Hili ni moja ya maswali yanayoleta mkanganyiko miongoni mwa wakristo wengi? Baadhi wanaamini kile kitendo tu cha yeye kujutia makosa yake mpaka kupelekea kutoona faida ya kuishi hadi kwenda kujinyonga ni toba tosha, baadhi wanaamini tayari alikuwa ni mtume aliyechakuliwa na Yesu, hivyo hata iweje hawezi kwenda kuzimu, kwasababu Mungu hachagui vilivyo dhaifu. Lakini baadhi bado wanashikilia kuwa alikwenda kuzimu, kwasababu alikuwa mwizi na mwisho wa kifo chake ilikuwa ni kujinyonga. Na hiyo ni uthibitisho kuwa alipotea.
Lakini tuangalie maandiko yanatupa alama gani kuhusiana na hatma ya Yuda, ndipo tutakapoitimisha kwamba Yuda alikwenda wapi.
Bwana Yesu alisema maneno haya kwa Yuda;
Mathayo 26:24 Mwana wa Adamu aenda zake, kama alivyoandikiwa; lakini ole wake mtu yule ambaye amsaliti Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu yule kama asingalizaliwa.
Pa kutilia umakini ni hilo Neno alilohitimisha nalo, “Ingekuwa heri kwake mtu yule kama asingalizaliwa”.linatupa picha mbaya kwamba mtu huyo alikuwa hana faida yoyote duniani, maisha yake ni kama bure.
Lakini pia, kuna maneno mengine ambayo Bwana Yesu aliyasema katika sala yake; Alisema..
Yohana 17:12 Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.
Kuonyesha kuwa Yuda alipotea.
Lakini andiko lingine, tunalisoma katika kitabu cha matendo ya mitume, wakati mitume wanapiga kura kuchagua mtume atakayesimama mahali pa Yuda. Nao pia walisema maneno haya;
Matendo 1:24 Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili, 25 ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe. 26 Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja.
Utaona hapo anasema “aende zake mahali pake mwenyewe”. Ikimaanisha kuwa Yuda hakwenda mbinguni bali mahali pake, na huko si kwingine zaidi ya kuzimu.
Hivyo kwa vifungu hivyo vyote, hatuoni mahali popote maandiko yanatupa viashiria kuwa Yuda alikwenda mahali pazuri, ukizingatia kuwa katika hatua zake za mwisho hadi kujinyonga, biblia inatuambia aliingiwa na “shetani”. Maana yake ni kuwa shetani alifanya kiti cha enzi ndani yake, hivyo maamuzi yote aliyokuwa anayafanya yalisukumwa na yule mwovu, sio Mungu. Kwahiyo hakuna kitendo cha ki-Mungu alichokifanya Yuda tangu wakati ule.
Hili ni fundisho kubwa sana, hususani kwa watumishi wa Mungu. Bwana kukuita haimaanishi kuwa huwezi potea. Au huwezi ingiliwa na shetani. Petro aliteleza mara kadhaa, na alivamiwa na shetani kinywani mwake, lakini hakukubali kumpa adui nafasi, vivyo hivyo na wewe, hupaswi kusema mimi nina kanisa kubwa, mimi ninahubiri, mimi nimetokewa na Yesu. Kumbuka Yuda aliishi na Yesu kwa zaidi ya miaka mitatu, sio kutokewa nusu saa, lakini alianguka, kwasababu aliipa dhambi nafasi katika maisha yake.
Nasi pia tunapaswa tusimame, dhambi isichukue nafasi yoyote mioyoni mwetu. Kwasababu hiyo inaanza kama tamaa, kisha inachukua mimba, kisha inazaa mauti. Kaa mbali na dhambi.
Bwana atusaidie..
Je! Umeokoka? Je unahabari kuwa hizi ni siku za mwisho, na Yesu yupo mlangoni kurudi?. Umejiandaaje, unaishije, unatazamia nini baada ya haya maisha? Ni heri utubu dhambi zako sasa, umrejee Bwana, usamehewe dhambi zako, Kumbuka adui anakuwinda sana, usiishi maisha kama ya wanyama, wewe ni wa thamani, mbele za Mungu wako. ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi waweza fungua hapa kwa msaada wa mwongozo wa sala ya Toba >>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
Je ni kweli Yuda hakuwa na dhambi kwa kumsaliti Bwana, kwasababu tayari ilikuwa imeshatabiriwa?
JINSI BWANA ALIVYOWACHAGUA MITUME WAKE.
YUDA ISKARIOTE! MTUME ALIYECHAGULIWA NA BWANA YESU.
Kwanini Bwana Yesu alitokea katika ukoo wa Yuda?
Ni kwa namna gani Yesu ni Simba wa Yuda?
Kitabu hiki katika lugha ya kiebrania kinasomeka kama “Devarim” ambayo tafsiri yake ni “Maneno”
Na ndio maana mstari wa kwanza kabisa un itaanza Kwa kusema. “Haya ndiyo maneno”
Kumbukumbu la Torati 1:1
[1]Haya ndiyo maneno Musa aliyowaambia Israeli wote ng’ambo ya Yordani barani, katika Araba lililoelekea Sufu, kati ya Parani, na Tofeli, na Labani, na Hazerothi, na Dizahabu.
Lakini katika tafsiri ya kigiriki Cha kale (septuagint), kilisomeka kama “deuteronomioni” chenye maana ya “Mrudio wa sheria” ambapo Kwa sisi kinasomeka kama “kumbukumbu la sheria/torati”.
Ni kitabu Cha Tano ambacho kiliandikwa na Musa karibia na mwisho wa Ile miaka 40, wakati walipokuwa ng’ambo ya Yordani katika nchi ya Moabu.
Lengo la kuandikwa kitabu hicho ni kukumbushwa sheria na maagizo ya Mungu, kwasababu kundi kubwa la Wana wa Israeli lililopokea sheria Kule mlima Sinai mwanzoni, lilifia jangwani, hivyo kile kizazi kipya Hakikuwa na msingi imara juu ya sheria za Mungu. Na ndio hapa Musa anaagizwa na Mungu awakumbushe Wana wa Israeli sheria yake.
Kitabu hiki kimeanza kuwakumbushia safari Yao Toka Misri, pia kikagusia jukumu lao la kumpenda Mungu na kuzishika sheria zake. Ikafuatana na baraka na laana ambazo zitampata mtu katika kutii au kutokutii, na mwisho kifo cha Musa.
Je ni Nini tunajifunza kuwepo kwa kitabu hiki ?
Bwana anataka na sisi tuweke kumbukumbu la agano lake mioyoni mwetu, Kwa vizazi vijavyo tupende kuwafundisha vizazi vinavyochipukia Neno la Mungu, tusiwaache tukadhani wataelewa tu wenyewe kisa biblia ipo, bila kukumbushwa Kwa kufundishwa.
Musa alifanya vile ndio maana kizazi kile kikawa imara baada ya pale.
Na sisi tuwe watu wenye tabia hii, Sio kwa watoto tu hata Kwa kondoo wa Bwana kanisani. Mara Kwa mara tuwakumbushe maagizo ya Mungu.
Kwa maelezo ya ziada kuhusu kitabu hichi pitia hapa >>> https://wingulamashahidi.org/2019/05/13/vitabu-vya-biblia-sehemu-ya-2/
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
Vitabu vya Deuterokanoni ni vya ki-Mungu?
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1
Mtiririko wa vitabu vya biblia kwanini upo vile?
Je! Mwendo wa Sabato ulikuwaje kibiblia?(Matendo 1:12)
NJIA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.
Nini maana ya “Atamwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake”. (2Wathesalonike 2:8).
Chetezo ni kifaa/chombo kidogo kilichotumika katika tendo la kuvukiza uvumba ndani ya Hema ya Mungu au katika hekalu la Mungu. (Tazama picha juu).
Wakati kuhani alipotaka kufanya kazi za kikuhani ndani ya hema/hekalu la Mungu. Kabla ya mambo yote ilikuwa ni lazima avukize uvumba ndani ya hema/hekalu, lengo la kufanya vile ni kukijaza chumba chote moshi wa ule uvumba.
Hivyo alitwaa kozi mbili za makaa ya moto ambayo yalikuwa yanapatikana katika madhabahu ndogo (ijulikanayo kama madhabahu ya uvumba), iliyokuwa inapatikana upande wa kushoto wa patakatifu pa patakatifu.
Na akiisha kuyachukua yale makaa, ndipo anayatia ndani ya hiko chetezo pamoja na manukato yenye kutoa harufu nzuri yaliyotengenezwa kwa viungo maalumu alivyoviagiza Mungu mwenyewe…
Kutoka 30:34 “BWANA akamwambia Musa, Jitwalie manukato mazuri, yaani, NATAFI, NA SHEKELETHI, NA KELBENA; VIUNGO VYA MANUKATO VIZURI PAMOJA NA UBANI SAFI; vitu hivyo vyote na viwe vya kipimo kimoja;
35 nawe utafanya uvumba wa vitu hivyo, manukato ya kazi ya ustadi wa mtengenezaji manukato, yatakuwa yamekolea, safi, matakatifu”.
Na baada ya kuhani, kuvichoma viungo hivyo (manukato) pamoja na yale makaa ndipo moshi huo huo wenye harufu nzuri hupanda juu na kukijaza chumba chote, na hivyo Mungu hushuka kuipokea ibada hiyo. (Tendo hilo ndilo linaloitwa kuvukiza uvumba).
Ilikuwa ni kosa kubwa kufanya kazi ya kikuhani bila kuvukiza uvumba kwanza, vile vile ilikuwa ni kosa kubwa kuhani kutumia viungo vingine katika manukato au moto mwingine mgeni tofauti na ule wa madhabahuni katika zoezi la kuvukiza uvumba..(Soma Kutoka 30:9, Hesabu 3:4).
Kwa mapana zaidi kuhusu Kuvukiza uvumba fungua na ujumbe gani umebeba kiroho fungua hapa >>> KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?
Swali ni je katika agano jipya tuna amri/agizo la kufukiza uvumba katika nyumba za Ibada kama makuhani walivyofukiza katika nyumba ya Mungu katika agano la kale?
Jibu ni la!.. Katika agano jipya hatuna amri wala agizo hilo, kwasababu agano letu si tena la mwilini bali la rohoni, kama vile tusivyozitumia tena damu za wanyama katika ondoleo la dhambi bali damu ya YESU vile vile, hatuvukizi tena uvumba kwa namna yakimwili bali uvumba wetu sisi ni “maombi”.
Sasa CHETEZO kinawakilisha nini kiroho?.
“Chetezo” inawakilisha “moyo wa mtu” kama vile moto unavyowekwa ndani ya chetezo na uvumba kuvukizwa juu ndipo utukufu wa Bwana uonekane…Vivyo hivyo na sisi ni lazima Moto wa Roho Mtakatifu uwashwe ndani yetu na ndipo tuweze kumtumikia Mungu na kuomba sawasawa na mapenzi yake, kwa maana ule uvumba katika nyumba ya Mungu ni ufunuo wa maombi ya watakatifu katika agano jipya. (Ufunuo 8:3).
Je Moyo wako umeufanya safi?.. Biblia inasema tulinde mioyo yetu zaidi ya vyote tuwezavyo kuvilinda (Mithali 4:23).
Bwana atubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
USICHELEWE KUMPAKA BWANA MARHAMU!
MUNGU HATAZAMI MOTO WA KIGENI,KUWA MAKINI!
SWALI: Ni ipi gharama sahihi ambayo Daudi aliilipia, kununulia shamba la Arauna, kwa ajili ya kumjengea Mungu hekalu. Je! Ni shekeli 600, au shekeli 50?. Je! Biblia inajichanganya.
JIBU: Tusome,
2Samweli 24: 24 Lakini mfalme akamwambia Arauna, La, sivyo; lakini kweli nitavinunua kwako kwa thamani yake; wala sitamtolea Bwana, Mungu wangu, sadaka za kuteketezwa nisizozigharimia. Hivyo Daudi akakinunua hicho kiwanja cha kupuria na wale ng’ombe kwa shekeli hamsini za fedha. 25 Naye Daudi akamjengea Bwana madhabahu huko, akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Basi Bwana aliiridhia nchi, na tauni ikazuiliwa katika Israeli.
1Nyakati 21:25 “Basi Daudi akampimia Arauna thamani ya mahali pale shekeli mia sita za dhahabu kwa uzani 26 Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu huko, akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, akamlingana Bwana; naye akamwitikia kutoka mbinguni kwa moto juu ya madhabahu hiyo ya sadaka ya kuteketezwa”
Vifungu hivyo havijichanganyi, vyote vipo sahihi. Mwandishi wa kitabu cha Samweli anaeleza lile eneo ambalo lilikuwa ni la kupuria tu, pamoja na wale ng’ombe gharama zake jumla ndio shekeli hamsini, lakini sio eneo lote la kiwanja. Tukirudi kwenye 1Nyakati mwandishi anaeleza sasa eneo lote, anatumia neno “mahali pale”. Kwamba jumla yake yote ni shekeli mia sita. Gharama zote za mahali pale zilikuwa ni shekeli 600
Kwamfano wewe unaweza ukawa umelenga kupanunua mahali Fulani kwa ajili ya shughuli zako za kimaendeleo. Lakini ikakugharimu ununue sehemu yote ili uweze kupamiliki vizuri na pale. Hivyo kama eneo lile tu moja gharama yake ilikuwa milioni 1, Lakini kwasababu ya kulipia fidia kwa watu kando kando kuwahamisha, na kodi, na ukarabati n.k. unajikuta unaenda mpaka milioni 20.
Ndicho kilichomkuta Daudi.
Kwahitimisho ni kuwa vifungu hivyo vipo sahihi havijichanganyi.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
Swali: Je idadi ya askari waliohesabiwa katika 1Nyakati 21:5 na 2Samweli 24:9 inajichanganya?.
Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.
KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?
NI KWANINI WATU WENGI WANASHINDWA KUMWELEWA MUNGU?
Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.
Je! Wamwona mtu mwenye bidii katika kazi zake?
Jibu: Neno “Novena” limetokana na neno la kilatini “Novem”… lenye maana ya “Tisa”(9). Madhehebu baadhi ikiwemo Katoliki na Orthodox yamelitoa neno hili na kulitumia katika aina Fulani ya mfululizo wa sala kwa kipindi cha siku 9.
Sala hizo zinahusisha kuomba kwaajili ya jambo fulani au kushukuru, na zinahusisha ibada za kuomba Rozari kwa wakatoliki (jambo ambalo si sahihi kibiblia). Na kwanini kusali Rozari sio agizo la biblia?, fungua hapa kwa maelezo Zaidi >>>JE SALA YA ROZARI TAKATIFU NI YA KIMAANDIKO?
Sasa msukumo wa kuomba Novena, (yaani siku 9) mfululizo umetokana na matukio maalumu yanayotokea baada ya siku 9, au miezi 9 kumalizika. Kwamfano utaona kabla ya Pentekoste kutimia, walikusanyika Mitume na watu wengine baadhi mahali pamoja kuomba, na wakaomba kwa muda wa siku 9, baada ya Bwana Yesu kupaa na siku ya 10 ikawa ni Pentekoste.
Hivyo ushawishi huu wa kupokea Roho Mtakatifu baada ya maombi ya siku 9, ukaaminika na madhehebu hayo kubwa ni lazima uendelee ili kupokea kitu kingine mfano wa hicho kutoka kwa Mungu, vile vile mwanamke anajifungua mtoto baada ya miezi 9, hili nalo likawafanya viongozi wa madhehebu haya kuamini kuna kitu katika 9, (novena).
Sasa swali ni je! Biblia imetuagiza kutumia mfumo wa Novena, katika maombi ili kupokea jambo maalumu kutoka kwa Mungu? Kwamba tuwe na maombi maalumu ya kurudia rudia kwa muda wa siku 9 ili tupokee jambo kutoka kwa Mungu?.
Jibu ni la!.
Biblia haijaagiza mahali popote tusali “Novena” kwamba tuwe na kipindi Fulani maalumu cha siku 9 mara kwa mara ili Mungu aachilie kitu juu yetu. Utaratibu huu umetengenezwa na wanadamu, kufuatia ushawishi wa siku ya Pentekoste. Hivyo kama umetengenezwa na wanadamu, hauwezi kuwa Sharti, au Agizo la lazima kwa wakristo, kwamba usipofanya hivyo ni kosa kibiblia!.
Agizo hili linaweza kuwa la binafsi, kama tu vile mfungo usivyokuwa sharti, ni jinsi mtu atakavyosukumwa na kuongozwa kufunga!.
Lakini mbali na hilo hata kama Novena ingekuwa ni agizo la biblia, bado inavyofanyika na madhehebu baadhi ikiwemo Katoliki, bado haifanyiki sawasawa na maandiko.. Kwasababu katika biblia tunaona kabla ya Pentekoste walikuwa wamekusanyika mahali pamoja wakisali, wakimwomba Mungu na Mariamu mama yake Yesu alikuwemo miongoni mwao, naye pia akimwomba Mungu, na hawakuwa na sanamu ya mtakatifu Fulani aliyetangulia kufa!, bali walikuwa wakimwomba Mungu aliye juu, (Matendo 1:12-14)
Lakini leo hii katika sala hizo za Novena ni kinyume chake!, wanaoombwa ni watakatifu waliokufa ikiwemo Maria mwenyewe, jambo ambalo ni kinyume kabisa na maandiko!, hivyo badala ziwe sala za Baraka, zinageuka na kuwa ibada za sanamu! (Bwana Yesu atusaidie sana!!).
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Novena haipo kibiblia,..kama mtu atajiwekea utaratibu wake binafsi wa kusali Novena, na sala hiyo ikawa ni kulingana na Neno la Mungu, isiyohusisha sanamu wala desturi za kipagani basi hafanyi dhambi!, huenda ikawa bora kwake.
Lakini inapogeuka na kuwa sharti, na tena ikahusisha ibada za sanamu basi inakuwa ni machukizo makubwa mbele za Bwana kulingana na maandiko.
Bwana atusaidie!.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)
Ni lazima mtu aongozwe sala ya toba ili awe ameokoka?
SALA YA UPONYAJI/MAOMBI YA UPONYAJI.
Kuna tofauti gani kati ya SALA na DUA?
Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi;
Waefeso 6:18 kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote
Yuda 1:20 Bali ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu sana, na kuomba katika Roho Mtakatifu
Watu wengi wanaamini kuomba katika Roho ni kuomba kwa “kunena kwa lugha tu”. Nje ya hapo sio kuomba kwa Roho. Lakini tukiwa na mtazamo huo basi tutakuwa na uelewa finyu kuhusu Roho Mtakatifu.
Ukweli ni kwamba hiyo ni namna mojawapo kati ya nyingi ambazo Roho wa Mungu anamjalia mtu kuomba.
Maana ya ‘kuomba katika Roho’ Ni kuomba ‘ndani ya Roho ya Mtakatifu/ ndani ya utaratibu/ uwepo wa Roho Mtakatifu’. Na hiyo ni zaidi ya kunena kwa lugha, Hii ikiwa na maana Mtu anaweza kuomba lakini asiwe katika uwepo huo. Na matokeo ya hivyo ni maombi kuwa makavu sana, yasiyo na nguvu.
Sasa mstari mama unaotufundisha juu ya uombaji wa Roho Mtakatifu ni huu;
Warumi 8:26 “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA”
Hapo anasema “kuugua kusikoweza kutamkwa” . Maana ya kuugua hapo ni kuweka uzito, au presha, au shauku ya kuomba ndani ya mtu isiyokuwa ya kawaida. Tofauti na angejitahidi kwa nguvu zake yeye mwenyewe. Sasa mtu akifikia hatua hiyo, basi tayari kuanzia huo wakati anaomba katika Roho hata kama maneno yake ni ya kawaida anayoyatumia. Maombi hayo yana nguvu na yanasikika sana mbele za Mungu.
Kwamfano, ndio hapo utakuta mtu anaomba, lakini mara anasikia kububujika machozi ndani yake, mwingine anazidi kuona kiu ya kuendelea kuombea jambo lile lile kwa muda mrefu tofauti na sikuzote. Mfano wakati ule Bwana Yesu alipokuwa Gethsamane anaomba.
mwingine anajisikia wepesi usio wa kawaida, uchovu wote umeondoka ijapokuwa alikuwa amechoka sana, anaanza furahia maombi, anafurahia kuendelea kubaki palepale muda mwingi kuendelea kuomba,
Sasa hali kama hizi ukizifikia, ujue tayari umeshazama katika Roho, umeshawezeshwa na Roho, maombi yako yanakuwa na nguvu sana,
Mwingine anasikia raha Fulani moyoni, akiwa anaomba, mwingine ndio anazama katika kunena kwa lugha (kwa kusukumwa na Roho), na sio kwa akili. Mwingine anasindikizwa na kuusikia uwepo wa Mungu umemfunika, nguvu za Mungu zinashuka mwilini mwake, n.k. na unajikuta unafurahia sana maombi..
Kusudi la sisi kuomba sio kwenda kujitesa au kujiumiza, hapana bali ni mahusiano, tena ya kama mtu anazungumza na Baba yake. Kiasi kwamba ukitoka kwenye maombi unaona umetoka kweli kuwasiliana na mtu, sio umetoka kuusemesha ukuta, usiokuwa na mrejesho wowote, umeomba hewani hewani tu
Sasa ni mapenzi ya Mungu kwamba sisi watoto wake kila tuombapo tuombe katika Roho Mtakatifu. Tuzame, tuyafurahie maombi yetu. Sasa tunawezaje kufikia hatua hiyo?
Kabla ya kuona namna ya kufikia hicho kilele. Tuone kwanza vikwazo vinavyomzuia mtu asiombe kwa Roho.
VIKWAVYO VINAVYOPINGANA NA MTU KUOMBA KATIKA ROHO.
Hawa ndio maadui wawili wakubwa wa mtu kuzama. Ndio maana wewe kama mwombaji ni lazima uwafahamu, na ujue kabisa huna budi kushindana nao na ni lazima ukutane nao. Vinginevyo usipowatilia maanani kila siku maombi yako yatakuwa ni ya “kawaida sana” na kila utakapofikiria kitu kinachoitwa maombi utaona kama vile unapelekwa gerezani.
Ndugu Mungu hajakusudia tujihisi hivyo sisi watoto wake tunapomkaribia yeye, tuwe kama tunaliomba sanamu lisilonena, amekusudia kutupa mrejesho, na ndio hiyo zawadi ya Roho kuugua ndani yetu. Lazima atupe mrejesho wake kwamba yupo nasi.
Sasa uanzapo, hakikisha unaunyima mwili wako, raha zote, zinazokinzana na wewe kuomba. Kwamfano, ukijiona mwili unasinzia au unapoa wakati wa kuomba usipende kukakaa kwenye kiti, ni heri upige magoti, ukishindwa tembea-tembea. Tena ni vizuri ukanyoosha na mikono yako juu, huku umefunika macho. Kisha anza kuomba.
Usiogope adhabu hizo za mwanzoni hazitadumu muda mrefu sana utaingia katika Roho, ni mwili tu unakuambia wacha, kunitesa, wewe ulazimishe tu, ukikuambia leo siku nzima umefanya kazi legea-legea, pinga hayo mawazo. Hivyo ukiwa Sasa katika hali hiyo. Anza kuomba lakini pia tumia ahadi za Mungu zilizopo kwenye biblia ni muhimu sana, kulingana na jambo unaloliombea, mkumbushe Bwana, ulisema hivi, na hivi kwenye Neno lako,, Ulisema ni nani aliye Baba, mtoto wake akimwomba mkate atampa jiwe, mkumbushe mwambie ulisema, kama ungetazama dhambi zetu ni nani angesimama,..mwambie ulisema niite nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa na magumu usiyoyajua n.k..Tumia njia hiyo, kujimimina kwa Bwana
Omba huku umetilia umakini(concentrate), mawazo yako ukiyalazimisha yasiende nje ya Mungu. Tengeneza picha halisi Mungu amesimama mbele yako kukusikia, fumba macho. Usiruhusu kufikia mambo ya nje, kwasababu akili yako itakuwa shapu kukutoa, ukitoka rudi, endelea kuomba. Ndio ni kipindi kifupi utataabika , lakini hatimaye utazama tu.. Sasa ukiendelea kudumu kwa kung’ang’ania huko kwenye maombi hayo kwa kipindi fulani. Hayo mazingira rafiki ya Roho Mtakatifu kuyaingilia maombi yako. Utashangaa tu, wepesi usio wa kawaida umezuka ndani yako. Tangu huo wakati endelea kuomba kwa jinsi usikiavyo rohoni, kwani hayo maneno unayoyaomba mengine hutaelewa unayatolea wapi, huyo ni Roho Mtakatifu anaomba na wewe.
Ndio maana akasema msifikiri-fikiri, kwasababu Roho mwenyewe atawajalia. Wengine kabla ya kuomba wanasema sijui nitaomba nini? Ndio hujui kwasababu bado hujazama, ukishazama utaweza tu kuomba kwasababu ni yeye ndio anayekujalia. Wengine wanasukumwa kunena kwa lugha n.k.
Adui wa pili ni shetani. Huyu anapaswa apingwe kwa kukemewa. Kabla ya kuanza maombi, hakikisha unayateka mazingira yako ya kimaombi. Ukimwomba Mungu, afukuze uwepo wote wa mapepo, hapo ulipo. Dalili ya shetani, ni pale unashangaa ukiwa unataka kuomba kichwa kinauma au tumbo, au hali Fulani isiyo ya kawaida inakuvaa katika mwili wako. Huyo ni shetani, mpinge kwa kukemea kisha endelea na maombi. Au mwingine anaona mazingira ya kusumbuliwa, mara kelele Fulani za nje, au simu zinaingia, ambazo si kawaida sikuzote kuwepo. Ndio maana ni vizuri katika kuomba kwako uzime simu. Ukae mbali na mazingira yenye mwingiliano, hiyo itakufanya umpe adui wakati mgumu kukusumbua.
Zingatia tu: Shetani haogopi sana maombi ilimradi maombi, anaogopa sana maombi yaliyo katika Roho, Hata kama ni ya muda mfupi, hayapendi, na ndio atakayoyapiga vita sana. Hivyo usiwe mwepesi mwepesi kupenda kuomba juu juu.
Kwahiyo ukizingatia mambo hayo mawili kutakufanya uzame rohoni katika maombi yako yote. Na utayafurahia na utaona matokeo pia.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika sanduku la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.
SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)
JE! TUNAPASWA TUOMBE MARA NGAPI KWA SIKU?
Wakili kibiblia ni mtu aliyepewa usimamizi wa nyumba (Au kaya) ya mtu mwingine. Na usimamizi huo unajumuisha kuanzia kwenye ngazi ya kifamilia, mpaka mali alizonazo bwana wake.
Uwakili tunaona tangu enzi za agano la kale, kwamfano, Eliezeri alikuwa ni wakili wa Ibrahimu. Na tunaona yeye ndio alikuwa mwangalizi wa mali zake, lakini pia ndiye aliyehusika kwenda kumtafutia Isaka, mke katika ukoo wa baba zake Ibrahimu (Mwanzo 15:2, Mwanzo 24).
Lakini pia tunamwona Yusufu, naye alikuwa ni wakili katika nyumba ya Potifa, aliachiwa vyote avisimamie, (Mwanzo 39:5-7).
Vilevile tukirudi kwenye agano jipya tunaona, Bwana Yesu alitumia mifano ya mawakili, kuwawakilisha watumishi wake wanaofanya kazi ya kuhudumu/kulichunga kundi lake, kwamba kwa mifano ya wao na sisi tujifunze utumishi uliosahihi kwake.
Kwamfano Luka 12:40-48 Inasema;
“Nanyi jiwekeni tayari, kwa kuwa saa msiyodhani ndipo ajapo Mwana wa Adamu.
41 Petro akamwambia, Bwana, mithali hiyo umetuambia sisi tu, au watu wote pia?
42 Bwana akasema, Ni nani, basi, aliye WAKILI mwaminifu, mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya utumishi wake wote, awape watu posho kwa wakati wake?
43 Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta anafanya hivyo.
44 Kweli nawaambia, atamweka juu ya vitu vyake vyote.
45 Lakini, mtumwa yule akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia kuja, akaanza kuwapiga wajoli wake, wanaume kwa wanawake, akila na kunywa na kulewa;
46 bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyojua, atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wasioamini.
47 Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana.
48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na zaidi”
Ikiwa wewe umepewa dhamana ya kulichunga/kulisimamia kundi, basi tambua kuwa Bwana anataka aone uaminifu wako wa kuwahudumia na kuwalinda watu wake aliokupa. Yesu alipomuuliza Petro Je! Wanipenda akasema ndio nakupenda!, Hapo hapo akamwambia chunga kondoo zangu, lisha kondoo wangu. Kuonyesha kuwa ikiwa wewe ni mtumishi na unasema unampenda Bwana, basi ujue upendo wako ni kuwachunga na kuwalisha kondoo wa Bwana.
Lakini pia uwakili sio tu kwa waliowatumishi wa Mungu, bali pia kwa kila mwaminio, aliyeokoka, amepewa uwakili wa kuifanyia kazi kwa ile talanta aliyopewa.
Bwana Yesu alitumia mfano wa Yule mtu aliyesafiri, akawaita watumwa wake, akawawekea mali yake yote wafanyie biashara, Hivyo mmoja akapewa talanta 5, mwingine 2, mwingine 1. Kama tunavyoijua habari wale wawili wa kwanza wakafanikiwa kuzalisha, lakini Yule mmoja wa mwisho hakuifanyia chochote talanta yake, akaiacha mpaka aliporudi bwana wake. Matokeo yake ikawa ni kunyang’anywa na kutupwa katika giza la nje (Mathayo 25:14-30).
Hiyo ni kutufundisha kuwa hakuna hata mmoja wetu, ambaye hajapewa karama na Mungu, hivyo unapaswa ujiulize, je! Talanta yangu ninaitumiaje, Uwakili wangu ninautumiaje Je! Ni katika kuujenga ufalme wa Mungu, au katika mambo yangu mwenyewe.
Hivyo kwa hitimisho ni kuwa waliokoka wote ni mawakili wa Kristo. Na hivyo Bwana anataka aone wakihudumu katika nyumba yake kwa uaminifu wote. Na ndivyo mitume wa Bwana walivyojiona mbele za Mungu.
1Wakorintho 4:1 Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu.
2 Hapo tena inayohitajiwa katika mawakili, ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu.
Vifungu vingine ambavyo utakutana na neno hili ni hivi; Luka 16:1-13, 1Wakorintho 9:17, Waefeso 3:2, Wakolosai 1:25.
Bwana akubariki.
Swali ni je! Umeokoka? Kama sio unasubiri nini? Mpokee sasa Bwana Yesu ili akupe uzima wa milele bure. Kumbuka hizi ni siku za mwisho, Yesu yu mlangoni kurudi , akikukuta hujaitendea kazi talanta yako utamjibu nini, Na umeshaisikia injili?
Ikiwa upo tayari leo kumpokea Bwana, akusamehe dhambi zako, basi fungua hapa kwa mwongozo huo wa sala ya toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Talanta ni nini katika biblia (Mathayo 25:14-30)
Tirshatha ni nini? (Ezra 2:63)
Beelzebuli ni nani? (Mathayo 12:24).
Swali: Je waliokufa kabla ya Bwana Yesu kuja (yaani watu wa agano la kale)wataokolewaje?.. kwamaana tunajua kupitia damu ya Yesu tu! ndio tunapata ukombozi wa hakika wa dhambi, sasa waliokuwa wanaishi katika agano la kale wataokolewaje na ilihali Kristo alikuwa hajafa bado, na damu iondoayo dhambi haijamwagika?.
Jibu: Ni kweli ukombozi unapatikana kupita damu ya Yesu tu!
Lakini ni vizuri kufahamu kuwa Agano jipya halikuja kulifanya agano la kale liwe uongo, badala yake limekuja kulikamilisha agano la kale, kama Bwana wetu Yesu alivyosema mwenyewe katika Mathayo 5:17..
Mathayo 5:17 “Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza”
Sasa Ili tuelewe vizuri hebu tutafakari mfano ufuatao.
Taasisi moja imedahili wanafunzi wake walioingia kupitia mfumo wa makaratasi, kwamba mwanafunzi ili akubalike kujiunga na chuo hana budi kuwasilisha fomu zake katika ofisi ya taasisi hiyo…. Lakini mwaka mmoja baadaye ikabadili mfumo na kuanza kudahili wanafunzi wapya kupitia mfumo wa kieletroniki kwamba ili mwanafunzi akubalike kujiunga na taasisi hiyo hana budi kutumia mfumo wa kielekroniki hata akiwa nyumbani kupitia internet. Na kwamba hakuna mwanafunzi yeyote atakayeweza kupokelewa bila kutumia mfumo huo, kwani ni mrahisi na mwepesi katika kutunza kumbukumbu.
Sasa swali ni je! mfumo huo mpya ulioanza utawafanya wale wanafunzi wa zamani ambao walitumia mfumo wa zamani kuwa si wanafunzi halali tena wa taasisi hiyo?.. au itawafanya wale waliokwisha kuhitimu zamani, waliotumia mfumo wa zamani vyeti vyao kuwa batili?.
Jibu ni la!.. Wataendelea kuwa wanafunzi, isipokuwa watakaojiunga upya hawana budi kutumia mfumo mpya..kwasababu mfumo wa zamani utakuwa umeshabatilika!.
Kadhalika na Agano la kale ni hivyo hivyo…Ulikuwa ni mfumo wa zamani wa kuwasogeza watu karibu na Mungu, lakini ulikuwa na mapungufu mengi!.. Lakini muda ulipofika, ulikuja mfumo bora Zaidi na mwepesi na wa haraka ambao utamwingiza mtu katika ufalme wa Mungu kirahisi na kihakika zaidi, na huo ndio mfumo wa Agano jipya kupitia agano la damu ya Yesu Kristo, na si tena damu ya mafahali na kondoo..kama maandiko yanavyosema katika Waebrania 10:4.
Waebrania 10:4 “Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.”
Na hivyo kulifanya Agano la kwanza liwe chakavu na agano la pili liwe jipya sawasawa na Waebrania 8:13.
Waebrani 8:13 “Kwa kule kusema, Agano jipya, amelifanya lile la kwanza kuwa kuukuu. Lakini kitu kianzacho kuwa kikuukuu na kuchakaa ki karibu na kutoweka”
Neno “kuukuu” maana yake ni “kuchakaa”… kwahiyo lilipokuja agano jipya, basi agano la kwanza likafanyika kuwa la kale, lisilotumika tena… hivyo kwasasa halifanyi kazi tena.
Kwahiyo waliokuwepo ndani ya Agano la kwanza kabla ya Bwana Yesu hao watahesabika kuwa watakatifu sawasawa tu waliopo sasa katika agano jipya leo, ndio maana akina Musa, Eliya, Henoko, Ibrahimu, Daudi, Danieli na wengineo wanatajwa kuwa miongoni mwa watakatifu, tena mashujaa wa Imani… ijapokuwa hawakubatizwa! Wala kumwona Masihi..
Lakini baada ya Bwana Yesu kuja na damu yake kumwagika basi wote watakaozaliwa baada ya hapo, hawana budi kulitumia agano jipya, na kuachana na lile la kale…na yeyote atakayejitumainisha kwa agano la kale basi hataweza kuokoka kabisa.
Hiyo ndio sababu kwanini tunapaswa tulijue sana Agano jipya na misingi yake, kwasababu tukianza kuwatanzama watu wa Agano la kale, pasipo kujua misingi ya agano jipya, tutajikuta tunachukua vitu visivyofaa kwa watati wa sasa….kwamfano tukimtazama Daudi na maisha yake na kanuni alizokuwa anatembelea si zote zitatufaa sisi watu wa agano jipya, kwamfano utasoma ijapokuwa Daudi aliupendeza Moyo wa Mungu sana lakini alikuwa na wake wengi na alikuwa na visasi na maadui zake.
Sasa tutachukua na kujifunza Imani ya Daudi, unyenyekevu wa Daudi na mengine mazuri, lakini hilo la kuoa wake wengi, Agano jipya inalikataza, hilo la kulipiza kisasi agano jipya limetuzuia..…hatuna budi kumsikiliza aliye mkuu Zaidi ya Daudi, na Sulemani, na Musa, na Eliya ambaye ni Yesu, anayetajwa kama Mjume wa Agano jipya (katika Waebrania 9:15 na Waebrania 12:24), ambaye anasema kila amwachaye mkewe na kuoa mwingine azini, na ndoa ni mke mmoja, mume mmoja..si Zaidi ya hapo!(Mathayo 19:4), ambaye amesema “tusilipe kisasi” (Mathayo 5:38-39). n.k
Bwana akubariki.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
LITURJIA NI NINI? NA JE IPO KIMAANDIKO?.
Biblia ilimaanisha nini iliposema “Mwanamke atamlinda mwanamume” Yeremia 31:22?
Nini maana ya “Bwana Yesu ni mzaliwa wa kwanza wa waliokufa?”(Ufunuo 1:5)
Jibu: Tusome,
Mwanzo 33:17 “Yakobo akaendelea mpaka Sukothi. Akajijengea nyumba, akawafanyia makundi yake vibanda. Kwa hiyo jina la mahali pale pakaitwa Sukothi”.
Tafsiri ya neno “Sukothi” ni “Mahema”.. Hii ni lugha ya kiebrania.
Mahali hapa ni pale ambapo Yakobo alipiga kambi baada ya kutoka Padan-aramu, mji aliokuwepo Labani.(Mwanzo 28:1-2), na alikaa huko Padan-aramu kwa muda wa miaka 21, baada ya kulaghaiwa na Labani kwa muda wote huo.
Akiwa njiani baada ya kutoka kwa Labani alifika mahali ambapo ilimgharimu kutulia kidogo kisha andelee na safari, hivyo badala ya kujenga makazi ya kudumu, yeye akajenga mahema machache tu, kwasababu ya muda kwani bado alikuwa katika safari ya kuelekea Shekemu (Mwanzo 33:18). Hivyo Yakobo akaliita eneo hilo Sukothi kutokana na mahema hayo, na eneo hilo likaendelea kuitwa hivyo kwa vizazi vingi baadaye.
Na eneo la Sukothi kijeografia lipo maeneo ya nchi ya Yordani mpakani na Israeli.
Waamuzi 8:4 “Basi Gideoni akafika Yordani, akauvuka, yeye na hao watu mia tatu waliokuwa pamoja naye, walikuwa wamepungukiwa na nguvu, lakini wawafuatia vivyo.
5 Naye akawaambia watu wa Sukothi, Tafadhali wapeni mikate hao watu waniandamao; kwa maana wanapungukiwa na nguvu, nami ni katika kuwafuatia Zeba na Salmuna, wafalme wa Midiani”.
Kujua ni somo gani lingine tunalipata kuhusu Sukothi?…Fungua hapa >>TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Raheli aliwalilia vipi watoto wake?
Kwanini Labani aseme Yakobo ni Mfupa wake na nyama yake?(Mwanzo 29:14)
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1
SWALI: Bwana Yesu asifiwe naomba kufahamu maana ya hili andiko;
1Wakorintho 14:20 “Ndugu zangu, msiwe watoto katika akili zenu; lakini katika uovu mgeuzwe watoto wachanga, bali katika akili zenu mkawe watu wazima”
JIBU: Kwa kawaida mtoto mchanga anakuwa kama mjinga, haelewi mambo mengi, anachofahamu ni kile tu kilichopo nyumbani, mambo mengine ya nje, hayajui, na ndicho kinachomfanya asijisumbue na hayo mengine, ambayo watu wazima wanayasumbukia,. Vivyo hivyo na Mungu anataka katika suala la uovu, tuwe hivyo. Kama wajinga, hatujui kinachoendelea, hatuna maarifa nayo, hatuwezi kuyaelewa. Na hiyo itatufanya tuwe salama.
Kwamfano ukiulizwa habari za nyimbo Fulani mpya za kidunia zilizotoka, huna taarifa nazo, Ukiulizwa habari za ligi za mipira, ni kama taarifa usizozielewa, ukisemeshwa na mambo ya kubeti, ni kama mtu anazungumza na wewe kwa lugha za mafumbo.
Ndio maana andiko hili linasema hivyo;
1Wakorintho 16:19b “…lakini nataka ninyi kuwa wenye hekima katika mambo mema, na wajinga katika mambo mabaya”
Kutokujua kila kitu katika huu ulimwengu sio dhambi, na wala hilo halitakuzuia uishi vema. Hivyo tunapaswa tuchuje, ni nini kinatufaa na kipi kisichotufaa, Vile visivyotufaa tuviweke kando, tuwe watoto katika hivyo, lakini vile vitujengavyo, ambalo ni NENO LA MUNGU, basi tuwe watu wazima. Tulijue sana hilo kwasababu ndio uzima wetu ulipo.
Bwana akubariki
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Nini maana ya “Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia?
Nini maana ya vifungeni viuno vya Nia zenu? (1Petro 1:13)
Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?
Je biblia inatufundisha tuwe wapole kiasi? (Wagalatia 5:22-23)
Je biblia inatufundisha tuwe wapole kiasi? (Wagalatia 5:22-23)