Category Archive maswali na majibu

Nini maana ya kikombe cha maji ya baridi(Mathayo 10:42)?

SWALI: Kikombe cha maji ya baridi ni  kipi Bwana alichokitaja katika;

Mathayo 10:42  Na mtu awaye yote atakayemnywesha mmojawapo wa wadogo hawa ngaa kikombe cha maji ya baridi, kwa kuwa ni mwanafunzi, amin, nawaambia, haitampotea kamwe thawabu yake


JIBU: Ni kawaida mtu anayetoka kufanya kazi ngumu, labda ya shamba, au wanaoshiriki katika michezo labda riadha au mipira, utaona huduma ya kwanza wanayoihitaji, sio chakula, bali ni maji, kwasababu mwili huwa unapoteza maji mengi sana pale jasho linapotoka. Na gharama ya maji sikuzote ni ndogo kuliko chakula. Hivyo mtu yeyote huwa ni rahisi kupata huduma hiyo, kwani mtu anaweza kumtolea ndani mwake kwenye pipa lake la kutunzia maji masafi, au kuchota kisimani, na kumpa n.k. Na pale anapompa ya baridi kabisa basi humfanya mtu yule ayanywe yale maji sio tu kwa kukata kiu lakini pia kwa burudiko.

Vivyo hivyo na Bwana naye anawafananisha watu wake, na watenda kazi waliotoka kufanya kazi ya kuchosha, hivyo na wenyewe huwa wanakuwa na kiu chao, wanahitaji maji yao. Lakini zaidi sana maji baridi. Na mtu anayefanya hivyo Mungu amemuahidia kumpa thawabu yake.

Maji ya mwaminio ni yapi?

Yanaweza kuwa ni vyakula: Kwamfano umuonapo, mtumishi wa Mungu labda anahudumu au anahubiri pengine kwenye masoko, au mahali fulani kwa muda mrefu, na wewe ukathamini kumpatia chakula au hata chupa ya maji. Akanywa au akala akashiba akamshukuru Mungu. Hiyo ni thawabu kwako kwa Mungu.

Yaweza pia kuwa sadaka yako: Kile kidogo, kinachoweza kumtunza hata kwa siku hiyo, kwa ajili ya usafiri, au sabuni, au vocha kwa ajili ya mahitaji yake madogo madogo. Bwana amekuahidia pia thawabu yako hata kama utakiona ni kidogo, si zaidi  ukampa vya ziada? Kinabadilika kuwa kikombe cha maji ya baridi.

Yaweza kuwa pia ni “vitu”: Mfano mwingine hana fedha au chakula, lakini ana kitu Fulani cha kumpa, labda nguo, au kiatu, au simu, au huduma n.k. Hicho nacho Bwana anakihesabu kama kikombe cha maji ya baridi.

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa zipo thawabu mbalimbali ambazo Bwana anatoa, kwa kutenda mema, zipo thawabu za kuwasaidia maskini, zipo thawabu za kuwasaidia ndugu, lakini zaidi pia Bwana ameahidi thawabu kwa wale wote wanaowajali watumishi wake.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mafundisho mengine:

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA.

JE NI KIKOMBE KIPI UTAKINYWEA SIKU ILE?

YESU ANA KIU NA WEWE.

UWE KIKOMBE SAFI 

AGENDA KUBWA YA SHETANI KWA KANISA HILI LA LAODIKIA.

MAJI YA UZIMA.

Rudi nyumbani

Print this post

Fahamu maana ya Mhubiri 10:9 Mwenye kuchonga mawe ataumizwa kwayo;

SWALI: Nini maana ya Mhubiri 10:9 Mwenye kuchonga mawe ataumizwa kwayo; Naye apasuaye miti huona hatari katika hiyo.


JIBU: Mstari huu unatuonyesha hatari ya kazi yoyote inayotendwa na mtu. Hapo ametumia mfano wa wanaochonga mawe. Wajenzi wa zamani walikwenda kuchonga mawe miambani kwa ajili ya ujenzi wa majengo yao, lakini wakiwa kule walikutana na hatari nyingi, aidha kuangukiwa na mawe hayo, na kuwaponda viungo vyao, vifaa vyao  vya uchongaji kuwajeruhi.

Vilevile anatumia tena mfano wa wanaopasua miti, kwa ajili ya mbao za ujenzi, bado na wao pia wanakutana na hatari, aidha kuangukiwa na miti yenyewe, au shoka kuteleza na kumjeruhi mtu au yeye.

Kumbukumbu 19:5 kama aingiapo mtu na mwenziwe mwituni kwenda kukata kuni, akapeleka mkono wake na shoka ili kukata mti, likatoka shoka katika mpini, likampiga yule mwenziwe hata akafa; basi na akimbilie katika miji hii mmojawapo awe hai.

Ni sawa na mjenzi ambaye amezoea kupiga sana nyundo au kuwepo maeneo ya ujenzi muda wake mwingi, utaona upo wakati nyundo itateleza na kumponda kidole chake, au atakanyaga msumari n.k. Tofauti na kama angekuwa hajishughulishi na kazi hiyo yupo nyumbani tu.

Hii ni kufunua nini rohoni?

Kama wana wa Mungu tufahamu kuwa kazi yake ya kwenda kung’oa mapando ya mwovu, katika shamba la Bwana  tutarajie kukutana na madhara yake, si wakati wote utakuwa ni mwepesi tu (yaani kuvuna), zipo nyakati tutakutana na kupigwa, au kudhalilishwa, au kufungwa na wakati mwingine hata kuuawa. (Mathayo 10:17-19)

Mtume Paulo alipokuwa katika ziara zake za kupanda ukristo Asia na Ulaya, alikutana na hatari nyingi, ikiwemo kupigwa mawe na watu wabaya, kufungwa, na kurushiwa vitisho mbalimbali. Wamishionari kama dr David Livingstone walioleta injili Afrika zamani walikutana na hatari za magonjwa kama malaria, na wanyama wakali.

Lakini katika yote, Bwana ameahidi, mafanikio makubwa,  kuliko hatari zake. Hivyo hatupaswi kuogopa na kudhani kuwa kazi ya Mungu ni kazi ya kwenda kujichinja wakati wote. Hapana, zipo nyakati nyingi za raha, na mafanikio makubwa ya rohoni yasiyokuwa na ghasia yoyote, lakini Bwana hajatuficha pia hatari zake wakati mwingine. Ili tutakapokutana nazo tusihuzunike moyo na kukata tamaa, bali tuendelee na kazi.

Bwana akubariki.

Je! Umeokoka? Je! Umesamehewa dhambi zako? Kama ni la, ni nini kinachokusubirisha? Ukifa leo utakwenda wapi, kumbuka lipo ziwa la moto, kumbuka ipo hukumu kwa waovu. Tubu leo mgeukie Kristo akusafishe dhambi zako,  Ukabatizwe katika jina la Yersu Kristo upokee ondoleo la dhambi. Hizi ni siku za mwisho, Kristo anakaribia kurudi.

Ikiwa upo tayari leo kufanya hivyo basi fungua hapa kwa mwongozo huo>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mafundisho mengine:

Yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.

Je! fedha ni jawabu la mambo yote? (Mhubiri 10:19).

TUUTAFUTE UMOJA WA ROHO.

Fahamu maana ya Mithali 28:20 Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele;

NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?

FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana jijaribuni wenyewe na ‘isipokuwa mmekataliwa’?

SWALI: Biblia inamaana gani inaposema jithibitisheni wenyewe kama mmekuwa katika imani, na pale pia inaposema “isipokuwa mmekataliwa”? Maana yake ni nini?

2 Wakorintho 13:5

[5]Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Isipokuwa mmekataliwa.

JIBU: Kama wakristo biblia inatuasa tuwe watu wa kufanyia mazoezi Imani yetu, ili tujithibitishe kama kweli tupo katika mstari sahihi wa Imani au la.

Ili kuelewa tuchukue mfano wa  kijana mdogo ambaye anajifunza kuendesha baiskeli. Kwa hatua za mwanzo ni dhahiri kuwa atatumia baiskeli yenye miguu mitatu, ili iweze kumsaidia kumpa uwiano asianguke, na hivyo akiwa katika baiskeli Ile anaweza kuiendesha Kwa jinsi awezavyo kwasababu akikosa ule uwiano( balance), basi Ile miguu ya pembeni itamsaidia..na hivyo ataendesha bila changamoto yoyote, kama tu yule mtu anayejua kuendesha.

Lakini ijapokuwa atakuwa  anaiendesha Kwa kasi au maringo kiasi gani bado hajaweza kuwa mwendeshaji kamili, Mpaka siku yatakapotolewa Yale matairi ya pembeni, na kumwacha aimudu  mwenyewe ile baiskeli kama waendeshaji wengine. Pale ndipo utakapojua kweli huyu alikuwa ameshaweza au la!. 

Hivyo tunaweza kusema, kama hajaweza kujisimamia mwenyewe tayari amekataliwa (yaani, hajakubalika kama mwendesha baiskeli kamili)

Ndivyo ilivyo katika ukristo. Kuna wakati utakuwa unashikwa mkono, lakini upo wakati utahitaji kusimama mwenyewe kujithibitisha, kwamfano labda ilikuwa ikifika muda wa maombi unapigiwa simu/ au unahimizwa na kiongozi wako kufanya hivyo, na kweli unaamka na unasali sana. Lakini huna budi kujijengea ufahamu huu ikiwa siku moja kiongozi wako hayupo, au amesahau kukupigia simu au amepoa  je utaamka mwenyewe uombe?. Ukiona Unaweza kufanya hivyo basi tayari wewe umethibitika katika Imani. Lakini ikiwa ni kinyume chake basi bado kiroho hujakubalika.

Jiulize unapokuwa Mazingira yasiyo ya kikanisa, mazungumzo unayozungumza ni ya namna gani. Ikiwa sio ya maana, hata kama utakuwa unahubiri na kuzungumza habari za Mungu, uwapo na wapendwa muda mrefu kiasi gani..bado kiroho hujakubalika (umekataliwa)..unapaswa ujitengeneze .

Hivyo yatupasa tujijaribu Kwa namna hiyo. Ukristo ni sisi kuwa Nuru katika Giza, sio Nuru katika Nuru tu. Hatuvai vizuri tunapokwenda kanisani tu, Bali hata tunapokuwa katika Mazingira yasiyo ya ibadani. Huko ndiko kujithibitisha. Mungu anavutiwa na mkristo anayethibitisha Imani yake miongoni mwa wenye dhambi zaidi ya yule anayefanya Kwa waaminio. Jitathimini unapokuwa mwenyewe, ni Nini unatazama mitandaoni, muda wako mwingi unautumiaje,ni nani unayechati naye?. Wajibu wako Kwa Bwana unautimizaje? Huko ndiko kujithibitisha.

Lakini ikiwa tuwapo nje tunashindwa kuwa kama tuwapo ndani basi hilo Neno “isipokuwa mmekataliwa”, ndio linakuja..maana yake bado hatujakidhi vigezo vya kiroho, Mungu anavyovitazamia kwetu. Ukiwa ni kundi la kusukumwa  kutenda jambo Fulani la kiroho lililo wajibu wako, bado hujakubalika.

ukiona hivyo basi yakupasa ufanye juhudi, kumaanisha wokovu wako Kwa Mungu. Kama mkristo usijisifu kwenye juhudi za kusimamiwa, jisifu kwenye juhudi za kujisimamia.

Hiyo ndio tafsiri yake, lakini Neno hilo halimaanishi kama watu wengine wanavyodhani kuwa wapo watu ambao “Mungu amewakataa” ambao hata iweje hawawezi kuupokea wokovu hapana, watu wote wanapokelewa na Mungu wanapotii sauti ya Mungu. Hakuna mtu ambaye akimfuata Mungu hata akionyesha juhudi kiasi gani  atakataliwa, hapana.

Bwana akubariki.

Je! Na wewe upo kundi gani? Una habari kuwa hizi ni nyakati za mwisho? Neema ya Kristo inakuita hata Leo, ujue kuwa haitafanya hivyo milele. Ni heri utubu dhambi zako ufanye badiliko, upate ondoleo la dhambi, Yesu Akupe uzima wa milele. 

Ikiwa upo tayari Kwa jambo hilo basi..fungua hapa Kwa mwongozo huo >>>  KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya Mathayo 23:15 inaposema namfanya kuwa mwana wa jehanum mara mbili zaidi kuliko ninyi wenyewe.

USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

Nini maana ya “wanawake saba watamshika mtu mume mmoja”

NI NANI ATAKAYEWAPA ILIYO YENU WENYEWE?

Kwanini Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasichukue chochote isipokuwa fimbo tu?

UNAVYOZIDI KUWA MWENYE HAKI, NDIVYO KUJITAMBUA KWAKO KUNAVYOPUNGUA.

Rudi nyumbani

Print this post

Jina Lusifa (lucifer), tunalisoma wapi kwenye biblia? 

JIBU: Hakuna Mahali popote katika biblia ya Toleo letu la Swahili Union version (SUV) au matoleo mengine kadha wa kadha ya kiswahili, utapishana na hili Neno Lusifa. Lakini swali, kama ni hivyo Kwanini tunalitumia kumwakilisha shetani. Je! Limetokea wapi?

Neno hili ni la kilatini, ambalo linamaanisha NYOTA YA ALFAJIRI. Hivyo tukirudi katika maandiko upo unabii katika kitabu Cha Isaya unaomwelezea shetani, na unamtaja yeye kama ndio  Ile “Nyota ya alfajiri”

Isaya 14:12

[12]Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi!  Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa!

Hivyo watakatifu wa zamani, walipokuwa wanatafsiri biblia kutoka katika lugha ya kiyahudi kwenda kilatini (vulgate), kwenye Karne ya 4  Ndipo Neno hili nyota ya alfajiri ambalo linalosomeka kama “Helel” Kwa lugha ya kiebrania likaandikwa kama “lusifa” Kwa kilatini.

Na baadaye Neno hili lilikuja kupata umaarufu, zaidi katika biblia ya Toleo la kiingereza inayojulikana  kama King James version (KJV), kwani waliendelea kuliacha Neno hili la kilatini, Mahali palepale  panaposema nyota ya alfajiri. 

Hivyo umaarufu wa Neno hilo ukasambaa sio tu Kwa waongeaji wa lugha ya kilatini, Bali mpaka Kwa wale wa kiingereza. Na ndio maana mpaka sasa wewe unalifahamu.

Lakini matoleo mengine mengi, Ikiwemo letu hili la kiswahili (SUV), haikutoa katika hiyo lugha ya kilatino, Bali imeacha vilevile kama nyota ya alfajiri.

Hivyo Kwa kuhitimisha ni kuwa shetani ndio huyo huyo Lusifa. Ikiwa utapenda kufahamu majina yake mengine kama yanavyotajwa kwenye biblia basi fungua hapa >>> APOLIONI.

Je! Unahabari kuwa hizi ni siku za mwisho na Yesu anakaribia kurudi? Umejiandaaje? Kumbuka shetani anatambua kuwa muda wake umeisha(Ufunuo 12:12), iweje wewe usitambue. Ni nini unachokisubiria usimkaribishe Yesu katika maisha Yako?  Huu ulimwengu hauna muda mrefu unaisha, itakufaidia nini upate kila kitu, kisha upate hasara ya nafsi yako? Jifikirie  usisubiri kukumbushwa kumbushwa, ni wewe mwenyewe kuona hali halisi, kisha uchukue hatua

, ikiwa upo tayari Kumpa Bwana Yesu maisha yako, basi fungua hapa Kwa mwongozo wa Sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

 Ubarikiwe.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

NYOTA ZIPOTEAZO.

Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?

Shetani ni nani?

YUKO WAPI MFALME WA WAYAHUDI?

Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?

Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 3)

Rudi nyumbani

Print this post

Washami ni watu gani katika biblia?

Jibu: Washami wametajwa mara nyingi katika biblia, baadhi ya mistari iliyowataja na kama ifuatayo.. 2Samweli 8:6, 1Wafalme 20:21, 2Wafalme 5:2, Yeremia 35:11, Amosi 9:7 na sehemu nyingine nyingi utaona jamii hii ya watu ikitajwa.

Tukio mojawapo maarufu lililozungumziwa katika biblia liwahusulo Washami, ni lile la Nabii Elisha kulipiga upofu Jeshi lao na kuliongoza mpaka katikati ya Samaria. (soma 2Wafalme 6:10-20).

Sasa swali hawa Washami walikuwa ni watu gani?

Washami walikuwa ni watu walioishi katika Nchi ijulikanayo kama Siria/Syria kwasasa,

Kiswahili cha Siria ni  “Shamu” hivyo wenyeji wa nchi ya Shamu ndio walioitwa Washami.

Jamii ya watu hawa Washami, kwasasa haipo!, wala haijulikani, kutokana na Falme nyingi kupita zilizotawala dunia na hivyo kuchanganya jamii za watu katika maeneo husika, hivyo hakuna jamii ya washami ijulikanayo leo duniani, lakini nchi hiyo bado ipo, na sasa wanaishi waarabu (Uzao wa Ishmaeli), ndio inayoitwa Siria, na makao makuu yake ni Dameski. (Kumbuka hawa waarabu sio washami  waliozungumziwa katika biblia, bali wapo tu kama wahamiaji waliohamia katika hiyo nchi)

Kiroho Washami wanawakilisha jeshi la Adui, kwani ukisoma katika biblia  utaona ni karibia mara zote jeshi hili lilikinzana na Israeli. Na utaona wakati ule Elisha alipokuwa na mtumish wake, walipoona jeshi la Washami limewazunguka, Elisha alimwambia mtumishi wake asiogope kwani walio upande wao ni wengi kuliko jeshi wanaloliona mbele yao.

2Wafalme 6:15 “Hata asubuhi na mapema mtumishi wake yule mtu wa Mungu alipoondoka, na kwenda nje, kumbe! Pana jeshi la watu, na farasi na magari, wameuzingira mji ule. Mtumishi wake akamwambia, Ole wetu! Bwana wangu, tufanyeje?

16 Akamjibu, USIOGOPE; MAANA WALIO PAMOJA NASI NI WENGI KULIKO WALE WALIO PAMOJA NAO.

17 Elisha akaomba, akasema, Ee Bwana, nakusihi, mfumbue macho yake, apate kuona. Bwana akamfumbua macho yule mtumishi; naye akaona; na tazama, kile kilima kilikuwa kimejaa farasi na magari ya moto yaliyomzunguka Elisha pande zote.”

Hali kadhalika na sisi ni lazima siku zote tuone, na kufahamu kuwa jeshi la Mungu linalotuzunguka ni kubwa kuliko lile la Adui, ikiwa tupo ndani ya Neema ya damu yake!, lakini kama tupo nje ya Neema ya damu yake (yaani wokovu), basi tufahamu kuwa adui atakuwa na nguvu juu yetu, na wala hakuna tutakachoweza kumfanya, Nguvu yetu na ujasiri wetu upo katika Yesu tu?

Je umeokoka? Kama bado ni afadhali ukaokoka leo, maana hujui kesho itakuwaje, na kama unahitaji msaada huo basi wasiliana nasi kwa namba zetu tajwa hapa chini.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Wasamaria walikuwa ni watu gani?

Kisiwa cha Patmo kipo nchi gani?.

KAMA MTUMISHI WA MUNGU, TAFUTA MAARIFA KWA BIDII.

BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.

Je Yuda alienda wapi, ni mbinguni au jehanamu?

Rudi nyumbani

Print this post

Je Yuda alienda wapi, ni mbinguni au jehanamu?

Hili ni moja ya maswali yanayoleta mkanganyiko miongoni mwa wakristo wengi? Baadhi wanaamini kile kitendo tu cha yeye kujutia makosa yake mpaka kupelekea kutoona faida ya kuishi hadi kwenda kujinyonga ni toba tosha, baadhi wanaamini tayari alikuwa ni mtume aliyechakuliwa na Yesu, hivyo hata iweje hawezi kwenda kuzimu, kwasababu Mungu hachagui vilivyo dhaifu. Lakini baadhi bado wanashikilia kuwa alikwenda kuzimu, kwasababu alikuwa mwizi na mwisho wa kifo chake ilikuwa ni kujinyonga. Na hiyo ni uthibitisho kuwa alipotea.

Lakini tuangalie maandiko yanatupa alama gani kuhusiana na hatma ya Yuda, ndipo tutakapoitimisha kwamba Yuda alikwenda wapi.

Bwana Yesu alisema maneno haya kwa Yuda;

Mathayo 26:24  Mwana wa Adamu aenda zake, kama alivyoandikiwa; lakini ole wake mtu yule ambaye amsaliti Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu yule kama asingalizaliwa.

Pa kutilia umakini ni hilo Neno alilohitimisha nalo,  “Ingekuwa heri kwake mtu yule kama asingalizaliwa”.linatupa picha mbaya kwamba mtu huyo alikuwa  hana faida yoyote duniani, maisha yake ni kama bure.

Lakini pia, kuna maneno mengine ambayo Bwana Yesu aliyasema katika sala yake; Alisema..

Yohana 17:12  Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.

Kuonyesha kuwa Yuda alipotea.

Lakini andiko lingine, tunalisoma katika kitabu cha matendo ya mitume, wakati mitume wanapiga kura kuchagua mtume atakayesimama mahali pa Yuda. Nao pia walisema maneno haya;

Matendo 1:24  Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili, 25  ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe. 26  Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja.

Utaona hapo anasema “aende zake mahali pake mwenyewe”. Ikimaanisha kuwa Yuda hakwenda mbinguni bali mahali pake, na huko si kwingine zaidi ya  kuzimu.

Hivyo kwa vifungu hivyo vyote, hatuoni mahali popote maandiko yanatupa viashiria kuwa Yuda alikwenda mahali pazuri, ukizingatia kuwa katika hatua zake za mwisho hadi kujinyonga, biblia inatuambia aliingiwa na “shetani”. Maana yake ni kuwa shetani alifanya kiti cha enzi ndani yake, hivyo maamuzi yote aliyokuwa anayafanya yalisukumwa na yule mwovu, sio Mungu. Kwahiyo hakuna kitendo cha ki-Mungu alichokifanya Yuda tangu wakati ule.

Hili ni fundisho kubwa sana, hususani kwa watumishi wa Mungu. Bwana kukuita haimaanishi kuwa huwezi potea. Au huwezi ingiliwa na shetani. Petro aliteleza mara kadhaa, na alivamiwa na shetani kinywani mwake, lakini hakukubali kumpa adui nafasi, vivyo hivyo na wewe, hupaswi kusema mimi nina kanisa kubwa, mimi ninahubiri, mimi nimetokewa na Yesu. Kumbuka Yuda aliishi na Yesu kwa zaidi ya miaka mitatu, sio kutokewa nusu saa, lakini alianguka, kwasababu aliipa dhambi nafasi katika maisha yake.

Nasi pia tunapaswa tusimame, dhambi isichukue nafasi yoyote mioyoni mwetu. Kwasababu hiyo inaanza kama tamaa, kisha inachukua mimba, kisha inazaa mauti. Kaa mbali na dhambi.

Bwana atusaidie..

Je! Umeokoka? Je unahabari kuwa hizi ni siku za mwisho, na Yesu yupo mlangoni kurudi?. Umejiandaaje, unaishije, unatazamia nini baada ya haya maisha? Ni heri utubu dhambi zako sasa, umrejee Bwana, usamehewe dhambi zako, Kumbuka adui anakuwinda sana, usiishi maisha kama ya wanyama, wewe ni wa thamani, mbele za Mungu wako.  ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi waweza fungua hapa kwa msaada wa mwongozo wa sala ya Toba >>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Je ni kweli Yuda hakuwa na dhambi kwa kumsaliti Bwana, kwasababu tayari ilikuwa imeshatabiriwa?

JINSI BWANA ALIVYOWACHAGUA MITUME WAKE.

YUDA ISKARIOTE! MTUME ALIYECHAGULIWA NA BWANA YESU.

Kwanini Bwana Yesu alitokea katika ukoo wa Yuda?

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

Ni kwa namna gani Yesu ni Simba wa Yuda?

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini kuwe na kitabu Cha kumbukumbu la Torati na kwanini kiitwe vile?

Kitabu hiki katika lugha ya kiebrania kinasomeka kama “Devarim” ambayo tafsiri yake ni “Maneno”

Na ndio maana mstari wa kwanza kabisa un itaanza Kwa kusema. “Haya ndiyo maneno”

Kumbukumbu la Torati 1:1

[1]Haya ndiyo maneno Musa aliyowaambia Israeli wote ng’ambo ya Yordani barani, katika Araba lililoelekea Sufu, kati ya Parani, na Tofeli, na Labani, na Hazerothi, na Dizahabu.

Lakini katika tafsiri ya kigiriki Cha kale (septuagint),  kilisomeka kama “deuteronomioni” chenye maana ya “Mrudio wa sheria” ambapo Kwa sisi kinasomeka kama “kumbukumbu la sheria/torati”. 

Ni kitabu Cha Tano ambacho kiliandikwa na Musa karibia na mwisho wa Ile miaka 40, wakati walipokuwa ng’ambo ya Yordani katika nchi ya Moabu.

Lengo la kuandikwa kitabu hicho ni kukumbushwa sheria na maagizo ya Mungu, kwasababu kundi kubwa la Wana wa Israeli lililopokea sheria Kule mlima Sinai mwanzoni, lilifia jangwani, hivyo kile kizazi kipya Hakikuwa na msingi imara juu ya sheria za Mungu. Na ndio hapa Musa anaagizwa na Mungu awakumbushe Wana wa Israeli sheria yake.

Kitabu hiki kimeanza kuwakumbushia safari Yao Toka Misri, pia kikagusia jukumu lao la kumpenda Mungu na kuzishika sheria zake. Ikafuatana na baraka na laana ambazo zitampata mtu katika kutii au kutokutii, na mwisho kifo cha Musa.

Je ni Nini tunajifunza kuwepo kwa kitabu hiki ? 

Bwana anataka na sisi tuweke kumbukumbu la agano lake mioyoni mwetu, Kwa vizazi vijavyo tupende kuwafundisha vizazi vinavyochipukia Neno la Mungu, tusiwaache tukadhani wataelewa tu wenyewe kisa biblia ipo, bila kukumbushwa Kwa kufundishwa.

Musa alifanya vile ndio maana kizazi kile kikawa imara baada ya pale.

Na sisi tuwe watu wenye tabia hii, Sio kwa watoto tu hata Kwa kondoo wa Bwana kanisani. Mara Kwa mara tuwakumbushe maagizo ya Mungu.

Kwa maelezo ya ziada kuhusu kitabu hichi pitia hapa >>> https://wingulamashahidi.org/2019/05/13/vitabu-vya-biblia-sehemu-ya-2/

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Vitabu vya Deuterokanoni ni vya ki-Mungu?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Mtiririko wa vitabu vya biblia kwanini upo vile?

Je! Mwendo wa Sabato ulikuwaje kibiblia?(Matendo 1:12)

NJIA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.

Nini maana ya “Atamwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake”. (2Wathesalonike 2:8).

Rudi nyumbani

Print this post

Chetezo ni nini katika biblia? (Walawi 10:1)

Chetezo ni kifaa/chombo kidogo kilichotumika katika tendo la kuvukiza uvumba ndani ya Hema ya Mungu au katika hekalu la Mungu. (Tazama picha juu).

Wakati kuhani alipotaka kufanya kazi za kikuhani ndani ya hema/hekalu la Mungu. Kabla ya mambo yote ilikuwa ni lazima avukize uvumba ndani ya hema/hekalu, lengo la kufanya vile ni kukijaza chumba chote moshi wa ule uvumba.

Hivyo alitwaa kozi mbili za makaa ya moto ambayo yalikuwa yanapatikana katika madhabahu ndogo (ijulikanayo kama madhabahu ya uvumba), iliyokuwa inapatikana upande wa kushoto wa patakatifu pa patakatifu.

Na akiisha kuyachukua yale makaa, ndipo anayatia ndani ya hiko chetezo pamoja na manukato yenye kutoa harufu nzuri yaliyotengenezwa kwa viungo maalumu alivyoviagiza Mungu mwenyewe…

Kutoka 30:34 “BWANA akamwambia Musa, Jitwalie manukato mazuri, yaani, NATAFI, NA SHEKELETHI, NA KELBENA; VIUNGO VYA MANUKATO VIZURI PAMOJA NA UBANI SAFI; vitu hivyo vyote na viwe vya kipimo kimoja;

35 nawe utafanya uvumba wa vitu hivyo, manukato ya kazi ya ustadi wa mtengenezaji manukato, yatakuwa yamekolea, safi, matakatifu”.

Na baada ya kuhani, kuvichoma viungo hivyo (manukato) pamoja na yale makaa ndipo moshi huo huo wenye harufu nzuri hupanda juu na kukijaza chumba chote, na hivyo Mungu hushuka kuipokea ibada hiyo. (Tendo hilo ndilo linaloitwa kuvukiza uvumba).

Ilikuwa ni kosa kubwa kufanya kazi ya kikuhani bila kuvukiza uvumba kwanza, vile vile ilikuwa ni kosa kubwa kuhani kutumia viungo vingine katika manukato au moto mwingine mgeni tofauti na ule wa madhabahuni katika zoezi la kuvukiza uvumba..(Soma Kutoka 30:9, Hesabu 3:4).

Kwa mapana zaidi kuhusu Kuvukiza uvumba fungua na ujumbe gani umebeba kiroho fungua hapa >>> KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

Swali ni je katika agano jipya tuna amri/agizo la kufukiza uvumba katika nyumba za Ibada kama makuhani walivyofukiza katika nyumba ya Mungu katika agano la kale?

Jibu ni la!.. Katika agano jipya hatuna amri wala agizo hilo, kwasababu agano letu si tena la mwilini bali la rohoni, kama vile tusivyozitumia tena damu za wanyama katika ondoleo la dhambi bali damu ya YESU vile vile, hatuvukizi tena uvumba kwa namna yakimwili bali uvumba wetu sisi ni “maombi”.

Sasa CHETEZO kinawakilisha nini kiroho?.

“Chetezo” inawakilisha “moyo wa mtu” kama vile moto unavyowekwa ndani ya chetezo na uvumba kuvukizwa juu ndipo utukufu wa Bwana uonekane…Vivyo hivyo na sisi ni lazima Moto wa Roho Mtakatifu uwashwe ndani yetu na ndipo tuweze kumtumikia Mungu na kuomba sawasawa na mapenzi yake, kwa maana ule uvumba katika nyumba ya Mungu ni ufunuo wa maombi ya watakatifu katika agano jipya. (Ufunuo 8:3).

Je Moyo wako umeufanya safi?.. Biblia inasema tulinde mioyo yetu zaidi ya vyote tuwezavyo kuvilinda (Mithali 4:23).

Bwana atubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

SISI TU MANUKATO YA KRISTO.

MADHABAHU NI NINI?

USICHELEWE KUMPAKA BWANA MARHAMU!

MUNGU HATAZAMI MOTO WA KIGENI,KUWA MAKINI!

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Habari iliyo katika 1Nyakati 21:25, na 2Samweli 24:24, ya Daudi kununua kiwanja  inajichanganya?

SWALI:  Ni ipi gharama sahihi ambayo Daudi aliilipia, kununulia shamba la Arauna, kwa ajili ya kumjengea Mungu hekalu. Je! Ni shekeli 600, au shekeli 50?. Je! Biblia inajichanganya.

JIBU:  Tusome,

2Samweli 24: 24 Lakini mfalme akamwambia Arauna, La, sivyo; lakini kweli nitavinunua kwako kwa thamani yake; wala sitamtolea Bwana, Mungu wangu, sadaka za kuteketezwa nisizozigharimia. Hivyo Daudi akakinunua hicho kiwanja cha kupuria na wale ng’ombe kwa shekeli hamsini za fedha.  25 Naye Daudi akamjengea Bwana madhabahu huko, akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Basi Bwana aliiridhia nchi, na tauni ikazuiliwa katika Israeli.

1Nyakati 21:25 “Basi Daudi akampimia Arauna thamani ya mahali pale shekeli mia sita za dhahabu kwa uzani  26 Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu huko, akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, akamlingana Bwana; naye akamwitikia kutoka mbinguni kwa moto juu ya madhabahu hiyo ya sadaka ya kuteketezwa”

Vifungu hivyo havijichanganyi,  vyote vipo sahihi. Mwandishi wa kitabu cha Samweli anaeleza lile eneo ambalo lilikuwa ni la kupuria tu, pamoja na wale ng’ombe gharama zake jumla ndio shekeli hamsini, lakini sio eneo lote la kiwanja. Tukirudi kwenye 1Nyakati mwandishi anaeleza sasa eneo lote, anatumia neno “mahali pale”. Kwamba jumla yake yote ni shekeli mia sita. Gharama zote za mahali pale zilikuwa ni shekeli 600

Kwamfano wewe unaweza ukawa umelenga kupanunua mahali Fulani kwa ajili ya shughuli zako za kimaendeleo. Lakini ikakugharimu ununue sehemu yote ili uweze kupamiliki vizuri na pale. Hivyo kama eneo lile tu moja gharama yake ilikuwa milioni 1, Lakini kwasababu ya kulipia fidia kwa watu kando kando kuwahamisha, na kodi, na ukarabati n.k. unajikuta unaenda mpaka milioni 20.

Ndicho kilichomkuta Daudi.

Kwahitimisho ni kuwa vifungu hivyo vipo sahihi havijichanganyi.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Swali: Je idadi ya askari waliohesabiwa katika 1Nyakati 21:5 na 2Samweli 24:9 inajichanganya?.

Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

NI KWANINI WATU WENGI WANASHINDWA KUMWELEWA MUNGU?

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.

Je! Wamwona mtu mwenye bidii katika kazi zake?

Novena ni nini? Na je ipo kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Novena ni nini? Na je ipo kibiblia?

Jibu: Neno “Novena” limetokana na neno la kilatini “Novem”… lenye maana ya “Tisa”(9). Madhehebu baadhi ikiwemo Katoliki na Orthodox yamelitoa neno hili na kulitumia katika aina Fulani ya mfululizo wa sala kwa kipindi cha siku 9.

Sala hizo zinahusisha kuomba kwaajili ya  jambo fulani au kushukuru, na zinahusisha ibada za kuomba Rozari kwa wakatoliki (jambo ambalo si sahihi kibiblia). Na kwanini kusali Rozari sio agizo la biblia?, fungua hapa kwa maelezo Zaidi >>>JE SALA YA ROZARI TAKATIFU NI YA KIMAANDIKO?

Sasa msukumo wa kuomba Novena, (yaani siku 9) mfululizo umetokana na matukio maalumu yanayotokea baada ya siku 9, au miezi 9 kumalizika. Kwamfano utaona kabla ya Pentekoste kutimia, walikusanyika Mitume na watu wengine baadhi mahali pamoja kuomba, na wakaomba kwa muda wa siku 9, baada ya Bwana Yesu kupaa na siku ya 10 ikawa ni Pentekoste.

Hivyo ushawishi huu wa kupokea Roho Mtakatifu baada ya maombi ya siku 9, ukaaminika na madhehebu hayo kubwa ni lazima uendelee ili kupokea kitu kingine mfano wa hicho kutoka kwa Mungu, vile vile mwanamke anajifungua mtoto baada ya miezi 9, hili nalo likawafanya viongozi wa madhehebu haya kuamini kuna kitu katika 9, (novena).

Sasa swali ni je! Biblia imetuagiza kutumia mfumo wa Novena, katika maombi ili kupokea jambo maalumu kutoka kwa Mungu? Kwamba tuwe na maombi maalumu ya kurudia rudia kwa muda wa siku 9 ili tupokee jambo kutoka kwa Mungu?.

Jibu ni la!.

Biblia haijaagiza mahali popote tusali “Novena” kwamba tuwe na kipindi Fulani maalumu cha siku 9 mara kwa mara ili Mungu aachilie kitu juu yetu. Utaratibu huu umetengenezwa na wanadamu, kufuatia ushawishi wa siku ya Pentekoste. Hivyo kama umetengenezwa na wanadamu, hauwezi kuwa Sharti, au Agizo la lazima kwa wakristo, kwamba usipofanya hivyo ni kosa kibiblia!.

Agizo hili linaweza kuwa la binafsi, kama tu vile mfungo usivyokuwa sharti, ni jinsi mtu atakavyosukumwa na kuongozwa kufunga!.

Lakini mbali na hilo hata kama Novena ingekuwa ni agizo la biblia, bado inavyofanyika na madhehebu baadhi ikiwemo Katoliki, bado haifanyiki sawasawa na maandiko.. Kwasababu katika biblia tunaona kabla ya Pentekoste walikuwa wamekusanyika mahali pamoja wakisali, wakimwomba Mungu na Mariamu mama yake Yesu alikuwemo miongoni mwao, naye pia akimwomba Mungu, na hawakuwa na sanamu ya mtakatifu Fulani aliyetangulia kufa!, bali walikuwa wakimwomba Mungu aliye juu, (Matendo 1:12-14)

Lakini leo hii katika sala hizo za Novena ni kinyume chake!, wanaoombwa ni watakatifu waliokufa ikiwemo Maria mwenyewe, jambo ambalo ni kinyume kabisa na maandiko!, hivyo badala ziwe sala za Baraka, zinageuka na kuwa ibada za sanamu! (Bwana Yesu atusaidie sana!!).

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Novena haipo kibiblia,..kama mtu atajiwekea utaratibu wake binafsi wa kusali Novena, na sala hiyo ikawa ni kulingana na Neno la Mungu, isiyohusisha sanamu wala desturi za kipagani basi hafanyi dhambi!, huenda ikawa bora kwake.

Lakini inapogeuka na kuwa sharti, na tena ikahusisha ibada za sanamu basi inakuwa ni machukizo makubwa mbele za Bwana kulingana na maandiko.

Bwana atusaidie!.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)

Ni lazima mtu aongozwe sala ya toba ili awe ameokoka?

SALA YA UPONYAJI/MAOMBI YA UPONYAJI.

Kuna tofauti gani kati ya SALA na DUA?

Ni lazima mtu aongozwe sala ya toba ili awe ameokoka?

Rudi nyumbani

Print this post