Title Devis

JIEPUSHE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

Jina la Bwana libarikiwe. Karibu tujifunze Biblia..

Hatari kubwa iliyopo katika siku hizi za mwisho ni Kunyanyuka kwa jopo kubwa la Manabii wa Uongo…Sasa biblia inapotaja uwepo wa manabii wa uongo, haimaanishi tu manabii bali hata waalimu, wainjilisti, mitume, wachungaji, maaskofu, mashemasi(2Petro 2:1) n.k…Yaani kwa ufupi kila karama ina waongo wake…Sasa watumishi wote hao wa uongo biblia imewapa jina moja la ujumla ambalo ndio hilo MANABII WA UONGO.

Kwahiyo akitokea mwalimu anafundisha uongo huyo ni Nabii wa Uongo wa siku za mwisho, kadhalika akitokea mchungaji anafundisha uongo huyo pia ni Nabii wa uongo kulingana na Biblia.

Sasa katika siku hizi za mwisho wameongezeka sana…Ni sababu gani imewafanya waongezeke kwa kasi kiasi hicho?? NI KWASABABU HIZI NI SIKU ZA MWISHO! HILO TU!..Hawajataka wenyewe kunyanyuka kwa nguvu zao hapana! bali kuna nguvu ya siku hizi za mwisho ndio zinazowanyanyua.

Umewahi kujiuliza kwanini karibia na mstari wa mwisho wa riadha, ndio watu wanongeza spidi? Na kelele za mashabiki ndio zinaongezeka?.. umewahi kujiuliza kwanini karibia na goli ndio nguvu za wachezaji zinajiongeza mara mbili?, na kelele zinakuwa nyingi uwanjani?..tofauti na mpira ukiwa katikati ya uwanja?…..ni kwasababu mpira unakaribia mwisho wa uwanja ambapo ni golini.…. karibia na mwisho kuna kitu kinawasukuma wamalizie kwa nguvu ili wafunge goli, na pia kama ukichunguza dakika 5 kabla mpira au mchezo wowote kuisha ndio kelele zinaongezeka uwanjani na wachezaji wanacheza kwa nguvu zaidi? Ni kwasababu mwisho umekaribia….kadhalika mstari wa siku za mwisho tunaoukaribia ndio unaoharakisha mambo kama tunavyoona….kama sio huo mstari wa siku za mwisho tunaoukaribia kuwa karibu na sisi, nguvu hii ya kuwasukuma watu kuzimu isingekuwa kubwa kiasi hiki…Kwasababu muda ungekuwa bado sana

Ndugu ipo nguvu kubwa ya upotevu katika hizi siku za mwisho, imeachiwa, ili imalizie kwa nguvu kuwapeleka watu upotevuni…Na pia kuna nguvu ya Mungu imeachiliwa kwa watu wa Mungu itakayowapeleka kwa nguvu uzimani. Hizo nguvu mbili ndio zinazotenda kazi sasa.

Wale wasiompenda Mungu, hii nguvu ya upotevu inawavaa…Sasa inawavaa vipi?

Mtu alikuwa anapenda ulevi, na haipendi injili inayomwambia aache pombe na hataki kutubu…Mungu anamletewa mhubiri wa uongo atakayemuhakikishia kwa maandiko kitu anachokifanya ni sawa mbele za Mungu..atahubiriwa pombe ni sawa kulingana na maandiko, na atatoka amesafishika akiamini anachokifanya ni sahihi, kumbe kasafishiwa Zaidi njia yake ya kwenda upotevuni…

Na ndio hivyo hivyo siku za mwisho Mungu atawaruhusu manabii wengi wa uongo, watimize kusudi lake, ingawa manabii hao watakuwa wametumwa na shetani.

2Timotheo 3:13 “Lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika”.

2Wathesalonike 2:10 “na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.

11 Kwa hiyo Mungu awaletea nguvu ya upotevu, wauamini uongo;

12 ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu”.

1 Wathesalonike 5: 3 “Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”.

Unaambiwa leo, uvaaji mbaya ni dhambi, uvaaji wa mawigi, vimini, na suruali kwa wanawake ni dhambi lakini hutaki kusikia..Utaletewa mhubiri, aliyesomea chuo cha Biblia kabisa, atakuhakikishia kwa maandiko kwamba vimini, mawingi, suruali, uwanja, lipstiki, sio dhambi…atakupa na vifungu vya biblia na atakuombea kabisa na utapokea hata uponyaji…

Na wewe utatoka umeamini kuwa upo sawa, kumbe tayari umepokea nguvu itakayokufanya kuendelea kufanya dhambi pasipo kuwa na mashaka yoyote..kwasababu mashaka ndio yanayomfanya mtu awe hapo katikati… na mtu aliye katikati anaonekana bado hajakomaa vizuri, hivyo ni ngumu kujua kama ni ngano au gugu…ili kujua ni ngano au gugu ndio inaachiliwa nguvu hiyo juu yake..ikishaachiliwa hiyo nguvu ndio inamfanya achague upande mmoja pasipo kuwa na mashaka…Hivyo ndivyo magugu na ngano vinavyotengwa.

Kadhalika Leo hii unaambiwa Ulimwengu na fahari zake unapita, na usijiwekee hazina duniani mahali ambapo nondo na kutu vinaharibu, unaambiwa usiupende ulimwengu, kwasababu kuwa Rafiki wa ulimwengu ni kuwa adui wa Mungu (Yakobo 4:4) na tena hivi karibuni dunia itafikia mwisho, kila kitu kitaharibiwa na waovu wote wataondolewa na hivyo kila kitu kitakuwa ni kazi bure.…lakini wewe hutaki kusikia hilo, unataka kulazimisha kuwa mambo ya ulimwengu huu yamekubaliwa na Mungu, na kwamba dunia haitaharibiwa kutaendelea kuwa na amani hivi hivi siku zote…. hata wakati mwingine unakejeli na kudharau wanaoukataa ulimwengu na kumtafuta Mungu…

Nataka nikuambie ukweli, ukweli kabisa wa dhati!! nguvu ya upotevu itaachiliwa juu yako…au pengine imeshaanza kuachiliwa ni hujui tu…Mungu atakuletea mhubiri, tena inawezekana akawa ni mhubiri maarufu sana, huyo atakuambia kwa kutumia maandiko matakatifu kuwa bado sana dunia iishe! Atakupa na historia ndefu yenye kutumia akili nyingi, atakuaminisha kuwa bado kuna miaka mingi ya hii dunia kuendelea kuwepo, hakutatokea vita wala matetemeko…hivyo usiogope! Endelea na shughuli zako, Mungu atafuata baadaye.

Ndugu yangu! Hao ni manabii wa Uongo, walioruhusiwa watokee siku hizi za mwisho..wanafanya kazi yao ya kupotosha ulimwengu mzima na wakishamaliza wataenda kuhukumiwa..

Tubu leo, ipende kweli na Itii Injili pasipo kuipunguza, Epuka kusikiliza injili hizi za manabii wa uongo, wanaokufariji katika dhambi, lakini hawakuambii ukweli kuwa, ukiendelea na Maisha ya dhambi unayoishi utakwenda kuzimu. Manabii hao ni asili yao ni kuzimu, na siku ile watu wengi sana watashangaa kuwaona Jehanamu.

Bwana anasema..

Yeremia 23: 15 “Basi Bwana wa majeshi asema hivi, katika habari ya manabii, Tazama, nitawalisha pakanga, nitawanywesha maji ya uchungu; kwa kuwa kutoka kwa manabii hao wa Yerusalemu kukufuru kumeingia katika nchi yote.

16 Bwana wa majeshi asema hivi, Msisikilize maneno ya manabii wakiwatabiria; huwafundisha ubatili; hunena maono ya mioyo yao wenyewe; hayakutoka katika kinywa cha Bwana.

17 Daima huwaambia wao wanaonidharau, Bwana amesema, MTAKUWA NA AMANI; nao humwambia kila mtu aendaye kwa ukaidi wa moyo wake, Hamtapatwa na ubaya wo wote.

18 Maana, ni nani aliyesimama katika baraza la Bwana, hata akalifahamu neno lake na kulisikia? Ni nani aliyelitia moyoni neno langu, na kulisikia?

19 Tazama, tufani ya Bwana, yaani, ghadhabu yake, imetokea; ni dhoruba ya kisulisuli; itapasuka, na kuwaangukia waovu vichwani.

20 Hasira ya Bwana haitarudi, hata atakapokwisha kuyatimiza makusudi ya moyo wake; katika siku za mwisho mtalifahamu neno hili kabisa.

21 Mimi sikuwatuma manabii hao, lakini walikwenda mbio; sikusema nao, lakini walitabiri”.

Kama hujayakabidhi Maisha yako kwa Kristo, unangoja nini?..Kama hujabatizwa ubatizo sahihi wa kuzama mwili wote na kwa Jina la Yesu ni nini unasubiri?..Mlango wa Neema upo wazi sasa, ila hautakuwa hivyo siku zote.

Bwana akubariki.


Mada Nyinginezo:

TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.

MPINGA-KRISTO NI NANI?

JE! MUNGU ATAIANGAMIZA DUNIA TENA BAADA YA GHARIKA YA NUHU?

MANENO HAYA YANA MAANA GANI? “..KWA SABABU HAMTOI ROHO KWA KIPIMO. (YOHANA3:34)”


Rudi Nyumbani:

Print this post

Apandacho mtu ndicho atakachovuna

Wagalatia 6:7 “Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.

8 Maana yeye apandaye kwa mwili wake, katika mwili wake atavuna uharibifu; bali yeye apandaye kwa Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele”.

Hapo inasema “chochote” ikiwa na maana kuwa hata vitu visivyokuwa na maana vikipandwa vinaleta majibu.

Na chochote kinachopandwa huwa kinapandwa kama mbegu…na kinapovunwa kinavunwa kama tunda…embe linapandwa kama mbegu, lakini linavunwa kama tunda..

Mtu akipanda mbegu ya dhambi yoyote moyoni mwake leo, akaipalilia hiyo tabia moyoni mwake, baada ya muda fulani, atavuna matunda ya dhambi hiyo..Na matunda yake ni ya aina mbili…MAUTI YA MWILI, na MAUTI YA ROHO…

Mauti ya Mwili, inaweza kuja kutokana aidha  Ugonjwa unaotokana dhambi hiyo au janga fulani kwamfano dhambi ya uasherati mauti yake ya kimwili inaweza kutokana na ugonjwa fulani kama HIV, GONOREA au kaswende au inaweza kuja kupitia chanel nyingine yeyote tofauti na hiyo..Wengi hawajui kuwa vifo vingi vya ghafla vinatokana na matokeo ya dhambi…hususani dhambi ya uasherati…

Aina ya pili ya tunda la dhambi ni Mauti ya kiroho. Hii ni ile hali mtu anakufa katika kuisikia Injili na kuiamini, upo usemi unaosema “sikio la kufa halisikii dawa” kadhalika, roho iliyokufa haiwezi kuisikia Injili tena, na mwisho wake ni ziwa la moto.

Jiepushe na uasherati kwasababu apandacho mtu ndicho atakachovuna, jiepushe na ushirikina, ulevi, anasa, ushoga, ulawiti, usagaji, utazamaji wa picha na video chafu, ulaji rushwa n.k kwasababu mambo hayo yote matunda yake ni kifo.

Kwasababu biblia inasema Mshahara wa dhambi ni Mauti.

Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Bwana akubariki.


Mada Nyinginezo:

JE! KUNENA KWA LUGHA MPYA KUKOJE?

JE! KUOMBA KWA BIDII KAMA ELIYA NI KUOMBA KWA NAMNA GANI?

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOKUJA JUU YA MTU.

USITAFUTE FAIDA YAKO MWENYEWE BALI YA WENGINE.


Rudi Nyumbani:

Print this post

KIELELEZO CHA MWANAMKE KATIKA NYUMBA.

Wanawake wamepewa na Mungu huduma kubwa sana, na huduma yenyewe ni ULEZI, Mungu aliiweke huduma hii ya kipekee kabisa kwa wanawake kwasababu alijua ikitumiwa ipasavyo italeta faida kubwa sana katika ufalme wake kuliko huduma nyingine yoyote.. lakini cha kusikitisha ni kuwa jambo hilo halitambuliki katikati ya wanawake wengi, wanadhani kuwa kulea ni jambo jepesi lisilo na heshima, na hiyo imewafanya waichukie na kukimbilia kufanya huduma ambazo haziendani na maumbile yao.
 
Nataka nikuambie mwanamke anayetambua nafasi yake hapa duniani, shetani anamchukia zaidi ya kitu kingine chochote ulishawahi kukijua, Kama ukisoma vizuri kitabu cha Ufunuo sura ya 12 utaona pale kuna Ishara ilionekana mbinguni na ishara yenyewe ilikuwa ni ya mwanamke, na mwanamke huyo alikuwa ni mjamzito ambaye anakaribia kujifungua,..Na shetani (ambaye ndio lile joka), lilipojua kuwa yupo katika hali ile, lilisimama limeze kile kilichokuwa ndani ya lile tumbo, kwasababu lilijua vizuri kile mwanamke anachokwenda kukileta kitamletea madhara makubwa kiasi gani huko mbeleni, lakini liliposhindwa basi likasimama pale ili lifanya vita naye, likawa linamuudhi sana mwanamke Yule likawa linafanya visa vya kila namna limuangamize yule mwanamke kisa tu kamzaa Yule mtoto…Lakini ukiendelea kusoma utaona baadaye lilikuja kushindwa, na liliposhindwa biblia inatuambia LILIMKASIRIKIA mwanamke Yule…
 
Ufunuo 12:17 “Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari.”
 
Unaona hapo lilimkasirikia, Halikuwa na haja ya uzao wake, bali lilipambana na yule mwanamke kwasababu lilijua Yule ndio chanzo uzao huo ambao utakuja kumsumbua.
 
Sasa Habari hiyo sio tu inafunua juu ya kanisa la Israeli katika siku za mwisho, lakini pia inatuonyesha picha ya mwanamke halisi na uzazi wake, mfano wa kilichotokea wakati wa Bwana wetu Yesu Kristo kuzaliwa na Mariamu..Shetani alijaribu kumwaangamiza mtoto Yesu na familia nzima mpaka Mungu akawaambia wakimbilie Misri,..
 
Embu fikiria uzao wa Mariamu, mwanamke mwenye hekima ameleta ukombozi mkubwa kiasi gani leo hii duniani, Na hiyo yote ni kwanini? Ni kwasababu alitambua huduma aliyopewa ndani yake na hivyo akaitendea kazi ipasavyo kama wanawake wengine waliomcha Mungu..Mariamu kwanza alikuwa ni bikira hapo kabla hakuwahi kukaribiwa na mwanamume pili alikuwa ni mwanamke mwenye heshima, aliyemcha Mungu..
 
Hivyo Mungu kwa neema zake akamfanya kuwa kituo cha kupitisha majeshi yake ya wokovu..Tukimwangalia tena mwanamke kama Hana vivyo hivyo alisimama katika nafasi yake ya kulea vizuri akamleta Samweli ambaye sio tu alikuwa mwamuzi wa Israeli wakati ule lakini hadi leo tunasoma habari zake na zinatujenga kiimani..
Na leo tutawaangalia wanawake wawili kwenye biblia pengine hukuwahi kuwafahamu, mmoja ni aliitwa LOISI, Huyu Loisi alikuwa ni mwanamke aliyedumu katika imani kweli kweli aliyeilelea familia yake katika misingi yote ya Imani ya Kikristo, mwanamke huyu Paulo alimjua kwa uthabiti wa imani yake…
 
Mpaka alipofikia hatua ya kuzaa, akazaa mtoto wa kike ambaye aliitwa EUNIKE, huyu alifundishwa na mama yake misingi ya imani hivyo mpaka alipokuwa akairithi, Imani isiyokuwa na unafki, naye huyu Eunike akazaa mtoto mwanamume, akamrithisha IMANI ile ile iliyokuwa ndani yake na ndani ya mama yake, akamlea akakua na mtoto huyo ndiye aliyeitwa TIMOTHEO tunayemsoma leo kwenye Biblia…
 
Tunafahamu kuwa Timotheo ndiye aliyekuwa mwangalizi wa makanisa yote yaliyokuwa Asia baada ya Paulo kuondoka kwake..
 
Tukisoma katika ule wakara wa pili ambapo Paulo anamwandikia Timotheo alimwambia maneno haya:
 
Timotheo 1:4 “Nami natamani sana kukuona, nikiyakumbuka machozi yako, ili nijae furaha;
5 nikiikumbuka imani uliyo nayo isiyo na unafiki, ambayo ilikaa kwanza katika bibi yako Loisi, na katika mama yako Eunike, nami nasadiki wewe nawe unayo.”
 
Unaona Bibi aliilea familia yake vizuri, lakini matokeo yanakuja kuonekana kwa wajukuu zake.. Sasa thawabu za wanawake hawa ni kubwa sana mbinguni, hawa ndio Mbinguni watakaokwenda kuketi kama mamalkia waliowazaa majemedari wa wokovu…
 
Na wewe mwanamke, ambaye unayofamilia au unatazamia kuwa na familia, maisha yako unayoishi sasa, jinsi unavyojiweka sasa, ni wazi yanaeleza uzao wako utakuja kuwa wa namna gani huko mbeleni.. Ikiwa wewe wakati wote huna habari na Mungu, unachofahamu ni kuvaa vimini tu, na kukatisha barabarani, na kwenda saluni, na kutembea nusu uchi barabarani,na kuketi vibarazani kuoshwa miguu na wanaume usitazamie kuwa utamletea Mungu matunda yoyote katika ufalme wake kupitia uzazi aliokupa,..Mungu alitazamia kwa uzao wako wainuke akina Samweli, lakini wewe unavyojiweka uzao wako unawanyanyua akina Baraba Yule mwizi na muuaji..Usifikiri kwa kinywa tu ndio unaweza kuulaani uzao wako, kwamba utajizuia usiwanenee vibaya..hapana ndugu! Matendo yako ndio yanayowanenea vibaya wanao..
 
Ukisoma tena utaona licha tu ya Mitume kuwaandika waraka wanaume, utaona pia waliwaandika na wanawake ukisoma kitabu cha Waraka wa pili wa Yohana utaona mtume Yohana anamwandikia mwanamke mmoja, ambaye alimwona analea watoto wake vizuri ambao ndio hao baadaye wanaenda kuwa wakina Timotheo, hivyo akawa anamtia moyo na kumpa maonyo ajiepushe na baadhi wa watu ambao ni wapinga Kristo majoka wanaotaka kuwaangusha wasisimame katika Imani..
 
2Yohana 1:4 “Nalifurahi mno kwa kuwa nimewaona baadhi ya watoto wako wanaenenda katika kweli, kama vile tulivyopokea amri kwa Baba.
5 Na sasa mama, nakuomba, si kwamba nakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo, kwamba tupendane.
 
Mpaka hapo naamini utakuwa umeona ni jinsi gani huduma ya ulezi wa mwanamke ilivyo na nguvu sana katika ufalme wa mbinguni..
 
Na Ndio maana maandiko yanasema:
 
Mithali 14:1 “Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.”
 
Kumbuka nyuma inayozungumziwa hapo sio tu nyuma hii ya mwilini bali pia makao yake huko atakapokwenda baada ya kifo.
Sasa ikiwa wewe hauwi kielelezo kwa mabinti zako, unavaa nguo mbaya mbele yao, wataacheje kukuiga na wewe, unasengenye mbele yao, wataachaje kukuiga… ikiwa wewe sio mwombaji, wataache na wao kuwa sio waombaji, ikiwa hulitafakari Neno la Mungu wataachaje na wao kuwa vivyo hivyo..ikiwa akili zako zimejaa miziki ya kihuni, na wewe huna hata muda wa kuwafundisha nyimbo za kumsifu Mungu unatazamia vipi Mungu atajitwalia watoto kutoka katika hao?
 
Mtu mmoja alisema.. “si kwamba Watoto wa siku hizi wamebadilika, la! Hapana Watoto wa siku hawajabadilika ni wazazi ndio waliobadilika, kwasababu Watoto ni wale wale, wanakaa tumboni miezi 9, wanazaliwa hawana meno, wala hawaongei…lakini wazazi ndio wanaowajaza vitu visivyo sawa, ndio maana tunawaona Watoto wapo hivyo walivyo leo”
Hiyo ni kweli kabisa! Kama mtoto ana mwaka mmoja tu! Tayari Umeshaanza kumsikilizisha midundo ya ulimwengu huu, na unafurahia anavyoserebuka! Ni nani kabadilika hapo?..ni mtoto au ni wewe? Sasa kwanini ulalamike anapokuwa mtu mzima na kuvaa hereni au kawa shoga?
 
Kumbuka tena Leo upo hivyo kesho utakufa, unadhani huko unapokwenda utajivunia nani? Wakati wanawake wengine mashujaa ambao walijitunza na kulea familia zao katika imani kama Sara wanajivunia akina Isaka, na Mungu kuwapa nafasi karibu nao, wakati huo wewe hutakuwa na lolote,..
Huduma uliyopewa wewe ni kubwa, ithamini, shetani hapendi uitumie,..Anza sasa kuishi kama mwanamke wa Kikristo, jenga nyumba yako, ambao kwa hiyo ndiyo itakayokupa thawabu ukifika kule.
 
Na hata kama hujajaliwa kupata Watoto wa kimwili…Pia Maisha yako matakatifu yatawajenga Watoto wengine wasio na wazazi, na hata ambao wana wazazi, lakini wameshindwa kutimiza wajibu wao….na hivyo na wewe kuwa umefanya kazi sawa tu, au hata kubwa kuliko ya walio na Watoto. Na siku ile mbinguni ukaoneshwa jopo la wanao walio mashujaa ulio walea katika Kristo.
 
Ubarikiwe sana.

Mada Nyinginezo:

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA.

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

MWAMBA WETU.

JIFANYIE RAFIKI KWA MALI YA UDHALIMU.

UCHUNGU WA KUIBIWA.

ROHO MBAYA KUTOKA KWA BWANA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNAPEWA PESA, KUNA MAANISHA NINI?

Awali ya yote ili upate ufasaha wa ndoto yako, na kuepuka kudanganywa na kila aina ya tafsiri mtu yeyote anayoweza kukuletea, awali ya yote unapaswa ufahamu ndoto yako inaangukia katika kundi lipi,

Yapo makundi makuu matatu (3) ya ndoto:

  1. Kundi la kwanza: ni zile ndoto zinazotokana na Mungu,
  2. kundi la pili: ni zile zinazotokana na adui(Shetani)
  3. kundi la tatu: ni zile zinazotokana na mtu mwenyewe,

Ndoto zinazoangukia katika kundi hili la tatu ndizo zinazootwa na watu mara kwa mara kila siku na kama mtu asipoweza kuzitambua atajikuta anahangaika nazo, na huku hazina maana yoyote ya kumsaidia, kwasababu ni ndoto zinazokuja kutokana na shughuli anazozifanya kila siku au mazingira yanayomzungumka muda wote hivyo hizi huwa hazibebi  ujumbe wowote..

Kwahiyo ni rahisi ubongo wake kuchukua yale matukio anayoyofanya kila siku na kuyatengenezea matukio yanayofanana na hayo katika ndoto usiku na kuota, ukijiona unaota hivyo basi puuzia ndoto hizo

Ikiwa unahitaji kufahamu kwa undani juu ya makundi haya basi pitia somo hili kwanza >>>> NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI?   kisha ndio tuendelee,

 Kwamfano ndoto za namna hii za kujiona unapewa pesa, utakuta mtu mmoja kazi yake kila siku ipo kwenye pesa kama vile benki au mfanyabiashara ambaye muda wote analipa na kulipwa pesa, hivyo kuota anapewa pesa linaweza kuwa ni jambo la kawaida kwake kutokea katika ndoto zake za kila siku, kwasababu ubongo ulishajiengenezea ulimwengu kama huo.

Lakini ikitokea umeota ndoto katika mazingira, ambayo hayaendani na wewe kupewa pesa, au umeota ndoto hiyo na ukaiona si ndoto ya kawaida, au ulikuwa katika maombi ya kumwomba Mungu kitu Fulani na imekuja na uzito Fulani hivi, au amani Fulani hivi, basi fahamu kuwa upo ujumbe unapaswa kujifunza ndani yake.

Kumbuka kibiblia Fedha inawakilisha chombo cha kuletea jawabu.

Mhubiri 10:19 “Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko, Na divai huyafurahisha maisha; Na fedha huleta jawabu la mambo yote”.

Hivyo Mungu kukuonyesha katika ndoto, unapewa fedha, ni ishara kuwa amekupa jawabu la ombi lako, na hivi karibuni utapata haja yako..Ila tilia maanani kitu kimoja hapo biblia inaposema, fedha huleta jawabu la mambo yote haimaanishi  kuwa inaleta majibu mpaka kwenye mambo ya rohoni hapana, fedha haiwezi kuleta uzima ndani ya mtu wala haiwezi kununua upendo..lakini kama ukichunguza hapo utaona mistari hiyo inalenga mambo ya ki mwilini..kama vile shughuli za karamu, nguo, chakula, nyumba, gari, biashara, ambavyo hivi kimsingi vinahudumiwa na fedha..

Pia tazama..

1  Kuota ajali.
2 Kuota upo nchi nyingine.
3 Kuota unajifungua
4 Kuota upo makaburini
5 Kuota unacheza mpira
6 Kuota unaanguka
7 Kuota upo kanisani
8 Kuota umeachwa na gari
9 Kuota unang’oka meno
10 Kuota unaanguka

Lakini tukirudi kwenye hiyo ndoto ya pesa vile vile usitegemee sana kuwa atatumia njia hiyo hiyo uliyoiona kwamba kweli kuna mtu atakujana  kukupa wewe fedha hapana, inaweza ikawa hivyo au isiwe hivyo, anaweza  kutumia njia pengine ya kuirutubisha kazi yako unayoifanya sasa hivi ,au ukapata kibali mahali Fulani pengine kazini kwako, ambapo boss wako atakulipa vizuri zaidi kuliko sasa hivi, au ukapata mkopo wa kufanya biashara yako n.k.Na kama ukijiangalia ndio utagundua vitu vya aina hiyo hiyo ndio ulivyokuwa unamwomba Mungu…

Hivyo ametumia ndoto ya fedha kama ishara ya kukuonyesha kuwa maombi yako ameyasikia,..Lakini usitazamie kuwa mtu anayemwomba Mungu mambo ya rohoni kama vile uzima wa milele, au Roho Mtakatifu, au nguvu za Mungu, ataonyeshwa ndoto za namna hiyo kama jibu la maombi yake hapana.. Mungu atamwonyesha Maono ya rohoni, pengine usishangae mtu kama huyo kuona maono ya mbinguni, au kukutana na malaika ndotoni, au kuisikia sauti ya Mungu ikisema naye, au kuota anahubiri au anafundishwa biblia n.k…

Hivyo kaa katika matarajio huku ukiulinda ukamilifu na utakatifu  katika kazi yako, ndipo Mungu ataitimiza ahadi yake juu yako. Lakini kama wewe upo nje ya Kristo ukaota ndoto kama hiyo, fahamu kuwa ni ishara mbaya nayo ni ishara ya upotevu zaidi..utakwenda kufanikiwa lakini ni ili upotee..

Mithali 1:32 “Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua, Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza”.

Usisibirie udanganyifu wa mali au mafanikio vikuangamize..Mrudi Muumba wako mapema, tubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha, ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi kwa Jina la YESU KRISTO ikiwa bado hukubatizwa kisha anza kumwangalia Mungu ili yeye atembee pamoja na wewe katika njia zako zote.

Ubarikiwe.

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mithali 1:32

kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza.

Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?

USHUHUDA WA RICKY:

MTETEZI WAKO NI NANI?

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

NOTI YA UFALME WA MBINGUNI.

LULU YA THAMANI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE! MAHUSIANO YA JINSIA MOJA NI DHAMBI?

Mahusiano yoyote yale yanayohusisha watu wa jinsia moja ni machukizo mbele za Mungu..Biblia imeweka wazi katika kitabu cha Mambo ya Walawi

Walawi 18:22 “Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni machukizo”.

 

Walawi 20:13 “Tena mtu mume akilala pamoja na mtu mume, kama alalavyo na mtu mke, wote wawili wamefanya machukizo; hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao”

 

Kutokana na anguko Ipo asili ya dhambi ambayo mtu anazaliwa nayo… inafanya kazi ndani ya mtu, tangu akiwa tumboni mwa mama yake…hiyo inamfanya mtu anazaliwa na tabia fulani fulani ambazo asili yake ni dhambi…mfano wa tabia hizo ni kama hasira zisizokuwa na sababu, kiburi, uchungu usiokuwa na sababu, ukorofu, utundu, tamaa ya uasherati n.k vyote hivyo vinatokana na ile asili ya dhambi mtu anayozaliwa nayo.

Lakini pamoja na hayo, kuna dhambi ambazo Mungu aliziweka mbali sana na mwanadamu kuzifikia, na hizo hazimo miongoni mwa dhambi za asili..Ni dhambi lakini mtu anakuwa hazaliwi nazo… Mtu mwenyewe kwa mapenzi yake anapokuwa mtu mzima anaweza kuzipachika ndani yake na kuzifanya.

Na moja ya dhambi hizo ni dhambi za kumtamani mtu wa jinsia moja na ya kwako. Hiyo tamaa ya namna hiyo haipo ndani ya mtu tangu anazaliwa. Mwanamke kumtamani mwanamke mwenzake au mwanamume kumtamani mwanamume mwenzake…

Dhambi hii ni moja ya dhambi mbaya sana kuliko nyingi kwasababu ipo kinyume na UHAI na UZIMA.

Hebu tafakari endapo Adamu angekuwa na Adamu mwenzake sisi tungetokea wapi? Au wakina Hawa wangeumbwa wawili, sisi tungetokea wapi leo?.. Neno la Bwana linalosema zaeni mkaongezeke lingekuwa wapi?…Hebu fikiri Wanyama wangekuwa wote wa jinsia moja..hii mifugo tuliyonayo leo ingekuwa wapi?…Maziwa tunayokunywa yangetokea wapi? Nyama tunazokula nazo zingetokea wapi, asali tunayoifurahia ingetoka wapi? Endapo nyuki wote wangekuwa wakike au wakiume?

Hata chakula tusingekuwa nacho, kwasababu hata mimea ina sehemu ya kike na ya kiume…sasa kama mimea yote ingekuwa na sehemu ya kiume tu, au ya kike tu…hiyo ngano tunayokula kila siku ingetokea wapi? Mboga tunazokula zingetokea wapi?..Kwahiyo dunia isingekuwa dunia wala Maisha yasingekuwepo endapo kungekuwa na jinsia moja tu duniani.

Kwahiyo dhambi ya mahusiano ya jinsia moja ni dhambi ya KIFO, Kwasababu ipo kinyume na UHAI…Chochote ambacho kipo kinyume na Uhai ni Kifo. Na yeyote afanyaye dhambi ya kifo atakufa.

 

Kaa mbali na ushoga ni dhambi, kaa mbali na usagaji, wapo wengi wanafanya dhambi hizi kwa siri, pasipo kujua madhara ya dhambi hiyo, Ni dhambi zinazoivuta ghadhabu ya Mungu kwa haraka sana….Dhambi zilizoifanya sodoma na ghomora ziteketezwe ni dhambi hizo za mahusiano ya jinsia moja. Na dhambi hizi hazina cha kujitetea kwasababu ni dhambi za makusudi..Mtu anazipandikiza ndani yake akiwa na akili timamu kabisa, hazina ushawishi wowote..hakuna mazingira yoyote yanayomshawishi mtu kumtamani mtu wa jinsia moja na yeye, ni mtu mwenyewe anazitengeneza ndani yake kwa msaada wa roho za mapepo.

Warumi 1:26 “Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili;

27 wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.

28 Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa”

Tubu, kama wewe ni mmojawapo, kisha uanze uanze kutafuta kuyafanya mapenzi wa Bwana. Naye atakuangazia neema zake.

Shalom.

Mada Nyinginezo:

INJILI YA MILELE.

NINI TOFAUTI KATI YA DHAMBI, UOVU NA KOSA KIBIBLIA?

LILE TUMAINI LILILO NDANI YETU LINAPOULIZIWA.

CHACHU YA MAFARISAYO NA CHACHU YA HERODE.

UNYAKUO.

NIFANYE NINI ILI NIIKWEPE HUKUMU.


Rudi Nyumbani:

Print this post

ZIFAHAMU HOJA SABA ZENYE NGUVU MBELE ZA MUNGU.

Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe..Karibu tujifunze Neno la Mungu…Bwana Mungu wetu anatuambia tupeleke hoja zenye nguvu mbele zake?.
 
Isaya 41:21 “Haya, leteni maneno yenu, asema Bwana; toeni hoja zenu zenye nguvu, asema mfalme wa Yakobo”.
 
Sasa swali hizi hoja zenye nguvu ni zipi?
 
Kwanza ni muhimu kufahamu kuwa anaposema tupeleke hoja, tunapaswa tuzipeleke vipi?…ni wazi kuwa hakuna njia nyingine ya kupeleka Zaidi ya kwenye maombi…maombi ndiyo njia pekee ya sisi kuzungumza na Mungu moja kwa moja!….Na pia kama anasema tupeleke hoja zenye nguvu…maana yake zipo pia hoja ambazo ni dhaifu!…Hivyo kwa kufupisha sentensi hiyo tunaweza kuiweka hivi “ tupeleke maombi yanayougusa moyo wa Mungu, au yanayoleta maana” kiasi kwamba yatamsukuma Mungu au kumshawishi kutupa majibu ya maombi yetu.
Sasa maombi hayo ni yapi?..Je ni ya kuomba muda mrefu?, au kupangilia maneno mazuri, au kuombewa na wengine? Au kufunga muda mrefu?…Hayo yote ni maombi ya hoja lakini si ya hoja zenye nguvu.
Maombi ya hoja zenye nguvu yapo SABA, Na hayo si mengine Zaidi ya yale tuliyofundishwa na Bwana wetu Yesu Kristo…alisema..
 
Mathayo 6:6 “Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.
 
7 Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke, kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi.
 
8 Basi msifanane na hao; maana Baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi hamjamwomba.
 
9 Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje,
10 Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.
 
11 Utupe leo riziki yetu.
 
12 Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.
 
13 Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina”.
Hizo ndio hoja zenye nguvu…Katika kusali/kuomba unahakikisha Unautambua kwanza uwepo wa Mungu, pale unaposema Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe, hapo unaliadhimisha moja kwa moja jina la Mwanawe mpendwa Yesu Kristo ambalo ndio jina la Baba alilompa Yesu(soma Yohana 17:6, 17:11) na kwa kupitia hilo, ndilo tunaokolewa kwalo, kwahiyo Unaliadhimisha na kutangaza kuwa linastahili kutukuzwa… Hii ni hoja ya kwanza yenye nguvu mbele za Mungu, Bwana anatamani sana tujue uwezo uliopo kwenye jina lake, si kwa kukariri wala kwa ushabiki, bali kwa ufunuo..Tukijua kuwa hakuna jina lingine, iwe la Raisi, au la Nchi, au la Mfalme, au la Kitu, au la Malaika ambalo sisi wanadamu tumepewa, isipokuwa jina la Yesu…Hii ni hoja moja yenye nguvu sana inayoleta majibu pasipo vipingamizi..
 
Wakolosai 3:17 “Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”
 
Hivyo katika sala pia, tunapaswa tuanze kwa kuliadhimisha na kulitukuza Jina la Yesu.
 
Hoja ya Pili: yenye nguvu ni Kuomba UFALME WAKE UJE!..
Ufalme wa Mungu unakuja kwa namna mbili, 1) Unakuja juu ya mtu, huu unaingia pale mtu anapochukua muda kumtafuta Mungu 2) Namna ya pili ufalme wa Mungu unakuja juu ya dunia nzima, watakatifu watakapofikia kilele cha kumfahamu Mungu, ndipo ufalme wa Mungu utashuka.
Sasa namna zote hizi mbili ni lazima mtu aziombe mbele za Mungu.
 
Wengi hawapendi kuomba ufalme wa MUNGU uje juu ya huu ulimwengu kwasababu wanaupenda bado ulimwengu huu…hivyo hawapendezwi sana wanaposikia tunaishi katika siku za mwisho, na hawapendi kuona siku za mwisho zinafika, kwasababu hawataenda tena disko, hawataenda tena vilabuni,n.k hawajui kuwa Kutokutamani au kutokuomba Ufalme wa Mungu uje ni kumhuzunisha Mungu…Hawajui kuwa kuomba ufalme wa Mungu uje ni hoja yenye nguvu ambayo Mungu anaithamini sana juu ya mtu, na hivyo kumsukuma Mungu kuuleta ufalme wake ndani ya huyo mtu mwenyewe na katika dunia nzima.
 
Hoja ya tatu: Ni kumwomba Mungu, mapenzi yake yatimizwe huku duniani kama huko mbinguni…Kwanini mbinguni kuna utukufu na tunatamani sana kwenda?…Ni kwasababu kule kila siku mapenzi ya Mungu yanatimizwa, ndio maana ni kuzuri na kuna utaratibu.. Wengi hawapendi kumwambia “Mungu mapenzi yako yatimizwe baada ya sala”..Utasikia nataka hiki nataka kile..hiyo sio hoja yenye nguvu na haileti majibu yeyote! Hoja yenye nguvu ni ile inayomalizia na “Baba mapenzi yako yatimizwe, si kama nitakavyo mimi bali kama utakavyo wewe” Bwana Yesu mwenyewe alikuwa na mapenzi yake siku ile kabla ya kusulibishwa kwamba kikombe kile kimwepuke lakini alimalizia na kusema “baba mapenzi yako yatimizwe” wewe na mimi ni nani..tuamrishe mambo kana kwamba dunia ni yetu!…hiyo ni hoja yenye nguvu sana. (SomaYakobo 4:13-16).
 
Hoja ya Nne: Ni kumwomba Mungu atupe riziki zetu, hakusema tumwombe atupe fedha!…sio vibaya kumwomba fedha lakini hapo hakusema tumwombe atupe fedha! Bali riziki…Wengi ndio wanarudi nyuma katika hili Eneo, Wanapomwomba Mungu awape riziki, na riziki ile wanaitafsiri katika fedha tu peke yake, mtu wa Mungu, Mungu anaweza kukupa nyumba pasipo hata kuwa na shilingi 10 mfukoni mwako, anaweza kukupa chakula pasipo hata kuwa na fedha…Kwamfano Mtu anaweza kumwomba Bwana anahitaji wanawe wakasome pengine nje ya nchi, wakati anatazamia Mungu ampe mamilioni ya fedha ya kuwapeleka huko nje ya nchi, Mungu anafungua mlango wale Watoto wanafanya vizuri na kwenda kusomeshwa na serikali na yule mzazi bado akawa hana fedha vile vile…
 
Sasa tayari kashajibiwa maombi yake, ingawa yeye anaweza asione amejibiwa kwasababu alitazamia Mungu ampe mamilioni ya fedha..Mungu hafanyi kazi kwa njia hiyo tu peke yake…
Hebu tafakari wewe mwanao akija na bajeti, na kukwambia baba naomba milioni moja anataka kwenda kununua vitu vya shule utampa?..jibu ni kwamba hutampa badala yake utamwambia aorodheshe anavyohitaji..ndipo uende ukamnunulie..vinginevyo ukimpa hela utampoteza badala ya kumpata, na Mungu wetu hataki tupotee… Usiende kamwe kumwambia Mungu ninashida ya milioni 5 ya ada, au ya nyumba, au ya kiwanja….
 
Nenda kamwambie Mungu nina shida ya kiwanja basi!! Au nina shida ya chakula….Usimtamkie pesa! Kwasababu Mungu haangalii tunahitaji pesa kiasi gani bali anaangalia tunamahitaji kiasi gani?… Utashangaa anakupa hicho kiwanja, au hicho chakula, au hicho kiwanja pengine hata pasipo kutumia hiyo fedha unayoitegemea (Yeye ana njia nyingi sio hiyo wewe unayoifikiria kichwani kwako)…Hebu leo mwulize Mkristo anahitaji nini atakwambia anataka kuwa na hela nyingi, mwulize hizo hela ni za nini?, atakwambia basi tu akaunti yangu iwe inasoma..(sio vibaya kuomba hivyo lakini si hoja yenye nguvu mbele za Mungu)…
 
Usiende kumwomba Mungu fedha ya kitu fulani, kamwombe hicho kitu unachokihitaji, ili atakapofungua njia zake usizozitegemea ukakipata usije ukasema huyo sio Mungu.
Hoja ya tano: Ni kumwomba atusamehe makosa yetu, kama sisi tunavyowasamehe wengine..Zingatia hilo Neno… “kama sisi tunavyowasamehe wengine”…Hii ni hoja ya sita yenye nguvu, usitengeneze desturi ya kuomba pasipo kutubu, wala pasipo kuwasamehe wengine, maombi yako hayatasikilizwa kabisa, kama uliseng’enywa kumbuka na wewe ulishawahi kusengenya hivyo unamsamehe kwanza huyu au Yule ndipo unaendelea mbele.
 
Hoja ya sita: Ni kumwomba Mungu asitutie katika majaribu, lakini atuokoe na yule mwovu…Kutiwa katika majaribu hapo ni hali ambayo Mungu anaruhusu mtu aingie chini ya mikono ya shetani…Na hiyo inaweza kutokana na dhambi za Mtu au ukamilifu wa Mtu…Ayubu aliingia majaribuni kutokana na ukamilifu wake, Lakini Petro aliingia majaribuni kujaribiwa na Ibilisi amkane Bwana Yesu kutokana na Ubishi wake wa kukataa kuomba…Hivyo kwa ufahamu huo kuomba Mungu atuepushe na adui zetu kwa namna yoyote ile ni hoja Mungu anayotaka sisi tuiombe mbele zake na anaiheshimu sana.
 
Hoja ya saba na ya Mwisho: Ni kutambua ya kuwa Ufalme, na Nguvu na Utukufu una Yeye MUNGU wetu Milele na Milele. Kwanini Mbinguni kuna utukufu mwingi?..Ni kwasababu Malaika usiku na mchana wana ukiri Ukuu wa Mungu…
 
Ufunuo 7:11 “Na malaika wote walikuwa wakisimama pande zote za kile kiti cha enzi, na za hao wazee, na za wale wenye uhai wanne, nao wakaanguka kifulifuli mbele ya kile kiti cha enzi, wakamsujudu Mungu,
 
12 wakisema, Amina; Baraka na utukufu na hekima na shukrani na heshima na uweza na nguvu zina Mungu wetu hata milele na milele. Amina”.
 
Kama malaika watakatifu wamepata ufunuo huo, na wanaheshimiwa na Mungu, nasi pia hatuna budi kukiri kuwa ni kweli heshima, utukufu, na nguvu zina yeye Milele na Milele siku zote katika Maisha yetu.Hoja hii ni hoja ya mwisho yenye nguvu..
 
Ndugu, iwapo kwenye maombi usisahau kila kipengele cha mambo hayo!, Na maombi yaliyomfanya Bwana kila saa asikiwe na Baba yake alipokuwa hapa duniani, na hivyo akatufundisha na sisi kusali kwa namna hiyo hiyo, tukizingatia hilo tutaona majibu yasiyo ya kawaida katika dua zetu na sala zetu za kila siku.
 
Bwana akubariki sana. Kama hujampa Kristo Maisha yako, unangoja nini?..Hizi ni siku za mwisho, na Kristo yupo mlangoni kurudi.

Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI.

NI JAMBO GANI LINALOMTAMANISHA SANA BWANA TUMWOMBE BILA KUKATA TAMAA?

WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU.

WEWE SI MALI YAKO MWENYEWE!

UTAJI ULIOKUWA JUU YA USO WA MUSA.

USIPIGE MATEKE MCHOKOO!


Rudi Nyumbani:

Print this post

KALAMU YA CHUMA.

Kitabu cha Ayubu kinasemekana kuwa ni kitabu kikongwe kuliko vitabu vyote katika biblia, ni ngumu kutabiri kiliandikwa mwaka gani au wakati gani, kwasababu habari zilizopo ndani yake hazihusiani hata kidogo na Taifa la Israeli, wala Ayubu mwenyewe hakuwa Mwisraeli. Tofauti na vitabu vingine ambavyo hata kama waandishi wake walikuwa hawajulikani lakini ukisoma maandishi yake ndani ni rahisi kugundua kiliandikwa wakati gani, aidha wakati wa waamuzi, au wafalme, au wakati wa agano jipya ndio maana ilikuwa ni rahisi wanatheolojia wengi kutabiri viliandikwa wakati gani, lakini kitabu cha Ayubu ni cha kitofauti kidogo…Inakadiriwa kuwa Ayubu aliishi kabla ya Taifa la Israeli kuundwa vizazi vichache tu mbeleni baada ya Nuhu, au vizazi vichache nyuma kabla ya Ibrahimu..
 
Lakini tunapaswa tujiulize ni kwanini tunakiona hichi kitabu cha Ayubu miongoni mwa vitabu vitakatifu?,
Tukisoma maisha ya Ayubu aliyopitia, hakuna asiyejua alipitia majaribu mazito, lakini mwisho wa siku Mungu alikuja kumrudishia kila kitu alichopoteza na kumpa utajiri mara mbili, lakini pia habari zake zingepaswa zifahamike na watu wa kizazi chake tu, au hata kama zingeandikwa basi zingekuja kusomwa na watu wa vizazi vichache mbeleni, au hata kam zingedumu basi kingewekwa na kuwa ni moja vya vitabu vya kihistoria tu za imani na mashujaa, ambavyo hata sasa vipo vingi ambavyo vilivyorekodi matukio ya mashujaa waliyoyafanya zamani za kale, kama vile kitabu cha YASHARI ambacho tunakiona katika (2Samweli 1:18)..
 
Lakini jambo moja tunalisoma, Ayubu alipokuwa katika hali ile ya shida, alitamani sana moyoni mwake mateso anayoyapitia yaandikwe kwa kalamu ya chuma, yadumu milele ili yasomwe na vizazi vyote mbeleni, pengine yeye alivyotamani vile alidhani kuwa Mungu anaweza asimsikie lakini Mungu alimsikia na maneno yake yote aliyokuwa anayazungumza yakaandikiwa kweli kwa kalamu ya Chuma..Na ndio maana hadi leo hii tunayasoma yamewekwa miongoni mwa vitatu vitakatifu.
 
Ayubu 19:23 “Laiti maneno yangu yangeandikwa sasa! Laiti yangeandikwa kitabuni!
24 Yakachorwa katika mwamba milele, Kwa kalamu ya chuma na risasi.
25 Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai, Na ya kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi.
26 Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi, Lakini, pasipokuwa na mwili wangu nitamwona Mungu;”
 
Kama tunavyofahamu kalamu ya chuma sikuzote ni tofauti na kalamu za kawaida, kalamu ya kawaida inatumika kuandika tu, na pale mtu anapohijita kufanya marekebisho ni rahisi kwani anafuta tu au anayapaka maandishi yale rangi, na kisha anaandika mengine tena..lakini kalamu ya chuma, yenyewe haina wino, bali yenyewe huwa inaandika kwa kuchonga, hususani kwenye mbao ngumu sana, au mwamba…wale ambao wapo katika sanaa ya uchoraji wanafahamu, inafanana na driller, kama ni Neno Fulani linaandikwa basi ile kalamu inapitishwa kwenye mbao inaichimba mbao ile kulingana na umbo la Neno lile, na ukikosea kidogo tu basi mbao hiyo inatupwa haifai tena, ukiandika umeandika maandishi yale yatadumu milele pale, na kufuta kwake ni kuharibu mbao hiyo yote au mwamba huo, hakuna njia nyingine…
Na ndio maana leo hii tunayasoma maneno ya Ayubu.. Hii ni kuonyesha kuwa hata rohoni ipo kalamu ya chuma ambayo Mungu anaitumia kuandika fadhili au mema ya Mtu anayoyoafanya hapa duniani..
 
Lakini kinyume chake pia ni kweli, kalamu hiyo hiyo ya chuma, inaandika dhambi na makosa ya watu wanayoyafanya hapa duniani.. Na hiyo nayo ikishaandikwa haifutiki tena milele hata iweje, kufutika kwake ni mtu huyo kuangamizwa basi, hakuna njia nyingine.
 
Tukisoma biblia enzi za wafalme wana wa Israeli walikuwa wanamkosea Mungu kwa kiwango cha hali ya juu sana, lakini Mungu kwa rehema zake alikuwa akiwapelekea manabii wake wengi kuwaonya waache dhambi zao na ibada za sanamu, wamrudie Mungu wao, lakini badala yake walikuwa wanawapuuzia, wengine wanawaua, wengine wanawapiga kwa mawe, mpaka ikafakia wakati Mungu akaiandika dhambi yao kwa kalamu ya Chuma..kukawa hakuna tena msamaha..Ndipo Wakati ulipofika walivamiwa na maadui zao ambao ni Mungu mwenyewe aliwaleta wakauliwa sana, wengine wakachukuliwa mateka Babeli wengine Ashuru, wengine walikufa kwa njaa, ndipo walipomlilia Mungu na kuombolezea lakini Mungu hakuwasikia…mji mzima ulichomwa kukawa hakuna tena kitu kinachoitwa Taifa la Israeli, na adhabu hiyo iliwaathiri mpaka watoto wao vizazi na vizazi, kwa muda wa zaidi ya miaka 2500, kulikuwa hakuna taifa linaloitwa Israeli,..Ni mwaka 1948 ndio limekuja kuundwa tena, na kuwa taifa huru kama zamani..
Unaona Siku ya uharibifu wao ilipofika hawakuamini kuwa ndio wao wanachukuliwa mateka tena kama ilivyokuwa kule Misri..
 
Yeremia 17:1 “Dhambi ya Yuda imeandikwa kwa kalamu ya chuma, na kwa ncha ya almasi; imechorwa katika kibao cha moyo wao, na katika pembe za madhabahu zenu;”
 
Hayo ndio madhara ya dhambi ya mtu kuandikwa kwa kalamu ya chuma, inawezekana na wewe, umesikia injili mara nyingi, Mungu amekuonya kupitia njia nyingi, uache hiki auche kile, umgeukie yeye ayatakase maisha yako, lakini hutaki, unaipuuzia hiyo sauti, unaona kama bado unao muda, kumbuka dhambi zako leo zinasameheka sasa, lakini kama utendelea kuukataa wokovu, ujue kuwa umeukataa mwenyewe na umechagua kwa akili zako mwenyewe kudumu katika dhambi. Mungu akishakuona upo hivyo anaiandika dhambi yako kwa kalamu ya chuma, ikishafika hiyo hatua ujue kuwa hakuna kugeuka tena..wewe ni ibilisi milele.
 
2Nyakati 36: 14 Na zaidi ya hayo wakuu wote wa makuhani, na watu, wakakosa mno sawasawa na machukizo yote ya mataifa; wakainajisi nyumba ya Bwana aliyoitakasa katika Yerusalemu.
 
15 Naye Bwana, Mungu wa baba zao, akatuma kwao kwa mikono ya wajumbe wake, akiondoka mapema, na kutuma; kwa sababu aliwahurumia watu wake, na makao yake;
 
16 lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, hata ilipozidi ghadhabu ya Bwana juu ya watu wake, hata kusiwe na kuponya.
 
17 Kwa hiyo akaleta juu yao mfalme wa Wakaldayo, aliyewaua vijana wao kwa upanga nyumbani mwa patakatifu pao, asiwahurumie kijana wala mwanamwali, mzee wala mkongwe; akawatia wote mkononi mwake”
 
Ndugu Neema si ya kuchezea kabisa…usijaze uovu juu ya uovu..Dunia hii tunayoishi, ipo siku itafika, Kutakuwa hakuna kuponywa tena! Unyakuo ukishapita, hata watu watubu vipi, kutakuwa hakuna msamaha.
 
Tubu angali unao muda, mlango wa neema upo wazi kwa ajili yako, mbingu inakuita, fungua moyo wako sasa.
 
Ubarikiwe sana. Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine. Ili nao waisikie injili.

Mada Nyinginezo:

DHAMBI YA MAUTI.

NGUVU YA UPOTEVU.

MIISHO YA ZAMANI.

MATUMIZI YA DIVAI.

MUNGU KUSEMA NA WEWE PEKEE, HAITOSHI KUKUPA USHINDI.

NABII ELISHA ALIKUWA ANA MAANA GANI KULIA NA KUSEMA”GARI LA ISRAELI NA WAPANDA FARASI WAKE”?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Mungu hawezi kukusahau

Kama unamcha Mungu kweli, na unakwenda katika njia zake, yeye ni mwaminifu hawezi kukusahau. Kabla maisha yako hayajaisha hapa duniani, atakuridhisha, atakufikisha mahali ambapo ni zaidi hata ya ulivyokuwa unafikiri.

Kama hakumsahau Yusufu, ambaye aliuzwa Kama Mtumwa Taifa la mbali kabisa, hawezi kukusahau wewe kama unakwenda katika njia zake.

Kama hakumsahau Musa ambaye aliacha hazina zote za Misri  na kwenda majangwani, hawezi kukusahau wewe uliyeacha kila kitu na kumfuata  Mungu..

Waebrania 11:26 “akihesabu ya kuwa kushutumiwa kwake Kristo ni utajiri mkuu kuliko hazina za Misri; kwa kuwa aliyatazamia hayo malipo.

27 Kwa imani akatoka Misri, asiogope ghadhabu ya mfalme; maana alistahimili kama amwonaye yeye asiyeonekana”

Kama hakumsahau Hana aliyekuwa Tasa na kumpatia watoto wengi..Hawezi kukusahau wewe unayemcha leo, hajabadilika ni yeye yule vizazi na vizazi,

Isaya 49:14 “Bali Sayuni alisema, YEHOVA ameniacha, Bwana amenisahau.

15 Je! Mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie mwana wa tumbo lake? Naam, hawa waweza kusahau, lakini mimi sitakusahau wewe.

16 Tazama, nimekuchora katika vitanga vya mikono yangu; kuta zako ziko mbele zangu daima”.

Mche tu yeye! Jitenge na uovu, kuwa mtumishi wake..Utauona wokovu wake, hatakusahau kamwe! hawezi kusema uongo. 

Isaya 44:21 “Kumbuka haya, Ee Yakobo; nawe Israeli, maana wewe u mtumishi wangu; nimekuumba; u mtumishi wangu; Ee Israeli, hutasahauliwa na mimi”

Kinachowakosesha wengi ni dhambi katika maisha ya watu,vitu kama uasherati, usengenyaji, wizi, ulaji rushwa, utukanaji, ibada za sanamu, wivu, biashara haramu, uvaaji mbaya, kutokusamehe n.k hivyo ndivyo vitu vinavyoharibu mpango wa Mungu juu ya maisha yetu…Lakini mtu akijitenga na hivyo Kamwe Mungu hawezi kumsahau, haijalishi itapita miaka mingapi lakini atakuja kuuona utukufu wa Mungu maishani mwake.

Ubarikiwe.


Mada Nyinginezo:

MNGOJEE BWANA

SAMEHE KUTOKA NDANI YA MOYO WAKO.

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA JIKANE MWENYEWE?

“HERI WALIO MASKINI WA ROHO MAANA UFALME WA MBINGUNI NI WAO” JE HATUNA RUHUSA YA KUWA MATAJIRI KATIKA ROHO?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Kuota unakimbizwa.

Moja kwa moja ndoto kama hii inatoka kwa Yule mwovu, kukimbizwa kwa namna yoyote ile maadamu ni kukimbizwa basi ni kutoka kwa yule mwovu, iwe ni kuota unakimbizwa na watu au kuota unakimbizwa na nyoka au kuota unakimbizwa na ng’ombe, au kuota unakimbizwa na simba, au kuota unakimbizwa na tembo au kuota unakimbizwa na nyuki, au kuota unakimbizwa na kichaa, ni ndoto kutoka kwa mwovu…Sikuzote kitu kinachokimbizwa ni kitu kilicho dhaifu, cha kuwindwa ili kiliwe, swala anakimbizwa na simba, ni kwasababu yeye ni dhaifu, lakini kitu chenye ujasiri kamwe hakikimbizwi.

Ukijiona unakimbizwa fahamu kabisa moja kwa moja kuwa wewe ni dhaifu rohoni, na hiyo  ni kutokana na kuwa upo nje ya Kristo au kama upo basi hauijatambua mamlaka uliyonayo ndani ya Kristo kwa uchanga wako wa kiroho au kwa uzembe wako wa kutokujishughulisha na mambo ya Mungu..

Mithali 28:1 Waovu hukimbia wasipofuatiwa na mtu; Bali wenye haki ni wajasiri kama simba.

Hivyo mrudie Mungu wako kama bado haujaokoka, Tubu ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na uwe kwa Jina la Yesu Kristo, ili upate ondoleo la dhambi zake. Au kama tayari ulikuwa ndani ya Kristo na ulikuwa unayumba yumba huu ni wakati wako sasa kusimama imara.

Kisha anza kujifunza biblia kwa bidii, na pia tafuta kanisa la kiroho la kwenda kujifunzia Neno la Mungu, ili likae kwa wingi ndani yako, upate kujua nafasi uliyonayo katika Kristo. Mpaka siku moja na wewe uote unamkimbiza shetani.

2Wakorintho 10:4 “(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)”

Usipuuzie ndoto hizo, kwasababu shetani kweli anakuwinda akumeze…Fanya uamuzi wa busara kumgeukia Mungu.

Ubarikiwe.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi


Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

MTETEZI WAKO NI NANI?

SIKU YA TAABU YA YAKOBO.

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Kuota unafanya Mtihani.

Hii ni moja ya ndoto ambayo inaotwa na watu wengi sana, na hii huwa inachukua maumbile tofauti tofauti, wengine utakuta wanaota wanafanya mitihani na hawajajiandaa, wanachoshtukia tu ni wakati wa mtihani umefika, na hakuna chochote walichofanya wanajiuliza siku zote alikuwa wapi…wengine wanaota wanafanya mtihani mgumu sana lakini wenzao wanaonekana wanafahamu cha kujaza yeye hajui,

wengine wanaota kama walikatisha masomo wakaondoka, baadaye waliporudi muda umeshapita mitihani ya mwisho imekaribia, wengine wanaota wamerudia madarasa ya nyuma ambayo tayari wameshayavuka siku nyingi na ni lazima wayavuke ili waendelee na madarasa ya mbele, wengine wanaota wapo wanafundishwa, wengine wanapewa adhabu, wengine wapo tu n.k.…Kwa ufupi ndoto unazoota upo katika mazingira ya shule, zote zina maudhui moja.

Na ndoto hizi huwa zinatesa sana, zinaweza kujirudia hata kila baada ya wiki au mwezi, au miezi kadhaa, inategemea na mtu na mtu, lakini ni ndoto ambazo haziachi kuja.

Biblia inasema..

Ayubu 33:14 “Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali.

15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani;”

Mungu siku zote huwa anapenda kutumia vitu vinavyotuzunguka kutufikishia sisi ujumbe fulani , na ndio maana utaona Bwana Yesu alipokuwa anafundisha mifano yake yote alikuwa anatumia mambo ya kawaida tu yanatozunguka sikuzote ili kutufikishia sisi ujumbe na tuulewe utaona wakati mwingine alitumia mifano ya ndege, wafanyabiashara, wafalme, harusi n.k…

Hivyo na Mungu ili kukufikisha ujumbe wake wa wokovu huwa anapenda kutumia mfano wa kitu ambacho kimetukuka sana mbele yako, kitu chenye maana sana kwako ambacho ukikikosa anajua kabisa umekosa maisha na hicho si kingine zaidi ya  ELIMU.

Kufunua kuwa Ipo elimu iliyokuu ambayo inayo ufunguo sio tu wa maisha ya hapa bali pia wa maisha ya ulimwengu unaokuja, na hiyo si nyingine zaidi ya Elimu ya Ufalme wa Mbinguni..Mungu anakuonyesha hali yako ya kiroho ilivyo kupitia maisha yako ya shuleni, kama unavyojiona upo shuleni hujajiandaa, au mtihani ni mgumu basi katika roho ndivyo hivyo ulivyo..  kuwa upo nyuma, na unapaswa ushinde, yapo madarasa haujayavuka bado, upo pale pale kiroho umekwama, unatamani uendelee mbele unashindwa au unaona ni ngumu kwasababu bado hujayamaliza madarasa ya nyuma Mungu aliyokupa.

Hivyo unapaswa uongeze bidii yako kwa Mungu, ili ufike pale Mungu anapotaka kufika, ongeza kiwango chako cha maombi, jifunze Neno la Mungu sana, ishi maisha yanayompendeza Mungu, punguza muda wa kuihangaikia dunia, na ongeza muda wako wa kumtafuta Mungu, kwasababu yeye ndio ufunguo wa kweli wa maisha yako ndugu. Ukimpata Mungu umepata vyote.

Mathayo 6:33 “Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.”

Hivyo ukiwa na bidii na  Mungu akaridhika na wewe basi atakuvusha na kukupeleka katika kiwango kingine cha kiroho na kiufahamu. Kumbuka Mungu anakupenda na ndio maana anakuonyesha ndoto kama hizo, Hivyo usipuuzie ungeza bidii yako kwake.

Ubarikiwe.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

NITAONGEZAJE NGUVU ZANGU ZA ROHONI?

TABIA ZA ROHONI.

NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?

ZIFAHAMU HUDUMA KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.

HATA ILIPOTIMIA SIKU YA PENTEKOSTE.

MTEGEMEE MUNGU, NA SI MWANADAMU.


Rudi Nyumbani:

Print this post