyo akafanya bidii kuwa na sifa njema katika jamii pia, na kwa Mungu.

Luka 2:52

[52]Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.

Umeona? Hakuwa mtu wa kusema Mimi ni Mungu tu, lakini alitafuta sifa nzuri pia Kwa wanadamu ili Mungu wake atukuzwe, hivyo aliishi vizuri na wanadamu, alikuwa mtiifu, mwaminifu, mwenye utu, mwenye adabu kwa watu. Vivyo hivyo na wewe kama mkristo kama sifa zako nje zinavuma vibaya.. hata kama ni mtu mzuri kiibada hapo ni sawa na umesafisha kikombe Kwa ndani lakini nje ni kichafu. Hivyo bado hujakamilika. Safisha pande zote, mbinguni na ulimwenguni.

2) UPENDO

Maandiko yanasema, Mpende Bwana Mungu wako Kwa moyo wako wote, na Kwa Roho yako yote na Kwa nguvu zako zote..lakini kabla hayajasema maneno hayo, Mungu alitangulia kusema kwanza mpende jirani Yako,ili Upendo wako kwake ukamilike.

1 Yohana 4:20-21

[20]Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona.

[21]Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.

Kabla hujampenda Mungu mpende mwanadamu. Safisha kikombe nje na ndani.

3) USAFI

Mungu anatutaka tuwe wasafi moyoni moyoni.(Mathayo 5:8)..Lakini usafi wa ndani unakamilishwa na ule wa nje.

Soma

2 Wakorintho 7:1

[1]Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu.

Umeona kumbe Kuna uchafu wa mwili na pia wa roho. Ule wa Roho ndio wivu, kiburi, uongo n.k. lakini ule wa mwili ndio ulevu, uvaaji mbovu, uchoraji mwili, utukanaji, mazungumzo mabaya.n.k

Ikiwa unajiita Mtakatifu halafu unatembea na vimini barabarani, Binti unatembea na suruali, na nguo za mgongo wazi, huna tofauti na yule mhudumu wa pale bar.Fahamu kuwa huo usafi wako wa roho ni kazi bure. Kijana unatembea na suruali za milegezo, unafuga Rasta na viduku, huna tofauti na yule msanii wa kidunia.halafu unasema wewe ni msafi wa moyo fahamu kuwa hapo unayo dosari mbele za Bwana.

UWE KIKOMBE SAFI.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KIKOMBE CHA GHADHABU YA MUNGU KINAJAA.

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

KIASI NI NINI KATIKA UKRISTO?

UTAYAFIKIAJE MANENO SAFI YA MUNGU?

Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe;(Mithali 16:2)

AINA SABA (7) ZA UNAFIKI, AMBAZO UNAPASWA UJIEPUSHE NAZO.

Maziara ni nini? Je! Na Tunaruhusiwa kuyajenga kwenye makaburi yetu?

Rudi nyumbani

Print this post

HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.

Mathayo 9:14  “Wakati ule wanafunzi wake Yohana wakamwendea, wakasema, Kwa nini sisi na Mafarisayo twafunga, BALI WANAFUNZI WAKO HAWAFUNGI?

15  Yesu akawaambia, Walioalikwa arusini wawezaje kuomboleza, muda bwana arusi akiwapo pamoja nao? Lakini siku zitakuja WATAKAPOONDOLEWA BWANA ARUSI; NDIPO WATAKAPOFUNGA”.

Wanafunzi walipokuwa na Bwana Yesu katika mwili, chochote walichokihitaji walikipata kirahisi kwasababu Neema walikuwa naye katika mwili, walipohitaji uponyaji Kristo alikuwepo kuwaponya, walipohitaji kuona ishara na miujiza kama ile ya mikate mitano kulisha elfu tano, waliiona kirahisi.

Kila walichokihitaji walikipata, kwasababu Mtenda miujiza walikuwa wanamwona dhahiri na kumshika. Lakini ulipofika wakati wa Kristo kuchukuliwa juu, mambo yalibadilika!!, ile hali ya kusubiria kufanyiwa mambo na Bwana ikapotea, ikawabidi waanze kutafuta wenyewe namna ya kufanya mambo!. Ni kama tu kifaranga cha kuku kilichoachwa na mama yake, kikawaida kinaanza kujitafutia chenyewe, kitatembea huku na kule kama mama yake kutafuta chakula.

Ndicho kilichowatokea Mitume Bwa Yesu, ulipofika wakati wanakutana na wagonjwa na yule Bwana Yesu wa kukimbiziwa  wagonjwa hayupo!!!.. ndipo ufahamu wa kutafuta nguvu alizokuwa nazo Bwana Yesu ukawajia!.

Ndipo wakaanza kutafiti ni vitu gani vilivyokuwa vinampa nguvu Bwana Yesu, kufanya miujiza ile na kuishi maisha yale!, ndipo wakaanza kutafakari maisha yake na kugundua kuwa muda mwingi Bwana aliutumia KUFUNGA na KUKESHA MILIMANI KUOMBA.

Na wao ikawabidi wabadilike na kuanza kuwa WAFUNGAJI NA WAOMBAJI kama Bwana Yesu ili baadhi ya mambo yawezekanike kama yalivyowezekanika kwa Bwana, vinginevyo baadhi ya mambo yasingeenda sawa, Ndio maana utaona akina Petro walipokuwa na Bwana ni kama walikuwa wanavutwa vutwa katika suala la uombaji (Utaona kuna mahali Bwana Yesu alikuja kuwaamsha Zaidi ya mara 2 waombe lakini wakarudi kulala).

Marko 14:34  “Akawaambia, Roho yangu ina huzuni nyingi kiasi cha kufa; kaeni hapa mkeshe.

35  Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akiomba ya kuwa, ikiwezekana, saa hiyo imwepuke. 36  Akasema, Aba, Baba, yote yawezekana kwako; uniondolee kikombe hiki; walakini, si kama nitakavyo mimi, bali utakavyo wewe.

37  AKAJA AKAWAKUTA WAMELALA USINGIZI, AKAMWAMBIA PETRO, JE! SIMONI, UMELALA? Hukuweza kukesha saa moja? 14.38  Kesheni mwombe, msije mkaingia majaribuni, roho i radhi ila mwili ni dhaifu.

39  Akaenda zake tena, akaomba, akisema neno lilo hilo.

40  AKAJA TENA AKAWAKUTA WAMELALA, maana macho yao yamekuwa mazito, wala hawakujua la kumjibu.

41  Akaja mara ya tatu, akawaambia, Laleni sasa, mpumzike; yatosha, saa imekuja; tazama, Mwana wa Adamu anatiwa mikononi mwao wenye dhambi”.

Hapa tunaona akina Petro wakiwa wanavutwa vutwa katika suala la uombaji, lakini tunaona mambo yanabadilika baada ya Bwana Yesu kuondoka, walianza kufunga na kukesha katika maombi mengi,.. Kuna mahali Petro anaonekana kufunga kwa kuomba mpaka anazimia kwa njaa.

Matendo 10:9  “Hata siku ya pili, walipokuwa wakisafiri na kuukaribia mji, Petro alipanda juu darini, kwenda kuomba, yapata saa sita ya mchana;

10  AKAUMWA NA NJAA SANA, AKATAKA KULA; LAKINI WALIPOKUWA WAKIANDAA, ROHO YAKE IKAZIMIA,

11  akaona mbingu zimefunuka, na chombo kikishuka kama nguo kubwa, inatelemshwa kwa pembe zake nne hata nchi”

Hii ikifunua nini?

Kristo mpaka sasa hayupo nasi katika Mwili, hivyo na sisi pia tupo katika Nyakati za KUFUNGA na KUOMBA.

Ndugu Hizi ni nyakati za “Kufunga na kuomba”. Bwana Yesu alisema mambo mengine hayawezekaniki isipokuwa kwa kufunga na kuomba/kusali.

Mathayo 17:21 “[Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga]”

Je Unataka kumwona Mungu katika maisha yako?..Funga na kuomba!..je  unataka kuongezeka viwango vya kumjua Mungu?..Funga na kuomba!…Je Unataka Neema iongezeke juu yako! Na mambo mengine mengi yaliyo mazuri uyaone??, basi funguo ni Mifungo na Maombi. (Na kumbuka hapa biblia inazungumzia Maombi na sio maombezi). Usifunge na kwenda kutafuta kuombewa na mtumishi!.. Bali funga na omba mwenyewe!.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

HATUA ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUTUONGOZA.

Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

Kwanini maombi kwa Marehemu si sahihi kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Maziara ni nini? Je! Na Tunaruhusiwa kuyajenga kwenye makaburi yetu?

Kwa utamaduni wa sasa mtu anapokufa, huwa anafukiwa chini ardhini, na juu huwekewa  kiashirio Fulani cha kawaida kuonesha eneo hilo lipo kaburi. Lakini  watu wengine hupenda kuyapa thamani makaburi ya watu wao, hivyo kwa juu hujengea, kichumba Fulani kinachopambwa kwa vito au mawe ya thamani , wengine wanaweka mnara Fulani n.k. Sasa vitu hivi vyote vinavyojengewa juu ndio huitwa Maziara.

Kwamfano katika picha hii, ni mfano wa Ziara ambalo lilijengwa na wenyeji wa Marekani kama kumuenzi raisi wao wa kwanza wa taifa hilo aliyeitwa George Washington.

Hata katika agano la kale, enzi za biblia, yapo makaburi yaliyokuwa ya kawaida, lakini pia yapo yaliyokuwa yamejengewa maziara. Na hayo yalikuwa hususani ya wafalme na manabii wakubwa waliotokea Israeli, ambao waliuliwa kikatili mfano wa hao  ni Zekaria, Hagai na Malaki.  Na waliohusika sana kutengeneza maziara haya walikuwa ni hawa waandishi na mafarisayo(Watu wa kidini). Wakidai kuwa wanawa-enzi manabii wao, lakini tunaona Yesu akiwakemea kwa dhambi ya unafki waliyokuwa wanaifanya kwa tendo hilo.

Tusome.

Mathayo 23:29  Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnayajenga makaburi ya manabii, na kuyapamba maziara ya wenye haki, 30  na kusema, Kama sisi tungalikuwako zamani za baba zetu, hatungalishirikiana nao katika damu ya manabii. 31  Hivi mwajishuhudia wenyewe, ya kwamba ninyi ni wana wao waliowaua manabii. 32  Kijazeni basi kipimo cha baba zenu. 33  Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum? 34  Kwa sababu hiyo, angalieni, mimi natuma kwenu manabii na wenye hekima na waandishi; na wengine wao ninyi mtawaua na kuwasulibisha, na wengine wao mtawapiga katika masinagogi yenu, na kuwafukuza mji kwa mji; 35  hivyo ije juu yenu damu yote ya haki iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habili, yule mwenye haki, hata damu ya Zakaria bin Barakia, mliyemwua kati ya patakatifu na madhabahu. 36  Amin, nawaambieni, Mambo hayo yote yatakuja juu ya kizazi hiki.

Soma pia (Luka 11:47-48).

Swali ni je! Walikuwa wanafanya makosa kutenda jambo lile?

Jibu ni hapana, Bali walichokuwa wanakifanya nje, hakikuendana na kile kilichokuwa mioyoni mwao na ndio maana akawaita wanafiki. Kwasababu walikuwepo pia manabii wa Mungu na watu wenye haki wakati wao, mfano wa Yohana, pamoja na yeye mwenyewe lakini walikuwa wanataka kuwaua. Na ndivyo walivyokuja kufanya kwa Bwana, pamoja na mitume wako na watakatifu wa kanisa la kwanza kama vile wakina Stefano.

Je! Sisi tujengapo maziara kama heshima  kwa wafu wetu tunatenda dhambi?

Jibu ni la, Endapo tu hatutashirikisha ibada yoyote ya wafu mahali pale. Lakini kama ni kwa kumbukumbu, au kumu-enzi marehemu wako, hakuna shida kuweka ziara (kupamba kaburi lako kwa jinsi upendavyo). Lakini fahamu tu hilo halitakuongezea jambo lolote rohoni. Wala halimfaidii kwa lolote Yule marehemu kule alipo.

Je! Ni sawa kwa Mkristo kusafisha kaburi la mfiwa wako, na kufanya ibada mahali pale?

Kutunza kaburi lolote, yaani kulisafisha, kulirepea, kulipandia bustani, kulilinda.. Si kosa kibiblia, kwasababu tunaona katika biblia makaburi yalitunzwa kwa bustani, soma (Yohana 20:15), pia yalilindwa, Na zaidi yalihifadhiwa yasiharibiwe. Soma

2Wafalme 23:16 Naye Yosia alipogeuka, aliyaona makaburi yale yaliyokuwako huko, juu ya mlima; akatuma watu, akaitoa ile mifupa katika yale makaburi, akaiteketeza juu ya madhabahu, akainajisi, sawasawa na lile neno la Bwana, alilolinena yule mtu wa Mungu, aliyetamka mambo hayo.  17 Kisha akasema, Ni kumbukumbu la nani, hili ninaloliona? Na watu wa mji wakamwambia, Ni kaburi la yule mtu wa Mungu, aliyetoka Yuda, akayanena mambo hayo uliyoyatenda wewe juu ya madhabahu ya Betheli.  18 Akasema, Mwacheni; mtu awaye yote asiiondoe mifupa yake. Basi wakaiacha mifupa yake, pamoja na mifupa ya yule nabii aliyetoka Samaria.

Hivyo, upendapo kutunza kaburi la mpendwa wako, aliyefariki hufanyi kosa.

Vipi katika kufanya ibada?

Zipo ibada za wafu, ambazo ndizo zinazofanyika mara nyingi katika makaburi ya marehemu, ibadani hizo, zinahusianisha kuwaombea wafu hao, n.k. Ibada hizi ni za kipagani, na mkristo hapaswi kuzifanya ni  ibada za miungu. Au wengine wanakwenda kuzungumza na kaburi wakiamini Yule mtu yupo pale makaburini anawasikia. Huo ni uchawi.

Hivyo hakuna mahusiano yoyote ya kiibada katika makaburi. Endapo imetokea unakwenda kufanya maziara (yaani kukarabati au kupamba), basi unachofanya ni kufungua kwa maombi na kufunga kwa maombi, kisha mnaendelea na kazi yenu, ili kutimiza hili andiko

Wakolosai 3:17  “Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”.

Na kama mmeguswa kutafakari maneno ya Mungu mahali pale, kama mfanyapo sehemu nyingine zozote, mfano kazini, shuleni, chini ya mwembe n.k..  Basi iwe ni kwa Mungu na sio kwasababu ya makaburi. Epuka Ibada za wafu.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Pango la Makpela ni lipi, je lina umuhimu wowote kwetu?

MAKABURI YAKAFUNUKA; IKAINUKA MIILI MINGI YA WATAKATIFU WALIOLALA;

MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.

Nini maana ya kuabudu?

Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani?

Praitorio ni nini? Na Kwanini ilikuwa ni najisi kwa wayahudi kuingia humo? (Yohana 18:28)

Nini maana ya Ukuta uliopakwa chokaa (Matendo23:3)?

Makanda ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

ANDALIZI LA MWISHO LA UJIO WA MPINGA KRISTO.

Je unajua kuwa roho ya mpinga-kristo imeshaanza kutenda kazi na inaendelea kutenda kazi hata sasa?

1 Yohana 4:3 “Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; NA SASA IMEKWISHA KUWAKO DUNIANI”.

Andalizi la mwisho la Mpinga Kristo kabla ya chapa yake kuanza kufanya kazi ni hili “MUNGU HAANGALII MWILI BALI ROHO”.

Roho ya Mpinga-kristo inawaandaa sasa watu na hiyo saikolojia, kwamba waamini Mungu haangalii mwili bali roho tu.

Na kwanini anafanya hivyo?.. ni ili iwe vyepesi kwake siku ile  kuwatia watu CHAPA mwilini (Usoni na mikononi)

Kwasababu asipowaandaa na hiyo saikolojia itakuwa kwake ni ngumu sana kuwashinikiza waipokee chapa katika vipaji vya nyuso na katika mwili siku zile baada ya unyakuo wa kanisa kupita.

Kwahiyo anaanza na saikolojia ndogo tu kwamba kuvaa hereni sio kosa, kutoboa pua sio kosa, kujichora tattoo na hina sio kosa na kupaka lipstick midomoni na wanja machoni sio dhambi.. ( kwamba Mungu hawezi kumhukumu mtu kwa vitu vinavyowekwa mwilini)

Ndugu usidanganyike,  je! Umewahi kujiuliza kwanini Mungu atawahukumu watu wote watakaoipokea  ile chapa ya mnyama  katika VIPAJI vya nyuso zao na katika MIKONO yao siku ile?..

Kama Mungu haangalii mwili kwanini chapa ya 666 itiwe katika mwili na Mungu awahukumu wale wote watakaoipokea chapa hiyo?, maana maandiko yanasema watu wote watakaoipokea chapa hiyo katika vipaji vya nyuso zao au katika mikono basi watahukumiwa katika lile ziwa la moto (Ufunuo 14:9-10).

Sasa kama tu alama ya kishetani katika kipaji cha uso au katika sehemu ya mkono, inaweza kuwa sababu ya mtu kukataliwa na Mungu milele!, vipi hizo tattoo unazochora mwilini, vipi hizo hina unazozipaka na  wanja unaoupaka machoni?, vipi hizo lipstick unazopaka mdomoni na rangi unazopaka kwenye kucha?… Vipi hizo hereni unazozining’iniza masikioni?.

Kama tu leo ni ngumu kuelewa kuwa kupaka wanja ni kosa kibiblia, utashawishikaje siku ile kuamini kuwa kuandikwa alama ya 666 kwenye kipaji cha uso wako ni kosa?..nataka nikuambie kuwa siku ile utaipokea tu chapa kama kawaida.  Kama tu leo kutoboa masikio na kuweka hereni na kutoboa pua na kuweka pini huoni shida, utaonaje shida siku ile utakapotobolewa  katika mkono wako na chipu kuwekwa mwilini mwako?.

Tafakari sana dada!!… tafakari sana kaka!! Tafakari sana Mama, tafakari sana Baba…Usiwe mwepesi kuiga mambo yanayoendelea na kuonekana ulimwenguni, hususani yanayofanywa na watu wengi!…(Mengi ya hayo yanaongozwa na roho ya mpinga kristo)…Ni kweli unajipenda, na ni vizuri kufanya hivyo, ni kweli unapenda uonekane vizuri na maridadi mbele za watu, ni vizuri pia kufanya hivyo lakini vipi na roho yako? Je itaendelea kubaki salama?.

Shetani amewafunga wengi macho siku hizi za mwisho wasiyaelewe maandiko! Na kuwaaminisha kuwa Mungu haangalii mwili bali anaangalia roho.

Dada usidanganyike! Kwasababu udanganyifu upo leo.. na utaendelea kuwepo mpaka wakati wa chapa ya mnyama.

Tupa hereni zote, kachome mawigi, ondoa pistick, na wanja machoni.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UTENDAJI KAZI MWINGINE WA ROHO MTAKATIFU USIOUFAHAMU.

JE CHANJO YA KORONA NI ALAMA YA MNYAMA?

KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

NIMEAZIMIA KUWAKUSANYA MATAIFA. NIPATE KUWAMWAGIA GHADHABU YANGU

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.

Rudi nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 29:21 “Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto, Mwisho wake atakuwa ni mwanawe”

Mithali 29:21 “Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto, Mwisho wake atakuwa ni mwanawe”.

Kutundua ni kujali mtu kupita kiasi, au kuonyesha wema uliopitiliza.

Hivyo hapo anaposema amtunduiaye mtumwa wake tangu utotoni, mwisho wake atakuwa ni mwanawe. Anamaanisha amjalie mtumwa wake, kupita kiasi, yaani kuishi naye kama sio mtumwa kwake, (kumdekeza), na kama mfano ikiendelea hivyo kwa kipindi kirefu, mwisho wake utakuwa ni kumfanya mwanawe, yaani mrithi.

Zamani enzi za biblia, watu walikuwa aidha wananunua watumwa, au wanawazalisha majumbani kwao, ikiwa na maana kama mtu huyo alikuwa na mtumwa, kisha mtumwa Yule akazaa, sasa wale watoto wanakuwa pia ni watumwa wa Yule bwana.

Na kulikuwa na sheria kwamba kila baada ya miaka 7, mbiu ilipigwa ya kuwafanya watumwa wote huru, hivyo waliotaka kuondoka waliondoka, lakini waliotaka kuendelea, basi waliendelea kwa mkataba mwingine wa miaka saba. Na hivyo mtumwa huyo aliwajibika kutumika ipasavyo muda wote huo wa mkataba wake (Kumbukumbu 15:1-18).

Sasa hapa, biblia inaeleza tabia ya bwana ambaye moyo wake ni wa kitofauti. Bwana ambaye, anatabia ya kumjali sana mtumwa wake kuliko uhalisia, huwenda anamuhurumia, kumwona anafanya kazi nyingi, hivyo anampa kidogo tu, au anapokwenda kwenye sherehe hamwachi nyumbani anakwenda naye pia, hata akiwa nyumbani majukumu anapewa machache sana, anakaa naye mezani pamoja wanacheka n.k… Sasa katika hali kama hiyo, ikiwa mtumwa huyo, atadumu kubaki kwa bwana wake, kwa kipindi kirefu, Yule bwana, atamfanya tu kuwa kama mmojawapo wa mwanawe, maana yake siku atakapotoa urithi, na huyu lazima apewe, kwasababu ameishi kama mtoto wake kwa kipindi kirefu.

Na hii ni kweli, hata katika kipindi hichi, labda mfanyakazi kaajiriwa kwenye nyumba fulani, kisha mwenye nyumba akampenda, akawa naye kwa kipindi cha miaka mingi, mwishowe, atamfanya tu kama mwanafamilia, na hatimaye atapata kitu kama mmojawapo wa watoto wake.

Ni kufunua nini rohoni?

Hii ni Tabia aliyokuwa nayo Mungu kwetu sisi watu wa mataifa.

Tulipokwenda kwake, hatukuwa wana wake, au warithi, bali warithi walikuwa ni wayahudi tu, lakini kwa ukarimu wake, akatutoa katika utumwa na kutufanya WANA, jambo ambalo si kawaida kwa bwana yoyote, kutenda kwa kijakazi aliyezaliwa kusikojulikana. Ndicho alichokuja kukifanya Yesu;

Yohana 15:15  Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki; kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu.

Yohana 8:35  “Wala mtumwa hakai nyumbani sikuzote; mwana hukaa sikuzote. 36  Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli”.

Hivyo mimi na wewe tunafanyika, WANA na WARITHI, wa Mungu kwa njia ya Bwana Yesu. Haleluya. Utukufu na heshima ni kwa Bwana wetu Yesu!! milele na milele.

Lakini ni nini tunapaswa kukifanya?

Ni kukubali tu kudumu katika nyumba yake. Kama vile mtumwa Yule ambaye aliamua kudumu tangu UTOTONI. Hivyo na wewe umepewa neema, dumu katika neema, dumu katika wokovu, acha kutanga tanga huku na kule. Mungu akaghahiri mema kwako. Ulimwengu hauwezi kukupa unafuu wowote, ni kwa Kristo tu ndio utapata raha nafsini, Hakuna mateso kwa Kristo, Utumwa wake ni mwepesi sana alisema hivyo. Soma (Mathayo 11:28-30).

Ikiwa hujaokoka unasubiri nini sasa? Embu fanya uamuzi wa haraka sana umgeukie Kristo akuokoe. Hizi ni siku za mwisho, anakaribia kurudi kuwanyakua wateule wake. Kama upo tayari kutubu leo dhambi zako, basi fungua hapa kwa  ajili ya mwongozo wa sala ya toba.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini tofauti ya Mtumwa, Mjakazi na kijakazi?

Maana ya Mithali 9:17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu, Na mkate ulioliwa kwa siri hupendeza”

Miimo ni nini na kizingiti ni nini?

Ni kwa namna gani haki huinua taifa? (Mithali 14:34)

AKAPITA KATIKA LILE SHAMBA AMBALO YAKOBO ALIMPA YUSUFU MWANAWE

Nini maana ya Mithali 27:6 “Jeraha utiwazo na rafiki ni amini;

Nini maana ya kukunguwazwa (Marko 14:27)

Rudi nyumbani

Print this post