BIRIKA LA SILOAMU…Bwana Yesu alisema..”Mtu akiona kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure”.
Shalom, karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu wetu ambalo ni mwanga wa njia zetu, na taa iongozayo miguu yetu.
Yohana 9:6 “Alipokwisha kusema hayo, alitema mate chini, akafanya tope kwa yale mate. Akampaka kipofu tope za macho,
7 akamwambia, Nenda kanawe katika birika ya Siloamu, (maana yake, Aliyetumwa). Basi akaenda na kunawa; akarudi anaona”
Bwana wetu Yesu angeweza kumponya mtu huyu pasipo hata kumwambia akanawe katika birika la Siloamu.. Tafsiri ya birika ilivyotumika hapo sio birika la kuwekea chai au maji ya moto..hapana! bali birika maana yake ni Bwawa dogo lililotengenezwa kwa kusudi maalumu…ni kama swimming pool kwa lugha ya kiingereza..
Katika Yerusalemu zamani za agano la kale, lilikuwepo birika hilo ambalo lilitengenezwa mara ya kwanza na Mfalme wa Israeli aliyeitwa Hezekia, ukisoma 2Wafalme 20:20 utaliona jambo hilo,..lakini birika hilo lilikuja kubomolewa na Mfalme wa Babeli Nebukadneza, lakini baadaye lilikuja kutengenezwa tena na Nehemia…na likaendelea kuwepo mpaka wakati wa kipindi cha Bwana Yesu…ingawa lilikuja kufanyiwa ukarabati tena na Herode.
Yohana 7: 37 “Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe.
38 Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.
39 Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa”.
Yohana 4: 6 “Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita.
7 Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe.
8 Kwa maana wanafunzi wake wamekwenda mjini kununua chakula.
9 Basi yule mwanamke Msamaria akamwambia, Imekuwaje wewe Myahudi kutaka maji kwangu, nami ni mwanamke Msamaria? (Maana Wayahudi hawachangamani na Wasamaria).
10 Yesu akajibu, akamwambia, Kama ungaliijua karama ya Mungu, naye ni nani akuambiaye, Nipe maji ninywe, ungalimwomba yeye, naye angalikupa maji yaliyo hai.
11 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, huna kitu cha kutekea, na kisima ni kirefu; basi umeyapata wapi hayo maji yaliyo hai?
12 Je! Wewe u mkubwa kuliko baba yetu, Yakobo, aliyetupa kisima hiki, naye mwenyewe akanywa maji yake, na wanawe pia, na wanyama wake?
13 Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;
14 walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.
15 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka.
16 Yesu akamwambia, Nenda kamwite mumeo, uje naye hapa”
Je umeyapata hayo maji?..Roho Mtakatifu ndiye maji ya Uzima..anakata kiu ya dhambi, kiu ya uasherati, kiu ya rushwa,kiu ya wizi na kila aina ya uchafu, maji hayo yanapatikana bure…
Ufunuo 21: 6 “Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure”
Ufunuo 22:17 “Na Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure”.
Pengine umesikia habari hizi za maji ya uzima mara nyingi sana zisizohesabika…lakini nataka nikuambie ukiyadharau haya maji leo yanayopatikana bure utayatamani siku ile katika ziwa la moto na utayakosa kama yule Tajiri aliyemwomba Lazaro achovye kidole chake kwenye maji hayo ili auburudishe ulimi wake akakosa…Na ndivyo siku ile utayatamani maji hayo utayakosa…usikazane kutafuta maji ya upako, au kutafuta kuzamishwa kwenye mabwawa yajulikanayo kama mabwawa ya upako..tafuta MAJI YA UZIMA…Bwana atusaidie tuyapate maji haya kwa wingi..ili tuwe na Uzima…Tunamshukuru sana Bwana wetu Yesu Kristo wa kutuletea maji haya ya uzima..jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Maran atha!
Mada Nyinginezo:
BWANA ANAPOTUKASIRIKIA ANA LENGO ZURI NA SISI NDANI YA MOYO WAKE.
Marko 3:5 “Akawakazia macho pande zote kwa hasira, akiona huzuni kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao, akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako. Naye akaunyosha; mkono wake ukawa mzima tena.
6 Mara wakatoka wale Mafarisayo, wakawa wakifanya shauri juu yake pamoja na Maherodi, jinsi ya kumwangamiza”
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima. Neno la Mungu ndio chakula kitupacho uzima wa milele,. hivyo tunapochukua muda kulitafakari kila siku,. basi tunafanya jambo ambalo faida yake hatutaiona hapa peke yake, bali hata miaka miaka trilioni moja mbele.
Leo kwa neema za Mungu tutaangazia jambo moja kwa ufupi juu ya Hasira ya Kristo..Tukiyatafakari hayo maneno hapo juu tunaona kuna wakati Bwana alikwenda kwenye sinagogi na kukutana na mtu ambaye alikuwa na mkono uliopooza…
Lakini alipotaka kumponya, aligundua kuwa Mafarisayo na Maherodi walikuwa wanamzivia ili wamjaribu kama atamponya mkono wake siku ya sabato, ili wapate kumshitaki..Lakini yeye alipogundua hilo akakasirika sana, akatulia kwa muda akiwaangalia wale watu kwa hasira..kuanzia kushoto kwake mpaka kulia kwake, wale waliokuwa mbele yake, hadi wale waliokuwa nyuma yake… wote aliwaangalia kwa makusudi ili wauone uso wa Kristo ulivyojaa hasira..
Ni rahisi kusema huyu mtu kashaanza kutuchukia,. Au huyu mtu anakinyongo Fulani ndani yake kwa ajili yetu, lakini tunasoma biblia inasema, ndani ya moyo wake,. Alikuwa na huzuni kubwa kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao.. Alikuwa anawaonea huruma ndani ya moyo wake, alikuwa anawapenda upeo na hivyo hataki wapotee na ndio maana japokuwa uso wake ulikuwa umejaa hasira nyingi,.. Lakini moyoni mwake alikuwa unadondosha machozi mengi ya huzuni.. Hiyo ndio hasira ya kweli ya ki-Mungu.
Mungu anapokukemea kwa ajili ya dhambi zao, usidhani kuwa Mungu anakuchukia, au anakutesa, au ni mkatili,. uso wa Mungu unapogeuka kwako, usidhani kuwa Mungu hakupendi, lakini badala yake anafanya hivyo kwasababu anataka ugeuke usipotee, moyoni mwake anakuthamini kushinda wewe unavyodhani..(kumbuka tena Bwana anapotukasirikia ana lengo zuri na sisi)
Mungu anapokuambia, uzinzi unaofanya utakupeleka kuzimu, usidhani anakuchukia,. Anapokuambia, rushwa unayokula, ushirikina unaoufanya, matambiko na kafara unazozitoa, moja ya hizi siku utakwenda kuchomwa katika moto usiozimika,. Sio kwamba anakuchukia, anapokuadhibu kwa dhambi zako, na kumwona Mungu kwako kama ni mkatili mwenye uso wa hasira sikuzote kwako..Furahia ni kwasababu anakupenda, na anataka ubadilike..wakati mwingine anakunyang’anya hata baadhi ya vitu ulivyonavyo, au unamwomba hakupi hata kimoja,. Sio kwasababu hakujali, au hakuoni, hapana, Kaonyesha uso wa hasira nyingi kwako kwasababu njia zako ni mbaya..
Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.
16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.
17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.
18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.
19 Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.
20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.
21 Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi.
22 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa”.
Mungu akikupenda hata acha kuonyesha uso wa hasira kwako, hataacha kukuonya juu ya dhambi zako, kama vile leo hii anavyokuonya.. Anakueleza ukiendelea kuvaa nguo za nusu uchi utaishi jehanamu ya moto,. ukiendelea kutazama pornography utaishi jehanamu ya moto, ukiendelea kwenda disko utakufa siku moja na kushukia kuzimu…kwasababu anasema wote niwapendao! anawakemea.
Hivyo usishupaze shingo yako,. bali utubu leo hii, mgeukie Bwana wako, ili uugeuze uso wake wa hasira na kuwa wa furaha. Unachotakiwa kufanya ni kujisalimisha kwa Bwana, ukiwa na mzigo wa dhambi zako, na kumwambia, nisamehe nimekosa Mungu wangu na leo hii ninataka kuanza upya tena..Ninaacha hiki, ninaacha kile kwa kumaanisha kabisa..
kwa kuanza kujishughulisha na mambo ya Mungu na kukaa mbali na dhambi ulizokuwa unazifanya hapo kabla,. kama ni nguo za kizinzi unazichoma, kama ulikuwa unaishi na mke/mume ambaye si wako unamuacha.. kama ulikuwa unakwenda bar, unaacha, kama ulikuwa unatazama picha chafu mitandaoni unazifuta,.. kama ulikuwa unafanya uasherati na girlfriend au boyfriend hamjaona, unaacha, kisha unaanza kutafuta ndugu wa kikristo na kukaa nao,..
Sasa Mungu akishaiona Imani kama hiyo, na toba yako iliyoambatana na matendo kama hayo,. yeye mwenyewe kuanzia huo wakati anachukua jukumu la kukufanya kuwa mwana wake kweli kweli, atakupa uwezo wa ajabu wa kuweza kuyashinda hata yale ambayo ulikuwa huwezi kuyaacha..Na mwisho wa siku utajikuta umeshaimarika ndani ya Kristo kwa viwango vya juu sana.
Lakini pia kumbuka, mara baada ya kutubu kwako unapaswa ukabatizwe,. na ubatizo sahihi ni ule wa kuzamwishwa katika maji mengi (Yohana 3:23), na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38,.Ubatizo sahihi ni muhimu, fanya hivyo na hapo utakuwa umezaliwa mara ya pili.
Kumbuka anasema wote niwapendao nawakemea au kwa lugha wote niwapendao niwaeleza ukweli..Hivyo umeusikia leo ukweli. Kubali na kugeuka.
Marko 3:5 “Akawakazia macho pande zote kwa hasira, akiona huzuni kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao”
Ubarikiwe. Tafadhali “Share” Ujumbe huu na kwa wengine. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Habari ya UZIMA? Naomba unisaidie tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu Kwa Sisi Tumwaminio/wafuasi wake. Je! Damu ya Yesu inakazi ya Kutulinda sisi au Mali zetu pale tunapoomba kupitia Damu? Ni sahihi kuomba hivyo? Je! Damu ya Yesu inatumikaje Kwa sisi wakristo?
JIBU: Ili kuelewa tofuati ya utendaji kazi wa damu ya YESU na Jina Jina la Yesu, Ni vizuri kwanza tukajifunza katika maisha ya kawaida…Katika maisha ya kawaida mtu anayo DAMU na vilevile analo JINA…Jina la mtu linaelezea utambulisho wa mtu yule, cheo alicho nacho, heshima aliyo nayo, nguvu aliyo nayo na mamlaka aliyonayo.. Kwamfano katika nchi yoyote mtu mwenye jina kubwa na lenye nguvu kuliko wote ni Raisi wa nchi hiyo…
Vilevile katika upande wa pili DAMU ya mtu inaelezea Uzima wa huyo mtu, asili ya mtu huyo, Undugu alionao na wanafamilia wenzake, na inaelezea pia Urithi alionao..yaani watu atakaowarithisha mali zake.
Sasa tukirudi katika mamlaka ya kimbinguni ambayo hiyo ni kuu kuliko ya kiduniani…Tunaye Mfalme mmoja, naye ni Yesu Kristo (Huyo ni Zaidi ya Raisi yeyote wa nchi)…Na huyu analo JINA vilevile na anayo DAMU.
Kama tulivyosema damu inaelezea undugu wa mtu, yaani uana-familia.….na Bwana Yesu pia anao ndugu zake wa damu,..ambao ni wale wote waliozaliwa mara ya pili…Hao wanayo mamlaka ya kumsogelea katika meza yake na kula naye, na kumwomba lolote kwa jina lake na kupewa…Mtoto wa mfalme akiomba apewe jimbo fulani kutoka kwa Baba yake…haitachukua mlolongo mrefu kupewa haja ya moyo wake..mara moja tu baba yake atamwandikia hati ya nakala kwa jina lake na kuipeleka mahali husika kupata anachokihitaji…Na huyo mtoto kwa jina la Baba yake anaweza kupata lolota katika nchi…..Lakini hebu mtu wa kawaida tu amsogelee mfalme wa nchi na kumwomba apewe hicho kipande cha ardhi uone mlolongo wake!…anaweza kufukuzwa au hata asipofukuzwa basi ombi lake linaweza kuchukua muda mrefu sana kujibiwa…
Ni kutokana na kwamba mtoto wa Mfalme anatumia DAMU kupata lolote kwa JINA la Baba yake…wakati wengine wanatumia bahati tu!..kwamba ombi lao likikubaliwa ni kama wamepata bahati tu!..wangeweza kukataliwa…lakini mtoto wa Mfalme anauhakika kwasababu anatumia damu.
Kwahiyo tukirudi kwenye swali: Tofauti kati ya damu ya Yesu na jina la Yesu ni ipi? Tumeshaiona hapo juu na …na je ni sahihi kuomba kutumia damu ya Yesu kutulinda sisi na mali zetu? (damu ya Yesu inatumikaje)
Jibu: Mtu aliyeokoka tayari damu ya Yesu inanena mema juu yake..kama kwa hiyo mifano tuliyoiona hapo juu…Haihitaji kumweleza sana Baba wa mbinguni kwamba unahitaji ulinzi..kitendo tu cha kuwa mwanawe wa damu tayari ni jukumu lake kukulinda wewe na mali zako..na kwa jina lake kupewa chochote katika huu ulimwengu..Tofauti na mtu ambaye hajaokoka…huyo si mwana wa Mungu,..huyo hana uhusiano wowote na damu ya Mungu…Kwahiyo hata akiomba lolote kwa jina la Yesu kwake ni bahati nasibu kupata anachokiomba…
Umefanyika kuwa mwana wa Mungu?..umekuwa damu moja na Mungu?..Kama hujaokoka basi fahamu kuwa ni ngumu wewe kupokea upendeleo wowote kutoka kwa Mungu..Kwasababu Mungu anawaangalia kwanza wanawe kuwapatia mema (Soma Warumi 8:28-29)..na hao ndio atakaowarithisha uzima wa milele…hawezi kuwarithisha watu wasio wanawe…hata wewe mwenyewe ni ngumu kumrithisha mtoto asiye wako mali zako na kuwaacha wanao bila urithi…
Sasa kwanini uwe kama Yatima siku ile?..wakati wenzako wanairithi mbingu…wewe unarithi ziwa la moto kutoka kwa baba yako ibilisi?..mwache shetani aende kuzimu mwenyewe wewe mgeukie Kristo, mwenye urithi udumuo.
Hivyo unachopaswa kufanya ni kutubu kama hujatubu, kama ulikuwa ni mwasherati unatubu kwa kuacha kufanya hivyo, kama ulikuwa unaweka make-up unaacha, kwasababu mabinti wa Mungu waliozaliwa kwa damu ya Mungu hawafanyi hivyo, ..kama ulikuwa unasuguliwa kucha na wanaume saloon, utubu na kuacha,.., kama ulikuwa unavaa vimini, unapamba uso, unavaa surali, unatubu na kuacha kama ulikuwa ni mlevi, mvutaji wa sigara na mfanyaji masturbation na mtazamaji wa picha chafu katika mitandao unatubu na kuacha, kama ulikuwa ni mwizi vivyo hivyo…
Na baada ya kutubu kwa kudhamiria kabisa na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu. …utakuwa umezaliwa mara ya pili na kuhesabika mwana-familia wa familia ya kimbinguni. Na hivyo kuwa mrithi, na ile damu ya thamani isiyoisha muda wa matumizi, damu ya Yesu Kristo itaanza kunena mema juu yako.
Bwana akubariki.
Tafadhali share na wengine. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Je! ni dhambi kuimba wimbo wa Taifa hata kama umetungwa kidunia?.Na je ni dhambi kwa watoto wa kikristo kuimba zile nyimbo za chekechea?
JIBU: Nyimbo karibia zote za kitaifa hazijatungwa kidunia… Nyingi zilitungwa wakati au baada kidogo ya uhuru wa Taifa husika..Zilikuwa ni nyimbo za Kumshukuru Mungu na kulitakia amani, baraka na mafanikio Taifa husika. Hivyo nyimbo nyingi zilitungwa kama sala iliyo katika mfumo wa kama wa wimbo hivi.
Hakuna wimbo wowote wa Taifa lolote duniani..unaiombwa kwa lengo la kunyanyua hisia za uasherati, wala kutukana kama nyimbo zinazotungwa siku hizi, wala kwa lengo la kujiburudisha, wala kutafuta fedha, wala kujulikana…Hata wengi wa watunzi wa nyimbo hizo hazikuwa mali zao wenyewe kwamba wana hati miliki nazo..bali zilikuwa ni mali za Taifa.
Lengo lingine pia la nyimbo hizo, zimetungwa kuinua morali ya kufanya kazi, kuishi kwa umoja, upendo na kuliheshimu Taifa.
Hivyo hakuna ubaya wowote wa kuimba wimbo wa Taifa mahali popote.
Na sio tu nyimbo za Taifa, bali hata nyimbo za Chekechea (Nursery) kwa watoto wa kikristo.
Mtoto wa kikristo si dhambi kushiriki nyimbo za shuleni na watoto wengine..Maadamu nyimbo hizo zimejulikana ni za kimaadili na za kujifunza na zipo katika mtaala wa shule!..Lakini nyingine zozote zilizosalia za kidua ambazo si za kielimu wala si za kiheshima, wala hazipo katika mtaala wowoe wa kishule watoto wa kikristo hawaruhusiwi kushiriki wa vyovyote vile.
Ubarikiwe. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
NYIMBO ZA WOKOVU
Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?
TENZI ZA ROHONI
Wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya.
Ipo ahadi kubwa sana ambayo Mungu kaitoa kwa wale walioamua kuiacha dunia na kumfuata yeye kwa gharama zote. Na ahadi yenyewe ni “kupokea nguvu mpya kipindi baada ya kipindi”. Mungu anafahamu kabisa safari ya wokovu ni ngumu kama ilivyosafari nyingine yeyote ya haya maisha…kuna milima na mabonde, kuna kuchukiwa na kudharauliwa, kuna kuonekana umerukwa na akili na kutokuthaminiwa, kuna kutengwa na kuudhiwa, kuna kupungukiwa na kuvunjwa moyo, kuna msiba na dhiki n.k. vyote hivyo mtu yeyote aliyeamua kumfuata Kristo, kwa namna moja au nyingine atakumbana navyo…
Lakini utajiuliza pamoja na hali kama hizo ni kwanini bado watu waliookoka wengi ki-kweli kweli wanaweza kustahimili?..Ni rahisi mtu kwa kidunia kuvunjika moyo au kukatishwa tamaa na mambo kama hayo lakini kwa mkristo aliyedhamiria kumfuata Yesu, ndio kwanza anazidi kuwa karibu na Mungu wake..Hiyo yote ni kwasababu ipo nguvu inayoachiliwa ndani yake kipindi baada ya kipindi..
Isaya 40:28 “Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, Bwana, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki.
29 Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.
30 Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka;
31 bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia”.
Kama sio neema hiyo, hakuna hata mmoja wetu angeweza kumwamini na kumtuamini Mungu asiyemwona sikuzote za maisha yake..Lakini kwasababu ipo nguvu anayoiachia ndani ya wale wanaomngojea wanajikuta tu wanazidi kumtafuta Mungu, safari yao ya wokovu wanaiona kama vile imeanza jana..
Hiyo ndio tofauti na mtu aliyeokoka na yule ambaye hajaokoka..Yule ambaye hajaokoka, anaweza akawa anajisumbua katika jambo Fulani, au katika shughuli yake,.. au katika elimu yake, lakini upo wakati atachoka, ataboreka, atazimia na kusema ngoja nipumzike kwanza, nitakuja kuendelea baadaye, lakini kwa mtu aliyejitwika msalaba wake na kumfuata Kristo, pale ambapo ataonekana anakaribia kuzimia hapo ndipo Mungu anapompa nguvu mpya, anapompa uwezo mpya.
Pale ambapo watu watasema sasa huyu ndio basi, kwa hali hii, anayoipitia hamalizi huu mwaka atakuwa amesharudi tu huku kwenye dunia, lakini wanashangaa mwaka unapita, miaka inapita,.. ndio kwanza anazidi kumpenda na kumtafuta Mungu wake Zaidi ya hapo mwanzo..Kwasababu gani, Ni kwasababu Mungu anahakikisha anawapa nguvu mpya wale wao waliodhamiria kujitwika msalaba wao na kumfuata..kama maandiko yanavyosema:
watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.
Ukristo ni safari ya kuwezeshwa, ukiona mtu anasema nimeishiwa pumzi njiani siwezi kuendelea mbele nimezidiwa na tamaa za ulimwengu, fahamu kuwa mtu huyo tangu mwanzo alikuwa bado hajadhamiria kumfuata Kristo kwa moyo wake wote.. Kwasababu ni kitu ambacho hakiwezekani kuishiwa pumzi katikati angali kila wakati unawezeshwa, unapokea nguvu mpya, sasa huko kuishiwa pumzi kunatoka wapi?.
Leo hii unaweza ukajiuliza hivi kweli nikiokoka, nitaweza kuishi bila uzinzi kwa muda mrefu?, nitaweza kuacha kunywa pombe kwa kipindi kirefu,.. nitaweza kuvumilia kutovuta sigara kwa miaka 2 kweli, nikiamua kumfuata Kristo nitaweza kujizuia kutokuweka make-up maisha yangu yote, na kutokuvaa suruali,.. nitaweza kutokwenda Disko, nitaweza kutokufanya Musturbation…Nataka nikuambie kwa akili zako na nguvu zako chache hutaweza, lakini ukiamua kwa kudhamiria kweli kumfuata Kristo kwa moyo wako wote, ukasema leo hii naanza upya kupiga mwendo na Kristo, hilo jambo ni rahisi sana kulishinda kuliko unavyodhani..
Kabla hata hujakaribia kuishiwa pumzi Bwana atakuwa pembeni yako kukutia nguvu mpya..Kila siku itakuwa fresh kwako, wiki itapita, mwezi utapita, mwaka utapita, miaka itapita na bado ile hamu ya kufanya hayo mambo haipo ndani yako, ..Hiyo ni neema kubwa Mungu aliyowahaidia wale wote watakaomngojea…Hapo ndipo tunapouna wepesi wa wokovu, vinginevyo hakuna ambaye angeweza kuushinda huu ulimwengu, si mchungaji, si mwinjilisti..hakuna atakayeweza kuushinda ulimwengu.
Hata kama utapitia hali ambayo unaona kesho au kesho kutwa haifiki, lakini maadamu upo kwa Bwana, na unamtazama yeye, utaona tu jinsi atakavyokufanyia njia mahali ambapo hapana njia na wewe mwenyewe utajikuta unamwimbia, EBENEZA MWAMBA WANGU!..
Hata katika magonjwa, au dhiki, katikati yake atakufungulia mifereji ya faraja na uponyaji, nawe utasema ni heri Mungu nilichagua kukufuata maana ninauona mkono wako ukinizunguka!..Hali hiyo hiyo utaendelea nayo mpaka utakapomaliza mwendo wako hapa duniani kama unyakuo hautakukuta..hata Katika raha atakuwa na wewe pia kukuongezea raha Zaidi..
Lakini ikiwa upo mbali naye, na unasema kuishi maisha ya wokovu haiwezekani hapa duniani..Nataka nikuambie utajikuta unaendelea kusema hivyo mpaka unakufa na dhambi zako,..
Bwana Yesu aliwaambia mafarisayo katika Yohana 8:24 ‘Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu’.
Kuna madhara makubwa sana kufa katika dhambi…Ukifika kule mbele ya kiti cha hukumu wataletwa watu wa kizazi chako walioweza kukishinda hicho kinachokushinda wewe leo hii,..Nao wataulizwa ilikuaje kuaje nyie mliweza kuushinda uzinzi katika dunia iliyojaa vishawishi namna ile? na wakati hawa wengine wameshindwa?..Nao watajibu kwa ku-unukuu mstari huo;
‘29 Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.
30 Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka;
31 bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia”.
Hapo utakosa cha kujibu, ukijua kuwa kumbe na wewe ulikuwa na fursa kama hiyo lakini uliikataa.
Hivyo usisibiri upendeleo wa kipekee kama huo ukupite, acha kufikiria fikiria kwa juhudi zako utawezaje. Leo hii dhamiria kutubu dhambi zako zote, hapo ulipo tenga muda mchache ukiwa peke yako piga magoti, anza kumweleza Mungu mambo yako maovu yote uliyomtendea,… kisha mwambie Naomba msamaha,..Fanya hivyo kwa kumaanisha kabisa kutoka moyoni mwako kwasababu yupo hapo kukusikia, na yupo hapo kukusamehe dhambi zako zote..
Na Ile damu yake Yesu Kristo itakusafisha kabisa, na uthibitisho wake ni kuwa, baada ya Toba Amani ya ajabu na utulivu wa kipekee utaingia ndani yako, ukishaona hivyo, dhamiria sasa kuacha kufanya yale yote uliyokuwa unafanya nyuma yasiyompendeza Mungu, kwasababu Mungu kashakukaribia….kama ulikuwa ni mlevi kaa mbali na walevi na pombe, ulikuwa ni mzinzi kaa mbali na wazinzi na acha uzinzi, Na Mungu akishaona mwitikio wako, na kwamba umegeuka kivitendo sawasawa na toba yako, Sasa ile nguvu yake ya kukufanya uzidi kupiga mbio upae juu Zaidi kwa mbawa za tai, itaanza kuachiliwa ndani yako..Na kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda ndivyo utakavyojiona tamaa ya vile vitu ulivyokuwa unavifanya vinakufa ndani yako, na mwisho wa siku vitapotea kabisa..
Hivyo ukishatubu bila kupoteza muda hakikisha unatafuta kanisa, ukabatizwe, katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi (Yohana 3:23) na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38 ili kuukamilisha wokovu wako.
Kumbuka ubatizo sahihi ni muhimu sana..Vilevile anza kujumuika na wakristo wenzako, wale unaoona wamesimama kweli kweli na anza kusoma Neno kwa bidii na kusali..Yaliyosalia Roho Mtakatifu atakuongoza kuyatenda..jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Shalom.
Mada Nyinginezo:
MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU.
MNGOJEE BWANA
INGIENI KWA KUPITIA MLANGO ULIO MWEMBAMBA.
HERI NINYI MLIAO SASA, KWA SABABU MTACHEKA.
Je! Vichwa saba vya mnyama wa kwenye Ufunuo 13 na 17, Ni nini?
JIBU: Tukisoma kitabu cha Ufunuo ni kweli tunamwona mnyama aliyetajwa mwenye vichwa saba na pembe kumi..Tofauti na idhaniwavyo na wengi kwamba zile pembe kumi zimejigawanya kwenye vichwa vyote 7..na kwamba kuna vichwa vingine labda vitakuwa vimepata pembe mbili mbili au zaidi…Lakini ukweli ni kwamba ni kichwa kimoja tu ndicho kilichokuwa na pembe zote 10..Hivyo vingine havikuwa na pembe yoyote.
Na kama ukitafakari kwa makini kwa msaada wa Roho utagundua kuwa vile vichwa saba ni Wanyama saba katika mwili mmoja na sio tu vichwa kama vichwa vilivyojiotea kwenye mwili mmoja…bali ni Wanyama saba tofauti wanaoshiriki mwili mmoja (yaani wana-share mwili mmoja)..
Ufunuo 17: 11 “Na yule mnyama aliyekuwako naye hayuko, yeye ndiye wa nane, naye ni mmoja wa wale saba, naye aenenda kwenye uharibifu”.
Hiyo inawezekana asilimia 100..wapo ng’ombe mapacha wanaozaliwa wakiwa na mwili mmoja lakini vichwa viwili tofauti, kadhalika wapo nyoka wanaozaliwa hata watatu au wanne wakiwa na wanashea mwili mmoja…Na Zaidi ya yote wapo pia wanadamu ambao wanaozaliwa wakiwa wameungana…Kuna mapacha wanaoishi leo duniani ambao wameungana kila kitu isipokuwa kichwa tu…yaani ukikutana nao unaweza kusema umekutana na mtu mmoja mwenye vichwa viwili lakini kumbe ni watu wawili waliozaliwa wameungana wanaoshea mwili mmoja..Na watu hao walioungana kila mmoja anatafakari kivyake na ana malengo yake na mipango yake, na matamanio yake.
Na katika tukio hilo la Ufunuo ni vivyo hivyo..Biblia imemtaja mnyama huyo kuwa mwenye vichwa saba..Lakini kiuhalisia ni Wanyama saba tofauti wenye mwili mmoja…Na kila mnyama (yaani kichwa kina mambo yake)…Na pia ni mnyama mmoja tu kati ya hao wote mwenye pembe kumi (yaani ni kichwa kimoja tu chenye pembe hizo kumi).
Biblia inasema ni wafalme saba..
Ufunuo 17:9 “Hapo ndipo penye akili zenye hekima. Vile vichwa saba ni milima saba anayokalia mwanamke huyo
10 Navyo ni wafalme saba. Watano wamekwisha kuanguka, na mmoja yupo, na mwingine hajaja bado. Naye atakapokuja imempasa kukaa muda mchache. ”.
Falme hizo kama zinavyojidhihirisha katika taifa la Mungu kwenye biblia ni MISRI, ASHURU, BABELI, UMEDI & UAJEMI, UYUNANI, RUMI YA KIPAGANI na RUMI YA KIDINI..Hizi ndizo falme hizo saba au Wanyama hao 7..Falme hizi ni Mataifa aliyotumia shetani kuutesa uzao wa Mungu kwa ujumla wake…
Mataifa Matano ya kwanza yaliwatesa wana wa Israeli peke yao, wakiwa Misri, na mengine baada ya kuchukuliwa tena mateka babeli..lakini haya mawili ya mwisho yaliwatesa wana wa Israeli pamoja na Kanisa la Kristo…Na hicho kichwa ndicho cha mwisho na ndiye mnyama wa 7 ambaye ni RUMI YA KIDINI,.. nacho ndicho chenye pembe zote saba.. mnyama huyu ndiye ambaye yupo sasa na anazidi kuongezeka nguvu siku baada ya siku,.atakapofikia kilele chake atazitumia pembe zake 10 ambayo ni mataifa yanayounda umoja wa ulaya (EU) kuhimiza ile chapa ya mnyama. Kwasasaba umoja huo una wanachama Zaidi ya 10..
Lakini unabii unaonyesha yatakuja kubakia 10 tu yenye nguvu kwenye umoja huo. Na Kwa pamoja yatashirikiana na mnyama huyo, (Rumi ya kidini Iliyopo chini ya kiongozi wa kanisa katoliki ,Papa) kuishawishi dunia kuendesha zoezi la kuwatia watu chapa. Kwa kipindi kifupi sana kisichozidi miaka mitatu na nusu, Chapa itakuwa imeshawafikia watu wote duniani…Watakaoikataa watakamatwa na kupelekwa kwenye kambi maalumu za mateso…
Wakati huo unyakuo utakuwa umeshapita…Watakatifu wameondolewa duniani,.kuepushwa na ghadhabu ya Mungu na majaribu ya mpinga-kristo.
Na huko katika magereza hayo ya mateso, watu watakitafuta kifo hawatakiona kama unabii unavyosema.. “kwasababu mtu anayekutesa siku zote hataki ufe haraka..lengo lake uteseke kwa muda mrefu”..Ndicho kitakachotokea siku hiyo..watu watateswa lakini hawatauawa kwa haraka (Yatakuwa ni mara 100 zaidi ya yale ya Hitler, ambayo alikuwa anawapiga watu kwa nyundo yenye uzani mdogo kichwani mara nyingi aangalie ni kwa kiwango gani watu wanasikia maumivu, na kiwango cha watu kustahimili vifo wanapouliwa taratibu..mtu huyo anapigwa nyundo hata saa 4 mpaka anazirai, na mwisho wa siku kufa..
Au wanamfanyia mtu operation bila ganzi huku anatazamwa uwezo wake wa kumudu maumivu, au wanawatia watu kwenye barafu kali wakiwa uchi kwa masaa kadhaa kila siku)…ndivyo atakavyofanya mpinga-kristo na ziadi wakati huo wa dhiki kuu, na mateso hayo yatadumu kwa muda mrefu sana kwenye kambi hizo..kwa miaka sio chini ya mitatu na nusu..baadaye ndipo watawaua..wakati wengine waliosalia huko nje wakiendelea kufurahia Maisha baada ya kuipokea chapa…Hivyo dhiki kuu haitawahusu watu wote, bali tu wale watakaoikataa chapa…
Baada ya wale waliokataa chapa kufa wote…Itakuwa ni zamu ya wale walioikubali chapa kupitia dhiki na wao…Dhiki hiyo ni ghadhabu ya Mungu mwenyewe atakayoimwaga juu ya wale wote walioipokea chapa…Ghafla tu wakati wanaona dunia ni tamu mambo yataanza kubadilika…Bahari itakuwa damu, mito na chemchemu zote zikuwa damu, majipu na magonjwa ya ajabu yataanza kuwatokea, roho za mapepo wabaya zitaachiwa juu ya wanadamu, kutokuelewana kutaanza kutokea,vita vya wenyewe kwa wenyewe vitazuka, mvua ya mawe makubwa kama talanta zitaanza kushuka juu ya wanadamu,.. jua litashushwa chini kuwaunguza wanadamu kwa kipindi kirefu..na mwisho jua na mwezi na nyota vitatiwa giza, tetemeko kubwa duniani litatokea, kila visiwa kitapotea na kuzama kwenye bahari ya damu, na milima itafumuka..
Wanadamu wote walioipokea chapa watakufa kifo kibaya kuliko hata cha wale walioikataa chapa..na baada ya kifo hicho wote wataelekea jehanamu ya moto..Na kabla hawajamalizika wote kufa, wale wa mwisho mwisho kufa wachache sana ambao ni washirika wa vita vya Harmagedono ndani ya giza hilo kuu watamwona Kristo akija katika mawingu wataomboleza sana , lakini biblia inasema wataangamizwa kwa upanga utokao katika kinywa chake..
Mathayo 24:29 “Lakini mara, baada ya dhiki ya siku zile, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka mbinguni, na nguvu za mbinguni zitatikisika;
30 ndipo itakapoonekana ishara yake Mwana wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa yote ya ulimwengu watakapoomboleza, nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi”
Je! Unatamani kuwepo kwenye dhiki kuu?.. mimi sitamani..Natumai hata na wewe pia hutamani, Lakini unafahamu kuwa huo wakati upo karibu sana yamkini mambo hayo yatatokea katika kizazi chetu? Je! umempa Kristo Maisha yako?..Una uhakika wa kwenda kwenye unyakuo?…au bado upo kwenye ulimwengu?..kama bado ni mwasherati endapo parapanda italia leo utabaki hapa kukutana na hayo yote tuliyoyasoma hapo juu..
Kama hujaokoka na unataka kuokoka, fanya hivyo sasahivi.. Hapo ulipo tubu..na mwambie Bwana unataka kufanyika kuwa kiumbe kipya..baada ya kutubu tafuta kanisa ushiriki na wengine wenye Imani moja na wewe.. Na baada ya hapo pia hakikisha unabatizwa katika ubatizo sahihi kama hujabatizwa…Ubatizo sahihi ni wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo..Na Roho Mtakatifu atakusaidia kufanya yaliyosalia katika Maisha yako, na kukuweka katika mstari wa wale watakaonyakuliwa na kuepushwa na hukumu ya Mungu ya milele.
Bwana akubariki. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
UFUNUO: Mlango wa 13
UFUNUO: Mlango wa 17
UFUNUO: Mlango wa 16.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza
Je mama mjamzito anaruhusiwa kufunga?..Na je watoto wadogo wanaruhusiwa kufunga na kusali? Na je inawezekana kufunga siku 40 bila kula?..
Kabla ya kufahamu kama mama mjamzito anaruhusiwa kufunga au la!..Hebu jiulize swali lifuatalo..{Je! Mtu katika hali ya kawaida anaruhusiwa kufunga siku 40 bila kula wala kunywa?..Au inawezekana mtu kufunga siku 40 bila kula wala kunywa na asife?}
Bwana Yesu alifunga siku 40 mchana na usiku bila kula wala kunya na hakufa…Na Mjaribu ibilisi alipomjia na kumwambia ageuze jiwe kuwa mkate..alimjibu na kumwambia imendikwa ..”mtu hataishi kwa mkate tu, bali kwa kila Neno litaokalo katika kinywa cha Mungu”
Mathayo 4:1 “Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ili ajaribiwe na Ibilisi.
2 Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa.
3 Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate.
4 Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu“
Kama imewezekana mtu kuishi siku 40 bila kula wala kunya na hajafa basi inawezekana mjamzito au mtu mwingine yeyote yule kufunga bila kupatikana na madhara yoyote isipokuwa tu afunge kwa Imani na si kwa kutimiza wajibu fulani, au kulazimishwa…
Nimewahi kukutana na kumthibitisha mtu binafsi ambaye amemaliza siku 40, bila kunywa wala kunywa na hawajafa…na wapo wengi tu wengine wanaokwenda mfungo hata wa wiki 2, 3 hadi 4..bila kula wala kunywa na wanaishi vizuri tu…Shetani anachowadanganya watu wengi siku hizi ni kwamba “jambo la kufunga siku 40 kama Bwana Yesu siku hizi halipo”…Huo ni uongo wa shetani..
Lakini afunge tu kwa Imani, na si kwa dini wala mazoea, wala kulazimishwa..kama atafunga kwa dini na mazoea au kwa kulazimishwa basi ni afadhali asifunge kwa maana atapata madhara…lakini akifunga kwa Imani, huku binafsi akijiweka katika imani, utakatifu na ukamilifu,.. anaweza kumaliza hata siku 40 na mtoto akazaliwa akiwa na afya yake kamili na baraka tele.
Na sio tu mama mjamzito anaruhusiwa kufunga bali hata watoto..Wengi hawawaruhusu watoto wao wafunge wakihofia kwamba watadhoofika..Huo pia ni uongo wa shetani..mtoto kama anasukumwa ndani yake kufunga, hapaswi kuzuiliwa kwasababu “Mtu hataishi kwa mkate tu bali kwa kila Neno litokalo katika kinywa cha Mungu”…Na Neno lenyewe ndio hilo kwamba ” mambo mengine hayawezekaniki isipokuwa kwa kufunga na kusali”. Hivyo watoto wadogo wanaruhusiwa kufunga kama watu wazima.
Maran atha!
Mada Nyinginezo:
Je! taratibu za kufunga ndoa [yaani harusi] ni agizo la Mungu au ni mapokeo tu ya kibinadamu?
Kwanza ni muhimu kufahamu kuwa kuna roho za malaika na roho za mashetani…Malaika walioasi ndio wanaojulikana kama mashetani leo…Na malaika hawa wanafanya kazi katika mamlaka ya giza…Yaani kazi yao ni kwenda kinyume na kila kazi ya Mungu…
Kadhalika malaika hao walioasi (yaani mashetani au kwa jina lingine Mapepo)..wapo wa aina nyingi na wenye tabia tofauti tofauti…Kama vile malaika walivyo wengi na wenye tabia tofauti tofauti…kadhalika na mapepo nao ni hivyo hivyo…Katika biblia tunasoma kuna malaika wa maji..(Ufu.16:5)..kadhalika kuna malaika wanaohusika na nchi, bahari, pia wapo malaika wa kuleta habari kama Gabrieli, ..wapo malaika wa sifa kama maserafi na makerubi, wapo wa vita kama Mikaeli na wengine wengi.
Na katika upande wa pili wa malaika walioasi ni hivyo hivyo wana vipawa tofauti tofauti..yapo mapepo yanayohusika tu na maji, mengine moto, mengine yanahusika kusababisha majanga kama ajali,.. mengine kuleta magonjwa, mengine kuharibu nchi n.k..Lakini yote lengo lao kuu ni kupambana dhidi ya ufalme wa Nuru..
Sasa Vibwengo ni aina ya mashetani/mapepo yanayoangukia katika moja wapo ya hilo kundi…Vibwengo vina kazi ya kuwasumbua wale watu ambao hawajaokoka au hawajasimama vizuri kiimani..Na kwasababu ni roho za mapepo zile zile ambazo zinatenda kazi katika ufalme wa giza..hivyo lengo lao ni kuleta mauti ndani ya Mtu.
Na mtu anaweza kuishi na jamii hiyo ya mapepo aidha kwa kujua au kwa kutokujua…wakati mwingine mapepo hayo (vibwengo) vinaweza kujidhihirisha dhahiri kwa mtu..na mtu kuvishuhudia kabisa kwa macho…
Mara nyingi vinajidhihirisha kwa umbo la mtu mfupi sana aliyejaa..au aina fulani ya wanyama ambao wanaonekana kama watu..mfano wa maumbo yanayoonekana mara nyingi na vibwengo ni maumbo ya mfano wa nyani..Anaonekana mtu kama nyani lakini si nyani n.k…Na mapepo hayo yasipopatiwa ufumbuzi mapema yanaweza kusababisha hata kifo cha kiroho na cha kimwili kwa mtu..au yanaweza kusababisha tatizo fulani lenye madhara makubwa…Hivyo si busara kuzipuuzia roho hizo chafu.
Jambo la kwanza ni dhambi ndani ya maisha ya mtu..Mtu yeyote ambaye anaishi katika maisha ya dhambi anafungua mlango mpana sana wa kusumbuliwa au kuingiliwa na roho zozote za mapepo..Mtu anayetenda dhambi ni kama mtu aliyewasha WIFI data kwenye simu yake ya mkononi.. kiasi kwamba simu yoyote iliyokaribu na yake inaweza kukamata mawimbi yatokayo katika hiyo simu yake…Kadhalika mapepo ni hivyo hivyo, mtu anayefanya dhambi ni kama amewasha WIFI katika ulimwengu wa roho,..kwamba hata mapepo yaliyokuwa yanatembea tembea huko na huko ni rahisi kupata habari za huyo mtu.. na kumwingia au kumletea madhara fulani.
Dhambi zifuatazo ndizo zinazoongoza kukaribisha uwepo wa vibwengo kwa mtu..na si tu vibwengo bali hata jamii nyingine zote za mapepo.
1) IBADA ZA SANAMU : Hii inahusisha aina zote za aubuduji sanamu, aidha za watu au za wanyama…unapoisujudia sanamu ya aina yoyote ile ni mlango mpana sana wa kuingiliwa na mapepo..au kuishi na vibwengo pamoja nawe…
2) UASHERATI : Dhambi hii inashika nafasi ya pili katika kukaribisha uwepo wa mapepo ndani ya mtu na hata kuvutia uwepo wa vibwengo..Asilimia kubwa ya watu wanaoona roho hizo za vibwengo lazima kwa namna moja au nyingine ni waasherati. wa kimwili.
3) USHIRIKINA/UCHAWI : Ushirikina ni hali ya kujihusisha husisha na masuala ya nguvu za giza,… kama kwenda kwa waganga au kwa watabiri wa nyota, au utambuzi…Mtu anayehudhuria kwa waganga huyo ni mshirikina hata kama sio mchawi kabisa…lakini kitendo tu cha kwenda kwa waganga kutafuta suluhisho fulani..huo tayari ni ushirikina..na ni mlango mpana sana unaoshika namba tatu kukusogeza karibu na uwepo wa roho za mapepo hususani vibwengo.
Ikiwemo uvaaji wa wigi, kujitoboa mwilini na kujiweka vito kama hereni, mabangili, mikufu…pia upakaji wa wanja, upuliziaji wa marashi makali yasiyojulikana hata yametengenezewa wapi,..uchoraji wa hina na uchoraji tattoo..Mambo hayo yanahusika sana katika kuvuta uwepo wa roho za vibwengo na jamii nyingine za mapepo…Ndio maana hata vibwengo vyenyewe vinakuwa kama vimepaka chokaa usoni, au vinatoa harufu ya marashi fulani yasiyojulikana..hiyo yote ni kuonesha vimekutana na mahali ambapo panastahili wao kuwepo..
5) UVAAJI MBAYA:
Mavazi yote yasiyopasa…kama suruali kwa wanawake, magauni kwa wanaume, mavazi ya nusu uchi kama vimini, vitop, nguo za kubana n.k…ni WIFI kwa mapepo….Hata roho hizo za vibwengo viwatokeapo watu zinakuwa kama zimevaa mavazi yasiyoeleweka, kiasi kwamba huwezi kukitambua kama ni jinsia ya kiume au ya kike…Sasa vinakuwa vinatafuta mahali panapowastahili…kwa watu wa jamii zao.
6) ULEVI, UVUTAJI SIGARA na ANASA: Disko ni makao ya mapepo, mtu anayeingia disko tayari anatoka na pepo pasipo hata yeye kujijua…Mapepo ndio makao yao huko, sehemu ambazo watu wapo akili nusu kutokana na ulevi…sehemu ambazo watu wanacheza cheza madansi na kucheka cheka na kuwa na mizaha…Ndio maana hata vibwengo vyenyewe viwatokeapo watu ni lazima viwe nusu-nusu kama vimelewa hivi…vinakuwa nusu vinaakili timamu nusu vitahira…vinachekacheka, mara vinacheza cheza, vinakuwa na mizaha mizaha…yote hiyo ni kwasababu ndiyo asili yao..Hivyo vinatafuta watu wenye asili kama yakwao vikae nao..na hao wapo bar, disko au kwenye vikundi vya kamari.
7) UTAZAMAJI WA PORNOGRAPHY: Pornograph ni picha za ngono..ambazo siku hizi zinatazamwa hata kupitia simu za mkononi…Ufahamu uliojaa zinaa ni lango kubwa la roho hizo…
Suluhisho pekee la kuepukana na roho hizo za vibwengo ni kuokoka!…Kuokoka maana yake ni kutubu kwa kudhamiria na kumaanisha kabisa kuacha dhambi…unaacha dhambi zote ulizokuwa unazifanya hizo zilizoorodheshwa hapo juu na nyingine zote ambazo hazijaorodheshwa…Unatubu na kumwambia Bwana Yesu unahitaji wokovu na unamuhitaji yeye..si tu kwaajili ya kuepukana na vibwengo, bali kwasababu unahitaji kufanyika kuwa kiumbe kipya na kuwa mkamilifu kama Mungu alivyo.
Ukisha tubu hatua inayofuata ni kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo kama ulikuwa hujabatizwa,.. na baada ya hapo Roho Mtakatifu aliyeingia ndani yako atafanya mengine yote yaliyosalia.
Ukishaokoka namna hiyo! na kudhamiria kuacha dhambi…basi wewe mlango wa mapepo hautakuwepo ndani yako…Haiwezekani funza kuwepo ndani yako au kwenye mazingira yanayokuzunguka kama umefanya usafi kweli kweli…Dawa ya kuondoa funza ndani kwako ni kuwa msafi sio kuwaambia funza ondokeni kwangu…kadhalika dawa ya kuondoa mapepo na vibwengo karibu na wewe ni kuwa msafi.. (yaani kujiweka katika hali ya utakatifu), ambayo hiyo inakuja kwa kutubu dhambi na kuziacha..(yaani kuokoka) na sio kwenda kutafuta maombezi huku na huko…
Ikiwa umeshawahi kusumbuliwa na roho hizo za vibwengo..basi hiyo ndio dawa pekee tuliyopewa katika biblia takatifu.
Bwana akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789 001 312 jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Kifo cha Reinhard Bonkey kinaacha ujumbe gani kwetu?
Mwinjilisti wa kimataifa Reinhard Bonkey, raia wa Ujerumani, aliyezaliwa tarehe 19 Aprili 1940.. Anaeleza jinsi alivyompa Kristo Maisha yake akiwa bado kijana mdogo mwenye umri wa miaka 9, baada ya kuhubiriwa na mama yake kuhusu habari za Yesu na dhambi zake.
Alidumu katika Imani mpaka kufika kwenda chuo cha biblia na Mara baada ya kumaliza chuo cha mafunzo ya biblia huko Wales na kusimikwa utumishi wa Uchungaji nchini kwake Ujerumani, ndipo alipoanza kuja Afrika, kwa ziara zake za umishionari na kuweka maskani yake rasmi katika nchi ndogo ya Lesotho.
Akiwa huko Lesotho Reinhard Bonkey anasema kabla hajaanza kazi ya Uinjilisti katika bara la Afrika akiwa na mke wake, usiku mmoja aliota ndoto ambapo aliona bara la Afrika likioshwa kwa damu ya Yesu kuanzia kusini kwenda kaskazini, na kutoka magharibi kwenda mashariki. kwa siku ya kwanza anasema aliipuuzia ndoto hiyo akidhani kuwa labda usiku uliopitia alikula ndizi, lakini ndoto hiyo ikajirudia kwa siku nne mfululizo ndipo alipotambua kuwa ni Mungu ndiye alikuwa anasema naye.
Akaenda kuwaeleza viongozi wake juu ya jambo hilo na nia yake lakini walimkataza na kumwambia afanye kazi kama za wamishionari wengine, lakini sio hiyo ya kuzunguka kuhubiri injili..Lakini Bonkey aliondoka na kwenda kukaa hotelini kwa kipindi kumwomba Mungu ampe ruhusu ya kupata kibali kwa viongozi wake, kama ikiwa ni yeye kweli aliyemuita lakini wakati akiwa anaomba alisikia sauti ya Mungu ikimwambia..“USIPOIFANYA HII KAZI, NITACHAGUA MTU MWINGINE WA KUIFANYA”
Aliposikia hivyo alishituka kwa hofu, ndipo akamfuata mke wake, na kumweleza kuwa siku hiyo hiyo ataandika barua ya kuacha, kazi yake ya utumishi aliyowekwa na viongozi wake..Na ndipo akaanza safari ya kuhubiri injili katika miji mbalimbali bila kugeuka nyuma.
Kwa kuwa hakuwa na mtu wa kumuuliza jinsi kuandaa mikutano na jinsi ya kufundisha kwenye mikutano ya hadhara, alitumia uzoefu wake ule ule akijua kuwa Roho Mtakatifu atakuwa naye katika kila hatua, japo alipotoka hakufundishwa juu udhihirisho wa nguvu za Mungu, hivyo kila mahali alipokuwa akiandaa mikutano watu walikuwa wakimtazama tu,
Anasema siku moja nguvu za Mungu zilishuka katika mkutanao ule, na yule mtafsiri wake alidondoka chini kwa kuzidiwa na nguvu hizo, na huku akiwa analia alisikia sauti ikimwambia “NENO LANGU LITOKALO KINYWANI MWAKO, LINA NGUVU ILE ILE SAWA NA LINAVYOTOKA KATIKA KINYWA CHANGU”..
Alivyosikia vile alishangaa, akapata msukumo mkubwa sana ndani yake, ndipo kwa ujasiri akasema “Vipofu wote walio katika huu mkutano wasimame, na leo hii kwa mara ya kwanza watakwenda kuuona uso wa Bonkey”..Alivyosema vile, ndani ya moyo wake alisikia sauti nyingine ikimwambia..Na ikiwa hatawataona utafanyaje…Lakini yeye alisema Ninalisema Neno la Mungu..Na alipotamka tu “KWA JINA LA YESU, MACHO YENU YAFUMBUKE!!” ..Alichosikia tu ni kelele za watu wakisema ninaona…wakirukaruka, na mara mda huo huo alimwona mtoto mdogo aliyekuwa amebebwa na mama yake, akipitishwa juu ya vichwa vya watu, na kurushwa mbele mpaka pale alipo na kujikuta mtoto yule yupo mikononi mwake..
Anasema mtoto huyo alikuwa na viungo vilivyokunjana mfano wa tambi…Lakini saa ile ile alipofika mikononi mwake, nguvu za Mungu zikaanza kumtetemesha mtoto yule, akamwachia akadondoka lakini hakutua vibaya bali alitua kwa miguu yake na kuanza kukimbia na kurukaruka. Na huo ndio ulikuwa mwanzo wa huduma yake iliyoambata na nguvu za Roho Mtakatifu.
Mwanzoni kabisa mwa huduma yake Alianza kwa kuitisha mikutano midogo midogo, japo anasema haikuwa na mwitikio mkubwa kwa siku za mwanzo, kwani mkutano ulio mkubwa sana uliweza kuhudhuriwa na watu mia nane tu (800). Lakini, baadaye alivyozidi kuhubiri idadi ya watu ilizidi kuongezeka kwa kasi, mpaka kufikia hatua kila mkutano anaouitisha haupungui watu laki moja na nusu (150,000). Na kwa jinsi ilivyozidi kuendelea alipoitisha tu mkutano mmoja katika mji mmoja, kuliweza kukusanyika watu Zaidi ya milioni moja na laki sita (1,600,000).
Zaidi ya watu milioni moja kwa siku walikuwa wanarekodiwa kumpa Kristo Maisha yao.
Na Tangu mwaka 1986, huduma ya Reinhard Bonkey inarekodi ya watu Zaidi ya milioni 77 waliokuja kwa Kristo. Hiyo ni Zaidi ya idadi ya watu waliopo katika la Tanzania.
Mnamo tarehe 7 Disemba 2019, safari ya mtumishi huyu mwaminifu wa Mungu ilifikia kikomo..Reinhard Bonkey, bila shaka watu kama hawa ndio wanaostahili waandikiwe kwenye makaburi yao maneno haya:
2Timotheo 4:7 “Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda”;
Ukweli ni kwamba Huduma ya mtumishi huyu ilifanikiwa kwa jambo moja linaloitwa utiifu. Alitii pale alipoitwa bila kujali mahali atakapokwenda, na kazi atakayoifanya.. Enzi hizo hakukuwa na miundo mbinu mizuri kama iliyopo sasa, lakini alijitoa kwa hali na mali kwa ajili ya injli ya Kristo..
Waebrania 12:1 Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,
2 tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.
Watu kama hawa, tutawezaje kwenda kupata thawabu moja na wao kama na sisi hatutapiga mbio kama za kwao?
Ikiwa bado upo nje ya Kristo, usisubiri kifo kikukute, tubu leo hii umpe Bwana Maisha yako, Akuokoe..Fanya hivyo kwa kumaanisha hapo ulipo kwa kupiga magoti na kumwambia Mungu, Nisamehe makosa yangu yote, na kuanzia leo ninakiri kukutumikia na kukufuata,. Nisafishe kwa damu ya mwanao mpendwa YESU KRISTO, nifanyike kuwa mwana wako kuanzia wakati huu.
Sasa ikiwa umefanya hivyo, kwa kumaanisha kutoka moyoni, unachopaswa kufanya ni kuithibitisha hiyo Imani yako kwa kuacha yale ambayo ulikuwa unayafanya nyuma, na kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kimaandiko wa kuzamishwa katika maji mengi, na kwa jina la YESU KRISTO, sawasawa na Matendo 2:38 ili uukamilishe wokovu wako.
Na Kristo akishaona mwitikio wako atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu, bure, ambaye huo ndio muhuri wa wokovu wako, atakayekaa nawe mpaka mwisho wa safari yako hapa duniani,..ikiwa unyakuo utakuwa haujapita. Fanya hivyo na Bwana akubariki sana.
Maran Atha!
Mbali na histori na Kifo cha Reinhard Bonkey, ungependa kupata habari za mashujaa wengine wa Imani?. Mtazame William Branham chini utajifunza mengi pia.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
HISTORIA YA WILLIAM BRANHAM
USHUHUDA WA RICKY:
MTETEZI WAKO NI NANI?
UNYAKUO.
NENO HILI NI GUMU, NI NANI AWEZAYE KULISIKIA?
Tuwe tayari pia kuyapokea maneno magumu kutoka kwa Kristo.
Si maneno yote aliyokuwa anayazungumza Bwana yalikuwa ni mepesi kuyapokea kwa namna ya kawaida,..
Kuna wakati aliwaambia wanafunzi wake,
Mathayo 10:37 “Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.
38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili.
39 Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona”
Jaribu kufikiria wakati huo, Kristo alikuwa bado hajasulibiwa, na wala hakukuwa na mtu yeyote aliyewahi kudhani kuwa siku moja atakwenda kutundikwa mtini uchi mfano wa wanyanganyi..Lakini tunaona hapa Kristo anawaambia wanafunzi wake juu ya kujitwika misalaba kana kwamba wanaelewa ni nini maana ya kujitwika msalaba na kumfuata yeye, au walishawahi kumwona yeye akijitwika msalaba wake…
Kwa namna ya kawaida, unaweza ukadhani ni rahisi kulipokea hilo neno,.. ni sawa na leo hii, umsikie raisi anasema mtu yeyote anayetaka nimfanye kuwa waziri ahakikishe kwanza anabeba bomu lake mkononi na kutembea nalo kila siku,.. na muda wowote awe tayari kujilipua…Unaweza kusema raisi anazungumza maneno gani haya..
Ndivyo ilivyokuwa kwa Kristo, misalaba ilikuwa ni kwa ajili ya watu waovu tena wale walioshindikana wenye kesi nzito za mauaji..sasa kusikia eti mtu mwema kama yeye anataja mambo ya misalaba ilikuwa ni kauli tata sana.
Yohana 6:53 “Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu.
54 Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.
55 Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
56 Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake”
Fikiria tena leo hii mtu anakuambia uule mwili wake, na uinywe damu yake, si utamwona kama ni mchawi?.. Vivyo hivyo na maneno mengine mengi, kama lile alilosema yeye ni chakula kitokacho mbinguni, na bomoeni hekalu hili nitalijenga ndani ya siku tatu. N.k.
Maneno kama hayo ndiyo yaliyowafanya wengi wa wanafunzi wake wasifuatane naye tena..
Yohana 6:60 “Basi watu wengi miongoni mwa wanafunzi wake waliposikia, walisema, Neno hili ni gumu, ni nani awezaye kulisikia?
61 Naye Yesu akafahamu nafsini mwake ya kuwa wanafunzi wake wanalinung’unikia neno hilo, akawaambia, Je! Neno hili linawakwaza?
62 Itakuwaje basi, mmwonapo Mwana wa Adamu akipaa huko alikokuwako kwanza?
63 Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; maneno hayo niliyowaambia ni roho, tena ni uzima”.
Hata leo hii Kristo anapowaita watu wamfuate sio kila jambo atalitolea sababu zake siku hiyo hiyo,…wewe unachopaswa kufanya ni kumtii tu na kumwamini maadamu ni mwanafunzi wake,… anapokuambia acha hiki, hata kama hukielewi vizuri leo wewe acha na umfuate, anapokuambia badilisha mavazi yako,tupa vimini, na mawigi, na malipstik na mahereni, usiwaze waze mara mbili anamaanisha nini,….wewe ni kipofu hivyo usijifanye unaona!.
Anapokuambia jitenge na marafiki wa aina hii usianze kuwaza dunia itanionaje, akikuambia acha hiyo kazi unayoifanya, usianze kuwaza Kesho nitakula nini,..Sababu zote hizo atakuja kukupa huko baadaye mbeleni kwa jinsi unavyozidi kutii…lakini kwasahivi mtii kwa kile atakachokuambia ufanye..
Mitume 12, walipoitwa waliambiwa neon moja tu! “NIFUATE”..wakaacha kila kitu hapo hapo na kumfuata, hawakupewa maelezo ya kutosha wanakwenda wapi…
walistahimili maneno magumu kama hayo, mpaka ukafikia wakati wa wao kuelewa sababu ya mambo yote, wengine walishindwa kuyapokea na ndio maana hawakufika Pentekoste, lakini mitume wale 11 wa Bwana na mwingine mmoja wa 12 aliyekuja kuongezeka walitii na ndio maana walifika Pentekoste. Na Mungu akawafanya kuwa nguzo za kanisa.
Sikuzote unapaswa ujue maneno ya Kristo Ni Roho tena ni uzima, hata kama huyaelewi kwasasa.. Ibrahimu aliambiwa akamtoe mwanawe kafara, lakini kwasababu alimwamini Mungu anayemtumikia, akahesabu kuwa Mungu anaweza kumfufua tena mwanae huko atakakokuwa hata kama atakuwa ameshaoza na kuwa udongo,..(Waebrania 11:18-19) hakujali kwamba kitendo anachokwenda kufanya ni kitendo cha kigaidi..lakini alitii, leo hii ndio tunaelewa Mungu alikuwa anafunua nini katika kumwambia afanye vile..Lakini badala ya kupoteza ilikuwa kinyume chake kupata..
Kubali kuipoteza nafsi yako leo kwa ajili ya Kristo, Ukifahamu kuwa siku moja utaipata. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Bwana akubariki.
Mada Nyinginezo:
INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA
KARAMA YA MUNGU NI UZIMA WA MILELE.
SIKU ILE NA SAA ILE.
MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU: